Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA MUFINDI DKT. RIZIKI SHEMDOE AKAGUA UPOKEAJI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA MIUNDOMBINU YA SHULE YA SEKONDARI MDABULO WILAYA YA MUFINDI

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Dkt. Riziki Shemdoe (katikati wa nne) akikagua upokeaji wa wanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya sekondari mdabulo katika iliyoko Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa. Shule hiyo ambayo iko umbali wa km 45 kutoka mji wa Mafinga upande wa mashariki mwaka huu imeanza kufundisha programu za masomo ya kidato cha tano na sita katika mchepuo wa Sanaa HGK,HKL na HGL.

Baadhi ya wanafuzi wa shule ya sekondari mdabulo iliyoko wilayani Mafinga mkoa wa Iringa wakipata huduma ya maji safi katika eneo la shule hiyo ambayo ni ya mchanganyiko wa wavulana na wasichana kwa “O – Level” na wasichana pekee kwa “A – Level”.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Dkt. Riziki Shemdoe (kushoto) akikagua uwepo wa madawati katika madarasa ya shule hiyo ambayo kwa mara ya kwanza imeanza kufundisha programu za masomo ya kidato cha tano na sita katika mchepuo wa Sanaa.
MkurugenziMtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Dkt. Riziki Shemdoe (katikati) akikagua mazingira na miundombinu ya shule hiyo akiwa ameambatana na viongozi wa shule hiyo.

KANALI MKISI AANZA KUSHUGHULIKIA KERO ZA USHURU WA MAZAO KWA WAKULIMA WADOGO KASULU

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kanali Martin Mkisi akiongea na wakulima wadogowadogo wanaosafirisha mazao yao ya chakula kutoka mashambani mwao wakati alipokutana nao njia akiwa katika ziara vijiji vya Kata ya Kagera Nkanda.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Martin Mkisi (mwenye sare za jeshi) akiongea na viongozi wa vijiji vya Kagera Nkanda, na kutafuta ufumbuzi wa kero za wananchi katika vijiji vyao.

Viongozi wa vijiji vya Kata ya Kagera Nkanda, pamoja na wakuu wa idara mbalimbali wa halmashauri ya Wilaya wa Kasulu, wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa wilaya.

Na Father Kidevu Blog, Kasulu

MKUU wa Wiaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kanali Martin Mkisi amepiga marufuku usafirishaji wa mazao nyakati za usiku na kuagiza wakulima wadogo Wilayani humo kutotozwa ushuru wa mazoa na badala yake ushuru huo utozwe kwa wakulima wakubwa pekee.

Kanali Mkisi alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza kwa nyakati tofauti alipofanya ziara katika ya Kagera Nkanda na vijiji vyake kutatua kero hiyo ya ushuru wa mazao iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa maeneo hayo kwa muda mrefu.

Mkisi aliyeambatana na watendaji wengine wa serikali Wilayani humo, akiwepo Mkurugenzi wa Hamashauri, Katibu Tawala Wilaya pamoja na Mwekahazina wa Wilaya na maafisa wengine.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ameagiza viongozi wa vijiji vyote kuweka utaratibu wa kuwatambua wakulima wadogo katika maeneo yao ili kupata vibali vitakavyowaruhusu kusafirisha mazao yao kutoka shambani hadi nyumbani bila kulipa ushuru.

“Wakulima wadogo wote watambuliwe na serikali za vijiji ili kupata vibali vitakavyowaruhusu kuondoa mazao yao mashambani bila kulipa ushuru, ni dhahiri ushuru huu ni kero ya muda mrefu kwa wakulima hawa wadaogo ambao hulima mazao yao ya chakula na si ya biashara,”alisema Kanali Mkisi.

Pia amewataka wakulima wakubwa wa kilimo cha biashara waishio mjini na kulima vijiji vya Kagera Nkanda waendelee kutoa ushuru kwa mujibu wa sheria namba 9 kifungu cha 7 ya mapato ya mazao na kupiga marufuku usafirishaji wa mazao usiku.

Kanali Mkisi pia amewataka watendaji wa Vijiji kuboresha namna ya usimamizi na udhibiti wa mapato na kuahidi kushirikiana nao katika kuboresha. “Ninaamuru kwamba matumizi ya mapato lazima yaelekezwe kwenye huduma za kijamii, maji,afya, elimu, miundombinu… hususan maboresho ya barabara korofi ya kutoka Kasulu mjini hadi vijiji vya Kagera Nkanda ambayo tayari ina mkandarasi kwaajili ya matengenezo,”aliongeza Kanali Mkisi.

Mkisi pia ameagiza mazingira ya kufanyia kazi kwa wakusanya ushuru wa mazao na mapato mengine kuboreshwa mara moja huku akiagiza wataalam wa kodi kufika maeneo yote ya vijijini na kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa wananchi.Kero ya wakulima wadogo kutozwa ushuru wa mazao watokapo kuvuna mazao yao hasa katika vijiji viliovyopo katika Kata ya Kagera Nkanda ilikuwa ni ya muda mrefu na imekuwa ikileta usumbufu kwa wananchi.

WANAFUNZI 382 NDIO WANA SIFA YA KUSOMA STASHAHADA YA UALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATI WANAFUNZI 7,805

$
0
0
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na waandishi habari juu ya hatua ya serikali waliochukua kwa wanafunzi waliondolewa katika chuo kikuu cha Dodoma leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Kulia ni Naibu Katibu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo, Kulia ni Kamishina wa Elimu wa Wizara hiyo, Eustella Balamsesa.
 Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii 

BAADA ya Serikali kufanya uchambuzi wa sifa za Wanafunzi wanaostahili kusoma program maalum ya Ualimu wa sekondari kwa masomo ya sayansi katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),ni wanafunzi 382 ndio wamekidhi kusoma program hiyo kati ya wanafunzi 7,805 waliondolewa katika mgomo wa walimu wa chuo hicho. 

Akizungumza na waandishi habari Ofisini kwake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema kuwa wamefanya uchambuzi huo ili kutoa haki kwa watu wenye sifa ya kusoma program maalum kwa walimu wa sekondari . 

Amesema kuwa vigezo vya wanafunzi hao kusoma ilikuwa ni ufaulu wa masomo ya sayansi kwa daraja C-A ambapo ni wanafunzi 382 ndio wameonekana na sifa hizo kati ya wanafunzi 6595 waliodahiliwa stashahada maalumu ya walimu wa sekondari . 

Amesema wanafunzi 52 walipata daraja la nne katika matokeo ya kidato cha sita ambapo ni kinyume cha matakwa stashahada maalumu ya walimu wa sekondari .Amesema kuwa wanafunzi 1,210 walidahiliwa kimakosa kutokana kundi hilo ni walimu wa shule ya msingi ambao hawako katika program maalumu ya walimu wa sayansi. 

Profesa Ndalichako amesema kuwa wanafunzi 4,586 wa mwaka wa kwanza program maalum ya stashahada ya walimu wa sekondari wamekidhi vigezo vya ufaulu lakini sio kwa masomo ya sayansi watahamishiwa katika vyuo vya serikali vya ualimu ambavyo ni ,Morogoro ,Butimba, Mpwapwa ,Songea, pamoja na Tukuyu kuendelea na masomo yao huku wanafunzi wa 1,337 wa mwaka pili wanahamishiwa katika vyuo vya ualimu wa shule ya msingi ambavyo ni Korogwe na Kasulu na watajighramia na huku wanafunzi 290 hawana sifa kabisa ya kusoma na wizara kuwataka waombe mafunzo ya sifa zinazolingana. 

