Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 48979 articles
Browse latest View live

TANZANIA NA DRC ZAJA KIVINGINE...!

$
0
0

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Tanzania, Prof. Makame Mbarawa na Mawaziri wa Miundombinu na Uchukuzi Alexis Gusaro na Cherubin Senga wa DRC wakisaini Makubaliano ya ujenzi wa miundombinu ya Reli, Meli, Bandari na barabara baina ya nchi hizo jijini Dar leo. 

Muonekano wa Reli ya SGR stesheni jijini Dar es Salaam.
Waziri wa ujenzi na uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa katika picha ya pamoja na mawaziri wa miundombinu na Uchukuzi wa DRC na ujumbe wao walipitembelea makao makuu ya TRC.

Waziri wa Miundombinu wa DRC, Alexis Mavunyi akisisitiza jambo mara baada ya makubaliano ya ujenzi wa miundombinu baina ya nchi hizo.

SERIKALI za Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwa pamoja zimeingia makubaliano ya kuboresha miundombinu ya Barabara, Reli na Bandari ili kuongeza ufanisi katika biashara na hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo.

Hafla ya makubaliano hayo imefanyika jijini Dar es Salaam ambapo Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Tanzania, Prof. Makame Mbarawa amesema makubaliano yataimarisha miundombinu ya Reli, Barabara, Bandari na ujenzi wa Meli za mizigo na abiria.

"Tunakusudia kuongeza ufanisi wa kibiashara katika nchi zetu na hivyo kuimarisha uhusiano wa kindugu na kukuza uchumi wa nchi zetu", amesisitiza Prof. Mbarawa.

Prof. Mbarawa amesema miradi hiyo ambayo ujenzi wake utatekelezwa kwa awamu utapunguza muda wa safari kutoka DSM kwenda Lubumbashi nchini DRC na hivyo kupunguza gharama za biashara na muda wa kusafirisha mizigo toka siku 30 hadi wiki moja.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Tanzania, Prof. Makame Mbarawa akijadiliana jambo na ujumbe kutoka DRC walipotembelea Bandari ya Dar es Salaam.


WAZIRI wa Miundombinu wa DRC, Alexis Mavunyi amesema namna mataifa hayo mawili yatakavyo nufaika kutachochea uzalishaji wa bidhaa, mazao na biashara zingine hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo na raia wao.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ushoroba wa Kati, Wakili Froly Okanju amesema makubaliano hayo yatafungua fursa kubwa ya usafirishaji kwa nchi za ushoroba wa kati ambazo zinakwenda kupata maendeleo kwa kuwa zinaitegemea Tanzania katika uingizaji wa mizigo na hivyo kuitaka Tanzania kujipanga kuhudumia nchi za ushoroba huo kikamilifu.

Pamoja na mambo mengine ujenzi wa Miradi hiyo inayotarajiwa kuanza utekelezaji wake baadae mwakani itatoa fursa kwa Serikali za Tanzania, DRC, Wadau wa Maendeleo ya kuzalisha nafasi za ajira.

Viongozi hao pamoja na ujumbe wao wametembelea Shirika la Reli TRC na Mamlaka ya Bandari nchini TPA na kufurahishwa na namna taasisi hizo zinavyofanya kazi kwa weledi na ubunifu.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na mawasiliano Serikalini Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.

Spika Dk Tulia Aguswa na Jitihada za Wanawake Benki ya NBC kuwanoa wenzao kiuchumi, atoa angalizo

$
0
0

 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), amepongeza jitihada zinazofanywa na Benki ya NBC kupitia Chama cha wanawake Wafanyakazi wa NBC (Women Network Forum) katika kuendesha mafunzo mbalimbali yanayolenga kuwakomboa wanawake dhidi ya changamoto za kiuchumi.


Kwa mujibu wa Dk Tulia jitihada mbalimbali zinazofanywa ili kuwakomboa wanawake kijamii zinaweza zisifanikiwe vema iwapo kipaumbele hakitawekwa katika kuwapatia mafunzo yanayolenga kuwajenga kiuchumi.

Spika Dk. Tulia alitoa rai hiyo jijini Dodoma leo wakati akifungua semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofahamika kama “Pamoja na NBC Bank” .

Kwa mujibu wa Dk. Tulia, kupitia mafunzo hayo wanawake wataweza kubadili fikra zao kuhusu vipaumbele vyao pindi wanapofanya maamuzi mbalimbali ya kiuchumi kwa kuwa licha ya jitihada mbalimbali za wanawake nchini katika kujiongezea kipato bado changamoto imebaki kwenye namna ambavyo wanatumia kipato chao.

“Nitolee mfano mdogo tu kwenye VICOBA, ni kweli wananawake tunafanikiwa kujiongezea kipato lakini sehemu kubwa ya kipato hiki mara nyingi imekuwa ikielekezwa kwenye matumizi yasiyo ya kipaumbele ikiwemo manunuzi ya mavazi mengi zikiwemo sare nyingi tunazoshona au kununua kwa ajili ya kila tukio tunalolifanya kina mama. Ndio maana nawapongeza Benki ya NBC kwasababu kupitia wabunge hawa elimu hii itawafikia wanawake kote nchini.’’ Alisema.

Alisema mbali na kuwasaidia wabunge wanawake ambao pia baadhi yao wamekuwa na udhaifu kwenye nidhamu ya matumizi ya fedha zao, semina hiyo pia itasaidia kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya kiuchumi wabunge hao hususani pale wanaposhiriki kwenye mijadala ya kibunge inayolenga kuishauri serikali kuhusu masuala mbalimbali ya kiuchumi yanayowahusu wanawake na nidhamu katika matumizi ya fedha za umma.

“Hivyo natarajia kuona matunda ya semina hii kwenye mijadala mbalimbali inayoendelea hususani kwenye vikao vya Bunge vinavyoendelea…nashukuru sana NBC mmefanya kitu sahihi wakati sahihi,’’ alisema.

Awali akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Bw Theobald Sabi, Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya NBC, Allelio Lowassa alisema semina hiyo iliwalenga wabunge hao kwa kuwa ni wawakilishi wa wananchi na wenye ushawishi mkubwa kwa jamii, hususan makundi ya wanawake, ili nao wafikishe ujumbe kwa walengwa.

Akizungumiza kuhusu Chama cha wanawake Wafanyakazi wa NBC (Women Network Forum) ambacho ndicho kilichoratibu semina hiyo, Bi Lowassa alisema kinalenga kuwanganisha na pia kukuza elimu ya kifedha miongoni mwa wanachama wake ili wakawe mabalozi kwa wanawake wengine.

