Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46360 articles
Browse latest View live

WAAJILI WAASWA KUWASILISHA MICHANGO YA WAFANYAKAZI WAO KATIKA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII.

$
0
0
WAAJIRI waaswa kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao katika mifuko Hifadhi ya jamii hapa nchini kwa wakati.

 Hayo yamesemwa na Kamishna wa kazi wa Wizara ya Ofisi ya Waziri  Mkuu, Sera, Bunge,Vijana, Kazi, Ajira na Walemavu, Hilda Kabisa wakati akizungumza na wanachama wa chama cha waajiri Tanzania jijini Dar es Salaam leo kwenye mkutano wa Mwaka wa Chama cha waajiri Tanzania. 

Amesema kuwa waajiri wengi huwa hawana tabia ya kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini.

Nae Mkurugenzi mtendaji wa Chama cha waajiri Tanzania(ATE), Agrey Mulimuka amewaasa waajili kuachana na uwakala wa Rushwa katika nafasi zao wakati wanaajili wafanyakazi katika sehemu zao za kazi.
Pia amesema kuwa waajili waajili wafanyakazi wenye kibali cha ukazi na kuwa na mabadili katika sehemu zao za kazi.
Kamishna wa kazi wa Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Vijana, Kazi, Ajira na Walemavu, Hilda Kabisa akizungumza kwa niaba ya Wizara wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Vijana, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenister Mhagama jijini Dar es Salaam leo wakati wa mkutano wa mwaka wa chama cha waajiri Tanzani (ATE) jijini Dar es Salaam leo.
 Mwenyekiti wa chama cha waajiri Tanzania, Almas Maige na Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini akizungumza katika Mkutano wa mwaka wa chama cha waajili Tanzania jijini Dar es Salaam leo. 
Baadhi ya wadau na wa chama cha waajiri Tanzania(ATE) wakisikiliza katika mkutano huo jijini Dar es Salaam leo.
 Mratibu wa Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP), Annamaria Kiaga akizungumza katika mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Waajiri Tanzania(ATE) jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya Viongozi wa chama cha waajiri Tanzania(ATE) wakiwa katika mkutano  uliofanyaka jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wadau na wa chama cha waajiri Tanzania(ATE) wakisikiliza katika mkutano huo jijini Dar es Salaam leo.

Mchezaji Thomas Ulimwengu amtembelea Mdau wa soka nchini Shaaban Tippo jijini Dar leo.

$
0
0

Mchezaji wa Kimataifa kutoka nchini Tanzania ambaye kwa sasa anaichezea timu ya TP Mazembe ya nchini Kongo-DRC,Thomas Ulimwengu mapema leo akiwa katika picha ya pamoja na Mdau mkubwa wa Soka hapa nchini (pichani shoto),Othman Shaaban Tippo a.k.a Zizzou.Mchezaji huyo Mshambuliaji wa TP Mazembe amemtembelea mdau huyo anaemiliki duka la vifaa vya michezo lililopo maeneno ya Bamaga,Sinza jijini Dar na kumjulia hali,Ulimwengu amemshukuru na kumtakia afya njema na heri  Mdau Tippo katika shughuli zake mbalimbali,Tippo amempatia vifaa kadhaa vya michezo mchezo huyo Thomas Ulimwengu.

Benki ya TIB yaendesha mafunzo ya bure ya ujasiriamali Sabasaba

$
0
0
Benki ya TIB kwa kushirikiana na Taasisi ya Ujasiriamali na Uongozi wa Biashara (IMED) wanaendesha mafunzo ya bure ya ujasiriamali katika banda la TIB lilipo katika viwanja vya Sabasaba.

Mafunzo hayo pia yanajumuisha elimu katika maeneo ya uongozi na sheria za biashara, masoko, utawala wa fedha pamoja na utawala wa biashara yanalenga wajasiriamali wadogo wadogo na wa kati ili kuwajengea uwezo wa kukuza biashara zao.

Akizungumzia mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB, bwana Charles Singili, alisema wameamua kutoa mafunzo hayo katika msimu huu wa Sabasaba ili kuwafikia wafanyabiashara wengi zaidi pamoja na wananchi wa kawaida.

‘Mafunzo haya ni bure, na yanafanyika katika banda letu la TIB hapa Sabasaba na wananchi wote wanakaribishwa kuja kujifunza ili waweze kuendesha biashara zao kwa faida na mafanikio’ alisema bwana Singili.

Mafunzo hayo ambayo yamejikita katika kuwapa wafanyabiashara mbinu za kuendesha miradi yao pamoja na kutumia vizuri mikopo inayotolewa na benki hiyo yanafanyika kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana, na yataendelea hadi tarehe 4 ya mwezi Julai.

‘Kimsingi mafunzo haya yanaendana na dhima ya mwaka huu ya maonyesho ya Sabasaba, Kuunganisha Uzalishaji na  Masoko, na hivyo kwa elimu tutakayowapa wajasiriamali tunaamini wataweza kupanua wigo wa masoko ya biashara zao’ alimaliza bwana Singili.

Naye mmoja wa wanufaika wa elimu hiyo, daktari Bayoum Awadh,kutoka kampuni ya Emergent Africa, aliipongeza benki ya TIB kwa kutoa mafunzo hayo kwani yatazidi kuwaongezea elimu na uzoefu zaidi wa kuendesha biashara zao.

‘Naishukuru sana benki ya TIB kwa kuendesha mafunzo haya, na nawaomba wajasiriamali wenzangu wajitokeze kwa wingi kujipatia elimu hii kwani itawasaidia sana kuendesha biashara zao kwa faida’ alisema daktari Bayoum Awadh.

