Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE ALIPOTEMBELEA KIWANDA CHA EAST COASTS OILS AND FATS KAMPUNI TANZU YA METL IKIWA NI KAMPENI YA KUHAMASISHA LISHE BORA NCHINI.

$
0
0
Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan akifafanua jambo kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kabla ya kukumimina Virutubishi vya Vitamini A katika Kinu cha kuzalisha mafuta kiwandani hapo ikiwa ni ishara ya kuhamasisha Lishe bora kwa walaji.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimimina mafuta ya virutubishi katika kinu cha kutengeneza mafuta ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kampeni ya kuhamaisha Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani, wakati alipotembelea Kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho ni kampuni tanzu ya MeTL kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Wanaoshihudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq (kushoto), Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan ( wa pili kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) (wa tatu kushoto) pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats ambayo ni Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan akitoa maelezo kwa Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete ya namna wanavyopima mafuta yao kwa Teknolojia ya Kompyuta wakati Rais Dkt. Kikwete alipotembelea kiwanda hicho kuhamasisha Kampeni ya Uongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani ili kutengeneza Lishe bora kwa walaji. Wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb).
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) akifafanua jambo kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipotembelea kiwanda cha East Coasts Oils and Fats ambacho ni kampuni tanzu ya MeTL.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL mara baada ya kumaliza zoezi la kutembelea kampuni hiyo inayozalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo mafuta ambapo amempongeza Mh. Mohammed Dewji kwa kutengeneza ajira kubwa kwa Watanzania kupitia kiwanda chake.


Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakimsikiliza Mh.Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa kwenye picha ya pamoja na Uongozi wa Kampuni ya MeTL pamoja na wadau wa masuala ya lishe alipotembelea Kiwanda cha East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL katika Kampeni ya Uongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq, Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema kwenye picha ya pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) (kushoto) mara baada ya kuhutubia wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq na mdau wa masuala ya lishe.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akiagana na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kumaliza ziara yake katika kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho kampuni tanzu ya MeTL ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni ya Uhamasishaji wa Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) wakati wakisubiri kuwasili kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL kuhamasisha Lishe Bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani yakiwemo mafuta ya kupikia. (Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog).

Picha juu na chini Viongozi mbalimbali wa Serikali na Wafanyakazi wa Kiwanda ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakisubiri kumpokea Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea kiwanda hicho ikiwa ni kampeni ya kuhamasisha Lishe Bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani yakiwemo mafuta ya kupikia.


Wafanyakazi wa Kiwanda ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakisubiri mkumpokea Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea kiwanda hicho ikiwa ni kampeni ya kuhamasisha Lishe Bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani yakiwemo mafuta ya kupikia.

Picha juu na chini ni Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akimlaki Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili Katika Kiwanda cha East Coasts Oils and Fats ambacho ni Kampuni Tanzu ya MeTL. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq.


Afisa Mwajiri wa kampuni ya East Coasts Oils and Fats ambayo ni Kampuni tanzu ya MeTL Bw. Eric Buberwa akisalimana na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili katika kampuni hiyo.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea kusalimiana na wadau mbalimbali wa masuala ya Lishe.

Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akiteta jambo na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wakielekea sehemu ya kiwanda cha East Coasts Oils and Fats. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq

WAJUMBE WA BODI YA UDHAMINI SSRA WALIPOTEMBELEA BANDA LA NSSF KATIKA MAONESHO YA WIKI YA HIFADHI YA JAMII MJINI DODOMA

$
0
0
 Ofisa Uwekezaji na Miradi Mwandamizi wa NSSF, Gerald Sondo (kushoto) akitoa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF katika maonesho ya Wiki ya Hifadhi ya Jamii.

Mjumbe wa bodi ya Wadhamini SSRA, Kabeho Solo akisaini kitabu cha wageni wakati wajumbe wa bodi hiyo walipotembelea banda la NSSF. Kulia ni Ofisa Mwandamizi Miradi na Uwekezaji, Gerlad Sondo na Ofisa Mwandamizi Uhusiano na Huduma kwa  Wateja, Theopista Muheta.
Ofisa Mwandamizi Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Theopista Muheta (kulia) akimkabidhi jarida lenye maelekezo ya kujiandaa kustaafu kwa mfanyakazi (staafu bila hofu), Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Irene Isaka  wakati wakati wa wajumbe wa bodi ya udhamini ya SSRA walipotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya Wiki ya Hifadhi ya Jamii inayoendelea mjini Dodoma. Katikati ni Ofisa Mwandamizi Miradi na Uwekezaji, Gerlad Sondo.
 Wajumbe wa bodi ya Wadhamini SSRA wakitembelea banda la NSSF.
 Wajumbe wa Bodi ya Udhamini SSRA wakiwa katika banda la NSSF.
 Ofisa Uwekezaji na Miradi Mwandamizi wa NSSF, Gerald Sondo (kushoto) akitoa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF katika maonesho ya Wiki ya Hifadhi ya Jamii.

MAMLAKA YA WANYAMAPORI KUANZISHWA NOVEMBA

$
0
0

PICHANI MBELE NI WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII AKIWA NA WALIOWAHI KUWA MAWAZIRI WA WIZARA HIYO NA MSITARI WA NYUMA NI WALIOWAHI KUWA MAKATIBU WAKUU WAKIFUATIWA NA WALIOWAHI  KUWA WAKURUGENZI WA IDARA YA WANYAMAPORI NA MAOFISA WAANDAMIZI WA  SASA WA IDARA YA WANYAMAPORI.