Amesema wanafunzi 29 watahamishiwa kusoma mafunzo ya ualimu wa shule ya msingi katika chuo cha Kasulu kwa gharama zao huku 1181 wametakiwa kuomba mafunzo ya ualimu wa shule ya msingi katika chuo chochote kwa gharama zao.

BAADA YA COPA AMERICA NA EURO 2016 SASA TWAELEKEA RIO 2016 OLIMPIKI.

$
0
0
Mara nyingi tumezoea kuangalia michezo fulani ikifanyika mahali fulani, mfano mwezi huu na mwezi uliopita tulishuhudia mashindano ya kabumbu ya Amerika ya kusini na yale ya Ulaya pia mashindano ya dunia ya riadha.
 
Lakini hivi sasa macho na masikio ya wapenda michezo duniani kote yataelekezwa jijini Rio de Jeneiro nchini Brazil ambako michezo ya OLIMPIKI itafanyika.

Michezo ya Olimpiki ni mashindano ya mkusanyiko wa michezo mbali mbali yanayofanyika pamoja (jiji moja) kila baada ya miaka minne.Baadhi ya michezo hiyo ni Mpera wa miguu,Mpira wa kikapu,Mpira wa magongo,Riadha, Ndondi,Judo,Kuogelea,Sarakasi nk.Michezo ya mwaka huu itajumuisha Nchi zipatazo 206,Michezo takribani 42 itashindaniwa katika viwanja 37 kwa matukio 306.Michezo hii inatazamiwa kuanza Agust 5-21/2016.

Pia michezo hii huwa na kitu tofauti sana na michezo mingine,kitu hicho ni MWENGE wa Olimpiki,Mwenge huu huwashwa na kuzungushwa katika baadhi ya nchi kwenye mabara yote matano ya dunia ili kusisitiza umoja ma ushirikiano.Ukiangilia nembo ya Olimpiki utaona ina viduara vitano vilivyoungana,ikiwa na maana ya mabara matano ya dunia.

Usikose kujumuika nasi kesho ambapo tutakuletea utamu mwingine kuelekea michezo hii,kidokezo ni kuwa Nani mwanzilishi wa michezo hii,ilianzishwa lini na wapi?

MADIWANI WA KYERWA NA BIHARAMULO MKOANI KAGERA WAPEWA SOMO LA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA FEDHA ZA SERIKALI ZA MITAA

$
0
0

Mwezeshaji kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3), Magdalena Katunzi akiwasilisha mada ya uzimamizina Udhibiti wa fedha katika Mamlaka za serikali za mitaa. Mada hiyo ilitolewa kwa madiwani wa Halmashauri za Wilaya za Kyerwa na Biharamuo Mkoani Kagera leo.
Lengo kuu la mada hiyo kwa Madiwani ahao ambao halmashauri zao zimechaguiwa kuanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za umma ni pamoja na kumuwezesha Diwani kupata taarifa na uweewa juu ya taratibu za usimamizi na udhibitiwa fedha katika Mamlaka za Serikali za mitaa.

Aidha Katunzi alianisha mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na vyanzo vya mapato vya Mamlaka za serikali za Mitaa, ikiwa ni mapato ya ndani, ruzuku kutoka serikali kuu na Mikopo. Madiwani walifundishwa mbinu za kuongeza mapato ya Hamashauri ambapo walifundishwa namna ya kubuni na kuanzisha vyanzo vipya vya mapato, kuboresha viwango vya tozo, kuboresha mbinu za ukusanyaji mapato, kusimamia matumizi ya fedha za serikali ya mitaa na udhibiti wa fedha za Halmashauri. Source:Father Kidevu Blog,Kagera

Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.
Wakuu wa Wiaya za Kyerwa na Biharamulo mkoani Kagera, Kanali Mstaafu, Shaabn Lissu (kushoto) wa Kyerwa na Saada Malunde wa Biharamulo wakiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo, Wende Ng'ahala (kulia) wakifuatilia mada hiyo.
Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.
Ofisa Mipango wa Wilaya ya Biharamulo, Andambike Kyomo akifafanua jambo kuhusu namna ya ugawaji wa fedha za Halmashauri kwa makundi ya Vijana, Wanawake na matumizi mengine.
Mratibu wa Mradi wa PS3 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bertha Swai akifafanua jambo kuhusu mada hiyo na maswali yaliyoulizwa na washiriki.

Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.
Ili kuondoa uchovu kwa washiriki kunakosababisha kusinzia wakati wa mafunzo, washiriki walifanya mazoezi kuchangamsha mwili na kuimarisha usikuvu.
Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo, Saada Malunde (kulia) akifurahia kuonana na Mkurugenzi Mpya wa Hlamashauri ya Wilaya ya Biharamulo, Wende Israel Ng'ahala. Watendaji hao ndio walioonana kwa mara ya kwanza na wote ni wapya katika Wilaya hiyo.

Serikali na British Council Tanzania zashirikiana kuwapiga msasa Mashirikisho ya Sanaa kuhusu Fursa ya Sanaa ya Afrika Mashariki.

$
0
0

Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge (kulia) akiwaelekeza baadhi ya Viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania pamoja na Wadau wa masuala ya Sanaa kuhusu Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na Taasisi hiyo, 19 Julai, 2016 jjijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Maendeleo ya Sanaa, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Leha Kihimbi (kulia) akiwasisitizia baadhi ya Viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania pamoja na Wadau wa masuala ya Sanaa kuhusu umuhimu wa Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na Taasisi hiyo, 19 Julai, 2016 jjijini Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM.
Kaimu Mkurugenzi British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge (wa pili kushoto waliokaa mbele) akiwaelekeza baadhi ya Viongozi wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania pamoja na Wadau wa masuala ya Sanaa kuhusu Fursa ya Sanaa inayodhaminiwa na Taasisi hiyo, 19 Julai, 2016 jjijini Dar es Salaam.
 
 
Serikali na British Council Tanzania yawapiga msasa Mashirikisho ya Sanaa namna ya kuandika Mapendekezo ya Mradi wa Fursa ya Sanaa ya Afrika Mashariki.

SERIKALI kwa kushirikiana na British Council Tanzania imekutana na baadhi ya Viongozi pamoja na Wawakilishi wa Mashirikisho mbalimbali ya Sanaa nchini na kuwapatia elimu juu ya namna ya kuandika Mapendekezo (Proposals) za Mradi wa kuwania fursa ya sanaa inayodhaminiwa na British Council Tanzania.

Elimu hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge pamoja na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sanaa, Bi. Leah Kihimbi lengo likiwa kuwahamasisha wasanii kote nchini kuchangamkia fursa hiyo inayodhaminiwa na Taasisi hiyo yenye Makao yake Makuu nchini Uingereza.

Awali akieleza kuhusu fursa hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa British Council Tanzania, Bi. Nesia Mahenge amesema kwamba fursa ya sanaa kwa Wasanii zinahusisha sehemu tatu ikiwemo fursa ijulikanao kama nAnA (new Arts new Audiences) ambayo ndiyo imefunguliwa kwa sasa na baadaye fursa nyingine mbili za Creative Hustle pamoja na Mobility East Africa zitafuata.

