Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46367 articles
Browse latest View live

WATALAAM WA TAKWIMU BARANI AFRIKA WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
mku1
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza leo na waandishi wa habari kuhusu mkutano wa siku tano ambao umekutanisha watalaam wa takwimu kutoka nchi mbalimbali barani Afrika kujadili Mfumo wa Uongozi Bora katika Ofisi za Takwimu pamoja na Uboreshaji wa Mitaala ya Ufundishaji wa Masomo ya Takwimu. Mkutano huo unafanyika katika hoteli ya Golden Tulip iliyopo Jijini Dar es Salaam.
mku2
Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Afrika Kusini Risenga Maluleke akizungumza leo na waandishi wa habari kuhusu madhumuni ya mkutano wa watalaam wa takwimu kutoka nchi mbalimbali barani Afrika ambapo wamekutana kujadili Mfumo wa Uongozi Bora katika Ofisi za Takwimu pamoja na Uboreshaji wa Mitaala ya Ufundishaji wa Masomo ya Takwimu. Mkutano huo ni wa siku tano na unafanyika katika hoteli ya Golden Tulip iliyopo Jijini Dar es Salaam.
mku3
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza leo Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa watalaam wa takwimu kutoka nchi mbalimbali barani Afrika ambao wamekutana kujadili Mfumo wa Uongozi Bora katika Ofisi za Takwimu pamoja na Uboreshaji wa Mitaala ya Ufundishaji wa Masomo ya Takwimu. Kushoto kwake ni Mtakwimu kutoka Kamisheni ya Uchumi Afrika Bw. Andry Andriantseheno.
mku4
Baadhi ya wakuu wa Ofisi za Takwimu kutoka barani Afrika wakifuatilia kwa makini majadiliano wakati wa mkutano wa kujadili Mfumo wa Uongozi Bora katika Ofisi za Takwimu pamoja na Uboreshaji wa Mitaala ya Ufundishaji wa Masomo ya Takwimu. Mkutano huo ni wa siku tano na unafanyika katika hoteli ya Golden Tulip iliyopo Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)
………………………………………………………………………….
Na: Emmanuel Ghula
Dar es Salaam.
 
VIONGOZI wa Ofisi za Takwimu barani Afrika leo wamekutana kujadili Mfumo wa Uongozi Bora katika Ofisi hizo pamoja na Uboreshaji wa Mitaala ya Ufundishaji wa Masomo ya Takwimu katika nchi za Afrika.
 
Wakizungumza katika mkutano wa wataalam wa takwimu ulioanza leo Jijini Dar es Salaam, viongozi hao wamesema ili takwimu bora zipatikane kwa wakati, ni lazima kuwepo na mfumo bora wa uongozi pamoja na wataalamu waliobobea katika fani ya takwimu.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa amesema lengo la mkutano huo ni kujadili mfumo wa uongozi bora katika Ofisi za Takwimu pamoja na namna ya kuboresha mitaala ya ufundishaji wa masomo ya takwimu barani Afrika.
 
“Leo tupo hapa wataalamu wa takwimu kutoka zaidi ya mataifa 25 barani Afrika ili kujadili namna ya kuboresha mifumo yetu ya uongozi katika Ofisi za Takwimu pamoja na kujadili mbinu bora za kuimarisha utoaji wa mafunzo kwa watakwimu vijana hasa kupitia upya mitaala ya ufundishaji,” amesema Dkt. Chuwa.
 
Dkt. Chuwa amesema kuimarishwa kwa mfumo wa uongozi pamoja na kuboresha mafunzo kwa wakwimu kutasaidia katika ukusanyaji wa takwimu bora zitakazotumika katika kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo.Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu wa Afrika ya Kusini, Risega Maluleke amesema mataifa mengi ya Afrika yanakabiliwa na changamoto kubwa ya kutokuwa na uwezo wa kujitegemea kifedha kitu ambacho hukwamisha upatikanaji wa takwimu kwa wakati.
 
Amesema licha ya changamoto hiyo, kwa kiasi kikubwa kazi ya ukusanyaji wa takwimu imekuwa ikifanyika kwa ufanisi mkubwa kutoka kwa watalaam hao wa takwimu na hivyo kupitia mkutano huu, wataweza kujadili namna ya kuboresha uimarishaji wa Ofisi za Takwimu.
 
Maluleke amesema ni vyema Serikali zikaziwezesha ofisi za ukusanyaji wa takwimu ili ziweze kujitegemea kibajeti na kuboresha utendaji kazi wake katika kuhakikisha takwimu bora zinapatikana kwa wakati muafaka.
 
Mkutano huo wa siku tano unatarajia kumalizika tarehe 06 Novemba, 2015 ambapo wataalam takribani 30 wamekutana kujadili Mfumo wa Uongozi Bora katika Ofisi hizo pamoja na Uboreshaji wa Mitaala ya Ufundishaji wa Masomo ya Takwimu katika nchi za Afrika.

FAINI ZILIVYOSAIDIA KUPUNGUZA MAKOSA YA UKATILI WA KIJINSIA MASOKONI

$
0
0
 Katibu wa Soko la Gezaulole lililopo Kiwalani Bomubomu Manispaa ya Ilala, Salum Yusuf (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo za kukomesha vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia sokoni hapo baada ya kuwezeshwa mafunzo ya kupinga ukatili huo na Shirika la Equality for Growth. Kushoto Mwenyekiti wa Soko hilo, Muhidin Waziri.
 Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa Shirika hilo, Samora Julius akitoa ushauri kwa Serikali hasa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali katika masuala mbalimbali yakiwemo ya ukatili wa jinsia. Kushoto ni mtaalamu wa kujitolea wa masuala ya kijinsia kutoka nje ya nchi, Ashley.
 Mwezeshaji wa Sheria, Khadija Mohamed (kulia), akielezea mafanikio waliyoyafikia ya kukabiliana na vitendo hivyo katika soko hilo baada ya kuwezeshwa na EfG.
 Mwezeshaji Asha Abbas akichangia katika mkutano huo.
 Mfanyabiashara wa samaki katika soko hilo, Asha Mohamed akihojiwa na wanahabari kuhusu namna wanavyo pambana na ukatili katika soko lao hilo la Gezaulole.
Mfanyabiashara Amina Mussa akilishukuru Shirika la EfG kwa kusaidia kupunguza unyanyasaji wa kijinsia katika soko hilo.

