Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

MADEREVA WATAKAOZIDISHA ABIRIA KWENYE VYOMBO VYA USAFIRI KUKIONA

$
0
0
 Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na Jeshi la Polisdi Nnchi zima kupambana na watu watakaovunja sheria ya usafirishaji wa watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
JESHI la Polisi Nchini limewatahadharisha madereva  watakaozidisha  idadi ya abiria kuliko uwezo wa chombo cha usafari kwani ni kosa kisheria na watakaozidisha abiria kwenye vyombo vyao vya usafiri watachukuliwa hatua za kisheria.

Operesheni hiyo inaanza leo baada ya tamko la Jeshi la Polisi na kuanza kutekeleza kwa wale wote wataobeba abiria wengi tofauti na uwezo wa basi, watachukuliwa hatua madereva wa daladala,mabasi ya mikoani pamoja na magari aina ya Noah.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba amesema kuwa Jeshi la polisi linaanza operesheni ambayo ni endelevu na kuwataka watu wafuate sharia ya ubebaji wa abiria.

Advera amesema kuwa katika kipindi hiki cha siku kuu Jeshi la polisi limejipanga katika kuwadhibiti waendesha bodaboda kwa wataopandisha watu zaidi  ya wawili (mishikaki) kukiona cha mtema kuni kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani.

Aidha amewataka wananchi kutoa taarifa za kihalifu katika msimu wa sikukuu na uimarishaji wa ulinzi wa watu na mali zao na maisha yaweze kuendelea baada ya sikukuu.

RC Makalla azindua mradi wa maji wenye thamani ya sh milioni 343

$
0
0

Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Amos Makalla mwenye miwani akizindua huduma ya maji katika kijiji cha Mabogini, mkoani Kilimanjaro wenye thamani ya Sh Milioni 343.Mradi wa maji wa sh Milioni 343 wazinduliwa kijiji cha Mabogini, RC Makalla ataka vyanzo vya maji vitunzwe


Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

ZAIDI ya wananchi 3000 wa kijiji cha Mabogini, kitongoji cha Shabaha, mkoani Kilimanjaro, watanufaika na huduma ya maji safi na salama, baada ya kupelekewa mradi wenye thamani ya Sh Milioni 343. Mradi huo uliozinduliwa leo na Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Amos Makalla, umesimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi Moshi (MUASA), ukiwa na lengo la kuwapatia huduma bora ya maji wakazi katika kijiji hicho.

Akizungumza katika uzinduzi huo, RC Makalla aliwataka wananchi kutunza mazingira na kulinda vyanzo vya maji, bila kusahau upandaji wa miti ili wasiharibu vyanzo vya maji. Alisema bila hivyo hali ya maji katika maeneo hayo itakuwa ngumu, hivyo kuna kila sababu ya wananchi hao kuielewa na kuiabudu sera ya utunzaji wa mazingira na upandaji wa miti katika maeneo yao. “Naomba wananchi tulinde miundo mbinu ya maji ili kuhakikisha kwamba miradi ya maji inakuwa endelevu katika maeneo yetu tunayoishi, maana maji ni uhai.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Amos Makalla akimtwishwa ndoo ya maji mkazi wa kijiji cha Mabogini baada ya uzinduzi wa mradi maji katika eneo hilo.
Mazungumzo yanaendelea katika uzinduzi huo wa maji.

RC Kilimanjaro Amos Makalla akifungua maji kama ishara ya kuzindua rasmi mradi huo.
RC Kilimanjaro Amos Makalla wa nne kutoka kushoto waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali mkoani Kilimanjaro na watendaji wa MUASA.

“Tunaamini tukiamua kwa pamoja kufuata maelekezo ya wataalaamu juu ya utunzaji wa mazingira tutaishi vizuri na huduma ya maji itapatikana kwa urahisi,” alisema RC Makalla.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Amos Makalla, amekabidhi hundi yenye thamani ya Sh Milioni 100 kwa vikundi 45 kwa Halmashauri ya Moshi, huku vikundi hivyo vikiwa ni 39 vya akina mama na 6 kwa vijana. Fedha hizo ni utekelezaji wa maelekezo ya serikali kwa Halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kutoa mikopo kwa akina mama na vijana.

RC Makalla ni miongoni mwa viongozi wa serikali wanaokwenda na kasi ya Hapa Kazi Tu inayoendeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli, akisimamia na kuzunguuka katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kufanikisha maendeleo ya wananchi wake.

TPB YATOA ZAIDI YA MILIONI 200 KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI KIUCHUMI, NI MKOPO NAFUU

$
0
0

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania, TPB, Sabasaba Moshingi, (kushoto), akikabidhi mfano wa hundi kwa Mkurugenzi wa Shirika la Vijana Wajasiriamali na Uwezeshaji Tanzania, (TYEEO), Ayub Gerald Luhuga, wakati wa hafla fupi iliyofanyika Wizara ya Fedha na Mipango, jijini Dar es Salaam Desemba 23, 2015. 

Benki hiyo imevipatia vikundi vinane vya wajasiriamali jumla ya shilingi milioni 244,500,000/- kama mpoko nafuu ikiwa ni awamu ya kwanza ya utoaji mikopo hiyo, kufuatia makubaliano baina ya benki hiyo na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC), kudhamini vikundi hivyo ili vifungue akaunti TPB na kujipatia mikopo huku NEEC ikiwa ndio wadhamini wakuu. Jumla ya shilingi bilioni 2 zimetengwa kwa lengo hilo. Wanoshuhudia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa NEEC, Anna Dominic, (wapili kushoto) na afisa wa baraza hilo
Bw. Moshingi akisalimiana na wana VICOBA

NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said


BENKI ya Posta Tanzania, TPB, imekabidhimkopo wa jumla ya shilingi milioni 244,500,000/- kwa vikundi vinane vya wajasiriamali.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Desemba 23, 2015 kwenye hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEEC).

