Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

TPB YATOA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA SACCOS KIGOMA, NI MPANGO WA KUINUA MITAJI YA WAJASIRIAMALI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya, (kushoto), akimpatia mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 75 Kaimu mwenyekiti wa Saccos ya Ishimwe Kigoma Bi.Gabriela Hangula wakati wa hafla ya kukabidhi fedha kwa vikudi vya benki za vijijini (VICOBA), mkoani humo,. 

Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma. John Ndungulu, Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania, (NEEC), Bi. Beng’ Issa na Afisa Mtendaji Mkuu, (CEO) wa Benki ya Posta Tanzania, Bw. Sabasaba Moshingi.Benki ya Posta imekabidhi jumla ya silingi milioni 175 kwa vikundi hivyo viwili ikiwa ni mpango wa kuwawezesha wananchi kwa kuwakooesha fedha kuinua mitaji yao chini ya udhamini wa baraza hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya (kushoto), akimpa mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 100 Mwenyekiti wa Saccos ya TWCC Kigoma, Dorothy Takwa. Wa pili kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma John Ndungulu, Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Uchumi Tanzania Bi. Beng’ Issa na Afisa Mtendaji wa Benki ya Posta Sabasaba Moshingi akishuhudia makabidhiano hayo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Sabasaba Moshingi akiongea na wana-saccos wa Manispaa ya Kigoma-Ujiji, kabla ya kuwakabidhi kiasi cha fedha Shs milioni 175/=kama mkopo ili kuinua mitaji yao. Kutoka kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, John Ndungulu, Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi Tanzania, (NEEC), Bi. Beng’ Issa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya.
Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo wa Benki ya Posta Tanzania, Henry Bwogi akimpa zawadi mmoja wa mwanachama wa Saccos, kulia ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano ya Benki Tanzania, Timotheo Mwakifulefule.

WAZIRI MKUU APOKEA MISAADA YA ZAHANATI, KOMPYUTA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa ambao unafanywa kwa ufadhili wa kampuni ya HUAWEI ya China , kijijini hapo, Februari 28, 2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Jordan Lugimbana. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea msaada wa kujenga zahanati na nyumba ya mganga kwenye kijiji cha Nandagala, wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi. 

Msaada huo wenye thamani ya dola za Marekani 55,000 (sawa na sh. Milioni 119.35)   umetolewa na kampuni ya Huawei Technologies yenye makao yake jijini Dar es Salaam.  Pia wametoa kompyuta za mezani (desktop) 25 pamoja na UPS  25 kwa ajili ya shule tano za sekondari wilayani humo. 


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo jana (Jumapili, Februari 28, 2016) Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei, Bw. Bruce Zhang alisema kampuni yake imetoa msaada huo ikiwa ni mwitikio wa sera ya Wizara ya Afya inayotaka kila kijiji kiwe na zahanati na kila kata iwe na kituo cha afya.


Wakati huohuo, kampuni ya mtandao wa simu ya Halotel ilimkabidhi  Waziri Mkuu hundi ya sh. Milioni 9/- ambazo ni mchango wao wa kumsaidia  Waziri Mkuu ambaye pia ni mbungewa jimbo la Ruangwa ili zisaidie kulipia familia zisizo na uwezo kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).


Akizungumza na wanakijiji hao kabla ya kukabidhi hundi hiyo, Meneja Mkuu Msaidizi wa Biashara wa Mkoa wa Lindi, Bw. Sebastian Innocent alisema: "Mchango huu utazihusu kaya 900 ambazo zinalipiwa sh. 10,000 kila moja. Kila kaya inatakiwa kulipia watu sita, hivyo tutaweza kuwafikia watu 5,400 kupitia mchango huu.


Alisema kampuni yao imejenga minara 50 katika mkoa wa Lindi ambapo 40 inafanya kazi na minara 22 kati ya 40 imeunganishwa na inatoa huduma ya 3G.  


Akitoa shukrani kwa misaada yote,  Waziri Mkuu alisema anaishukuru kampuni ya Halotel kwa kumsaidia kulipia sh. Milioni 9/- kwa ajili ya CHF ambazo alisema zimegawanywa katika vijiji 90 vya wilaya nzima ya Ruangwa na kwa kaya 10 za watu sita sita.


Aliwashukuru kwa kuweka minara katika wilaya hiyo jambo ambalo alisema litasaidia wananchi kupata mawasiliano ya simu kwa urahisi zaidi.


Kuhusu zahanati,  Waziri Mkuu Majaliwa aliishukuru kampuni ya Huawei Technologies kwa msaada huo ambao alisema utakapokamilika, utawapunguzia wananchi adha ya kwenda kijiji cha jirani kupata huduma ya matibabu. 


Alisema ana mpango wa kuweka nguvu ya umeme jua (solar power systems) kwenye shule zote za msingi, shule zote za sekondari  na zahanati zote kwenye wilaya ya Ruangwa ambayo ndiyo jimbo lake ili asiwepo mtoto wa kushindwa kusoma au mtu kupata matibabu kwa sababu ya kukosa umeme. Wilaya ya Ruangwa ina shule za msingi 82, shule za sekondari 15, vituo vya afya vitatu na zahanati 28.


Waziri Mkuu alirejea Mtwara jana hiyo hiyo na leo hii amerejea Jijini Dar es Salaam.



IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S.  L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
JUMATATU, FEBRUARI 29, 2016.

ETIHAD YAPATA TUZO YA HESHIMA YA KIFEDHA.

$
0
0
SHIRKA la ndege la Etihad limepokea tuzo ya heshima katika mabadiliko ya kifedha kwa mwaka 2015 kutoka kwa kampuni ya kimarekani ya Innovation Enterprise inayoongoza kwenye masuala ya uvumbuzi katika sekta uwekezaji.

Tuzo hiyo ilitolewa kwa Shirika la Ndege la Etihad ambalo lilifanikiwa kuzishinda kampuni nyingine kupitia kituo chake cha nje cha mpango wa Mabadiliko ya kifedha. Programu hiyo iliundwa mahususi  kwa ajili ya shughuli za utendaji na uendeshaji wa shirika hilo katika mazingira ya gharama nafuu.