Na Dotto Mwaibale

FAINI zinazotolewa kwa watu wanaobainika na makosa ya unyanyasaji wa kijinsia katika soko la Gezaulole lililopo Kiwalani Bomubomu Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam zimesaidia kupunguza vitendo hivyo kwenye soko hilo.

Hayo yamebainishwa Dar es Salaam leo asubuhi na Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Khadija Mohamed wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari waliotembea soko hilo kujua ni kwa kiwango gani vitendo hivyo vimepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa elimu ya kupinga unyanyasaji katika masoko ya Manispaa ya Ilala.

"Faini tunazo watoza wafanyabiashara wanaobainika na makosa ya kutumia lugha chafu, kupigana na kuwadhalilisha wenzao kwa kuwakamata  maunguni na unyanyasaji mwingine zimesaidia kupunguza makosa hayo katika soko letu" alisema Mohamed.

Alisema mara zote matusi katika masoko yamekuwa yakichangia kuwakimbiza wateja na ndio maana wana lishukuru shirika la EfG kwa kuwapa elimu iliyowasaidia na kuwafanya waendelee na biashara zao kama kawaida.

Mwezeshaji wa Sheria Amina Mussa alisema hapo awali wanaume walikuwa wamekubuhu kwa kutukana tusi la mama jambo ambalo lilikuwa linawakera lakini hivi sasa wanashukuru mungu baada ya wanaume hao kujitambua na kuacha matusi hayo.

Mwenyekiti wa soko hilo, Muhidin Waziri alilipongeza shirika hilo kwa kuwasaidia wafanyabiashara katika masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala na kujitambua hivyo kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia masokoni.

Katibu wa soko hilo, Salum Yusuf alisema changamoto kubwa waliyokuwa nayo hapo awali kabla ya kufikiwa na EfG ilikuwa ni kutojua maana ya unyanyasaji ambapo mtu aliyekuwa akishikwa mwilini au kutukanwa alikuwa hachukui hatua yoyote.

Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa Shirika hilo, Samora Julius alitoa ushauri kwa Serikali hasa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali katika masuala mbalimbali yakiwemo ya ukatili wa jinsia.

Julius aliomba serikali kuyaunga mkono mashirika yanayofanya vizuri kwa kuyapa ruzuku itakayosaidia kuwafikia wananchi kwa wingi na jamii kwa ujumla.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com

WASICHANA WAPEWA KIPAUMBELE NA TAASISI YA DON BOSCO NET

$
0
0
Baadhi ya Wanafunzi wakiwa Darasani.
Baadhi ya wanafunzi wakijifunza kushona.
Masomo yakiendelea kwa baadhi ya wanafunzi.

TAASISI ya Don Bosco Net Tanzania yahamasisha wasichana katika kujiendeleza kimapato na kimawazo kutokana na wasichana wengi baada ya kumaliza elimu ya Msingi au  Sekondari  kutofanikiwa kuendelea na masomo yao ya juu kwasababu mbali mbali. Moja wapo ikiwa ada, hali ngumu ya uchumi na maisha inayositisha ndoto yao yakujimudu na kujiendeleza.

Taasisi hiyo imeaanda Kampeni ya uhamasishaji kwa ajili ya wasichana katika Mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma kuwahimiza wasichana wapende na kushiriki mafunzo ya ufundi stadi yatolewayo na vyuo vya ufundi Don Bosco- Tanzania.
.
Taasisi hiyo ambayo huwasaidia vijana wa hali ya chini, inaamini vijana wa kiume na kike wana uwezo sawa, hivyo inatoa vipaumbele kwa wasichana na imeandaa kampeni maalum kwa  ajili ya wasichana ijulikanayo kama BINTI THAMANI. Kampeni hii inanuia  kumkwamua msichana kiuchumi pamoja na kimawazo.

Taasisi ya Don Bosco Tanzania, inatoa mafunzo mbalimbali kwa wasichana ambayo ni Ufundi umeme, uchomeleaji vyuma, ufundi uashi , fundi bomba, uchapishaji, ushonaji ,ufundi magari, ufundi umeme, Kompyuta na uaziri.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Don Bosco Net,  Fr. Celestine Kharkongor wakati akizungumza na mwandishi wetu jijini Dar es Salaam leo katika kituo cha Taasisi hiyo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Nae Afisa Mipango wa Taasisi ya Don Bosco Net-Tanzania, Rosemary Njoki amewasihi wasichana na jamii kwa ujumla kuwa wapanue mawazo yao hasa katika jamii hii ya sasa ambapo msichana baada ya kumaliza masomo ana uwezo mkubwa wa kujifunza na kujiwezesha kiuchumi kupitia mafunzo haya.

Njoki amesema kuwa wasichana ambao wamekata tamaa ya maisha na elimu kuwa wanauwezo na nafasi ya kujikwamua tena kupitia kampeni hii. Sanjali na hayo, anawasihi wasichana wote kutembelea vyuo vyao vya ufundi vya Don Bosco ilikutimiza azima yao ya kujitegemea.

