Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

TAARIFA YA MSIBA

$
0
0
Eng Joseph Shega wa Nyumbu Kibaha anasikitika kutangaza kifo cha mama yake mzazi MARIETHA  LUSAMBO kilicho tokea jana asubuhi katika Hospitali ya Mpanda Katavi Mazishi yatafanyika kesho Jumatatu kuanzia mchana tarehe 31 Janary 2017 wilayani Mpanda.

HABARI ZIWAFIKIE 

Kaka wa marehemu Emily Lusambo akiwa Kisa Rukwa

Mh Sebastian Kapufi Mbunge wa Mpanda mjini

Wifi wa marehemu Angelina Kisunga wa Kibaha Pwani

Watoto wote wa marehemu wajuu wote waliopo Dar es salaam Arusha Kilimanjaro 
Kibaha  Sumbawanga 

Wafanyakazi wa shirika la nymbu kibaha, majirani wote wa kwa matiasi kibaha, pamoja na marafiki wote

Bwana ametoa Bwana ametwa jinalake lihimidiwe Amen

NEWZ ALERT: TRENI YA DELUXE YAPATA AJALI,HAKUNA VIFO VILIVYORIPOTIWA

$
0
0
 Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetoa taarifa kuwa leo  Januari 29, 2017 mnamo  saa 9:40 alasiri treni ya abiria ya Deluxe ilipokuwa ikirejea Dar es Salaam kutoka Kigoma imepata ajali kati ya vituo vya Ruvu na Ngeta ambapo mabehewa 9 yamepata ajali . Kati ya hayo manne yameanguka, mawili yametenguka na matatu yameacha njia.

Imeripotiwa watu kadhaa wamepata majeraha mepesi isipokuwa mmoja ndiye aliyepata majeraha makubwa ambaye amekimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi.

Hizi ni taarifa za awali baada ya Kikosi cha uokoaji kikimaliza kazi ya kuinua mabehewa ndio taarifa ya kamili ya ajali itakamilika!

Wakati taarifa hii ikipatikana Waziri wa  Ujenzi na Uchukuzi  Profesa Makame  Mbarawa  .Mkuu wa TRL Ndugu Kagosa Kamanda Kikosi , Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Nd Masanja Kungu Kadogosa na Kamanda wa Kikosi cha Polisi Reli Mhandisi S. Chillery wako  katika eneo la ajali! .

Halikadhalika taarifa imefafanua kuwa sehemu ya treni ya Deluxe yenye mabehewa kumi na abiria wake iko njiani kuja Dar es Salaam na  inatarajiwa kuwasili saa 2 usku.

Aidha  uongozi wa TRL umehakikisha umma na wateja wake kuwa njia ya reli  kati ya Ruvu na Dar es Salaam itafunguliwa ndani ya saa 24 ili shughuli za usafirishaji  zirejee kama kama kawaida.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano:
 Kwa niaba ya  Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Januari 29, 2017
DAR ES SALAAM 
Baadhi ya Mabehewa ya  TRENI ya mwendo haraka, (DELUX), iliyokuwa ikitokea Kigoma kuja jijini Dar es Salaam, yakiwa yameanguka eneo la Ruvu mkoani Pwani jioni hii ya Januari 29, 2017.
 Baadhi ya Mabewa mengine yakionekana kuacha njia

Baadhi ya Abiria waliokuwa wamependa  TRENI ya mwendo haraka, (DELUX), iliyokuwa ikitokea Kigoma kuja jijini Dar es Salaam,wakitoka kwenye mabehewa hayo mara baada ya kupata ajali eneo la Ruvu mkoani Pwani jioni hii ya Januari 29, 2017.

RAIS DKT. MAGUFULI AHUTUBIA KATIKA KUTANGAZA JINA RASMI LA KITUO CHA AMANI NA USALAMA KILICHOPEWA JINA LA MWALIMU JULIUS NYERERE KATIKA MAKAO MAKUU YA UMOJA WA AFRICA (AU) ADDIS ABABA NCHINI ETHIOPIA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na viongozi wa mataifa mabalimbali wakiwa katika picha ya pamoja katika jengo jipya la kituo cha  Amani na Usalama (JULIUS NYERERE) lililopo katika Makao makuu ya Umoja wa Afrika Addis Ababa nchini Ethiopia. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia Viongozi Wakuu wa Mataifa mbalimbali hawapo (pichani) katika Jengo jipya la Kituo cha Amani na Usalama kilichopewa jina Rasmi la Mwalimu Julius Nyerere, Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kutangazwa rasmi kwa Jina la Mwalimu Julius Nyerere katika kituo hicho cha Amani na Usalama.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Rais wa Rwanda Paul Kagame wakati wakielekea katika Kituo cha Amani na Usalama cha Makao Makuu ya Umoja wa Afrika kilichopewa jina la Rais wa kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere, Addis Abba nchini Ethiopia. PICHA NA IKULU

DC Tanganyika afanya ziara ya siku tatu kukagua hali ya kilimo cha mazao

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi,Saleh Mhando akiwa sambamba na kamati ya Ulinzi na Usalama,kwa pamoja wakiwa kwenye ziara ya  siku tatu ya kukagua hali ya Kilimo cha mazao ya Mahindi, Mpunga, Alizeti na Tumbaku.Dc Mhando amesema kuwa kwa ujumla hali ni nzuri sana na Wananchi wanatarajia kupata mavuno ya kutosha pamoja na ziada.
 
