Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

TANZANIA YASHIKA NAFASI YA TATU AFRIKA KWA SHERIA BORA YA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA KEMIKALI

$
0
0
 Mkemia Mkuu wa Serikali Prof. Samwel Manyele akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu Tanzania kushika nafasi ya tatu barani Afrika kwa kuwa na Sheria bora ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali hali iliyopelekea Taasisi hiyo kuwa moja ya Taasisi bora zenye maabara ya kisasa.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma ya Ubora wa Bidhaa, Daniel Ndiyo na kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Biashara, George Kasinga.
 Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma ya Ubora wa Bidhaa, Daniel Ndiyo akiwaeleza waandishi wa habari umuhimu wa wananchi kupata taarifa na maamuzi ya mkutano wa Kimataifa kuhusu Udhibiti wa kemikali na kemikali taka uliofanyika hivi karibuni  Geneva, Uswisi kuanzia Aprili 24 hadi Mei 5 mwaka huu.
Meneja wa Kanda ya Kaskazini GCLA, Christopher Anyango akifafanua kuhusu mkakati wa Serikali kuwajengea uwezo wananchi kuelewa madhara yatokanayo na kemikali ambazo zimepigwa marufuku. (Picha na Frank Mvungi-Maelezo)

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Tanzania imeshika nafasi ya tatu barani Afrika ikiongozwa na nchi ya Afrika Kusini na Nigeria kwa kuwa na Sheria bora ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Prof. Samweli Manyele alipokua akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkutano wa Kimataifa wa Udhibiti wa Kemikali na Kemikali Taka uliofanyika Geneva, Uswisi kuanzia Aprili 24 hadi Mei 5 mwaka huu.

Prof. Manyele amesema kuwa katika Bara la Afrika Tanzania ndio nchi pekee ambayo ina taasisi ya Serikali inayosimamia kemikali wakati nchi zingine usimamizi wa masuala ya kemikali upo katika taasisi za mazingira kitu ambacho kinapelekea usimamizi hafifu wa kemikali hizo.

“Tanzania ni nchi pekee Afrika ambayo taasisi inayohusika na masuala ya kemikali ipo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na pia ni taasisi yenye kusimamiwa na wataalamu wa kemikali waliobobea pamoja na kuwa na maabara kubwa inayojulikana kimataifa,”alisema Prof. Manyele.

Akiongelea kuhusu mkutano huo, Prof. Manyele amesema kushiriki katika mkutano huo ni jambo la kisheria hivyo kupeleka watumishi watatu kutoka kwenye taasisi hiyo inadhihirisha kuwa Tanzania imetimiza majukumu yake kama Taifa.

Amefafanua kuwa mkutano huo unaisaidia taasisi kutoa taarifa kuhusu utendaji kazi, kujifunza nchi zingine wanafanyaje kazi zao, kupata majibu ya moja kwa moja pamoja na kujadiliana namna ambavyo wataboresha utendaji kazi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma ya Ubora wa Bidhaa, Daniel Ndiyo ametaja wadau wanaotakiwa kupata taarifa na maamuzi ya mkutano huo kuwa ni wafanyabiashara, watumiaji wa kemikali hizo pamoja na mamlaka mbali mbali za usimamizi wa kemikali. 

Naye Meneja wa Kanda ya Kaskazini GCLA , Christopher Anyango amesema mkutano huo unawasaidia wananchi kupata msaada wa haraka kutoka katika Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kuwa wana uelewa pamoja na kupata mafunzo ya kemikali zinazoruhusiwa na zisizoruhusiwa kulingana na mahitaji kwa wakati husika.

Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilishiriki katika mkutano huo wa utekelezaji wa mikataba mitatu ikiwemo ya usafirishaji wa taka sumu kimataifa (Basel), mkataba unaohusu kemikali zenye madhara na zinazochukua muda mrefu kuoza katika mazingira (Stockholm) pamoja na mkataba wa Rotterdam unaohusu upashanaji taarifa juu ya kemikali hatari na viuatilifu katika biashara ya kimataifa.

WAZIRI WA FEDHA ZANZIBAR AZUNGUMZA NA WAANDISHI LEO.

$
0
0
 Waziri wa Fedha Zanzibar Dk Khalid Salum Mohd akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mipango Mapendekezo ya Bajeti (Mapato na matumizi) ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017-2018.Katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Vuga Mjini Unguja.
 Mwandishi wa Habari wa Hits Fm Jazaa Kombo katikati akiuliza maswali kwa Waziri wa Fedha Zanzibar Dk Khalid Salum Mohd  alipozungumza na Waandishi kuhusiana na Mipango Mapendekezo ya Bajeti (Mapato na matumizi) ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017-2018.Katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Vuga Mjini Unguja.
 Mwandishi wa Habari wa Habari Leo Khatib Suleiman akiuliza maswali kwa Waziri wa Fedha Zanzibar Dk Khalid Salum Mohd  alipozungumza na Waandishi kuhusiana na Mipango Mapendekezo ya Bajeti (Mapato na matumizi) ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017-2018.Katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Vuga Mjini Unguja.
Waziri wa Fedha Zanzibar Dk Khalid Salum Mohd akifafanua jambo kwa  Waandishi wa Habari kuhusiana na Mipango Mapendekezo ya Bajeti (Mapato na matumizi) ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017-2018.Katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Vuga Mjini Unguja.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari waliohudhuria katika mkutano wa waandishi wa habari na  Waziri wa Fedha Zanzibar Dk Khalid Salum Mohd kuhusiana na Mipango Mapendekezo ya Bajeti (Mapato na matumizi) ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017-2018.Katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha Vuga Mjini Unguja.