=========  ============  ========

Na Tulizo Kilaga

Wizara ya Maliasili na Utalii imeanza mikutano ya mchakato wa kupokea maoni kutoka kwa watu na makundi mbalimbali kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA).

Mkutano wa kwanza umefanyika leo jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Utalii kampasi ya Bustani kwa kuanzakupokea maoni kutoka kwa viongozi waliowahi kuwa mawaziri,makatibu wakuu na wakurugenzi wa wizara kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka hiyo.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Khamis Kagasheki wakati akifungua mkutano huo alisema Sheria ya Wanyamapori ya Mwaka 2009 inaitaka Wizara kuanzisha Mamlaka ya Wanyamapori kazi ambayo itakamilika Novemba mwaka huu.

Mhe. Waziri alisema kuwa Wizara kwa kutambua umuhimu wa ushirikishwaji imeamua kuanza na viongozi waliowahi kuitumikia Wizara ili waweze kutoa maoni juu ya Sheria na Muundo wa Mamlaka ya Wanyamapori pamoja na Sheria ya Idara ya wanyamapori itakayobaki katika Wizara.

“Nyalaka hizi zimetengenezwa na watu wa ndani ya Wizara wenye uzoefu wa muda mrefu na hivyo tumeona ni vizuri tuwashirikishe ninyi viongozi mliowahi kuitumikia Wizara ili muweze kutoa michango yenu itakayotuwezesha kupata kitu bora kitakachopelekwa katika Baraza la Mawaziri na kisha kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ili Bunge la Novemba tuweze kuiwakilisha ikiwa ina baraka na maoni kutoka kwa kamati ya Bunge ili ipitishwe kama Sheria ya Mamlaka ya Wanyamapori,” alisema Mhe. Waziri.

Kuanzishwa kwa Mamlaka ya Wanyamapori kutasaidia katika kurahisisha usimamizi wa rasilimali watu, kujitegemea kimaamuzi, na kuwa na uwezo wakujiendesha yenyewe bila kutegemea fedha kutoka hadhina. Miongoni mwa mawaziri waliohudhuria mchakato huo ni Mhe. George Kahama, Mhe. Getruda Mongella,  Mhe. Ezekiel Maige, Mhe. Dkt. Juma Ngasongwa, Mhe. Zabehi Mhita na Mhe. Arcado Ntegazwa.

Makatibu wakuu waliofika ni Mhe. Philimon Luhanjo, Mhe. Marten Rumbanga, Mhe. Rose Lugembe, Mhe. Balozi Dkt. Ladislaus Komba, Mhe. Alhaj Muhidin Ndolanga, Mhe. Salehe Pamba na waliowahi kuwa wakurugenzi wa Idara ya Wanyamapori.

ZIFF yatangaza Filamu zilizochaguliwa

$
0
0
 The 16th ZIFF official selection has just been announced. A total of 80 films are featured in 4 categories:   ZIFF Competition, Sembene Prize, Bongo Movies, Out of Competition. (Click on link or image). The festival kicks off on 29th June until 7th July. Here's the complete selection of ZIFF 2013 films including the country and the director for easy reference.



N ZIFF COMPETITION



100 Bucks

short fiction

Oshosheni Hiveluah

Namibia

A Story About Wendy

short fiction

Sean Hodgkinson

Trinidad and Tobago

Adamt

Sembene

Zelalem Woldemariam

Ethiopia

Al Wassia

short fiction

Allal El Alaqui

Morocco

Atate Na Panya

Animation

Anaeli Kihunrwa

Tanzania

Between Friends

fiction

M. Omar Jackson

Trinidad & Tobago

Blitz Patrollie

Fiction feature


South Africa

Bobby

short fiction

Mehdi Barsaoui

Tunisia

Brotherly Love

short fiction

Choice Skinner

USA

Burning Nests

fiction

Shahram Maslakhi

Iran and Iraq

Calling Home

short fiction

Inna

Kenya

Camera Women

Documentary

Karima Zoubir

Morrocco

 Chairman And The Lion

documentary

Peter Biella

USA/Tanzania

Children Of Troumatron

Fiction Feature

Harri & Sharvan Anenden-

Mauritius

Death Metal Angola

documentary

Jeremy Xido

USA & Angola

Death Of Time

fiction

Ali Molaghoulipor

Iran

Dialemi

short fiction

Nadine Otsobogo

Gabon

Dragonfly's Pond

fiction

Mohammedreza Arab

Iran

Drama Consult

documentary

Dorothee Wenner

Germany

Elelwani

Fiction feature

Ntshaveni Wa Luruli

South Africa

Everything We Want

documentary

Beatrice Moller

Germany

Fluorecent Sin

short fiction

 Amirah Tajdin

Kenya

Forerunners

documentary

Simon Wood

UK

Gangster Project

Documentary

Teboho Edkins

South Africa

Garifuna In Peril

fiction

Ali Allie & Ruben Reyes

USA/ Honduras

Geuko

short fiction

Peter Mbwago

Tanzania

Gog Helen

Fiction feature

Adze Ugah

South Africa

Golchehreh

fiction

Vahid Mousain

Iran

Gun To Tape

documentary

David Forbes

Kenya

Half An Hour Later

fiction

Mr. Lotfi

Iran

Hasaki Ya Suda

short fiction

Cedric Ido

Burkina Faso

 Haunted Souls

short fiction

Godwin Otwoma

Uganda

In Gods Land

documentary

Pankaj Rishi Kumar

India

Inspiration From Zanzi With Love

documentary

Salim Mwandoro

Tanzania

Joy, Its Nina

documentary

Jane Thrbuurn

UK/Nigeria

King Naki And The Thundering Hooves

documentary

Tim Wege

South Africa

Kinshasa Wickedland

documentary

Dovglas Douglas

DRC/ Belgium

Kivuto

short fiction

Sesonga Poupoune

Rwanda

Land Of the Dogon- World Heritage In Peril

documentary

Gregor Lutz

Germany

Leo

Fiction feature

Jinna Mutune

Ihiiii ndiyo yangaaaaa...... yaikuna simba 2-0

$
0
0
Nahodha wa Yanga, Nidir Haroub 'Canavaro' akiwa amenyanyua kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na wachezaji wenzake.

