Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

RAIS MAGUFULI AZINDUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO NA KUHUTUBIA WANANCHI KWENYE MIKUTANO MBALIMBALI YA HADHARA

$
0
0
 Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  pamoja na viongozi mbalimbali wakifungua kitambaa kuashiria kuweka jiwe la msingi la ufunguzi wa Barabara  ya Kibondo -Nyakanazi kiwango cha lami.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  pamoja na viongozi mbalimbali serikali wakikata Utepe  kuashiria kuweka jiwe la Msingi la Uzinduzi wa Ujenzi wa  Barabara  ya Kibondo -Nyakanazi 
 Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,  Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Kakonko kabla ya kuzindua Ujenzi wa barabara ya Kibondo -Nyakanazi yenye urefu wa kilometa 54, katika mkoa wa Kigoma.
 Wananchi wa Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Uzinduzi wa  Ujenzi wa Barabara  ya Kibondo -Nyakanazi yenye urefu wa kilometa 54, kwenye Sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Standi Mpya ya Mabasi Kakonko katika mkoa wa Kigoma Rais yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya siku Tatu
Baaadhi ya Viongozi wa vyama vya siasa na wananchi wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma wakisikiliza Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Uzinduzi wa  Ujenzi  wa Barabara  ya Kibondo -Nyakanazi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwasalimia wananchi wa mji wa Kibondo wakati akiwa safarini kutoka Ngara kuelekea Mkoani Kigoma.
 Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisalimiana na kijana mwenye ulemavu amabye ni fundi wa kushona nguo ndugu Aron Michael Kapililo mkazi wa Kibondo ambaye alisimiana na Rais Magufuli 
 Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mamia ya wananchi wa kijiji cha Kifura,  Kibondo Mkoani kigoma waliokuwa wamesimama njiani ili kusalimiana na mh Rais akiwa njiani  safarini kutoka Ngara kuelekea Mkoani Kigoma
 Mamia ya wakazi wa Kasulu Mkoani Kigoma waliojitokeza kumsikiliza Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisalimiana na mamia ya wananchi wa Mamia ya wakazi wa Kasulu Mkoani Kigoma waliojitokeza kumsikiliza wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwapungia mikono mamia ya wakazi wa Kasulu, Mkoani Kigoma.
Mamia ya wakazi wa Kasulu Mkoani Kigoma waliojitokeza kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya viongozi walioshiriki uzinduzi wa uzinduzi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu
  Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mbunge Kigoma Mjini Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe mara baada ya kuzindua  ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Kigoma akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa  ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu Mkoani Kigoma,
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi waliokuwa wamefurika njiani mara baada ya  Uzinduzi wa  ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 63 Kidawe - Kasulu Mkoani Kigoma.

DKT. MPANGO ATANGAZA MAPATO KODI YA MAJENGO SHILINGI BILIONI 32.5.

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akivipongeza Vituo vya Mafuta vya Puma na Total kwa kuonesha mfano wa kufunga mashine za EFDs katika Pampu zote za mafuta kwenye vituo vyao, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.(Picha: Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akiwaomba wananchi kulipa kodi ya Majengo mapema kwa mwaka wa Fedha 2017/18 ili kuepuka usumbufu wa msongamano, alipofanya Mkutano na Waandishi wa habari katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akitoa agizo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha kuwa mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFDs) zinatumika ipasavyo na kutengenezwa mara moja zinapoharibika na kwamba zisipotengenezwa ndani ya saa 48 zifungwe na wamiliki wake watozwe faini, alipozungumza na wanahabari, Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam wakiwa katika Mkutano na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani) ambapo Waziri huyo aliwashukuru wananchi kwa kulipa kodi ya Majengo kiasi cha Sh. Bilioni 32.5 kufikia Julai 15, 2017, katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Jijini Dar es Salaam.

………………………………………………………………..

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya Sh bilioni 32.5 ya kodi ya majengo, kwa mwaka wa fedha 2016/17 kutoka katika Majiji, Miji na Manispaa 30 nchini.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb) amewaambia waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam kwamba makusanyo hayo ni sawa na asilimia 56 ya lengo lililowekwa Mwaka wa Fedha uliopita la kukusanya shilingi bilioni 58.

Alisema kuwa hatua niyo ni mafanikio makubwa tangu TRA ipewe jukumu la kukusanya kodi hiyo ambapo mwaka wa fedha 2015/2016 katika maeneo hayo, Halmashauri zilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 28.3 wakati TRA imekusanya kiasi hicho cha shilingi bilioni 32.5 tangu ianze kukusanya kodi hiyo mwezi Oktoba mwaka wa fedha 2016/2017.

“Mpaka kufikia tarehe 15 Julai mwaka huu TRA imekusanya sh. bil 32.5 kipindi ambacho ni kifupi, na kwamba mapato hayo yanatarajiwa kuongezeka kutokana na mwitio mkubwa wa wananchi kulipa kodi ya majengo”Alisema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango aliwapongeza wananchi kwa mwitio wao mkubwa wa kulipa kodi ya majengo na kwamba wameonesha uzalendo wa kweli na ndio maana Serikali imeamua kuongeza muda wa kulipa kodi hiyo bila adhabu hadi Julai 30 mwaka huu, hali anayoamini itapandisha zaidi mapato hayo.

Katika hatua nyingine Dkt, Philip Mpango aliwapongeza wamiliki wa vituo vya mafuta waliotii maagizo ya Serikali, kwa kufunga mashine stahiki za EFDs, akitolea mfano vituo vya PUMA na TOTAL ambavyo vimefunga mashine hizo kwenye pampu zao zote.

Aliwaonya wamiliki wote wa vituo vya mafuta ambao hawatafunga mashine hizo za EFDs ndani ya siku 14 kama agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli linavyoelekeza na kwamba yeye kama Waziri mwenye dhamana atahakikisha analisimamia kikamilifu na kwamba baada ya muda huo mtu asijekuilaumu Serikali baada ya kuanza kuchukua hatua kali za kisheria.

Aliwataka wamiliki wa vituo hivyo kupitia chama chao cha wamiliki wa vituo vya mafuta TAPSOA kuheshimu maelekezo ya Serikali na kuacha majibizano yasiyo na tija kuhusu amri hiyo ya Rais kwenye vyombo vya habari kwa kuwa huo ni utovu wa nidhamu.

Aliwageukia wenye maduka ya vifaa vya ujenzi, vileo na maduka makubwa ‘supermarket’ nao watumie mashine hizo za kukusanyia mapato ya Serikali (EFDs) kikamilifu na kutoa risiti kwa wateja wao huku akiwaasa wateja nao kudai risiti wanapofanya manunuzi kulingana na kiwango halisi cha bidhaa wanazonunua.

Alipiga marufuku wafanyabiashara wanaosingizia mashine za EFDs kuwa mbovu na kuwaonesha wateja wao makaratasi waliyotoa taarifa TRA kwamba mashine zao zilikuwa mbovu kwa kipindi kifrefu na kuaigiza Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, kusimamia jambo hilo ili kuhakikisha kuwa linakoma kabisa.

“TRA mtimize majukumu yenu mliyodhaminiwa na Serikali na kuhakikisha kuwa wafanyabiashara ambao mashine zitakuwa hazitumiki ndani ya saa 48 kwa kisingizio cha kuharibika zifungiwe na wamiliki watozwe faini na kulipa kodi ya Serikali ipasavyo” aliagiza Dkt. Mpango.

