Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

IBADA YA KRISTMASI YAFANYIKA KITAIFA MJINI BUKOBA KATIKA KANISA LA MWOKOZI KKKT LEO

$
0
0



Ibada ya Krismasi Kitaifa imefanyika katika kanisa la Mwokozi KKKT Mjini Bukoba huku viongozi wa dini wakitoa wito wa kudumishwa kwa amani na kuepuka vitendo vyovyote vya ubaguzi vinavyoweza kuwatenga wananchi.

Katika mahubiri hayo Askofu wa Dayosisi ya Ksikazini Magharibi Dokta Abednego Keshomshahara pia aliwataka wananchi kufanya kazi kwa bidii badala ya kutegemea mafanikio yanayotokana na miujiza badala ya kufanya kazi.


Ibada hiyo ilianza kwa maandamano yaliyoongozwa na Askofu huyo ambapo Jumuiya ya Kikristo Nchini iliwakilishwa na Moses Matonya aliyetoa wito wa kuendelea kudumisha amani na kusisitiza upendo miongoni mwa wananchi

Ibada hiyo ilitanguliwa ma maandamano


Kulia ni Mbunge wa Bukoba Mjini/ Chadema Bw. Wilfred Muganyizi Lwakatare
Waumini





Wanakwaya wakiimba Nyimbo za Kumsifu na Kumtukuza Bwana leo
Bw. Wilfred Muganyizi Lwakatare na Mkewe katika Misa hiyo iliyofanyika Kitaifa kwenye Kanisa la Mwokozi KKKT Mjini Bukoba.
Askofu Abedinego Keshomshahara wa Kanisa hilo la kirutherli Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Magharibiakiwasalimu na kuwapa Neno Waumini leo hii
Askofu Abedinego Keshomshahara akitoa neno
Askofu Moses Matonya akiwasalimu Waumini na pia alipata muda na kutoa wito wa kuendelea kudumisha Amani na kusisitiza upendo miongoni mwa Wananchi.
Mkuu wa Mkoa mpya wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salim Mustafa Kijuu akiwasalimia waumini katika kanisa la Mwokozi KKKT Mjini Bukoba mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo
Mkuu wa Mkoa mpya wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salim Mustafa Kijuu akiwasalimia waumini katika kanisa la Mwokozi KKKT Mjini Bukoba.
Waumini wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa.

WENGI WAJITOKEZA KWENYE MSIBA WA MPOKI BUKUKU TABATA

$
0
0
 Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania, Absalom Kibanda akimfariji mjane wa marehemu Mpoki Bukuku, Lilian nyumbani kwa marehemu, Tabata Bwawani, Dar es Salaam. Bukuku alifariki juzi baada ya kugongwa na gari Barabara ya Bagamoyo karibu na Kituo cha ITV, Mwenge. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Kibanda akimfariji mama mzazi wa marehemu Mpoki Bukuku
 Kiongozi wa Chama cha ACT, Zitto Kabwe (kulia) akizungumza jambo na Shemeji wa marehemu Mpoki Bukuku, Edwin Mjwahuzi alipokwenda kuwafariji wafiwa nyumbani kwa marehemu, Tabata Bwawani.
 Zitto Kabwe (kulia) akizungumza na kaka wa Marehemu Mpoki, Gwamaka Bukuku wakati wa msiba huo
 Waandishi wa habari wakiwa kwenye msiba wa marehemu Mpoki Bukuku ambaye alikuwa Mpigapicha mwandamizi wa magazeti ya Kampuni ya The Guardian
 Wanahabari wakijadiliana mambo wakati wa msiba huo

 Mmmiliki wa Blogu hii, Kamanda Richard Mwaikenda, ambaye pia ni Mpigapicha Mkuu wa gazeti la Jambo Lelo, Kamanda Richard Mwaikenda (kulia) akiwa na wanahabari wenzie kwenye msiba huo.Kutoka kushoto ni Mpigapicha wa Waziri Mkuu, Hilary Bujiku, Mmiliki wa Blog ya K-VIS, Khalfan Said, Mmiliki wa Blog ya Michuzi, ambaye pia ni Mpiga Piacha na Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais, Muhidini Issa Michuzi, Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Mwananchi, ambaye ni shemeji wa marehemu Mpoki, Edwin Mjwahuzi na Francis Chirwa ambaye ni mmoja wa viongozi wa Bodi ya Wahariri wa Gazeti la Raia Mwema. ,

 Waombolezaji wakiwa kwenye msiba




Jirani rafiki wa karibu wa marehemu, Mpoki, maarufu kwa jina la Mijisu  akilia wakati wa msiba

