Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

MPOGOLO AZINDUA MATEMBEZI YA UVCCM, ZANZIBAR LEO

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akizungumza kabla ya kuzindua matembezi ya UVCCM ya miaka 52 ya CCM, kwenye Viwanja vya Donge, Vijibeni, Wilaya ya Kaskazini Jimbo la Donge, mkoa wa Kaskazini Unguja.

Vijana wakihamasika na kuonyesha kuwa tayari kuanza matembezi ya UVCCM ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibara, baada ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, kutoa maneno yaliyoshiba nasaha, wakati wa hotuba yake ya kuzindua matembezi hayo leo.

Mpogolo akikabidhi picha ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere kwa mmoja wa viongozi wa matembezi hayo
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Lodrick Mpogolo (wanne kushoto-mstari wa mbele), akizindua matembezi ya UVCCM ya Miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kutembea na vijana hao kutoka kwenye Viwanja vya Donge, Vijibeni, Wilaya ya Kaskazini Jimbo la Donge, mkoa wa Kaskazini Unguja. Picha zote na Bashir Nkoromo. 


Matembezi yakaanza
.


Mpogolo akikabidhi picha ya Rais wa Zanzibar na Mweneyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein

Mpogolo akikabidhi picha ya Amirijeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli kwa mmoja wa viongozi wa matembezi hayo 
 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akisalimia baadhi ya viongozi wa UVCCM, baada ya kuwasili kwenye uzinduzi wa matembezi ya miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwenye Viwanja vya Donge, Vijibeni, Wilaya ya Kaskazini Jimbo la Donge, mkoa wa Kaskazini Unguja. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka na Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Khamis Juma.
Vijana wa Kikundi cha Sarakasi cha Mtimkavu wakionyesha uhodari wao wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo.
Vijana wa Kikundi cha Sarakasi cha Mtimkavu wakionyesha uhodari wao wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo.


Vijana wa Kikundi cha Sarakasi cha Mtimkavu wakionyesha uhodari wao wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo.
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM- Zanzibar Abdulghafar Idrisa Juma akitoa maneno ya utangulizi, wakati wa uzinduzi wa matembezi hao, leo
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka akimkaribisha Mwenyekiti wa UVCCM, kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara kuzindua matembezi hayo, leo.
Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini, Issa Juma Ame, akizungumza baada ya kukaribishwa na Mwenyekiti wa UVCCM, wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo, leo
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais, Mama Asha Balozi, Seif Ali Idi, akizungumza baada ya kukaribishwa na Mwenyekiti wa UVCCM kusalimia wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo, leo.

Mama Asha Balozi Seif, akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo sh. milioni tatu, kwa ajili ya kusaidia watakaokuwa matembezini, wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo, leo.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo, akimshukuru Mama Asha Balozi Seif, kwa kutoa msaada wa mchele na mafuta kwa ajili ya chakula cha vijana watakaoshiriki matembezi ya Miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar, wakati wa uzinduzi wa matembezi hayo leo.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo akimkabidhi mifuko ya saruji, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini, Issa Juma Ame wakati wa uzinduzi wa Matembezi hayo. saruji hiyo ambayo ni mifuko 100, imetolewa na UVCCM, kwa ajili ya ujenzi wa shule katika wilaya hiyo.

Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Khamis Juma akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo kuzindua matembezi hayo, leo.

Vijana wa Brass Bandi ya UVCCM, wakitumbuiza kumkaribisha Naibi Katibu Mkuu wa CCM-Bara kuzindua matembezi hayo.
PICHA ZAIDI ZA MATEMBEZI HAYO/>BOFYA HAPA

BODI YA FILAMU NCHINI YAWAOMBA WATANZANIA KUZIPIGIA KURA FILAMU ZA KITANZANIA KWENYE TUZO ZA AMVA 2017

$
0
0
BMGHabari
Bodi ya Filamu nchini imewahamasisha watanzania kuongera ari ya kuzipigia kura filamu za kitanzania zinazowania tuzo za Africa Magic Viewers Awards (AMVA 2017) za nchini Nigeria.

Katibu Mtendaji wa bodi hiyo, Bi Joyce Fissoo (pichani juu) ametoa hamasa hiyo hii leo, wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Power Break Fast On Saturday kinachoendeshwa na watangazaji Philip Mwihava na Godfrey Kusolwa.

“Filamu hizo ni Naomba Niseme, Aisha na Home Coming ambazo zinawania tuzo za filamu bora na Siri ya Mtungi ambayo inagombea filamu bora ya lugha ya Kiswahili. Niwaase Wanzania, ushindi wa filamu hizi ni sisi kuwapigia kura hawa vijana wetu ambao wameshika bendera yetu kwenda kutuwakilisha kule Nigeria, niwasihi waweze kuzipigia kura na wahakikishe wanahamasisha marafiki zao pia kuzipigia kura ili nafasi zote tuzo zije Tanzania”. Amesisitiza Fissoo.
Naye Mtayarishaji wa filamu nchini, Staphord Kihole (pichani) ambaye pia alikuwa kwenye kipindi hicho, ametumia fursa hiyo kuwaomba watanzania kuzipigia kura filamu za kitanzania ili zishinde tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards ikiwemo filamu yake ya "Naomba Niseme" inayowania vipengele viwili, kikiwemo kipendele cha Best East Africa na Best All Africa kinachoamuliwa na majaji.

Ili kuzipigia kura filamu za Tanzania ambazo ni Naomba Niseme, Aisha na Home Coming, unapakua Application ya We Chat, unajisajiri kwenye Africa Magic kwa kutumia nambari ya simu na kisha unatafuta kipengele cha AMVCA na utaweza kupiga kura kadri upendavyo ambapo mtu mmoja anaweza kupiga kura hadi 100 kwenye filamu tofauti tofauti.

WAZIRI MKUU ATAKA TANCOAL ITIMIZE MASHARTI YA MKATABA MGODI WA NGAKA

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka kampuni ya TANCOAL Energy inayochimba makaa ya mawe kwenye mgodi wa Ngaka itimize masharti ya mkataba iliouingia na Serikali mwaka 2008.

Kampuni ya TANCOAL iliundwa Aprili 3, 2008 na kampuni tanzu ya Atomic Resources Limited ambayo wakati huo ilikuwa ikijulikana kama Pacific Corporation East Africa (PCEA) na kwa sasa inaitwa Intra Energy (T) Limited ambayo hisa zake ni asilimia 70 na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) lenye asilimia 30 ya hisa.

Ametoa kauli hiyo jana mchana (Ijumaa, Januari 6, 2017) mara baada ya kutembelea mgodi huo na kukagua shughuli za uzalishaji. Mgodi wa Ngaka uko wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma na unamilikiwa na kampuni ya TANCOAL kwa ubia baina ya Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) na kampuni ya Intra Energy Corporation ya Australia.