 Moja ya shamba la Mahindi yakiwa yamestawi vyema
  Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi,Saleh Mhando akiwa sambamba na kamati ya Ulinzi na Usalama wakikagua mashamba ya mpunga na kujionea hali halisi ya kilimo cha mpunga.
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi,Saleh Mhando akiwa sambamba na mmoja wa Wanakamati ya Ulinzi na Usalama wakikagua moja ya mashamba ya mahindi na kujionea hali halisi ya kilimo



 Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi,Saleh Mhando akiwa sambamba na kamati ya Ulinzi na Usalama wakikagua mashamba ya mpunga na kujionea hali halisi ya kilimo cha mpunga.
 Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi,Saleh Mhando akiwa sambamba na kamati ya Ulinzi na Usalama wakijadiliana jambo mara baada ya kumaliza kukagua baadhi ya mashamba ya Mahindi na Mpunga wilayani humo mkoani Katavi

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU UMOJA WA MATAIFA (UN) PIA AHUDHURIA MKUTANO WA AU MJINI ADDIS ABABA ETHIOPIA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Marais wa wa mataifa mbalimbali  katika mkutano wa AU unaoendelea mjini Addis Abba nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres kabla ya kuanza mazungumzo yao katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres mara baada ya mazungumzo yao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Malawi Peter Mutharika kabla ya kuanza mazungumzo yao katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na Rais wa Malawi Peter Mutharika pamoja na viongozi wengine mara baada ya kumaliza mazungumzo yao katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Kidemokrasia ya Sahrawi(SADR) Brahim Ghali katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia. 

PICHA NA IKULU

RAHEL PALANGYO AULA KAMATI YA UTENDAJI CHAMA CHA WAAMUZI JIJINI DAR

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


MWANDISHI wa Gazeti  la HabariLeo na SpotiLeo, Rahel Pallangyo amechaguliwa kuwa mjumbe wa kamati ya Utendaji  wa Chama cha Waamuzi wa Soka Mkoa wa Dar es Salaam kuwakilisha wanawake.

Rahel ambaye pia ni kocha mwenye leseni B inayotambuliwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) alimwangusha mpinzani wake Isabela Kapera ambaye ni mwamuzi mstaafu wa FIFA aliyepata kura moja dhidi ya tano za Rahel.

Nafasi ya Mwenyekiti ilikwenda kwa Omar Abdulqudir aliyepata kura tano na Makamu Mwenyekiti ni Sijali Mzeru aliyepata kura sita na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa alichaguliwa Jovin Ndimbo kwa kura sita.

Katibu Mkuu alichaguliwa Said Mbwana kwa kura tano, msaidizi ni Waziri Hunda aliyepata kura sita na Mhazini ni Job Wandiba aliyepata kura sita.

Awali akizungumza kwa niaba ya wenzake wa uongozi uliopita muda, Hemed Nteza alishukuru kwa ushirikiano wa wajumbe na wachama kipindi chote walichokaa madarakani na kuwaasa watakaochaguliwa kuendeleza umoja.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Victor Mwandike alishukuru kwa kufanikisha uchaguzi kufanyika na kushukuru wajumbe wa mkutano kamati yake kwa kushirikiana vema.

"Nashukuru wajumbe na mwanasheria wa kamati kwa kutusaidia kutafsiri vifungu vya katiba na hatimaye tumemaliza kazi, nawatakia kila la heri katika kutekeleza majukumu yenu," alisema Mwandike.

Katika hatua nyingine  Mwenyekiti mpya, Abdulqudir  aliwateua Hemed Nteza na Mzee Malipula kuwa wajumbe wa heshima wa kamati ya utendaji.

MAWAKALA MPAKA WA TUNDUMA/NAKONDE WAONYWA KUKWAMISHA BIASHARA

$
0
0

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda, amewaonya mawakala wa forodha katika mpaka wa Tanzania na Zambia wa Tunduma/Nakonde kuacha Mara moja tabia ya kuwachelewesha madereva wa malori yaendayo masafa marefu kwa makusudi ili wapewe rushwa.

Prof. Mkenda ametoa onyo hilo katika mpaka huo wa Tunduma na Nakonde, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya madereva wa malori waliodai wamekuwa wakicheleweshwa kuvuka mpaka huo kwa zaidi ya siku tatu hadi tano.Habari kamili hii hapa video yake.

AZAM MARINE YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA MKOANI TANGA YASHUSHA MELI ITAKAYOKWENDA PEMBA NA UNGUJA KUTOKA MKOANI TANGA

$
0
0

Meli Kubwa inayoweza kuingia abiria na mizigo kwa pamoja ambayo itafanya safari zake kati ya Tanga-Unguja na Pemba ikiwa inaingia bandari ya Tanga leo wakati wa uzinduzi wake ambapo uwekezaji huo mkubwa umefanywa na kampuni ya Azam Marine ili kuwanusuru wananchi wa mkoa wa Tanga na changamoto za usafiri huo .

Meli Kubwa inayoweza kuingia abiria 1600 na magari hamsini yenye mizigo kwa pamoja ambayo itafanya safari zake kati ya Tanga-Unguja na Pemba ikiwa inaingia bandari ya Tanga leo wakati wa uzinduzi wake ambapo uwekezaji huo mkubwa umefanywa na kampuni ya Azam Marine
Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed wa pili kulia akitazama namna wananchi wanavyoshuka kwenye meli hiyo itakayopunguza adha na usumbufu kwa wananchi wanaosafiri kutoka mkoani Tanga kwenda Unguja na Pemba
Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed katikati akizungumza na watumishi wa mamlaka ya Bandari Mkoani Tanga wakati wa ujio wa meli hiyo kwenye bandari ya Tanga kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Tryphoni Ntipi kushoto ni PRO wa Mamlaka hiyo,Moni Jarufu.
Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed katikati akisalimiana na Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Tryphoni Ntipi wakati wa ujio wa meli hiyo kushoto ni PRO wa Mamlaka hiyo,Moni Jarufu.
Mazungumzo yakiendelea

Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ujio wa meli hiyo kulia Mkurugenzi Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa vyombo vya majini (SUMATRA) Kaptain Mussa Mandia .