 Raha ya ushindi.
 Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.
 Kiduku
KARIBU JANGWANI NGASA
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao. 
Mashabiki wa yanga.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa  jijini Dar es Salaam


Beki wa Simba, Musa Mudde (kushoto) akichuana na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo. 
Beki wa Simba, Shamte Ramadhani akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva.

Beki wa Simba, Shomari Kapombe akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Msanii Juma Nature akitumbuiza wakati wa mchezo huo.
Shabiki wa Yanga akipelekwa kupewa huduma ya kwanza baada ya kuzimia wakati mchezo ukiendelea.
Kikosi cha Simba.
Makocha wa yanga wakipanga mikakati ya Ushindi.
Timu zikiingia uwanjani.
Timu zikisalimiana.
Kocha wa Simba, Patrick Liewig
Kocha wa Yanga, Ernst Brandts 
Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa Yanga. 
Mashabiki wa Yanga.
Kipa wa Simba, Juma Kaseja akijaribu bila mafanikio kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

KARIBU NYUMBANI
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao. 
Refa wa mechi ya Simba na Yanga, Nartin Saanya akiwa chini baada ya kugongwa kwa bahati mbaya na mchezaji wa Yanga, Didir Kavumbagu.
Refa, Martin Saanya akipata matibabu.

WALEMAVU WAASWA KUTOBWETEKA

$
0
0



Na Edwin Moshi, Makete.

Walemavu wilayani Makete wametakiwa kutobweteka na hali ya ulemavu waliyonayo na badala yake wajishughulishe kufanya kazi mbalimbali zitakazowafaa kulingana na ulemavu walionao.

Kwa kufanya hivyo kutawapunguzia hali ngumu ya maisha waliyonayo walemavu wengi wilayani hapo kwani kwa kiasi kikubwa ni wategemezi.Hayo yamesemwa na Niko Mbwilo ambaye ni mlemavu anayejishughulisha na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na miti aina ya mianzi wakati akifanya mahojiano na mtandao huu.

Mbwilo amesema ulemavu unatofautiana baina ya mtu mmoja na mwingine, hivyo mtu anatakiwa kuangalia ni kazi gani itakayomuingizia kipato ambayo anaweza kuifanya badala ya kukaa na kubweteka ama kutegemea misaada mbalimbali “Kwa mfano mimi ni mlemavu wa mguu, lakini nikaona ni bora kubuni shughuli hizi za mikono kwania sina ulemavu wa mikono, hivyo nafanya kazi kulingana na jinsi nilivyo, hivyo nadhania kila mlemavu akiliangalia hilo nafikiri maisha yaoa yatakuwa na unafuu”alisema Mbwilo.

Amesema ingawa kuna changamoto anazokutana nazo wakati wa kufanya kazi yake ikiwemo umbali wa kufuata mitia aina ya mianzi anayoitumia kutengenezea kazi yake, uchakavu wa jingo analofanyia biashara pamoja na ugumu wa soko lakini hakati tamaa kwa kuwa shughuli hiyo ndiyo inayomuingizia kipato kwa ajili yake na familia.

Ameongeza kwa kiasi kikubwa bidhaa anazotengeneza huwa zinategemea wateja wa nje ya wilaya ya Makete kwa kuwa wanaotengeneza bidhaa kama hizo ni wengi
Baadhi ya bidhaa anazozitengeneza ni nyungo, vikapu, viti, meza, ambavyo anavitengeneza kwa kutumia mianzi 

SASA INATOSHA WAHUSIKA KARABATINI BARABARA ZA MAKETE-MDAU.

$
0
0


Picha hizi zinaonesha maeneo mbalimbali ya barabara wilayani Makete mkoani Njombe ambazo zimeharibika kutokana na mvua zilizokuwa zikinyesha wilayani humo, kwa hivi sasa mvua zimemalizika tunaomba wahusika waanze kuzifanyia ukarabaiti(Picha na Edwin Moshi).

