Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all articles
Browse latest Browse all 48933

ASIA IDAROUS,GYMKHANA HILALL NA MARTIN KADINDA WATEULIWA NA KUTOA UAMUZI UNIQUE MODEL 2012

$
0
0


Baraza la sanaa la taifa limeteua majina matatu ya wabuni wa mavazi nchini Tanzania kuwa waamuzi wa shindano la wanamitindo bora wa mwaka wenye sifa za kipekee nchini Tanzania.

Uteuzi  wa majaji hawa umezingatia sifa za cv za majaji sita zilizowakilishwa baraza la sanaa la taifa na hatima yake yakarudi majina matatu ambayo ni Asia Idarous,Gymkhana Hilall(paka wear) na Martin Kadinda.

Fainali za unique model  2012 zinafanyika ijumaa ya wiki hii tarehe 28 Desemba katika kumbi la maraha lililoko kule Oysterbay yaani naongelea  New Maisha club ambapo wanamitindo 12 watapanda jukwaani kuwania taji hilo.

Burudani ya bendi mahili katika muziki Mashujaa band ikiongozwa na Chalz Baba watatoa burudani kali kwa mashabiki watakaohudhulia fainali hizo siku ya Ijumaa hii.pia msanii B-shop kwa mara ya kwanza  ataonekana jukwaani. Ikiambatana  na mashamushamu ya Costa siboka na  burudani ya wanamuziki mbalimbali kwa kiingilio cha Tsh 15,000 tu.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 48933

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>