KANISA LA KKKT KIVULE DAR WAMPIGIA SALUTI YESU KRISTO IBADA YA KRISMASI

$
0
0
 Wanakwaya wa Vijana ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kivule, wakimpigia saluti Yesu Kristo walipokuwa wakiimba wimbo wa kumsifu Yesu wakati wa Ibada ya Krismasi.
 Mchungaji wa Kanisa la KKKT Mtaa wa Kivule, Dar es Salaam, Michael Mgaya akitoa mahubiri wakati wa Ibada ya Kuzaliwa Yesu Kristo ya Krismasi asubuhi
 Waumini wakiomba wakati wa ibada hiyo
 Waumini wakimwimbia Yesu Kristo
 Waumini wakiimba wimbo wa kumsifu Yesu Kristo




 Mwandishi wa Habari wa Kujitegemea, Spear Patrick  (kushoto) na mkewe wakishiriki kuimba wimbo wa kuzaliwa Yesu Kristo
 Lusekelo Mwaikenda (kushoto) ambaye ni Mtoto wa mmiliki wa Blog hii, Richard Mwaikenda akiwa miongoni mwa waumini akishiriki kuimba wimbo wakati wa Ibada ya Krismasi
 Waumini wakiomba

 Mwinjilisti Michael Mgaya (wa pili kushoto) akitoa neno alipokuwa akihitimisha Ibada ya Krismasi

 Waumini wakiondoka baada ya Ibada ya Krismasi kumalizika
Mpigapicha wa kupitegemea, Spear Patrick akipiga picha na familia yake pamoja na familia ya mmiliki wa blog hii, Richard Mwaikenda baada ya kumalizika kwa Ibada ya Krismasi

WATENDAJI IDARA YA UJENZI NATUMBO WANUSURIKA KUTUMBULIWA

$
0
0

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Said Jaffo akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Namtumbo Mkoani Ruvuma ambao hawaonekani katika picha.Picha na www.ruvumatv.com

IBADA MAALUMU YA KRISMASI, KANISA LA EAGT LUMALA MPYA LABARIKI WATOTO.

$
0
0
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola, hii leo Disemba 25, 2016 akihubiri kwenye ibada maalumu ya Krismasi ambayo imeenda sambamba na kubariki watoto ikiwa ni ishara njema katika siku hii ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Somo limetoka Kitabu cha Marko Mtakatifu 10:07.

Ibada hiyo pia imekuwa njema kwani Mhubiri wa Kimataifa, Josephine Miller kutoka Marekani amehitimisha mahubiri na mafundisho yake ya mwisho ya zaidi ya wiki moja (Disemba 19-Disemba 25) katika Kanisa hilo la EAGT Lumala Mpya.

Mchungaji Miller amefurahishwa na huduma katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya ambapo ametoa rai kwa waumini wote kumtumikia Mungu. Ameonya juu  ya wale wote wasiomwabudu Yesu Kristo aliye kufa na kufufuka na badala yake wanaabudu miungu wengine kwa mwamvuli wa dini kwa mnajiri ya kujipatia pesa. Somo limetoka Kitabu cha Matendo ya Mitume 01:11
Waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya wakifuatilia mahubiri kutoka kwa Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola.
Miongoni mwa watoto waliobarikiwa hii leo katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, wakiwa wamebebwa na wazazi/walezi wao
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola (kulia) pamoja na Mama Mchungaji, Mercy Kulola, wakiendelea na ibada ya kuwabariki watoto katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya hii leo.
Baadhi ya akina mama wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, wakiwa katika picha ya pamoja na Mchungaji Josephine Miller kutoka Marekani baada ya kumaliza mahubiri na mafndisho yake hii leo.
Akina mama wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, wakiwa katika picha ya pamoja na Mchungaji Josephine Miller kutoka Marekani baada ya kumaliza mahubiri na mafndisho yake
Mchungaji Josephine Miller kutoka Marekani akimtakia baraka njema George Binagi, mmoja wa waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya.
Baadhi ya vijana wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, wakiwa katika picha ya pamoja na Mchungaji Josephine Miller kutoka Marekani baada ya kumaliza mahubiri na mafndisho yake hii leo.
Mwimbaji wa nyimbo za Injili kutoka EAGT Lumala Mpya, Happy Shamawele, akitumbuiza kwenye ibada ya Krismasi katika kanisa hilo hii leo
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola (kushoto) pamoja na waumini wengine wakifuatilia ibada maalumu ya Krismasi hii leo
Mchungaji Josephine Miller (kushoto) kutoka Marekani pamoja na Mama Mchungaji Mercy Kulola (kulia) wakifuatilia ibada ya Krismasi hii leo
Happness Materego kutoka EAGT Lumala Mpya akifuatilia ibada
Waumini wa EAGT Lumala Mpya wakifuatilia ibada
Waumini wa EAGT Lumala Mpya wakifuatilia ibada ya Krismasi
Waumini wa EAGT Lumala Mpya wakifuatilia ibada ya Krismasi hii leo.
BMG inawatakia Krismasi Njema, Sherehekea kwa Amani na Utulivu kwa kuzaliwa Emmanuel (Yesu), Mungu pamoja nasi aliyeuokoa ulimwengu huu. Picha na Craty Cleophace wa EAGT Lumala Mpya.

