Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live

KAMPUNI ZA PUMA NA AITEL ZAZINDUA HUDUMA KUNUNUA MAFUTA KWA KADI YA “AIRTEL MONEY TAP TAP”

$
0
0
MENEJA Mkuu wa Puma Energy Tanzania Philippe Corsaletti amesema  wanalo jukumu la kuhakikisha huduma wanazitoa kwa ajili ya  Watanzania zinakuwa salama wakati wote ikiwa ni sehemu ya kuunga  mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano za kuhamasisha kutumia  njia za kieletroniki kwenye malipo ya fedha.
 
Corsaletti alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa  huduma mpya inayojulikana kwa jina la Airtel Money Tap Tap ambayo  inamuwezesha mteja wao anapotaka kununua mafuta kwa kutumia  kadi ya Airtel badala ya kutoa fedha taslimu akiwa kituo cha mafuta. 
 
Alisema wanahisi kwamba wanawajibu wa kufanya huduma zao kwa  usalama, senye ufanisi na rahisi zaidi kwa wateja wao na kufafanua ni  hatari kubeba fedha wakati wote maana ni rahisi kuhatarisha maisha.
 
Aliongeza hivyo ili kufanya jamii ya Watanzania inakuwa salama wakati  wote imeona kuna haja ya kuwa na huduma hiyo ambayo  itamuwezesha anayehitaji kununua mafuta kwenye vituo vya Puma  vilivyopo maeneo mbalimbali ya Dar es salaam wanatumia kadi za Airtel  kununua mafuta.
 
“Milango yetu iko wazi kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma zetu  na kuna jambo lolote ambalo tunaweza kulifanya ili jamii yetu  kuwa  salama wakati wote.Hivyo kuna umuhimu wa kuwa na matumizi ya  kadi ya Airtel katika kununua mafuta kwenye vituo vyetu vya  Puma,”alisema.
 
Akifafanua zaidi kuhusu huduma ya Airtel Money Tap Tap, Corsaletti  alisema chini ya utaratibu huo mtu yeyote aliyejisajili na huduma ya  Airtel Money atakuwa na uwezo wa kulipia bidhaa za Puma katika vituo  vyake vyote nchini kwa kutumia kadi  ya huduma ya Airtel Tap Tap   badala ya kutumia fedha kwa ajili ya huduma kama hizo.
 
“Kadi hii imeundwa kwa namna ambayo wakati wa kutumika kufanya  malipo , hupunguza fedha kwa kiasi cha malipo kutoka katika akaunti  ya Airtel Money ya mnunuzi kwenda kwenye akaunti  ya muuzaji. “Kadi hii itakuwa inauzwa kwa bei ya Sh 2, 000 kwenye vituo vyote vya  Puma Dar es Salaam na maduka yote ya Airtel Tanzania .Kuanzia mwakani kadi hii itakuwa pia inapatikana katika vituo vyote vya mikoani  ambavyo vipo chini ya Puma,”alisema.
 
Alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa Puma Tanzania ina jumla ya vituo 46  nchini kote na kwa kuanza, vituo vyote vya Dar es Salaam vitakua  vinatoa huduma hiyo, hali vituo vingine vilivyosalia vitaunganishwa hivi  kuanzia mapema mwakani.“Lengo letu ni kuhakikisha kwamba aina yoyote ya biashara  tunayofanya, inafanyika kwa namna ambayo mtumiaji wa mwisho  anaridhika, na kubaki salama. 
 
“Tunaamini  hili kuwa jukumu letu kwa jamii popote wanapotumia  huduma zetu. Kwa kutumia kadi hii ya Airtel Money Tap Tap, mtu  hatahitaji kubeba tena hela tasilimu ili kupata huduma katika kituo cha  Puma,”alisisitiza.
  Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania Philippe Corsaletti kushoto na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso wakionesha mikataba yao pamoja na kadi ya Airtel Money Tap Tap mara baada ya hafla hiyo fupi ya kutiliana saini ya makubaliano hayo,hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Mafuta cha Puma Oysterbay,jijini Dar.
 MENEJA Mkuu wa Puma Energy Tanzania Philippe Corsaletti kushoto na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso  wakiasini  mkataba wa makubaliano ya uuzaji wa mafuta kwa kutumia kadi ya Aiter Money Tap Tap , Hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Mafuta cha Puma Oysterbay jijini  Dar es salaam.
 Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania Philippe Corsaletti kushoto na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso  wakibadilishana mikataba mara baada ya kutiliana saini  makubaliano ya uuzaji wa mafuta kwa kutumia kadi ya Aiter Money Tap Tap , Hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Mafuta cha Puma Oysterbay.
Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania Philippe Corsaletti akizungumza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani),wakati wa hafla fupi ya makubaliano ya uuzaji wa mafuta kwa kutumia kadi ya Aiter Money Tap Tap , Hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Mafuta cha Puma Oysterbay jijini Dar es salaam. kushoto na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso
 Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania Philippe Corsaletti kushoto akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso  mara baada ya kumaliza kutiliana saini na kukabidhiana mikataba makubaliano ya uuzaji wa mafuta kwa kutumia kadi ya Airtel Money Tap Tap , Hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Mafuta cha Puma Oysterbay.
Meneja Rasilimali Watu wa Puma Tanzania Bi Loveness Hoyange pamoja na maofisa wengine wa kampuni hiyo na kampuni ya simu ya Airtel wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika hafla hiyo.

PATO LA TAIFA LAKUA KWA ASILIMIA 7.9-NBS.

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Mkuu wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu hali ya pato la Taifa kwa robo ya pili  kuanzia Aprili hadi Juni 2016 jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa, Daniel Masolwa na kulia ni Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi, Joyce Sawe.
Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii. 

PATO la Taifa limeendelea kukua kwa asilimia 7.9 katika kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni 2016 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 5.8 katika kipindi kama hicho mwaka 2015.

Takwimu hizo zimetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya pato la Taifa kwa robo ya pili  kuanzia Aprili hadi Juni mwaka 2016.

Dkt Chuwa  alisema kuwa ukuaji wa pato la Taifa umetokana na shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo, mifugo, misitu na uvuvi ambapo shughuli  hizo zilikuwa kwa asilimia 3.2 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 1.9 katika kipindi kama hicho mwaka 2015.