James Rigney, Afisa Mkuu wa fedha wa shirika la ndege la Etihad alisema…”Tunajisikia fahari kupokea tuzo hii kwa kazi kubwa iliyofanywa na Timu yetu ya mipango ya fedha. Tulikuwa na muda mfupi tu wa miezi sita katika kuhakikisha tunatekeleza mabadiliko ya mpango wetu, na juhudi yao kwenye kazi hii ulitufanya tuweze kupunguza nguvu kazi kifedha, kuanza kusonga mbele na muundo wa kikanda uliopunguza gharama na kukuza kipato hadi kufikisha dola za kimarekani milioni 28 kama akiba huku lengo likiwa kufikia dola za kimarekani milioni 50 milioni hadi mwisho wa mwaka huu.”

Awamu ya kwanza ya kituo cha nje cha mpango wa Mabadiliko ya kifedha kilihitaji kuundwa kwa kituo kimoja chenye ubora kitakachoshughulikia miamala yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 1 kutoka nchi zaidi ya hamsini. 

Awamu ya pili ilitazamia shirika la ndege la Etihad kupitisha mipango ya kuboresha michakato muhimu na kuondoa vikwazo, ili kuhakikisha shughuli hizo zinafanyika kituoni hapo bila kukiuka viwango vya juu vya kuongoza ndege Shirika la Innovation Enterprise ndio linaongoza katika kukuza ubunifu katika mipango ya fedha na taaluma ya uchambuzi, na ni mratibu mkubwa wa matukio katika sekta ya Mipango ya fedha na uchambuzi.

RAIS WA MAGUFULI AMEFANYIA KAZI SUALA LA BANDARI YA DAR ES SALAAM-SYROSE BHANJI.

$
0
0
BUNGE la Afrika Mashariki limesema kuwa changamoto zilizokuwepo katika Bandari ya Dar es Salaam zimeweza kufanyiwa kazi na Rais Dk.John Pombe Magufuli na kufanya Bandari hiyo kutoa huduma kwa ufanisi.


Hayo ameyasema leo Mwakilishi Bunge hilo, Shy Rose Bhanji wakati Wabunge wa Afrika Mashariki Tanzania walipokutana na Spika Bunge, Job Ndugai kwa ajili ya kufahamiana kutokana wabunge hao wanatokana na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema kuwa Bunge la Afrika Mashariki lilikuwa walikuwa wakizungumzia juu ya bandari ya Dar es Salaam katika utoaji uwa huduma lakini sasa Rais Dk.John Pombe Magufuli ameweza kufanyia kazi.
Shyrose amesema wataendelea kutoa ushirikino kwa Rais katika kutumia farsa yake ya Hapa Kazi Tu katika kuwahudumia watanzania.

Nae Mwakilishi wa Spika Owen Mwandumbimbya ambaye ni Afisa Habari wa Bunge amesema kuwa Spika atatoa ushirikiano kwa wabunge kupitia kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
 Spika wa Bunge, Job Ndugai akiwatambulisha wabunge wa bunge la Afrika Mashariki waliofika ofisini kwake leo katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam kwaajili ya kumpongeza kwa kuchaguliwa kuwa spika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa serikali ya awamu ya tano.
Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki, Shy Rose Banji akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufika katika ofisi  ndogo za bunge kwaajili ya kumpongeza Spika wa Bunge, Job Ndugai na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mbunge wa Bunge la Afrika, Shy Rose Banji jijini Dar es Salaam leo katika Ofisi ndogo za Bunge.
Picha na Avila kakingo wa Globu ya Jamii.

WANAFUNZI WACHEZEA BAKOLA ZA FFU LEO JIJINI DAR.

$
0
0
Mwanafunzi wa chuo cha St. Joseph kampasi ya Dar es Salaam akiwa miguuni wa Askari leo mara baada ya kuishiwa nguvu wakati wakitawanywa na Askari hao jijini Dar es Salaam leo walipokuwa wakiandamanda kuelekea wizara wizara ya elimu, Sayansi na mafunzo ya Ufundi.
  Wanafunzi wa Chuo cha St. Joseph tawi la jijini Dar es Salaam wakitawanywa na askali wa kutuliza Ghasia (FFU) leo wakati wanafunzi hao wakiandamana wanaelekea wizara ya elimu, Sayansi na mafunzo ya Ufundi kudai kushinikiza chuo hicho (Kampasi)tawi la Arusha kifunguliwe.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

MAKAMU WA RAIS MSTAAFU DKT. BILAL AKABIDHI ZAWADI ZA WASHINDI WA MASHINDANO YA KUTAFUTA WAWAKILISHI WA NCHI KATIKA MASHINDANO YA KIMATAIFA YA QUR'AN TUKUFU.

$
0
0
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi, mshindi wa kwanza wa Mashindano ya kumtafuta mwakilishi wa Nchi atakayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa ya Qur'aan Tukufu, Rajai Ayoub, aliyepata pointi 95 kwa upande wa Tajweed, wakati wa mashindano hayo yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, jana Feb 28, 2016. Mashindano hayo yameandaliwa na Kamati maalum chini ya Mwenyekiti wake, Saleh Omary. . Kushoto ni Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mahd Aghajafar.
Makamu wa Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mashindano ya kumtafuta mwakilishi wa Nchi atakayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa ya Qur'aan Tukufu, yaliyoandaliwa na Kamati Maalum chini ya Mwenyekiti wake Saleh Omary, yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, jana.
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi, mshindi wa kwanza wa Mashindano ya kumtafuta mwakilishi wa Nchi atakayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa ya Qur'aan Tukufu, Abubakar Mohamed, aliyepata pointi 86 kwa upande wa washindani wa Juzuu 30, wakati wa mashindano hayo yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, jana Feb 28, 2016. Mashindano hayo yameandaliwa na Kamati maalum chini ya Mwenyekiti wake, Saleh Omary. Kushoto ni Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mahd Aghajafar. 
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi, mshindi wa pili wa Mashindano ya kumtafuta mwakilishi wa Nchi atakayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa ya Qur'aan Tukufu, Ibrahim Omary, aliyepata pointi 90 kwa upande wa Tajweed, wakati wa mashindano hayo yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, jana Feb 28, 2016. Mashindano hayo yameandaliwa na Kamati maalum chini ya Mwenyekiti wake, Saleh Omary. Kushoto ni Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mahd Aghajafar.
Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu, waliohudhuria mashindano hayo, wakimsikiliza Dkt. Bilal, wakati akihutubia. 
Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu, waliohudhuria mashindano hayo, wakimsikiliza Dkt. Bilal, wakati akihutubia.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sl-had Mussa Salum, akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, kufunga mashindano hayo.
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya mashindano hayo,Saleh Omary, akizungumza wakati wa mashindano hayo. 
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wakati akiondoka kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, baada ya kumalizika kwa mashindano ya kumtafuta mwakilishi wa Nchi atakayeiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Kimataifa ya Qur'aan Tukufu
Dua baada hafla hiyo


Mshiriki Rajab Juma, mshindi wa pili aliyepata pointi 78 katika Juzuu 30

Mshiriki Mbwana Dadi, mshindi wa tatu aliyepata pointi 75 katika Juzuu 30.
Mshindi wa kwanza katika juzuu 30, Abubakar Mohamed, aliyepata Pointi 86, akitafakari kabla ya kupanda jukwaani kushiriki.
Abubakar Mohamed, mshindi wa kwanza akishiriki....
Mshindi wa tatu kwa upande wa Tajweed, Ally Saleh, aliyeibuka na pointi 82
Mshindi wa kwanza kwa upande wa Tajweed, Rajai Ayoub, aliyeibuka na pointi 95.

