Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

SIKU YA WATOTO NJITI

$
0
0
 Mwanzilishi wa Mfuko wa Doris Mollel, Doris Mollel akizungumza katika kilele cha maazimisho ya siku ya watoto waliozaliwa kabla ya siku (njiti) katika mkutano ambao umefanyika leo kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Kulia ni mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick akizungumza kwenye maadhimisho hayo leo.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja, Aminiel Aligaesha akifuatilia mkutano huo leo pamoja na wauguzi waandamizi wa hospitali hiyo.

 Mmoja wa kinamama akiwa na mtoto wake ambaye alizaliwa kabla ya kutimiza siku akishiriki maadhimisho hay oleo katika hospitali hiyo.
 Mashine iliyotolewa kwa ajili ya kuwatunza watoto wanaozaliwa kabla ya muda. Mashine hiyo imetolewa leo na mfuko wa Doris Mollel kwa ajili ya kutunza watoto hao.
 Mmoja wa kinamama, Lipina Lyimo akizungumza katika kilele cha maazimisho ya siku ya watoto waliozaliwa kabla ya siku (njiti). Katika mkutano na waandishi wa habari Mama Lyimo amesema alijifungua mtoto kabla ya kutimiza muda na kwamba madaktari na wauguzi walimwelekeza jinsi ya kumtunza mtoto wake, Emmanuel Mgumba hadi amekuwa mkubwa na kuwa na afya bora.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick akiwa amembeba mtoto, Emmanuel Mgumba  ambaye alizaliwa kabla siku. Mama wa mtoto huyo Lipina Lyimo ameleza jinsi alivyopewa huduma nzuri na wauguzi na madaktari wa ‘Huduma ya Mama Kangaroo’ baada ya kujifungua mtoto kabla ya muda (njiti).

NEC YATANGAZA VITI VYA MADIWANI WATEULE1393

$
0
0
              Mkurugenzi wa Uchaguzi wa  NEC Bw. Kailima Ramadhani                           akizugumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya  viti maalumu vya Udiwani ambavyo Madiwani wake wameteuliwa na Tume hiyo  ni viti 1393, kutoka katika Vyama vya CCM,CHADEMA,NSSR-MAGEUZI pamoja na CUF.Mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam ,Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Huduma za Sheria wa NEC Emmanuel Kawishe.

Waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Uchaguzi wa  NEC Bw. Kailima Ramadhani
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii)

TUME ya Taifa ya Uchaguzi( NEC) imesema hadi sasa viti maalumu vya Udiwani ambavyo Madiwani wake wameteuliwa na Tume hiyo  ni viti 1393, kutoka katika Vyama vya CCM, CHADEMA, NSSR- MAGEUZI  pamoja na CUF.

Hayo yamesemwa leo Jijijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka NEC Bw. Kailima Ramadhani wakati akitoa  taarifa kwa Umma kuhusu uteuzi wa madiwani wanawake wa Viti Maalumu.

Aidha Bw.Ramadhani amesema kuwa idadi ya Viti maalumu Vya Udiwani ni  1,408 nakwamba kutokana na majimbo nane na kata thelathini na Nne ambapo  Uchaguzi haujakamilika kwa Sababu mbalimbali, hatua hiyo itasababisha kubakia viti 15 ambavyo vitagawanywa mara baada ya Uchaguzi kukamilika ili kufikia idadi ya viti 1,408 kutoka viti 1393 vinavyo tambulika kwa sasa.

Aidha amefafanua kuwa kutokana na Viti hivyo  Maalumu Vya Udiwani Vilivyoteuliwa  na NEC, Chama Cha Mapinduzi CCM kimepata viti 1,022,Chama Cha Demokrasia na Mawendeleo CHADEMA 280,Chama Cha Wananchi CUF-79, ACT WAZALENDO viti 6 pamoja na NSSR  MAGEUZI viti 6.

Amesema kuwa tume imeamua kutoa taarifa ya uteuzi wa  viti maalumu Vya Udiwani Nchi nzima ya Madiwani waliyoteuliwa na Tume  kutokana na Kanuni za Kudumu za Mikutano ya Halmashauri, Mabaraza ya Madiwani yanatakiwa kuitishwa siku thelathini tangu tarehe ya Uchaguzi ifanyike.

Katika hatua Nyingine Mkurugenzi huyo wa Uchaguzi  NEC amesema kuwa  mwisho wa Uchaguzi katika Majimbo na Kata ambazo hazikufanya Uchaguzi ni Desemba 20 mwaka huu, ambapo katika jimbo la Uranga Mashariki pamoja na Lushoto uchaguzi utafanyika Novemba 22 mwaka huu,nakuwaomba  Wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuchagua kiongozi wanaomtaka.

SERIKALI KUBORESHA HUDUMA YA MAJI KWA WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM.

$
0
0
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maji, Athumani Sharif akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mikakati ya Serikali kutatua tatizo la upatikanaji wa maji jijini Dar es Salaam mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa. (Picha na Fatma Salum.)

Na. Georgina Misama - Maelezo
SERIKALI  inatarajia kuzalisha maji lita milioni 270 kwa siku baada ya kukamilika kwa mradi wa upanuzi wa Chanzo cha Maji cha Ruvu Chini na upanuzi wa mtambo wa kusafishia maji.

Mradi huo  unaotekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimarekani la Millenium Challenge Co-operation umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 66.24 na unatarajiwa kukamilika wakati wowote baada ya kukamilika kwa kazi ya kulaza bomba linalosafirisha maji toka Ruvu chini kuja Jijini Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari, leo Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maji, Bw. Shariff Athumani amesema kwamba mradi wa upanuzi wa mtambo wa ujenzi wa bomba la Ruvu Chini utapunguza kero ya maji kwa wakazi wote wanaotumia maji kutoka Ruvu Chini.

Akiyataja maeneo yatakayofaidika na kukamilika kwa mradi huo ni pamoja na Bagamoyo na vitongoji vyake, Bunju, Mabwepande, Boko, Tegeta Kunduchi na Mbezi Beach. Maeneo mengine ni pamoja na Mbezi Juu, Salasala, Kawe, Makongo, Chuo Kikuu, Mikocheni, Msasani, Masaki, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Sinza, Manzese, Ubungo, Mabibo, Kigogo, Buguruni, Ilala, Kurasini, Bandarini na maeneo yote ya katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Jaji mkuu wa Tanzania akutana na watendaji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

$
0
0
 
Jaji mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman (wa tatu kutoka kulia) katika picha ya pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi walipomtembelea ofisini kwake hivi karibuni, Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Alphayo Kidata akifuatiwa na Subira Sinda Msajili wa Hati. Nyuma ya Katibu Mkuu ni David Mushendwa Kamishna wa ardhi Msaidizi Sheria, Blasia Kibano (Wa kwanza kulia) aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria pamoja na Juma Lughela.

