Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

Ilala Boys mabingwa Airtel Rising Stars Ilala

$
0
0





Timu ya Simba Queen wakishangilia baada ya kushinda mechi ya fainali ya wasichana katika Wilaya ya Ilala juzi katika michuano ya U-17 Airtel Rising Stars iliyokuwa ikichezwa katika uwanja wa Karume.
Mshambulaiji wa Timu ya Bombom SC, Jamal Abdul (Katikati) akipambana na mabeki wa Timu ya Ilala Boys wakati wa mechi ya Fainali ya U-17 ARS kwa wavulana katika uwanja wa Karume juzi. Timu ya IlalaBoys ilishinda 3-0


Mbunge wa Ilala (CCM) Mussa Zungu akimkabidhi kombe Nahoza wa Timu ya Ilala Boys, Rajabu Ally baada ya kushinda mechi ya fainali kwa wavulana Wilaya ya Ilala juzi katika michuano ya U-17 Airtel Rising Stars iliyokuwa ikichezwa katika uwanja wa Karume.Ilala Boys ilishinda 3-0 dhidi ya Bombom.


Mbunge wa Ilala (CCM) Mussa Zungu akimkabidhi kombe Nahoza wa Timu ya Simba Queen, Hadija Ally baada ya kushinda mechi ya fainali ya wasichana Wilaya ya Ilala juzi katika michuano ya U-17 Airtel Rising Stars iliyokuwa ikichezwa katika uwanja wa Karume.Simba Queen ilishinda 5-0 dhidi ya Ilala.
Timu ya wavulana ya soka Ilala Boys ya kimkoa wa Ilala jana imetwaa uchampioni wa michuano ya soka kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Aitel Rising Stars kwa kuwafunga Bom Bom FC 3-0 kwenye uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wa wasichana timu ya Simba Queens ndio iliyotawazwa mabingwa kwa kushinda timu ya Ilala Queens kwa magoli 5-0 katika mchezo mkali uliovuta hisia za watamazaji waliojitokeza kushuhuduia mtanange huo.

Katika mchezo wa wavulana, timu ya Ilala Boys walionyesha dalili za ushindi mapema baada ya kuanza mchezo kwa mashambulizi mfululizo na walichukua dakika sita kuandika bao ya kwanza likifungwa na Rajabu Ally baada ya kungona vyema na mshambuliaji mwenzake Issa Abushiri.

Dakika ya saba ya mchezo Ilala Boys waliandika bao la pili baada kupingwa mpira wa kona na mabeki wa Bom Bom FC kushindwa kuokoa. Bao la tatu lilipatikana dakika ya 42 ya kipindi cha pili baada ya kupingwa mpira mrefu huku mabeki wa Bom Boma wakisimama wakifikiri mfungaji, Issa Abushiri ameotea.

Akikabidhi vikombe kwa washindi, Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu amewataka wachezaji waliochaguliwa kuiwakilisha Mkoa wa Ilala vyema kwenye fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zinatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba mwaka huu. ‘Mkoa wa Ilala ulikuwa kila mwaka ukifanya vizuri kwenye mashindano, nina imani nanyi mtaendelea kulinda heshima ya mkoa wetu, alisema Zungu. Zungu pia alitoa pongezi kwa Kampuni ya Airtel kwa kutoa fursa kwa vijana kuonyesha vipaji vyao vya kandanda.

Naye Meneja Huduma za jamii wa Airtel Tanzania Hawa Bayumi alizipongeza timu zote kwa kushiriki na kuwaasa wachezaji kulinda na kuviendeleza vipaji vyao ambavyo ni hazina kwa taifa. Aliseema lengo lilikuwa ni kuibua vipaji na kuwaasa vijana ambao hawakuchaguliwa kutokata tama na badala yake wajinge kufanya vizuri mwakani.

Kukamilika kwa michuano hiyo mkoa wa Ilala ndio kunafunga pazia la Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa huo iliyoanza kutimua vumbi mwezi uliopita.

Mashindano ya Airtel Rising Stars ambayo mwaka huu yanashirikisha mikoa ya Ilala, Kinondoni, Temeke, Morogoro, Mbeya, Mwanza, Zanzibar, Lindi na Arusha na zinatarajiwa kuingia kwenye hatua nyeti ya fainali za Taifa iliyopangwa kufanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, kuanzia Septamba 6 hadi 11 nmwaka huu.

MCHENGERWA:WILAYA YA RUFUJI INA UMASIKINI MKUBWA ,AIOMBA SERIKALI KUIANGALIA KWA JICHO LA KIPEKEE

$
0
0
MBUNGE wa Rufiji Mohamed Mchengerwa ameiomba serikali kuiangalia kwa jicho la pekee wilaya ya Rufiji kwani katika mkoa wa Pwani ndiyo ambayo haina kiwanda chochote hivyo kuna umasikini mkubwa.

 Pia ameiomba kufufua kiwanda cha pamba na kusukuma Wakala wa Bonde la Mto Rufuji (Rubada) kutekeleza majukumu yake ili kuondokana na umaskini uliopo kwenye wilaya hiyo. Alisema ni zaidi ya miaka 41 sasa Rubada imekuwa haifanyi kazi yake ipasavyo na kwamba wakati wakala huo unaanzishwa kulikuwa na kiwanda cha pamba ambacho sasa kimekufa.

Kauli hiyo aliitoa  jana katika kijiji cha mkongo wakati wa uzinduzi wa Programu ya mafunzo ya kilimo na ujasiriamali kwa vijana ambayo yamefadhiliwa na Shirika la Chakula duniani(FAO) na kufunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo.

 "Wilaya hii ina umasikini mkubwa tunaomba serikali ituangalie jitihada hizi za rubada leo ndizo zilitakiwa kufanyika miaka 41 iliyopita,malalamiko mengi ya wananchi yalikuwa juu yarubada itusaidie kupima ardhi.

 Tupate viwanda wilaya zote za mkoa huu hatuna kiwanda hata kimoja lakini wakati wanapewa miaka ya 70 kulikuwa na kiwanda cha pamba ila kilikuwa kimekufa na hadi sasa hakuna kiwanda chochote hapa mkoani,"alisema Mchangelwa.

 Alisema kukosekana kwa rubada hiyo kumesababisha wananchi kukosa imani na serikali yao na kwamba hiyo inatokana na kuwa nyuma kimaendeleo hivyo inabidi suala hilo lifanyiwe kazi lengo likiwa ni kurudisha imani hiyo kwa serikali yao. Aidha, aliiomba serikali kuwapa vijana wa mkoa huo elimu ya ujasiriamali ili waweze kujiajiri wenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

 Akizindua mafunzo hayo,RC Ndikilo alisema uzinduzi wa mafunzo ya kilimo katika kambi ya mkongo ya namna ya kuongeza tija ya uzalishaji chakula na biashara ya awamu ya kwanza wataanza vijana 62 kutoka rufiji na nje ya mkoa wa pwani na badae watarudi katika mashamba yao kuelimisha wengine. Alisema vijana hao watapata mafunzo kwa kipindi maalum kwa hiyo na kwamba watayatumia katika maeneo mbalimbali nchini.