“Chama hiki pia kimeenda mbali kwa kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa makundi ya wanawake katika maeneo mbalimbali nchini.Kupitia chama hiki, Benki pia imeweka utaratibu maalum wa kuwapa nafasi wafanyakazi wanawake ili kushika nafasi za uongozi.’’ Alisema huku akibainisha kuwa kwasasa benki hiyo ina wafanyakazi zaidi ya 900 ambapo asilimia 47% kati yao ni wanawake.

Katika semina hiyo ilishuhudiwa maofisa mbalimbali wanawake kutoka benki ya NBC wakitoa elimu kwa wabunge hao kuhusu mada mbalimbali za kiuchumi ikiwemo usimamizi wa fedha, mafunzo kuhusu bima za biashara na maisha na pamoja na Hati fungani ya NBC.


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), (Kulia – meza kuu) akifurahia pamoja na washiriki mbalimbali wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma. Wengine ni pamoja na viongozi waandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya NBC, Allelio Lowassa (katikati



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na washiriki mbalimbali wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.


Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya NBC, Allelio Lowassa akizungumza na washiriki mbalimbali wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.


Baadhi ya washiriki mbalimbali wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake akiwemo Mbunge wa Mchinga ambae pia ni mke wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete (Pichani) wakichangia mada wakati wa semina hiyo.


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki mbalimbali wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), (wanne kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa waandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya NBC, Allelio Lowassa (katikati) wakati wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.


Mbunge wa Mchinga ambae pia ni mke wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa waandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya NBC, Allelio Lowassa (wa tatu kushoto) wakati wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.

Mbunge wa Mchinga ambae pia ni mke wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete (wa tano kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki mbalimbali wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.


Kwa heri! Maofisa waandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya NBC, Allelio Lowassa (katikati) wakimuaga Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) (kushoto) mara baada ya uzinduzi wa wa semina ya fursa za uchumi iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa ajili ya wabunge wanawake iliyofanyika leo jijini Dodoma.


WAZIRI MABULA ASITISHA VIBALI VYA UJENZI WA VITUO VYA MAFUTA

$
0
0

 

Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Nyumba na Makazi akiongea na vyombo vya Habari leo Jijini Dodoma kuhusu maagizo yake ya kusitisha ujenzi holela wa vituo vya mafuta na kanununi za mipango miji.

WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Angeline Mabula amesitisha utoaji wa vibali vipya vya ujenzi wa vituo vya mafuta na mabadiliko ya matumizi ya ardhi kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo kwa muda wa miezi mitatu kuanzia sasa.

Waziri ametoa agizo hilo ili kutoa nafasi kwa Wizara ya Ardhi na Wizara zinazohusika na utoaji vibali kufanya tathimini ya kina kuhusu ujenzi wa vituo vya mafuta kufuatia kuwepo kwa ujenzi unaokiuka maelekezo ya mipango kabambe iliyopo.

Waziri Mabula ametoa agizo hilo leo tarehe 10, Novemba 2022 mbele ya vyombo vya habari Jijini Dodoma nakuongeza kuwa baadhi ya wamiliki wamekuwa wakiomba vibali vya ukarabati wa majengo chakavu mijini na baadae kufanya uendelezaji wa Maeneo hayo kinyume mipango kabambe iliyopo.

Waziri Mabula aliongeza kuwa pamoja na kuwepo kwa kanuni husika, kumekuwepo na hujenzi holela wa vituo vya mafuta nchini usiozingatia matakwa ya Sheria ya Mipangomiji na Kanuni zake jambo linalochagiza uwepo wa agizo hilo la kusitisha vibali hivyo.

Aidha Waziri Mabula ameelekeza kusitisha kutoa vibali vya ujenzi vinavyokiuka Mipango kabambe wa Majiji, Manispaa, Miji na kusitisha ugawaji viwanja kiholela unaopelekea taswira ya miji yetu kuharibika akisisitiza kuwa kama kuna mpango wa kujenga magorofa eneo husika ufuatwe mpango uliopo.

Aidha Dkt. Mabula amezitaka mamlaka za upangaji kuhakikisha uendelezaji upya maeneo ya ndani ya miji na mgawanyo wa maeneo unaofuata Mipango Kabambe iliyopo na mipango kina iliyoandaliwa.

Waziri Mabula amewaelekeza wataalamu katika ofisi za ardhi kote nchini zisimamiwe utekelezaji wa Mipango Kabambe na kuwe na ukaguzi wa mara kwa mara ili kuhakikisha mapendekezo ya mipango hiyo yanatekelezwa.

Waziri Mabula ameitaja sheria ya Mipango miji Sura 355 kupitia fungu 77(1)b kuwa inampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya Ardhi, mamlaka ya kutoa kanuni za viwango vya matumizi ya ardhi.

Dkt. Mabula ameitaja Sheria hiyo na kanuni ya 93 ya mwaka 2018 kuwa ndiyo inayotoa maelekezo kuwa umbali wa kituo kimoja hadi kingine ni mita 200 kwa maeneo yaliyopangwa na mita 500 kwa maeneo yasiyopangwa.

Aidha Waziri Mabula amesema tayari Wizara yake imetoa imeidhinisha Mipango Kabambe 26 ikiwemo ya Majiji 6 ya Dodoma, Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya na Tanga pamoja na Mipango Kabambe ya Mikoa ya Iringa, Morogoro, Mtwara Mkindani, Songea, Singida, Tabora, Kigoma Ujiji, Mpanda, Sumbawanga, Bukoba, Shinyanga na Musoma.


MECHI ZENYE ODDS KUBWA MERIDIANBET WIKIENDI HII

$
0
0

 

BAADA ya EPL kusimama kupisha michuano ya Carabao Cup, Wikiendi Hii itaendelea tena kwa michezo kadhaa kabla ya michuano ya Kombe la Dunia kuanza. Hispania Copa Del Rey, Serie A, na Ligue 1 nazo zitatimua vumbi. Sehemu ya kupata odds kubwa ni Meridianbet pekee.

EPL ya kibabe ni michezo ya mwisho kabla ya Ligi kusimama, Manchester City waliopo nafasi ya 2 kwenye msimamo wa EPL, watakuwa wanahitaji kupata matokeo mazuri kwenye Uwanja wao wa nyumbani dhidi ya Brentford ili kwenda kwenye mapumzika mafupi wakiwa kileleni Meridianbet wameweka odds kubwa kuliko kawaida.

Bayern Munich ikimkosa mchezaji wao hatari Sadio Mane aliyeumia goti, watakuwa ugenini kukipiga na Schalke, wakati huo kwenye dimba jingine utashuhudia pira likitembea ni Leverkusen dhidi ya Stuttgart. Pia Bremen waliotoka kupoteza dhidi ya Bayern bao 6-1 watakipiga na RB Leipzig. Beti sasa na Mabingwa.