KOBE 201 WALIOKUWA WAKISAFIRSHWA NJE YA NCHI WAKAMATWA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA J.K NYERERE

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akikagua mabegi matano yenye Kobe 201 yaliyokamatwa usiku wa kuamkia leo na askari wanyamapori kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika uwanja wa Kimataifa wa J.K. Nyerere jijini Dar es Salaam.  

Watuhumiwa hao wa usafirishaji wa wanyamapori wametajwa kuwa ni David Mungi mkazi wa Muheza Mkoani Tanga na Mohammed Suleiman (43) mkazi wa Zanzibar ambao katika tukio hilo walishafanikiwa kupita kwenye mitambo ya ukaguzi lakini mbwa maalum (sniffer dogs) wakasaidia kugundua uhalifu huo. Kwa pamoja watuhumiwa hao walikamatwa na tiketi za kusafiria kuelekea nchini Malaysia. 

Kobe wapatao 201 waliokamatwa na askari wanyamapori kwa ushirikiano na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutumia mbwa maalum (sniffer dogs).   
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii Bi. Dorina Makaya kulia na Mmoja wa Askari wanyamapori wakiangalia kobe 103 waliotelekezwa eneo la Tabata hivi karibuni baada wahalifu waliohusika kuhofia kukamatwa na vyombo vya dola. 
(Picha na Hamza Temba - Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii)

RAIS MAGUFULI ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO KATIKA UBALOZI WA UFARANSA NCHINI

$
0
0
po1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha Maombolezo katika Ubalozi wa Ufaransa nchini kufuatia vifo vya Watu zaidi 130 vilivyotokana na mashambulizi ya kigaidi.
po2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Malika Berak kufuatia vifo vya Watu zaidi 130 vilivyotokana na mashambulizi ya kigaidi.
po3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Balozi wa Ufaransa nchini Malika Berak Tanzania mara baada ya kusaini Kitabu cha Maombolezo na kutoa salamu za pole kwa Rais wa Ufaransa Mheshimiwa Francois Hollande kufuatia vifo vifo vya Watu zaidi 130 vilivyotokana na mashambulizi ya kigaidi.
po4
. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wa pili akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ufaransa (kushoto) pamoja na Maofisa mbalimbali wa Ubalozi huo mara baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo.
po5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Malika Berak mara baada ya kusaini kitabu cha Maombolezo Ubalozini hapo.
………………………………………………………………………………..
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli amesaini kitabu cha Maombolezo katika Ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es salaam kufuatia vifo vya watu zaidi 130 vilivyotokea November 15, 2015 kutokana na mashambulizi ya ugaidi mjini Paris, Ufaransa.
 Pamoja na kutia saini kitabu cha maombolezo, Mheshimiwa Dr. Magufuli ametoa salamu za pole kwa Rais wa Ufaransa Mheshimiwa Francois Hollande na kumuombea uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu Dokta Magufuli ambaye amepokelewa na Balozi wa Ufaransa hapa Nchini Bibi Malika Berak amesema Tanzania imeguswa na vifo hivyo na inaungana na Ufaransa katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
 Aidha Rais Magufuli amewaombea majeruhi wote wa tukio hilo wapone haraka ili waweze kuungan a na familia zao na kuendelea na shughuli zao za kila siku Katika hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli amewasili Mjini Dodoma jioni hii kwa shughuli mbalimbali za kikazi.
 Mheshimiwa Magufuli amesafiri kwa gari kutoka Dar es salaam hadi Dodoma na taarifa ya shughuli atakazozifanya mtaarifiwa baadaye.

Imetolewa na;Gerson MsigwaKurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,IKULUNovember 17, 2015

JAHAZI MODERN TAARAB KUTAMBULISHA NYIMBO ZAO MPYA NDANI YA JIJI LA ARUSHA DECEMBER 11

$
0
0
 Mfalme mzee Yusuphy akiwa anawatumbuiza wapenzi wa bendi ya Jahazi modern taaraba Woinde Shizza,Arusha



Bendi ya muziki wa taarabu ijulikanayo kwa jina la Jahazi  modern taarab inayomilikiwa na  mfalme mzee yusuphy inatarajia kutua rasmi jijini Arusha kwa ajili ya kuitambulisha  album mpya inajulikana kwa jina la Mahaba niuee.



Akizungumza na waandishi wa habari muandaaji wa onyesho hilo ambaye ni mkurugenzi wa phide entertainment, Phidesia Mwakitalima alisema kuwa  bendi hiii ya jahazi inatarajiwa kutua jijini Arusha na kufanya onyesho lao December 11  ambapo litafanyika ndani ya ukumbi wa Triple A com lex uliopo ndani ya jiji hili.



Alisema kuwa mpaka sasa utaratibu wote umekamilika na wanangoja tu siku ya onyesho ambapo alieleza kuwa onyesho hili litakuwa rasmi kwa ajili ya kutambulisha albamu mpya ya jahazi pamoja na kutambulisha nyimbo zilizopo katika alibamu hiyo.



Aidha alitaja baadhi ya nyimbo zilizopo katika albamu hiyo na ambazo zitatambulishwa kwa wapenzi wa jahazi modern taarabu kuwa ni pamoja na nyimbo iliyobeba albamu  Mahaba niueee,alibainisha kuwa pamoja na uzinduzi huu hii pia itakuwa  ni sehemu ya ziara yao kufunga mwaka Tanzania nzima kwa bendi hii ya muziki wa Taarabu.



Phidesia aliwasihi wakazi wa mji wa Arusha pamoja na vitongoji vyake wajitokeze kwa wingi kwani wasanii wote ,waimbaji wote wacheza show wote na wake wote wa mzee yusuphy watakuwepo katika onyesho hilo.



Aliwataja baadhi ya wadhamini wa onyesho hilo kuwa ni pamoja na Geo security, kwa udhamini mkubwa wa Geo Security Arusha kampuni  bora ya ulinzi, security power fance na alarm  ambapo alisema na katika siku hiyo ya onyesho  watakuwepo pia kwa ajili ya usalama wa wapenzi wote   kuhakikisha mnarudi salama majumbani salama .


