Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

Katibu mkuu wa ccm,ndugu Kinana apata mapokezi makubwa mjini songea ,afungua semina ya viongozi wa mashina

0
0
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia mikono mabalozi wa mashina,Matawi na Kata mara baada ya kuwasili  kwenye uwanja wa Maji Maji mjini Songea mapema leo mchana mkoani Ruvuma.Ndugu Kinana alifungua Semina ya viongozi hao juu ya kuimarisha chama na kuhusu mambo muhimu ya kuzingatia katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha CCM,alikuwa ameambatana pia na Mbunge wa jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dkt. Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani).
Pichani ni mabalozi na Wenyeviti wa mashina wakiwa wamekusanyika kwenye uwanja wa Maji Maji mjini Songea mapema leo mchana,tayari kwa kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana aliyewasili mjini humo mapema leo kwa ajili ya kufanya semina na viongozi hao.
 Mbunge wa jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dkt. Emmanuel Nchimbi  akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,Ndgu Kinana mara baada ya kuwasili mjini Songea leo na kupata mapokezi makubwa akitokea mkoani Jombe baada kuhitimisha ziara yake ya siku saba.
Ndgu Kinana akijadiliana jambo na Mh.Nchimbi mara baada ya kuwasili mjini Songea leo na kupata mapokezi makubwa akitoka mkoani Jombe kwa ziara ya siku saba.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akivalishwa skafu mara baada ya kuwasili leo kwenye Ofisi kuu ya chama cha CCM mjini Songea, ambapo pia alifanya mkutano mfupi na baadhi ya Wanachama katika suala zima la kuhimiza namna ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi.

Rais Kikwete akutana na Mwenyekiti wa mambo ya nje wa bunge la Japan

0
0
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje ya bunge la Japan Mh.Katsyuki Kawai wakati mwenyekiti huyo alipomtembelea na kufanya naye mazungumzo jijini Yokohama leo .Wengine katika picha kushoto ni Mbunge wa Nzega Dkt.Hamisi Kigwangala na kulia ni Mbunge wa Kasulu mjini Mh.Moses Joseph Machali.Wabunge hao ni wajumbe walioko katika msafara wa Mheshimiwa Rais anayehudhuria Mkutano wa tano wa TICAD unaoendelea jijini Yokohama Japan(picha na Freddy Maro).

SALSHIA ISDORE NDIYE REDD'S MISS GEITA 2013

0
0


Mshindi wa taji la Redd’s Miss Geita 2013, Salshia Isidore (katikati) akiwa mwenye furaha wakati wa kupiga picha ya pamoja na warembo wqenzake Stella Magerezi (kulia) aliyeshika nafasi ya pili na Mshindi wa tatu wa shindano hilo, Nurieth Rashid. Salshia aliwashinda warembo wenzake 12 waliokuwa wakiwania taji hilo pamoja nae.
******      *******
Na Father Kidevu Blog, Geita.

MREMBO Salshia Isidore amechaguliwa kuwa Redd’s Miss Geita 2013 baada ya kuwashinda warembo wenzake 12 katika shindano lililifanyika Jumamosi  Juni 1,  kwenye ukumbi wa Desire uliopo mjini Geita.

Wengine walioingia nafasi ya tatu bora ni pamoja na Nurieth Rashid aliyeshika nafasi ya tatu na Stella Magerezi alishika nafasi ya pili.

Katika shindano hilo lililosindikizwa na burudani safi kutoka kwa msanii Baby Madaha na Bob Haisa huku mgeni rasmi akiwa ni Mbunge wa Viti Maalum wa Geita Vicky Kamata.

Washindi hao watatu watawakilisha mkoa wa Geita kwenye shindano la Kanda ya Ziwa ili kuwapata washiriki watakaoenda ngazi ya taifa.

Akizungumza na washindi pamoja na warembo wengine kwa ujumla Vicky aliitaka jamii ya watu wa Geita kuyatambua mashindano hayo kuwa ni muhimu na yanasaidia suala la ajira.

Alisema kuwa kupitia mashindano hayo kuna mengi ambayo yanaweza kufanyika kwa kuwa mashindano hayo ni fursa ya kuzungumza na wananchi kuielezea masuala mbalimbali ya kimaisha.

“ Najua kwa sasa hata katika Bunge hili la bajeti kuna mengi ambayo tumeyajadili na kuyapitisha kwa ajili ya vijana na hasa pia kupitia sanaa na hivyo mashindano kama haya yanahusika kabisa” alisema Vicky.

Naye mwandaji wa shindano hilo alisema kuwa washindi hao mshindi wa kwanza amepewa laki tatu, huku wa pili amepewa laki mbili na wa tatu laki tatu.
 Warembo waliofanikiwa kuingia hatua ya tano bora wakiwa katika picha ya pamoja.
 Wanyange walioshiriki shindano la Redd's Miss Geita 2013 wakiwa katika picha ya pamoja jukwaani.
Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoani Geita, Vicky Kamata (kulia) akitoa nasaha zake kwa washindi na warembo wote walioshiriki shindano hilo.

semina elekezi ya Airtel Rising Stars yafanyika jijini dar.

0
0
Baadhi ya makatibu wakuu wa mikoa wa vyama vya soka vya mikoa inayoshiriki michuano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars wakifuatilia kwa makini kanuni za mashindano hayo wakati wa semina elekezi iliyofanyika TFF leo.
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Bw. Jackson Mmbando akiongea na makatibu wakuu wa mikoa na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TFF leo.
Katibu mkuu mkoa wa kisoka wa Temeke Mbarouk Mhamed (kulia) akichukua karatasi wakati wa kupanga makundi na ratiba ya michuano ya Taifa ya Airtel Rising Stars iliyopangwa kuanza mwezi Julai, 2013 uwanja wa Kumbu Kumbu ya Karume jijini Dar es Salaam. Kushoto ni katibu wa DRFA Msafiri Kondo.