Kwenye Serie A, Napoli hawatakuwa na kingine Zaidi ya kuwakaribisha Udinese kwenye raundi ya 15, Napoli ni kinara wa kwenye msimamo kwa alama 38 wakati Udinese wakiwa kwenye nafasi ya 7 na alama zao 24. Pia Atalanta watakuwa wenyeji wa Inter Milan waliopo nafasi ya 8, Huku Roma na Torino watakipiga kwenye mchezo wa raundi ya 15 ya Serie A. Nao AC Milan moto utawaka pale ambapo watacheza dhidi ya Fiorentina. Juventus nao watawakaribisha Lazio kuikamilisha raundi ya 15 ya Serie A. mechi imepewa odds kubwa zaidi Beti hapa.

Paris Saint-German wababe wa Ligue 1 wakiwa kwenye dimba lao la nyumbani, watawakaribisha Auxerre, wakati Lille wakiwa wenyeji wa Angers ambapo hawapo sehemu nzuri kwenye msimamo wapo nafasi ya 20. Na Monacoakiwa nafasi ya 5 atakutana na jirani yake aliyepo nafasi ya 4, hawa wote rekodi zao zinawapa nafasi ya kuzinyakua alama 3. Kwa USSD ni rahisi kushinda kwa dau dogo sana la TZS 250/= tena unabeti bure kabisa.

Haiishii hapo tu, Ile michuano ya Kombe la Mfalme ‘Copa Del Rey’ nchini Hispania Jumamosi utapigwa mchezo mmoja kati ya Villarreal atakuwa ugenini dhidi ya Santa Amalia, na siku ya Jumapili sasa Sevilla atakuwa ugenini pia kucheza na Velarde, hawajasahaulika Getafe wakiwa ugenini kukipiga dhidi ya CD San Roque de Lepe. Beti hapa.

Lakini pia Copa del Rey itaendelea kwa mchezo mwingine ambao utawakutanisha Cazalegas wenyeji wa Real Sociedad na upande mwingine Atletico Madrid ni wageni waalikwa wa Almazan. Meridianbet wana machaguo Zaidi ya 1000.

Lakini pia mbali na michezo ya mpira wa miguu, Meridianbet wamekuletea Promosheni chungu nzima, kwa USSD ukibeti kwa kitochi kwa dau la kuaznia TZS 250/= pekee Piga *149*10# ili kuweka mkeka wako. Pia unaweza kushinda TV ya Inchi 50 Mpyaa kabisa !!!!

REGINA NDEGE-TUMUUNGE MKONO RAIS SAMIA

$
0
0

 

Na Mwandishi wetu, Simanjiro
MBUNGE wa viti maalum wa Mkoa wa Manyara, Regina Ndege amewataka wanawake nchini wamuunge mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ndege ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye kikao cha Baraza la wanawake wa jumuiya ya (UWT) wa Wilaya ya Simanjiro, kilichofanyika mji mdogo wa Orkesumet.

Amesema wanawake nchini wanapaswa kumuunga mkono Rais Samia kwani amefanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya afya, elimu, maji na mengineyo.

“Tumeona miradi mingi ya maendeleo inavyofanyika nchini, vituo vya afya vimejengwa vipya, hospitali na vituo vya afya, madarasa mapya ya shule za msingi na sekondari na miradi mingi ya maji,” amesema Ndege.

Amesema wanawake hawana namna nyingine ya kufanya kwa Rais Samia, zaidi ya kumuunga mkono katika utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo ambayo inafanyika kila pembe ya nchi.

Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Simanjiro Anna Shinini amesema Rais Samia amewaheshikisha mno wanawake kwa namna anavyoongoza nchi hivyo watamuunga mkono kwa juhudi zote.

Shinini amesema wanawake UWT Simanjiro watamuunga mkono Rais Samia kwa kutangaza mazuri yote anayoyafanya.

MATUKIO; MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIANCHI MISRI

$
0
0

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na wageni mbalimbali waliotembelea banda la maonesho la Tanzania katika Mkutano wa 27 wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Sharm El-Sheikh, Misri. Wengine pichani kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Switbert Mkama, wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Hassan Mitawi na Mkurugenzi wa Mazingira Dkt. Andrew Komba. 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Hassan Mitawi akitoa ufafanuzi kwa wageni waliotembelea banda la banda la maonesho la Tanzania katika Mkutano wa 27 wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi unaoendelea Sharm El-Sheikh, Misri.

(PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)


MERIDIANBET YAWASHIKA MKONO HOSPITALI YA TUMBI

$
0
0

 


KAMPUNI ya Meridianbet iliyoambatana na timu nzima ya masoko, akiwemo meneja masoko wa kampuni hiyo Ndugu Matina Nkurlu, pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Maudhui Bw Twaha Ibrahimu, leo Novemba 11, 2022 ilitembelea Hospital ya Rufaa ya Tumbi mkoa wa Pwani, kwaajili ya kutoa msaada wa vifaa kwa matumizi ya wagonjwa katika hospitali hiyo.

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, Wizara ya Afya chini ya Waziri mwenye dhamana hiyo Mhe Ummy Mwalimu, Meridianbet iliguswa na mahitaji ya hospital hiyo na hivyo waliamua kuchangia neti, barakoa na vifaa vingine ikiwa ni sehemu ya utamaduni wao wa kurudisha kwa jamii kile kidogo wanachokipata.

Meridianbet pamoja na uongozi wa Hospitali ya Tumbi walishiriki owa pamoja katika zoezi hilo la kukabidhiana vifaa hivyo, na mara ya kukamilika kwa zoezi la kutoa msaada huo, mwakilishi kutoka Hospitali hiyo, Christina Salusi alitoa shukrani zake kwa kampuni ya Meridianbet kwa msaada huo.

"Kwa niaba ya Uongozi na Menejimenti nzima ya Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, napenda kuwashukuru kampuni ya Meridianbet kwa kuguswa na kuamua kutoa msaada huu mkubwa wa vifaa vya matibabu, hakika hili ni jambo kubwa kwetu na kwa jamii nzima" alisema Christina Salusi- Muuguzi.

Aidha timu nzima ya Meridianbet walioambatana na Meneja Masoko Matina Nkurlu hawakusita kuzungumza kile kilichowasukuma kutoa msaada huo tena kwa mara ya kwanza kwa Hospitali ya Mkoa wa Pwani-Tumbi.