Mkurugenzi Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa vyombo vya majini (SUMATRA) Kaptain Mussa Mandia katikati akizungumza na waandishi wa habari kushoto ni Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed .

Nahodha wa Meli hiyo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufika Bandari ya Tanga.

Waandishi wa Habari wakiwa kazini kushoto ni Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania katikati ni Mariam Shedafa wa Azam TV
Vifaa vya uokozi wakati wa majanga ya ajali hivyo
Baadhi ya Sehemu ya VIP ndani ya Meli hiyo kama inavyo onekana

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

MAKAMU WA RAIS APOKEA TAARIFA YA TATHMINI YA UJENZI WA BOMBA JIPYA LA MAFUTA SAFI LA TAZAMA

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasikiliza Mawaziri wa Nishati kutoka Tanzania na Zambia wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya tathmini ya ujenzi wa bomba jipya la mafuta safi kutoka Tanzania mpaka Zambia, Mawaziri hao ni Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania Mhe.Profesa Sospeter Muhongo (kulia) na Waziri wa Nishati wa Zambia Bw. David Mabumba (kushoto), Ikulu jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania Mhe.Profesa Sospeter Muhongo (kulia) na Waziri wa Nishati wa Zambia Bw. David Mabumba (kushoto) mara baada ya kumaliza mkutano wa kumpa taarifa Makamu wa Rais ya tathmini ya ujenzi wa bomba jipya la mafuta safi, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Nishati wa Zambia Bw. David Mabumba (kushoto) mara baada ya kupokea taarifa ya tathmini ya ujenzi wa bomba jipya la mafuta safi litakalotoka Dar es Salaam, Tanzania mpaka Ndola, Zambia, Ikulu jijini Dar es Salaam.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe wa Tanzania na Zambia ambao ulifanya ziara ya kukagua pampu na bomba la mafuta la TAZAMA kutoka Ndola, Zambia mpaka Dar es Salaam Tanzania wakiongozwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo na Waziri wa Nishati wa Zambia Bw. David Mabumba ambapo walifanya tathmini ya ujenzi wa bomba jipya la mafuta safi litakalotoka Dar es Salaam, Tanzania mpaka Ndola, Zambia.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Bharti Airtel yakanusha uzushi unaondelea kuhusu biashara zake Afrika- Yasema bado ipo sana.

$
0
0
NAIROBI 30th January, 2017: Airtel Africa, a leading telecommunications company with operations in 15 countries across Africa, has refuted speculative media reports erroneously stating its possible exit from Africa. The organization has reaffirmed that it remains committed to Africa and will continue to invest in its operations to grow sustainably in Africa.

Airtel Africa’s recent 3rd quarter results were strong. The underlying Africa revenues for the quarter accelerated by 6.0 per cent Y-o-Y, the highest over the last 9 quarters. The organizations efforts to improve the quality of customer acquisitions have resulted in a reduction in customer churn to 4.9 per cent from 6.0 per cent. 
 
Data consumption and revenues have grown by 91.0 per cent & 24.0 per cent Y-o-Y respectively, led by stronger data networks. The strong focus on cost management has led to a significant underlying EBITDA margin expansion of 4.5 per cent Y-o-Y, which now stands at 24.5 per cent. Africa is now generating positive free cash and is PBT positive in constant currency.

Raghunath Mandava, Managing Director and Chief Executive Officer, Airtel Africa, said’ “All the steps taken recently with regard to human resources and infrastructure have been geared towards readying the organization to grow efficiently and sustainably in the medium to long term. 
 
The company remains committed to competing in various markets and providing more choice to customers through further investments to ensure consistent delivery of quality and value for money services to our customers. We are also accelerating our investments in new data networks and to modernize our existing networks. We are committed to launch 4 G in multiple countries.”

He added “Mergers and acquisitions continue to be the norm for any multinational organization and they affect all global organizations in equal measures as and when they happen. As a strategy, we look for opportunities to acquire or merge in opcos that are operating in a fragmented market structure with too many players in a small market.
 
 Last year, Airtel and Orange reached a mutually beneficial agreement on the assets in Sierra Leone and Burkina Faso. Similarly, Airtel also acquired assets in Uganda, CongoB and Kenya in recent times. The agreements brought together the strengths of Airtel, Warid and Essar. This has offered benefits to customers in the form of a superior and wider network, affordable voice / data services and better customer care. Away from Africa, recently, we merged with Robi in Bangladesh to create a solid and profitable No.2 player in the market.”

The recent results demonstrate the effectiveness of Airtel’s business strategy in Africa. The organization sees an opportunity ahead to emerge with a broader reach and sharper execution.

GAZETI LA MWANAHALISI LAPEWA SAA 24 LIOMBE RADHI

WATANZANIA WAOMBWA KUMUUNGA MKONO RAIS DK.JOHN MAGUFULI

$
0
0
 Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini, John Shibuda (katikati), akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa kuuaga mwaka wa 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 Dar es Salaam jana. Kulia ni Msajili Msaidizi Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ADA na Waziri wa Nchi asiye na Wizara Maalum, Zanzibar.
 Mkutano ukiendelea.
 Waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo.
Mwanahabari Suleiman Msuya akiuliza swali katika mkutano huo.
Na Dotto Mwaibale

WATANZANIA wameombwa kumuunga mkono Rais Dk.John Magufuli kwa jitohada zake anazozifanya za kupongoza nchi.

