Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

MSD YAZINDUA HUDUMA MAALUMU KWA WATEJA WAKUBWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee naWatoto Dk. Mpoki Ulisubisya (kulia), akizungumza na viongozi mbalimbali wa sekta ya afya wakati akizindua mpango wa huduma maalumu kwa wateja wakubwa Dar es Salaam leo asubuhi.
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)  Profesa Mohamed Janabi (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo. 

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu akizungumza kwenye mkutano huo.
Meneja Huduma kwa Wateja wa MSD, Salome Malamia akizungumza katika hafla hiyo.
Mmoja wa maofisa kutoka Ofisi ya Inayosimamia Utekelezaji wa Mapendekezo ya Maboresho (SMO), Naomi Shangani akitoa maelezo kwa mgeni rasmi kuhusu mpango huo.
Ofisa wa SMO, Frankie Nkone akieleza kazi za eneo lake zinavyofanyika.
Kikosi kazi cha SMO. kutoka kushoto ni Benjamin Mtesigwa, Frankie Nkone, Naomi Shangali, Marko Masala na kiongozi wao, Cosmas Nalimi.
Naomi Shangali (kulia), akiwaelekeza jambo wenzake.
Wajumbe wa mkutano huo kutoka sekta ya afya wakiwa wameinamisha vichwa vyao kwa dakika moja kumkumbuka aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya MSD, marehemu Profesa Idrissa Mtulia aliyefariki jana.
viongozi  wa sekta ya afya wakiwa kwenye hafla hiyo.
mazungumzo ya hapa na pale yakiendelea.
Mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya  Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee naWatoto Dk. Mpoki Ulisubisya (kulia), akiwa na viongozi wenzake katika uzinduzi huo.
Mkutano ukiendelea.

Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.


Baadhi ya wafanyakazi wa MSD wakiwa kwenye hafla hiyo.





Viongozi wa sekta ya afya wakiwa wameinua mikono juu kuridhia mpango wa huduma maalumu kwa wateja wakubwa wakati wa uzinduzi wa mpango huo ulioandaliwa na Bohari ya Dawa (MSD), katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam leo.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa SMO.
Picha ya pamoja ya  viongozi na mgeni rsami.

Na Dotto Mwaibale

BOHARI  ya dawa (MSD) imezindua mpango wa huduma maalumu kwa wateja wake wakubwa, kama moja ya hatua za kuboresha huduma kwa wateja. 

Mpango huo utawawezesha wateja hao kupata huduma ya haraka zaidi pindi wanapokuwa wanahitaji mahitaji yao.

Wateja hao ni pamoja na hosipitali ya Taifa ya Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI), Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, hosipitali ya Sekoutoure Mwanza, Hosipitali ya Kibong’oto, Mirembe, Hosipitaliza Amana, Temeke, Mwananyamala, KCMC, Hospitaliya Benjamin Mkapa na Taasisi ya Moyo ya JakayaKikwete.

Akizindua mpango huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee naWatoto Dk. Mpoki Ulisubisya amesema mpango huo ni moja ya maboresho yanayofanywa na MSD, ili kuhakikisha huduma zake zinatolewa kama inavyohitajika.

Dk. Mpoki pia amewasisitiza wateja hao wakubwa wa MSD kuhakikisha wanafanya maoteo sahihi ya mahitaji yao na kuyaleta MSD kwa wakati ilikuepusha ucheleweshwaji wa taratibu za manunuzi ambao pia tasababisha dosari kwenye upatikanaji wa dawa kwa wateja. 

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu  amesema hatua ya kuwahudumia wateja hao kwa kiwango kizuri na cha uhakika itafanikiwa, hivyo Watarajie maboresho makubwa ya huduma.

Waziri Nape afunga Mkutano Mkuu wa Waandishi wa habari za Mitandao 'Tanzania Bloggers Network' (TBN),aahidi kuanzisha tuzo

0
0
 Na Beatrice Lyimo, Maelezo

Serikali inatarajia kuanzisha tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii (blogs) nchini kuanzia mwaka 2017.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar  es salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na semina ya wanachama wa umoja wa waendeshaji wa blog nchini.

Waziri Nape alisema kuwa lengo la tuzo hizo ni kuzisaidia blogs za Tanzania kubobea katika nyanja tofauti ikiwemo kilimo, mifugo, viwanda, hifadhi ya jamii kwa nia ya kuipa heshima tasnia ya habari nchini.

Aidha, Waziri Nape alisema kuwa tayari Serikali imeanza mazungumzo na   makampuni na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kudhamini tuzo hizo ili kuhakikisha kuwa washindi wanapatikana kwa uwazi.

“Tuzo hizo zitakuwa za kwanza kwa namna zitakazovyoendeshwa kwa uwazi hivyo makampuni zaidi yanakaribishwa kuweza kuzidhamini mashindano hayo yatakayojielekeza kwenye nyanja tofauti” alisema Waziri Nape.

Waziri Nape pia alisema amewataka wamiliki na watendaji wa blogs nchini kushirikiana na Serikali ili kuweza kuijenga nchi.