Ameeleza kuwa kuhusu vigezo vya kujiunga na fursa hiyo ni pamoja Wasanii kuwa na umri kuanzia miaka 18-35, kuwa na Ushirikiano (Partnership) katika ya nchi tano zinazohusisha fursa hiyo, kuwa na Kampuni binafsi au ya Shirikisho, fursa inahusisha fedha ya uandikaji wa Pendekezo (Proposal) zitakazotolewa ni kuanzia paundi 2,000 hadi paundi 20,000 pamoja na kuwa na akaunti namba katika benki fulani.

Amefafanua kuwa, fedha zitakazotolewa na British Council Tanzania sio za mkopo bali ni kwa ajili ya wasanii wote ambao watafanikiwa kuwania fursa hiyo ambapo kwa sasa amesema kwamba wanaanza na fursa ya nAnA, hivyo amewahimiza wasanii nchini kupitia mmoja mmoja pamoja na Mashirikisho yao kuanza kuandika mapendekezo ya kuomba fursa hiyo kwa kujaza fomu ambayo inapatikana katika tovuti ya www.britishcouncil.or.tz

“Fedha hizi sio za mkopo, mtu akifanikiwa kuzipata haimaanishi kuwa anapaswa kuzirejesha, isipokuwa British Council wao watakuwa wanafuatilia ni kwa namna gani fedha hizo umeweza kufanikisha wazo lako na lina faida gani katika jamii ama wengine wamenufaika vipi na wazo lako”, alisema Bi. Mehenge.

Ameongeza kuwa, Wasanii pamoja na Mashirikisho hayanabudi kusaidiana katika kufanikisha suala hilo kwa kuelekezana juu ya namna ya kuwapata watu wenye ujuzi wa jinsi ya kuandika Mapendekezo (Proposals) na kuziandika kwa wingi ili Wasanii wa Tanzania wapate nafasi ya kushinda fursa hiyo kwani kuna nchi nyingine nazo zinahusika na fursa hiyo ambazo ni za Afrika Mashariki.

Kuhusu mwisho wa kuwasilisha maombi hayo, amesema kwamba, tarehe ya mwisho ni 31 Julai mwaka huu,lakini wasanii hawanabudi kuwa na hofu kwani bado wana nafasi kubwa ya kuandika na kuweza kushinda hiyo fursa, kwani kinachomata ni wazo zuri msanii alilokuwa nalo na sio tu uandishi mzuri.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Leah Kihimbi amewasisitizia Wasanii kote nchini kuchangamkia fursa hiyo bila kuwa na woga kwani ni fursa ya pekee ya kuwanufaisha na kazi zao na kuiletea sifa Taifa.

“Msiogope kuandika kuomba hii fursa, kwani kuna wenzenu pia wanaitafuta, jitahidini kushirikiana ili mwisho wa siku Tanzania iwe na miongoni mwa wasanii watakaowania fursa hii, na kwa kufanya hivyo mtakuwa mmelejengea heshima Taifa letu”, alisema Kihimbi.

Fursa ya Sanaa kwa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla ni fursa inayodhaminiwa na British Council Tanzania ambapo wasanii wanatakiwa kuiomba kwa kuandika mapendekezo kuhusu mawazo yao juu ya mambo wanayotarajia kuyafanya kupitia sanaa na namna gani itanufaisha jamii huku ikihusisha nchi tano za Afrika Mashariki zikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia.

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA MSD JUU YA UAMUZI WA BODI YA WADHAMINI KUHUSU WAKURUGENZI WALIOSIMAMISHWA ,SOMA HAPA

MAJALIWA: MALIASILI NA UTALII JIPANGENI VIZURI

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii
kujipanga vizuri na kufanya mapitio ya idara zake hususan ya misitu baada ya kubainika kuwepo kwa matatizo makubwa.“Eneo la misitu limekuwa na matatizo makubwa, watendaji wengi si waaminifu na sura ya wizara si nzuri miti mingi inakatwa na fedha haiingii Serikalini. Huu ni mgogoro mpya,” alisema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana alipokutana na watumishi wa wizara hiyo jana (Jumatatu, Julai 18, 2018) jijini Dar es Salaam, na kusisitiza kwamba hakuna sababu ya Serikali kuendelea kuwa na watumishi wasiokuwa na uaminifu, uadilifu na uwajibikaji.Alisema lengo la mkutano huo ni kukutana na watumishi kusikiliza changamoto zao, kukumbushana wajibu, pamoja na kutoa maagizo ili  yatekelezwe kwa utaratibu unaokubalika kisheria.

Alisema mtumishi ambaye atabainika kuwa haitendei haki nafasi yake kwa
kutokutimiza majukumu ipasavyo hana sababu ya kuwepo kwa sababu serikali inapoteza fedha nyingi kuwalipa watu wasio na tija. Waziri Mkuu alisema sababu inayoikosesha Serikali mapato ni uwepo wa watumishi wasio waadilifu kwenye ofisi za Serikali ikiwemo Wizara ya Maliasili na Utalii hivyo kuna umuhimu wa kuzisafisha.

Alisema kuna uvunaji mkubwa wa misitu kuliko upandaji huku asilimia 50 ya mapato yatokanayo na uvunaji huo yanapotea na kuisababishia Serikali hasara ambapo alihoji sababu ya wizara kushindwa kusimamia jambo hilo. Katika hatua nyingine; Waziri Mkuu aliitaka wizara hiyo kupunguza idadi ya vizuizi vya ukaguzi wa mazao ya misitu kwenye barababara mbalimbali baada ya kukosa tija kutokana na upotevu wa misitu unaotokea kila siku.

Alitoa mfano wa barabara ya kwenda mikoa ya kusini  kuanzia Dar es Salaam ambapo alisema ina vizuizi visivyopungua sita na kila kizuizi kinatumika kwa ajili ya kukagua mazao ya misitu na maliasili inayotoka kuvunwa. “Vizuizi vya katikati ya safari havina umuhimu na badala yake kuwe na vizuizi mwanzo na mwisho ili rasilimali zingine zitumike kuongeza nguvu na umakini wa ukaguzi kwenye vituo vichache vitakavyosalia,”.

“Kwa mfano ukitokea Ikwiriri kuja Dar, kuna vituo vya ukaguzi wa maliasili
visivyopungua sita, kuna Ikwiriri, Kibiti,  Jaribu Mpakani,Mkuranga, Vikindu  kote huku wanakagua lakini linapofika kituo cha mwisho cha Mbagala linakutwa na makosa kwenye mzigo kwanini’’?

“Yule mkaguzi wa kwanza alifanya kazi gani? Kuna tatizo la uadilifu na
ninyi ni mashahidi, sasa naagiza ongezeni nguvu kwenye vituo vikuu vya
ukaguzi yaani mwanzo na mwisho,” alisema. Aidha alisema ni muhimu kukawa na mabadiliko kwenye mfumo wa mauzo ya misitu kutoka wa sasa (kuuza kwa eneo) na kuhamia kwenye mfumo wa mnada ambao utaongeza mapato ya Taifa na utaweka uwazi.