Mshindi wa pili kwa upande wa Tajweed, Ibrahim Omaru, aliyeibuka na pointi 90.

WAZIRI MKUU MAJALIWA ATEMBELEA HOSPITALI YA MKOA WA MTWARA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim majliwa akitoa agizo la kusimamishwa kazi Daktari wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara, Fortunatus Namahala (kulia) baada ya kutajwa kuwa alidai rushwa ya sh.100, 000/= ili aweze kumtibu baba mzazi wa Tatu Abdallah (wapili kulia) wakati alipoitembelea hospitali hiyo Februari 29, 2016.
 Wamawake wakiwa wametandika khanga kwenye wodi ya wazazi ya Hospitali ya Mkoa wa Mtwara, Februari 29, 2016.Waziri Mkuu, Kassim majaliwa alitembelea wodi hiyo na kukemea mtindo huo akiwataka wauguzi na waganga kutandika mashuka yahospitali ambayo alisema ana taarifa kuwa yapo ili kuepusha hatari ya wananwake hao kubeba magonjwa kupitia kahanga hizo watokapo hospitalini hapo.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea hospitali ya Mkoa wa Mtwara Februari 29, 2016. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Halima Dendego na kulia Ni Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dkt.Shaibu Maarifa.
 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waganga, Wauguzi na wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakati alipoitembelea Februari 29, 2016.


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea msaada wa kujenga zahanati na nyumba ya mganga kwenye kijiji cha Nandagala, wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi. 

Msaada huo wenye thamani ya dola za Marekani 55,000 (sawa na sh. Milioni 119.35)   umetolewa na kampuni ya Huawei Technologies yenye makao yake jijini Dar es Salaam.  Pia wametoa kompyuta za mezani (desktop) 25 pamoja na UPS  25 kwa ajili ya shule tano za sekondari wilayani humo. 


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo jana (Jumapili, Februari 28, 2016) Mkurugenzi Mtendaji wa Huawei, Bw. Bruce Zhang alisema kampuni yake imetoa msaada huo ikiwa ni mwitikio wa sera ya Wizara ya Afya inayotaka kila kijiji kiwe na zahanati na kila kata iwe na kituo cha afya.

Wakati huohuo, kampuni ya mtandao wa simu ya Halotel ilimkabidhi  Waziri Mkuu hundi ya sh. Milioni 9/- ambazo ni mchango wao wa kumsaidia  Waziri Mkuu ambaye pia ni mbungewa jimbo la Ruangwa ili zisaidie kulipia familia zisizo na uwezo kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Akizungumza na wanakijiji hao kabla ya kukabidhi hundi hiyo, Meneja Mkuu Msaidizi wa Biashara wa Mkoa wa Lindi, Bw. Sebastian Innocent alisema: "Mchango huu utazihusu kaya 900 ambazo zinalipiwa sh. 10,000 kila moja. Kila kaya inatakiwa kulipia watu sita, hivyo tutaweza kuwafikia watu 5,400 kupitia mchango huu.

Alisema kampuni yao imejenga minara 50 katika mkoa wa Lindi ambapo 40 inafanya kazi na minara 22 kati ya 40 imeunganishwa na inatoa huduma ya 3G.  

Akitoa shukrani kwa misaada yote,  Waziri Mkuu alisema anaishukuru kampuni ya Halotel kwa kumsaidia kulipia sh. Milioni 9/- kwa ajili ya CHF ambazo alisema zimegawanywa katika vijiji 90 vya wilaya nzima ya Ruangwa na kwa kaya 10 za watu sita sita.

Aliwashukuru kwa kuweka minara katika wilaya hiyo jambo ambalo alisema litasaidia wananchi kupata mawasiliano ya simu kwa urahisi zaidi.

Kuhusu zahanati,  Waziri Mkuu Majaliwa aliishukuru kampuni ya Huawei Technologies kwa msaada huo ambao alisema utakapokamilika, utawapunguzia wananchi adha ya kwenda kijiji cha jirani kupata huduma ya matibabu. 

Alisema ana mpango wa kuweka nguvu ya umeme jua (solar power systems) kwenye shule zote za msingi, shule zote za sekondari  na zahanati zote kwenye wilaya ya Ruangwa ambayo ndiyo jimbo lake ili asiwepo mtoto wa kushindwa kusoma au mtu kupata matibabu kwa sababu ya kukosa umeme. Wilaya ya Ruangwa ina shule za msingi 82, shule za sekondari 15, vituo vya afya vitatu na zahanati 28.


Waziri Mkuu alirejea Mtwara jana hiyo hiyo na leo hii amerejea Jijini Dar es Salaam.


 Baadhi ya Wauguzi na Madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao hospitalini hapo Februari 29, 2016. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akiagana na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara, Shaibu Maarifa kwenye uwanja wa ndege wa Mtwara kabla ya kurejea Dar es slaam Februari 29, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim majaliwa akitazama ngoma kwenye uwanja wa ndege wa Mtwara kabla ya kuondoka kurejea Dar es salaam Februari 29, 2016.
 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZUNGUMZA NA WAZEE WA MKOA WA TANGA JANA JIONI MKOANI TANGA.

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wazee wa Mkoa wa Tanga katika kikao maalum kilichoangaliwa kwa ajili yake kilichofanyika Ikulu ndogo mjini Tanga jana jioni Februari 28, 2016. 
(Picha na OMR)

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA WARSHA YA PILI YA KIMATAIFA YA UNESCO MKOANI TANGA LEO.