========== ======= ==============
FAINALI za Taifa za michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 za Airtel Rising Stars zimepangwa kuanza kutimua vumbi uwanja wa Kumbu Kumbu ya Karume jijini Dar es Salaam Julai 2 kwa mabingwa watetezi Temeke wavulana kupambana na Kinondoni. 

 Akizungumza wakati wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars 2013 iliyofanyika Juni mosi katika ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Ofisa Maendeleo wa shirikisho hilo Bw. Salum Madadi alisema ARS ngazi ya mikoa imepangwa kuanza Juni 15 hadi 29. 
 Mikoa inayoshiriki Airtel Rising Stars mwaka huu kwa upande wa wavulana ni mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke. Mikoa mingine ni Morogoro Mwanza na Mbeya ambapo kila mkoa unatakiwa kushirikisha timu sita. 

Usajili wa timu umepangwa kuanza rasmi kesho Juni 2 na kumalizika Juni 11. Kwa upande wa timu za wasichana, alisema, mikoa itakayoshiriki ni Tanga, Kigoma na Ruvuma na mikoa yote inayoshiriki Airtel Rising Stars mwaka huu iliwakilishwa kwenye semina elekezi na makatibu wakuu ambao walipata fursa ya kupitia kanuni na taratibu za michuano hiyo ya vijana. 
Upangaji wa ratiba uliofanyika leo ni wa fainali za taifa pekee kwa kuwa mashindano ya ngazi ya mkoa yataendeshwa na uongozi wa mkoa husika ikiwa ni pamoja na kupanga ratiba yake. 

Kwa upande wa wasichana timu zitakazofungua dimba katika fainali za taifa ni Ilala na Kinondoni. Kwa ujumla timu 12 zitashiriki fainali za Taifa, sita za wasichana na sita za wavulana. 

 Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo, Meneja wa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mbando alitoa rai kwa makatibu wakuu wa mikoa kuwa makini wakati wa usajili ili kupata vijana wenye vipaji ambao wataiwakilisha vema Tanzania kwenye michuanoa ya kimataifa ya Airtel Rising Stars. 

Vile vile Tanzania itawakilishwa kwenye klini itakayofanyika chini ya makocha wa Manchester United. Alisisitiza alisema nia thabiti ya Airtel Tanzania kuendelea kusaidia mashindano ya vijana kwa nia ya kuendeleza soka nchini na kuishukuru TFF na wizara inayohusika na michezo kwa kuyaunga mkono mashindano haya. 


Naye mgeni rasmi katika semina hiyo , Katibu Mkuu wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Msafiri Kondo aliwaomba wadhamini kuendelea kudhamini michuano hiyo ili vijana wa kike na kiume waweze kufikia malengo yao katika soka. 

Mashindano ya mbuzi ya hisani Dar 2013 yatimua vumbi jijini Dar.

0
0
Mbuzi wakishindana ili kumpata mshini wa katika mbio zilizopewa jina ‘The Southern Sun Fillies Frolic’ wakati wa mashindano ya mbio za mbuzi za hisani jijini Dar es Salaam jana.
Ni wakati wa mashindao ya mavazi ya kufurahisha wakati wa mashindano ya mbio za mbuzi za hisani jijini Dar es Salaam jana.
Mbuzi wakiwekwa tayari kuchuana katika mbio za ‘The Coca Cola Open Happiness Sweep Stakes’ wakati wa mashindano ya mbio za mbuzi za hisani jijini Dar es Salaam jana.

Air Tanzania yatua Tabora

0
0
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Gulam Remtullah, (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mda mfupi baada ya kupokea abiria wa kwanza kutumia ndege ya Shirika la ndege la Taifa Air Tanzania, baada ya shirika hilo kurejesha huduma zake mkoani Tabora, iliyositishwa kwa kipindi ya zaidi ya mwaka mmoja  kupisha marekebisho ya uwanja huo. ATCL imekuwa ndege ya kwanza kubwa kuanza safari zake mkoani hapo. Kulia ni Afisa Mwongozaji wa ndege wa shirika la ndege la ATCL, Kabel Msumeno.
 Abiria wa kwanza kutumia ndege ya Shirika la ndege la Taifa ya Air Tanzania, wakishuka katika uwanja wa ndege wa Tabora, baada ya kufurahia safari yao kutoka Dar es Salaam. Ddege ya ATCL imekuwa ya kwanza kubwa kuruka mkoani hapo, baada ya huduma ya safari za ndege ya abiria kusitishwa kwa zaidi ya mwaka mmoja ili kupisha ujenzi wa uwanja huo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Gulam Remtullah, akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la ndege la Taifa ya Air Tanzania mda mfupi baada ya ndege ya shirika hilo kurejesha huduma zake mkoani Tabora, iliyositishwa kwa kipindi ya zaidi ya mwaka mmoja  kupisha marekebisho ya uwanja huo. ATCL imekuwa ndege ya kwanza kubwa kuanza safari zake mkoani hapo.

========  =======  =========  ========
Air Tanzania yatua Tabora

NDEGE ya Shirika la Ndege la Taifa la Air Tanzania Jumamosi ilitua katika uwanja wa ndege uliokarabatiwa wa Tabora, na kulifanya kuwa ndege ya kwanza kubwa kuruka katika njia hiyo baada ya kuhairisha huduma hiyo kwa zaidi ya mwaka mmoja kupisha ukarabati wa uwanja huo.

