Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46379 articles
Browse latest View live

MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA KIJIJI CHA LAMADI – BUSEGA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akionyesha usinga na mkuki ambavyo alipewa na wazee wa Kisukuma wa Busega katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Lamadi Machi 2, 2016. Wazee hao pia walimbatiza jina la Massanja.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutanowa hadhara katik kijiji cha Lamadi wilayani Busega Machi 2, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi wa Lamadi wilayani Busega kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara wenye uwanja wa michezo Machi 2, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mbunge wa Busega Dkt Raphael Chegeni (kushoto) na Mbunge wa zamni wa jimbo hilo, Dkt Titus Kamani ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Simiyu wametangaza rasmi kuzika tofauti zao na kushirikiana kuleta maendeleo kwenye jimbo hilo. Pichani viongozi hao wakiwadhihirishia wananchi kuwa hawana chukui wala ugomvi tena na kuwa uchaguzi umekwisha katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa kwenye kijiji cha Lamadi wilayni Busega Machi 2, 2016. .
Mbunge wa Busega Dkt Raphael Chegeni (kushoto) na Mbunge wa zamni wa jimbo hilo, Dkt Titus Kamani ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Simiyu wametangaa rasmi kuzika tofauti zao na kushirikiana kuleta maendeleo kwenye jimbo hilo. Pichani viongozi hao wakiwadhihirishia wananchi kuwa hawana chukui wala ugomvi tena na kuwa uchaguzi umekwisha katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa kwenye kijiji cha Lamadi wilayni Busega Machi 2, 2016.

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA MKUTANO WA17 WA KAWAIDA WA WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI JIJINI ARUSHA

$
0
0
Kijana Simon Sahaya Mollel (18) wa Shule ya Sekondari ya Mzumbe ya mjini Morogoro akionesha dola 1500 alizopewa kama zawadi baaya ya kuibulka mshindi wa kwanza wa kuandika Inshawakati wa Mkutano wa 17 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Mashariki jijini Arusha leo Machi 2, 2016.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini ya Kanuni za Madili ya Mfuko wa Sekta Binafsi wakati wa Mkutano wa 17 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Mashariki jijini Arusha leo Machi 2, 2016.
Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda akijiandaa kuweka saini ya Kanuni za Madili ya Mfuko wa Sekta Binafsi wakati wa Mkutano wa 17 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Mashariki jijini Arusha leo Machi 2, 2016

Rais Paul Kagame  wa Rwanda akiweka saini ya Kanuni za Madili ya Mfuko wa Sekta Binafsi wakati wa Mkutano wa 17 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Mashariki jijini Arusha leo Machi 2, 2016.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya akiweka saini ya Kanuni za Madili ya Mfuko wa Sekta Binafsi wakati wa Mkutano wa 17 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Mashariki jijini Arusha leo Machi 2, 2016
Wanafunzi walioshinda mashindano ya Insha ya EAC wakipata selfie na viongozi baada ya Mkutano wa 17 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Mashariki jijini Arusha leo Machi 2, 2016
Watoto walioshinda wakijipiga picha kwa simu na marais wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.PICHA NA IKULU

DONDOO ZA MAGAZETI

LEO MAGAZETINI YALIYOJIRI NYUMA NA MBELE KWA UFUPI

$
0
0

Add caption



--

RAIS DKT.MAGUFULI NA RAIS UHURU KENYATTA WAWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA BARABARA YA ARUSHA-HOLILI/TAVETA-VOI YA KM 234.3

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli leo aweka jiwe la msingi la Ujenzi wa barabara ya Arusha- Holili/Taveta-voi (km 234.3) kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyatta katika eneo la Tengeru jijini Arusha. 
Muonekano wa Barabara ambayo jiwe la msingi linawekwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyatta.







NAIBU WAZIRI MHE.POSSI KATIKA ZIARA YA KUTEMBELEA SHULE NA VITUO VYA WATU WENYE ULEMAVU MKOANI MANYARA.

$
0
0
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akizungumza na wanafunzi na uongozi wa shule ya msingi Katesh “A” na “B” (hawapo pichani) wakati alipofanya ziara shuleni hapo ili kuona hali ilivyo katika kitengo cha watoto wenye mahitaji maalum, Machi 2, 2016.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akisalimiana na watoto wenye ualbino wanaolelewa na kituo cha 4 Angle Disabled Children kilichopo Wilaya ya Haydom Mkoani Manyara wakati wa ziara yake ya kutembelea vituo, shule na vyuo vya watu wenye ulemavu.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa na Kituo cha kulelea watoto wenye Ualbino cha 4 Angle Disabled Children kilichopo Wilaya ya Haydom Mkoani Manyara wakati wa ziara yake kituoni hapo. 
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MHADISI GERYSON LWENGE AZINDUA MRADI WA CHANZO CHA CHEMICHEMI YA KISIMENI MKOANI KILIMANJARO.