 "Vijana wasiendelee kuwa wahuni changamoto za ajira zinaanza kutaftiwa ufumbuzi,wasikae tu,nimefarijika kuona changamoto zinatatuliwa,vijana wapatiwe mbegu bora baada ya mafunzo na kutafutiwa masoko,"alisema.

 Alitoa Rai kwa wakuu wote wa mikoa hiyo kuunda vikundi vya vijana na kuendelezwa katika shughuli mbalimbali na kwamba Kambi hiyo iwe endelevu kwani rais mstaafu aliweka jiwe na msingi lakini hakuna kilichoendelea.

 "Tunaomba mambo haya yawe endelevu,kambi iwe mfano wa kuigwa katika mkoa wa pwani kuna zaidi ya ekari 200 ziko hapa kwa hiyo ardhi si tatizo hivyo tukiwatoa vijana vijiweni na wakija hapa msiseme hakuna ardhi maana kambi hii ni yao hivyo iwe endelevu kwa kuwapa mafunzo vijana,"alisema.

HOJA YA HAJA: WAZIRI WA MAWASILIANO NA WAHUSIKA TAFADHALI ANGALIENI BEI ZA INTERNET KWA MAKAMPUNI YA SIMU NCHINI TANZANIA

$
0
0
Imekuwa ni kawaida kwa makampuni ya simu za Mikononi za Tanzania katika kufanya maamuzi binafsi katika kupanga bei za internet bila ya kumuangalia mtumiaji wa mwisho ambae ni Mtanzania Masikini.

Napata ugumu kuamini Tanzania inayotafuta maendeleo kwenye nyanja hii kwanini iweze kukubali na kuwaachia makampuni ya simu kufanya Price Fixing watakavyo huku wakishusha viwango vya internet (MB) na kuongeza thamani ya gharama kwa watumiaji wa Tanzania ambao ni masikini huku wizara husika ipo, Competition Commission, Competition And Consumer Protection Policies zipo na wahusika wapo wanafumbia macho tu.

Tukitaka Tanzania iendane na dunia inavyokwenda na kuongezeka kimaendeleo katika nyanja hii na tukitaka kwenda sambamba na Mtazamo madhubuti na ulio mzuri wa Mheshimiwa Rais wetu Magufuli wa kuiletea Tanzania maendeleo kwenye kila nyanja na kutaka kufanya Tanzania liwe Taifa lenye nguvu duniani na lenye watu walio elimika ni vyema wahusika wakahakikisha haya makampuni ya simu hayafanyi Price Fixing maana ukiangalia kwa undani viwango vyao vya kuuza internet vyote vimepangwa sawa sawa na vyote wamevishusha kwa wakati mmoja bila ya kutoa sababu ya msingi inayo wafanya kuongeza gharama na kushusha viwango vya internet wakati Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano umepita Tanzania.

Wahusika kama mkishindwa kuwatetea Watanzania walio wanyonge, Mheshimiwa Rais Magufuli hili ni jipu tunaomba uanze kutumbua kwenye sekta hii ya mawasiliano.

Ni matumaini yetu wahusika na wadau wote watakutana na kuweza kulitafutia mchakato madhubuti kwa kuwatetea watumiaji wa simu na internet nchini Tanzania na vile ili kuweza kuleta maendeleo nchi nzima na kuwawezesha ata Mtanzania aliyepo Chato au Sumbawanga aweze kupata fursa ya kuunganishwa na dunia kwa kupata viwango vya bei iliyo nzuri na viwango vikubwa vya internet. Vile vile kuanzia sasa haya makampuni ya simu kamwe yasifumbiwe macho kwa bei wanazozipanga kwenye huduma ya mawasiliano kwa maana yanawanyonya Watanzania ambao ni masikini kwa manufaa yao!

HAPA KAZI TU

MZEE AKILI MALI ASALIMU AMRI,AKUBALI YAISHE AOMBA RADHI WANACHAMA

$
0
0
Hatimaye mzee mkongwe katika baraza la wanayanga Yahya Akilimali amesimamishwa rasmi uanachama licha ya kujitetea na kujisafisha.Katika mkutano wa dharura uliofanyika Jangwani leo asubuhi mzee Akilimali alikiri kauli zake na kuwasilisha utetezi.

“Katika watu tunaompenda Manji, mimi namba moja lakini ikumbukwe Mwana umleavyo ndivyo akuavyo, Manji alikuwa anatuita akitaka kufanya jambo. Ila siku hizi hatuiti hatuambii lolote anafanya tu, nimemwambia Manji, mimi ndio nimempa ukuu wa Yanga. Sisi tunampenda kweli Yusuf na nimemtaka radhi jana”.

“Labda niseme hivi Kama kukurupuka ni Tusi kama nilivyomwambia Yusuf, basi naomba radhi kwake Manji na wanayanga wote”. Licha ya kuwasilisha utetezi huo kikao Cha viongozi wa Matawi ya klabu ya Yanga imemsimamisha Katibu wa baraza la Wazee, Yahya Akilimali kwa kile kinachoitwa kumkashifu Mwenyekiti wa klabu hiyo kongwe nchini Yusuph Mehboob Manji.Mzee Akilimali amesimamishwa kwa muda usiojulikana.

Kwa ufupi tuuu wanachama wa Yanga wameomba mzee Akilimali asimamishwe japo kuwa ameomba radhi.

MGOGORO KATI YA MWEKEZAJI NA WANANCHI WAMALIZIKA.

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mang’onyi wakati wa kutatua mgogoro kati ya wananchi na muwekezaji Shanta Gold Mine
Wanachi Kijijini Mang’onyi wakisikiliza kwa makini maelezo ya Mkuu wao wa Wilaya
Baadhi ya viongozi wakisikiliza maelezo ya awali katika ufunguzi wa mkutano huo uliodumukwa zaidi ya masaa matatu
Dc Mtaturu akikemea tabia ya wanasiasa kutoa matamko ya kisiasa kwa maslahi yao binafsi huku wakiwa mbali na eneo la wawakilishi wao.
Wananchi wakimlaki Mkuu wao wa Wilayaya Ikungi
Dc Mtaturu akikemea tabia ya wananchi kuwachagua viongozi ambao wakipewa ridhaa tu wanahamia Dar es salaam ilihali wananchi wao wanabaki kuteseka pasina kuona umuhimu wa viongozi wao
Dc Mtaturu akitoa agizo kwa muwekezaji Shanta Gold Mine kuwalipa fidia haraka wananchi ili mradi huo uanze haraka iwezekanavyo
Nyumbani ni salamu na unyumbani ni kuongea Kinyumbani, moja ya tabasamu kati ya mwananchi na Dc wake wakizungumza kwa lugha moja baada ya mkutano
Wananchi wakielemishwa na Mkuu wa wilaya juu ya siasa zinazokwamisha maendeleo yao huku wanasiasa wenyewe wakishindwa kufanya uwakilishi katika maeneo yao badala yake wamekuwa wawakilishi wa kitaifa
Msingi wa kikao ni kusikilizana Mkuu wa Wilaya ya ikungi Miraji jumanne Mtaturu, Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya, Uongozi wa Shanta Gold Mine na wananchi Kijijini Mang’onyi wakiwa kwenye mkutano wa kutatua mgogoro wao

Na Mathias Canal, Singida

Mgogoro uliodumu katika kipindi cha zaidi ya miaka kumi kati ya wananchi wa Kijiji cha Mang'oni na Muwekezaji Shanta Gold Mine umechukua sura mpya ya maelewano baada ya wananchi kupatiwa elimu kuhusu umuhimu wa uwekezekezaji na fursa watakazozipata ikiwa ni pamoja na ajira kwa wananchi wenyewe na maendeleo ya Vijiji, Kata, Tarafa, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Akiwa katika kijiji cha Mang'onyi, Kata ya Mang'onyi Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amezungumza na wananchi hao kujua kadhia iliyopelekea kutoelewana kwa kipindi chote hicho jambo ambalo limerudisha nyuma maendeleo tarajiwa kwa pande zote mbili.