MJENGO WA GHOROFA ALIOUACHA MPOKI BUKUKU TABATA DAR

$
0
0
 Nyumba ya ghorofa moja iliyopo Tabata Bwawani, Dar es Salaam, aliyoiacha aliyekuwa MpigaPicha Mwandamizi wa  The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku. Waliopo nje ni baadhi ya waombolezaji akiwemo Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe (katikati).PICHA NA RICHARD MWAIKENDA:KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Upande wa nyuma wa mjengo huo.

Profesa Muhongo asheherekea Krismasi kwa kufanya makubwa Musoma Vijijini

$
0
0
Mbunge wa Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ametoa mifuko 300 ya saruji kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Zahanati ya Kigeraetuma iliyopo Kijiji cha Kamuguruki, Musoma Vijijini ikiwa ni zawadi ya sikukuu ya Krismasi.

Zawadi hiyo imetolewa leo kijijini humo katika hafla ya chakula aliyoiandaa kwa ajili ya wananchi wa Kijiji hicho pamoja na vijiji vingine mara baada ya ibada iliyofanyika katika kanisa la Menonite lililopo kijiji cha Nyakatende, Musoma Vijijini..

Katika hafla hiyo Profesa Muhongo aliongozana na familia yake pamoja na rafiki zake kutoka Ujerumani ambao kwa pamoja walijumuika na wananchi wa Musoma vijijini kusherehekea.
 Kanisa la Menonite la kijiji cha Nyakatende ambapo Mbunge wa Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, familia yake na rafiki zake kutoka Ujerumani walishiriki ibada ambapo aliahidi kuchangia ujenzi wake. 
 Mbunge wa Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa tatu kutoka kushoto waliokaa katika viti) katika picha ya pamoja na waumini wa Kanisa la Menonite mara baada ya kumalizika ibada.
Diwani wa Kata ya Nyakatende, Rufumbo Rufumbo (katikati) akionesha vifaa vya umeme jua alivyokabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) . 
 Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (aliyeshika kipaza sauti) akiwa amepanga foleni na wananchi wa jimboni mwake kwa ajili ya kuchukua chakula.
 Wananchi wa Kata ya Nyakatende wakichukua chakula
Mbunge wa Musoma Vijijini na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kulia) akionesha vifaa vya umeme jua ambavyo Balozi wa Korea nchini anatarajiwa kupeleka mtaalamu jimboni humo ili kuwafundisha vijana namna ya utengenezwaji wake ili kujipatia kipato

ULEGA ATOA SALAM ZA SIKUKUU KATIKA KANISA LA KIGANGO CHA MWANAMBAYA WILAYANI MKURANGA

$
0
0
 Mbunge wa Mkuranga Bw Hamisi Abdala Ulega Akisalimiana na Mmoja wa Waumini Bw Alfred John Kanisani hapo
 Akiwa Katika Dua ya Pamoja na waumini wa Kanisa hilo la Kigango cha Mwanambaya Wilayani Mkuranga.
Mbunge wa Mkuranga Bw Hamis Abdala Ulega Akiongea na Waumini wa Kanisa la Kigango cha Mwanambaya lililopo Mwanambaya Wilayani Mkuranga na Kuwataka kumkumbuka Muumba katika kila Jambo Katika Maisha yao kila siku.Picha na Yasir Adam Globu ya Jamii

RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA MKEWE MAMA JANETH WASHIRIKI IBADA YA KRISMASI KATIKA KANISA KATOLIKI (KANISA KUU LA MOYO MTAKATIFU WA YESU) MKOANI SINGIDA

$
0
0


Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda akimuombea na kumbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakiwa katika Misa ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.
Hapa wakiwa katika sala.
Rais Magufuli na mkewe wakisilkiliza neno

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasalimia waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo mkoani Singida

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakisalimiana na waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya ibada ya Krismasi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakipunga mkono wakati wakitoka kwenye Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida. PICHA NA IKULU