$
0
0
Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Lwenge akiondosha kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa Maji wa chanzo cha maji cha Chemichemi ya Kisimeni.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru ,akimuongoza Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge alipofika kwa ajili ya uzidunzi wa mradi wa chanzo cha maji cha Kisimeni.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru ,akitoa maelezo kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge juu ya mradi wa chanzo cha maji cha Kisimeni .kushoto kwake ni Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Novatus Makunga.wengine ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa MUWSA,Prof,Faustine Bee,(kushoto) na anayemfuatia ni Mkurugezi wa Halamshauri ya Manspaa ya Moshi,Jesh Lupembe.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru ,akitoa maelezo kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge juu ya mradi wa chanzo cha maji cha Kisimeni 

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru ,akitoa maelezo ya hatua mbalimbali yanapo chukuliwa maji kutoka katika Chemichemi ya Kisimeni kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge alipofika kwa ajili ya uzidunzi wa mradi wa chanzo cha maji cha Kisimeni .
Meneja ufundi wa  Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi MUWSA,Mhandisi Paatrick Kibasa akimueleza Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Geryson Lwenge namna ambavyo maji yanayopatikana katika chemichemi ya Kisimeni yanavyotibiwa kabla ya kwenda kwa mtumiaji wa mwisho.
Waziri Lwenge akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Moshi mjini,Jafary Michael walipokutana katika uzinduzi wa mradi huo.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Lwenge akitia saini katika kitabu cha wageni alipofika katika mradi wa Chemichemi ya Kisimeni kwa ajili ya uzinduzi.anayeshuhudia ni mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,Joyce Msiru.


Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Lwenge akiwasili katika viwamja vya shule ya sekondari ya Longuo kwa ajili ya kuzungumza na wananchi wa eneo hilo watakaofaidika na uzinduzi wa mradi huo wa maji.
Vijana wa Skauti wakimvisha Skafu Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Mhandisi Lwenge alipowasili uwanjani hapo.
Vijana wa Skauti wakionesha umahiri wao mbele ya Waziri Lwenge.
Diwani wa kata ya Uru Kaskazini,Wilhad Kitally akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa chanzo cha maji chemi chemi ya Kisimeni.
Mameneja wa idara mbalimbali katika Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,wakiwa katika uzinduzi huo.
Makamu mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Prof Faustine Bee akizungumza katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Joyce Msiru akitoa taarifa ya mamlaka hiyo kwa Mh,Waziri wa maji na umwagiliaji ,Mhandisi Geryson Lwenge pamoja na taarifa ya mradi wa maji ya Chemichemi ya Kisimeni ambao umetekelezwa ndani ya siku 100.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Joyce Msiru akikabidhi taarifa ya mamlaka hiyo kwa Mh,Waziri wa maji na umwagiliaji ,Mhandisi Geryson Lwenge.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akizungumza katika uzinduzi huo.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Anthony Mtaka akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo.
Mbunge wa jimbo la Moshi Vijijini ,Anthony Komu akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Mhandisi Geryson Lwenge akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji yanayotokana na Chemichemi ya Kisimeni.
Wanafunzi wa Shule ya msingi ya Longuo wakitoa burudani ya wimbo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa maji wa Kisimeni.
Walimu wa shule ya msingi Longuo wakiimba shairi wakati wa uzinduzi wa mradi huo.
Mkurugenzi wa MUWSA ,Joyce Msiru akiwatunza waimbaji wa kikundi cha Msanja duzi kilichotoa burudani katika uzinduzi huo.
Mkaguzi wa Mahesabu wa ndani wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Benson Maro akiwatunza waimbaji wa kikundi cha Msanja.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Lwenge akizindua rasmi mradi wa maji katika kata Uru kaskazini.
Waziri Lwenge akimbebesha ndoo mmoja wa wakazi wa Longuo mara baada ya kufanya uzinduzi wa mradi huo.
Mgeni rasi katika uzinduzi huo ,Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Geryson Lwenge akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi,mameneja wa mamlaka hiyo na viongozi wengine waliofika katika uzinduzi huo.
Wakuu wa wilaya ,Anhtony Mtaka,(wilaya ya Hai) Novatus Makunga (wilaya ya Moshi mjini ) na Mbunge wa Moshi vijijini Anthony Komu wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

NAFASI YA KAZI.

$
0
0
tangazo-la-kaziMuzecom.com is the number one online marketing company in Tanzania. We are looking for someone who is addicted to social media to manage our social media accounts. His/Her responsibilities will include uploading images and videos to social media accounts and to upload videos to our new website .

kunanileo.com We are looking for someone who can quickly think on his/her feet and come up with catchy and engaging titles for our videos and social media contents If you believe you are the right person for this position, send your CV to muzegroup@gmail.com or call +255 622 430 083 for more information.

CCM MKOA WA ARUSHA YAMCHAGUA LEKULE KUWA MWENYEKITI ,HUKU SHABANI MDOE AKIIBUKA KATIBU MWENEZI

$
0
0
SAM_7665
Mwenyekiti mpya wa ccm mkoa wa Arusha   Maiko Lekule aliyepata kura 515akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi wa kiti hicho hivi karibuni jijini Arusha(Habari  Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_7696
Katibu mwenezi wa chama hicho Mkoa wa Arusha Shabani Mdoe aliyeshinda na fasi hiyo kwa kupata kura 36 ambaye kwa taaluma ni mwandishi wa habari akitoa neno la shukurani kwa wajumbe wa mkutano huo mara baadaa  ya kutangazwa rasmi kushinda nafasi hiyo
SAM_7636
Msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya ccm taifa Stephen Wassiraakitangaza rasmi nafasi ya mwenyekiti wa mkoa ambapo pia aliwataka wanaccm kuhakikisha wanashirikiana
SAM_7656
Mjumbe wa NEC taifa toka wilaya ya Monduli Namelock Sokoine akizungumza katika mkutano huo mara baada ya uchaguzi kuisha ambapo aliwataka wanaccm kuchapa kazi na kuhakikisha wanawashuhulikia mamluki waliopo ndani ya chama hicho
SAM_7676
Mjumbe wa NEC taifa toka wilaya ya Monduli Namelock Sokoineakiteta jambo na Mbunge viti maalum Catherine Magige katika mkutano huo.
SAM_7680
Emanuel Makongoro ambaye alikuwa akiwania nafasi wa uwenyekiti wa mkoa akifurahia jambo na katibu wa wazazi mkoa wa Arusha Mayasa Kimbau 
SAM_7689
Semi Kiondo ambaye alikuwa akiwania nafasi ya ukatibu mwenezi akizungumza mara baada ya uchaguzi kuisha ambapo alihaidi kutoa ushirikiano wake kwa chama cha mapinduzi huku akishirikiana na viongozi waliochaguliwa
SAM_7684
viongozi wa chama cha mapinduzi wakiwa katika pozi la picha
SAM_7630
Wajumbe wa mkutano
 CHAMA cha Mapinduzi ( CCM)mkoa wa arusha kimefanya uchaguzi wa mwenyekiti wa mkoa  na kufanikiwa kumchagua  Maiko Lekule aliyepata kura 515 dhidi ya mgombea mwenza Emanuel Makongoro aliyepata kura 338,huku katibu mwenezi wa chama hicho akichaguliwa kuwa ni Shabani Mdoe aliyeshinda na fasi hiyo kwa kupata kura 36.

