TGNP WAGUSWA NA MUME KUWABAKA WANAE WAWILI, MMOJA AMPA UJAUZITO
Benki ya NMB yaimarisha mfumo wake kuongeza tija utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu
Na Mwandishi Wetu
Benki ya NMB imekamilisha zoezi la kuunganisha mfumo wake mkuu wa kibenki na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ikiwa ni utekelezaji wa sehemu ya dhamira ya benki hiyo kuimarisha utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
Hatua hiyo inalenga kuwawezesha wanafunzi katika vyuo vikuu kupata bidhaa za kibenki zenye hali ya juu ya usalama, ufanisi na uvumbuzi.
Akizungumza wakati wa kongamano lililofanyika jijini Dar es Salaam jana lililoandaliwa na Bodi ya Mikopo na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa elimu chini, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NMB Filbert Mponzi alisema mfumo huo kwa kiwango kikubwa umerahisisha utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
“Wanafunzi sasa wataweza kufurahia huduma za kibenki bila matatizo baada ya kuunganishwa kwa mfumo mkuu wa benki ya NMB na Bodi ya Mikopo. Muunganisho huu utahakikisha kuwa mikopo sasa inatolewa kwa wanafunzi kwa haraka na kwa urahisi zaidi,” Mponzi alisema.
Aliwataka wanafunzi wa vyuo vikuu kufungua akaunti na benki yake ilikunufaika na faida lukuki zikiwemo mikopo ya papo kwa papo yenye masharti nafuu kuanzia shilingi elfu moja hadi shilingi laki 5.
Mponzi wakati wa kongamano hilo alisisitiza dhamira ya benki hiyo kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali pamoja na taasisi za elimunchini ili kusaidia maendeleo ya sekta ya elimu kuanzia ngazi ya chini.
“Sekta ya elimu ni miongoni mwa vipaumbele vyetu muhimu. Ili kusisitiza dhamira yetu ya kusaidia elimu ya juu, mwaka jana tulitenga mikopo ya shilingi bilioni 200 kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kufuatia majadiliano ya karibu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,” Mponzi alisema.
Aliongeza, “Wanafunzi wanaweza kuomba mikopo kuanzia shilingi laki mbili hadi hadi shilingi milioni 10 kwa riba nafuu ya asilimia 9 tu,”
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Dk.Bill Kiwia wakati wa hafla hiyo alisema lengo la kongamano hilo ni kupokea maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wanaohusika na utendaji wa utoaji wa fedha kwa taasisi yake.
Alisema kuwa bodi hiyo kwa sasa inawafikia zaidi ya wanafunzi laki mbili wenye uhitaji lakini tayari imepanga mipango ya kuwafikia wanafunzi wengi zaidi na kuongeza kuwa hata hivyo itategemea upatikanaji wa rasilimali fedha.
“Hatujaridhishwa na hali ya sasa kwa sababu mahitaji ni makubwa kuliko rasilimali zilizopo. Bado tunatafuta rasilimali fedha mbadala ili kuwafikia wanafunzi wengi zaidi,” alisisitiza.
Aliwataka wanufaika wa mikopo ya bodi yake kuhakikisha wanarejesha mikopo yao kwa wakati ili kuiwezesha taasisi yake kujiendesha kwa ufanisi kwa manufaa ya wanafunzi wengi wenye uhitaji.
WAZIRI WA ULINZI AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MEJA JENERALI GIMONGE (MSTAAFU)
Promosheni ya Super Heli Yaanza Kutoa Zawadi
Tusua Kijanja na Mechi za Europa Leo
KAMATI YA BUNGE YAGUSWA NA MAONO YA DKT. SAMIA UTALII MALIKALE
“Tunaposema tunapongeza juhudi za Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kwa vitendo kama hivi. Hapa katika miaka hii mitatu Serikali yake imetoa fedha kuendeleza utalii wa malikale ikiwemo boti mpya ya kisasa ambayo watalii wanaweza kuona ndani ya maji, gati la kushuka abiria, jengo jipya la kufikia abiria na miundombinu mingine ambayo imechagiza idadi ya watalii kuongezeka hapa kutoka wastani wa 2900 hivi hadi 6,400. Haya ndio mafanikio yenye maono,” alisema Mhe. Mnzava.