“Tutumie fursa za kisiasa zilizopo, fursa za teknolojia ili kuhakikisha tiunajenga Tanzania tunayoitaka, ishaurini Serikali kwa kutumia taaluma mliyonayo ili kuweza kuipeleka nchi ya Tanzania tunayoitaka” alifafanua Waziri Nape.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa Ufafanuzi wakati alipokuwa akieleza namna ya kuitambua mitandao ya Kijamii pamoja na uanzishaji wa Tuzo kwa Waendeshaji mitandao hiyo.
Waziri Nape alisema kuwa lengo la tuzo hizo ni kuzisaidia blogs za Tanzania kubobea katika nyanja tofauti ikiwemo kilimo, mifugo, viwanda, hifadhi ya jamii kwa nia ya kuipa heshima tasnia ya habari nchini.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye wakati akizungumza mapema leo jijini Dar wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Tanzania Bloggers Network (TBN) iliokwenda sambamba na semina ya wanachama wa umoja wa waendeshaji wa blog nchini.Picha na Michuzi Jr.

Mmoja wa Wajumbe wa mkutano huo,Mzee John Kitime ambaye amebobea katika mambo ya Hakimiliki,akitoa elimu ya mambo ya Hakimiliki kwa washiriki wa mkutano huo.

Baadhi ya Wadau wakiendelea kusikiliza yaliyokuwa yakiendelea ukumbini humo.
Mmoja wa wajumbe Daniel Mbega akiuliza swali wakati wa mkutano huo ulipokuwa ukiendelea 
Baadhi ya Waendeshaji wa mitandao hiyo wakiwa kwenye mkutano wao wa Mwaka wakifuatilia yaliyokuwa yanaendelea

Mwenyekiti wa Muda wa chama cha Waendesha mitandao ya Kijamii Tanzania Bloggers Network-TBN,Joachim Mushi akimkaribisha mgeni rasmi,Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kwa ajili ya kufunga mkutano huo na pia kuyotolea ufafanuzi baadhi ya mambo.
Baadhi ya Waendeshaji wa mitandao hiyo wakiwa kwenye mkutano wao wa Mwaka wakifuatilia yaliyokuwa yanaendelea

WAZIRI NAPE AJIUNGA NA PSPF, AWASIFU KWA HUDUMA ZA "MWENDO KASI"

0
0
NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Moses Nnauye, amejiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF na kuusifu kwa huduma zake za haraka.

Waziri Nape, amejiunga muda mfupi baada ya kufunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mtandao wa Bloggers Tanzania, (TBN), kwenye jingo la kitega uchumi la Jubilee Towers linalomilikiwa na Mfuko huo jana.
Aidha washiriki wa mkutano huo nao pia walijiunga na Mfuko huo kupitia uchangiaji wa Hiari yaani PSS.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa kadi yake ya uanachama iliyotengenezwa chini ya dakika 15, Waziri Nape alisema, “Aise, kitambulisho change tayari, hongereni sana kwa huduma za haraka, mimi sikujua kama mnafanya kazi kwa kasi yanamna hii,” alisema Mh. Nape wakati akikabidhiwa kadi hiyo na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi ofisini kwake.

Tangu kujaza fomu, kupiga picha na kukabidhiwa kitambulisho hicho, Waziri alitumia kiasi cha dakika 25 tu, ikiwa ni muda mfupi baada ya kufunga mkutano huo.Nao wanachama wa Mtandao wa Bloggers Tanzania, (TBN), waliokuwa wakishiriki mkutano huo, wamejiungana PSPF, baada ya kupatiwa maelezo ya kina kuhusu umuhimu wa kujiunga na Mfuko, kutkana na manufaa mengi ukiachilia mbali kujiwekea akiba.

“Ukiwa Mwanachama wa Mfuko, moja ya faida kubwa ni kujipatia bima ya Afya, itakayokusaidia wewe na familia yako, nikiwa na maana ya mke/mume na watoto,” alisema Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdyul Njaidi katika mada yake aliyoitoa kwa washiriki kuhusu kazi za Mfuko huo.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Moses Nnauye, (wapili kushoto), akipokea fomu ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Bw. Adam Mayingu, wakati wa Mkutano Mkuu wa Mtandao wa Bolggers Tanzania, (TBN), uliomalizika jana jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa TBN, Bw. Joachim Mushi.
 Waziri Nape, akipokea kadi yake ya kujiunga na Mfuko huo kutoka kwa Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Abdul Njaidi.
 Waziri Nape, akijaza fomu hiyo, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Mayingu na kulia ni Bw. Njaidi