 Mkufunzi wa Mafunzo ya Ujasiriamali  yanayoendeshwa na benki ya TIB katika viwanja vya Sabasaba, Louis Mkuku, akitoa mafunzo kwa baadhi ya wahudhuriaji wa semina hizo zinazoendelea katika viwanja vya Sabasaba.
 Baadhi ya wafanyabiashara wakifatilia mafunzo ya uajasiriamali yanayoendeshwa na benki ya TIB katika viwanja Sabasaba.

Rais Dkt Magufuli Awataki wakuu wa Wilaya na mikoa kuchapa kazi.

$
0
0

Na Daudi Manongi,MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli amewataka wakuu wa wilaya na mikoa kuchapa kazi kwa bidii kwani viongozi hao ndio wawakilishi wa wananchi wa vijijini.

Mhe.Rais Magufuli ameyasema hayo alipokuwa akizungumza wakati wakuu wa wilaya na mikoa walipokuwa Ikulu wakila kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa mikoa yao.

Rais Magufuli pia amewataka viongozi hao kufanya kazi na kutimiza majukumu yao kwani wananchi wana changamoto nyingi,na wao waende kutatua matatizo ya wananchi walio maskini.

Aidha amewataka viongozi hao kutokuwa chanzo cha kutengeneza matatizo katika jamii na hivyo wasimamie haki na ukweli,wasiwe wala rushwa,wazingatie maadili na kuwatumikia wananchi wote bila kujali itikadi za vyama zao,dini au kabila uku akiwataka kutekeleza waliyohaidi kwenye ilani ya chama cha mapinduzi.

Pia amewataka viongozi hao kuweke mkazo katika kutatua kero za wananchi na kuwataka kutimiza kwa vitendo kwa kushirikiana na viongozi watakaowakuta katika maeneo yao waliyopangiwa.

Hata hivyo amewataka viongozi hao kusimamia mapato ya Serikali katika miradi yote kwenye maeneo yao ili kuhakikisha serikali inapata kodi ambayo itasaidia katika maendeleo ya Taifa hili.

DKT. NDUGULILE ATAKA MABUNGE KUSHIRIKISHWA KWENYE MPANGO WA “AFYA MOJA” (ONE HEALTH)

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Kigamboni (CCM) Dkt Faustine Ndugulile(Mb) ameyataka Mataifa kushirikisha Mabunge katika kufanikisha mpango wa Usalama wa Afya Duniani (Global Health Security Agenda).

Akizungumza kwenye mkutano wa masuala ya Usalama wa Afya ulioandaliwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na kufanyika Jijini Bali, Indonesia,, Dkt Ndugulile alisema, “Mabunge yanaweza kutoa mchango mkubwa sana kwenye utekelezaji wa Mpango wa Usalama wa Afya Duniani kwa kusimamia Serikali na kuhakikisha hatua zote muhimu zinatekelezwa; kutunga Sheria zitakazosimamia utekelezaji wa mpango huu pamoja na kuhakikisha mpango huu unapata fedha za kutosha kutoka kwenye Bajeti ya Serikali”.

Dkt Ndugulile alisema kuwa muingiliano wa shughuli za kilimo, mifugo na shughuli nyingine za kibinadamu zimesababisha baadhi ya magonjwa ya wanyama kuleta athari kwa binadamu na pia usugu wa madawa ya aina ya antibiotiki. Hivyo, kuna haja ya wadau wa sekta hizi kuwa na ushirikiano wa karibu chini ya mpango wa “Afya Moja” (One Health).

Mbunge wa Jimbo la Kigamboni (CCM) Dkt Faustine Ndugulile (Mb) (kulia), akizungumza kwenye mkutano wa masuala ya Usalama wa Afya ulioandaliwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na kufanyika Jijini Bali, Indonesia.

Alisema kuwaIli mpango wa “Afya Moja” ufanikiwe in lazima maboresho yafanyike kwenye uratibu wa sekta mbalimbali ndani ya nchi na pia kuandaa mpango wa pamoja wa udhibiti na kushughulikia majanga.

Dkt Ndugulile aliyasema hayo kwenye mkutano wa Mpango wa Usalama wa Afya Duniani unaofanyika mjini Bali, Indonesia. Mkutano huu ulioanza tarehe 27 Juni unatarajia kuisha tarehe 30 Juni.

Dkt Ndugulile mbali ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Mabunge Duniani (Inter Parliamentary Union) kuhusiana na masuala ya UKIMWI, Afya ya Wanawake, Vijana na Watoto.

Makamu wa Rais awataka wakuu wa wilaya na mikoa kukamilisha zoezi la madawati kabla ya June 30.

$
0
0
Na Daudi Manongi,MAELEZO

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu amewataka wakuu wa wilaya na mikoa kuhakikisha wanamaliza zoezi la upatikanaji wa madawati kwa shule za msingi na sekondari.

Mhe. Suluhu ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati wakuu wa wilaya na mikoa walipokuwa Ikulu wakila kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu wa mikoa yao.

Aidha amewaagiza viongozi hao kusoma alama za nyakati kwa kuangalia makosa ya waliokuwepo kabla yao ili kuhakikisha hawarudii makosa yaleyale.

Mhe.Suluhu pia amesema kuwa Serikali haitaki kusikia wananchi wanalia njaa na hivyo wakuu wa wilaya wahakikishe chakula kinapatikana katika maeneo yao kwani hilo ni jukumu lao.

Aliongeza kuwa wakuu wa wilaya wana majukumu makubwa ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma zote za muhimu katika maeneo yao kwani wananchi wana mategemeo makubwa juu yao.