Kwa mujibu wa mkataba huo, ilikubaliwa kwamba mbali ya kuzalisha makaa ya mawe, kampuni hiyo ilipaswa kuzalisha umeme wa megawati 400 kutokana na makaa hayo. TANCOAL ina migodi miwili; Mbalawala na Mbuyura ambao umetengwa mahsusi kwa ajili ya kuzalisha umeme.

“Kwenye mkataba tulikubaliana kuwa mtazalisha umeme lakini hadi hadi leo hamjaanza mnadai kuwa TANESCO wanawachelewesha. Nitafuatilia nione kama ni wao au la ili tujue ukweli,” alisema.

Kwa mujibu wa mikataba huo, TANCOAL ilipaswa kugharamia dola za Marekani milioni 14.49 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja ili kuwezesha malori makubwa na madogo yaweze kufika mgodini na kusomba makaa hayo.

“Mlisema mngetengeneza barabara lakini hadi sasa bado hamjafanya hivyo na ndiyo maana malori yanaishia kule. Yangefika hapa moja kwa moja, mngeweza kubaini kwa urahisi mahitaji ya makaa ya mawe ni kiasi gani,” alisema Waziri Mkuu.

Hivi sasa, malori ya kutoka mgodini yanashusha makaa yaliyochimbwa kwenye eneo lililokodishwa na TANCOAL la Amani Makolo ambalo liko umbali wa km.55 kutoka mgodini na malori makubwa yanapakia makaa hayo kutoka kwenye eneo hilo jambo ambalo linazidisha gharama za usafirishaji.

Kwa mujibu wa mkataba huo, TANCOAL ilipaswa kuwekeza mtaji wa Dola za Marekani milioni 82 lakini hadi sasa imewekeza kiasi cha dola milioni 14 ambazo ni sawa na asilimia 12 tu ya ahadi iliyotolewa.

“Makubaliano yalikuwa ninyi mtawekeza Dola za Marekani milioni 81.69 lakini hadi sasa mmetumia dola za Marekani milioni 14, hamjafikia hata nusu,” alisema Waziri Mkuu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemtaka Mwenyekiti wa Bodi ya NDC, Dk. Samuel Nyantahe afuatilie kwa makini mambo yanayoendelea ndani ya shirika hilo. “Wewe unaendesha vikao lakini haya ndiyo mambo yanayoendelea kwenye taasisi unayoiongoza,” alisema.

Alimtaka afuatilie pia uwasilishaji wa mkataba huo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili vipengele vinavyoibana NDC kiuendeshaji na kupata gawio viweze kuangaliwa upya.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewapongeza viongozi wa kampuni ya TANCOAL kwa kuwashirikisha wajasiriamali wadogo kupata teknolojia ambayo itasaidia kupunguza tatizo la ukataji miti kwa matumizi ya kuni na mkaa.

Alisema mgodi huo umeanza kuwanufaisha wenyeji kwani ameona kazi nzuri inayofanywa na kikundi cha akinamama cha Mbalawala (mbalawala Women Group) ambacho kinatumia vumbi la makaa hayo (ambayo ni mabaki) kutengeneza mkaa wa kupikia majumbani (briquettes).

“Hii teknolojia ikisambazwa kwenye shule, mahospitali na kwenye magereza itasaidia kupunguza matumizi makubwa ya kuni yanayofanywa na taasisi hizi,” alisema.

Meneja wa kikundi hicho, Bibi Leah Kayombo alisema wanatumia chengachenga na vumbi la makaa hayo kwa kuchanganya na kemikali nyingine ili kupunguza joto halisi la makaa hayo, jambo linalowezesha mkaa huo kutumika majumbani bila kuharibu masufuria.


IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMAMOSI, JANUARI 7, 2017.

Diwani wa CHADEMA Kata ya Tanga Manispa ya Songea mkoani Ruvuma ajiunga na CCM

$
0
0
Aliyekuwa mwana chama wa Chadema na Diwani wa Kata ya Tanga Manispa ya Songea na Mwenyekiti wa Wawanafunzi katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu John kilichopo Songea, Musa Ndomba arudi CCM. Kufuatia maamuzi hayo, mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemkabidhi Ndomba kadi ya CCM na shughuli hiyo imefanyika katika ukumbi wa CCM mkoani Ruvuma

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 8, 2017

Timu ya kuchunguza chanzo cha moto soko kuu la Kayanga yaundwa

$
0
0
 Katibu tawala Mkoa wa Kagera Kamishina, Diwani Athumani akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, Adeodata Agustine juu ya janga la moto katika soko kuu la Kayanga alipotembelea soko hilo kujionea athari za moto tarehe 7 Januari 2017.
Katibu tawala Mkoa wa Kagera Kamishina, Diwani Athumani (katikati) akipata maelezo ya uratibu wa majanga kutoka kwa  Mkurugenzi Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brg. Jen. Mbazi Msuya wakati alipotembelea soko hilo kujionea athari za moto tarehe 7 Januari 2017 (kushoto) ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, Adeodata Agustine.(PICHA ZOTE NA OFFISI YA WAZIRI MKUU)
 Baadhi ya Wafanyabiashara wa mazao ya nafaka wakipakia mabaki ya mazao  yao baada ya vibanda vyao vya biashara kuungua moto kufuatia moto uliozuka usiku wa saa 9:00 usiku wa tarehe 7Januari, 2017,  na kuteketeza sehemu ya soko kuu la Kayanga wilayani Karagwe kwa mara ya pili ikiwa limewahi kuungua tarehe 11 Machi 2016.
 Muuonekano wa Soko Kuu la Kayanga  baada ya vibanda  vya baadhi ya wafanyabiashara kuungua moto kufuatia moto uliozuka usiku wa saa 9:00 usiku wa tarehe 7 Januari, 2017, ikiwa soko hilo limewahi kuungua tarehe 11 Machi 2016.

 
Na Mwandishi wetu.
Kufuatia kuungua kwa mara ya pili kwa soko kuu la kayanga katika Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, Ofisi ya Mkuu wa mkoa Kagera imeiagiza Halmashauri hiyo kuunda timu mara moja na kuanza uchunguzi wa chanzo cha moto huo katika soko hilo, ambalo kwa mara ya kwanza liliungua  tarehe 11 Machi, 2016.

Sehemu ya soko kuu la Kayanga imeungua usiku wa kuamkia tarehe 7 Januari, 2017, saa 9:00 usiku, ambapo vibanda 52 vilivyojengwa kwa mbao na meza 24 za wafanyabashara wadogowadogo wa nafaka, matunda na mbogamboga vimeteketea kwa moto pamoja na mali za wamachinga waliokuwa wanapanga chini wapatao 33 nao mali zao zimeteketea kwa moto.

