Quantcast
Channel: JIACHIE

ELIMU YA MLIPA KODI ILIVYOMUOKOA MIKONONI MWA MATAPELI

$
0
0

 

MFANYABIASHARA Marik Ngutti wa Machimbo ya Matabi wilayani Chato Mkoa wa Geita ameeleza namna ambavyo ufuatiliaji wake wa elimu ya mlipa kodi ilivyomnasua kutoka kwenye mikono ya matapeli waliojifanya maofisa Mamlaka ya Mapato (TRA).

Ngutti ametoa ushuhuda huo leo Aprili 23, 2024 alipotembelea banda la TRA katika maonesho ya Wakandarasi Geita Mjini kwenye viwanja vya EPZ ambapo amesema aliwapa elimu na wafanya biashara wenzake ambao pia walishindwa kutapeliwa baada ya kupata taarifa muhimu kuhusu maofisa wa TRA.

"Kuna watu walikuja kwenye maeneo yetu ya biashara pale Machimbo ya Matabi walijitambulisha kuwa ni maofisa wa TRA niliwajengea mashaka kwa kuwa niliona hawana utambulisho wa TRA na hawakuwa wanatoa lisiti kwa wenzetu waliotangulia kupita nikawaambia wafanyabiashara wenzangu kuwa hao sio maofisa wa TRA nikawapa namba ya TRA"

Amesema kwa kuwa tayari alishawapa elimu ya mlipa kodi walivyofika wale maofisa bandia wa TRA wale wafanyabiashara waliwahoji mambo muhimu yanayohusu TRA waliposhindwa kujibu wakaondoka zao na .

Ngutti amesema kuwa ufahamu juu ya masuala muhimu ya kodi na maofisa wa TRA ameyapata kutokana na jitihada zake za kufuatilia vipindi mbalimbali vya runinga na radio na kuwasisitiza wananchi wote kujielimisha katika masula muhimu ya kodi.

KATIBU MKUU WAZAZI HAPI AMETEMBELEA TRENI YA MWENDOKASI DODOMA

$
0
0

 KATIBU Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania Jumuiya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg.Ally Salum Hapi (MNEC) ametembelea na kuona treni mpya ya kisasa ya mwendokasi iliyowasili, Jijini Dodoma jana usiku ikitokea Jijini Dar Es Salaam iliyokuja na viongozi mbalimbali wa dini na serikali, wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Ndg.Masanja Kadogosa, pamoja na waandishi kwa ajili ya kuahiriki Dua Maalumu ya Kuliombea Taifa iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, leo, ambapo Mgeni Rasmi Alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Phillip Isdor Mpango.


Akizungumza baada ya kutembelea na kuona ubora, uzuri na utendaji kazi wa treni hiyo, Katibu Mkuu Wazazi, Ndg.Hapi, aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kutekeleza Ilani ya CCM ya Mwaka 2020 - 2024 kwa vitendo na kusema anastahili kuongezewa hali, morali na moyo wa kuendelea kuwatumikia wananchi wa Tanzania.

"Kwa niaba ya viongozi, wanachama na wapenzi wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM nichukue fursa hii adhimu kumpongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuhakikisha mradi wa ujenzi wa reli ya mwendokasi kutoka Dar Es Salaam hadi Dodoma imekamilika kwa asilimia kubwa pamoja na majaribio ya treni ya mwendokasi na mabehewa yake kuletwa nchini na kuanza kufanyia majaribio yanayotoa matokeo chanya;

"Ama kwa hakika hii ni furaha na faraja kubwa sana kwetu sisi wamiliki wa duka kuona muuza duka wetu anaiendesha vizuri biashara yetu na matokeo chanya yanaonekana, lakini pia nitoe pongezi kwa watumishi wote wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa usimamizi bora wa fedha za mradi huu ambao ni Tshs.Bilioni 23.5 ni fedha nyingi mnoo ila ndugu zetu hawa wanastahili pongezi kwa kusimamia vyema fedha hizo" alisema Hapi.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa TRC, Ndg.Masanja Kadogosa, alitoa shukurani kwa viongozi na wanachama wa Jumuiya ya Wazazi kwa kutembelea mradi huo kwa kusema kwao watumishi wa Shirika la Reli Tanzania hujisikia ufahari wa hali ya juu inapotokea nafasi ya viongozi wa CCM na Jumuiya zake wanapotembelea mradi wa ujenzi wa reli ya mwendokasi na kusifia kwa kile kilichofanyika inawatia moyo na morali wa kuendelea kutumikia shirika na serikali kwa maslahi mapana ya nchi.

Katika msafara wake Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi, Ndg.Hapi, aliongozana na Naibu Katibu Mkuu Wazazi Bara, Ndg.Joshua Mirumbe Chacha, viongozi wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dodoma, Wilaya pamoja na kata husika kwa kujitoa kuungana nao kutembelea na kutazama mradi huo.





Benki ya Absa yaendeleza udhamini wake Absa Dar City Marathon

$
0
0

BENKI ya Absa Tanzania imeendeleza udhamini wake kwa mwaka wa nne mfululizo katika mbio za Absa Dar City Marathon , ikilenga  kuifanya Tanzania kuwa Taifa lenye watu wenye afya njema.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio za Absa Dar City Marathon 2024, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Bwana Aron Luhanga alisema afya njema ni mtaji namba moja katika maendeleo ya Taifa la Tanzania na wanaokimbia wanajenga Afya.

Alisema lengo lingine kuu la Absa Dar City Marathon ni mapato yatayakayopatikana katika mbio hizo kuelekezwa katika shughuli za kijamii Kwa kununua vifaa  vitakavyosaidia wodi ya wanawake    katika hospitali ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 

“Pamoja na hayo kama kauli mbiu ya mbio hizi isemayo ‘Kata Mtaa, Ujue Jiji’ sisi kama Absa Bank, tukiwa na Matawi ya kibenki hapa jijini,  tunajisikia fahari kusapoti mbio hizi zenye lengo pia la kutangaza vivutio vya utalii vilivyomo katika jiji letu.

“Kauli yetu ya Absa inasema ‘Story Yako ina Thamani’ hivyo tunaamini kuwa ukienda kukimbia unaandika Story Yako, ukienda kusaidia jamii, unaandika Story Yako, nasi kama Absa, Story Yako Ina thamani sana kwetu”, alisema Bwana Luhanga.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa The Runners Club, Bwana Godfrey Mwangungulu alisema mbio za mwaka huu zinazofanyika chini ya udhamini mkubwa wa Benki ya Absa Tanzania zitashirikisha mbio za Kilomita, 21, 10 na Kilomita tano.

“Absa Dar City Marathon ya  mwaka huu inayotarajiwa kufanyika Mei 5 mwaka huu ikianzia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, ni zaidi ya mbio, ni zaidi ya sherehe, ni kilele cha sherehe za mbio zote zinazoendelea kufanyika hapa nchini.

“Tumefanya mbio hizi kwa miaka mitatu mfululizo, mwaka huu tunataka kuzifanya Kwa mafanikio zaidi, tunatarajia zaidi ya wakimbiaji 3000 kushiriki, tunawashukuru sana wadhamini wetu wakuu, Benki ya Absa pamoja na wadhamini wengine”, alisema Bwana Mwangungulu. 

Mbali na Benki ya Absa kama mdhamini mkuu, wadhamini wengine ni Kampuni  ya Alliance Life Assurance, Hill Water, Kilimanjaro Milk na Kampuni  ya Garda Security. 
Mwisho.



Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga ( wa pili kushoto ) akionyesha fulana zitakazovaliwa siku ya mbio  za Absa Dar City Marathon wakati wa hafla ya uzinduzi wa mbio hizo jijini Dar es Salaam jana, zinazotarajiwa kufanyika Mei 5 mwaka huu, jijini Dar es Salaam
  Kutoka kushoto ni Ofisa Masoko wa Hill Water, Sylvia Shoo, Mkuu wa Kitengo cha Habari wa Klabu ya The Runners, waandaaji wa Absa Dar City Marathon ,Godfrey Mwangungulu, Meneja wa Bima Kibenki wa Alliance Life Assurance, Juma Patrice na Meneja Bima Binafsi, Jumanne Muruga.
Mkuu wa  Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga ( wa tatu  kushoto ), Mkuu wa Kitengo cha  Mawasilino wa The Runners Club, Bwana Godfrey Mwangungulu (kushoto kwa Aron), pamoja na wawakilishi wa wadhamini wengine, wakionyesha fulana na vitu vingine vitakavyotumika wakati wa mbio za Absa Dar City Marathon, jijini Dar es Salaam Mei 5 mwaka huu, zikianzia katika Viwanja  vya Mnazi Mmoja. Hafla hiyo ilifanyika jijini humo jana.

420 BLAZE IT KASINO YENYE DROO 10 ZA USHINDI MERIDIANBET

$
0
0

JE, umewahi kucheza mchezo wa droo wenye droo 10? Ikiwa hujawahi, sasa unapata nafasi kamili ya kufanya hivyo. Kupitia Meridianbet Kasino ya Mtandaoni kuna furaha inakusubiri kupitia droo moja tu ya ushindi.

Taarifa za Msingi
420 Blaze It ni mchezo wa kasino ya mtandaoni kutoka kwa mtoa huduma 1x2 Gaming na una droo 10. Kila droo ina safu tatu, na kila safu ina alama moja. Vivyo hivyo, kila droo moja ina mstari mmoja wa malipo. Ili kupata mafanikio yoyote, lazima uunganishe alama tatu zinazolinganisha katika mfululizo wa ushindi.

Kwenye kasino ya mtandaoni hii ushindi huzingatiwa tu kutoka kushoto kwenda kulia, ukitoka kwenye safu ya kwanza upande wa kushoto. Kwenye mstari mmoja wa malipo, unaweza kupata ushindi mmoja tu. Hakuna uwezekano wa kupata mafanikio zaidi kwenye mstari mmoja wa malipo.

Unapoucheza mchezo huu wa kasino pale Meridianbet utaona sehemu ya kuweka dau lako au Stake, utaona vitufe vya plus na minus ambavyo unaweza kutumia kurekebisha thamani ya dau kwa kila droo.

Alama za Ushindi Droo ya 420 Blaze It
Alama za mchezo huu wa kasino ya mtandaoni ziko nyingi kuna alama ya cheri huleta mafanikio madogo. Ikiwa utapata matunda ya cheri matatu kwenye mstari wa malipo, utapata mara mbili ya dau lako kwenye droo.