Safari hiyo ilipokelewa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Bw. Gulam Remtullah, ambaye alisema kuwa kuahirishwa kwa huduma za ndege kwa mwaka mmoja kumesababisha kuzorota kwa biashara mjini Tabora na mkoa wote kwa ujumla kwa kuwa mkoa huo ulibaki na barabara pekee kama kiungo muhimu na mikoa mingine, hivyo kuwa changamoto kwa maendeleo ya biashara.
      
“Kurejeshwa kwa safari za Ndege za Air Tanzania kumeupa mkoa nguvu mpya ya kujikita katika maendeleo zaidi. Kuna biashara nyingi zilizodhurika pamoja na huduma zinazohitaji usafiri wa haraka hazikuwa zikitolewa kwa kuwa mkoa haukuwa na shirika lolote la ndege linalotoa huduma katika mkoa wetu.

“Sasa kwa kuwa shirika letu la Ndege la Taifa limeanza kutoa huduma mkoani hapa tena, ningependa kuuomba uongozi wa shirika kufikiria kuruka Tabora kila siku kwa kuwa watu wengi wanahitaji huduma hii. Hii inathibitishwa na idadi kubwa ya abiria waliokata tiketi kwa ajili ya safari hii ya kwanza kuja Tabora na kutoka Tabora kuelekea sehemu nyinginezo. Kama shirika litaendelea kutupatia huduma nzuri, litaendelea kuaminiwa na wateja wengi zaidi,” alisema Remtullah.

Safari zilizotambulishwa zitakuwa katika siku za Jumatatu, Alhamis na Jumamosi ambapo muda wa kuruka kwa Jumatatu na Jumamosi utakuwa ni saa 5:30 asubuhi, ndege ikiruka moja kwa moja kuelekea Tabora na Jumatano saa 12:30 asubuhi ikiruka kupitia Kigoma, kwa kutumia ndege aina ya De-Havilland Dash8 – Q300 ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 50.    

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Kapteni Milton Lazaro, wakati wa kutangaza kuanzishwa safari za Tabora ilisema kuwa shirika hilo limejipanga kutoa huduma ya usafiri, yenye bei nafuu, salama na ya uhakika kwa abiria watakao tumia njia hiyo.

Alisema kuwa maamuzi ya uongozi wa ATCL kurejesha njia ya Tabora ni suala jema katika kutimiza azma yake ya kukuza ushirikiano  wa Tabora na mikoa mingine.
“Tunaamini kurejeshwa kwa safari katika njia hii kutakuwa ni chachu ya maendeleo ya uchumi katika mkoa wa Tabora na Kanda ya Ziwa kwa ujumla,” alisema.

Kpt. aliongeza kuwa kurejea kwa njia hiyo ya Tabora kumetokana na kilio cha wananchi, maombi toka kwa mawakala wa usafiri na Bunge wakilitaka shirika la ndege la taifa kutimiza dhamira yake ya kufanya biashara na kuwahudumia wananchi.
Aidha, alibainisha kuwa shirika lake limejidhatiti kwa kuwa na mpango madhubuti ambao utapelekea shirika kufungua njia mpya nchini ikiwa ni pamoja na Songwe, na kurejesha safari za Arusha, Zanzibar na Mwanza.

“Njia hizi mpya zitaanza kufanyakazi baada ya kupokea ndege yetu mpya baadae mwaka huu. Baada ya upatikanaji wa ndege hiyo ukithibitishwa wananchi watapatiwa taarifa,” alisema.

President Kikwete and former Japanese Prime Minister Yoshiro Mori speaks on Efforts to Fight Infectious Diseases

0
0
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete speaks during a high level panel on “Accelerating the Global  Fight against Infectious Diseases,” held as TICAD V official side event in Yokohama, Japan this morning.on Right side is the former Japan Prime Minister Yoshiro Mori 
  President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete and former Japan Prime Minister Yoshiro Mori shortly after they participated in a high level panel on” Accelerating the Global fight against Infectious Diseases,” held in Yokohama this morning.
 A cross section of the participants to the high level panel on ““Accelerating the Global  Fight against Infectious Diseases,” held as TICAD V official side event in Yokohama, Japan this morning claps as President Jakaya Mrisho  Kikwete concludes his keynote address.(photos by Freddy Maro).

NSSF YAENDESHA ZOEZI LA UPIMAJI MACHO KWA WABUNGE

0
0
Dk. Yasinta Shobola akimchukuwa vipimo, Mbunge wa Mfindi Kusini(CCM), Mendrad Kigola wakati wa zoezi la kupima  afya kwa wabunge lililoendeshwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Viwanja vya ukumbi wa Bungeni Mjini Dodoma.
Mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Said Bungala (kulia) akipima macho wakati wa zoezi la kupima  afya kwa wabunge lililoendeshwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Viwanja vya ukumbi wa Bungeni Mjini Dodoma.
Mbunge wa Mufindi Kusini (CCM), Mendrad Kigola akipima macho wakati wa zoezi la kupima  afya kwa wabunge lililoendeshwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Viwanja vya ukumbi wa Bungeni Mjini Dodoma.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA RASIMU YA KATIBA MPYA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KARIMJEE DAR LEO

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiinua juu na kunyesha Kitabu cha Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, (kushoto) ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.  Katikati ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya,Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Iddi baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Rasimu ya Katiba mpya, Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Asha-rose Migiro, baada ya uzinduzi rasmi wa rasimu hiyo uliofanyika leo Juni 03, 2013 katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa Makamu, ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd (kushoto) ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, Joseph Sinde Warioba.

kutoka bungeni.