Ziara hiyo pia walikuwepo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki, Naibu wake, Mhe. Dunstan Kitandula, Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi na watendaji waandamizi kutoka Idara za Wanyamapori, Malikale na Misitu.
DKT. NCHIMBI AENDESHA KIKAO CHA SEKRETERIETI YA HALMASHAURI KUU CCM TAIFA
Machi ni Mwezi wenye Neema Tu| Pata Bonasi za Kasino Mpaka Tsh 2,500,000/=
TAMWA ZNZ Yawashukuru Wadau Kufanikisha Zoezi la Utoaji Tuzo Kwa Waandishi wa Habari 2024.
MKURUGENZI Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, TAMWA ZNZ kwa niaba ya ZAFELA na PEGAO ametoa shukrani za dhati kwa wote waliochangia kufanikisha hafla ya utoaji tuzo kwa waandishi wa habari iliyofanyika Jumamosi, Machi 9, 2024, katika Ukumbi wa SHAA mjini Unguja.
Sherehe ya Kuadhimisha Miaka 40 Tangu Kuanzishwa kwa Shincheonji, Usalama na Utaratibu Bora Hata Ikiwa na Umati Zaidi ya Watu 30,000
DKT. NCHIMBI AKUTANA NA BALOZI WA CHINA MHE. CHEN MINGJIAN
KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA UJENZI BANDARI YA MWANZA KASKAZINI
Hayo yamesemwa tarehe 16 Machi, 2024 Jijini Mwanza na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Seleman Kakoso ( Mb) wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini.
“ Kamati inaridhika na usimamizi wa mradi huu pamoja na miradi mingine yote ya TPA ambayo imetembelewa. Simamieni huu mradi uweze kukamilika kwa wakati na kuwa na tija kwa Watanzania”, amesema Mhe. Kakoso.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile ( Mb) akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, amesema Wizara imepokea maoni, mapendekezo na maelekezo ya Kamati na itaenda kuyafanyia kazi na kuyatekeleza.
Mradi wa Utekelezaji wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 18.6 na utachukua miezi 18 kukamilika kwake ambapo hadi sasa umefikia Asilimia 30%.
MERIDIANBET YATOA MSAADA MWENGE
*Trilioni 2.53 yaipaisha TARURA ndani ya miaka mitatu*
Benki ya Absa yaendelea kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya Salum (kulia), akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Irene Msungu ( katikati ) kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdhamini Mkuu katika uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), wakati wa hafla iliyofanyika, Kizimkazi, Zanzibar jana. Kushoto ni Meneja wa Absa Tawi la Zanzibar, Bi. Rabia Aboud.Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada za mwezi wala makato ya miamala.
Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Irene Msungu (kushoto), akipokea tuzo ya shukurani kutoka Kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dk. Saada Mkuya Salum, Kwa kutambua mchango wa Absa kama mdhamini mkuu katika uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), wakati wa hafla iliyofanyika Kizimkazi, Zanzibar jana. Mbele kushoto ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan aliyekuwa mgeni rasmi. Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wala makato ya miamala.
Mjane wa Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Bi. Fatma Karume ( kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. mwilongo Irene Msungu ( kulia ) na Meneja wa Absa Tawi la Zanzibar, Bi. Rabia Aboud, wakati wa uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), uliodhaminiwa na Benki ya Absa na kufanyika mjini Kizimkazi, Zanzibar jana. Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wa makato ya miamala.