Aidha katika uchaguzi huo wa mwenyekiti  wajumbe  halisi waliopaswa kuhudhuria  ni 960 ambapo waliohudhuria ni 903 huku wajumbe halisi waliopiga kura wakiwa ni 861.

Akitangaza matokeo hayo jana msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya ccm taifa Stephen Wassira alisema kuwa uchaguzi huo umefanyika kwa huru na amani na hivyo ana imani kuwa uongozi huo utakiletea mabadiliko makubwa chama cha mapindizi katika mkoa huo.

Alisema kuwa katika mkoa wa arusha matatizo ya umoja  na tofauti yapo na kwamba atakayemaliza mzizi huo ni mwenyekiti aliyepatikana kwa kuhakikisha kuwa anawaunganisha wana ccm ili wawe kitu kimoja.

“hapa arusha yapo matatizo sana naomba tu nitumie fursa hii kumtaka mwenyekiti aliyeshinda kuhakikisha kuwa anakijenga chama na ndie atakayeifanya arusha iungwe mkono na watu wote hatutaki kusikia tena kuwepo kwa makundi ya kuvunja chama muda wa uongozi wa mwaka mmoja ni mkubwa sana katika kukirejesha chama sehemu yake”alisema Wassira.

Alileleza kuwa kwa arusha hawataki  kusikia ccm  inayoendeshwa kwa fedha ya mtu binafsi wala kampuni bali wanaitka ccm yao irudishe kwa wananchi na jamii iweze kunufaika na rasilimali zake sio kwa ajili ya watu binafs ambao  ndio wamekuwa wakikisaliti chama.

Kwa upande wake mwenyekiti aliyechaguliwa Maiko Lekule  akitoa neno la shukrani  alisema kuwa anawashukuru wajumbe hao kwa kumchagua na kwamba nafasi aliyopewa hataweza mwenyewe kuimaraisha chama hicho ambacho kipo mahututi hivyo anaomba ushirikiano uwepo.

Lekule alisema kuwa chama hicho kinahitaji kufanyiwa ukarabati mkubwa sana hivo kamati za siasa ,wenyeviti na kamati inabidi waungane kwa pamoja kukijenga chama hicho kwa upya ili kirudi katia hali yake.

“mimi nahidi tu ntakiimarisha chama hiki kwa kushirikiana na wenzangu ila niwaombe tu mamluki wote walioko kwenye hiki chama ambao ndio wasaliti wakuu waondoke mapema wenyewe na kama hawataondoka tutawaondoa sisi”alisema Lekule.

Nae katibu mwenezi Shabani mdoe ambaye ni mwandishi mwandamizi wa gazeti la Uhuru  aliwashukuru wajumbe hao kwa kumuamini kwa kumchagua na kuahidi kuwa atatumia taaluma yake ya uhabari kuimarisha chama hicho kwani waandishi wana nguvu kubwa ya kujenga palipobomoka.

Siku Ya Sikio Duniani

MRADI WA KUTOKOMEZA VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA WAZINDULIWA

$
0
0
  Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom nchini, Balozi Mwanaidi Maajar akihutubia katika  uzinduzi wa Mradi wa Moyo awamu ya Pili unaofadhiliwa na mtandao wa simu nchini Vodacom katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika wilayani Sengerema mkoani Mwanza juzi.
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao akihutubia katika  uzinduzi wa Mradi wa Moyo awamu ya Pili unaofadhiliwa na mtandao wa simu nchini Vodacom katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika wilayani Sengerema mkoani Mwanza juzi.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk.Hamis Kigwangalla akihutubia wakati wa hafla ya  uzinduzi wa Mradi wa Moyo awamu ya Pili unaofadhiliwa na Vodacom Foundation iliyofanyika wilayani Sengerema mkoani Mwanza juzi.
 Mkazi wa Sengerema mkoani Mwanza, Lawrencia John akimuonyesha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk.Hamis Kigwangalla,Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom Foundation, Balozi Mwanaid Sinare Maajar, Mkurugenzi wa Vodacom nchini, Ian Ferrao(kulia) mtoto wake Mwalu John aliyejifungua baada ya kupata msaada wa mradi wa Moyo unaofadhiliwa na Vodacom Foundation jana katika uzinduzi wa Mradi huo awamu ya pili mkoani humo.
Kaimu Mkurugenzi wa USAID nchini, Bethany Haberer akisoma hotuba  wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Moyo awamu ya Pili unaofadhiliwa na Vodacom Foundation iliyofanyika wilayani Sengerema mkoani Mwanza juzi.