0
0
 

Naibu Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi,Gudluck Ole Medeye,katikati,akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion,Alex Msama,(kushoto)walipokutana nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma,mara baadaya kuahirishwa kikao cha bunge kilichojadil na kupitisha bajeti ya Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa,kulia,ni Naibu Waziri wa Maji Dk,Binirith Mahenge.

Mbunge wa Viti maalum CCM,Dk Mary Mwanjelwa,akiuliza swali kwa Wizara ya Sayansi na  Teknolojia,Bungeni mjini Dododma, kuhusu mawasiliano mipakani mwa Nchi,swali hilo pamoja na la nyongeza yalijibiwa na Naibu waziri wa Wizara hiyo,January Makamba.

CHUO CHA UALIMU KASULU KINAKABILIWA NA CHANGAMOTO KUBWA YA UFUNDISHAJI WA SOMO LA IT

0
0
Mkuu wa Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoa wa Kigoma Mwl.Joseph Mwangamila,wa pili toka kushoto akikabidhiwa msaada wa Kompyuta Tano zenye thamani ya shilingi Milioni 6 na mshindi wa”Vodacom Mahela”Bw.Valerian Kamugisha ambae ni mwanafunzi wa chuo hicho kwa niaba ya Vodacom Foundation.Wanaoshuhudia kushoto ni Meneja wa Vodacom Foundation Bi.Grace Lyon na Mwenyekiti wa bodi wa Chuo hicho Askofu Dkt Gerald Mpango watatu toka kushoto.
Mkuu wa Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoa wa Kigoma Mwl.Joseph Mwangamila pamoja na Mwenyekiti wa bodi wa Chuo hicho Askofu Dkt Gerald Mpango wakiwa na nyuso za furaha wakiinua moja ya Kompyuta juu kati ya tano zenye thamani ya shilingi Milioni sita,walizopewa msaada na mshindi wa ”Vodacom Mahela”Bw.Valerian Kamugisha(kulia) ambae ni mwanafunzi wa chuo hicho kwa niaba ya Vodacom Foundation.anaeshuhudia kushoto ni Meneja wa Vodacom Foundation Bi.Grace Lyon.
Mkuu wa Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoa wa Kigoma Mwl.Joseph Mwangamila(kulia)akimkabidhi sehemu ya msaada wa Kompyuta Tano zenye thamani ya shilingi Milioni 6,Mwanafunzi wa chuo hicho,Rehema Romani,baada ya kukabidhiwa na mshindi wa”Vodacom Mahela”Bw.Valerian Kamugisha,wa pili toka kushoto,kwa niaba ya Vodacom Foundation.Anayeshuhudia kushoto ni Meneja wa Vodacom Foundation, Bi.Grace Lyon.
Picha ya pamoja.

WAZIRI MKUU PINDA AZINDUA TAMASHA LA BULABO 2013 KWA KUSIMIKWA KUWA MSHAURI WA WATEMI

0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akisimikwa kuwa Mshauri wa Watemi wa Kabila la wasukuma katika tamasha la Bulabo alilolizindua rasmi jana katika viwanja vya Kisesa wilaya ya Magu mkoani Mwanza likidhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti.


Mtemi Antonia akimkabidhi fimbo ya watemi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda ikiwa ni ishara ya kuwa Mtemi
Mheshimiwa waziri mkuu akiwa sambamba na Mhasham Baba Askofu wa Jimbo la Mwanza Yuda Thadei Ruwaichi wakipiga ngoma kuashiria uzinduzi rasmi wa Bulabo 2013, huku wakishuhudiwa na mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo pamoja na Naibu wa Nishati na Madini Mh. Stephen Masele (aliyesimama nyuma ya waziri mkuu).


“Tutaendelea kutambua juhudi za Kanisa na Kituo cha bujora katika kudumisha mila na serikali itahakikisha inashirikiana na kituo hiki kuhakikisha tamaduni ,sana na mila zinadumishwa kwa ukanda wa ziwa Victoria “alisema Pinda.



'Ngoma imenoga lazima nijumuike'


Naibu waziri wa wizara ya Nishati na madini ambaye vilevile ni mbunge wa Shinyanga mjini Mh. Stephen Masele akisalimia wananchi waliofurika kwenye tamasha la Bulabo 2013.


Wake kwa waume na watoto wao wote wamekuja hapa.


Usikivu kusanyikoni..


Kundi la Makhilikhili toka mkoani Shinyanga likionyesha kazi.


Safu ya watemi na viongozi.


Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula (kulia) akiwa na mwenyekiti wa zamani wa CCM mkoa wa Mwanza ambaye ni diwani wa Kisesa Mabina (katikati).


Waziri mkuu alisema kwamba Duniani kote urithi wa utamaduni umekuwa ukiathiriwa  na mabadiliko ya Kijamii, Uchumi na Siasa ambayo ukosefu wa nia au kutaka uelewa na kuthamini mila na desturi za Jamii nyingine.



Wananchi waliofurika hapa uwanjani.

Ndungulile mgeni rasmi Redd's Miss Kigamboni Ijumaa

0
0

MBUNGE wa Jimbo la Kigamboni, Faustine Ndungulile, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika onyesho la kumsaka malkia wa kitongoji cha  Kigamboni mwaka huu "Redd's Miss Kigamboni 2013" katika shindano litakalofanyika Ijumaa Juni 7 kwenye ukumbi wa Navy Beach kuanzia saa 2:00 usiku hapa jijini Dar es Salaam.