UZINDUZI WA WIKI YA FISTULA ULIVYOFANA BUKOBA

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Zaipora Pangani akiongea kwenye hafla ya uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya wiki ya fistula leo mjini Bukoba. Wa kwanza kulia ni Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacam Salum Mwalim. Wengine pichani kushoto ni Mwakilishi wa CCBRT Kasper Mmuya na Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Nassor Mnambila.Maadhimisho hayo yanafadhiliwa na Vodacom, Vodafone na CCBRT
 Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Zaipora Pangani akiongea kabla ya kukabidhi  funguo ya gari kwa Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA tayari kuanza safari ya kuanza Bukoba kwenda Dar salaam kupitia mikoa mbalimbali kuelimisha jamii juu ya tatizo la fistula na jinsi matibabu yanavyopatikana bila malipo katika hospitali ya CCBRT kwa ufadhili wa Vodacom. Kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Nassor Mnambila na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim.Kilelele cha maadhimisho hayo kitafanyika Mei 23 siku ya fistula duniani.
 Mwakilishi wa Taasisi ya CCBRT Kasper Mmuya akiongea kwenye hafla ya  uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya wiki ya fistula leo mjini Bukoba. Wengine pichani ni Kkatibu Tawala Mkoa wa Kagera Nassor Mnambila, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Zzaipora Pangani, Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim na Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA.Maadhimisho hayo yanafadhiliwa na Vodacom, Vodafone na CCBRT.
 Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Zaipora Pangani akikabidhi funguo ya gari kwa Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA tayari kuanza safari ya kuanza Bukoba kwenda Dar salaam kupitia mikoa mbalimbali kuelimisha jamii juu ya tatizo la fistula yakiwa na ujumbe fistula inatibika, jitokeza upate matibabu bila ya malipo katika hospitali ya CCBRT kwa ufadhili wa Vodacom na Vodafone ya nchoini Uingereza.
 Wakaazi wa Mji wa Bukoba waliofurika kushuhudia uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya wiki ya fistula uliofanywa leo mjini humo kueleka siku ya fistula duniani Mei 23. Maadhimisho hayo yanaratibiwa na kufadhiliwa na Vvodacom, Vodafone na CCBRT yakiwa na ujumbe “Fistula inatibika, jitokeza upate matibabu bila ya malipo.”
Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA akichana mistari kukonga nyonyo za wakazi wa mji wa Buko wakati wa uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya wiki ya fistula uliofanywa leo mjini humo kueleka siku ya fistula duniani Mei 23. Maadhimisho hayo yanaratibiwa na kufadhiliwa na Vvodacom, Vodafone na CCBRT yakiwa na ujumbe “Fistula inatibika, jitokeza upate matibabu bila ya malipo.”

Sera ya Gesi: Maoni ya Awali-Rasimu ya GesiAsilia -TanzaniaNatural Gas Policy

$
0
0

Draft 3- The Natural Gas Policy of Tanzania -2013
Draft 3- The Natural Gas Policy of Tanzania -2013(Rasimu ya Sera ya Gesi Asilia)
Nimepata muda kidogo wa kuipitia hii rasimu ya 3 nikiwa safarini kwenda Tabora kwa shughuli za chama changu cha CHADEMA , nina maoni ya awali kama ifuatavyo;
1). Kwa ujumla kupata Sera mpya ya gesi asilia ni hatua muafaka japo imechelewa sana. Hata hivyo ni bora kuchelewa kuliko kutofika kabisa. Ni vema wananchi wachukue fursa hii kuisoma na kuijadili rasimu hii na kuiboresha ili iwezeshe wananchi wenyewe kufaidika na utajiri ambao nchi yetu imejaaliwa.
2). Sera ina jumla ya sura Sita. Sura ya kwanza ya inaweka sababu na masuala ya jumla na utangulizi . Sura ya pili inaweka sababu za kuwepo kwa sera mpya na madhumuni maalumu, Sura ya tatu ndio yenye matamko ya msingi ya kisera (fundamental policy issues) ikiwemo masuala ya miundombinu ya gesi kwa ajili ya soko la ndani, usimamizi wa mapato yatokanayo na gesi asilia na masuala ya ‘’ local content’’. Sura hii pia imezungumzia masuala ya uwazi na uwajibikaji. Sura ya nne ni masuala ya mfumo wa kisheria na udhibiti na sura ya tano ni taasisi za usimamizi wa sera ya gesi asilia. Sura ya sita ni hitimisho. Kila sura imeweka matamko ya kisera.
3). Rasimu ya sera imeshindwa kutofautisha suala la Mafuta na Gesi kuwa ni suala la Muungano au sio suala la muungano katika muktadha wa Katiba mpya inayojadiliwa sasa. Hii inadhihirisha umuhimu wa kuwianisha mchakato wa katiba na michakato mingine inayoendelea nchini. Hivi sasa Zanzibar inajiandaa kuwa na sera na sheria yao ya mafuta ya gesi, iweje sera hii itamke gesi asilia ni mali ya Jamhuri ya Muungano wakati upande mmoja wa Muungano utakuwa unafaidi utajiri wake peke yake? Rasimu ya sera imeshindwa kutambua kuwa kuna vitalu vya mafuta na gesi ya (vitalu namba 9-12) vimesimamisha shughuli kwa sababu Serikali ya Zanziabar haitambui mafuta na gesi kuwa suala la muungano. Rasimu inapaswa kuzingatia jambo hili kabla ya kupata sera yenyewe.
4). Rasimu imetamka katika ukurasa wa 9 kwamba sera hii haitambui shughuli za utafutaji (‘This policy document only covers mid-and downstream segments’ ndio nukuu ya neno kwa neon ya Sera hii). Hiki ni kichekesho cha milenia .
Taifa linawezaje kuandika sera ya gesi asilia kwa upande wa uchuuzi tu (biashara) na kuacha kazi yenyewe haswa ya utafutaji na uchimbaji (exploration and exploitation are upstream). Shughuli za utafutaji na uchimbaji ndio msingi haswa wa sera ya gesi asilia.