“Serikali ya Awamu ya Tano haijaribiwi, tumeazimia tutafanya kazi kwa niaba ya wanyonge ili nchi yetu iende mbele na kwa hili watusamehe.” Alisisitiza Dkt. Mpango

Dkt Mpango alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kujitoa kwake kuwatumikia wananchi na kuongoza mapambano ya uchumi yatakayo ifikisha nchi kwenye uchumi wa kati ambao hata watu wa kawaida watajisikia kuwa unakua kwa kutatua changamoto zao za maisha.

Alisitiza watanzania wafanye kazi kwa bidii kujenge nchi ili kila Mtanzania apate huduma bora, barabara bora, tiba nzuri, maji, yote haya hayawezi kufanyika bila mapato yakutosha na kwamba Tanzania itajengwa na Watanzania wenyewe.

Marianus: Mchezo wa Biko utakuza uchumi wa Watanzania wengi

$
0
0
MJASIRIAMALI mdogo mkazi wa Chanika, jijini Dar es Salaam, Enos Marianus, amesema bahati nasibu ya Biko inayaoendelea kuchanja mbuga nchini Tanzania, utakuza uchumi wa washiriki na Watanzania kwa ujumla, akiwamo yeye ambapo ana mpango wa kuendeleza biashara zake..

Hayo yamesemwa na mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Marianus wakaati anakabidhiwa fedha zake katika makabidhiano yaaliyofanyika jana katika benki ya NMB, Posta, jijini Dar es Salaam.

Marianus alisema ukosefu wa ajira unasababisha watu wengi watamani kuingia kwenye ujasiriamali, hivyo uwapo wa mchezo wa Biko utapunguza changamoto hiyo, hivyo ni jambo la msingi la kuhakikisha kuwa kila mtu anacheza Biko ili ashinde mamilioni ya Biko.

“Nashukuru leo kwa kukabidhiwa fedha zangu Sh Milioni 20 kutoka kwa watu wa Biko, hivyo ninaamini kabisa mchezo huu utakuza uchumi wetu hususan sisi wajasiriamali wadogo ambao fedha hizi zitaingia kwenye kupanua wigo wa biashara zetu kwa namna moja ama nyingine,” Alisema.

Naye Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko, Hassan Melles, alisema ushindi wa Biko ni rahisi husuan kwa wale wanaocheza mara nyingi kwa kufanyaa miamala kwenye simu za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo namba yao ya kampuni ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456.

“Sh 1,000 ya Biko inayochezwa inampa mtu ushindi wa papo kwa hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni Moja inayolipwa papo hapo kwenye simu iliyotumika kuchezea Biko pamoja na zawadi nono ya Sh Milioni 20 inayotoka Jumatano na Jumapili,” Alisema Melles.

Zaidi ya Sh Bilioni moja tayari zimelipwa kwa washindi wa Biko kwa kipindi cha mwezi Mei na Juni pekee, ikiwa ni mwendelezo wa kutoa mamilioni ya fedha kwa washindi wake wanaocheza Biko tangu kuanzishwa kwa mchezo huo hapa nchini.
 Meneja Masoko wa Biko Tanzania, Goodhope Heave wa pili kutoka kulia akimkabidhi fedha zake mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Enos Marianus mwenye shati jeupe, jana jijini Dar es Salaam, katika benki ya NMB. Wa kwanza kulia ni Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko Tanzania, Hassan Melles.
 Mratibu wa Matukio na Mawasiliano wa Biko Tanzania, Hassan Melles wa pili kutoka kulia akimkabidhi fedha zake mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko, Enos Marianus mwenye shati jeupe, jana jijini Dar es Salaam, katika benki ya NMB. Wa kwanza kulia ni Goodhope Heaven, Meneja Masoko wa Biko Tanzania.
Mshindi wa Sh Milioni 20 wa Biko droo ya 24, Enos Marianus kulia aakiwa na furaha tele baada ya kukabidhiwa fedha zake jana katika benki ya NMB, jijini Dar es Salaam, siku moja baada yaa kutangazwa mshindi wa bahati nasibu ya Biko. Kushoto kwake ni mkewe Bi Kisa Kasito aliyemsindikiza katika kukabidhiwa fedha zake.

BALOZI WA ISRAEL NCHINI MHE. YAHEL VILAN AWAAGA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) BAADA YA KUMALIZA MUDA WAKE WA KUFANYA KAZI HAPA NCHINI

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimshukuru Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan (kulia) kutokana na nchi yake kuisaidia Taasisi hiyo kuwapatia mafunzo madaktari, wauguzi na kutoa matibabu kwa watoto. Katikati ni Daktari Bingwa wa Moyo kwa watoto na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo Sulende Kubhoja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Israel imekuwa ikiisadia JKCI kwa kutoa mafunzo kwa madaktari, wauguzi na matibabu kwa watoto.
Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Israel imekuwa ikiisadia JKCI kwa kutoa mafunzo kwa madaktari, wauguzi na matibabu kwa watoto.
Mwanamuziki kutoka nchini Israel Maestro Nir Brand akiwaimbia wimbo watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati balozi wa nchi hiyo Mhe. Yahel Vilan alipotembelea Taasisi hiyo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Balozi wa Israel nchini ambaye makazi yake yapo Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan (watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi pamoja wa wafanyakazi wa Taasisi hiyo na wageni kutoka nchini Israel.
Daktari Bingwa wa Moyo kwa watoto na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo Sulende Kubhoja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akizungumza na Daktari Bingwa wa mfumo wa chakula kwa watoto Cohen Shlomi kutoka nchini Israel wakati wa ziara ya balozi wa nchi hiyo alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuwaaga wafanyakazi.
Baadhi ya watoto wanaotiba katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Balozi wa Israel nchini ambaye makazi yake yapo Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan alipokuwa akiwaaga wakati wa ziara yake aliyoifanya leo katika Taasisi hiyo. Serikali ya Israel kupitia Taasisi ya Save Child Heart (SACH) imegharamia matibabu ya watoto 40 tangu Novemba 2015 hadi sasa ambao walitibiwa nchini humo.
Balozi wa Israel nchini ambaye makazi yake yapo Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan akizungumza na wafanyakazi pamoja na watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wakati wa ziara yake ya kuwaaga aliyoifanya leo baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Israel imekuwa ikiisadia Taasisi hiyo kutoa mafunzo kwa madaktari, wauguzi na matibabu kwa watoto.

Picha na JKCI

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMAMOSI LEO JULAI 22,2017

WAZIRI MKUU AAGIZA KUANZA UJENZI WA HOSPITALI TUNDUMA

$
0
0



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma wilayani Momba kuanzisha mradi wa ujenzi wa hospitali.

Amesema sh. milioni 900 zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Halmashauri kwa sasa zianze kutumika katika kuanzisha ujenzi wa hospitali hiyo.

Agizo hilo alilitoa jana jioni (Ijumaa, Julai 21, 2017) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma.

“Kwa kuwa afya ni jambo muhimu katika utekelezaji wa kauli mbiu ya Rais Dkt. John Magufuli ya Hapa Kazi Tu, hivyo naagiza fedha zilizotengwa kuanza ujenzi wa ofisi zitumike katika ujenzi wa hospitali.”

Waziri Mkuu aliwataka viongozi wa halmashauri hiyo kuongezea sh. milioni 126 katika ujenzi huo. Fedha hizo zilitengwa kwa ajili ya kuwafidia wamiliki wa eneo lililotengwa awali kwa ajili ya kujenga hospitali, ambapo aliwataka watafute eneo lisilohitaji fidia.