Akizungumza na gazeti hili jana, Mratibu wa shindano hilo, Somoe Ng'itu, alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yamekamilika na mbunge huyo amekubali kuja kubariki shindano hilo. Mratibu huyo alisema kwamba Kamati ya Miss Kigamboni imejiandaa kufanya onyesho lililo na kiwango cha juu na wadau wa sanaa hiyo watarajie kuona mshindi anapatikana na kwenda kutetea taji la Redd's Miss Temeke na baadaye kushinda taji la taifa.

Alisema kuwa bendi ya FM Academia maarufu Wazee wa Ngwasuma itatumbuiza shindano hilo ambalo kiingilio cha viti maalum ni Sh. 10,000 na viti vya kawaida ni Sh. 5,000. Aliongeza kuwa mpaka sasa jumla ya warembo 12 wanaendelea na mazoezi hapa jijini chini ya Blessing Ngowi.

"Shindano la Redd's Miss Kigamboni mwaka huu litakuwa bomba na wadau wasisite kujitokeza safari ya Miss Tanzania inaanzia katika kitongoji hichi Ijumaa hii," Somoe aliongeza. Aliwataja washiriki watakaopanda jukwaani kuwania taji hilo ni pamoja na Rogathe Michael, Irene Rajab, Magdalena Olotu, Latifa Mohammed, Axsaritha Vedastus, Angella Lutataza, Sara Makembo, Amina Mussa,  Ellen Sulle na Zuhura Masoud.

Warembo watano watakaoshika nafasi za juu kwenye shindano hilo watapata nafasi ya kushiriki kinyang'anyiro cha Redd's Miss Temeke baadaye mwaka huu. 
Wadhamini ambao wamethibitisha kusaidia shindano hilo ni pamoja na kampuni ya bia Tanzania kupitia kinywaji cha Redd's Premium Original, Montage Limited, Clouds Media Group, Papa Z , Silver Boutique, Jambo Leo, Machapta Production na Logikit.

Mdau dada domina anatafuta mchumba.

0
0
Habari yako ndugu mwenyekiti (Michuzi Junior). Mimi ni mwanamke, naandika kwenye blog yako natafuta mchumba, kijana ambaye yupo makini na anayetaka kuanzisha familia hivi karibuni. Awe na umri kuanzia miaka 35 mpaka 39. Naomba sana ambao hawako makini kwenye hili swala wasiniandikie.

Rafiki ninayemtafuta awe hajawahi kuoa, awe hana watoto, awe na elimu kuanzia chuo, awe tayari kupima ukimwi, awe mtu wa kumcha mungu (mkristo), mpole, anayejali na mwenye mapenzi ya dhati.
Napatikana kwenye email address:

Sekondari za Kata Mzigo Mpya kwa Wakuu wa Shule

0
0
Victus Kiwango, Mkuu wa Sekondari ya Tanya. 

  Na Thehabari, Rombo .

KUANZISHWA kwa Sekondari za Kata maeneo mbalimbali nchini kulikuwa na matumaini makubwa kwa wananchi. Maeneo mengi uitikio wa wananchi umekuwa mkubwa na shule hizo kujengwa kwa wingi hali ambayo imegeuka kuwa mzigo tena kwa Serikali kutokana na kuelemewa katika kuzihudumia baadhi ya shule hizi kwa baadhi ya maeneo. Baadhi ya shule hizi zimekuwa zikikubwa na changamoto kadha wa kadha hivyo kuwa kikwazo kikubwa katika kufanya vizuri kitaaluma. Uchache wa vifaa vya muhimu vya kujifunzia na kufundishia, walimu stahili hasa wa sayansi na uduni wa miundombinu ya kutosha ya shule imebaki kuwa changamoto zaidi.

Kimsingi kwa tafsiri rahisi inaonekana wazi wazi kuwa Serikali imeelemewa na mzigo wa kuziendesha kihuduma shule hizi. Na sasa mzigo huo umeangukia kwa walimu wakuu wanaoziongoza shule hizo. Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro ni miongoni mwa maeneo yaliokuwa na muitikio mkubwa wa ujenzi wa shule hizi. Wilaya hii kwa sasa imefikisha jumla ya Shule za Sekondari 41 za Serikali, idadi ambayo ni kubwa ukilinganisha na hapo nyuma kabla ya zoezi la uhamasishaji wa ujenzi wa shule hizo. Mwandishi wa makala haya amezungukia baadhi ya shule hizi na kufanya mahojiano na walimu, wanafunzi, wazazi/walezi, wadau wa elimu pamoja na viongozi wa maeneo hayo kuangalia changamoto anuai zinazo zikabili shule hizi. [caption id="attachment_33486" align="aligncenter" width="640"] Baadhi ya wanafunzi wa moja ya Sekondari za kata, Rombo wakiwa darasani[/caption] Urauri Sekondari ni miongoni mwa shule za Kata zilizoanzishwa Tarafa ya Tarakea wilayani Rombo ikiwa ni mpango wa Serikali kuendelea kusogeza elimu ya sekondari kwa wananchi wake. Shule hii licha ya kukabiliwa na changamoto nyingine kadhaa, hadi sasa haina walimu wa masomo ya sayansi kama Baiolojia, Hisabati, Kemia pamoja na Fizikia. Sim Silayo ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Urauri, anakiri kuwa kukosekana kwa walimu wa sayansi kuwafundisha wanafunzi muda wote kiutaratibu ni miongoni mwa vikwazo vya kufanya vizuri kitaaluma kwa shule yake. Hata hivyo anasema hali hiyo haimkatishi tamaa ya wanafunzi wake kufundishwa masomo ya sayansi shuleni hapo.