JIJI LA MBEYA HATARI KUKUMBWA NA UGONJWA WA KIPINDUPINDU

$
0
0

Wafanyabiashara ndogo ndogo katika eneo la Makunguru jijini Mbeya wakiendelea na shughuli zao kama kawaida .

Na Mwandishi wetu,Mbeya
Halmashauri ya jiji la Mbeya limewataka wafanyabiashara ndogondogo hususani wa chakula  kujijengea tabia ya kuchoma taka nyakati za jioni mara wamalizapo kuuza biashara zao na si kusubili gari ya taka kuja kuzoa.

Aidha imewataka  wakazi hao kuondokana na fikra duni  ya kuamini kuwa kazi ya uzoaji wa taka na kusafisha mazingira ni ya halmashauri ya Jiji na sio mali ya mtu.

Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Jiji la Mbeya, Dkt. Samweli Lazaro, amesema, wananchi wanatakiwa kujenga tabia ya usafi na sio kusubili kupigizana kelele na serikali kwa kuwahimiza kufanya usafi kwani adui mkubwa wa afya ni uchafu hivyo kila mmoja anapaswa kuwa mlinzi wa mwezake katika kutunza mazingira.

Hali hiyo imesababisha kuwepo kwa malimbikizo mengi ya taka  kwenye sehemu zisizorasmi  ndani ya JIji la Mbeya na kupelekea jiji hilo kuwa chafu hususani katika maeneo ya  sokoni.

Amesema, hivi sasa halmashauri ilianzisha mpango wa uzoaji wa taka barabarani ambapo mpango huo umeonekana  kupokelewa na wananchi kwa asilimia 100 changamoto inakuja kwa upande wa halmashauri kuonekana kuzidiwa kutokana na ukosefu wa vitendea kazi.

“Halmashauri ilianzisha zoezi la kupitia taka zinazozalishwa na wananchi ambazo huziweka barabarani na magari yanapitia lakini mapango huu umeonekana kuzaa matunda kwa jamii kuupokea lakini tatizo ni uhaba wa vitendea kazi,”alisema.

Alisema, ili zoezi hilo lifanikiwe halmashauri inahitaji zaidi ya gari saba za ubebaji taka na kontena 80 lakini mpaka sasa magari yaliyopo ni manne na kontena 30 .

Hata hivyo kutokana na changamoto hiyo, Lazaro anawasihi wananchi kujenga tabia ya kuweka mazingira safi hasa kipindi hiki cha mvua kwani ndipo magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu yanapoibuka na kusababisha vifo vya watu.

JAMIIMOJABLOG MBEYA

DK. TULIA NJIA NYEUPE UNAIBU SPIKA

$
0
0
 Dk. Tulia Ackson amepita bila kupingwa baada ya kuchaguliwa na wabunge wa CCM kugombea nafasi ya Unaibu Spika katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mmoja wa wagombea wa nafasi ya Unaibu spika Bahati Abeid akizungumza mbele ya wabunge wa CCM.
 Mhe. Mariam Kisangi akizungumza mbele ya wabunge wa CCM kwenye ukumbi wa NEC mjini Dodoma ambapo yeye pamoja na Bahati Abeid walijitoa na kumpa nafasi Dk.Tulia Ackson kupita bila kupingwa
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiongea wakati wa kuendesha zoezi la kumpata Naibu Spika  kwenye ukumbi wa NEC, CCM Makao Makuu mjini Dodoma.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

MWANAMITINDO WA KIMATAIFA MIRIAM ODEMBA KUWA JAJI MAALUM

$
0
0
Maandalizi ya fainali ya shindano la Miss Universe Tanzania 2015 bado yanaendelea Mwanamitindo wa Kimataifa Miriam Odemba atakuwa jaji maalum katika kinyang’anyiro hiki cha kumpata mrembo wa Miss Universe Tanzania 2015. 

Majaji wengine watakaoshiriki katika kumtafuta mnyange wa mwaka huu ni Sheria Ngowi, Maria Sarungi Tsehai, Mariam Ndaba na Priyal wa sia couture.

Zoezi la usaili limeshakamilika na hatimaye kupata warembo watakaojiunga na kambi ya Miss Universe kesho siku ya jumatano kabla ya fainali tarehe 20 mwezi huu.

Warembo waliobahatika kuingia kambini ni 14 tu, majina na mikoa waliyotoka kwenye mabano Mariam Isack (Dar es salaam), Lilian Luth(Dar es salaam), Stacey Sulul(Dar es salaam),Willice Donard(Dar es salaam), Lorraine Marriot(Dar es salaam), Dalena David(Dar es salaam), Mercy Zephania(Dar es salaam), Dinnah Kaijage(Dar es salaam), Melody Typhone(Dar es salaam), Joselyn Mirashi(Arusha), Nancy Matta(Mbeya), Christina Shimba(Iringa), Belinda (Mwanza).

 Mwaka huu Miss Universe imefanya usaili katika mikoa sita tofauti ikiwamo Tanga, Iringa, Mbeya, Arusha, Mwanza na Dar es salaam.

Vijana nchini kuendelea kunufaika na Programu ya Kukuza Ajira zenye Staha Dar es Salaam (YEID)

$
0
0
z2
Afisa mwelekezi wa wa Programu ya kukuza Ajira zenye staha kwa Vijana Dar es Salaam,kupitia Elimu ya Biashara na Ujasiriamali. Bi. Emiliana Muchu akiwasilisha mada kuhusu mafanikio ya program hiyo hivi karibuni jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa Kamati inayokutanisha wadau wa program hiyo.Picha na Frank Shija, WHVUM
z3
Meneja wa Programu ya kukuza Ajira zenye staha kwa Vijana Dar es Salaam Bibi. Maria Fustiniano ( wapili kutoka kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano wa kamati ya wadau wa program hiyo uliofanyika mapema wikiendi hii jijini Dar es Salaam.
z4
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya True Maisha Bw. Erick Crispin akiwasilisha mada namna taasisi yake inavyofanya shughuli zake katika kutoa mafunzo kwa Vijana hivi karibuni jijini Dar es Salaam

KLABU YA ROTARY YA DAR ES SALAAM OYSTERBAY WATOA MATIBABU YA BURE KWA WAKAZI WA KEREGE-BAGAMOYO

$
0
0
DSC_1602
Rais wa klabu ya Rotary Dar es Salaam Oyster Bay kwa mwaka huu wa 2015-2016, Mohamed Versi akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo pichani) katika mji wa Kerege jana Novemba 15. wakati wa zoezi hilo la kambi ya bure ya upimaji wa afya. (Picha zote na Andrew Chale ).
DSC_1655
Mkuu wa kitengo cha Masoko kutoka benki ya Diamond Trust Bank [DTB] akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa zoezi hilo la kambi ya matibabu bure. DTB ndio wadhamini wakuu katika kambi hiyo.
DSC_1629
Daktari na mratibu wa magonjwa ya Kisukari, Dk. Bashiru Rajab akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo la kambi ya bure ya Matibabu katika mji wa Kerege,Bagamoyo Pwani.
DSC_1640
Mkazi wa Kerege akiwa katika mstari wa kwenda kumuona Daktari kwa ajili ya kupima afya zake sambamba na mtoto wake wakati wa kambi hiyo Novemba 15.2015.
DSC_1644
Zoezi la Kambi hiyo ya matibabu bure likiendelea katika mji huo wa Kerege.