Mikataba yote huamuliwa kwa kuzingatia kwanza utafutaji, shughuli nyingine ni biashara tu ya kitakachogunduliwa . Rasimu kuacha kabisa eneo la utafutaji na uendelezaji (upstream) ni sawa na kutokuwa na sera kabisa.
Kwa namna eneo hili lilivyoachwa kuna harufu ya mkakati wa siri wa kuwanyima wananchi msimamo wa kisera kuhusu utajiri wao unavyonyonywa . Sentensi hii yenye maneno 10 katika uk. wa 9 wa kijitabu cha rasimu ya sera unaondoa kabisa umuhimu wa sera yenyewe wakati dhumuni kuu la sera linatamkwa uk.6 kwamba Gesi asilia ni mali ya wananchi wa ‘Jamhuri ya Muungano’ wa Tanzania’’ kurasa tatu baadaye zinaiondoa sera kwenye eneo hilo la umiliki wa mali hii ( Upstream). Tumeamua kuandika sera ya uchuuzi wa gesi asilia?
5). Rasimu katika 3.2.2(uk.24) imeweka matamko ya kisera kuhusu uwazi na uwajibikaji . Uwazi ndio eneo ambalo watanzania wengi walikuwa wanasubiri kwa hamu sana . Usiri wa mikataba katika sekta mbali mbali nchini ni chanzo cha ufisadi na uporaji wa utajiri wa mali yetu. Sera hii imeJibu swala hili? HAPANA. Sera haisemi ni namna gani mikataba itakuwa wazi kwa wananchi. Sera haisemi ni namna gani wananchi wataiwajibisha Serikali na vyombo vyake (Accountability) kwenye masuala ya mafuta na gesi. Sera imepiga porojo kuhusu uwazi na uwajibikaji. Bila misingi imara ya Uwazi na Uwajibikaji katika rasilimali ya gesi asilia, sera haina maana yoyote ile.
6). Serikali ni lazima ijue kwamba hivi sasa nchi yetu nchi tajiri yenye watu masikini.[i] sera ya gesi inapaswa kutuondoa kuwa nchi yenye laana ya rasilimali. Sera hii haina mwelekeo huo kabisa . Sera inapaswa kuwezesha wananchi kupata thamani ya maliasili yetu na kuwezesha matumizi mazuri ya mapato yatokanayo na utajiri wa nchi.
Sera yetu lazima ioneshe dhahiri kwamba gesi asilia ni mali ya wananchi na uendelezaji na unyonyaji wa rasilimali hii utafaidisha wananchi kwanza na kwa ruhusa yao (Prior informed Consent Principle) sera ni lazima itamke hilo kinagaubaga.Sera ni lazima ionyeshe kuwa katika ushindani wa soko makampuni ya mafuta na gesi asilia yatapata faida ya halali ( normal retuns) ya uwekezaji wao na kwamba lolote linalozidi litabakia kuwa mali ya wananchi wa Tanzania.
Mkakati wa makampuni ya mafuta na gesi asilia ni kuhakikisha taifa linapata kiduchu na wanasaidia serikali kutoa majibu ya kipato hicho kiduchu. Watanzania hawatakubali tena.
7). Ni lazima tuseme kuwa tunataka utajiri wetu uwe neema kwa wananchi wetu, na siyo laana. Maendeleo yetu yatategemea ni namna gani tunafaidika na utajiri wetu wa maliasili kama gesi asilia. Sera ya Gesi Asilia itujengee imani hiyo. Hii Sera (Rasimu) inapaswa iangaliwe upya na hasa maeneo ya uwazi na uwajibikaji.
 
Kabwe Z. Zitto, Mb Kigoma Kaskazini
Tabora, tarehe 18 Mei 201

Miss Tabata kutembelea Mikumi Mei 26

$
0
0
Washiriki wa Miss Tabata 2013  (pichani) watatembelea mbuga ya wanyama ya Mikumi wikiendi ijayo. Mratibu wa shindano hilo Godfrey Kalinga anasema lengo la ziara hiyo ni kukuza utalii wa ndani, na kwamba  warembo hao pia watapata fursa ya kujua vivutio vilivyomo kwenye mbuga hiyo iliyoko mkoani Morogoro.

 “Hii siyo mara yetu ya kwanza kuwapeleka warembo wetu mbugani. Tumekuwa tukifanya kila mwaka,” alisema Kalinga. Kapinga alisema kuwa ziara hiyo imedhaminiwa na CXC Africa. 

 Shindano la kumsaka Miss Tabata litafanyika Mei 31 katika ukumbi wa Da’ West Park, Tabata. Wadhamini wa shindano hilo ni Nipashe, Redds, Dodoma Wine, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, CXC Africa, Brake Point, Michuzi Blog  na Saluti5. 

Warembo watakaoshiriki kwenye shindano hilo  (pichani) linaloandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts ni Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Musa Kitereja (19), Rehema Kihinja (20), Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23), Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na Suzan Daniel (18). 

 Warembo watano watachaguliwa kushiriki mashindano ya Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania. Anayeshikilia taji la Miss Tabata kwa sasa ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.

DIAMOND, NEY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE

$
0
0
Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.
Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.
Diamond na Ney wakiwapagawisha mashabiki.
Ney wa Mitego akisema na wapenzi wake.
Diamond Platnumz akionyesha umahiri wake stejini.
Diamond akifanya makamuzi sambamba na kundi lake.
Ney wa Mitego akilishambulia jukwaa la Dar Live.
Mashabiki wakiburudika wakati wa shoo hiyo ndani ya Dar Live.
Diamond na kundi lake katika pozi kabla ya makamuzi.

DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa 'Muziki Gani'.

Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar. 
(PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY/GPL)

Waraka kuhusu muswada wa Baraza la Vijana la Taifa wa Mwaka 2013

$
0
0

Vijana wenzangu na wote wenye dhamira ya kuwezesha maendeleo ya vijana nchini, salaam! 


Mtakumbuka kwamba mwezi Januari 2013 nilitoa taarifa kwa umma ya kueleza kuwa niliwasilisha kwa Katibu wa Bunge Muswada Binafsi wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa na kuomba hatua za ziada toka ofisi ya Bunge kwa kuzingatia Kanuni ya 21 na Kanuni ya 81 ya Kanuni za Kudumu za Bunge. 