"Sisi kama Meridianbet huwa tuna utamaduni wa kutoa kwa jamii kile kidogo tulichopata kama faida kwenye biashara yetu, na hii sio mara ya kwanza tumewahi kufanya kwenye hospitali ya Mwananyamala, Amana n.k

“Na tumeamua kuja hapa Hospitali ya Tumbi ili kuwashika mkono katika juhudi zenu za kuokoa maisha ya wapendwa wetu, hivyo tunawaahidi kuendelea kushirikiana nanyi" Twaha Ibrahimu

Hata hivyo, Muuguzi ndugu Salusi alitoa nafasi ya wawakilishibwa Meridianbet kutembelea baadhi ya maeneo katika Hospitali hiyo ili kuwajulia hali wagonjwa waliofika kutibiwa.  Moja ya eneo lililotembelewa ni wodi ya wajawazito ambao  nao hawakusita kutoa neno lao kwa kampuni  hiyo namba moja Tanzania na Afrika Mashariki kwa michezo ya kubashiri kutokana na msaada huo.

Mmoja ya wazazi waliojifungua katika hospitali hiyo, Bi Zuwena Rashi mara baada ya kupokea msaada huo hakusita kuonesha hisia zake za furaha.

"Kwakweli mimi kama mzazi nimefurahishwa na hiki mlichokifanya kwetu, nawashukuru sana kampuni ya Meridianbet kwa kugusa maisha yetu, hususani ya mama wajawazito na wagonjwa wengine, msaada huu utasaidia wagonjwa wengi wanaotibiwa kwenye Hospitali ya Tumbi" -Zuwena Rashid

Kampuni ya Meridianbet inapenda kuushukuru Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi, Mkoa wa Pwani, kwa ushirikiano wao walioutoa mwanzo wa zoezi mpaka mwisho, na unapongeza juhudi zinazofanywa na Hospitali hiyo kuokoa maisha ya watanzania wengi na kurejesha matumaini zaidi. Unaweza kubeti Meridianbet kwa dau dogo la kuanzia TZS 250/= kwa kupiga *149*10#.

 

Mbali na michezo ya kubashiri, pia Meridianbet wana michezo mingine mingi ya kasino mtandaoni, unaweza kucheza mchezo wa Aviator ukawa rubani wa maisha yako, kuna mchezo wa Roulette, Poker, n.k. Pia Kampuni hiyo inaendesha promosheni kibao ya michezo ya kubashiri, ambapo unaweza kujishindia Bajaji droo hii itatangazwa Novemba 22 mwaka huu, lakini pia kuna promosheni ya SHINDA TV ya Inchi 50 kubeti kwa USSD Code.

DKT. KIRUSWA ATATUA MGOGORO BAINA YA MWEKEZAJI NA JAMII BUTIAMA

$
0
0
Na Mwandishi wetu
NAIBU Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amefungua Kikao cha kutatua mgogoro baina ya mwekezaji mgodi wa Cata Mining na jamii inayozunguka mgodi huo baada ya malalamiko kuhusu ulipwaji wa fidia kwa wananchi waliyopisha eneo la uwekezaji.


Mgodi wa Cata Mining uliopo wilayani Butiama mkoa wa Mara unashutumiwa kwa kuchelewesha ulipaji wa fidia kwa wananchi waliopisha maeneo yao kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya dhahabu.


Aidha, Dkt. Kiruswa amesema, kwa mujibu wa Sheria ya Madini, suala la kuchangia huduma kwa jamii inayozunguka leseni ya mgodi ni jambo la kisheria na sio msaada kwa jamii, hivyo ameitaka Kampuni ya Cata Mining kuchangia huduma kwa jamii inayozunguka mgodi huo kwa mujibu wa Sheria.


Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo ameiagiza Kampuni ya Cata Mining kutekeleza takwa la kuchangia huduma kwa jamii inayozunguza mgodi pamoja na kulipa fidia kwa walio pisha eneo la mgodi.


Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee ameahidi kufuatilia kwa karibu suala hilo ili kuhakikisha jamii inayozunguka mgodi huo inapata haki yake na mwekezaji anaye miliki leseni ya eneo hilo anachangia huduma kwa jamii.


Pia, Kaimu Kamishna wa Madini Msechu Mwaluvoko amasema, baada ya mabadiliko ya Sheria ya Madini ya Mwaka 2017, kifungu cha kumtaka mmiliki kiliongezwa kwa msisitizo kifungu namba 105 kiliongezwa kusisitiza mmiliki wa leseni kuchangia huduma kwa jamii zinazozunguka mgodi.


Amesema upo mwongozo wa kuchangia huduma kwa jamii inayo zunguka mgodi ambao unamtaka mwekezaji kuandaa mpango wa kuchangia huduma kwa jamii inayo zunguka mgodi na kuiwasilisha Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa ajili ya mapitio na baadaye utekelezaji.


Kikao hicho, kimehudhuliwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa, Katibu Mkuu wa Madini Adolf Ndunguru, Naibu Katibu Mkuu Madini Msafiri Mbibo, Kaimu Kamishna wa Madini Msechu Mwakavuko, Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee, Mkuu wa Wilaya ya Butiama Moses Kaegele, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Butiama Patricia Kabaka pamoja na Madiwani wanao hudumu katika maeneo yanayozunguka mgodi huo wakiongozwa na Rajabu Mjengwa.


KINGAI, KAGANDA, MWAMBASHI WALA KIAPO KUWA WAJUMBE WA TUME YA UTUMISHI YA JESHI LA POLISII DODOMA LEO

$
0
0

 DCI KINGAI, KAMISHNA KAGANDA NA SACP MWAMBASHI WALA VIAPO KUWA WAJUMBE WA TUME YA UTUMISHI YA JESHI LA POLISI, MAGEREZA, ZIMAMOTO NA UOKOAJI NA UHAMIAJI JIJINI DODOMA LEO NOVEMBA 11, 2022.

Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimaliwatu wa Jeshi la Polisi, Suzan Kaganda akila kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu, jijini Dodoma leo Novemba 11, 2022. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Ramadhani Kingai akila kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu, jijini Dodoma leo Novemba 11, 2022. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza (Sheria na Uendeshaji), SACP George Mwambashi akila kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu, jijini Dodoma leo Novemba 11, 2022. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Jaji wa Mahakama Kuu, Mheshimiwa Gerson Mdemu akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji na Uhamiaji baada ya kula kiapo cha kuwa Wajumbe wa Tume hiyo jijini Dodoma leo Novemba 11, 2022. Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Ramadhani Kingai, Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimaliwatu wa Jeshi la Polisi, Suzan Kaganda (kushoto) na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (Sheria na Uendeshaji), SACP George M

TPSF yazindua maadhimisho ya Siku ya Sekta Binafsi

$
0
0

 

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Angelina Ngalula (kushoto) na Meneja Masoko wa GSM, Rukia Yazid, wakizindua kwa pamoja leo Novemba 10, 2022 Maadhimisho ya Siku ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSD22) yatakayofanyika mwanzoni mwa Desemba. 
(PICH NA EMMANUEL MASSAKA WA MICHUZI TV)

MELI KUBWA YENYE WATALII ZAIDI YA 1500 KUTOKA MAREKANI IMEWASILI NCHINI TANZANIA

$
0
0

 

MELI kubwa yenye watalii zaidi ya 1,500 kutoka Marekani imetia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam huku ikielezwa kwamba itakuwepo kwenye bandari hiyo kwa siku mbili na kisha itakwenda visiwani Zanzibari.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Amoss Nnko amesema  meli ya kitalii ya Zaandam mali ya Kampuni ya Holland America Line imewasili nchini asubuhi ya leo ikiwa na watalii 1060 ikiwa ni sehemu za safari za kitalii za meli hiyo.