PICHA NA YUSSUF SIMAI /MAELEZO ZANZIBAR.

MAKAMU WA RAIS AWATEMBELEA MAJERUHI WA AJALI YA KARATU HOSPITALI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali  Sadia Isamel Awadhi mwenye umri wa miaka 11 ambaye ni mmoja wa majeruhi waliolazwa kwenye hospitali mkoa wa  wa Arusha ya Mt. Meru, Sadia ni mmoja ya waliojeruhiwa katika ajali waliopata wanafunzi wa Lucky Vincent (Picha na Ofisi ya Maku wa Rais)
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali  Godfrey Tarimo mwenye umri wa miaka 11 ambaye ni mmoja wa majeruhi waliolazwa kwenye hospitali mkoa wa  wa Arusha ya Mt. Meru, Godfrey ni mmoja ya waliojeruhiwa katika ajali waliopata wanafunzi wa Lucky Vincent (Picha na Ofisi ya Maku wa Rais)
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali  Doreen Mshana mwenye umri wa miaka 13ambaye ni mmoja wa majeruhi waliolazwa kwenye hospitali mkoa wa  wa Arusha ya Mt. Meru, Doreen ni mmoja ya waliojeruhiwa katika ajali waliopata wanafunzi wa Lucky Vincent (Picha na Ofisi ya Maku wa Rais)

KIJANA GIRL GUIDES APAMBANA MEXICO KUWA MLIMA KILIMANJARO UPO TANZANIA BADALA YA KENYA

$
0
0
 Mmoja wa viongozi wa vijana wa Chama cha  Tanzania Girl Guides  (TGGA), Dk. Helga Mutasingwa (kulia), akilakiwa na Katibu wa Taifa wa TGGA, Grace Shaba baada ya kuwasili jana kwenye Uwanja wa wa Kimataifa wa  Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam jana. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)


Na Richard Mwaikenda 
KIONGOZI wa Vijana wa Chama cha  Tanzania Girl Guides  (TGGA), Dk. Helga Mutasingwa amefanya kazi kubwa ya kuwashawishi Wananchi wa Mexico kuwa Mlima Kilimanjaro upo Tanzania badala Kenya.

Dk. Mutasingwa ambaye alikuwa nchini Mexico kwa mafunzo ya miezi minne ya kubadilishana uzoefu katika nyanja za utamaduni na  uongozi alitumia fursa hiyo kutangaza vivutio vya Tanzania.

Akizungumza  mara baada ya kuwasili jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, alisema kuwa moja ya mambo yaliyompa wakati mgumu ni kuwabadilisha wamexico kuwa Mlima Kilimanjaro upo Tanzania na si Kenya kama wanavyofahamu wao.

Alisema Wamexico wengi kwanza wanajua Afrika ni nchi, jambo ambalo pia ilibidi awaeleze kuwa  siyo nchi bali ni bara kama yalivyo mabara mengine duniani na katika bara hilo kuna nchi nyingi na mojawapo ni Tanzania anayotokea yeye.

Alisema akiwa huko licha ya kuwafundisha kiswahili pia alitangaza vivutio vingi  vya utalii vilivyopo nchini, ambapo aliwatajia wadudu, ndege za kila aina na  wanyama mbalimbali waliomo kwenye hifadhi za Serengeti, Ngorongoro Crater na nyinginezo.

Pia aliwafundisha kuhusu utamaduni wa Tanzania zikiwemo ngoma za asili, upikaji wa vyakula vya kitanzania kama vile ndizi na pilau, mambo ambayo walifurahishwa nayo.

Dk. Mutasingwa alisema kuwa ambaye katika ziara hiyo ya mafunzo alikuwa na vijana wenzie wa Girl Guids kutoka Venezuela,  Canada, Uingereza  na Argentina alipata wasaa wa kujifunza utamaduni wa mexico na kutoka nchi hizo zingine.

Alisema kuwa alijifunza mambo mengi ikiwemo ujasiri wa kufanya kazi bila woga, siasa za mataifa mbalimbali,  mambo ambayo ameahidi kuwafundisha vijana wenzie wa TGGA hapa nchini.

Dk. Mutasingwa aliwasili nchini jana, ambapo kwenye Uwanja wa Ndege wa JNIA, alilakiwa na Katibu wa Kitaifa wa TGGA, Grace Shaba pamoja na wanachama wenzie Elieshupendo Michael na Maryrehema Kijazi.





