Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 48993 articles
Browse latest View live

Exim Bank sponsors National Swimming Championships 2013

$
0
0
 The Exim Bank Tanzania Managing Director Anthony Grant (left) explains a point to the Assistant Director for Sports Development in the Ministry of Information Youth, Culture and Sports Juliana Yassoda (right) who was the Guest of Honor for the event. 
 The Exim Bank Tanzania Managing Director Anthony Grant (left) gives a gold medal to Elia Imhoff  (centre) who emerged winner in the Under 25 Breast Stroke  competition during the National Swimming Championships held at the weekend. 
 The Exim Bank Tanzania Managing Director Anthony Grant (left) congratulates Hilal Hillary (centre) winner of the 800 meter free style competition during the National Swimming Championships held at the weekend
 Tanzania’s representative in last year’s Olympic Games held in London Ammaar Ghadiyali (right) shares a light moment with the Director for Sports Development in the Ministry of Information Youth, Culture and Sports Juliana Yassoda (left) during the National Swimming Championships held at the weekend. Centre is the Exim Bank Tanzania Managing Director Anthony Grant
 Young boys take part in the swimming competition.
 Young girls take part in the Breast Stroke swimming category.
  Men take part in the 800m free-style swimming competition
 A cross section of fans that turned out to cheer their respective teams
 The Exim Bank Assistant Marketing Manager Anita Goshashy briefs reporters on the bank’s commitment to support development of various sports activities in the country.

Journalists interview Hilal Hillary (left) shortly after emerging winner of the 800m free-style swimming competition

KINANA n aujumbe wake wATUA BEIJING, wapokelewa na Balozi wa Tanzania nchini China, Philip Marmo

$
0
0

"KARIBU BEIJING", Balozi wa Tanzania nchini China, Philip Marmo (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing, China, baada ya Kinana na ujumbe wake kuwasili akitokea jimbo la Sichuani, leo Machi 17, 2013. Kinana na ujumbe wa viongozi 14 wa CCM wapo nchini china kwa ziara ya siku kumi ya mafunzo, kwa mwaliko wa Chama CHa Kikomunisti cha China.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza, nyumbani kwa Balozi wa Tanzania mjini Beijing, China, Philip Marmo (wapili kushoto), baada ya kuwasili leo, Machi 17, 2013 akitokea Sichuan. Kinana na Ujumbe wa viongozi 14 wa CCM yupo nchini China tangu Machi 11, mwaka huu, akiwa katika ziara ya mafunzo kwa mwaliko wa Chama CHa Kikomunisti cha China. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai na Kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro na Mjumbe wa Kamti Kuu ya CCM,  Kadija  Aboud.
Balozi wa Tanzania Nchini China, Philip Marmo akizungumza baada ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake, nyumbani kwake, kwenye Ubalozi wa Tanzania mjini Beijing, China, baada ya kuwasili leo Machi 17, 2013, akitokea jimbo la Sichuan.  Kinana na ujumbe wa viongozi 14 wa CCM wapo nchini China kwa ziara ya siku kumi ya mafunzo, kwa mwaliko wa Chama CHa Kikomunisti cha China. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vuai Ali Vuai.
Baadhi ya Watanzania waliopo jijini Beijing, China wakichangamkia kupigapicha na Katibu wa NEC, Siasa na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (Katikati) nyumbani kwa Balozi wa Tanzania nchini China.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Mbunge wa Busega, Dk. Titus Kamani akiwasalimia baadhi ya Watanzania wanaoishi Beijing China, baada ya kuwasili na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, nyumbani wa Balozi wa Tanzania nchini China, Philp Marmo, Machi 17, 2013. Kamani ni miongoni mwa viongozi 14, wa CCM waliopo katika msafara wa Kinana ambaye yupo nchini China na ujumbe huo kwa ziara ya Kikazi nchini humo, kufuatia mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China.
Baadhi ya Watanzania wanaoishi Beijing, wakilaki Kinana na msafara wake, nyumbani kwa Balozi Marmo, Beijing China, leo Machi 17, 2013. Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Beijing, Daninga Daniel.Picha na Bashir Nkoromo.

msikilize khadija kopa ndani ya mkasi wa salama jabir alivyofunguka live.

