Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

MKUTANO WA MAHUBIRI YA INJILI YA NABII MALISA JIJININI ARUSHA

$
0
0
Kiongozi mkuu wa kanisa la Ukombozi ,Nabii B.G Malisa akihubiri katika mkutano mkubwa wa maombezi wa siku 8 katika viwanja vya reli jijini Arusha ambapo amewatakaWatanzaniakudumisha amani ya nchi kwa kuepuka kufanya matukio ambayo yanaweza kuchochea vurugu na hatari ya kuliingiza taifa katika hali ya machafuko. (Picha na Pamela Mollel).
Kulia ni mama mchungaji Grace Mshindi wa kanisa la ukombozi tawi la Arusha akiwa anazungumza na watu waliojitokeza katika mkutano huo wa maombezi na kupokea uponyaji.
.Watu mbalimbali waliojitokeza katika mkutano wa Kiongozi mkuu wa kanisa la Ukombozi ,Nabii B.G Malisa unaofanyika katika viwanja vya reli jijini Arusha. 
Taswira ya watu waliojitokeza katika mkutano huo .

Pamela Mollel,Arusha


Watanzania wametakiwa kudumisha amani ya nchi kwa kuepuka kufanya matukio ambayo yanaweza kuchochea vurugu na hatari ya kuliingiza taifa katika hali ya machafuko. 

Wito huo umetolewa jana na mchungaji kiongozi wa kanisa la Ukombozi hapa nchini, Nabii B. G Malisa wakati alipokuwa akihubiri neno la Mungu katika viwanja vya reli jijini Arusha na kuhudhuriwa na maelfu ya watu

Nabii Malisa alisema kwamba watanzania wana jukumu kubwa la kuhakikisha wanaombea amani ya nchi iendelee kutawala kwa kuwa bila amani hakuna kitu kitakachoweza kuendelea katika nchi hii.

Aidha alisema kuwa amekuwa akifanya ziara mbalimbali katika nchi mbalimbali duniani na kushuhudia hali ya usalama ikiwa tete ambapo askari wamekuwa wakitembea mitaani huku wameshika silaha za moto. 

"Hivi karibuni nilikuwa Nigeria wakati nashuka uwanja wa ndege nilipokelewa na askari wenye silaha za moto nikajiuliza maswali mengi sana kuhusu amani tuliyonayo hapa Tanzania "alisema Malisa 

Hatahivyo, alitoa wito kwa serikali kuunga mkono juhudi za viongozi mbalimbali wa dini hapa nchini katika kuwasaidia vijana na kusema viongozi wa dini wanafanya kazi kubwa katika kuwainua watu kiuchumi na kuwaepusha na vitendo viovu. 

Awali akizungumza na waandishi wa habari mchungaji wa kanisa la Ukombozi tawi la Arusha Mchungaji Ushindi alisema kwamba mhubiri huyo atakwenda kufanya huduma ya maombezi mkoani Arusha kwa siku nane na kuwataka wakazi hao kujitokeza kwa wingi. 

Mchungaji Ushindi alisema kuwa wakazi wa jiji la Arusha wamepata neema kubwa ya kupata neno la Mungu kupitia mkutano huo wa maombezi .

UDSM YATAKIWA KUHAKIKISHA INAENDELEA KUWA CHUO KIKUU KIONGOZI

$
0
0

Rais Mstaafu wa awamu ya nne ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na washiriki wa kongamano la kuazimisha miaka 55 toka kuanzishwa kwa Chuo Kikuu hicho mapema hii leo Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri wa Heshima Prof. Tade Aina toka nchini Nigeria akielezea hali ya vyuo vikuu vya Afrika katika muktadha wa Kimataifa wakati wa kongamano la kuazimisha miaka 55 toka kuanzishwa kwa Chuo Kikuu hicho mapema hii leo Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa kongamano maalum la kuazimisha miaka 55 toka kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakimsikiliza kwa makini Mhadhiri wa Heshima Prof. Tade Aina toka nchini Nigeria wakati akielezea hali ya vyuo vikuu vya Afrika katika muktadha wa Kimataifa mapema hii leo Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kushoto) wakati wa kongamano la kuazimisha miaka 55 toka kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mapema hii leo Chuoni hapo, katikati ni Mhadhiri wa Heshima Prof. Tade Aina toka nchini Nigeria.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Wakuu wa Vitivo wa Chuo hicho wakati wa kongamano la kusherehekea kutimiza miaka 55 toka kuanzishwa kwa chuo hicho.

Picha na Eliphace Marwa – Maelezo

……………………………………………………….

Na: Frank Shija, MAELEZO.

UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) takiwa kuhakikisha Chuo hicho kinaendelea kuwa kiongozi miongoni mwa Vyuo Vikuu nchini.

Ushauri huo umetolewa na Rais mstaafu wa awamu ya Nne ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipokuwa akifungua maadhimisho ya miaka 55 ya chuo hicho leo Jijini Dar es Salaam.

“Hiki ndicho Chuo kiongozi kati ya Vyuo Vikuu vyote hapa nchini, mnatakiwa kuhakikisha kinaendelea kuwa kiongozi huku Vyuo vingine vikifuatia”. Alisema Dkt. Kikwete

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Lwekaza Mukandara amesema kuwa pamoja na changamoto zinazo kikabili chuo hicho wanaishukuru Serikali kwa kuendelea kusaidia katika kuleta maendeleo ya chuo hicho.

Alisema kuwa baadhi ya changamoto zimetatuliwa kwa pamoja kati ya Serikali na wahisani ambapo alisema kuwa ujenzi wa kumbi mpya za mihadhara, Maabara za Kisasa na jengo la malazi,pamoja na ujenzi wa hosteli za wanafunzi unaoendelea katika Kampasi ya Julius K. Nyerere ambayo itakuwa na uwezo wa kutumiwa na wanafunzi 4000 mara itakapo kamilika.

Akiwasilisha mada juu ya “hali ya Taaluma Barani Afrika katika Muktadha wa Kimataifa” Mhadhiri wa Heshima kutoka nchini Nigeria, Profesa Tade Aina amesema kuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni moja kati ya Vyuo Vikuu mahiri barani Afrika ambapo kimetoa mchango mkubwa kwa ukombozi wa nchi nyingi za bara hili.

Aliongeza kuwa yeye binafsi ni mnufaika mkubwa wa UDSM kwani amekuwa na ushirikiano mkubwa na baadhi ya wahadhiri kutoka chuo hicho katika masuala mbalimbali ya taaluma.

Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wakati wa uwasilishaji mada alisema kuwa kipindi Chuo hiki kinaanzishwa aina ya masomo yaliyokuwa yanafundishwa chuoni hapo yalikuwa na muelekeo kuandaa wafanyakazi wa Serikali kwa wakati huo.

Na kuongeza kuwa muelekeo wa aina ya masomo uliendelea kubadilika kadri ya siku zilivyokwenda kutokana na mabadiliko ya teknolojia na uhitaji wa soko la ajira.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinaadhimisha miaka 55 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1961 kikiwa ni tawi la Chuo Kikuu cha London, ambapo awali kilianzia katika mtaa wa Lumumba kikiwa na wanafunzi 14 kabla ya kujengwa mahali kilipo sasa katika eneo la Mlimani.

WAZIRI WA FEDHA DK MPANGO AMWAKILISHA RAIS MKUTANO WA TANO WA USHIRIKIANO KATI YA NCHI ZA KIAFRIKA NA KOREA KUSINI

$
0
0
MKUTANO wa Tano wa Ushirikiano kati ya Nchi za Kiafrika na Korea Kusini (Korea-Africa Economic Cooperation (KOAFEC), Umefunguliwa leo Jijini Seoul, Korea Kusini, huku agenda kubwa ikiwa ni kuzungumzia namna nchi za Kiafrika zinavyoweza kutumia kilimo katika muktadha wa maendeleo ya viwanda ili ziweze kujikwamua haraka kiuchumi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, anawakilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb) katika mkutano huo unahusisha nchi 54 za kiafrika na nchi ya Korea Kusini.

Dkt. Mpango ameuelezea mkutano huo ulioandaliwa na Serikali ya Korea Kusini kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya EXIM ya nchini humo, kwamba utaleta mapinduzi makubwa katika nchi za kiafrika ikiwemo Tanzania kwa kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika kilimo, rasilimali watu na teknolojia ya habari na Mawasiliano-TEHAMA.

Amesema kuwa nchi ya Korea Kusini ilipata uhuru mwaka mmoja na nchi ya Ghana, Mwaka 1954 miaka michache kabla ya Tanzania Bara kupata uhuru wake, lakini imepiga hatua kubwa kimaendeleo na kuwa moja kati ya nchi za ulimwengu wa kwanza kiuchumi, lakini Ghana na Tanzania bado ni nchi masikini.“Ni jambo zuri kwamba tuimarishe ushirikiano na Korea Kusini ili njia walizotumia kupiga hatua kubwa kimaendeleo, na sisi tuweze kujifunza kwa haraka” alifafanua Dkt. Mpango

Amesema kuwa Baadhi ya Mawaziri wenzake wa Fedha aliozungumza nao wanaokuwa uongozi thabiti wa nchi na uwekezaji mkubwa katika rasilimali watu na kilimo cha kisasa, vinaweza kuzikwamua nchi za Kiafrika kuondokana na umasikini.

“ Ni muhimu sana elimu na ujuzi tuyasisitize tunapoanza hatua ya kujenga Tanzania mpya kwa nguvu zaidi lakini jambo linguine ni ukweli kwamba kilimo ndio msingi ambao watu wetu wengi wako huko wanaishi kwa kutegemea kilimo kwa hiyo mkutano huu unaendana kabisa na mkakati wetu wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa” alisema Dkt. Mpango

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Utafutaji rasilimali kutoka serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Sabra Issa Machamo, amesema kuwa uhusiano wa Zanzibar na Korea Kusini ni wa kuigwa ambapo nchi hiyo inafadhili mradi mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji unaotarajiwa kujengwa visiwani humo.

Akifungua Mkutano huo, Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Fedha wa Korea Kusini II Ho YOO (ILU Ho Yuu), amesema kuwa serikali yake imeamua kuwekeza kiasi kikubwa cha rasilimali zake kuendeleza nchi za Afrika kupitia sekta za kilimo, rasilimali watu na viwanda.

Amesema mkazo mkubwa utakuwa kuishirikisha sekta binafsi kusisimua uchumi wa nchi zinazonufaika na mpango huo ili kuharakisha maendeleo ya nchi hizo.“Hatua hii itachangia sana kupunguza umasikini uliokithiri pamoja ja kuzalisha ajira nyingi ambazo zitaleta matumaini kwa kizazi za vijana” Alisema Yoo.

Bw. Yoo amesema kuwa katika miongo miwili iliyopita, nchi za kiafrika zimapiga hatua kubwa katika nyanza za afya, elimu na mambo mengine kadha wa kadha lakini akaonya kuwa matukio ya uvunjifu wa Amani na mizozo ya kivita vinakwaza maendeleo ya nchi hizo.

Naye Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika, Akinwumi Adesina, amesema kuwa benki yake hivi sasa imeelekeza nguvu zake katika vipaumbele vitano ambavyo baadhi yake ni kuimarisha kilimo biashara kitakacholisha Afrika, kuboresha miundombinu ya sekta ya umeme, viwanda na kuiunganisha Afrika kiuchumi na kiuwekezaji, kuboresha huduma za jamii kama vile maji, chakula, usafi wa mazingira na mambo mengine kama hayo.

Mkutano wa tano wa KOAFEC mwaka huu umebeba kaulimbiu ya kuibadili Afrika kwa njia kilimo na mpango jumuifu wa watu unaolenga kuimarisha sekta ya fedha kwa njia ya mitandao ya simu” (Transforming Africa’s Agriculture through Industrialization and Inclusive Finance)

TAZAMA PICHA MBALIMBALI ZA HAFLA YA UTILIAJI SAINI MIKATABA 21 KATI YA TANZANIA NA MORROCO

$
0
0


Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco Akisalimiana na baadhi ya wananchi waliojitokeza kumpokea leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco wakiwaangalia wapigaji ngoma mara baada ya kuwasili Leo Ikulu Jijiji Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco wakipiga ngoma mara baada ya kuwasili Leo Ikulu Jijiji Dar es Salaam.


Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliohudhuria hafla ya utiaji saini wa mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.

Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustino Mahiga akiizungumzia mikataba 21 itakayosainiwa kati ya Tanzania na Morocco.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akieleza namna Tanzania itakavyonufaika na mikataba 21 iliyosaniwa katika ya Nchi ya Morocco na Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano ya Morocco Bw. Salahddine Mezouar akimueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli sababu za kuja kuwekeza Tanzania Ikiwamo utulivu wa Kisiasa na ushirikiano wa Muda mrefu.
Mwenyekiti wa shirikisho la wafanyabiashara wa Morocco Bi. Miriem Bensalah akiongea na kwenye hafla utiaji saini ambapo wamekubaliana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania kuanzisha Baraza la Biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano ya Morocco Bw. Salahddine Mezouar na Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustino Mahiga wakisaini moja ya mikataba 21 leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano ya Morocco Bw. Salahddine Mezouar na Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustino Mahiga wakibadilishana mikataba leo Jijini Dar es Salaam.



Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Sekta binafsi Tanzania pamoja na wenzao wa Morocco wakisaini na kubadilishana mikataba leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na viongozi wa serikali na sekta binafsi wa Tanzania na Morocco wakati wa hafla ya utiaji saini wa Mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili kwa ajili ya kumpokea Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na viongozi wa ulinzi wakati wa kumpokea Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco kwa ajili ya hafla utiaji saini wa mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiwaeleza jambo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco mara baada ya kuwasili Ikulu leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya hafla utiaji saini wa mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.
Picha na Hassan Silayo



Na Daudi Manongi .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli amesema kuwa wamekubaliana na Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco kujenga Uwanja wa Mpira wa miguu wa kisasa mkoani Dodoma utakaogharimu dola milioni 100.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam baada ya kutiliana saini kwa mikataba 21 ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi za Tanzania na Morocco.

“Mbali na mikataba baina ya Tanzania na Morocco nimezungumza mambo mbalimbali na Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco na nimemuomba atujengee Uwanja mkubwa wa mpira pale Makao Makuu yetu Dodoma utakaokuwa na thamani kati ya dola milioni 80 hadi 100 na amesema ataujenga, kwa hiyo utakuwa Uwanja mkubwa kuliko wa Dar es Salaam”. Alisema Rais Magufuli.

Mbali na hayo Rais Magufuli amewahakikishia wafanyabiashara wa Morocco kuwa Tanzania ni salama na inapenda kushirikiana nao, na kuwa nchi yetu iko katika mwelekeo mzuri wa uwekezaji ambapo uchumi wa nchi yetu unategemea kukua kwa asilimia 7.2 mwishoni mwa mwaka.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco Bw.Salahddine Mezour ameishukuru nchi ya Tanzania kwa ushirikiano iliounyesha na kusema kuwa Morocco itaendelea kushirikiana na Tanzania katika Nyanja mbalimbali kwa kuwa ina utulivu wa kisiasa na icho ndo kimekuwa kivutio kikubwa katika kuwekeza kwao nchini hapa.

Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais, Dk John Pombe Magufuli ikiwa na lengo la kuimarisha uhusiano uliopo baina ya nchi hizi mbili na kutiliana saini mikataba 21 ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

MKURUGENZI WA JIJI LA MWANZA ASHIKILIA MSIMAMO WAKE DHIDI YA WATENDAJI WA SERIKALI ZA MITAA

$
0
0
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba, akihojiwa na Waandishi wa Habari Jijini Mwanza, kuhusiana na sakata la Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Jijini Mwanza kugoma kukabidhi mihuri yao ya utendaji kazi.

Na George Binagi-GB Pazzo

"Hii mihuri ya Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ni dili, hivyo haitambuliki kwa sasa, kwanza imesababisha migogoro mingi kwa wananchi ikiwemo uuzaji wa viwanja kiholela". Amesisitiza Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba.Ameshikilia msimamo wake kwamba mihuri ya Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Jijini Mwanza haitambuliki kama awali alivyosema kwamba waikabidhi ofisini kwake.

Leo Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Jijini Mwanza wameendelea kushikilia msimamo wao wa kutorudisha mihuri hiyo huku wakitishia kutoshirikiana na Watendaji Jijini Mwanza.Juzi jumamosi Wenyeviti 174 wa Serikali za Mitaa Jijini Mwanza, walivunja kikao na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, baada ya Mkurugenzi huyo kuwataka kukabidhi mihuri yao.

#Lakefm #BinagiBlog #BMG #Mwanza

MAHAKAMA YA RUFAA YASHIDWA KUTOA HUKUMU KESI YA UCHAGUZI INAYOWAKIBILI ONESMO NANGOLE NA DKT KIRUSWA

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiongea na waandishi wa habari mara baada ya maamuzi ya rufaa iliyofunguliwa na aliyekuwa mbunge wa jimbo la longine Onesmo Nangole.
Na Woinde Shizza,Arusha 

Mahakama ya rufaa kanda ya Arusha imeshindwa kutoa maamuzi ya rufaa iliyofunguliwa  na aliyekuwa mbunge wa jimbo la Longido ,Onesmo Nangole(CHADEMA) ambaye anapinga maamuzi ya mahakama kuu iliyomvua ubunge wake, badala yake imeagiza mwanasheria mkuu wa serikali na msimamizi mkuu wa uchaguzi katika jimbo hilo aunganishwe katika shauri hilo.


Aidha mahakama hiyo imetoa siku 21 kwa mrufani kwa ajili ya kufanya marekebisho ya notisi yake ya rufaa na kuyaleta mahakamani hapo ili msimamizi wa uchaguzi pamoja na mwanasheria mkuu wa serikali waingizwe  kama mashaidi  muhimu katika rufaa.


Akisoma taarifa ya majaji watatu walikuwa wakisikiliza rufaa hiyo mahakamani hapo Msajili wa mahakama rufaa John Kayanza alisema kuwa mahakama ya rufaa aitatenda haki katika hukumu yake iwapo haita msikiliza mwanasheria wa serikali pamoja na msimamizi wa uchaguzi jimbo la Longido na imewataja kama mashaidi muhimu kwa upande wa mrufani


“kama mahakama itatoa uamuzi bila kusikiliza mwanasheria wa serikali na msimamizi wa uchaguzi haitakuwa imetenda haki  katika mahamuzi hivyo mahakama imeonelea ni vizuri  mrifani akaifanyie marekebisho notisi yake na ndani ya siku 21 aiwasilishe mahakamani”alisema Kayanza


Katika rufaa hiyo mrufani Onesmo Nangole aliyekuwa mbunge wa jimbo la Longido alikata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama kuu kanda ya Arusha ambayo ilitengua ubunge wake na kuagiza msimamizi  wa uchaguzi atangaze jimbo hilo kuwa lipo wazi.


Katika kesi hiyo Onesmo Nangole( CHADEMA) anawakilishwa na mawakili wawili ambao ni  Methodi kimomogoro akisaidia na wakili John Materu ambapo kwa upande wa warufaniwa Dkt.Steven Kiruswa (CCM) anawakilishwa na mawakili watatu wakiongozwa na DKT.Masumbuko Lamwai akisaidiwa na Daudi Haraka pamoja na Edmond Ngemela.


