Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46193 articles
Browse latest View live

MTOTO HATUMWI DUKANI LEO . NI KATIKA UFUNGAJI WA KAMPENI ZA CCM JIJINI MWANZA.

0
0
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu (Pichani) amesema kuwa maandalizi kwa ajili ya shughuli ya kufunga kampeni za Uchaguzi Mkuu kitaifa kwa upande wa Chama hicho inayotarajiwa kufanyika hii leo katika Uwanja wa CCM Kirumba yamekamilika.

Na:George Binagi-GB Pazzo
Screen kubwa itafungwa nje ya uwanja huo kwa ajili ya wale watakaokosa nafasi ya kuingia uwanjani kwa kuwa shughuli hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na Maeneo jirani.
Mbali na Mgombea Urais wa CCM Dkt.John Pombe Magufuli kuwepo katika mkutano huo, pia Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaemaliza muda wake Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa miongoni mwa viongozi watakaohudhuria katika Mkutano huo wa Ufungaji wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa upande wa CCM 
Wakati Watanzania wakitarajia kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu siku ya kesho jumapili ya Octoba 25, Chama cha Mapinduzi CCM kimejihakikishia ushindi mnono katika maeneo mbalimbali nchini kuanzia ngazi ya udiwani, Ubunge na Urais.
Shamra shamra kwa makada wa CCM zimepamba moto katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Mwanza katika kuelekea kwenye ufungaji wa kampeni za chama hicho kitaifa unaofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba.

UCHAMBUZI WA MAGAZETI OKTOBA 24,2015

0
0
Magufuli afunika Dar ,Lowassa awanadi viongozi CCM kwenye kampeni ,UKAWA kufunga kampeni jangwani. Tazama uchambuzi wa magazeti. 
Mahakama yapiga marufuku kukaa mita 200,Magufuli afunika,Lowassa asema mwisho wa CCM kesho. Fuatilia uchambuzi wa magazeti ya leo. https://youtu.be/0OygojVUywg
UKAWA wapata pigo,mwisho wa CCM ni kesho asema lowassa, Mahakama yapiga marufuku mita 200.Fuatilia habari kupitia uchambuzi wa magazeti. https://youtu.be/TuyqynV3cuY
Van Gaal na Wenger watofautiana,Yanga yazitega Simba na Azam,Kocha wa Simba byebye.Fuatilia uchambuzi wa magazeti. https://youtu.be/aCc_l0GXYq0

SERIKALI YASAINI MKATABA WA UNUNUZI WA MAGARI NA KAMPUNI YA ASHOK LEYLAND KWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA, JIJINI DAR

0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima (kulia), Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kutengeneza Magari ya ASHOK LEYLAND ya nchini India, Bhimasena Rau wakisaini Mkataba wa ununuzi wa magari kwa ajili ya matumizi ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama ambavyo ni Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, jijini Dar es Salaam. 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima (kulia), Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kutengeneza Magari ya ASHOK LEYLAND ya nchini India, Bhimasena Rau wakipongezana baada ya kusaini Mkataba wa ununuzi wa magari kwa ajili ya matumizi ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama ambavyo ni Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima (watatu kushoto), akitoa neno la shukrani baada ya kusaini mkataba wa ununuzi wa magari ya Kampuni ya ASHOK LEYLAND ya nchini India. Magari hayo ni kwa ajili ya matumizi ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI. Kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Jumanne Sagini, wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wapili kulia) akipokea Mkataba wa Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Watumishi wa Jeshi la Magereza kutoka kwa Makamu wa Rais wa Kampuni ya Ujenzi ya Poly Technologies ya nchini China. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja. Halfa hiyo ilifanyika katika Ukumbi mdogo wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima (katikati aliyevaa tai), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wakumi kulia), Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Jumanne Sagini (wanane kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Viongozi wa Kampuni ya Kutengeneza Magari ya ASHOK LEYLAND ya nchini India. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi


SERIKALI ya Tanzania imeingia Mkataba wa ununuzi wa magari kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini na Kampuni ya Motorrama (T) LTD ambayo ni Wakala wa Magari aina ya ASHOK LEYLAND kutoka nchini India.