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATATU DEC 26

WANAUME WASINDIKIZENI WAKE ZENU KILINIKI-Father Festus

$
0
0

Festus Makwame wa Kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo la Arusha akiwa anafurahiajambo wakati akiwa anaendesha ibadaya mkesha wa sikukuu ya christimas hapo jana usiku Jijini Arusha.Picha naVero Ignatus Blog.
Baadhi ya waumini waliohudhuria katika ibada hiyo ya mkesha wa sikukuu ya Christmass ni pamoja na maharusi hawa .Picha na Vero Ignatus Blog
Father Festus Makwame akiwa amembeba mafano wa mtoto Yesu aliyezaliwa ilipotimia majira ya saa sita kamili za usiku katika kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo la Arusha .Picha na Vero Ignatus Blog.
fFather Festus Makwame akiwa anahubiri katika mkesha wa sikukuu ya christimasiliyofanyika katika kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo laArusha.

Maharusi Denis na bi Joviety wakiwa ibadani muda mfupi kabla ya kufunggishwa ndoa kanisani hapo.Picha na Vero Igantus Blog

Maharusi hawa bwana Charles na bi Sabilina waliweza kufunga ndoa katika mkesha huo wa sikukuu ya christma katika kanisa la Katoliki Sent Treza Jimbo la Arusha .Picha na Vero Ignatus Blog.




Na,Vero Ignatus.Arusha.

Wito umetolewa kwa wanaume kuwa makini na kuwasindikiza wake zao kiliniki wakati wakiwa wajawazito kwani yapo mambo muhimu watakayojifunza wakiwa pamoja yatakayomsaidia mama na mtoto kuwa salama hadi wakati wa kujifungua.

Hayo yamesemwa na father Festus Makwame wa kanisa katoliki Sent Treza jimbo la Arusha alipokuwa kwenye ibada ya mkesha wa sikukuu ya krismas na kusema kuwa wanaume wengi hawana tabia ya kuwa na wake zao pindi wanapokuwa wajawazito jambo ambalo ni kosa kubwa

“Wanaume wasindikizeni wake zenu kiliniki huoni kwamba anashirikiana na Mungu katika uumbaji tena anakujengea heshima yawewe kuitwa baba Fulani?nenda nae yapo mambo mengi mtakayoelekezwa hata namna ya vyakula anavyotakiwa kula akisahau kwa vile ulikuwepo utamkumbusha?hebu igeni mfano wa Joseph na Maria hadi Yesu Kristo anazaliwa walikuwa pamoja.”alisisitiza

Amewataka waumini waliohudhuria ibada hiyo ya mkesha wa christmas waamue kubadilika waruhusu Kristo azaliwe mioyoni mwao ili mambo yao yawe mapya ,huku akisisitiza msamaha wa kweli pale mmoja anapomkosea mwingine kwani ni jambo ambalo Mungu analifurahia

“Wacha tuwe wakweli hakuna jambo gumu kama kumsamehe mtu aliyekukosea tena kwa makusudi,lakini kwa vile Mungu ameagiza tusameheane ni lazima tufanye hivyo na ukweli utabakia kuwa hivi Msamaha wa kweli ni ule ambao unautoa huku Unauma umekosewa lakini unasamehe kwa faida yako mwenyewe pia.”Alisisitiza father Festus.

Aidha amesema kuwa katika ibada hiyo ya mkesha wa krismas amewataka waumini kuachana mila na desturi potofu ambazo hazimpendezi Mungu kwani ni uvuli wa mauti.
“Wacheni michanganyo michanganyo kwani haimpendezi Mungu jamani kama umeamua kuwa kwa Mungu ,basi mfuate ili upate uzima wa milele ,na kama mwenzetu umeamua kumfuata shetani basi mfuate uangamie kwaani mambo haya ya michanganyiko michanganyiko mkiiendekeza huwa inaleta balaa na mikosi katika familia zenu”alisema father Festus.

MWIMBAJI MAARUFU WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA AFUNGA PINGU ZA MAISHA.

$
0
0
Mbali ya kuwa Sikukuu ya Krismasi kwa Wakristo duniani, pia jana Disemba 25,2016 ilikuwa siku ya furaha kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Bwana harusi Mathew Akrama Rwekila na Bibi harusi Agnes Martine (wawili katikati), baada ya kufunga pingu za maisha katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza.

