Quantcast
Channel: JIACHIE

TGNP WAGUSWA NA MUME KUWABAKA WANAE WAWILI, MMOJA AMPA UJAUZITO

0
0
WADAU wa Maendeleo kwa kushirikiana na Serikali wameitaka jamii kuendelea kukemea vikali vitendo vya ukatili vinavyofanywa na baadhi ya watu wasiokuwa waadilifu jambo ambalo linapelelea kuongezeka kwa mmong'onyoko wa maadili  na kuacha baadhi ya familia kukosa malezi na kuwa na hali ya tegemezi Nchini.

Akizungumza leo Machi 13, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati Wadau wa Kupinga Ukatili wa Kijinsia kutoka nchini Ethiopia walipotembelea Kituo Cha Taarifa na Maarifa Kata ya Majohe kwa lengo la kujifunza na kubadilishana changamoto za ukatili, Mwanachama wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Rehema Mwateba, amesema kuwa wakati umefika wa kuzungumza ukweli kuhusu Ukatili unaofanyika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kituo Cha Taarifa na Maarifa Kata ya Majohe Tabu Ally, amesisitiza umuhimu wa kuwachukulia hatua za kisheria wahusika wa matukio hayo na akienda mbali zaidi kuiomba serikali kuweka sheria kali juu ya watu ambao wameendelea kufanya vitendo visivyo rafiki katika jamii husika.

Aidha, aliongeza kuwa kuna hitajika jitihada za wadau mbalimbali wa maendeleo na serikali kutoa elimu kwa baadhi ya watu ambao bado wanauelewa mdogo kwenye masuala ya haki ya binadamu ili kupunguza vitendo vya ukatili, pia amewataka watumishi wa umma wakiwemo Mawaziri, Wabunge na viongozi wengine wa ngazi za juu kutembea kwenye majimbo hasa ya ngazi za nchini ili kujionea vitendo vya kikatili vinavyozidi kushamiri hasa kwa watoto wa kike wenye umri mdogo.

Naye Mkazi wa Mtaa wa Kivule Majohe Wivina Alkadi, ambaye alifanyiwa ukatili na Mume wake kwa kuwabaka wanaye wawili na mmoja kumpa ujauzito jambo ambalo lilipelekea mtuhumiwa huyo kufungwa kifungo cha miaka 60 jela ambapo ameiomba jamii iweze kumsaidia baadhi ya mahitaji ya Familia kwani anaishi katika mazingira magumu.

Pia ametumia fursa hiyo kuomba Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na watanzania kiujumla kumsaidia ili watoto wake waweze kuendelea na masomo kwani wananishindwa kusoma kutokana na hali ya maisha ambayo amekuwa akiyapitia mama huyo mara baada tu ya mume wake kuhukumiwa kifungo cha miaka 60 jela.

Huku Wadau wa Kupinga Ukatili wa Kijinsia kutoka nchini Ethiopia Rediet Asfew wamesema kuwa wataendelea kutoa ushirikiano kwa TNGP katika kufanya uwezeshaji wa kiuchumi kwa Wanawake ili kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na wadau na serikali katika kuhakikisha masuala ya ukatili yanadhibitiwa ili kumkwamua mwanamke kiuchumi .













Benki ya NMB yaimarisha mfumo wake kuongeza tija utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu

0
0

 

Na Mwandishi Wetu

Benki ya NMB imekamilisha zoezi la kuunganisha mfumo wake mkuu wa kibenki na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ikiwa ni utekelezaji wa sehemu ya dhamira ya benki hiyo kuimarisha utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.

Hatua hiyo inalenga kuwawezesha wanafunzi katika vyuo vikuu kupata bidhaa za kibenki zenye hali ya juu ya usalama, ufanisi na uvumbuzi.

Akizungumza wakati wa kongamano lililofanyika jijini Dar es Salaam jana lililoandaliwa na Bodi ya Mikopo na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa elimu chini, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NMB Filbert Mponzi alisema mfumo huo kwa kiwango kikubwa umerahisisha utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.

“Wanafunzi sasa wataweza kufurahia huduma za kibenki bila matatizo baada ya kuunganishwa kwa mfumo mkuu wa benki ya NMB na Bodi ya Mikopo. Muunganisho huu utahakikisha kuwa mikopo sasa inatolewa kwa wanafunzi kwa haraka na kwa urahisi zaidi,” Mponzi alisema.

Aliwataka wanafunzi wa vyuo vikuu kufungua akaunti na benki yake ilikunufaika na faida lukuki zikiwemo mikopo ya papo kwa papo yenye masharti nafuu kuanzia shilingi elfu moja hadi shilingi laki 5.

Mponzi wakati wa kongamano hilo alisisitiza dhamira ya benki hiyo kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali pamoja na taasisi za elimunchini ili kusaidia maendeleo ya sekta ya elimu kuanzia ngazi ya chini.

“Sekta ya elimu ni miongoni mwa vipaumbele vyetu muhimu. Ili kusisitiza dhamira yetu ya kusaidia elimu ya juu, mwaka jana tulitenga mikopo ya shilingi bilioni 200 kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kufuatia majadiliano ya karibu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,” Mponzi alisema.

Aliongeza, “Wanafunzi wanaweza kuomba mikopo kuanzia shilingi laki mbili hadi hadi shilingi milioni 10 kwa riba nafuu ya asilimia 9 tu,”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Dk.Bill Kiwia wakati wa hafla hiyo alisema lengo la kongamano hilo ni kupokea maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wanaohusika na utendaji wa utoaji wa fedha kwa taasisi yake.

Alisema kuwa bodi hiyo kwa sasa inawafikia zaidi ya wanafunzi laki mbili wenye uhitaji lakini tayari imepanga mipango ya kuwafikia wanafunzi wengi zaidi na kuongeza kuwa hata hivyo itategemea upatikanaji wa rasilimali fedha.

“Hatujaridhishwa na hali ya sasa kwa sababu mahitaji ni makubwa kuliko rasilimali zilizopo. Bado tunatafuta rasilimali fedha mbadala ili kuwafikia wanafunzi wengi zaidi,” alisisitiza.

Aliwataka wanufaika wa mikopo ya bodi yake kuhakikisha wanarejesha mikopo yao kwa wakati ili kuiwezesha taasisi yake kujiendesha kwa ufanisi kwa manufaa ya wanafunzi wengi wenye uhitaji.






WAZIRI WA ULINZI AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MEJA JENERALI GIMONGE (MSTAAFU)

0
0

 

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) leo Machi 13, 2024 ameongoza Waombolezaji kuaga Mwili wa Marehemu Meja Jenerali Christopher Keraryo Gimonge (Mstaafu) katika Hospitali Kuu ya Jeshi, Lugalo Jijini Dar Es salaam.

Akitoa salamu za rambirambi, Waziri Stergomena Tax aliwasilisha salaam za pole toka kwa Amri Jeshi Mkuu, Mhe Daktari Samia Suluhu Hassan,kwa kusema kuwa kuwa, Serikali pamoja na Jeshi limepoteza Kamanda na Kiongozi muhimu kwani wakati wa uhai wake, marehemu alilitumikia Jeshi katika nafasi mbalimbali kwa mafanikio makubwa ambapo ametoa wito wa kuiga yote mambo mema na uchapakazi aliounyesha marehemu Meja Jenerali Gimonge (Mstaafu)

Viongozi wengine waliohudhuria tukio hilo ni pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Luteni Jenerali Salum Haji Othman, Wakuu wa Majeshi Wastaafu, Majenerali, Maafisa Wakuu, Maafisa Wadogo, Askari pamoja na waombolezaji, ambapo mwili wa Meja Jenerali Gimonge umesafirishwa leo kwenda Mkoani Mara kwa maziko.













Promosheni ya Super Heli Yaanza Kutoa Zawadi

0
0

 

HATIMAYE sasa zile zawadi zilizotajwa kutolewa kwa washindi wa mchezo wa Super Heli unaopatikana kwenye kasino ya mtandaoni. Washindi mbalimbali wa TV,Smartphones, na bonasi za kasino zinazidi kutolewa, kama bado hujacheza huu mchezo basi wakati ni sasa. Cheza Super Heli Hapa.

Super Heli kasino unataka kufanana na mchezo maarufu wa AVIATOR ambao pia unapatikana Meridianbet kasino ya mtandaoni, lakini utofauti wake ni kwenye dau na muonekano, Super Heli UNARUSHA ndege ya helikopta kisha itakupa bonasi za kasino kibao.

Super Heli mchezo kutoka Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet unakufanya kuwa tajiri, cha kwanza dau lake ni kuanzia Tsh 100/= lakini pesa hii ina maajabu makubwa ambayo huwezi kuamini imetajirisha wengi ambao wamechagua kucheza huu mchezo. Jisajili hapa ili ufurahie maajabu ya Super Heli Kasino.

Zawadi na Ushindi.
Super Heli mchezo wa kasino mtandaoni kutoka kwa Expanse Studios. Katika mchezo huu, utapata bonasi za kasino kubwa. Kuna malipo ya pesa taslimu papo hapo.