Pia, Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) iandae ramani kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo na kuhusu suala la ujenzi wa ofisi Serikali italishughulikia.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo baada ya Mbunge wa jimbo la Tunduma, Mheshimiwa Frank Mwakajoka aliyeiomba kuiomba Serikali kuwajengea hospitali kwa kuwa halmashauri hiyo haina hospitali, hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi pale wanapohitaji huduma hiyo.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo, Bw. Juma Irando alitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili wilaya hiyo kuwa ni ukosefu wa hospitali ya wilaya, ukosefu wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya na ofisi za Halmashauri.

Pia changamoto nyingine ni ubovu wa miundombinu ya barabara iliwemo ya Makamba-Ikana inayotakiwa kukarabatiwa inayounganisha ukanda wa juu na chini ili wananchi wa ukanda wa juu waweze kufika makao makuu ya wilaya.
 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, JULAI 22, 2017
                                

 

WAZIRI LUKUVI AONYA MAAFISA ARDHI WASIO WAADILIFU

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwaonya maafisa ardhi na maafisa mipango miji wasio waadilifu na kusababisha kero za migogoro ya ardhi nchini wakati wa uzinduzi Master Plan ya mji wa Iringa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimkabidhi kitabu cha Master Plan ya mji wa Iringa Meya wa Halmashauri ya Iringa Alex Kimbe.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiteta jambo na Meya wa Halmashauri ya Iringa Alex Kimbe na Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akipongezwa na Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa mara baada ya Uzinduzi wa Master Plan ya mji wa Iringa.
Baadhi ya wakazi wa mji wa Iringa waliofika kushuhudia Uzinduzi huo.

……………………………………………………………………………………….

Na Hassan Mabuye Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Ardhi


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amewaonya maafisa ardhi na maafisa mipango miji wasio waadilifu na kusababisha kero za migogoro ya ardhi nchini.

Waziri Lukuvi aliyasema hayo leo katika ukumbi wa shule ya sekondari Lugalo mjini Iringa wakati wa Uzinduzi wa Master Plan ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Amesema mchezo huo wa ufisadi ambao umekuwa ukitumiwa miaka yote na maofisa ardhi nchini ameubaini na kuwataka wakurugenzi wa Halmashauri nchini kutokubaliana na ramani za maeneo mapya zinazoletwa na wataalam hao bila ya wao kufika maeneo husika na kuoneshwa maeneo hayo ili kujiridhisha.

Waziri Lukuvi amefichua kuwa ufisadi unaofanywa na maafisa ardhi nchini kwa kupima viwanja hewa kwa ajili ya maslahi yao na kusema kuwa mbinu ambayo wamekuwa wakiitumia kuiibia serikali amekwisha ibaini na hata kubali kuona mbinu hiyo inapewa nafasi katika serikali hii ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli .

Maafisa ardhi wakishirikiana na maafisa mipango miji pamoja na wapima wamekuwa wakitajirika sana kwenye idara zao na wanatakata kwa ujanjaujanja na ufisadi wanaoufanya kwa kutengeneza ramani zinazoonesha maeneo mazuri na muhimu katika miji kwamba hayafai kutumika, kumbe wameyauza maeneo hayo kwa mlango wa nyuma na kwa bei za juu.

Unakuta kwenye ramani inayonyesha kuna bonde kubwa lisilofaa kujengwa kumbe ukifuatilia eneo hilo ni zuri kuliko yote na hapo wametenga viwanja vya kuuza. Unakuta ukipima kuna viwanja vingi na vizuri ambavyo ni vyao wao wanachofanya baada ya kuuza viwanja halali za Halmashauri hurudi kupima maeneo hayo walioonyesha ni mabonde na kugawana wao kwa ajili ya kuuza kwa faida yao.



Lukuvi amesema kuwa wathamini nao pi wamekuwa wakiwapunja wananchi wasio elewa kwa kuwafanyia tathimini kubwa zaidi ya uhalisia wake na pindi pesa inapotoka utakuta nyumba inathamani ya milioni 7 wakati wao wanasema inathamani ya milioni 20 ili cha juu wapate wao.

“wakati nilipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam niliweza kubaini ujanja wa wathamini baada ya eneo ambalo nyumba zake zina thamani kati ya milioni 20 hadi 50 kwa maana nyumba hizo ni za udongo ila maofisa hao walimtafuta mtu na kutafuta nyumba nzuri zaidi na kumshikisha kibao kisha kumpiga picha na kuandika kuwa nyumba hiyo inathamani ya zaidi ya milioni 200.

Niliamua kufanya uchunguzi wangu na kumtafuta mtu aliyekwenye picha na kumbana ndipo aliniambia ukweli kuwa mthamini huyo ni ndugu yake hivyo walikubaliana pesa ikitoka atalipwa milioni 70 na milioni 130 ni za afisa huyo”

Hata hivyo alisema kuwa ujenzi holela katika miji na halmashauri imesababishwa na ukilitimba wa utoaji wa vibali kwa wakati na ndio sababu ya wananchi kuvamia maeneo yasiyo pimwa japo kuanzia sasa wote waliopo katika maeneo yasiyo pimwa watapewa leseni ya makazi ya miaka mitano na watalipa kodi ya ardhi na baada ya miaka mitano wahakikishe wamepimiwa ili kupewa hati.

Hivyo Lukuvi aliwataka maafisa ardhi na wathamini wa ardhi manispaa ya Iringa kutofanya kama maeneo mengine kwa kufuata mpango maeneo yote ambayo yameelekezwa kwenye Masta Plan hiyo na kwenda kutenda haki.

Katika hatua nyingine waziri Lukuvi alitoa agizo kwa wale wote waliopewa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa hoteli na viwanda na wale waliouziwa viwanda vya serikali, hotel na mashamba ya serikali kuviendeleza haraka kabla ya ardhi hiyo haijapokonywa .

Nae Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bibi Amina Masenza akimkaribisha waziri Lukuvi amesema kuwa mkoa wa Iringa umeendelea kuhamasisha wananchi kuzingatia sheria na taratibu za ujenzi na kuachana na ujenzi holela na ndio sababu ya kuja na Masta Plan hiyo ambayo imeanzishwa na aliyekuwa mstahiki meya wa halmashauri hiyo Amani Mwamwindi.

Akitoa taarifa ya uandaaji wa Masta Plan hiyo kwa ajili ya mwaka 2015-2035 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Dkt William Mafwere, alisema kuwa dhumuni la mpango huo ni kutatua changamoto zilizokuwa zinaikabili Manispaa na kuwa dhana kuu ya mpango huo ni dhana unganishi ikijumuisha dhana nyingine.

Alisema jumla ya miradi 31 itatekelezwa katika awamu ya kwanza 2015-2020 kuwa baadhi ya miradi hiyo ni kituo cha mabasi Igumbilo, kituo hicho kimeanza ujenzi na hatua ya utekelezaji imefikia asilimia 30.

Nae Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa alisema kuwa kazi inayofanywa na Waziri Lukuvi ni tofauti na mawaziri wengine kwani amekuwa ni waziri wa mfano katika kuchapa kazi.

“Kwa mnaonifahamu vizuri mimi sio mbunge wa kusifia sifia ni mbunge mwenye msimamo ila nampongeza sana Waziri Lukuvi ni waziri mchapakazi na kazi zake zinaonekana na ndio maana hata bungeni ni waziri pekee ambaye bajeti yake ilipitishwa kwa kishindo hata na sisi wabunge wa kambi ya upinzani”

Mpango Kabambe ni chombo cha kuchochea utumiaji wa fursa zilizopo katika mji, kuongeza kasi ya upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii na kupunguza na kumaliza migogoro ya ardhi. kudhibiti ujenzi holela mijini na hutumika pia kuongoza, kusimamia na kudhibiti ukuaji na uendelezaji wa mji na kutoa uhakika kwa wawekezaji katika Halmashauri za Manispaa ya husika.