DSC_1727
Mmoja wa wananchi wa Kerege (kulia) akimwelezea Daktari wa kambi hiyo..
DSC_1730
Upande wa huduma za macho...katika kambi hiyo
DSC_1759
Kitengo cha dawa wakiwa tayari kwa kutoa huduma hiyo wakati wa kambi hiyo..
DSC_1754
Wananchi wakipatiwa dawa bure wakati wa kambi hiyo..
Rotary Medical Camp-44
Huduma ya kinywa ikiendelea..
DSC_1714
Baadhi ya vifaa maalum kwa ajili ya matibabu ya kinywa ikiwemo meno kutoka Elite Dental Clinic wakati wa kambi hiyo..
DSC_1718
Baadhi ya madaktari wa magonjwa ya kinywa wakiwa tayari kwa ajili ya kutoa huduma kwa mmoja wa wakazi wa Kerege aliyefika katika kambi hiyo. Huduma ya Kinywa ilitolewa na Elite Dental Clinic.
DSC_1721
Huduma hizo za kinywa zikiendelea..
DSC_1712
DSC_1710
Picha za juu na chini ni eneo la upimaji wa magonjwa wa kinywa na meno iliyokuwa ikitolewa na Elite Dental Clinic
DSC_1700
Rotary Medical Camp-62
Mtaalamu wa tiba ya macho akiendelea na uchunguzi kwenye kambi hiyo
DSC_1742
Zoezi hilo la upimaji likiendelea katika vitengo mbalimbali wakati wa kambi ya upimaji na matibabu bure katika mhi wa Kerege.
Rotary Medical Camp-108
zoezi likiendelea kwa wananchi kupitia hatua moja hadi nyingine...
DSC_1d684
Baadhi ya wanachama wa Rotary Klabu ya Dar es Salaam Oyster Bay wakiwa katika kambi hiyo kutoa huduma..
DSC_1690
Rotary Medical Camp-7
DSC_1723
DSC_1664
Baadhi ya wananchi wa Kerege waliojitokeza wakiwa kwenye foleni katika Kambi hiyo huku wakipatiwa maelezo mbalimbali juu ya afya..
DSC_1666
Baadhi ya wananchi upande wa wanawake waliojotokeza kwenye kambi hiyo..
DSC_1673
Wananchi wakipata kusajiliwa kwa lengo la kuelekea kumuona Daktari na vipimo..
DSC_1681
Baadhi ya waanachi hao wakiwa kwenye moja ya foleni kuingia kwa madaktari na vipimo mbalimbali wakati wa zoezi hilo.
Rotary Medical Camp-2-3
Wananchi hao wakiwa katika kambi hiyo..
Rotary Medical Camp-15
Huduma na somo likiendelea wakati wa kambi hiyo..


Na Andrew Chale, Modewjiblog
[BAGAMOYO] Klabu ya Rotary ya Dar es Salaam Oyster Bay, kwa mara nyingine tena imeendesha matibabu katika kambi maalum ya matibabu ya bure katika mji wa Kerege uliopo Bagamoyo, Mkoani Pwani.

Kambi hiyo iliyofanyika siku ya Jumapil Novemba 15.2015 ambapo zaidi ya wahudumu 50 wa Afya walipima na kutibu magonjwa kwa wakazi hao wa Kerege waliojitokeza kwa wingi wanaokadiriwa kufikia zaidi ya 700.

Kambi hiyo ya matibabu bure imedhaminiwa na benki ya Diamond Trust Bank (DTB) imeweza kuwa faraja kubwa kwa wananchi na wakazi wa Kerege kupata Huduma hiyo kwani imeweza kuwafikia muda muafaka kwao kupata fursa za matibabu na vipimo bure.
Akizungumza na wanahabari Rais wa klabu hiyo ya Rotary Dar es Salaam Oyster Bay kwa mwaka huu wa 2015-2016, Mohamed Versi amebainisha kuwa wito mkubwa kwa wananchi wa Kerege kujitokeza kunawapa faraja kuendelea kutembelea na kuweka kambi kwa mwaka mara moja katika mji huo.

“Mwaka huu ni wa tano tokea kuanza kutoa matibabu bure kwa kuweka kambi hizi za matibabu. Kwa hapa Kerege huu ni mwaka wa nne tunafika hapa na kuhudumia wananchi huku zaidi ya wananchi, 600 hadi 700 wanahudumiwa ikiwemo vipimo na matibabu” alisema Versi.
Aidha, Rais huyo alibainisha kuwa, mbali na kutoa matibabu bure pia wameweza kutoa dawa pamoja na neti za kuzuia mbu kwa kila mwananchi aalijitokeza kwenye kambi hiyo.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Masoko kutoka benki hiyo ya DTB, Bw. Sylvester Bahati amebainisha kuwa kujitokeza kudhamini kambi hiyo ni miongoni mwa taratibu za benki hiyo kuweza kusaidia jamii.

“Tunawapongeza Rotary Klabu kwa kuona umuhimu wa kusaidia kambi hii ya Kerege matibabu bure na ufadhili wetu hapa unaendana na sawa na taratibu tulizojiwekea za kutoa gawio kwa jamii kama zilivyotaratibu nyingine tulizonazo” alibainisha Bw. Bahati.

Aidha, ameeleza kuwa Benki hiyo ya DTB ina matawi zaidi ya 20 nchini huku ikitarajia kufungua matawi zaidi kwa nchi nzima ikiwemo Zanzibar.
Kwa upande wake daktari na mratibu wa magonjwa ya Kisukari, Dk. Bashiru Rajab ameeleza kuwa, wengi wa wa wagonjwa walipatikana katika kambi hiyo ni wale wa matatizo ya mapigo ya moyo (Blood pressure ).