Toka wakati huo muswada huo mpaka sasa Mei 2013 haujachapwa katika gazeti la Serikali na nimepokea barua toka kwa ofisi ya Bunge kwamba wamepokea ushauri toka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa muswada huo hauwezi kuchapishwa katika gazeti la Serikali kwa kuwa umekiuka masharti ya ibara ya 99 ya Katiba ya Nchi. 

Sababu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutoa ushauri huo ni kuwa muswada unalenga pamoja na mambo mengine kupitia kifungu cha 31 kipengele cha kwanza kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa madhumuni ya kugharamia shughuli za baraza la vijana la taifa, mipango ya baraza na kutekeleza miradi ya vijana kwa ajili ya maendeleo ya vijana. 

Kwa maoni yangu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametoa ushauri huo bila kuzingatia kwamba kifungu cha 31 kipengele cha pili kinataja vyanzo mbalimbali vya fedha za mfuko ikiwemo kutaja kuwa fedha za mfuko zitatokana na fedha zilizotengwa na Serikali na Bunge kwa ajili ya Baraza kwa mujibu wa Ibara ya 135 kifungu cha pili cha katiba ya Nchi.

Ibara ya 135 (2) ya Katiba ya Nchi inatamka kuwa “fedha ambazo hazitawekwa kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ni zile zote ambazo zimetajwa na sheria ya kwamba zitumike kwa shughuli maalum au ziwekwe kwenye mfuko mwingine kwa ajili ya matumizi maalum”. 

Hivyo, ni maoni yangu kuwa ibara hiyo ya Katiba ya Nchi inaweza kutumika kuwezesha kuanzishwa kwa Baraza la Vijana na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana bila kufungwa na Ibara ya 99 ya Katiba kifungu cha kwanza ambacho kimeweka masharti kuwa “Bunge halitashughulikia jambo lolote kati ya mambo yanayohusika na ibara hii isipokuwa kama Rais amependekeza kwamba jambo hilo lishughulikiwe na Bunge na pendekezo hilo la Rais liwe limewasilishwa kwenye Bunge na Rais.” 

Kifungu cha pili kinataja mambo yanayohusika na ibara hiyo ya 99 ni pamoja na muswada wa sheria kwa ajili ya “kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko mwingine wowote au kubadilisha kiwango hicho kwa namna nyingine yoyote isipokuwa kupunguza”. 

Toka Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 itamke kwamba Serikali itawezesha kuanzishwa kwa Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007; miaka takribani 17 imepita marais wote wa awamu husika na mawaziri wenye dhamana hawajawasilisha bungeni muswada huo hali ambayo imenifanya niandae muswada binafsi kuwezesha baraza kuundwa. 

Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa 2013 niliouwasilisha kwa maoni yangu hauna lengo la kuagiza malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko mkuu wa Hazina ya Serikali au Mfuko mwingine wowote kwa mujibu wa ibara ya 99 bali unalenga kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 135. 

Hata hivyo, kwa kuwa muswada huu unahusu mustakabali wa vijana na ni suala la kitaifa kupitia waraka huu naomba kupata maoni yenu kuhusu suala hili, mapendekezo ya marekebisho yanayohitajika kufanyika na hatua zinazopaswa kuchukuliwa. 

Maoni, mapendekezo na hatua hizo zitumwe kupitia mbungeubungo@gmail.com au kwa Afisa wa Ofisi ya Mbunge Ubungo Gaston Garubimbi (0715825025) kabla ya tarehe 24 Mei 2013. 

Nakala ya rasimu ya muswada wa Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 inapatikana katika mtandao wa http://mnyika.blogspot.com kwa ajili ya rejea. 


Aidha, nawaalika kushiriki mikutano ya kupokea maoni kupitia mtandao huo tarehe 20 mpaka 23 Mei 2013 saa 9 alasiri mpaka 10 Jioni ambayo nitashiriki na kutoa maelezo ya zaidi kwa kadiri itakavyohitajika. 

Natarajia kupokea maoni ya vijana na wananchi wengine bila kujali tofauti mbalimbali kwa kuwa madai ya kutaka kuundwe Baraza la Vijana la Taifa yamekuwa yakitolewa na vijana, asasi na taasisi kwa muda mrefu. 

Vyama vya siasa kwa kuzingatia matakwa hayo viliahidi kutekeleza azma hiyo kwa mfano Ilani ya CHADEMA ya mwaka 2010-2015 kipengele 6.4.1 (viii) ilitamka “Kwa kuwa vijana ndio kundi kubwa hapa nchini, na kwa kuwa uhai wa muda mrefu wa taifa letu upo mikononi mwa vijana, Serikali ya CHADEMA itawezesha vijana kuunda Baraza la Vijana (BAVITA) ambalo limekwamishwa na Serikali ya CCM kwa muda mrefu”. 

Kwa upande mwingine, Ilani ya CCM ya mwaka 2010-2015 iliahidi katika kipengele 80 (k) “Kuhamasisha ushiriki wa vijana katika ngazi mbalimbali za maamuzi ikiwa ni pamoja na kukamilisha uanzishaji wa Baraza la Vijana”. 

Mwaka 2011 niliihoji Serikali bungeni ni lini itakamilisha uanzishwaji wa baraza hilo na ikaahidi kwamba kazi hiyo itakamilishwa katika mwaka wa fedha 2011/2012 hata hivyo sasa ni Mei 2013 Serikali haijakamilisha. 

