Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

Miradi ya JUMEME yaziondoa gizani kaya 5,000 Ukerewe

$
0
0

 Moja ya mitambo ya kuzalisha umeme jua kutoka kampuni ya JUMEME iliyopo katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. 
 Baadhi ya mafundi mitambo wa kampuni ya JUMEME, wakifunga mitambo ya umeme jua katika moja ya miradi ya kampuni hiyo huko kisiwani Ukara, Ukerewe mkoani Mwanza.



ZAIDI ya kaya 5,000 katika kisiwa cha Ukara kilichopo wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, zimenufaika na umeme jua unaozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya usambazaji umeme vijijini (JUMEME).


Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mmoja wa wakurugenzi wa kampuni hiyo, Profesa Costa Mahalu katika hotuba yake kwa maofisa kutoka Umoja wa Ulaya na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), waliotembelea miradi ya umeme jua iliyopo wilaya hapo.


Profesa Mahalu alisema kaya hizo zimenufaika kutokana na awamu ya kwanza ya mradi wa usambazaji umeme katika kisiwa hicho cha Ukara.

“Awamu ya kwanza ya iliyopewa jina la "Uzalishaji umeme wa katika kukuza uchumi wa Tanzania’ imeonesha utofauti kutokana na faida za kiuchumi na kijamii zilizopatikana.


“Kwa sababu mbali na kaya 5,000 kunufaika pia, wafanyabiashara wadogo na viwandani pia wameunganishwa. Lakini taasisi mbalimbali zinazotoa huduma za kijamii kama vile maji vijijini na hospitali zimeunganishwa,” alisema.


Alisema huduma za JUMEME zimevifikia vijiji 20 kwenye visiwa 10 tofauti, na kuchochea uchumi wa eneo hilo jambo lililosaidia kuibua fursa nyingi za ajira.


"Malengo ya muda mrefu kwa JUMEME ni kuendelea  kushirikiana na wazalishaji wadogo ikiwa ni pamoja na kuwekeza kwa waajiriwa wa eneo husika," alisema Prof. Mahalu ambaye pia ni Makamu wa Chuo Kikuu cha Mt. Agustino (SAUT).


Aidha, alisema kampuni hiyo imekuwa ikizingatia utoaji wa fursa za ajira kwa watanzania ili kuisaidia Serikali kukabiliana na uhaba wa ajira kwa vijana nchini.


"Kila mmoja wa wafanyakazi wanaofanya kazi ya uhandisi katika miradi 12 ya JUMEME, ni Mtanzania. Kati ya watu 25 wanaounda timu ya kudumu ya JUMEME wenyeji ni 22, ambao hupewa upendeleo wa wazi linapokuja suala la kufanya kazi.


“Kwa kuzingatia mafanikio ya awamu hii ya kwanza, tunatumaini kuwa na uwezo wa kutoa fursa zaidi za kazi kwa vijana wetu kwa kuendelea nao katika awamu ya pili, ya tatu na kuendelea zaidi katika miradi ya JUMEME. " alisema.


Alisema ili kuongeza uweledi na ufanisi wa waajiriwa wazalendo, kampuni hiyo inaendelea kutoa mafunzo yanayowajengea uwezo wahandisi wa ndani na vijana wataalamu kwa madhumuni ya kuendesha gridi ndogo ndogo zinazoendelea kujengwa hapa nchini.


Pia alisema lengo la JUMEME ni kutoa umeme wa uhakika na wa bei nafuu kwa wakazi husika hususani maeneo ambayo umeme gridi ya Taifa haiwezi kufika.


“Lengo letu ni kufunga mifumo 300 ya uzalisha umeme utakaoweza kuingizwa kwenye ya gridi ya Taifa na kusaidia watu zaidi ya 1,000,000 ifikapo mwaka 2023 katika vijiji mbalimbali nchini Tanzania.


Aliongeza kampuni hiyo ya JUMEME ilioundwa mwaka 2014  chini ya mradi wa "Micropower Economy roll out in Tanzania" na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU), inalenga kukuza, kujenga, na kuendesha gridi ndogo za umeme jua katika vijijini mbalimbali  nchini.



TCRA yapeleka kampeini ya Haachwi Mtu Nyuma kamilisha usajili wako mkoa Mtwara

$
0
0

 
 
 
Mtwara Jumatano 11 Disemba 2019

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezindua kampeini ya ‘Haachwi Mtu Nyuma Kamilisha Usajili mkoani Mtwara huku ikiwahimiza mwananchi wa mkoa kukamilisha usajili wa laini zao za simu kwa alama ya vidole kabla ya mwisho wa mwezi.

Kampeini ya Haachwi Mtu Nyuma Kamilisha usajili ya laini ni ushirikiano wa makampuni yote ya simu za mkononi hapa nchini huku ikisimamiwa na TCRA kwa udhamini wa FSDT.

Akizungumza Mtwara wakati wa kuzindua kampeini hiyo ya Haachwi Mtu Nyuma kamilisha usajili wako, Mmwakilishi wa TCRA Kanda ya Mashariki Viollet Essoko amesema changamoto zilizopo zimekuwa zikifanyiwa kazi na kusisitiza kuwa licha ya kuwekwa matangazo ya kuhamasisha umma haachwi mtu nyuma kamilisha usajili bado kuna wananchi wanasua sua kufuatilia michakato ya NIDA ili kupata namba na kusajili line zao za simu.

Amesema idadi kubwa ya vijana wamekuwa wakipuuzia zoezi hilo huku watu wenye umri mkubwa wameonyesha kujitokeza kwa wingi kufuatilia vitambulisho vya nida lakini pia kusajili line zao za simu.

Wakati huo huo, baadhi ya wakazi wa mkoa wa mtwara ambao bado hawajapatiwa vitambulisho vya taifa vya NIDA wameiomba mamlaka hiyo kuongeza watendaji na vitendea kazi ili kurahisisha zoezi hilo ambalo kwa sasa limekuwa na muamko mkubwa kwa wakazi wake.

Wakazi hao wametoa ombi hilo kutokana na kukaa kwenye foleni ili kupata huduma hiyo kwa muda mrefu na hivyo kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo ipasavyo.

Hata hivyo wakazi hao wameiomba mamlaka hiyo kuongeza watendaji sambamba na vitendea kazi ili zoezi hilo liweze kwenda kwa haraka hasa kipindi hiki ambacho idadi ya watu imeongezeka.

Mapema akifungua zoezi hilo ambalo litadumu takribani wiki nzima katika wilaya zote za mkoa wa Mtwara Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evodi Mmanda amewataka wananchi kutopuuzia zoezi hilo ambalo umuhimu wake ni mkubwa.

Amesema huwezi kuitwa Mtanzania kama huna kitambulisho cha NIDA na kuwataka watambue kuwa huduma muhimu zitapatikana tu kwa mtu mwenye kitambulisho cha nida na hivyo kuwasihi kukamilisha zoezi la nida na kupata usajili wa laini zao za simu.

Zoezi la usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole linatarajiwa kukamilika disemba 31 mwaka huu.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA INNOCENT BASHUNGWA ATEMBELEA KIWANDA CHA MWATEX MWANZA

$
0
0
Mhe. Innocent Bashungwa Waziri wa Viwanda na Biashara akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoa Mwanza amekitembelea kwa mara ya pili kiwanda cha Mwatex (2001) LTD kilichobinafisiswa na Serikali kwa mwekezaji Amin Radhanin na chenye wafanyakazi 600.

Kwenye ziara ya kwanza ya tarehe 30/09/2019 alitoa maelekezo kwa kiwanda kuhusu kuandaa mpango mkakati wa biashara wa kuendesha kiwanda lakini mpaka sasa huo mpango mkakati haujafika wizarani.

Waziri baada ya kufika kiwandani hapo aliomba uongozi na menejiment nzima kutoka nje na mkutano ili kusikiliza kero na changamoto pia na maoni yao yatakayofanya kiwanda hicho kinafanye kazi kwa asilimia 100. 

Amabapo kwa sasa kinafanya kazi asilimia 60 tofauti na matalajio ya serikali ya kiwanda kufanya kazi kwa asilimia 100 Waziri baada ya kusikiliza maona na kero za wafanyakazi ameagiza wizara kuunda kamati maalum ambayo itafika kiwandani kufanya uchambuzi wa uendeshaji wa kiwanda kwa kushirikiana na msimazi anaekiendesha kiwanda hicho na amewapa muda mpaka 01/01/2020 kamati hiyo iwe imeshamfikishia ripoti ya uchambuzi wa mwenendo wa kiwanda cha Mwatex Ripoti hiyo itaisaidia serikali kupata mwelekeo wa nini kifanyike ili kupata Mwatex iliyokuwepo enzi za Mwalimu Nyerere.