Rufaa  hiyo inasikilizwa  na Majaji  watatu ambao ni jaji Sauda   Mjasiri,Jaji Musa Kipenka pamoja na Profesa Ibrahimu Juma.


Akiongea mara baada ya kesi hiyo kuairishwa Onesmo Nangole alisema kuwa anaishukuru mahakama kwa kuwapa nafasi na kuona umuimu wa mwanasheria wa serikali pamoja na msimamizi wa uchaguzi wilayani longodo kuja kutoa ushaidi katika shauri hilo na anaamini mahakama hiyo itamtendea haki.


Kwa upande wa Dkt,Kiruswa (CCM) alisema yeye atatizo na maamuzi ya mahakama na anaiachia mahakama iendelee kushulikia shauri hilo na anaamini itatenda haki.

SERIKALI YAKANUSHA TAARIFA ILIYOSAMBAA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII KUWA ITAANZA KUTOA AJIRA, KUPANDISHA VYEO NA KULIPA STAHIKI MBALIMBALI ZA WATUMISHI WA UMMA MWEZI FEBRUARI, 2017.

Morocco kujenga uwanja wa Mpira mkoani Dodoma.

$
0
0

Na Daudi Manongi; MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli amesema kuwa wamekubaliana na Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco kujenga Uwanja wa Mpira wa miguu wa kisasa mkoani Dodoma utakaogharimu dola milioni 100.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam baada ya kutiliana saini kwa mikataba 21 ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi za Tanzania na Morocco.

“Mbali na mikataba baina ya Tanzania na Morocco nimezungumza mambo mbalimbali na Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco na nimemuomba atujengee Uwanja mkubwa wa mpira pale Makao Makuu yetu Dodoma utakaokuwa na thamani kati ya dola milioni 80 hadi 100 na amesema ataujenga, kwa hiyo utakuwa Uwanja mkubwa kuliko wa Dar es Salaam”. Alisema Rais Magufuli.

Mbali na hayo Rais Magufuli amewahakikishia wafanyabiashara wa Morocco kuwa Tanzania ni salama na inapenda kushirikiana nao, na kuwa nchi yetu iko katika mwelekeo mzuri wa uwekezaji ambapo uchumi wa nchi yetu unategemea kukua kwa asilimia 7.2 mwishoni mwa mwaka.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco Bw.Salahddine Mezour ameishukuru nchi ya Tanzania kwa ushirikiano iliounyesha na kusema kuwa Morocco itaendelea kushirikiana na Tanzania katika Nyanja mbalimbali kwa kuwa ina utulivu wa kisiasa na icho ndo kimekuwa kivutio kikubwa katika kuwekeza kwao nchini hapa.

Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais, Dk John Pombe Magufuli ikiwa na lengo la kuimarisha uhusiano uliopo baina ya nchi hizi mbili na kutiliana saini mikataba 21 ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Serikali kupitia mpango wa kuinua ubora wa Elimu Tanzania

$
0
0
 
Na. Lilian Lundo-Dodoma.

(Education Quality Improvement Programme Tanzania- EQUIP-T) umepunguza kiwango cha utoro na idadi ya wanafunzi wasiojuakusoma na kuandika shule za Msingi mkoani Dodoma.Hayo yamesemwa leo, Mjini Dodoma na Kiongozi wa mpango huo Mkoa wa Dodoma Francis Liboy katika semina ya mawasiliano ngazi ya Wilaya na jinsi ya kupashana simulizi ya mabadiliko iliooandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na EQIP-T.

"Mradi wa EQUIP-T umewezesha walimu shule za msingi kupata mafunzo mbalimbali ya njia bora ya ufundishaji kea wanafunzi wa madarasa ya Awali mpaka darasa la Nne kujua kusoma,kuandika na kuhesabu kwa ufasaha na kwa muda mfupi," alifafanua Liboy.

Kutokana na mafunzo hayo kwa walimu idadi ya wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu imepungua kwa kiasi kikubwa kwa mkoa wa Dodoma na wilaya zake kutokana na walimu kuwa na mbinu mbalimbali za ufundishaji.Mpango huo pia umeweza kuifanya jamii kuona shule ni mali
yao hivyo jamii imekuwa mstali wa mbele kufuatilia mahudhurio ya watoto wao hivyo kupunnguza utoro kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake Afisa Elimu Vifaa na Takwimu Wilaya ya Mpwapwa Anderson Njolegwa amesema kuwa mpango huo umeweza kupunguza utoro katika Wilaya hiyo kutoka wanafunzi 828 mwaka 2013 mpaka wanafunzi 572 mwaka 2016 ambao wanaendelea kupungua kila siku.

Mpango wa EQUIP-T ni mpango wa miaka minne ambao ulianza mwaka 2014 ukiwa na dhamira ya kuinua ubora wa Elimu Nchini ambapo mpaka sasa mpango huo upo katika mikoa ya Dodoma, Kigoma, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Mara na Lindi.

AJALI ZA BARABARANI ZAENDELEA KUUA NA KUACHA MAJERUHI MKOANI MWANZA.

$
0
0

Baada ya Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kufanyika Kitaifa mkoani Geita kuanzia Septemba 29 hadi Oktoba Mosi Mwaka huu, Maadhimisho kama hayo kwa mkoa wa Mwanza yamezinduliwa hii leo kwenye Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza ambapo imeelezwa kwamba bado juhudi za kila mtumiaji wa barabara zinahitajika ili kutokomeza ajali za barabarani.

Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani Mwanza, Robert Hussein, amebainisha kwamba kwa kipindi cha mwaka jana kati ya mwezi januari na septemba kulikuwa na ajali 161 zilizosababisha vifo 132 na majeruhi 187 na kwamba kwa kipindi kama hicho mwaka huu kulikuwa na ajali 159 zilizosababisha vifo 150 na majeruhi 162 ambapo takwimu hizo zinaonesha kuwepo kwa ongezeko la vifo 18 sawa na asilimia 12 na upungufu wa majeruhi 25 sawa na asilimia 13.3

Pichani juu ni maandamano ya bodaboda pamoja na wa watumiaji wengine wa barabara yakiingia Uwanjani kwenye maadhimisho hayo ambayo yamezinduliwa na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella.