Kwa upande wa shughuli za uchumi za viwanda na ujenzi, Dkt. Chuwa alisema kumekuwa na ongezeko la asilimia 20.5 katika kipindi hicho ukilinganisha na ukuaji wa asilimia 11.2 mwaka 2015 katika shughuli za uchimbaji madini, mawe na kokoto.

Aidha katika shughuli za uzalishaji bidhaa na viwanda kumeongeza kwa asilimia 9.1 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2016 ukilinganisha na kasi ya asilimia 5.2 ya mwaka 2015.

Katika shughuli za uchukuzi na uhifadhi, Dkt Chuwa alisema kuwa shughuli hizo zimekuwa kwa kiwango cha asilimia 30.6 zimetokana na usafirishaji wa abiria kwa njia ya reli na barabara ikiwa ni pamoja na usafiri wa UDART.

Hata hivyo katika shughuli za fedha na bima ziliongezeka kwa kasi ya asilimia 12.5 ikilinganishwa na asilimia 10.0 iliyopatikana katika kipindi kama hicho mwaka 2015.

Wakati huo huo huduma za elimu zilikuwa kwa kasi ya asilimia 8.0 katika robo hiyo ya mwaka ikilinganishwa na aslimia 7.4 ya kipindi kama hicho kwa mwaka 2015 ambapo ukuaji wa shughuli hii imetokana na ongezeko la wanafunzi waliodahiliwa mwaka 2016.

Mbali na hayo pato la Taifa kwa nchi za Afrika ya Mashariki zimechambua na kutoa tathimini hiyo katika kipindi kinachoishia Juni 2016, ambapo Rwanda imeendelea kukuwa kwa asilimia 5.4 ukilinganisha na asilimia 7.2 ya miezi kama hiyo mwaka 2015, kwa upande wan chi za Kenya, Uganda na Burundi zinaendelea na uchambuzi wa takwimu hizo.

WAFANYABIASHARA WA UTALII WANATANGAZIWA KUSAJILI NA KULIPIA ADA YA LESENI YA MWAKA 2016

MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA KURINDIMA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA INJILI JIJINI MWANZA.

$
0
0

Kanisa la EAGT Posta “B” Mabatini Jijini Mwanza chini ya Mchungaji Lameck Nkumba, linawakaribisha watu wote kwenye mkutano mkubwa wa injili utakaofanyika katika viwanja vya kanisa hilo vinavyotizamana na geti la polisi Mabatini nyuma ya iliyokuwa Orange Tree Hotel.

Mhubiri wa kitaifa na kimataifa ambaye amehubiri mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Marekani, Canada, Uingereza, Ireland, Wales , Scotland, Ujerumani, Dernmark, Swirtzland, Afrika Kusini, DRC Congo na mengine mengi, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), atahudumu kwenye mkutano huo akishirikiana na wahubiri wengine.

Ni wiki moja yenye miujiza na uponyaji wa nguvu ya Mungu, kuanzia jumapili tarehe 9.10.2016 hadi jumapili tarehe 16.10. 2016 muda ni kuanzia saa 9.00 mchana hadi saa 12 jioni, kila siku.

Waimbaji mbalimbali akiwemo Mwanyamaki kutoka Morogoro, Emannuel Mgogo kutoka Dar es salaam pamoja na kwaya zinatotamba Jijii Mwanza kama vile Havillah Gospel Singers kutoka EAGT Lumala Mpya, na kwaya ya EAGT Posta “B” zitahudumu kwenye mkutano huo.

Ewe baba, mama, kaka, dada, ndugu, jamaa na marafiki, fika kwenye mkutano huo ili ukutane na nguvu ya Mungu ambapo wagonjwa mbalimbali, wenye mapepo, mikosi na waliofungwa na vifungo vya ibirisi watafunguliwa kwa jina la Yesu, bila malipo.

Kwa msaada wa Kiroho, piga simu nambari 0784 43 77 82 
Bonyeza HAPA Kusikiliza, Au Bonyeza Play hapo chini .

Muhimbili Yaendesha Semina Leo Kuimarisha Utoaji Huduma

$
0
0
Mtoa Mada, Martha Mkony akizungumzia vifo vya watoto na jinsi ya kutoa huduma bora kwa watoto wanaozaliwa kabla ya muda na njia ya kuzuia vifo kwa watoto hao.
semi2
Baadhi ya washiriki wakisikiliza mada hiyo Leo katika hospitali hiyo.
semi3
Dk Arvinder Singh akizungumzia umuhimu wa kununua vifaa tiba, kuwapo kwa madaktari na wauguzi wa kutosha, kuwapo kwa gesi ya uhakika, chumba cha kisasa cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu na madaktari na wauguzi kutoa huduma kwa wakati kwa watoto hao.
semi4
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakiwamo madaktari na wauguzi wakifuatilia mada kwenye semina hiyo.
semi5
Dk Hassan Mtani akitoa mada kuhusu kifafa cha mimba katika mkutano uliofanyika Leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
semi6
Baadhi ya washiriki wakisikiliza mada hiyo Leo katika hospitali hiyo.

SERIKALI YATOA RAMBIRAMBI KWA WAFIWA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA

$
0
0
Yusta Jonas mkazi wa Hamugembe Manispaa ya Bukoba akipokea rambirambi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu ambayo imetolewa na Serikali pamoja na kampuni ya simu za mkononi ya Halotel.
Mzee Vedasto Kato kutoka mtaa wa Hamgembe Manispaa ya Bukoba akipokea rambirambi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu ambayo imetolewa na Serikali pamoja na kampuni ya simu za mkononi ya Halotel.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu (katikati aliyekaa) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa wanafamilia waliofiwa na ndugu zao wakati wa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu.





Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akiongea na wawakilishi wa familia waliopoteza ndugu zao (hawapo pichani) kwa tetemeko la ardhi lililotokea mapema Septemba 10 mwaka huu Bukoba mjini wakati wa kukabidhiwa rambirambi iliyotolewa na Serikali milioni 17 pamoja na kampuni ya simu ya Halotel ambayo imetoa shilingi milioni 15.kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Maafa
(Picha na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba)

…………………………………………………………………

Na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba

Familia 15 zilizofiwa na ndugu zao 17 wakati wa tetemeko la ardhi lililotokea mkoani wa Kagera zimepokea rambirambi ya jumla ya shilingi milioni 32 ikiwa ni mkono wa faraja kwa msiba uliwafika familia hizo na taifa kwa ujumla.