Akizungumza kwenye makabidhiano hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, fedha hizo ni awamu ya kwanza ya benki kutoa mikopo hiyo yenye masharti nafuu, baada ya kutiliana saini na NEEC Julai mwaka huu wa 2015, ambapo baraza hilo litadhamini vikundi hivyo ambavyo vitapaswa kwanza kufungua akaunti TPB kabla ya kupatiwa mikopo hiyo ambayo jumla ya shilingi bilioni 2 zimetengwa kwa dhumuni hilo.


“Ninayo furaha kubwa kuwakabidhi nyinyi wajasiriamali ili muweze kutimiza ndoto zenu za kujikwamua kiuchumi.” Alisema Bw. Moshingi na kuhimiza vikundi zaidi vya wajasiriamali kujiunga na benki hiyo ili navyo vifaidi kwa wanachama wake kujiongezea mitaji kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, mgeni rasmi ambaye ni Kaimu Katibu Mtendaji wa NEEC, Bi. Anna Dominic, alisema, baada ya NEEC kuona takwimu zinaonyesha kuwa hapa nchini ukosefu wa ajira ni moja ya changamoto kubwa kabisa na hivyo inahimiza wananchi kujiunga kwenye vikundi ili NEEC kwa kushirikiana na taasisi nyingine kama TPB, kuweza kuwapatia mikopo kwa ajili ya kufanya shughuli za kiuchumi.

“Ningependa kuwaasa wajasiriamali mliopokea mikopo hiyo, kufanya kazi kwa bidii kama ulivyo msimamo wa serikali ya awamu ya tano chini ya Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya “Hapa Kazi Tu”.” Alisema na kuwahimiza kutumia vizuri mikopo hiyo kwa shughuli zilizokusudiwa ili waweze kurejesha tena kwa wakati.

Akitoa shukrani zake baada ya kupokea mkopo huo kwa niaba ya wenzake, Mkurugenzi wa Shirika la Vijana Wajasiriamali na Uwezeshaji Tanzania, (TYEEO), Bw. Ayub Gerald Luhuga, aliishukuru TPB kwa kuwaunga mkono katika kuhakikisha wajasiriamali wanakuza mitaji yao ili kujikwamua kiuchumi, na kuahidi kuwa mikopo hiyo itatumika kama ilivyokusudiwa na kurejeshwa kwa wakati.

Bi. Anna akitoa hotuba yake
Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo ya TPB, Bw.Henry Bwogi, (kulia), Mkurugenzi wa Masoko wa TPB, Bw.Deogratius Kwiyukwa, (katikati), na Meneja Mikopo ya Vikundi ya TPB, Bw.Ramadhan Liganga, wakibadilishana mawazo
Bw.Moshingi, (kushoto), akimsikiliza Bw. Kwiyukwa, huku Afisa Habari Mwandamizi wa TPB, Bw.Theo Mwakifulefula akisikilzia
Mmoja wa wajasiriamali akipiga makofi kufurahia jambo.





Mkurugenzi wa Idara ya Mikopo ya TPB, Bw.Henry Bwogi,(kushoto) na Mkurugenzi wa Masoko wa TPB, Bw.Deogratius Kwiyukwa, (katikati), wakimsikiliza mkurugenzi wa TYEEO, Bw. Ayubu
Bw. Ayubu akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wajasiriamali wenzake
Picha ya pamoja

Kuchelewa kwa Miradi ya umeme, DSM Dkt. Kalemani aagiza iendelee kutekelezwa Jan 20

$
0
0
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, (wa kwanza kushoto), akiongozwa na Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO, Gregory Chegere kukagua maendeleo ya  mradi wa kuboresha miundombinu ya usafirishaji na  usambazaji umeme katika Jiji la Dar es Salaam katika kituo cha Mbagala. Kulia ni Mhandisi wa miradi (TANESCO), Frank Mashalo. Wengine nyuma ni Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Paul Masanja (nyuma kulia) na Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia maendeleo ya Nishati, James Andilile.
 Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO, Gregory Chegere (kushoto) akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kulia) kuhusu maendeleo ya kituo cha usafirishaji na usambazaji umeme cha Mbagala jijini Dar es Salaam. Kituo hicho kimejengwa kupitia mradi wa Tanzania Energy Development and Acess Program (TEDAP) chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia. Wengine wanafuatilia ni Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Paul Masanja (nyuma kulia) na Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia maendeleo ya Nishati, James Andilile, wengine ni Maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO.
 Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Paul Masanja (wa pili kulia) akibadilishana jambo na Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile (wa kwanza kulia) huku Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza kushoto) akibadilishana jambo Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO, Gregory Chegere (wa pili kulia) wakati Dkt. Kalemani alipotembelea maendeleo ya ujenzi huo unajengwa na Kampuni ya SAE Power Line ya Italia kwa ushirikiano na Transrail Structures.
 Mkandarasi Kampuni ya SAE Power Line ya Italia inayoshirikiana na kampuni Transrail Structures, inayojenga miradi ya kuboresha miuundombinu ya kusafirisha na kusambaza umeme katika jiji la Dar es Salaam kupitia mradi wa Tanzania Energy Development and Access Program (TEDAP), akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) kuhusu ujenzi wa Kituo cha Kurasini wengine wanaofuatilia ni viongozi waandamizi Wizara ya Nishati na Madini, Maofisa kutoka TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini.