Aidha ameagiza wakuu wa Wilaya hao kufanya kazi karibu na Maafisa Tarafa ili kujua kero za wananchi na kuzifanyia kazi kwa kasi ili wananchi wafaidike na maendeleo yawafikie kwa haraka.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene ivi karibuni aliwaagiza wakua wa wilaya na mikoa kuhakikisha wanatimiza agizo la Rais John Pombe Magufuli kuhakikisha hakuna mwanafunzi atakayekaa chini kwa uhaba wa madawati kufikia June 30,2016.

TRA yakutanisha wadau wa kodi kujadili uanzishwaji wa chombo cha kuratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi

$
0
0
.
Katika kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya walipa kodi na wakusanyaji wa kodi, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imefanya kongamano la pamoja na wadau wa kodi nchini likiwa na lengo la kujadili kwa pamoja kuhusu uanzishwaji wa chombo cha kuratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kamishna wa Sera na Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Shogholo Msangi alisema wamekutanisha wadau hao wa kodi ili waweze kutoa maoni na kukubaliana kwa pamoja jinsi gani chombo hicho kitaweza kufanya kazi.

"Kutakuwa na chombo ambacho kitakuwa kinaratibu na kusimamia wanataaluma wa kodi na lengo ni kupitia kongamano hilo wadau wa kodi wataweza kukubaliana kwa pamoja kuona ni jinsi gani chombo hicho kitafanya kazi,
Kamishna wa Sera na Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Shogholo Msangi akitoa neno la ufunguzi katika kongamano lililoandaliwa na TRA na kukutanisha wadau mbalimbali wa kodi. (Picha zote na Rabi Hume - MO Blog)

"Unaweza kukuta kuwa mlipa kodi kwa sasa ndiyo anaumia au TRA ndiyo inaumia lakini chombo hicho kitaweza kusimamia na kuweka kila jambo sehemu sahihi kama linavyotakiwa kuwapo," alisema Msangi.

Nae Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Kodi (ITA), Prof. Isaya Jairo alisema kuwa chombo hicho kama kikianzishwa kitaweza kufanya kazi zake kwa uhuru bila kuingiliwa na TRA ili kuhakikisha kuwa kinatoa na haki kati ya mlipa kodi na wakusanyaji wa kodi (TRA) bila kuumiza upande wowote kwani jambo hilo linawahusu wote.
Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Kodi (ITA), Prof. Isaya Jairo akitoa neno la ukaribisho katika ufunguzi wa kongamano hilo lililofanyika Bagamoyo, Pwani.

Alisema kupitia kongamano hilo wamekutanisha wataalam wa kodi, wahasibu, walipa kodi, wanasheria, washauri wa kodi na walimu wa kodi kutoka vyuoni ili kuweza kupata maoni ya pamoja na kupata maoni ya makubaliano ya pande zote ambayo yatatumika katika kuendesha chombo hicho.Na Rabi Hume - MO Blog)
Baadhi ya wadau waliohudhuria kongamano hilo la siku moja lililofanyika Bagamoyo, Pwani.






Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja (group one).
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja (group two).

KILI CHALENGE MWAKA HUU KUPANDISHA WATU 50 KATIKA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO.

$
0
0
 Meneja wa Uhusiano na Mawasiliano wa Mgodi wa Geita (GGM), Tenga Tenga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu Mgodi wa GGM kupandisha watu 100 Mlima Kilimanjaro na wengine watazunguka mlima wa Kilimanjaro kwa baiskeli kwaajili ya kuchangia fedha za mfuko wa Kili challenge ambao ni mapambano dhidi ya Ukimwi. Katikati ni  Balozi wa Kili challenge Msanii, Mrisho Mpoto, Kushoto ni  Mwakilishi wa tume ya Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Peter Dickson.
Balozi wa Kili Challenge na msanii wa muziki wa kughani, Mrisho Mpoto akifafanua jambo jijini Dar es Salaam, kuhusu tukio la kupandisha watu 50 katika kilele cha mlima Kilimanjaro na waendesha baiskeli 50 kuuzunguka mlima huo kwaajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi. Kulia ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), Tenga Tenga.

Julai 16 hadi 22 Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) ukishirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi wanatarajia kuwapandisha katika Kilile cha Mlima wa Kilimanjaro watu 50 na wengine 50 watauzunguka mlima kwa baiskeli ikiwa ni kampeni ya kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Mawasiliano na Mahusiano wa Mgodi wa Geita (GGM), Tenga Tenga wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa Kilimanjaro Challenge kwa mwaka huu litajumuisha watu kutoka nchi mbalimbali.

Amesema kuwa Balozi wa Mgodi wa dhahabu wa Geita kwa mwaka huu ni Msanii wa nyimbo za Mashahiri, Mrisho Mpoto atakuwa na watu watakaoshiriki wa Kili challenge hadi katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.

Nae Msanii wa nyimbo za Mashahiri, Mrisho Mpoto amesema kuwa watanzania tuunge mkono kwa pamoja katika sehemu kuchangia au kumuelimisha jamii kuhusina na mapambano dhidi ya UKIMWI yalete mabadiliko.

“Mimi kama balozi wa Kili challenge, naamini kwamba jitihada zinazofanywa na mfuko huu zinahitaji kuungwa mkono na watanzania wote na wadau wenye machungu na nchi hii” Alisema Mpot. Hebu tuungane kwa pamoja kila mmja wetu katika sehemu yake eitha kwa kuchangia au kumuelimisha mwenzake ili mapambano haya yalete mabadiliko” alisema Balozi Mpoto. 