Pia utaona tunda jingine, ambalo ni limao. Ukiwa na malimao matatu katika mchanganyiko wa mafanikio, utapata mara tano zaidi ya dau.

Alama ya Bar zambarau huleta mafanikio madogo zaidi. Ikiwa unashikamana na alama tatu hizi katika mchanganyiko wa ushindi, utapata mara kumi zaidi ya dau lako.

Inafuata alama ya Bar ya bluu ambayo itakuletea mafanikio makubwa kidogo. Ukishikamana na alama tatu hizi katika mchanganyiko wa mafanikio, utapata mara kumi na tano zaidi ya dau.

Thamani kubwa zaidi kati ya alama za Bar ni ile ya rangi ya machungwa. Alama tatu hizi kwenye droo moja itakuletea mara ishirini zaidi ya dau.

Bila shaka, nguvu kubwa ya kulipa inaletwa na alama za Lucky 7 na utawaona katika mchezo wa msingi katika rangi tatu. Ili kupata mafanikio madogo zaidi miongoni mwao, unapaswa kupata Lucky 7 za kijani. Ikiwa utashikamana na alama tatu hizi katika mchanganyiko wa mafanikio, utapata mara ishirini na tano zaidi ya dau.

Inafuata alama ya Lucky 7 ya rangi ya bluu, na alama tatu hizi kwenye mstari wa kulipa huleta mara hamsini zaidi ya dau la droo.

Mkubwa zaidi katika mchezo huu wa kasino ya mtandaoni ni alama ya Lucky 7 yenye rangi nyekundu. Alama tatu za hivi kwenye droo moja itakuletea x100 ya dau lako.

Michezo ya ziada yenye Bonasi za Kasino.
Mchanganyiko wa mafanikio ya alama tatu za Lucky 7 huleta zawadi nyingine. Hufungua mizunguko ya bure kulingana na sheria zifuatazo:

Alama Tatu za kijani za bahati zinaweza kuleta mizunguko ya bure 10
Alama Tatu za bluu za bahati zinaweza kuleta mizunguko ya bure 15
Alama Tatu nyekundu za bahati zinaweza kuleta mizunguko ya bure 20

Wakati unaendelea kutumia mizunguko ya bure kwenye mchezo huu wa kasino ya mtandaoni, alama za Lucky 7 tu huonekana.

NB: Jisajili na Meridianbet na cheza michezo ya kasino ya mtandaoni upate ushindi kirahisi, Pia ongeza maokoto yako kwa kubashiri michezo mbalimbali yenye ODDS KUBWA. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Rais Samia Suluhu Hassan Atunuku Nishani Viongozi Mbalimbali

$
0
0
RAIS Samia Suluhu Hassan Atunuku Nishani Viongozi Mbalimbali katika shamrashamra za miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Samwel Malecela kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tatu Mhe. Fredrick kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mohamed Gharib Bilal kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Janeth Magufuli Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024. Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hutunukiwa kwa Wakuu wa Nchi Wastaafu (hai au marehemu) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioingia madarakani kwa njia ya kikatiba na wameendelea kuonesha Maadili mema yenye nidhamu, heshima na mfano wa kuigwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Salma Kikwete Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024. Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hutunukiwa kwa Wakuu wa Nchi Wastaafu (hai au marehemu) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioingia madarakani kwa njia ya kikatiba na wameendelea kuonesha Maadili mema yenye nidhamu, heshima na mfano wa kuigwa.

WANAFUNZI FANYENI VIZURI KATIKA ELIMU,MTUPE HESHIMA- KIKWETE

$
0
0

 Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze, April 24

NAIBU Waziri wa Utumishi na Utawala Bora ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete amewataka wanafunzi na vijana kuacha matumizi mabaya ya mitandao, mambo yaliyo nje ya tamaduni za kitanzania na badala Yake watumie mitandao hiyo kujifunza na kujipa uelewa zaidi katika masuala ya masomo na elimu.

Aidha amewaasa kusoma kwa bidii kwani elimu ndio nguzo ya maisha yao.

Ridhiwani alitoa rai hiyo alipokuwa akihutubia wahutimu wa kidato cha sita shule ya sekondari ya Lugoba , Halmashauri ya Chalinze, mkoani Pwani.

Aliwaasa wahitimu hao kuhakikisha wanafaulu ili waache deni la kufuatwa na wadogo zao wanaowafuata kwa upande mmoja, wawape heshima walimu na wazazi kwa kufaulu vizuri.

Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ,Abdallah Sakasa aliishukuru serikali kwa kuendelea kupeleka pesa za elimu bure , vifaa na kuongezeka kwa madarasa na walimu shuleni hapo .

Alimuomba mbunge kuendelea kuikumbuka shule hiyo kwa kuisaidia vifaa na kuongeza mabweni ya wanafunzi.



TAKUKURU PWANI YAONGEZA MAPATO MACHINJIO MTAKUJA

$
0
0

 


Na Khadija Kalili,Michuzi TV
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani imefanya uchambuzi wa mfumo wa ukusanyaji wa mapato yatokanayo na machinjio ya Mtakuja iliyopo Halmashauri ya Mji Kibaha .

"Uchambuzi huu umefanywa baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba kuna miaya ya rushwa katika ukusanyaji wa mapato yatokanayo na ushuru katika machinjio hayo,hali inayodababisha upotevu wa mapato na Halmashauri hiyo hivyo kushindwa kufikia lengo la

ukusanyaji waliyojiwekea kutoka kwenye chanzo hiki" amesema Kaimu Kamanda TAKUKURU Mkoa wa Pwani Ally Sadiki alipozungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari ambao umefanyika leo Aprili 24.

"Uchambuzi huu umebaini kwamba, pamoja na kuwepo kwa mashine za kieletroniki za POS katika machinjio kumekua na taarifa zinazokinzana ,kuwepo kwa tatizo la miundombinu na ucheleshaji wa kuweka fedha benki zinazo kisanywa.

TAKUKURU imebaini pia kuna uzembe katika kusimamia idadi ya ng'ombe wanao chinjwa kwa siku husika na hakuna ukaguzi kuhusu idadi ya ng'ombe waliopo eneo la kusibiri kuchinjwa.

"TAKUKURU imebaini kuwa idadi ndogo ya watumishi walioajiriwa eneo husika ndiyo chanzo cha kushindwa kutekeleza majukumu ipasavyo"amesema Kaimu Kamanda TAKUKURU Sadiki.

Aidha amesema kuwa baada ya TAKUKURU kuingilia kati makusanyo yameongezeka tofauti na ilivyokua katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita kati ya Oktoba na Desemba 2023 ambapo Oktoba hadi Desemba makusanyo yalikua Mil.7,418,000 na sasa makusanyo yameongezeka na kufikia kiasi cha Mil.9,615,000.

"Katika hatua ingine Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibaha Mji ameongeza watumishi eneo hilo la machinjio ya Mtakuja kuimarisha ufuatiliaji na ukaguzi hivi sasa unafanyika kila mara ili kuondoa fedha za makusanyo ya kila siku na kuhakikisha fedha zinapelekwa benki kila siku.

Kaimu Kamanda wa TAKUKURU amesema kuwa kwa kipindi tajwa wamefanya chambuzi nyingine za mifumo tano katika sekta ya Ardhi,Elimu, AMCOS na ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya serikali ili kupata tija ya mifumo imara usiyokwamisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Ameongeza kwa kusema kuwq TAKUKURU Mkoa wa Pwani wamefuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo 23 yenye thamani ya Bilioni6.3 katika sekta za Elimu, Maji,Afya na Ujenzi (Barabara),ambapo kati ya miradi hiyo mradi mmoja umeonekana kuwa na upungufu ufuatiliaji u aendelea ii kurekebisha kasoro hizo.

Kaimu Kamanda TAKUKURU Mkoa wa Pwani Sadiki amesema kuwa katika kipindi hicho cha miezi mitayu wameweza kutoa elimu kwa umma kwa kufanya semina 19,mikutano yahadhara21,

vipindi vya redio 9 kuimarisha klabu za wapinga rushwa 54 uandishi makala 4 na TAKUKURU Rafiki6.

Aidha TAKUKURU Mkoa wa Pwani imefungua kesi mpya mbili Mahakamani ambapo kesi sita zimeamuliwa huku kesinne watuhumiwa wametiwa hatiani na jumla kesi sita zinaendelea Mahakamani.

Ameongeza kwa kusema kuwa mikakati waliyojiwekea ni kwamba wamejipanga kuendelea kufanya udhibiti wa mapato ya serikali na usimamizi wa rasilimali za umma ikiwa ji pamoja na udhibiti wa fedh zinazotolewa na serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

”KILA LA HERI, KAZI NJEMA”

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi akipunga mkono kuwaaga mamia ya wananchi, walioongozwa na viongozi wa chama na Serikali Mkoa wa Ruvuma, waliofika Uwanja wa Ndege wa Songea, kumuaga kiongozi huyo baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku tatu mkoani humo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku 13 iliyomfikisha katika mikoa sita, akianzia Katavi, kisha Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma.

Balozi Nchimbi, ambaye katika ziara hiyo aliambatana na Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Oganaizesheni na Amos Gabriel Makalla, Katibu wa NEC ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, akiwa ziarani kwenye maeneo mbalimbali ya mikoa hiyo, amekagua na kuhamasisha uhai na ujenzi wa chama.

Aidha, katika ziara hiyo pia, Balozi Nchimbi ametoa maelekezo mbalimbali kwa baadhi ya viongozi na watendaji wa wizara yaliyolenga kuboresha na kuongeza kasi ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020 - 2025, hasa maeneo ya miradi ya maendeleo ya wananchi na kuwatumikia watu.

Kupitia ziara hiyo, CCM katika ngazi ya taifa, hasa kupitia kwa Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, imeendeleza utaratibu wake wa kusikiliza kero za wananchi na kuzitolea maelekezo kwa ajili ya kuzitatua, huku Gavu akiendelea kuhamasisha wanachama na viongozi kuendelea kukiimarisha CCM na kujiandaa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (2024) na Uchaguzi Mkuu (2025).