HAPPY BIRTHDAY MAMA wa FATHER KIDEVU BIBI.MARY NATHAN

$
0
0

TAREHE ya leo ni ndio aliyo zaliwa Mama mzazi wa Blogger na Mpigapicha nguli Tanzania, Mroki Mroki, Bi. Mary O.Nathan  (pichani) wa Kinyenze, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro ambaye leo anatimiza miaka 60 tangu kuzaliwa kwake tarehe kama ya leo. 



Kipekee anamshukuru Mungu kwa kumjalia umri huo alionao hivi sasa. Anawashukuru wote ambao wamechangia yeye kuishi vyema. Anaishukuru sana Familia yake yote kwa umoja na upendo walio nao jambo mabalo anasema linamfanya aishi kwa furaha na amani. 



Aidha watoto wake wote wanampa Pongezi za dhati na Kumuombea Mungu amjalie zaidi Afya njema, akimpa zawadi ya Hekima na Busara katika kipindi hiki cha maisha yake ya utu uzima ambao Busara yake na Hekima vinahitajika sana ndani ya Familia yake na Jamii kwa ujumla.



Wajukuu zako na Vitukuu wako pia wanakusalimia sana na wanakuimbia kale kawimbo ka Happy Birthday Bibi!!! Happy Birthday Bibi!!! Happy Birthday Bibi!!! Happy Birthday Bibi!!! Dear Bibi Happy birthday to youuuuuuuu!!!!



Wananchi na majirani zako wa pale Kijiji cha Kipera , Kitongoji cha Kinyenze,Kata na Tarafa ya Mlali , Wilayani Mvomero mkoani Morogoro pia wanakutakia heri na fanaka.



HAPPY BIRTHDAY MAMA TUNAKUPENDA SANA NA TUNAJIVUNIA KUWA NA MAMA WA NAMNA YAKO, MUNGU AKUJALIE HEKIMA NA BUSARA ZAIDI KATIKA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKO.



BY: FAMILIA YAKO.

pini la Rich Mavoko - One Time (Official Video)

Diamond - Kesho [Official Video HD]

Usiku wa Tusker Lite ulvyofana ndani ya kibo palace jijini Arusha wikend

ajali:TRAFIKI AGONGWA NA GARI ENEO LA BAMAGA

$
0
0

Trafiki wa kike aliyejulikana kwa jina moja la Elikiza aliyekuwa akiongoza magari eneo la Bamaga, Mwenge jijini Dar, akifunikwa na wasamaria wema baada ya kugongwa na gari na inadhaniwa kuwa amekufa papo hapo.
Baadhi ya wananchi waliofika eneo la tukio.
Hali ilivyokuwa eneo la tukio baada ya ajali hiyo.
Trafiki mmoja ambaye amefahamika kwa jina moja la Elikiza, muda huu amegongwa na gari aina ya VX ambayo haikujulikana namba na inadhaniwa kuwa amekufa papo hapo wakati akiongoza magari eneo la mataa ya Bamaga, Mwenge jijini Dar es Salaam. Taarifa zilizopatikana eneo la tukio zinadai kuwa Trafiki huyo alikuwa akiongoza msafara na baada ya msafara huo, aliruhusu magari mengine yaendelee na safari ndipo ghafla gari lilipotoka upande wa pili na kumgonga.
(Picha zote kwa hisani ya Shauri Kati / GPL)

HABARI NJEMA KWA WATU WENYE SHIDA NA MATATIZO MBALIMBALI.

$
0
0

Dk.  Mungwa   Kabili   ni  mtaalamu  wa  tiba  za  jadi  kutoka  Bagamoyo   pwani. Ninatoa  msaada  kwa  watu  wenye  shida  na  matatizo  mbalimbali.  Huduma  ninazo  toa  ni  pamoja  na  :  1. Pete  za   Bahati   2.  Dawa  za  Mapenzi; Utampata   mtu yoyote  unaye  mtaka   3.   Kesi     4. Mtu  aliyekudhulumu    atakulipa  pesa  au  mali  zako  ndani  ya  siku  arobaini  21.  Dawa  za  Biashara   5.  Kinga  ya  mwili, biashara  na  nyumba   6. Kumuita  mtu  aliye  mbali    7. Kuacha  pombe  na  sigara    8.  Ugumba   9. Uwezo  wa  Masomo  Darasani  pamoja  na  magonjwa  mbalimbali  kama  vile  kisukari, presha, kupunguza  uzito , kifafa  nakadhalika.
 