Fedha zinazopatikana katika mfuko huu zinapelekwa katika kusaidia mapambano dhidi ya ukimwi ikiwa ni pamoja na kujenga vituo vya ushauri nasaha na upimaji wa ukimwi ambapo baadhi yao ni vie vilivyoko Tanga pale Segera, Manyoni na Geita. Kituo cha watoto yatima Moyo wa Huruma na asasi nyingine zaidi ya 30 zimenufaika na mfuko huu.” Alisema mwakilishi wa TACAIDS, Dickson Peter.

Viwanda visivyo endelezwa kurudishwa kwa watanzania

$
0
0

Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma



Viwanda vilivyobinafsishwa na Serikali ambavyo haviendelezwi kutwaliwa ili kutolewa kwa wawekezaji wenye uwezo wa kuviendesha.


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage ameyasema hayo leo mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Tabora Mjini Mhe. Emmanuel Mwakasaka aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa juu ya mwekezaji wa kiwanda cha nyuzi Tabora kwa kushindwa kuendeleza kiwanda hicho.


“Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina inaendelea na tathmini ya viwanda vyote vilivyobinafsishwa na Serikali kikiwemo kiwanda cha nyuzi cha Tabora ili kujiridhisha kama wawekezaji wa viwanda hivyo wanatimiza matakwa ya mkataba na Serikali,” alifafanua Mhe. Mwijage.


Aliendelea kwa kusema kuwa, ikiwa viwanda hivyo vitabainika kubadilishwa matumizi yake au kutoendelezwa basi Serikali itavirudisha kwa watanzani ili viweze kuendelezwa.


Aidha Mhe. Mwijage amesema kuwa, kwa sasa mwitikio wa kuviendeleza viwanda ambavyo vilikuwa havizalishi ni mzuri kwani viwanda vingi vimeanza kufanya kazi lakini kwa wale ambao watashindwa kabisa  kuviendeleza basi viwanda hivyo vitarejeshwa kwa watanzania.


Vile vile Mhe. Mwijage amesema kuwa dhana ya Serikali ya awamu ya Tano ya kujenga uchumi wa viwanda inaenda pamoja na kurejesha Serikalini viwanda vyote vilivyobinafsishwa lakini haviendelezwi ili vitolewe kwa wawekezaji wengine.


Sambamba na hayo Mhe. Mwijage amesema kuwa kufufua viwanda, hasa viwanda vya nguo ni pamoja na wakulima wa pamba kulima zao hilo kwa wingi kwa ajili ya uchakataji pamoja na kudhoofisha uingizaji wa nguo za mitumba nchini.


Wizara hiyo inaendelea na kushawishi wawekezaji mbalimbali ili kujenga viwanda vingi iwezekavyo kwa ajili ya uchakataji wa mazao yanayolimwa nchini pamoja na mifugo.

MFUKO WA PENSHENI WA PPF KUTOA HUDUMA ZOTE KWA WATEJA WAKE VIWANJA VYA SABASABA

$
0
0

Baadhi ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya Banda lao Namba 86 lililopo katika Viwanja vya Sabasaba.Picha Zote na Mafoto Blog.
Muonekano wa nje ya Jengo la PPF lililopo Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa vya Mwalimu Nyerere jijini Dar esSalaam (Sabasaba).

Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Pauline Msanga, akitoa maelezo kwa wananchi kuhusu Huduma za uendeshaji Mfuko huo, wakati walipotembelea katika Banda lao lililopo kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, leo.
Sehemu ya wananchi waliotembelea Banda la Mfuko wa Pensheni wa PPF wakipata elimu kuhusu Mafao yatolewayo na Mfuko huo na jinsi mwanachama anavyoweza kujiunga na kuchangia.


Maandalizi
Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally (katikati) na Afisa Michango Glory Maboya, wakijiandaa kuhudumia wateja leo asubuhi katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba.

Afisa Utafiti Neema Mjema (nyuma) na Mwanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nyambilila Ndoboka, pia wakijiandaa kuweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Bandao lao la Maonesho kwenye Viwanja vya Sabasaba leo.
Afisa Uwekezaji wa Mfuko huo, Jonas Mbwambo akiweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Banda lao namba 86 viwanja vya Saba saba.
Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally, akimfafanulia mwanachama wake kuhusu uchangiaji wa michango ya Wanachama,
Afisa Huduma kwa Wateja, wa PPF Mwajuma Msina, akizungumza na Mwananchi aliyefika kutembelea Banda hilo wakati akimwelezea kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko huo.
Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) akifafanua jambo kwa mstaafu wa PPF.
Mtaalamu wa Mifumo ya Habari wa Mfuko wa PPF, Isabela Ngalawa, akimwelekeza mmoja kati ya Wanachama wa Mfuko huo kuhusu 'PPF Taarifa Mobile Apps' ili mwanachama aweze kupata taarifa za michango yake kupitia simu yake ya mkononi.
Afisa Huduma kwa Wateja, Mohamed Siaga, akizungumza na Mwananchi aliyefika katika Banda la PPF kuhusu jinsi ya kujiunga na Mfumo wa 'Wote scheme kutoka sekta isiyo rasmi
Mmoja kati ya Wanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nyambilila Ndoboka, akimwelekeza jambo mwanachama wa Mfuko huo kuhusu masuala ya Kisheria, wakati alipofika kutembelea Banda la Maonesho la PFF leo.
Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Temeke, Sostenes Lyimo (kushoto) akifafanua jambo kwa baadhi ya wananchi waliotembelea Banda hilo.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA MWENYEKITI WA GATES FOUNDATION MELINDA GATES

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Mwenyekiti wa Gates Foundation Bi. Melinda Gates Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Gates Foundation Bi. Melinda Gates watatu kutoka kushoto mara baada ya kumaliza mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mwenyekiti wa Gates Foundation Bi. Melinda Gates mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.