“Katika kambi hii wengi wa wananchi wanaofika hapa wanakabiriwa na matatizo ya Presha na ugonjwa wa Maralia huku wa kisukari wakiwa wachache. Inatia faraja sana kwani wamepata kujua hali ya afya zao za mwili na tunawashahuri wawe na taratibu ya kupima afya mara kwa mara” alibainisha Dk. Bashiru.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi walipongeza waandaaji wa kambi hiyo ambapo imewasaidia kujua afya zao hivyo kuchukua hatua ikiwemo suala la kuzingatia kanuni za kufuata pamoja na ushahuri wa kitabibu.

Matibabu, sehemu mojawapo ya Miradi ya Afya ya Jamii, ambayo hufanyika kila mwaka toka ilipozinduliwa mwaka 2011 katika kitongoji cha Chanika jijini Dar es Salaam ambapo takribani wananchi 600 walijitokeza kupima malaria, VVU, Kisukari, magonjwa ya mfumo wa upumuaji, macho na viashiria vya magonjwa sugu na baadae kuamia katika mji huo wa Kerege kwa mwaka wa nne sasa huku wakitoa dawa na miwani bure.

Kwa mwaka huu imedhaminiwa na benki ya Diamond Trust Bank, Rotary Club of Seattle4 huku ikiandaliwa kwa kushirikiana na Shree Hindu Mandal Hospital, Vital Supplies, Kids Care Tanzania, Elite Dantal Clinic, Whitedent, Sayona, Ultimate Security na wengine wengi.

Soma zaidi hapa:

MKESHA WA KUOMBEA AMANI KUFANYIKA ZANZIBAR

$
0
0
indexAskofu Charles Gadi wa Kanisa la Good News For All Ministries akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuombea Amani Zanzibar mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Katibu wa Kanisa hilo Mchungaji Palemo Masawe.

AWAMU YA SHINDANO LA UFADHILI WA KILIMO CHA BIASHARA KUANZA

$
0
0


Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la AECF linalo jishughulisha na kutoa mikopo ya kilimo  cha biashara Bw. Hugh Scott akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu awamu ya nne ya shindano la ufadhili wa kilimo cha biashara mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni afisa Muendeshaji Mkuu wa shirika hilo Bw.  Sam Ng'ang'a.
Picha zote na Eliphace Marwa – Maelezo.

MKUU WA WILAYA YA KAKONKO MKOANI KIGOMA AIKABIDHI SERIKALI MIRADI YA THAMANI YA SHILINGI MILIONI 700 KWA SHULE YA EMBOREET WILAYANI SIANJIRO MKOANI MANYARA

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma, Peter Toima akipokea hati ya pongezi aliyokabidhiwa na Mkuu wa mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera, baada ya kukabidhi miradi ya thamani ya sh700 milioni ya shule ya sekondari Emboreet ya wilaya Simanjiro.
 Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma, Peter Toima akionyesha hati ya pongezi aliyokabidhiwa na Mkuu wa mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera, (kulia) baada ya kukabidhi miradi ya thamani ya sh700 milioni ya shule ya sekondari Emboreet ya wilaya Simanjiro.
Wanafunzi wa shule ya sekondari Emboreet Wilaya Simanjiro Mkoani Manyara, wakimkabidhi risala yao Mkuu wa mkoa huo Dk Joel Bendera, baada ya kukabidhiwa juzi miradi ya shule ya thamani ya sh700 milioni na Mkuu wa mkoa wa Kakonko Mkoani Kigoma, Peter Toima.

Anania Ngoliga na John Kitime watambulisha muziki wao

$
0
0
Anania Ngoliga na John Kitime ni wanamuziki wa zamani ambao hufahamika zaidi kwa muziki wa Dansi. Anania ambaye alipoteza uwezo wake wa kuona akiwa bado mtoto mdogo, amewahi kupitia bendi kama Jambos na Afriso Ngoma ambapo alikuwa akiimba na mwanamuziki nguli Lovy Longomba akiwa na  wakali wengine kama Ramadhani Kinguti, kisha akapigia bendi ya Legho Stars akiwa na wanamuziki kama Joseph Mulenga (King Spoiler) na Tchimanga Assossa, na katika bendi hii licha ya kuimba pia alikuwa anapiga kinanda na gitaa. 

Akapitia bendi nyingine kama Ram Choc Stars, Living Light Band na VICO Stars za Iringa hatimae akajiunga na TACOSODE Band  ilipokufa akajiunga na Tango Stars na kwa sasa yuko Karafuu Band ya Zanzibar. John Kitime nae amepitia bendi kama Orchestra Mambo Bado iliyokuwa chini ya uongozi wa Tchimanga Assossa, Orchestra Makassy, TX Seleleka, Tancut Almasi Orchestra ya Iringa ambako alikuwa jukwaa moja na Abdul Salvador, Kasaloo Kyanga na pacha wake, akina Kawelee, Kalala Mbwebwe na majina mengine makubwa katika historia ya muziki Tanzania, kisha Vijana Jazz akiwa Hemed Maneti , Jerry Nashon na wengine wengi , baadae Magoma Moto Sound na kwa sasa yuko na Kilimanjaro Band.

 Lakini wanamuziki wawili hawa wamekuwa na staili yao ya muziki ya peke yao, ambayo tayari wamekwisha jikuta wakifanya 'tour' mbili Marekani zilizowazungusha majimbo mengi ya nchi hiyo katika 'tour' zilizochukua jumla ya miezi mitatu, pia wakajikuta Mumbai India wakifanya maonyesho kupitia muziki wao huu. 

Kwa mara ya kwanza walifanya maonyesho ya aina ya muziki huu katika tamasha la Karibu lililokuwa Bagamoyo siku chache zilizopita na kufuatiwa na onyesho jingine katika jukwaa la Baraza liliokuwa Alliance France. Video hii iliyopigwa 'live' ni vionjo vya staili yao faidi utamu, kwa zaidi wasiliana kupitia anania.john@gmail.com au +255713274747

SERIKALI YAIPONGEZA JUHUDI ZINAZOFANYWA NA TAASISI YA DORIS MOLLEL FOUNDATION ZA KUSAIDIA WATOTO NJITI!