Bibi harusi ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili Jijini Mwanza, akifahamika zaidi kwa jina la Agnes Akrama, wote wakimtumikia Mungu katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza.
Picha na Craty Cleophace
Maharusi na wasaidizi wao, wakimsikiliza Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpywa, Dkt.Daniel Moses Kulola, wakati wa ibada yao
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola, akisisitiza jambo wakati wa ibada ya ndoa
Bwana harusi Mathew Akrama Rwekila na Bibi harusi Agnes Martine, wakila kiapo cha ndoa."Mungu akasema, Si vyema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye". Mwanzo 02:18
BMG inawatakia maisha mema, Amen!
Tazama picha zaidi HAPA

MAONESHO KAHAWA NA UTALII YAFANYIKA MJINI RIYADH, SAUDI ARABIA

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, H.E Hemed Mgaza, mwenye suti nyeusi akifanya mazungumzo na wadau mbalimbali wa biashara katika maonyesho yaliyofanyika mjini Riyadh, Saudi Arabia.


Na Mwandishi Wetu, Riyadh Saudi Arabia.

Maonesho makubwa ya kahawa na chocolate (coffee and Chocolate) yamemalizika kwa mafanikio jijini Riyadh Saudi Arabia, huku kwa mara ya kwanza maonyesho hayo yakishirikisha Ubalozi wa Tanzania, nchini Saudi Arabia. Katika maonyesho hayo yaliyoanza Desemba 20 hadi 23 mwaka huu, yalihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwamo wafanyabiashara wa Tanzania kwa nia ya kutangaza bidhaa za mazao ya kilimo na viwanda kutoka Tanzania.

Akizungumza katika maonyesho hayo, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, H.E Hemed Mgaza, aliyasifu maonyesho hayo akisema kuwa yamekuwa na tija kwa nchi ya Tanzania pamoja na wafanyabiashara waliohudhuria. Alisema ofisi yake ilidhamilia kuyatumia maonyesho hayo kwa ajili ya kutangaza bidhaa za Tanzania pamoja na wafanyabiashara wake ili kufanikisha maendeleo yao kwa ujumla kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi yao.

“Tumeweka historia nchini Saudi Arabia kwa kuhakikisha kwamba tunashiriki kwa mara ya kwanza kwa ajili ya kuitangza nchi yetu, wafanyabiashara wetu pamoja na bidhaa zetu ili kila mmoja afahamua mazuri tuliyokuwa nayo. “Tulichofanya ni kuandaa banda letu lenye kila aina ya zuri letu hususan katika mazao ya kilimo ambayo kwa kawaida kila mtu alionyesha kuvutiwa na maonyesho hayo,” alisema H.E Mgaza.

Mazao mengine yaliyoonyeshwa katika maonyesho hayo ni pamoja na kahawa, chai, asali, katani, viungo, maziwa, mchele, karafuu, ufuta na nyinginezo huku mfanyabiashara Bi Khadija Naif akialikwa na Ubalozi ili kuwawakilisha wafanyabiashara kadhaa wa Tanzania kwa kubeba jukumu la kuleta bidhaa mbalimbali zilizooneshwa kwa siku hizo 4.

Mazungumzo yanaendelea kwenye banda hilo.
Balozi Hemed Mgaza akizungumza na wawekezaji wa Saudi Arabia waliohudhuria katika maonyesho hayo.
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, H.E Hemedi Mgaza mwenye suti nyeusi alipata fursa ya kukutana na wawekezaji mbambali waliotembelea banda la Tanzania wakati wa maonesho hayo.

Mfanyabiashara wa Tanzania aliyehudhuria maonyesho ya biashara ya Saudi Arabia, Bi Khadija Naif, akiwa na wasaidizi wake wakitoa maelekezo kwa watembeleaji wa banda lao.

Uvumi juu ya Noti ya Shilingi 500

$
0
0
Benki kuu ya Tanzania inapenda kuwafahamisha wananchi wote kuwa,habari inayoenea katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba noti ya shilingi mia tano haitatumika tena kuanzia Desemba 31,2016; sio taarifa ya kweli na ni uvumi unaopaswa kupuuzwa. Ukweli ni kwamba noti ya shilingi 500 itaendelea kuwepo katika mzunguko sambamba na ile sarafu ya shilingi 500 hadi pale noti hiyo itakapotoweka mikononi mwa wananchi. Tafadhali mpuuze taarifa hizo sio za ukweli. Marcian Kobello. Mkurugenzi wa Huduma za kibenki- BoT .