TOGABE MILLS, KISHINDO CHA MAMA WATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI

$
0
0

  WANACHAMA wa Kishindo cha Mama kwa kushirikiana na TOGABE Mills watoa Msaada kwa waathirika wa Mafuriko Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

Wametoa misaada mbalimbali ya kibinadamu vikiwemo Unga, Maharage, Mchele, Mafuta ya Kupikia pamoja na nguo.
MKuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele na Wanachama wa Kishindo cha Mama na TOGABE Mills wakiondoka na vyakula vilivyotolewa waathirika wa Mafuriko Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.
MKuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele (Watano kutoka kushoto) Wanachama wa Kishindo cha Mama na TOGABE Mills wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa na vyakula vilivyotolewa waathirika wa Mafuriko Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

Baadhi ya wanakibiti wakisaidia kushusha baadhi ya misaada iliyotolewa na Wanachama wa Kishindo cha Mama na TOGABE Mills mara baada ya kutolewa walipotembelewa na wanachama hao.



MKuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele (Wapili kutoka kushoto) akizungumza na Wanachama wa Kishindo cha Mama na TOGABE Mills mara baada ya kukabidhi msaada kwa waathirika wa Mafuriko Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

MKuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele akiwa na Tisheti aliyopewa na wanachama wa Kishindo Cha Mama.
Wanachama wa Kishindo cha Mama na TOGABE Mills wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kutoa Msaada kwa waathirika wa Mafuriko Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

Picha ya pamoja.

MKuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa misaada na Wanachama wa Kishindo cha Mama na TOGABE Mills vilivyo kwa waathirika wa Mafuriko Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.
Afisa Masoko wa TOGABE Mills, Ramadhan Kimomwe akizungumza na waandishi mara baada ya kutoa msaada kwa waathirika wa Mafuriki Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani.

USIKU WA KUPIGA MKWANJA NA EPL, LIGUE, NA COPPA ITALIA

$
0
0

 


KWA wale wote wanaobashiri na mabingwa wa michezo ya kubashiri kampuni ya Meridianbet kwa taarifa tu leo ni ile siku ya kupiga mkwanja kupitia ligi kuu ya Uingereza, Ufaransa, pamoja na michuano ya Coppa Italia kutoka nchini Italia.

Michezo mbalimbali itapigwa usiku wa leo katika ligi hizo zilizotajwa hapo hivo wewe mteja wa Meridianbet unachotakiwa kukifanya ni jambo moja tu kusuka mkeka wako na kuweka dau lako na kusikilizia mkwanja, Kwani michezo itakua ya kutosha na kama ilivyo kawaida mabingwa wa kubashiri Meridianbet wanaweka machaguzi ya kutosha.

EPL
Moja ya michezo mikali inayosubiriwa leo ni mchezo mkali kati ya Everton na klabu ya Liverpool ambapo huu ni mchezo wa Derby, Mchezo huu licha ya kua derby lakini unakua mkali zaidi kwakua Liverpool wanahitaji ushindi katika kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza lakini upande wa Everton wao wanapambania kutoshuka daraja.

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye michuano mbalimbali barani ulaya na duniani kote. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Man United wao baada ya kutoka suluhu katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Bournamouth wiki mbili zilizopita leo watakua nyumbani kumenyana na klabu ya Sheffield United inayoshika mkia kwenye ligi hiyo.

Mchezo mwingine mkali utakua baina ya klabu ya Crystal Palace ambao wametoka kuwapa kipigo kizito Westham United wikiendi iliyomalizika dhidi ya Newcastle United, Mchezo huu unatarajiwa kua mkali vilevile kwakua vilabu vyote vimekua kwenye kiwango kizuri kwenye michezo kadhaa iliyiopita.

LIGUE 1
Pale kwenye ligi kuu ya Ufaransa Ligue 1 mabingwa watetezi klabu ya PSG watakua ugenini kumenyama na klabu ya Lorient, Olympique Marseille watakua nyumbani kumenyana na OGC Nice, Mchezo mwingine utakua kati ya Monaco na klabu ya Lille ambapo ni moja ya michezo mikali kwenye ligi hiyo usiku wa leo.

COPPA ITALIA
Pale nchini Italia leo itapigwa nusu fainali ya marudiano ambapo klabu ya Atalanta watakua nyumbani kuikaribisha klabu ya Fiorentina ambao walishinda mchezo wa kwanza wakiwa kwao, Hivo mchezo wa leo ndo utaamua ni timu gani itacheza fainali ya michuano hiyo msimu huu ambapo watamenyana na Juventus ambao tayari wametangulia fainali baada ya kuitupa nje klabu ya Lazio usiku wa jana.

SHINDANO LA BINGWA MSIMU TATU KUWAFIKIA VIJANA MIKOANI

$
0
0

 

 Meneja programu wa shindano la Bingwa Ombeni Phiri akieleza namna Shindano hilo litakavyoshirikisha Mikoa mitano ambayo ni Arusha,Mbeya,Mwanza,Dodoma pamoja na Dar es Salaam.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Parimatch Levis Paul akizungumza machache mara baada ya Kuzinduliwa kwa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo msimu huo Kampuni hiyo ikiwa wadhamini wakuu wa shindano.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,2024  Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam  wakati wa Uzinduzi wa Msimu wa tatu wa Shindano la Bingwa ambapo amewataka wateja wa Kisimbuzi cha Startimes kulipia kifurushi ili kuendelea kuona shindano hilo kupitia Tv3

SHINDANO la Mtindo wa Maisha (Life style) Kwa Vijana wenye ushawishi Mitandaoni ( BINGWA ) Msimu wa tatu umezundiliwa rasmi Vijana Mikoani wapewa nafasi .

Akizungumza na Wanahabari Leo Aprili 24,024 Ukumbi wa Serena Hoteli Jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua Shindano hilo kwa Msimu wa tatu Meneja wa Shindano hilo Ombeni Phiri amesema Shindano hilo limewapa fursa Vijana wengi mitandaoni kubadilisha maisha kutokana na fursa mbalimbali ambazo wamekuwa wakizipata na hivyo kulazimika Shindano hilo kuendelea kuwepo ambapo msimu huo wa tatu umekuwa wa kitofauti zaidi.

"Misimu miwili imekuwa yenye Mafanikio makubwa zaidi na Vijana wengi wa mitandao kuonesha Maisha yao halisi wanapokuwa kwenye mjengo huo hivyo kwa Msimu huu watatu Umepewa nguvu na Kampuni ya Kubashiri ya Parimatch ili kumsukuma Mshindi huyo kufanya vitu vikubwa zaidi Pape Shindano linapomalizika

Msimu Mpya wa tatu wa show ya Bingwa itatembelea Mikoa mitano kwa ajili ya kutafuta Vijana wengine ambapo maoni mengi yamekuwa yakiwafikia Vijana wakihitaji kushiriki Shindano hilo.

"Msimu wa tatu umefanya Maboresho mbalimbali ikiwemo ongezeko la Mikoa mitano ya washiriki ikiwemo Arusha, Dodoma,Mwanza, Mbeya pamoja na kitovu chenyewe Dar es Salaam.

Pia ameeleza kuwa usahili kila Mkoa utachukua washiriki 10 kila Mkoa na kufatia mchujo katika App ya Startimes (Startimes On) ambapo washiriki 08 watatoka Dar hivyo kukamilisha Jumla ya watakaoingia ndani ya nyumba washiriki 24 huku zawadi ya Mshindi kugharimu zaidi ya Milioni 35 za Kitanzania.

Kwa Upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa amesema Msimu wa tatu utaendelea kuwapa fursa vijana zaidi na Atakaeibuka Mshindi Kampuni ya Startimes itaweza kumpa Ubalozi.

Aidha amewapongeza Kampuni ya Parimatch kuona haja ya kuwapa Moyo Vijana hao wenye ushawishi Mitandaoni kukuza vipaji vyao.

Pia amewataka wateja kulipia vifurushi cha Uhuru elfu 23000 ili kuweza kuona shindano hilo kupitia Tv3 ndani ya King'amuzi cha Startimes.

Nae Meneja Masoko wa Parimatch Levis Paul ameeleza sababu ya Kampuni hiyo kuishika mkono Shindano hilo la " Bingwa".

"Sababu ya Parimatch kuungana na Msimu wa tatu wa Shindano la bingwa ni kutokana na shindano hilo Kuhusisha Vijana na Kauli mbiu ikibeba Jumba la Washindi ambapo Kampuni yetu inalenga zaidi kutafuta Washindi walipo kwa kupitia ubashiri."

Paul ameeleza wao kama Parimatch wanatambua kuwa Washiriki wanahitaji kukaa siku 70 ambapo kila kitu kinahitaji uwezeshwaji kuanzia Malazi na vitu mbalimbali hivyo Tv3 na Startimes peke wanahitaji nguvu ya ziada ya kuendesha Shindano hilo hivyo sisi tumeona tuongeze nguvu hiyo kwa msimu huu wa tatu."

Pia amefafanua zaidi kuwa Wana amini kuwa chapa ya Kampuni hiyo ipo sehemu na sahihi hivyo kudhamini shindano hilo itaongeza na kujiweka kwenye nafasi nyingine nzuri zaidi ya kujitangaza kama Kampuni

TAMWA ZANZIBAR YAPIGANIA UPATIKANAJI WA UHURU WA HABARI NA KUJIELEZA KATIKA JAMII

$
0
0

 



WAANDISHI wa habari wametakiwa kupaza sauti zao kuwatetea wananchi kupitia vyombo vya habari kwa maslahi ya kukuza uhuru wa habari na uhuru wa kujieleza ambao utasaidia kuleta maendeleo ya haraka kwa taifa.

Uhuru huo unaweza kupatikana endapo kutakuwa na sheria rafiki za habari sambamba na waandishi wenyewe kufanya kazi kwa kufuata maadili ya tasnia yao na kuendeleza jukumu la huleta maendeleo kutokana na kuwa kiungo cha kupaza sauti kwa wasio na sauti .

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA-ZNZ) Dkt Mzuri Issa Ali wakati wa mafunzo ya siku moja ya kupitia Mikataba ya kikanda na ya Kimataifa na kujadili mapungufu ya sheria zinazokwamisha uhuru wa habari Zanzibar.

Ameeleza kuwa lengo la mafunzo hayo yaliyowakutanisha watendaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo , Tume ya kurekebisha Sheria Zanzibar, Tume ya Utangazaji na waandishi wa habari ni kukumbushana umuhimu wa kuangalia ni kwa kiasi gani kama nchi imeweza kuzingatia mikataba hiyo ili kupata sheria na sera bora zitakazo simamia masuala ya haki ya kupata habari na kutoa maoni na kukuza demokrasia nchini .

Aidha amebainisha kuwa pamoja na kuridhia Mikataba ya bado sauti za wananchi hazipewi kipau mbele kusikika katika vyombo vya habari ukilinganisha na sauti za viongozi jambo ambalo linawanyima wananchi haki yao ya kikatiba ya kutoa maoni.