SGA Security Comes to the Rescue of Abandoned Patients at MOI

$
0
0
In response to appeal in both mainstream and social media, the largest and oldest security company in the Tanzania, SGA Security, responded with donations. 

These were presented on 21st July 2017 to the management of Muhimbili Orthopaedic Institute(MOI) and received by the Director of Nursing – Ms. MF Kimaro. She expressed their gratitude to SGA for being the first to respond to the plight of the patients.  
Security Group Africa Group (SGA),Managing Director, Eric Sambu (right) handing over donations worth 2.5m/- to the Nursing Director at the Bone Institute (Moi), Ms. Flora Kimaro during a special visit to patients.

The donations included foodstuff, sanitary items and wheel chairs, all valued at TZS.2.5 Million. The SGA Customer and Public Relations Manager, Ms. Aikande Makere, explained that it is their practice to support community initiatives, in line with their corporate social responsibility. 

SGA has health and safety core theme and that extends to the public. She explained that she heard the appeal and felt that they needed to chip in and called upon other institutions to follow suit. “The patients belong to all of us and we have to shoulder this responsibility, as a society, jointly”, she added.

Mr. Jumaa Tram Almasi, MOI’s Manager, Welfare& Public Relations Unit expressed gratitude to SGA Security for choosing their institution to make the donation. “As you might be aware, treatment of the destitute patients is costly and we cannot do it alone, that is, provision of both medical and social needs. 

We need support from Well-Wishers and Good Samaritans to support us”, he said. “Patients dumped by their relatives add a strain in the already overloaded health services. 

The support from SGA security is timely and a stitch in time. We kindly urge the rest to support us through their CSR Programs”, he added.


SGA Security Managing Director, Mr. Eric Sambu, explained that they have spent over TZS.55 million this year on CSR programs, with a few activities remaining before end of the year. He explained that being part of the society, they always decide on areas to provide support as a way of giving back to the public.

 He was there with the ambulance team and guards during the presentation. They visited the patients in wards to give them a word of encouragement.
Security Group Africa Group (SGA),Managing Director, Eric Sambu and the Customer  and Public Relations Manager (SGA), Ms.Aika Makere were informed that the patient was undergoing treatment for mental disorder at Moi.

SGA Security was the first Private Security Company registered in Tanzania in 1984, as Group Four Security, following deregulation of the sector from Government control. Today, after more than 33 years of successful operations, SGA is the largest private security company in Tanzania, represented in every service area in the sector. Employing about 5,000 employees in Tanzania and over 18,500 in the region, SGA is one of the largest employers in the region.

Speaking during the presentation at MOI, the Managing Director, Mr. Eric Sambu, said that they aid to entrench corporate citizenship by playing bigger role in the society as they strive to continuously add value to their customers. 

SGA recently launched a new fleet of ultra-modern and fully-equipped armored vehicles to provide alarm response services and cash in transit services in the country. SGA provides a full spectrum of integrated security services, which ensures that its clients enjoy a cost-effective interfusion of manpower and technology, safeguarding their personal and business assets, wherever they may be located. “We  are presently updating skillsets for all our employees to empower deliver our promises in line with our mission. 

The training cuts across all cadres and facilitators are from all sectors, including our disciplined forces.”, he added. In addition to donations like this, SGA conducts free awareness training to selected public to improves health and safety in the society. They recently completed such training to bodaboda riders that covered 230 riders. They also donated reflective jackets and helmets after the awareness training.
Mr. Sambu continued to explain that SGA is the largest provider of Cash in Transit and Cash Management services in Tanzania and the provider of choice for over 85 Banks and Financial Institutions in the East Africa region. Our large fleet of fully armoured CIT vehicles visit over 750 bank branches in Tanzania, safely moving tens of billions of shillings, millions of kilometres each year. 

All our Cash Management services are fully insured through reputable, internationally renowned insurers. Our expertise extends to the Diplomatic and NGO sectors with over 65 Embassies and Development Aid clients in the region. We understand the specific risk profile of these clients and have specifically trained staff for these.

Dk. Kigwangalla afanya ziara mikoa ya Rukwa, Katavi na Tabora

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla ameendelea na ziara yake ya kikazi ya kukagua huduma za Afya ‘Imarisha Afya’ katika Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali mbalimbali kwenye mikoa ya Rukwa, Katavi pamoja na Tabora. 

Akiwa katika mkoa wa Rukwa, Dk. Kigwangalla aliweza kutembelea Hospitali ya Sumbawanga ambayp ni ya Mkoa wa Rukwa na kujionea mambo mbalimbali huku akiwapongeza kwa namna walivyoboresha huduma zao ikiwemo ile ya Maabara, Chumba cha upasuaji na huduma zingine ambapo aliwaagiza kuhakikisha wanakuwa na hakiba ya kutosha ya damu salama kwa ajili ya dharura kwa wagonjwa wa ukanda huo. 

 Mbali na Hospitali ya Mkoa wa Rukwa, pia aliweza kutembelea kituo ca Laela ambapo pia mbali ya kujionea utendaji kazi wa kituo hicho alipongeza juhudi za Mbunge wa jimbo la Kwera, Mh. Ignas Alloyce Malocha kwa kushirikiana na wananchi wake katika masuala ya huduma za Afya.Ziara hiyo katika mkoa wa Rukwa, aliweza kumalizia katika Kituo cha Afya Wampembe kilichopo Wilayani Nkasi ambapo alijionea shughuli mbalimbali ikiwemo huduma za Upasuaji hata hivyo aliutaka uongozi wa kituo hicho ambacho kipo mwambao wa Ziwa Tanganyika kuhakikisha wanakamilisha mifum ya maji safi na salama ndani ya kituo pamoja na kuboresha huduma za Maabara na usafi kwa ajumla. 

Akiwa katika Mkoa wa Katavi, Dk. Kigwangalla aliweza kufanya ziara ya kushtukiza kituo cha Afya Inyonga,kilichopo Mlele majira ya Saa Sita mchana na kuweza kukagua maeneo mbalimbali ikiwemo Chumba cha Maabara, Chumba cha Upasuaji na wodi ya akina mama wanaosubiria kujifungua. 

Hata hivyo, Dk. Kigwangalla amemtaka Kaimu Mganga Mkuu wa Kituo hicho kumuandikia maelezo juu ya kutokuwepo kwa watoa huduma kwenye jingo la chumba cha upasuaji na eneo la wodi ya akina mama wanaosubiria kujifungua kwani licha ya kufika hapo hakukuta mtoa huduma hata mmoja kwa wakati huo hali ambayo inaweza kuleta hatari. 

“Nataka kupata maelezo kwa maandishi. Kwa nini hakukua na watoa huduma ndani ya Chumba cha upasuaji na kule kwa wodi ya wamama wajawazito. Nilifika kuwakagua kwa upande wa Maabara nimekuta safi mumeweza kuboresha huduma na mumezingatia maelezo yangu niliyoyatoa kipindi nilichofika kukagua mwaka jana. Lakini pia hali niliyoikuta katika maeneo hayo niliyotembelea bila kuwakuta wahusika hii ni hatari nitahitaji maelezo ya kimaandishi” alieleza Dk. Kigwangalla wakati akitoa maagizo kwa Kaimu Mganga Mkuu wa kituo hicho. 