Wachezaji bora wakati wa promosheni ya Super Heli watapokea zawadi zifuatazo kutoka Meridianbet:

Nafasi ya 1 - Samsung TV inchi 55.
Nafasi ya 2 - Samsung A24.
Nafasi ya 3 na ya 4 - TZS 200,000 beti za bure.
Nafasi ya 5-6 - TZS 100,000 beti za bure.
Nafasi ya 7-10 - TZS 50,000 beti za bure.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Tusua Kijanja na Mechi za Europa Leo

0
0

 

ALHAMIS ya Leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za marudiano ambapo hizi zitakuw azikiamua nani kwenda hatua inayofuata na nani kubaki. Liverpool, Milan, Leverkusen, Roma wote wapo dimbani. Suka mkeka wako sasa utusue na meridianbet.

Mechi ya kwanza kabisa itakuwa ni hii ya Slavia Prague dhidi ya AC Milan katika dimba la Fortuna Arena ambapo mechi ya kwanza walipokutan, Pioli na vijana wake waliondoka na ushindi mkubwa na jumla ya faida ya mabao mawili. Milan kushinda mechi hii amepewa ODDS 2.03 kwa 3.33. Je mwenyeji atalipa kisasi au kupindua meza?. Suka mkeka wako hapa.

Kumbuka kucheza michezo ya Kasino ya Mtandaoni ambayo inatolewa ndani ya meridianbet kama vile Poker, Roullette, Aviator, Rockertman, Keno, Sloti na mingine kibao. Ingia mchezoni na ucheze sasa.

Mechi nyingine yenye ODDS za kibabe ni hii hapa inayowakutanisha kati ya West Ham United dhidi ya SC Freiburg kutoka kule Ujerumani majira ya saa 2:45. David Moyes na vijana wake wanaingia kwenye mchezo huu huku malengo yakiwa ni kushinda tuu baada ya mechi iliyopita kupoteza. Mechi hii imepewa ODDS 1.71 kwa 4.60. Jisajili hapa.

Pesa nyingine ipo kwenye mechi hii ya Nyambizi wa Njano, Villarreal dhidi ya Olympique Marseille ambao mechi ya kwanza walishinda kwa kishindo cha ajabu. Mwenyeji ambaye anakipiga katika ligi ya Hispania ana kibarua kizito sana kwani anadaiwa mabao manne. Meridianbet wamempa nafasi ya kushinda mwenyeji kwa ODDS 2.25 kwa 2.79. Wewe unampa nani nafasi ya kushinda?.

Naye SL Benfica baada ya kulazimishwa sare mechi iliyopita akiwa nyumbani, leo hii atakuwa ugenini kusaka ushindi dhidi ya Glasgow Rangers katika dimba la Ibrox huku nafasi ya kusonga mbele wakipewa wageni kwa ODDS 2.30 kwa 2.84. Je nani ni nani leo?. Tengeneza jamvi lako sasa.

Majira ya saa 5:00 usiku Atalanta kutoka kule Italia itakipiga dhidi ya Sporting Lisbon ya Ureno. Mechi ya kwanza walipokutana walitoshana nguvu. Je leo hii aktaika dimba la Gewiss nani kuibuka kidedea?. Mechi hii ina machaguo zaidi ya 1000 ndani ya meridianbert. Bashiri na meridianbet.

Pia vijana wa Roberto De Zerbi, Brighton watapepetana dhidi ya AS Roma ambayo ina faidia ya mabao manne ambayo walioyapata kwenye mechi ya kwanza baada ya kushinda. Mwenyeji amepewa ODDS 1.71 kushinda mechi hii kwa 4.21. Je Roma atakubali kichapo leo? Au ataendeleza moto wake dhidi ya timu hii ya Uingereza? Beti kijanja hapa.

Kivumbi kingine kitakuwa kwenye mechi hii ya Liverpool dhidi ya Sparta Prague ambao mechi ya kwanza wakiwa kwao walichapika vibaya mno. Klopp na vijana wake watahitaji heshima ya kutopoteza mechi kwani wana faida kubwa. 1.27 kwa 8.62 ndio ODDS za mechi hii. Suka jamvi lako sasa.

Huku kimbembe kingine kitakuwepo kule BayArena ambapo Bayer Leverkusen chini ya Xabi Alonso watakinyuka dhidi ya Qarabag FK anbao waliwalazimisha sare mechi iliyopita. Leverkusen wakiwa kileleni pale Bundesliga wanataka kombe hili sana na meridianbet wao wamempa nafasi kubwa ya ushindi leo kwa ODDS 1.16 kwa 14.7. Weka jamvi lako hapa.

KAMATI YA BUNGE YAGUSWA NA MAONO YA DKT. SAMIA UTALII MALIKALE

0
0
Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Timotheo Mnzava leo Machi 14, 2024, imetembelea miradi inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufungua utalii wa Malikale kwenye magofu ya Kisiwa cha Kilwa Kisiwani ikiwa ni juhudi mpya za kuongeza zao jipya la utalii huo.

“Tunaposema tunapongeza juhudi za Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kwa vitendo kama hivi. Hapa katika miaka hii mitatu Serikali yake imetoa fedha kuendeleza utalii wa malikale ikiwemo boti mpya ya kisasa ambayo watalii wanaweza kuona ndani ya maji, gati la kushuka abiria, jengo jipya la kufikia abiria na miundombinu mingine ambayo imechagiza idadi ya watalii kuongezeka hapa kutoka wastani wa 2900 hivi hadi 6,400. Haya ndio mafanikio yenye maono,” alisema Mhe. Mnzava.

Ziara hiyo pia walikuwepo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki, Naibu wake, Mhe. Dunstan Kitandula, Katibu Mkuu Dkt. Hassan Abbasi na watendaji waandamizi kutoka Idara za Wanyamapori, Malikale na Misitu.



DKT. NCHIMBI AENDESHA KIKAO CHA SEKRETERIETI YA HALMASHAURI KUU CCM TAIFA

0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akiendesha Kikao cha Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kilichoketi Alhamis, Machi 14, 2024, Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam.




Machi ni Mwezi wenye Neema Tu| Pata Bonasi za Kasino Mpaka Tsh 2,500,000/=

0
0

 


HUJAWAHI kuwa mwezi wa kinyonge hata kidogo inapofika mwezi Machi. Ni promosheni na bonasi za kasino deilee. Na hatimaye unapocheza michezo ya kasino ya mtandaoni ya Meridianbet kutoka kwa mtoa huduma Evoplay unaingia kwenye nafasi ya kujishindia mgao wako mpaka 2,500,000/=

Promosheni hii ya "Zawadi za Machi" imeanza kuanzia 14.03. hadi 22.03.2024. Promo itapatikana kwa wachezaji tu waliojisajili na meridianbet. Jisajili hapa ili ufurahie promosheni hii.

Kiwango cha chini cha beti katika promosheni hii ya kasino ya mtandaoni ni TZS 500 au sawa na hiyo katika sarafu ya ndani.

Wakati wa promosheni, wachezaji watashindania jumla ya kiasi cha ushindi kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni ifuatayo kutoka kwa mtoa huduma wa Evoplay:

Penalty shoot-out, Penalty shoot-out street, Legacy of Sages, Hot Triple Sevens X, Demon Bonus Buy, Jhana of God Bonus Buy, Cursed Can Bonus Buy, Budai Reels, Cycle of Luck Bonus buy, Hot Volcano, Elven Princesses, Patrick's Magic Field, Inner Fire Bonus Buy, Temple Of Thunder II Bonus Buy, The Greatest Catch Bonus Buy, Camino de Chili Bonus Buy, Juicy Gems, Bandit Bust, Scratch Match - Book of Rest.

kiasi cha ushindi = idadi ya pointi Viwango vitaonyeshwa kwenye UI ya michezo inayoshiriki katika promosheni. Zawadi zitagawanywa kati ya nafasi za kwanza 10 kama inavyoonyeshwa:

1. TZS 750,000

2. TZS 500,000

3. TZS 375,000

4.-10. TZS 125,000 Kila mmoja.

Fedha zilizolipwa zinapatikana mara moja kwa mchezaji kwa kutoa au kucheza ofa nzima kwenye tovuti. Ofa hii inatumika kwa mtumiaji mmoja, anwani ya IP, na kaya.

Kwa maelezo Zaidi juu ya Promosheni hii, tembelea tovuti ya Meridianbet kasino ya mtandaoni, kujua unatakiwa kufanya nini ili ushinde mihela na Bonasi za Kasino kutoka Meridianbet.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

TAMWA ZNZ Yawashukuru Wadau Kufanikisha Zoezi la Utoaji Tuzo Kwa Waandishi wa Habari 2024.

0
0

 MKURUGENZI Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, TAMWA ZNZ kwa niaba ya ZAFELA na PEGAO ametoa shukrani za dhati kwa wote waliochangia kufanikisha hafla ya utoaji tuzo kwa waandishi wa habari iliyofanyika Jumamosi, Machi 9, 2024, katika Ukumbi wa SHAA mjini Unguja.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko ofisi za TAMWA ZNZ Tunguu, Mkurugenzi wa TAMWA ZNZ, Dkt. Mzuri Issa ametoa pongezi kwa waandishi wote waliowasilisha kazi zao kwa ajili ya kushiriki tunzo za umahiri wa waandishi wa habari za wanawake na uongozi.