 Bw. Njaidi akitoa mada kuhusu kazi za Mfuko huo kwa washiriki wa mkutano wa TBN
  Bw. Njaidi akitoa mada kuhusu kazi za Mfuko huo kwa washiriki wa mkutano wa TBN
 Washiriki wa Mkutano wa TBN, wakijaza fomu, huku Bw. Njaidi akitoa maelezo zaidi kwa baadhi yao
 Bw. Mayingu akimkabidhi zawadi Waziri Nape
 Waziri Nape, baadhi ya wafadhili wa mkutano kutoka PSPF, na NMB, wakiwa aktika picha ya pamoja na baadhiya washiriki wa mkutano huo wa TBN
 Mmiliki wa Blogu ya Libeneke la Kaskazini kutoka Arusha Bi. Woinde Shizzah akijaza fomu za kujiunga na PSPF

 Baadhi ya washiriki wakijaza fomu za kujiunga na PSPF




 Waziri Nape akimkabidhi Bw. Seria Tumainieli kadiya kujiungana PSPF
 Waziri akimkabidhi Bi. Veronika kadi ya kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF
  Waziri akimkabidhi Bw. Gadiola Emmanuel kadi ya kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF

SSRA YAPATA TUZO YA NBAA YA UTUNZAJI BORA WA MAHESABU

0
0
MAMLAKA ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) yatwaa ushindi wa NBAA katika utunzaji bora wa mahesabu kwa mwaka 2014/15. SSRA imekuwa mshindi wa pili kati ya Mamlaka za Udhibiti zinazotumia viwango vya Kimataifa vya mahesabu ya Taasisi za Umma (IPSAS)
Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Bibi. Irene Isaka akipokea Tuzo ya NBAA ya utunzaji bora wa mahesabu ya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).
Mwenyekiti wa Bodi ya SSRA Bw. Juma A Muhimbi aliyeshikilia Tuzo ya NBAA baada ya SSRA kuibuka mshindi katika utunzaji bora wa mahesabu wengine pichani ni watumishi wa Mamlaka.
Bw. Juma Muhimbi, Mwenyekiti wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii akimpongeza Bibi. Irene Isaka, Mkurugenzi Mkuu wa SSRA.
Bi. Latifa Mazengo, akiwa ameshikilia Tuzo hiyo. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Bibi Irene Isaka akiwa pamoja na watumishi wa Mamlaka hiyo.

USIPITWE NA HABARI HIZI KUU AMBAZO ZIMEGONGA VICHWA VYA DUNIA

0
0

SERIKALI YA ZANZIBAR YAANDAA MKAKATI WA KUVILINDA VIWANDA

0
0
WAZIRI wa Biashara, Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum Ali ameutaka uongozi wa CocaCola kufikiria  kurejesha uzalishaji katika kiwanda cha Maruhubi na Serikali imeandaa mikakati ya kuvilinda viwanda vya Zanzibar ili wananchi wafaidike kupata ajira.
Amesema miongoni mwa mikakati hiyo ni kuhakikisha bidhaa zote zinazoingizwa Zanzibar kutoka nje zinalipiwa ushuru unaostahiki na kudhibiti mbinu za wafanyabiashara za kukwepa kulipa kodi.
Balozi Amina ameeleza hayo alipofanya ziara ya kutembelea Kiwanda CocaCola Maruhubi ambacho kinaendelea kusambaza soda zinazozalishwa Dar es salaam kufuatia kiwanda hicho kusitisha uzalishaji kwa muda mrefu sasa.
Amesema kitendo cha kusitisha uzalishaji wa soda katika Kiwanda cha Maruhubi kinawanyima fursa wananchi wengi kutoa mchango wao na ni kinyume cha sera ya kuwa na viwanda venye tija.
Meneja Uendeshaji wa Kiwanda cha CocaCola Zanzibar na Tanzania Bara Ndugu Haji Ali amemueleza Waziri Amina wamelazimika kusitisha uzalishaji Zanzibar kutokana na ushindani uliopo wa bidhaa hiyo kutoka nje bei yake kuwa chini kutokana na kuingizwa bila kulipiwa ushuru.
Ametaja sababu nyengine kuwa ni uchakavu wa mitambo ya uzalishaji iliyokuwa ikitumika imepitwa na wakati na haiendani na teknolojia ya usazalisha wa sasa.
Hata hivyo amesema Kiwanda cha CocaCola Zanzibar kimeongeza mauzo ya bidhaa za aina tofauti za soda zinazozalishwa Tanzania  Bara kwa asilimia 40.