 Aidha, akiwa katika mkoa wa Tabora, aliweza kutembelea eneo la jengo linalojengwa Hospitali ya Wilaya ya Uyui na baadae aliweza kumalizia ziara yake katika Zahanati ya Isikizya ambapo aliagiza Mkurugenzi wa Wilaya ya Uyui kuhakikisha wanatenga bajeti pamoja na kushirikiana na nguvu za wananchi na mbunge wa jimbo hilo wanajenga majengo ya kulazwa wagonjwa, chumba cha upasuaji, maabara na miundombinu mingine ili Zahanati hiyo ije kupanda na kuwa Kituo cha Afya kwani kinahudumia eneo kubwa katika mji huo wa Isikizya ambayo hipo ndani ya Makao makuu ya Wilaya hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikaguachumba cha upasuaji Hospitali ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua Maabara ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikaguachumba cha upasuaji Hospitali ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo kwa viongozi wa Hospitali ya Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akiingia chumba cha Wodi ya wanawake kituo cha Afya Laela Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akielekea kukagua Maabara ya Kituo cha Afya Laela Mkoa wa Rukwa
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Saidi Mtanda akihutubia wakati Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla alipotembelea kituo cha Afya Wampembe Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua kitanda ndani ya chumba cha kujifungulia katika kituo cha Afya Wampembe Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akitembelea kituo cha Afya Wampembe, Mkoa wa Rukwa. kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Mh. Said Mtanda
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua mfumo wa maji unaoingia kituo cha Afya Wampembe, kutokea Ziwa Tanganyika, Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua chumba cha upasuaji mdogo cha Kituo cha Afya Nkasi alipotembelea hapo majira ya saa mbili usiku, Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua eneo litakalojengwa majengo ya utanuzi wa kituo hicho cha Afya ambapo kikikamilika kinatarajia kuwa Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akipatiwa maelezo ya maendeleo ya jengo linalojengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Uyui, Mkoani Tabora, kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini Mh. Almasi Maige
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua jengo litakalojengwa Hospitali ya Wilaya ya Uyui, Mkoani Tabora.
Jengo linaloendelea kujengwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Uyui
 
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akikagua ndani ya Maabara ya Kituo cha Afya Inyonga, Mlele, Mkoani Katavi
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mh. Dk.Hamisi Kigwangalla akisaini kitabu cha wageni Kituo cha Afya Inyonga, Mlele, Mkoani Katavi

IGP SIRRO AMALIZA ZIARA YAKE MKOANI KAGERA NA KUSISITIZA UWELEDI

$
0
0
Na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, amewataka askari wa Jeshi hilo kufanyakazi kwa weledi na kwa kuzingatia sheria na taratibu zitakazosaidia kujenga taswira chanya hasa wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.

IGP Sirro, ameyasema hayo alipokutana na kuzungumza na askari na maofisa wa mkoa wa Kagera, wakati akiwa kwenye muendelezo wa ziara zake zenye lengo la kujitambulisha pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo wakati wakitekeleza majukumu yao.

Alisema kuwa, kila askari analojukumu mbele yake la kuhakikisha suala la uhalifu na wahalifu linadhibitiwa hususan kwa kuimarisha usalama wa raia na mali zao huku wakizingatia kuwa, mkoa huo unapakana na nchi jirani za Uganda, Rwanda na Burundi.

Hata hivyo, katika ziara yake, IGP Sirro, amewahakikishia askari na maofisa kuwa, yupo tayari kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza na kuwataka askari kuongeza kasi ya kukabiliana na matishio ya kiuhalifu na wahalifu ili kuifanya jamii kuishi kwa amani na utulivu.

Aidha, katika ziara hiyo, masuala mbalimbali yamejadiliwa huku mbinu mpya za kukabiliana na uhalifu katika mkoa huo pamoja na wilaya zake zikiibuliwa kwa kuzingatia kuimarisha usalama wa raia na mali zao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (kushoto), akizungumza na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Kamishna Msaidizi Muandamizi wa Polisi (SACP) Augusine Ollomi, muda mfupi alipowasili, IGP Sirro yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kujitambulisha na kuzungumza na askari pamoja na kujua chamgamoto wanazokutananazo wakitekeleza majukumu yao. Picha na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi.

JPM KUWASILI TABORA JUMAPILI-RC TABORA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kesho tarehe 23 Julai 2017 ,anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili mkoani hapa kwa ajili ya uzinduzi wa miradi ya mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Ofisi kwake Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw. Aggrey Mwanri alisema Mhe. Rais Dkt.Magufuli atawasili mkoani Tabora akitokea Kigoma ambapo wanatarajia kumpokea katika Wilaya ya Kaliua siku ya Jumapili .

Alisema kuwa mara baada ya kuwasili Wilayani Kaliua kuzindua uzinduzi wa barabara kutoka Kaliua hadi Kazilambwa na baadaye atapata fursa ya kuwahutubia wananchi.

Bw. Mwanri aliongeza kuwa akiwa njiani kuelekea Tabora Mhe Rais Magufuli atazinduza barabara ya Urambo hadi Tabora siku hiyo hiyo na ambapo pia atawahutubia wakazi wa Urambo na kisha kuelekea Tabora.

Alisema kuwa siku ya Jumatatu Rais ataweka Jiwe la Msingi ujenzi wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuja katika miji ya Nzega , Igunga na Tabora na baadae kuzindua upanuzi na ukarabati wa njia za kurikia Ndege katika Uwanja wa Tabora.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora aliongeza kuwa siku hiyo hiyo ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atazindua barabara ya Tabora hadi Nzega na ile ya Tabora hadi Nyahua na mchana atawahutubia wakazi wa Tabora katika Viwanja vya Chipukizi.

Alisema ujio wa Rais Magufuli kwa wakazi wa Mkoa wa Tabora ni sawa na usemi usemao Mgeni Njoo Mwenyeji Apone kwani zara yake mkoani hapa inazidisha matumaini kwa wakazi wa Mkoa wa Tabora na jirani zake ya kuendelea kufunguka milango au fursa mbalimbali za uchumi baada ya kuzindua miradi mbalimbali ya miundo mbinu.

Bw. Mwanri alitoa wito kwa niaba ya wananchi wa Tabora kuwakaribisha wananchi kujotokeza kwa wingi kumlaki na kumsikiliza Rais Magufuli.
 
Na Tiganya Vincent-RS_TABORA
 

ZSSF Yatiliana Saini na Banki Tpb Bank Utowaji wa Mikopo Kwa Wanachama wa ZSSF Zanzibar.