Tuzo hizo zilitolewa katika vipengele vinne tofauti ikiwemo Radio Jamii, Radio za kitaifa, magazeti pamoja na mitandao ya kijamii ambapo habari zilizowasilishwa zilikua zikiangazia maeneo mbalimbali ya kupigania haki za wanawake na mabadiliko.

Washindi wa tuzo hizo walizawadiwa zawadi ya vyeti, ngao pamoja na fedha taslim ambapo mshindi wa jumla ni Amina Masoud aliyezawadiwa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tatu za Kitanzania, ikionesha kutambuliwa kwa mchango wake wa kipekee katika tasnia hiyo.

Akizungumza wakati wa mkutano huo Jaji Mkuu wa Tuzo hizo Dkt. Abdalla Mohammed Juma alisema waandishi wa habari wanawake wameonesha muamko mkubwa katika kuwasilisha kazi zao ambapo katika waandishi wote walioleta kazi wanawake walikua ni 379.

Dkt. Abdalla aliongeza kuwa kazi hiyo ya kuwatafuta washindi wameifanya kwa uadilifu mkubwa kuhakikisha washindi waliopatikana ni wale waliowasilisha kazi zenye ubora.

“Kazi tuliyopewa tumeifanya kwa uadilifu mkubwa, na kama kuna mapungufu ni sisi majaji tunayabeba mapungufu hayo kwa asilimia 100”, Dr. Abdalla Mohammed alisema Jaji.

Bi Nasra Mohammed, mwandishi wa habari mkongwe ambae pia alikua ni miongni mwa majaji amewahimiza waandishi kuandika kazi zao katika viwango vya juu ili kuweza kuisaidia jamii katika masuala hayo ya takwimu.

"Sisi waandishi wa habari tufanye kazi kwa bora na zenye viwango kila siku ili kuweza kuipasha jamii taarifa sahihi zilizoshiba na kuleta tija katika jamii." Alisema Bi Nasra

Mwisho Dkt Mzuri alitoa wito kwa waandishi wa habari kuendelea kuandika habari zinazohusiana na wanawake, ikiwa ni pamoja na changamoto zinazokwamisha upatikanaji wa nafasi za uongozi.

Huu ni mwaka wa tatu mfululizo kufanyika kwa tuzo hizi, na kwa mwaka huu kumekua na ongezeko kubwa la idadi ya kazi zilizowasilishwa ambapo jumla ya kazi 529 kutoka vyombo vya habari mbalimbali Zanzibar ziliwasilishwa.

Tuzo hizi zinafanyika ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi ambao unatekelezwa na TAMWA ZNZ, ZAFELA na PEGAO kwa ushirikiano mkubwa na ubalozi wa Norway ambapo Kaulimbiu ya Tuzo hizi ni "Kalamu Yangu, Mchango Wangu kwa Wanawake" inayoakisi dhamira endelevu ya waandishi wa habari kuongeza sauti za wanawake na kuchangia katika maendeleo yao.

Sherehe ya Kuadhimisha Miaka 40 Tangu Kuanzishwa kwa Shincheonji, Usalama na Utaratibu Bora Hata Ikiwa na Umati Zaidi ya Watu 30,000

0
0

 

Asubuhi ya tarehe 14, Mwenyekiti Man-hee Lee anatoa mahubiri wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 40 iliyofanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Amani cha Shincheonji huko Cheongpyeon g.
Wakati sherehe ya kuadhimisha miaka 40 ilifanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Amani cha Shincheonji huko Cheongpyeong asubuhi ya tarehe 14, waumini wanasonga mbele chini ya mwongozo wa usalama ili kuhudhuria katika eneo.
Sherehe ya kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwake inafanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Amani cha Cheongpyeong Shincheonji asubuhi ya tarehe 14.
Asubuhi ya tarehe 14, sherehe ya kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwake inafanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Amani cha Cheongpyeong Shincheonji. [Picha imetolewa na Shincheonji Kanisa la Yesu]


MNAMO Machi 14, sherehe ya kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 ya uanzilishi ulifanyika katika kituo cha mafunzo ya Amani cha Cheongpyeong Shincheonji

Zaidi ya wahudhuriaji 30,000 kwente tukio... Washiriki wa kanisa kutoka nyumbani na nje ya nchi walishiriki kwa wakati mmoja kupitia matangazo ya moja kwa moja ya mtandaoni.

Wakati Kanisa la Shincheonji la Yesu, Hekalu la Hema ya Ushuhuda (Mwenyekiti n Lee Man-hee) walifanya sherehe na ibada ya ukumbusho katika Kituo cha Mafunzo ya Amani cha Cheongpyeong Shincheonji kusherehekea kumbukumbu ya miaka 40. , usimamizi wake bora wa usalama na matengenezo ya utaratibu mara nyingine tena uling'aa.

Sherehe ya kuadhimisha siku hii ilitayarishwa kama fursa ya kutazama nyuma ukuaji wa Kanisa la Shincheonji la Yesu tangu kuanzishwa kwake Machi 14, 1984 na kumtukuza Mungu. Zaidi ya hayo, mipango na maono ya mwaka ujao yalishirikiwa, na ahadi zilifanywa ili kutimiza wajibu wa kanisa katika jumuiya za kiraia na kutumika na kufanya mazoezi kama nuru na chumvi.

Takriban watakatifu 30,000 walihudhuria hafla hiyo, na ilitangazwa moja kwa moja kutoka kwenye sehemu hiyo na kurushwa wakati huohuo katika nchi 66, pamoja na Korea.

Kanisa la Shincheonji Kanisa la Yesu lilisema kwamba, kwa kuzingatia idadi kubwa ya watu waliokusanyika ikilinganishwa na saizi ya eneo, walitayarisha hafla hiyo kwa kudumisha utaratibu na usimamizi wa usalama wa waliohudhuria kama kipaumbele cha juu. Waandaaji walianzisha mpango wa kina wa usimamizi wa usalama, unaoakisi uzoefu wa kufanya mara tatu za sherehe za kuhitimu 100,000 kwa usalama na kwa utulivu. Kusanyiko pia lilionyesha usikivu wa hali ya juu wa kiraia, lilifuata kikamilifu mwongozo , na kusaidia kudumisha utaratibu mzuri.

Ibada ya kuadhimisha siku hii ilifanyika kwa utaratibu ufuatao:

▲ Utangulizi wa tukio la maadhimisho ya miaka 40

▲ Video ya ukumbusho

▲ Ripoti juu ya historia ya Shinc heonji, Ikifuatiwa na mahubiri ya Mwenyekiti Lee.

Mwenyekiti Lee alieleza maana na ukuaji huo thabiti, akisema, "(Kanisa la Shincheonji la Yesu) lilikuwa na mwanzo mnyenyekevu sana. Hata hivyo, watu wengi wamekuja hadi leo kwa sababu Mungu alituma malaika kutoka mbinguni kama inavyoelezwa katika Biblia. " .

Aliendelea kusema, “Yesu naye alitoa mwili wake wote na kutaka kufanya mapenzi ya Mungu. Hivyo basi, hatupaswi kuwa na imani kipofu, bali ni lazima tumjue Mungu na matakwa yetu na mapenzi Yake yatimizwe.” Aliongeza, “Lazima tufuate mapenzi ya Mungu na kuwapenda jirani zetu.” alisisitiza

Mwisho alisema, "Idadi ya watu wanaojifunza kuhusu kitabu cha Ufunuo ambacho ni kusudi la Mungu lililoandikwa katika Biblia inaongezeka. Nashukuru," na kuongeza, "Tuhakikishe watu wengi zaidi wanaokolewa kupitia Neno. kufanya kazi pamoja ili kuunda Dunia njema."

Alasiri hii, maonyesho ya sherehe yaliyotayarishwa na makabila 12 yaliendelea kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa Shincheonji.

Wakati huo huo, Kanisa la Shincheonji la Yesu limepata maendeleo endelevu bila kuwa na muda kutokuongezeka tangu kuanzishwa kwake, licha ya hali ya kudumaa kwa ukristo duniani. Tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Misheni cha kikristo cha sayuni huko Sadang, Seoul mnamo Juni 1990, kumekuwa na ongezeko la mara kwa mara la idadi ya wahitimu. Katika sherehe ya kuhitimu darasa la 110 mnamo 2019, wahitimu 103,764 walihitimu, na kufungua enzi ya wahitimu 100,000. Baadaye, mnamo 2022 na 2023, wanafunzi 106,186 na 108,084 walimaliza kozi hiyo, na kupata uandikishaji zaidi ya wanafunzi 100,000 kwa miaka miwili mfululizo.