Miongoni mwa mikataba hiyo ni pamoja na Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu (Universal Declaration of Human Rights (UDHR), Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa (The International Covenant on Civil and Political Rights (ICCPR) na Mkataba wa Haki za Binadamu na Haki za Watu wa Umoja wa Afrika (African Charter on Human and Peoples Rights - ACHPR)

“Nchi nyingi za Afrika zimeweza kupiga hatua za kimaendeleo kwa kuvitumia vyema vyombo vya habari kwa uhuru na kupelekea kuinua uchumi wa nchi ambapo ni pamoja na Ghana, Afrika ya kusini na Mozambique.

Mapema akiwasilisha mada kuhusiana na “Mapungufu ya Sheria za habari” Bibi Hawra Shamte ambae ni mwandishi wa habari mkongwe amesema ingawa kuna sheria zinazosimamia sekta ya habari bado zinaonekana kiuhalisia hazifanyi kazi ipasavyo kwa kulinda usalama wa waandishi wa habari na wananchi hivyo zinahitaji kufanyiwa marekebisho.

“Baadhi ya sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Usajili wa Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu No. 5 ya mwaka 1988 iliyofanyiwa marekebisho na sheria No. 8 ya mwaka 1997 na Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar No. 7 ya mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho na sheria No 1 ya 2010”, alieleza muwasilishaji huyo.

Wakichangia katika mafunzo hayo, miongoni mwa waandishi wahabari wamesema wamaekuwa wakikutana na vikwazo mbalimbali katika kufanikisha majukumu yao, hali inayosababisha kukosa uhuru na kutowajibika ipasavyo.

Mafunzo hayo yametolewa na TAMWA-ZNZ kwa watendaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo,Tume ya kurekebisha Sheria Zanzibar, Tume ya Utangazaji na waandishi wa habari yenye lengo la kuonesha umuhimu wa kuzingatia mikataba ya kikanda na ya kimataifa ili kuwa na sheria na sera bora zitakazo simamia masuala ya haki ya kupata habari na kutoa maoni kwa uhuru.

IKIWA MTU ANATAMANI MBINGU NA UZIMA WA MILELE, NI LAZIMA WAENDE HADI MWISHO WA DUNIA- LEE

$
0
0

 


*MWENYEKITI Lee Man-hee -Jukumu langu ni kushuhudia matukio ya Ufunuo kama nilivyoyasikia na kuyaona."

*Ushuhuda juu ya ukweli uliotimizwa wa Ufunuo' ulielezea kimantiki na kwa utaratibu.

MWENYEKITI wa kanisa la Shincheonji, Lee Man-hee amesema ikiwa mtu anatamani mbingu na uzima wa milele, ni lazima waende hadi mwisho wa dunia ikiwa ni lazima ili kujua kama ni ukweli unaotimizwa kulingana na Biblia.

Hayo amesema Wakati wa Semina ya bibilia iliyofanyika Barani Asia katika nchi ya Uphilipino Aprili 20, 2024. mkutano huo ulikuwa na lengo la kuwajulisha wakristo wote kuhusu ukweli uliotimizwa kwenye kitabu cha Ufunuo.

Mwenyekiti Lee alisisitiza, "Imani sio kutafuta pesa," na "Sio wakati wa kuwa na imani na mawazo ya zamani. Mtu lazima athibitishe. Baada ya kuthibitisha, lazima aamue kuamini au la."

"Ni kazi ya mtu huyu kufikisha kile kilichoonekana na kusikika kutoka kwa matukio ya Ufunuo sura ya 1 hadi 22. Nilichokiona na kusikia, kile nilichogusa na kile kilichopo katika hali halisi, ndicho nilichokuja hapa kushiriki nanyi. Sasa sio wakati wa kusema chochote na kukubaliana tu na 'Amina'. Lazima uelewe nyakati za ukweli. Ni wakati ambao ahadi zimetimizwa."

Katika ukumbi wa mihadhara ya ndani huko Ufilipino, makofi yalijaza nafasi, ambayo ilionekana kukaa maelfu kwa mtazamo wa kwanza. Sauti yenye nguvu na hotuba ya ujasiri inayotokana na kimo kidogo, ambayo ilionekana kuwa haiwezekani kwa mtu zaidi ya miaka tisini, ilifanya maneno rahisi hata mtoto anaweza kuelewa. Katika muda mfupi, hali ilizidi kuwa kali. Mtu ambaye alifanya hivyo kutokea hakuwa mwingine isipokuwa Shincheonji Kanisa la Yesu, Hekalu la Hema ya Ushuhuda, Mwenyekiti Lee Man-hee.

Siku hiyo, Mwenyekiti Lee alizindua Semina za Biblia za Shincheonji za 2024 za Bara la Asia (I)' kwa kutembelea Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Ufilipino. Mfululizo wa hotuba utaendelea mwaka mzima huko Ulaya, Afrika, Amerika, Oceania, na kuhitimisha tena Asia (II). Kanisa la Shincheonji la Yesu liliandaa Semina hiyo ya Neno kutokana na majibu mengi na maombi ya dhati kutoka kwa wachungaji na waumini wengi ulimwenguni kote kufuatia 'Semina ya Neno la Ufunuo Shincheonji '.

Akiwa na ukumbi wa mihadhara ambao una viti 4,000 vilivyojaa watu, Mwenyekiti Lee alichukua hatua na kwanza akajitambulisha na kile kilichomfanya aamini. Ilitoa hisia sawa na jinsi waandishi wa kibiblia walivyoanza kuelezea ukoo wao na nyakati kabla ya maudhui kuu

Mwenyekiti Lee alisema kwa nguvu, "Sasa si wakati wa kusema chochote na kukubaliana tu na 'Amina,'" na "Lazima uelewe nyakati ya ukweli. Ni zama ambazo ahadi zimetimizwa." Alisisitiza, "Ufunuo unatia ndani mnyama mwenye vichwa saba na pembe kumi, na pia nyota saba. Ni juu ya kuelewa kile ambacho kuonekana kwa kweli kunawakilisha," na akasisitiza kwamba "wakati Mungu anaandika kuibuka kwa watu kama hao, ni ili leo utimizo utimie. kuona, kusikia, na kuamini."

Akirejelea Ufunuo 22:18-19, Mwenyekiti Lee alisisitiza mara kwa mara kwamba mtu hawezi kuingia mbinguni ikiwa wataongeza au kuondoa kutoka kwa Kitabu cha Ufunuo. Kwa kufanya hivyo, aliamsha hisia ya uharaka katika imani kwa kusema, "Mtu lazima ajue kila kitu bila kupunguza. Ni vigumu kutosha kufanya mazoezi hata wakati wa kujua kila kitu; bila ujuzi, mtu angeweza kupoteza matumaini."

Pia alikazia kwa mara nyingine tena kwamba ni lazima mtu afahamu kikamili Ufunuo na kutiwa muhuri kana kwamba anapigwa muhuri. Mwenyekiti Lee aliuliza, "Kwa nini unafikiri imeandikwa katika Ufunuo 22:18-19 kwamba mtu hataingia katika ufalme wa mbinguni na atalaaniwa ikiwa ataongeza au kupunguza kutoka humo?" Akajibu, "Ni kwa sababu maneno haya yanatimia kana kwamba yanapigwa muhuri."

Mwenyekiti Lee alisisitiza umuhimu wa kuandika maneno katika moyo wa mtu, kuwa 'Biblia inayotembea' na 'neno lililo hai.' Alitaja kwamba wale wanaofanya hivyo wanakuwa wale waliotiwa muhuri wanaotajwa katika Ufunuo 7, ambao wameokolewa. Mwenyekiti Lee alitangaza, "Hakuna wokovu unaotajwa isipokuwa wale waliotiwa muhuri 144,000 na kundi kubwa la watu waliovaa mavazi meupe; mtu ye yote ambaye hajatiwa muhuri anakuwa kama udongo, asiye na uhusiano wowote nalo. Ni wale tu waliotiwa muhuri wanaweza kuingia ufalme wa mbinguni." Pia alisema kwa uthabiti, "Wale ambao wametiwa muhuri wanaweza kuishi mbinguni, kuwa na uzima wa milele, na kuwa sehemu ya familia ya Mungu, lakini wale ambao hawana basi hawana uhusiano na Mungu."

Kwa wenyeji, Mwenyekiti Lee mara kwa mara aliwasilisha salamu kama vile "Nina uhusiano wa kina na Ufilipino,""Ufilipino ilikuwa mahali pa kwanza nilipokuja kutoa ushahidi baada ya kupokea neno," na "Ninaipenda sana Ufilipino.

Kwa kweli, Ufilipino imedumisha uhusiano na Mwenyekiti Lee kwa zaidi ya muongo mmoja. Mbali na shughuli zake za kidini, akiwa mwakilishi wa shirika lisilo la kiserikali la kimataifa la HWPL (Heavenly Culture, World Peace, Restoration of Light), alitembelea Ufilipino na kupatanisha makubaliano ya kwanza ya amani ya kiraia huko Mindanao, ambayo yamekuwa katika migogoro kwa muda mrefu. miaka 40. Kufuatia hili, amani ilianzishwa katika kanda, na habari hii ilipata tahadhari ya kimataifa.



WADAU WAOMBA WANAWAKE MAULAMA WAWE SEHEMU YA MAAMUZI

$
0
0

Na Nihifadhi Issa Zanzibar.
SHERIA ya Ofisi ya Mufti wa Zanzibar ya mwaka 2021 kwenye kipengele cha ufafanuzi imefafanua Ulamaa kuwa ni “ Mwanachuoni wa Kiislamu mwenye elimu ya kutosha ya fani mbalimbali ya dini ya kiislam na lugha ya kiarab”. Hapana hakuna sehemu iiyowekwa jinsia maana wanawake na wanaume wenye uwezo wa kielimu wapewe nafasi. Ila suala hili kwa baadhi ya dini ni jambo lisilopewa kipaombele.

Sheikh Khamis Shabaan Khamis ni Iman wa Msikiti pia ni Kiongozi wa dini anayepinga suala la wanaume kuona na kuzungumza kuwa wanawake hawana haki ya kuwa kwenye sehemu za maamuzi, amesema suala la kuharamisha na kuhalilisha suala lolote la kidini ni jambo ambalo linatakiwa litokane na Quran na Mafundisho ya Mtume Muhammad (S.W.A).”Kumzuia mwanamke asishiriki katika utowaji wa Fatwa au maamuzi, kumharimisha wanamke asishiriki katika harakati za kijamii au kutokuwa kadhi au kiongozi basi lazima awe na Ushahidi.” Sheikh Khamis amesema maana yake ni kwamba hakuna pingamizi ya wanamke kuwa kiongozi au kuwepo kwa masuala ya kusema hili halifai.