$
0
0
MKURUGENZI Mkuu wa Tpb Bank Sabasaba Moshingi kushoto na Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Jamii Zanzibar (ZSSF) Makame Mwadini wakitiliana saini makubaliano ya kutowa mikopo ya Kielimu na Kuazia Maisha kwa Wanachama wa (ZSSF)hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa ZSSF kilimani Zanzibar, wakishuhudia Mwanasheria wa ZSSF Mohammed Fakih na Afisa Mawasiliano wa Tpb Bank Chichi Banda
Mkurgenzi Mkuu wa Tpb Bank Sabasaba Moshingi kushoto akibadilishana mikataba wa mikopo kwa Wanachama wa ZSSF kupata mikopo kupitia Banki ya Tpb Bank, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Mwadini Makame,  kuwawezesha kupata Mkopo wa Elimu ya Juu na kuaza maisha kwa Wanachama wa ZSSF, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Kilimani Zanzibar.wakiwa katika picha ya pamoja na Maofisa wa pande hizo mbili.
Maofisa wa Tpb Bank wakifuatilia mkutano huo wa utilianaji saini ya kutowa mikopo kwa Wanachama wa ZSSF Zanzibar kupitia benki hiyo hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi za ZSSF Kilimani Zanzibar.
Maofisa wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF wakifuatila mkutano huo wa utilianaji wa saini.
Afisa Mawasiliano wa Tpb Bank Chichi Banda akitowa nafasi kwa waandishi wa habari kuuliza maswali wakati wa hafla hiyo.
Mkurgenzi Mkuu wa Tpb Bank Sabasaba Moshingi, akizungumza wakati wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini kuelezea madhumuri ya hafla hiyo kuwanufaisha Wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar kupata mikopo kupitia Banki yake Tpb Bank. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Mwadini Makame
akizungumza wakati wa hafla hiyo ya makubaliani ya kupata mikopo kwa Wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF, kupitia Banki ya Tpb Bank.
Maofisa wa Tpb Bank wakifuatilia hafla hiyo ya utilianaji wa saini na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF. 
Mwandishi wa habari akiulisa swali wakati wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini baina ya ZSSF na Tpb Bank, kutowa mikopo kwa Wanachama wa ZSSF kupata Elimu ya Juu na Mkopo wa kuazia maisha. 
Mwandishi wa habari akiuliza swali wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi Mikopo wa Banki ya Tpb Bank Ndg. Henry Bwogi akifafanua na kujibu maswali yalioulizwa na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo ya utilianaji wa saini baina ya pande hizo mbili. 
Afisa Masoko na Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF Bi Raya Hamad Khamis akitowa shukrani kwa washiriki wa hafla hiyo ya utilianaji wa saini uliofanyika katika Ofisi za Jengo la ZSSF Kilimani Zanzibar. 
Viongozi wa Tpb Bank na ZSSF wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa hafla hiyo. 
Mkurugenzi wa Banki ya Tpb Bank Sabasaba Moshingi akiwa na Maofisa wa ZSSF wakibalishana mawazo baada ya kumaliza hafla ya utilianaji wa saini na ZSSF, katikati Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZSSF Ndg.Mwadini na Afisa wa ZSSF Miradi Ndg. Muumin.
Mkurugenzi wa Banki ya Tpb Bank Sabasaba Moshingi akisalimiana na Afisa wa ZSSF Ndg Filifili. 

Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.com
Zanzinews.com.

ONYO KALI KWA WAUZA PEMBEJEO FEKI, HATUA KALI ZITACHUKULIWA KWA WATAKAOBAINIKA.

$
0
0
Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida Beatus Chowaji akisoma bango mara baaa ya kuzindua mradi wa Faida Mali unaoshirikiana na shirika la AMDT katika kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida.

Mkurugenzi wa Shirika la AMDT Michael Kayombo akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa Faida Mali wenye lengo la kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida kulima kibiashara.

Baadhi ya wadau waliohudhuruia uzinduzi wa mradi wa Faida Mali wenye lengo la kuwasaidia wakulima wa Alizeti Singida kulima kibiashara.

Mkurugenzi wa mradi wa Faida Mali mkoa wa Singida Tom Silayo akisoma taarifa ya mradi huo kwa wajumbe waliohudhuria uzinduzi wa mradi utakaowasaidia wakulima kulima alizeti kibiashara.

Mtendaji Mkuu wa Chama cha wasindikaji wa Mbegu za alizeti Tanzania Daud Musa Mwasantaja akiwahakikishia wakulima wa alizeti upatikanaji wa soko katika uzinduzi wa Mradi wa Faida Mali.

……………………………………………………………………….

Wauzaji wa pembejeo ambao sio waaminifu wamepewa onyo kali na endapo atabainika yeyote anayewalaghai wakulima na kuwauzia pembejeo ambazo sio hali hatua kali dhidi yake zitachukuliwa.

Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida Beatus Chowaji ametoa onyo hilo wakati akizindua mradi wa Faida Mali unaoshirikiana na shirika la AMDT katika kuwasaidia wakulima wa alizeti Mkoani Singida ili kulima zao hilo kibiashara zaidi.

Chowaji amesema kumekuwepo na malalamiko kwa baadhi ya wakulima ambao hukumbana na wauzaji wa pembejeo ambao sio waaminifu na kuwalaghai kwakuwa wakulima hao hawana elimu na uelewa hasa wa viuatilifu au mbegu ambazo ni halisi.

Ameongeza kuwa mkono wa serikali ni merfu na utawabaini popote walipo hivyo waache mara moja kwani kwa kufanya hivyo wanakirudisha nyuma kilimo cha alizeti ambacho ni tegemeo kwa ajili ya uchumi wa viwanda Mkoani Singida.

“Singida tuna Viwanda vya kuamua mafuta ya alizeti vikubwa viwili, vya kati vitatu na vidogo 115 na kufanya jumla ya viwanda vya alizeti kuwa 120, vyote hivyo vinategemea alizeti ya mkulima, lakini pia mkulima anakuwa na matarajioa makubwa, hao wauzaji pembejeo wasio waaminifu hatutawavumilia, tena waache mara moja”, amesisitiza Chowaji.


Aidha amelipongeza shirika la AMDT kupitia mradi wa Faida mali kwa kuuchagua Mkoa wa Singida ili kuboresha kilimo cha alizeti hasa kwa ajili ya mkulima mdogo.

Chowaji amesema viwanda vya alizeti Mkoani Singida hufanya kazi kwa miezi minane kwa mwaka badala ya mwaka mzima kutokana na kuwa alizeti inayozalisha bado haitosheleshi viwanda hivyo kufanya kazi mwaka mzima.

Amesema matumaini makubwa ya serikali mkoani hapa ni kuwa mradi huo utasaidia kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili kuifanya Singida ya Viwanda kuwa bora zaidi pamoja na kuliboresha zao lenyewe la alizeti kwa kutumia pembejeo za kisasa zaidi.

Chowaji amewataka wakulima wote wa alizeti kuchangamkia fursa hiyo kwa kujiunga katika vikundi ili waweze kufikiwa kwa urahisi na kunufaika, pia waache kilimo cha mazoea kwakuwa alizeti ni biashara kubwa ambayo itawakomboa kiuchumi na kukupa pato la mkoa wa Singida.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la AMDT Michael Kayombo amesema shirika hilo kupitia Mradi wa Faida mali utahakikisha unasaidia upatikanaji wa mikopo kwa wakulima wadogo wa alizeti Mkoani singida.


Kayombo ameongeza kuwa mradi utaboresha huduma za ugani kwa kutoa taarifa sahihi na mapema juu ya kilimo cha alizeti kwa wakulima na taarifa hizo zitatolewa kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno hivyo kuwafikia mapema.

Amreongeza kuwa watahakikisha wakulima wanapata soko la uhakika la zao hilo ndani na nje ya mkoa wa singida pamoja na kuhakikisha bei ya zao hilo ni yenye kumnufaisha mkulima na sio kumdidimiza zaidi.

Naye Mtendaji Mkuu wa Chama cha wasindikaji wa Mbegu za alizeti Tanzania Daud Musa Mwasantaja amesema viwanda vya alizeti bado vina uhitaji mkubwa wa alizeti kwa kuwa viwanda vyao vimekuwa vikiendeshwa chini ya malengo kutokana na mbegu hizo kuwa chache.