 Zaidi ya masomo ya ufundi, Taasisi Tasisi ya Don Bosco inaitoa masomo mtambuka kama (ujasiria mali,chuo cha maisha , na pia somo la uajiri) ili kumuwezesha msichana  kujiajiri au kuajiriwa. Hivyo kila binti ana uwezo wa kusoma, kujihusisha na kujiendeleza.

BEI YA MADAFU HII LEO

Toyota Brevis inauzwa Bei nzuri kabisa

$
0
0
Toyota Brevis Inauzwa 
Ipo Kwenye hali Nzuri sana.
Maker: Toyota
Model: Brevis
YoM:  2001
CC: 2500
Color: Silver
Registration: Yes
Reg #:  T 740 CUG
Bei: Milioni 10
Ipo kwenye Hali Nzuri kabisa na Imeshalipiwa kila kitu
Kwa mawasiliano piga namba hii 0688 94 94 54

MISA YA MAREHEMU MAMA GREN JUDICA MOSHI Washington DC

$
0
0
Ndugu, jamaa na marafiki mbalimbali, jana (Novemba mosi 2015) walijumuika na wanafamilia katika misa na kusherehekea maisha ya Mama Gren Judica Moshi iliyofanyika hapa Washington DC.

Watoto wawili wa Marehemu Donald na James Moshi, na ndugu wengine, waliungana kwa misa hiyo iliyofanyika alasiri na kufatiwa na chakula cha pamoja
Mchungaji kiongozi wa Kanisa la The Way of the Cross Gospel Ministries Ferdnand Shideko, akiwakaribisha watu waliohudhuria misa hiyo
Mch John Kadyolo akifungua misa kwa maombi
 Wanafamilia


 Richard Mollel akisoma somo la kwanza.
Janice Manse akisoma somo la pili
 Joseph Maro akisoma historia ya marehemu Gren Judica Moshi
 Julius Manase, akiongoza utaratibu wa ibada
Mchungaji Ferdnand Shideko akihubiri
 Wachungaji wakiombea familia
 Watoto wa Marehemu, Donald na James Moshi wakifuatilia Ibada
Wachungaji wakiongoza maombi kwa wanafamilia
 Andrew Mushi akitoa shukrani kwa niaba ya familia



WAJUMBE WA CHAMA CHA KUENDELEZA UFUGAJI NYUKI TANZANIA WATEMBELEA SHAMBA LA PINDA DODOMA

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaongoza baadhi ya wajumbe wa Chama cha Kuendeleza wafugaji Nyuki Tanzania (TABETO) kukagua shamba lake la Zuzu  siku moja baada ya kuzindua chama hicho mjini Dodoma Oktoba 31, 2015.
 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

TAWI LA CCM EMPRESS KWA MUSA MTAA WA SAMORA WASHEREHEKEA USHINDI WA DK. JOHN POMBE MAGUFULI.

$
0
0
1
MBUNGE mteule wa Muleba Kaskazini (CCM) na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Mwijage akisalimiana na Godson Kaligo Mjumbe wa tawi la CCM Epress Social lililopo mtaa wa Samora maarufu kwa Musa Shoeshine alipowatembelea wakati wa sherehe yao ya kusherehekea ushindi wa Rais Mteule Dr. John Pombe Magufuli mara baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu nchini kote, Wana CCM hao wamesherehekea kwa muziki na kupata supu ya mbuzi na nyama choma huku wakiwakaribisha wananchi mbalimbali bila kujali itikadi zao kwani Dr John Pombe Magufuli ni Rais wa Watazania wote.(PICHA NA RASHID SHOTI-DAR ES SALAAM)
3
MBUNGE mteule wa Muleba Kaskazini (CCM) na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Mwijage akibadilishana mawazio na Godson Kaligo na wana CCM wa tawi hilo.
4
Katibu wa Tawi hilo Musa Mtulia ambaye pia ni Shoeshine Maarufu mtaa wa Samora akiendelea na kazi yake huku wana CCM wengine na wadau wengine wakiendelea na sherehe hiyo kwa kupata supu.
5
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa tawi hilo Hassan Mneo. Mjumbe Godson Kaligo pamja na wadau wengine wakipata supu kutoka kulia ni Bw. Haogwa na Mzee Mnonji shabiki maarufu wa timu ya Simba.
6
Mwana CCM Richard Wambura aliyesimama nyuma naye alijumuika na wana CCM wenzake wakati alipowatembelea tawini hapo
7
Hapa ni mwendo wa kutafuna mbuzi tu.
89
Mwenyekiti Hassan Mneo kushoto na we nzake wakipata supu na kahawa katika wtawi hilo.
10
Katibu wa tawi Musa Mtulia akifurahi na wadau mbalimbali waliofika katika tawi hilo wakati wa sherehe hiyo.

MVUA ILIYONYESHA JIJINI MWANZA YASABABISHA MAAFA IKIWEMO VIFO NA UWANJA WA NDEGE KUFUNGWA KWA MUDA.

$
0
0
Na:George Binagi-GB Pazzo
Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Jijini Mwanza, zimesababisha Uwanja wa ndege wa Jiji hili kufungwa kwa muda wa masaa matano kutokana na kujaa maji.


Meneja wa Uwanja huo Easter Madale alisema kuwa shughuli za usafirishaji uwanjani hapo, hii leo zilikwama kuanzia majira ya saa tatu asubuhi hadi saa nane mchana, baada ya maji ya mvua kujaa katika maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la kukimbilia ndege.


Alisema kuwa tatizo la maji kujaa uwanjani hapo halikusababishwa na ubovu wa miundombinu, bali ni kutokana na uwanja huo kuzungukwa na vilima vipatavyo saba ambavyo wakati wa mvua za masika hutiririsha maji ambayo huingia hadi uwanjani.