Akiongea mara baada  ya kukagua athari za janga la moto katika soko hilo Katibu tawala wa Mkoa wa Kagera Kamishina Diwani Athumani, leo tarehe 7 Januari, 2017,  na kuteketeza sehemu ya soko kuu la Kayanga wilayani Karagwe kwa mara ya pili ikiwa limewahi kuungua, amebainisha kuwa tayari Halmashauri ya wilaya hiyo imeshatekeleza maelekezo yao ya kuunda timu ya uchunguzi ambayo inaanza kutekeleza majukumu yake kesho, tarehe 8 Januari, kwa muda wa siku nne.

“Tumeunda timu tujue kwa nini hili soko linakuwa na majanga ya moto ya mara kwa mara, nawaomba wananchi wote wa Kayanga toweni ushirikiano wa kutosha kwa timu hii na yeyote mwenye taarifa ya chanzo cha moto awasilishe taarifa zake kwenye kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hii”  Alisisitiza Athumani.
Aidha, Athumani alifafanua kuwa yeyeyote atakaye bainika kuwa ndo chanzo cha kusababisha majanaga ya moto kutokea mara kwa mara katika soko  hilo hatua stahiki zitachukuliwa kwa kuwa  kuungua kwa soko hilo kumekuwa kusababisha hasara kubwa kwa wafanyabiara wa soko hilo.
Akiongea wakati wa ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Adeodata  Agustine, amefafanua kuwa thamani ya awali ya mali iliyoteketea inakisiwa kuwa Tsh, 80,000,000/= (mazao ya nafaka, mbogamboga , matunda pamoja na nguo na bidhaa za dukani), na thamani ya vibanda ni Tsh, 52,000,000/= na meza ni 9,600, 000/=.

“Chanzo cha moto hadi sasa hakijajulikana na kikosi cha zimamoto kwa kushirikiana na na Polisi na TANESCO wanaendelea na uchunguzi, taarifa hii ni ya awali tutapata taarifa kamili ya thamani ya mali na chanzo cha  janga la moto baada ya timu kukamilisha kazi kwa muda uliopangwa” alisema Adeodata.

Naye mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Soko kuu la Kayanga, Wilton William, aliishukuru halmashauri hiyo kwa juhudi walizo zifanya za kuzima moto huo pamoja na hatua walizozichukua za kuchunguza chanzo cha moto huo amabao umeunguza soko hilo kwa mara ya pili mfululizo.

Soko la Kayanga lina jumla ya vibanda 257, ambapo  vibanda 122  vimejengwa kwa matofari, na vibanda 135 vimejengwa kwa mbaao.  Katika tukio la janaga la moto la mwaka jana vibanda 117 ikiwa  ni viband 83 vya mbaao na 34 vya tofari viliteketea kwa moto.

MKURUGENZI MALINYI AJITOLEA KUMSOMESHA MWANAFUNZI ALIYEOLEWA KABLA YA MATOKEO YA DARASA LA SABA

$
0
0
Dotto Charles Heka (13) aliyekuwa Mwanafunzi wa shule ya msingi Lupungu wilayani Malinyi hatimaye amefufua ndoto zake za kuendelea na elimu ya sekondari.

Awali baada ya kuhitimu elimu ya msingi tu wazazi wake walimshinikiza na kumlazimisha aolewe pasipo yeye mwenyewe kuridhia kuishi na mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Masenga, kama mme na mke, akielezea kwa uchungu mbele ya Mkurugenzi wa wilaya ya Malinyi ndugu Marcelin Ndimbwa, Afisa elimu wa wilaya Kalagila Silivesta na mwanasheria Sospeter Kalekwa, mwanafunzi Doto Charles Heka anasema,kwakuwa hakupata kuungwa mkono na hata mmoja wa wazazi na ndugu zake alikubali kuoelewa hivyo hivyo. 

Baada ya matokeo kutoka baadhi ya wasamaria wema waligundua kwamba amefaulu na amechaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya kutwa ya Ngoheranga na kuamua kutoa taarifa wilayani iliyopelekea mkurugenzi kulivalia njuga jambo hilo na baada ya kujiridhisha aliweka mtego na jeshi la polisi lilifanikiwa kumkamata baba wa mtoto na kumchukua mtoto huyo ambaye mpaka sasa bado yupo chini ya uangalizi wake mkurugenzi na mtoto anaishi kwa mwalimu, akisubilia kufunguliwa kwa shule . 

Mbali na hayo yote pia Mkurugenzi ameamua kujitolea kumsomesha mwanafunzi huyo kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita na amemwomba afisa elimu mkoa amtafutie nafasi ya shule ya bweni huku Ndugu Masenga aliyetoroka akiendelea kutafutwa na jeshi la polisi na kuhakikisha anatiwa nguvuni na sheria kuchukua mkondo wake na kuwa onyo na somo kwa wengine wote wenye mawazo na tabia za namna hizo ndani ya halmashauri yake. Aidha mkurugenzi amewapongeza maafisa elimu, watumishi wa halmashauri hiyo pamoja na wasamaria wema waliotoa ushirikiano na kumnusuru binti huyo. Mungu atawalipa kwa haya mliyomtendea malaika wake Dotto.

DC BUHIGWE KANALI GAGUTI AWATAKA WAKUU WA SHULE KUTUNZA MADAWATI WANAYOPEWA NA KUKOMESHA UTORO WA WANAFUNZI WILAYANI HUMO

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti  akikabidhi madawati 1600 kwa wakuu wa Shule 50 zilizokuwa na upungufu wa madawati katika Shule ya Msingi Buhigwe
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti  akikabidhi madawati 1600 kwa wakuu wa Shule 50 zilizokuwa na upungufu wa madawati katika Shule ya Msingi Buhigwe.

 Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti  akizungumza na baadhi ya waalimu hao kabla ya kuwakabidhi madawati 1600 kwa wakuu wa Shule 50 zilizokuwa na upungufu wa madawati katika Shule ya Msingi Buhigwe.


Na Rhoda Ezekiel- Globu ya Jamii ,Kigoma,

Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marco Gaguti amewataka Wakuu wa Shule Wilayani humo pamoja na Wazazi kuhakikisha wanatunza madawati waliyo kabidhiwa pamoja na kukomesha utoro wa Wananafunzi. Aidha, aliwataka Kuhakikisha ufaulu wa Wanafunzi unaongezeka kutoka asilimia 74.3 kufikia asilimia 84% kutokana na Miundombinu ya kufundishia kuboreshwa ikiwa ni pamoja na kutatua suala la upungufu wa madawati.

Rai hiyo aliitoa jana wakati akikabidhi madawati 1600 kwa wakuu wa Shule 50 zilizokuwa na upungufu wa madawati katika Shule ya Msingi Buhigwe ambapo aliwaomba kuhakikisha wanayalinda madawati hayo yasiharibiwe pamoja na kuhakikishi wanafunzi wote wanahudhuria Shuleni kwasababu changamoto kubwa iliyokuwa ikichangia elimu kushuka ni pamoja na wanafunzi kukaa chini na utoro wa wanafunzi suala ambalo limetafutiwa ufumbuzi.