Mwasantaja amesema wana imani kuwa mraadi wa Faida Mali utasaidia kuongeza uzalishaji wa alizeti hivyo kuwasaidia kuongeza pia uzalishaji katika viwanda vyao.

Ameongeza kuwa watatoa ushirikiano wa kutosha na hivyo wakulima wasiwe na wasiwasi walime zao hilo kwa wingi watapata wateja na kwa bei ambayo ni nzuri.

Nao wakulima walioshiriki uzinduzi wa maradi huo wamesema mradi huo umekuja muda muafaka kwakuwa na wao wanatamani kupata faida kutokana na kilimo hicho kwakuwa baadhi bado wanalima kwa mazoea na kwa kutumia mbegu ambazo hazizalishi kwa wingi.

TAZAMA LIVE: Rais Magufuli Akiwahutubia Wananchi Uwanja wa Lake Victoria Kigoma

WATANZANIA NA WAZAMBIA WAUNGANA PAMOJA WASHEREKEA USIKU WA TAMASHA LA CASTLE LITE UNLOCKS JIJINI DAR

$
0
0
Pichani ni WATANZANIA alioungana na WAZAMBIA kusherekea usiku wa CASTLE LITE UNLOCKS party iliyofanyika jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuelekea kwenye tamsaha kubwa linalotarajia kufanyika leo Julai 22, 2017 viwanja vya Leaders Club na kuwakutanisha wasanii toka mataifa mbali mbali. Wasanii watakaopamba tamasha hilo ni Diamond Platnumz, Casper Nyovest Kutoka Afrika kusini, Vanessa Mdee, kundi la Weusi na Navy Kenzo ambao ni wa hapa hapa nchini Tanzania.
WAZAMBIA wakisherekea shangwe za CASTLE LITE UNLOCKS party iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Wazambia wameingia nchini kwa udhamini wa bia ya Castle Lite kuja kuhudhuria tamasha kubwa 
Shangwe zikiendelea.
Wazambia wakisherekea utamu wa Castle Lite.
Brand Manager wa Castle Lite, Isaria Kilewo akitoa salamu za shukrani kwa WATANZANIA na WAZAMBIA waliodhuria kusherekea usiku wa CASTLE LITE UNLOCKS party iliyofanyika jijini Dar es Salaam 
Kila mmoja alishow love...
Msosi nao ulikuwa wa kutoshaaaa...

Serikali Yapongezwa kwa Kuwaleta Pamoja wadau wa Mazingira na Wazalishaji Mifuko ya Plastiki

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais,Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akifungua Kikao cha Wazi cha kupokea maoni ya wadau kuhusu dhamira ya Serikali kupiga marufuku uzalishaji,uuzaji,usambazaji na matumizi ya mifuko ya plastiki leo Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Prof. Faustine Kamuzora akiongea wakati wa ufunguzi wa Kikao hicho leo Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais,Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba.

Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi akiongea wakati wa Kikao hicho mapema leo.

Mwenyekiti wa Umoja wa wazalishaji wa mifuko isiyo na athari kwa mazingira Bw. Jumanne Mgude akionesha mfuko unaozalishwa hapa nchini usio na athari kwa mazingira wakati wa Kongamano hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Wande Printing and Packaging (T) Ltd Bw. Joseph Wasonga akitoa maoni ya wamiliki wa Viwanda vya Kuzalisha mifuko ya plastiki hapa nchini wakati wa kikao hicho.

Katibu wa Umoja wa wazalishaji wa mifuko isiyo na athari kwa mazingira Bw. Sadick Mgonge akitoa maoni ya umoja huo wakati wa Kikao hicho leo.

Sehemu ya wadau walioshiriki kikao hicho leo Jijini Dar es Salaam wakifuatilia mjadala na maoni ya washiriki .(Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo)


Frank Mvungi-Maelezo

Wadau wa Mazingira na Wazalishaji wa Mifuko ya Plastiki hapa nchini wameipongeza Serikali kwa kuwakutanisha pamoja ili kujadili kuhusu matumizi ya mifuko ya plastiki na kutoa maoni yao kwa Serikali juu ya kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira.

Akizungumza wakati akifungua kikao cha wazi cha kupokea maoni ya wadau kuhusu dhamira ya Serikali kupiga marufuku uzalishaji, uuzaji, usambazaji na matumizi ya mifuko ya plastiki, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amesema dhamira ya Serikali ni kupata maoni ya wadau na wazalishaji wa mifuko hiyo ili Serikali ifanye tathmini kabla ya kuchukua hatua na kuweka mazingira yatakayowezesha utekelezaji wa Sheria ya Mazingira kwa kila mdau.

“Changamoto imekuwa kubwa katika matumizi ya mifuko ya plastiki katika swala la mazingira kwani tumeshuhudia miundo mbinu yetu ikiathirika, mifugo na hata viumbe vya baharini na kwa mujibu wa tafiti kuna hatari baadae mifuko hii ikawa mingi zaidi baharini kuliko samaki” Alisisitiza Makamba.

Akifafanua Makamba amesema kuwa Serikali imeona ni vyema ikakutana na wadau ili ipate maoni yao kwa kuzingatia kifungu cha 178 cha Sheria ya Mazingira kinachotaka wananchi na wadau kushirikishwa na kupata taarifa kuhusu maswala ya mazingira.

Aliongeza kuwa kuanzia sasa Ofisi yake itakuwa ikishirikiana na wadau katika mambo yote yanayohusu mazingira ili kuongeza tija na kutoa fursa kwa wadau hao kutoa maoni yatakayosaidia katika usimamizi wa Sheria na Kanuni.Naamini kutakuwa na kuvumiliana wakati wa kutoa maoni ili Serikali ipate maoni ya wadau wote kwa ufasaha na hii itasaidia Serikali katika kuchukua hatua ikiwemo kuhakikisha kuwa kuna usimamizi dhabiti wa Sheria ya Mazingira.

Pia Waziri Makamba alilitaka Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kusimamia Sheria ya Mazingira kikamilifu ili kulinda rasilimali za Taifa.Kwa upande wake Naibu Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Plastiki Tanzania Bw. Ahmed Abdallah amepongeza utaratibu huo wa Serikali kukutana na wadau.

Kumekuwa na maoni mbalimbali kuhusu matumizi ya mifuko ya plastiki huku baadhi ya wadau wakidai imekuwa na athari kubwa katika mazingira zikiwemo magonjwa, uharibifu wa miundo mbinu na kuleta mabadiliko ya tabia nchi .

WAZIRI UMMY AZINDUA ZAHANATI NGUVUMALI JIJINI TANGA

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katika akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Zahanati ya Kata ta Nguvumali leo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa na wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Said. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katika akisisitiza jambo kwa Muuguzi wa Afya wa Zahanati ya Nguvumali baada ya kuizindua kushoto ni Mganga Mfawidhi wa Zahanati hiyo,Dkt Ally Bughe 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akizungumza katika uzinduzi huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa na kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nguvumali na wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga(CUF)Alhaj Mussa Mbaruku 
Mbunge wa Jimbo la Tanga(CUF)Alhaj Mussa Mbaruku akizungumza katika halfa hiyo 
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nguvumali akizungumza katika hadhara hiyo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga,Alhaj Mussa Mbaruku 
Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudi Mayeji akizungumza katika halfa hiyo 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akisalimiana na madiwani wa Jiji la Tanga mara baada ya kuwasili katika zahanati hiyo kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapa Selebosi
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kushoto katikati ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi kulia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akipanda mti wa kumbukumbu mara baada ya kuzindua zahanati hiyo leo
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa Mbaruku akipanda mti kwenye zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa na Waziri Ummy. 
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali Jijini Tanga wakifuatilia uzinduzi huo
Waheshimiwa madiwani kutoka Kata mbalimbali Jijini Tanga wakifuatilia uzinduzi huo
Wananchi wakifuatilia uzinduzi huo 
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali Jijini Tanga wakifuatilia uzinduzi huo
Msanii wa maigizo mkoani Tanga ,Dkt Njau akionyesha umahiri wake katika uzinduzi huo

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

VYUO NA VYUO VIKUU-UVCCM WAMKINGIA KIFUA RAIS.DK MAGUFULI

$
0
0
Na Nassir Bakari

Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), kupitia Idara yake ya Vyuo na Vyuo vya Elimu ya Juu, umemkingia kifua Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. John Magufuli ukisema kwamba hafanyi uteuzi kwa njia za kibaguzi bali anafanya hivyo kwa kuzingatia weledi na uwezo wa anayemteua.