Pia Waziri amesisitiza kuwa mkakati wa serikali ni kuona viwanda vyote vinafufuliwa na vinafanya kazi ili serikali iweze kutengeneza mnyororo wa thamani ya mazao yote hapa nchini.

SAMPULI 5106 ZIMEFANYIWA UCHUNGUZI NA MAABARA YA MKEMIA KANDA YA KATI

$
0
0
Na.Catherine Sungura.Dodoma.

Jumla ya sampuli 5106 zimefanyiwa uchunguzi katika maabara zikiwemo za masuala ya kijamii na kijinai katika mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali kanda ya kati.

Hayo yamesemwa na Meneja wa mamlaka hiyo kanda ya kati Musa Kuzumila wakati wa ziara ya maofisa habari wa wizara ya afya na taasisi zake wakati wa kutembelea mamlaka hiyo kujionea mafanikio yaliyofanywa katika kuboresha sekta ya afya nchini.

Kazumila amesema kwamba tangu kuanzishwa kwa kanda hiyo miaka miwili na nusu sasa ,kanda yake imefanikiwa kupima sampuli hizo ambazo zimefanyiwa uchunguzi katika maabara na kuzitolea ushahidi mahakamani

"Mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu inasimamia sheria na kudhibiti kemikali hivyo tumeweza kufanyia uchunguzi sampuli na hivyo kupunguzia wateja umbali na hivyo kusaidia wananchi kupata haki na kutoa ushahidi kwa wakati".Amesema Kazumila.

Kwa upande wa vinasaba Kazumila amesema kati ya sampuli walizopokea jumla ya sampuli 36 zilizowasilishwa asilimia 90 zilikua zinaangalia uhalali wa baba wa mtoto.

Hata hivyo amesema kwamba mamlaka hiyo imeweza kukagua maeneo yanayojihusisha na kemikali zipatazo 360 pamoj na kutoa vibali 139 za kuingiza na kusafirisha kemikali nchini kwa kanda ya kati.

Kwa upande wa wajasiriamali wadogo wadogo mamlaka hiyo imewapatia mafunzo wajasiriamali 315 namna ya matumizi salama ya kemikali pamoja na kutoa elimu kwa wachenjuaji wa dhahabu wanaotumia kemikali aina ya sodium cyanide.

Mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali kanda ya kati inahudumia mikoa ya morogoro,iringa,dodoma,singida na tabora na ilianzishwa mwaka 2017.
Meneja wa kanda ya kati ya mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali Musa Kazumila wakati akiongea na maofisa habari wa wizara na taasisi zake 

WANANCHI WANAOTUMIA BANDARI YA MAGARINI WILAYANI MULEBA WAIPONGEZA SERIKALI KWA KUAMUA KUBORESHA MIUNDOMBINU

$
0
0
 Baadhi ya abiria wakipakia mizigo katika boti za abiria katika Bandari ya Magarini wilayani Muleba mkoani Kagera.Bandari hiyo imeboreshwa kwa kujengwa kwa miundombinu yake ikiwemo majengo ya ofisi, vyoo na gati kwa ajili ya meli na boti kuegesha bandarini hapo.

 Baadhi ya abiria wakiingia ndani ya boti ya abiria kabla ya kuanza kwa safari kutoka Bandari ya Magarini kuelekea katika visiwa vingine vilivyomo katika Ziwa Victoria.

 Abiria wakiwa wamekaa ndani ya boti kwa ajili ya kuanza safari katika bandari ya Magarini.

 Mmoja wa wakazi wa Muleba akiwa katika bandari ya Magarini (aliyenyoosha vidole) akiwa amezungukwa na baadhi ya waandishi wa habari waliofika bandarini hapo kuangalia uboreshwaji wa miundombinu katka bandari hiyo.

 moja wa wananchi akielekea kupanda boti ya abiria katika bandari ya Magarini wilayani Muleba mkoani Kagera.
Boti ya abiria ikiwa imeegesha ikisubiri kuanza kupakia abiria katika Bandari ya Magarini wilayani Muleba mkoani Kagera.



Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Muleba


WANANCHI wa Wilaya ya Muleba mkoani Kagera na hasa wanaoutumia usafiri wa meli na boti za abiria kufanya safari zao mbalimbali katika Visiwa vilivyomo ndani ya Ziwa Victoria wameipongeza Serikali Kuu na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA) kwa hatua yake ya kuboresha miundombinu ya Bandari ya Magarini ambayo sasa imekamilika.


Wakizungumza na Michuzi Globu ya Jamii pamoja na Michuzi TV, wananchi hao wamesema kuwa hakika Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Magufuli kupitia TPA umeonesha namna ambavyo umedhamiria kuboresha maisha ya watu kwa kuhakikisha huduma muhimu zinapewa kipaumebele na kwamba wao miundombinu ya bandari katika Ziwa Victoria ni muhimu kwani ndio njia rahisi ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine.


Akizungumza leo kuhusu bandari ya Magarini, Mkazi wa eneo hilo Paul Stephen amesema kuwa wanathamini kazi inayofanywa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari katika kuboresha miundombinu ya bandari hiyo ambayo kabla ya uboreshwaji wa miundombinu wananchi walikuwa wanapata huduma ya usafiri wa boti za abiria katika mazingira magumu.


"Tunatoa shukrani kwa Serikali pamoja na Mamlaka ya Bandari kwa hatua hii iliyochukua ya kuboresha majengo , gati na ofisi za Bandari ya Magarini ambayo kwetu ni muhimu katika shughuli za kiuchumi.Tunaitegemea sana kwani ndio ambayo tunaitumia tunapotaka kufanya safari zetu za kila siku.Kwa uboreshaji wa miundombinu ambao umefanyika, tutaona manufaa yake na itakuwa chachu ya maendeleo kwetu,"amesema Stephen.


Wakazi wengine wa eneo hilo wametoa ombi kuhusu kuangaliwa upya kwa ushuru ambapo walisema wanalipa Sh.600 wakati katika maeneo mengine bei ya ushuru kwa kila abiria ni Sh.200 au Sh.400.Hivyo ni matarajio yao Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari itasikia kilio chao kwa kushusha gharama za ushuru.


Hata hivyo Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari katika Bandari za Ziwa Victoria Morric Mchindiuza amesema kuwa amesikia maombi ya wananchi hao kuhusu bei ya ushuru.Amesema kuwa katika bandari zote nchini gharama ya ushuru kwa kila abiria ni Sh.600 na kinachotokea kuna bandari bubu ambazo zenyewe zinatoza bei ya Sh.200 hadi Sh.400.


"Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania, tunao utaratibu ambao unatambulika kisheria kuhusu ushuru na tozo nyingine.Hili la ushuru wa abiria bandari zote nchini bei yake ni moja na hivyo kinachosemwa na wananchi ni ushauri ambao tumeuchukua na tutaufanyia kazi.Hata hivyo kama ambavyo tumekuwa tukielekeza kila siku bandari bubu zinakwenda mwishoni , hivyo bei ya ushuru itabaki ile inayotambuliwa na TPA,"amesema Mchindiuza wakati anafafanua kuhusu gharama za ushuru bandarini.


Kuhusu bandari hiyo ya Magarini amesema kuwa kwa sasa ujenzi wa miundombinu umekamilika kwa asilimia kubwa na kilichobaki ni kuanza kutumika rasmi kwa majengo ya bandari hizo ingawa kwa upande wa gati imeanza kutumika.


"Tumejipanga kuhakikisha tunaboresha miundombinu ya bandari zetu za Ziwa Victoria na ndio maana kila mahali ambapo tunakwenda utakuta aidha ujenzi umekamilika au unaendelea na mkakati wetu ni kuhakikisha usafiri wa meli unakuwa wa uhakika ili wananchi sasa waweze kusafiri kutoka eneo moja kwenda jingine,"amesema Meneja huyo.