Pia aliwataka watumie mashine za malipo za kielektroniki (EFD),wanapofanya mauzo ya mazao ya misitu ili
kuepusha matumizi ya daftari na risiti bandia ambazo hazitambuliwi na
wizara.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
JUMANNE, JULAI 19, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje ashiriki maadhimisho miaka 59 ya Aga Khan kuongoza Ismailia

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba (Mb.), akizungumza katika maadhimisho ya Miaka 59 ya Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Shia Ismailia, Mtukufu Aga Khan tangu aliposhika nafasi hiyo.Katika hotuba yake Dkt. Kolimba alitumia nafasi hiyo kumpongeza Mtukufu Aga khan kwa mafanikio katika kipindi cha uongozi wake na kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo iliyochini ya Taasisi yake. Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Ismailia hapa nchini, Bw. Amin Kurji. 
Sehemu ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo nao wakimsikiliza Dkt. Kolimba, wa pili kutoka kulia ni Balozi wa Japan hapa nchini Mhe. Masaharu Yoshinda. 
Wageni waalikwa . 
Mhe. Dkt. Kolimba na Bw. Kurji wakiwatakia afya njema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Mtukufu Aga Khan wakati wa hafla hiyo. 
Dkt. Susan Kolimba akipokea maelezo kutoka kwa mtaalam aliyebuni mchoro waa Chuo Kikuu cha Aga Khan kitakachojengwa Jijini Arusha. 
Picha na Reginald Philip 
Mkurugenzi wa masuala ya kidiplomasia katika Taasisi ya Aga Khan, Balozi Arif Lalani pamoja na wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo wakimsikiliza Mhe. Kolimba (hayupo pichani) alipokuwa akiendelea kuzungumza kwenye maadhimisho hayo. 
Katibu wa Naibu Waziri, Bw. Adam Isara(Kulia) akifuatilia hotuba ya Mhe. Kolimba pamoja na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Hellen Mgeta. 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Ramla Khamis (wa pili kutoka kushoto), akiwa pamoja na Maafisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa hafla hiyo. 
Dkt. Kolimba akitambulishwa kwa wageni waalikwa na Bw. Kurji

GESI YA MAJUMBANI KUAGIZWA KWA PAMOJA.

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo wa pili kutoka kulia akiwa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) Michael Mjinja wa nne kutoka kulia pamoja na wadau wa gesi ya mitungi inayotumika majumbani (LPG) kutoka nchi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tatu wa Afrika 2016 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo anayeelezea jambo, akiwa pamoja na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) Michael Mjinja wakiwa katika maonesho ya gesi hiyo ya mitungi inayotumika majumbani (LPG)
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati) akiwa katika banda akipata maelezo kutoka kwa wadau wa LPG. Wengine katika picha ni Viongozi Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake.

Na Rhoda James

Imeelezwa kuwa kuanzia mwezi Septemba mwaka huu Serikali itaanza Uagizaji wa Pamoja wa Gesi inayotumika Majumbani (LPG).

Hayo yalielezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo mwazoni mwa wiki wakati akifungua Mkutano wa Tatu wa mwaka 2016 kuhusu masula ya Gesi ya Mitungi inayotumika majumbani kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, uliofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Dkt. Pallangyo alisema kuwa lengo la mkutano huo lilikuwa ni kupata uzoefu kutoka kwa nchi zilizoendelea na pia kuangalia namna ya kutatua changamoto zinazokabili sekta hiyo ikiwemo usambazaji, usalama na ujazaji wa mitungi hiyo.

Aliongeza kuwa, Uagizaji wa gesi hiyo ya mitungi (LPG) utafanywa kwa Pamoja lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa kodi ya serikali inakusanywa ipasavyo kutoka kwenye Sekta hiyo na kuhakikisha kuwa wafanyabiashara hao hawamiliki soko hilo.

“Bei ya gesi ya mitungi inayotumika majumbani ni ghali, upatikaniji wake ni mgumu na pia haipatikani kwa mitungi midogo zaidi ambayo kila mwananchi wa kawaida anaweza kumudu,” alisema Pallangyo

Aliongeza kuwa, nishati hiyo inaleta ushindani ukilinganishwa na mafuta ya taa, na kutolewa mfano kuwa mafuta ya taa yanapatikana kwa urahisi na kwa viwango tofauti ambavyo mwananchi wa kawaida anaweza kununua kulingana na uwezo wake tofauti na ambavyo gesi inapatika na kwenye maduka makubwa na kwa bei ya juu. Na kuongeza kuwa ni vema gesi hiyo ya mitungi (LPG) ikapatikana kwa viwango vya kununulika na kwa bei nafuu.

“Ni vema wafanyabiashara wakubwa wa gesi hii ya mitungi (LPG) wakashirikiana na wafanyabiashara wadogo ili kukabili changamoto zilizopo kwenye sekta hii. Pia waangalie wapi kuna fursa hasa upande wa Afrika,” alisema Pallangyo.

Aidha, Dkt. Pallangyo alisema kuwa gesi hiyo ni muhimu kutokana na fursa nyingi na usalama wake, kutokana na utafiti wa Shirika la Afya Dunia (WHO) uliofanywa kuwa ikiwa nusu ya watu duniani wataitumia gesi hii ya mitungi (LPG) wataokoa kiasi cha Dola za Marekani bilioni 900 kwa karne ijayo.

Pia, aliongeza kuwa utumiaji wa gesi hiyo ya mitungi imekua kwa kiasi kikubwa na kusema kuwa mwaka 2010 hadi 2011 tani 2,225 zilitumika ikilinganishwa na 2014 hadi 2015 tani 5,762 zilizotumika ongezeko ambalo ni kubwa.

Mkutano huo ulishirikisha washiriki kutoka nchi 33 mbalimbali wakiwemo waoneshaji (Exhibitors) kutoka sehemu mbalimbali duniani na ulifadhiliwa na kampuni za Oryx gesi na Hexagon Ragasco.

TAFF yaipongeza Serikali kwa juhudi za kupambana na Uharamia wa kazi za sanaa nchini

$
0
0
CHAMA cha Wasambazaji wa  Filamu Tanzania  na Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) vimepongeza hatua iliyochukuliwa na Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo kupitia waziri wake,Nape Nnauye katika kuhakikisha wanatokomeza waharamia na uuzaji wa kazi za wasanii bila kufuata utaratibu za kisheria zilizowekwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa chama cha wasambazaji wa filamu nchini,Moses Mwanyilu,alisema kuwa hatua ya serikali imekuja katika muda muafaka kufuatia kilio cha muda mrefu kutokana na baadhi ya wafanyabiashara na wasambaji wa filamu na muziki kutoka nje ya nchi wamekuwa wakiingiza na kuuza bidhaa hizo bila ya kufuata utaratibu ikiwemo kulipa kodi.

Amesema kuwa wafanyabiashara hao pia wamekuwa wakidurufu filamu za ndani ya nchi na kuziingiza sokoni bila ya wasanii kunifaika na kazi zao ikiwemo kazi hizo kutolipiwa kodi hivyo kupelekea kuziuza kwa bei ya chini ukilinganisha na filamu hapa nchini jambo ambalo linasababisha soko la filamu za ndani kudidimia.

Aidha Mwanyilu ameongeza kuwa  baada ya kilio cha muda mrefu hatimaye wameona jitihada za serikali kupitia kwa wizara inayohusika na masuala ya sanaa kuanza kuchukua hatua za makusudi kufanya oparesheni ya nguvu ya kukamata walanguzi wa kazi za wasanii nchini katika maeneo ya kariakoo.