WAKAGUZI WA NDANI WATAKIWA KUSIMAMIA UBORA WA MIRADI MIKUBWA YA UJENZI WA MIUNDOMBINU

0
0
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika (kulia), akimsikiliza Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi (kushoto) wakati akielezea mafanikio na changamoto zinazokikabili chuo hicho. Kushoto kwa Mkuu wa Chuo ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Bw. Mohamed Mtonga, Msaidizi wa Mkuu wa Chuo Dkt. Samwel Werema, Mkaguzi wa Ndani Mkuu Msaidizi– Ukaguzi Mamlaka za Mitaa Bw. Mwanyika Musa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Kiufundi Bw. Amin Mcharo.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika (kulia), akijibu hoja zilizotolewa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi (kushoto) alipofika Ofisi Kuu ya Chuo hicho kabla ya kufungua mafunzo ya siku nne ya wakaguzi kutoka mikoa ya Kanda ya Kaskazini.
Wakaguzi wa Ndani kutoka Serikali za Mtaa na Sekretarieti za Mikoa wakiwa kwenye mafunzo ya ukaguzi, Mgeni Rasmi katika mafunzo hayo ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika. Mafunzo haya yanafanyika katika ukumbi wa Chuo cha Uhasibu Arusha, mkoani Arusha.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika (aliyesimama) akisoma hotuba ya ufunguzi wa mafunzo ya wakaguzi wa ndani ambapo alisema mpaka sasa wakaguzi wa ndani 308 wamepata mafunzo hayo na wakaguzi 32 wameshafanya mafunzo hayo kwa vitendo.
Wakaguzi wa Ndani kutoka Serikali za Mitaa na Sekretarieti za Mikoa katika picha ya pamoja. Waliokaa ni Mgeni Rasmi na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Kiufundi Bw. Amin Mcharo na kushoto kwake ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Mohamed Mtonga na Mkaguzi wa Ndani Mkuu Msaidizi wa Serikali – Ukaguzi mamlaka za mitaa Bw. Mwanyika Musa.
Mgeni Rasmi na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika (katikati) wakibadilishana mawazo na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi (Kushoto) na kulia ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Mohamed Mtonga.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika akimsikiliza Mkaguzi wa Ndani Mkuu Msaidizi wa Serikali – Ukaguzi mamlaka za mitaa Bw. Mwanyika Musa ambapo alisema mafunzo hayo ni muhimu kwani yamelenga kuimarisha ukaguzi wa miradi mikubwa ili ujenzi wake ulingane na thamani ya fedha iliyotumika.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi akumfafanulia jambo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika.

NEC YATANGAZA RATIBA YA UCHAGUZI MDOGO HAPA NCHINI.

0
0


Na Eliphace Marwa – MAELEZO

TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza ratiba ya uchukuaji wa fomu za kujaza nafasi zilizo wazi ya Mbunge na Madiwani katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Imesema kuwa inatarajia kuendesha Uchaguzi Mdogo katika Jimbo la Dimani , Mkoa wa Mjini Magharibi ,Tanzania Zanzibar kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo hilo.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini Dar es salaam na Tume hiyo, hatua hiyo itanatokana na vifungu vya 37(1)(b) na 46(2) vya sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Vifungu vya 13(3) na 48(2) vya Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura 292.

Aidha ,Tume hiyo pia itaendesha Uchaguzi Mdogo wa kujaza nafasi za wazi za Udiwani katika kata 22 kwenye baadhi ya Halmashauri za Tanzania Bara zilizokuwa wazi kutokana na sababu mbalimbali.

Imezitaja Kata hizo Ng’hambi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Ihumwa ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, Kiwanja cha Ndege ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Igombavanu na Ikweha za Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa pamoja na Ngarenanyuki iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mkoani Arusha.

Kata nyingine ni Kijichi ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Mkoani Dar es Salaam, Kata ya Kinampundu ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida, Isegehe ya Halmashauri ya Mji wa Kahama Mkoani Shinyanga, Kasansa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi, Malya na Kahumulo Mkoani Mwanza, Maguu na Tanga Mkoani Ruvuma pamoja na Kata ya Kimwani Mkoani Kagera.

Imeongeza kuwa Kata nyingine ni pamoja na Nkome Mkoani Geita, Kata ya Lembeni Mkoani Kilimanjaro, Mkoma ya Mkoani Mara, Duru ya Mkoani Manyara, Mwamtani ya Mkoani Simiyu, Misugusugu ya Mkoani Pwani pamoja na Mateves ya Mkoani Arusha.

Tume hiyo imesema kuwa zoezi la kutoa fomu za uteuzi litaanza Desemba 10 hadi 22 na kufuatia kwa zoezi la uteuzi wa wagombea siku ya tarehe 22 mwezi Desemba na Desemba 23 hadi Januari 21 mwakani itakuwa ni kipindi cha kampeni ambapo Januari 22 mwakani itakuwa siku ya kupiga kura.

BALOZI WA CUBA AMUAGA KINANA LEO

0
0
  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Balozi wa Cuba, Jorge Luis Lopez (kushoto), alipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kumuaga kufuatia kumalizika kwa mda wake wa kazi hapa nchini. (Picha na Bashir Nkoromo-MAKAO MAKUU YA CCM).
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha Balozi wa Cuba, Jorge Luis Lopez (kushoto), alipofika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, kumuaga kufuatia kumalizika kwa mda wake wa kazi hapa nchini. (Picha na Bashir Nkoromo-MAKAO MAKUU YA CCM).