Rambirambi hiyo imetolewa mjini Bukoba na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu kwa niaba ya Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya simu za mkononi nchini ya Halotel ili kuwashika mkono wafiwa hao kwa kupoteza ndugu na jamaa zao.

Katika rambirambi hiyo, Serikali imetoa shilingi milioni 17 na kampuni ya simu ya Halotel imetoa shilingi milioni 15 ambapo kila familia ya mfiwa amepokea shilingi 1,000,000 kutoka Serikalini na shilingi 885,000 kutoka kampuni ya Halotel.

Hatua hiyo inapelekea kila familia ya mfiwa kupokea jumla shilingi 1,885,000 ambapo familia mbili zilizopoteza ndugu zao wawili wawili wamepokea jumla ya shilingi 3,770,000 ikiwa ni rambirambi kwa kila ndugu aliyefariki wakati wa tukio hilo la tetemeko la ardhi.

Akikabidhi rambirambi hiyo kwa familia hizo, Mkuu wa Mkoa wa huo akiwa pia Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa mkoa Meja Jenerali Mstaafu Kijuu amesema kuwa Serikali imetoa rambirambi hiyo kwa lengo kuwapa pole wafiwa hao kutokana na kuwapoteza ndugu na jamaa zao wakati wa tetemeko hilo lililotokea Septemba 10, mwaka huu.

Katika kuwahakikishia usalama na utunzaji wa fedha walizopokea wafiwa hao, Mkuu wa mkoa huo amewaasa wasikuwa na akaunti wafungue akaunti katika benki yeyote ili waweze kuziweka fedha hizo walizopokea ili kuwahakikishia usalama badala ya kutembea nazo mkononi.

Wawakilishi wa familia zilizopokea rambirambi hiyo ni pamoja na Vedasto Katto (Hamugembe), Geofrey Gerald (Mafumbo), Alex Felix (Hamugembe), Orestus Aron (Hamugembe), Justa Mkalisa Jonas (Hamugembe), Albert Tibangayuka (Barabara ya Sokoine), Sheikh Mikidadi Abdallah (Hamugembe) na Maria Stella John (Hamugembe).

Wanafamilia wengine waliopokea rambirambi ni Swidick Miyonga (Hamugembe), Jackson Evason (Rwamishenye), Jasson Rugemalila (Rwome), Augustine Muhigi (Rwome), Edson S. Rwetabula (Kashenye), Anitha Evalista (Omurushaka) na John Mulokozi Kahangwa (Kanyigo-Kikukwe).

Aidha, mkuu huyo wa mkoa ameishukuru Kampuni ya simu ya mkononi ya Halotel kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutoa rambirambi na kuwafuta machozi familia za marehemu hao na kuwahakikishia kuwa Serikali inathamini mchango wao kwa jamii.

Akitoa neno la shukrani mara baada ya kupokea rambirambi hiyo kwa niaba ya wafiwa wenzake, Mzee Vedasto Kato kutoka mtaa wa Hamgembe Manispaa ya Bukoba ametoa shukrani kwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuona haja ya kuwashika mkono baada ya kupoteza ndugu zao.

“Tunaishukuru Serikali kwa kutujali wafiwa tuliopoteza ndugu zetu wakati wa tetemeko la ardhi lililotokea katika mkoa wetu mwezi huu na kutuonea huruma katika kipindi hiki kigumu kilichotuachia majonzi makubwa katika familia zetu” alisema mzee Vedasto.

Mzee Vedasto amesema kuwa hatua iliyochukuliwa na Serikali katika kuwapa mkono wa pole imewapa faraja na ameiomba Serikali kuendelea kuwajali wananchi wake kama ilivyokuwa kwao.

Tetemeko la ardhi lilitokea mkoani Kagera mapema mwezi huu, limesababisha vifo ambapo wananchi 17 waliopoteza maisha yao, majeruhi 440 ambao walitibiwa katika vituo mbalimbali vya afya pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Pamoja na rambirambi hiyo, Serikali pia iliwahudumia marehemu waliopoteza uhai wakati wa tukio hilo kwa kutoa majeneza pamoja na usafiri wa kusafirisha miili ya marehemu hao kutoka Bukoba mjini hadi kwenye maeneo ambayo familia zao walipo ambapo yalipofanyika maziko ya wapendwa wao.

BOMBADIER KUIPAISHA TANZANIA KIUCHUMI

$
0
0

Benjamin Sawe-Maelezo
Dar es Salaam

MTAFITI wa uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Haji Semboja aimepongeza hatua ya Serikali ya kununua ndege mbili za abiria aina ya Bombadier- 8 Q400 na kusema zitasaidia kuimarisha sekta ya usafiri wa anga nchini na kuchangia katika ukuaji wa uchumi.

Prof. Semboja aliyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano maalum na MAELEZO kuhusu mikakati na hatua ya Serikali ya kulifufua upya shirika la ndege nchini (ATCL).

Profesa Semboja alipingana na maoni ya baadhi ya watu wanaokosoa kasi ya ndege hizo, kwani kulingana ndege hizo zimekidhi mahitaji ya usafiri wa abiria wa ndani na nje ya nchi ikilinganishwa na ndege nyingine za aina yake kama ATR

Akizungumzia kuhusu kupanda kwa gharama za matengenezo na uendeshaji wa baadhi ya ndege nyingine nchini, ikiwemo mahitaji ya ongezeko la mishahara kwa marubani, Profesa Semboja alisema kuna uwezekano mkubwa kwa Bombardier- 8 Q400 kuendeshwa kwa bei rahisi na ikauza tiketi zake kwa bei rahisi zaidi kuliko ndege nyingine.