NAIBU Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamis Kigwangala amezindua mradi wa kutokomeza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga nchini,Mradi huo umezinduliwa jana wilayani Sengerema mkoani Mwanza ambapo unafadhiliwa na taasisi ya Vodacom Foundation kwa kushirikiana na mashirika ya kimataifa ya USAID,Path Finder na Touch Foundation.
Mradi huu ambao unajulikana kama”MOYO”awamu ya pili umelenga kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha sekta ya afya nchini na adhma ya kutokomeza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga nchini.

Akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika mjini Sengerema Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamis Kigwangala amesema kuwa mradi huu unaenda sambamba na malengo ya serikali ambayo imejipanga kuhakikisha matukio ya vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga vinavyojitokeza wakati wa kujifungua kutokana na ukosefu wa huduma za matibabu vinatokomezwa.

“Katika kukabiliana na tatizo hili ambalo limetukutanisha  hapa siku ya leo na kuboresha huduma za matibabu nchini,serikali inatarajia kujenga wodi za akina mama wajawazito katika vituo vyote vya Afya nchini vilivyopo vijijini na mijini hivyo nawapongeza kwa kuiunga mkono serikali na natoa wito kwa wananchi wote kuelewa jitihada hizi na kuvitumia vituo hivi na huduma hizi ili kufanikisha lengo lililokusudiwa”.Alisema Dk. Hamis Kigwangala.

Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania, Ian Ferrao amesema tangu mradi wa MOYO awamu ya kwanza ulianza kutekelezwa mwaka 2009 na umefanikiwa kuandikisha wanawake zaidi ya elfu 16,000 katika vituo vya afya, na kuokoa maisha ya akina mama wajawazito na Watoto zaidi ya 450.
Alisema zipo baadhi ya changamoto kadhaa za baadhi ya akina mama wajawazito kutojifungua katika vituo vya Afya, ambapo licha ya changamoto hizo  mradi huo umewezesha mafunzo  kwa wahudumu wa Afya wa ngazi ya Jamii wanaopita kila kaya kutoa elimu, ili kubadili mitazamo hasi ya baadhi ya akina mama kutofika kwenye vituo vya afya kupatiwa huduma za uzazi.

“Kupitia mradi huu ambao pia umelenga kurejesha fadhila kwa wateja wetu tutagharamia usafiri wa akina mama wajawazito kupitia huduma ya M-Pesa kama ambavyo ilikuwa kwenye awamu ya kwanza ya mradi ili waweze kufika kwenye vituo vya afya kupata matibabu haraka pindi patakapohitajika msaada “,Alisema.

Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom Foundation, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar, amesema pamoja na mafanikio  ya kiafya  yaliyopatikana kwa kukabiliana na ugonjwa wa Fistula na huduma ya ujumbe mfupi wa maneno ya kuelimisha akina mama masuala ya uzazi kupitia mradi wa WAZAZI NIPENDENI kusaidia akina mama wengi, vilevile zoezi hilo limekuwa likiviwezesha vikundi vya kuweka na kukopa vya Wanawake na kuwapatia mafunzo ya kuwawezesha kijikwamua  kiuchumi.

“Kupitia matumizi ya teknolojia ya huduma za simu za mkononi, kampuni imeweza kuboresha maisha ya wananchi.Nawapongeza wadau wote ambao tumekuwa tukishirikiana nao hasa Shirika la Msaada la watu wa Marekani (USAID).

Mkazi wa Sengerema Mwanza Lawrencia John, ambaye ni mmoja wa wanawake walionufaika  aliupongeza mradi huu na kusema ulimsaidia alipokuwa kwenye hali ya uchungu wakati wa kujifungua mtoto wake wa kwanza. Alipopiga simu aliweza kusaidiwa mara moja na amejifungua salama kabisa na anatoa wito kwa wadau wengine waweze kujitokeza kunufaika na huduma hii.

MAGUFULI: MARAIS WA EAC WAMEFANYA KOSA SANA KUNICHAGUA MWENYEKITI

MFUKO WA HIARI WA PSPF WANUFAISHA MAMIA YA WAKAZI WA UKONGA

$
0
0
Afisa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Delphin Richard akizungumza na wananchi wa Ukonga pamoja na maeneo mengine ya mji wa Dar es Salaam kuhusu Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa Semina ya Ujasiriamali Ukonga jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Delphin Richard akifafanua jambo kwa wajasiriamali kuhusu Mfuko wa Hiari wa PSPF jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mjasiriamali kwanza Enterprises Dr. Didas Lunyungu.
Wajasiriamali kutoka maeneo ya Ukonga na maeneo mengine ya mji wa Dar es Salaam wakisikiliza kwa makini elimu iliyokuwa ikitolewa kuhusu uchangiaji wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa semina ya wajasiriamali jana jijini Dar es Salaam
Afisa Masoko kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bibi. Sarah Adebe akitoa elimu kwa wachangiaji wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa kuandikisha wachangiaji wapya wa mfuko huo jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bibi. Sarah Adebe akitoa elimu kwa wachangiaji wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakati wa kuandikisha wachangiaji wapya wa mfuko huo jana jijini Dar es Salaam.
Afisa kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Mrisho Ngongo (kulia) akitoa fomu za kujisajiri kwa wachangiaji wapya wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF jana jijini Dar es Salaam
Baadhi ya wanachama wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF wakiwa katika mstari kwa ajili ya kukamilisha hatua za mwisho za kujisajiri katika mfuko huo jana jijini Dar es Salaam.
Afisa Masoko kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bibi. Sarah Adebe (kushoto) akikagua fomu za uanachama wa hiari katika Mfuko wa Hiari wa PSPF baada ya kusajili wanachama wapya jana jijini Dar es Salaam.Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo.
…………………………..