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Warsha ya pili ya Kimataifa inayojadili kuhusu Bayoanuwai  katika hifadhi ya kupunguza umaskini na uhifadhi ya viumbe hai na maendeleo endelevu kusini mwa Jangwa la Sahara. Warsha hiyo imefunguliwa leo Februari 29, 2016 katika ukumbi wa Hoteli ya Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.
\Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Mkurugenzi Msaidizi wa UNESCO kanda ya Afrika Firmin Matoko katikati na mwakilishi Mkaazi wa UNESCO Tanzania Zulmira Rodrigues kabla ya kufungua rasmi Warsha ya pili ya Kimataifa inayojadili kuhusu Bayoanuwai  katika hifadhi ya kupunguza umaskini na uhifadhi ya viumbe hai na maendeleo endelevu kusini mwa Jangwa la Sahara. Warsha hiyo imefunguliwa leo Februari 29, 2016 katika ukumbi wa Hoteli ya Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Balozi wa Korea kusini Nchini Geum-Young Song kabla ya kufungua rasmi Warsha ya pili ya Kimataifa inayojadili kuhusu Bayoanuwai  katika hifadhi ya kupunguza umaskini na uhifadhi ya viumbe hai na maendeleo endelevu kusini mwa Jangwa la Sahara. Warsha hiyo imefunguliwa leo Februari 29, 2016 katika ukumbi wa Hoteli ya Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Cheti kiongozi wa Spice kutoka Zanzibar ambae ni mmoja kati ya washiriki Warsha ya pili ya Kimataifa inayojadili kuhusu Bayoanuwai  katika hifadhi ya kupunguza umaskini na uhifadhi ya viumbe hai na maendeleo endelevu kusini mwa Jangwa la Sahara. Warsha hiyo imefunguliwa leo Februari 29, 2016 katika ukumbi wa Hoteli ya  Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Cheti Judith Mwambela mmoja kati ya washiriki Warsha ya pili ya Kimataifa inayojadili kuhusu Bayoanuwai  katika hifadhi ya kupunguza umaskini na uhifadhi ya viumbe hai na maendeleo endelevu kusini mwa Jangwa la Sahara. Warsha hiyo imefunguliwa leo Februari 29, 2016 katika ukumbi wa Hoteli ya  Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Warsha ya pili ya Kimataifa inayojadili kuhusu Bayoanuwai  katika hifadhi ya kupunguza umaskini na uhifadhi ya viumbe hai na maendeleo endelevu kusini mwa Jangwa la Sahara. Warsha hiyo imefunguliwa leo Februari 29, 2016 katika ukumbi wa Hoteli ya  Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.
(Picha na OMR)

Mke wa Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa WAMA asisitiza umuhimu wa Chama cha Girl Guide Tanzania Kuongeza Wanachama

$
0
0
 Mke wa Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa WAMA akisalimiana na Mama Othman Chande alipowasili katika Shule ya Sekondari Tambaza kuhudhuriaWorld Thinking Day iliyoandaliwa na Tanzania Girl Guide Association.
 Wanachama wa Girl Guide wakiwasili katika Shule ya Sekondari Tambaza  katika kusherekea World Thinking Day  ambao walipokelewa na Mgeni Rasmi Mama Salma Kikwete.
 Mama Salma Kikwete akiingia katika ukumbi wa Tambaza Sekondari akiwa na viongozi wa Girl Guide kushoto ni Mama Symphorosa Hangi, Kamishna Mkuu  na kulia ni Mama Matilda Balama na Mkuu wa Shule ya Tambaza.
Na Philomena Marijani- Meneja Uraghbishi na Mawasiliano, WAMA

CHAMA cha Girl Guide Tanzania kimetakiwa kuweka mikakati ya kuhakikisha inaongeza wanachama watakaojiunga na chama hicho ili vijana wengi waweze kunufaika.


Rai hiyo imetolewa mwishoni wa wiki na Mke wa Rais Mstaafu na  Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA, Mama Salma Kikwete wakati wa maadhimisho  ya kilele cha  siku ya  World Thinking Day yenye kauli mbiu ya Ungana, Shirikiana, Sherekea  iliyoadhimishwa na Tanzania Girl Guides Association. Sherehe hizo zilianza kwa maandamano ya wanafunzi Wanachama kutoka Upanga katika Makao Makuu ya Girl Guide Tanzania na kumalizikia  katika Shule ya Sekondari Tambaza ambapo  sherehe rasmi ilifanyika hapo.


Akiongea katika sherehe hizo Mama Salma Kikwete  alipongeza uongozi wa Girl Guide  kwa kufikia mikoa 19 ambapo  mpaka sasa chama kina  wanachama 97,143 na aliongeza kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni kuongeza Wanachama zaidi kwani Tanzania ina watu wengi sana.


“Wito wangu kwenu ni kuongeza juhudi ya kuwafikia vijana wengi zaidi kwani sote tunajua umuhimu wa TGGA katika kuwasaidia vijana kujiepusha na changamoto mbalimbali katika makuzi yao. Ni lazima tuweke malengo ya muda mfupi, kati na mrefu ndani ya miaka mitatu ili ifikapo  mwaka 2018 tuwe tumeingiza wanachama zaidi ya 100,000/= Tumieni vizuri shule za msingi na sekondari , nina hakika mtafanikiwa kwa kiasi kikubwa sana. ” Alisema Mama Kikwete

Mama Kikwete pia alishauri uongozi wa Girl Guide Tanzania kubuni mbinu za kukabiliana na changamoto kwa kutumia rasilimali walizonazo.


“Kwa kuwa TGGA ni chama kikongwe, chenye rasilimali kama ardhi ambazo ziko sehemu nzuri kibiashara  naamini kwamba ikitayarishwa mipango mizuri  mnaweza kupata wabia wenye tija au mkawekeza kama chama kwa kushirikiana na mabenki. Mtakusanya kodi ambazo zitasaidia uendeshaji na kuongeza uwekezaji. ”Alisema Mama Kikwete.


Akielezea maana ya World Thinking Day Mkufunzi wa Taifa wa Tanzania Girl Guide Association, Mama Magreth Olumbe alisema kuwa sherehe hii ilianza rasmi mwaka 1926 ambayo ni siku ya; kuwakumbuka Girl Guide wote duniani na hasa wale walio kwenye mazingira magumu;kuongelea mambo yanayowagusa wasichana kwa mfano mimba za utotoni, kuolewa katika umri mdogo; na kukumbuka mwanzilishi wa Chama Lord Baden Powell na mke wake Olave Baden Powell.  