WAZIRI NAPE AFUNGA MAFUNZO YA BLOGGERS TANZANIA

0
0

MHARIRI WA HABARI MSTAAFU WA MAGAZETI YA UHURU, MZEE NAKAJUMO ATINGA NEWSROOM LEO KUWANOA VIJANA

0
0
 Mhariri wa Habari Mstaafu wa Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru Mzalendo na Burudani Mzee Joe Nakajumo akimpiga msasa Kaimu Mhariri wa Makala Selina Wilson, katika chumba cha habari cha kampuni hiyo, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Mzee Nakajumo alifika leo katika chumba cha habari kwa mwaliko rasmi wa Kaim Mhariri Mtendaji wa UPL, Ramadhani Mkoma ili kuwapiga msasa waandishi wa habari. Kulia ni Mpigapicha Mwandamizi wa UPL, Bashir Nkoromo ambaye kwa sasa ameazimwa Katika Idara ya Itikadi na Uenezi, Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Makao Makuu ya CCM.
 Kaimu Mhariri wa Makala, Selina Wilson akimshukuru Mzee Nakajumo kwa msasa aliompiga
 Mpigapicha Mwandamizi wa UPL, Bashir Nkoromo ambaye kwa sasa ameazimwa Katika Idara ya Itikadi na Uenezi, Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Makao Makuu ya CCM, akimshukuru Mzee Nakajumo baada na yeye kupata nasaha na kukumbushwa namna kazi zilivyokuwa zikifanyika wakati akipigapicha UPL ambapo picha zilikuwa lazima zitathminiwe ubora  wake na Mzee huyo, Nakajumo wakati akiwa bado hajastaafu UPL
Mzee Nakajumo akiendelea kusikiliza kila liyetaja kulifahamu kwa undani jambo linalohusu uandishi wa habari ulio wa makini zaidi. PICHA ZOTE NA JUMAANE GUDE

WATEJA WA DCB KUNUFAIKA NA KAMPENI ZA BORESHA MAISHA NA PATA FAIDA

0
0
Meneja mwandamizi wa Shughuli za Kibenki DCB Samwel Dyamo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni ya boresha maisha na DCB pamoja na Pata faida na DCB itakayoanza kuchezwa kwa droo ya kwanza Desmba 17, Kushoto ni Meneja Masoko Boyd Mwaisame.


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BENKI ya DCB imedhamiria kuendelea kuwa kuwajali wateja wake imeanzisha kampeni ya "boresha maisha na DCB" na " Pata faida na DCB" itakayoanza Desemba 17 kwa ajili ya kuwazawadia zawadi mbalimbali pamoja na fedha taslimu kwa wateja wapya na wa zamni.

Akizungumzia kampeni hiyo, Meneja mwandamizi wa Shughuli za Kibenki DCB Samwel Dyamo amesema kampeni boesha maisha na DCB na Pata faida na DCB itadumu kwa miezi mitatu na kila mwezi kutakuwa na droo moja itakayotoa washindi watatu wa fedha taslimu laki mbili,

Dyamo amesema kuwa mbali na fedha taslimu kutakuwa na washindi wengine wawili watakaopata simu za mkononi na washindi 20 watapata kila mmoja na watatangazwa mbele ya waandishi wa habari na kukabidhiwa zawadi zao.

Droo ya kwanza itachezeshwa Desemba 17 na itamalizika Februri 17 na wateja wanatakiwa kuweka fedha mara kwa mara kwenye akaunti mojawapo ya akiba binafsi, akaunti ya watoto na akaunti ya WAHI kiasi cha kuanzia sh 50.,000 na kuendelea na kuongeza mana mara mbili zaidi ya sh 500,000.

Dyamo amesema kuwa, mteja atakayeweka fedha hizo ataingia moja kwa moja kwenye droo hizo, mbali na kampeni hiyo pia kutakuwa na kutakuwa na Pata faida na DCB itakayokuwa inawapa faida wateja kwa kuwekeza nkupitia huduma yetu ya akaunti ya muda mrefu (fixed account) kwa kuweka kiais cha milioni 50 na kuendelea kwa kipindi cha mwaka mmoja na watapata faida ya asilimia 15 ya fedha zako.

Alisisitiza kuwa, hata kama utaziweka fedha zako kwa kipindi cha miezi sita bado utaendelea kufaidika zaidi na kuwataka kujitokeza kwa wingi hususani kwa wajasiramali, watu binafsi na taasisi mbalimbali.

Meneja wa matawi wa  DCB, Haika Machaku amewataka watanzania kujiunga na benki yao kwani asilimia kubwa ya faida inaenda kwa wananchi kwa ajili ya miradi mbalimbali.
Meneja wa matawi wa  DCB, Haika Machaku akizungumza na waandishi wa habari juu ya umuhimu wa wananchi kujiunga na benki yao ili kuweza kufaidika zaidi.

IN LOVING MEMORY OF MAMA ROSE SHOMARI

0
0
Its is 11 years since you departed from us, in this day a memory of a life so beautifully lived and a heart so deeply loved. We will always remember you and the lessons of life you gave us. May God hold you in the palm of his hand. In our hearts, you will always be remembered by your sons and daughters, grandsons and granddaughters and the whole Shomari's clan.
 