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akizungumza na Meneja Mawasiliano Ofisi ya TANESCO, Kinondoni Kusini. Naibu Waziri alifika ofisini hapo katika ziara ya kushtukiza ili kujua kero mbalimbali zinazokutana nazo wananchi ikiwa pia kuangalia namna ofisi hizo zinavyowahudumia wananchi. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja na Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile. Kushoto ni Meneja wa TANESCO, Kinondoni Kusini, Gasper Msigwa.
 Meneja wa TANESCO, Kinondoni Kusini, Gasper Msigwa, kulia akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza kushoto) wakati Dkt. Kalemani alipofanya ziara ya kushtukiza ofisini hapo kuona namna TANESCO inavyowahudumia wananchi. Nyuma ya Dkt. Kalemani na Naibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja. Kulia nyuma ni Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James Andilile na wengine ni Maofisa wa Wizara na Wanahabari.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa kwanza kulia) akiongea jambo na watumishi wa ofisi ya Huduma kwa Wateja (TANESCO) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika ofisi ya TANESCO Kinondoni Kusini.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja, wakimsikiliza Mzee Rashid Bago Mkazi wa Manzese aliyefika ofisi za TANESCO Kinondoni Kusini kupata huduma. Naibu Waziri alifanya ziara ya kushtukiza ofisini hapo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akizungumza na baadhi ya wateja waliokuwa wakisubiri kuhudumiwa sehemu ya huduma za wateja katika Ofisi ya TANESCO Kionondoni Kusini.  Wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja. Wengine ni Maofisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO.


Kuchelewa kwa Miradi ya umeme, DSM
ØDkt. Kalemani aagiza iendelee kutekelezwa Jan 20

Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam
Kufuatia kuchelewa kukamilika kwa miradi ya ujenzi wa Kuboresha miundombinu ya Kusafirisha na Kusambaza umeme katika jiji la Dar es Salaam kupitia mradi wa Tanzania Energy Development and Access Program (TEDAP) chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, Mkandarasi Kampuni ya SAE Power Line ya Italia kwa ushirikiano na Transrail Structures, wametakiwa kukamilisha miradi hiyo ifikapo mwezi Februari mwakani.

Hatua hiyo inafuatia ziara ya Dkt. Kalemani kutembelea ujenzi wa miundombinu hiyo jijini Dar es Salaam, katika vituo vya Kurasini, Mbagala, Kipawa na Gongolamboto, inayosimamiwa na TANESCO, ambayo kukamilikwa kwake kutawezesha zaidi ya wakazi 10,000 wa jijini Dar es Salaam, kuunganishwa na nishati  ya umeme.

Dkt. Kalemani ameiagiza TANESCO, kuhakikisha kuwa, hadi ifikapo  tarehe 15 Januari mwakani, iwe imekwishawalipa fidia wakazi 83 wa Mbagala  Charambe, Kiburugwa na Kitunda  ambao walikubali  fidia ya kiasi cha shilingi 717 milioni zilizotengwa kupisha ujenzi wa mradi huo.

“Bado kuna wananchi wapatao 23 ambao hawajaridhia malipo ya fidia yao. TANESCO kamilisheni mazungumzo hayo haraka walipwe ili kupisha ujenzi uendelee, kwa sababu hatuwezi kusababisha watu zaidi ya elfu 10 kukosa umeme sababu ya watu 23. Nataka ifikapo tarehe 20 Januari Mkandarasi aendelee na kazi,”alisema Kalemani.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kalemani aliwataka wananchi kushirikiana na Serikali ili kuwezesha miradi mbalimbali ya umeme kutekelezwa kutokana na umuhimu wa nishati hiyo kiuchumi. “Kama kuna wananchi wanazuia miradi ya umeme tupeni nafasi tufanye kazi, umeme ni uchumi na maendeleo”,aliongeza Dkt. Kalemani.

Pia, ameitaka TANESCO, kuhakikisha inaacha urasimu wa kukatwa kwa umeme hasa kipindi cha kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka za Christmas na mwaka mpya ili kuwafanya wananchi wapate huduma hiyo muhimu.

Naye, Mhandisi Mkuu wa Miradi, Frank Mashalo, kutoka TANESCO alieleza kuwa, kuchelewa kukamilika kwa wakati kwa miradi hiyo kumetokana  na wananchi wa baadhi ya maeneo ya Mbagala kugomea malipo ya fidia.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Paul Masanja, akitoa majumuisho alieleza kuwa, ziara hiyo imesaidia kuona udhaifu wa utekelezaji wa miradi hiyo na hivyo aliahidi kuhakikisha kwamba mapungufu yote yanayafanyiwa kazi na kukamilika kwa mujibu wa maagizo na maelekezo ya Dkt. Kalemani. 

Kwa upande wake Kamishna Masaidizi wa Nishati, anayeshughulia Maendeleo ya Nishati, James Andilile, alisema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo utafuatiliwa kwa karibu ikiwemo kuhakikisha kwamba changamoto za mradi huo zinatafutiwa suluhisho la kutosha.

Gharama za ujenzi wa mradi huo ulioanza mwaka 2010 na kusainiwa mwaka 2012 ni Dola za Marekani milioni 34.2 ambapo tayari serikali imekwishalipa dola za Marekani milioni 28. 

Mbali na Dar es Salaam, mradi wa kuboresha miundombinu ya Kusafirisha na Kusambaza Umeme wa (TEDAP) pia unatekelezwa katika mikoa ya Arusha, na Kilimanjaro.

Katika hatua nyingine, Dkt. Kalemani alifanya ziara ya kushtukiza katika ofisi ya TANESCO, Kinondoni Kusini ili kuona namna wananchi wanavyohudumiwa katika ofisi hizo na kuangalia utendaji kazi wa ofisi hiyo.

Serikali yamaliza mgogoro wa timu ya soka ya Shinyanga Stand United

$
0
0
un2
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hatua zilizofikia katika kutatiua mgogoro baina ya Timu ya Stand Unite ya mjini Shinyanga na kamati ya uendeshaji ya timu hiyo iliyopo chini ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa leo jijini Dar es Salaam.Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,WHUSM.
un1
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji ya timu ya Stand United ya mjini Shinyanga wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Habaroi, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (hayupo pichani) wakati wa kikao baina yao na Waziri huyo leo jijin Dar es Salaam.
un3
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (kushoto)akifuatilia maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa timu ya Stand United Bw. Aman Vicent (katikati)wakati wa kikao baina ya wajumbe wa Kamati tendaji ya Club hiyo na Mhe. Waziri ili kujadili mgogoro unaoikabili timu hiyo leo jijini Dar es Salaam.