KITABU CHA MTOTO WA MIAKA 8 “BIBLIA YANGU” CHA ZINDULIWA KWENYE FURSA YA DAR

$
0
0
Mtoto Samwel Michael Gimeno (miaka 8) akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu chake 

MAMA Mzazi wa Samweli Suzana Senso akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Mkurungezi wa Fursa Bi Suma Mwaitenda kulia akimkabidhi kitabu hicho Samweli mara baada ya kufanya uzinduzi
MAMA Mzazi wa Samweli Suzana Senso kushoto akimpatia nakala ya kitabu kilichoandikiwa na Mwanae Mtangazaji wa Kipindi cha Njia Panda cha Clouds FM Radio Dkt Isaac Maro wakati wa uzinduzi huo 
Mtoto Samwel Michael Gimeno (miaka 8) akiwa kwenye picha ya pamoja na familia yake na mdogo wake Alan Michael Gimeno 

Mtoto Samwel Michael Gimeno (miaka 8) katikati akiwa kwenye picha mara baada ya uzinduzi wa kitabu chake

Jumamosi tarehe 7/12/2019 ilikuwa siku ya pekee wa mtoto Samwel Michael Gimeno (miaka 8) ambae alibahatika kuzindua kitabu chake cha kwanza ndani ya fursa ya Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Julius Nyerere International Conference Center 

Kitabu cha BIBLIA YANGU kilizinduliwa na Mkurungezi wa Fursa Bi Suma Mwaitenda 

Samwel amekuwa mtoto wa pekee kwenye familia ambae Mungu Ameweka kipaji cha kuandika na kuchora na Sisi kama wazazi wake tumeamua kumsaidia ili kuiishi ndoto yake maneno hayo yamesema na mama mzazi wa Bi Suzana Senso

Kitabu cha kwanza cha Samwel kitakwenda Kuwa kinatolewa kwa watoto Yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu ikiwa sehemu ya samwel kurudisha kwa watoto wezake wanaoishi kwenye mazingira magumu ambao ni mara chache sana kupata kitabu kinzuri na chenye hadithi za kwenye Biblia kutokana na mazingira wanayoishi maneno hayo yamesemwa na baba wa Samwel Bw Michael Samwel Gimeno 

KAMPENI KALAMU YANGU
Ni maneno yatakayo kwenda kutumika kwenye kampeni samwel ambayo itakuwa nikutembelee vituo vya watoto yatima na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na kuwagawia vitabu ili nao waweze kusoma sio tu kusoma kitabu tu ila pia kusoma kitabu kilichoandikwa na mtoto mwezao 

Kampuni hii inaanza mwezi huu wa 12 hadi siku ya wapendanao tarehe 14/2/2020 ambapo samwel atakwenda kula na watoto wanaoishi kwenye kituo cha watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu ambacho tutakitaja siku zijazo na pia kuwagaia vitabu ya BIBLIA YANGU 

Gharama ya kitabu itakuwa shilingi elfu 20,000 kuanzia 15/2/2020 baada ya kampuni ya KARAMU YANGU ukisha tarehe 14/2/2020

Mama Samwel alisema Kwa sasa tunatamani kupata watu wa ku support kutoa nakala ya vitabu ambavyo tunatajia kuvigawa kwenye vituo vya watoto yatima Kwani hii kampeni haina mfadhili wa kufanya Ila ni wazazi tu ndio tunaifanya na tunatamani kuwafikia watoto wengi sana 
Kwa yeyote atakae wiwa kuungana nasi kwenye Hii kampuni anaweza ku wasiliana Kupitia namba 0736 372138 

Tukiwa kama wazazi wa Samwel tunapenda kuwashukuru Joel Kiiya ambae ni mentor wa Samwel, Bi Ezabel Simuyu ambae ndie ame design kitabu, photography wake Muki, Emanuel, Mkurungezi wa Fursa na wale waliotumia muda wao kufanikisha kitabu cha “BIBLIA YANGU” hadi kutoka.


MUNGU AWABARIKI

Airtel yazindua kampeni ya LIPA ADA kwa kutumia Airtel Money

$
0
0
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza na kuzindua kampeni maalum ambayo inayojulikana kama LIPA ADA kwa Airtel Money itakayotoa  suluhisho kwa  wateja wake kuweza kufanya malipo yoyote ya karo za shule ambapo kwa sasa wateja wataweza kulipa karo kwa kutumia akaunti zao za Airtel Money wakiwa popote katika  kipindi hiki cha msimu wa sikukuu na kuendelea.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Airtel Money Isack Nchunda alisema kuwa LIPA ADA kwa kutumia Airtel Money itakuwa ni suluhisho kwa wazazi wengi ambao wamekuwa wakipoteza muda mwingi wa kwenda kupanga foleni benki ili kulipia watoto wao karo na vile vile itaendela kutoa hamasa kwa wateja wa Airtel kuendelea kutumia Airtel Money kulipia malipo mbali mbali ya bidhaa na huduma.
‘Kama mnavyojua, hiki ni kipindi cha wazazi na familia kuwa katika mapumziko, lakini pia muda huu wazazi huutumia kulipia karo za shule za watoto wao. Natoa wito kwa Watanzania kuendelea kutumia Airtel Money kwa malipo yao kwani ni njia rahisi, haraka na nafuu kwa malipo wakiwa popote wanaweza kulipa sio lazima kwenda bank na kupanga foleni, Nchunda alisema.
Nchunda alisema kuwa Airtel imeamua kuja na kampeni ya LIPA ADA kwa Airtel Money kama njia mojawapo ya kutoa suluhisho ya kifedha kwa Watanzania. ‘Kama mnavyojua, kulingana na utafiti wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wa hivi karibuni kuonyesha kuwa zaidi ya Watanzania milioni 22.9 wanatumia huduma za kifedha kwa kutumia simu zao huku miamala yenye dhamani ya zaidi ya Trilioni 8 ikifanyika mpaka kufikia Juni 2019. Kwa miaka ya hivi karibuni, huduma za kifedha kwa simu za mkononi imebadilika kutoka huduma ya kawaida kama vile kununua muda wa maongezi mpaka kuwa moja ya huduma muhimu inayowezesha ukuaji sekta na  mzunguko wa fedha kila mahali.
Jinsi ya kulipia Ada Kwa Airtel Money:
  • Piga *150*60# Ili kufikia Kwenye Menyu ya Airtel Money
  • Chagua 5: Lipia Bili
  • Chagua 4: Weka namba ya kampuni (Namba ya Malipo ya Shule)
  • Ingiza Kiasi cha pesa
  • Ingiza Namba ya Kumbukumbu (Jina la mwanafunzi na Kidato / Namba ya kitambulisho cha mwanafunzi )
  • Ingiza Namba ya siri
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema kuwa Airtel inajivunia kuwa kampuni ya simu za mkononi ambayo sasa inakuza kwa kasi mtandao wa huduma za kifedha hapa nchini.
“Airtel tumejipanga na kujikita katika mipango yetu ya kuendelea kupanua wingo wa huduma zetu, Airtel kwa sasa tuna maduka ya Airtel Money branches Zaidi ya 1000 nchi nzima ikiwa ni moaja kati ya mpango yetu ya kuleta suluhisho za kifedha pamoja na kusambaza huduma na bidhaa zetu karibu na wateja. Dhamira yetu ni kuendelea kujenga mtandao imara na unaotegemewa’. Alisema Singano huku akiongeza kuwa huduma na bidhaa za Airtel kama vile kurundisha muamala uliokosewa, kubadilisha PIN, kusajili laini za simu kwa kutumia alama ya vidole zinapatikana kwenye maduka yote ya Airtel Money branches.
 Mkurugenzi wa Airtel Money, Isack Nchunda  akizungumza wakati wa kuzindua kampeni maalum inayojulikana kama LIPA ADA kwa Airtel Money itakayotoa suluhisho  kwa wateja wa Airtel Money kuweza kufanya malipo yoyote ya karo za shule  kwa kutumia akaunti zao za Aitel Money wakiwa popote katika kipindi hiki cha msimu wa Sikukuu na kuendelea Kushoto ni Meneja wa Airtel Jackson Mmbando

 
Meneja wa Airtel Jackson Mmbando akifafanua jambo wakati wa kuzindua kampeni maalum inayojulikana kama LIPA ADA kwa Airtel Money itakayowawezesha  kwa wateja Airtel kuweza kufanya malipo yoyote ya karo za shule kupitia akaunti zao za Aitel Money wakiwa popote wakati msimu huu wa Sikukuu na kuendelea, hafla ya uzinduzi ilifanyika ofisi kuu ya Airtel  jijini Dar es Salaam jana.Katikati ni Mkurugenzi wa Airtel Money, Isack Nchunda na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha lipa Ada kwa Airtel Money. Emmanuel Mwaisoloka
 

SHANGWE ZATAWALA ZANZIBAR MSHINDI WA TIGO CHEMSHA BONGO APOKEA GARI YAKE RASMI NYUMBANI KWAKE

$
0
0
Msheheshaji  akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Bwana Hassan Khatib Hassan katika halfa ya kumkabidhi zawadi ya gari mshindi wa TIGO Chemsha Bongo #MshindiTigoChemshaBongo