 Dk. Mutasingwa akiwa na Katibu wa TTA Taifa, Grace Shaba (kushoto), Elieshupendo Michael na Maryrehema Kijazi baada ya kulakiwa akitokea Mexico
Dk. Mutasingwa akifurahia jambo na  Elieshupendo Michael na Maryrehema Kijazi.
 Dk Mutasingwa akikumbatiana kwa furaha na Maryrehema Kijazi
 Ni furaha iliyoje kukutana
  Dk. Mutasingwa akifurahi wakati akilakiwa na Elieshupendo Michael
Grce Shaba na Dk. Mutasingwa wakiwa na furaha

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

SHIRIKA LA POSTA LATOA POLE KWA WAFIWA MSIBA WA WANAFUNZI WA SHULE YA LUCKY VICENT JIJINI ARUSHA

Benki Kuu ya Tanzania imesimamisha shughuli zote za FBME Bank Ltd, imefuta leseni yake ya kufanya shughuli za kibenki na kuiweka chini ya ufilisi

Tahadhari ya matapeli-wizara ya afya


uzinduzi wa ujenzi wa madrasa Mujahirina,Ukonga Jijini Dar es salaam

$
0
0
Mstahiki Meya  wa Jiji la Dar es salaam, Isaya Mwita (kulia) akiwa meza kuu, kushoto ni Diwani wa Kata ya Ukonga, Juma Mwipopo, wakiwa meza kuu tayari kwa kuanza kwa hafla hiyo mara baada ya kutoka katika dua iliyoandaliwa na Shekh Abdul Hamid ikiashiria kuanza salama na kumaliza salama jana.
Inline image 1

Inline image 2
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam, Mh:  Isaya Mwita, akiambatana na viongozi wa dini wakielekea katika uzinduzi wa  ujenzi wa madrasa Mujahirina uliopo mtaa wa Mongolandege kata ya Ukonga Jijini Dar es salaam jana , ambapo ujenzi huo ulifanikishwa kwa kiasi kikubwa na  nguvu ya wazazi  wakishirikiana na viongozi wa dini katika mtaa huo.
Inline image 3
Mstahiki  Mstahiki Meya Isaya Mwita (aliye vaa koti jeusi) , akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo hilo umekamilika,Inline image 4
Mstahiki  Meya wa Jiji la Dar es salaam, Isaya Mwita, akizungumza na waandishi wa habari jana katika uzinduzi wa Madrasa Mujahirina, uliopo Kata ya Ukonga, mtaa wa Mongo la Ndege huku akafafanua  kuhusiana na mtazamo  walionao Serikali kataika kusaidia maendeleo ya dini hapa nchini ili kujenga uhusiano wa kukuza amani pamoja maadili mema kwa kizazi cha Tanzania na hatimaye kufanikisha malengo yetu na Serikali kwa ujumla,
Inline image 5
Mstahiki  Viongozi wa dini pamoja na waratibu wa maonesho ya Madrasa, na wadau mbalimbali wa maswala ya elimu ya dini, wakiwa pamoja na Meya wa Jiji la Dar es salaam, Isaya Mwita (wa tatu kutoka kulia) wakiwa ndani ya jengo la Madrasa Muhajirina,  wakati wa dua maalumu  iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Rahma Foundation, Shekh Abdul Hamidi.
Inline image 6
 picha 67 . Meya Isaya (wa tatu kutoka kulia ) pamoja na Viongozi wa dini wakijiandaa kutoka ndani ya chumba cha Madrasa hiyo mara baada ya dua mahususi iliyosomwa na Shekh Abdul Hamidi kwa ajili ya uzinduzi wa Madrasa Mujahirina  kumalizka.
Inline image 7
. Mstahiki Meya Isaya (katikati mwenye koti jeusi) , akisalimiana  na baadhi ya  Viongozi wa dini, waratibu wa maonesho ya Quruan katika Madrasa Mujahirina jana  mara baada ya dua kukamilika
Inline image 8
Mstahiki  Meya Isaya Mwita (kushoto) wakielekea katika meza kuu mara baada ya kukamilika kwa dua
Inline image 9
Mstahiki Meya  wa Jiji la Dar es salaam, Isaya Mwita (kulia) akiwa meza kuu, kushoto ni Diwani wa Kata ya Ukonga, Juma Mwipopo, wakiwa meza kuu tayari kwa kuanza kwa hafla hiyo mara baada ya kutoka katika dua iliyoandaliwa na Shekh Abdul Hamid ikiashiria kuanza salama na kumaliza salama jana.
Inline image 10
NA CHRISTINA MWAGALA, OFISI YA MEYA WA JIJI.

Meya  Mwita alitoakauli hiyo mwishoni mwa wiki Meya Mwita alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki katika uzinduzi Madrasat Muhajiriina ambapo pamoja na mambo mengine alisema kwamba ili kujenga Taifa lenye viongozi wadilifu , wazazi hawana budi kuwajenga kwenye misngi ya elimu ya dini ,elimu dunia.

...............................................
MEYA wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amechangia shilingi milioni 1.5 na mifuko 100 ya simenti kwa ajili ya ujenzi wa Madrasat ya Muhajiriina iliyopo Gombo la Mboto katika halmashauri ya Manispaa ya Ilala. 
            
Aidha Meya amewataka wazazi kulea watoto katika misingi ya kidini ili kutengeza Taifa lenye viongozi walio wadilifu, wachamungu na wenye hofu ya mungu.

Meya Mwita alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki katika uzinduzi Madrasat Muhajiriina ambapo pamoja na mambo mengine alisema kwamba ili kujenga Taifa lenye viongozi wadilifu , wazazi hawana budi kuwajenga watoto kwenye misngi ya elimu ya dini na elimu dunia.