Mgogoro huo umemalizika kwa Mkuu huyo kuamua kuwa wananchi walipwe fidia haraka iwezekenavyo ili kupisha uanzishwaji wa Mgodi huo ambapo tayari takribani wananchi 67 watalipwa katika awamu ya kwanza huku wengi zaidi 130 kulipwa katika awamu ya pili.

Dc Mtaturu amefanya mkutano wake wa hadhara wa mwanzo tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi ambapo amewaagiza wawekezaji hao kukutana na kuwa na kikao cha pamoja kati yao na wananchi waliofanyiwa tathmini kwa ajili ya makubaliano ya namna bora ya malipo yao ikiwa ni pamoja na kuwashauri kila mmoja kufungua Account Bank ili iwe rahisi na salama katika uhifadhi wa fedha zao.

Baadhi ya Wananchi katika kijiji hicho cha Mang'oni hivi karibuni walizuia njia kwa kuweka magogo na mawe barabarani kama ishara ya kuwazuia wawekezaji hao kupita katika eneo lao kwa madai ya kutolipwa fidia kwa wakati na mwekezaji kuweka alama za mipaka ya eneo lake pasina wananchi kushirikishwa.

Hata hivyo Dc Mtaturu alisema kuwa huenda wananchi walikuwa na hoja ya msingi lakini kutolipwa fidia hakumfanyi mtu kupata uhalali wa kuharibu mali za muwekezaji kwani kufanya hivyo ni sehemu mojawapo inayochelewesha ulipaji wa fidia.

Mtaturu ameonyesha kukerwa na viongozi wanaowapotosha wananchi hao ilihali wakiwa wamejificha ama wanaishi mbali na kijijini hapo na kusema kuwa hiyo ni nidhamu ya woga kwani muwakilishi mzuri wa wananchi ni yule anayetanguliza maslahi ya wananchi mbele kuliko masalahi ya kisiasa, Chama ama maslahi yake binafsi.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa kiongozi mzuri daima ni yule anayetatua changamoto za wananchi sio kuzipinga kwani siasa safi na nzuri ni ile inayoleta maendeleo sio kupinga maendeleo.
Amewataka wawekezaji hao kuwa na mahusiano mazuri na wananchi kwani unapokuwa na mradi wako katika Kijiji chochote nchini usipokuwa na mawasiliano mema na wananchi wa eneo husika ni dhahiri kuwa mradi wako utakuwa hauna tofauti na mradi mfu.



Hata hivyo pamoja na faida kwa wananchi kulipwa fidia na serikali kupata pato lake lakini wananchi 60 kutoka Kijijini hapo wataajiriwa katika Mradi huo kati ya ajira 120 zilizopo ambapo wengine 60 watatoka nje ya eneo hilo ili kutoa fursa kwa watanzania wote kujipatia ajira.

BENKI YA ACB NA BLACK WOOD WAZINDUA HUDUMA YA MIKOPO YA KUBORESHA MAKAZI JIJINI DAR LEO.

$
0
0

 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabulla, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya ACB, Israel Chasosa na Mkurugenzi wa Mipango kampuni ya Black Wood, Zouhra wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya ACB na wafanyakazi wa kampuni ya Black Wood jijini Dar es Salaam mara baada ya uzinduzi wa huduma ya mikopo ya kuboresha Makazi.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabulla akizungumza na wadau wa benki ya ACB jijini Dar es Salaam leo katika uzinduzi wa  huduma ya mikopo na kuboresha makazi kati ya Black wood na Benki ya ACB.
Mkurugenzi wa Mipango kampuni ya Black Wood, Zouhra akizungumza na wa wadau wa benki ya ACB na kampuni ya Black Wood jijini Dar es Salaam leo. amesema kuwa kampuni ya Black Wood inakukopesha Viwanja vilivyopimwa na vya bei nafuu kwa watu wote wenye kipato cha chini anaweza kupata kiwanja kilichopimwa na chenye miundombinu yote.
 Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya ACB, Israel Chasosa akizungumza katika uzinduzi wa huduma ya mikopo jijini Dar es Salaam leo kati ya Benki ya ACB na Kampuni ya Black wood katika kununua viwanja vya kuanzia shilingi milioni tatu tu.

Rais Magufuli awatembelea na kuwajulia hali Mzee Malecela na Mhe. Ndugai.

$
0
0


 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 16 Agosti, 2016 amewatembelea na kuwajulia hali Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. John Samuel Malecela Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na kuwajulia hali, Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewaombea kwa Mwenyezi Mungu wapone na kupata nguvu haraka ili waweze kuendelea na majukumu yao ya kawaida katika ujenzi wa Taifa.Akizungumza na Rais Magufuli nyumbani kwake Salasala Jijini Dar es Salaam spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amemshukuru Rais Magufuli kwa kumtembelea, kumjulia hali na kufuatilia kwa ukaribu wakati wote alipokuwa akipata matibabu nchini India hadi aliporejea hapa nchini.

"Kwa kweli nimefarijika sana, kwanza naomba nimshukuru sana Mhe. Rais kwa sababu nilipopata matatizo haya ya maradhi alikuwa karibu sana na mimi nikiwa hapa nchini na hata nilipopelekwa nchini India alinipigia simu mara kwa mara na kunifariji sana, na hapa amekuja kuniona kwa niaba ya watanzania kwa kweli namshukuru sana na namuombea kwa Mwenyezi Mungu aendelee kumpa moyo huu wa kuwajulia hali wale wenye matatizo mbalimbali"
Lakini niwahakikishie Watanzania, kwamba kwa sasa nina nafuu kubwa sana, naweza kufanya kufanya kazi nyingi tu sasa lakini tuendelee kuombeana"Ameeleza Mhe. Ndugai alipokuwa akizungumzia hali yake kwa sasa.

Kwa upande wake Makamu wa Rais Mstaafu na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. John Samuel Malecela pamoja na kumshukuru Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli kwa kumtembelea amesema afya yake inazidi kuimarika na pia amewashukuru Madaktari wanaompatia matibabu.

"Mheshimiwa Rais nakushukuru sana, namshukuru pia Mama Janeth Magufuli kwa kunitembelea na kunifariji, naendelea vizuri na matibabu na afya yangu imeimarika kwa kiasi kikubwa" Ameeleza Mhe. Malecela.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
16 Agosti, 2016.