Kwa niaba ya chama cha wasambazaji wa filamu na shirikisho la filamu Tanzania na vyama vyote vya shirikisho wanapenda kutoa shukrani za dhati kwa wizara ya habari kupitia waziri wake,Nape Nnauye kwa kushirikiana na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA),Bodi ya filamu,Cosota na Baraza la Sanaa Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kazi za wasanii nchini zinauzwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa na unaotambulika.

 Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF),Simon Mwakifamba,akizungumza na waandishi wa habari,Dar es Salaam,leo kuhusu kuipongeza serikali kupitia wizara husika katika kuanzisha oparesheni ya kuwakamata walanguzi wa kazi za wasanii nchini. Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Wasambazaji wa Filamu nchini,Moses Mwanyilu.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wasambazaji wa Filamu nchini,Moses Mwanyilu,akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano huo wa kwanza kulia ni Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini Bw. Simon Mwakifamba.
 Waandishi wa habari wakimsikiliza mwenyekiti wa chama cha wasambaji wa filamu nchini,Moses Mwanyilu (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kuhusu wizi wa ulanguzi wa kazi za wasanii nchini.
 Katibu wa Chama cha Wasambaji wa Filamu Tanzania,Suleiman Ling'ande wa katikati,akizungumza katika mkutano huo wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Wasambaza filamu Bw. Moses Mwanyilu.
 Muigizaji wa Filamu za Bongo Movie nchini,Kulwa Kikumba Al maarufu Dude wa pili kushoto ,akitoa ufafanuzi katika mkutano huo juu ya athari za uharamia wa kazi za wasanii mbele ya waandishi wa habari.
 Muanzilishi wa Mtandao wa Filamu Central,Myovela Mfwaisa,akiuliza swali katika mkutano huo.Habari/Picha Na Ally Daud-Maelezo.
Naye Katibu Mkuu wa chama cha Wasambaji wa Filamu Tanzania,Suleiman Ling’ande alisema kuwa tatizo la uharamia katika kazi za wasanii nchini ni changamoto ya muda mrefu kufuatia kuwepo na sheria ambayo imeshindwa kukidhi na kusimamia utaratibu unaofaa hasa katika kuhakikisha kazi za wasanii zinawanufaisha wasanii pamoja na kuliongezea kipato taifa pamoja na kulipa kodi.

Pia Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF),Simon Mwakifamba,amesema kuwa anaunga mkono zoezi linaloendelea kwa wadau wa kazi za wasanii cnhini wakishirikian na serikali katika kuhakikisha wanatokomeza uharamia wa kazi za wasanii wote nchini ili walau kuwapa motisha ya maisha mazuri waigizaji hao ili waendelee kutengeneza kazi nzuri za kuelimisha jamii.

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA-AfDB YAIPIGA JEKI TANZANIA DOLA MILIONI 200

$
0
0
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na  Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou, baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali kiasi cha shilingi 433.6bn.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (Kulia), akiwa katika picha ya pamoja  na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, Dkt. Alberic Kacou (kushoto), Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (wa pili kushoto) na Mwakilishi Mkazi wa AfDB, Tania Kandiero (wa tatu kushoto), baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn.Picha Zote na Wizara ya Fedha na Mipango
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb), akipeana mkono na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika -AfDB, Tania Kandiero, alipotembelea Makao Makuu ya Wizara hiyo Jijini Dar es salaam, kwa mazungumzo maalumu, akiwa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Alberic Kacou, ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (Kushoto), akimsikiliza kwa makini  Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Alberic Kacou (katikati) aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo nchini Tanzania, Tania Kandiero (kulia) ambapo Benki hiyo imeahidi kuchangia Mfuko Mkuu wa Bajeti wa serikali mwaka 2016/2017, kiasi cha shilingi 433.6bn. Aliyeketi kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb).

Na Benny Mwaipaja-WFM 

BENKI ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, imeahidi kuchangia Dola Milioni 200, sawa na Shilingi 433.6b, kwenye Mfuko wa Bajeti Kuu ya Serikali katika kipindi cha mwaka wa Fedha 2016/2017. 

Ahadi hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo anayeshughulikia Utawala na Rasilimali watu, Dkt. Alberic Kacou, alipomtembelea Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Ofisini Kwake Jijini Dar es salaam 

Makamu huyo wa Rais wa AfDB aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki hiyo, Tania Kandiero, amesema kuwa mchango huo umeongezeka kwa dola Milioni 50 ikilinganishwa na Bajeti ya mwaka jana ambapo Benki hiyo ilichangia Dola Milioni 150. "Misaada na mikopo inayotolewa na Benki yetu kwa serikali ya Tanzania imefikia Dola za Marekani 1.9b hivi sasa" Alieleza Dkt. Kacou 

Ameeleza kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza katika Bara la Afrika kupewa kiasi kikubwa cha fedha kutokana na mipango yake mahili ya maendeleo inayokidhi vigezo na viwango vya taasisi hiyo. "Tuna malengo matano ambapo tunataka kuwekeza katika sekta ya nishati, uzalishaji wa chakula, kuiendeleza kiviwanda, kuiunganisha na kuboresha maisha ya waafrika kwa ujumla" aliongeza Dkt. Kacou 

Amepongeza jitihada zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, kwa kusimamia vizuri nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na kwamba uamuzi huo utaharakisha maendeleo ya nchi. Akizungumza na ujumbe huo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ameshukuru uamuzi wa Benki hiyo wa kuongeza mchango wake katika Bajeti Kuu ya serikali kupitia mfuko mkuu wa Bajeti (GBS). 

Amesema kuwa serikali imedhamiria kutekeleza mipango yake ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge), pamoja na kununua ngege tatu za abiria ili kuboresha usafiri wa anga. 

"Vilevile tumeamua katika Bajeti ya mwaka huu kununua meli mpya itakayo tumika kutoa huduma Ziwa Viktoria na kukarabati meli nyingine mbili ambapo moja iko Ziwa Tanganyika na nyingine Ziwa Viktoria ili kuimarisha usafiri wa majini" Aliongeza Dkt. Mpango 

Dkt. Mpango amebainisha kuwa katika kutekeleza Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo, serikali imejipanga kukuza sekta ya viwanda ili kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. "Mpango huo utakwenda sambamba na kuboresha sekta ya kilimo ili malighafi itakayozalishwa na wakulima, licha ya kuinua uchumi wa wakulima wetu, lakini pia viwanda vitapata malighafi ya kutosha" alisisitiza Dkt. Mpango 

Amerejea msimamo wa serikali kuwa haitakubali kupokea misaada inayoambatana na masharti magumu na isiyo na tija kwa nchi na kwamba jitihada zinazofanyika hivi sasa ni kuhakikisha kuwa rasilimali zilizopo nchini zinawekezwa kwa utaratibu mzuri ili ziweze kutumika kuleta maendeleo. 

"Hatutakubali misaada isiyozingatia vipaumbele vyetu na ile inayohatarisha uhuru wetu wa kujiamulia mambo yetu wenyewe" alieleza Dkt. Mpango.Ameeleza kuwa uamuzi wa serikali wa kukusanya mapato yake ya ndani kwa kuwahimiza watu kulipa kodi na kubana matumizi yasiyo ya lazima umeanza kuleta matunda na kuongeza pia nidhamu ya matumizi ya pesa katika jamii. 