Alifafanua kwamba wazazi hususani wa kina mama ndio ambao wanatakiwa kuwaangalizi zaidi  watoto wao, kutokana na  muda mwingi hukaa nao karibu.

Alisema   kuwa muda huo ambao hukaa na watoto wao, wautumie sio kufundisha mambo ya nyumbani tu, lakini pia hata kwenye  misingi ya kimaadili ya kidini.

“ Mtatengeneza Taifa baya kama wazazi mtashindwa kuwaeleza watoto wenu mambo muhimu yenye maadili yanayofuatana na misingi ya dini, leo hii hapa tunaona watoto mmewavisha mavazi mazuri yenye heshima, lakini mkifika nyumbani mnawavalisha mavazi ambayo hayana heshima, hili ni tatizo” alisema Meya Mwita.

Lazima tusimame kwenye misingi ambayo itawajenga watoto wenu hata huko badae ambapo hamtakuwepo, leo hi mkiwa hai, wenyenguvu msiwajengee misingi mibovu.
“ Leo hii ukimwambia kiongozi acha rushwa, ufisadi hawezi kukusikia kwakua tangu awali hakujengewa wala kulelewa kwenye misingi ya uadilifu” alifafanua Meya Mwita.

Aliongeza kwamba” kila mzazi hapa alipo, kama ulimpeleka mwenyewe matoto wako kujifunza elimu hii ya dini, sasa niwakati pia wakumsimamia ili aweze kuyaishi haya ambayo ameyapata leo” alifafanua.

Katika hatua nyingine Meya Mwita aliwataka vijana waliofikia hatua ya kuoa, watimize wajibu wao na kuacha kusingizia hali ngumu ya kimaisha.

Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana ambao wamefikia umri wa kuoa , kuwanafamilia lakini wanashindwa kufanya hivyo kutokana na kukwepa majukumu na hivyo kusingizia kuwepo kwa hali ngumu ya kimaisha.

“ Tunalowimbi kubwa la vijana ambalo halitaki kujitegemea ,kufanya kazi,  kijana anamiaka kuanzia 25 hadi 35 yupo nyumbani kwa baba na mama , anakwambia hawezi kutoka kuanza maisha mengine kwa sababu hali ya maisha ni ngumu, nahao hao ndio wanajiingiza kwenye makundi ya kihalifu, sasa huko tulipo tunatakiwa kutoka.

“ Hakuna maisha marahisi wala magumu, tunatakiwa kujenga utamaduni huo, msikubali kujibweteka kwa kisingizo cha maisha magumu halafu mnajiingiza kwenye makundi mabaya, jifunzeni kujitegemea” alisisitiza.

Mstahiki  Meya wa Jiji la Dar es salaam, Isaya Mwita (kushoto) wakijaribu kubadilishana mawazo na Shekh Abdul Hamid (kulia)ambaye ni mshauri wa maswala ya elimu ya dini, mbali na mshari pia ni Mwenyekiti wa Rahma Foundation iliyopo Jijini Dar es salaam makutano ya Morogoro Road na Bibi Titi katika hafla ya uzinduzi wa Madrasa Muhajirina uliofanyika jana Kata ya Ukonga, Mtaa wa Mongolandege.

Taasisi ya Mama's & Papa's Kutoa Tuzo Kwa Wanaothamini Jamii

$
0
0
 Mshauri wa Taasisi ya Mama’s & Papa’s For Community Reform Rehabilitation Center (MPFCR) Balozi Patrick Chokala akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utoaji wa TUZO kwa baadhi ya watu wenyemkachango katika jamii leo Jijini Dar es Salaam. Tuzo hizo zitatolewa tarehe 12 mwezi huu. Watakaopewa tuzo hizo ni Dkt. Reginald Mengi, Mchungaji Dkt. Getrude Rwakatale, Mhe. Agustino Lyatonga Mrema, Mustafa Sabodo, na Mohamed Gulam Dewji. Kulia ni Mjumbe wa Taasisi hiyo Omary Kombe.
 Msanii wa muziki wa Bongo Fleva ambaye pia ni Balozi wa Taasisi ya Mama’s & Papa’s For Community Reform Rehabilitation Center (MPFCR), Nurdin Bilal maarufu kama Shetta (baba Kaira) akielezea jambo mbele ya waandishi wa habari kuhusu yeye kuwa Balozi wa Taasisi hiyo kwa lengo la kuunga mkono jitihada za kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya leo Jijini Dar es Salaam.Taasisi hiyo pia imetoa Tuzo za heshima kwa baadhi ya watu wenye mchango katika jamii. Kutoka kulia ni Mshauri wa Taasisi hiyo Balozi Patrick Chokala na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Bibi. Emmi Ally Ghahae. 
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wao na wawakilishi wa Taasisi ya Mama’s & Papa’s For Community Reform Rehabilitation Center (MPFCR) leo jijini Dar es Salaam. Taasisi hiyo inatarajia kutoa Tuzo za heshima kwa baadhi ya wadau wanajali na kuthamini jamii.Watakaopewa tuzo hizo ni Dkt. Reginald Mengi, Mchungaji Dkt. Getrude Rwakatale, Mhe. Agustino Lyatonga Mrema, Mustafa Sabodo, na Mohamed Gulam Dewji.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MAY 9,2017