WANACHAMA YANGA WAMLILIA MANJI, WATAKA AKILIMALI AFUTWE UANACHAMA.

$
0
0
 Baadhi ya wanachama wa Yanga wakiwa inje ya Jengo la Makao Makuu ya Yanga.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KUFUATIA tetesi za Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji kutaka kujiengua pamoja na  kubadili msimamo wake wa kuikodi timu hiyo, wanachama wa klabu ya Yanga Kanda ya Dar es Salaam wamempigia magoti na kumsihi asibadili maamuzi yake.

Wanachama hao wamemuomba Manji kutobadili msimamo wake leo katika kikao cha dharula kilichofanyika leo kwenye Makao Makuu ya timu hiyo yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Aidha wanachama hao wameikemea tabia ya baadhi ya viongozi wa timu hiyo kuzungumza na vyombo vya habari pasipo kupata ridhaa ya chama.

Mwenyekiti wa Matawi ya Yanga Kanda ya Dar es Salaam, Robert Lyungu Kasera ameutaka uongozi wa timu hiyo kuweka mkutano mkuu wa dharula ili kupitisha pendekezo lao la kumvua uanachama katibu wa Baraza la wazee Ibrahim Akilimali kwa madai kuwa kiongozi huyo anashirikiana na timu pinzani kukwamisha mpango wa Manji kuikodi timu.

“Huyu mzee ana mikakati ya  kuiharibu Yanga na hatufahi, haiwezekani aongee masuala ya Yanga pasipo ridhaa ya uongozi wa klabu na viongozi mfikishe taarifa hii kwa usahihi bila kumun'gunya na kikao hiki kinalaani kitendo alichofanya,” amesema Lyunga.

Katika hatua ya kujitetea Mzee Akilimali ameomba radhi na kuwataka wanachama wa Yanga wasifikirie  vibaya kwa kauli aliyoiongea kwani wao kama Baraza la Wazee wanamuhitaji sana Mwenyekiti wao Manji na ameweza kuisaidia timu yao kwa takribani miaka 10. "Labda niseme hivi Kama kukurupuka ni tusi kama nilivyomwambia Yusuf, basi naomba radhi kwake Manji na wanayanga wote”.

Kufuatia hilo Kaimu Katibu Mkuu Yanga amethibitisha kupokea pendekezo hilo ila amesema wao hawana uwezo wa kumfukuza mwanachama hadi mkutano mkuu ufanyike.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAJULIA HALI SPIKA WA BUNGE JOB NDUGAI PAMOJA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU JOHN SAMUEL MALECELA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana kwa furaha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Sala sala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai nyumbani kwake Sala sala jijini Dar es Salaam alipokwenda kumjulia hali.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli kushoto akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai nyumbani kwake Sala sala jijini Dar es Salaam walipokwenda kumjulia hali. Kulia ni mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Spika Sala sala jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela ambaye anapata matibabu jijini Dar es Salaam.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimsalimia Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela ambaye anapata matibabu jijini Dar es Salaam.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa pamoja na Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Sala ya kumuombea Waziri Mkuu mstaafu John Samwel Malecela pamoja na mkewe Anne Kilango Malecela.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akizungumza na Mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai wakati alipokwenda na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwajulia hali nyumbani kwao Sala sala jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai huku Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiagana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwajulia hali nyumbani kwao Sala sala jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

KIPINDI CHA "SAFARI YA DODOMA" TAREHE 17 AUGUST 2016

$
0
0
 Katika kufanikisha agizo la mhe. Rais John Magufuli, na kutekeleza maamuzi ya kuhamishia makao makuu ya serikali Dodoma, TBC imeamua kuandaa kipindi maalum ili kuwafahamisha wananchi juu ya uamuzi huo, faida zake na pia nini kifanyike au nini kimefanyika mpaka sasa. Kipindi hiki kinaitwa “SAFARI YA DODOMA” ambacho kinarushwa kila siku ya jumatano saa 3:00 usiku, TBC1.
Kipindi hiki cha muda wa saa moja, kinawakaribisha wadau mbalimbali toka serikalini, mashirika na jamii kupata fursa kuja kuelezea umuhimu na jinsi ambavyo wamejiandaa kuhamia Dodoma, pia ni fursa gani zilizopo Dodoma, zikiwemo jitihada za wafanyabiashara na wawekezaji kutumia nafasi hii kuelezea namna ambavyo wanaweza kustawisha makao makuu ya nchi, Dodoma.

Kipindi cha kwanza kilichorushwa jumatano iliyopita ya tarehe 10 agosti 2016, tulikuwa na mhe. Cleopa Msuya, waziri mkuu mstaafu. Ambaye alitueleza hali ilivyokuwa wakati huo ameteuliwa kuwa waziri mkuu, na jinsi ambavyo maamuzi ya kuhamia Dodoma yalitekelezwa.

Katika kipindi cha jumatano tarehe 17 Agosti 2016, saa 3:00 usiku, kwenye studio za TBC1 tutakuwa na mgeni, mhe. Jenister Mhagama, waziri wa nchi, ofisi ya waziri mkuu, sera, bunge, kazi, vijana, ajira na wenye ulemavu.

Pia tutakuwa na nafasi ya kuwasikiliza wadau mbalimbali wakitoa maoni yao kuhusiana na maamuzi haya, pia tutakaribisha simu ili kujibu maswali mbalimbali yatakayotolewa kwenye kipindi, ambapo mshindi atajipatia zawadi toka chuo kikuu cha Dodoma (udom).

Nakukaribisha kutazama kipindi hiki, jumatano saa 3 usiku, TBC1

Kwa maoni tutumie barua pepe: maonidodoma@tbc.go.tz

Pia jiunge nasi katika mitandao ya kijamii:
SMS: Andika dodoma, acha nafasi, Ujumbe wako, tuma kwenda 15559
WhatsApp: 0678 279 107
Facebook: tbconetanzania
Twitter: tbconetanzania
Instagram: tbconetanzania
Youtube: TBC1.

KAMISHNA WA TRA AZINDUA KAMPENI YA KUHAKIKI NAMBA YA MLIPA KODI (TIN)

$
0
0
Kamishna wa TRA Bw. Alphayo Kidata akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za TRA jengo la Milenium Makumbusho leo wakati akielezea kampeni ya kuhakiki namba ya utambulisho wa mlipa kodi TIN itakayoendelea mpaka mwezi wa kumi mwaka huu nchini kote, kulia ni Kamishna wa Kodi za Ndani Bw.Elaijah Mwandumbya. Kamishna wa TRA Bw. Alphayo Kidata akipata maelezo kutoka kwa Rehema Shayo Meneja wa Usajili TRA wakati akikagua utekelezaji wa uhakiki huo.

......................................................

TRA kupitia kwa Kamishina Mkuu wa Ofisi hiyo wamezindua zoezi maalumu kwa ajili ya kuhakiki na kuboresha taarifa za usajili wa namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN) . Uzinduzi huo umefanywa na Kamishna Mkuu wa Ofisi hiyo Bw, Alphayo Kidata kwa kushirikiana na wafanyakazi wa ofisi hiyo mapema hii leo jijini Dar es salaam, hivyo kuanzia sasa zoezi hilo litakuwa endelevu katika mikoa yote nchini ya bara na visiwani .