Tunashukuru jinsi kampuni ya mawasiliano ya TIGO inavyoleta hamasa kwa vijana kupitia miradi mbalimbali ya kuwainua. Leo tunakabidhi gari kwa mshindi wa TIGO Chemsha Bongo toka Zanzibar Bw. Shaban Hamis” 
Mh. Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Khatib Hassan
#MshindiTigoChemshaBongo

“Tunampongeza mshindi wa Tigo Chemsha Bongo Bw. Shaban Hamis aliejishindia gari aina Renault Kwid kutoka Tigo kampuni ambayo tunashirikiana nayo kwenye mambo mengi ya kimaendeleo”
Aljazeera - Mwakilishi wa Jimbo Raha Leo #MshindiTigoChemshaBongo

PICHA ADIMU ya mshindi wa TIGO Chemsha Bongo Bw. Shaban Khamis akiwa na “mke mdogo” katika gari yake mpya aina ya Renault KWID yenye thamani ya Tsh 23,000,000 (Zero Km)‬
#MshindiTigoChemshaBongo 

Mh. Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Khatib Hassan akikabidhi nyaraka za usajili wa gari aina ya Renault KWID yenye 0 Km (yenye thamani ya 23,000,000) kwa mshindi wa TIGO Chemsha Bongo Bw. Shaban Khamis akiwa na “mke mdogo” wake. 
#MshindiTigoChemshaBongo

NJOO KWEREKWE USHUHUDIE sasa hivi gari la mshindi wa TIGO Chemsha Bongo akiwepo na Mshindi mwenyewe Bw. Shaban Khamis #MshindiTigoChemshaBongo



GARI IMEFIKA salama nyumbani kwa Bw. Shabani Khamis wakapata na picha ya ukumbusho na familia. Tukumbuke hii ni Renault Kwid yenye thamani ya Tsh 23,000,000 (Zero Km)

#MshindiTigoChemshaBongo

Wadau wakutana kujadili namna ya kutatua changamoto za watoto na vijana mijini

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk John Jingu akitoa hotuba ya ufunguzi wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa  TULab kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Dr. Lorah Madete akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Mipango wakati wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho wakati wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Sera ya Jamii kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF) nchini, Dr. Paul Quarles Van Ufford akitoa salamu za UNICEF wakati wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mtathimini kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF) nchini, Mr. Hong Vu akiendesha chemsha bongo wakati wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau kutoka taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi wakifurahia jambo wakati wa chemsha bongo kwenye kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk Tausi Kida, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk John Jingu, Mwenyekiti wa  TULab kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Dr. Lorah Madete pamoja na Mkuu wa Sera ya Jamii kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF) nchini, Dr. Paul Quarles Van Ufford wakati wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk Tausi Kida (katikati) akitoa maelezo mafupi kuhusu ESRF kwa mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk John Jingu (wa pili kulia) alipofika ofisini kwa mkurugenzi huyo kusaini kitabu cha wageni wakati wa kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene(wa kwanza kushoto), Mkuu wa Sera ya Jamii kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF) nchini, Dr. Paul Quarles Van Ufford (wa pili kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa  TULab kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Dr. Lorah Madete (wa kwanza kulia).
Baadhi ya wadau kutoka Serikalini, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Asasi za Kiraia, Taasisi za Elimu, Wahisani wa Maendeleo na Sekta binafsi walioshiriki kongamano la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wakishiriki kuchangia maoni wakati wa kongamano la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk John Jingu akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau kutoka Serikalini, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Asasi za Kiraia, Taasisi za Elimu, Wahisani wa Maendeleo na Sekta binafsi walioshiriki kongamano la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana la kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji lililoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF jijini Dar es Salaam.
 
Na Mwandishi Wetu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk John Jingu amewataka watafiti wa programu ya Utafiti itakayoangalia huduma na ubunifu kwa watoto na vijana katika miji nchini Tanzania kutoa suluhisho la kudumu kuhusu mahitaji na usalama wa watoto na vijana ili kuwa na taifa lenye watoto wenye kujitambua.
 
Alisema ingawa anatambua kwamba tafiti zikifika mwisho wataitwa kuelezwa matokeo lakini kutokana na haja ya kutafuta suluhu ya changamoto zilizopo kwa sasa ni vyema watafiti wakapata muda wa kueleza maendeleo ya tafiti zao na hasa matokeo ya awali kabla ya kufika mwisho.
 
Alisema hayo katika kongamano la wadau la kujadili programu ya utafiti kuhusu vijana lililofanyika juzi kujadili namna bora ya kutatua changamoto zinazowakumba watoto na vijana katika miji. Programu hiyo inaandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Fedha na Mipango chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab).
 
Kongamano hilo lilihudhuriwa na wadau takribani 40 kutoka Serikalini, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Asasi za Kiraia, Taasisi za Elimu, Wahisani wa Maendeleo na Sekta binafsi.
Alisema hali hiyo itasaidia Serikali kuchukua hatua mapema zaidi za kukabiliana na changamoto za watoto na hasa suala la malezi.
 
Alisema kwa sasa kumekuwa na changamoto nyingi za malezi na hivyo kusababisha uwapo wa watoto wengi kwenye mazingira magumu na pia mitaani.
 
Alisema utafiti unaokusudiwa ni utafiti wenye maana kubwa kwa kuwa unaangalia mazingira ya leo kwa manufaa ya taifa la kesho na kuondoa viashiria vya hatari katika malezi na hatima ya watoto wa Tanzania hasa wale wanaoishi mijini.
 
Alisema watoto na vijana wanaoishi mijini wanakabiliwa na changamoto nyingi na ni wajibu wa jamii kuhakikisha kwamba changamoto hizo zinaondolewa kwa kuwepo kwa mbinu bora za kukabiliana na changamoto hizo, mbinu zenye manufaa na zinazowezekana.
 
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk Tausi Kida, akifafanua zaidi kuhusu warsha na programu ya tafiti inayoandaliwa na ESRF kwa kushirikiana na UNICEF alisema wanatengeneza programu hiyo kwa ajili ya kutanzua shida zinazowapata watoto na vijana wanaoishi katika miji.
 
Alisema warsha hiyo iliyojumuisha watafiti na wadau kadha wa masuala ya utafiti imelenga kukusanya maoni kutoka kwa wadau ili kuweza kutengeneza programu mpya inayogusa masuala ya watoto na vijana katika miji yetu.
 
Dk Tausi Kida, akifafanua zaidi kuhusu kongamano hilo, alisema kwamba utafiti huo utafanywa chini ya Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab) na kusema  mipango miji ni suala muhimu kwa nchi ya Tanzania hasa wakati huu inapoelekea katika uchumi wa viwanda.
 
Alisema wakati Tanzania inatarajia kuwa na watu milioni 45 wanaoishi katika miji ifikapo mwaka 2030, ikiwa ni nchi ya sita kwa kasi ya ongezeko la idadi ya watu Duniani ifikapo mwaka 2050 na hivyo ipo haja ya kuwa na sera madhubuti inayohusu ulinzi kwa watoto na vijana wanaoishi mijini.
 
Alisema kutokana na serikali kutilia umuhimu wa masuala ya ukuaji wa miji katika Mpango wa Pili Miaka 5 wa Maendeleo  2016/17 – 2020/21 (FYDP II) kulianzishwa  TULlab mwaka 2017 ambapo sekretarieti yake ni ESRF wakati mwenyekiti ni Wizara ya Fedha na Mipango.
 
Kazi ya TULab ni kuisaidia serikali  katika masuala ya ukuaji wa miji Tanzania. Kwa kuzingatia  tayari TULab imefanya tafiti na kuandaa Mpango Kazi kuelekea Maendeleo ya Miji.

Ubingwa wa Liverpool, Ubabe wa Van Djik na Falsafa ya Pedigree

$
0
0

Charles James, Michuzi TV

MMOJA wa abiria waliokua wakishuka kwenye ndege katika uwanja wa kimataifa wa John Lennon, Merseyside January 1, 2018 alikua ni Virgil Van Djik.

Beki huyu wa Southampton alikua akielekea kukamilisha usajili wake wa kujiunga na wababe Liverpool katika uhamisho ambao ulivunja rekodi ya mauzo kwa Klabu zote mbili.

Ni usajili ambao pia ulimfanya Van Djik kuwa beki ghali duniani na kuingia katika rekodi za Dunia.

Aliwindwa na Barcelona, Manchester zote mbili na Chelsea. Yeye mwenyewe alipaona Liverpool kama sehemu bora zaidi kwa kipaji chake na familia yake.

Siku nne tu baada ya kutambulishwa na kukabidhiwa jezi ya dhahabu no4 alicheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Everton na kufunga goli la pili na la ushindi.