Gaguti alisema pamoja na kero hiyo ya ukosefu wa madawati kutatuliwa, Serikali imejipanga kila mwanafunzi kupata elimu bora na inayo stahili; hivyo ni jukumu la wazazi kwa kushirikiana na walimu kuhakikisha wanafunzi wanapata malezi mazuri na kuwahimiza watoto kuhudhuria shuleni ilikuweza kusoma kwa juhudi na waweze kufaulu.

Aidha Kanali Gaguti aliwataka wakuu wa shule kuweka malengo ya kupandisha ufaulu ili wilaya iweze kujipima kutoka asilimia 74.33% mwaka jana na kupanda hadi kufikia asilimia 84.3% ikiwa ndio njia sahihi ya kutathimini kama jitihada za Serikali zimefanikiwa na malengo yamefikiwa.

"Niwashukuru Wadau wote walio jitokeza kuchangia madawati katika Wilaya yetu, na Wananchi kwa kufanikisha jukumu hili. Mwitikio wenu ni ishara ya uzalendo kwa Nchi yenu na kutambua dhana ya maendeleo ya kweli ni lazima Wananchi washirikishwe. Aidha,dhana na mawazo ya Serikali kufanya kila kitu imepitwa na wakati hivyo nimefurahishwa sana na Wananchi wa Buhigwe kujitoa katika suala hili",alisema Gaguti.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Anosta Nyamoga alisema wakati zoezi la utengenezaji wa madawati linaanza uhitaji ulikuwa ni madawati 18896 na madawati yaliyo kuwepo ni 7908, awamu ya kwanza yalipatikana madawati 9156 upungufu ukawa madawati 1832 siku chache zilizo pita Wilaya imekamilisha zoezi hill kwa asilimia 100% na yamekabidhiwa katika shule 88 za Wilaya hiyo.

Nyamoga aliwapongeza Wananchi pamoja na Mkuu wa Wilaya kwa juhudi alizo zifanya za kuwashawishi watu na taasisi mbalimbali kichangia madawati kwa kiasi kikubwa na kuhakikisha hadi sasa tatizo hilo linatatuliwa na kukamilika kwa Wakati na Wanfunzi wetu wataendelea kupata elimu nzuri .

Akisoma Risala kwa niaba ya Wakuu wa Shule Kaimu Afisa elimu Wilaya ya Buhigwe Issa Kambi alisema katika kuunga mkono juhudi za serikali walijitahidi kuwahimiza Wananchi kuchangia madawati ambapo Wananchi walichangia madawati 430 kwa vijiji vyote na mengine kutolewa na serikali pamoja na wadau wengine na kukamilisha idadi ya madawati iliyo hitajika.

Alisema watahakikisha Miondombinu ya serikali inalindwa kwa kuweka sheria kali kwa watakao sababisha uharibifu na kuhakikisha wanafunzi wote wanahudhuria ili kupunguza utoro na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wote.

WAZIRI CASTICO AWEKA JIWE LA MSINGI NYUMBA ZA WAFANYAKAZI WA HOSPITALI YA MAKUNDUCHU

$
0
0
Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Maudline Castico akifungua pazia kuashiria uwekaji wa Jiwe la msingi la nyumba za wafanyakazi wa Hospitali ya Makunduchi, Mkoa Kusini Unguja ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 53 ya Mpinduzi ya Zanzibar.
Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Idrissa Muslim Hija akizungumza na wananchi wa Makunduchi baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la katika la nyumba za wafanyanyakazi wa Hospitali hiyo, wa tatu (kushoto) Naibu Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman.
Baadhi ya wananchi wa Makunduchi na vijiji jirani waliohudhuria uwekaji wa jiwe la msingi la nyumba za wafanyakazi wa Hospitali ya kijiji hicho wakimshangiria mgeni rasmi katika sherehe hiyo.
Picha ya pamoja Waziri Maudline Castico na baadhi ya viongozi wa Mkoa Kusini Unguja na Wizara ya Afya baada ya sherehe za kuweka jiwe la msingi la nyumba zawafanyakazi wa Hospitali ya Makunduchi.

Picha na Makame Mshenga/Maelezo Znz.

MBUNGE AGOMA KUWASAIDIA POLISI KISA KWANINI HAWAMPIGII SALUTI

$
0
0

 MBUNGE wa Kilombero, Peter Lijualikali kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amemueleza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba , kuwa hayupo tayari kutoa fedha za Mfuko wa Jimbo kuchangia kazi za maendeleo ya Polisi jimboni humo.
Amesema hawezi kufanya hivyo, kwa sababu Polisi wa jimbo lake hawamtii na wanashindwa kumpigia saluti.
Lijualikali aliweka bayana msimamo huo wakati akizungumzia changamoto mbalimbali kwa waziri huyo, kabla ya kupanda jukwaani kuwahutubia mamia ya wananchi waliojitokeza mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Ifakara.
Mbunge huyo alisema. “ Huu ni ugeni wa kwanza wa hadhi ya kitaifa kuja kwenye jimbo hili kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara… sasa tufanye kazi ya kujenga taifa letu badala ya kuendeleza siasa”.
Mbunge huyo alimuomba waziri huyo wa mambo ya ndani, atoe majawabu mbele ya mkutano huo ikiwa ni pamoja na suala la bodaboda kufukuzana na polisi na dawa za kulevya. Pia, Lijualikali alihoji kwa nini polisi wa Ifakara katika Jimbo la Kilombero, hawampigii saluti wakati yenye ni mbunge .
“Hii ni hoja ya bungeni… mbunge kupigiwa saluti, lakini Polisi wa Ifakara hawanipigii saluti,” alisema Lijualikali, akimuarifu waziri huyo mwenye dhamana na jeshi la polisi.
Hivyo, alisema hawezi kuhamasisha uchagiaji wa ujenzi wa vituo vya polisi au kutoa fedha za Mfuko wa Jimbo kwenda kusaidia juhudi za ujenzi wa vituo hivyo.
Mbunge huyo alimuomba waziri kuwa kituo cha sasa cha polisi, kihamishwe kutokana kilipo ni eneo linalokumbwa na mafuriko nyakati za masika hivyo kutofikika kirahisi. Kwa upande wake, Mwigulu alisema hoja hiyo ni ya kiutawala na kiutendaji zaidi na pia ni ya kuangalia historia ya wabunge waliomtangulia.