$
0
0
DSC_1839
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki akizungumza mbele ya wanahabari, madaktari na baadhi ya akina mama waliokuwa na watoto waliozaliwa kabla ya wakati maarufu kama Njiti (Hawapo pichani). Kushoto ni DoriS Mollel ambaye ni Mwanzilishi na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) na wengine ni maafisa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
DSC_1855
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Muhimbili wakishuhudia tukio hilo maalum la taasisi ya DMF ilipotoa vifaa hivyo katika kitengo cha Jengo la Watoto.
DSC_1865
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadik akipata maelezo juu ya vifaa hivyo vilivyotolewa na Taasisi ya DMF.
DSC_1870
Msimamizi wa wodi ya akina mama wanaopatiwa huduma ya Kangaroo dhidi ya watoto wao ambao walizaliwa njiti, akimpatia maelezo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alipotembelea wodi hiyo leo.
DSC_1924
Picha ya juu na chini Mkuu wa Mkoa wa Dar e Salaam akiwafariji baadi ya wakinamama waliojifungua watoto kabla ya wakati maarufu njiti wakati alipotembelea wodi hiyo ya watoto mapema leo.
DSC_1929
DSC_1939
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimpatia zawadi ambayo ni jozi ya soksi kwa ajili ya kusaidia watoto njiti kwa mmoja wa wamama waliokuwa katika wodi hiyo ya watoto njiti.

DSC_1873
Keki maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya siku maalum ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati maarufu njiti
DSC_1885
Mtoto Amne Salim (3) ambaye ni njiti akikata keki maalum kwa niaba ya watoto wenzake katika tukio hilo mapema leo.
DSC_1890
DSC_1891
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimlisha keki mtoto Amne Salim katika tukio hilo.
DSC_1897
Mtoto Amne Salim akimlisha keki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik katika tukio hilo.
DSC_1954
Baadhi ya akina mama waliokwenye mpango maalum wa kutunza watoto wao waliozaliwa njiti ujulikanao kama Kangaroo wakiwa wodini mapema leo wakati wa ugeni wa DMF na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walipotembelea wodi hiyo.
DSC_1882
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaamm Meck Sadik akipokea na kukabidhi vifaa maalum kwa ajili ya kusaidia watoto njiti katika Hospitali ya Taifa Muhimbili vilivyotolewa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation mapema leo.
DSC_1907
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik akipanda mti maalum baada ya zoezi hilo la Taasisi ya Doris Mollel Foundation kutoa misaada ya vifaa vya watoto njiti.
DSC_1912
DSC_1921
DSC_1918
Shughuli hiyo ya upandaji mti wa kumbukumbu ikiendelea..
DSC_1900
Mama mzazi wa Doris Mollel akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Na Andrew Chale, Modewjiblog.

[DAR ES SALAAM] Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongeza juhudi binafsi zinazofanywa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) katika harakati zake za kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) na mambo ya elimu hapa nchini huku ikiahidi kuendelea kushirikiana nayo kufikia malengp yake.

Kauli hiyo imetolewa mapema leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki wakati wa kupokea vifaa maalum vya kusaidia watoto njiti vilivyotolewa na taasisi hiyo ya Doris Mollel Foundation tukio lililofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jengo la Watoto.

“Tunatambua mashine hizi ni bei kubwa na Serikali pekee yake haina pesa hivyo kwa kusaidiana na wadau kama hivi n faraja sana na tunapongeza juhudi hizi za taasisi ya DMF kwa kujitokeza kusaidia mashine kwa watoto njiti” ameeleza Mkuu wa Mkoa huyo.
Mkuu wa Mkoa huyo aliongeza kuwa, Mashirika mengine yaendelee kujitokeza kusaidia huduma za kijamii ikiwemo vifaa kama taasisi ya Doris Mollel kwani asilimia 100 ya wagonjwa na watu wengine wenye mahitaji katika tiba wanakimbilia Dar es Salaam hasa Hospitali ya Muhimbili.

“Tunaomba tena mukipata nyingine musisite kutiletea hapa maana Mkoa huu unapokea wagonjwa wengi kutoka maeneo mengi ya Tanzania na vifaa vya tiba mara nyingi vinakuwa ni vichache, Huko mikoani wanapewa rufaa waanakuja hapa pia hivyo DMF musisite kuja tena” alimalizia Mkuu wa Mkoa huyo.

Hata hivyo kwa upande wake Mwanzilishi na mtendaji Mkuu wa DMF, Doros Mollel amemweleza Mkuu wa Mkoa Meck Sadik kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega katika juhudi za kusaidia watoto njiti nchini ikiwemo kutoa elimu, vifaa na usaidizi kwa jamii dhidi ya kukabiliana na watoto njiti nchini.

Katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa alishudia vifaa hivyo na kupokea kutoka DMF sambamba na kutembelea wote ya watoto njiti pamoja na ile ya Kangaroo ambayo wamama wenye watoto njiti wanakuwa wanapatiwa uangalizi maalum dhidi ya watoto wao ikiwemo kupata joto la Mama na baadae alipanda mti maalum mbele ya jengo hilo la Watoto kama kumbukumbu na juhudi za wadau katika kusaidia jamii dhidi ya watoto njiti.

DMF imeweza kusaidia vifaa katika wodi hiyo ya watoto Muhimbili vikiwemo (Suction machines, Oxygen Concentrators na Feeding tubes). Aidha Doris Mollel amebainisha kuwa baada ya hapo wanatarajia kuelekea mikoa ya Kanda ya Ziwa kutoa vifaa kama hivyo huku lengo ikiwa ni kufika mikoa yote ya Tanzania.

VIONGOZI WA KIMILA WAPITISHA AZIMIO LA KUMLINDA MTOTO WA KIKE

$
0
0
IMG_1623
Pichani juu na chini ni baadhi ya viongozi wa mila (Laigwanan na Laiboni) na akina mama mashuhuri (Ngaigwanan) wilayani Lolilondo wakisoma na kujadili azimio la pamoja la kumlinda mtoto wa kike kabla ya kulipitisha na kusaini wakati wa kongamano kubwa la siku mbili lililofanyika katika ofisi za halmashauri ya wilaya Ngorongoro, jijini Arusha.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
IMG_1611
Viongozi hao pia wamesema ni vyema jamii ya kifugaji kuacha kuendelea na vitendo vya kuwaoza watoto wa kike wakiwa bado wadogo na wakati mwingine kwa kuwakatisha masomo na kuwalazimisha kuolewa.
IMG_1627
Azimio hilo la Loliondo ambalo pia lilitiwa saini na waganga wa tiba asilia limetoa mwelekeo wa kuboresha afya ya uzazi, elimu na malezi kwa watoto wa kike katika jamii ya Kimaasai.