Dkt Mzuri Issa ni Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar – TAMWA-Z amekuwa akizungumzia suala la usawa na ushirikishwaji wa wanawake kwenye vyombo vya maamuzi anasema .”Kikatiba wanawake wanahaki ya kuwa kwenye sehemu za maamuzi, ni ukweli usioficha kuwa wanawake wanakuwa huru kuzungumza na wanawake wenzao kuliko wanaume hususan kwenye matatizo kama hayo ambayo yanayowakumba zaidi wanawake “Dkt Mzuri anaendelea kusema kuwa kukosekana kwa wanawake kwenye sehemu za maamuzi inaweza kuwa wanawake hawaridhiki na maamuzi yanayotolewa “Ikiwa wanawake wanakosekana kwenye vyombo vya maamuzi ambavyo vinawajibika kwenye masuala haki basi hapo hakuna utekelezaji wa haki,wala usawa na inawavunja moyo sawa wanawake waliosomo kwenye kada hizo wakikosa nafasi za kushirikishwa au kupatiwa nafasi naweza kusema hawatendewi haki” Amemalizia Dkt Mzuri Issa.

Amina Salum Khalfan ni Mwanarakati wa Kiislam anapingana na mawazo ya viongozi wa dini wasioamini nafasi ya mwanamke kwenye masuala ya kijamii na upatikanaji wa haki. “Nikiletewa kesi nawaambia nendani ofisi ya Kadhi au ya Mufti wanawake wanakataa kwa sasa huwezi kuzungumza faragha zako za ndani zinamhusu mwanaume mbele ya wananaume wenzao ni aibu na sio jambo linakubalika kidini “Anaendelea kusema “Kuna madhara makubwa ikiwa wanawake hawatapata nafasi kwenye sehemu hizo maana dini haijasema hivyo, wanaona uzito kwenye suala hili maana waliowengi wameshikilia dini na kukosa maarifa ya hio dini lakini zaidi ni mitazamo yao” Amemalizia kusema Amina.

Mwaka 2019 kupitia Baraza la Wakilishi kulizuka mjadala mkubwa juu ya suala la wanawake kupatiwa nafasi kwenye sehemu za maamuzi huku baadhi ya wawakilishi wakipinga suala hilo kwa kunasabisha dini kukataza baadhi ya masuala ya wanawake kuwa hawafai kuwa kwenye baraza la Maulama .Novemba 27, 2019 kupitia kikao cha kwanza,Mkutano wa 16 wakati wa kuwasilisha Mswada wa Marekebisho ya Kuanzishwa Afisi ya Mufti Nam.9 ya Mwaka 2001 ambao kupitia kikao hicho wajumbe wa Baraza la Wakilishi walijadili kuhusu nafasi ya kuwepo wa maulamaa wanawake.

Akichangia muswada huo Rashid Makame Shamsi ambaye alikuwa Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni alihoji juu ya kuwepo kwa wajumbe 16 wanaume katika baraza la Maulama “Sasa Wajumbe waliotajwa katika Baraza hilo ukipiga mahesabu ni wajumbe 16, sasa ndani ya Wajumbe 16 ni Masheikh, Shekhe mmoja mmoja kutoka kila wilaya na wilaya tuna 10. Sasa ukitizama sitarajii kwamba ndani ya hao Masheikh watakuwemo Masheikh wanawake sitarajii. Kwa sababu ulamaa ni mtu mwenye elimu ya juu katika uwanja wa dini kwa mujibu wa kamusi zote za kiswahili na watu wenye upeo wa dini ya kiislamu wanawake hivi sasa wako wengi sana na kazi kubwa sio kutoa fatwa ni kumshauri Mufti wa Zanzibar.Mimi sifikirii kabisa na nimefanya utafiti kwa Masheikh maulamaa na wasomi wa dini ya kiislam suala hili halina madhara kuwaingiza wanazuoni wanawake katika Baraza la Maulamaa la Zanzibar” Alimalizia Rashid Makame Shamsi – Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni- Zanzibar.

Kupitia Hansad za Baraza la Wakilishi Zanzibar aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Khamis Juma Mwalimu akijibu hoja na wajumbe waliochgia mjadala huo aliunga mkono hoja ya kufanyika kwa marekebisho ya baadhi ya vifungu hivyo na wanawake wapate nafasi ya kuingia kwenye Baraza ma Ulamaa kupitia Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar “hili la uanzishwaji wa Baraza la Ulamaa, sisi binafsi ushauri huu ulitolewa awali kuona uwezekano pengine na akina mama waweze kuwemo katika Baraza hili.Lakini vile vile, tuangalie uwezekano kwamba kina mama wanaweza kwamba hapa wasiorodheshwe kwamba wawepo katika hii sheria na mimi naungana nao moja kwa moja kwamba ziwepo pengine nafasi mbili za kina mama za wanawake katika Baraza hili.” Alimalizia kuchangia hoja hio.

Jamila Mahmoud ni Mkurugenzi wa Chama Cha Wanasheria Wanawake Zanzibar – ZAFELA amesema suala la kuwepo kwa msisitizo wa kuchaguliwa na kupatiwa nafasi kwa Maulama wanawake halipo kisheria hivyo hio ni miongoni kwa sababu kubwa ya wanaotoa nafasi cha kuchagu kuona hili jambo sio lazima na halina umuhimu “ Kwa mfano Sheria ya Mahakama ya Kadhi yam waka 2003 Kifungu cha 10(4) “Sheri ya Ofisi ya Mufti wa Zanzibar yam waka 2021 kwenye kipengele cha ufafanuzi imefafanua Ulamaa kuwa ni “ Mwanachuoni wa Kiislamu mwenye elimu ya kutosha ya fani mbalimbali ya dini ya kiislam na lugha ya kiarab”. Hapana hakuna sehemu iiyowekwa jinsia maana wanawake na wanaume wenye uwezo wa kielimu wapewe nafasi.

Jamila ameongeza kuwa changamoto kubwa iliyopo kwenye suala la wanawake Maulama kutokuwepo kwenye ngazi za maamuzi ni kwa sababu wanaopata nafasi za kuwateuwa hao maulama bado wanaamini kwenye mifumo dume”. Amemalizia Jamila.

Ofisi ya Mufti Mkuu kutokuwateua wanawake kwenye baraza la Maulamana Sheikh Khalid Ali Mfaume ni Katibu Mtendaji Ofisi ya Mufti Mkuu Zanzibar amesema wao hawana jukumu la kuwapatia wanawake nafasi ila Serikali ndio inajukumu hilo na pia serikali inazingatia vigezo maalum vya kupewa ajira. “Wanawake wanamchango wao kwenye jamii ila bado suala la wanawake kuwa kwenye baraza la ulama ani suala ambalo linahitajika kufanyiwa kazi” Alimalizia Sheikh Khalid.

LENGO LA SERIKALI NI KUBORESHA MAISHA YA KILA MWANANCHI TARAFA YA NGORONGORO-NCAA

$
0
0

 



SERIKALI kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema kuwa ina lengo la kuboresha maisha ya wananchi wa tarafa hiyo kwa kuwaelimisha na kuwahamisha wananchi waliojiandikisha kuhama kwa hiyari kwenda Kijiji cha Msomera Handeni Mkoani Tanga na maeneo mengine nchini.

Akizungumza na wananchi wa tarafa ya Ngorongoro kwa nyakati tofauti katika zoezi la uelimishaji, uhamaishaji na uandikishaji kaimu meneja wa Uhusiano kwa Umma wa mamlaka hiyo Hamis Dambaya amesema zoezi la kuwaelimisha wananchi hao litaendelea ili kuhakikisha kila mkazi wa tarafa ya Ngorongoro anahama kwa hiyari.

Amewaeleza wananchi hao kwamba serikali haina nia mbaya kwa kuwashawishi kuhama kutoka ndani ya hifadhi kwani inatambua kuwa iwapo wananchi hao watakubali kuhama wataweza kuboresha maisha yao katika maeneo mbalimbali watakayoamua kuelekea sambamba na kulinda usalama wao kutokana na uwepo wa matukio ya wanyama wakali ndani ya hifadhi.

“Mnaishi katika mazingira magumu hasa kutokana na kukosa uhuru wa kuingia na kutoka ndani ya hifadhi, kuhofia Wanyama wakali ambao wamekuwa hatari kwa mifugo na baadhi ya wananchi, serikali imefanya uamuzi sahihi wa kuwahamasisha ili kuwa na Maisha bora na huru nje ya hifadhi,”alisema bwana Dambaya.

Bwana Dambaya amesisitiza kuwa serikali imejipanga vizuri katika kuhakikisha kila mwananchi anayekubali kuhama kwa hiyari kutoka ndani ya hifadhi anapata stahiki zake zote za kisheria ikiwemo kitita cha shilingi milioni kumi wanaohamia msomera na shilingi Milioni kumi na tano wanaohamia maeneo mengine ambapo fedha hizi zinatolewa kama motisha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Amewataka wananchi hao kuachana na propaganda za baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wasiowatakia mema kwa kuwashawishi kuendelea kubaki ndani ya hifadhi huku wao na familia zao wakiishi katika miji mbalimbali nchini na kufanya shughuli zao katika mazingira magumu.

“Msihadaike na watu wenye nia ovu wanaowashawishi mbaki ndani ya hifadhi, hameni kwa hiyari kuelekea katika Kijiji cha Msomera na maeneo mengine ambayo huduma za kijamii zimeboreshwa kwa mustakabali wenu na vizazi vyenu”,alisema bwana Dambaya.

Katika ziara hiyo ya tarafa ya Ngorongoro timu ya uhamasishaji imeweza kutembelea kaya mbalimbali katika Kijiji cha Naiyobi, Kapenjiro na endulen ambapo wananchi kadhaa walielimishwa na kukubali kuhama kwa hiyari na kuamua kujiandikisha.

AIRTEL TANZANIA YAINGIA UBIA NA TADB KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO

$
0
0

 

Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Dinesh Balsingh wakibadilishana mkataba wa kuendeleza sekta ya kilimo na kuwa ya Kidijitali.
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Dinesh Balsingh wakisaini Mkataba wa kuendeleza sekta ya kilimo na kuwa ya Kidijitali.