Toka hapo, Virgil amekua bora kwetu, ametushika sisi mashabiki, benchi la ufundi mpaka wachezaji wenzake. 

Na Sasa anatajwa kama mchezaji bora kwenye Ligi Kuu ya England huku akiwekwa katika daraja la juu la mabeki bora duniani.

Amechukua tuzo ya Mchezaji bora wa Ulaya lakini pia akishika nafasi ya pili nyuma ya Lionel Messi kwenye tuzo ya mchezaji bora wa Dunia.

Sikudhani kama kuna siku mtu mmoja angekuja kumaliza tatizo letu la ulinzi.

Nilifahamu fika ubora wa Van Djik lakini bado hakunifanya niamini ya kwamba tatizo sugu la ulinzi tulilokua nalo litakwisha baada ya ujio wake.

Wengi walibeza ubora wake, wengine wakaponda kiwango cha fedha tulicholipa kumnasa. 

Hivi unawezaje kumsajili kwa Pauni Milioni 75 beki asiye na rekodi ya mataji tena anaecheza timu kama Soton? Tulitukanwa sana na wapinzani.

Mkurugenzi wa ufundi, Michael Edward na Jurgen Klopp ndio waliojua jinsi gani Van ni hodari linapokuja suala la ulinzi.

Mwanzoni msimu ulivyokua ukianza alikua akipangwa na Joe Gomez. Gomez aliekua akionekana dhaifu akabadilika na kuwa jemedari hodari wa vita.

Wengine wakamuita Joe kuwa ni John Terry mpya.. Akachukua hadi namba timu ya Taifa. Tu kwa sababu anacheza pacha na Van.

Dejan Lovren haonekani akifanya makosa siku hizi kwa sababu anacheza na Le Commandment Field Marshall.

Joel Matip takwimu zake za ubora ziliongezeka baada ya kuanza kupangwa kama pacha wa Van baada ya Dejan na Joe kuumia.

Wote hawa wamebadilika kwa sababu ya mtu mmoja. Mabeki wa pembeni Andy Robertson na Anord Trent huwaambii kitu kuhusu mbabe huyu wa kati.

Amewafanya kujiamini sana. Kama hujui Robertson na Trent Anord waliweka rekodi ya kuwa mabeki wanaotoa assist nyingi barani Ulaya msimu uliopita.

Ubabe wa Van Djik umemfanya kila mmoja ndani yetu ajiamini..Golini Allison Becker hana presha, mabeki na viungo wote wanajua nyuma kuna kamanda yupo.

Hata akina Salah na Mane wakifunga sasa wana uhakika magoli hayarudi maana kamanda yupo.

Unataka kuujua Ubabe wa Van Djik? Kawaulize Spurs watakusimulia vizuri.

Msimu uliopita game ya Liverpool ugenini White Hart Lane, Spurs walifanya shambulizi la kushtukiza dakika ya 84 langoni mwa Liverpool, Heung Son na Sissoko walikua wakija kwa kasi wakiwa wamebaki na Van Djik. 

Yaani wawili dhidi ya mmoja na bado wakashindwa kufunga. Huyu jamaa anakaba watu wawili peke yake.

Kumbuka chini yake msimu uliopita Liverpool walifungwa mchezo mmoja huku wakiwa timu iliyoruhusu magoli machache kwenye Ligi na kipa wao Allison Becker akiongoza kwa cleensheet akiwa nazo 20.

Msimu huu mpaka sasa Liverpool ipo kileleni mwa Ligi ikiwa haijafungwa mchezo hata mmoja.

Ndio namba nne wetu, mtazameni akikaba tunamtazama akifunga, anapiga pasi na anaongoza wenzake. Virgil Van Djik! Virgil Van Djik!

UBINGWA WA LIVERPOOL

Ebana huamini kama Liverpool ndio mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya England? Ugumu unakuja wapi mpaka ushindwe kuamini?

Ukitazama namna ambavyo tunacheza utaona kabisa timu inahitaji kitu. Mechi zilizobaki zinatubeba kulinganisha na Manchester City ambao tunachuana nao.

Tayari tumecheza michezo yote migumu kulinganisha na wapinzani wetu. Mpaka sasa tunapokaribia kumaliza mzunguko wa kwanza vigogo wote tumeshawamaliza.

Ukiangalia jinsi ambavyo tunapata ushindi utakubaliana na Mimi kwamba ubingwa ni wa kwetu.

Alex Ferguson alikua alisema ubingwa wa England unapatikana Machi na April..Akiwa na msemo wake wa Tricky Bum Time, lakini sidhani kama Klopp ataisubiri hiyo presha, mpaka kufikia mwishoni mwa Januari atakua ameshajua mbivu na mbichi.

Tazama namna tunavyopata matokeo katika njia ngumu. Niliwaambia Njia ya mafanikio ya Liverpool ni ngumu siku zote.

Hebu kumbukeni sare ya kibishi pale Old Trafford kwa United, ushindi dhidi ya Newcastle, Leceister, Spurs na hata Sheffield United utaona kabisa Liverpool ya msimu huu inacheza kibingwa sana.

FALSAFA YA PEDIGREE

Kuna kitu kinamea sana kwa sasa pale Anfield. Kinaitwa Pedigree. Klopp ni wazi ameamua kuacha alama isiyofutika kwetu.

Na kama akifanikiwa kubeba taji la Ligi kuu basi hapana shaka atajengewa mnara wenye sura yake nje ya dimba letu.

Oke. Pedigree ni nini? Hii ni ile hali ya kuwa na vitu vyenye muendelezo wa muda mrefu. Nitakupa mifano yake.

Ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Spurs msimu huu ni muendelezo wa ubabe wetu mbele yao hasa katika uwanja wa Anfield.

Ni lini umewahi kuiona Liverpool imara katika dimba lake la nyumbani kama hii ya Klopp? Jamaa hataki kabisa mchezo na ‘home’ anakubutua bila masihara.

Liverpool ilikua na tatizo la kushinda michezo mikubwa na kupoteza dhidi ya zile ‘timu ndogo’. 

Sasa toka tufungwe na Swansea msimu wa mwaka juzi hatujapoteza kwenye Ligi dhidi ya hizo mnazoziita timu ndogo. Hii nayo ni Pedigree. 

Hata ukiangalia msimu uliopita ni Leceister City na West Ham pekee ambao angalau wameambulia sare. Wengine wote tumebutua.

Pedigree nyingine ni hii ya kusajili wachezaji Kwa fedha nyingi. Ni wazi sisi ni miongoni mwa timu zinazoogopwa kwenye soko la usajili kwa sasa.

Tuliwapiku Man city na Chelsea kuinasa saini ya Van Djik, tukaigaraza Man United kwa Fabinho, tukaipiga bao tena Man City kwa Naby Keita.

Real Madrid waliangaika kumnasa Allison Becker lakini mwenyewe akachagua kuja kwetu. Hii Pedigree haikuwepo mwanzoni. 

Jurgen Klopp kayafanya maisha yawe mepesi kwetu sasa.

0683015145

Soko la ajira halikidhi Idadi ya Wahitimu Nchini-Naibu Katibu Wizara ya Fedha na Mipango

$
0
0

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

 Serikali imesema kuwa Soko la ajira rasmi  nchini ni dogo sana na  hivyo halikidhi mahitaji ya wahudumu wote kwa hali hiyo wahitimu hao wanatakiwa kukabiliana na changamoto ya Soko hilo kwa kuelekeza mawazo yao kwenye kujiajiri badala ya kuajiriwa.

Hayo ameyasema Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara ya Fedha na Mipango  Amina Shaban wakati akimwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango katika mahafali ya 17 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Kampasi ya Dar es Salaam na Mtwara yaliyofanyika katika Viwanja vya Kampasi jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa kwa wale wahitimu wenye ajira msingi mkuu wa mafanikio ni kufanya kazi kwa kuzingatia sera,Sheria,Taratibu na Kanunu ikiwa ni pamoja na kujiepusha na vishawishi au vitendo vya rushwa na ubadhirifu kwa kuwa vina madhara makubwa ya maisha ya mtu Mmoja moja na uchumi wa Taifa letu kwa ujumla.

Shaban amesema elimu inayotolewa na TIA imejikita kwenye fani za Uhasibu ikiwemo Uhasibu wa Fedha za Umma, Ununuzi na Ugavi,Usimamizi  wa Biashara, Uongozi wa Rasilmali Watu pamoja na Masoko  hivyo fani hiyo ni nguzo muhimu katika kuendesha Uchumi wa Taifa hususani katika kusimamia mapato na matumizi ya Fedha za Umma.