Wakati huo huo, kama matokeo ya kukuza ubadilishanaji wa neno na thamani ya ukuaji wa pamoja kupitia maelewano na jumuiya za kidini ndani na nje ya nchi, MOU ya kubadilishana neno ilitiwa saini na makanisa 443 nchini Korea na makanisa 9,462 katika nchi 77 nje ya nchi. Baada ya kubadilishana neno, makanisa 1,382 katika nchi 38 yalitambua ubora wa neno kwa kubadilisha ishara zao hadi Shincheonji Kanisa la Yesu.

Afisa kutoka Kanisa la Shincheonji Kanisa la Yesu alisema, “Tunapotayarisha tukio hilo tulizingatia kuhusu usalama na utaratibu, tunahisi tumebarikiwa kwa maendeleo mazuri ya tukio hilo. Pia alisema, “Tungependa kutoa shukrani zetu kwa waumini walioshiiriki kikamilifu katika mwongozo huo,” na akaongeza, “Mwaka huu, tutajiimarisha kama kanisa linaloweka mfano kwa jamii na kutimiza wajibu wake wa kijamii kama jumuiya ya kanisa, na kuwa kanisa ambalo ni nuru na chumvi.”

DKT. NCHIMBI AKUTANA NA BALOZI WA CHINA MHE. CHEN MINGJIAN

0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi amekutana na Balozi wa China nchini, Mhe. Chen Mingjian, leo Ijumaa, Machi 14, 2024, Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam na kufanya mazungumzo juu ya masuala mbalimbali yanayohusu uhusiano na urafiki wa kidugu kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na Tanzania na China.



KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA UJENZI BANDARI YA MWANZA KASKAZINI

0
0
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini iliyopo Jijini Mwanza.

Hayo yamesemwa tarehe 16 Machi, 2024 Jijini Mwanza na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Seleman Kakoso ( Mb) wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini.

“ Kamati inaridhika na usimamizi wa mradi huu pamoja na miradi mingine yote ya TPA ambayo imetembelewa. Simamieni huu mradi uweze kukamilika kwa wakati na kuwa na tija kwa Watanzania”, amesema Mhe. Kakoso.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile ( Mb) akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, amesema Wizara imepokea maoni, mapendekezo na maelekezo ya Kamati na itaenda kuyafanyia kazi na kuyatekeleza.

Mradi wa Utekelezaji wa ujenzi, upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Mwanza Kaskazini unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 18.6 na utachukua miezi 18 kukamilika kwake ambapo hadi sasa umefikia Asilimia 30%.






MERIDIANBET YATOA MSAADA MWENGE

0
0

 

MABINGWA wa michezo ya kubashiri kampuni ya Meridianbet leo mapema wamefanikiwa kufika katika eneo la Mwenge jiji Da-es-salaam na kutoa msaada kwenye Zahanati inayopatika eneo hilo ikifahamika kama Mlalakuwa.

Huu ni utaratibu ambao Meridianbet imekua miaka na miaka wa kuhakikisha wanarudisha kwenye jamii yake, Ndivyo walivyofanya leo baada kufika kwenye Zahanati ya Mlalakuwa na kutoa msaada wa vifaa vya kuhifadhia takataka (Dustbins) ili kuimarisha usafi kwenye Zahanati hiyo.

Meridianbet wamefanya hivo kwakua hospitali ni sehemu ambayo inatoa huduma za kiafya hivo itakua sio jambo la busara kama sehemu ya kutoa huduma za kiafya ikawa sehemu ya kuharibu afya kwasababu ya uchafu, Na ndio maana mabingwa hao wa michezo ya kubashiri wameamua kutoa msaada wa vifaa vya kuhifadhi takataka.

Aidha mkuu wa kitengo cha mawasiliano na masoko kutoka Meridianbet Bi. Nancy Ingram alipata wasaa wa kuongea baada ya kutoa msaada wa vifaa hivo "Meridianbet tunajua na tunathamini sana umuhimu wa Utunzaji wa Mazingira hasa hasa katika zahanati, Kama wadau wa utunzaji wa mazingira tutaendelea kuimarisha na kuhamasisha zaidi utunzaji wa mazingira."

"Pia tunashukuru Uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Mlalakuwa na Uongozi wa Zahanati ya Mlalakuwa kuungana na sisi katika zoezi hili nakutuunga mkono katika hili tulilolifanya leo”

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye ligi mbalimbali barani ulaya na dunia kwa ujumla. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Mganga Mfawidhi katika Zahanati hiyo ya Mlalakuwa inayopatikana maeneo ya Mwenge Bi. Zamzam Said Omar alipata nafasi ya kuzungumza na kutoa shukrani zake kwa Meridianbet “Kiukweli ningependa kuwashukuru sana Meridianbet kutuchagua sisi Zahanati ya Mlalakuwa kua moja ya Zahanati ambazo zimepata msaada huu, Lakini kubwa zaidi ni sisi tutahakikisha tunaimarisha usafi eneo hili kwani kwa msaada huu mmetupa sisi deni asanteni sana”.

*Trilioni 2.53 yaipaisha TARURA ndani ya miaka mitatu*

0
0
Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa akielezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha huduma za AfyaMsingi, Elimumsingi na miundombinu.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto akielezea  namna mradi wa DMDP-1 ilivyo wanufaisha wakazi wa Dar es Salaama


*Mameya wa Ilala na Kinondoni wafurahia mradi wa DMDP*

Na. Catherine Sungura, Dar es Salaam

Katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, bajeti ya kuboresha miundombinu chini ya TARURA takribani Trilioni 2.53 zimepokelewa kwaajili ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara za vijijini na mijini.

Hayo yameelezwa  na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akielezea mafanikio ya miaka mitatu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mkoani Dar es Salaam.

Mhe. Mchengerwa alisema nyakati ambayo Serikali imefanya kazi kubwa upande wa miundombinu ni kipindi cha Awamu ya Sita ndio maana Rais aliliona hilo na kuongeza bajeti ya TARURA.

Alitaja mafanikio ya ujenzi wa barabara za lami na miradi ya kimkakati, zimejengwa barabara za Lami Km 819.22 ambazo zimeongeza mtandao wa barabara za lami toka Km 2,404.90 hadi Km 3,224.12.

“Wakati wa Baba wa Taifa alipoanzisha msingi wa kukuza miji kupitia dhana ya ujamaa, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendeleza misingi  ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere”.

Kwa upande wa ujenzi wa barabara za changarawe Waziri Mchengerwa alisema Km 11,924.36 zimejengwa na kuongezeka mtandao wa barabara za changarawe toka Km 29,183.17 hadi Km 41,107.52 na ujenzi wa Madaraja Wakala imejenga madaraja makubwa sita (6) ambayo ni ya Berega (140m) -(Kilosa,) Msadya (60m) -(Mpimbwe DC), Mwasanga (40m)- (Mbeya) yamejengwa na yanatumika.  

“Rais amewagusa wananchi wengi wa vijijini kwa  ujenzi wa madaraja ya Kiwila-(40m)-Ileje, Mkomanzi-Korogwe (60m) na Kalambo (80m)-(Kalambo) ujenzi ambao unaendelea kukamilishwa, tunawapongeza TARURA”.

Aidha, alitaja mafanikio mengine ni ujenzi wa barabara na madaraja kwa kutumia malighafi za ujenzi zinazopatikana maeneo ya kazi zinapotekelezwa kama mawe, matofali ya kuchoma, ujenzi wa barabara kwa kutumia mawe.

“Mpaka sasa jumla ya Km 23.18 za Barabara ya Mawe zimejengwa kwa gharama ya bilioni 8.1 ambapo ni sawa na bilioni 12.8 kama tungetumia lami nyepesi (double surface dressing) na bilioni 33.6 kama tungetumia lami ya zege (Asphat Concrete)”, aliongeza kusema
 
Vilevile  alisema ujenzi wa madaraja kwa kutumia mawe ni mojawapo ya kipaumbele cha TARURA ni kutumia malighafi zinazopatikana maeneo ya kazi ili kupata ufanisi wa gharama za ujenzi. 

Hata hivyo alisema hadi Mwezi Februari, 2024 TARURA imejenga madaraja 226 ya mawe yenye thamani ya bilioni 12.52 ambapo gharama imepungua kwa zaidi ya asilimia 50.

Wakala unaendelea kufanya majaribio ya teknolojia mbalimbali ili kutumia udongo uliopo eneo la kazi badala ya kusomba kutoka maeneo mengine ya mbali. 

Hadi sasa kwa kutumia Teknolojia ya ECOROADS zimejengwa Km 22 na ujenzi upo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji.

Naye, Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto alisema ndani ya miaka mitatu mradi wa DMDP kwa wilaya ya Ilala umeweza kuondosha kero za barabara kwa wakazi wengi wa Ulongoni hadi Gogolamboto ambao awali walijiona wametengwa.

Alisema walipata bilioni 17.6 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na mifereji na hivyo kuweza kuondoa changamoto na kuifanya Ilala kufunguka.

Wakati huo huo Naibu Meya wa Kinondoni, Mhe. Joseph Rugasira alisema DMDP-1 walipata ujenzi wa barabara Km 55 na mitaro zaidi ya Km 8.9 na kufanya  maeneo mengi ya Mwananyamala, Tandale na Kinondoni kwa ujumla kupendeza.

