Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all articles
Browse latest Browse all 49642

GAVANA WA BoT ATANGAZA BANK M SASA IKO CHINI YA USIMAMIZI WAO

$
0
0

*Ni baada ya mtaji wake kutetereka, yapewa siku 90 kujitathimini

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

BENKI Kuu ya Tanzania(BOT) imeamua kuchukua usimamizi wa Bank M kuanzia leo na uamuzi huo unachukuliwa baada ya kubainika benki hiyo ina upungufu mkubwa wa ukwasi.

Akizungumza leo Dar es Salaam Gavana BoT Profesa  Florens Luoga amesema kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha Sheria namba 56 (1)(g)(III)cha sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 ameamua kuchukua uamuzi huo kwa Benk M na sasa itakuwa chini ya usimamizi wa BoT.

"Upungufu huu wa ukwasi unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na pia kuendelea kutoa huduma za kibenki kwa Bank M kutahatarisha usalama wa amana za wateja wake,"amesema Profesa Luwoga.

Amefafanua kutokana na uamuzi huo ,Benki Kuu imeisimamisha Bodi ya Wakurugenzi na uongozi wa Bank M kuanzia leo(Agosti 2) mwaka huu na kutokana na uamuzi huo BoT imemteua Meneja Msimamizi atakayesimamia shughuli za benki hiyo kwa kipindi ambacho itakuwa chini ya usimamizi.

Ameongeza Watanzania wafahamu kuwa katika kipindi kisichozidi siku 90 kuanzia leo , shughuli zote za utoaji wa huduma za kibenki za Bank M zitasimamiwa ili kuipa nafasi BoT kutathmini hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa suala hilo.

P ia kuwa BoT itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 49642

Latest Images

Trending Articles

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>