Madale alibainisha kuwa mara ya mwisho maji kujaa uwanjani hapo ilikwa mwaka 2012 na kwamba tatizo hilo lilishughulikiwa kwa kujengewa mifereji mikubwa kwa ajili ya kuzuia maji kuingia katika uwanja huo huku akiongeza mvua iliyonyesha leo imesababisha mifereji na mitaro kuharibika.


Baadhi ya wasafiri wamelalamikia hali hiyo kwa kile walichoeleza kuwa ni ratiba zao za kusafiri kwa ajili ya shughuli zao kukwama na hivyo kuingia kupata usufumbu mkubwa.


Katika hatua nyingine,Mvua hiyo zimesababisha athari mbalimbali kwa wakazi wa Jiji la Mwanza wakiwemo wakazi wa Kihewa, baada ya nyumba zao kujaa maji na hivyo baadhi ya kaya kuhifadhiwa katika shule ya Msingi Kilimahewa.




Kwa mjibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza Charles Mkumbo, mvua hiyo imesababisha vifo vya watu wawili, mmoja akifahamika kwa jina la Zainab Shaban (18) ambae alikuwa ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Nyamanoro aliesombwa na maji wakati akijaribu kuwahi kwenye mtihani wa kuhitimu kidato cha nne pamoja na dereva pikipiki ambae jina lake halikufahamika mara moja.


Alfajiri ya leo Jiji la Mwanza lilikumbwa na mvua ambayo ilidumu kwa zaidi ya masaa matano, hali iliyosababisha adha mbalimbali kwa wakazi na wageni wa Jiji hili.


Hata hivyo Meneja wa Mamlaka ya hali ya hewa Kanda ya Ziwa Augustino Duganda amebainisha kuwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa itaendelea kuwa na mvua nyingi hadi kufikia mwezi wa 12 mwaka huu hivyo ni vyema wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi ikiwemo yenye mafuriko na mkondo wa maji wakahama kutoka kwenye maeneo hayo ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza.
Karibu Uwanja wa ndege wa Mwanza ila si wakati wa Mvua
BINAGI MEDIA GROUP, KWA PAMOJA TUIJUZE JAMII
Picha Zaidi BONYEZA HAPA

FRED SWAGG AACHIA ‘NIMEWAKA’ MTANDAONI

$
0
0
IMG-20151102-WA0031
Na Modewjiblog, team.

Mwanamuziki anayekuja kwa kasi katika tasnia ya muziki Bongo, Fredrick Kalala ama jina la usanii akijulikana zaidi, Fred Swagg ameachia wimbo mpya mtandaoni ‘NIMEWAKA’ au ‘Nimelewa’.

Akizungumza na Modewjiblog kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza, Fred Swagg mkali wa vibao vya Maandishi alichowashirikisha Younf Killer na Kad Go. Ameeleza kuwa katika wimbo wake huo mpya wa Nimewaka, upo katika mahadhi ya rap, ni maalum kwa watu wa rika zote hasa sehemu za starehe ikiwemo Club.

“Wimbo huu mpya wa Nimewaka ni wa ku-Party’ ndani yake kuna komediani ikielezea watu wanavyotumia pesa na kulewa pombe za aina mbalimbali.. hivyo fans wakae mkao wa kula kuanzia sasa itakuwa mtandaoni ikiwemo mkito.com “ ameleza Fred Swagg.

Fred Swagg anabainisha video ya wimbo huo zinatarajia kuanza muda wowote kuanzia mwezi ujao huku kwa sasa akiendelea na promo za nyimbo zake zingine zinazofanya vyema kwenye vituo vya radio mbalimbali za ndani na nje wimbo wa ‘Kikomo’ aliomshirikisha Msanii, Da Prince na wimbo wa Maandishi aliowashirikisha Young Killer na Kad-Go.

NAIBU KATIBU MKUU MPYA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AANZA KAZI RASMI NA KUWATAKA WATUMISHI KUTEKELEZA KAULI MBIU YA “HAPA KAZI TU”

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aliyeteuliwa hivi karibuni, John Mngodo, akijitambulisha kwa Watumishi  mara baada ya kuanza kazi rasmi  katika Wizara hiyo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Lilian Mapfa na kushoto ni Mwenyekiti wa TUGHE,  Obedi Mbaga.

Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba akijitambulisha mbele ya Naibu Katibu Mkuu mpya, John Mngodo (hayupo pichani) wakati wa Mkutano kati ya Watumishi na Naibu Katibu Mkuu huyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara.
Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo, akizungumza na Watumishi mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara (hayupo pichani) alipofanya mkutano na watumishi hao mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).

Imeandaliwa na Kitengo Cha Mawasiliano  Serikalini-Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

NAIBU KATIBU MKUU-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aliyeteuliwa hivi karibuni, John Mngodo, akijitambulisha kwa Watumishi  mara baada ya kuanza kazi rasmi  katika Wizara hiyo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Lilian Mapfa na kushoto ni Mwenyekiti wa TUGHE,  Obedi Mbaga.
 Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba akijitambulisha mbele ya Naibu Katibu Mkuu mpya, John Mngodo (hayupo pichani) wakati wa Mkutano kati ya Watumishi na Naibu Katibu Mkuu huyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara.
 Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo, akizungumza na Watumishi mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara (hayupo pichani) alipofanya mkutano na watumishi hao mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).