“Shirika letu la ndege lilikuwa na hali mbaya kutokana na kushindwa kujiendesha kutokana na gharama kubwa za uendeshaji na abiria wachache, wanaotumia usafiri wa anga”.Alisema Profesa Joseph Semboja

Alisema ndege hizo zitaimarisha mtandao wa huduma za usafiri wa anga kwa soko la ndani, lakini pia zitaongeza ushindani na kuleta unafuu wa bei kwa watumiaji wa usafiri wa anga,
 
“Zitaimarisha sekta za biashara na uwekezaji na kuwezesha watalii kutembelea vivutio vya ndani ya nchi" Alisema Profesa Joseph Semboja.

Aidha Prof. Semboja aliwataka Watanzania wote wakiwemo wafanyabiashara, wakulima na wafanyakazi kusafiri kwa kutumia ndege hizo ili Kampuni ya ATCL ijiimarishe na iweze kujiendesha kibiashara baada ya kutegemea bajeti ya Serikali.

Wanafunzi shule ya msingi Kashai wanaendelea na masomo.

$
0
0


Tatizo lolote linapotokea katika jamii huambatana na mambo mbalimbali ikiwemo kutembelewa na wageni wakiwemo waandishi wa habari.

Hali hiyo imetokea katika Manispaa ya Bukoba kufuatia tetemeko la ardhi lililoathiri mkoa huo pamoja na miundombinu mbalimbali ambapo shule ya msingi Kashai nayo ilipata athari za tetemeko hilo.

Athari hiyo ya tetemeko ilipelekea chombo kimoja cha habari cha televisheni nchini kuripoti katika taarifa ya habari kuwa shule hiyo imefungwa na wanafunzi wamerudishwa nyumbani mara baada ya kumaliza likizo fupi badala ya kuendelea na masomo.

Taarifa ya kufungwa kwa shule hiyo inakanushwa na aliyekuwa Mwalim Mkuu wa Shule ya Msingi Kashai, Gideon Kenjori Akizungumzia kuhusu suala hilo na kusema kuwa shule haijafungwa na wanafunzi wanaendelea kusoma kama kawaida.

Mwalimu huyo amesema kuwa habari hiyo iliyotangazwa haikuwa na ukweli wowote kwa kuwa wanafunzi wanaendelea na masomo kwa madarasa yote huku akimshangaa mwandishi wa habari aliyetoa habari hiyo na kusema alijitengenezea habari aliyeitaka yeye na sio hali halisi ya shule ya Kashai.

“Shule haijafungwa, mimi sikuja na mwandishi wala sikuwepo,mwandishi alikurupuka na kuenda nyuma na wala hakuja ofisini na hajaonana na sisi, yeye aliripoti ya kwake aliyeyaona na hakuna mtu ambaye aliongea nae, aliandika ya kwake na amepata taarifa alizotaka alikojua” alisema Mwalimu Gideon.

Mwalimu huyo amesema kuwa athari za tetemeko limeharibu vyumba saba vya madarasa ambavyo havifai kutumika, vyumba nane vinaweza kutumika na nyumba ya mwalimu imepata nyufa hatarishi.

Ili kuhakikisha wanafunzi wote wanasoma umefanyika utaratibu wa wanafunzi kusoma kwa awamu ambao ni wanafunzi wa darasa la kwanza na pili na wanafunzi wengine wa darasa la tano na la sita wamehamishiwa katika shule ya msingi Tumaini ambapo kuna madarasa manne yaliyowazi wakati wanafunzi wa madarasa mengine yaliyobaki wanaendelea na masomo shuleni hapo.

Mwl. Gideon ameongeza kuwa uwezo wa kufunga shule haupo chini ya Mwalimu Mkuu bali mamlaka ya kufunga shule inatoka kwa uongozi wa juu ambao ndio wenye uwezo huo, kwa maana hiyo shule haikufungwa.

Katika kuhakikisha wanafunzi wanaendelea na masomo kulingana na ratiba ya muhula wa masomo, Uongozi wa Manispaa ya Bukoba umeagiza walimu ambao nyumba zao hazifai kutumika watafute nyumba za kupanga na manispaa italipia gharama za nyumba hizo wakati utaratibu wa kukarabati au kujenga nyumba zao unaendelea ili maisha yao yaendelee kama kawaida waweze kutimiza majukumu yao ya kufundisha.

UZINDUZI WA MATOKEO YA UTAFITI WA MAPATO NA MATUMIZI YA KAYA BINAFSI YAFANYIKA ZANZIBAR.

$
0
0
 Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dk,Khalid Salum Mohammed wamwanzo kushoto akionesha kitabu cha Uzinduzi wa  Matokeo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2014/15 uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar. katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Yubu Mohd Mahamoud na mwengine ni Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya zanzibar Mayasa Mahfoudha Mwinyi.
Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dk,Khalid Salum Mohammed akimkabidhi Muakilishi wa UNICEF Francesca Morandini kitabu cha  Matokeo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2014/15 uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar. 

 Baadhi ya Waalikwa waliohudhuria katika Uzinduzi wa Matokeo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2014/15 uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
 Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mayasa Mahfoudha Mwinyi akitoa maelezo kuhusu utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya binafsi wa Mwaka 2014/15 katika Uzinduzi uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
 Muakilishi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa Zanzibar Anna Senga akitoa maelezo kuhusu  utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya binafsi wa Mwaka 2014/15 katika Uzinduzi uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
 Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohd Mahmoud akitoa hotuba ya makaribisho kwa mgeni rasmi katika Uzinduzi wa  utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya binafsi wa Mwaka 2014/15  katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.

 Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dk,Khalid Salum Mohammed akitoa hotuba ya Uzinduzi wa Matokeo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2014/15 uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar.
 Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dk,Khalid Salum Mohammed wamwanzo kushoto akizindua Matokeo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2014/15 uliofanyika katika Ukumbi wa Sanaa Rahaleo Zanzibar. katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Yubu Mohd Mahamoud na mwengine ni Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya zanzibar Mayasa Mahfoudha Mwinyi.
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

JUMUIA YA KANGA MATERNITY TRUST YAANDAA MAFUNZO KWA MADAKTARI WA GANZI NA USINGIZI WA ZANZIBAR

$
0
0
 Mkufunzi wa mafunzo ya siku tatu ya Madaktari wa ganzi na usingizi wa Zanzibar Dkt. Lee Ngungi kutoka Kenya akielezea umuhimu wa taaluma ya ganzi na usingizi katika sherehe ya ufungaji wa mafunzo hayo iliyofanyika Hoteli ya Mazson Shangani Mjini Zanzibar.
 Mratibu wa Mafunzo ambae ni Mkuu wa kitengo cha ganzi na usingizi Hospitali kuu ya Mnazimmoja Dkt Khamis Waziri akitoa shukurani kwa wafadhili wa mafunzo hayo Kanga Martenity Trust

 Mwenyekiti wa Kanga Martenity Trust Dkt Mohd Hafidh (aliyesimama) akifunga mafunzo ya siku tatu  yaliyowashirikisha madaktari wa ganzi na usingizi wa Hospitali kuu ya Mnazimmoja yaliyofanyika katika Hoteli ya Manson Shangani mjini Zanzibar
 Mshiriki wa mafunzo ya Ganzi na Usingizi Dkt. Mohd Rashid akikabidhiwa cheti na Mwenyekiti wa Kanga Trust  Mohd Hafidh.
Washiriki wa mafunzo ya Ganzi na Usingizi wakiwa katika picha ya pamoja (Picha na Makame Mshenga   Habari Maelezo Zanzibar),

Na Ramadhan Ali/Maelezo Zanzibar 29.9.2016

Mtaalamu wa Sayansi ya ganzi na usingiza Dkt. Lee Ngungi kutoka Kenya amesema teknolojia ya taaluma hiyo inabadilika kwa haraka hivyo kuna haja kwa madaktari wanaoshughulika na fani hiyo kuandaliwa mafunzo ya mara kwa mara ili kwenda sambamba na mabadiliko hayo duniani.

Dkt. Ngungi ambae alikuwa mkufunzi wa mafunzo ya siku tatu ya madaktari wa ganzi na usingizi wa Zanzibar yaliyofadhiliwa na Jumuia ya Kanga Maternity Trust katika Hoteli ya Mazsons Shangani, amesema elimu kwa ajili ya madaktari wa kada hiyo inahitaji kupewa kipaumbele ili kuwajengea uwezo wa kuhudumia jamii kwa ufanisi zaidi.

Amesema lengo la teknolojia ya ganzi na usingizi kwa sasa hasa kwa upande wa mama wajawazito inapobidi kufanyiwa upasuaji ni kuwawezesha kujifungua bila matatizo na baada ya kupata fahamu wasiweze kupata maumivu makali.

Dkt. Ngungi amezishauri jamii za nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki kuunga mkono na kuthamini juhudi zinazochukuliwa na Serikali na Taasisi nyengine za Kimataifa na Kitaifa za kuwapatia elimu madaktari wa ganzi na usingizi katika nchi zao.

Mratibu wa mafunzo hayo ambae ni Mkuu wa Kitengo cha ganzi na usingizi katika Hospitali kuu ya Mnazimmoja Dkt. Khamis Wazir amesema mafunzo hayo ya kwanza, ndani ya kazi, kwa wafanyakazi wa kada hiyo Zanzibar yataongeza ufanisi katika kuhudumia mama wajawazito.

Ameishukuru Kanga Maternity Trust kwa kushirikiana na Hospitali kuu ya Mnazimmoja kufadhili mafunzo hayo na kusema kuwa wataalamu wa fani ya ganzi na usingizi wanahitaji vifaa na elimu zaidi ili kupunguza vifo vya mama wajawazito wakati wa kujifungua.

Ameongeza kuwa wataalamu wa kada hiyo kwa kipindi kirefu walikuwa hawatambuliki umuhimu wao lakini ametanabahisha kuwa wao ni muhimili mkubwa wa Hospitli hasa zinazoendesha upasuaji.

Akifunga mafunzo hayo yaliyowashirikisha madaktari 25 wa ganzi na usingizi kutoka Hospitali za Unguja na Pemba, Mwenyekti wa Kanga Maternity Trust Dkt. Mohd Hafidh amesema akinamama wanapo beba ujauzito wanakuwa na wakati mgumu na siku ya kujifungua shida inaongezeka hivyo wananchi wenye uwezo wa kusaidia nyenzo kuokoa maisha ya mama na mtoto kupitia Jumuia hiyo wanakaribishwa.

Amesema mafunzo yaliyotolewa kwa wataalamu wa ganzi na usingizi kutoka Hospitali mbali mbali za Zanzibar ni kuthamini kazi nzuri wanayofanya na lengo ni kuwapatia taaluma zaidi .

Ameahidi kuwa Kanga Meternity Trust itaendelea kusaidi ufanisi kwa wataalamu wa fani ya usingizi na ganzi ili kusaidia wagonjwa hasa akinama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua.

MWISHO IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR.

ASILIMIA 80 YA WANANCHI WANATAKA MAENDELEO NA SI SIASA- TWAWEZA.

$
0
0
Na Abushehe Nondo,Maelezo.

ASILIMIA 80 ya Watanzania wamesema juhudi za maendeleo hazina budi kupewa kipaumbele baada ya uchaguzi na kukataa mikutano ya kisiasa ambayo wanadai hukwamisha shughuli za maendeleo.

Taarifa ya utafiti huo iliyotolewa leo Jijini Dar es Salaaam na Shirika la Utafiti la TWAWEZA ilisema kuwa utafiti huo umebeba maoni ya wananchi kuhusu demokrasia, udikteta na maandamano nchini Tanzania.

Aidha taarifa hiyo iliongeza kuwa takwimu za muhtasari huo zinatokana na na utafiti wa sauti za wananchi ikiwa ni moja ya programu za Twaweza.

Pia katika utafiti huo, wataalamu hao waliweza kubaini kuwa asilimia 49 ya wananchi wanakubaliana na kuzuiwa kwa mikutano ya vyama vya siasa kutokana na kwamba huvuruga umakini wa Serikali na Wananchi.

Katika suala la kumhusisha Rais Maguli na udikteta utafiti huo umebaini kuwa asilimia 58 ya Watanzania wanapinga uwepo wa udikteta katika serikali ya awamu ya Tano ya Rais John Magufuli.