Kiwanda cha Mbolea chenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.5 kujengwa wilayani Kilwa

$
0
0

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akizungumza kwenye kikao na mabalozi kutoka Ujerumani na Denmark (hawapo pichani) hivi karibuni katika Ukumbi wa Wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo(Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ujerumani, Egon Kochanke(Kulia) na Balozi wa Denmark, Einar Jensen(Kushoto).
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo(Kulia) akijadiliana jambo na Balozi wa Denmark, Einar Jensen (Kushoto). Katikati ni Balozi wa Ujerumani, Egon Kochanke akiweka sahihi kwenye kitabu cha wageni ofisini kwa Waziri jijini Dar es Salaam hivi karibuni.


Kina thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.5
Kuzalisha tani milioni 1.35 kwa mwaka

Na Devota Myombe

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke pamoja na Balozi wa Denmark nchini, Einar Jensen kujadili ujenzi wa Kiwanda cha mbolea wilayani Kilwa.

Katika mkutano huo, ilielezwa kuwa matayarisho ya ujenzi wa kiwanda hicho cha mbolea chenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.5 yanaendelea na kwamba kiwanda hicho kinatarajiwa kuzalisha tani milioni 1.35 za mbolea kwa mwaka.

Waziri Muhongo alisema ardhi kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda hicho ipo na kuwa gesi asilia itakayotumika kiwandani hapo ipo ya kutosha.

Alisema kampuni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi zitakuwa na hisa katika kiwanda hicho ambapo kwa upande wa Tanzania, alizitaja kampuni hizo kuwa ni Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Minjingu Mines pamoja na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Aidha, kwa upande wa kampuni za nje, Profesa Muhongo alizitaja kuwa ni Ferrostaal ya Ujerumani, Haldor Topsoe ya Denmark na Fauji kutoka nchini Pakistan.

Profesa Muhongo aliwahakikishia mabalozi hao pamoja na ujumbe wao kuwa ardhi kwa ajili ya uwekezaji wa kiwanda hicho ipo na kwamba gesi asilia itakayohitajika ipo ya kutosha na kuwa bado nafasi za uwekezaji zinapatikana. “Ardhi ipo, gesi ipo hivyo mnakaribishwa,” alisema Prof. Muhongo.

Naye Balozi wa Ujerumani nchini, Egon Kochanke alimshukuru Profesa Muhongo kwa kukubali kukutana na ujumbe huo kupokea maombi ya mpango wa ujenzi wa Kiwanda hicho cha mbolea ambapo alisema, hiyo ni njia mojawapo ya kuboresha uzalishaji Tanzania. “Nimefurahi sana kushiriki kikao hiki na nina kushukuru kwa kukubali kwako kupokea maombi haya,” alisema.

Kwa upande wake Balozi Einar Jensen alitumia nafasi hiyo kumshukuru Profesa Muhongo kwa jinsi alivyoupokea ujumbe huo na namna alivyoendesha majadiliano husika.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na baadhi ya watendaji wa Wizara pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na Madini.

MBUNGE WA UKONGA MWITA WAITARA-AFUTURISHA WAPIGA KURA WAKE

$
0
0

Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa,akizungumza katika Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara(Chadema) kwa wananchi wa jimbo hilo nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa,akizungumza na waandishi wa habari baada aya kushiri Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara(Chadema), akizungumza katika Futari aliyowaandalia wananchi wa jimbo hilo nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
Wananchi wakifuturu Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
Wananchi wakifuturu Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
Wananchi wakifuturu Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA WAKUU WA MIKOA WATATU IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Charles Mlingwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mara Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Zainab Telack kuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wapya wa Wilaya mara baada ya kuwaapisha wakuu wapya watatu wa Mkoa Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan watatu kutoka kushoto, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa watatu kutoka kulia na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakwanza kushoto.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wakuu wa mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya wateule mara baada ya kumaliza kuwaapisha wakuu wa mikoa ya Shinyanga, Mara na Ruvuma Ikulu jijini Dar es Salaam.
. Baadhi ya Wakuu wa Wilaya wateule wakila kiapo cha uadilifu Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Juni, 2016 amewaapisha wakuu wa Mikoa watatu aliowateua Jumapili iliyopita tarehe 26 Juni, 2016.

Wakuu wa Mikoa walioapishwa leo Ikulu Jijini Dar es salaam ni Dkt. Binilith Satano Mahenge ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Charles Ogesa Mlingwa ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mara na Bi. Zainab Rajab Telack ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Hafla ya kuapishwa kwa wakuu hao wa Mikoa imehudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wakuu wa wilaya wateule ambao waliteuliwa na Rais Magufuli Jumapili iliyopita tarehe 26 Juni, 2016.

Aidha, miongoni mwa wakuu wa wilaya 139 walioteuliwa, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo katika wilaya tatu ambapo ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Rombo Mteule Mhe. Fatma Hassan Toufiq na badala yake amemteua Bi. Agness Elias Hokororo kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, ametengua uteuzi wa Mkuu wa wilaya ya Serengeti Mteule Bw. Emile Yotham Ntakamulenga na badala yake amemteua Bw. Nurdin Hassan Babu kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo na ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mteule Bw. Fikiri Avias Said na badala yake amemteua Bw. Miraji Mtaturu kuwa Mkuu wa wilaya hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka wakuu wa wilaya wateule kwenda kuchapa kazi na kutatua kero za wananchi katika wilaya zao huku wakizingatia kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu.

Rais Magufuli pia amewataka kusimamia ukusanyaji mapato ya serikali na matumizi ya fedha na rasilimali nyingine za umma, kuhakikisha wananchi wapo salama na pia kuhakikisha wananchi wanafanya kazi za uzalishaji mali.