UVCCM imesema, hayo leo jijini Dar es Salaam, na kupinga vikali kauli iliyotolewa hivi karibuni na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, kwamba Rais Dk. Magufuli amekuwa akifanya uteuzi kwa kuzingatia ubaguzi wa ukanda, ukabila, dini na jinisa.

Akifungua Kikao cha kazi cha Viongozi wa Vyuo na Vyuo vikuu mkoa wa Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu- UVCCM, Daniel Zenda alisema, UVCCM kupitia Idaya yake, inapinga na kulaani vikali kauli hizo za Tundu Lissu kwa sababu ni kauli za hatarai kwa kuwa zina lengo la uchochezi, kudhalilisha na kugawa Wananchi kwa misingi ya kibaguzi.

"Ndugu Watanzania kauli hii ya Tundu Lissu ni yenye lengo la kuchonganisha, kudhalilisha na kuwagawa wananchi, Sisi Vjana wa Vyuo na vyuo Vikuu, tunalaani kwa nguvu zetu zetu kauli hii. Kwa mfano ukitazama uteuzi wa Mkuu wa Majeshi nchini anatoka Bara, lakini hupo chini ya Waziri wa Ulinzi Dk. HusseinMwinyi ambaye anatoka Zanzibar", sasa hapo ubaguzi unakujaje", alisema na kuhoji.

Alisema, kimsingi katika kufanya uteuzi, Rais anazingatia haki yake ya kikatiba ambayo inampa mamlaka ya kuteua na kutengua kwa kadri anavyoona inafaa. "ibara ya 36 kifungu cha pili ambayo kinasema Rais atakuwa na madaraka ya kuteua watu wa kushika nafasi za madaraka ya viongozi wanaowajibika kuweka sera za idara za taasisi za Serikali na watendaji wakuu wanaowajibika kusimamia utekelezaji wa sera za idara hizo", alifafanua.

"Mnajua siasa ni kama dawa, dawa huwa inaisha muda wake, sasa huyu Tundu Lissu naye amekwisha muda wake kisiasa, ndiyo maana inafika wakati anazungumza maneno ya kipuuzi katika jamii, nawaomba ndugu Watanzania wenzangu tuyapuuze maneno yake, hayana maana, Ndugu Wananchi wa Singida Mashariki tunawaomba 2020 msifanye makosa tena tuleteeni anayefaa kuliko huyu Tundu Lissu", alisema Zenda.

Alisema, kuisha kisiasa kwa Tundu Lisu na upinzani kwa jumla, kunatokana na uchapakazi ulioonyeshwa na uongozi wa awamu ya tano, chini ya Rais Dk. Magufuli. " Hawa kina Tundu Lisu kwa sasa hawana hoja, ndiyo maana sasa wanatapatapa kujaribu kutafuta pa kushika.

"Sisi kama vijana wasomi tunaiunga mkono Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. Magufuli kwa mambo yote inayoyafanya, Watanzania wenyewe tumekuwa ni mashahidi wazuri wa hayo mambo, tunaomba Mungu ampe afya njema ili aendelee kututumikia Watanzania" alisema Zenda.

Kaimu Katibu Mkuu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu-UVCCM Daniel Zenda akizungumza wakati wa kikao cha kazi na viongozi wa Vyuo na Vyuo Vikuu mkoa wa Dar es Salaam, leo .


Kaimu Katibu Mkuu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu-UVCCM Daniel Zenda (kulia) akiongoza kikao cha Kazi cha Viongozi wa Vyuo na Vyuo Vikuu-UVCCM mkoa wa Dar es Salaam, leo katika ukumbi wa jengo la Makao Makuu ya UVCCM jijini Dar s Salaam. PICHA NA BASHIR NKOROMO

SH. BILIONI 1.669 KUTEKELEZA MIRADI YA MAJI ILEJE-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga sh. bilioni 1.669 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji katika wilaya ya Ileje mkoani Songwe.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Julai 22, 2017) wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Ileje katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Itumba.

Waziri Mkuu amesema kati ya fedha hizo sh. bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji katika miji miwili ya Isongole na Itumba wilayani Ileje.“Kiasi kingine cha sh. milioni 669 kimetengwa kwa ajili ya maji katika vijiji mbalimbali vya wilaya ya Ileje katika mwaka wa fedha wa 2017/2018.

Hata hivyo, amesema Serikali inaendelea na utekelezaji wa Kampeni ya Rais Dkt. Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani kwa kusogeza huduma ya maji kwa urahisi.Waziri Mkuu amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400.

Wakati huo huo Waziri Mkuu ameiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Songwe kuhakikisha inaimarisha ulinzi katika maeneo ya mipaka.Amesema kamati hiyo inatakiwa kuimarisha ulinzi katika maeneo yote ya mipaka ili kuizua wageni kuingia bila ya kufuata taratibu zilizowekwa kisheria.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Bw. Joseph Mkude alisema katika kipindi cha Julai 2016 hadi Juni 2017 jumla ya wahamiaji haramu 38 walikamatwa kwenye wilaya hiyo.Alisema kati ya wahamiaji hao haramu 36 ni raia wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na wawili walikua raia wa Malawi na wote walirudishwa makwao.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, JULAI 22, 2017.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Ileje baada ya kuwasili kwenye makazi ya Mkuu wa wilaya hiyo  akiwa katika ziara ya mkoa wa Songwe Julai 22, 2017.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wabunge Janet Mbene wa Ileje (kulia) na Juliana Shonza wa Viti Maalum baada ya kuwasili kwenye makazi ya Mkuu wa wilaya ya Ileje kuanza ziara wialyani humo Februari 22, 2017. (Picha na ofisi ya Wziri Mkuu). 
 Baadhi ya watumishi wa umma, viongozi wa dini na taasisi binafsi wakimsikiliza  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao mjini Ileje Julai 22, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa umma, viongozi wa dini na viongozi wa taasisi binafsi mjini Ileje Julai 22, 2017. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa jengo la hospitali ya wilaya ya Ileje akiwa katika ziara ya mkoa wa Songwe, Julai 22, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary  (kushoto) wakitazama mbegu za mahindi zinazozalishwa na Kikundi cha SAM cha Ileje wakati alipotembelea banda la kikundi hicho kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye stendi ya mabasi ya Ileje Julai 22, 2017
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama vifaranga wa samaki wakati alipotembelea banda la Kikundi cha wanawake cha Tukazane cha Ileje  kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye stendi ya mabasi ya Ileje Julai 22, 2017.

ANAPAMBANA NA HALI YAKE,HAONI UMUHIMU WA USALAMA WAKE

Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images