AIRTEL TANZANIA imeingia makubalino na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa kusaini makubaliano (MoU) ya miaka mitatu ikiwa na lengo la kuinua na kuleta maendeleo katika sekta ya kilimo kwa njia ya mtandao yaani kidijitali.

Makubaliano ya ushirikiano huu kati ya Airtel Tanzania na TADB yanadhamira ya kufanikisha kupanua ushirikiano wa sekta ya kifedha kwa wadau mbalimbali ndani ya sekta kilimo, wakiwemo wakulima, wajasiriamali wadogo vijijini, hasa wanawake na vijana. Ushirikiano wa Airtel na TADB ni moja kati ya juhudi za Airtel Tanzania kuunga mkono serikali katika kuleta matokeo chanya katika maisha ya Watanzania.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuweka saini makubaliano hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Dinesh Balsingh, alisema “Airtel kwa kushirikiana na TADB tunadhamira ya dhati ya kusaidia Watanzania kupitia ubunifu katika sekta ya mawasiliano. Hii ni kwakuwa tunaamini wakulima wanastahili kuwa miongoni mwa vikundi vinatakiwa kunufaika na ukuaji wa teknolojia nchini. Hivyo, Ushirikiano wetu na TADB unalenga katika kutatua changamoto zinazowakabili wakulima kwa kutumia bidhaa mbalimbali za kidijitali ambazo zitaibua masoko mapya kwa wakulima mijini na vijijini. Bidhaa hizo zitawezesha uzalishaji wa wakulima na kuongeza mapato yao”.

Balsingh alieleza kuwa ushirikiano wa Airtel na TADB unaungana moja kwa moja na maono ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ya ukuaji wa sekta ya kilimo kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030. (Chanzo World Economic Forum). " Na hii inaonesha jinsi kilimo kilivyo muhimu katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi kwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ya watu wamejiajiri katika sekta ya Kilimo.".

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege alitoa shukrani zake kwa Airtel Tanzania akisema, ushirikiano wa Airtel na TADB utafungua milango ya fursa katika sekta ya kilimo. Ushirikiano huu utatoa fursa kwa wakulima kujipatia masuluhisho kwenye mahitaji na changamoto wanazokutana nazo katika shughuli zao za kila siku.

“Ubia wa Airtel na TADB unalenga kukuza ukuaji sekta ya kilimo. Ushirikiano huu ni mwanzo wa mabadiliko makubwa yatakayowagusa wakulima wote nchini Tanzania,” alisema Bw. Frank Nyabundege – Mkurugenzi Mkuu wa TADB.

Ushirikiano huu wa Airtel na TADB unakwenda sambamba pia na mikakati ya serikali ya kuunga mkono juhudi za wadau wa kilimo kwa kupambaa na changamoto mbalimbali ndani ya sekta ya kilimo kwa kuwawezesha wakulima kifedha kama ilivyotajwa na Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa mkutano wa wadau wa COP28 uliofanyika Disemba 4, 2023. Alisema, “tunatakiwa kubadilika na kufanya kilimo endelevu kwa kuunga mkono ubunifu mbalimbali unaoendana na hali ya sasa.”

WAKUU WA SHULE, MADEREVA ZINGATIENI USALAMA WA WANAFUNZI KIPINDI CHA MVUA - MAJALIWA

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wamiliki wa shule na madereva wa mabasi yanayotoa huduma za usafiri kwa wanafunzi wajiridhishe kuhusu njia wanazopita ili kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa wanafunzi wanaowabeba katika vyombo vya usafiri.

“Wazazi, Walezi na Jamii ya Watanzania kwa ujumla tushiriki kikamilifu katika kuhakikisha usalama wa wanafunzi wanapokwenda na kurudi Shuleni wakati wote hususan katika kipindi cha mvua.”


Kadhalika amesema kwa kuwa Serikali imetoa maelekezo ya kufunga shule zilizoathiriwa na mafuriko, halmashauri na wamiliki wa shule zisizo za Serikali waweke utaratibu wa kufidia muda wa vipindi ili kukamilisha kalenda ya muhula kama ilivyopangwa.

Ametoa wito huo leo (Alhamisi, Aprili 25, 2024) wakati akitoa taarifa ya serikali kuhusu changamoto za hali ya hewa bungeni jijini Dodoma.

Pia, amezitaka Taasisi za Serikali ziendelee, kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau kutekeleza majukumu yaliyoanishwa katika Mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na Madhara ya El-Nino pamoja na mipango ya kisekta ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.

“Kamati za Maafa za Wilaya na Mikoa ziendelee kuchukua hatua stahiki ikiwemo kutoa tahadhari kwa wananchi na kusaidia wananchi kwa wakati pindi maafa yanapojitokeza.”

Aidha, amewataka Wakuu wa mikoa na wilaya, maafisa tarafa, watendaji kata, mitaa na vijiji wasimamie ipasavyo usafi katika maeneo yao na kudhibiti utupaji taka ovyo unaosababisha kuziba kwa mitaro badala ya kusubiri usafi unaofanyika kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi.

“Kwa kuwa uharibifu wa mazingira umekuwa na athari kubwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi, viongozi wa ngazi zote washirikiane na wananchi kudhibiti uharibifu wa mazingira katika maeneo yao.”


Mheshimiwa Majaliwa pia amelitaka Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani liendelee kutoa tahadhari kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara wakati wa mvua;

“Kamati za Maafa katika ngazi za Vijiji, Wilaya na Mikoa zisimamie kikamilifu ugawaji wa misaada inayotolewa kwa waathirika wa mafuriko na kuhakikisha kuwa misaada inawafikia walengwa”.

Kadhalika amewataka Viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya Vijiji wahamasishe na kuelimisha wananchi wanaoishi mabondeni kuhamia maeneo salama ili kuepusha maafa wakati wa mafuriko na kuhakikisha wanatenga maeneo salama yatakayotumika na wananchi watakaohamia kutoka mabondeni.

Katika hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa amesema kutokana na maafa yaliyotokea nchini, Serikali kupitia Kamati za Usimamizi wa Maafa na wadau imechukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kuzuia, kukabiliana na kurejesha hali.

“Hatua hizo zinajumuisha utoaji wa elimu kwa jamii ya kujikinga na kuchukua tahadhari, kukabiliana na maafa na kurejesha miundombinu iliyoharibika. Aidha, Serikali imetoa misaada ya kibinadamu ikiwemo chakula, vifaa vya ujenzi, vifaa vya malazi na vifaa vya usafi.”

Amesema, hatua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa na misaada kutoka Serikalini na wadau kama vile uokoaji, vyakula, mahema, madawa, marekebisho ya miundombinu ya utoaji huduma imeendelea kutolewa.

“Serikali imejipanga kikamilifu na inaendelea kuchukua hatua stahiki ili kuzuia na kupunguza makali ya majanga sambamba na kurejesha hali katika maeneo mbalimbali yaliyoathirika.”

Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya hali ya hewa nchini ikiwemo kufunga miundombinu ya kisasa ya hali hewa, mafunzo kwa watumishi kwa kuzingatia vigezo vya kitaifa na kimataifa, na kuweka mifumo wezeshi ya usambazaji wa taarifa ya hali ya hewa pamoja na kuimarisha mifumo ya uhakiki wa ubora wa huduma.

Amesema uwekezaji wa miundombinu uliofanyika unajumuisha ununuzi wa Rada za Hali ya hewa ambapo Rada mbili zinakamilishwa kufungwa katika mikoa ya Kigoma na Mbeya. Vilevile, Rada nyingine mbili zinatarajiwa kufungwa Mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro ifikapo mwishoni mwa mwaka 2024.

“Nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika sekta ya hali ya hewa na kuijengea uwezo nchi yetu na kuifanya kuwa kinara Afrika na nje ya Afrika katika masuala ya utabiri wa hali ya hewa.”

TANZANIA NA CZECH MBIONI KUONDOA UTOZAJI WA KODI MARA MBILI

$
0
0

 

Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakibadilishana nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakisaini nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakionesha nyaraka za kukamilisha majadiliano, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Usimamizi wa Uchumi, Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwamdumbya na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech aliyeongoza ujumbe wa Czech Bw. Václav Zíka, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilika kwa majadiliano ya kuondoa vikwazo vya kikodi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)

Na. Saidina Msangi, WF, Dar es Salaam
SERIKALI ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Czech zimekamilisha majadiliano ya Mkataba wa Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili yatakayowezesha wawekezaji na wafanyabiashara watakaofanya shughuli zao kati ya nchi hizi mbili kutozwa kodi katika mapato yao katika nchi moja badala ya kila nchi kutoza kodi ya mapato.

Majadiliano hayo ambayo yamefanyika katika duru ya tatu yalikutanisha pande hizo mbili Tanzania ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwandumbya na Serikali ya Czech ikiongozwa na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech, Bw. Václav Zíka, katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kikao hicho Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwandumbya ambaye aliongoza ujumbe wa Tanzania katika majadiliano hayo, amesema kuwa hatua hiyo itavutia mzunguko wa biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Czech na kufungua fursa mpya za kiuchumi.

‘‘Mkataba huo utakaposainiwa utawezesha wawekezaji na wafanyabiashara watakaofanya shughuli zao kati ya nchi hizi mbili kutozwa kodi katika mapato yao katika nchi moja badala ya kila nchi kutoza kodi mapato ya aina moja na kusababisha changamoto ya utozaji kodi mara mbili (Double Taxation)’’, alifafanua Bw. Mwandumbya.

Naye kiongozi wa ujumbe wa Czech, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Masuala ya Kodi Kimataifa wa Wizara ya Fedha ya Czech Bw. Václav Zíka, alieleza kuwa Serikali ya Czech inatambua umuhimu wa Mkataba huo katika kuibua fursa za ajira, biashara na uwekezaji ambazo zitakuwa endelevu kutokana na kuweka mazingira ya kisera yanayotabirika.

Pamoja na hayo, amefafanua kuwa Mkataba huo utakaposainiwa unatarajiwa kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato kwa nchi hizo mbili kupitia upatikanaji wa taarifa za kikodi na utatuzi wa migogoro ya kikodi.

Kufuatia kukamilika kwa majadiliano hayo, kwa sasa inasubiriwa kukamilika kwa taratibu za ndani za kisheria kwa kila nchi kuwezesha Mkataba huo kusainiwa na hatimaye kuridhiwa ili kuanza kutekelezwa.