Na BMG
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya usalama barabarani mkoani Mwanza
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Ahmed Msangi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya usalama barabarani mkoani Mwanza
Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani Mwanza, Robert Hussein, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya usalama barabarani mkoani Mwanza
Viongozi mbalimbali mkoani Mwanza
Baadhi ya maofisa wa polisi mkoani Mwanza
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella (kushoto) akiteta jambo na Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Ahmed Msangi (kulia) kwenye uzinduzi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mary Tesha (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Dkt.Leonald Massale (kulia) kwenye uzinduzi huo.
Mwanahabari Simba Kabonga wa Barmedas Tv akipokea cheti cha utambuzi wa kampuni hiyo katika kutoa elimu ya usalama barabarani
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Bodaboda mkoani Mwanza, Seifu Kagoma, akionesha cheti cha utambuzi kwa taasisi hiyo kutoka kwa Kamati ya usalama barabarani mkoani Mwanza.
Wanafunzi wa shule ya Msingi Butimba Jijini Mwanza wakiingia uwanjani kuimba wimbo wa kuhamasisha matumizi sahihi na salama ya barabarani.
Askari wa usalama barabarani mkoani Mwanza, wakitoa elimu ya usalama barabarani kwa baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani mkoani Mwanza.

Na George Binagi-GB Pazzo

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amewataka watumiaji wa barabara mkoani Mwanza, kuzingatia sheria za usalama barabarani jambo ambalo litasaidia juhudi za kupambana na ajali kufanikiwa.

Mongella ametoa kauli hiyo hii leo kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani mkoani Mwanza, uliofanyika katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza, ambapo elimu ya usalama barabarani itaendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo kwa juma zima.

Amesema watumiaji wote wa barabara wanao wajibu wa kufuata sheria za usalama barabarani huku akikemea tabia ya baadhi ya abiria wanaowahimiza madereva kuendesha vyombo vyao kwa mwendo kasi.

Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani Mwanza, Robert Hussein, amebainisha kwamba kwa kipindi cha mwaka jana kati ya mwezi januari na septemba kulikuwa na ajali 161 zilizosababisha vifo 132 na majeruhi 187 na kwamba kwa kipindi kama hicho mwaka huu kulikuwa na ajali 159 zilizosababisha vifo 150 na majeruhi 162 ambapo takwimu hizo zinaonesha kuwepo kwa ongezeko la vifo 18 sawa na asilimia 12 na upungufu wa majeruhi 25 sawa na asilimia 13.3

Akizungumza kwa niaba ya watumiaji wa barabara, Makamu Mwenyekiti wa Waendesha bodaboda mkoani Mwanza, Seifu Kagoma, amesema kila mtumiaji wa barabara anao wajibu wa kuwa na tahahadhali awapo barabarani badala ya kusubiri wajibu huo kutoka kwa mwenzake.

Maadhimisho ya wiki ya usalama barabarani hufanyika kila mwaka nchini lengo likiwa ni kutoa elimu ya matumizi sahihi na salama ya barabara kwa makundi yote ya watumiaji wa barabara ambapo mwaka huu kitaifa yalifanyika mkoani Geita kuanzia Septemba 29 hadi Oktoba Mosi ambapo kauli mbiu yake ni “Hatutaki ajali, tunataka kuishi salama”.

BALOZI MAHIGA AWAASA VIJANA NCHINI KUCHANGAMKIE FURSA ZA AJIRA ZINAZOPATIKANA UMOJA WA MATAIFA (UN)

$
0
0

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa afrika mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga amesema ushirikiano wa Tanzania na umoja wa mataifa (UN) wataendeleza ulinzi wa amani katika mataifa mbalimbali kama wanavofanya kwa Sudan ya kusini.

Akizungumza katika hafla ya miaka 71 ya umoja huo Dar es salaam , Balozi Mahiga amewataka Vijana nchini kuchangamkie fursa za ajira zinazopatikana umoja huo.hafla za miaka 71 za umoja wa mataifa zimehudhuliwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa huku suala la ulinzi ' pamoja na amani likiwa limepewa kipaumbele kwa mataifa

Naye Mwakilishi wa Mashirika wa Umoja wa Mataifa Alvaro Rodriguez amezitaja changamoto zinazoikabili UN ni ongezeko la vijana ambapo wengi huwa wanashindwa kuendana na ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia kutokana na miundombinu ya Elimu kutokuwa Rafiki.

Rodriguez ameongeza kuwa Ili kuhakikisha UN inakabiliana na Changamoto hiyo wameweka nguvu zaidi katika kuboresha Miundombinu ya Elimu barani Afrika ili vijana kuweza kuendana na kasi ya utandawazi ili kuweza kujiajiri. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Balozi Augustine Mahiga akizungumza kwenye hafla ya miaka 71 ya umoja wa mataifa (UN) leo jinini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza kwenye hafla ya miaka 71 ya umoja mataifa (UN) leo jinini Dar es Salaam.

MFALME WA MOROCCO MOHAMED VI AWASILI IKULU NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS DKT. MAGUFULI

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakipita katika gadi ya mapokezi iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakilakiwa na wafanyakazi pamoja na wageni mbalimbali katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia Taaswira ya Kinyago alichomkabidhi mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.

MATUKIO MBALIMBALI UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIUCHUMI WA KOREA NA AFRIKA MJINI SEOUL, KOREA KUSINI