We thank the Lord for your life, great advice, teacher, counselor and a big blessing for us. May the almighty Lord rest your soul in Peace until we meet again.Our hope comes from the Lord as he says he will wipe every tear from their eyes there will be no more death or mourning or crying or pain…Rev 21:4.

MAJENERALI WAPYA WAVISHWA VYEO MAKAO MAKUU JWTZ

0
0

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (Kushoto), akimvisha cheo cha Meja Jenerali,Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga Brigedia Jenerali George William Ingram,Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange (kushoto) akimvisha cheo cha Meja Jenerali Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Michael Isamuhyo, Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange (Wa pili kushoto) pamoja na mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Salvatory Mabeyo (Wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na ma Meja Jenerali wapya, Makao Makuu JWTZ Upanga Dar es Salaam.

Picha kwa hisani ya kurugenzi ya habari na uhusiano JWTZ

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JKT

0
0

JESHI LA POLISI MKOANI KIGOMA LAKAMATA RISASI 408 ZILIZOKUWA ZIKIMILIKIWA NA MTU MMOJA WILAYANI KASULU MKOANI KIGOMA

0
0
Na Rhoda Ezekiel -Globu ya Jamii,Kigoma.

JESHI la polisi Mkoani Kigoma limefanikiwa kukamata risasi 408 za bunduki zilizo kuwa zikimilikiwa na Mtu mmoja ambaye jina lake halikutajwa mkazi wa Kijiji cha Makere Wilayani kasulu Mkoani Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake leo Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Kigoma,DCP Fredinand Mtui alisema mnamo tarehe 5Desemba majira ya 08:20 huko maeneo ya makere Center katika kijiji cha Makere askari wakiwa doria walipokea taarifa kutoka kwa raia wema wanao chukia uhalifu kuwa kuna mtu wana wasiwasi nae kuwa anamzigo usio kuwa wa kawaida.

Mtui alisema Askari walianza ufuataliaji na kufanikiwa kukamata mtuhumiwa mmoja ambaye jina lake limehifashiwa kwa shughuli za kiusalama, alipo fanyiwa upekuzi mtuhumiwa huyokatika Sanduku lake alilokuwa amebeba alikutwa akiwa na risasi 408 za bunduki aina ya SMG/SAR alizokuwa amezifunga ndani ya nguo zake .

Aidha Mtui alisema upelelezi bado unaendelea ,Mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria pindi upelelezi utakapo kamilika ilikutoa fundiaho kwa wananchi wengine wanao nunua siraha kwa lengo la kufanyia uhalifu.

"nichukue fursa hii kuwaasa wahalifu wanao jihusisha na biashara ya kuuza na kununua risasi na siraha nyingine waache biashara hiyo, wafanye kazi nyingine ambazo zinatambulika kisheria vyombo vya ulinzi na usalama viko imara kuwatafuta wahalifu hao na kuwachukulia hatua za kisheria,"alisema Mtui.

Sambamba na tukio hilo alisema mnamo tarehe 6Desemba huko maeneo ya Mwanga Vamia Manispaa ya Kigoma ujiji Hussen Athuman (36) Mkazi wa mwanga Vamia alikutwa chumbani kwake akiwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani. 

Mtui alisema usiku wa tarehe5 marehemu alimpigia simu Dada yake na kudai kuwa walikuwa na ugomvi na mkewe ugomvi huo uliopelekea mkewe kuondoka siku nne zilizo pita , na kumwambia amueleze kaka yake kwamba atachukua maamuzi magumu.

Alisema chanzo cha kujinyonga ni ugomvi baina ya baina ya marehemu na mkewe, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospital ya rufaa maweni  kusubili kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi.
 Risasi 408 za bunduki zilizo kuwa zikimilikiwa na Mtu mmoja ambaye jina lake halikutajwa, mkazi wa Kijiji cha Makere Wilayani kasulu Mkoani Kigoma. 
Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Kigoma,DCP Fredinand Mtui akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani),kuhusiana na tukio hilo la kukamatwa risasi za moto 408,zilizokuwa zikimilikiwa na mtu mmoja mkoani humo.

WANANCHI WA SINGIDA KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME WA UPEPO

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mheshimiwa January Makamba akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa umeme kujadili mkakati ya kuzalisha nishati ya Umeme kwa njia ya Upepo leo katika ukumbi wa Hotel ya Hyatt Jijini Dar
 Mkurugenzi Mtendaji Six Telecoms, Rashid Shamte (wa kwanza kushoto) akiwa kwenye kongamano la wadau wa umeme wenye lengo la kuzalisha umeme wa nguvu ya Upepo wenye lengo la kuanza kuzalisha umeme katika mkoa wa Singida.
Baadhi ya wadau wakiwa kwenye kongamno la wadau wa umeme 
 Mkurugenzi Mtendaji Six Telecoms, Rashid Shamte akizungumzia uzalishaji wa umeme kwa njia ya upepo utakaosimamiwa na Kampuni ya kuzalisha umeme huo ya Afrika Masharikana awamu ya kwanza itaanzia mkoani Singida.  
Alex Moulds kutoka Energy Net Limited akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuzalisha umeme wa Upepo

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Mh. January Makamba amesema kuwa mpango wa serikali ni kuwa na vyanzo vingi vya uzalishaji umeme ili kuwa na vyanzo vya nchi endelevu na kuunga mkono juhudi za benki ya dunia kuzalisha umeme wa upepo katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.