"Katika kazi hizi wapo watakaowakejeli, katika kazi hizi wapo watakaowadhihaki, nyinyi kavumilieni na mmuweke Mungu mbele na mkawaweke watanzania mbele, mkafanye kazi kadiri Mungu atakavyokuwa amewaongoza.

"Nataka kuwahakikishia tunawaunga mkono kwa nguvu zote, mkafanye kazi bila uwoga wowote, katembeeni kifua mbele, kwa sababu tumewaamini wala msiwe na wasiwasi, ukifanya kitu kizuri kwa dhamira yako iliyo njema kitazaa matunda mazuri, ukifanya kitu kwa unafiki hakitafanikiwa" Amesema Rais Magufuli

Katika hafla hiyo, wakuu wa mikoa walioapishwa na wakuu wa wilaya wateule wamekula kiapo cha ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi ambalo limeongozwa na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Salome Kaganda.

Katika hatua nyingine, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na mwenyekiti mwenza wa taasisi ya Bill and Melinda Gates ya Marekani Bi. Melinda Gates ambapo Rais Magufuli amemuhakikishia mwenyekiti mwenza huyo kuwa serikali ya awamu ya tano itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano wake na taasisi hiyo ambayo imekuwa ikishirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Afya, Uongozi na Kilimo.

Kwa upande wake Bi. Melinda Gate amempongeza Rais Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya katika kukabiliana na rushwa na kuongeza ukusanyaji wa mapato ya serikali, na pia kwa nia yake thabiti ya kuinua sekta ya kilimo inayotegemewa na idadi kubwa ya watanzania na ameahidi kuwa taasisi ya Bill and Melinda Gates itaendelea kushirikiana na Serikali ya awamu ya tano katika kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao ya kilimo.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
29 Juni, 2016 .

Bunge limepitisha muswada wa marekebisha ya sheria ya ununuzi wa umma wa mwaka 2016

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma
——————–

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limepitisha muswada wa marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa Mwaka 2016 wenye lengo la kupunguza gharama na muda wa mchakato wa manunuzi Serikalini.

Marekebisho hayo yametokana na gharama kubwa ambayo Serikali imekuwa ikitumia kutokana na huduma na Bidhaa zinazonunuliwa na Serikali kuwa za juu ikilinganishwa na bei ya wastani ya soko.

“Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016 una lengo la kuongeza ufanisi katika ununuzi wa Umma kwa kuondoa mapungufu yaliyopo katika Sheria ya sasa kwa kupunguza gharama na muda wa michakato ya ununuzi, kutoa upendeleo kwa kampuni za ndani, vikundi maalum, malighafi na bidhaa zinazozalishwa nchini pamoja na kuweka viwango mahsusi kwa bidhaa zitakazotumiwa na Serikali,” alifafanua Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju.

Mhe. Masaju ameendelea kwa kusema kuwa sheria hiyo imeweka kifungu cha dharura ili kuwezesha vitu vya kuokoa uhai na vinginevyo kununuliwa kwa dharura pindi inapobidi.

Kwa upande wake Mbunge wa Babati Vijijini Mhe. Jitu Soni yeye ameiomba Serikali kuruhusu kununua vifaa tiba vilivyotumika ambavyo muda wake wa kutumia hauna mwisho, kwa mfano vitanda vya kujifungulia ili kupunguza gharama ya kununua vitanda vipya na kuweza kununua vitanda vingi kwa wakati mmoja.

Aidha Mhe. Jitu ameiomba Serikali kuirudisha tena Sheria hiyo Bungeni baada ya mwaka mmoja ili kufanyiwa marekebisho na kuziba mianya yote ambayo itakuwa imebainika mara baada ya utekelezaji wake kuanza.

Muswada wa marekebisho ya sheria hiyo yanasubiri kusainiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli ili kuanza utekelezaji wake.

WAZIRI WA VIWANDA AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI MKUU WA SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA(TBS).

$
0
0
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania(TBS), Joseph Masikitiko.


WANANCHI WAJITOKEZA KUPATA HUDUMA ZA 4G YA TTCL, KATIKA VIWANJA VYA SABASABA.

$
0
0

Wateja wakipata maelezo kuhusu huduma za TTCL, katika viwanja vya sabasaba
 Afisa kutoka TTCL, Fredrick Benard (kushoto) akitoa maelezo kwa mteja aliyetembelea banda la TTCL.



 TTCL wakitoa huduma kwa wateja katika maonesho ya Sabasaba 
 Wafanyakazi wa TTCL wakitoa huduma kwa wateja.
 Wafanyakazi wa TTCL wakiwakaribisha wateja katika Banda.

Wananchi waendelea kujitokeza kwa wingi katika Banda la Kampuni ya Simu Tanzania(TTCL) kununua bidhaa bora za  4G katika viwanja vya Maonesho ya Kibiashara ya Kimataifa ya Sabasaba. 

Akizungumza katika Maonesho hayo, Emerco Mashele Afisa kutoka TTCL amesema kuwa katika msimu huu wa Maonesho ya Kimataifa ya SabaSaba, kampuni imeendelea kuwaletea watanzania bidhaa nzuri za 4G – LTE, zenye kiwango kikubwa cha ubora, bei nafuu na uhakika. 

“Safari hii tumewaletea Wananchi bidhaa bora na nzuri katika matumizi ya mawasiliano ya simu. Kwa huduma zetu tunatoa fursa kwa wateja wetu kupata intaneti yenye kasi ya 4G ukiwa na Laini za 4G ambazo zinapatikana hapa katika Banda TTCL na ofisi za TTCL katika jiji la Dar es salaam” amesema Emerco. 