Na: Genofeva Matemu – Maelezo


Wananchi zaidi ya 500 kutoka zoni ya ukonga jijini Dar es Salaam wamejitokeza na kujisajiri kuwa wanachama wa hiari katika mfuko wa hiari wa PSPF ili kuweza kunufaika na mafao yatolewayo na mfuko huo.

Wananchi hao walipata fursa ya kujisajiri wakati wa semina ya ujasiriamali iliyofanyika siku ya jana maeneo ya Ukonga jijini Dar es Salaam na kuudhuriwa na wananchi wapatao 1600 kutoka zoni ya Ukonga na maeneo mengine ya jiji la Dar es Salaam na mikoa ya jirani.

Akizungumza wakati wa semina hiyo Afisa Uendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Bw. Delphin Richard amesema kuwa mfuko wa hiari wa PSPF uliundwa kwa ajili ya kutoa fursa kwa wananchi kuwa na akiba ya ziada kwa kutoa uhuru kwa mwanachama kuchangia kwa kutegemea upatikanaji wa kipato cha ziada kitakachomwezesha kujiwekea akiba.

Bw. Richard amesema kuwa lengo la PSPF ni kushiriki katika masuala mbalimbali ya kijamii ili kuweza kutoa elimu ya mfuko wa hiari wa PSPF hivyo kutoa nafasi kwa wajasiriamali, wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, na watu binafsi kuchangia katika mfuko wa hiari kipato chao cha ziada kwa ajili ya akiba ya ziada.

Kwa upande wake Afisa Masoko Bibi. Sarah Adebe amesema kuwa jamii imekua na muitikio mkubwa wa kujisajiri katika mfuko wa hiari wa PSPF kwani mfuko huo unatoa huduma kwa kuchangia gharama ndogo hivyo kuwanufaisha wanachama hasa wa kipato cha chini.

Naye Mjasiriamali kutoka zoni ya Ukonga Bi. Doris Kimaro amesema kuwa ujio wa elimu ya mfuko wa hiari wa PSPF ni mafanikio makubwa katika familia yake kwani atatumia nafasi aliyoipata kwa kuchangia kipato chake cha ziada ili aweze kunufaika na fao la elimu litakalomuwezesha kukidhi mahitaji yake ya baadae.

Mfuko wa hiari wa PSPF umelenga kusaidia jamii kwa kuwa na mafao saba ambayo ni fao la elimu, fao la ujasiriamali, fao la uzeeni, fao la kifo, fao la ugonjwa/ulemavu, fao la kujitoa na fao la matibabu.

UNCDF LAUNCHES REGIONAL CONSULTATIONS ON MUNICIPAL FINANCE

$
0
0
-First meeting in Dar es Salaam focuses on local finance challenges in African LDCs

In collaboration with the Financing for Development Office of the United Nations Department of Economic and Social Affairs and the Government of Tanzania, UNCDF launched a global series of expert group consultations on municipal finance in Dar es Salaam, Tanzania on 29 February – 1 March 2016.

The meeting brought together a unique set of practitioners, local government representatives, academics, policy makers and the private sector from African countries, as well as UN entities and other development partners. In an interactive format, experts exchanged their experiences and suggested policy measures on how municipal governments especially in the Least Developed Countries can access long-term finance to implement the ambitious 2030 Agenda for Sustainable Development.

“According to figures from the United Nations, 1.2 billion people live in over 650 secondary cities in developing countries. Yet most government finance and development aid is directed to central government agencies whilst private finance often avoids local governments”, said David Jackson, Director of Local Development Finance at UNCDF. The Africa expert consultation is the first in a series of regional consultations that aim to pave the way for increased and more effective international cooperation on subnational finance as called for Addis Abba Action Agenda and reaffirmed in the preparation of the Habitat III Conference later this year.

The discussion delved deep into lessons learned from fiscal, political and administrative decentralization experiences across African LDCs, many involving UNCDF support. There was a consensus view that enabling and empowering local authorities to unlock resources for long-term finances requires a holistic approach to municipal finance. Sound financial management and improved internal revenue generation including through effective property taxes, user fees, and land value capture can pave the way for better access to private and public domestic finance.

“Collaboration between banks and local government in Africa has to step up. Both actors have to meet in a middle area called trust where they share strategy, ambitions and solutions” said Ms. Zienzi Musamirapamwe, Head of Public Sector, Corporate and Investment at Barclays South Africa. Central government support and a conducive governance environment are equally important and intergovernmental fiscal transfers will remain a key source of local government finance.
Participants noted that many municipalities in Africa have come a long way in getting their finances in order while promoting affordable access to essential services for all. Experts discussed the positive experiences of an increasing number of African cities such as Dakar and Kampala City, both of which have received investment grade ratings from well-known regional rating agencies. The progress of secondary African cities has also been reviewed and noted.

According to Khady Dia Sarr, Program Director, Dakar Municipal Finance Program, development is primarily local; and finance is one of the keys to development. “We have to strengthen local authorities in Africa to tap into capital markets to respond to the needs of populations.”

“Decentralization is essential, especially fiscal decentralization” said Youssouf Séga Konaté, Technical Adviser, Ministry of Decentralization of Mali. Experts also agreed that successful decentralization hinges on a carefully sequenced series of policy measures. It is a process that requires continuous assessment of what works and what doesn’t and policies can change down the road. The discussion also featured lively exchanges between local authorities and central government representatives, including on the appropriate level and types of fiscal transfers and the authority for municipalities to borrow. Participants agreed that good communication and buy-in from all stakeholders are crucial factors for success.