Aidha limetoa namna bora ya utekelezaji na kupitisha taratibu zitakazosaidia watoto wa kike wanaokimbia tishio la ukeketaji na kuhakikisha kwamba watasoma na kupata huduma zote za afya.

Katika maeneo yao baada ya kutia saini viongozi hao wameahidi kuonyesha ushirikiano wa karibu kwa viongozi wa serikali katika ngazi zote, viongozi wa dini, vyombo vya habari, walimu, wataalamu wa afya na wadau wa maendeleo katika maeneo yote ndani ya wilaya ili kuboresha afya ya uzazi, elimu na malezi bora kwa watoto.

Pamoja utiaji saini wa Azimio la Loliondo,viongozi hao wameliomba shirika la UNESCO na halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro kushirikisha viongozi wengi zaidi, kuendelea kutoa elimu kwa viongozi wa kimila na kuendelea kuwasaidia katika majukumu yao ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu na kuwasaidia uratibu wa shughuli zote za kupingana na unyanyasaji na ukatili wa kijinsia.
IMG_1632
Katibu wa Baraza la Mila (W) Ngorongoro, Laanoi Munge akisoma azimio la kumlinda mtoto wake baada ya kulifanyia marekebisho ya pamoja mbele ya viongozi wa mila wa wilaya ya Ngorongoro.

Kongamano hilo lililozaa Azimio la Loliondo ni mwendelezo wa warsha zinazotolewa na UNESCO kwa ajili ya kutoa elimu ya kuwajengea uwezo na kugawa majukumu kwa viongozi wa kimila, wamama mashuhuri, viongozi wa dini, wakunga wa jadi pamoja na waandishi wa habari ili kutekeleza vizuri ufuatiliaji wa afya ya uzazi na malezi bora kwa watoto katika jamii ya Kimaasai.

Utiaji saini wa Azimio la Loliondo ulishuhudiwa na Katibu Tawala Wilaya ya Ngorongoro Bw. Lemuel Kileo, maafisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bw.Herman Mathias na Bi.Rose Haji Mwalimu.

Kongamano hilo la siku mbili lililofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro limeendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro.

IMG_1636
Katibu wa Baraza la Mila wilayani Ngorongoro, Laanoi Munge (kushoto aliyesimama) akimsomea baadhi ya maboresho ya vipengele vilivyomo ndani ya azimio hilo Ofisa Elimu ya Uzazi na UKIMWI kutoka UNESCO, Mathias Herman (kulia).
IMG_1643
Laigwanan wa kata ya Pinyinyi, Moses Mollel akiwasilisha maboresho ya azimio hilo baada ya kulijadili kabla ya kusaini.
IMG_1676
Ofisa Elimu ya Uzazi na UKIMWI kutoka UNESCO, Mathias Herman akifafanua jambo kwa viongozi hao baada ya kuridhishwa na maboresho ya azimio hilo katika kongamano kubwa la siku mbili lililofanyika katika ofisi za halmashauri ya wilaya Ngorongoro, jijini Arusha. Kutoka kushoto ni Mkalimani wa kwenye kongamano hilo Mchungaji, Mark Murenga, Katibu Tawala wa Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kileo, Mwenyekiti wa Baraza la Malaigwanan wilaya ya Ngorongoro, Joseph Oletiripai pamoja na Kiongozi wa Malaiboni wilaya ya Ngorongoro Bw. Sangau Naimodu.
IMG_1692
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka redio ya jamii Loliondo FM nao walikuwepo kuhudhuria tukio hilo la utiaji saini wa azimio la kumlinda mtoto wa kike.
IMG_1698
Baadhi ya maafisa wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro na waandishi wa habari waliokuwepo ukumbini kushuhudia tukio hilo.
IMG_1768
Mwenyekiti wa Baraza la Malaigwanan wilaya ya Ngorongoro, Joseph Oletiripai (kushoto), Kiongozi wa Malaiboni wilaya ya Ngorongoro Bw. Sangau Naimodu (wa pili kushoto) Laigwanan wa kata ya Pinyinyi, Moses Mollel (wa pili kulia) pamoja na Ngaigwanan wa Malambo, Miriam Lembirika wakisaini kwa niaba ya viongozi wengine wa mila wa Wilaya ya Ngorongoro, Azimio la Liliondo.Wanaoshuhudia (waliosimama) ni KatibuTawala wa Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kileo (kulia), Ofisa Ustawi wa Jamii wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Benezeth Bwikizo (wa pili kulia), Mtaalamu wa masuala ya vyombo vya habari vya kijamii na Mkufunzi kutoka UNESCO, Rose Haji Mwalimu (wa tatu kulia) pamoja na Ofisa Elimu ya Uzazi na UKIMWI wa UNESCO, Mathias Herman.
IMG_1772
Walioshuhudia tukio hilo wakipiga makofi baada ya zoezi hilo.
IMG_1701
Baadhi ya viongozi wa kimila na waandishi wa habari wakishuhudia tukio hilo la kusainiwa kwa azimio la kumlinda mtoto wa kike.
IMG_1782
Zoezi la utiaji saini likiendelea kwa kila kiongozi aliyeshiriki kongamano kubwa la siku mbili lililoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambalo limefanyika katika ofisi za halmashauri ya wilaya Ngorongoro, jijini Arusha.
IMG_1821
Picha ya pamoja baada ya zeozi kukamilika.

VIONGOZI wa kimila wa jamii ya Kimaasai na wanawake mashahuri wamepitisha Azimio la Loliondo lenye lengo la kumlinda mtoto wa kike na kuhakikisha maendeleo yake kiafya, kielimu na kitamaduni.

Azimio hilo ambalo limetiwa saini na viongozi hao mwishoni mwa kongamano kubwa la siku mbili lililofanyika, katika ofisi za halmashauri wilayani Ngorongoro, linapinga mila na desturi zinazomkandamiza mtoto wa kike. Mila na desturi ambazo zimepitwa na wakati.

Kabla ya kupitishwa na kusaini maazimio hayo viongozi hao wa kimila na mashuhuri walipatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo ili kuendeleza mijadala na uelewa na hatimae kuamini kwamba baadhi ya mila na desturi zinachangia na kuchochea athari za kiafya na kijamii hasa kwa watoto wa kike na kina mama.

Viongozi hao wamepitisha azimio hilo baada ya kupitia kifungu hadi kifungu na kuridhia yaliyomo kwa kuzingatia wajibu wao ndani ya jamii na uwezo mkubwa wa ushawishi kama viongozi wa mila (Laigwanan na Laiboni) na akina mama mashuhuri (Ngaigwanan) .