Kidata alisema kuwa lengo kubwa la uzinduzi wa zoezi hilo ni kubadili mfumo wa sasa wa kuhifadhi kumbukumbu za walipa kodi kwa kuweka mfumo mpya unaoendana na ukuaji wa teknolojia ambao utakuwa na walipa kodi wake wanaostahili kuwepo kwenye wigo.

Aidha aliongeza kuwa mfumo huo utasaidia kuwaondoa walipa kodi hewa ,kuongeza ufanisi katika suala zima la usimamizi wa ukusanyaji kodi kwa kiwango cha juu na kuwezesha ulipaji kodi kuwa nafuu kwa mlipaji.

Hata hivyo katika hatua nyingine Kidata ametoa wito kwa yeyote mwenye namba ya utambulisho wa mlipa kodi kufika katika ofisi za mamlaka hiyo ili kuweza kupata utaratibu wa zoezi zima jinsi linavyokwenda

CHUO CHA CBE, TFDA NA AFRICAN RELIEF ORGANISATION WAMKABIDHI RC MAKONDA SHILINGI MILIONI 31.7 ZA MADAWATI LEO.

$
0
0

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Dk. Emmanuel Munishi (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda (kushoto) Mfano wa hundi ya shilingi milioni 8,000,000/= zilizotolewa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kama mchango wa chuo hicho kwa jamii kwa ajili ya kununulia madawati yatakayotumiwa na wanafunzi wa shule za msingi katika mkoa huo.Katikati ni Afisa Uhusiano wa Jamii wa Chuo hicho Leonidas Tibanga.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Dk. Emmanuel Munishi (katikati) akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhi mchango wa wa madawati wa shilingi milioni 8 kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda (kulia) leo jijini Dar es salaam. Mchango huo umetolewa na chuo hicho kununulia madawati yatakayotumiwa na wanafunzi wa shule za msingi za mkoa huo, Kushoto ni Afisa Uhusiano wa Jamii wa Chuo hicho Leonidas Tibanga.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Hiiti Sillo (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 17,700,000/= Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda (kushoto) kama mchango wa madawati kwa wanafunzi wa shule za Msingi jijini Dar es salaam leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda (kushoto) akiangalia mfano wa hundi ya shilingi milioni 6 zilizotolewa na Taasisi ya Kijamii inayojihusisha na masuala ya Kijamii ya African Relief Organisation ya jijini Dar es salaam kwa ajili ya kununulia madawati. Kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Shekh Abdallah Ndauga na Mratibu wa Miradi wa Taasisi hiyo Moadh Shannawi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kupokea msaada wa Fedha kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Taasisi ya Kidini ya Masuala ya Kijamii ya African Relief Organisation kwa ajili ya kununulia madawati kwa shule za Msingi za Dar es salaam. Picha/Aron

Na. Aron Msigwa – Dar es salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ametoa wito kwa Taasisi na Mashirika mbalimbali jijini Dar es salaam kujitokeza kwa wingi kuunga mkono zoezi la uchangiaji wa hiari wa madawati kwa shule za msingi linaoendelea jijini humo ili kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia yatakayozalisha wanafunzi bora wa shule za msingi.

Akizungumza mara baada ya kupokea mchango wa fedha za kununulia madawati kiasi cha shilingi milioni 31.7 kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE),Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Taasisi ya kidini ya masuala ya jaamii ya African Relief Organisation leo jijini Dar es salaam Mhe. Makonda amesema kuwa bado jamii inao wajibu na jukumu la kuhakikisha kuwa mazingira ya kusomea ya wanafunzi wa shule za msingi yanakuwa bora ili kuzalisha wahitimu walio na msingi imara.

“Napenda kutumia fursa hii kuzishukuru taasisi hizi ambazo zimeitikia wito wa kutoa michango yao ili kuwezesha upatikananji wa madawati, nawashukuru sana viongozi wa taasisi hizi kwa kuitikia wito wa mkoa wetu na kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuhakikisha shule zetu zina madawati na hakuna mwanafunzi anayekaa chini” Amesisitiza Makonda.

Ametoa wito kwa wananchi ambao wanaguswa kwa namna moja au nyingine kuendelea kutoa michango yao ili kuwasaidia wanafunzi wa shule za Msingi katika jiji la Dar es salaam ambao walikuwa wanapata shida ya kusomea katika mazingira magumu.

Ameongeza kuwa ili taifa liweze kuwa na wataalam wazuri katika Nyanja zote lazima msingi wa elimu katika shule za msingi uwe mzuri na kufafanua kuwa ndoto ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkoa wa Dar es salaam ni kukamilisha upatikanaji wa madawati na majengo ya madarasa.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Dkt. Emmanuel Munishi akizungumza mara baada ya kukabidhi mfsno wa hundi ya shilingi milioni 8 kama mchano wa chuo hicho kwa jamii amesema kuwa wao kama Chuo cha Elimu ya Biashara chenye kampasi mikoa minne ya Tanzania ukiwemo Mwanza, Dar es salaam, Dodoma na Mbeya kimeguswa kuchangia kiasi hicho cha fedha kwa kuwa kinawategemea wanafunzi waliofundishwa vizuri kutoka shule za Msingi.

Amesema wameamua kuunga mkono Juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kuhakikisha kuwa shule Zote za Dar es salaam zinaondokana na shida ya madawati.

“Sisi tumeguswa na uchangiaji wa madawati kwa kuwa ni taasisi ya ya elimu ya juu, kama taasisi ya elimu ya juu hatuwezi kupata wanafunzi wetu kama hakuna shule za msingi, tumeamua tusiwe watu wa kuvuna tu tukaamua kwenda moja kwa moja kwenye msingi ili kujenga msingi imara wa shule zetu” Amesisitiza.

Ameziomba taasisi zote za Elimu ya juu nchini kuiga mfano wa CBE katika kuchangia sekta ya elimu hapa nchini.

Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya Kidini ya Masuala ya Kijamii ya African Relief Organization ya jijini Dar es salaam Shekh Abdallah Ndauga iliyochangia shilingi milioni 6 amemshukuru Mkuu wa Mkoa huo kwa moyo wake wa kuendelea kuwahamasisha wananchi ambao wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kuchangia madawati.

Amsesema Taasisi ya African Relief Organisation itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na mkoa wa Dar es salaam katika kuleta maendeleo ya wananchi wake kupitia miradi mbalimbali wanayotekeleza ikiwemo uchimbaji wa visima katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Hiiti Sillo akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada uliotolewa na Mamlaka hiyo wa shilingi milioni 17.7 amesema TFDA inaunga mkono jitihada za Rais, Dkt. John Pombe Magufuli za kuhakikisha kuwa kila mtoto anakaa katika dawati ambapo katika bajeti yake ya mwaka 2015/16 inatoa mchango wa madawati 236.

Sillo ameongeza kuwa TFDA pamoja na majukumu iliyonayo inatambua kuwa elimu ndiyo nguzo muhimu katika kupambana na maadui wakubwa wa maendeleo, hivyo itaendelea kutoa mchango wake katika kusaidia sekta ya elimu hapa nchini.