Tangazo - Wafanyakazi Wenye Vyeti Vya Kughushi Hospitali ya Taifa Muhimbili

BENKI YA CBA YAIMWAGIA SHULE YA SING'ISI MSAADA WA SHILINGI MILIONI NNE

$
0
0
Na Pamela Mollel, Arusha .
      Shule ya msingi Sing’isi iliyopo katika wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha iliyokuwa ikikabiliwa  na changamoto ya madarasa kujaa maji imepatiwa msaada wa kiasi cha shilingi Milioni nne na benki ya biashara ya Africa (CBA) kwa ajili ya ukarabati wa baadhi ya madarasa

Akikabidhi hundi katika shule hiyo juzi Mkurugenzi wa CBA Gifti Shoko alisema kuwa lengo la msaada huo ni kusaidia wanafunzi kuondokana na changamoto ya kutoa maji katika madarasa pindi mvua zinaponyesha hali inayosababisha kukosa vipindi viwili hadi vitatu kwa siku

Alisema kuwa msaada huo utumike kama ulivyokusudiwa kuboresha madarasa hayo kwani ubora wa elimu unaletwa na mazingira mazuri ya watoto  kusomea  

‘’Hapa nawaona Marais, mawaziri wa kesho pamoja na wafanyakazi wazuri wa benki yetu hivyo hatuna budi kutuoa msaada huu ikiwa kama mchango wetu wa kuboresha sekta ya elimu na tunawahidi hatutaishia hapa tutaendelea kuwasaidia kadri ya uwezo wetu ‘’

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Faith Mushiro akitoa neno la shukrani alisema kuwa wanafunzi wa darasa la tano na la sita ndiyo hasa walikuwa wakipata hadha hiyo ya kuondoa maji madarasani pindi mvua zinapoanza kunyesha

Aidha alisema kuwa zaidi ya vipindi viwili hadi vitatu vya asubuhi hushindwa kuhudhulia kutokana na changamoto hiyo hivyo kupitia msaada huo wanafunzi watasoma katika vyumba  vya madarasa vizuri tofauti na kipindi cha nyuma 

Awali akisoma Risala mwalimu wa shule hiyo Bw.Simon Mbawala  kwa niaba ya shule hiyo alisema kuwa pamoja na msaada waliopatiwa bado shule inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa makataba ya kuhifadhi vitabu, kuharibika kwa sakafu za madarasa pamoja na kupasuka kwa vioo vya madirisha 

Hata hivyo tunatoa shukrani zetu za dhati kwa mssada huu wa ujenzi wa vyumba vinne ambayo vilikuwa na tatizo la kuvuja kwa maji kutokana na bati zake kuwa chakavu hali iliyokuwa ikiwathiri sana wanafunzi na walimu hasa ikifika wakati wa kufundisha

 Mkurugenzi wa Benki ya biashara ya Africa (CBA) Gifti Shoko akikabidhi hundi ya kiasi cha shilingi Milioni nne kwa Mwalimu mkuu wa Shule ya msingi Sing’isi iliyopo katika wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha juzi Bi.Faith Mushiro kwaajili ya kukarabati madarasa manne ambayo hujaa maji kipindi cha mvua hali ambayoilikuwa ikiwasababishia wanafunzi kukosa vipindi viwili hadi vitatu kwa siku.
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Sing'isi Bi.Faith Mushiro akionyesha sehemu ambayo husababisha maji kujaa ndani ya madarasa pindi mvua inaponyesha, wakatikati ni Mkurugenzi wa Benki ya biashara ya Africa(CBA)Gifti Shoko pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo
 Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi  Sing'isi Bi.Faith Mushiro akitoa neno la shukrani kwa uongozi wa benki ya CBA mara baada ya kupata msaada wa shilingi Millioni nne kwa ajili ya ukarabati wa madarasa.
 Mkurugenzi wa Benki ya biashara ya Africa(CBA)Gifti Shoko akiangalia baadhi ya vifaa vya umeme ambavyo walitoa msaada kwa shule hiyo
 Wanafunzi wakiimba

RAIS DKT MAGUFULI ATOA MSAADA WA MAGARI YA KUBEBEA WAGONJWA (AMBULANCE) KWA WABUNGE WA NKASI, TABORA NA SHINYANGA

$
0
0
 Wabunge wa Nkasi, Tabora na Shinyanga wakiwasili tayari kukabidhiwa magari la kubebea wagonjwa waliyopewa msaada na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 9, 2017
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akiwakaribisha  Wabunge Mhe Ali Mohamed Kessy (Nkasi Kaskazini)  Mhe. Munde tambwe (viti maalumu - Mkoa wa Tabora) na Mhe Lucy Mayenga (viti maalumu-mkoa wa Shinyanga) kupokea magari ya kubebea wagonjwa waliyopewa saada na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 9, 2017
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akimwangalia Mbunge wa Nkasi Mhe Ali Mohamed Kessy baada ya kumkabidhi gari la kubebea wagonjwa alilopewa msaada na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 9, 2017
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akimwangalia Mbunge wa Viti Maalumu Mhe Lucy Mayenga baada ya kumkabidhi gari la kubebea wagonjwa alilopewa msaada na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 9, 2017
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akimwangalia Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Munde baada ya kumkabidhi gari la kubebea wagonjwa alilopewa msaada na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 9, 2017
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi (kati) akiwa na Katibu Mkuu Ikulu Mhe. Alphayo Kidata (Kushoto) na Mkurugenzi wa Huduma Ikulu  Bw. Charles Mwankupili (kulia) na  Wabunge Mhe Ali Mohamed Kessy (mbunge wa Nkasi Kaskazini)  Mhe. Munde tambwe na Mhe Lucy Mayenga (wabunge viti maalumu)  baada ya kuwakabidhi magari la kubebea wagonjwa waliyopewa msaada na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam leo Mei 9, 2017.