Anasema ili kuziba pengo la walimu wa sayansi shuleni hapo ametafuta walimu wa muda ambao ni vijana waliomaliza kidato cha sita na wanaendelea kumsaidia kufundisha masomo ya Fizikia, Baiolojia, Kemia pamoja na Hisabati. Anasema vijana hao wanalipwa ujira wao na shule kwa kutumia michango inayopatikana shuleni. Anasema mwitikio wa ulipaji ada wa wazazi ni mdogo na fedha zinazotolewa na Serikali hazitoshi kuendesha shule, hivyo hulazimika kutumia mbinu kadhaa kuchangishana na wazazi kuhakikisha wanapata chochote kusaidia baadhi ya gharama za shule.



 "Shule hii ni mchapuo wa kilimo lakini watoto walikuwa hawasomi somo hilo kutokana na kutokuwa na mwalimu husika wa somo...juzi nimejitahidi kwa kushirikiana na wazazi tumechanga na kumpata mwalimu wa kilimo wa muda...hapa michango ya wazazi pamoja na fungu la taaluma limetuokoa," anasema Silayo. Kama hiyo haitoshi mwalimu Silayo anasema shule yake haina vitabu vya kutosha, maktaba, maabara na changamoto ya mazingira ya kuvutia kimiundombinu kwa wanafunzi kusoma" width="535"] Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rombo, Judethadeus Mboy.

Hata hivyo kilio kama hicho cha ukosefu wa walimu wa sayansi kimeangukia tena katika Sekondari ya Holili, Wilayani Rombo. Benson Samizi ni Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule hiyo, anasema shule hiyo haina kabisa walimu wa masomo ya sayansi na badala yake hutumia wanafunzi wa kidato cha sita kufundisha kwa muda na uongozi wa shule kuwalipa ujira wao. "Shule yetu imebahatika kuwa na vitabu vya sayansi vya kutosha, lakini hatuna kabisa mwalimu wa masomo ya Fizikia na Hisabati...pamoja na hali hiyo ili mambo yasiwe mabaya zaidi tunakodi vijana ambao hutusaidia masomo haya kwa muda kuwafundisha wanafunzi wetu na kulipwa na shule chochote kinachopatikana," anasema mwalimu huyo.

 Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya ya Rombo, Erasmo Mwingira anasema shule nyingi za kata zina walimu wa masomo ya sanaa zaidi na hazina walimu wa Sayansi wa kutosha. Anaongeza kuwa licha ya Serikali kujua tatizo hilo bado imeendelea kuwapa mitihani ya masomo ya sayansi wanafunzi bila kujali kama wanafunzi hao wamefundishwa masomo hayo. "...Katika Shule nyingi zina walimu wa sanaa, walimu wengi katika shule hizi ni wa sanaa lakini wanapokuja kumpima mtoto (mwanafunzi) anapimwa kwa masomo ya sanaa na sayansi bila kujali kama amefundishwa kwa njia gani masomo hayo Mwingira anabainisha kuwa fedha zinazotolewa kuziendesha shule hizo 'capitation' hazitoshi na mara nyingine huwa hazifiki kwa kwa wakati shuleni hali ambayo huwalamimu walimu wakuu kubuni mbinu mbalimbali za uendeshaji wa shule zao, ikiwemo kuweka utitiri wa michango kwa wazazi ili kuhakikisha mambo yanaendelea. "Sasa hivi shule hizi zinaendeshwa na mifuko ya walimu wakuu...'capitation' haifiki kabisa shuleni, fedha inayowafikia ni kidogo sana na haiwezi kuendesha zile shule, walimu wanatumia mbinu zao kuziendesha shule ndio maana unaona michango inakuwa mingi shuleni," anaeleza Mwingira akizungumza na mwandishi wa makala haya. Anaongeza kuwa licha ya serikali kusisitiza kwamba ada ya sekondari ni shilingi 20,000 kwa sasa michango katika shule hizo ni mingi kiasi cha kufikia 120,000 jambo ambalo limewafanya baadhi ya wazazi kuzidiwa na mzigo wa michango na wengine kushindwa kabisa kuimudu. Mdau huyu wa elimu anasema vijana wa kidato cha sita ambao hutumiwa na shule nyingi kuokoa jahazi ya masomo ya sayansi wamekuwa wakiwakaririsha wanafunzi kujibu mitihani na sio kuwafundisha jambo ambalo ni hatari kwa elimu ya Tanzania hapo mbeleni. "Kujua kusoma na kuandika si kigezo cha kumfundisha mtu...vijana hawa wa kidato cha sita hawana mbinu za ufundishaji wanachokifanya ni kuwakaririsha wanafunzi. Pamoja na hayo anaishauri serikali kutojitoa katika jukumu la kuziendesha shule za kata na kuwaachia wazazi kwani shule hizo ziko katika hali mbaya na zinahitaji kuongezewa fedha za uendeshaji. Victus Kiwango ni Mkuu wa Sekondari ya Tanya, anaishauri Serikali kuongeza fungu la uendeshaji wa fedha shuleni kwani fedha za michango zinazotolewa na wazazi hazitoshi kuendesha shule. Anasema shule huwa zinakodi wanafunzi waliomaliza kidato cha sita na kuwasaidia wanafunzi kwa muda masomo ya sayansi hivyo shule kuwa na gharama kubwa za uendeshaji. "Sisi tumelazimika kuajiri kwa muda wanafunzi sita waliomaliza kidato cha sita kufundisha masomo ya sayansi kwa fedha za shule...tunajibanabana kwa michango pamoja na wazazi na kuhakikisha tunapata chochote kuwalipa walimu hawa wa muda bila hivyo mambo hayaendi," alisema Mkuu Msaidizi wa Sekondari ya Nduweni, Venance Mramba akizungumza na mwandishi wa habari hizi. Pamoja na hali hiyo uchunguzi wa kina uliofanywa katika shule za Sekondari za Tanya, Nduweni, Urauri, Holili na Ngaleku na nyinginezo za wilayani Rombo, umebaini uwepo wa ongezeko la michango shuleni hali ambayo imelalamikiwa na baadhi ya wazazi na wadau wa elimu wilayani waliozungumza. Uchapaini shule ya Sekondari Tanya imefikisha jumla ya michango sh. 115,000; mgawanyiko wake ukiwa kama ifuatavyo; Ada sh 20,000, Madawati sh 15,000, Chakula sh 60,000, Tahadhari sh 5,000, Ulinzi 5,000, Taaluma sh 5,000 na Kitambulisho sh 5,000. Aidha uchunguzi zaidi umebaini shule nyingi za sekondari za kata hazina walimu wa masomo ya sayansi jambo ambalo huwalazimisha walimu wakuu kutafuta walimu wa kukodi hasa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita kuja kuwafundisha wanafunzi masomo ya sanyansi kama Hisabati, Fizikia, Kemia, Baiolojia na mengineyo huku wakitumia mbinu anuai kukusanya michango kuwalipa walimu hao wa kukodi. Judethadeus Mboya ni Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rombo, katika mazungumzo na makala haya anakiri kuwepo na tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi katika shule nyingi za wilaya yake, hivyo walimu kulazimika kuajiri kwa muda vijana wa kidato cha sita kusaidia wanafunzi huku jitihada zikiendelea kufanya kukabiliana na tatizo hilo. "Walimu wa sayansi ni tatizo Rombo hawatoshi...mwaka huu tumejitahidi na kuajiri takribani walimu 134 wakiwemo wachache wa masomo ya sayansi lakini tatizo bado lipo," alisema Mboya kikilitolea ufafanuzi suala hilo ofisini kwake wilayani Rombo hivi karibuni. Hata hivyo kiongozi huyu mtendaji wa wilaya anasema licha ya changamoto zilizopo katika shule hizo bado zinanafasi ya kufanya vizuri kitaaluma endapo walimu wa kuu watajitoa kikamilifu katika kusimamia utendaji wa shughuli shuleni hapo. "...Walimu wakuu ndio msingi wa kufanya vibaya kitaaluma katika shule, endapo mwalimu mkuu atatumia uwezo na ukakamavu katika kuongoza shule yake itafanikiwa...mwalimu huyu akitumia uwezo wake kuwaongoza vizuri walimu wengine lazima atafanikiwa na shule itafanya vizuri kitaaluma," anasema Mboya. Imeandaliwa na www.thehabari.com