VIVUTIO VYA UTALII LUKUKI VYAIBULIWA KATIKA HIFADHI YA MKINGU

$
0
0

Huyu ni aina mojawapo ya chura ambaye hapatikani mahali popote duniani isipokuwa katika Hifadhi ya Mazingira asili ya Mkingu ambaye ni mojawapo ya kivutio cha utalii katika hifadhi hiyo. ( Picha na Lusungu Helela- Wizara ya Maliasili na Utalii)
Baadhi ya sehemu za kuvutia katika Hifadhi ya Mazingira Asili ya Mkingu ambayo ni njia mojawapo inayotumiwa na watalii kwenda kijiji cha Maskati kuangalia vivutio vya Utalii vinavyopatikana katika Hifadhi hiyo. ( Picha na Lusungu Helela- Wizara ya Maliasili na Utalii).
 Maporomoko Lusingizo yenye mita zaidi ya 50 yaliyoko katika Hifadhi ya Mazingira Asili ya Mkingu ambayo ni mojawapo ya kivutio cha Utalii katika Hifadhi hiyo, Hadi hivi sasa kuna wawekezaji wamejitokeza ili waweze kuzalisha umeme katika kivutio hicho cha utalii. ( Picha na Lusungu Helela- Wizara ya Maliasili na Utalii).

Hifadhi asili ya Mkingu ipo wilaya ya Muvemero Mkoani Morogoro. Hifadhi hii ni eneo muhimu sana kiutalii kutokana na upekee wake wa maisha ya viumbe, mimea pamoja na maisha ya binadamu kiujumla.

Hifadhi hii ina ukubwa wa hekta 26, 334 na imezungukwa na vijiji vitano ambavyo vipo ndani ya kata sita na tarafa mbili.

Tangu kuanzishwa kwake Hifadhi hii mwaka 2016, Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii chini ya Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania ( TFS) imekuwa ikihudumia hifadhi hii kutokana na kuwa na mimea na viumbe ambavyo ni vivutio pekee vya Utalii nchini ambavyo havipatikani mahali popote duniani.

Mhifadhi Mkuu wa Mazingira asili ya Mkingu, Bw. Abeid Kindo anasema kutokana na sifa hizo za kipekee zinazopatikana katika Hifadhi hiyo imekuwa na umuhimu wa aina mbili ambao ni umuhimu wa kidunia na umuhimu wa kitaifa, Katika umuhimu wa kidunia upo katika viumbe, mimea na wanyama.

Anasema hifadhi hii ina wanyama wenye uti wa mgongo 392 kati ya hao 32 hawapatikana mahali popote duniani isipokuwa ni Mkingu tu yaani ni endemic species. Aidha , alisema kuna vyura na ndege wanaopatikana katika hifadhi hiyo tu.

Bw. Kindo anasema kuwa hifadhi hiyo imejaliwa kuwa na wanyama wanaotambaa 42 kati ya hao 14 hawapatikanimahali popote duniani isipokuwa Mkingu tu pamoja na aina ya ndege 214 kati ya hao ni aina nne ndio wanaopatikana katika hifadhi hiyo.

Mbali na hiyo, Anasema kuwa ndani ya hifadhi kuna msitu unaotumika kwa masuala ya mila za Waluguru kuwa eneo hilo ni zuri sana amabalo nalo ni kivutio cha utalii ndani ya msitu huo

Mbali ya kupatikana kwa wanyama na mimea katika Hifadhi hiyo Bw, Kindo anaeleza kuwa kuna pango la Malolo ambalo wenyeji wa Mkindo wana historia kubwa ya pango hilo ambalo wenyeji hawataweza kusahau kwani kuna mwanaume mmoja aliiba mke wa Mtu akaishi naye ndani ya pango hilo kwa muda wa miaka 3 bila kujulikana kijini. Pango hilo lina vyumba mithili ya nyumba iliyojengwa.

Pia anasema kuwa nadni ya hifadhi hiyo kuna pango ambalo ukikaa nje kuna upepo unaotoka ndani unapuliza hiyo ni ishara tosha kuwa humo ndani ndani kuna uhai. Anabainisha kuwa hifadhi hiyo ina jiwe lenye alama za nyayo za binadamu, kwato za mifugo ikiwa hiyo ni ishara tosha kuwa maisha ya kale ya binadamu yalianzia ndani ya hifadhi hiyo. .

Aliongeza kuwa mbali ya mapango ndani ya hifadhi hiyo , kuna maporomoko Lusingizo yenye mita zaidi ya 50 , hadi hivi sasa kuna wawekezaji wamejitokeza ili waweze kuzalisha umeme katika kivuto hicho cha utalii.

Pia kuna magofu ya kale ya Wajerumani ambayo waliishi ndani ya hifadhi kabla vita vya pili vya dunia na baada ya kuondoka kwa Wajerumani ilikuwa shule ya msingi ya kijiji cha Mafuta, na baada ya eneo hilo likatangazwa kuwa hifadhi , Shule ile ilitolewa na kujengwa kijijini.

Bw. Kindo anasema licha ya hifadhi hiyo kuwa na vivutio lukuki bado imekuwa ikitembelewa na idadi ya watalii isiyoridhisha licha kwa mwaka jana wameweza kupata watalii 75 kutoka Ujerumani,

‘’Tokea mwaka jana hadi hivi sasa tumeweza kuibua vivutio saba vya utalii na tunaendelea kufanya jitihada za makusudi ili kuhakikisha tunakuwa na vivutio vingi vya utalii ili tuweze kuwavutia watalii wa ndani na nje ya nchi ‘’.alisema Bw. Kindo

Aidha,Alisema Hifadhi hiyo ndio chanzo cha mto Wami, mto Ruvu na Mto Mkingu ambapo maji hayo yamekuwa yakitumika katika shughuli za kiuchumi kama vile kilimo,uvuvi,mazalia na makazi ya mimea na wanyama bila kusahau maji hayo ndiyo hutumika kuwanyesha wakazi wa Dare s Salaam na mikoa ya jirani

Amewataka wanafunzi wa vyuo mbalimbali wasisubili watafiti kutoka nje ya nchi kwenda kufanya tafiti katika Hifadhi hiyo badala yake wao wawe mstari wa mbele katika kuvumbua vitu vingi ambavyo vinapatikana katika hifadhi hiyo

Vyama vya michezo nchini vyaaswa Kutoa shukrani.

$
0
0
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Vyama vya michezo nchini vimeaswa kuthamini na kutoa shukrani baada ya kumaliza mashindano kwa lengo la kuimarisha ushirikiano pamoja na kuwapa moyo wanamichezo na wadhamini wa mashindano.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Mohamed Kiganja wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi na vyeti kwa washiriki, wadhamini na waandishi wa habari waliofanya vizuri katika kupiga picha na kuandika habari za Mashindano ya Magari yaliyofanyika Julai 8 hadi 10 wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani na kusimamiwa na Taasisi ya Automobile Association Tanzania (AATanzania). 

 “Vyama vingine vya michezo nchini vinapaswa kuiga mfano wa AATanzania wa kutoa shukrani baada ya mashindano, hili ni fundisho kubwa, wanapaswa kuthamini na kutambua msaada wa kufanikisha mashindano yeyote wanayoyaandaa” alisema Kiganja.