………………………………………………………………………………………….
Na: Frank Shija, WHUSM.

Serikali imeagiza kumalizika kwa mgogoro uliopo baina ya Timu ya mpira wa miguu ya Stand United na Kamati ya uendeshaji wa timu hiyo iliyopo chini ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Agizo hilo limetolewa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye mara baada ya kumaliza kikao na uongozi wa Stand United.

Nape amesema kuwa imefika wakati vilabu vikapewa uhuru wa kujiendesha kwa kutumia katiba zao badala ya kingiliwa na chombo kingine chenye  maslahi binafsi.

“Wizara itasaidia kuona mgogoro huu unaisha kwa Stand United kupewa uhuru wa kujiendesha yenyewe na uongozi uliokuwapo kupewa mamlaka yake ya kusimamia na kuendesha shughuli za Timu yao kwa mujibu wa Katiba”

Aidha aliongeza kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kusimamia uendeshaji wa mchezo wa mpira wa miguu kwa kuzingatia sheria ,kanuni na taratibu za mchezo huo ili kuepuka migogoro isiyokuwa na tija.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Timu ya Stand United Bw. Aman Vicent ameishukuru Serikali kupitia Wizara yenye dhamana na masuala ya michezo kwa kuona umuhi wa kushughulikia na kumaliza mgogoro wao.

Aman amesema kuwa kutokana na makubaliano waliyofikia katika kikao hicho imani yao ni kuwa suala hili litamalizika mapema kwa kuwa Waziri mwenye dhamana ameonyesha nia na utayari wa kuhakikisha suala hili linaisha kwa wakati ili Timu iweze kusonga mbele katika kujiletea maendeleo.

Kikao baina ya Waziri na uongozi wa Timu hiyo kimefanyika ikiwa ni matokeo ya juhudi za uongozi wa Timu ya Stand Uinted kuinusuru timu yao baada ya kujikuta katika mgogoro usiokuwa na tija zaidi ya maslahi binafsi kutoka na udhamini walionao.

Serikali yasisitiza Umuhimu wa Utunzaji Nyaraka kwa Waombaji Kazi

$
0
0

Msemaji wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bi. Riziki Abraham (kushoto) akiongea na waandishi wa Habari kuhusu Umuhimu wa Utunzaji Nyaraka kwa waombaji kazi katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Jijini Dar es Salaam, kulia ni Naibu katibu anayehusika na Udhibiti na Ubora Bw. Humphrey Mniachi .
Naibu Katibu Kutoka Sekretarieti ya Ajira anayesimamia Idara ya Udhibiti na Ubora Bw.Humphrey Mniachi akitoa Ufafanuzi wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari kuelezea Umuhimu wa Utunzaji Nyaraka kwa waombaji kazi kushoto ni Msemaji wa Sekretarieti ya Ajira Bi. Riziki Abraham.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bi. Riziki Abraham (Kushoto) akionyesha vipeperushi kwa waandishi wa Habari vinavyoelezea utekelezaji wa Mchakato wa Ajira Serikalini kulia ni Naibu katibu Ofisi hiyo anayehusika na Udhibiti na Ubora Bw. Humphrey Mniachi .

Sehemu ya waandishi wa habari wakifuatilia Mkutano
huo.  Picha na Fatma Salum)

……………………………………………………………………………………….
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma katika kutekeleza jukumu lake la uendeshaji wa mchakato wa Ajira serikalini imekuwa ikikumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya matukio ya upotevu wa vyeti vya kitaaluma na nyaraka nyingine za msingi kutoka kwa waombaji kazi.
Tunaendelea kusisitiza na kuwakumbusha wadau wetu kwamba miongoni vya vigezo vya msingi vinavyotumiwa na Sekretarieti ya Ajira pamoja na Waajiri ili kujua kama muhusika anayeomba kazi ana sifa na vigezo vinavyotakiwa katika nafasi husika ni pamoja na kuwa na
vyeti vya kuhitimu taaluma husika. 

Takribani waombaji kazi 256,928 wamekosa fursa ya kuitwa
kwenye usaili ili kuweza kuajiriwa Serikalini kutokana na sababu mbalimbali  zikiwemo za kutokuwa na vyeti vya kitaaluma, kutozingatia vigezo vya tangazo la kazi, kuomba nafasi ya kazi ambayo mwombaji hana sifa zinazokidhi nafasi hiyo.  

Kumekuwa na tatizo kutoka kwa baadhi ya Waombaji kazi wengi kutotambua umuhimu wa kutunza Vyeti vyao vya kitaaluma na nyaraka nyinginezo kama vitambulisho, vyeti vya kuzaliwa, hati ya kusafiria pamoja na barua za utambulisho. Imekuwa  ni kawaida kwa waombaji kazi wanaowasilisha maombi ya ajira kukuta baadhi yao hawana
vyeti kwa maelezo kuwa vyeti/cheti kimepotea/kimeibiwa, kimeungua, kimeliwa na panya, kiliingia maji ya mafuriko na baadhi yao kutunziwa vyeti na wazazi wao kama ”Custodian” wao wa kuhifadhi vyeti ama nyaraka husika.  

Baada ya kukutana na changamoto hizi, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma itaendelea kuimarisha mifumo yake ya utambuzi ili waombaji kazi wasio na vigezo wasiweze kupata fursa ya kuajiriwa katika Utumishi wa Umma. Hii inatokana na sababu kwamba kuwaajiri watu wasio na sifa katika Utumishi wa Umma kuna athari kubwa katika maendeleo ya Nchi yetu na ina athari kwa jamii yote ya Watanzania. 