Aidha utafiti huo wa Twaweza pia umebainisha kuwa asilimia 50 ya wananchi wamesema hakuna uwezekano wa wao kushiriki kwenye maandamano yoyote.

Kuhusu uamuzi wa Rais Magufuli kuzuia mikutano ya hadhara utafiti huo unaonyesha kuwa asilimia 60 wanamuunga mkono Rais katika kuzuia mikutano ya hadhara ya kisiasa.

Utafiti huo wa Twaweza umekuja baada ya Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli kujipatia pongezi nyingi kwa jitihada zake za kupambana na na vitendo vya rushwa.

KATIZO LA UMEME MKOA WA KINONDONI KUSINI MWISHO WA WIKI HII.

$
0
0
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa Mkoa wa Kinondoni Kusini kuwa kutakuwa na katizo la umeme kama ifuatavyo:-

TAREHE:    Jumamosi 01 Oktoba, 2016
MUDA:       02:00 Asubuhi hadi 11:00 jioni
SABABU:   Kujenga laini mpya ya Mburahati na ukarabati wa laini za Tandale Textile ili kuboresha hali ya umeme.

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:
Maeneo yote ya Tandale, Manzese, Sinza Uwanja wa TP, Sinza Vatican, Namnani Hotel, Iteba, Sinza Kijiweni,  Sinza Kumekucha, Sinza Mwika, TTCL Manzese , Urafiki Quarters, Urafiki Textile,TSP Ltd Millenium business, Sinza Lion Hotel, Rombo Sunflower, Strabag compound, Engen petrol station, Masamaki Plastic Bags Ltd pamoja na maeneo ya jirani.

TAREHE:     Jumapili 2 Octoba, 2016
MUDA:       02:00 Asubuhi hadi 11:00 jioni
SABABU:   Matengenezo kwenye Kituo cha Kupozea Umeme Ubungo 33kv ili kuboresha hali ya umeme.

MAENEO YATAKAYOATHIRIKA:
Parts of Mandela road, I ndustrial area near Mandela road, Ubungo NBC, Tbs  Ubungo, Ubungo Bus Terminal, Parts of  Sinza, Part of Kimara, Baruti,Kimara Kimara Korogwe,Kimara Mwisho, Kimara Matangini, Kimara Mavurunza, Ubungo Maziwa, TTCL Ubungo Kisiwani,  Mabibo,TGNP Mabibo, Mabibo Hostel, Mabibo Jeshini, Mabibo, Makabe, Mpigi Magohe, Goba,Kimara King’ong’o, Tegeta A,Mavurunza, Suka, Stopover, Changanyikeni, Makongo Mwisho pamoja na maeneo ya jirani.

Tafadhali usishike waya uliokatika, toa taarifa kupitia simu zifuatazo Magomeni 0222171759/66, 0784/0715271461, Kimara Ofisi ya Wilaya 0717/0788379696, Au Kituo cha miito ya simu 2194400 Au 0768 985100.

Uongozi unasikitika kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Imetolewa na:  Ofisi ya Uhusiano, TANESCO Makao Makuu                      

Maafisa watatu wa serikali na meneja wa CRDB tawi la Bukoba wafikishwa mahakama

$
0
0
Maafisa watatu wa serikali na meneja wa CRDB tawi la Bukoba wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Bukoba wakituhumiwa kula njama kwa kufungua akaunti ya bandia inayofanana na ile inayotumika kukusanya fedha za waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.     
                   
Aliyekuwa Ofisa tawala Mkoa wa Kagera (RAS) Bw Amantius Msole,Aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba BW Kelvin Makonda,AliyekuwaMhasibu wa Mkoa Kagera Simbaufoo Swai na Meneja CRDB Kagera Karlo Sendwa wamefikishwa mahakamani leo mchana kwa kudaiwa kutengeneza akaunti bandia iliyo na jina sawa na lilioandaliwa na serikali kukusanya fedha kwa ajili ya waathirika wa Tetemeko mkoani Kagera.

 Wakati ya serikali ikiitwa KAMATI MAAFA KAGERA ikiwa na kianzio cha 0152..wao wamefungua ya jina hilo hilo lakini ikiwa na kianzio cha 0150...Kwa hiyo ya Serikali iliyopitishwa ni 0152225617300 CRDB Bukoba Huku bandia ina jina hilo hilo lakini ikiwa na tofauti ya namba moja tu yahani 0150225617300.

Watuhumiwa hawakutakiwa kujibu chochote na wamenyimwa dhamana hadi septemba 30,2016 itakapotajwa tena.




WAZIRI MKUU KUWASILI KESHO DODOMA,AKITEKELEZA AHADI YAKE YA KUHAMIA MKOANI DODOMA

MRADI WA URASIMISHAJI ARDHI UBUNGO WAINGIA MIZENGWE WATENDAJI WATISHIA KOGOMA KWA KUKOSA POSHO

$
0
0
Waziri wa Ardhi, William Lukuvi
Na Dotto Mwaibale

WATENDAJI na vibarua wanaofanya kazi ya kupima ardhi katika mradi wa urasimishaji wa ardhi katika maeneo yaliyojengwa kiholela katika Kata ya Kimara  wilayani Ubungo umeingia mdudu baada ya kutishia kugoma kutokana na kutolipwa fedha za posho ya kazi hiyo kwa zaidi ya miezi mitatu.

Hatua hiyo imefikiwa baana ya kuona baadhi ya vongozi wanaosimamia mradi huo wa kuanza kujinufaisha wenyewe na kuwanyonya watendaji wakiwemo vibarua 
hao.

Wafanyakazi wa upimaji wa ardhi kutoka wizarani na vibarua hao wakiongea kwa nyakati tofauti na gazeti hili kwa masharti ya kuto andikwa majina yao gazetini  wamesema  viongozi hao kupitia mradi huo wamejenga mazingira ya  kujinufaisha kupitia fedha zilizotoka Benki ya Dunia kufanya mradi huo.

"Tunachangamoto kubwa ya kupata fedha za malipo kwa kazi tunayoifanya tumefanya kazi miezi minne lakini tumelipwa mwezi mmoja tu na si sisi peke yetu na hata  watendaji wa wizara wanaofanya kazi hii nao hawajalipwa wakati fedha zipo " alisema mmoja wa vibarua hao.