Mwito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini John Shibuda wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa kuuaga mwaka wa 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 Dar es Salaam jana.

Alisema Serikali ya awamu ya tano imekuwa ikifanyakazi kubwa ya kudhibiti mirija ya unyonyaji wa pato la Taifa kupitia watumishi hewa, wanafunzi hewa, kaya masikini bandia na kupitia wahujumu uchumi wa matumizi mabaya ya dhamana za Taifa mambo ambayo yalikuwa yakipigiwa kelele na vyama vya upinzani.

"Binafsi nawaomba watanzania bila ya kujali itikadi za vyama vyao kumuunga mkono Rais wetu Dk.John Magufuli na wasaidizi wake Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na wengine wote kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuongoza Taifa letu la Tanzania" alisema Shibuda.

Alisema anaupongeza utumishi wa Serikali ya awamu ya tano kwa uzinduzi wa urejeshaji wa uwajibikaji wa watumishi wote kwani hivi sasa watumishi wengi wanatabia za miiko ya utiifu kwa umma.

Akizungumzia Zanzibar alisema uchaguzi umekwisha pita na Rais wa nchi hiyo ni Dk. Ali Mohammed Shein ambaye anatakiwa kuongoza nchi hiyo na wenzake waliochaguliwa ili kuiletea maendeleo Zanzibar hivyo siasa za mihemuko ziachwe.

Shibuda alitumia nafasi hiyo kuwapongeza wazanzibar hasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ushindi walioupata Jimbo la Dimani na kuwaomba walioshindwa wasivunjike moyo kuvunjika jembe siyo mwisho wa uhunzi kwani hata timu kubwa hufungwa na timu ndogo.

Akizungumzia katazo la vyama vya siasa kutofanya mikutano hadi mwaka 2020 alisema majibu ya suala hilo yatatolewa baadae baada ya kulifanyia kazi jambo hilo. 

Katika hatua nyingine Shibuda alisema Baraza la Vyama vya Siasa litakuwa mshirika rafiki wa wadau wote wa siasa na kusimamia maslahi mapana ya jamii na Taifa yanayosimamiwa na Serikali na kuungwa mkono na Bunge mfano Azimio la EPA.

Shibuda alitoa ushauri kwa vyama vyote vya upinzani kuzingatia umakini wa mabadiliko ya Tabia nchi ya mfumo wa uwajibikaji wa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli.

TAASISI YA MOYO YAPATA WAGENI KUTOKA VYUO VIKUU VYA WITWATERSRAND NCHINI AFRIKA YA KUSINI NA MINESSOTA NCHINI MAREKANI

$
0
0
Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielezea jinsi upasuaji wa Magonjwa ya Moyo unavyofanyika katika taasisi hiyo wakati wageni kutoka Chuo kikuu cha Witwatersrand cha Nchini Afrika ya Kusini walipotembelea wodi aliyokuwa amelazwa mmoja wa wagonjwa aliyefanyiwa upasuaji. Kutoka kulia ni Prof. Martin Valler, akifuatiwa na Afisa Muuguzi Roger Kibula, watatu kulia ni Prof. Simon Nemutandani na wa pili kushoto ni Dkt. Marion Bergman.
Daktari bingwa wa Magonjwa ya Moyo na Mhadhili kutoka chuo Kikuu kishiriki cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS) Prof. Johnson Rwakatare akimuonyesha vipimo vya moyo (ECHO) Prof. Martin Valler Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Afya wa Chuo kikuu cha Witwatersrand cha Nchini Afrika ya Kusini alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwaeleza wataalamu wa afya kutoka Chuo Kikuu cha Minnesota cha nchini Marekani huduma za matibabu ya moyo wanazozitoa wakati walipoitembelea Taasisi hiyo hivi karibuni. Picha na Anna Nkinda - JKCI
Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwaonyesha wageni kutoka Chuo kikuu cha Witwatersrand cha Nchini Afrika ya Kusini sehemu ya malipo ambapo wagonjwa wanalipia huduma. Wageni hao walitembelea Taasisi hiyo hivi karibuni ili kuona huduma za matibabu ya moyo wanazozifanya pia waliahidi kuimarisha mahusiano kati yao hii ikiwa ni pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa madaktari wataokwenda kusoma katika chuo hicho.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi na Prof. Martin Valler Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Afya wa Chuo kikuu cha Witwatersrand cha Nchini Afrika ya Kusini wakiangalia jinsi upasuaji wa bila kufungua kifua (Catheterization) unavyofanyika katika chumba Cath Lab kilichopo katika Taasisi hiyo.

UONGOZI WA BODABODA MKOANI MWANZA WAPONGEZA ZOEZI LA UKAGUZI WA POLISI.

$
0
0
Binagi Media Group
Umoja wa waendesha bodaboda mkoani Mwanza umepongeza zoezi la ukaguzi wa vyombo hivyo linaloendeshwa na jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani.

Jana Mwenyekiti cha umoja huo, Makoye Kayanda, amesema zoezi hilo linaangazia maeneo makuu manne ambayo yamekuwa yakihatarisha usalama wa watumiaji wa bodaboda wakiwemo abiria.

"Cha kwanza ni uvaaji wa kofia ngumu, cha pili leseni ya udereva, cha tatu kuwa na BIMA na ni ubebaji wa mishikaki. Kuna baadhi ya abiria zaidi ya 14 wametozwa faini kwa kukataa kuvaa kofia ngumu, sasa lazima tufuate sheria bila shuruti". Alisema Kayanda huku akipongeza zoezi hilo.