Baadhi ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA) uliofanyika, Kizimkazi, Zanzibar jana. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi sambamba na akaunti maalumu ya wanawake ya Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wala makato ya miamala.Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Irene Msungu (wa tatu kushoto) na Meneja wa Absa Tawi la Zanzibar, Bi. Rabia Aboud ( wa tatu kulia ) wakionyesha tuzo iliyopewa benki hiyo, kama mdhamini mkuu katika hafla ya uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), uliofanyika, Kizimkazi, Zanzibar jana.Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wala makato ya kufanya miamala.
DK. NCHIMBI AWASILI ZIMBABWE MKUTANO WA VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA
Mkutano huo ambao pia utashirikisha watendaji wakuu wa Jumuiya za Wazazi, Wanawake na Vijana wa vyama hivyo, utafanyika kwa siku tatu, kuanzia Machi 17 hadi 20, 2024, katika Mji wa Victoria Falls, kwa ajili ya kujadili agenda mbalimbali zinazohusu urafiki na uhusiano wa vyama hivyo ambavyo vyote viko madarakani, vikiongoza Serikali na Nchi husika.
Katika msafara wake, Katibu Mkuu Balozi Dk. Nchimbi ameambatana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Komredi Gilbert Kalima, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa CCM (UVCCM), Komredi Fack Raphael Lulandala, na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Zanzibar, Komredi Tunu Juma Kondo.
Mbali ya Chama Cha Mapinduzi, vyama vingine vinavyoshiriki mkutano huo ni pamoja na mwenyeji ZANU – PF (Zimbabwe), MPLA (Angola), SWAPO (Namibia), FRELIMO (Msumbiji), ANC (Afrika Kusini) na Botswana Democratic Party (BDP – cha Botswana).
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akisalimiana na kuzungumza jambo na Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia), Komredi Mama Sophia Shaningwa walipokutana mara baada ya kuwasili nchini Zimbabwe, leo mchana Machi 17, 2024, kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 11 wa Makatibu Wakuu wa Vyama Marafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, utakaofanyika nchini humo.
WANANCHI ELFU 9,659 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI MALUNGU NYASA
Mhandisi Mahundi ametoa maagizo hayo leo Machi 17, 2024 akiwa katika muendelezo wa ziara ya kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Maji Mkoani Ruvuma
Akiwa ziarani pia Mhandisi Mahundi ametoa rai kwa wananchi kuendelea kutunza vyanzo vya maji ili miradi ya maji iwe endelevu.
Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe.Jackson Kiswaga ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa usimamizi na utekelezaji wa miradi.
"Mradi huu ukamilike kwa wakati pia wananchi muweze kutunza Miundombinu yake ili mradi uwe endelevu. Lakini chombo cha watumiaji maji katika jamii kiundwe ili kiweze kukusanya fedha na kufanya matumizi mazuri ya ukarabati wa mradi pindi inapotokea mradi umeharibika"amesema Mhe.Kiswaga
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa maji Malungu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa Mhandisi Masoud Samila amesema mradi wa Malungu unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.2
Mhandisi Samila amesema kukamilika kwa mradi huo kunalenga kuwanufaisha wananchi wapatao 9,659 kutoka vijiji vya Malungu na Tingi vilivyopo katika kata ya Tingi.
" Mradi pia utasaidia kupunguza magonjwa mbalimbali ya mlipuko kwa jamii. Vilevile kutokana na kuimarika kwa huduma ya maji, jamii itapata muda wa kufanya shughuli za maendeleo"amesema Mhandisi Samila
DKT. BITEKO ASHIRIKI MISA TAKATIFU YA KUMWOMBEA HAYATI DKT. JOHN POMBE MAGUFULI CHATO
--Dkt. Samia ajenga Makumbusho ya Hayati Magufuli Chato
--Familia ya Magufuli, Mbunge Chato wamshukuru Rais
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo amejumuika na viongozi na wananchi mbalimbali katika misa Takatifu ya kumwombea Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli iliyofanyika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mt. Yohana Maria Muzeyi, wilayani Chato mkoani Geita.
Akitoa Salaam za Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Dkt. Biteko amesema kuwa, Dkt. Samia na Serikali yake inaendelea kumkumbuka Hayati Dkt. John Pombe Magufuli si tu kama Rais katika Serikali Awamu ya Tano, bali pia kama kiongozi aliyeweka misingi mbalimbali ambayo Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuitekeleza.