Ameiahidi Benki hiyo ya maendeleo ya Afrika-AfDB, kwamba fedha waliazoahidi kuzitoa zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba awaagiza JKU kuanzisha kilimo mbadala badala ya kutegemea mpunga

$
0
0



Na Masanja Mabula –Pemba 

MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman amewaagiza wapiganaji wa Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) kanda ya Pemba kuanzisha kilimo mbadala ili kujiongezea kipato na kuacha kutegemea kilimo cha zao la mpunga pekee . 

Alisema , ni vyema jeshi hilo kujikita katika kilimo cha mboga mboga na matunda , ikiwemo matikiti na pili pili boga bidhaa ambazo zinavunwa kwa muda mfupi na soko lake linapatikana ndani ya Kisiwa cha Pemba .
Kauli hiyo ameitoa wakati akizindua zoezi la uvunaji wa mpunga kwenye bonde la Shinyanga katika Kambi ya JKU Msaani , na kuwataka maafisa kilimo wa Jeshi hilo kuhakikisha wanatenga maeneo kwa ajili ya kilimo cha mboga mboga na matunda. 

“Kilimo cha matikiti kinastawi vyema katika ardhi ya Pemba , na soko lake lipo kwani wanaozalisha kwa sasa hawajaweza kulitosheleza soko kutokana na kuwepo na watumiaji wa wengi ”alieleza. 

“Wapo wakulima wa matikiti wanayozalisha kwa wingi hapa Kisiwani Pemba , lakini bado hawajaweza kulimudu soko la bidhaa hiyo , hi
Akizungumzia zoezi la uvunaji wa mpunga , alisema uongozi wa JKU unapaswa kuandaa utaratibu maalumu ambao utawezesha kumaliza kwa wakati uvunaji ili zao hilo lisiharibiwe na mvua ambazo zinanyesha kwa baadhi ya maeneo ya kisiwa cha Pemba . 

Mapema Afisa Mdhamini Wizara ya Nchi , Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa , Juma Nyasa alisema zoezi la uvunaji wa mpunga katika bonde hilo linafanyika kwa kanda ya Pemba . Alisema kunahitajika nguvu za pamoja kati ya Serikali na taasisi zake na binafsi katika kufanikisha zoezi hilo , ambapo aliitaka Serikali ya Mkoa kuongeza nguvu kwa kupeleka nguvu kazi kuokoa zao hilo . 

“Nguvu za pamoja zinahitajika ili kufaniakisha zoezi la uvunaji kukamilika kwa wakati , hivyo tunaiomba Serikali ya Mkoa kuongeza nguvu kazi kuokoa zao hili ”alifahamisha Nyasa . Bwana Shamba wa Jeshi la Kujenga Uchumi kanda wa Pemba Kapeni Said Abdalla alisema , bado katika mabonde yanayotumiwa na Jeshi hilo kwa ajili ya kilimo yanategemea mvua ambazo kwa msimu huu zilikuwa haba .

MH. LUHAGA MPINA ATEMBELEA KIWANDA CHA PEPSI

$
0
0
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Luhaga Mpina (Kulia) akifurahia Jambo na Meneja Mahusiano wa kiwanda cha Pepsi bw,Alexander Nyirenda alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Kiwalani Temeke Jijini Dar es salaaam mapema hii leo.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh.Luhaga Mpina akiwa ameambatana na Maafisa wa Mazingira kutoka Baraza la Usimamizi wa Mazingira Nchini( NEMC)akikagua mfereji unaotiririsha maji machafu kutoka katika kiwanda hicho na kusababisha madhara kwa wanainchi wanaozunguka eneo hilo.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mh,Luhaga Mpina akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kufanya ziara katika kiwanda cha Pepsi kilichopo Kiwalani,Temeke jijini dar es salaam

BARABARA YA NJOMBE-MAKETE KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI

$
0
0


Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (mbele) akitoka kukagua eneo lililoathirika na mmomonyoko wa ardhi eneo la Lukumburu Mkoani Njombe. 
Muonekano wa barabara ya Njombe–Makete yenye urefu wa KM 109.4 inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami. 

Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiongea na wakazi wa kijiji cha Usalule, Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe alipotembelea kukagua ujenzi wa barabara ya Njombe–Makete yenye urefu wa KM 109.4 inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.

Wakazi wa Kijiji cha Usalule, Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe wakimsikiliza Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipotoa taarifa ujenzi wa barabara ya Njombe–Makete yenye urefu wa KM 109.4 inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.

Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto) akisalimiana na Wakazi wa kijiji cha Usalule, Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe mara baada ya kutoa taarifa ya ujenzi wa barabara ya Njombe–Makete yenye urefu wa KM 109.4 inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.


Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akimbeba mtoto aliyehudhuria kikao cha Wakazi wa Kijiji cha Usalule, Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe mara baada ya kutoa taarifa ya ujenzi wa barabara ya Njombe–Makete yenye urefu wa KM 109.4 inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akicheza na wakazi wa Kijiji cha Usalule, Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe waliokuwa na furaha mara baada ya kupewa taarifa ya ujenzi wa barabara ya Njombe–Makete yenye urefu wa KM 109.4 inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
Meneja wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Mkoa wa Iringa Bi. Elikael Manase akitoa maelezo kwa Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu athari ya mmomonyoko wa ardhi unavyoathiri sehemu ambayo Mkongo wa Taifa umepita eneo la Lukumburu Mkoani Njombe. 

Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiongea na wafanyakazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo wakati alipotembelea kuangalia utendaji kazi, Mkoani Njombe. Wafanyakazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakimsikiliza Waziri Profesa Makame Mbarawa wakati alipotembelea kuangalia utendaji kazi, Mkoani Njombe.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

……………………………………………………………………………………………

Serikali imesema ipo katika hatua za mwisho kuanza ujenzi wa barabara ya Njombe-Makete kwa kiwango cha lami yenye urefu wa KM 109.4 inayounganisha mikoa ya Mbeya na Njombe ili kurahisisha huduma ya usafiri wa barabara kwa wakazi wa mikoa hiyo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema hayo mkoani Njombe wakati akiongea na wakazi wa kijiji cha Usalule, kata ya Ulembwe, wilaya ya Wanging’ombe mara baada ya kukagua barabara hiyo.Profesa Mbarawa amesema kuwa Serikali kwa kutambua umuhimu wa barabara hiyo imetenga kiasi cha sh.bilioni 19 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

“Tumejipanga na tuna nia dhabiti kuhakikisha barabara hii tutaijenga kwa kiwango cha lami na katika kuharakisha kazi hii tutatafuta makandarasi wawili ili ujenzi huu ukamilike kwa haraka”, amesema Prof. Mbarawa.Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amewataka wananchi kushirikiana na Makandarasi watakapoanza ujenzi huo ili kazi hiyo iweze kukamilika kwa wakati na kulete tija kwa wananchi wa Mikoa ya kanda ya kati.

Amesema kuwa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mkoa wa Njombe upo katika hatua za kutangaza zabuni ili kupata Makandarasi wenye uwezo wa kujenga barabara hiyo kwa kuzingatia viwango kulingana na mkataba.Naye Meneja wa TANROADS Mkoa wa Njombe Eng. Yusuph Mazana amesema kuwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Njombe-Makaete yenye urefu wa KM 109.4 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami umekamilika na Mhandisi mshauri M/s Crown Teach Consult Ltd ameshawasilisha taarifa ya usanifu wa kina.