PICHA NA IKULU

WAZIRI MKUU AONGOZA MAZISHI YA DIWANI WAKE

$
0
0
Waziri  Mkuu Kassim  Majaliwa  na Mbunge wa Ruangwa,  akiweka mchanga  kwenye kaburi la aliyekuwa  Diwani wa  CCM Kata ya Mnacho ,Kijij cha Nandagala , Bw.  Daniel Petro  Mtawa ambaye amefariki tarehe   May 7,2017 na kuzikwa  kijijini  kwake  Nandagala  Wilaya ya Ruangwa  Mkoani  Lindi May 8 ,2017. (PICHA NA OWM)
 Waziri Mkuu Kassim  Majaliwa  akitoa salamu za Pole  Katika  Msiba kwa  aliyekuwa Diwani wa  CCM Kata ya Mnacho ,Kijij cha Nandagala , Bw.  Daniel Petro  Mtawa aliyefariki tarehe May 7,2017 na kuzikwa  kijijini  kwake  Nandagala  Wilaya ya Ruangwa  Mkoani  Lindi May 8 ,2017. (PICHA NA OWM)
Waziri  Mkuu  Kassim  Majaliwa  akiwa ameongozana na  Viongozi  wa Mkoa  wa  Lindi na Mtwara   pamoja na wananchi kuelekea makaburini kwa ajili  ya  mazishi ya aliyekuwa Diwani wa  CCM Kata ya Mnacho, Kijiji cha Nandagala , Bw.  Daniel Petro  Mtawa aliyefariki tarehe May 7,2017 na kuzikwa  kijijini  kwake  Nandagala  Wilaya ya Ruangwa  Mkoani  Lindi May 8,2017. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Halima Dendego na wa pili kulia, ni Mkuu  wa Mkoa  wa Lindi,  Bw.  Godfrey  Zambi. Kushoto  ni Kaimu   Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa , Bi. Rukia Mhango. (PICHA NA OWM)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameongoza mamia ya wakazi wa kata ya Mnacho, wilayani Ruangwa kwenye mazishi ya aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Bw. Daniel Mtawa ambaye alifariki dunia Mei 7, 2017. 

Akizungumza na waombolezaji katika ibada ya mazishi iliyofanyika kwenye kijiji cha Nandagala, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi jana (Jumatatu, Mei 8, 2017), Waziri Mkuu alisema msiba uliowapata wana-Mnacho ni mkubwa, na akatumia fursa hiyo kuwapa pole wanafamilia na wanakijiji wenzake.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Ruangwa, anatoka katika kijiji cha Nandagala, kwenye kata hiyohiyo ya Mnacho.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kufikisha salamu za rambirambi ambazo zilitolewa na Mheshimiwa Rais, Dk. John Pombe Magufuli pamoja na Mheshimiwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan. “Mheshimiwa Rais ametoa salamu za pole kwa mke wa marehemu, familia na wana-Ruangwa wote. Pia Mheshimiwa Makamu wa Rais, anawapa pole wana-Ruangwa wote kwa msiba huu mzito,” aliongeza.

“Ndugu yetu Mtawa amemaliza safari yake na ametangulia mbele ya haki. Tuendelee kumuombea marehemu Mtawa, kila mtu kwa imani yake. Ninatoa pole kwa familia, kwa Mwenyekiti wa Halmashauri na madiwani wenzangu wote,” alisema.

Akitoa salamu za rambirambi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ruangwa, Bw. Rashid Nakumbya, alisema Bw. Mtawa alikuwa diwani wa kata hiyo tangu mwaka 2015 lakini alianza kupata tatizo la shinikizo la damu Desemba mwaka jana. “Alilazwa katika hospitali ya Nyangao kwa mwezi mmoja, na baadaye akahamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alilazwa kwa miezi miwili kabla ya kupata nafuu na kuruhusiwa kurudi nyumbani kuendelea na dawa,” alisema.

Marehemu Mtawa ameacha mjane, watoto saba (wa kiume watano na wa kike wawili) na wajukuu wanane.

Kwa upande wake, Mwinjilisti Sebastian Francis wa Kanisa la Anglikana Ruangwa alisema mshahara wa dhambi ni mauti na akawataka waombolezaji wote kila mmoja kwa imani yake wajiepushe na anasa za dunia ili waweze kuurithi ufalme wa mbinguni.

“Baada ya kifo yapo maisha na Bw. Daniel Mtawa amemaliza safari yake, lakini je mimi na wewe tumejiandaa vipi kufika mwisho wa safari yetu? Ndugu zangu, maisha ya starehe na anasa yasitufanye tuukose ufalme wa Mbinguni,” alisema.

Akitoa mfano kutoka kitabu cha Luka (16:19-31) wa Lazaro maskini ambaye alikuwa akiomba chakula lakini hapewi hadi kutamani makombo kutoka kwa tajiri, Mwinjilisti Francis alisema wanadamu tunapaswa kubadilika na kujaliana.