Imeandaliwa na Kitengo Cha Mawasiliano  Serikalini-Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Katibu Mkuu wa Uchukuzi atembelea eneo inapojengwa Reli Mpya ya kisasa ya standard gauge

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka,akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu Rwanda, Rwakunda Christian,wakati walipotembelea ujenzi wa reli mpya ya kisasa, iliyoanza kujengwa Mkoani Pwani, katika eneo la Soga.
 Muonekano wa ujenzi wa reli mpya wa kisasa Standard Gauge, ambayo inaendelea kujengwa katika eneo la soga mkoani Pwani.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka (wa tatu kutoka kulia), akiwa katika picha pamoja na Uongozi wa Taasisi inayosimamia usafirishaji katika Ukanda wa Kati pamoja na Viongozi wa Nchi zinazotumia ukanda wa Kati, wakati walipotembelea ujenzi huo hivi karibuni, katika eneo la Soga, Pwani.
Muonekano wa Vituo vya Reli hiyo Mpya ya kisasa ya standard Gauge, itakapokamilika.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu Rwanda, Rwakunda Christian, akiteta jambo na maafisa kutoka nchi zinazotumia ukanda wa kati kusafirisha bidhaa zao, wakati wakiangalia ramani ya reli mpya ya kisasa, walipotembelea ujenzi wa reli mpya ya kisasa ya standard gauge, hivi karibuni Mkoani Pwani. Viongozi hao walifurahishwa na maendeleo ya ujenzi huo kwa sababu utarahisisha usafirishaji wa mizigo kwani itapitisha mzigo zaidi na ukubwa wa reli hiyo utaongeza spidi ya treni.(Habari Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)

KAMPENI YA BINTI THAMANI KUFANYIKA NOVEMBA 17 KATIKAUKUMBI WA KING SOLOMONI JIJINI DAR

$
0
0
Mratibu wa Kampeni ya BINTI THAMANI wa Taasisi ya Don Bosco Net Tanzania, Agnes Mgongo akizunumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO kuhusiana kampeni ya BINTI THAMANI itakayofanyika katika ukumbi wa King Solomoni jijini Dar es Salaam na kampeni hiyo itakuwa inawalenga hasa wasichana ili kufikia malengo yao kwa kutumia fursa zinazotolewa na vyuo vya Don Bosco hapa nchini.
Mkurugenzi wa malezi ya vijana wa Taasisi ya Don Bosco Net Tanzania, Padre, Dustan Haule akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa habari MAELEZO kuhusiana na harakati za kuwakomboa wasichana na uwepo wa kampeni ya BINTI THAMANI ambayo itafanyika katika ukumbi wa King Solomoni jijini Dar es Salaam, pia amewakaribisha wadau na wafadhili mbalimbali katika kufanikisha kampeni ya BINTI THAMANI itakayo wawezesha wasichana ili kufikia maelengo na waweze kujitegemea katika jamii. Aidha alimtambulisha Msanii wa Kizazi Kipya Elias Barnaba (Barnaba Boy Classic) pamoja na Mshereheshaji na Mchekeshaji MC, Pilipili kuwa watakuwepo katika kampni ya BINTI THAMANI  itakayofanyika Novemba 17 mwaka huu katika ukumbi wa King Solomon jijini Dar es Salaam. 

Kutoka kushoto ni Msanii wa Kizazi Kipya Elias Barnaba (Barnaba Boy Classic) na Mshereheshaji na Mchekeshaji MC, Pilipili wakiwa katika mkutano ulioandaliwa na Taasisi ya Don Bosco Net-Tanzania leo katika ukumbi wa Habari MAELEZO jijini Dar es Salaam.
Msanii wa Kizazi Kipya Elias Barnaba (Barnaba Boy Classic) akizungumza na waandishi wa habari kuwa atatumbuiza katika kampeni ya BINTI THAMANI ambayo itafanyika Novemba 17 katika ukumbi wa King Solomoni  jinini Dar es Salaam. Pia aliwasihi wasichana kujitokeza kwa wingi ili waweze kuwahamasisha wasichana wengi zaidi ili kujipatia mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Don Bosco Net Tanzania.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwasikiliza waandaaji wa kampeni ya BINTI THAMANI itakayofanyika Novemba 17 mwaka  katika ukumbi wa King Solomoni jijini Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

Zantel staff meets with Benoit Janin new CEO

$
0
0
 

Dar es Salaam-November 2,2015: Zantel Tanzania, welcomed Benoit Janin new Chief Executive Officer taking over the reigns from Pratap Ghose.
A 17-year telecom industry veteran, Benoit is best known for his tenure as a Tigo Chad CEO, where he successfully led Tigo Chad to experience a significant double-digit growth to become the unchallengeable market leader and also launching 3G and 4G services.

Prior to joining Millicom Group Benoit has worked for almost 3 years in Vimpelcom group as the CCO of their Cambodia operation and before that, he worked for 10 years within Orange Group in various consultant and then C-level roles.

Speaking of his new role, Benoit said he is excited to join Zantel and looks forward to work together with the Zantel team to reenergize the Zantel brand.
"I am motivated by the challenge in creating the new era for Zantel where we are going to leverage the current brand status, increase the quality of service, improve mobile money services and expand areas of Corporate Social Responsibility ’ said Benoit.

Benoit has a Master of Science (MSc) degree in Business Administration and Management from the ICN High Business School in France. 

He also has a Leadership program certificate from Stanford Business School, together with a Post-Graduate degree in Foreign languages (DEUG LEA in English & German) from Aix-en-Provence University.

In Zantel he would be responsible for enhancing market share and margins along with growth of alternate revenue streams including 4G, Data, Ezypesa and value added services, taking Zantel to next phase.
Mr. Beneth Kagoro receiving “Long service awarded” handed over to him by CEO, accompanied by Mrs. Joanitha Mrengo HR Director on the right.
CEO addressing Zantel staff during the event.
Flash mob dancers performing during the event. 