Hivyo vijana, wabunge na wananchi kwa ujumla ni muhimu kuboresha muswada huo na uwasilishwe bungeni kuwezesha baraza la vijana na mfuko wa maendeleo vijana kuanzishwa; maslahi ya umma kwanza. 

Wenu katika uwakilishi wa wananchi,

John Mnyika (Mb) 
19 Mei 2013 
Dodoma
 

Muswada wa Baraza la Vijana 2013-Rasimu ya Kwanza; pakua hapa (download here): 

lami ya makete nayo yaanza kufumuka

$
0
0

Kama unavyoona, hii ni barabara ya lami iliyopo wilayani Makete, ambapo kamera ya mtandao huu imenasa jinsi inavyoanza kuharibika, Mara nyingi kuchelewa kukarabati uharibifu kama huu ndiyo huzaa matatizo makubwa katika barabara hiyo ikiwemo mashimo makubwa ambayo yatakuja kukarabatiwa kwa gharama kubwa
Shimo dogo hilo na ndivyo linavyoanza, mwishowe sijui itakuja kuwaje
 Mara nyingi navyohisi uharibifu huu umesababishwa na magari kuzidisha uzito kwa kuwa barabara ya makete-njombe haina mizani
Hii ndiyo hali halisi msomaji wetu
Ushauri wetu, naomba mamlaka husika zifanye ukarabati mapema hasa ukizingatia wamamkete wanaitamani lami balaa, maana adha ya vumbi na matope daaaaah usiseme(Picha na Edwin Moshi)

MKUTANO WA MWENYEKITI WA CCM RAIS KIKWETE NA WABUNGE WA CCM

$
0
0
  Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
  Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
 Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
  Wajumbe kwenye kikao cha Mwenyekiti wa CCM na Wabunge wa CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migoiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai na Katibu wa NEC Oganaizesheni Dk. Muhammed Seif Khatib kwenye kikao hicho.
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro(kulia) akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum Vicky Kamata wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mbunge wa Same Anne Kilango Malecela.

Mbunge wa Songea na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akitaniana kuhusu Uyanga na Simba na Mwenyekiti wa Simba, Mbunge wa Tabora Aden Rage nje ya ukumbi kabla ya kuanza mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya. (Picha na Bashir Nkoromo).

KAMPUNI YA MONTAGE YAIKABIDHI WAMA MILIONI 70 KUSAIDIA AFYA YA MAMA NA MTOTO TANZANIA

$
0
0
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Salma Kikwete akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni 70 kutoka kwa Mkurugenzi wa Montage Limited, Teddy Mapunda ikiwa ni mchango wa kampuni hiyo katika kuchangia Afya ya Mama na Mtoto. Fedha hizo ni sehemu ya michango ya wadau mbalimbali iliyopatikana katika harambee maalum iliyopendeshwa na Montage hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Fedha wa Montage, Zainabu Mkindi (wapili kushoto)na kulia ni Katibu wa WAMA, Daud Nassib. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki.
 Mkurugenzi wa ITV, Joyce Mhavile (kushoto0 akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited, Teddy Mapunda kabla ya kukabidhi hundi kwa Uongozi wa WAMA.
 Mke wa Rais  na Mwenyekiti wa WAMA, Salma Kikwete (katikati) akisalimina na Mkurugenzi wa ITV, Joyce Mhavile na kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Limited, Teddy Mapunda.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA, Salma Kikwete (kulia) akizungumza na Uongozi wa Montage pamoja na wadhamini wa Harambee iliyoongozwa na Kampuni ya Montage kwaajili ya kuchangisha fedha kwaajili ya kusaidia matibabu ya Mama na Mtoto nchini Tanzania.

sensei Rumadha Fundi anyakua nondo zake marekani

$
0
0
 Sensei Rumadha Fundi akielekea kuchukua Nondozzzz zake
 Sensei Rumadha na mkewe Anita pamoja na mdogo wake Rumadha,Kibwana Fundi katika shangwe
 Sensei Rumadha Fundi (mstari wa nyuma) akiwa na wataalamu wenzie wa mapafu
Sensei Rumadha akiwa na ndugu na marafiki.
Sensei Rumadha akiwa na binamu yake Dotto Haruna.
=====  =====  ===== ======

Mtanzania mtaalamu wa Karate na Yoga Sensei Rumadha Fundi (3rd Dan,Black Belt ) mwenye maskani yake kule marekani juzi Mei 17, 2013 Sensei Rumadha Fundi amekula nondozzz ya "Associate in Applied Science Cardiopulmonary Respiratory Care" katika chuo cha "Collin College, McKinney, Texas, USA. 

Sensei Rumadha sasa amekuwa mtaalam wa hewa na gesi ya kupumua (wa Respiratory Therapist) anayetibu mapafu na moyo chini ya maelekezo ya mganga wa mapafu"pulmonalogist. 

Respiratory therapist ana majukumu mengi kama kuwatibu wagonjwa wa pumu,COPD,Ephysema,Asthma,TB na majonjwa yote yanayohusu mapafu na moyo. Pia ana uwezo wa kutafsiri damu baada ya kupima hali ya mgonjwa kama ana oxygen ya gesi ya kutosha na kama inahitaji tiba yeyote. 

Kwa mengi zaidi kuhusiana na utaalam wa Respiratory Therapist nenda"Who is a Respiratory Therapist? http://en.wikipedia.org/wiki/Respiratory_therapy

Lori la mafuta la kampuni ya Lake Oil lapata ajali mlima nyoka jijini mbeya leo.