Naibu Katibu Mkuu huyo amesema sera yetu kwa sasa ni uchumi wa viwanda hivyo umahiri wa  wataalam wanaozalishwa  unatakiwa kuonekana ili kufanikisha azima ya serikali ya Tanzania ya Viwanda.

Shaban amekazia katika kukabiliana na changamoto za Usimamizi wa Mapato na matumizi ya Fedha za Umma,mahitaji ya Soko ,Ushindani na Utandawazi hamna budi Taasisi ya Uhasibu nchini (TIA) Kuendesha Shughuli  kwa kutumia Teknolojia ya Kisasa ya kupeana na kubadilishana taarifa kwani watalaam wanaohitajika ni wenye weledi,maarifa na umahiri wa kutatua za changamoto na si kuongeza changamoto kwa Wananchi katika kupata huduma.

Amesema kuwa TIA izingatie  umakini wa suala la umahiri katika mitaala ili kuweza kuwa na wataalam wenye uwezo wa kulifikisha Taifa kwenye uchumi wa Kipato cha kati kabla ya 2025.
Mwenyikiti wa Bodi ya Wizara ya Fedha na Mipango Wakili Said Chiguma amesema kuwa waajiri wa sekta ya Umma na binafsi wamekuwa wakiona mafanikio kwa wahitimu wa TIA kuwa na sifa zilizotukuka katika kufanya kazi licha ya kuwapo kwa Vyuo vingi nchini na kufanya Chuo hicho kuendelea kuongeza idadi ya udahili kwa wanafunzi kusoma kwa  kila mwaka.
Amesema Taasisi ina wanafunzi zaidi ya  19,000 katika Kampasi Sita za Kimkakati.

Nae Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Luciana Hembe amesema kuwa wahitimu katika Chuo hicho wameweza kjfundishwa ujasiriamali ili kuweza kujiajiri katika kukabiliana na changamoto ya ajira nchini.
Amesema Chuo kumekuwa na mikakati mbalimbali ya kuhakiksha wahitimu wanajiajiri katika maeneo Mbalimbali ya kuweza kukidhi mahitaji yao pamoja Taifa kunufaika na maarifa yao ya kujiajiri.

Aidha amesema kuwa Baadhi wahitimu katika Taasisi hiyo wa miaka iliyopita wameweza kuanzisha Kampuni mbalimbali ambazo ziko katika Ushindani wa kibiashara na Kampuni zingine.
Amesema wahitimu wa mwaka 2019 nao watumie ujuzi na maarifa yao katika kufungua milango ya ajira ya kujiajiri ili wasitumie muda mwingi wa kusubiri ajira katika sekta ya Umma na binafsi.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Amina Shaban akizungumza katika Mahafali ya 17 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliyofanyika katika Kampasi Dar es Salaam.
 Picha ya Pamoja na baadhi Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA).
 Baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakifatilia Hutuba ya Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 17 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika Viwanja vya Kampasi Kuu ya Jijini Dar es Salaam.
 baadhi ya Wahitimu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika mahafali ya 17 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika Viwanja vya Taasisi jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe wa Bodi ya Ushauri wa Wizara ya Fedha na Mipango Thabit Dokodoko akitoa shukurani kwa Mgeni Rasmi katika mahafali ya 17 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliyofanyika Viwanja Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Amina Shaban akiwa katika picha ya pamoja na Meza Kuu mara baada ya kuhitimisha mahafali ya 17 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliofanyika katika Kampasi Kuu ya Dar es Salaam.
 Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Luciana Hembe akitoa akizungumza na waandishi habari mara baada ya kuhitimishawa kwa Mahafali ya 17 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyikiti wa Bodi ya Ushauri wa Wizara ya Fedha na Mipango Wakili Said Chiguma akitoa maelezo kuhusiana na uendeshaji wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) katika Mahafali ya 17 yaliyofanyika katika Viwanja vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

TANAPA WAZINDUA KAMPENI IJULIKANAYO KWA JINA LA TALII NA TANAPA

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha 

Shirika la Hifadhi za Taifa{TANAPA} limezindua kampeni maalumu ijulikanyo kwe jina la ‘’Talii na TANAPA msimu huu wa sikukuu ya X mass na Mwaka mpya’’ kwa kushirikisha wasanii maarufu,warembo ,watangazaji maarufu na watu maarufu lengo ni kutaka kuhamashisha watanzania kutembele hifadhi za Taifa badala ya kwenda kutalii nje ya nchi katika kipindi hicho.

Hayo yalisemwa na Kaimu Kamishina wa Uhifadhi wa TANAPA,Witness Shoo mbele ya waandishi wa habari kwa kushirikisha viongozi mbalimba wa uhifadhi,wasanii na watangazaji tukio lililofanyika katika Makao Makuu ya Shirika hilo Jijini Arusha..

Shoo alisema kuwa lengo la TANAPA ni kutaka kila mtanzania kuwa mzalendo na nchini yake kwa kutembelea vivutio vilivyokuwa katika hifadhi 22 hapa nchini kwa kuvitembelea na kuwa balozi wakubwa wa kuvitangaza.

Alisema kundi la kwanza la wasani,watangazaji na watu maarufu litaanza kufanya kampeni hiyo desemba 20 mwaka huu katika hifadhi sita ikiwemo Ruaha,Katavi,Mkomazi,Rubondo,Mikumi na hifadhi ya Gombe iliyopo Mkoani Kigoma.

Kamishina huyo alisema katika Hifadhi ya Ruaha msanii Idrisa Sultan atakwenda kutalii katika mbuga hiyo na kuitangaza ndani na nje ya nchi katika mitandao ya kijamii kwani anawafuasi wengi katika mitandao ya kijamii hivyo anawajibu wa kutoa ujumbe kwa watanzania kuacha kukimbilia nje ya nchi kutalii badala yake watembelee hifadhi Taifa.

Alisema msanii Mrisho Mpoto atakuwa katika Hifadhi ya Katavi,mrembo wa mwaka Nancy Sumary atakuwa katika hifadhi ya Mkomazi,mtangazaji kijana aliyejipatia umaarufu hapa nchini,Milard Ayo na Miss wa mwaka 2018 Elizaberth Makune watakuwa na jukumu la kuwakumbusha watanzania kutembelea hifadhi ya Robondo.

Wengine ni pamoja na wasanii wa muziki wa Bongo flava Lulu Abas maarufu kwa jina la Lulu Diva atakuwa katika Hifadhi ya Mikumi na msani aliyetambulika kwa jina moja la Rubby atakuwa katika hifadhi ya Gombe.

Naye Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete alisema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kuwataka watanzania kuwa na tabia ya kutembelea mbuga za wanyama katika vipindi vyote vya sikukuu ya X Mass na Mwaka mpya na sikukuu nyingine kwa kutumia kiasi kidogo cha fedha na pia kuvitangaza vivutio hivyo kwa faida ya nchi.

Shelutete alisema kuwa wasanii wa fani mbalimbali,watu maarufu na watangazaji watashirikishwa katika kampeni hiyo iliyolenga kumtaka mtanzania kupenda cha nchi yake na kuacha kujali vya nje .

Naye Msanii Idrisa Sultan alisema kuwa katika maisha yake hajawahi kufika katika hifadhi ya Ruaha hivyo kwa fursa aliyopewa atahakikisha anaitangaza hifadhi hiyo kwa kadri awezavyo lengo ni kutaka watanzania kuwa wazalendo na kupenda cha kwao na kuacha ulimbukeni wa kikumbilia nje ya nchi kama Dubai na kungine kwa kutumia mamilionin ya pesa bila ya sababu za msingi.
Kaimu Kamishina wa Uhifadhi wa TANAPA,Witness Shoo akizindua rasmi  kampeni ya Talii na TANAPA , ambayo mabalozi wake ni baadhi ya wasanii pamoja na watangazaji ndani ya ukumbi Wa ofisi za makao makuu ya shirika hilo.
Mabalozi  Wa kampeni hiyo ambao ni wasanii Wa muziki ,vichekesho na watangazaji pamoja na baadhi ya wafanyakazi Wa TANAPA wakiwa katika   picha ya pamoja

Tumeanzisha Vifurushi Ili Kuwafikia Watanzania Wengi Zaidi – Bi. Anne Makinda

$
0
0
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bi. Anne Makinda amesema kuwa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umejielekeza katika kumhudumia mtanzania wa kila aina kulingana na uwezo wake na sio kufanya biashara kama inavyoelezwa na baadhi ya watu.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na Vifurushi vya Bima ya Afya Bi. Makinda amesema kuwa NHIF kuanzisha vifurushi kwamba ni kufanya biashara si kweli bali ni kuhakikisha watanzania ambao nchi yao ipo huru na wana amani wapate pia amani ya huduma ya afya.