Makamba amesema hayo wakati wa Kongamano la wadau wa Nishati ya umeme walipokutana kuzungumzia matumizi ya Nishati ya umeme inayozalishwa kwa njia ya upepo itakayounganishwa kwenye gridi ya taifa na mfumo huo utawasaidia wananchi wa Singida .

"Kwa kuwa umeme huo utazalishwa kwenye maeneo ya vijijini, wananchi wanatakiwa kupata umeme kwa bei rahisi kulingana na uchumi wao na sio kuuziwa umeme kwa bei juu, na zaidi Wizara yake inapenda kuweka  wazi kuwa huu mradi una faida kubwa sana kulingana na mfumo wa nchi ulivyo,"amesema Makamba.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo Afrika Mashariki Six Telecoms,  Rashid Shamte amessema kuwa mfumo huu wa gridi ndogondogo una faida kubwa sana kwa wananchi kwani asilimia kubwa kulingana na ripoti ya benki ya dunia wananunua umeme wa bei nafuu kwahiyo serikali imekubaliana na kampuni yetu na  imeweza kukubali kuwa mradi huu una  tija na  utasimamiwa na serikali yenyewe kupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida pamoja na Halmashauri.

Shamte ameendelea na kusema, kwa Phase ya kwanza watatoa umeme megawati 100 na itaendelea mpaka kufika megawati 300 na wataunganisha kwenye gridi ya taifa, na huu mradi utakuwa na faida kwa wananchi pamoja na wale watakaotolewa kwenye maeneo yao watafaidika kwa kulipa stahiki zao.

Kwa upande wa Wizara ya Nishati na Madini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo amewataka wawekezaji hao kuuza umeme kwa bei rahisi kwani mara nyingi mipango ya serikali imekuwa haiendani na mikakati ya wawekezaji kwahiyo wanategemea kuona kuwa mradi huu uwe nafuu ya wananchi wa vijijini kupata umeme kwa bei rahisi.

WAHARIRI WAKUTANA KUPITIA SHERIA YA HUDUMA YA VYOMBO VYA HABARI ILIYOPITISHWA NA BUNGE

0
0
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga (kulia), akizungumza Dar es Salaam leo wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa wahariri  kupitia sheria ya huduma ya vyombo vya habari uliyopitishwa na Bunge pamoja na kujadili mpango mkakati wa TEF wa kuendeleza tasnia ya habari nchini. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura.
 Mtaalamu Mshauri Rosemary Mwakitwange akiongoza 
mkutano huo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura.
 Mwakilishi kutoka Jukwaa la Wahariri la Afrika Kusini akizungumza kwenye mkutano huo.
 Makamu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile akizungumza kwenye mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga (kulia) na Mtaalamu Mshauri Rosemary Mwakitwange wakiangalia mada zitakazo jadiriwa katika mkutano huo.
 Wahariri Idrisa Jabir na Charles Mwankenja (kulia), wakijadili jambo.
 Wahariri kutoka kushoto, Joseph Kulangwa, Abdallah Majura na Ibrahim Issa ambaye ni mjumbe wa TEF wakifurahia jambo kwenye mkutano huo.
 Wahariri wakifurahia jambo.
 Wahariri wakiwa kwenye mkutano huo.
 Wahariri, Joseph Kulangwa na Abdallah Majura wakipitia mada zitakazo jadiriwa.
 Wahariri, Shermax  Ngahemera (kushoto), Julian Msacky na Flora Wingia (kulia), wakifuatilia mada za mkutano huo.
 Taswira ndani ya ukumbi wa mkutano huo
Wahariri ndani ya chumba cha mkutano.

Na Dotto Mwaibale

WAHARIRI wa vyombo vya habari wamekutana katika mkutano maalumu wa siku mbili kwa ajili ya kujadili mambo kadhaa yanayohusu tasnia hiyo nchini.

Akizungumza wakati akifungua mkutano huo Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga alisema mkutano huo utawajumuisha wadau wa sekta ya habari kutoka ndani na nje ya nchi.

"Tumewaalika wenzetu wa nje ili watupe uzoefu wa jinsi wanavyofanya katika tasnia ya habari katika nchi zao" alisema Makunga.

Alisema katika mkutano huo ambao unafanyika Hoteli ya Protea Court Yard mambo yatakayo zungumziwa ni kupitia sheria ya huduma ya vyombo vya habari iliyopitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais Dk. John Magufuli pamoja na kujadili mpango mkakati wa Jukwa la Wahariri wa kuendeleza tasnia ya habari nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura alisema ni muhimu kwa wanahabari kuwa na mpango mkakati wa miaka 10 ili kupata majibu sahihi ya tasnia hiyo.