Amesema meli hiyo ina wafanyakazi na wahudumu zaidi ya 500 na kwamba  ilianza safari yake siku 71 nchini Marekani katika jimbo la Florida na baada ya kuwasili Tanzania itaelekea Shelisheli.
 
"Baada ya kutiananga kwenye bandari ya Dar es Salaam itakaa hapa nchini kwa siku nne ambapo Tanzania Bara itakaa siku mbili na Zanzibar itakaa siku mbili.Ujio wa meli hii unachochea jitihada za kukuza utalii nchini na ni matokeo ya kazi kubwa inayofanywa katika kutangaza vivutio vilivyopo Tanzania,"amesema Nnko 

Aidha amesema watalii hao kutoka Marekani wametembea katika nchi kadhaa na sasa ni zamu ya Tanzania ambapo pamoja na kwenda katika hifadhi ya Selous, watatembelea mji wa kihistoria Bagamoyo na kuzunguka jiji la Dar es Salaam.

Wakati huo huo Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mathew Antony amesema ni mafanikio kwa bandari hiyo kuendelea kupokea meli kubwa ikiwa ni matokeo ya uboreshaji wa miundombinu.

Amefafanua kwamba imezoeleka bandari ya Dar es Salaam huwa inahudumia  meli za mizigo pekee, lakini ukweli hata hizi za watalii wanazihudumia na
 wanaomba wadau wengine kupeleka meli zao kwani miundombinu ni mizuri na wanaendelea kuboresha.

Kwa upande wake mmoja wa watalii hao Roseline Richard ameeleza kwamba ilikuwa ndoto yake kubwa kutembelea barani Afrika na hatimaye amefika Tanzania nchi inayosifiwa kwa ukarimu."Hakika ilikuwa ndoto yangu ya miaka mingi sasa imetimia na nimekuja Tanzania kwenye nchi nzuri inayosifika kwa watu wake kuwa wakarimu."

Meli ikiwasili katika Bandari ya Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA  EMMANUEL MASSAKA WA MICHUZI TV)
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Amoss Nnko akimkabidhi zawadi mtalii aliekuja na meli kubwa iliyokuja na watalii zaidi ya 1,500 kutoka Marekani leo kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Amoss Nnko akiteta jambo na watalii leo kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mathew Antony.
Kaimu Kamishina Msaidizi TANAPA,Hassan Nguluma.






PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSAKA WA MICHUZI TV

BILIONI 200 ZIMETENGWA KWAAJILI YA UNUNUZI WA DAWA NA VIFAA TIBA- DKT.MOLLEL

$
0
0

 

NAIBU Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amebainisha kuwa Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 200 kwaajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba katika mwaka wa fedha 2022/2023 huku Bilioni 74.3 zikiwa tayari zimetolewa katika kumaliza changamoto ya upungufu wa dawa na vifaa tiba nchini.

Dkt. Mollel amesema hayo leo Novemba 11,2022 wakati akijibu swali la Mhe. Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa viti maalumu katika kikao cha kumi cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jijini Dodoma. 

Amesema, Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kutatua changamoto za huduma za afya kwa wananchi, huku kiasi cha shilingi Bilioni 74.3 zikiwa tayari zimetolewa kati ya Bilioni 200 zilizotengwa katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwaajili ya ununuzi wa dawa pamoja na vifaa tiba.

"Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga bajeti ya shilingi Bilioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba na hadi kufikia tarehe 30 Oktoba, 2022 Serikali imekwisha toa jumla ya shilingi bilioni 74.3 kwa ajili ya manunuzi ya dawa na vifaa tiba ili kuimarisha upatikanaji wake katika ngazi zote za utoaji wa huduma za Afya." Amesema Dkt. Mollel. 

Aidha, amesisitiza kuwa, Serikali itaendelea kuboresha na kuimarisha upatikanaji wa huduma za Afya nchini kwa kuboresha miundombinu ikiwemo kuweka vifaa tiba vya kisasa, kuajiri Wataalamu wa Afya pamoja na kuwapandisha madaraja ili kuongeza morali ya kuendelea kutoa huduma kwa wananchi.

Akijibu swali la nyongeza Dkt. Mollel amesema,  Serikali imepeleka vifaa vyenye thamani ya shilingi Bilioni 3 katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara - Kwangwa vitavyosaidia kutatua changamoto ya wananchi kwenda mikoa ya mbali kutafuta huduma hizo.

Ameendelea kusema kuwa, ifikapo Desemba 12, 2022 hospitali hiyo itaanza kutoa huduma zote, huku akisisitiza tayari CT-SCAN imeshafungwa na MRI ikisubiri chumba kikamilike ili huduma hiyo nayo ianze kuwanufaisha wananchi wa Mkoa wa Mara na nchi za jirani.

Sambamba na hilo, Dkt. Mollel amesema, Serikali imejipanga katika udhibiti wa dawa kwa kutengeneza mfumo mzuri kutoka zinapotoka ngazi ya taifa mpaka zinapofika katika kituo husika, huku akisisitiza ushirikiano baina ya viongozi, kamati za afya na wananchi katika kusimamia dawa ili ziweze kuwafikia walengwa. 

Pia, ameelekeza hospitali kutumia mapato ya ndani kutatua changamoto za dawa endapo zitajitokeza ili kutatua changamoto hizo kwa wagonjwa wanaoenda kupata huduma katika maeneo hayo ya kutolea huduma. 
Naibu Waziri wa Afya Dkt  Godwin Mollel akijibu maswali ya Wabunge kwa niaba ya Waziri wa Afya. 

KIKAO CHA TATHMINI YA USAJILI WA WATOTO WA UMRI CHINI YA MIAKA MITANO- TABORA

$
0
0

 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Buriani ameongoza Kikao cha Tathmini ya Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya Miaka Mitano ulioanza kutekelezwa mkoani Tabora Mwezi June 2022. 