Akisoma risala kwa Mgeni Rasmi, Kamishna Mkuu wa  Tanzania Girl Guides Association, Mama Symphorosa Hangi alisema kuwa katika kuadhimisha  World  Thinking Day walikuwa na wiki mbili za kutoa huduma kwa jamii ikiwemo kuwatembelea wagonjwa katika hospitali ya Ocean Road na kutoa chakula, mavazi   na nauli za kuwarudishwa makwao wale waliokuwa wameruhusiwa baada ya matibabu. Aliongeza pia walitumia muda huo kuhamasisha wasichana wengine kujiunga na chama cha Tanzania Girl Guides ili nao waweze kupata fursa ya kujikwamua kifikra kwa kupitia mafunzo yanayotolewa na chama.



Chama cha Girl Guides Tanzania (TGGA) kilianzishwa hapa nchini mwaka 1928. TGGA ni chama kisicho cha serikali na ni cha kujitolea chenye lengo la kuwaendeleza watoto wa kike na wanawake kwa ujumla kushiriki katika maswala ya kijamii na kiuchumi kwa kupitia elimu na mafunzo yanayotolewa kwa kuzingatia kanuni za Girl Guides pamoja na kuwajenga kimaadili.

 Picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi  na baadhi ya wanafunzi Wanachama na viongozi wa  Girl Guide
 Mama Salma Kikwete akiangalia kazi za wakinamama wajasiriamali ambao walifanya maonyesho katika sherehe hizo


PICHA NA YUSUPH BADI

DK. KIGWANGALLA AAGIZA KUFUNGWA KWA DUKA LA DAWA LA SHINE CARE PHARMACY LA TEMEKE KWA KUKIUKA UENDESHAKI WAKE.

$
0
0
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza kufungwa kwa Duka la dawa za binadamu la Shine Care Pharmacy lililopo Temeke, baada ya kubainika kuendeshwa kinyume cha sharia ikiwemo kutokuwa na kibali cha uendeshaji na mfamasia husika.

Dk. Kigwangalla ambaye aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi, Mfamasia Mkuu wa Serikali pamoja na msajili wa Baraza la famasia nchini na maafisa wengine, ambapo katika tukio hilo mapema leo Februari 29.2016, walikuta madawa mbalimbali yaliyokwisha muda wake na yale ambayo hayatakiwi kuuzwa katika duka kama hilo.

Aidha, Dk. Kigwangalla akitoa agizo la kufungwa kwa duka hilo, ameagiza kuchukuliwa hatua ikiwemo kupelekwa Mahakamani mara moja il iwe fundishi na kwa maduka mengine yenye kufanya hivyo.

Kwa upande wake, Mfamasia wa Serikali, Bw. Henry Irunde amebainisha kuwa, dawa hiza za binadamu zilizokutwa hazifai kuuzwa katika maduka hayo na pia duka ambalo linaendeshwa bila kuwa na Mfamasia ni kinyume na sharia kwani watumiaji wakitumia dawa bila kuwa na maelezo ya kutosha kutoka kwa mtaalam wa dawa zinaweza kusababisha usugu kwa mwili wa binadamu n ahata kumsababishia matatizo.

Duka hilo la dawa ambalo lipo hatua chacche kutoka Hospitali ya Temeke, ni miongoni mwa maduka makubwa ya dawa za binadamu ambapo pia wachunguzi ha wa madawa ya binadamu walibaini kuwa milango mingi zaidi kinyume na ile inayotakiwa kuwa kwa maduka ya dawa hali ambayo walitilia mashaka huenda vitendo vingine vya kutoa huduma vinatumika licha ya kuwa milango hiyo ilifungwa kwa kile kilichoelezwa kuwa wahusika hawakuwapo.

Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, zoezi hilo la kukagua maduka ya dawa ni la nchi nzima na watazunguka nchi nzima kufanya ukaguzi huo bila kutoa taarifa hivyo kwa yeyote atakaekutwa anaendesha kinyume cha sharia atachukuliwa hatua stahiki.


Tazama  tv, Kuona video hiyo hapa: 
Imeandaliwa na Andrew Chal.
Mmoja wa maafisa wa TFDA, akikagua dawa katika duka hilo
Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akiwaonyesha waandishi wa habari cheti cha Famasia kilichoisha muda wake huku akiendelea na biashara yake hiyo kinyume na sheria.
Baadhi ya maafisa walioambatana na Naibu Waziri wa Afya. Dk Kigwangalla wakimsikiliza kwa makini, Dk. Kigwangalla (hayupo pichani) wakati wa tukio hilo.
Naibu Waziri wa Afya, Dk.Kigwangalla akiongea kwa njia ya simu na mmiliki wa duka hilo la Shine Pharmacy , Abraham Mathayo...ambaye alieleza kuwa yupo Mkuranga, hivyo waliamua kuongea naye kwa njia ya simu kwa nini anaendesha duka bila ya kutokuwa na vibali.
Mfamasia Mkuu wa Serikali Henri Irunde, akitoa taarifa yake ya ukaguzi katika duka hilo kwa wanahabari na Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla (Hayupo pichani).
Naibu Waziri Dk. Kigwangalla akitoa maagizo hayo ya kufungwa kwa duka hilo.
Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla akitoka katika duka hilo la dawa baada ya kuagiza kulifunga.
(Picha zote na Andrew Chale.)

TANGAZO LA MSIBA WA DK MICHAEL KISAMO

$
0
0
Mrs Elipina Kisamo Mlaki na Linda Kisamo wanasikitika kutangaza kifo cha baba yao mpendwa Dr Michael Kisamo aliyefariki Jumapili 28/2/2016. 

Mipango ya Mazishi inafanyika Nyumbani kwake Kinondoni Mkwajuni/Sokoni Magengeni. na Mazishi yanataraji kufanyika Usangi Jumatano 2.03.2016.

Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa jina lake lihimidiwe

Ahsante kwa Ushirikiano.