NINATIBU  KWA  UWEZO  WA    MUNGU  NA  HAKUNA  JAMBO  LOLOTE  LINALOSHINDIKANA
 
                                      MALIPO   NI   BAADA     YA   MAFANIKIO
 
                                    WASILIANA  NAMI  KWA  SIMU  :   0656306725

KITABU CHA KIFO NI HAKI YANGU KUANZA KUUZWA JUMATATU MACHI 25, 2013

UFAFANUZI WA TUME KUHUSU MKAZI WA KUDUMU NA MABADILIKO YA TAREHE ZA UCHAGUZI WA WAJUMBE NGAZI YA KIJIJI NA MITAA

$
0
0

Tume ya Mabadiliko ya Katiba imewakumbusha wananchi wanaopenda kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya kutumia siku mbili zilizobaki kuwasilisha maombi yao kwa Maofisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa na kusisitiza kuwa siku ya mwisho ya kuwasilisha maombi hayo ni  siku ya Jumatano, tarehe 20 Machi mwaka huu (2013).
 
Wananchi wanaopenda kuwa Wajumbe wa Mabaraza hayo wawasilishe maombi yao yakiwa na taarifa zifuatazo: Majina Kamili; Jinsi; Umri; Eneo analoishi kwenye Kijiji/Mtaa; Kiwango cha Elimu; na Kazi yake.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Tume leo (Jumatatu, Machi 18, 2013), wananchi wamekumbushwa kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na sifa zifuatazo: Awe ni Raia wa Tanzania na awe na umri wa miaka 18 au zaidi na awe na uwezo wa kusoma na kuandika. Sifa nyingine ni pamoja na kuwa mkazi wa kudumu wa kijiji, mtaa au shehia husika na awe ni mtu mwenye hekima, busara na uadilifu na pia awe mtu mwenye uwezo wa kujieleza na kupambanua mambo.
  
Katika hatua nyingine, Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Jospeh Warioba imefafanua kuhusu sifa ya ukazi wa kudumu kwa waombaji na kusema kuwa sifa hiyo haina maana kuwa mwananchi anapaswa kumiliki nyumba katika mtaa au kijiji husika. 
 
"Tume inapenda kuwafahamisha wananchi kuwa mkazi wa kudumu ni mwananchi yeyote anayeishi katika mtaa au kijiji husika na sio lazima awe anamiliki nyumba katika mtaa au kijiji hicho," imesema sehemu ya taarifa hiyo iliyosambazwa kwa vyombo vya habari.
 
Kuhusu wananchi kuhakiki majina ya waombaji, Tume hiyo imewataka wananchi walioomba kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya kuhakiki majina katika orodha ya majina ya waombaji wote itakayobandikwa katika eneo la wazi au mbao za matangazo katika Mtaa, Kijiji au Shehia husika kwa siku saba kuanzia tarehe 22 hadi tarehe 28 mwezi machi mwaka huu.
  
Katika taarifa hiyo, Tume pia imesema imefanya mabadiliko madogo katika mwongozo wake (uliotolewa hivi karibuni) katika tarehe za vikao vya mitaa na vijiji vitakavyowachagua Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba. Kwa mujibu wa mwongozo uliotolewa na Tume mwezi uliopita, vikao hivi vilipaswa kufanyika kati ya tarehe 30 mwezi Machi mwaka huu (2013) na tarehe 3 Aprili mwaka huu (2013).
 
"Kwa mujibu wa mabadiliko mapya, vikao hivyo sasa vitafanyika kati ya tarehe 30 Machi mwaka huu (2013) hadi tarehe 5 Aprili mwaka huu (2013). Kwa msingi huu kila kijiji au mtaa kitachagua tarehe atika vikao hivyo, wananchi watapiga kura za siri kuwachagua wananchi wanne kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya," imeongeza sehemu ya taarifa hiyo.
 
Kufuatia mabadiliko haya, Tume imeongeza, Vikao Maalum vya Kamati za Maendeleo za Kata vya kuwachagua wajumbe wanne kutoka miongoni mwa wananchi waliochaguliwa na vijiji na mitaa navyo vimesogezwa mbele na sasa vitafanyika kati ya tarehe 7 Aprili mwaka huu (2013) na tarehe 10 Aprili mwaka huu (2013). Awali, vikao hivi vilipangwa kufanyika kati ya tarehe 5 Aprili mwaka huu (2013) na tarehe 9 Aprili mwaka huu (2013).
 