“Tunampongeza Mhe. Rais kwani DMDP-2 itaenda kutatua changamoto za barabara na wananchi wanafurahia kuona maendeleo katika miundombinu”.
Wataalamu kutoka TARURA wakiongozwa na Mtendaji Mkuu Mhandisi Victor Seff wakiwa kwenye mjadala wa kuelezea mafanikio ya TARURA.

Benki ya Absa yaendelea kuwawezesha wanawake kiuchumi.

0
0

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Saada Mkuya Salum (kulia), akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Irene Msungu ( katikati ) kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama  mdhamini Mkuu katika uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), wakati wa hafla iliyofanyika, Kizimkazi, Zanzibar jana. Kushoto ni Meneja wa Absa Tawi la Zanzibar, Bi. Rabia Aboud.Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi  sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya  Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada za mwezi wala makato ya miamala.

Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Irene Msungu (kushoto), akipokea tuzo ya shukurani kutoka Kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dk. Saada Mkuya Salum, Kwa kutambua mchango wa Absa kama mdhamini mkuu katika uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), wakati wa hafla iliyofanyika Kizimkazi, Zanzibar jana. Mbele kushoto ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan aliyekuwa mgeni rasmi. Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi  sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya  Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wala makato ya miamala.

Mjane wa Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Bi. Fatma Karume ( kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. mwilongo Irene Msungu ( kulia ) na Meneja wa Absa Tawi la Zanzibar, Bi. Rabia Aboud,  wakati wa uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), uliodhaminiwa na Benki ya Absa na kufanyika mjini Kizimkazi, Zanzibar jana. Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi  sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya  Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wa makato ya miamala.

Baadhi ya washiriki  wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA) uliofanyika, Kizimkazi, Zanzibar jana. Benki ya Absa ilikuwa mdhamini mkuu wa uzinduzi huo.Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi  sambamba na akaunti maalumu ya wanawake ya  Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wala makato ya miamala.

Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi ya Benki ya Absa Tanzania, Bi. Mwilongo Irene Msungu (wa tatu kushoto) na Meneja wa Absa Tawi la Zanzibar, Bi. Rabia Aboud ( wa tatu kulia ) wakionyesha tuzo iliyopewa benki hiyo, kama mdhamini mkuu katika hafla ya  uzinduzi wa Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), uliofanyika, Kizimkazi, Zanzibar jana.Hii ni moja ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwezesha wanawake kiuchumi  sambamba na akaunti maalumu Ya wanawake ya  Absa She account, iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo haina ada ya mwezi wala makato ya kufanya miamala.



DK. NCHIMBI AWASILI ZIMBABWE MKUTANO WA VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA

0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akiambatana na baadhi ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu CCM ya CCM ya Taifa (NEC), amewasili nchini Zimbabwe kushiriki Mkutano wa 11 wa Makatibu Wakuu wa Vyama Marafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika (FLMS), ambao pamoja na masuala mengine utajadili maendeleo ya mshikamano wao na kuuendelea kuuimarisha zaidi.

Mkutano huo ambao pia utashirikisha watendaji wakuu wa Jumuiya za Wazazi, Wanawake na Vijana wa vyama hivyo, utafanyika kwa siku tatu, kuanzia Machi 17 hadi 20, 2024, katika Mji wa Victoria Falls, kwa ajili ya kujadili agenda mbalimbali zinazohusu urafiki na uhusiano wa vyama hivyo ambavyo vyote viko madarakani, vikiongoza Serikali na Nchi husika.

Katika msafara wake, Katibu Mkuu Balozi Dk. Nchimbi ameambatana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Komredi Gilbert Kalima, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana wa CCM (UVCCM), Komredi Fack Raphael Lulandala, na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Zanzibar, Komredi Tunu Juma Kondo.

Mbali ya Chama Cha Mapinduzi, vyama vingine vinavyoshiriki mkutano huo ni pamoja na mwenyeji ZANU – PF (Zimbabwe), MPLA (Angola), SWAPO (Namibia), FRELIMO (Msumbiji), ANC (Afrika Kusini) na Botswana Democratic Party (BDP – cha Botswana).


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akisalimiana na kuzungumza jambo na Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia), Komredi Mama Sophia Shaningwa walipokutana mara baada ya kuwasili nchini Zimbabwe, leo mchana Machi 17, 2024, kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 11 wa Makatibu Wakuu wa Vyama Marafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, utakaofanyika nchini humo.





WANANCHI ELFU 9,659 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI MALUNGU NYASA

0
0
NAIBU Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi amemuagiza Meneja wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga, kuhakikisha anapeleka huduma ya maji kwenye vitongoji ambavyo bado havina huduma ya maji.

Mhandisi Mahundi ametoa maagizo hayo leo Machi 17, 2024 akiwa katika muendelezo wa ziara ya kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Maji Mkoani Ruvuma

Akiwa ziarani pia Mhandisi Mahundi ametoa rai kwa wananchi kuendelea kutunza vyanzo vya maji ili miradi ya maji iwe endelevu.

Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Mhe.Jackson Kiswaga ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa usimamizi na utekelezaji wa miradi.

"Mradi huu ukamilike kwa wakati pia wananchi muweze kutunza Miundombinu yake ili mradi uwe endelevu. Lakini chombo cha watumiaji maji katika jamii kiundwe ili kiweze kukusanya fedha na kufanya matumizi mazuri ya ukarabati wa mradi pindi inapotokea mradi umeharibika"amesema Mhe.Kiswaga

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa maji Malungu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa Mhandisi Masoud Samila amesema mradi wa Malungu unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.2

Mhandisi Samila amesema kukamilika kwa mradi huo kunalenga kuwanufaisha wananchi wapatao 9,659 kutoka vijiji vya Malungu na Tingi vilivyopo katika kata ya Tingi.

" Mradi pia utasaidia kupunguza magonjwa mbalimbali ya mlipuko kwa jamii. Vilevile kutokana na kuimarika kwa huduma ya maji, jamii itapata muda wa kufanya shughuli za maendeleo"amesema Mhandisi Samila



DKT. BITEKO ASHIRIKI MISA TAKATIFU YA KUMWOMBEA HAYATI DKT. JOHN POMBE MAGUFULI CHATO

0
0
--Asema Rais, Dkt. Samia anatekeleza kwa kasi kubwa misingi iliyowekwa na Hayati Magufuli
--Dkt. Samia ajenga Makumbusho ya Hayati Magufuli Chato
--Familia ya Magufuli, Mbunge Chato wamshukuru Rais

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo amejumuika na viongozi na wananchi mbalimbali katika misa Takatifu ya kumwombea Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli iliyofanyika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mt. Yohana Maria Muzeyi, wilayani Chato mkoani Geita.

Akitoa Salaam za Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Dkt. Biteko amesema kuwa, Dkt. Samia na Serikali yake inaendelea kumkumbuka Hayati Dkt. John Pombe Magufuli si tu kama Rais katika Serikali Awamu ya Tano, bali pia kama kiongozi aliyeweka misingi mbalimbali ambayo Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuitekeleza.

Ametaja miradi mbalimbali ambayo ilianzishwa katika Serikali ya Awamu ya Tano ambayo inaendelea kutekelezwa kwa kasi kubwa na Serikali ya Awamu ya Sita, ni pamoja na mradi wa umeme wa Julius Nyerere ( JNHPP) ambao sasa umeshaanza kuzalisha megawati 235, mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam ambao tayari umeshaanza kufanyiwa majaribio na ujenzi wa Daraja kubwa la Kigongo-Busisi mkoani Mwanza ambao umefikia asilimia 80.

Dkt. Biteko amewahakikishia Watanzania kuwa, masuala yaliyobuniwa na Hayati Magufuli yanaendelea na yataendelea kutekelezwa kwa kasi kubwa na Serikali ya Awamu ya Sita ili kuendelea kumuenzi kwa vitendo.

“Hayati Magufuli anasifika kote duniani kwa uwezo wake wa kiongozi, karama ya kutatua matatizo ya wananchi, kuwasikiliza wananchi, kuondoa kero, uzembe, ubadhirifu, rushwa na kuhimiza uwajibikaji serikalini, nataka niwahakikishie kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita inayasukuma masuala yote hayo ili kutoa huduma kwa ufanisi kwa watanzania.” Amesisitiza Dkt. Biteko

Vilevile, amempongeza, Mjane wa Hayati Magufuli, Mama Janet Magufuli kwa kuendelea kusimama kama mhimili wa familia na kuendelea kuunganisha na kuiongoza familia hiyo.

Kwa upande wake, Mjane wa Hayati Magufuli, Mama Janeth Magufuli amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa pamoja na familia hiyo tangu kifo cha Hayati Magufuli ambapo pia amewashukuru viongozi waliojumuika na familia katika adhimisho hilo la misa Takatifu, akieleza kuwa hiyo ni alama ya upendo kwa familia hiyo.