Kompyuta za Bayport zaifuta machozi Halmashauri ya Same

$
0
0
Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Mheshimiwa Said Mecky Sadick moja ya kompyuta sita zilizotolewa na taasisi yao kwa mkoa huo kama msaada wa kuweza kuongeza utendaji kazi mzuri kwa watumishi wa umma, hususan kwa Manispaa ya Moshi, Halmashauri ya Mwanga na Halmashauri ya Same, huku kila moja ikipewa kompyuta mbili. Kushoto kwa RC Sadick ni Katibu Tawala wa Mkoa huo wa Kilimanjaro, Mheshimiwa Aisha Amour. Picha zote na Mpiga Picha Wetu.


Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro.

HALMASHAURI ya Wilaya Same imeanza kupokea faraja za msaada wa kompyuta mbili kati ya sita zilizofikishwa mkoani Kilimanjaro, ikiwa ni siku chache baada ya ofisi yao kuungua moto na kutekeza vifaa mbalimbali vya kiofisi.


Kompyuta hizo zilipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mheshimiwa Said Mecky Sadick, akiambatana na wakuu wa idara wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na watumishi mbalimbali kutoka kwenye halmashauri za Same na Mwanga.
Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Mheshimiwa Said Mecky Sadick wa pili kutoka kushoto, akimkabidhi kompyuta hizo alizopokea kwa Taasisi ya Bayport Financial Services, Katibu Tawala wake wa Mkoa, Mheshimiwa Aisha Amour.

Akizungumza mwishoni mwa wiki katika hafla ya kupokea kompyuta hizo, Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, alisema wamekabidhi kompyuta hizo, ikiwa ni siku chache baada ya ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Same kuungua moto.


Alisema ingawa msaada wao umekuja kabla ya ofisi hizo kuungua moto, lakini wanaamini kuwa kompyuta hizo zinaweza kupunguza adha ya watumishi wa umma kufanya kazi kwa wakati mgumu, huku zikilengwa kwa Halmashauri ya Same, Mwanga na Manispaa ya Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mheshimiwa Said Mecky Sadick katikati akizungumza jambo na Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa kulia bada ya kukabidhiana kompyuta sita za msaada kwa Mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mheshimiwa Said Mecky Sadick kushoto akimkabidhi kompyuta mwakilishi wa Halmashauri ya Same.

“Taasisi yetu inatoa pole kubwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na watumishi wote wa Same, ila tunaamini kwa kiasi kidogo kompyuta tulizotoa zitawafuta machozi wadau wenzetu wa Same na Serikali yote kwa ujumla hapa nchini,” alisema Mercy.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mheshimiwa Mecky Sadick, aliwashukuru sana Bayport kwa msaada wao wa kompyuta na kuwataka waendelee kuwasaidia watumishi wa Same kwa kuongeza idadi ya kompyuta zao.


“Tunapokea kompyuta hizi kwa mikono miwili lakini tunawaomba wenztu wa Bayport muongeze idadi ya kompyuta kwa Halmashauri ya Same kwa sababu kule kuna uhitaji mkubwa zaidi baada ya ofisi kuungua moto.


“Ofisi yetu imepata pigo kubwa mno hivyo mtusaidie kwa hilo kwa sababu tunafahamu msaada wenu ni muhimu kwetu na taasisi yenu imekuwa karibu sana na jamii kwa kusaidia mambo mbalimbali ya kijamii ambayo yana tija kwetu sote,” alisema RC Sadick.


Utaratibu wa utoaji wa kompyuta 205 kwa ofisi za serikali zenye thamani ya Sh Milioni 500 umeanzishwa ili kuwafanya watumishi wa serikali wafanye kazi zao kwa ufanisi ili kuhamasisha masuala ya kimaendeleo hapa nchini.

Safari ya Mwisho ya Mpendwa wetu , Marehemu Mpoki Bukuku

$
0
0

Na Humphrey Shao ,Globu ya Jamii

Waziri wa habari, utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye amesema  amejifunza mengi kupitia kazi za mwandishi na mpiga picha wa kampuni ya TheGurdianLtd marehemu Mpoki Bukuku kutokana na mchango wake  mkubwa katika tasnia ya habari.

"Bukuku ameacha pengo kubwa hivyo hatosahaulika... wanahabari hatuna cha kufanya ila tunamshukuru Mungu na kupitia kazi zake tujifunze yale yote aliyoyafanya," alisema.

Akisoma historia ya Bukuku, kaka wa marehemu, Alfred Mwakaposa alisema marehemu alizaliwa 15/3/1972 katika Hospitali ya Mount Meru mkoani Arusha,  akiwa mtoto wa tano kwenye familia ya Bukuku.

Alisema alianza elimu ya msingi katika Shule ya Forodhani, Mlimwa Dodoma na baadae kuhamia Kisarawe, elimu ya sekondari alisoma Canon Andrea mkoani Dodoma na kidato cha tano na sita katika Shule ya Makumira Arusha.