UFAFANUZI WA TUKIO LA KUANGUKA KWA JUKWAA LA JENGO LA NHFI MKOANI MBEYA

$
0
0
nh1
Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti akifafanua jambo wakati akizungumza waandishi wa habari kuhusu kuvunjika kwa uzio wa jengo la mfuko huo linalojengwa mkoani Mbeya kutokana na kukumbwa na mvua na upepo mkali, amesema jengo hilo liko salama kabisa ila uzio unaosaidia kuwakinga wajenzi ndiyo ulioanguka kutokana na upepo huokulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa NHIF,Bw Rehani Athuman.
nh2
Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti akifafanua jambo wakati akizungumza waandishi wa habari kuhusu kuvunjika kwa uzio wa jengo la mfuko huo linalojengwa mkoani Mbeya.
nh3
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa NHIF,Bw Rehani Athuman akionyesha mchoro wa jengo hilo kwa waandishi wa habari, kushoto ni Mkurugenzi wa Uendeshaji (NHIF),Eugen Mikongoti
......................................................................................................
Utangulizi:
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) hivi sasa unaendelea na ujenzi wa majengo katika mikoa mbalimbali nchini, kwa lengo la kujitosheleza kwa majengo ya ofisi na kukidhi mahitaji ya wanachama wake na wadau wengine.Moja ya mikoa ambayo inaendelea na ujenzi huo ni Mbeya, ambako Mfuko unajenga jengo la ghorofa kumi na mbili litakalokuwa na nafasi za ofisi na huduma nyingine ndani yake.

Tukio la Kuanguka kwa jukwaa:
Wakati shughuli hizo za ujenzi zinaendelea, jana mchana katika hali isiyotarajiwa mvua iliyoambatana na upepo mkali ilinyesha mjini Mbeya. Upepo na mvua hizo vilisababisha kuanguka kwa jukwaa la jengo hilo na kutua juu la paa la jengo la ofisi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Mbeya. 

Kuanguka kwa jukwaa hilo hakukuwa na madhara yoyote kwa maisha ya binadamu, kwa maana kuwa hakuna mtu aliyepoteza maisha au kupata majeraha. Hata hivyo tukio hilo lilisababisha taharuki kwa wafanyakazi wapatao hamsini waliokuwemo ndani ya jengo hilo na hivyo kusababisha kazi kusimama kwa muda. Aidha tathmini ya awali iliyofanyika katika paa la jengo la TANESCO lililoangukiwa na jukwaa hilo inaonyesha kuwa paa hilo ilipata hitilafu ndogo ambayo itafanyiwa marekebisho kwa gharama za Mkandarasi anayejenga jengo la NHIF.

Hatua za kisualama zilizochukuliwa:
Kama sheria za ujenzi zinavyoagiza, kabla ya kuanza kwa ujenzi wa jengo hilo Mkandarasi alishajenga uzio kuzunguka jengo zima ili kuhakikisha kuwa shughuli za ujenzi hazileti madhara kwa wapita njia au ofisi zilizo jirani. Umakini wa Mkandarasi huyo katika kuzingatia taratibu za tahadhari katika shughuli za ujenzi, umewezesha jengo hilo la ghorofa kumi na mbili kufikia hatua nzuri ya ujenzi bila madhara yoyote kwa wajenzi wenyewe, wapita njia au ofisi za jirani.

Aidha kufuatia tukio la Jumatatu 02/11/2015, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeshamwandikia Mkandarasi anayeendelea na ujenzi katika jengo hilo kuhakikisha kuwa uzio unaozunguka jengo zima unaimarishwa zaidi hususani wakati huu tunapokaribia kipindi cha mvua za masika ili kuepuka uwezekano wa madhara yoyote kwa binadamu wakati shughuli za ujenzi zinaendelea.

Namna Habari ilivyoripotiwa:
Tunapenda kuufahamisha umma kwamba habari zilizoripotiwa jana na baadhi ya vyombo vya habari kwamba jengo la NHIF mkoani Mbeya limeporomoka, zilipotosha ukweli wa tukio hilo, kwani kilichoporomoka siyo jengo, bali ni jukwaa.Tunapenda kusisitiza kuwa tukio hilo limesabishwa na mvua kubwa na upepo uliovuma katika mji wa Mbeya, wala siyo uzembe wa Mkandarasi anayejenga jengo hilo.

Wito kwa Wanachama wa NHIF:
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya unawaomba wanachama na wadau wake nchini kote waendelee kuwa watulivu na kuvuta subira kwani changamoto ya ufinyu wa ofisi katika mikoa itakuwa imepatwa ufumbuzi baada ya kukamilika kwa ujenzi wa majengo ya unaoendelea hivi sasa katika mikoa mbali mbali nchini.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu,
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI WILLIAM LUKUVI AAGA RASMI SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokea ngao yenye picha ya chui ikiwa ni ishara ya tuzo ya Shirika la Nyumba la Taifa kwa Waziri huyo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Kyando Mchechu kwa kuonyesha utendaji uliokuwa wa kasi usiochoka wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokea ngao yenye picha ya chui ikiwa ni ishara ya tuzo ya Shirika la Nyumba la Taifa kwa Waziri huyo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Kyando Mchechu kwa kuonyesha utendaji uliokuwa wa kasi usiochoka wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokea kadi ya pongezi ya Shirika la Nyumba la Taifa kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii, Susan Omari kwa kuonyesha utendaji uliokuwa wa kasi usiochoka wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Baadhi ya mameneja wa Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) wakifuatilia mazungumzo wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Waziri Lukuvi akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Waziri Lukuvi akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Fatma Chillo akizungumza kwa niaba ya Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo kumshukuru Waziri huyo wakati Waziri alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi ameiagiza Menejimenti ya Shirika hilo kuhakikisha inaendeleza kasi ya ujenzi wa nyumba za makazi na biashara bila kusahau misingi iliyoliunda shirika hilo.