Kayanda aliwasihi waendesha bodaboda wote kuzingatia utii wa sheria bila shuruti ili kuondokana na mazoea yanayoweza kuhatarisha maisha yao na abiria wao pia huku akiwaonya baadhi ya abiria kuepuka tabia ya kukataa kutumia kofia ngumu kwa kisingizio cha uchafu.

"Kupanga ni kuchagua, kama hutaki kuvaa kofia nguvu ya unayopewa na bodaboda, nunua ya kwako ama mfuko wa plastiki ili ukipewa kofia uvalie maana kuna watu wanapata ajali wanapasuka vichwa na inakuwa ni tatizo kwa familia zao na taifa kwa ujumla". Alihimiza Kayanda.
Mwenyekiti wa bodaboda mkoani Mwanza, Makoye Kayanda

DC BUHIGWE,KANALI MARCO GAGUTI AWATAKA VIONGOZI WA SERIKALI NGAZI ZOTE KUANZISHA NYUMBA KUMI ZA KIUSALAMA

$
0
0

Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

MKUU wa Wilaya Ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti amewataka Viongozi wa Serikali ngazi zote kusimamia ipasavyo zoezi la ulinzi na usalama la kuanzisha Nyumba kumi za kiusalama litakalo saidia kukomesha wahamiaji halamu wanao ingia nchini kinyume na sheria na vitendo vya kiuhalifu vinavyo fanywa na watu wasio na mapenzi mema na Nchi yao.

Rai hiyo aliitoa mapema juzi usiku wakati wa doria ya kukagua zoezi la ulinzi wa Nyumba kumi za kiusalama linaloendelea wilayani humo,ambapo Dc Gaguti alibaini baadhi ya Mabalozi wa Nyumba kumi za kiusalama hawana uelewa juu ya uendeshaji wa zoezi hili,hivyo aliwataka maafisa watendaji pamoja na wenyeviti wa vitongoji kutoa elimu hiyo kama walivyo pewa mafunzo kabla ya zoezi hilo kuanza.

Gaguti alisema lengo la kuanzisha Nyumba kumi za kiusalama ni kuhakikisha Kila balozi wa Nyumba hizo, anafahamu kila nyumba ina wakaazi wangapi Pamoja na kuweka daftari la kumbukumbu na kufahamu wageni wanao ingia na kutoka katika kaya hizo, ilikuhakikisha Wahamiaji halamu wanaiingia nchini kinyume na utaratibu wanakamatwa na na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema kumekuwa na Matukio ya kiuhalifu yaliyo kuwa yakifanywa na Wahamiaji halamu wanaoingia Nchini wakiwa na silaha na kushirikiana na baadhi ya Wananchi wa Wilaya hizi zilizopo Mpakani kufanya unyang'anyi kwa kutumia silaha. Zoezi hili la ulinzi wa Nyumba kumi likifanyika kwa ufanisi litasaidia sana kupunguza vitendo hivyo na kubaini wahamiaji wanaoingia.

Aidha Mkuu huyo aliwaomba Wananchi kuacha tabia ya kuwahifadhi wahamiaji halamu wanao ingia kinyume na utaratibu na atakae gundulika anaishi na muhamiaji hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

" Lengo ni kuhakikisha hakuna Wahamiaji haramu Wanao ingia Wilayani mwetu bila kufuata utaratibu. kumekuwa na matukio ya kiuhalifu Wilayani kwetu yanafanywa na Wahamiaji hao. Nimepita katika vijiji nimeona baadhi wanafahamu jinsi gani ya kufanya zoezi hilo na wengine hawaelewi. nitoe siku tatu kwa watendaji na wenyeviti wa vijiji na vitongoji kufanya marekebisho ya mspungufu Pamoja na kufanya ukaguzi. mimi pamoja na kamati yangu ya ulinzi na usalama tutakuwa tukipita kwa kushtukiza",alisema Kanali Gaguti.

Nae mwenyekiti wa Kitongoji cha Mgwaga, Joseph Mzegwe alisema yeye kama kuongozi katika kitongoji chake wameendelea kufanya zoezi la ulinzi na wameanzisha zoezi hilo na kila nyumba kumi za kiusalama zina viongozi wao wanao endelea na ulinzi na matokeo wanayaona, kuanzia zoezi hilo lianzishwe amani na utulivu vimeendelea kuwepo katika kitongoji hicho na hakuna tukio lolote baya lililo tokea.

Hata hivyo aliwaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa mabalozi wao wanapo hitaji kuwahoji juu ya nyumba zao waseme ukweli ilikuepusha usimbufu na kuhakikisha zoezi hilo linakamilika na linaleta manufaa kwa jamii.
MKUU wa Wilaya Ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti akisalimiana na baadhi ya wakazi wa Buhigwe,hivi karibuni alipofanya doria ya kukagua zoezi la ulinzi wa Nyumba kumi za kiusalama linaloendelea wilayani humo mkoani Kigoma
MKUU wa Wilaya Ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti akikagua moja ya daftari lililowekwa kwa na balozi wa nyumba kumi kwa ajili ya kuorodhsha majina ya wakazi wa balozi husika,Kanali Gagugti alifanya doria ya kukagua zoezi la ulinzi wa Nyumba kumi za kiusalama linaloendelea wilayani humo mkoani Kigoma

SERIKALI YATENGA SHULE 55 , YAUNGA MKONO JITIHADA ZA TFF KUINUA MICHEZO

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imesema kwamba inaunga mkono juhudi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika programu za maendeleo ya vijana, hususani nia yake ya dhati kushiriki michuano ijayo ya Olimpiki itakayofanyika Tokyo, Japan mwaka 2020.