"Baadaye marehemu alijiunga na elimu ya chuo cha uandishi wa habari TSJ ngazi ya cheti na Diploma... Amewahi kufanya kazi katika gazeti la Majira, Mwananchi na kuhamia Guardian mpaka mauti yalipomfika," alisema.
Akizungumza kwa niaba ya wasanii wa filamu, Muigizaji maarufu Steve Nyerere alisema tasnia ya filamu imepata pigo kubwa kumpoteza Bukuku hivyo wanaamini anapoenda ni sehemu nzuri.

"Nimemjua Mpoki wakati tupo Singida, tunaamini anapoenda Mpoki ni sehemu nzuri, tuko pamoja na familia yake, " alisema

Sehemu ya umati wa watu mbalimbali waliojitokeza kutoa heshima zao mwisho kwa mwili wa Marehemu Mpoki Bukuku.









Jeneza lenye mwili wa mpiga picha maarufu Marehemu Mpoki Bukuku likiwa katika eneo la uwanja wa Shule ya Wazazi, Tabata Kimanga jijini Dar mchana huu tayari kwa kutoa heshima za mwisho 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza jambo wakati wa kuagwa kwa mwili wa mpiga picha maarufu  Mpoki Bukuku  katika eneo la uwanja wa Shule ya Wazazi, Tabata Kimanga jijini Dar mchana huu.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akizungumza jambo wakati wa kuagwa kwa mwili wa mpiga picha maarufu  Mpoki Bukuku.
Mbunge wa jimbo la Ubungo, Saed Kubenea akitoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Mpoki Bukuku wakati wa kuagwa kwa mwili huo.
Mpigapicha Mkuu wa gazeti la Jambo Lelo pamoja na Muwakilishi wa Bloggers, Richard Mwaikenda akitoa salamu za rambirambi katika Msiba wa Mpoki Bukuku, viwanja vya Shule ya Wazazi, Tabata Kimanga jijini Dar.

JIPATIE DVD YAKO YENYE NYIMBO SITA KUTOKA KWA MWIMBAJI MAHIRI WA NYIMBO ZA INJILI JENNIFER MGENDI

$
0
0

  Albam ya Nyuma ya Mlima (DVD) imeingia sokoni ikiwa na nyimbo 6 ambazo ni
1., Nyuma ya Mlima
2. Tamaa Mbele
3. Penda unapopendwa
4. Yesu wa thamani
5.,Mitihani ya kausha
6. Nawashukuru adui (Kumpiga teke chura)

Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) kuwanufaisha wanawake wengi nchini Tanzania

$
0
0
Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani "WOMAN ON WHEEL" (WOW) umelenga kuwapa fursa wanawake kujiajiri na kuajiriwa katika sekta ya usafirishaji kwa kuendesha vyombo vya moto vya abiria na mizigo.

Mradi wa WOW kwa sasa unasajili wanawake kwa ajili ya kuwapatia fursa ya kufundishwa udereva bure katika viwango mbalimbali na baadae kuwatafutia ajira na wengine kuwawezesha ili waweze kujiajiri.

Mradi wa WOW umelenga katika kipindi cha mwezi Disemba hadi Februari uwe umesajili wanawake 600 nchi nzima ili waweze kupatiwa mafunzo.

Lengo kubwa la mradi ni kuondoa mila potofu za mfumo dume wa uwepo wa kazi za kiume na kike.Mradi wa WOW utawezesha wanawake kushiriki kikamilifu kuchangia pato la taifa kwa kujiwezesha kulipa kodi mbalmbali za serikali kupitia sekta ya usafirishaji.
1
Martin Gabone-Mkurugenzi Mkuu Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akizungumza na washiriki wa semina hiyo ya siku moja hawapo pichani, iliyolenga kuwapa fursa wanawake kujiajiri na kuajiriwa katika sekta ya usafirishaji kwa kuendesha vyombo vya moto vya abiria na mizigo kupitia mradi huo.
2
Martin Gabone-Mkurugenzi Mkuu Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akizungumza na washiriki wa semina hiyo ya siku moja , iliyolenga kuwapa fursa wanawake kujiajiri na kuajiriwa katika sekta ya usafirishaji kwa kuendesha vyombo vya moto vya abiria na mizigo kupitia mradi huo.
3
Baadhi ya wanawake washiriki wa semina hiyo ya siku moja wakifurahia maelezo na umuhimu wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW).
4
Baadhi ya wanawake washiriki wa semina hiyo ya siku moja wakifuuatilia maelezo ya umuhimu wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW).
5
Victor Francis-Meneja Mafunzo wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akielezea jambo wakati alipotoa mafunzo kwa wanawake washiriki wa semina hiyo.
6
Victor Francis-Meneja Mafunzo wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akifafanua jambo huku akisikilizwa kwa makini na baadhi ya washiriki.
7
Baadhi ya washiriki wakifuatilia maelezo kutoka kwa Victor Francis-Meneja Mafunzo wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW)
8
Victor Francis-Meneja Mafunzo wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akitoa maelekezo kwa baadhi ya washiriki wa semina hiyo.
9
Victor Francis-Meneja Mafunzo wa Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akigawa baadhi ya vipeperushi vyenye maelezo muhimu kuhusu mradi huo.