Ametaja miradi mbalimbali ambayo ilianzishwa katika Serikali ya Awamu ya Tano ambayo inaendelea kutekelezwa kwa kasi kubwa na Serikali ya Awamu ya Sita, ni pamoja na mradi wa umeme wa Julius Nyerere ( JNHPP) ambao sasa umeshaanza kuzalisha megawati 235, mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam ambao tayari umeshaanza kufanyiwa majaribio na ujenzi wa Daraja kubwa la Kigongo-Busisi mkoani Mwanza ambao umefikia asilimia 80.
Dkt. Biteko amewahakikishia Watanzania kuwa, masuala yaliyobuniwa na Hayati Magufuli yanaendelea na yataendelea kutekelezwa kwa kasi kubwa na Serikali ya Awamu ya Sita ili kuendelea kumuenzi kwa vitendo.
“Hayati Magufuli anasifika kote duniani kwa uwezo wake wa kiongozi, karama ya kutatua matatizo ya wananchi, kuwasikiliza wananchi, kuondoa kero, uzembe, ubadhirifu, rushwa na kuhimiza uwajibikaji serikalini, nataka niwahakikishie kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita inayasukuma masuala yote hayo ili kutoa huduma kwa ufanisi kwa watanzania.” Amesisitiza Dkt. Biteko
Vilevile, amempongeza, Mjane wa Hayati Magufuli, Mama Janet Magufuli kwa kuendelea kusimama kama mhimili wa familia na kuendelea kuunganisha na kuiongoza familia hiyo.
Kwa upande wake, Mjane wa Hayati Magufuli, Mama Janeth Magufuli amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa pamoja na familia hiyo tangu kifo cha Hayati Magufuli ambapo pia amewashukuru viongozi waliojumuika na familia katika adhimisho hilo la misa Takatifu, akieleza kuwa hiyo ni alama ya upendo kwa familia hiyo.
Naye Mbunge wa Chato, Mhe. Dkt. Medard Kalemani amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuijali wilaya ya Chato kwani pamoja kuitembelea Chato mara kwa mara, ameendelea kutoa fedha zinazotekeleza miradi mbalimbali kama ya maji, shule, afya ( hospitali ya kanda), barabara n.k
Aidha, amemshukuru Dkt. Samia kwa kuendelea kumuenzi Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna mbalimbali ikiwemo kujenga makumbusho ya Hayati Magufuli wilayani Chato ambayo itafanya historia yake na kazi alizofanya kuendelea kujulikana ndani na nje ya nchi, kizazi cha sasa na cha baadaye
Huu ni mwaka wa Tatu tangu Hayati, Dkt. John Pombe Magufuli afariki dunia tarehe 17 Machi, 2021.
Misa hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigella, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na Mbunge wa Chato, Mhe. Dkt. Medard Kalemani.
SUKA MKEKA WAKO NA MERIDIANBET LEO
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YATEMBELEA MAGHALA YA JESHI NA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI
TANZANIA NA ITALIA KUIMARISHA USHIRIKIANO SEKTA ZA KIMKAKATI
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Italia, Balozi Riccardo Guariglia akiteta jambo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbaouk (kulia) wakati wa Iftari iliyoandaliwa na Ubalozi wa Italia nchini Tanzania jana jioni Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Italia nchini, Mhe. Marco Lombardi.
JOKER ICE FRENZY EPIC KASINO YENYE BONASI KUBWA
DKT. NCHIMBI ASHIRIKI MKUTANO WA 11 WA MAKATIBU WAKUU WA VYAMA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA ( FLMS)
TAWA YATOA KONGOLE KWA RAIS DKT. SAMIA KATIKA UTATUZI WA MIGOGORO
Mashine za Kilimo: Zilizotengenezwa Italia na Zinalenga Kukuza Sekta ya Kilimo Tanzania