Kibarua huyo alisema kuwa kuna mmoja wa kiongozi wa wizara hiyo anayesimamia mradi huo ndiye kikwazo kikubwa cha mradi huo na jitihada za makusudi  zisipochukuliwa mradi huo hautafikia malengo yake.

“Binafsi acha niseme ukweli mradi huu ulianza vizuri lakini sasa utakwama kwani viongozi waliopo pale wizarani wameanza kutumia fedha vibaya na hawataki kutupa licha ya fedha za mradi kuwepo na tunapowadai wanasema eti Rais John Magufuli hajaidhinisha fedha hizo wakati sio kweli" alisema mtendaji mwingine wa  mradi huo kutoka wizarani.

Mtendaji huyo alisema changamoto hiyo yakutopewa fedha zao imewapunguzia mori wa kazi hivyo kuingia mashaka kama mradi huo utakwisha.


“Kiukweli ndugu mwandishi hapa watu wanaishi kama ndege wafanyakazi kila kukicha ila hawajalipwa mwezi wa tatu, ukiangalia kwa sasa wanasema eti hela zao  zimetoka ila wanalipwa siku 20 wakati mwezi unasiku 30 sasa hizo hela zinazobaki za siku 10 viongozi wanazipeleka wapi? kama si wizi wa macho macho" alihoji  mtendaji huyo.

Mtendaji huyo aliongeza kuwa jambo hilo limekuwa ni janga kwani watendaji wa mradi huo wapo zaidi ya 50 sasa anapokatwa siku 10 kila mmoja anapata  shilingi ngapi hanazikosa na fedha hizo zinapelekwa wapi.

Akizungumzia changamoto hiyo Diwani wa Kata ya Kimara ambapo mradi huo upo, Pascal Manota alikiri kwa watendaji hao kutolipwa fedha hizo na tayari amekwisha  mjulisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi juu ya changamoto hiyo.

"Changamoto kubwa ipo kwa viongozi wa wizara waliopewa kufanyakazi hiyo fedha zipo lakini hawawalipi watendaji hali inayozoofisha mradi huo tunamuomba  waziri aliangalie suala hilo kwa karibu kabla ya mambo kuharibika" alisema Manota.

Manota alisema watendaji hao wa serikali hivi sasa wapo tu ofisini wakisoma magazeti hawana ari ya kazi hali hii imechangiwa na viongozi hao wasiokwenda na kasi ya Rais wetu Dk. John Magufuli ya hapa kazi tu.

Jitihada za gazeti hili za kumpata mratibu wa urasimishaji wa ardhi wa wizara hiyo ambaye anasimamia mradi huo, Lydia Bagenda zilishindikana baada ya kwenda  ofisini kwake na kuambiwa alikuwa nje ya ofisi kikazi na hata halipopigiwa simu mara kadhaa simu yake ilikuwa imefungwa.


RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kabla ya kuanza kwa Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongoza Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na balaza la mawaziri jijini Dar es Salaam leo.

DC KINAWIRO AKUTANA NA BARAZA LA MADIWANI MKOANI KAGERA NA KUKAGUA UKARABATI MIUNDOMBINU YA SHULE NA BARABARA

ZIMWI LA TEGETA ESCROW LAMTISHA PROFESA TIBAIJUKA, AKATAA KUPOKEA DOLA 300,000 BAADA YA KUPEWA TUZO YA KIMATAIFA

$
0
0

 Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka akionesha tuzo ya kimataifa (UN) ya Maendeleo Endelevu ya Mwana Mfalme Khalifa Bin Salman Al Khalifa aliyotunukiwa hivi karibuni New York Marekani wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo.
 Profesa Anna Tibaijuka akionesha cheti alichokabidhiwa sanjari na tuzo hiyo.
 Profesa Tibaijuka akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari. Kulia ni Mratibu wa mkutano huo, Mussa Ally.
 wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale


MBUNGE wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka amekacha kuchukua dola 300,000 alizopewa baada ya kutunukiwa tuzo ya  Maendeleo Endelevu aliyopewa na Umoja wa Mataifa (UN), kutokana na sakata la fedha za Escrow Tegeta.


Tuzo hiyo aliipokea Septemba 23 mwaka huu New York Marekani ambayo mfadhili wa tuzo hiyo ni wa waziri mkuu wa Bahrain mwana mfalume Khalifa bin Al Khalifa.

Akizungumza jana Dar es Salaam Profesa Tibaijuka alisema kwa sasa umoja wa mataifa umeingia katika awamu ya pili ya maendeleo, ambao umekuja kupisha yale malengo 17 ya mileniam ambayo yote yeye alikuwepo, hivyo aliokuwa wanatoa tuzo walinona kwa namna alivyoshiriki kwa kiasi kikubwa.

"Tuzo hizi si za kuomba, ni watu wanakaa na kupendekeza mtu wa kupewa, na hii ni mara ya pili, mara ya kwanza   nilipewa mwaka 2009 nchini Swideni," alisema na kuongeza.

"Tuzo zinatoka kwa niaba ya jamii inayotoka au kuitumikia na kufanya nayo kazi, hivyo wamatambua mchango wangu katika kuwatumikia wananchi wa Muleba," alisema.

Aidha Profesa tibaijuka alitaja sababu zilizpokekea yeye kutochua dola 300,000 za Marekeni za tuzo hiyo.

"Sikuichukua kwa sababu ya yaliyonikuta hapo mapema, kulikuwa na uwezekano wa kuichukua lakini nikasema kwa hali halisi ya nyumbani, hatuna sheria ya kupokea tuzo, michango na zawadi kwa hiyo mimi nikaicha mezani wao wafanye wanayotaka," alisema na kuongeza. 

"Unapoona mtu kama mimi nafanya kazi nakwenda kuchafulia kwenye kitu ambacho siusiki nacho, sasa Unapoipokea hapa utaonekana kama umevunja maadili au umejinufaisha kwa kuwa ndio mambo ya kwetu, hivyo nikawaachia," alisema.

Aliongeza kwa sasa umeshapeleka mswada binafsi bungeni wa kuweka sheria ya michango ili vitu vya hiari kama hivi vinapokuja katika jamii visimamiwe na si kupotoshwa kisiasa.