Naye Mbunge wa Chato, Mhe. Dkt. Medard Kalemani amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuijali wilaya ya Chato kwani pamoja kuitembelea Chato mara kwa mara, ameendelea kutoa fedha zinazotekeleza miradi mbalimbali kama ya maji, shule, afya ( hospitali ya kanda), barabara n.k

Aidha, amemshukuru Dkt. Samia kwa kuendelea kumuenzi Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna mbalimbali ikiwemo kujenga makumbusho ya Hayati Magufuli wilayani Chato ambayo itafanya historia yake na kazi alizofanya kuendelea kujulikana ndani na nje ya nchi, kizazi cha sasa na cha baadaye

Huu ni mwaka wa Tatu tangu Hayati, Dkt. John Pombe Magufuli afariki dunia tarehe 17 Machi, 2021.

Misa hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigella, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa na Mbunge wa Chato, Mhe. Dkt. Medard Kalemani.





SUKA MKEKA WAKO NA MERIDIANBET LEO

0
0

 


BAADA ya ligi kibao kupigwa hapo jana, hatimaye leo hii mwendo ni ule ule hakuna kupoa yani si Ujerumani, Uingereza, Italia na kwingineko mechi kibao za pea zipo meridianbet. Ingia na ubashiri sasa

Uingereza pale kutakuwa na mchezo mmoja wa EPL ambapo West Ham United atamkaribisha Aston Villa nyumbani kwake katika dimba la London kusaka pointi tatu muhimu. Vijana wa Moyes wapo nafasi ya 7 na vijana wa Unai wapo nafasi ya 4. Meridianbet wamempa mwenyeji nafasi kubwa ya kushinda kwa ODDS 2.55 kwa 2.60. Wewe unampa nani?. Beti sasa hapa.

Ligi nyingine ni ya LALIGA ambapo mapema tuu majira ya saa 10:00 jioni Sevilla atakiwasha dhidi ya Celta Vigo huku mara ya mwisho kukutana walitoshan nguvu. Mwenyeji kapewa 1.90 kushinda mchezo huu kwa 4.01. Je nani kuondoka na ushindi hii leo. Jisajili hapa.

Kumbuka kucheza michezo ya Kasino ya Mtandaoni ambayo inatolewa ndani ya meridianbet kama vile Poker, Roullette, Aviator, Rockertman, Keno, Sloti na mingine kibao. Ingia mchezoni na ucheze sasa.

Saa 12:15 Villarreal watapepetana dhidi ya Valencia ambapo timu zote mbili zimetoka kushinda mechi zao zilizopita. Nyambizi wa njano wapo nafasi ya 12 na mgeni wake yupo nafasi ya 8. Mara ya mwisho kukutana, Valencia alishinda. Je leo hii mwenyeji kulipa kisais?. Mechi hii imepewa ODDS KUBWA, bashiri sasa.

Usiku wa saa 5:00 Barcelona ya Xavi itakiwasha dhidi ya Atletico Madrid ya Simeone Diego ambao wapo nafasi ya 5 kwenye ligi. Atletico kushinda mechi hii wamepewa ODDS 2.21 kwa 2.99. Je mwenyei atalipa kisasi leo baada ya kupoteza mechi ya kwanza walipokutana?. Tengeneza mkeka wako hapa.

Vilevile ligi kuu ya Italia SERIE A, itaendelea hii leo kwa mechi kadhaa AC Milan atakuwa ugenini hii leo kusaka alama tatu dhidi ya Hellas Verona ambao wapo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi. Pioli na vijana wake wamepewa ODDS 1.62 kwa 5.48 kushinda mechi hii. Suka mkeka na meridianbet leo.

Saa 2:00 Atalanta atakuwa katika dimba la Gewiss kukichapa dhidi ya Fiorentina ambao wamepewa ODDS 3.82 kwa 1.91 kushinda mecgi hii. Gasperini na vijana wake wapo nafasi ya 6 kwa ya 8 huku tofauti ya pointi ikiwa ni 4 pekee. Je unadhani alama tatu zinaenda kwa nani leo?. Bashiri kijanja hapa.

Nao AS Roma watamenyana dhidi ya Sassuolo Calcio ambao wanashika nafasi ya 19 kwenye msimamo wa ligi. Mwenyeji yupo nafasi ya 5 na 1.42 ndio ODDS yake ya ushindi kwa 7.05. Weka mkeka wako sasa.

Na mechi kati Itali leo hii ni hii hapa ambayo inawakutanisha kati ya kinara wa ligi hiyo Inter Milan dhidi ya bingwa mtetezi ambaye amepoteana msimu huu Napoli. Mechi hiyo itapigwa katika dimba la Giuseppe Meazza huku Inzaghi baada ya kutolewa UEFA sasa anaelekeza nguvu huku akiwa na ODDS ya 1.60 kwa 5.09. Mara ya mwisho Inter alishinda, je leo hii atashinda pia?. Suka mkeka hapa.

BUNDESLIGA moto utawaka kama kawaida baada ya jana mechi kibao kupigwa leo hii zitapigwa mechi mbili katika viwanja tofauti, SC Freiburg atamulaika kinara wa ligi hiyo Bayer Leverkusen ambao hawajapoteza mechi yoyote msimu huu. Tofauti ya pointi kati yao ni pointi 34 huku ODS zao ikiwa ni 5.88 kwa mwenyeji na 1.50 kwa mgeni. Jisajili na ubeti hapa.

Saa 1:30 usiku Borussia Dortmund uso kwa uso dhidi ya Eintracht Frankfurt huku timu zote zikiwa zimetoka kushinda mechi zao zilizopita. Dortmund yupo nafasi ya 5 na mgeni wake yupo nafasi ya 6, tofauti ya pointi ni 7. 1.59 kwa 4.90 ndio ODDS za mechi hii. Beti sasa.

Na sasa tunamulika ligi kuu ya Ufaransa LIGUE 1 ambapo leo hii huku kuna mechi nyingi za pesa kuanzia mechi ya AS Monaco dhidi ya FC Lorient ambapo mwenyeji anapendelewa kushinda mechi hii akiwa na ODDS 1.32 kwa 7.84. Mara ya mwisho walitoa sare. Je nani kuibuka kidedea leo?

Huku mechi nyingine itakuwa saa 1:05 Stade Rennes itakipiga dhidi ya Olympique Marseille ambaye yupo nafasi ya 7 kwenye ligi. Tofauti ya pointi ni 3 pekee ambapo leo hii kila mtu anahitaji ushindi kusonga mbele. 2.65 kwa 2.60 ndio ODDS za mechi hii bashiri sasa.

Naye bingwa mtetezi wa ligi hiyoPSG atakuwa ugenini leo dhidi ya Montpellier ambao wametoka kushinda mchezo wao uliopita. Paris wamekuwa na matokeo ambayo hayaridhidi mechi zao tatu zilizopita za ligi na leo wana ODDS 1.52 kwa 5.29. Je na leo wataangusha pointi. Suka jamvi lako hapa.



KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YATEMBELEA MAGHALA YA JESHI NA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI

0
0
*Wafurahishwa Na Utekelezaji Wa Miradi Hiyo
WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Stergomena Tax, leo Machi 16, 2024 ameshiriki katika ziara ya Kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya mambo ya Nje,Ulinzi na Usalama kukagua miradi ya maendeleo unayoendeshwa na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga kupitia Jeshi la Ulinzi wa Tanzania Maghala ya Kuifadhia VIfaa ya Gongolamboto na Chuo cha Ulinzi wa Taifa, Kunduchi, Dar-es-salaam.

Kamati hiyo ya Bunge ya Nje,Ulinzi na Usalama iliongozwa na Mwenyekiti wake Mheshimiwa Vita Rashid Mfaume Kawawa ilikagua utekelezaji wa mradi wa maghala mapya yanayojengwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kambi ya Gongolamboto na baadaye kamati hiyo pamoja na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ilitembelea Chuo cha Taifa cha Ulinzi ambapo pia ilikagua mradi wa Ujenzi wa nyumba za makazi za washiriki wa kozi za chuo hicho.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nje ,Ulinzi na Usalama iliipongeza Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa katika kusimamia miradi hiyo ya Kimkakati Jeshini na kwa kuhakikisha pesa inayotolewa na Serikali inatimiza malengo yaliyokusudiwa. Aidha Kamati hiyo ya Bunge imeonyesha kufurahishwa Ubora wa majengo na Maghala hayo yanayojengwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania.










X

TANZANIA NA ITALIA KUIMARISHA USHIRIKIANO SEKTA ZA KIMKAKATI

0
0

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Italia, Balozi Riccardo Guariglia akiteta jambo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbaouk (kulia) wakati wa Iftari iliyoandaliwa na Ubalozi wa Italia nchini Tanzania jana jioni Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Italia nchini, Mhe. Marco Lombardi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbaouk akistoa hotuba yake wakati wa Iftari iliyoandaliwa na Ubalozi wa Italia nchini Tanzania jana jioni Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbaouk akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Italia, Balozi Riccardo Guariglia wakati wa Iftari iliyoandaliwa na Ubalozi wa Italia nchini Tanzania jana jioni Jijini Dar es Salaam


SERIKALI ya Tanzania na Italia zimeahidi kuimarisha ushirikiano katika sekta za kimkakati ambazo ni kilimo, nishati, elimu pamoja na uchumi wa buluu kwa maslahi ya pande zote mbili.


Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbaouk (Mb.) alipokutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Italia, Balozi Riccardo Guariglia wakati wa Iftari iliyoandaliwa na Ubalozi wa Italia nchini Tanzania jana jioni.


Balozi Mbarouk ameipongeza Serikali ya Italia kwa kuipa Serikali ya Tanzania kipaumbele cha kuwa moja kati ya nchi nne za Bara la Afrika zitakazonufaika na mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan). “Tanzania tunaamini kuwa kupitia mpango wa Mattei ushirikiano wa kiuchumi kati yetu na Italia utazidi kuimarika,” alisema Balozi Mbarouk.


Balozi Mbarouk aliongeza kuwa mpango wa mattei utainua sekta za kimkakati ambazo ni kilimo, nishati, elimu na uchumi wa buluu kwa upande wa Zanzibar, Sekta hizi zimepewa kipaumbele kufuatia umuhimu wake katika kukuza uchumi.


Pamoja na masuala mengine Tanzania imeihakikishia Italia ushirikiano katika kuunda kamati ya kuratibu mpango wa mattei ambayo itahakikisha sekta za kimkakati zilizoainishwa katika mpango huo zinananufaika kama ilivyopangwa kwa maslahi ya pande zote mbili.


Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Italia, Balozi Riccardo Guariglia alisema kuwa Italia ni rafiki wa Tanzania wa muda mrefu na mataifa hayo yamekuwa yakishirikiana katika sekta mbalimbali. Hivyo mpango wa Mattei ni moja ya njia za kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi baina ya Italia na Tanzania na Afrika kwa ujumla.


“Tupo hapa kuonesha na kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika na mpango wa mattei, lakini pia kuiona Afrika ikifanikisha kuweka vipaumbele vya malengo na kutekeleza majukumu yake kupitia mpango wa mattei kwa ufanisi,” alisema Balozi Guariglia


Balozi Guariglia aliongeza kuwa lengo la mpango wa mattei ni kuendelea kuimarisha uchumi wa Bara la Afrika kwa kuzishirikisha sekta za umma na binafsi za Italia katika kufadhili mpango huo kwa maslahi ya pande zote mbili.


Mwezi Januari 2024, baada ya kumalizika kwa mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na Italia, serikali ya nchi hiyo iliahidi kutuma ujumbe wa wataalam kutoka Chemba ya Biashara ya Italia kuja Tanzania kwa ajili ya kukutana na timu ya wataalam ya upande wa Tanzania kwa lengo la kukamilisha hatua za awali za utiaji saini wa ushirikiano za kutekeleza mpango wa mattei.


Aidha, katika kutekeleza hilo, mwezi Machi 15, 2024 Ujumbe wa Italia ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Ushirikiano wa Maendeleo katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Italia, Mhe. Stefano Gatti ulikutana na timu ya wataalamu wa Tanzania na kuainisha sekta za kipaumbele zitakazo nufaika na mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan).

JOKER ICE FRENZY EPIC KASINO YENYE BONASI KUBWA

0
0

 


JOKER ICE FRENZY EPIC STRIKE ni sloti iliyopo kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet ina nguzo tano zilizopangwa kwenye mistari mitatu yenye njia 20 za malipo. Ili kupata ushindi wowote, ni lazima kupata alama tatu au zaidi kwenye mstari wa malipo.

Mtiririko wowote wa ushindi, isipokuwa wale wenye alama za sketi na bonasi za kasino huhesabiwa kutoka kushoto kwenda kulia kuanzia nguzo ya kwanza upande wa kushoto.

Katika kasino ya mtandaoni hii unaweza kupata ushindi mmoja kwenye mstari mmoja wa malipo. Ikiwa una muunganiko wa ushindi zaidi kwenye mstari mmoja wa malipo, utalipwa ushindi wenye thamani kubwa zaidi.

Kiwango kikubwa cha ushindi kinawezeka ikiwa kitaunganishwa kwenye ushindi zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja

Ndani ya eneo la Bet, kuna vitufe vya plus na minus ambavyo unaweza kutumia kubadilisha thamani ya dau kwa kila mzunguko. Wachezaji wakubwa watapenda sana kitufe cha Max Bet. Kwa kubonyeza eneo hili, unaweza kuweka moja kwa moja dau kubwa zaidi kwa kila mzunguko.

Kuna pia chaguo la Autoplay unaloweza kulifanya wakati wowote. Unaweza kuweka hadi mizunguko 100 kwa pamoja kupitia chaguo hili.

Ikiwa unapenda mchezo wenye kasi zaidi, wezesha mizunguko ya haraka kwa kubonyeza eneo lenye picha ya radi. Jisajili na Meridianbet kasino ya mtandaoni kufurahia mchezo huu.

Alama za sloti ya Joker Ice Frenzy Epic Strike.
Linapokuja suala la alama za mchezo wa kasino, malipo ya chini zaidi ni cherry, alama za Bar, kengele, na nyota. Ni muhimu kusema kwamba alama zote za mchezo huu zimeganda.

Alama za kimsingi zenye nguvu za malipo ni alama za Lucky 7 moja, mbili, na tatu. Thamani kubwa kati yao ni Lucky 7 tatu. Ikiwa unapata alama tano za hizi katika mtirirko wa ushindi, utashinda mara 37.5 zaidi ya dau lako.

Jambo kubwa ni kwamba unaweza kuunda safu ya ushindi kutoka kwa alama tofauti za Lucky 7 pia. Kwa kweli, malipo ni kidogo kidogo wakati huo.

Joker anawakilishwa na nembo ya wild. Inachukua nafasi ya alama zote, isipokuwa bonasi na sketi, na kuwasaidia kuunda muunganiko wa ushindi.

Wakati huo huo, hii ni alama yenye nguvu ya malipo. Ikiwa unakusanya alama tano za hizi katika muunganiko wa ushindi, utashinda mara 125 ya dau lako.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

DKT. NCHIMBI ASHIRIKI MKUTANO WA 11 WA MAKATIBU WAKUU WA VYAMA RAFIKI VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA ( FLMS)

0
0

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi akizungumza wakati wa kutoa salaam za CCM za mshikamano kwenye Mkutano wa 11 wa Makatibu Wakuu wa Vyama Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika (FLMS), leo Jumatatu, Machi 18, 2024. Mkutano huo unaofanyika katika Mji wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe, umewakutanisha Makatibu Wakuu wengine wa vyama hivyo rafiki, ambao ni pamoja na Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia) Komredi Sophia Shaningwa, Katibu Mkuu wa Chama cha ANC (Afrika Kusini), Komredi Fikile Mbalula, Komredi Roque Silva Samuel (FRELIMO - Msumbiji), Komredi Paulo Pombolo (MPLA - Angola), Komredi Kavis Kario (BDP – Botswana) na Komredi Albert Mpofu (ZANU – PF - Zimbabwe), ambaye ni mwenyeji na mwenyekiti wa mkutano huo.



Mkutano wa 11 wa Vyama Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika (FLMS), unaowakutanisha wajumbe wake, ambao ni pamoja na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia), Komredi Sophia Shaningwa, Katibu Mkuu wa Chama cha ANC (Afrika Kusini), Komredi Fikile Mbalula, Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO (Msumbiji), Komredi Roque Silva Samuel, Katibu Mkuu wa Chama cha MPLA (Angola), Komredi Paulo Pombolo, Katibu Mkuu wa Chama cha BDP (Botswana), Komredi Kavis Kario na Katibu Mkuu wa Chama cha ZANU – PF (Zimbabwe), Komredi Albert Mpofu, (mwenyeji na mwenyekiti wa mkutano), ukiendelea kujadili agenda, leo Jumatatu, Machi 18, 2024, katika ukumbi ulioko Mji wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe, unakofanyikia.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi (wa pili kutoka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja, leo Jumatatu, Machi 18, 2024, pembezoni mwa siku ya kwanza ya Mkutano wa 11 wa Makatibu Wakuu wa Vyama Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, unaofanyika katika Mji wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe. Makatibu Wakuu wengine pichani, (kutoka kulia) ni Komredi Roque Silva Samuel (FRELIMO - Msumbiji), Komredi Paulo Pombolo (MPLA - Angola), Komredi Albert Mpofu (ZANU – PF - Zimbabwe, mwenye suti), Komredi Sophia Shaningwa (SWAPO – Namibia) na Komredi Fikile Mbalula (ANC – ANC).

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi (kushoto) kwenye picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia) Komredi Sophia Shaningwa (katikati) na Katibu Mkuu wa Chama cha ANC (Afrika Kusini), Komredi Fikile Mbalula (kulia), wakionesha alama ya salaam za CCM, Chama cha ANC na Chama cha SWAPO, leo Jumatatu, Machi 18, 2024, pembezoni mwa siku ya kwanza ya Mkutano wa 11 wa Makatibu Wakuu wa Vyama Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, unaofanyika katika Mji wa Victoria Falls, nchini Zimbabwe. Makatibu Wakuu  wa Vyama wengine wanaoshiriki mkutano huo ni pamoja na Komredi Roque Silva Samuel (FRELIMO - Msumbiji), Komredi Paulo Pombolo (MPLA - Angola), Komredi Kavis Kario (BDP – Botswana) na Komredi Albert Mpofu (ZANU – PF - Zimbabwe), ambaye ni mwenyeji wa mkutano huo.