JAMBO LEO WALIVYOUPOKEA MWAKA MPYA 2017

$
0
0
 Wafanyakazi wa Gazeti la Jambo Leo linalochapishwa na Kampuni ya Quality Media Group Limited wakiwa na furaha wakati wa hafla ya kuukaribisha Mwaka Mpya 2017 kwenye Ukumbi wa Ground Zero, Kurasini Dar es Salaam juzi.
 Wakigongeana ikiwa ni ishara ya kutakiana heri ya Mwaka Mpya wa 2017
 Wakicheza kwa furaha muziki uliokuwa ukiporomoshwa wakati wa hafla hiyo
 Mwenyekiti wa Kamati ya hafla hiyo ambaye ni Mpiga Picha Mkuu wa gazeti hilo, Richard Mwaikenda akimtambulisha Mkurugenzi wa Gound Zero Lounge, Juma Pinto kwa madereva wa Kampuni Mama ya Quality Group Limited (QGL), Salumu (kushoto) na Ramadhan
 Mhariri Mtendaji wa gazeti la Jambo Leo, Anicetus Mwesa akisalimiana na Juma Pinto. Kushoto ni Mhariri Mwandamizi wa gazeti hilo, Leon Bahati.
 Wajumbe wa Kamati ya Sherehe hiyo wakijadiliana kuweka mambo sawa. Kutoka kushoto ni Zahoro Mlanzi, Grace Sima, Asha Kigundula na Neema Mgonja.
 Katibu wa Kamati ya Sehetrehe, Neema Mgonja (aliyesimama) akiwapa utaratibu wa maakuli wajumbe. Kutoka kushoto ni Mwnyekiti wa Kamati hiyo, Richard Mwaikenda, Grace Sima, Jemmah Makamba na Dalila Sharif
 Mhariri wa Habari wa Jambo Leo, Kachenje 9kulia0 akitaniana na Mhariri Mwandamizi, Frank Balile na Mhariri Mwandamizi wa Jambo Leo Wikiend, Said Mwishehe.
 Ni furaha kwa wote
 Sasa ni wakati wa msosi.

 Charity James na Charles Jemes wakiserebuka
 Ni msosi, vinywaji kwa kwenda mbele
 Mpigapicha wa gazeti la Jambo Leo, Janeth Shekunde akimlisha ndafu Asha Kigundula ambaye alikuwa mweka hazina wa kamati hiyo ilifanikisha sherehe hiyo
 Mpigapicha wa gazeti la Jambo Leo, Khamisi Mussa (kulia0 na Frank Balile wakila nyama choma ya mbuzi
 Chief Sub Editor wa Jambo Leo, Joseph Kulangwa akicheza muziki na Stelah Kessy  pamoja na Charity James
 Sasa ni wakati wa supu ya mbuzi
 Ni furaha, furaha, furahaaaaaaaa
 Mwaikenda akiwa na Jemmah Makamba (katikati) pamoja na Dalila Sharif
 Baadhi ya waandishi wa kike wa Jambo Leo wakiwa na sura zenye bashaha wakati wa hesrehe hiyo
 Sasa ni mwendo mdundo
 Mhariri Mtendaji wa Jambo Leo, Mwess (katikati) akifurahi na baadhi ya waandishi wa habari wa gazeti hilo
 Mmoja wa Wakurugenzi wa Ground Zero Lounge, Benny Kisaka akisalimiana na Mhariri wa Jambo Leo, Kachenje. Kushoto ni Mhariri Mwandamizi wa gazeti hilo, Mashaka Mgeta na Kulangwa.
 Maakuli, maakuli, maakuli
 Mwesa na Bahati wakiwa na furaha
 Mwaikenda akiserebuka na Jemmah
 Kachenje na Charity ni muziki tu
Wasanifu kurasa wa gazeti hilo wakipata supu ya mbuzi. Kutoka kulia ni Grace Sima, Robert na Khamisi Kumbuka

TANZIA

$
0
0
Familia ya marehemu Julius Dunstan Mganga wa 21 Ali Hassan Mwinyi Road (Old Bagamoyo Rd),Dar es salaam, wanasikitika kutangaza kifo cha mama yao mpendwa Flora Agnes Mganga kilichotokea tarehe 7 Januari 2017 katika hospital ya Muhimbili, Dar es Salaam.

Mazishi yatafanyika siku ya jumanne Tarehe 10 Januari,2017 kama ifuatavyo:

5.00 - 7.00 Mchana heshima za mwisho nyumba kwa marehemu 21 Ali Hassan Mwinyi Road,Dar es salaam
8.00 - 9.30 Misa St. Peters church Oysterbay
10.00 Mazishi makaburi ya Kinondoni

Raha ya milele umpe eeh Bwana na Mwanga wa milele umwangazie, apumzike kwa amani,AMINA




WAZIRI MKUU AAGIZA MAAFISA WANNE WAKAMATWE

$
0
0
Watuhumiwa wakipelekwa kupanda gari la polisi kwa ajili yakuwapeleka rumande
Kaimu Meneja wa Mamcu bwana Kelvin Rajabu akipanda gari la polisi tayari kwakwenda rumande.Picha na Chris Mfinanga 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimuhoji Kaimu Meneja mkuu wa chama kikuu cha ushirika Masasi Mtwara (MAMCU) Bwana Kelvin Rajabu kuhusiana na upotevu wa koroshozaidi ya tani 2000 Waziri mkuu alifanya kikao na Bodi ya korosho pamoja na baadhi ya wanaushirika Mamcu kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano Ikulu ndogo Mkoani Ruvuma
Kamanda wa polisi mkoani Ruvuma Zuberi Mwombeji akiwatarifu Maofisa wa Mamcu na Yurap wako chini ya ulinzi wa polisi kuhusiana na upotevu wa korosho tani 2000 kulia mwenye kaunda suti Kaimu meneja mamcu Bwana Kelvin Rajabu anayefuatia Mkurugenzi wa YURAP inayojishughulisha nauhifadhi korosho katika Ghala la BUCO Masasi Bwana Yusuf Namkula anayefuatia Mkurugenzi mwenzake Bwana Ramadhan Nama na Meneja tawi la Mamcu Bwana Lawrence Njozi

*Ni kwa tuhuma za uzembe na upotevu korosho zaidi ya tani 2,000
* Wapelekwa Masasi chini ya ulinzi wakajibu tuhuma zinazowakabili

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Zuberi Mwombeji awakamate maafisa wanne na kuhakikisha wanapelekwa Masasi chini ya ulinzi ili wajibu tuhuma za upotevu wa tani 2, 138 za korosho.

Maafisa hao ni Kaimu Meneja Mkuu Chama Kikuu cha Ushirika cha Masasi (MAMCU), Bw. Kelvin Rajab na Meneja Tawi wa MAMCU, Bw. Lawrence Njozi. Wengine ni wakurugenzi wa kampuni ya YURAP ya Masasi inayohusika na uhifadhi wa mazao kwenye maghala, Bw. Yusuph Namkukula na Bw. Ramadhani Namakweto.

Waziri Mkuu alifikia uamuzi huo kwenye kikao alichokiitisha Songea mjini jana jioni (Jumamosi, Januari 7, 2017) baina ya watendaji kutoka Bodi ya Korosho Tanzania, MAMCU, wamiliki wa ghala la BUCO – Masasi na kikundi cha wakulima sita waliowawakilisha wenzao kutoka vyama vya msingi (AMCOS) za wilaya za Mtwara na Masasi.