“Tumepokea taarifa ya usanifu wa kina kutoka kwa Mhandisi Mshauri hivyo tunahaidi kusimamia utekelezaji wa mradi huu kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi wa mkoa wa Njombe na mikoa jirani”,amesisitiza Eng. Mazana.Waziri Prof. Mbarawa ameendelea na ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara hiyo Mkoani Njombe.

KATIBU MTENDAJI WA BARAZA LA UWEZESHAJI BENG'I AFUNGA MAHAFALI YA WAJASIRIAMALI WA MRADI WA MKUBWA

$
0
0

Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi pamoja wakati wa hafla hiyo ya kuhitimu mafunzo jijini Dar es Salaam leo.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akisalimiana na mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Mwenyekiti TGT, Epeineto Toroka na Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.

atibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akizungumza jambo na mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Wanawake wajasiriamali, Jane Baseka aliyenufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akizungumza jambo na mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akisalimiana na mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), Deborah Kiunsi alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Mwenyekiti TGT, Epeineto Toroka.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), Deborah Kiunsi alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Pamoja naye ni Mwenyekiti TGT, Epeineto Toroka na Naibu Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania, Hinke Nauta.



Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kulia ni Meneja Mradi wa MKUBWA, Wanke Kinyau.










Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimpongeza mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kumkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo. Kulia ni Mwenyekiti wa TGT, Epeineto Toroka







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya TGT, Olive Luena.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya TGT, Olive Luena.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya TGT, Olive Luena.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akimkabidhi cheti mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuhitimu mafunzo hayo. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya TGT, Olive Luena.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakishangilia baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakishangilia baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.










Wanawake wajasiriamali wakifurahi na Meneja Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), Wanke Kinyau (mwenye zawadi) baada ya kumkabidhi wakati wa mahafali yao kwenye maonesho ya bidhaa zao, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT) .







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi baada ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi pamoja na Meneja Mradi Wanke Kinyau walipomkabidhi zawadi wakati wa hafla hiyo ya kuhitimu mafunzo hayo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi pamoja na Meneja Mradi Wanke Kinyau walipomkabidhi zawadi wakati wa hafla hiyo ya kuhitimu mafunzo.







Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi pamoja na Meneja Mradi Wanke Kinyau wakati wa kumpa zawadi katika hafla hiyo ya kuhitimu mafunzo.







Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa, Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya TGT, Olive Luena na Mmoja wa wageni Jane Kelly wakifuarahia pamoja na Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), baada ya kuwakabidhi vyeti vya kuhitimu mafunzo hayo.

Mwenyekiti TGT, Epeineto Toroka akimshukuru mgeni Rasmi baada ya kukamilisha zoezi la kukabidhi vyeti wahitimu wa mafunzo hayo. Kulia ni Naibu Balozi wa Uholanzi Nchini Tanzania, Hinke Nauta.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akiwa katika picha ya pamoja na Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA).

Mmoja wa wageni Jane Kelly (wa tano kushoto) akiwa katika picha pamoja na Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA).

Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya TGT, Olive Luena akiohojiwa na waandishi wa habari.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akiwa katika picha ya pamoja na Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA). (Imeandaliwa na Robert Okanda blogspot)

Baadhi ya Waandaaji wa Filamu zilizokamatwa waanzaa kujisalisalimisha Bodi ya Filamu nchini

$
0
0

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo akiangalia Poster ya Filamu ya Mapenzi Uchizi iliyowasilishwa kwa ajili ya uhakiki na kubainika kuwa ni moja kati ya Filamu iliyotangazwa kuingia sokoni ikiwa na alama ya uhakiki kutoka Bodi ya Filamu Tanzania wakati bado haijahakikiwa leo jijini Dar es Salaam
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo akisikiliza utetezi kutoka kwa jambo wakati wa mahojiano na muandaaji wa Filamu ya Mapenzi Uchizi Bw. Akim Igembe (kushoto) kutoka Kampuni ya Akim Master Film, baada ya kubainika kuwa ni moja kati ya Filamu zilizokamatwa wakati wa Operesheni maalum kutokana na kutangazwa kuingia sokoni ikiwa na alama ya uhakiki kutoka Bodi ya Filamu Tanzania wakati bado haijahakikiwa leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Afisa Utamaduni kutoka Bodi ya Filamu Wilhad Tairo.

……………………………………………………………………….

Na: Frank Shija,MAELEZO

Baadhi ya waaandaaji wa Filamu nchini waanza kujisalimisha Bodi ya Filamu Tanzania baada ya Filamu zao kukamatwa zikiwa sokoni wakati hazijafanyiwa uhakiki na Bodi hiyo.

Haya yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo alipokuwa akifanya mahojiano na mmoja wa waandaaji wa Filamu nchini aliyekutwa na kadhia hiyo Bw. Akim Igembe kutoka Kampuni ya Akim Master Film baada ya Filamu yake ijulikanayo kwa jina la “Mapenzi Uchizi” bango lake lilikutwa sokoni likiwa na alama ya Uhakiki kutoka Bodi ya Filamu wakati ilikuwa bado haijahakikiwa na Bodi hiyo.

Operesheni ya kukamata Filamu zilizoingizwa sokoni kinyume cha sheria ambayo ilimshirikisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye ki ukweli imekuwa ya mafanikio sana maana sasa wameanza kujileta wenyewe.”Alisema Fissoo

“Wakati tunapitia fomu ya Uhakiki wa Filamu hii tulibaini kuwa ni moja kati ya kazi tulizozikamata kutokana na kuwa na alama ya uhakiki bila kupitia kwetu, tena ikiwa na daraja 18 wakati katika daraja hali la filamu hiyo inapaswa kuwa ni daraja 16”. Alisema Fissoo.

Awali akitoa utetezi wake mbele ya watendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, muandaaji wa Filamu ya Mapenzi Uchizi Bw. Akim Igembe kutoka Akim Master Film amesema pamoja na kuwa ndiye mmiliki wa Filamu hiyo, ahusiki moja kwa moja na mabango yaliyokutwa sokoni ya kiitangaza filamu hiyo kwani bado ndiyo alikuwa anafuatilia kibali kutoka Bodi ya Filamu.

Nakuongeza kuwa ata yeye mwenyewe anashangaa kuona mabango yanayoitangaza Filamu hiyo ili hali alikuwa bado haijafanyiwa uhakiki na Bodi ya Filamu na kwanza ndiyo alikuwa anafuatilia kibali.

Ata hivyo alieleza kuwa Master ya Filamu hiyo aliiuza kwa mfanyabiara mmoja kutoka nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo aliyemtaja kwa jina la Baraka Sunzu uende ndeye aliyehusikana na udanganyifu huo.

Akihitimisha mahojiano na mtuhumiwa huyo Katibu huyo amesema ofisi yake imeamua kuchukua uamuzi wa kuzuia Kibali cha Filamu hiyo hadi hapo atakapopatikana mfanyabiashara Raia wa Congo, Baraka Sunzu anayedaiwa kuuziwa kazi hiyo na kudurufu atakapo patikana kutoa maelezo ya wapi alipata nembo hiyo ambayo imetumika kinyume cha sheria na watakapojiridhisha hatua stahiki zitachukuliwa.