Katibu huyo aliongeza kuwa, yanafanyika mashindano ya michezo mbalimbali nchini yakiwa lengo la kuburudisha na kuelimisha jamii, ni wajibu wao kuiga mfano uliouoneshwa na AATanzania wa kutoa shukrani baada ya mashindano.

Naye Rais wa AATanzania Bw. Nizar Javan ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na BMT ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mashindano hayo yaliyofanikiwa kwa ufanisi mkubwa.

Bw. Nizar aliongeza kuwa mashindano hayo yaliisha salama bila ya kutokea ajali yeyote hatua ambayo inaendana na kauli mbiu yao inayosema “Usalama kwanza”.

Kwa upande wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Afisa Mnadhimu Kikosi cha Usalama Barabarani (SACP) Fortunatus Musilimu amewashukuru AATanzania kusimamia, kuandaa na kufanikisha mashindano hayo ambayo yamezingatia usalama wa washiriki wa mashindano na magari yaliyotumika.

Katika kuitangaza Tanzania kupitia mchezo wa magari, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Zamaradi Kawawa amewasihi waandaaji wa mashindano hayo kuebdelea kuhamasisha wachezaji wa mchezo huo kujitokeza kwa wingi na kushiriki mashindano hayo, hatua ambayo itasaidia kuongeza ushindani na kuitangaza Tanzania Kimataifa kwa kuwa mchezo huo unashirikisha mataifa malimbali.

Waandishi wa habari waliopata vyeti na zawadi kwa kuuhabarisha umma juu ya mashindano hayo ni pamoja na Mohamed Ugassa kutoka gazeti la The Guardian, Jimmy Tara wa ITV, Brown Msyani kutoka gazeti la Citizen, Timzoo Kalugira na Michael Maluwe kutoka Azam Tv, Nasongelya Kilyinga gazeti la Daily News na Miguel Suleyman ambaye ni wandishi wa habari wa kujitegemea.

Pamoja na waandishi hao, wadau waliopewa zawadi kwa kutambua mchango wao katika kufanikisha mashindano hayo ni Jeshi la Polisi, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Baraza la Michezo Tanzania na Hoteli ya Southern Sun. 

Mashindano hayo ya magari yaliyofanyika nchini yanatambuliwa na Shirikisho la Michezo ya Magari Duniani (FiA) ambayo AATanzania ni mwanachama.

MABALOZI NA WAWAKILISHI WA MABALOZI HAPA NCHINI WASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO.

$
0
0
Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Finland Bw. Simo Pekla Parvianen akisaini kitabu cha Maombolezo katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam leo kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Bi. Monica Patricio Mussa akisaini kitabu cha Maombolezo katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam leo kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Bi. Monica Patricio Mussa akitoa heshimza zake mara baada ya kusaini kitabu cha Maombolezo katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam leo kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Elitrea Bw. Saleh Azaril
Kaimu Balozi wa Burundi nchini Tanzania Bw. Pierre Ndayishimiye
Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Angola Bw. Joel Cumbo .Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Selikarini, Ofisi ya Makamu wa Rais.


Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefungua kitabu cha maombolezo kwa ajili ya Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa walioko nchini kutoa salaam zao za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Pili wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mzee ABOUD JUMBE MWINYI. 

Kitabu hicho kitakuwa wazi katika Ofisi ya Makamu wa Rais iliyopo Mtaa wa Albert Luthuli, Dar es salaam kuanzia leo siku ya Jumanne Agosti 16 hadi Ijumaa Agosti 19, 2016 toka saa 4 asubuhi hadi saa 9.30 alasiri. 

Mzee ABOUD JUMBE ambaye pia alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifariki dunia juzi nyumbani kwake Mji Mwema, Kigamboni, Dar es salaam na kuzikwa jana katika makaburi ya Migombani Unguja, Zanzibar. 

Wana-diplomasia wanaowakilisha nchi zao hapa nchini kutoka Finland, Msumbiji, Burundi, Uganda na Angola tayari wameweka saini kwenye kitabu cha maombolezo. 

Mzee JUMBE alishika madaraka ya kuongoza Zanzibar mwaka 1972 baada ya kuuawa kwa aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar, hayati Abeid Amani Karume baada ya Baraza la Mapinduzi kumchagua kwa kauli moja. Kutokana na kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar mwaka 1984, Mzee JUMBE alilazimika kujiuzulu na viongozi wengine. 

Imetolewa na 
Ofisi ya Makamu wa Rais 
Dar es salaam.

CHAMA CHA WAKULIMA (AFP) CHALAANI VIKALI HUJUMA ZILIZOANDALIWA NA UKAWA

$
0
0
Na Maelezo-Zanzibar 16/8/2016

Chama cha Wakulima (AFP) kimelaani vikali dhidi ya hujuma zilizoandaliwa kufaywa na Umoja wa Wananchi UKAWA ifikapo tarehe 1mwezi ujao.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mwenyekiti wa Chama hicho Said Soud Said katika Ukumbi wa Sanaa uliopo Rahaleo Zanzibar amesema hujma hizo zilizoandaliwa na UKAWA za kufanya maandamano makubwa ya kupinga Serikali iliopo madarakani zilizopangwa nchi nzima zina lengo la kuvuruga amani nchini.

Amesema Jeshi la Polisi na Wananchi kwa ujumla wametakiwa kuwa macho kutokana na kauli zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa siasa za kutaka kuchafua kwa makusudi na kuipeleka nchi katika vurugu jambo ambalo litasababisha kuwepo vitendo vibaya ikiwemo ubakaji na mauaji.

Aidha amesema Zanzibar haiwezi kuvumilia kuingia katika vurugu hivyo Wananchi wasikubali kushawishiwa na Wanasiasa wasiopenda maendeleo wanaotaka kuvuruga amani iliopo.

“Vijana msikubali kushawishiwa na Wanasiasa wamejitokeza kwa ajili ya biashara hivyo natoa indhari hii kwa kuwatahadharisha wazanzibari wenzangu kuachana na hujuma hiyo inayoandaliwa,”Alisema Said Soud.

Hata hivyo amewaasa Vijana kutokubali kushawishiwa na Wanasiasa kushiriki katika vurugu na badala yake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika shughuli za kiuchumi na maendeleo kwa lengo la kujikimu kimaisha.

Akizungumzia suala la amani na utulivu Pemba Mwenyekiti huyo amefahamisha kuwa hali sasa ni yakuridhisha kutokana na kupungua kwa kasi vitendo vya hujumaVisiwani humo na.

“Jeshi la polisi kwa kushirikiana na Serikali wamesaidia kwa kiasi kikubwa na kuwadhibiti wale wote walioshiriki kufanya vitendo hivyo kwa kuchukuliwa hatua za kisheria,” ameeleza Mwenyekiti huyo .

Sambamba na hayo Mwenyekiti huyo ameipongeza Serikali iliopo madarakani kwa kuchukuwa hatua nzuri ya kuimarisha Mji wa Zanzibar pamoja na Wafanya Biashara wa Darajani kwa kuitikia agizo lililotolewa na Serikali la kuhama katika maeneo yao ya kufanyia biashara na kuwataka kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki ujenzi.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO- ZANZIBAR.