AKUKURU YAFANIKISHA MAREJESHO YA SH.MILIONI 439.2 KUTOKA KWA WANUFAIKA WA MIKOPO ASILIMIA 10 JIJI LA TANGA

$
0
0

 

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella akizungumza na waandshi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella akizungumza na waandshi wa habari ambao hawapo pichani wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.


Na Oscar Assenga,TANGA.
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru Mkoani Tanga imefanikisha marejesho ya kiasi cha Sh. Milioni 439,279,300.00 kutoka kwa wanufaika wa mikopo asilimia 10 katika Halmashauri ya Jiji la Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Tanga Victor Swella wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi kwaa kipindi cha Januari hadi Machi 2024 ambapo alisema kwamba moja ya kazi walioifanya ni ufuatiliaji wa ufanisi katika utekelezaji mkakati wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.

Alisema kwamba miongoni mwa changamoto waliozozibaini katika ufuatiliaji huo ni kutokuzingatiwa kwa masharti ya urejeshaji mikopo hiyo kwa wakati kutoka kwa wanufaika ambapo kabla ufuatiliaji kufanyika kiasi cha Bilioni 2,152,229,900 zilikuwa hazijarejeshwa kutoka kwa wanufaika wa mikopo hiyo na muda wa marejesho ulikuwa umeshapita.

Aidha alisema baada ya kulibaini hilo taasisi hiyo iliwakutanisha wadau na kuweka mapendekezo ya kurejesha fedha hizo na hadi kufikia mwezi Februari 2024 Jumla ya Sh.Milioni 439,279,300.00 zilikuwa zimerejeshwa katika Halmashauri ya Jiji la Tanga na kufanya fedha ambazo hazijarejeshwa kuwa ni Bilioni 1,712,950,600.00 huku jitihada za ufuatiliaji zinaendelea.

Mkuu huyo wa Takukuru alisema pia katika kipindi hicho walifanikiwa kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo 46 yenye thamani ya Bilioni 8,041,998,680.00 katika sekta za kipaumbele kama vile elimu,barabara ,maji na afya.

Alisema katika ufuatiliaji huo walibaini miradi 32 yenye thamani ya Bilioni 4,866,068,966.00 kuwa na mapungufu na ushauri ulitolewa wa kurekebisha mapungufu hayo kupitia vikao na wadau husika pamoja na kuanzisha uchunguzi wa miradi ambayo walibaini uwepo wa tuhuma za vitendo vya rushwa.

“Miongoni mwa miradi tunayoichunguza katika Halmashauri ya wilaya ya Korogwe ni manunuzi ya Sh. Milioni 6,400,000 ya uwekaji milango kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba za wakuu wa idara wenye thamani ya Milioni 245 lakini pia ujenzi wa madarasa mawili ,matundu 18 ya vyoo na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua wenye thamani ya Milioni 70,000,000 na uchunguzi unaofanyika ni wa ubadhirifu wa Sh.Milioni 30,000,000.00 kwenye ujenzi wa matundu hayo ya vyoo na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua.

Makamu wa Rais Dkt. Mpango Amewaagiza UCSAF Kuendelea Kusimamia Ujenzi wa Minara ya Mawasiliano

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye mara baada ya hafla ya Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule,Mtendaji Mkuu wa UCSAF Justina Mashiba na viongozi mbalimbali katika picha ya pamoja watumishi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) mara baada ya kuzindua jengo la Taasisi hiyo lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiweka jiwe la msingi la Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisikiliza maelezo kutoka kwa Msanifu Majengo Arch. Msuya Abdulkarim kuhusu Jengo la Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) wakati alipowasili kwaajili ya kuzindua jengo hilo lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Tarehe 25 Aprili 2024.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa maagizo kwa Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kuendelea kusimamia kwa karibu ujenzi wa minara ya mawasiliano na kuhakikisha vijiji ambavyo havina huduma za uhakika za mawasiliano ya simu vinapata mawasiliano.


Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo wakati wa uzinduzi wa Jengo la Makao Makuu ya Ofisi ya Taasisi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) lililopo eneo la Njedengwa mkoani Dodoma. Amesema ni muhimu kuhakikisha Wananchi wanapata mawasiliano ya uhakika wakati wote ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi hususan katika kipindi hiki ambapo huduma nyingi zinawezeshwa na huduma za mawasiliano. 


Aidha Makamu wa Rais ameitaka UCSAF kuendelea kutekeleza miradi ya kuongeza uwezo wa minara kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G na 4G.  Amesema huduma nyingi za jamii hivi sasa zinawezeshwa kwa kutumia intaneti ni muhimu kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma hiyo mijini na vijijini.


Vilevile Makamu wa Rais ameiagiza UCSAF kujipanga kuongeza misaada ya vifaa vya TEHAMA hususan kwenye shule za umma ili kuongeza hamasa kwa wanafunzi kupenda masomo ya TEHAMA na kukuza matumizi ya intaneti nchini. Ametoa  wito kwa sekta binafsi na sekta ya umma kushirikiana na UCSAF kuongeza idadi ya shule zinazopokea huduma hiyo na vifaa vya TEHAMA ili kuwezesha watoto kujifunza kwa urahisi.


Halikadhalika ametoa wito kwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kushirikiana na wadau ikiwemo sekta binafsi kuona uwezekano wa kuiongezea UCSAF uwezo, ikiwemo fedha na rasilimali nyingine ili kuiwezesha kufikisha huduma za mawasiliano katika maeneo yasiyo na huduma ya televisheni na redio za hapa nchini. Amesema ni vema  UCSAF iangalie uwezekano wa kuwezesha matangazo ya televisheni na redio kuwafikia wananchi kwa njia ya mtandao.


Kwa upande wake Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema kupitia UCSAF asilimia 98 ya wananchi waliopo katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mjini yasio na mvuto wa kibiashara wamenufaika na huduma za mawasiliano. Ameongeza kwamba wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini wamepata fursa ya kushiriki katika mageuzi ya kidijiti nchini kwa kuwa sehemu ya watumiaji wa huduma za fedha kwa njia ya mtandao.


Aidha Waziri Nape amesema sekta ya mawasiliano imeendelea kukua kwa kasi hapa nchini ambapo kufikia mwaka 2024 jumla ya laini za simu milioni 72 zimesajiliwa kulinganisha na laini za simu milioni 51 mwaka 2020. Pia amesema zaidi ya minara 600 hapa nchini inatumia huduma ya 5G.


Amesema kwa sasa ni muhimu kufanya uwekezaji wa namna ya kutengeneza vifaa vinavyotumia mtandao ikiwemo simu janja hapa nchini ili uwekezaji unaofanywa na serikali katika kuboresha mawasiliano kuendelea kuwa na tija.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Mngereza Mzee Miraji amesema kupitia UCSAF kwa kipindi kifupi jumla ya minara 47 imejengwa Zanzibar pamoja na ujenzi wa vituo 11 vya tehama Unguja na Pemba ambavyo imekua vikisaidia vijana kwa kiasi kikubwa. 


Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ni Taasisi ya Serikali ambayo ina jukumu la kuhakikisha mawasiliano yanafikishwa katika maeneo ya vijijini na mjini yasio na mvuto wa kibishara. Mfuko huo hushirikiana na watoa huduma za mawasiliano katika kujenga minara inayowezesha upatikanaji wa mawasiliano ya simu pamoja na uimarishaji wa matangazo ya redio na televisheni.


Uzinduzi wa Jengo hilo ni shamrashamra kuelekea Miaka 60 ya Muungano.

Imetolewa na 

Ofisi ya Makamu wa Rais

25 Aprili 2024

Dodoma.

TANZANIA YACHAGULIWA KUWA MAKAMU MWENYEKITI BARAZA LA MAWAZIRI WA MAJI KAMISHENI YA BONDE LA MTO ZAMBEZI

$
0
0
TANZANIA imechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa ZAMCOM katika mwaka 2024-2025 kwenye Mkutano wa 11 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (Zambezi Watercourse Commission - (ZAMCOM) unaoendelea mjiji Tete Nchini Msumbiji.

Uchaguzi huo umefanyika kufuatia Msumbiji kumaliza muda wake na kukabidhi uenyekiti kwa Namibia, Hivyo, Tanzania inategemewa kuwa Mwenyekiti wa ZAMCOM.

Katika mkutano huo, Tanzania imewakilishwa na Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew.

Licha ya kushiriki Mkutano wa 11 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi (Zambezi Watercourse Commission - ZAMCOM), Tanzania imefanya mazungumzo na wadau wa maendeleo na kuwakaribisha kuwekeza katika Sekta ya Maji nchini Tanzania.

Mhandisi Kundo ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo amekutana na kufanya mazungumo na Mwakilishi wa Shirika la Sweden, SwedFund.

Katika mazungumzo hayo, Tanzania imeikaribisha Taasisi ya SwedFund nchini ili kushirikiana katika maeneo ya maandalizi ya miradi ya miundombinu yenye ukubwa wa kati na wa juu.

Nae mwakilishi wa SwedFund ameahidi kushirikiana na Tanzania katika kufanya majadiliano kuhusu kuandaa miradi mahsusi.



MWENGE WA UHURU KUINGIA MKOA WA PWANI APRILI 29

$
0
0

 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge akizungumza  na Waandishi wa Habari  Ofisini kwake leo Aprili  25, 2024 hawapo pichani.

Na Khadija Kalili, Michuzi Tv
MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge ametoa ratiba ya kuukimbiza Mwenye wa Uhuru ambao utaingia Mkoa wa Pwani Aprili 29 ukitokea Mkoa wa Morogoro.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano leo Aprili 25 amesema kuwa Mwenge huo wa Uhuru utakimbizwa kwa siku saba.

RC Kunenge amesema kuwa baada ya kuupokea Mwenge wa Uhuru utaanza kukimbizwa Aprili 29 ndani ya Halmashauri ya Chalinze na Aprili 30 utakimbizwa Halmashauri ya Bagamoyo huku Mei mosi utaikimbiza Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Mei mbili utakimbizwa Halmashauri ya Mji Kibaha Mei tatu utakimbizwa Kisarawe, Mei 4 Mkuranga, Mei tano Mwenge wa Uhuru utakimbizwa Rufiji na Mei 6 utakimbizwa Kibiti huku Mei 7 utakimbizwa Mafia na Mei nane utakabidhiwa Mkoa wa Dar es Salaam.