$
0
0
 Lori la kampuni ya Mafuta ya Lake Oil likiwa limepata ajali maeneo ya Mlima Nyoka-Mkoani Mbeya,Aidha katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha isipokuwa baadhi ya watu kadhaa walijeruhiwa.
 Baadhi ya Wakazi kutoka maeneo mbalimbali ya Mlima Nyoka ikiwemo jirani na mji maarufu wa kibiashara,Uyole jijini Mbeya wakiwa wamejumuika kwa pamoja wakigombea mafuta yaliyokuwa yakimwagika,mara baada ya Lori la Lake Oil kupata ajali.Picha kwa hisani ya Mbeya Yetu Blog.

Mkuu wa Mkoa wa Geita atangaza kujitolea kuwa balozi wa kampeni ya Fistula kumaliza tatizo hilo ifikapo 2016

$
0
0
Muuguzi na Mnasihi wa CCBRT Theodola Millinga akielimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na namna ya kupata matibabu yake bila malipo kwenye hospitali ya CCBRT kupitia ufadhili wa Vodacom na Vodafone ya Uingereza. Zoezi hilo ni sehemu ya kampeni ya kusambaza ujumbe wa "Fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ya malipo inayondelea mikoani kwa ufadhili wa Vodacom na Vodafone ikishirikiana na CCBRT.
Mkuu wa Mkoa wa Geira Said Magalula(katikati), Balozi wa Chapa Vodacom Mwana FA na Meneja Uhusiano wa Mambo ya nje wa Vodacom Salum Mwalim wakifurahia moja ya tukio wakati wa kampeni ya kuelimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na kufikisha ujumbe wa "Fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bilaya malipo" liliondeshwa mjini Geita ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuelekea siku ya fistula duniani Mei 23. Vodacom na Vodafone hufadhili matibabu kwa wanawake wenye fistula kwenye hospitali ya CCBRT.
Shuhuda wa fistula akitoa ushuhuda wa jinsi alivyoteseka na fistula kwa mika mine kabla ya Vodacom kufadhili matibabu yake kwenye hospitali ya CCBRT. Ushuhuda huo ulitolewa wakti wa kampeni ya kuelimisha wakazi wa Geita kuhus fistula na kufikisha ujumbe wa "Fistula inatibika jitokeza upate matibabu bila ya malipo.
Balozi wa Chapa Vodacom Mwana FA akiwahamasisha wakazi wa Geita kuunga mkono kampeni ya kumaliza tatizo la fistula ifikapo mwaka 2016 inayofadhiliwa na Vodacom an Vodafone ya Uingereza kupitia hospitali ya CCBRT.
Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA akichana mistari mbele ya wakazi wa Mji wa Geita waliofika katika kampeni ya uelimishaji umma kuhusu fistula na kusambaza ujumbe wa "fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ua malipo". Mwana FA yupo kwenye msafara wa kueneza ujumbe huo kw amikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Singida, Dodoma, Morogoro na Pwani kwa ufadhili wa Vodacom.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Bw. Said Mgalula akimakbidhi kipaza sauti Balozi wa Vodacom Msanii Mwana FA ili awashushie mistari wakazi wa mji huo waliojitokeze kwenye kampeni ya uelimishaji jamii kuhusu fistula na kwamba matibabu yake yanapatikana bila malipo kwenye hospitali ya CCBRT kwa gharama za Vodacom na Vodafone ya Uingereza.
Meneja wa Vodacom Mwanza Victoria na mwenzake wa Misungwi Gift wakihifadhi nambari maalum ya kupiga bure 0800752227 kwa masuala yoyote yanayohusu fistula baada ya kutangazwa kwenye kampeni ya kuwaelimsisha wakazi wa mji wa Geita kuelekea kilele cha siku ya fistula duniani Mei 23. Nambari hiyo ni kwa wateja wa Vodacom pekee.Vodacom na Vodafone ya Uingereza hugharamia matibabu bila malipo kwa wagonjwa wote wa fistula wanaoitibiwa katika hospitali ya CCBRT.

RAIS JAKAYA KIKWETE ALIPOTEMBELEA BANDA LA NSSF

$
0
0
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkrugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau wakati alipowasili kwenye maonesho ya Wiki ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii mjini Dodoma. 


Rais Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Mkrugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk Ramadhan Dau alipotembelea banda la NSSF wakati wa kufunga maonesho ya Wiki ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma. Wa pili kushoto ni Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka. (Na Mpiga Picha Wetu)


 Rais Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifandji ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori wakati alipotembelea banda la NSSF katika maonesho ya Wiki ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyofanyika mjini Dodoma
 Rais Jakaya kikwete akikaribishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shiorika la taifa la hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhani Dau alipowasili katika banda la NSSF. Kulia ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifandji ya Jamii (NSSF), Crescentius Magori.
 Mh. Rais Jakaya Kikwete akisoma jarida linaloonyesha kazi za NSSF.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau akifafanua jambo wakati wa mahojiano na waandishi wa habari.

TASWA FC YAWAFUNGA TIMU YA MPIRA YA MABONDIA KWA TABU 2.1

$
0
0

Bonia Daudi Muhuzi akishindana na Mbuyu wa timu ya TASWA FC Majuto Omari wakati wa mpambano wao
Kocha wa kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Nchini Rajabu Mhamila ' Super D' akisisitiza jambo wakati wa mapumziko picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mchezaji wa timu ya Taswa akipambana na bondia kuwania mpira
SUPER D BOXING COACH AKISISITIZA JAMBO WAKATI WA MAPUMZIKO WA MCHEZO HUO
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images