$
0
0
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt. Philip Mpango (Mb), akipokea zawadi ya kitabu kinachoelezea njia zilizotumiwa na nchi ya Korea Kusini, kupiha hatua kubwa ya maendeleo, kutoka kwa Afisa Mikopo wa Benki ya Exim ya Korea Kusini, Park Gil Jong, kabla ya kuhudhuria ufunguzi wa mkutano wa tano wa ushirikiano wa Korea Kusini na nchi za Afrika  (KOAFEC), Mjini Seoul, Korea Kusini.(Picha zote na Benny Mwaipaja-WFM (Wizara ya Fedha na Mipango)
rea2
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akionesha kitabu alichozawadiwa na kuelezea umuhimu wake kwa nchi za Kiafrika kukisoma na kukielewa kitabu hicho ili ziweze kuiga mbinu ambazo nchi hiyo imezitumia hadi kuwa miongoni mwa nchi za kwanza kiuchumi duniani.
rea3
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, (Katikati) akiwa na ujumbe wa maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Mipango makao makuu, TRA Tanzania Bara na Zanzibar, Ofisi ya Mwanasheri Mkuu wa Serikali, wanaoshiriki kujadili mkataba wa kuepusha kutoza kodi mara mbili kwa raia wa nchi mbili za Tanzania na Korea, wakiwa mjini Seoul, Korea Kusini.
rea4
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea kwaajili ya ufunguzi wa mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Afrika (KOAFEK), Mjini Seoul, Korea Kusini.
rea5
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akibadilishana mawazo na maafisa kutoka Tanzania kabla ya kuanza kwa mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Kiafrika( KOAFEC), uliofanyika mjini Seoul Korea Kusini. Katikati ni Mkuu wa idara ya kutafuta rasilimali kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Sabra Issa Machamo  na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa  TANESCO, Decklan Mhaiki.
rea6
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, akibadilishana mawazo na watendaji wakuu wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini Kabla ya kufunguliwa Rasmi kwa Mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), unaofanyika Mjini Seoul, Korea Kusini.
rea7
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa katika picha ya pamoja na wapili kushoto, akiwa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Fedha wa Korea Kusini, Yoo II Ho (kushoto kwake) na Rais wa Benki ya EXIM-Korea, Lee Duk-Hoon (Kulia kwa Waziri), kabla ya kuanza rasmi kwa Mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), katika ukumbi wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini.
rea8
Mawaziri wa Fedha kutoka nchi 54 za kiafrika wanaoshiriki Mkutano wa Tano wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi Afrika (KOAFEC) wakiweka alama ya kiganja cha mkono kwenye kibao chenye malighafi maalumu yanayoshika alama za vidole kuonesha ushirikiano na umoja, baada ya kufunguliwa rasmi kwa mkutano huo katika ukumbi wa  Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini.
rea9
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa ameshika kibao alichoweka alama ya kiganja chake, kuunga mkono umoja na mshikamano wa nchi za Kiafrika zinazohusiana kiuchumi na Korea Kusini baada ya kufunguliwa kwa mkutano wa Tano wa ushirikiano huo kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC) katika ukumbi wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini.
rea10
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), (Katikati) (Kulia kwake) na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Akinwumi Adesina, (Kushoto) Baada ya kufunguliwa Rasmi kwa Mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Kiafrika, unaofanyika Mjini Seoul, Korea Kusini
rea11
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa na Maafisa kutoka Tanzania, wakitoka kwenye Ukumbi wa Mikutano  wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini, baada ya kufunguliwa rasmi kwa mkutano wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika, mjini Seoul, Korea.

PICHA MBALIMBALI ZA TUKIO LA RAIS DKT MAGUFULI ALIVYOMKARIBISHA MFALME MOHAMED VI WA MOROCCO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM, MIKATABA 21 YA USHIRIKIANO YASAINIWA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakilakiwa na wafanyakazi pamoja na wageni mbalimbali katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakipigiwa  ngoma pamoja na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kushuhudia uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kushuhudia uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakisoma muhtasari wa shudhuli  katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kabla ya  uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakisoma muhtasari wa shudhuli  katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kabla ya  uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakimsikiliza  Waziri wa Viwanda, Biashara na uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage  katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kabla ya  uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Morocco Mhe. Salahddine Mezour akiongea
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Wafanya Biashara wa Morocco Bi. Miriem Bensalah-Chaqroun akiongea
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kushuhudia uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI  pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kushuhudia uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.
 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo wakibadilishana hati na Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Morocco Mhe. Salahddine Mezour baada ya kutiliana saini makubaliano ya jumla katika mashirikiano ya Kiuchumi, Kisayansi, Kiufundi na Kiutamaduni baina ya serikali ya nchi hizo mbili
 Maafisa wahusika wakiweka  saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.

 Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa Air Tanzania Eng. Ladislaus Matindi akibadilishana hati ya mkataba wa makubaliano na afisa wa Shirika la ndege la Morocco
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  Profesa  Makame Mbarawa wakibadilishana hati na Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Morocco Mhe. Salahddine Mezour baada ya kutiliana saini makubaliano ya Mashirikiano katika sekta za gesi, nishati, madini na Sayansi ya miamba
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Bw. Masanja kadogosa akibadilishana hati  na Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Usafirishaji ya Taifa ya Morocco Bw. Mohamed Ben Ouda baada ya kutiliana saini makubaliano ya Mashirikiano
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Tanzania Bw. Sam kamanga wakiweka saini
 Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. Charles Tizeba na Waziri wa Kilimo wa Morocco Mhe. Aziz Akhannouchi wakipeana mikono baada ya kutia saini makubaliano ya Ushirikiano katika miradi ya Mtangamano wa kuwasaidia Wakulima wadogo Tanzania
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Wafanya Biashara wa Morocco Bi. Miriem Bensalah-Chaqroun akibadilishana hati na Mkurugenzi Mtendaji wa Taaisi ya Sekta Binafsi Tanzania Bw. Godfrey Simbeye
 Maafisa wakipeana mikono baada ya kusaini hati za makubaliano
 Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa akibadilishana hati za makubaliano na Mwenyekiti wa MASEN Bw. Moustapha Bakkoury
 Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa Bw. Sam Kamanga akibadilishana hati za makubaliano na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Bima la Morocco Bw. Hicham Belmrah
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uwekezaji Bw. Joseph Leon Simbakalia akibadilishana hati za makubaliano na Mkrugenzi Mkuu wa SNTL Group ya Morocco Bw. Mohamed Ben Ouda
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Bw. Masanja kadogosa akibadilishana hati  na Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Usafirishaji ya Taifa ya Morocco Bw. Mohamed Ben Ouda baada ya kutiliana saini makubaliano ya Mashirikiano
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Superstar Forwarders Bw. Seif A. Seif akibadilishana hati ya Mkataba wa Mkopo na Mkurugenzi wa Benki ya Afrika (BOA) Bw. Amine Bourati
Mkurugenzi wa CCBRT Bw. Telemans Erwin akibadilishana  hati ya Mkataba wa Mkopo na Mkurugenzi wa Benki ya Afrika (BOA) Bw. Amine Bourati
 Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCBRT Tanzania Bi. Brenda Msangi akipeana mikono Mkurugenzi wa Benki ya Afrika (BOA) Bw. Amine Bourati

Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Bi. Tonia Kandiero kibadilishana hati za Mkataba wa Ubia na Mwenyekiti Mtemdaji Mkuu wa Benki ya Centrale Populaire ya Morocco Bw. Mohamed BenChaaboun
 Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa Bw. Sam Kamanga akibadilishana hati za makubaliano na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Bima la Morocco Bw. Hicham Belmrah
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea wakati a Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia mgeni  wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI 