SABODO AMSHAURI RAIS MAGUFULI AZIDI KUPUNGUZA BARAZA LA MAWAZIRI

$
0
0
 Mfanyabiashara maarufu nchini, Jaffar Sabodo akizungumza nyumbani kwake Upanga Dar es Salaam  mwishoni mwa wiki, ambapo alimtaka Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Rais John Magufuli azidi kupunguza Baraza la Mawaziri kufikia 15 na Kamati Kuu 15 pamoja na Halmashauri Kuu wajumbe 55. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG


MFANYABIASHARA maarufu nchini, Jaffar Sabodo, amemshauri Rais John Magufuli kupunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri, akisema hali hiyo itamsaidia kuleta tija zaidi katika utendaji wake.

Aidha, Sabodo amemshauri Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupunguza idadi ya wajumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho pamoja na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na JAMBO LEO nyumbani kwake Dar es Salaam, Sabodo alisema hatua hiyo itasaidia Serikali kutekeleza falsafa yake ya kubana matumizi.

“Kupungua kwa ukubwa wa Baraza la Mawaziri kutajenga uwajibikaji zaidi kwa mawaziri, lakini pia kubana matumizi ya Serikali kuhudumia baraza kubwa la mawaziri pia kusaidia kujenga mfumo imara zaidi wa utawala na itakuwa rahisi kudhibiti siri za Serikali,” alisema Sabodo na kuongeza:

“Hata ukubwa wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu za CCM nao ukipungua utaiimarisha zaidi CCM, kwani viongozi wake watakuwa na nguvu zaidi, lakini pia matumizi yatapungua na mambo ya chama hayatavujishwa kirahisi.”

Alipoulizwa kuhusu idadi anayopendekeza iwe kwa vyombo hivyo, Sabodo ambaye amewahi kuwa mfadhili wa CCM na Chadema kwa nyakati tofauti alisema: “Ili kulinda zaidi maadili ya CCM yawe kama alivyoacha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliyeiasisi, kwa mawazo yangu Halmashauri Kuu ingekuwa na wajumbe wasiozidi 55 na Kamati Kuu wawepo wajumbe wasiozidi 15.”

Kuhusu Baraza la Mawaziri Sabodo alisema linapaswa kupungua kutoka idadi ya sasa hadi kufikia mawaziri wasiozidi 15. “Cabinet’ baraza liwe dogo, kuna wizara zinaweza kufutwa, ili kuleta tija zaidi. Hili linawezekana,” alisema Sabodo.

Ushauri huo wa Sabodo umekuja wakati hivi karibuni CCM ilitangaza mabadiliko na kupunguza idadi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa kutoka 388 hadi 158 huku wajumbe wa Kamati Kuu ikipunguzwa kutoka 34 hadi 24.

Kwa upande wa mawaziri, Baraza la Mawaziri la Rais Magufuli lina mawaziri kamili 20 pamoja na Waziri Mkuu, likiwa na naibu mawaziri 16.

Akizungumzia uamuzi wa Rais Magufuli kuhamia Dodoma, Sabodo alisema ameonesha uthubutu ulioshindikana kwa zaidi ya miaka 45.

Alisema anakumbuka uamuzi wa kuhamia Dodoma ulifikiwa na Bunge enzi za utawala wa hayati Mwalimu Julius Nyerere aliyeshindwa kuufanikisha kutokana na sababu mbalimbali za msingi, lakini waliofuata katika uongozi hakuna aliyeonyesha uthubutu kama wa Rais magufuli.

Sabodo alisema hatua hiyo ya kuhamia Dodoma ikifanikiwa inaweza kusaidia hata rushwa na ubadhirifu kupungua kwani baadhi ya mambo yatashindikana kufanyika Dar es Salaam litakalobaki kama jiji la kibiashara hivyo kuwalazimu wahusika kwenda makao makuu ya Serikali.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMANNE DEC 27

Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images