Sekretarieti ya Ajira inapenda kuwasisitizia wadau wake hususani waombaji kazi kuwa ni muhimu wakatambua vyeti ni ajira, vyeti ni maisha, vyeti ni utambulisho na uthibitisho. Kwa kuwa hakuna anaeweza kuajiriwa serikalini bila ya kuwa na vyeti halisi na halali maana Serikali inaendesha mchakato wa Ajira kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu na si vinginevyo. Hivyo ni vyema wakavihifadhi katika sehemu iliyo salama ili kuvitumia pindi vinapohitajika na kwa wale waliopoteza, kuibiwa, kuungua wakatoe taarifa kwa mamlaka husika ili waweze kujua taratibu za kufuata ili kuweza kuendelea kupata huduma katika mamlaka mbalimbali. 

Aidha, chombo hiki kitaendelea kukagua nyaraka zinazowasilishwa na waombaji kazi ili kubaini wale wote wasiokuwa na sifa stahili pamoja na wanaotumia vyeti vya kughushi kwa ajili ya kupata kazi serikalini ili kuhakikisha kuwa watu wa namna hiyo hawapati nafasi ya kuingia katika Utumishi wa Umma.  Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. 23 Desemba, 2015.

Utanipenda ya Diamond yatazamwa na watu zaidi ya 800,000

$
0
0
DiamondVideo mpya ya staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz imetazamwa na watu zaidi ya laki nane na tisini kwa muda wa wiki moja tangu itoke Desemba 11, mwaka huu. Mkali huyo wa Bongo Fleva anatarajia kuangusha bonge moja la shoo ndani ya Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakhem, jijini Dar siku ya Krismasi, keshokutwa.
DIAMOND (3) 
 Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz.
Akizungumzia maandalizi ya shoo hiyo, Diamond alisema itakuwa ya tofauti. Kila atakayelipia fedha yake ( kawaida shilingi 15,000 na V.I.P shilingi 30,000) hatojutia. "Tukutane pale Dar Live, tuimbe na kucheza nyimbo zote za Diamond kuanzia Kamwambie, Lala Salama, Moyo Wangu, Mbagala, Nimpende Nani, Nitarejea, Ukimuona, Nataka Kulewa, Kesho, Nasema Nao, Mawazo, Number One, Nana, Nitampata Wapi, Kizaizai, MdogoMdogo, BamBam na Utanipenda ambao ndiyo habari ya mjini kwa sasa," alisema Diamond. https://www.youtube.com/watch?v=LSk_M7d_OWM

WAZIRI KITWANGA ATANGAZA OPERESHENI YA KUKAMATA WAHAMIAJI HARAMU NCHINI

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai) akiwasalimia wananchi  wanaosubiri kupata huduma ya Hati za Kusafiria katika Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Waziri Kitwanga alifanya ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na Uhamiaji. Katika hotuba yake, licha ya maelekezo mengine aliyoyatoa kwa viongozi wakuu, pia aliitaka Idara hiyo ya Uhamiaji kuanza rasmi kwa operesheni ya kuwakamata Wahamiaji Haramu nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Afisa Uhamiaji anayeshughulika na uchapaji wa Hati za Kusafiria, Amir Hassan (kushoto), akitoa maelezo ya jinsi wanavyozichapisha Hati za Kusafiria, kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) ambaye alifanya ziara ya kikazi katika ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile (kushoto) akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, wakati Waziri huyo alipokuwa anafanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Uhamiaji. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiwaeleza jambo Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya idara hiyo, Kurasini, jijini Dar es Salaam leo. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (wasita kulia), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (watano kushoto), Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo (wanne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati Waziri huyo alipotembelea Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Wasita kushoto ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akimsalimia Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile wakati alipowasili Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil, na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Katika ziara hiyo, Waziri Kitwanga aliitaka Idara hiyo ya Uhamiaji kuanz rasmi kwa operesheni ya kuwakamata Wahamiaji Haramu nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

Ma-RC, Ma-DC DHIBITINI MIGOGORO YA ARDHI – WAZIRI MKUU

$
0
0

maj2

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa wanaongeza udhibiti na usimamizi wa migogoro ya  ardhi kwenye maeneo yao husika.
 Ametoa agizo hilo leo mchana (Jumatano, Desemba 23, 2015) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa wa Lindi kwenye Ikulu ndogo mara baada ya kuwasili akitokea jimboni kwake Ruangwa.

“Ardhi ni mali ya Serikali lakini maeneo yanayotwaliwa kwa sababu mbalimbali za maendeleo yasiwe chanzo cha migogoro na wananchi tunaowaongoza,” alisema.

Akitoa mfano, Waziri Mkuu alisema anatambua kuna mgogoro wa eneo la mgodi katika wilaya ya Ruangwa baina ya wananchi na wawekezaji wa kampuni ya Uranex. Na hii ni kwa sababu wao ndiyo waliamua kufanya tathmini (evaluation) ya eneo hilo. Yale ni makosa kwa sababu aliyepaswa kufanya tathmini ni Halmashauri na siyo mwekezaji,” alisema.

Alisema wawekezaji wanaruhusiwa kisheria kufanya tathmini lakini sheria waliyoitumia ni sheria namba 8 peke yake. “Kama Halmashauri ingefanya kazi hiyo ni lazima wangetumia sheria ya ardhi ya vijiji pamoja na sheria ya madini na wananchi wangepata thamani halisi ya ardhi yao,” alisema.

“Ninaagiza Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ikahakiki lile eneo na kubaini kama ni la kilimo au la madini na kama ni la kilimo, wananchi wamelima mazao gani na kwa muda gani kisha wafanye tathmini upya. Yuko valuer wa Halmashauri mwenye dhamana hiyo na siyo wao,” alisema.

“Nasisitiza tena ni vema Wakurugenzi wote, Wakuu wa Wilaya chini ya uongozi wa Wakuu wa Mikoa mjiridhishe kuwa hakuna migogoro kwenye maeneo yenu. Kama ipo, imalizeni kwa kukaa mezani na kuzungumza na pande husika, inawezekana kabisa,” alisisitiza.

WAZIRI WA AFYA AMSIMAMISHA KAZI KAIMU MKURUGENZI WA TAASISI YA OCEAN ROAD DK.DIWAN MSEMO.