Wageni wakifurahia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  wakati akiongea katika  Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia mgeni  wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI 
Wageni wakifurahia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  wakati akiongea katika  Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia mgeni  wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI 
Wageni wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  wakati akiongea katika  Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia mgeni  wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB  Dkt. Charles Kimei na wageni wengine wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  wakati akiongea katika  Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia mgeni  wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiwa na watangazaji mashuhuri wa Clouds 360 Baby Kabaye na Bw. Samwel Sasali ambao pia walihudhuria hafla hiyo Ikulu
Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii(TTB), Jaji Mstaafu Thomas Mihayo, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania Bi Devota Mdachi na Meneja Masoko wa TTB Bw. Geofrey Meena na maafisa waandamizi wa bodi hiyo walikuwepo pia
Mpiga picha wa Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI akifurahia ngoma za utamaduni
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimlaki  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI alipowasili kwa dhifa ya Taifa Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI alipowasili kwa dhifa ya Taifa Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na   mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na meza kuu wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa kwenye  dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na   mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na meza kuu wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa kwenye  dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na   mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na meza kuu wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa kwenye  dhifa ya Taifa Ikulu
Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba na wageni wakati wa nyimbo za Taifa
Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na wageni 
Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume na wageni
Mawaziri na wageni
Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa
Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa
Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali George Waitara na Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa
Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa
Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa

Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa
Wageni waalikwa wakisimama wakati wa nyimbo za Taifa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa meza kuu na  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa meza kuu na  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi kwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid karume  kwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha viongozi wa dini  kwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwatambulisha mawaziri kwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulishaWaziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha Waziri wa Kilimo Maliasili Mifugo na Uvuvi Zanzibar Mhe Hamad Rashid Mohammed  kwa  mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakati wa dhifa ya Taifa Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na viongozi wengine wakiangalia ngoma za utamaduni mara baada ya dhifa ya kitaifa ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na viongozi wengine wakiangalia ngoma za utamaduni mara baada ya dhifa ya kitaifa ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na viongozi wengine wakiangalia ngoma za utamaduni mara baada ya dhifa ya kitaifa ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na viongozi wengine wakiangalia kundi la Usambara Mountain Brass Band  mara baada ya dhifa ya kitaifa ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na  Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI na mkewe Mama Janeth Magufuli kabla  ya mgeni kuondoka
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na mkewe Mama Janeth Magufuli baada ya mgeni kuondoka
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na mkewe Mama Janeth Magufuli baada ya mgeni kuondoka. PICHA NA IKULU

VIJUSO VYA BAADHI YA MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 25,2016


MAENDELEO BENKI YAFUNGUA TAWI JIPYA

$
0
0



Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Benki Bw. Ibrahim Mwangalaba akizungumza na wageni waalikwa jana katika uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam,kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Maendeleo Benki Bw. Amulike Ngeliama na Mjumbe wa Bodi hiyo Bw. Naftal Nsemwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Benki Bw. Ibrahim Mwangalaba akiwaongoza wageni waalikwa katika maeneo mbalimbali ya tawi jipya la Mwenge, Dar es Salaam lililozinduliwa jana.
Wageni waalikwa katika hafla fupi ya ufunguzi wa tawi jipya la Maendeleo Benki la Mwenge wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa tawi hilo mapema jana
Baadhi ya wateja wakipata huduma za kibenki katika tawi la Maendeleo Benki lililofunguliwa leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Maendeleo Benki Bw. Amulike Ngeliama akipata huduma katika tawi jipya la benki hiyo baada ya uzinduzi Mwenge, Dar es Salaam

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA BALOZI WA INDIA PAMOJA NA WASUDANI

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa India nchini Mhe. Sandeep Arya (kushoto) aliyemtembelea Makamu wa Rais ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Sudan nchini Mahgoub A. Sharfi (kushoto) alimtembelea na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.
...............................................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema serikali itaendelea kudumisha uhusiano na ushirikiano wa kihistoria kati ya Tanzania na India ambayo yamedumu kwa muda mrefu hasa katika sekta mbalimbali ikiwemo za elimu,afya na biashara.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo leo 25-Okt-2016 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa India nchini Sandeep Arya Ikulu jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais amesema mahusiano kati ya Tanzania na India yamesaidia kunufaisha wananchi wa nchini mbili hasa katika masuala ya kibiashara,miradi ya maendeleo na hivyo mahusiano hayo ni muhimu yakaendelezwa na kudumishwa.

Makamu wa Rais katika mazungumzo na balozi huyo wa India hapa nchini Sandeep Arya pia ameiomba serikali kuisaidia Tanzania katika mpango utakaosaidia wakulima kupata taarifa mbalimbali zinazohusu kilimo na masoko ya bidhaa zao kupitia simu za mkononi ili kuondoa usumbufu mkubwa wanaopata wakulima kwa sasa hasa kuhusu masoko.

Kwa upande wake, Balozi wa India nchini Tanzania Sandeep Arya amemhakikishia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan serikali yake itakuwa bega kwa bega na Tanzania katika kuhakikisha wananchi wa pande Mbili wananufaika na mahusiano yaliyopo.

Balozi Sandeep Arya amesisitiza kuwa serikali ya India itaendelea kuisaidia Tanzania katika uimarishaji wa teknolojia ya habari na mawasiliano pamoja na miradi ya maendeleo na uimarishaji wa shughuli za kiuchumi.

Wakati huo huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Sudan nchini Tanzania Mahgoub Sharfi mazungumzo yaliyolenga pamoja na mambo mengine kuhusu namna ya kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Sudan.

WATANZANIA WAASWA KUTUMIA BIDHAA ZINAZOZALISHWA NA VIWANDA VYA NDANI-MWIJAGE

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, imesema kulinda viwanda vya ndani ni lazima watanzania wanunue bidhaa zinazozalishwa ndani na kuacha bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.

Hayo ameyasema leo, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, wakati akitangaza maonesho ya viwanda vya ndani yatakayofanyika Desemba 7 hadi 11 katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.

Mwijage amesema nchi zilizofanikiwa kwa viwanda imetokana na watu wao kupenda kununua bidhaa zao ambapo na Tanzania inatakiwa kufanya hivyo kwa wananchi kupenda bidhaa zao

Amesema viwanda vya ndani katika kuweza kuzalisha bidhaa na zikaweza kutoka ni lazima wazalishe bidhaa zenye ubora kwa kupata soko la ndani na nje ya nchi. ‘’Kauli mbiu ya maonesho hayo ni Tanzania sasa tunajenga viwanda ambapo kila mtu anaweza kuanzisha kiwanda chake na kuzalisha na kuweza kupata soko la uhakika’’.