Mkataba huo umesaniwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima pamoja na Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo ya Utengenezaji wa magari, Bhimasena Rau ukishuhudiwa na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, jijini Dar es Salaam.


Akizungumza mara baada mkataba huo kusainiwa, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja aliishukuru Serikali kwa msaada huo ambao utasaidia kutatua tatizo la uhaba wa magari katika Jeshi la Magereza.


“Utekelezaji wa mpango huu katika Jeshi la Magereza utakuwa na manufaa makubwa kwani utapunguza tatizo la uhaba wa magari kwa ajili ya shughuli za uendeshaji na utawala pamoja na utekelezaji wa jukumu la kuwasafirisha Mahabusu kwenda mahakamani na kurudi magerezani,” alisema Minja.


 Lengo kubwa la ununuzi wa Magari hayo unalenga kuboresha huduma za usafiri pamoja na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama hapa nchini.

DAWA ZA KULEVYA AINA YA HEROINE NA COCAINE ZATEKETEZWA CHINI YA UANGALIZI MKALI JIJINI DAR

0
0

 Sehemu ya Kinu cha Kiwanda Cha Saruji Cha Wazo Hill Jijini  Dar es Salaam  ambako dawa za kulevya zimeteketezwa jana chini ya uangalizi mkali . Akizungumza  na waandishi wa habari mara baada ya kuzichoma moto katika kinu hicho Jaji  wa Mahakama Kuu Edison Mkasimongwa alizitaja aina ya dawa hizo kuwa  ni Heroine mifuko 179 na Cocaine mifuko 81 zenye thamani ya Shilingi Bilioni tano ambapo  zilikuwa na Gram 175,000 ambazo zilikamatwa miaka kadhaa Mbezi Jogoo jijini Dar.
Jaji wa Mahakama Kuu Edison Mkasimongwa(kulia) akihakiki sehemu ya kinu cha kuchomea madawa hayo ya kulevya uku akisindikizwa na Mkurugenzi wa Mashtaka  Biswalo Mganga(kushoto) katika Kiwanda Cha Saruji Cha Wazo Hill Jijini  Dar es Salaam
Hii ndio sehemu ya mfuniko wa kinu kilichotumika kuchomea dawa za kulevya
Majaji kutoka mahakama kuu pamoja na polisi wakifuatilia kwa umakini uteketezaji wa dawa za kulevya
Askari wakifungua maboksi yaliyokuwa yamebeba dawa hizo za kulevya kwa ajili ya kuziteketeza katika kinu cha kiwanda cha Saruji hapa jijini Dar.
Jaji wa Mahakama Kuu Edson Masimongwa(kushoto) akifungua moja ya boksi lililobeba dawa za kulevya kwa ajili ya kuhakiki pamoja na kuziteketeza dawa hizo
Askari akizihakiki dawa za kulevya kwa kuzihesabu ili kuziteketeza ambapo zoezi hili lilifanyika katika Kiwanda Cha Saruji Cha Wazo Hill Jijini  Dar es Salaam jana mchana
Sehemu ya Dawa za kulevya zilizoteketezwa jana katika Kiwanda Cha Saruji Cha Wazo Hill Jijini  Dar es Salaam uku zikisimamiwa na majaji wa mahakama Kuu, jeshi la Polisi pamoja na mamlaka ya kudhibiti Dawa za kulevya hapa nchini
Mfanyakazi kutoka kampuni tya Saruji ya Twiga akiziteketeza dawa uku akisimamiwa na jeshi lapolisi, maofisa wa mahakama pamoja na viongozi wa kudhibiti Dawa za kulevya hapa nchini hapo jana katika kiwanda hicho
Maofisa kutika mahakama pamoja na maofisa kutika mamlaka ya udhibiti wa dawa za kulevya wakifuatilia tukio la kuteketeza dawa hizo

TUPIGE KURA, TUPOKEE MATOKEO KWA AMANI NA UTULIVU, KUNA MAISHA BAADA YA UCHAGUZI

0
0

Bendera na ramani ya Tanzania
JUMAPILI ya Oktoba 25, 2015, Tanzania inafanya Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge pamoja na kumpata Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Uchaguzi ni nini? Zipo tafsiri mbalimbali lakini mojawapo na iliyo wazi ni kwamba, hii ni njia ya kidemokrasia inayotumiwa na watu katika kuchagua viongozi wa kuwaongoza kwa kipindi fulani kwa mujibu wa Katiba au utaratibu waliojiwekea wenyewe. 