“Mfuko huu ulianzishwa na Serikali, sio mfuko wa kufanya biashara, tunachukua hela za wanachama, ili wakatibiwe , unalipa 192,000 kwa mwaka halafu unaenda hospitali mara nne mara tano kwa mwaka kwa gharama zaidi ya pesa uliyowekeza, lengo letu ni kumhudumia mtanzania”-Bi Anne Makinda.

“Ukitaka kwenda hospitali leo, kumuona daktari ni shughuli, hapo bado matibabu, sasa bima ya afya ni hela unayoweka ukiwa na uwezo, ukienda hospitalini utatibiwa kwa mamilioni hata usiowahi kuyatoa wewe, utatibiwa tu na hela yako ndogo uliyokata nayo wewe kwa mwaka mzima”-Alisema Bi. Anne Makinda

Aidha Bi. Anne  Makinda amewataka watanzania kujiunga na Bima ya Afya hasa baada Mfuko huo kuja na vifurushi vya bima ya afya vinavyotoa wigo kwa watu wengi kujiunga kulingana na uwezo wake ili kusaidia Katika huduma za matibabu ambazo zimezidi kuwa kubwa kwa sasa.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Chemba Bw. Simon Odunga ameupongeza mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuja na mpango wa vifurushi kwani umejumuisha makundi tofauti katika jamii na kuwawezesha kila mmoja kujipimia kwa uwezo wake na hivyo kuwa na uhakika wa huduma za afya.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Bw. Bernard Konga amesema katika wiki tatu tangu waanzishe mpango huu wa Vifurushi vya Bima ya Afya Idadi kubwa ya watanzania wamejitokeza kujiunga.

“Ndani ya wiki tat utu tangu tuzindue vifurushi hivi idadi ya watanzania wanaojiunga na mfuko imekuwa kubwa ambapo mpaka sasa tumeshaunga watanzania zaidi ya elfu ishirini na idadi hii imeendelea kuongezeka siku hadi siku”-Alisema Bw. Konga

Muwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Edward Mbanga amewataka watumishi wa NHIF kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kujiunga na vifurushi hivyo na kuachana na kelele zapembeni.

Wawakilishi wa Vyama via BodaBoda na Machinga wamepongeza mango huo na kuahidi kuhamasisha wanachama wao kujiunga na mango huo kwani ni mkombozi kwa afya ya watanzania wote
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bi. Anne Makinda akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya, leo Mkoani Dodoma
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Bw. Bernard Konga akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya leo Mkoani Dodoma, ambapo amesema katika wiki tatu tangu waanzishe mpango huu wa Vifurushi vya Bima ya Afya Idadi kubwa ya watanzania wamejitokeza kujiunga. 
Mkuu wa Wilaya ya Chemba Bw. Simon Odunga akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya, ambapo aliwasisitiza watanzania kujitokeza kujiunga na vifurushi hivyo
Muwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Edward Mbanga akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya, leo Mkoani Dodoma ambapo amewataka watumishi wa NHIF kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kujiunga na vifurushi hivyo na kuachana na kelele zapembeni.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bi. Anne Makinda akiwapatia kadi za Bima ya Afya baadhi ya wakazi wa Dodoma waliojiunga na vifurushi vya bima ya afya leo Mkoani Dodoma

Benki ya NBC yakutana na wateja wake kuwashukuru kwa mahusiano bora kwa mwaka 2019

$
0
0
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kulia), akifurahi pamoja na baadhi ya wateja wa benki hiyo katika hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Kutoka Kushoto ni Mkuu wa Kampuni  G4S Cash Solutions Tanzania, Hassan Nuru na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya G4S Secure Solutions Tanzania, Barry Hogg.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Fedha wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Abdallah Mwaduga katika hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Katikati ni Ofisa katika kitengo cha wateja binafsi wa NBC, Rehema Chonde.  
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto), akisalimia na Mkurugenzi wa Kampuni ya Enterprises Business Department, Tony Wu huku Ofisa Fedha Mkuu wa Kampuni ya Huawei Technologies Tanzania, Mao Jinbao akiangalia katika hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.

 Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya NBC, Dk. Kassim Hussein (kulia), akisalimiana na baadhi ya wateja waliohudhuria  hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.

 Mkurugenzi wa Wateja wa Makampuni wa Benki ya NBC, Linley Kapya (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Fedha wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Abdallah Mwaduga katika hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Katikati ni Ofisa katika kitengo cha wateja binafsi wa NBC, Rehema Chonde.

 Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NBC, Dk. Kassim Hussein (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Anga Tanzania, Hamza Johari, huku Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe (katikati), akiangalia,  katika hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.            
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya NBC, Elvis ndunguru (katikati), akizungumza jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Theobald Sabi (kushoto), huku Mwenyekiti wa Kampuni ya Chelsea Starway Group, Martin Mbwana akisikiliza, katika hafla waliyowaandalia wateja wao jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa mahusiano bora ya kibiashara kati ya NBC na wateja hao kwa mwaka 2019. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.

Mkurugenzi Mtendaji wa NBC afanya ziara ya kikazi Kanda ya Ziwa.*akutana na kufanya mazungumzo na mkuu wa mkoa wa Kagera

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kulia), akizungumza na wafanyakazi wa benki hiyo wa Tawi la Mwanza, wakati wa ziara yake mkoani humo hivi karibuni.
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Marco Saguti (wa tatu kushoto), akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, wakati yeye na ujumbe wake walipomtembelea ofisini kwake katika ziara yao mkoani Kagera hivi karibuni.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (katikati), akipozi kwa picha na wafanyakazi wa benki hiyo wa tawi la Mwanza  wakati mkurugenzi huyo pamoja na ujumbe wake wakiwa katika ziara ya kikazi mkoani humo hivi karibuni. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (katikati), akipozi kwa picha na wafanyakazi wa benki hiyo wa tawi la Musoma wakati mkurugenzi huyo pamoja na ujumbe wake wakiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Mara hivi karibuni. 
Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Ziwa, Japhet Mazumira (kulia), akizungumza na wafanyakazi wa benki hiyo wa Tawi la Mwanza wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi mkoani humo hivi karibuni.  

BENKI YA NMB YAKABIDHI VITANDA 15 VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 45 HOSPITALI YA MUHIMBILI NA MLOGANZILA.

$
0
0
Katika kutambua afya ni suala muhimu sana kwa maendeleo ya jamii, Benki ya NMB imekabidhi vitanda 15 vyenye jumla ya thamani ya milioni 45 kwa ajili ya chumba cha watoto wagonjwa waliopo kwenye uangalizi maalum (ICU) katika hospitali za Muhimbili na Mloganzila za jijini Dar es Salaam.

Akikabidhi msaada huo kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Afisa Mkuu wa Mahesabu wa Benki ya NMB, Juma Kimori, alibainisha kwamba thamani ya vitanda vyote ni Sh. Milioni 45 huku  akifafanua kuwa kitanda kimoja cha ICU ya watoto kimegharimu Sh. Milioni 7.5 na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali kuboresha sekta ya afya.

Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Zuhura Mawona, aliishukuru na kuipongeza NMB kwa msaada huo na kuiomba iendelee kutoa msaada zaidi kwa ajili ya chumba hicho maalum kwa watoto.

“Tulipeleka maombi NMB na wametujibu hatuchoki, tunaendelea kuwaomba mtushike tena mkono, maana mahitaji ya vitanda katika chumba hicho muhimu cha kuokoa maisha ya watoto ni mkubwa, bado tunahitaji vingine saba mkiguswa tena mtukumbuke.

“Kabla ya wodi hii kuanza watoto walikuwa wanachanganywa kwenye ICU za wakubwa na kule vitanda sio sawa na hivi tulivyopokea vya NMB hata sisi  wahudumu hatupati tabu sana kuvinyanyua wala mgonjwa haumii kila kitu kinasetiwa kwenye umeme asanteni sana NMB,” alisema Mawona aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Hospitali ya Taifa Muhimbili.#NMBKaribuYako
Afisa Mkuu wa Ukaguzi wa Mahesabu ya Ndani wa Benki ya NMB, Peter Kimori akimkabidhi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto; Mh. Ummy Mwalimu masada wa vitanda 15 kwa ajili ya chumba cha watoto wagonjwa waliopo kwenye uangalizi maalum(ICU) katika hospitali za Muhimbili na Mloganzila za jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto; Mh. Ummy Mwalimu na Afisa Mkuu wa Ukaguzi wa Mahesabu ya Ndani wa Benki ya NMB, Juma Komori  wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao kutoka hospitali za Muhimbili na Mloganzila.