Tume inawaomba wananchi kushiriki na kuendesha mchakato wa kuwapata Wajumbe kwa amani na utulivu na kuzingatia mwongozo uliotolewa na Tume

Tanzania must ensure that digital migration promotes freedom of expression

$
0
0

Dar-es-Salaam 18.3.2013: ARTICLE 19 is concerned that the recent transition to digital broadcasting in Tanzania did not take into account the needs of viewers and broadcasters and as a result many people are no longer able to watch TV.

ARTICLE 19 calls on the government and the Tanzania Telecommunication Regulatory Authority to fulfil the right to freedom of expression and respect media pluralism by providing information on digital migration and financial assistance to disadvantaged viewers and listeners, as well as to broadcasters to cope with the transition.

“ARTICLE 19 has consistently called upon governments to ensure openness, transparency and universal access as the only way to guarantee that all people enjoy the benefits that come from digital broadcasting. It is not acceptable for digital communication to be an exclusive service available only to the few,” said Henry Maina, Director for ARTICLE 19 Eastern Africa.

Digitalisation - the process of turning the analogue broadcasting system into a system of digital television and radio – affects the right of freedom of expression of viewers and listeners and of broadcasters. In an ideal situation, digitalisation will foster media pluralism by enabling the broadcasting of more channels with a wider range of programming. As a result viewers and listeners would be able to receive more diverse information and opinions.

However, the technical and financial aspect of the switch to digital broadcasting will be burdensome for vulnerable people in Tanzania, many of whom are economically disadvantaged. According to available statistics, since the transition to digital TV at the end of December 2012, 50% of TV owners cannot access TV services because they do not have digital set-top boxes. So far, they have received insufficient information about the new digital technology and about financial assistance in cases when they cannot afford the set top boxes

Similarly the financial burden imposed on commercial and public broadcasters to purchase technical equipment necessary to the transition to digital broadcasting may affect their ability to continue operating. Many local and regional TV stations are already in disadvantageous positions due to high operation costs and low advertisement revenues. Lack of consideration for media diversity and pluralism in the digital process might drive they them out of business and creating a monopoly of “big players.”

Digital switchover policies must therefore take into account the interests of all stakeholders and ensure that media pluralism and the right to freedom of expression are respected. Tanzanian government should also consider allowing simultaneous digital and analogue broadcasting until all stakeholders are prepared to switch completely to digital TV and facilitate access to information in the process.

ARTICLE 19 calls on the Tanzanian government and the Tanzania Telecommunication Regulatory Authority to adopt a rights-based approach to digitalisation directed at promoting and protecting human rights, analysing inequalities, and redressing discriminatory practices and the unjust distribution of power, information and resources.

ARTICLE 19 also calls upon all Eastern Africa states to specifically think through the digital migration process and ensure that it promotes and safeguards freedom of expression and access to information.

JIACHIE NA VIDEO MPYA YA KALA JEREMIAH FT BEN POL - KARIBU DAR

MABONDIA PRINCE NAIDJALA NA SEKOTSWE NUSU WAZIPIGE KAVU KAVU

$
0
0

Mabondia Immanuel “Prince” Naidjala  wa Namibia and Lesley Sekotswe wa Botswana wamekutana leo katika mkutano wa waandishi wa habari. Kukutana kwao nusura kulete balaa kubwa baada ya mabondia wenyewe kuingia midadi na kutaka kuzipiga kavu kavu mbele ya vyombo vya habari 


                          Immanuel "Prince" Naidjala.

 Mkutano huo ulifanyika katika hotel ya Windhoek Country Club Resort ambayo ni moja ya Casino kubwa katika nchi ya Namibia. Vyombo mbalimbakl vya habari kutoka nchi za Afrika na Ulaya zilishiriki katika mkutano huo ambao wawili hao walitambiana kupeana mkongoto wa uhakika watakapokutana siku ya jumatano tarehe 20.
  
Mabondia hao wanakutana tena kesho tarehe 19 katika hoteli hii katika zoezi la kupima uzito kabla ya mpambano wao siku ya Jumatano ambayo ni siku ya Uhurru wa nchi ya Namibia. Viongozi wakuu wa serikali ya Namibia watahudhuria mpambano huo ambao ni mkubwa kuwahi kufanyika katika nchi hii yenye wakazi milioni mbili na ushee!