BWENI LA WAVULANA SHULE YA SEKONDARI IYUNGA JIJINI MBEYA LATEKETEA KWA MOTO

$
0
0
Baadhi ya wanafunzi waliofanikiwa kuokoa vifaa vyao kwa masaada wa watu wa zima moto wakiwa nje wakisubiri utaratibu mara baada ya bweni lao kuteketea kwa moto. 
Baadhi ya wanafunzi wakiwa nje kusbiri utaratibu mara baada waliofanikiwa kuokoa baada ya bweni lao kutektea kwa moto.Picha na David Nyembe 
 
Moto ukiendelea kuteketeza Bweni la Wavulana (Mkwawa ) katika shule ya sekondari ya Iyunga jijini Mbeya ambapo chanzo chake kimetajwa kuwa ni hitilafu ya umeme ambapo moto huo ulizuka majira ya saa 3 asubuhi february 29 mwaka huu wakati wanafunzi wakiwa madarasani. 
 
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyirembe Munasa mwenye suti akisaidiana na kikosi cha Zima moto kuuzima moto ulioteketeza Bweni la wavulana katika shule ya sekondari ya Iyunga jijini Mbeya linalolaza wanafunzi 95 February 29 mwaka huu ambapo hakuna 
 
Muonekano wa bweni la Wavulana katika shule ya sekondari Iyunga jijini Mbeya mara baada ya kuteketea kwa moto uliosababishwa na hitilafu ya umeme majira saa3 asubuhi ambapo hakuna mwanafunzi yeyote aliyejeruhiwa kutokana na ajali hiyo ya moto. . 
 
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyirembe Munasa akizungumza na Walimu pamoja na wanafunzi (hawapo pichani )katika shule ya sekondari Iyunga jijini Mbeya mara ya baada ya kukumbwa na tukio la kuungua kwa moto kwa mabweni ya wavulana ya (Mkwawa) February 29 mwaka huu. 
 
Kamati ya ulinzi na Usalama wilaya ya Mbeya na baadhi ya viongozi wakitizama athari zilizotokea mara baada ya mabweni ya wavulana katika shule ya sekondari Iyunga jijini Mbeya kuungua moto uliosababishwa na hitilafu ya umeme February 29 mwaka huu . 
Afisa elimu Mkoa wa Mbeya Charles Mwakalila akizungumzia athari zilizojitokeza mara baada ya mabweni ya wavulana katika shule ya sekondari ya Iyunga jijini Mbeya ambayo yaliteketea kutokana na hitilafu ya umeme majira ya saa3 asubuhi wakati wanafunzi wakiwa madarasani .

OLDUVAI GORGE IKO TANZANI SI KENYA

$
0
0


BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imekuwa ikifuatilia kwa makini majadiliano yanayoendelea katika mitandao mbalimbali ya kijamii kufuatia video iliyotumwa katika YouTube https://www.youtube.com/watch?=iveX49WE7fw na imekuwa ikisambazwa kupitia njia mbalimbali za habari ikimuonesha mtu mmoja kutoka nchi jirani akisema kuwa Olduvai Gorge ambayo kimsingi iko Tanzania kwamba iko Kenya.

Video hii imeibua majadiliano katika mitandao ya kijamii baina ya watanzania na watu wengine ambao wanaitakia mema Tanzania na wanaoelewa vizuri kuwa Olduvai Gorge iko Tanzania.

Bodi ya Utalii Tanzania kama taasisi ya Umma yenye jukumu la kuvitangaza vivutio vyetu vya utalii imeshtushwa na video hii iliyojaa upotoshwaji mkubwa ambao tunaamini mbali ya malengo mengine inalenga kuchafua kazi nzuri ambayo imekuwa ikifanywa na Bodi kwa kushirikiana na wadau wengine katika kutamgaza vivutio vya utalii vya Tanzania ikiwemo Olduvai Gorge.

Tunapenda kuchukua fursa hii kupinga vikali upotoshwaji huu uliofanywa na mtu huyo wakati akihutubia mkutano amabao tumeambiwa ulikuwa ni wa Vijana wa Umoja wa Mataifa uliofanyika Amerika mwezi Agosti mwaka jana. Tunapenda dunia ifahamu kuwa kama ilivyo kwa Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Zanzibar n.k Olduvai Gorge mahali panapoaminika kuwa ndipo binadamu wa kwanza duniani aliishi na ambako Dr. Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la binadamu huyo wa kale anayesadikiwa kuishi miaka takribani milioni 2 iliyopita iko pia Tanzania na si mahali pengine popote duniani. Eneo hili la Olduvai Gorge liko katika bonde la ufa katikati ya bonde la Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Manyara nchini Tanzania.

Tunatoa wito kwa watanzania mahali popote walipo kuendelea kuunga mkono juhudi za Bodi ya Utalii Tanzania za kuitangaza Tanzania na vivutio vyake vya Utalii kwa kujibu na kusahihisha papo hapo bila woga mara tu taarifa ya upotoshaji kuhusu nchi yetu inapotolewa iwe ni kwenye mikutano ya ndani ya nchi au ya Kimataifa. Tunaamini kuwa ni jukumu la kila mtanzania kuitangaza Tanzania na vivutio vyake vya Utalii badala ya kuiachia TTB kazi hii peke yake. 

Yawezekana katika mkutano huo wa vijana ambao mjumbe huyo wa nchi jirani alipata fursa ya kuzungumza na kufanya upotoshaji huzo, wajumbe wa Tanzania pia walikuwepo ambao wangweza kukosoa upotoshaji huo papo hapo na kuelezea ukweli na usahihi wa mahali ilipo Olduvai Gorge.

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano



BODI YA UTALII TANZANIA.

SHIWATA wamlilia Mapili

$
0
0
MTANDAO wa Wasanii TAnzania (SHIWATA) umetoa salamu za rambirambi kwa familia, wanamuziki wa dansi, wadau wa muziki wa dansi nchini na wengine walioguswa na msiba wa mkongwe wa muziki nchini marehemu Mzee Kassim Mapili (&() aliyefariki na kuzikwa wiki iliyopita makaburi ya Kisutu, Dar es SAlaam.

Mwenyekiti wa SHIWATA, CassimTaalib alisema marehemu Mapili atakumbukwa kwa ushirikiano, uwazi na uchangamfu kwa wanamuziki katika kipindi chote cha maisha yake.

Alisema SHIWATA imesikitishwa kuondokewa na mshauri wa wanamuziki ambaye alikuwa mmoja wa waanzilishi wa mtandao huo akiwakilisha Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (CHAMUDATA) na muda wote wa uhai wake marehemu Mapili alikuwa akichangia ukuaji wa muziki wa dansi na kuimarika kwake ingawa umekuwa ukikabiliwa na ujio wa muziki wa kizazi kipya.