Akizungumza leo wakati akiaga rasmi Shirika hilo alisema amejifunza mengi katika uwepo wake ndani ya Wizara na hasa dhamira na utendaji wa kasi wa Shirika hilo na akaiagiza menejimenti ya Shirika hilo kufanya kazi bila kuchoka likihakikisha linapigania makazi bora kwa kila mtanzania.

"Kabla ya kuingia katika Wizara , na hata nilipoingia sikuwa nafahamu kwa kina kwamba Shirika la Nyumba limebadilika kutoka lile la kuangalia nyumba za msajili wa majumba na kuwa sasa limejenga nyumba nyingi na kuziuza kwa Watanzania, sasa nimefahamu kwa kujifunza kwamba Shirika letu hili limebuni utaratibu unaolifanya lifanye kazi kwa kasi kubwa kibiashara lakini pia likibakia na 'human face', "alisema Lukuvi.

Alisema Serikali inafahamu changamoto linazokabiliana nazo Shirika hilo za ulipaji wa VAT mara mbili na gharama za miundombinu kama maji, umeme na barabara ambazo mara kadhaa zimekuwa zikirudi kwa mnunuzi wa mwisho na kwamba zinafanyiwa kazi pia akaliagiza Shirika na mamlaka hizo kukaa pamoja na kuweka mipango yao pamoja ili angalau kuliwezesha Shirika kuwafikia Watanzania wengi.

Waziri Lukuvi alisema kuwa Serikali inaitambua sekta ya nyumba kuwa ni sekta mtambuka kwa kuwa hukuza uchumi, huongeza ajira na kusaidia kudumisha amani ya nchi yetu. Hivyo, alilihimiza Shirika hilo liendelee na mipango yake kabambe ya kujenga nyumba za gharama nafuu ili kuwawezesha wananchi wengi kumiliki nyumba.

Alisema wananchi wengi wakimiliki nyumba utakuwa mkakati mmojawapo wa kupunguza umaskini nchini maana wananchi hao wataweza kutumia nyumba zao kupata mikopo benki ya kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.
Akiungumzia Serikali ya awamu ya Tano ijayo alisema kama kuna watumishi wa umma ambao walikuwa wakifanya mambo kwa mazoea katika awamu zilizopita basi awamu hii wahakikishe wanakuwa mguu sawa kwani Serikali ya Magufuli ambayo inaingia madarakani ni serikali isiyotaka mchezo wala lele mama na kwamba wala rushwa, na wazembe watatafuta mlango wa kutokea.

Akimkaribisha Waziri Lukuvi, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu alisema Shirika hilo linatekeleza miradi yake ili kuhakikisha linaweka makazi bora kwa Watanzania
Alisema kwa shirika hilo lonafanya hivyo kwa kuwa sekta ya nyumba ni sekta mtambuka katika maendeleo ya uchumi. 

Sekta ya nyumba husaidia kuleta maendeleo ya haraka ya sekta zinginena kutoa ajira. Taifa linalozingatia sekta ya nyumba huwezesha nchi yao kuwa na amani, kwani mtu mwenye makazi bora, huthamini uwepo wa amani.

RAIS KIKWETE AMTEUA PROFESA MBETTE KUWA MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI WA KAMPUNI YA SIMU TANZANIA

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAWASILIANO SAYANSI NA TEKNOLOJIA 
TAARIFA KWA UMMA 
UTEUZI WA MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI WA KAMPUNI YA SIMU TANZANIA 
        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Prof. Tolly Salvatory Augustin Mbwette  kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kwa kipindi cha miaka miaka mitatu kuanzia tarehe 12 Oktoba 2015. 


Uteuzi huo ni kwa mujibu wa kifungu Na. 9 (4) (a) cha Sheria Na. 20 ya Mwaka 1993 iliyoanzisha Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Prof. Tolly Salvatory Augustin Mbwette amekuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania kwa kipindi cha miaka kumi kuanzia tarehe 13 Aprili 2005 hadi tarehe 13 Aprili 2015. Pia amekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwa taaluma ni Mhandisi ujenzi aliyobobea kwenye maeneo ya Mazingiria, TEHAMA, Utawala na Menejimenti kwa zaidi ya miaka 25 na amesoma Vyuo Vikuu vya Dar es Salaam, Tanzania; IHE Delft, Netherland; na Chuo Kikuu cha London, Uingereza kwa ngazi ya Shahada ya Kwanza, Uzamili na Uzamivu. Pia ameshirikiana na Vyuo Vikuu mbali mbali duniani kutoka Bara la Ulaya, Amerika, Asia na Afrika katika maeneo ya uhandisi, utafiti, TEHAMA, uandishi wa vitabu na majarida mbali mbali.

Imetolewa na:


KATIBU MKUU


Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI WILLIAM LUKUVI AAGA RASMI SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokea ngao yenye picha ya chui ikiwa ni ishara ya tuzo ya Shirika la Nyumba la Taifa kwa Waziri huyo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Kyando Mchechu kwa kuonyesha utendaji uliokuwa wa kasi usiochoka wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Waziri wa ArdhiNyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokea ngao yenye picha ya chui ikiwa ni ishara ya tuzo ya Shirika la Nyumba la Taifa kwa Waziri huyo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Kyando Mchechu kwa kuonyesha utendaji uliokuwa wa kasi usiochoka wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Waziri wa ArdhiNyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi akipokea kadi ya pongezi ya Shirika la Nyumba la Taifa kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii, Susan Omari kwa kuonyesha utendaji uliokuwa wa kasi usiochoka wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Baadhi ya mameneja wa Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) wakifuatilia mazungumzo wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati Waziri Lukuvi alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.
Waziri Lukuvi akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Waziri Lukuvi akizungumza na Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo wakati alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Fatma Chillo akizungumza kwa niaba ya Wakurugenzi na Mameneja wa Makao Makuu ya Shirika hilo kumshukuru Waziri huyo wakati Waziri alipotembelea katika Shirika hilo kuaga rasmi.