“Huu mfano unaonyesha kuwa hakuna aliyemjali wala hakuna aliyemhudumia yule maskini. Tunafundishwa kuwa watu wa kuhurumiana na kujaliana bila kujali dini, rangi au kabila la mtu,” alisisitiza.

Waziri Mkuu alirejea Dodoma jana usiku kuendelea na ratiba za vikao vya Bunge.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
40480 - DODOMA.
JUMANNE, MEI 9, 2017.

MAPAMBANO YA DAWA ZA KULEVYA NA UVUVI HARAMU YASHIKA KASI WILAYANI NYAMAGANA.

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Mhe.Marry Tesha (kushoto), akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mapambano ya dawa za kulevya, uvuvi haramu na makosa mengineyo wilayani humo.
#BMGHabari
Mkuu wa polisi wilayani Kamagana akizungumza kwenye kikao hicho.
Katibu wa mkuu wa wilaya ya Nyamagana akizungumza kwenye kikao hicho
Afisa uvuvi halmashauri ya Jiji la Mwanza akizungumza kwenye kikao hicho
Wakili wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mkoani Mwanza, akizungumza kwenye kikao hicho.
Wakili wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mkoani Mwanza, akizungumza kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana (kulia), wakiwa kwenye kikao hicho
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Mhe.Marry Tesha, amesikitishwa na taarifa za utekelezaji wa mapambano ya dawa za kulevya, uvuvi haramu na makosa mbalimbali ya kiusalama wilayani humo katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.

Akizungumza ijumaa iliyopita kwenye kikao hicho mwishoni mwa wiki, Mhe.Tesha, alisema taarifa zilizowasilishwa na baadhi ya watendaji hazikuwa zimejitosheleza na kuwataka watendaji hao kuhakikisha kikao cha mwezi ujao wanaandaa taarifa kamili ikiwemo mafanikio na mapungufu halisi katika mapambano hayo. 

Kikao hicho kiliwahusisha viongozi kutoka idara mbalimbali ikiwemo polisi, uvuvi, serikali za mitaa na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ambapo taarifa ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Nyamagana, OCD Ochieng Asiago, ilibainisha kukamatwa kwa watuhumiwa 15 na kesi 16 kutokana na dawa za kulevya.

Awali baadhi ya wajumbe katika kikao hicho waliwatupia lawama maofisa wa serikali kwa kuharibu ushahidi wa dawa za kulevya ikiwemo kuita kokeini kwamba ni unga sembe.

Hata hivyo Wakili wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mkoani Mwanza, Seth Mkemwa, alifafanua kwamba dawa zinazohisiwa ni za kulevya zinapokamatwa lazima zifikishwe ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya uchunguzi na ikibainika ni dawa halisi watuhumiwa kufikishwa mahakamani na dawa kuteketezwa.

ANATAFUTWA NA WAZAZI WAKE

$
0
0
MTOTO HUYU PICHANI ANAITWA LINDA RAYMOND KOMBE AMEPOTEA NYUMBANI KWAO KINONDONI MKWAJUNI TAR 6/05/2017 KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA,YEYOTE ATAKAYEMUONA AWASILIANE NA WAZAZI WAKE KWA NAMBA 0714 282527, 0654 700777. ZAWADI NONO ITATOLEWA KWA ATAKAYEFANIKISHA KUPATIKANA KWAKE

BALOZI FATMA AWASILISHA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO NCHINI QATAR

$
0
0

Mhe. Fatma Mohammed Rajab, Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Qatar akiwa katika mazungumzo na Mhe. Sultan bin Saad Al Muraikhi, Waziri wa Nchi, Mambo ya Nje wa Qatar. Mazungumzo hayo yalifanyika baada ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho. Wawili hao walizungumza masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar.
Balozi Mteule wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Fatma Mohammed Rajab akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Sultan bin Saad Al Muraikhi, Waziri wa Nchi, Mambo ya Nje wa Qatar ofisini kwa Mhe. Waziri. Mhe. Fatma Rajab anakuwa Balozi Mkazi wa kwanza kuiwakilisha Tanzania katika Taifa la Qatar. Mhe. Balozi alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Doha alipokelewa na Idara ya Itifaki ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar. Aidha, wawakilishi wa Watanzania wanaoishi nchini humo walifika Uwanja wa Ndege kumlaki
Mhe. Balozi Fatma Mohammed Rajab, akiwa na viongozi wa Watanzania wanaishi nchini Qatar.

10 of 22 Print all In new window MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA ISHIRINI MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO MAY 9, 2017.

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Najma Giga akiongoza  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba akijibu hoja Mbalimbali za Wabunge  katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Mbunge wa Segerea Mhe.Bonnah Kaluwa  akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI Mhe.Selemani  Jafo akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Waziri wa mabo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza jambo Mbunge wa Arusha Mjini Mhe.Godbless Lema katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Jumanne Maghembe akizungumza na Mbunge wa Arumeru Mashariki Mhe.Joshua Nassari katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Mbunge wa Mwibara (CCM) Mhe.Kangi Lugora akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
Mbunge wa Madaba Mhe.Joseph Mhagama akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Isack Kamwelwe akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Maria Kangoye akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mhe.Dk Charles Tizeba akijibu maswali mbalimbali ya wabunge kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017.
 Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Edwin Ngonyani akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 9, 2017. 