Alisema SHIWATA itamkumbuka marehemu MApili kwa uhamasishaji wake kuwartaka wasanii wajiunge na mtandao huo na kwa mara ya mwisho aliwahasisha wasanii wa fani mbalimbali kujiunga na PPF katika mkutano ulioandaliwa na mtandao huo kuwaunganisha wasanii kupata bima ya aAfya.

Marehemu Mapili ambaye alistaafu muziki katika bendi ya Polisi Jazz mwaka 1981 alikuwa mwanamuziki mwalikwa katika bendi mbalimbali.Atakumbukwa kwa wimbo wake maarufu wa Napenda nipate lau nafasi niseme nawe kidogo... alioutunga na kuimba akiwa na Bendi ya Kilwa Jazz.

Mungu ilaze roho ya marehemu mahali Pema Peponi. Amen.

HARMONIZE AUFUNGA MWEZI WA PILI NA BADO KAMSHIRIKISHA DIAMOND PLATNUMZ.

$
0
0
Dar es Salaam, Tanzania– February 29, 2016: Mwimbaji anaekuja kwa kasi kwenye muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva) kutoka Tanzania anayewakilisha kundi la Wasafi Classic Baby(Wcb),Harmonize ameachia wimbo wake wimbo mpya unaoitwa ‘BADO’ aliyomshirikisha Diamond Platnumz.
SABABU YA KUREKODI WIMBO HUU.
Kwa singo mbili alizosikika Harmonize(Aiyola,Kidonda Changu) kwenye vyombo vya habari,jamii imekua ikimfananisha sana na Diamond kwenye uimbaji,ndipo siku moja Harmonize wakati akiimba Diamond alivutiwa na Melody ya wimbo huu na kusema hii itakua nafasi ya Watanzania kuwatofautisha kwenye uimbaji.
KUHUSU WIMBO WA BADO.
Harmonize alikaa na Diamond akamuuliza ni msichana gani alishamuumiza kiasi kwamba hawezi kumsahau,ingawa Diamond hakumwambia ni msichana gani,lakini akamwambia hiyo ni idea(Mwanga) mzuri wa kutunga wimbo ‘mkali’ Beat ya wimbo huu imetengenezwa na Mtayarishaji(Producer) anaitwa Fraga na kabla ya kurekodi kwenye studio ya Wasafi,producer Fraga alimtumia midundo (Beat) 3 Harmonize  achague,ndipo akachagua beat ya wimbo huu na kurudi Wasafi Records kwa ajili ya kurekebishwa na kuanza kurekodiwa.
VIDEO YA WIMBO WA BADO.
Video ya wimbo huu imefanyika Afrika Kusini na Muongozaji(Director) anaitwa Nick ambaye ametengeneza video kadhaa ikiwemo Aiyola ya Harmonize mwenyewe,Make Me Sing ya Aka na Diamond,Love Boat Kcee na.Diamond,Walk it off ya Fid Q na nyingine nyingi.
Note:Wimbo wa BADO na interview ya Harmonize vimeambatanishwa kwenye barua pepe hii.

TAS NA UTSS WAMTAFUTA MWENZAO ALIYEPOTEA.

$
0
0
Jacquiline Mrisho – MAELEZO. Dar es Salaam.

Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS) wameiomba Serikali kuwasaidia kumtafuta Bw. Said Abdalah Ismail (47) mkazi wa Kijiji cha Mbezi Mlungwana Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa (TAS) Josephat Torner alipokua akiongea na waandishi wa habari juu ya taarifa hii ya kupotelewa na mwenzao.

“TAS kwa kushirikiana na Shirika la Under The Same Sun (UTSS) tunaendelea kufanya juhudi ya kumtafuta na juhidi zetu tunaomba Serikali ituunge mkono” alisema Torner

Torner aliongeza kuwa, Said alionekana kwa mara ya mwisho Januari 31 mwaka huu katika Kijiji cha Mtipule alikokwenda kuuza mboga za majani na baadae alionekana katika kilabu cha pombe ya kienyeji ambapo inasemekana aligombana na wenzie waliokua wakinywa pamoja kabla hajaondoka kilabuni hapo.

“Tunalitaka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na lile la Afrika Mashariki kujadili kwa kina tatizo hili na kulitafutia ufumbuzi wa kudumu pia vyombo vya dola kuhakikisha wakatili hao wanatafutwa, wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria ili sisi wenye ualbino tuweze kuishi kwa amani.” Alisema Torner.

Amesema kuwa pamoja na juhudi za kumtafuta Said kuendelea taarifa ya kupotea kwake ilipelekwa kituo cha Polisi Wilaya ya Mkuranga na kupewa RB namba MKU/PE/05/2016 pia kituo kidogo cha polisi Kimanzichana kwa RB namba KIM/RB/50/2016.

Aidha, Polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo ambapo jina la muuza pombe pamoja na majina ya wale aliogombana nao tayari yamewasilishwa polisi kwa ajili ya uchunguzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha Albino wilayani Mkuranga mkoani Pwani Hassan Kambangwa akizungumzia tukio amesema amelipokea kwa masikitiko makubwa na kuiomba Serikali kuwachukua hatua kali za kisheria wote waliohusika katika tukio hilo.

Kambangwa ametoa wito kwa uongozi wa Serikali ya Kijiji kutafuta mbinu za kuzuia ukatili huo.

Ikumbukwe kuwa tukio hilo kwa Bw.Said Abdalah Ismail ni la pili kwa kuwa aliwahi kupatwa na mkasa wa kukatwa kiganja cha mkono akiwa mkoani Morogoro miaka michache iliyopita.

WAZIRI MKUU AAGIZA DAKTARI WA HOSPITALI YA LIGULA MKOANI LINDI ASIMAMISHWE KAZI.

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waganga, Wauguzi na wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara wakati alipoitembelea Februari 29, 2016.

  • Ni baada ya kudai rushwa ya sh. 100,000/- kumfanyia upasuaji mgonjwa.
  • Mama alilazimika kuuza shamba ili apate fedha za kumtibia baba yake
  • Aagiza maduka ya dawa nje ya hospitali hiyo yafungwe leo hii
  • Amwagiza RAS aitishe kikao cha watumishi wote leo saa 9 alasiri
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kusimamishwa kazi kwa Dk. Fortunatus Namahala wa kitengo cha upasuaji katika hospitali ya Ligula ambayo ni hospitali mkoa wa Mtwara kutokana na tuhuma za kumdai mgonjwa rushwa ya sh. 100,000/-.