MWAKYEMBE AWAFUNDA WAJUMBE WA KAMATI YA KUZUIA MUAJI YA KIMBARI KWA NCHI ZA MAZIWA MAKUU

0
0

Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Dkt Harrison Mwakyembe amewataka wajumbe wa Kamati ya Kimataifa inayojishughulisha na kuzuia mauaji ya kimbari katika nchi za ukanda wa Maziwa Makuu kuangalia upya mikakati ya kuondoa vitendo vya mauaji ya kimbari na ukiukwaji wa haki za binadamu katika ukanda huo.

Dkt. Mwakyembe amesema Ukanda wa Maziwa Makuu umekuwa ukishuhudia vitendo vya mauaji ya kimbari vikishamiri licha ya kwamba kila nchi imekuwa ikichukua jitihada mbalimbali na kusaini makubaliano ya kikanda na kimataifa ya kuzuia vitendo hivyo.

Amesema wakati sasa umefika wa kujiangalia ni kwanini vitendo hivyo vimekuwa vikishamiri pamoja na jitihada zote ambazo kila nchi imekuwa ikizichukua ili kukomesha vitendo hivyo.

“ Ni wazi kuwa siku hizi mwelekeo wa matukio ya kihalifu umebadilika, zimeibuka njia nyingi mpya zinazosababisha mauaji ya kimbari na hata ukiukwaji wa haki za binadamu, kutokana na hali hiyo kuna haja ya kuboresha mikakati yenu ili kuzuia kuendelea kutokea kwa mauaji ya kimbari na ukiukwaji wa haki za binadamu,” alisema.

Aidha Mhe. Waziri pia amewaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni jukumu lao kuangalia namna ya kukabiliana changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza na hivyo kufanya vitendo hivyo kuendelea kuwepo miongoni mwa nchi za maziwa makuu.Amewataka wataalamu hao kwenda mbali zaidi na kubainisha hatua zitakazofaa kuchukuliwa za kisera, kisheria na kiutawala ili kukabiliana na changamoto ya kuendelea kuwepo kwa vitendo hivyo ili kuvikomesha ndani ya nchi za ukanda wa maziwa makuu 

Mhe. Dkt Mwakyembe alikuwa akifungua mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo na kubadilisha na uzoefu wajumbe wa Kamati hiyo kwa nchi za Maziwa Makuu yanayofanyika jijini Dar es salaam. Mafunzo hayo yanajumuisha wajumbe kutoka nchi za Zambia, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Congo DRC, Sudani Kusini na mwenyeji Tanzania.

SERIKALI YAOMBWA KUWAPATIA BIMA YA AFYA WALEMAVU WA NGOZI

0
0
Na Anthony John Globu ya Jamii.

CHAMA cha watu wenye ualbino Tanzania (TAS) kimetoa wito kwa Serikali kuwapatia bima ya Afya watu wenye ulemavu wa ngozi ili kuweza kuwasaidia pale wanapokuwa na matatizo ya kiafya.

Akiongea  na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam katika Ofisi ya chama hicho iliyopo hospitali ya Ocean Road, Muweka hazina Abdilah Omary amesema watu wenye ualbino hasa waliopo vijijini wanapata changamoto kubwa ya upatikanaji wa matibabu hasa pale wanapo sumbuliwa na magonjwa mbali mbali.

 Abdilah ametoa wito kwa jamii na familia zenye watu wenye ualbino kuwapa malezi yanayoendana na hali yao tofauti na Jamii nyingi kwa hivi sasa wanawalazimisha watu wenye ualbino kufanya kazi ngumu kama kuchunga ngo'mbe na kulima.

Wakati huo huo wajumbe wa chama cha watu wenye ualbino Tanzania wamemchangia kiasi cha sh.milioni moja Leonard Gaspar mwenye ulemavu wa ngozi Mkazi wa Morogoro Matombo anayesumbuliwa na kansa ya ngozi.

Hata hivyo Leonard  amewashukuru wajumbe wa chama hicho kwa mchango huo huku akiomba jamii na wadau mbalimbali kuwapa msaada pale wanapoweza ili apate mtaji wakumsaidia katika maisha ya kila siku na matibabu.

Chama hicho cha watu wenye ualbino Tanzania wametoa wito kwa jamii kumsaidia kijana Leonard anaye sumbuliwa na tatizo la kansa ya ngozi kwa muda mrefu.

Hata Hivyo Abdilah ameomba Jamii ya watanzania watakaoguswa na tatizo alilonalo Leonard wanaweza kutoa michango yao kwa kuwasiliana na Ofisi za Chama Cha Watu Wenye Ualbino kilichopo Katika Hospital ya Ocean Road.
Muweka hazina wa Chama cha Watu wenye Ualbino Tanzania, Abdilah Omari  akiwa pamoja Leonard Gasper anayesumbuliwa na tatizo la kansa na kumpatia msaada wa kiasi cha fedha milioni moja kwa ajili ya matibabu.
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images