NAPE AFUNGUA KAMPENI ZA UDIWANI SENGEREMA

0
0

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa, Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya Nyampulukano, Sengerema wakati wa ufunguzi wa kampeni za udiwani. Juni, 3, 2013.
Mgombea kiti cha udiwani kata ya Nyampulukano  kupitia CCM,Ndugu Charles Gabriel Rugabandana akisalimia wananchi mara tu baada ya kutambulishwa rasmi.Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika tarehe 16,Juni,2013.

 Mbunge wa Sengerema ,William Ngeleja akihutubia wakazi wa kata yaNyampulukano na kuelezea jinsi ilani ya uchaguzi ilivyotekelezwa pamoja na ufafanuzi juu ya mradi mkubwa wa maji kwa wakazi wa Sengerema.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Ndugu Joseph  Kasheku  'Musukuma' akihutubia wakazi wa Sengerema wakati wa ufunguzi wa kampeni za udiwani kata Nyampulukano,Sengerema, Mwanza.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishuka kutoka kwenye kivuko cha MV Sengerema tayari kufungua kampeni za udiwani kata ya Nyampulukano.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akisalimia na wakazi wa Sengerema waliokuja kumpokea Busisi leo.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akisalimiana na Hashimu Lundenga,mara baada ya kuwasili Busisi ,Sengerema leo.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisalimiana na wakazi wa Sengerema katika viwanja vya shule ya Msingi Sengerema.
 Mzee  Bukilo akiongoza kundi lake wakati wa mkutano wa hadhara wa ufunguzi wa kampeni kata ya Nyampulukano, wilaya ya Sengerema ,Mwanza. Picha na Adam H. Mzee

JWTZ yakanusha vikali ujumbe wa tetesi za kurushwa mabomu kutoka Malawi

0
0
Picture
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA


Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limepata ujumbe  kupitia simu za mkononi ambao umesambazwa kwa wananchi mbalimbali ukisadikishwa kuwa unatolewa na JWTZ.

Ujumbe huo wa simu ya mkononi unasema ‘Habari zilizotufikia hivi punde. Mtanzania yeyote, kaa makini usiokote kitu chochote ambacho una shaka nacho, kuna bomu zimerushwa toka nchi jirani Malawi zaidi ya 30 zenye uzito usiopungua tani 100. Hivyo basi uonapo kitu kipo kama chupa la chai chenye rangi ya fedha. Usiguse’

 Piga namba 0756 000042. SMS hii tuma kwa watu uwezavyo. Imetolewa na JWTZ’.


JWTZ linapenda kuwaondoa wananchi hofu kutokana na taarifa hiyo. Kwanza, Ujumbe huo haujatolewa na  JWTZ. JWTZ  haliwezi likatumia mfumo huo wa SMS kuwapa wananchi wake taarifa za hatari kama hizo. Aidha, JWTZ hutangaza kupitia vyombo rasmi kama vile Magazeti, Radio na Television.