Naye Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi amewasili jijini Windhoek leo akitokea nchini Ghana kulisimamia pambano hili la ubingwa wa “IBF International Title”

Rais Ngowi ametokea jijini Accra, Ghana ambapo alishughudia mabondia Richard Commey na Bilal Mohammed wakitoana jasho ambako Richard Commey aliibuka kuwa bingwa wa uzito mwepesi katika bara la Afrika.

Promota wa mpambano huo Nestor Tobias wa kampuni maarufu ya Sunshine Boxing Promotions ana uhakika wa mpambano huu kuvunja rekodi ya kuingiza watu wengi zaidi ya mapambano yote yaliyowahi kufanyika nchini Namibia.

Pambano hili litawakutanisha pia baadhi ya mabondia kadhaa katika mapambano ya awali ambako bondia Martin Haikali wa Namibia atakutana na Nelson Banda wa Zambia katika mpambano wa raundi 8.

INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA.

ziara ya rais kikwete jijini dar leo

$
0
0

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Waziri wa Elimu Dkt.Shukuru Kawambwa(kulia),Balozi wa Korea ya Kusini Mhe.Chung(wapili kulia),Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bwana Sadik Meck Sadik(Wapili kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa VETA Injinia Zebadia Moshi(kushoto) wakikata utepe kufungua rasmi Chuo Cha TEHAMA VETA huko Kipawa jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt.Jakaya Mriusho Kikwete,Waziri wa Elimu dkt.Shukuru Kawambwa(kulia) na Balozi wa Korea ya Kusini Mhe.Chung na viongozi wengine wakipiga makofi wakati wa uzinduzi wa Chuo cha TEHAMA VETA Kipawa jijini Dar es Salaam leo mchana. Picha zote na Freddy Maro wa Ikulu.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi msaada wa Usafiri aina ya Bajaji Bwana Bashir Msanda ambaye ni mlemavu wakati wa mwanzo wa ziara yake ya kukagua na kufungua miradi ya maendeleo jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Makabidhiano hayo  ambayo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Kikwete kumsaidia mlemavu huyo ,yalifanyika katika viwanja vya Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi kuzindua rasmi ujenzi wa Taasisi ya mifupa na mishipa ya fahamu katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam leo
Mkurugenzi wa Huduma za Maabara Bibi Charys Ugullum akimweleza Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete jinsi maabara ya ukaguzi wa dawa na vyakula inavyofanya kazi wakati Rais alipotembelea maabara ya kisasa ya TFDA iliyopo Mabibo External jijini Dar es Salaam leo mchana wakati wa siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Dar es Salaam

WAJUMBE WA KAMATI YA BUNGE YA MAENDELEO YA JAMII WAKUTANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII NA WIZARA YA HABARI

$
0
0
 Baadhi ya Watendaji Wakuu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Wakifuatilia kikao kati yao na kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii.

Katika picha ni kikao kati ya Kamati ya Bunge  ya  Kudumu ya Maendeleo ya Jamii na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wakati Wizara hizo zilipokuwa zikiwasilisha  taarifa za Majukumu yao kwa Kamati hiyo, katika Ukumbi mdogo wa Mikutano, Kalimjee Hall.
Picha zote na Asteria Muhozya.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii,Mhe.Jenister Mhagama akiongea wakati wa kikao. Kulia kwake ni Naibu Waziri Ummy Mwalimu na Kulia kwake ni Waziri wa Habari Dr.Fenella Mukangara
 Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge Maendeleo ya Jamii wakifuatilia taarifa za kikao
 Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Fenella Mukangara akiwasilisha taarifa ya Majukumu ya Wizara yake kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Bw.Seth Kamuhanda akiwasilisha taarifa ya Wizara yake kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii.
 Naibu Waziri Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwasilisha taarifa ya Wizara kwa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii
Kaimu Katibu Mkuu, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bibi. Anna Maembe akiwaeleza Wajumbe wa Kamati Majukumu ya Wizara

UZINDUZI WA MRADI WA KUKABILIANA NA ATHARI ZITOKANAZO NA MABADILIKO YA TABIANCHI

$
0
0

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira dkt Terezya Huvisa, amezingua moja ya miradi wa maji safi na salama, katika kijiji cha Ng’mbo wilaya mpya ya Nyasa katika mkoa wa Ruvuma ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.