Pia ametoa agizo la kufungwa kwa maduka yote ya dawa yaliyo nje ya hospitali hiyo kuanzia leo na kumtaka Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw. Alfred Luanda asimamie zoezi hilo mara moja.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Februari 29, 2016) kwenye kikao cha watumishi wa hospitali hiyo alichokiitisha baada ya kutembelea maeneo kadhaa ya hospitali hiyo na kupokea malalamiko kutoka kwa wagonjwa na ndugu wenye wagonjwa waliolazwa.

Mara baada ya kuwasili, Waziri Mkuu aliamua kwenda mojamoja mapokezi badala ya wodini kama alivyopangiwa na kuuliza maswali ni kwa nini wana dirisha moja la kupokelea wagonjwa wote. "Dirisha la wazee lipo?" akajibiwa hakuna. "Dirisha wa watu wa Bima ya Afya (NHIF) lipo" nalo pia akajibiwa halipo. "Je wazee wana daktari wao", hakupata jibu.


"Mganga Mkuu ni kwa nini hujatenga dirisha la wazee wakati haya maelekezo yalishatolewa siku nyingi? Tengeni dirisha la wazee  na uhakikishe wana daktari wao. Siyo kuwaleta huku ili waje kusukumana na wagonjwa vijana,"  alisema wakati akimwagiza Mgaga Mkuu wa Mkoa huo, Dk. Shaibu Maarifa.

Akiwa njiani kuelekea wodi aliyopangiwa kuiona, Waziri Mkuu alikutana na kundi la wagonjwa waliokuwa wakiimba "tuna jambo, tuna jambo" wakiashiria kutaka kusikilizwa. Kati ya wauguzaji watatu aliowasikiliza, Waziri Mkuu alipokea kero za kuuziwa dawa kwa bei za juu kwenye maduka ya dawa binafsi, lugha mbaya za madaktari na wauguzi, uchafu wa vyoo na uhaba wa maji.

Lakini kero ya Bi. Tatu Abdallah aliyelazimika kuuza shamba la baba yake ekari 2.5 ili apate fedha za kulipa gharama za kufanya upasuaji kwenye hospitali binafsi baada ya baba huyo kutimuliwa kutoka hospitali ya Ligula ndiyo ilimgusa zaidi Waziri Mkuu.

"Februari mosi nilimleta baba yangu hapa nikaambiwa anatakiwa kufanyiwa upasuaji. Nikaandikiwa ninunuue dawa za sh. 85,000/- hapo nje (pharmacy haikumbuki jina) pia uzi wa kushonea kwa sh. 25,000/-. Lakini pia daktari akasema anataka sh. 100,000/- ya kwake. Lakini hadi Februari 7 hakufanyiwa huo upasuaji."


"Tarehe 12 Februari  baba alitolewa wodini na kuambiwa arudi tarehe 16 Februari. Niliumia sababu kijiji tunachotoka ni mbali na hali ya baba ilizidi kuzorota. Ndipo baba akaniambia nirudi kijijini kwetu Kilomba nikauze ekari 2.5 za shamba lake ili tulipie matibabu. Niliuza na kumpeleka baba katika zahanati ya Sajora. Huko nililipa sh. 560,000/- na baba akafanyiwa upasuaji sasa hivi yuko nyumbani".


"Leo nataka huyu daktari aje achukue boksi hili la dawa alizoniandikia na pia anirudishie hela yangu iliyopotea bure. Mie sijazitumia, ni kwa nini aliniandikia wakati baba hajampa huduma yoyote?" Alipoulizwa kama anaweza kumtambua akimuona, mama huyo alikiri kuwa anaweza. 

Waziri Mkuu alitembelea pia wodi ya akinamama waliojifungua na kukuta wakiwa wametandikiwa shuka moja na wagonjwa kulazimika kuweka khanga juu ya mipira wanayolalia wodini ambayo pia wanaambiwa wajinunulie kabla ya kwenda hospitali kujifungua.

Akiwa njiani kuelekea theatre, Waziri Mkuu alipata kilio cha wagonjwa wengine ambao walisema hospitali hiyo haina maji, choo kinachotumika ni kimoja na kwamba usafi umefanyika leo waliposikia kuwa atatembelea hospitali hiyo. 


Akiwa katika kikao na watumishi hao, Waziri Mkuu aliwainua madaktari wote ili wajitambulishe ndipo akamuomba mama aliyedaiwa rushwa aende kumshika mkono daktari mhusika.


"Gwaride la utambuzi ni jambo la kawaida. RPC hakikisha huyu mama hasumbuliwi. Lakini leo nitaanza na huyu Daktari kwa sababu rushwa haivumiliki. RAS simamia suala lake lakini pia shirikiana na TAKUKURU na Polisi kufanya uchunguzi wa jambo hili hadi mwisho," alisema. 


Kuhusu madai na stahili za watumishi, Waziri Mkuu amemwagiza RAS, RMO na Afisa Utumishi wa mkoa wafanye kikao na watumishi wote wa hospitali hiyo leo saa 9 alasiri na kisha wamletee taarifa.


Kabla ya kufikia uamuzi wa kumsimamisha Dk. Namahala, Waziri Mkuu alitumia muda mwingi kuwaelezea watumishi hao jinsi walivyo na umuhimu katika huduma zao na kwamba nafasi yao ni nyeti kwa maisha ya binadamu hivyo wanapaswa kuwa na huruma na siyo kuwaumiza wananchi wa kipato cha chini ambao hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Aliwataka waache tabia ya kuwatoza fedha watoto wanaolazwa hospitalini hapo na wanawake wanaojifungua kwani wanapaswa kutibiwa bure kwa mujibu wa sera ya Serikali. 
Sakata la hospitali ya Ligula lilianza juzi (Jumamosi, Februari 27, 2016) wakati Waziri Mkuu akiwahutubia mamia ya wakazi wa Mtwara kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa mashujaa ambapo baadhi yao walikuwa wakichomekea kuwa aende hospitalini hapo kwa kuwa kuna majipu ya kutumbua.

Waziri Mkuu aliwajibu kuwa amesikia ujumbe wao na ataenda huko lakini alishindwa kutokana na ratiba za siku hiyo kumalizika jioni sana.

Waziri Mkuu amerejea Jijini Dar es Salaam mchana huu.

Global Peace: Rosemary Odinga needs to apologise to Tanzanians for misleading the world that Olduvai Gorge is in Kenya!

MAGAZETINI LEO

Viewing all 46334 articles
Browse latest View live


Latest Images