TAWA YATOA KONGOLE KWA RAIS DKT. SAMIA KATIKA UTATUZI WA MIGOGORO

0
0

Kamishina  wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mabula Misungwi Nyanda, akizungumza   Mafanikio ya TAWA katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Mheshimwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kikao kazi na Wahariri wa vyombo vya Habari kilichofanyika chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Jijini Dar es Salaam.
Afisa Habari Mwandamizi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Sabatho Kosuri, akizungumza kuhusiana na vikao kazi kati ya Taasisi zilizochini ya Msajili wa Hazina ,jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania TEF, na Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Jukwaa hilo, Neville Meena, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Mwenyekiti wa Jukwaa hilo


Baadhi ya washiriki katika mkutano wa Mfuko wa Self na wahariri na waandishi wa habari ,jijini Dar es Salaam.

*Ni mafanikio ya Utawala wa Serikali ya Awamu ya Sita ndani ya miaka mitatu

Na Chalila Kibuda,Michuzi Tv
MAMLAKA Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) imesema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan migogoro saba imetatuliwa na kubaki mmoja ambao uko hatua za niwsho.

Migogoro iliyokuwepo ilikuwa ni kikwazo kwa mamlaka kutekeleza majukumu yake huku wananchi wakishindwa kuelewa mipaka ya hifadhi.

Hayo ameyasema Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA Mabula Misungwi Nyanda wakati akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari juu ya mafanikio ya Miaka Mitatu Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Jijini Dar es Salaam.

Amesema katika migogoro katika TAWA ilikuwa inanyima usingizi lakini kutokana msukumo wa Rais umewezesha kutatua na kupunguza migogoro ya mipaka ya ardhi kati ya Hifadhi na wananchi.

Amesema TAWA imeendelea kutekeleza maelekezo ya Serikali yaliyotolewa kupitia Kamati ya Mawaziri nane wa Wizara za Kisekta waliozunguka katika maeneo yenye migogoro.

Amesema kuwa kwa ushirikiano huo migogoro ya mipaka katika Mapori ya Akiba saba (7) ya Swagaswaga, Mkungunero, Wamimbiki, Igombe, Liparamba, Mpanga Kipengere na Selous kati ya nane (8) yaliyotolewa maelekezo na Kamati ya Mawaziri Nane wa kisekta imemalizika ambapo jumla ya vigingi 1,681 vimesimikwa kuzunguka mipaka ya hifadhi .

Aidha, amesema kuwa katika utatuzi wa migogoro hiyo eneo lenye ekari 103,544.48 limemegwa kutoka kwenye hifadhi na kuwapatia wananchi kwa ajili ya shughuli za kiuchumi, na kwamba Serikali kupitia TAWA inaendelea kukamilisha zoezi la kulipa fidia kaya 145 zilizo katika Pori la Akiba Mkungunero.

Kamishina Nyanda amesema kuwa Mamlaka hiyo imekuwa na mipango ya muda marefu katika ya matumizi ya ardhi katika kutatua migogoro hiyo.

"Tumejipanga na tuna kazi kubwa ya kufanya maeneo hayo ili kuokoa maisha ya watu wasidhurike na wanyama wakali na waharibifu” ameongeza.

Kamishna Nyanda amesema TAWa imejiwekea mipango mikakati imkatika utatuzi wa migogoro hiyo, ambapo eneo la ekari 103,544.48 limetengwa kutoka kwenye hifadhi, na kuwapatia wananchi kwaajili ya shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania TEF, na Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Jukwaa hilo, Neville Meena, amesema kutaniko hilo limekuwa na manufaa kwa Wahariri na waandishi kujifunza na kazi mbalimbali za Mamlaka hiyo, huku akiwashauri waandishi kuendelea kujifunza kwa kusoma taarifa mbalimbali za Mamlaka hiyo ili kuwa na wigo mpana wa kuifahamu Taasisi hiyo.

Mashine za Kilimo: Zilizotengenezwa Italia na Zinalenga Kukuza Sekta ya Kilimo Tanzania

0
0

 

Balozi wa Italia nchini Tanzania, Marco Lombardi, (Katikati) akizungumza na wafanyabiashara na wadau wa kilimo wakati wa mkutano ulioandaliwa na Italian Trade Agency kwa kushirikiana na FederUnacoma ambacho ni Chama cha kilimo kutoka Italia mkutano huo umefanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mkutano huu amefanyika Machi 18, ukilenga kutoa elimu na ufafanuzi wa mashine za kilimo kutoka nchini Italia kwa wakulima, wasafirishaji, na wataalamu kutoka Tanzania juu ya umuhimu wa teknolojia za kisasa kwenye sekta ya kilimo ulioandaliwa na Italian Trade Agency kushirikiana na FederUnacoma ambacho ni Chama cha kilimo kutoka Italia. Pia Marchi 19 kampuni hizo zitatembelea biashara za ndani ya Tanzania.

Mbali na mkutano huo Kuanzia Aprili 2024, Italian Trade Agency wataanza mchakato wa kuchagua makampuni yatakayolipiwa safari ya kwenda Italia kwa lengo la kujifunza na kuona fursa za kibiashara zinazopatikana nchini humo.

Kampuni za mashine za kilimo kutoka Italia ambazo ni Masscar, Barbieri na Ocmis Irrigazione wamekuja kueleza na kutoa elimu kwa Wakulima na watumiaji wa teknolojia ya mashine za kilimo nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na wakionesha dhamira ya kampuni za Italia katika kusaidia ukuaji wa sekta ya kilimo nchini Tanzania.

Washiriki muhimu walikuwa ni pamoja na Balozi wa Italia Marco Lombardi, Fabio Ricci wa FederUnacoma na Riccardo Zucconi, Mkurugenzi wa Italian Trade Agency wa Addis Ababa na wazinduzi wa mkutano wa 46 EIMA.

Pia fursa nyingine muhimu ilikuwa ni kuunganisha wafanyabiashara kwa kuongeza ushirikiano baina yao na ushiriki wa moja kwa moja kati ya makampuni ya Italia na wafanyabiashara wa Tanzania.

Fabio Ricci, Naibu Mkurugenzi wa FederUnacoma, alisisitiza jukumu kubwa kwao na Italia ni kukidhi mahitaji ya teknolojia ya kilimo ya Tanzania. Alisisitiza ongezeko kubwa la uagizaji kutoka Italia lilianza mwaka 2022, akithibitisha kuwa ongezeko la soko na ushawishi unakua kwenye kilimo cha mashine nchini Tanzania.

Maonesho ya kimataifa ya kilimo yamepangwa kufanyika kuanzia Novemba 6 hadi 10 huko Bologna, ikiwa imeandaliwa na FederUnacoma ambapo mkutano huu unatoa jukwaa muhimu kwa ushirikiano kati ya Italia na Tanzania.

Kwa zaidi ya mashine za aina tofauti tofauti 50,000 ikiwa ni mashine na vifaa vya kuonyesha, mkutano huo unatoa suluhisho kwa shughuli mbalimbali za kilimo, ikiwa ni pamoja na kupanda, ulinzi wa mimea, na mavuno.(Components, Digital,Energy,Green,Idrotech)

Kwa umuhimu maalum ni onyesho la Idrotech, linaloonesha teknolojia za umwagiliaji zenye ubunifu muhimu kwa kuboresha uzalishaji na ustahimilivu wa mazao. Mkutano huo unalenga kuimarisha uchumi wa kilimo nchini Tanzania kwa kukuza maendeleo ya biashara za ndani na kukuza ushirikiano wa kimataifa.

Riccardo Zucconi, Mkurugenzi wa Italian Trade Agency kutoka Addis Ababa na muwakilishi wa Tanzania, amegusia umuhimu wa ushirikiano kati ya Wakala na FederUnacoma.

Wakala ambae amefanya mapinduzi makubwa kutokana na ushirikiano wa kampuni za Italia alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Italian Trade Agency na FederUnacoma katika kuhamasisha kilimo cha mashine Italia kimataifa. Alisisitiza mafanikio ya toleo la zamani la EIMA International na kurudia dhamira ya mashirika hayo katika kufanikisha ushirikiano wa kimataifa.

Tukio hili la kimataifa la EIMA Iinalenga ubunifu na ustahimilivu unalingana na kutatua changamoto za kilimo duniani, na kufanya iwe mahali muhimu kwa wadau wa sekta ya kilimo.

Mkutano huo uliofanyika Serena Hotel Dar es Salaam unawakilisha hatua muhimu kuelekea kuimarisha ushirikiano kati ya Italia na Tanzania, na hivyo kufungua njia kwa ushirikiano unaofaidika pande zote katika sekta ya mashine za kilimo.




Latest Images