Katika hotuba yake Dkt. Buriani amesema kwamba Usajili kupitia mpango huu umeweza kuongeza kiwango cha Usajii wa Watoto kwa Mkoa wa Tabora kutoka asilimia 9 mpaka asilimia 49 hivyo kuna ongezeko la asilimia 40.

Ameongeza kwamba Mkoa utahakikisha kwamba watoto wote ambao hawajapata huduma wanasajiliwa kwani ni haki yao ya Msingi ya Kutambuliwa na kuwataka Wasajili wasaidizi wote waendelee kutekeleza majukumu yao kwa weledi na uadilifu ili kuhakikisha watoto wanaopata vyeti vya kuzaliwa ni wale tu wanaostahili.

Akiwasilisha salamu za Wizara ya Katiba na Sheria, Katibu Mkuu Bi. Mary Makondo amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kwa lengo la kuleta maboresho ya mfumo wa usajili kupitia Mkakati wa Kitaifa wa Usajili wa Matukio Muhimu ya Binadamu na Takwimu na kuongeza kwamba Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya Miaka Mitano ni uthibitisho wa sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha watoto wanasajiliwa na kupata nyaraka ya awali na ya msingi ya utambulisho ambayo ni cheti cha kuzaliwa.

Naye Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi. Angela Anatory ameeleza kwamba Mpaka sasa Mpango huu unatekelezwa katika Mikoa 23 ya Tanzania Bara ambapo zaidi ya watoto 8,106,469  wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa hivyo kuongeza kiwango cha usajili wa watoto nchini kutoka asilimia 13 na kufikia asilimia 65 hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi ya mfano katika kuleta mageuzi makubwa katika usajili barani Afrika.

Ameongeza kwamba anatoa shukrani kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa, viongozi na watendaji wote kwa ushirikiano ambao wametoa kwa Wakala na wadau wengine kuanzia hatua za mwanzo za maandalizi mpaka kufikia hatua hii.
Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi. Angela Anatory akifafanua jambo katika kikao cha Tathmini ya Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya Miaka Mitano ulioanza kutekelezwa mkoani Tabora Mwezi June 2022. 
Katibu Mkuu  Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo akisoma hotuba yaka wakati wa kikao cha Tathmini ya Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya Miaka Mitano ulioanza kutekelezwa mkoani Tabora Mwezi June 2022. 
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Buriani Akizungumza wakati wa kikao cha Tathmini ya Mpango wa Usajili wa Watoto wa Umri chini ya Miaka Mitano ulioanza kutekelezwa mkoani Tabora Mwezi June 2022. 

Sehemu ya Watumishi na wadau mbalimbali  wakatika kikao hicho.
Picha ya pamoja

NUNUA TIKETI YA USHINDI KWENYE KASINO YA MTANDAONI YA MERIDIANBET

$
0
0

 

*Ushindi bila kikomo na Sloti ya Lucky Betting Shop!
*Sloti ya Lucky Betting Shop

SLOTI nyingine mpya iliyotengenezwa na Expanse Studios kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet iitwayo Lucky Betting Shop. Sloti hii isiopingika na yenye kupendwa na watu wengi ulimwenguni, itakupa fursa ya kununua tiketi na kuitumia tiketi hiyo kwenye michezo mbalimbali. Chaguo ni lako. Iwe mbio za mbwa, masubwi au soka, haijarishi ni mchezo upi unataka kuitumia tiketi hiyo, yote hayo utayapata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet kupitia sloti ya Lucky Betting Shop.

Sloti ya Lucky Betting Shop ina kolamu 5 na njia 1,024 za miunganiko ya ushindi. Tunaposema ushindi bila kikomo na Kasino ya Mtandoni ya Meridianbet tunamaanisha! Sloti hii ina uwezo wa kukuzidishia hadi mara 50 ya dau uliloliweka na kukupa faida ya hadi mara 250. Unasubiri nini? Nunua na utumie tiketi yako sasa kupitia sloti ya Lucky Betting Shop kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet sasa!
Jinsi ya Kucheza Sloti ya Lucky Betting Shop

Ili ushinde kupitia sloti ya Lucky Betting Shop, unatakiwa kuunganisha alama tatu zinazofanana kwenye mstari wa ushindi. Ushindi unahesabiwa kutoka upande wa kulia kwenda kushoto. Ni mstari mmoja tu ndo wenye kutoa malipo na kama utashinda zaidi ya mstari mmoja, mstari wenye thamani kubwa ndo utakaolipwa.

Kasino hii ya mtandaoni ya Meridianbet ina alama mbalimbali. Alama za karata, kundi la watu likishangilia na opareta. Alama ya Opareta ndio alama yenye thamani kubwa na yenye uwezo wa kukurudishia mara 250 ya dau uliloliweka. Vilevile ina machaguo ya kila aina ikiwemo chaguo la kubashiri ambalo linakupa mara mbili ya faida uliyoipata kama ukibashiri karata ipi itawekwa mezani. Jiunge sasa na ujishindie mapene kupitia sloti ya Luck Betting Shop ukiwa kwenye Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.

Maji ya kuingia Mto Ruaha yamezuiliwa na shughuli za Kibinadamu

$
0
0

 


Maporomoko ya Kimani-Kipengele Game Reserve yakitiririsha maji kwenye mto Ruaha huku Mto Ruaha ukiwa umekauka.
Afisa wa TAWA wa Kipengele Game Reserve David Titus Akizungumza kuhusiana na maporomoko ya kimani yanayopeleka maji mto Ruaha yakiwa yanatiririsha maji wakati wote si kianga wala masika.

*Maporomoko yote ya maji ya Mto Ruaha yako vizuri

Na Chalila Kibuda ,Michuzi Tv,Njombe
WAKATI Mto Ruaha ukiwa umekauka na kuadhiri uchumi wa nchi wa mgao wa umeme na wanyama kukosa maji huku vyanzo vya maji vikiwa viko imara kwa kuwa na maji kunaacha sintofahamu maji yanakopotelea.

Hali hiyo imebainika baada ya Kituo cha Wanahabari, Watetezi, Rasilimali na Taarifa (MECIRA) na Waandishi wa Habari kutembelea vyanzo vya maji maporomoko ya Kimani-Kipengele Game Reserve na Hifadhi ya Kitulo ambapo hayo maji yanaingia kwenye mto Ruaha na kunaibua maswali juu maji yanakopotelea na kushindwa kutiririsha kwenye Mto Ruaha.

Akizungumza Afisa wa Wanyamapori wa TAWA, Kipengele Game Reserve David Titus amesema maporomoko ya kimani maji hayajawahi kupungua hata mara moja huku maporomemoko mengine yapo yanaendelea kutiririsha maji.