Waziri wa ArdhiNyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi ameiagiza Menejimenti ya Shirika hilo kuhakikisha inaendeleza kasi ya ujenzi wa nyumba za makazi na biashara bila kusahau misingi iliyoliunda shirika hilo.

Akizungumza leo wakati akiaga rasmi Shirika hilo alisema amejifunza mengi katika uwepo wake ndani ya Wizara na hasa dhamira na utendaji wa kasi wa Shirika hilo na akaiagiza menejimenti ya Shirika hilo kufanya kazi bila kuchoka likihakikisha linapigania makazi bora kwa kila mtanzania.

"Kabla ya kuingia katika Wizara , na hata nilipoingia sikuwa nafahamu kwa kina kwamba Shirika la Nyumba limebadilika kutoka lile la kuangalia nyumba za msajili wa majumba na kuwa sasa limejenga nyumba nyingi na kuziuza kwa Watanzania, sasa nimefahamu kwa kujifunza kwamba Shirika letu hili limebuni utaratibu unaolifanya lifanye kazi kwa kasi kubwa kibiashara lakini pia likibakia na 'human face', "alisema Lukuvi.

Alisema Serikali inafahamu changamoto linazokabiliana nazo Shirika hilo za ulipaji wa VAT mara mbili na gharama za miundombinu kama maji, umeme na barabara ambazo mara kadhaa zimekuwa zikirudi kwa mnunuzi wa mwisho na kwamba zinafanyiwa kazi pia akaliagiza Shirika na mamlaka hizo kukaa pamoja na kuweka mipango yao pamoja ili angalau kuliwezesha Shirika kuwafikia Watanzania wengi.

Waziri Lukuvi alisema kuwa Serikali inaitambua sekta ya nyumba kuwa ni sekta mtambuka kwa kuwa hukuza uchumi, huongeza ajira na kusaidia kudumisha amani ya nchi yetu. Hivyo, alilihimiza Shirika hilo liendelee na mipango yake kabambe ya kujenga nyumba za gharama nafuu ili kuwawezesha wananchi wengi kumiliki nyumba.

Alisema wananchi wengi wakimiliki nyumba utakuwa mkakati mmojawapo wa kupunguza umaskini nchini maana wananchi hao wataweza kutumia nyumba zao kupata mikopo benki ya kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.

Akiungumzia Serikali ya awamu ya Tano ijayo alisema kama kuna watumishi wa umma ambao walikuwa wakifanya mambo kwa mazoea katika awamu zilizopita basi awamu hii wahakikishe wanakuwa mguu sawa kwani Serikali ya Magufuli ambayo inaingia madarakani ni serikali isiyotaka mchezo wala lele mama na kwamba wala rushwa, na wazembe watatafuta mlango wa kutokea.

Akimkaribisha Waziri Lukuvi, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu alisema Shirika hilo linatekeleza miradi yake ili kuhakikisha linaweka makazi bora kwa Watanzania
Alisema kwa shirika hilo lonafanya hivyo kwa kuwa sekta ya nyumba ni sekta mtambuka katika maendeleo ya uchumi.

 Sekta ya nyumba husaidia kuleta maendeleo ya haraka ya sekta zinginena kutoa ajira. Taifa linalozingatia sekta ya nyumba huwezesha nchi yao kuwa na amani, kwani mtu mwenye makazi bora, huthamini uwepo wa amani.

UCHAMBUZI WA HABARI TOKA VITUO MBALIMBALI VYA TELEVISHENI NOVEMBA 3, 2015.

$
0
0
Huu ni uchambuzi wa Habari toka vituo mbalimbali vya Televisheni Mchana Huu November 3, 2015.

Watu 6 wamefariki dunia na 1 kujeruhiwa katika matukio 4 tofauti yaliyotokea mkoani Singida toka oktoba 31 na November 1.

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama Vya siasa nchini Peter Mziray avishauri vyama vya siasa kutumia baraza hilo kutatua Migogoro kwa Njia ya Mazungumzo. https://youtu.be/Z90lI_ga7Mg

Wahamiaji Haramu raia Wa Ethiopia waliokamatwa wakiwa ndani ya lori wamehukumiwa kutumikia kifungo cha miezi 6 jela au faini ya laki 5  https://youtu.be/xc637Ykh6Mw

Halmashauri ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa imefanikiwa kutatua baadhi Ya changamoto zinazoikabili sekta ya Kilimo kwa kuongeza idadi ya Afisa Ughani. https://youtu.be/nqk4rGU6hvE

Kamati kuu Ya Chama Cha Mapinduzi CCM imetangaza kurudiwa kwa zoezi la kura za maoni katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Handeni. https://youtu.be/RVTSjWOxPGc

Aliyekuwa mgombea Uraisi CCK aliyeenguliwa na NEC Dkt. Godfrey Malisa akusudia kuwania nafasi ya Spika wa Bunge. https://youtu.be/m4gnvAcUJn4

Kukusekana kwa Umeme na Huduma za Maji kumetajwa kukwamisha maendeleo ya wanafunzi wa mchepuo wa sayanzi katika Shule Ya Wel Wel. https://youtu.be/PcmWUOA-v-o
Raisi Jakaya Kikwete azungumzia ushindi wa ccm kuwa umetokana na kazi kubwa iliofanywa na vijana katika kuhakikisha ushindi wa Kishindo kwa Dkt. Magufuli huku akiviponda baadhi ya Vyombo vya Habari kuegemea Upande wa wapinzani na kunyima Fursa ya wananchi kusikia Sera za Chama Cha Mapinduzi. https://youtu.be/OoQicJcNJAI

Viewing all 46367 articles
Browse latest View live




Latest Images