Akizindua kisima hicho, Dkt Hufisa alieleza kuwa, mradi huo wa maji safi na salama kwa matumizi ya binadamu katika kijiji hicho umewalenga zaidi wanawake kwani wao wamekuwa wakitumia muda mwingi kwenda kutafuta maji ziwani au katika visima vya muda kwa matumizi ya nyumbani,hivyo kisima hicho kitawasaidi kuokoa muda na kushiriki katika shughuli nyingine za kimaendeleo.

Dkt Hufisa aliongeza kwa kusema kuwa, wananchi wana haja na kila sababu ya kupata elimu ya kutosha juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na mazingira, na halmashauri iweke mikakati ya kutunza vyanzo vya maji pamoja na kupanda miti na kuitunza.

Aidha dkt Huvisa amewaasa wananchi kushirikiana na police jamii wanaosimamia masuala ya mazingira katika kubaini waharibifu wa mazingira wanaovua kwa kutumia nyavu na uvuvi haramu.

Awali  mratibu wa kitaifa wa mradi huo kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira bw. Faraja Ngeregeza ameeleza kuwa, lengo la mradi huo ni kujengea uwezo wananchi na wanakijiji ili kuweza kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi hasa zinazotokana na upungufu wa maji safi na salama.

Bw. Faraja alisema kuwa kijiji cha Ng’ombo hakikuwa na maji safi na salama kwa muda mrefu hali iliyowalazimu wanakijiji hichohususan kina mama kutembea muda mrefu kutafuta maji kwa matumizi ya nyumbani. “kukamilika kwa mradi huu kumetoa fursa kwa kina mama kupata maji kwa muda mfupi na kupata muda wa kushiriki katika shughuli nyinine za kimaendele.”alisisitiza.

Mradi huu unaotekelezwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira unafadhiliwa na serikali ya japan kupitia shirika la maendeleleo la umoja wa mataifa unatarajia kukamilisha ujenzi wa visima vingine katika wilaya ya misenyi mkoani Kagera,Igunga mkoani Tabora na maeneo ya Nungwi mjini Zanzibar ikiwa ni kwa ajili ya kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

Evelyn Mkokoi
Afisa Habari Ofisi ya Makamu wa Rais
19/3/2013

rais kikwete azindua maabara ya kisasa ya mamlaka ya chakula na dawa

$
0
0
 Mhe. Rais akikata utepe kuizindua maabara ya kisasa ya TFDA, wengine katika picha ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid, Mkuuwa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadiki, Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya Huduma za Jamii, Margreth Sitta, Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dar es salaam, Ramadhani Madabida
Mhe. Rais akiwa ameshika Tuzo ya kutambua mchango wake katika uzinduzi huo mara baada ya kukabidhiwa na TFDA.
Rais Kikwete akihutubia wageni waalikwa na wafanyakazi wa TFDA.


 Rais akiwa katika maabara ya TFDA, ambapo Mkurugenzi wa Maabara Bi. Charys Ugullum akimweleza namna maabara inafanya chunguzi mbalimbali na kutoa majibu ya maswali yaliyoulizwa. 
Mhe. Rais akitazama dawa bandia ambayo ilikamatwa katika soko na baada ya kuchunguzwa na maabara ya TFDA iligundulika ndani ya kidonge kumewekwa unga wa mahindi badala ya dawa. Anayetoa maelezo ni Meneja mchunguzi wa dawa, Bw. Yonah Hebron 
 Mkurugenzi mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, akitoa maelezo kuhusu TFDA kwa Mhe. Rais

 Rais wa Tanzania, Dkt. Kikwete akiwa ameongozana na Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti  Sillo mara baara ya kuwasili na kuelekea kuzindua maabara

Rais na ujumbe wake ukitoka maabara ya TFDA na kuelekea jukwaa kuu.
Wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete.


=======  =======  =====
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE AZINDUA MAABARA YA KISASA YA MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA (TFDA), TAREHE 18 MACHI, 2013

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, amezindua Maabara ya kisasa ya TFDA  ya uchunguzi wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi na Vifaa tiba kwa lengo la kulinda afya ya wananchi.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bw. Hiiti, Sillo, alieleza kuwa mifumo ya utendaji kazi ya TFDA ni ya kiwango cha Kimataifa cha ISO/ 9001:2008, ambapo maabara hii ya TFDA inayozinduliwa  ni ya kwanza barani Afrika kutambuliwa na WHO miongoni mwa maabara za taasisi za Serikali za udhibiti wa bidhaa yaani “National Regulatory Authorities”, ambapo ni moja ya maabara 23 duniani zilizotambuliwa na WHO wakati kati ya hizo saba (7) ziko Afrika na tatu (3 ) zipo Afrika Mashariki.