"Mkoa wa Pwani haturudi nyuma tutakuwa na mipango mizuri zaidi awali ya yote tumegundua changamoto ambazo zimetukabili za mvua hivyo kuna baadhi ya miradi ambayo imebidi tuighairi kutokanaa na mvua.

"Kimkoa tumejipanga vizuri na tunatarajia utakimbizwa katika Wilaya zetu zote tisa pia napenda kuchukua fursa hii kiwaomba wananchi wote wajitokeze kukimbiza Mwenge na kukahikisha tunafanikisha mbio za mwaka huu za mwaka 2024, huku tukitarajia kufumisha upendo,amani utu na heshima.

Amesema pindi mwenge ukikimbizwa Mkoa ni pwani utakua nakauli mbiu za Kuzuia na kuoambana a rushwa ni jukumu lako na langu tutimize wajibu,jamii iunge jitihada za kutokomeza uonjwa wa UKIMWI, Epuka dawa za kukevya zingatia utu boresha tiba na kinga na mwisho Lishe siyo kujaza tumbo zingatia unachokula,

Ziro Malaria inaanza na mimi chukua hatua kuotokomeza.

TFS WACHANGIA MIL.20 KWA WENYE MAAFA KIBITI NARUFIJI

$
0
0

 

Na Khadija Kalili ,Michuzi Tv
MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge leo amepokea hundi yenye thamani ya Mil.20 kutoka Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) ikiwa ni katika muendelezo wa kuchangia watu wa Kibiti na Rufiji ambao wamepata changamoto ya mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea nchini kote.

Imeelezwa na Afisa Uhusiano wa TFS Johary Kachwamba kuwa msaada huo umetolewa na Kamishna wa Uhifadhi TFS ikiwa na lengo la kuwapa pole wakazi hao.

Afisa Uhusiano Kachambwa ndiye aliyemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Pwani Kunenge hundi hiyo ambapo makabidhiano yamefanyika katika viwaja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Pwani.

"Wakaazi wa Kibiti na Rufiji ni wenzetu kwani tunazo hifadhi za misitu zaidi ya kumi zenye Hekta 32,000 hivyo ni wajibu wetu kuwapa pole" amesema Kachwamba.

"Tunatoa pole kwa RC Kunenge

Akizungumza mara baada ya kupokea hundi hiyo RC Kunenge ametoa shukrani zake za Mkoa kwa TFS dhati kwa hundi hiyo pia kwa kuwapa eneo ambalo watahamishiwa watu ambao wamepata chagamoto ya nyumba zao kukumbwa na mafuriko katika maeneo ya Kibiti na Rufiji.

"Pia namshkuru Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa misaada ya hali na mali aliyowapatia wananchi wa maneo yaliyokumbwa na changamoto ya mafuriko ndani ya Mkoa wa Pwani ,Tunawashukuru TFS kwani fedha hizi zitasaidia kutatua changamoto zilizowakumba wenzetu wa KibitinaRufiji.

Tanzania na Urusi Kushirikiana Kudhibiti Uhalifu wa Kimtandao

$
0
0


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa wizara hiyo, Miriam Mmbaga(kulia) wakionyeshwa jinsi Mfumo wa Kudhibiti Uhalifu wa Kimtandao unavyofanya kazi na Mtaalumu wa Teknolojia ya Habari kutoka Kampuni ya KOMIB,Egor Bogomolov wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini Urusi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

Na Mwandishi Wetu,URUSI
SERIKALI imedhamiria kushirikiana na nchi ya Urusi katika kudhibiti uhalifu nchini ikiwemo uhalifu wa mtandao ambao umeanza kushamiri katika maeneo mbalimbali nchini huku ikiweka wazi dhamira ya kujengewa uwezo kwa askari wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na nchi zilizoendelea kiteknolojia katika kudhibiti uhalifu huo unaotajwa kuvuka mipaka.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama unaoendelea nchini Urusi ambao ulifunguliwa na Rais wa Shirikisho la Urusi na kuongozwa na Katibu wa Baraza la Usalama la Shirikisho la Urusi, Nikolai Patrushev.

‘Katika kudhibiti masuala ya uhalifu wa kimtandao matumizi ya teknolojia hayaepukiki ndio maana serikali imeona kuna haja ya kuimarisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama katika Nyanja mbalimbali ikiwemo ujuzi kwa askari wetu sasa kupitia mkutano huu tunaenda kujenga mahusiano kati ya Jeshi la Polisi la Tanzania na Jeshi la Polisi la Urusi ili tuweze kudhibiti uhalifu wa kimtandao ambao umekua ukisababisha madhara mbalimbali katika jamii ikiwemo ya kiusalama,kiuchumi na hata maadili’. Alisema Waziri Masauni

Akizungumza wakati wa Mkutano huo Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Miriam Mmbaga alisema muelekeo wa wizara katika kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ina mkakati maalumu wa kuwajengea uwezo askari waliopo katika Vyombo vya Ulinzi hasa katika masuala ya teknolojia huku akiweka wazi juu ya suala la ajira pia kuweka kipaumbele kwa watu waliosomea masuala ya teknolojia ya Habari.

Mkutano huo wa Kimataifa wa Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama umehudhuriwa na nchi takribani 20 huku msisitizo zaidi ukiwekwa katika kupambana na uhalifu wa kutumia teknolojia ambao umekua ni tishio katika mataifa mbalimbali.
Katibu wa Baraza la Usalama la Shirikisho la Urusi, Nikolai Patrushev (wa kumi na tano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani ya nchi 20 Duniani waliokutana nchini Urusi katika Jiji la St.Petersburg kujadili changamoto ya uhalifu wa kimtandao na jinsi ya kupambana nao.Tanzania pia inashiriki mkutano huo ikiwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kushoto) akionyeshwa jinsi ndege isiyo na rubani inavyoweza kupambana na uhalifu na Afisa kutoka Kampuni ya DOMINA,Alexeen Alexander wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini UrusiPicha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa wizara hiyo, Miriam Mmbaga(wapili kushoto) wakisikiliza ufafanuzi wa programu maalumu ya kudhibiti uhalifu wa Kimtandao kutoka kwa Meneja Mauzo wa Kampuni ya SOLAR,Timul Solovev wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini Urusi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
aziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu wa wizara hiyio, Miriam Mmbaga(katikati) wakisikiliza maelezo ya kudhibiti uhalifu wa kimtandao kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya Kupambana na Uhalifu wa Kimtandao(CyberED),Gadzhi Akhmedov wakati wa Maonesho ya Teknolojia ya Kudhibiti Uhalifu huo yanayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa EXPOFORUM ambapo Maafisa wa Daraja la Juu kutoka serikalini wanaohusika na mambo ya Usalama kutoka takribani nchi 20 Duniani wamekutana nchini Urusi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

ROMBO MPYA YA KUWEKEZA KWENYE ELIMU - DC MWANGALA

$
0
0

 



Na Mwandishi wetu, Rombo
MKUU wa wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, Raymond Mwangala amewataka wakazi wa eneo hilo kuwekeza kwenye elimu kwani mataifa mengi yameendelea kutokana na kuwekeza katika elimu.


Mwangala akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya elimu ya sekondari na kugawa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu vyema kidato cha nne, shule zilizofaulisha na walimu wao amesema Rombo mpya ya maendeleo imezaliwa hivyo jamii iwekeze kwenye elimu.


Amesema hivi sasa wilaya ya Rombo imezaliwa upya ikilenga kutazamwa kwa mtazamo chanja tofauti na awali ilivyozungumzwai na ndiyo sababu eneo la kwanza la Mamsera itawekwa taa za barabarani hadi Mkuu.


"Tunaiona Rombo mpya ya maendeleo, tuna maprofesa wengi nchi nzima wametokea Rombo, kuna madokta, mapadri hata marehemu Gadna G Habash kumbe kwao ni Tarakea na aliyekuwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) Ludovick Utouh ametokea Rombo," amesema.


Amesema amelenga kushirikiana na jamii ya Rombo kuwekeza kwenye elimu ili maendeleo yapatikane kwani nchi nyingi zilizoendelea zimewekeza katika elimu.


"Matajiri wengi wa Dar es salaam, Dodoma, Arusha na kwingine wametokea Rombo, tunataka Rombo mpya ya maendeleo, watu waje Rombo kuona utalii wa mtori na ndizi na watu wenye maendeleo," amesema.


Ofisa elimu sekondari wa halmashauri ya wilaya ya Rombo, Silvanus Tairo amesema kikao hicho kitakuwa chachu ya kuongeza ufaulu mzuri kwa wanafunzi kwani wamejipangia mikakati ya kuboresha elimu na kupambana na changamoto zilizopo.


Tairo amewapongeza walimu waliofanikisha wanafunzi 1,700 kupata daraja la kwanza hadi daraja la tatu ambao ndiyo wenye sifa za kuendelea na elimu ya juu na vyuo mbalimbali.


"Lengo ni kufanya tafakuri ya elimu na kuweka mikakati ambayo itatusaidia kufanya vzuri zaidi kwenye mitihani ijayo na pia kuwapa motisha wanafunzi, walimu na shule husika kufanya vyema zaidi," amesema Tairo.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda ambaye pia ni mbunge wa Rombo, akizungumza kwa njia ya simu, amewapongeza walimu kwa namna wanavyojitahidi kunyanyua kiwango cha elimu kwa kuwafundisha wanafunzi.


"Nawaahidi kuwa tutaendelea kushirikiana pamoja walimu wangu ili sekta hii muhimu iweze kuwanufaisha watoto wetu ambao watakuwa na manufaa kwa Taifa," amesema Prof Mkenda.


Kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Rombo, Christina Marwa ameipongeza idara ya elimu sekondari kwa ubunifu huo wa kufanya tathimini na kutoa zawadi kwa ufaulu.


"Tumeona jambo hili ni jema mno hivyo mwakani mjipange upya na kulifanya kwani litakuwa na matokeo chanya kutokana na hamasa hii iliyofanyika kwa walimu na wanafunzi," amesema Marwa.


Mmoja kati ya wanafunzi walipatiwa zawadi kwa ufaulu mzuri Deus Mdee wa shule ya sekondari Kelamfua amesema motisha walizopata zitaongeza ari kwa wanafunzi kusoma zaidi na walimu kufundisha kwa moyo wote.


"Nashukuru kwa zawadi ya madaftari kwani lengo langu ni kuwa daktari na sasa nasubiria kupangiwa shule ili niende na masomo ya kidato cha tano," amesema.






Latest Images