Vyama vya michezo nchini wameaswa kuiga mfano wa AATanzania.

$
0
0
 
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO

Vyama vya michezo nchini vimeaswa kuthamini na kutoa shukrani baada ya kumaliza mashindano kwa lengo la kuimarisha ushirikiano pamoja na kuwapa moyo wanamichezo na wadhamini wa mashindano.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Mohamed Kiganja wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi na vyeti kwa washiriki, wadhamini na waandishi wa habari waliofanya vizuri katika kupiga picha na kuandika habari za Mashindano ya Magari yaliyofanyika Julai 8 hadi 10 wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani na kusimamiwa na Taasisi ya Automobile Association Tanzania (AATanzania).

“Vyama vingine vya michezo nchini vinapaswa kuiga mfano wa AATanzania wa kutoa shukrani baada ya mashindano, hili ni fundisho kubwa, wanapaswa kuthamini na kutambua msaada wa kufanikisha mashindano yeyote wanayoyaandaa” alisema Kiganja.

Katibu huyo aliongeza kuwa, yanafanyika mashindano ya michezo mbalimbali nchini yakiwa lengo la kuburudisha na kuelimisha jamii, ni wajibu wao kuiga mfano uliouoneshwa na AATanzania wa kutoa shukrani baada ya mashindano.

Naye Rais wa AATanzania Bw. Nizar Javan ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na BMT ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mashindano hayo yaliyofanikiwa kwa ufanisi mkubwa.

Bw. Nizar aliongeza kuwa mashindano hayo yaliisha salama bila ya kutokea ajali yeyote hatua ambayo inaendana na kauli mbiu yao inayosema “Usalama kwanza”.

Kwa upande wa Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Afisa Mnadhimu Kikosi cha Usalama Barabarani (SACP) Fortunatus Musilimu amewashukuru AATanzania kusimamia, kuandaa na kufanikisha mashindano hayo ambayo yamezingatia usalama wa washiriki wa mashindano na magari yaliyotumika.

Katika kuitangaza Tanzania kupitia mchezo wa magari, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Zamaradi Kawawa amewasihi waandaaji wa mashindano hayo kuebdelea kuhamasisha wachezaji wa mchezo huo kujitokeza kwa wingi na kushiriki mashindano hayo, hatua ambayo itasaidia kuongeza ushindani na kuitangaza Tanzania Kimataifa kwa kuwa mchezo huo unashirikisha mataifa malimbali.

Waandishi wa habari waliopata vyeti na zawadi kwa kuuhabarisha umma juu ya mashindano hayo ni pamoja na Mohamed Ugassa kutoka gazeti la The Guardian, Jimmy Tara wa ITV, Brown Msyani kutoka gazeti la Citizen, Timzoo Kalugira na Michael Maluwe kutoka Azam Tv, Nasongelya Kilyinga gazeti la Daily News na Miguel Suleyman ambaye ni wandishi wa habari wa kujitegemea.

Pamoja na waandishi hao, wadau waliopewa zawadi kwa kutambua mchango wao katika kufanikisha mashindano hayo ni Jeshi la Polisi, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Baraza la Michezo Tanzania na Hoteli ya Southern Sun.

Mashindano hayo ya magari yaliyofanyika nchini yanatambuliwa na Shirikisho la Michezo ya Magari Duniani (FiA) ambayo AATanzania ni mwanachama.

MBUNGE ULEGA ASHIRIKI KUHAMASISHA WANANCHI KUFYATUA MATOFALI KWA AJILI YA UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI

$
0
0

 Mbunge wa Jimbo la mkuranga Abdallah Ulega akishiriki kufyatua tofari za  ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kikundi kilichopo kata ya Mkamba wilayani Mkuranga,mbali na kushiriki huko pia alichangia viloba vya unga wa sembe,maharagwe,maji ya kunywa kutokana na vijana wa kijiji hicho kuweka kambi ya kufyatua matofali hay oleo mkoani Mpwni.
 Wazee wa kijiji cha Kikundi ,kilichopo kata ya Mkamba wilayani mkuranga  wakiteta jambo na mbunge wa jimbo hilo Abdallah ulega, ambapo pamoja na mambo mengine walimpongeza mbunge huyo kwa kuonesha moyo wa kuitumikia wilaya hiyo nakudai katika wabunge saba waliotangulia haijawahi kutokea katika kile anachofanya Ulega ikiwamo kufanya ziara za vijiji kwa lengo lakuwashukuru.
Vijana wa kijiji cha kikundi ,kata ya mkamba wakiwajibika katika kufyatua matofali ya ujenzi wa Zahanati kijijini hapo ambapo kwa muda mrefu imekuwa kero kubwa hali inayowafanya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hiyo katika kijiji cha kizapala wilayani humo.
(Pichs na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega ameshiriki na kuhamasisha wananchi wa Kijjji cha kikundi ,kata ya mkamba kufyatua matofali Kwa ajili ya Ujenzi wa Zahanati ya kijiji hicho. 

Akiwa katika eneo la tukio alishirikiana kikamilifu na vijana ,wazee ,na akina mama waliojitokeza Kwa wingi Kwa ajili ya kujitolea,akizungumza katika eneo hilo akiwa sambamba na Diwani wa Kata hiyo Hassan Dunda, mbunge Ulega aliwaeleza wananchi hao kuwa ameshiriki shughuli hiyo ikiwa sehemu ya majukumu yake na ahadi alizotoa Kwa watu wake na kwamba maendeleo ya kijiji cha kikundi na Mkuranga Kwa ujumla yataletwa na wao wenyewe. 

Alisema kuwa katika kipindi chake chote cha ubunge atahakikisha anafanya mambo makubwa Kwa ajili ya maendeleo ya wilaya hiyo huku akidai kuwa Mkuranga imechelewa sana lazima wakimbie mbio. Kwa upande wa Wazee wa kijjji hicho wamesema kuwa Ulega ameonesha nia ya dhati mno katika uongozi wake na wanaimani naye sana kwamba atafanya mambo mengi makubwa. 

Akizungumza kwa niaba ya Wazee wezake Idrisa Pelete amesema kuwa kuna wabunge wengi wamepita na hawakuweza kufanya lolote lakini Kwa sasa wanaamini wamepata kiongozi wa kweli na hicho ndicho walikuwa wanakihitaji.Pia Kijana aliyejitambulisha kuwa ni shaweji Mohammed akitoa neno la shukrani Kwa mbunge alisema kuwa pamoja na kwamba yeye ni mpinzani lakini kwa kazi kubwa alionesha Mbunge kwakweli wanampenda mno.

Marufuku kutumia mafuta ya transfoma kukaagia chipsi- Profesa Muhongo.

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amepiga marufuku matumizi ya mafuta ya transfoma kwa ajili ya kukaangia chips na kutengeneza mikorogo.

Profesa Muhongo ameyasema hayo alipokuwa akihutubia wakazi wa kijiji cha Kirongo wilayani Muheza mkoani Tanga alipokuwa katika ziara ya kukagua miradi ya umeme  vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika mkoa huo.
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images