Katika kikao hicho, Waziri Mkuu alitaka apatiwe maelezo ya kina ni wapi zilipo hizo tani 2,138 za korosho wakati taarifa waliyompatia viongozi hao jana inaonyesha kuwa waliuza korosho zote na hakuna hata kilo moja ambayo haijanunuliwa katika mnada wa tano uliofanyika Novemba 10, mwaka jana.

Kaimu Meneja Mkuu wa MAMCU, Bw. Kelvin Rajab alikiri mbele ya Waziri Mkuu kwamba korosho zote ziliuzwa na zilishalipwa an wanunuzi wa mnda wa tano lakini akadai hakupewa taarifa ya kukosekana kwa kiasi hicho cha korosho. Naye mmiliki wa ghala la BUCO, Bw. Ramadhan Namakweto alikiri kupokelewa kwa korosho hizo ghalani kwake lakini akashindwa kutoa maelezo ni kwa nini hazionekani zilipo.

“Tangu mnada wa tano, mmekwishafanya minada mingine mitano hadi kufikia mnada wa 10. Kama kweli hizo korosho zipo ghalani, ni kwa nini korosho za hawa wakulima hazijatolewa ghalani na kuuzwa katika minada iliyofuata huku taarifa yenu ya fedha kuwa mlishazipokea na kuziuza?” alihoji Waziri Mkuu bila kupata majibu ya kueleweka.

Tuhuma zinazowakabili maafisa hao wanne ni kuwalipa kilo pungufu ya zile zilizowasilishwa ghalani, wakulima wa korosho katika wilaya ya Masasi na kutowapa maelezo yoyote juu ya upungufu huo. Mfano ni kufanya makato ya unyaufu kwa wakulima wa chama cha msingi CHAMALI kinyume na maagizo ya Serikali.

Nyingine ni kutowalipa fedha kwa wakati wakulima waliouza korosho kwenye mnada wa tano wa tarehe 10 Novemba 2016 na kutokutoa maelezo yoyote licha ya kuwa MAMCU ilishauza korosho hizo kwenye minada iliyofuatia na kupokea malipo.Nyingine ni kutopelekwa mnadani kwa makusudi kwa tani 2,138 za korosho zilizokuwa katika maghala ya Mtandi na BUCO tangu Novemba 11, mwka jana; kutokutolewa taarifa ya kuwepo korosho hizo kwa mamlaka husika na kuwasababishia hasara wananchi.

Tuhuma nyingine ni kushindwa kufuatilia malipo ya korosho ya tani 1,156,262 ambazo ziliuzwa kwenye mnada wa 10 uliofanyika Desemba 21, 2016. Korosho hizo zilinunuliwa na Maviga East Africa (tani 503,297); Machinga Transport (tani 104,200); Tastey (319,576) na Saweya Impex (tani (229,189).

Kutokana na mapungufu hayo, Waziri Mkuu aliagiza watu hao wapelekwe Masasi chini ya ulinzi ili uchunguzi ufanyike na pia amemuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) afanye ukaguzi wa hesabu za MAMCU na kujiridhisha kiasi cha korosho kilichonunuliwa; fedha zilizolipwa na kuingia akaunti za MAMCU; kiasi cha fedha zilizolipwa kwa vyama vya msingi na wananchi kwa ulinganifu na bei ya korosho kwa kila mnada husika.

Mapema, wakisoma risala yao kwa Waziri Mkuu, wakulima hao walisema wana kero nyingi sana kama vile kutolipwa fedha zao kwa wakati; kutoeleweka mahali zilipo korosho ambazo walishaziuza kwa MAMCU, kukatwa makato ya unyaufu ambayo Serikali ilikwishapiga marufuku na kutosikilizwa malalamiko yao na viongozi wa MAMCU pamoja na viongozi wa mkoa na wilaya.

“Makubaliano yalikuwa ni kwamba mkulima atapewa fedha yake siku sita baada ya mnada kufanyika lakini hivi sasa baadhi yetu tumeuza korosho tangu Oktoba, mwaka jana lakini hadi imefika Januari hii bado hatujalipwa. Pia kuna makato yaliyoondolewa kwenye mfumo, kwa mfano unyaufu lakini wao wameyaacha na unapoenda kuuza wanahesabu na kukukata kuwa utalipia gharama za unyaufu,” alisema msoma risala Bw. Sylvester Mtimbe ambaye pia ni mkulima kutoka AMCOS ya Chiungutwa.

Wakulima hao wa korosho kutoka Masasi mkoani Mtwara walikutana Januari 3, 2017 katika kijiji cha Chiungutwa na kuazimia kuwa wangeandamana hadi Dar es Salaam ili wawasilishe kilio chao kwa Waziri Mkuu au kwa Mheshimiwa Rais Dk. John Magufuli.

Kwa kutambua umbali uliopo kutoka Masasi hadi Dar es Salaam na kwamba yeye hakuwepo katika siku waliyopanga kwenda huko, Waziri Mkuu aliamua kuwaita wakulima hao wamfuate Songea ambako alikuwa na ziara ya kikazi ya siku nne.

IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMAPILI, JANUARI 8, 2017.

MNAJIMU HASSAN YAHYA HUSSEIN ATABIRI VIFO KWA VIONGOZI WA DINI, SIASA, WASANII, WANAHABARI MWAKA HUU,

$
0
0
Maalim Hassan Yahya Hussein akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo , kuhusu utabiri wake wa mambo mbalimbali yatakayotokea mwaka huu.PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Baadhi ya mabo aliyotabiri ni;Kutatokea kashfa kubwa sana ya ngono \au fumanizi itakayowahusu viongozi wa dini, siasa na wasanii maarufu itakayosababisha  viongozi hao kufedheheshwa  na kuanguka kabisa katika tasnia zao.

Mwaka huu pia kutakuwa na vifo vya viongozi wakubwa maarufu wa kisiasa  na kidini, kufa ghafla vifi hivyo vitatokana na msongo wa moyo na shinikizo la damu.

Mioto mingi mikubwa itatokea nchini na duniani.

Viongozi wakubwa wa upinzani duniani na Tanzania kurejea kwenye vyama walivyovihama.

Vifo vya vya ghafla vya wasanii maarufu dunianiani ikiwemo Tanzania vinaweza vikatokana na fumanizi kuuliwa au kuana wenyewe.

Wimbi kubwa la vifo viliwakumba wanahabari duniani 2016 vitaendelea mwaka huu  Ajali nyingi kuwakuta wanasiasa, watawala na viongozi wa dini katika mwaka huu.

GURU PLANE YAANDAA SEMA YA MAFUNZO YA KAZI KWA VITENDO KWA WAHITIMU WA VYUO VIKUU.