Mr. Shomary Mukhandi, Director, Regional Administration and Local Government – President’s Office in Tanzania, gathered from the discussions that there is a need to consider other feasible ways of financing local government infrastructure development projects to meet and reduce the fiscal gap between actual needs and available resources. “We have learnt some valuable lessons from participating in this key meeting. Pertinent issues have been raised in improving municipal finance that can be applied by local governments in Tanzania to stimulate and improve local economic growth.”

The consultation will result in a publication that summarizes major findings and provide some general guidelines for policy makers at the international, national and local levels of the Least Developed Countries. In addition, the published results will feed into the discussions leading to the Habitat III conference later this year, which should focus on how to implement the global agenda through cities.

Serikali kujenga machinjio ya kisasa Vingunguti

$
0
0



Na Raymond Mushumbusi, MAELEZO

Serikali imejipanga kujenga machinjio ya kisasa katika eneo la Vingunguti  Jijini Dar es Salaam ili kuondoa changamoto zilizopo machinjioni hapo ikiwa ni pamoja na kulinda afya za wachinjaji na walaji wa nyama.
.
Akiongelea mipango hiyo kwa njia ya simu Msemaji wa Manispaa ya Ilala Bi.Tabu Shahibu amesema Halmashauri iko katika mchakato wa kutangaza zabuni kwa makampuni yatakayoweza kujenga machinjio hayo kwa kiwango kinachotakiwa.

“Tupo katika harakati za kutafuta mkandarasi wa kujenga machinjio na hivi karibuni tutatangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi huo”

“ Napenda kuwahakikishia kwamba tutafanya jitihada zote za kumpata mkandarasi mapema ili tuanze mapema ujenzi huu wa machinjio mapya na kuondokana na changamoto zinazokabili machinjio yaliyopo”Alisema Bi Tabu.

Aidha, Bi Tabu Shaibu amesema kuwa kabla ya kujenga machinjio mapya wanaendelea na ujenzi wa mabanda ya machinjio, njia za kushushia ng’ombe ,bucha na kupanua eneo la machinjio na wameshapima na kufanya tathimini ya gharama ambazo zitatumika katika marekebisho hayo.

Mpango huu umekuja mara baada ya ya agizo la mawaziri, akiwemo Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mhe. Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Hamis Kigwangalla na Waziri wa Nchi ofisi ya Raisi TAMISEMI MHE. George Simbachawene walipotembelea machinjio ya Vingunguti Januari 2 mwaka huu.

Machinjio ya Vingunguti yalianza kutumika tangu miaka ya 1950 ikiwa inahudumia idadi ya watumiaji wa mazao ya wanyama waliokuwa kwa wakati ule. Machinjio hayondio bado  yanatumika hadi sasa wakati idadi ya watumiaji wa mazao ya nyama wameongezeka  hivyo kukumbana na changamoto mbalimbali. Ili kukabiliana na changamoto hiyo Serikali imepanga kuyarekebisha yaliyopo na kujenga mapya na ya kisasa.

MFUMO DUME NI KIKWAZO CHA WANAWAKE KUTOKUMILIKI ARDHI - ANNA MGHWIRA

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Anna Mghwira

Na Fredy Njeje-Blogs za Mikoa
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Anna Mghwira amesema umiliki wa ardhi kwa wanawake hapa nchini bado unasuasua kutokana na mfumo dume uliopandikizwa tokea miaka ya nyuma.

Bi Mghwira ambaye alikuwa mwanamke pekee aliyegombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015 kupitia ACT Wazalendo, ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Blogs za Mikoa kuhusu sababu za wanawake wengi nchini kutomiliki raslimali muhimu ya ardhi.

Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2012 idadi ya wanawake hapa nchini ni asilimia 51% lakini wanaomiliki ardhi ni asilimia 19% tuu jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa wanawake wengi bado hawamiliki ardhi ukilinganisha na wanaume.

''Tatizo lililopo hapa nchini ni tatizo la kitamaduni, ilikuwa kazi ya mwanamke akishazaliwa ni alelewe na baadaye akiolewa anaendeleza kizazi huko alikoolewa lakini kumiliki ardhi ni mfumo mpya ambao unatoa fursa sawa katika kumiliki raslimali hiyo muhimu kwa ajili ya kuitumia katika shughuli za kiuchumi''Amesema Mghwira.

Bi Mghwira ameenda mbali zaidi na kuona tatizo la umiliki wa ardhi pia lipo kwa upande wa wanaume hasa inapotokea suala la makubaliano na mwekezaji ndiyo maana kuna kesi nyingi kuhusiana na wawekezaji na wananchi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Baadhi ya wanaume waliopo katika mmoja ya Kijiji Wilayani Lushoto Mkoani Tanga wakiongea na Blogs za Mikoa kutoa maoni yao ya namna ambavyo walikuwa hawakubaliani na wanawake kumiliki Ardhi

Katika jitihada za kuunga mkono Serikali katika jitihada mbalimbali za kutatua kero kwa wananchi Bi Mghwira amesema kwamba mara kwa mara amekuwa akielimisha wanawake hapa nchini katika kutambua haki zao na kujikwamua na umasikini.

Hata hivyo ameitaka serikali kutizama upya sheria ya ardhi na pia kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na umiliki wa ardhi ili kuwezesha wananchi kutambua kuwa umiliki wa ardhi ni wa haki kwa pande zote kwa upande wa wanaume na wanawake.