$
0
0
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
WAZIRI wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk.Diwani Msemo ili kupisha uchunguzi pamoja na mambo mengine ili kubaini  mgongano wa kimaslahi ulioathiri utendaji wa taasisi  hiyo chini ya kaimu mkurugenzi huyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto mwenye Wizara hiyo, Ummy Mwalimu imesema kuwa kutokana na ziara alizofanya Rais Dk. John Pombe Magufuli inaonyesha kukosekana kwa dawa katika hospitali za Serikali huku vituo vya afya vya  binafsi vikiwa na dawa.

Taarifa ya Waziri huyo imesema kuwa upungufu wa dawa umeendelea kujitokeza kwa karibu zaidi na baadhi ya wagonjwa walieleza kwa uchungu jinsi wanavyopata dawa kwa tabu hatazile wanazotakiwa wapate kwa bei ya ruzuku au zilezinazotakiwa kutolewa bure na serikali.

Kwa msingi wa uwazi na uwajibikaji ameagiza watendaji wote wa sekta afya hususani wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya, Wafamasia, Wauguzi na Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya kukiri kwa maandishi kwa ngazi zao za uwajibikaji endapo wanamiliki Hospitali, Zahanati, Kiliniki, Maduka ya Dawa ndani ya siku 21 kuanzia leo Desemba 23 mwa huu ambapo  agizo hilo limeotolewa.

Aidha taarifa hiyo imedai kuwa kufanya hivyo kutaziba mianya ya upotevu wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya umma.

Bodi ya Taasisi ya Ocean Road imeagizwa kutafuta mtu atakayekaimu nafasi iliyoachwa wazi na Dk.Msemo anayefanyiwa uchunguzi.

TTCL Yazindua Teknolojia ya 4G LTE

$
0
0


Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya (kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE inayotolewa na kampuni hiyo. Kushoto ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota akiwa katika mkutano huo.

Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) katika hafla ya TTCL kuzinduwa teknolojia ya 4G LTE iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya (kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.


Uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE toka TTCL leo.

Kulia ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE.

Kulia ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE.

Kushoto ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL na maofisa waandamizi wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE


KAMPUNI ya Simu nchini Tanzania (TTCL) leo imezinduwa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE unaoanza kutoa huduma jijini Dar es Salaam. Mtandao huo wenye teknolojia mpya na ya kisasa wenye kasi kubwa utatoa huduma katika maeneo 11 ambayo ni pamoja na Uwanja wa Ndege wa Mwalimu J.K. Nyerere, Pugu Road, Posta Mpya, Upanga, Kinondoni, Ubungo, Oysterbay, Mwenge, Mbezi Tangibovu, Mbezi Exchange, Kunduchi Salasala, na Wazi Tegeta.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akizinduwa rasmi teknolojia hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura alisema licha ya kuzinduwa huduma hiyo katika maeneo 11 kwa sasa mafundi wa kampuni hiyo wapo kazini wakiendelea na awamu ya pili ya kufunga mitambo ili huduma hiyo itolewe pia katika maeneo mengine 14 ya jiji la Dar es Salaam.

Aliyataja maeneo mengine ambayo mitambo inaendelea kufungwa kwa sasa kuwa ni pamoja na Kigamboni, Masaki, Temeke, Kimara, Jangwani, Kariakoo, Chuo Kikuu, Kurasini, Mbezi Chini Gongo la Mboto, Tabata, Kibamba, Kongowe na Bunju.

"...Awamu ya pili ya mradi huu itakuwa imekamilisha maeneo yaliyobaki ya mkoa wa Dar es Salaam na pia kupeleka mawasiliano hayo katika mikoa mingine ikiwa ni pamoja na Arusha, Mwanza, Mbeya, Dodoma na kwingineko," alisema Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kazaura.

Alisema uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE unakuwa umekamilisha nia ya siku nyingi ya kampuni ya TTCL ya kuwahudumia wateja katika nyanja zote za mawasiliano (Fixed-mobile convergence) kwa kutumia teknolojia ya simu za mezani na simu za mkononi.

Akifafanua zaidi Dk. Kazaura alisema uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE utakuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kuongeza kasi ya shughuli za maendeleo ya kijamii na kiuchumi, kuchangia katika kukuza teknolojia ya habari na mawasiliano na pia kuongeza uzalishaji kwenye sekta mbalimbali za maendeleo.

Aidha aliongeza kuwa TTCL inaamini mtandao wa 4G LTE utafungua fursa pekee katika kukuza sekta ya elimu nchini kwa njia ya mtandao (E education). Na pia ubora wa huduma hiyo ya intaneti utatoa fursa kwa wanafunzi, wakufunzi, wataalam, wanazuoni na walimu kutumia teknolojia katika kujifunza mambo mbalimbali ya kitaaluma na nje ya taaluma.

Kwa upande wake Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota akifafanua zaidi kwa wanahabari alisema mtandao wa 4G LTE utaongeza fursa katika sekta ya afya ambapo hospitali, vituo vya afya, vyuo vya afya na wadau mbalimbali wataweza kutumia mtandao huo katika kuongeza ufanisi wa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi tena kwa haraka zaidi.

Alisema mtandao huo pia utazinufaisha sekta nyingine za kiuchumi kama vile sekta ya biashara, viwanda, kilimo na nyinginezo. "...Wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa wanahitaji mawasiliano ya uhakika katika shughuli zao. Mtandao huu wa 4G LTE utakuwa mkombozi wao na utaleta mageuzi katika kuongeza uzalishaji, kupanua wigo wa masoko ya bidhaa kwa wakulima, masoko kwa wajasiliamali, masoko kwa makampuni ndani na nje ya mipaka ya Tanzania," alisema Peter Ngota.

Hata hivyo, Ngota aliongeza kuwa uzinduzi huo unaenda sambamba na uboreshaji vifurushi rafiki vya intaneti kwa wananchi hivyo kuwaomba wananchi kuiunga mkono kampuni ya kizalendo ya TTCL katika kuboresha huduma za mawasiliano nchini.