Mkurugenzi wa Michezo, Yusuph Omari aliyasema hayo mara baada ya kusikia program za TFF kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Makamu Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Henry Tandau katika hafla ya uzinduzi wa kampeni maalumu za kuifanikisha Tanzania kushiriki michuano ijayo ya Olimpiki.

“Nimesikia program mbalimbali za TFF, naona zinakuja wakati mwafaka. Nimewapongeze kwa mipango yenu mizuri kwa sababu inaleta matumaini. Jambo kubwa ambalo linanisukuma na kuwapongeza ni kuwa na program ya vijana, hatuwezi kufanikiwa kama hatutakuwa na program ya vijana," amesema Omary. Serikali inatambua haya yote mnayofanya. Na ili kuboresha, Serikali imetenga shule 55 ambazo zitakuwa ni maalumu kwa ajili ya vijana, lengo ni kupata vipaji bora ambavyo vitakuwa vikiendelezwa, huku wakiwa wanapata elimu.

Aliendelea, kusema kuwa anasikia  TFF wameunda Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu hususani vijana ni jambo zuri, lakini rai yangu ni kwamba watakapounda kamati ya mfuko huo wawe watu wenye heshima ili wananchi waipende na ikiwa hivyo itafanikiwa wao kama Serikali watafanya kazi bega kwa bega na kamati hiyo na jambo kubwa ni kwamba lazima wakutane mara kwa mara.


Kabla ya Mkurugenzi Singo kuzungumza, Makamu Rais wa TOC, Ndugu Tandau, alipongeza pia harakati za kuanza mapema akisema: “Shukrani TFF kwa kuthamini TOC. Ni vizuri tumeanza mapema. Michuano ya Olimipiki ni mikubwa na inahitaji timu zenye viwango vya juu kufanikiwa kufuzu.”

Alieleza hadhara iliyohudhuria hafla hiyo, kuwa TOC inakuwa na Mawasiliano ya maandalizi Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki inayoitwa ‘Olympic Solidarity Program’ ambayo hutoa sehemu ya fungu ya maandalizi na kwamba TFF haina budi kuwasilisha program yake kwa ajili ya kuingia kwenye bajeti ambayo inaitwa ‘Team Support Grant’.

Awali kabla ya viongozi hao kuzungumza, Rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema kinachofanywa sasa na Shirikisho si kutafuta miujiza kwenye matokeo badala yake ni kujenga timu (Maandalizi) kwa dhana kwamba Timu za Taifa haziokotwi kama embe dodo.“Mhe. Mkurugenzi, kujenga timu hizi ni gharama kubwa. Hata matunda ambayo tunasubiri moshi mweupe ya timu ya vijana, hayakutokea hivi hivi ni maandalizi. Si ajabu kabla ya mwisho wa wiki hii tukaona moshi mweupe,” alisema Malinzi.


Alisema ili vijana wa Tanzania waweze kufanya vema, hakuna budi wadau wakiwamo Serikali, Kampuni, Mashirika ya umma na watu binafasi kusapoti mbio hizo za kwenda Tokyo, Japan pamoja na timu nyingine za taifa. “Program nzima ni gharama kubwa,” Kadhalika, ili kutekeleza program hiyo, Rais Malinzi alizungumzia utulivu katika kufanya kazi kwa sasa kwa kuwa historia inaonesha kuwa kumekuwa na nia ovu ya baadhi ya wadau kutaka kutibua mambo mazuri yanayofanywa na uongozi wa mpira wa miguu.


 Mkurugenzi wa Michezo, Yusuph Omari akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni maalumu za kuifanikisha Tanzania kushiriki michuano ijayo ya Olimpiki 2020 na kuipongeza Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzaniana nchini  kwa  juhudi za kuandaa programu za maendeleo ya vijana.




 Rais wa    Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) Jamal Malinzi akizungumza wakati wa  uzinduzi wa kampeni maalumu za kuifanikisha Tanzania kushiriki michuano ijayo ya Olimpiki 2020 na kuwataka wadau wa michezo kuunga mkono jitihada zake na wasimuache peke yake katika kulisongesha gurudumu la michezo.
  Picha ya pamoja ya viongozi wa mpira wachezaji wa timu ya vijana  sambamba na Mkurugenzi wa Michezo, Yusuph Omari.

Wachezaji watimu ya vijana wakiwa katika mazoezi leo wakati wa  uzinduzi wa kampeni maalumu za kuifanikisha Tanzania kushiriki michuano ijayo ya Olimpiki 2020.Picha na Zainab Nyamka.

MHANDISI MTIGUMWE AWAONDOA HOFU WATUMISHI KUHAMIA DODOMA

$
0
0
Mhandisi Mtigumwe ametoa kauli hiyo wakati wa kikao maalumu cha kuhusiana na uamuzi wa serikali kuhamia Makao Makuu ya Nchi mkoani Dodoma kilichokuwa na lengo la kujadili kwa pamoja namna ya utendaji kazi katika wizara hiyo sambamba na kutoa utaratibu utakavyokuwa kuelekea mjini Dodoma.

Mtigumwe amebainisha kuwa Awamu ya Kwanza ya uhamisho utawahusisha watumishi 88 kutoka Idara Kuu ya Mazao, ambapo katika mchakato huo watumishi 41 watahamia Dodoma kuanzia tarehe 14 – 15/2/2017 na wengine 47 waliobaki watahamia muda wowote katika kipindi cha kuanzia mwezi Februari hadi kufikia mwezi Juni.

Mtigumwe amewaeleza watumishi hao kuwa maandalizi ya ofisi za Wizara ya kilimo zilizopo mjini Dodoma zinaendelea vizuri na tayari baadhi ya maeneo yamekamilika huku mengine yakiendelea kukamilishwa ili kukidhi matakwa kwa ajili ya watumishi wote watakapohamia mjini Dodoma.