Aidha, Bw. Emerco aliongeza kuwa katika Maonesho haya ya SabaSaba, TTCL inatoa fursa ya wananchi kupata   laini ya 4G, Modemu ya 4G, Mi-Fi ya 4G na Routers ya 4G.

Katika maonesho haya tuna laini za 4G ambazo zinapatika hapa na katika ofisi zetu za TTCL, Mteja anaweza kifaa cha 4G Mi-Fi ambapo mteja anaweza kuunganisha watu wengine 10 na kupata intaneti katika ubora ule ule. 4G Routers inauwezo wa kuunganisha watu 32 na inauwezo kwenda katika ubora ule ule, Aidha pia Routers inatoa fursa kwa watumiaji kupata huduma simu ya Mezani. 

MTU MMOJA ANAYEDAIWA KUWA NI JAMBAZI SUGU ADAKWA JIJINI DAR

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam, limefanikiwa kumkamata mtu mmoja anayedaiwa kuwa jambazi sugu Abdallah Said (45) kwa  makosa ya ujambazi wa kutumia silaha na uvamizi kwenye vituo vya Polisi ikiwemo kituo cha Stakishari na taasisi mbalimbali za fedha  zikiwemo benki jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari , Kamishna wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa katika eneo la Kariakoo baada ya askari kufanya upelelezi wa kuwasaka watuhumiwa sugu wanaojihusisha na makosa yakiwemo ujambazi wa kutumia silaha.

Amesema  katika uchunguzi wa  wamebaini kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa anatafutwa kwa muda mrefu kwa makosa ya  ujambazi wa kutumia silaha ikiwa ni pamoja na kufanya mauaji ya kutumia silaha.

Kamanda, Sirro amesema mtuhumiwa baada ya kufikishwa kituo cha polisi na kuhojiwa, alikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya mauaji katika kituo cha Polisi Stakishari na taasisi za fedha ambazo ni  Benki ya Access Mbagala, Benki ya NMB Mkuranga, Benki ya CRDB na CBA Chanika, Road Block ya Polisi Kongowe na matukio mengine.  

Aidha kamanda huyo  maesema kuwa mtuhumiwa huyo pia aliwataja baadhi ya viongozi waanzilishi wa mipango ya uvamizi na uporaji wa silaha na mauaji kwa kutumia pikipiki ambao ni Abdulaazizi  Ndobe, Sheykh Mtozeni, Omari Matimbwa,Haji Ulatule,Nasoro Utaule Sasoro Mpemba na wenzake.

Mtuhumiwa huyo pia alitaja mipango yote ilifanyika katika msikiti wa Kitonga na yeye akiwa mtaalam na mshauri wa kitaalam kwa upande wa utumiaji wa silaha.

Wakati huo huo.Jeshi hilo  linamtafuta, Heri Mpopezi mwenye umri kati ya miaka 35-45 kwa tuhuma za ujambazi wa kutumia silaha. Mtuhumiwa huyo ameshiriki katika matukio mbalimbali ya uvamizi wa vituo vya Polisi, na taasisi za kibenki na kupora fedha pamoja na mauaji.

Amesema mtuhumiwa huyo alikuwa mfanyakazi wa chuo  cha JKU Zanzibar na anapendelea kutembelea na kuishi Zanzibar, Chanika, Mbagala, Mbande, Kimara, Kitonga, Mwamdimkongo, Bupu, Bagamoyo,Tanga, Kilwa, Ikwiriri, Rufiji na Dondwe.

Amesema  kuwa muonekano wa mtuhumiwa huyo ni Maji ya kunde, urefu wa wastani, kipara kidogo na anapendelea kuvalia vazi la Kanzu na mavazi mengine ya kawaida. Hivyo basi, natoa rai kwa wananchi raia wema watoe taarifa za uhakika za kukamatwa  kwa mtuhumiwa huyo  kituo chochote cha Polisi.

Akizungumzia suala la Mbunge wa Singida  Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amesema walimkamata mbunge huyo Juni 29 mwaka huu  na wamemhoji kutokana na kutoa maneno ya uchochezi na  kutoa lugha za kashfa dhidi ya Rais Pombe Magufuli ambayo aliyatoa baada ya kutoka Mahakamani Kisutu juzi.

Tundulisu alikuwa akituhumiwa kwa kosa la uchochezi na alikuwa katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alipotoka alitoa maneno ya kumkashifu Rais na maneno ya kichochezi sasa leo(jana) tumempeleka Mahakamani kujibu mashtaka hayo.  

MAKAMU WA RAIS AFUTURU NA WATOTO YATIMA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa Nasaha maalum mara baada ya kumaliza kufuturu na watoto Yatima kwenye viwanja vya Karimjee iliyoandaliwa na kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa kipindi television cha Mboni Show.
Mkuu wa Wilaya ya kinondoni Mhe. Ally Hapi (kushoto) akiwa kwenye dua pamoja na wageni waalikwa wengine.
Watoto Yatima wakiswali wakati wa tafrija ya kufuturisha watoto Yatima iliyoandaliwa na kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa kipindi cha televisheni cha Mboni Show ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na kufanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akisalimiana na Mkuu mpya wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (kulia) mwingine pichani ni Mkurugenzi wa kampuni ya Chocolate Princess inayotengeneza kipindi cha television cha Mboni Show Bi. Mboni Masimba wakati wa tafrija ya kufuturisha watoto yatima iliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee. 
Mkurugenzi wa kampuni ya Chocolate Princess kinachoandaa kipindi cha The Mboni Show akizungumza wakati wa kufuturisha watoto yatima .
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza kwenye tafrija ya kufuturisha Watoto Yatima iliyoandaliwa na kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa na kipindi cha television Mboni Show ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Watoto wakipewa juisi wakati wa Tafrij ya Futari.
Naibu Mufti Mkuu Sheikh Hamid Jongo akizungumza kwenye tafrija hiyo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema serikali inaendelea kuvisimamia kwa ukaribu vituo vyote vya kulelea watoto yatima nchini na vituo ambavyo vitabainika kuwa vinanufaisha wamiliki na vinaendeshwa bila ubora vitafungiwa mara moja. 