Katika hotuba yake baada ya kuzindua maabara ya TFDA, Dkt. Kikwete amepongeza Maabara ya TFDA kwa hatua zote ilizozifikia ikiwa ni pamoja na kupata ithibati kwenye uchunguzi wa chakula na mikrobiologia kwa kiwango cha kimataifa cha ISO/IEC 17025 toka “Southern African Development Community Accreditation Services “ (SADCAS) na kwa kuteuliwa kwa maabara hiyo na Shirika la “International Federation for Animal Health” (IFAH) kuwa maabara rejea (reference laboratory) katika uchunguzi wa dawa za mifugo kwa nchi za Afrika Mashariki.

Dkt. Kikwete pamoja na kuipongeza Menejimenti na wafanyakazi wa TFDA kwa kufanya kazi kwa uadilifu, utaalamu, uaminifu na kujituma ambako kumepelekea kufikia hatua kubwa ya mafanikio yaliyopo, alieleza kuwa “ hii ni ziara ya kihistoria kwangu na kwa kweli haya ni mafanikio makubwa kwa Serikali na Taifa kwa ujumla, TFDA imeiletea sifa Taifa na ninawapongeza kwa kuipepeza vema bendera ya Taifa”. 

Aidha, Dkt. Kikwete amewataka watumishi wa TFDA kutokubweteka na mafanikio yaliyofikiwa bali kuendeleza kasi katika udhibiti wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi na Vifaa tiba nchini kwa lengo la kulinda afya ya Jamii.

Aidha, Mhe. Rais ameahidi kuijengea uwezo TFDA ili kusambaza mtandao wake katika kuimarisha  udhibiti wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi na Vifaa tiba kwenye maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuhakikisha afya za wananchi zinalindwa. 

Kutokana na ubora wa mifumo ya utendaji, TFDA imeendelea kupokea wataalam kutoka nchi mbalimbali za Kenya, Zambia, Rwanda, Uganda, Ethiopia, Nigeria, Cameroon, Sudan Kusini, Burundi, Liberia, Msumbiji na Ghana kujifunza juu ya mifumo ya udhibiti wa ubora na usalama wa chakula, dawa, vipodozi na Vifaa tiba.

Mafanikio haya ni sehemu ya safari ya kuifikia Dira ya TFDA ambayo ni kuwa mamlaka inayoongoza barani Afrika katika udhibiti wa usalama, ubora na ufanisi wa vyakula, dawa, vipodozi na Vifaa tiba kwa wote. 


Dkt.Huvisa azindua mradi wa maji safi na salama mkoani ruvuma

$
0
0
waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira  dkt Terezya Huvisa akizindiua mradi wa maji safi na salama katika kijiji ng'ondo wilayani Nyasa Mkoani Ruvuma ikiwa ni jitihada za serikali katika kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.picha na evelyn mkokoi.
Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira dkt Terezya Huvisa, akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Ng'ondo kabla ya ufunguzi wa maradi wa maji safi na salama katika kijiji hicho kilichopo katika wilaya mpya ya Nyasa mkoani Ruvuma, ikiwa ni jitihada za serikali katika kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi..picha na evelyn mkokoi
waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira dkt Terezya Huvisa akicheza Ngoma aina ya Kioda na wananchi wa kijiji cha Ng'ondo katika Wilaya Mpya ya Nyasa...ikiwa ni ishara ya kufurahia pamoja nao baada ya kukamilika kwa mradi wa maji safi na salama katika kijiji hicho kilichopo katika wilaya mpya ya nyasa mkoani Ruvuma....picha na Evelyn mkokoi

singo mpya ya kisharo-kisharo kutoka kahama.

$
0
0
Huyu ndiye J One, Msanii katika mahadhi ya Bongo Flava kutoka katika mji wa madini Kahama. Anatambulisha Ngoma yake mpya ikiambatana na Video akimshirikisha Msanii wa Mwanza Baraka Prince, Ngoma Inakwenda kwa jina la Kisharo sharo.
Viewing all 48993 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>