Amesema maonesho hayo yatakutanisha wadau mbalimbali wa viwanda ambapo watanzania wenye nia kuanzisha viwanda watumie maonesho hayo kuweza kupata mwongozo kutoka kwa wataalam jinsi ya kuanzisha kiwanda. Aidha amesema katika maonesho hayo kwa wanafunzi waliohitimu katika vyuo watumie fursa katika ya kutafuta ajira kwa viwanda vitavyoshiriki maonesho hayo.

Amesema Wakuu wa Mikoa wote wataalikwa kuweka maeneo yao waliopanga kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda ikiwa ni pamoja kuondoa masharti magumu kwa wawekezaji wanakwenda kuomba ardhi.

SERIKALI MKOANI RUVUMA YATEKETEZA ZANA HALAMU ZA UVUVI ZENYE THAMANI ZAIDI YA MILIONI 42.

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dokta Binilith Mahenge akichoma mitego ambayo imekuwa ikitumiwa kuvua samaki katika ziwa nyasa.

-------------------------------------

Asilimia 80 ya wakazi wa wilaya ya nyasa mkoani Ruvuma ,wanategemea uvuvi kuendesha maisha yao, huku baadhi yao wamekuwa wakitumia zana ambazo zimepigwa marufuku na serikali ambazo ni nyavu nchi moja na nusu hadi inchi mbili , vyandarua na mfumo wa uvuvi unaodaiwa kuwa ni wakienyeji uitwao gonga ambao uharibu mazalia ya samaki. Habari zaidi bonyeza lingi hiyo hapo chini.

WANAFUNZI WA LONGIDO SEKONDARI MWISHO KULALA MADARASANI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (pili kushoto) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo(kwanza kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido Mhe. Esupat Mulupa wakielekea kukagua ujenzi wa mabweni katika Shule ya Sekondari Longido .
Afisa Elimu wa Halmashauri ya Longido Ndg. Gerson Mtera(mbele) akisoma taarifa ya ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari ya Longido wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wilayani hapo.
Ujenzi unaendelea katika mabweni ya Shule ya Sekondari Longido na hivi ndivyo yanavyoonekana kwa sasa.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(kwanza kulia) akishirki kwenye ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari Longido.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(aliyesimama) akizungumza na walimu pamoja na watumishi wasio walimu katika Shule ya Sekondari Longido wakati wa ziara ya Kikazi Wilayani hapo.
Baadhi ya walimu na watumishi wa Shule ya Sekondari Longido wakiwa kwenye Kikao na Mkuu wa Mkoa wa Arusha (hayupo pichani)
Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe. Daniel Chongolo akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakati wa kikao na walimu wa Shule ya Sec. Longido.

…………………………………………………………………..

Nteghenjwa Hosseah – Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo amechangia mabati 136, mifuko ya Saruji 30 pamoja na Fedha taslimu Tsh 500,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa mabweni mawili yaliyoungua moto hivi karibuni katika Shule ya Sekondari Longido.

Rc Gambo ametoa msaada huo wakati wa ziara yake ya Kikazi wilayani hapo ambapo alitembelea Shule hiyo na kukuta wanafunzi wakilala madarasani tangu Mabweni hayo yalipoungua na uongozi wa Shule hiyo kuamua kutumia madarasa hayo katika kipindi hiki cha mpito wakati wakiwa wanaendela na ujenzi wa mabweni hayo ambayo ujenzi wake unagharimu zaidi ya Tsh Mil 45.

Akisaoma taarifa ya ujenzi wa mabweni hayo Afisa Elimu Sekondari Bw.Gerson Mtera alisema endapo wangetumia Mkandarasi ujenzi huo ungegharimu zaidi ya Ths Mil 75 lakin kwa kuwa wanajenga kwa kutumia mafunzi wa jamii pamoja na wataalamu wa Halmashauri mabweni hayo yatagharimu Tsh Mil 45 tu.

Nimeona jitihada za uongozi wa Wilaya pamoja Shule katika kukabiliana na changamoto hii na jitihada zenu hakika sio za kupuuzia na mimi kama Kiongozi wa Mkoa nawiwa kuchangia kazi hii ili iweze kukamilika haraka na wanafunzi warudi katika malazi yaliyo bora na madarasa hayo yaweze kutumika kwa shughuli stahiki alisema Gambo.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa alikutana na walimu pamoja na wafanyakazi wasio Walimu kusikiliza malalamiko na kubaini baadhi wa walimu kutolipwa malimbikizo ya Fedha za Likizo pamoja na watumishi kuajiwa kwa zaidi ya miaka kumi pasipo kuwa na mkataba wala barua ya ajira kutoka kwa Mwajiri wake.

Akiongea katika Kikao hicho Mhe. Gambo alisemani ni muhimu kwa kila Halmashauri kuwajali watumishi wake haswa walimu na wafanyakazi wa kada za chini ili kuwaongezea ari ya kufanya kazi na kuwatia moyo waweze kutumikia Taifa hili kwa uzalendo sio kila siku mnatoa vipaumbele kwa watumishi wa Kada za juu kufanya hivi mnasababisha matabaka yasiyo ya lazima katika utendaji kazi wenu wa kila siku.

Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe. Daniel Chongolo aliahidi mbele ya Mkuu wa Mkoa kuwa atasimamia ipasavyo wote wanaohusika na ujenzi wa mabweni ya Sekondari ya Longido ili kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa na kumhakikishia kwamba mpaka mitihani ya Kidato cha nne itkapoanza wanafunzi hao watakua wameshahamia kwenye Mabweni hayo na madarasa hayo yatatumika kwa ajili ya kazi hiyo na baadae wanafunzi wataendelea kuyatumia katika masomo yao.

Pia aliongeza kuwa atafuatilia malimbikizo ya Fedha za waalimu wanazodai kwa ajili ya Likizo ili kuangalia uwezekano wa kuwalipa kutoka katika Mapato ya Halmashauri na kuwaagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kushushulikia malalamiko ya watumishi wote ambao hawana barua za ajira hadi sasa.

Kuanzai wiki ijayo Mkurugenzi pamoja na Menejiment ya Wilaya kupitia vikao vyenu mliangalia suala hili kwa makini na Bodi ya Ajira iweze kuketi ili watumishi hawa waweze kupata haki yao.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo yuko katika muendelezo wa ziara yake ya Kikazi katika Wilaya ya za Mkoa wa Arusha amabapo mpaka sasa amekwisha tembelea Wilaya ya Ngorongoro.
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live


Latest Images