MAKKMAR HOTEL, MSATA, MKOA WA PWANI INAKUKARIBISHA MWAKA MPYA

KIFAA CHA KUDHIBITI WIZI WA PIKI PIKI NA VYOMBO VYA MOTO HIKI HAPA

$
0
0
Na Grace Gurisha


MENEJA Mauzo na Masoko wa Kampuni inayojihusisha na uundaji wa mifumo mbalimbali ya kiteknolojia ya MD Technology, Mohamed Kaddy amesema wameleta  kifaa maalumu chenye uwezo wa kudhibiti wizi wa pikipiki na vyombo vya moto.

Kaddy aliyasema hayo  jana  Desemba 14, mwaka huu, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kifaa hicho, ambapo alisema kwa kutumia teknolojia hiyo,pikipiki ikiibiwa, itapatikana na mmiliki atapata taarifa kupitia simu yake ya mkononi.

Meneja huyo alisema teknolojia hiyo ni rahisi, "Ukifunga kifaa cha kudhibiti wizi katika pikipiki yako,hata kama ikiibiwa usiwe na wasiwasi,itapatikana tu, lakini pia kama kuna mtu amesimama katika pikipiki yako utajulishwa”,.

"Kifaa hichi maalumu kitafungwa katika pikipiki na kuunganishwa na simu ya mkononi ambapo mteja atapata taarifa zote za uendeshaji wa pikipiki katika simu yake ya mkononi na pia hata akipoteza simu yake anaweza kutumia simu ya mtu mwingine na kupata taarifa kifaa chake kilipo," alisema 

Alisema mfumo huo husaidia kudhibiti udanganyifu wa madereva au marafiki katika matumizi ya umbali aliotumia kwa siku katika uendeshaji wa pikipiki,jambo litakalowawezesha wamiliki wa pikipiki kuwa na uhakika wa mapato, kwa zile zinazofanya usafiri wa abiria.

“Mfumo huu utawasaidia wamiliki wa pikipiki kupata taarifa kwa haraka pale chombo chake kikitaka kuibiwa au kushikwa na mtu, pia mfumo huo utamsaidia mtu kuzima au kuwasha chombo mahali popote atakapokuwa, kama umeibiwa unauwezo wa kuizima pikipiki yako kabla haijafika mbali," alisema

Alisema kifaa hicho tayari kimeshaanza kuuzwa kwa bei nafuu, hivyo madereva wajitokeze kwa wingi kununua ili kudhibiti wezi kutokana na wimbi la wizi wa Bodaboda linaloendelea hivi sasa.

Pia, alisema wanafunga vifaa kwenye nyumba kwa mfumo wa kisasa ambapo hata mwizi atakapokwenda kuiba hata gundua kama kuna kifaa cha usalama kimefungwa kwa hiyo itakuwa ni rahisi yeye kukamatwa kwa sababu kifaa kitaonesha kuna mtu ameingia.
 Meneja Mauzo na Msoko wa Kampuni inayojihusisha na uundaji wa mifumo mbalimbali yabkiteknolojia ya MD Technology, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na kifaa cha kisasa cha kuzuia wizi wa vyombo vya moto.

 Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya MD Technology, Brian Kessy akiwaeleza madereva wa Bodaboda faida ya kifaa hicho ambacho kitawasaidia katika suala nzima la ulinzi wa pikipiki zao
 Mtaalamu wa Mifumo kutoka MD Technology, Salum Mntitiwa akionesha jinsi ambavyo kifaa hicho kilivyofungwa na kuunganishwa na simu ya mkononi kinavyoweza kufanya kazi kwa kuliweka gari katika hali ya usalama,

Vodacom Tanzania Plc yawafikia wateja wake wa kanda ya ziwa, msimu huu wa sikukuu yazindua simu mpya ya Smart Kitochi jijini Mwanza

$
0
0


 Wafanyakazi wa Kampuni ya mawasiliano ya  Vodacom wakiwa wamebeba bango lenye picha ya simu ya Smart Kitochi  wakati wa uzinduzi wa simu hiyo uliofanyika jijini Mwanza.
Kaimu  mkuu wa mauzo wa Kampuni ya mawasiliano ya  Vodacom kanda ya Ziwa, Ayubu Kalufya akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa simu ya Smart Kitochi, uliofanyika jijini Mwanza.
Wateja wa simu mpya za Smart Kitochi zenye uwezo wa 4G kutoka Vodacom wakipatiwa maelezo ya kuhusu simu hizo zitakazopatikana kwenye maduka ya Vodacom  nchini kote kwa bei ya shilingi 45,000/=  katika msimu huu wa sikukuu wakati wa uzinduzi wa simu hizo jijini Mwanza.

Wateja wa simu mpya za Smart Kitochi zenye uwezo wa 4G kutoka Vodacom, wakijipiga selfie kwa kutumia simu hiyo baada ya kuinunua jijini Mwanza, wakati wa uzinduzi wa simu hiyo inayopatikana kwenye maduka ya Vodacom nchini kote kwa bei ya shilingi 45,000/= katika msimu huu wa sikukuu.

NHIF Yawapiga Msasa Wanahabari Mkoa wa Mbeya Kuhusu Vifurushi vya Bima ya Afya

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF) Bw. Bernard Konga akiongea na wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya, ambapo aliwasisitiza kuhusu umuhimu wa kutumia vyombo vyao vya habari kuwaeleza wananchi faida za kujiunga na vifurushi vipya kwani vimezingatia makundi yote katika jamii kwa lengo la kuhakikisha kila mtanzania anakuwa na uhakika wa huduma ya matibabu. Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya
Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF)Bw. Christopher Mapunda akiongea na wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya, ambapo alisema kuwa viwango katikavifurushi vya bima ya afya sio gharama za matibabu bali ni uchangiaji ndio maana hata ukiumwa na kutumia zaidi ya kiwango cha laki moja na tisini na mbili, mfuko utagharamikia matitabu hayo. Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya
Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF) Bw. Hipoliti Lello na akitoa mada kwa wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya, ambapo aliwaeleza kuwa mpango wavifurushi sio mpya na NHIF imeanzisha mpango huo kwa lengo la kuwafikia watanzania wengi zaidi kulingana na mahitaji yao. Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya.
wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya wakifuatilia uwasilishaji wa mada kutoka kwa wataalam wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF), Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya
PICHA NA IDARA YA HABARI-MAELEZO

**************************
NA MWANDISHI WETU, MBEYA

Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF) Umewapiga Msasa wanahabari Mkoa wa Mbeya kuhusu Vifurushi vya Bima ya Afya na kuwasisitiza kutumia kalamu zao kuwaeleza wananchi umuhimu wa kujiunga ili kuwa na uhakika wa matibabu. 

Akiongea wakati wa Kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Bw. Bernard Konga amewaeleza wanahabari hao kuwa kwa namna ambavyo mfuko umetengeneza vifurushi umezingatia gharama za matibabu ya kawaida ambayo ukienda hospitalini lazima uyapate. 

“Leo hii wapo wanaopotosha kuhusu gharama hizi, hatuwezi kuwaacha watanzania ambao wapo tayari kutumia bima ya afya ili kupata matibabu na kusema tusubiri, niwahakikishie tumefanya tafiti, kiasi cha Shilingi laki moja na tisini na mbili kimezingatia gharama za matibabu ya kawaida ambayo ukienda hospitalini lazima uyapate na utaratibu huu ni niwa hiari”-Alisema Bw. Konga. 

Aidha, Bw. Konga alisema kuwa umefika wakati kwa wananchi kujikatia bima ya afya kabla ya kuugua hasa katika kipindi hiki ambacho mfuko umeanzisha mpango wa vifurushi ili kuwa na uhakika wa matibabu na kupuuza maneno ya baadhi ya watu wanaoendesha mijadala isiyo na tija. 

Naye Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama wa Mfuko huo Bw Christopher Mapunda alisema kuwa viwango katika vifurushi vya bima ya afya sio gharama za matibabu bali ni uchangiaji tu na ndio maana hata ukiumwa na kutumia zaidi ya kiwango cha laki moja na tisini na mbili, mfuko utagharamikia matitabu hayo bila kujali kuwa umetibiwa kwa kiasi gani. 


Awali akiongea wakati akiwasilisha mada kwa wanahabari hao Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF) Bw. Hipoliti Lello alisema kuwa mpango wa vifurushi sio mpya na NHIF imeanzisha mpango huo kwa lengo la kuwafikia watanzania wengi zaidi kulingana na mahitaji yao
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images