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam katika hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa kipindi cha Mboni Show hafla iliyojumuisha watoto yatima 283 kutoka Vituo vitano vya Mkoa wa Dar es Salaam.

Makamu wa Rais amesema kuwa azma ya serikali ni kuona vituo vyote vya kulelea watoto yatima kote nchini vinatoa huduma bora na inayokidhi mahitaji ya watoto hao na sio vinginevyo. Kuhusu malezi ya Watoto yatima, Makamu wa Rais ametoa wito kwa jamii iendelee kusaidia watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi kwa kuwapatia elimu bora,upendo na si kuiachia serikali mzigo huo au mashirika yasiyo ya kiserikali. 

Aidha, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ameiomba jamii kuweka mipango mizuri ya kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto yatima kwa kuwa nao wana haki ya kuishi vizuri kama watoto wengine. BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

WAZIRI UMMY MWALIMU, MELINDA GATES WAYAPONGEZA MASHINDANO YA MAMA SHUJAA WA CHAKULA YANAYO ENDESHWA NA OXFAM TANZANIA

$
0
0
Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na mke wa tajiri namba moja duniani na mwenyekiti mwenza wa Bill and Melinda Gates Foundation, Melinda Gates kwa pamoja wamelipongeza Shirika la Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow kwa kufanya Shindano la Mama Shujaa wa Chakula kama moja ya mbinu za kumkomboa mwanamke mnyonge kiuchumi.

Wawili hao waliyasema hayo kwenye mdahalo uliofanyika Juni 29 mwaka huu katika bustani ya Hoteli ya Serena jijini Dar ambapo walikuwa wageni waalikwa waliopata fursa ya kuzungumzia jinsi ya kumuwezesha kiuchumi mwanamke mzalishaji na namna ya kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Akizungumza kwenye mdahalo huo, Melinda Gates alisema kuwa yeye kupitia Bill and Melinda Gates Foundation wamelenga kusaidia nchi nyingi hasa za ukanda wa Afrika Mashariki kama Tanzania katika kubadilisha maisha yao kwa kutengeneza fursa za ajira na kuwasaidia vitendea kazi. 

Aliongeza kuwa kwa nchi kama ya Tanzania ambayo asilimia 25 ya mapato yake yanatokana na kilimo, taasisi yao imejikita katika kuwawezesha wakulima wadogowadogo ambao hata hivyo huwezi kuwaacha wakina mama kwa kuwa ndiyo wanaotoa mchango mkubwa kwenye sekta hiyo. 

Akizungumzia kuhusu Shindano la Mama Shujaa wa Chakula, Melinda Gates alitoa pongezi zake za dhati kwa shirika la Oxfam na kuongeza kuwa, ikiwa nchi za Kiafrika hususan Tanzania itataka kupiga hatua lazima iwawezeshe kiuchumi wanawake kwa kuwa wao ndiyo wenye uwezo wa kubadilisha maisha yao na hilo ndiyo jambo muhimu zaidi. 

Naye Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ambaye alikuwa ni mgeni rasmi kwenye mdahalo huo alisema kuwa; kwa kipindi kirefu amekuwa mfuatiliaji wa mashindano hayo na kuahidi kuwa sera ya serikali ya awamu ya tano ni kuongeza vipaumbele kwa mwanamke kwa kutoa mianya kwa taasisi zinazomsaidia mwanamke ikiwemo shirika la Oxfam kupitia shughuli zake hasas shindano la mama shujaa wa chakula. “Nikiri tu kuwa nimekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa shindano hili tangu zamani, naahidi kuwapa ushirikiano mkubwa kwenu kwa kila jambo kwa kuwa mnaisaidia sana serikali,” alisema Ummy. 

Aidha mdahalo huo pia ulioongozwa na mwanaharakati, Maria Sarungi Tsehai ulihudhuriwa na wanaharakati wengine wa masuala ya jinsia akiwemo Mkurugenzi wa Msichana Initative, Rebecca Gyumi, Mwanaharakati wa Mtandao wa Masuala ya Kijinsia, Marjorie Mbilinyi, Mwezeshaji kutoka Forum CC, Faizal Issa na Mshindi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2011, Anna Oloishuro.

Mwenyekiti mwenza wa taasisi ya Bill and Melinda Gates ya Marekani Bi. Melinda Gates akiongea na wadau mbalimbali na kulipongeza shirika la Kimataifa la Oxfam Tanzania kwa kuendesha Shindano la Mama Shujaa wa Chakula ambalo lengo kubwa ni kuwawezesha wakulima wadogo wadogo wanawake kufanikiwa katika Kilimo cha chakula na umiliki wa ardhi.
Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akitoa neno la utangulizi wakati wa sherehe hiyo.
Waziri wa Afya,Jinsia,Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akilipongeza Shirika la Kimataifa la Oxfam Tanzania kwa kuendesha Shindano la Mama Shujaa wa Chakula ambalo linaonesha changamoto za wazalishaji wa chakula wadogo ikiwemo umiliki wa ardhi.
Mshereheshaji katika Hafla hiyo Maria Sarungi Tsehai akiendelea kutoa muongozo.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA 
Viewing all 46360 articles
Browse latest View live




Latest Images