WAZIRI NAPE MGENI RASMI TAMASHA LA PASAKA JIJINI MWANZA

$
0
0
Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotions,Alex Msama ambaye pia ni Mwenyekiti wa tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni jijini Mwanza,akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari alipokuwa akizungumza nao Ofisi kwake,Kinondoni jijini Dar leo.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Pasaka  linalotarajiwa kufanyika jijini Mwanza mnamo Machi 27.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maaandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama,amebainisha kuwa Waziri Nape amekubali kuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo ambalo litaanzia Geita Machi 26 na kumalizia Kahama Machi 28.

Msama alisema kamati yake inaendelea na maandalizi ya kuelekea tamasha hilo ambalo litashirikisha waimbaji mbalimbali hapa nchini.“Maandalizi kuelekea Tamasha la Pasaka yanaendelea vema, hivyo wakazi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa wajiandae kupokea ujumbe wa neno la Mungu kupitia viongozi wa dini na waimbaji wa muziki wa Injili,” alisema Msama.

Msama alisema baadhi ya waimbaji waliothibitisha kushiriki tamasha hilo ambao ni pamoja na Rose Muhando, Bonny Mwaitege, Upendo Nkone, Jesca BM Honore, Christopher Mwahangila, Joshua Mlelwa, Sifael Mwabuka, Jenipher Mgendi, Kwaya ya AIC Makongoro na Kwaya ya Wakorintho Wapili.

Msama pia alidokeza kuhusiana na suala zima la viingilio,alisema kuwa viingilio hivyo vinaendana na tukio hilo ambalo mbali ya kumuimbia na kumtukuza Mungu pia lina dhamira ya kusaidia jamii yenye uhitaji maalum.

“Nawaomba wakazi wa mikoa Geita, Mwanza na Shinyanga kujitokeza kwa wingi ili kufanikisha tamasha hilo,” alisema Msama.

Msama alisema kupitia viingilio vya tamasha hilo wanatarajia kutoa kipaumbele kwa wakazi wa mikoa itakayopitiwa na tamasha kwa kupatiwa  baiskeli zaidi ya 100 za walemavu, ambazo zitagawiwa mikoa mbalimbali.

Wasambazaji wa Filamu Tanzania waipongeza Serikali

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Bw. Saimon Mwakifamba (Kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati akitoa pongezi za Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) kwa Serikali ya Awamu ya Tano katika mkutano na waandishi wa habari.picha na Jacquile Mrisho MAELEZO


Na Jacquiline Mrisho, MAELEZO

Chama cha Wasambazaji wa Filamu Tanzania kimeipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa juhudi zake inazozifanya katika kupambana na uharamia kwenye sekta ya filamu Tanzania.

Hayo yamesemwa na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Bw. Saimon Mwakifamba alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam kuhusu kuunga mkono juhudi madhubuti za Serikali za kudhibiti uharamia wa kazi za filamu haswa kwenye eneo la mauzo la sokoni Kariakoo.

“Kwa takribani miaka mitatu sasa tumekuwa na kilio cha wazi kwa Serikaliya Tanzania iliitusaidie kuwabana wahujumu wa mapato ya nchi unaofanyika kupitia njia za kiharamia zinazotumika kuuza kazi za filamu ndani na nje ya nchi.Kilio chetu kimesikilizwa natunaamini tija ya soko la filamu litaanza kuonekana ndani ya muda mfupi kuanzia sasa.”AlisemaMwakifamba.


Aidha, Mwakifamba amefafanua kuwa, idadi ya watu walioulizia kuwekeza katika usambazaj iimeongezeka kutokana na kazi ya usambazaji kufanyika kwa uhalali baada ya juhudi za Serikali za kupunguza uharamia unaofanyika kwenye usambazaji wafilamu.Pia,ametoa rai kwa Serikali kutolegeza kamba bali kuzidi kulidumisha zoezi hili la kudhibiti mianya yote ya uharamia ili wasambazaji watumie utaratibu unaotakiwa na Serikali katika usambazaji wa kazi za filamu.

Kwa kipindi kirefu sasa wasanii nchini wamekuwa wakipambana na unyonywaji wa kazi zao za filamu unaofanywa na wasambazaji wa filamu wasio halali ambao wanapunguza mapato ya wasanii na taifa kwa ujumla.

MAKUMBUSHO YA TAIFA NA SWEDEN WAANDAA ONESHO LA MATUMIZI YA ARDHI NA HADHARI ZAKE.

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Prof Audax Mabula akizungumza na waandishi wa habari,hawapo pichani.
 Pichani kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Prof Audax Mabula akizungumza na waandishi wa habari.

 Pichani kushoto ni Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw Achiles Bufure, kushoto kwake ni Mratibu wa Onesho la Matumizi ya Ardhi na Athari zake Bi Adelaide Salema pamoja na wanahabari mbalimbali wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho, hayupo pichani.
Pichani ni ni mtafiti mzamivu katika taaluma ya mazingira na matumizi bora ya ardhi kutoka Sweden Bi. Emma Li Johansson akizungumza na waandishi wa habari. hawapo pichani.


Na mdau Sixmund J. Begashe
Makumbusho ya Taifa Tanzania kwa ushirikano na Chuo Kikuu cha Lund Sweden wameandaa onesho la pamoja kuhusu mabadiliko ya matumizi ya ardhi katika bonde la Kilombero. Kwa mara ya kwanza utafiti unatumia njia ya sanaa shirikishi katika kubainisha madhara ya umilikishaji wa ardhi kwa wawekezaji wakubwa dhidi ya jamii ya Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Makumbusho ya Taifa Prof Audax Mabula alitaja sababu ya onesho hili la Umoja ni kutoa elimu kwa umma juu ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi ambayo kwa upande mwingine husababisha migogoro ndani ya jamii.