$
0
0
Mkurugenzi wa guru plane Nickosn Magezi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo

Na Antony John ,Globu ya Jamii

TASISI inayoshughulika na uandaaji wa Semina na Makongamano ya Mafunzo ya kazi kwa vitendo ya Guru Plane, imeandaa Semina ya kuwajengea uwezo vijana walio hitimu vyuo vikuu pamoja na vyuo mbalimbali ilikuepukana na tatizola ajira nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mkurugenzi mtendaji wa tasisi hiyo Nickosn Magezi amesema Vijana wengi ukumbwa na kizingiti cha changamoto ya uzoefu wa kazi wanapoingia katika soko la ajira.

Magezi amesema utafiti unaonyesha vijana wengi wanao hitimu vyuo vikuu na vyuo vingine Nchini wanakumbana na changamoto za kutopata ajira kutokana sababu ambazo zimekuwa zikitumiwa na waajiri wengini ni suala la wahitimu kukosa uzoefu wa kazi.

“ Semina hii itakuwana lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na kuwapatia uzoefu wahitimu wa vyuo mbalimbali kwa mafunzo ya vitendo hilo ndio lengo kubwa ya semina yetu” amesema Magezi.

Sanjari na hayo ameongeza kuwa semina ya mafunzo ya kazi kwa vitendo imeweza kutatua changamoto za ukosefu wa ajira hasa pale taasisi na makampuni zinapokuwa zimehakikishiwa uzoefu wa kazi unaoendana na soko la ajira.

DC WA BUHIGWE,KANALI GAGUTI AANDAA UTARATIBU WA KUPANDA MITI ZAIDI YA MILIONI MOJA KUPAMBANA NA TATIZO LA NYUMBA KUEZULIWA PAA

$
0
0

Na Rhoda Ezekiel-Globu ya Jamii Kigoma

MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti amewataka Wananchi Wa Wilaya ya Buhigwe kuzingatia kanuni za ujenzi kwa kujenga Nyumba zenye ubora na kupanda miti katika Nyumba zao ili kuepukana na majanga yatokanayo na Upepo mkali pamoja na Mvua kubwa zinazo endelea kunyesha na kusababisha madhara makubwa .

Akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Mnyegera ambapo upepo mkali ulitokea huko na kusababisha nyumba tisa kuezuliwa na kusababisha uharibifu wenye thamani ya Shilingi milioni 13 wakati akitembelea kuangalia uharibifu huo, Gaguti alisema nyumba nyingi zilizoezuliwa hazijajengwa kwa kuzingatia kanuni za ujenzi.

Gaguti alisema ili kuhakikisha tatizo hilo linakwisha Wilaya imeandaa utaratibu wa kupanda miti milioni moja na laki moja kwa Wilaya nzima na wananchi wote wanatakiwa kuzingatia utaratibu huo,Viongozi wa vijiji wanatakiwa kuzingatia zoezi hilo kila nyumba kupanda miti ya kutosha ili kuepukana na madhara ya kuharibikiwa Nyumba.

Aidha Gaguti aliwaomba viongozi wa kijiji kuwasaidia wote waliopatwa na majanga hayo kwa kipindi hiki ambacho serikali inatafuta namna ya kuwasaidia ili waweze kupata mahali pa kuzihifadhi familia zao.

"Poleni sana kwa majanga yaliyo wapata nimetembelea kote ambapo kimbunga kimeezua nyumba lakini hakuna majanga yaliyo tokea ya watu kupoteza maisha wala uharibifu wa mazao ni jambo la kumshukuru mungu kunabaadhi ya Bati zinaweza kutumika nahisi tasmini iliyofanyika inaweza kupungua, niwaombe tupande miti ilikujikinga na tatizo hili wakati tunasikitika kwa tukio lililojitokeza na niwaombe viongozi nione jitihada zenu kwa kuwasaidia sisi tutawasaidia kama Wilaya baada ya kuona juhudi zenu za kusaidiana",alisema Gaguti.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mnyegera Alfonce Ntatie alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 6 Januari, ambapo kulitokea upepo mkubwa ambao ulieezua nyumba tisa na Kusababisha uharibifu wa shilingi milioni 13 ambapo Mpaka sasa juhudi za kuwasaidia wathilika wa tukio hilo zinaendelea kufanyika na Wananchi wanaendelea kuwachangia wenzao. 

kwa upande wao Baadhi ya Wananchi walio haribiwa nyumba zao na upepo mkari walisema Mpaka sasa wanalazimika kulala nje na familia zao suala ambalo linawapa wakati mgumu hasa ukuzingatia wakati huu ni wakqti wa Mvua.zinaendelea kunyesha na zikinyesha wanalazimika kunyeshewa na watoto wao.
 Moja ya nyumba iliyoezuliwa paa kama ionekanavyo pichani.
  MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti akiratibu tukio la kuezuliwa paa baadhi ya nyumba za wakazi wa kijiji cha Mnyegera wilayani Buhingwe kufuatia upepo mkali uliotokea wilayani humo na kupelekea nyumba tisa kuezuliwa paa zake. 
 MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti akiwapa pole Wananchi wa kijiji cha Mnyegera wilayani Buhingwe kufuatia upepo mkali uliotokea na kusababisha nyumba tisa kuezuliwa na kusababisha uharibifu wenye thamani ya Shilingi milioni 13.
MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti akiwa pamoja na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Mnyegera wilayani Buhingwe waliothiriwa na  
upepo mkali uliotokea na kusababisha nyumba tisa kuezuliwa mapaa.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 9, 2017

Kenya, Get Ready For A New All Female Cast TV Talk Show Dubbed The Squad

$
0
0

“...the show is inspirational, fun, provocative and educational; it will give you nostalgic moments about hanging out with your favourite girls.” – The Squad


NAIROBI, December  9, 2017Kenya should brace itself for a first of its kind TV talk show that has an all female cast of the country’s hottest entertainment talent.
The TV show produced by Future Pics Studios, owned by Nice Githinji and Janet Kirina is titled The Squa. It boasts of a stellar cast of entertainers who are not afraid of tackling any issue however controversial or taboo it may be. They will make you re-evaluate your squad goals.

Directed by award winning actress and producer Janet Kirina, the show is inspirational, fun, provocative and educational; it will give you nostalgic moments about hanging out with your favourite girls.

“I'm not sure how original I can sound at this point, but darn, these ladies slay. I remember being nervous when the D.O. P, Eric Ndungu told me we can roll...after that I checked into a moment that I still can't explain. It was surreal. I ran and whispered to Nice, 'Babe, we're doing it'," said Janet. Nice adds, that the casting has been a game of musical chairs. At this point Janet and I had gotten used hearing "No".
Nice jokes, "Ladies walking away and refusing to work with us was the new version of "lit"."

That did not stop them from getting the most interesting mix of talent to work with.
The panel tackles day to day issues like weight gain and loss, careers and parenting, cyber bullying and online personas and much more.They speak what you think, but are afraid to say, they aren’t afraid to pull out their wigs and show what lies underneath.
 
The Squad will be airing every Thursday8pm on newly launched Ace TV.
Meet the squad....