RAIS MAGUFULI AONANA NA MJUMBE MAALUMU WA RAIS PAUL KAGAME WA RWANDA NA MABALOZI WA USWISI NA KUWAIT

$
0
0
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Al Najem Ikulu jijini Dar es salaam leo Disemba 23, 2015.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na Mjumbe Maalum wa Rais Paul Kagame wa Rwanda ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Mhe. Louise Mushikwabo Ikulu jijini Dar es salaam leo Disemba 23, 2015.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na balozi wa Uswisi hapa nchini Mhe. Florence Tinguely Ikulu jijini Dar es salaam leo Disemba 23, 2015.

MAJALIWA AKABIDHI MSAADA WA PIKIPIKI NA PAMPU ZA MAJI

$
0
0
pu3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi  Bw.Bakari Amir pampu  mbili za kusukuma maji na mipira yake, Mwenyekiti wa kikundi cha kufyatua matofali ya kuchoma cha Jitumecha kilichopo eneo la Gogovivu wilayani Ruangwa  Desemba 23, 2015.  Pampu hizo zitawapunguzia wnakikundi mzigo wa kubeba maji toka mtoni. 
pu4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi funguo na kadi ya pikipiki Mwenyekiti wa kikundi cha Bodaboda Mkowe cha kijiji cha Nandagara, Yahya Chitanda ambayo ameikipatia kikundi hicho  Desemba 23, 2015 ili kiweze kukuza mtaji wake.
pu1
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa  akisalimiana na  maofisa wa jeshi la Polisi wakati alipotembelea kituo kikuu cha polisi zcha wilaya ya Ruangwa kusalimana na Askari Desemaba 23, 2015. Wapili kushoto ni mkewe Mary na watatu kushoto ni Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Lindi, Renata  Mzinga. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI ZA SIKUKUU YA KRISMASI KWA WATOTO WANAOISHI KWENYE KITUO CHA KUHUDUMIA WATOTO WA KIJIJI CHA MATUMAINI MKOANI DODOMA.

$
0
0
 Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Dodoma Bi. Ziada Nkinda (Aliyebeba Mtoto) akikabidhi zawadi za siku kuu ya Noeli (Christmas) zilizotolewa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa watoto wanaoishi kwenye kituo cha kuhudumia watoto cha kijiji cha matumaini Mkoani Dodoma.
Meneja wa kituo cha kuhudumia watoto cha kijiji cha matumaini kilichopo Dodoma  Padiri Vicent, kwa niaba ya watoto wa kituo hiko, akimshukuru Bi. ziada Nkinda kwa kukabidhi zawadi zilizotolewa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli zikijumuisha mchele kilo 121, Mbuzi wawili na mafuta ya kupikia lita 40 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya laki sita.
(PICHA NA OFISI YA MKUU WA MKOA DODOMA)

DAWASCO YAONGEZA USAMABAZAJI WA MAJI SAFI KUPAMBANA NA UGONJWA WA KIPINDUPINDU DAR

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Said Meck Sadick akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani ofisini kwake leo alipokutana nao kuelezea utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa kwa DAWASCO kuhusu usambazaji wa maji safi na salama ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Afisa Mtendaji Mkuu wa  DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani Dar es salaam  leo alipokutana nao kuelezea utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na  Serikali kuhusu usambazaji wa maji safi na salama ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.Picha zote na Ally Daud-Maelezo.


NA ALLY DAUD-MAELEZO

Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASCO) limeongeza uzalishaji na usambazaji wa Maji safi na Salama kwa wakazi wa jiji hilo hadi kufikia mita za ujazo 280,000 kwa siku ili kubabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu  uliolikumba jiji hilo hivi karibuni. 

Hatua hiyo inatokana na utekelezaji wa maagizo ya Serikali yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadiki kuitaka DAWASCO kusambaza maji safi na salama kwa wakazi wa jiji hilo ili kupambana na Ugonjwa wa Kipindupindu.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mkuu wa mkoa huo Bw. Sadick amesema kuwa kufuatia maagizo aliyoyatoa kwa shirika hilo ikiwemo kusambaza maji safi na salama kwa wananchi pamoja na kutengeneza mifereji ya kupitsha maji taka ili yasiingiliane na mikondo ya maji safi, DAWASCO wametekeleza kwa kiasi kikubwa maagizo hayo.

“Dawasco imehakikisha inazalisha maji safi na salama kati ya mita za ujazo 270,000 na 280,000 kila siku kwa muda wote tangu mlipuko ulipotokea na imehakikisha inasafisha na kusambaza kwa wananchi yakiwa katika viwango vya ubora unaokubalika kwa ajili ya matumizi kwa binadamu” amesema Bw. Sadick.

Ameongeza kuwa Dawasco imejenga vizimba vya maji  safi na salama kwenye maeneo mbalimbali ambayo hayajakumbwa na yaliyokumbwa na athari za mlipuko wa ugonjwa huo kwa jumla ya vizimba 48 ambavyo maeneo ya Kinondoni vizimba 5, Magomeni vizimba 38 na Ilala vizimba 5.

Aidha, amesema kuwa DAWASCO kwa kushirikiana na Ofisi ya Bonde Wami Ruvu imeanza kazi ya kusajili na kuwatambua watu binafsi wenye visima virefu vilivyopo kisheria ambao wanauza maji kwa wananchi ili kuvitambua na kudhibiti ubora wa maji na bei yake ambapo zoezi hili litaendelea hadi Machi 2016.

“Dawasco imefanya jitihada za kuweka dawa ya kuua wadudu aina ya chrolination kwenye maboza  wakati wa  usajili kabla ya kuruhusiwa kufanya biashara ya kuuza maji kwa wananchi na kuongeza sehemu za kuchota maji kwa kuwapelekea wananchi huduma hiyo wakitumia magari yenye matanki yaliyokuwepo kutoka 12 mpaka kufika 49 kwa sasa” aliongeza Bw.Sadick.Katika hatua nyingine Bw. Sadick alitoa rai kwa wakazi wa jiji hilo kuendelea na tabia ya kufanya usafi mara kwa mara ili kutokomezakabisa ugonjwa wa kipindupindu kwani kuanzia juzi hakuna wagonjwa waliopokelewa katika vituo vyote.