Amesema maji katika kipindi cha kiangazi maji kwenye maporomoko hayajawahi kupungua ikiwa kasi yake hiyo kila siku.

Mragibishi na Mdau wa Mazingira Seleman Msindi amesemq kuwa shughuli za kibinadamu ni tatizo na kusababisha mto Ruaha kuwa na ukame.

Amesema maporomoko yote yana maji yakutosha lakini mto Ruaha umebaki mabwawa bila kujua maji yanakopotelea.

Msindi amesema kuwa kiini kimeshaonekana na kutaka serikali kuchukua hatua kwa watu wanaozuia maji hayo kwa makusudi tu ili Ruaha isipate maji.

Uvuvi haramu changamoto nyingine kwenye mto Ruaha kukauka

$
0
0

Mfuko wa Samaki zilizoharibika zilizotelekezwa wakati operesheni wa Askari wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Ruaha wakati walivyofanya operesheni eneo la Matopetope-Ikoga wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Hili ndo eneo ambalo wavuvi haramu wanaendesha Shughuli uvuvi haramu ambapo kutokana na operesheni imepungua.
Mragibishi na Mdau wa Mazingira Seleman Msindi 'Afande Sele'  akionesha Mtumbwi ulioharabiwa na Askari wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Ruaha wakati walivyofanya operesheni eneo la Matopetope-Ikoga wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
Mragibishi na Mdau wa Mazingira Seleman Msindi akizungumza na waandishi habari kuhusiana Uvuvi haramu unaofanyika kwenye Mto Ruaha na Hifadhi ya Ruaha katika eneo la Matopetope-Ikoga wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

* Wananchi waingiza mitumbwi na nyavu kwenye hifadhi

Na Chalila Kibuda,Michuzi Tv Mbarali
WAKATI serikali ikiweka mkazo wa kutoendesha shughuli za Uvuvi katika hifadhi imekuwa tofauti kwa wananchi wa Bonde la Usangu/Ihefu kuendesha shughuli hizo ndani ya hifadhi ya Ihefu na Mto Ruaha.

Hali hiyo imebainika baada Kituo cha Wanahabari ,Watetezi wa Rasilimali na Taarifa (MECIRA) kutembelea Mto Ruaha kwenye Bonde la Usangu/Ihefu eneo la Matopetope-Ikoga wilaya ya Mbarali mkoani.

Akizungumza eneo la Matopetope ambapo shughuli za Uvuvi zinafanyika Mragibishi na mdau wa Mazingira Seleman Msindi 'Afande Sele' amesema kuwa wananchi kuendesha shughuli za uvuvi ndio chanzo cha kukauka mto Ruaha na kupotea kwa Uoto wa asili bonde la Usangu/Ihefu.

Msindi amesema kuwa mabadiliko ya tabianchi yametokana na shughuli za kibinadamu na kusababisha mto Ruaha kukauka katika kipindi kufupi cha kiangazi.

Amesema kuwa uvuvi haramu kwenye mto Ruaha haukubaliki kutokana na maji hayo yanashughuli za kiuchumi ya kuzalisha umeme kwenye vituo vya Mtela ,Kidantu pamoja na kihansi.

Aidha amesema kuwa wananchi wanaingiza mitubwi na kufanya uvuvi haramu na miti ya mtumbwi imekatwa kwenye hifadhi ya Ruaha Bonde la Usangu/Ihefu.

DKT.JAFO-TANZANIA YAFANYA VIZURI MWONGOZO HEWA UKAA

$
0
0

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo akijibu maswali ya Waandishi wa Habari pamoja na kuelezea mafanikio yaliyopatikana kufuatia ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan nchini China na Misri kwenye Mkutano uliofanyika leo Novemba 12, 2020 Ikulu Jijini Dar es Salaam


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amesema katika Mkutano 27 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP27), Tanzania imekuwa ni nchi kinara katika uandaaji wa Mwongozo wa Biashara ya Hewa ya Ukaa.

Amesema hayo leo Novemba 12, 2022 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano wa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu Bi. Zuhura Yunus na waandishi wa habari kuhusu ziara ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan nchini China na Misri hivi karibuni.

Dkt. Jafo alisema hapo hapo mwanzo hatukuwa na kanuni wala mwongozo wa biashara hii na hivi sasa kukamilika kwake kutasaidia Tanzania kuweza kupata rasilimali fedha za kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari alisema katika mkutano huo unaendelea Sharm El Sheikh nchini Misri alimshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan aliyeungana na wakuu wengine wa nchi zinazoendelea kupaza sauti kuzitaka nchi zinazoendelea kutimiza wajibu wao.

“Ni kweli changamoto ya uzalishaji wa hewa ukaa ni kubwa na nchi yoyote dunia inapofanya uchafuzi huo wa hewa zinaathrika nchi zote duniani na ndio maana wataalamu wanatuambia ifikapo mwaka 2050 kuna uwezekano barafa katika mabara mbalimbali katika milima ukiwemo Kilimanjaro zitayeyuka kutokana na ongezeko la joto,” alisema.

Waziri Jafo alisema kutokana na hali hiyo Mkutano wa Paris wa mwaka 1992 uliazimia nchi zinazoendelea ambao ndio wazalishaji wakubwa wa hewa ukaa wanapaswa kuchangia zaidi ya Dola za Marekani bilioni 100 kwa nchi zinazoendelea kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

‘Kutokana na msukumo mkubwa kwa nchi zinazoendelea kutakiwa kutoa fedha, tayari katika awamu iliyopita Tanzania ilipokea Dola za Marekani milioni 23.6 na kwa mgao unaotarajiwa kutolewa tutapata Dola za Marekani milioni 52.8 na hii ni ni kutokana na efforts (jitihada) zilizofanyika katika Mkutano uliopita wa COP26,” alisema.




BIRIANI FESTIVAL NA COCA-COLA AWAMU YA PILI KUFANYIKA DODOMA

$
0
0
Kampuni ya Coca-Cola Kwanza kupitia kampeni yake ya Biriani Friday na Coka ambayo ilianza rasmi mwaka jana na kuendelea mpaka sasa, ikiwa na lengo kubwa la kuendeleza utamaduni wa Misosi na Coca-Cola, ambapo huwa tunatembelea wadau wetu mbalimbali wanao jishughulisha na upikaji biriani kila Ijumaa kwa kuwaunga mkono na kuhakikisha tunawapatia wateja wao wote Coca-Cola ya baridi pale wapatapo Biriani kwenye migahawa yao, na kuwawezesha migahawa na vitendea kazi kama T-shirts, Aprons na mikeka ya kutumia Biriani inapoliwa. Kampeni Birian Friday na Coke mpaka sasa imeshafikia migahawa zaidi ya 50,kwa mikoa ya Dar-es salaam, Dodoma, Morogoro, Tanga, Mtwara, Zanzibar na Mbeya.

Akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa kutangaza Tamasha hilo la Birian Friday na Coke, Meneja Biashara na Masoko Coca-Cola Kwanza Wahida Mbaraka alisema kuwa tamasha la Birian Festival na Coke awamu ya pili itafanyika Dodoma mnamo tarehe 26 Novemba mwaka huu.

‘Kwenye tamasha ili, tutawakutanisha kwa Pamoja wapishi wa Biriani wa mkoa huu na wateja wao, tamasha la mwaka huu litakuwa ni la kipekee kabisa na utofauti mkubwa, sababu tutaweza kupata Ladha pia ya vyakula vya asili vya Dodoma, Vionjo vingi vya kiasili ambavyo vinabeba utaifa wetu, na vile vile kuangalia mechi za Kombe la Dunia’, Mbaraka alisema.

Mbaraka aliongeza kuwa kutakuwa na Migahawa Zaidi ya 15, Michezo ya Watoto wetu, tukiburudishwa na Bendi ya Bushoke na Dj mkali Dj D-ommy Pamoja na burudani nyengine nyingi, na zawadi mbali mbali.

Kupitia jukwaa hili napeda kuchukua nafasi hii kuwakaribisha watanzania wote, wapenzi na wadau wa biriani na Coca-Cola, Familia, Marafiki kuja kujionea na kushiriki kwenye utamaduni huu, Tanzania nchi yetu, Dodoma ndio makao makuu yetu, Biriani na Coca-Cola ndio chaguo letu na Mpira wa Kombe la dunia ndio raha yetu.Tarehe ni 26/11/22 ( Jumamosi), Mahali ni viwanja vya wajenzi Maili Mbili Dodoma,kuanzia saa nne asubuhi, aliongeza Mbaraka.
Meneja biashara na Masoko Coca-Cola Kwanza Wahida Mbaraka (kati kati) akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni wa wiki wakati akitangaza Tamasha la Birian Friday na Coke awamu ya pili ambalo litafanyika Dodoma mwishoni mwa mwezi huu. Lengo la tamasha la Birian Friday na Coke ni kuwakutanisha pamoja wapishi wa birian kwa kuendeleza utamanduni wa Msosi na Coca-Cola. Kulia ni Meneja wa Beni ya Bushoke Anileth Bushoke.


DCB yashinda Tuzo ya Benki Bora kwa Kutoa huduma Bora kwa Wateja Nchini.

$
0
0

BENKI ya Biashara ya DCB imesema ushindi wa benki bora katika utoaji huduma kwa benki zenye ukubwa wa kati ilioupata, umetokana na mabadiliko makubwa iliyoyafanya katika mfumo mzima wa utoaji wa huduma kwa wateja wao.

Akizungumza katika hafla za utoaji zawadi za Tuzo za Chaguo la Mlaji Afrika (CCAA) jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa alisema ushindi huo uliotokana na uboreshaji mkubwa walioufanya katika huduma zao umekuja kwa wakati mzuri kipindi hiki DCB ikisherehekea miaka 20 tokea ilipoanzishwa.

“Kwa niaba ya familia ya DCB, napenda kushukuru sana wateja wetu na wasio wateja wetu kwa kutupigia kura kwa kuwa benki bora kabisa nchini kwa kutoa huduma bora, kupata tuzo hii kunazidisha furaha yetu wakati tukiendelea kusherehekea miaka 20 ya benki yetu.

“Mimi na wafanyakazi wenzangu tunafuraha kuona wateja wetu wameweza kuona uboreshaji mkubwa tulioufanya wa jinsi tunavyowahudumia, hii ni safari tuliyoanza miaka minne iliyopita na tunashukuru kuona matunda yake yanaonekana na wateja wameweza kuyaona,” alisema Bwana Ndalahwa.

Pamoja na hayo Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa mafanikio hayo wao kama wanafamilia wa DCB wanayachukulia kama changamoto ya wao kuzidi kuboresha zaidi huduma zao na kuwa zaidi ya mahali walipo.

Hii ni mara ya pili kwa DCB kushinda tuzo hii japo kwa mara ya kwanza mwaka 2021 ilitwaa ushindi wa pili wa tuzo hizi zenye lengo la kuleta ushindani kati ya makamapuni na biashara mbali mbali barani Afrika, kuhamasisha utoaji huduma na bidhaa bora kwa wateja pamoja na kutambua kazi bora za watoa huduma.

 Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Amina Baamary (wa tano kushoto), akipokea tuzo ya mshindi wa kwanza ya Benki Bora kwa kutoa Huduma Bora kwa Wateja nchini kwa mwaka 2022 katika hafla ya utoaji zawadi kwa washindi wa Tuzo za Chaguo la Mlaji Afrika (CCAA) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia kwake ni. Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Godfrey Ndalahwa.

Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Amina Baamary (wa tatu kulia),  Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa (wa nne kushoto), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, wakishangilia mara baada ya kupokea  tuzo ya mshindi wa kwanza ya Benki Bora kwa kutoa Huduma Bora kwa Wateja nchini kwa mwaka 2022 katika hafla ya utoaji zawadi kwa washindi wa Tuzo za Chaguo la Mlaji Afrika (CCAA) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa akizungumza muda mfupi baada benki hiyo kutangazwa mshindi wa kwanza wa Benki Bora kwa Kutoa huduma Bora kwa Wateja Nchini ya Tuzo za Chaguo la Mlaji Afrika (CCAA) kwa mwaka 2022 katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 

MWENYEKITI WA CCM, RAIS SAMIA AONGOZA KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA (NEC), MAKAO MAKUU YA CCM JIJINI DODOMA LEO

$
0
0

  

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akiongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM, Makao Makuu ya CCM (White House) jijini Dodoma. (PICHA ZOTE NA CCM MAKAO MAKUU)


Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Daniel Chongolo akizungumza katika kikao kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu, Makao Makuu ya CCM (White House) jijini Dodoma.
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwa katika kikao kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri  Kuu, Makao Makuu ya CCM (White House) jijini Dodoma.

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Akipitia nyaraka  katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, kilichofanyika katika Ukumbi wa Kamati Kuu Makao Makuu ya CCM (White House) jijini Dodoma. Kushoto wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia kwa karibu.

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akiimba wimbo kabla ya kuanza kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, kilichofanyika katika Ukumbi  wa Halmashauri Kuu ya CCM, Makao Makuu ya CCM (White House) jijini Dodoma.

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akiongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu  Makao Makuu ya CCM (White House) jijini Dodoma. Kushoto wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia kwa karibu.

Viewing all 48979 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>