NICE GITHINJI.
 Multiple award winning actor, director, producer, host and mentor, this lady needs no introduction. She is intelligent, witty and brutally honest. Her quick comebacks will catch you off guard and her strong sense of “self” will impress you. Most of all, you’ll enjoy her morbid sense of humor. 

CHANTELLE BLESSING.

This musician and actor, is a wife, mother and sister. Chantelle is a fun loving person who’s favourite topics include marriage & motherhood. She is passionate about ending violence against men and women and curbing female circumcision. Don’t be fooled by her smile though, because she hides her claws behind her gel manicured nails. Sweet, sassy and loyal to the bone.
 
LUCY MUTURI.
 
This health, fitness & wellness motivator is also a model, nutritionist and blogger. She is a self professed feminist and adds that she’s impatient, temperamental, confident, kind and quite humble. Her greatest desire is to help people; make an impact in someone’s life, change the world in any way she can. 

“Being part of The Squad is a dream come true, a platform by women for women” Lucy says, “I get to spend time with three other amazing ladies with totally different personalities which I think, is what makes the show even more interesting.”

ELLA CIIRU.
 Constantly evolving is one way to describe Ella. From marketing manager, to actress, to a blunt reality star that got tongues wagging by refusing to play dirty. This dynamic go getter lives to surprise herself as much as her audience..... 
What comes next only time will tell. Ladies let's get in formation.

MKUU WA MKOA WA RUKWA APIGA MARUFUKU KUPOKEA, KUINGIZA, KUIHAMISHA, KUSAFIRISHA NA KUPITISHA MIFUGO NDANI YA MKOA WA RUKWA

$
0
0
Mkuu wa mko wa Rukwa kamishna Mstaafu Zelote Stephen amewaagiza wakuu wa Wilaya kutokubali kupokea mifugo kutoka katika wilaya nyingine bila ya mifugo hiyo kuipa kibali maalum cha kuhamia katika wilaya zao.

Ameyasema hayo katika amri halali namba 1/2017 kuhusu kupokea, kuingiza, kuihamisha, kusafirisha na kupitisha mifugo ndani ya mkoa wa rukwa kwa mamlaka aliyopewa na kifungu cha 7 cha sheria Nambari 19 ya mwaka 1997 ya Tawala za Mikoa Sura Namba 97 mapitio ya mwaka 2002, kwa lengo la kusimamia na kutekeleza maagizo ya waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 2002 unaokataza kabisa usafirihaji kiholela wa mifugo.

“Mifugo isihamishwe kutoka katika Kijiji, Wilaya ama Mkoa kabla ya kupata kibali cha Kijiji, Wilaya ama Mkoa inakopelekwa. Hivyo Kijiji, Wilaya na Mkoa itatoa kwanza idhini ya kupokea mifugo hiyo ndipo kibali cha kusafirisha mifugo kitolewe,” Zelote Stephen alisema.

Zelote Stephen alisisitiza kuwa Vijiji, Wilaya na Mkoa usitoe vibali vya kupokea mifugo kabla ya kujiridhisha kwamba wanayo maeneo ya kutosha ya malisho ya mifugo, yaliyopimwa na kuthibitishwa na wataalamu kama yanafaa kwa malisho na maji ya kutosha na majosho ya kuoshea mifugo.

Vile vile Mkuu wa Mkoa aliwaagiga maafisa mifugo kuanzia ngazi ya Kijiji, Wilaya na Mkoa kusisimamia na kuhakikisha hakuna mifugo inayosafirishwa kutoka Kijiji, Wilaya na Mkoa kwenda Mkoa mwingine au kuingia katika Kijiji, Wilaya au Mkoa bila ya kupimwa na kuchanjwa chanjo lengo likiwa ni kuthibiti uenezaji wa magonjwa ya mifugo nchini.

“Kabla ya kutoa vibali vya kusafirisha mifugo, madaktari wa mifugo wa Wilaya ama wawakilishi wao wahakikishe kwamba mifugo inaogeshwa na kuchanjwa dawa za kuzuia magonjwa husika kabla ya kuiruhusu mifugo hiyo kusafirishwa ili kuzuia uenezaji wa magonjwa ya mifugo,” Zelote Stephen alifafanua.

Aidha Mkuu wa Mkoa amewatahadharisha maafisa mifugo ambao sio waaminifu wanaotumia njia ya kuingiza mifugo kwenye wilaya kwa njia ya biashara za minada na matokeo yake mifugo hiyo kubaki eneo husika bila ya kufuata taratibu zozote.

Amri hii itafanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia tarehe 9 January, 2017 hadi tarehe 31 Desemba, 2017.

Miji Sita ya Zanzibar Kufanyiwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi Ifikapo 2020

$
0
0
Na. Lilian Lundo – MAELEZO.

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inatarajia kukamilisha upangwaji wa matumizi ya ardhi kwa ajili ya maboresho ya  Miji Sita ifikapo 2020.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, Mhe. Salama Aboud Talib katika mahojiano na mwandishi wa habari hii kuhusu mafanikio ya Mkakati wa Matumizi ya Ardhi Zanzibar wa mwaka 2015.

Mhe. Salama amesema kuwa kumekuwa na mafanikio makubwa katika sekta ya  ardhi mara baada ya kuanzishwa kwa Idara ya Mipango Miji na Vijiji ambayo ilipelekea kuanzishwa kwa  mpango mkuu wa matumizi ya Ardhi uliosaidia kwenda kasi kwa shughuli za upangaji  wa matumizi ya ardhi ukilinganisha na miaka ya nyuma.

“Malengo ya Awamu ya Saba katika kupanga Miji ni kutengeneza mipango ya matumizi ya Ardhi (Master Plan) ya miji Mikuu miwili ambayo ni Zanzibar na Mji wa Chake-Chake na kufanya Mipango ya Maendeleo (Local Area Plan) ya miji midogo 14,” alifafanua Mhe. Salama.

Aliongeza kuwa kati ya miji Mikuu miwili, Mji wa Zanzibar umeshafanyiwa mipango ya matumizi ya ardhi na kati ya Miji 14, Miji 3 ya Nungwi, Chwaka na Mkokotoni imeshafanyiwa mipango yake.

Aidha amesema kuwa hadi kufikia mwaka 2020, Miji 6 itakuwa imefanyiwa mpango wa matumizi ya Ardhi. Aliitaja Miji hiyo kuwa ni Chake-Chake, Wete, Mkoa, Mkunduchi, Dunga na Mahonda.

Mhe. Salama amesema kuwa tangu  mwaka 1964 ni awamu hii ya saba ndiyo inayotoa kipaumbele katika masuala ya miji, ambapo taasisi maalum ya masuala ya miji imeundwa.

Pia kumekuwa na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi ya mwaka 1968 ambayo imepata nguvu tena kwa kurudisha dhana adhimu iliyotungwa baada ya Mapinduzi ya kuwa na kitovu cha mji “Ngambo Tuitakayo”.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images