Uamuzi wa Watumishi wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi kuhamia mjini Dodoma ni kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuitaka Serikali yote kuhamia Dodoma ili kutekeleza uamuzi uliofikiwa tangia miaka ya 70 na Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutambua na kutangaza kuwa Dodoma ndio Makao Makuu ya Nchi.

Mhandisi Mtigumwe amebainisha hayo hii leo katika kikao cha pamoja na watumishi wa wizara ya kilimo katika Mkutano huo ulifanyika Makao Makuu ya Wizara hiyo Manispaa ya Temeke Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Mhandisi Mathew John Mtigumwe akisisitiza jambo wakati wa kikao cha pamoja na wafanyakazi wa wizara hiyo.

Watumishi wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi wakimsikiliza kwa makini Katibu mkuu wa wizara hiyo Mhe Mhandisi Methew Mtigumwe
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Mhandisi Mathew John Mtigumwe hii leo amewaondoa hofu watumishi wa wizara yake kuhusu zoezi la serikali kuhamia Dodoma kuwa litafuata misingi na stahili za watumishi kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa Umma.

WAZIRI MKUU AZITAKA HALMASHAURI ZIFANYE KAZI KWA WELEDI

$
0
0
Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa akihutubia leo wakati wa kufungua baraza la ushauri (RCC) Mkoa wa Dodoma ambapo lilishirikisha Wizara,Idara na Wadau mbalimbali wanaoratibu ujio wa Serikali kuhamia Makao makuu Dodoma Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Chuo cha mipango ya Maendeleo Vijijini Dodoma ( Picha na PMO)
WAZIRI MKUU Kassm Majaliwa amesema wakati umefika wa kuwa na watumishi wenye weledi wa kutosha kwenye Halmashauri zote nchini na pia hazitakiwi kuwa pango la wezi, wazembe au jalala la kutupa wabadhilifu walioshindikana kwingineko.

Aidha, Waziri Mkuu amesemma Serikali za Mitaa na Halmashauri zote nchini zinatakiwa zianze kujitathmini na kujipanga vizuri zaidi kuona ni kwa namna gani zitakuwa chachu ya maendeleo ya viwanda vinavyotarajiwa.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatatu, Januari 30, 2017) wakati akifungua Kikao cha Baraza la Mashauriano (RCC) mkoani Dodoma. Amesema kikao ni chombo muhimu na endapo kitatumika vizuri kitaweza kusaidia kusukuma maendeleo ya Mkoa na kupunguza migogoro kwenye Halmashauri.

Amesema Serikali itaendelea kuongeza kiwango cha ruzuku kwa Halmashauri zote nchini kwa kadiri uwezo utakavyoruhusu na kusisitiza kwamba fedha hizo lazima zisimamiwe vizuri na zielekezwe kwenye miradi ya maendeleo inayowagusa wananchi.

“Endapo itabainika kwamba kuna baadhi ya Sheria zinazokwamisha utendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, hatutasita kuzifanyia mapitio na hatimaye kuzibadili ili ziendane na azma yetu ya kutoa huduma bora kwa wananchi,” amesema.

Amesema Serikali ina maslahi makubwa kwa Serikali za Mitaa, sio tu kwa kuwa ni Serikali kamili katika ngazi hiyo, bali pia kutokana na ukweli kwamba kero nyingi za wananchi ziko katika ngazi hiyo.

Waziri Mkuu amesema vyanzo vingi vya mapato ya Serikali vinapatikana kwenye Halmashauri huku changamoto kubwa ikiwa ni kulegalega kwa  Halmashauri nyingi katika ukusanyaji wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi jambo linalozorotesha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hivyo Waziri Mkuu ametoa rai kwa Halmashauri hizo kuendelea kuboresha huduma kwa wananchi na kutatua kero zao kikamilifu na kwa wakati pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato.

Pia zihakikishe malipo yote yanafanyika kwa njia za kielektoniki na zihamasishe vijana na akina mama wajiunge kwenye vikundi vya uzalishaji mali na kuwapatia stadi za kazi na mikopo yenye masharti nafuu ili waweze kuwa chanzo cha mapato hapo baadaye.

Amesema watendaji wa Halmashauri wanatakiwa  kujiepusha na vitendo vya rushwa na ubadhilifu wa mali za umma na uzembe kazini na watakaobainika kufanya vitendo hivyo  wachukuliwe hatua kali za kisheria na kinidhamu.

“Someni taarifa ya CAG (Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali) na kutoa majibu ya kina ya namna mtakavyodhibiti mianya ya rushwa na ubadhilifu kama ilivyoainishwa kwenye ripoti hizo,” amesema.

Hata hivyo amesema kila Halmashauri iandae mpango wa utekelezaji wa Ilani ya CCM kwenye maeneo makubwa ya kipaumbele kama vile ujenzi wa miundombinu ya shule,  maboresho kwenye sekta ya afya (ujenzi wa hospitali, zahanati na vituo vya afya).

“Endeleeni kuwa na mahusiano mazuri miongoni mwenu, mfanye kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.  Kila mmoja kwa nafasi aliyonayo atimize wajibu wake na kuzingatia mipaka ya nafasi yake. Punguzeni migogoro, matusi, dharau, bezo na vitisho. Mshirikiane na jamii ione mpo wamoja,” amesema.

HATIMAYE NJIA YA RELI KATI YA DAR ES SALAAM NA RUVU YAFUNGULIWA !

$
0
0
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetoa taarifa kuwa kuanzia saa 9 alasiri leo Januari 30, 2017 njia ya reli kati ya Kituo Kikuu cha Dar es salaam na Ruvu imefunguliwa rasmi kwa shughuli za uendeshaji wa reli.