Aidha walisema kwamba watatumia nafasi zao kuelimisha jamii juu ya malezi bora ikiwa ni pamoja na mahali salama pa kulala watoto wa kike na kiume na kuelimisha jamii umuhimu wa elimu kwa kuwapeleka shuleni hasa kwa watoto wa kike.

“Naomba viongozi wenzangu twende tukaelimishe jamii juu ya madhara ya tohara kama tulivyoazimia na kuanzisha mchakato utakaosaidia kupunguza au kumaliza kabisa matendo ya tohara ndani ya jamii yetu,” alisema Mwenyekiti wa Baraza la Malaigwanan wilaya ya Ngorongoro, Joseph Oletiripai.

“Sisi kama viongozi tusiendelee kuwa chanzo cha kuendeleza matukio haya kwani ni ya ukatili kwa watoto wetu wa kike na tutumie nafasi hii kwenda kuwaelimisha viongozi wenzetu wengine mashuhuri ili kusambaza ujumbe na jamii ijue athari zinazotokana na ukeketaji pamoja na kuozesha watoto wetu wakiwa katika umri mdogo,” alisema Laanoi Munge.
Viongozi hao pia wamedhihirisha kuwa matukio ya vitendo vya ukeketaji na ndoa za utotoni vimechangia utoro nyumbani na kwenda kuishi kwa muda kwenye vituo maalum kwa kuogopa kufanyiwa tohara.

Watoto hao wamekuwa na hali ya kutoroka baada ya kugundua kwamba kuna matukio ya ulemavu na athari nyinginezo za kiafya zinazotokana na ukeketaji na salama yao ni kujitoa katika jamii hiyo na kutafuta hifadhi kwingine.

Jameson to host Live Pre Party Tanzania at George and Dragon

$
0
0

Jameson yaandaa pre-party George and Dragon Dar kuelekea Jameson Live Party itakayofanyika Nairobi.

  • Mshindi mmoja kujishindia tiketi ya watu wawili kwenda Kenya kwenye party ya Jameson itakayotumbuizwa na B.O.B

Dar es Salaam, Tanzania, 17thNovember 2015: Jameson inaandaa pre-party itakayofanyika tarehe 21 ya mwezi huu katika bar ya George and Dragon jijini Dar es Salaam.

Watumiaji wa Jameson watakaonunua chupa ya kinywaji hicho watafanikiwa kuingia moja kwa moja kwenye droo ya kushinda tiketi ya kwenda Kenya kushuhudia party ya Jameson itakayofanyika hapo tarehe 12, December.

Jameson Live 2015 Party, inamleta msanii wa hiphop kutoka Marekani, Bobby Ray Simons, maarufu kama B.O.B, ambayo itafanyika Ngong Racecourse hapo tarehe 12 December.Rapa huyo mzaliwa wa Atlanta amezungumzia kuhusu show yake hiyo ya Nairobi katika ukurasa wake wa Facebook, akiwataka mashabiki wake wajiandae kwa show kali.

B.O.B ambaye alitambulika katika ulimwengu wa muziki kupitia kupitia mixtape yake ya Cloud 9, amefanikiwa kufanya show sehemu mbalimbali duniani huku wimbo wake wa ‘Airplanes’ na ‘Nothing on You’ aliyomshirikisha Bruno Mars zikiongoza chati mbalimbali za mziki duniani.
Nyimbo zake za hivi karibuni kama ‘So Good’ na ‘Headband’ nazo zimefanikiwa kumfanya B.O.B kuwa mmoja ya wanamuziki wakubwa duniani.

Huku akiwa ameshinda tuzo mbalimbali za BET, MTV pamoja na Teen Choice na huku akifanikiwa kuchaguliwa kuwania tuzo za Grammy zaidi ya mara sita, B.O.B ameshawahi kufanya show na wanamuziki mahiri kama Janelle Monae, Eminem, Linkin Park, Kanye West, Drake, Usher, Paramore na wengine wengi.

Jameson wamejipanga kukuza viwango vya burudani kwa nchi za Afrika Mashariki na awamu hii wamejipanga kwa kuwapa burudani ya pekee mashabiki watakaohudhuria burudani hiyo huku wakizidi kuwekeza zaidi katika kuwaleta wasanii wa kimataifa.
                                                                                            
Mwaka 2014 Jameson ilifanikiwa kuandaa matamasha mawili makubwa nchini Kenya ambayo yote tiketi zake zilimalizika kabla huku la kwanza burudani ikitolewa na wasanii wa ndani, na la pili burudani ilitolewa na msanii 2 Chainz huku balozi mashuhuri wa Afrika Akon akihudhuria pia.

Akizungumzia kuhusu show hiyo, Balozi wa Jameson, Antony Owich amesema party ya mwaka huu itazidi kuwa kubwa na bora kuliko miaka iliyopita.

‘Jameson imejikita katika kuwapa kumbukumbu za kipekee mashabiki wake na kwa mwaka huu inawaahidi kuwapa burudani ya pekee kabisa na watu wasikose kuhudhuria’ alisema Owich.

Kwaya ya Wakorintho wa pili kushiriki tamasha la shukrani

$
0
0
KWAYA  ya  Wakorintho  wa Pili ya Wilayani Mafinga mkoani Njombe, imekuwa ya kwanza  kuthibitisha kushiriki Tamasha la Kushukuru linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema uongozi wa kwaya hiyo umekubali kushiriki katika tamasha hilo baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 nchini kote.

“Kwaya  ya Wakorintho wa pili  wameanza kuthibitisha kushiriki tamasha la Shukrani baada ya kufanyika uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu, tunaendelea na maandalizi ya kufanikisha tamasha hilo ambalo litashirikisha idadi kubwa ya Watanzania,” alisema Msama. 

Aidha Msama alisema katika tamasha hilo, Kwaya hiyo itafanya uzinduzi  wa albamu yake ya Mchepuko sio dili yenye nyimbo nane.Nyimbo zilizoko kwenye albamu ya Mchepuko sio dili ni pamoja na Tanzania, Mchepuko sio dili, Watenda mabaya, Eee bwana, Tuokoe baba, Dunia hii, Yahwe Tunakuinua na Hana.  

“Kwaya  ya Wakorintho itafanya matukio mawili katika tamasha hilo, la kwanza ni kushiriki Tamasha la Kushukuru na la pili ni kuzindua albamu yenye nyimbo nane,” alisema Msama.
Mwisho 
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images