Kwa upande wa Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja alisema kuwa wako katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa mifereji ya kupitisha maji machafu ili isiingiliane na maji safi kwa wiki mbili zijazo.

“kufikia Februari mwakani tutaweza kutoa maji safi na salama ya kutosha kwa wananchi  wote wa Dar es salaam bila ya matatizo yoyote” alisisitiza Mhandisi Cyprian.   

Wanafunzi wa msingi International School of Tanganyika (IST) Alyanz Nasser na Shilen Dawda watengeneza mifuko mipya

$
0
0

Mkurugenzi Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Ofisi ya Mazingira, Bwana Julius Ningu (kulia) akiwapongeza Vijana wa Shule ya International School of Tanganyika (IST) mbele ya Waandishi wa Habari leo 23 Desemba, 2015 katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) kwa ubunifu wa kutengeneza mifuko kwa ajili ya utunza mazingira dhidi ya utupaji taka ovyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko Limited, Bwana Constantine Majavika, anaemfuatia ni Alyanz Nasser na mwenzie Shilen Dauda (wa pili kulia).
Mkurugenzi wa Masoko Limited, Bwana Constantine Majavika (kushoto) akifafanua kuhusu ubunifu uliofanywa na vijana wa Shule ya International School of Tanganyika (IST) mbele ya Waandishi wa
Habari leo 23 Desemba, 2015 katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) wa kutengeneza mifuko kwa ajili ya utunza mazingira dhidi ya utupaji taka ovyo. Kushoto ni Shilen Dauda na katikati ni Alyanz Nasser.

Kijana wa Shule ya International School of Tanganyika Alyanz Nasser (katikati) aieleza dumuni lao kubwa la kubuni mifuko ya Envirobags inayowezesha kuepukana na utupaji taka ovyo nchini wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo 23 Desemba, 2015 katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). Kulia ni Mkurugenzi Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Ofisi ya Mazingira, Bwana Julius Ningu, kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko Limited, Bwana Constantine Majavika na wa pili kulia ni kijana wa shule hiyo Shilen Dauda.
Mkurugenzi wa Masoko Limited, Bwana Constantine Majavika (kushoto) akionyesha aina za mifuko ijulikanayo kama Envirobags mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) itakayoweza kusaidia kuondokana na tatizo la utupaji taka ovyo nchini. Kulia ni Mkurugenzi Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Ofisi ya Mazingira, Bwana Julius Ningu akiangalia moja ya mifuko ya Envirobags.


Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia taarifa ya ubunifu uliofanywa na Vijana wa Shule ya International School of Tanganyika (IST) leo 23 Desemba, 2015 katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam.  (Picha zote na Benedict Liwenga) .
………………………………………………………
Na Skolastika Tweneshe.

VIJANA wawili wa Shule ya Msingi International School of Tanganyika (IST) Alyanz Nasser na Shilen Dawda wametangaza mifuko mipya ambayo imetengenezwa kwa malighafi nzuri
isiyoweza kuathiri mazingira.

Wakizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kwa nyakati tofauti wabunifu hao wamesema kuwa wameguswa na uharibifu wa mazingira hasa unaotokana na matumizi ya mifuko ya plastiki, hivyo wamebuni mradi wa kutengeneza mifuko ambayo haitaathiri mazingira hasa kwenye fukwe za bahari.

“Watanzania ni watumiaji wa mifuko ya plastiki hasa kwenye
fukwe hivyo maji yanapoelemewa na mifuko maji yanakuwa katika hatari.” alisema Alyanz Nasser.

Mbunifu mwingine Shilen Dawda ameeleza kuwa mifuko hiyo
imetengenezwa kwa ukubwa tofauti na inauzwa kati ya shilingi 400 mpaka 1200 ambapo hadi hivi sasa wameuza jumla ya mifuko 10,000 hivyo vijana hao wanaamini kuwa kwa matumizi ya mifuko hiyo Tanzania itakuwa safi na salama.

“Mpaka sasa tumeuza mifuko 10,000 na tunaamini kwa matumizi
ya mifuko hii Tanzania itakuwa safi na salama na viumbe hai wataendelea kuishi.” Alisema Dawda. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa
Rais Bwana Julius Ningu amesema kuwa Serikali inawapongeza vijana hao kwa kuguswa na uharibifu mazingira na kuwataka watanzania wote waunge mkono juhudi hizo za utunzaji wa Mazingira na kuacha kutumia bidhaa zinazoharibu Mazingira.

WE WISHING YOU HAPPY HOLIDAYS

SIMBACHAWENE AMSIMAMISHA KAZI MTENDAJI MKUU WA DART ASTERIA MAHIMBO

RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA MAWAZIRI KUJAZA NAFASI ZILIZOKUWA WAZI

$
0
0

pombe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
………………………………
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri alizobakiza wakati akitangaza baraza la Mawaziri la kwanza katika awamu ya tano ya utawala wake.

Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;
1. Profesa Jumanne Maghembe – Ameteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.
2. Dkt. Philip Mpango – Ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge).
3. Mhandisi Gerson Lwenge – Ameteuliwa kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.
4. Dkt. Joyce Ndalichako – Ameteuliwa kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi. (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge)
5. Mheshimiwa Hamad Masauni – Ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
6. Prof. Makame Mbarawa – Amehamishwa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na kwenda Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano
Katika hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia heri watanzania wote katika Sikukuu za Maulid, Christmas na Mwaka Mpya na kuwataka washerehekee kwa amani na utulivu. 
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
23 Desemba, 2015

WAZIRI SIMBACHAWENE ALIVYOMSIMAMISHA KAZI MTENDAJI MKUU WA BRT,BI ESTARIA MLAMBO

Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images