Fedha za Mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kutolewa baada ya uhakiki wa wanafunzi hewa

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako ameeleza kuwa fedha kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo zitatolewa mara baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki wa wanafunzi waliombewa fedha hizo toka vyuo mbalimbali hapa nchini.

Prof. Ndalichako aliyasema hayo leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya ucheleweshwaji wa fedha hizo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.

“Kuna zaidi ya wanafunzi 2,736 hewa ambao majina yao yamewasilishwa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kwa ajili ya kulipwa fedha za mafunzo kwa vitendo, yakiwemo majina ya wanafunzi waliofariki na waliofukuzwa chuo,” alifafanua Prof. Ndalichako.

Aliendelea kwa kusema kuwa, kuna chuo ambacho kilituma ripoti ya wanafunzi waliofukuzwa chuo mwaka 2013/2014 lakini majina hayo yametumwa tena kwa ajili ya kupewa fedha za mafunzo kwa vitendo kwa mwaka huu.

Kutokana na kasoro zilizojitokeza katika majina ya wanafunzi wanaotakiwa kupewa fedha kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo Prof. Ndalichako amesema kuwa Serikali haitatoa fedha mpaka uhakiki wa wanafunzi wanaotakiwa kupata fedha hizo utakapo kamilika kwa vyuo vyote nchini.

Aidha, Mhe. Ndalichako amesema kuwa majina ya wanafunzi hao hewa yamewekwa katika mitandao wakitakiwa kujihakiki TCU ili kujiridhisha kama kweli ni wanafunzi na wanaendelea na masomo.

Vile vile, Prof. Ndalichako amevitaka vyuo vikuu kutoa ushirikiano kwa timu zilizotumwa katika vyuo vyao kufanya uhakiki wa wanafunzi wanaotakiwa kupata fedha hizo kwani kuna baadhi ya vyuo vimekuwa havitoi ushirikiano kwa kisingizio cha kuwepo kwenye mitihani.

Aliongeza kwa kusema kuwa, vyuo kutotoa ushirikiano kwa timu zilizotumwa kufanya uhakiki wa wanafunzi hao kutazidi kuchelewesha fedha hizo kutoka mapema.

MHE. MAJALIWA AAGIZA MAUZO YA VITALU VYA UVUNAJI WA MITI YAFANYIKE KWA NJIA YA MNADA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watumishi wa Wazara ya Maliasili na Utalii (hawapo pichani) kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha LAPF, Kijitonyama jijini Dar es salaam Julai 18, 2016 .

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kubadilisha mfumo wa uvunaji wa vitatlu vya miti kwenye mashamba ya Serikali ili kuweka uwazi kwenye biashara hiyo na kuipatia zaidi Serikali mapato.

Mhe. Majaliwa alisema hayo jana kwenye Mkutano na Viongozi pamoja na Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga uliopo Kijitonayama Jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Mhe. Majaliwa alisema kuwa utaratibu uliokuwa ukitumika hapo awali wa kuuza miti kwenye mashamba ya Serikali kwa njia ya vibali hauna tija kwakuwa umekuwa ukiikosesha Serikali mapato na kuwanufaisha wafanyabiashara wachache.

“Utaratibu wa sasa wa kutumia vibali unatuletea migongano ndani ya Wizara na kuikosesha Serikali mapato, hivyo ni lazima tuubadilishe” Aliongeza Majaliwa. Aliuagiza Uongozi wa Wizara kufanya marekebisho kwenye utaratibu huo na kuweka utaratibu wa mnada ili kuweka uwazi zaidi na kuondoa manung’uniko kwenye biashara hiyo. “vibali visitishwe, mnada uanze kama inavyofanyika kwenye mitiki” Alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Hivi karibuni Mhe. Majaliwa alisitisha utoaji wa vibali vya uvunaji wa miti kwenye mashamba matano yanayomilikiwa na Serikali kutokana na kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Majaliwa aliagiza mabadiliko ya haraka katika vizuizi vya ukaguzi wa Maliasili ambavyo amesema vimekuwa havina tija na kuagiza baadhi yake vifutwe kabisa. Miongoni vya vizuizi alivyoagiza vifutwe ni Kibaha Stendi, Kimanzichana na Mbagala, pia aliagiza kuimarishwa kwa kituo cha Vikindu, Kibiti na Vigwaza.

Mhe. Majaliwa aliwaagiza wataalamu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kushirikiana na Tamisemi kwa ajili ya kuweka mfumo mzuri wa kuhifadhi na kuvuna mazao ya misitu yaliyopo katika Halmashauri na kutenga Misitu ya Asili tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo kumekuwepo muingiliano katika kutekeleza majukumu hayo jambo linalopelekea uharibifu wa misitu.

Hapo awali Mhe. Majaliwa alieleza lengo kuu la Mkutano huo kuwa ni katika utaratibu wake wa kawaida aliojiwekea wa kutembelea Wizara na kuzungumza na watumishi kwa ajili kukumbushana majukumu yao, kuangalia changamoto mbalimbali na kuzitafutia ufumbuzi. Aliwaasa watumishi wa Wizara ya Maliasili kuwa wazalendo, waadilifu, waaminifu na kuongeza uwajibikaji ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake ya kuwahudumia vizuri wananchi.

“Ninyi ni watu muhimu sana katika utoaji wa huduma kwa wananchi, tekelezeni majukumu yenu kwa uadilifu wa hali ya juu. Kamilisheni malengo yenu kulingana na mpangokazi wenu mliojiwekea” Alisema Mhe. Majaliwa.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe alisisitiza watumishi wa Wizara hiyo kuhakikisha kuwa wanalinda misitu kule iliko na sio kusubiri katika vituo na kukamata rasilimali zake ambazo zimevunwa isivyo halali na kuzitoza faini, kinyume chake rasilimali hizo zilipiwe kihalali kabla ya kuvunwa. Aliahidi pia kuisuka upya Idara ya Misitu.

kampuni ya chemcotex yatimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwake,yawazawadia wateja wake kwa kutoa gari

$
0
0



Gari lililoandaliwa na kampuni ya chem&cotex inayotengeneza na kusambaza dawa ya meno ya whitedent ambayo itashindaniwa na watumiaji wa dawa hiyo kwa kubuni idadi ya dawa zilizondani ya gari hiyo ikiwa ni katika kusherehekea miaka 25 ya dawa ya whitedent. 
Katika kusherehekea miaka 25 tangu kuanzishwa kwa dawa ya meno ya whitedent kampuni ya chem&cotex imeamua kuwazawadia wateja wake kwa kutoa gari itakayoshindaniwa kwa wateja hao kujaza idadi ya dawaza meno zilizo ndani ya gari hiyo, kampeni iliyozinduliwa mkoani morogoro.

Mgeni rasmi katibu tarafa wa manispaa ya morogoro Pakalapakala Mlenge akiongea na akiongea na wakazi wa morogoro waliojitokeza katika hafla ya kusherehekea miaka 25 ya dawa ya meno ya whitedent.
Wanyakazi wa kampuni ya chem&cotex inayotengeneza na kusambaza dawa ya meno ya white dent wakiwa katika picha ya pamoja na katibu tarafa manispaa ya morogoro Pakalapakala Mlengekatika hafla ya kusherekea miaka 25 ya dawa hiyo iliyokwenda sambasa na uzinduzi wa bahati na sibu ya kushinda gari kwa wateja kutaja idadi ya dawa zilizo ndani ya gari hiyo.
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live


Latest Images