Picha Zote na Daudi Manongi- Dodoma MAELEZO, DODOMA

RAIS SHEIN ATEMBELEA BANDARI YA NCHINI DJIBOUTI

$
0
0
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi  Ukaguzi Nd.Mohamoud Houssein (wa pili kushoto) wakati  alipotembelea  katika Bandari ya Doraleh  Container Terminal jana,ambayo ni maalum kwa upokeaji wa Makontena kutoka kwenye meli mbali mbali  zinazowasili katuika Bandari hiyo,akiwa katika ziara ya kiserikali chini Djibouti na ujumbe aliofuanata nao.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Viongozi mbali mbali  alipowasili katika Bandari ya   Doraleh  Container Terminal  jana ambayo ni maalum kwa upokeaji wa Makontena kutoka kwenye meli mbali mbali zinazowasili katika Bandari hiyo, alipotembelea  akiwa katika ziara maalum ya kiserikali nchini Djibouti akiwa na ujumbe aliofuanata nao
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Viongozi mbali mbali  alipowasili katika Bandari ya   Doraleh  Container Terminal  jana ambayo ni maalum kwa upokeaji wa Makontena kutoka kwenye meli mbali mbali zinazowasili katika Bandari hiyo, alipotembelea  akiwa katika ziara maalum ya kiserikali nchini Djibouti akiwa na ujumbe aliofuanata nao.
 Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi  Ukaguzi Nd.Mohamoud Houssein (katikati) mara baada ya mapokezi alipotembelea  katika Bandari ya   Doraleh  Container Terminal  jana ambayo ni maalum kwa upokeaji wa Makontena kutoka kwenye meli mbali mbali zinazowasili katika Bandari hiyo, alipotembelea  akiwa katika ziara maalum ya kiserikali nchini Djibouti akiwa na ujumbe aliofuanata nao terehe 08/05/2017.
 Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) pamoja na Viongozi wengine wakipata maelezo kutoka kwa Mtaalam wa Mashine  karika Bandari  ya   Doraleh  Container Terminal  jana  ambayo ni maalum kwa upokeaji wa Makontena kutoka kwenye meli mbali mbali zinazowasili katika Bandari hiyo, Dk.Shein yupo nchini Djibouti katika  ziara maalum ya kiserikali   akiwa na ujumbe aliofuanata nao
 Makontena yenye mizogo mbali mbali yakiwa katika eneo maalum lililotengwa na kuwekwa katika Bandari  ya   Doraleh  Container Terminal nchini Djibouti ambapo  Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na ujumbe wake jana walitembelea eneo hilo akiwa katika ziara maalum ya kiserikali.
 Mashine za kuchukulia Makontena katika meli zinazofunga gati katika  Bandari  ya   Doraleh  Container Terminal nchini Djibouti ambapo  Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na ujumbe wake  jana walitembelea eneo hilo akiwa katika ziara maalum ya kiserikali.
 Makontena yenye mizogo mbali mbali yakiwa katika eneo maalum lililotengwa na kuwekwa Mizigo mbali mbali katika Bandari  ya   Doraleh  Container Terminal nchini Djibouti ambapo  Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na ujumbe wake jana walitembelea eneo  hilo   katika ziara maalum ya kiserikali.
  Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akisalimiana  na Mkuu wa Bandari ya Djibouti Bw, Saad Omar  Guelleh  mara alipowasili katika Bandari  ya   Doraleh  Multipurpose nchini Djibouti akiwa katika ziara maalum ya kiserikali alitembelea jana akiwa na ujumbe wake,(kushoto) Waziri wa Vifaa na Usafirishaji Mhe.Mohamed Abdoulkader Moussa.
 Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akitambulishwa na Mkuu wa Bandari ya Djibouti Bw,Saad Omar  Guelleh (katikati) kwa viongozi wakati aliposalimiana nao jana  wakati  alipotembelea katika Bandari  ya   Doraleh  Multipurpose  nchini Djibouti  akiwa katika ziara maalum ya kiserikali  na ujumbe wake,(kushoto) Waziri wa Vifaa na Usafirishaji Mhe.Mohamed Abdoulkader Moussa.
 Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akitambulishwa na Mkuu wa Bandari ya Djibouti Bw,Saad Omar  Guelleh (katikati) kwa viongozi wakati aliposalimiana nao jana  wakati  alipotembelea katika Bandari  ya   Doraleh  Multipurpose  nchini Djibouti  akiwa katika ziara maalum ya kiserikali  na ujumbe wake,(kushoto) Waziri wa Vifaa na Usafirishaji Mhe.Mohamed Abdoulkader Moussa.
 Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akitambulishwa na Mkuu wa Bandari ya Djibouti Bw,Saad Omar  Guelleh (katikati) kwa viongozi wakati aliposalimiana nao jana  wakati  alipotembelea katika Bandari  ya   Doraleh  Multipurpose  nchini Djibouti  akiwa katika ziara maalum ya kiserikali  na ujumbe wake,(kushoto) Waziri wa Vifaa na Usafirishaji Mhe.Mohamed Abdoulkader Moussa.

(Picha na Ikulu)
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images