’’Afrika ni moja ya maeneo ambayo yanahodhisha ardhi kwa gharama ndogo na kutoa malipo madogo kwa wafanyakazi. Hata hivyo watafiti wengi wamekuwa wanalalamikia hali hii ya umilikishaji holela ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa migogoro kwenye vyanzo asili na kuleta ushindani na changamoto katika jamii za maeneo athirika’’ Alisema Prof Mabula.

Prof Mabula aliongeza kuwa Watu wanayabadilisha mazingira hali ambayo huathiri watu na maisha yao. Mabadiliko ya tabia nchi, kupungua kwa maji na ubora wake, kupungua kwa mazalio ya samaki na wanyamapori, ongezeko la mifugo, vita baina ya wafugaji na wakulima ni baadhi tu ya matatizo yanayosababishwa na binadamu.

Nae Bi.Emma Li Johansson ambae ni mtafiti mzamivu katika taaluma ya mazingira na matumizi bora ya ardhi amesema onesho hili ni matokeo ya utafiti alioufanya huko Kilombero Mkoani Mprogoro kwa kutumia sanaa za maonesho kuruhusu watu kuelezea mtazamo wao juu ya matumizi na mgawanyo wa ardhi katika maeneo ya vijijini mwao.

”Lengo ni kujua namna vijiji vilivyobadilika tangu kukaribishwa kwa makampuni makubwa ya kilimo ya kigeni ambayo yamehodhi ardhi kubwa kwa ajili ya kilimo cha kisasa. Sanaa hii imetengenezwa kwa ushirikiano wa vijiji viwili athirika ambavyo vimeonesha muonekano wake wakati uliopita, sasa na mpango maendeleo kwa wakati ujao.” Alieleza Bi Emma

Akielezea program ya onesho, Mratibu wa Onesho hilo Bi Adelaide Salema amesema kuwa, pamoja na onesho hilo ,kutakuwa na mjadala kwa la lengo la kupaza sauti za wakulima wadogowadogo na kukusanya hadhara ya wadau wa kada mbali mbali katika muktadha huu kuzungumzia mabadiliko ya matumizi ardhi ili kuunda daraja baina yao na kuleta ufumbuzi wa kadhia hii.

Onesho hilo litafunguliwa rasmi tarehe 4 Machi 2016 saa tano kamili asubuhi na Bw. Jörgen Eriksson kutoka ubalozi wa Sweden nchini Tanzania katika Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni iliyopo Mtaa wa Shaaban Robert Kitalu Na. 6 mkabala na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) na litadumu kwa muda wa mwezi mmoja tu

UUZAJI WA TIKEKI ZA UWANJANI KWA MFUMO WA ELEKRONIKI KUANZA KUTUMIKA

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Makoye Alex Nkenyenge akizungumza wakati wa kikao baina ya Wizara, TFF na Kampuni ya MaxCom kuhusu matumizi ya mfumo wa Kielektroniki katka ukataji Tiketi kwa ajili ya kuingilia wakati wa mechi mbalimbali jana jijini Dar es Salaam. Mkakati huo ni utekelezaji wa agizo la Mhe. Waziri Mkuu alilolitoa wakati akiongea na wadau wa michezo hivi karibuni.
Mwakilishi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Boniphace Wambura (kulia) akichangia hoja wakati wa kikao baina ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, TFF pamoja na Kampuni ya MaxCom ili kujadili kuhusu uanzishwaji wa matumizi ya mfumo wa Kielektroniki katika ukataji Tiketi kwa ajili ya kuingilia wakati wa mechi mbalimbali leo jijini Dar es Salaam. Mkakati huo ni utekelezaji wa agizo la Mhe. Waziri Mkuu alilolitoa wakati akiongea na wadau wa michezo hivi karibuni.Kushoto ni Afisa Tehama wa wizara hiyo Nuru Bakari.
Mwakilishi wa Kampuni ya MaxCom Deogratius Lazaro (katikati) akifafanua jambo wakati wa kikao baina ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, TFF pamoja na Kampuni ya MaxCom ili kujadili kuhusu uanzishwaji wa matumizi ya mfumo wa Kielektroniki katika ukataji Tiketi kwa ajili ya kuingilia uwajnjjani wakati wa mechi mbalimbali leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Muhasibu wa TFF Daniel Msangi na kulia ni Mwakilishi mwenza wa MaxCom Erick Charles.
Mwakilishi wa Kampuni ya MaxCom Erick Charles (wapili kutoka kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao baina ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, TFF pamoja na Kampuni ya MaxCom ili kujadili kuhusu uanzishwaji wa matumizi ya mfumo wa Kielektroniki katika ukataji Tiketi kwa ajili ya kuingilia uwajnjjani wakati wa mechi mbalimbali leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Ugavi na Ununuzi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Cecilia Kasonga, Mwakilishi wa Kampuni ya MaxCom Deogratius Lazaro na Muhasibu wa TFF Daniel Msangi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kujjadili namna ya kuanza kwa matumizi ya mfumo wa Elekroniki katika ukataji wa tiketi za kuingilia uwanjani kwenye mechi mbalimbali. Kikao hicho kimejumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo,TFF na Kampuni ya MaxCom ambao ndiyo wataalamu wa kuendesha mfumo huu.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kujjadili namna ya kuanza kwa matumizi ya mfumo wa Elekroniki katika ukataji wa tiketi za kuingilia uwanjani kwenye mechi mbalimbali. Kikao hicho kimejumuisha wajumbe kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo,TFF na Kampuni ya MaxCom ambao ndiyo wataalamu wa kuendesha mfumo huu.
Viewing all 46379 articles
Browse latest View live




Latest Images