Taarifa hiyo imesema kuwa kazi ya ufunguaji njia imewezekana baada ya Wahandisi na Mafundi wa reli kuyaondoa Mabehewa yaliopata ajali l kutoka relini na pia kuikarabati sehemu iliyo haribika . Kazi hiyo imefanyika kuanzia usiku wa Januari 29, 2017 hadi mchana wa Januari 30, 2017.

Aidha treni ya abiria iliyoahirisha safari ya kuondoka kwenda bara jana imeondoka leo saa 9:05 alasiri kutoka kituo kikuu cha Dar es Salaam kwenda bara..

Wakati huo huo imefahamika kuwa msafiri mmoja aliyetambulikana kama Nd Basekena O. Bango kutoka Bujumbura Burundi akiwa anasafiri kutoka Kigoma amelazwa katika Hospitali ya Tumbi Kibaha mkoani wa Pwani kwa ajili ya matibabu zaidi. Aligunduliwa kuwa amechanika mguu wake wa kulia hivyo basi kuhitaji kushonwa mguu wake huo.

Taarifa kutoka Muhimbili zinaeleza kulazwa kwa majeruhi wawili waliopokelewa hospitalini hapo usiku wa Januari 29, 2017. Majeruhi wamefamika kuwa ni Nd. Stephania Mbona (46) kutoka Kigoma alikuwa amekuja Muhimbili kuendelea na matibabu ya ugonjwa wa tumbo, hata hivyo alitibiwa majeraha ya kawaida na anaendelea kulazwa kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wake wa tumbo.

Mgonjwa wa pili Nd Alice Jovin (37) mkazi wa Salasala Dar es Salaam alikuwa anatoka Kigoma kuja Dar es Salaam amepata majeraha ya kawadia ametibiwa na alitarajiwa kuruhusiwa leo asubuhi.

Kuhusu idadi ya wasafiri treni ya Deluxe yenye uwezo wa kusafirisha abiria zaidi ya 1000 wakati inapata ajali ilikuwa na abiria 480.

Aidha imefahamika kuwa ili kufahamika hasara na sababu za ajali hiyo taarifa rasmi itatolewa baada ya uchunguzi wa Kamati maalum inayoundwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za uendeshaji reli za kimataifa. Taarifa hiyo itatolewa baada ya wiki mbili.

 
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano:
Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Januari 30, 2017
DAR ES SALAAM
Share

SERIKALI YALAANI VIKALI MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUENDELEA KUCHOCHEA MGOGORO WA PORI TENGEFU LA LOLIONDO

$
0
0
Kundi la mifugo likiwa ndani ya Pori Tengefu la Loliondo, karibu kabisa na mpaka wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Picha na Lusungu Helela- Maliasili

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Waandishi wa habari jana  mjini Dodoma,  kuhusiana na  uchochezi unaofanywa na Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Loliondo na Ngorongoro ya kuwahimiza wananchi kuchunga, kulima na kukata miti katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo hali inayochangia kukausha  vyanzo maji yanayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.


Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii inalaani vikali uchochezi unaofanywa na Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Loliondo na Ngorongoro ya kuwahimiza wananchi kuchunga, kulima na kukata miti katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo hali inayochangia kukausha vyanzo maji yanayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

Akizungumza na Waandishi wa habari jana mjini Dodoma, Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amesema maelfu ya mifugo kutoka nchi jirani ya Kenya imekuwa ikiingizwa ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti muda wa saa 11 jioni, Amesema katika kukabiliana na changamoto ya uharibu wa chanzo kikuu cha maji ya Serengeti kwa asilimia 47.2 ya maji yote, tayari mifugo 1700 imeshakamatwa Mbali na mifugo hiyo.

Waziri Maghembe alisema kuwa maelfu ya Matrekta ya kutoka nchini Kenya yameletwa kulima katika maeneo yanayopakana na Serengeti Aliongeza kuwa hivi karibuni kilimo kimeshamiri ambapo kipindi cha nyuma wakazi walikuwa wanalima na ng’ombe (maksai) ila sasa matrekta ya Kenya yanalima na kufungua mashamba makubwa.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Maghembe ameagiza kuwa raia wa Kenya wenye mifugo Loliondo warudi makwao mara moja, Mkoa na Wilaya uchukue hatua kuwaondoa mara moja Pia, Matrekta yote ya nchi ya Kenya yawe na usajili wa kodi (Tax Clearance) toka TRA au yarudi kwao mara moja Aidha, ameagiza kuwa eneo la 1,5002km liwekewe alama mara moja na uwekaji alama ukamilike ifikapo tarehe 30 Machi, 2017. 

 Kwa upande wa Utalii, ameziagiza kampuni zote za utalii ambazo hazina usajili wa kitaifa zinazofanya biashara kwa mikataba ya vijiji ziripoti Wizarani ndani ya siku saba, Ikiwa pamoja na kuonyesha usajili wao, kuonyesha vitalu walivyopewa na Serikali pamoja kuiridhisha Serikali kama wanalipa kodi. 

 Awali, akizungumzia kuhusu mgogoro huo wa Pori Tengefu la Loliondo, Waziri Maghembe alisema anatambua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo anasimamia mazungumzo ya wadau wote ili kuleta utatuzi wa mgogoro huo. ‘’Nimeambiwa kuwa mwelekeo wa mazungumzo ni mzuri nahimiza mazungumzo yaendelee, lakini nimeona nikingoja hadi mazungumzo hayo yaishe Hifadhi ya Taifa ya Serengeti itakuwa haipo.’’ alisisitiza

Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images