"Kwa maana jambo hili halina kificho, yaani huwezi kumzungumzia Anna Tibaijuka bila kutaja suala la Escro, hayo hayakwepeki kwa sababu yalitengenezwa yakawa hivyo, mtu asiyehusika anavalishwa joho lisilo muhusu.

"Lakini kwa sababu jamii haina uwezo wa kuchimba chini, unabaki kuwa uongo na kushindwa kujua ukweli umesimama wapi, lakini wao (UN) wanajua hii ni propanda la sivyo nisingesimama hapa na tuzo," alisema.

Aliongeza licha ya yeye kuwa mstaafu wa umoja wa mataifa bado wanamfuatilia katika shughuli za kimaendeleo ambazo anazifanya akiwa ndani na nje ya nchi.

"Kama ukijikwaa, ukianguka na kusimama watu wanaangalia kulikoni, na huu ni utamaduni wao, kwa hiyo pale uongo na fitina havina nafasi," alisema kwa msisitizo wakati akizungumza na wanahabari.

Diwani wa Kata ya Karambi ambaye pia ni Mjumbe wa mkutano Mkuu wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM),  Felix Bwahama ambaye aliongozana na  Profesa Tibaijuka alishukuru UN kwa kumtunuku tuzo hiyo ambapo alisema ni fahari kwa wanakagera na taifa kwa ujumla licha ya baadhi ya watu nchini kubeza kazi anazizifanya ambazo zinaonekana kimataifa.

SERIKALI YARIDHIA UTEKELEZAJI WA UJENZI WA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA-MAJALIWA

$
0
0

SERIKALI ya Tanzania imeridhia rasmi utekelezaji wa mradi ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Kabaale katika Wilaya ya Hoima nchini Uganda hadi bandariya Tanga nchini Tanzania.

Uamuzi huo umefikiwa katika Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika leo (tarehe 29 Septemba, 2016) Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Taarifa ya kuridhiwa rasmi kwa mradi huo imetolewa naWaziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambaye amesema ujenzi wa mradi huo utakaoanza wakati wowote kuanzia sasa unatarajiwa kukamilika mwaka 2020.

Amesema ujenzi wa bomba hilo unatarajiwa kugharimu dola za Marekani Bilioni 3.5 ambapo kati yake Dola Bilioni 3 zitatumika kujenga bomba upande wa Tanzania.

Mradi huom kubwa utatekelezwa kwa ubia wa ujenzi na uendeshaji kwa kushirikishaka mpuni za Total ya Ufaransa, CNOOC ya China, Tullow ya Uingereza na Serikaliza Tanzania na Uganda.

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilometa 1,443 linatarajiwa kusafirisha mapipa 200,000 kwa siku ambapo kila pipa litaliingizia taifa Dola za Marekani 12.2.

Amebainisha kuwa pamoja na kusafirisha mafuta ya kutoka nchini Uganda bomba hilo pia linatarajiwa kusafirisha mafutakutoka nchi nyingine zaJ amhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudani Kusini ambazo zimeonesha nia ya  kusafirisha mafuta yao kupitia bandari ya Tanga.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametaja faida nyingine ambazo Tanzania itazipata kutoka na namradi huo kuwa ni kupatika na kwa ajira zaidi ya 15,000 wakati wa ujenzi na ajira 2,000 baadaya ujenzi kukamilika, kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia, kukuza biashara katika ukanda wa kaskazini mwa Tanzania, kampuni za ujenziza Tanzania kupata kazi za ujenzi.

Aidha, amesema Tanzania inatarajia kunufaika zaidi kwa kutumia bomba hilo kupitisha mafuta yanayotarajiwa kupatikana katika maeneo ya ziwa Tanganyika na Ziwa Eyasi

 IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMATANO, SEPTEMBA  28, 2016  

WATANZANIA WAASWA KUEPUKA VYAKULA VISIVYO BORA KUEPUKA UGONJWA WA MOYO

$
0
0

Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi

………………………………………………………..

Na Ally Daud-MAELEZO-Dar es Salaam

IMEBAINIKA kuwa ulaji wa vyakula visivyo bora husababisha maradhi ya magonjwa ya moyo kwa watu wazima wa miaka 45 hadi 60

Aidha tafiti zinaongeza kuwa watoto wadogo pia ni miongoni mwa waathirika wa ugonjwa wa moyo, wanaoupata kutokana na kurithi kutoka kwa wazazi wao.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Msemaji Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Bw. Maulid Kikondo wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo duniani ambapo kitaifa ilifanyika katika taasisi hiyo.

Kikondo alisema kuwa katika kuadhimisha siku hiyo Taasisi hiyo imeamua kupima wagonjwa wa moyo bure ili kuwasaidia wananchi kuweza kufahamu njia bora za kuweka kukabiliana na magonjwa hayo.

Kikondo alisema kuwa wazee na watoto hupata maradhi ya moyo kwa wingi nchini kutokana kula vyakula visivyo na mpangilio pamoja na kukosa kufanya mazoezi kwa muda mrefu.

“Ugonjwa wa moyo huwapata zaidi watoto kutokana kwa kurithi au kutopata mlo ulio bora na mpangilio wakati wazee hupata ugonjwa huu kutokana na msongo wa mawazo pamoja na kutofanya mazoezi mara kwa mara hivyo kupelekea kupata presha na mwisho wake ni ugonjwa wa moyo” alisema Kikondo.

Aidha Kikondo alisema kuwa wagonjwa wa moyo wanaopatikana kwa siku ni kuanzia wagonjwa 200 na kuendelea kiasi ambacho ni hatari kwa maendeleo ya nchi hasa kwa taifa linaloelekea katika uchumi wa kati.

Kwa upande wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Delilah Kimambo imesema kuwa inasadikika duniani kote kati ya watu milioni 17.3 hupoteza maisha yao kutokana na ugonjwa wa moyo.

Siku ya Moyo Duniani huadhimishwa Septemba 29 kila mwaka ili kuhamasisha watu kuhusu afya ya Moyo ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “YAPE NGUVU MAISHA YAKO”
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live




Latest Images