Pili, bomu la tani 100 ni zito mno,  halijawahi kutengenezwa duniani. Na kama lipo, haifahamiki bomu hilo litarushwa vipi , kwa kutumia ndege au Mzinga?.  Lakini pia, mzinga wa aina hiyo haupo duniani kote na wala hakuna ndege yenye uwezo huo, hasa kwa bomu lenye umbile dogo kama hilo(Chupa ya Chai).

Tatu, habari hizi hazina ukweli kisayansi wala kiuhalisia au fikra za kawaida. Tunawaomba wananchi wazipuuzie taarifa hizi kwani sio za kweli ni uongo mtupu. JWTZ lipo kwa ajili ya Wanachi hivyo, kwa taarifa hizi za hatari,lazima lingewajulisha wananchi kwa njia zilizoelezwa hapo juu na si kwa simu za mkononi.

Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP 9203, Simu: 0764-742161
Email:ulinzimagazine@yahoo.co.uk

UPDATES:MWILI WA ALBERT MANGWEHA WAAGWA NCHINI SOUTH AFRICA,KUWASILI LEO MCHANA

0
0
Muda huu wa saa kumi na Mbili kwa saa za Afrika mashariki kwa saa za South Africa ni saa kumi na Moja jioni.....tukiwa bado tupo kwenye majonzi  makubwa yakupotelewa na ndugu yetu Albert Mangweha.....Baada ya ratiba kupangika watanzania waishio nchini South Africa wamepata nafasi ya kuaga mwili wa Albert Mangweha kuelekea katika safari ya  mwisho...wakiongozwa na Msanii Bushoke na Mtoto wa Mhe. Kingunge Ngombale mwiru, Kinjeketile wanaosimamia mipango ya kuaga mwili nchini South Africa.Picha kwa hisani ya Clouds FM.

MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEHA UTAWASILI LEO MCHANA UWANJA WA KIMATAIFA WA JK NYERERE  KUPITIA SHIRIKA LA NDEGE LA SOUTH AFRICA AIRWAYS.

MKUTANO MKUU WA 12 WA MWAKA WA VITUO VYA ELIMU KWA NJIA YA MTANDAO KUTOKA NCHI 15 ZA AFRIKA(AADLC) WAFANYIKA DAR ES SALAAM TANZANIA

0
0

 Katibu Mkuu ofisi ya Raisi na utumishi wa umma Bw Georg Yambesi c akijadiliana jambo na Rais wa (AADCL) na Mkurugenzi (DLC) kutoka  Senegal Bwana Mor Seck kushoto kwa Yambesi ni Mkurugenzi mtedaji wa (TAGLA) Charles Senkoro.
Katibu mkuu wa ofisi ya rais menejimenti ya utumishi wa umma GEORGE YAMBESI amewataka wajumbe wa umoja wa vituo vya elimu kwa njia ya mtandao barani AFRIKA washirikiane na makampuni ya TEHAMA na simu za mikononi kuwafikishia elimu wananchi walio maeneo ya Vijijini.Bwana Yambesi ndiye aliyeufungua mkutano huo leo picha na Chris Mfinanga

Wizara yaadhimisha wiki ya Mazingira kwakufanya usafi wa katika stesheni ya Buguruni Bahresa

0
0
 Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira na Usalama, Bi. Tumpe Mwaijande akiongea na wafanyakazi wa Wizara na taasisi zilizo chini ya Wizara (hawapo pichani) hiyo baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Buguruni Bahresa leo asubuhi. Pamoja na zoezi la Usafi Wizara ya Uchukuzi ilikabidhi Majembe, mafyekeo na reki kwa Shule ya Msingi Hekima na Zahanati ya Buguruni.

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi akifagia katika Stehseni ya Buguruni Bahresa, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Mazingira, leo asubuhi. Kilele cha wiki hiyo kitakuwa tarehe 5 Mwezi huu.

 Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira na Usalama wa Usafiri Majini, Bi. Tumpe Mwaijande (aliyeshika mfuko) akifanya usafi katika eneo la Buguruni Bahresa kama ishara ya kuadhimisha Wiki ya Mazingira Duniani. Wafanyakazi wa wizara ya Uchukuzi pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo walifanya usafi katika eneo hilo kama ishara ya kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani ambapo Kauli mbiu ya Wizara hiyo ikiwa ni "Hifadhi Maazingira kwa Uchukuzi Endelevu".

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Mhandisi Aman Kisamfu (wa pili kutoka kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dkt. Agnes Kijazi (wa tano kutoka kushoto) wakisubiria kuanza kazi ya Usafi katika eneo la Stehseni ya Buguruni Bahresa. Wizara ya Uchukuzi na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo wamefanya usafi kwenye eneo hilo leo asubuhi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani mbayo kitaifa inaadhimishwa Mkoani Rukwa.

 Wafanyakazi wa Wizara ya Uchukuzi na taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo wakifanya usafi katika Stesheni ya Buguruni Bahresa kama ishara ya kuadhimisha wiki ya Mazingira Duniani, Zoezi hilo la kufanya usafi limebeba kauli mbiu inayosema "Hifadhi Maazingira kwa Uchukuzi Endelevu".

Wafanyakazi wa Wizara ya Uchukuzi na Taasisi zilizo chini ya Wizara wakiwa ndani ya Treni kuelekea katika kituo cha Buguruni Bahresa, ambapo waliadhimisha Wiki ya Mazingira Duniani kwa kufanya usafi katika eneo hilo leo asubuhi. Kauli Mbiu ya Wizara katika siku hii ni "Hifadhi maazingira kwa Uchukuzi Endelevu". Aidha Kauli mbiu ya Kitaifa ni 'Fikiri, kula; hifadhi Mazingira".

(Picha na  Kitengo cha Mawasiliano-Uchukuzi).
 
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images