 Huu ni Uchaguzi Mkuu wa Tano kufanyika tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanza tena mwaka 1992, lakini ni wa 11 tangu Tanganyika na Zanzibar zilipoungana mwaka 1964.

 Uchaguzi wa mwaka huu una umuhimu wa kipekee kwa sababu kadha wa kadha, mojawapo ikiwa umri wa miaka 23 tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanza.

 Huu ni umri mkubwa, na kwa hakika vijana wengi waliojitokeza kujiandikisha safari hii ni wenye umri wa kati ya miaka 18-35, ikimaanisha kwamba wengi wao walizaliwa kuanzia mwaka 1992.

 Hawa wanatengeneza asilimia 57 ya wapigakura wote. Umuhimu mwingine ni kwamba, kulinganisha na uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995, safari hii demokrasia imekua na kupanuka kiasi cha kushuhudia wapigakura 22.75 milioni, idadi ambayo ni kubwa zaidi kuwahi kutokea nchini tangu tupate Uhuru. 

 Kwa upande mwingine, uhuru wa habari umepanuka ukiwamo ukuaji wa sekta ya habari na mawasiliano, hususan mitandao ya kijamii. Haya yote yanatokea kutokana na kuwapo kwa amani na utulivu, sifa ambazo zimeendelea kuitambulisha vyema Tanzania hata katika jumuiya za kimataifa.

 Uchaguzi Mkuu ni gharama kubwa kifedha, rasilimali watu na muda, na kama mambo yatakwenda mrama maana yake nchi itakuwa imeingia hasara kwa kupoteza fedha, lakini pia itaingia kwenye machafuko ambayo yatatowesha amani iliyodumu kwa miaka mingi.

 Madhara ya machafuko au vita – kama tulivyoshuhudia kwa majirani zetu Rwanda na Kenya ni vifo, ulemavu wa kudumu, kutengana na familia, ukimbizi na kuvurugika kwa uchumi, jamii na siasa kwa ujumla. Kwa miaka yote tangu Uhuru, licha ya uchanga na umaskini kama taifa, Watanzania hatujazoea maisha ya vurugu na machafuko na ndiyo maana tuna wajibu wa kuhakikisha uchaguzi huu unapita salama.

 Wajibu wa kulinda amani ya nchi yetu ni wa kila Mtanzania bila kujali rangi, dini, kabila ama nafasi yake katika jamii. Tunaposema hivyo tunamaanisha kwamba, vyombo vya dola vinapaswa kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kuhakikisha Watanzania wanapiga kura kwa amani kuchagua viongozi wao kwa utaratibu waliojiwekea. 

 Kimsingi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ndio wasimamizi wa chaguzi zote, hivyo wana dhamana kubwa kuhakikisha kila aliyejiandikisha na kujitokeza siku hiyo anatumia haki yake ya kikatiba kupiga kura bila kubughudhiwa. Ili kuondoa utata huo, NEC pia inapaswa kuhakikisha kunakuwa na uwazi kuanzia hatua ya kupiga kura mpaka wakati wa kutangaza matokeo, ambayo pia yanatakiwa kutolewa kwa wakati ili kuondoa mashaka miongoni mwa wagombea na wananchi kwa ujumla.

 Wanasiasa, hususan wagombea ama wapambe wao, wanapaswa kutoa kauli za kuhamasisha amani na utulivu kwa siku hizi chache zilizosalia kuelekea uchaguzi mkuu, siku ya uchaguzi na baada ya kutangazwa kwa matokeo.

 Wanasiasa wanaaminika kwa wananchi, kwa hiyo kauli yoyote watakayoitoa ama inaweza kujenga au kubomoa amani iliyopo, hivyo kuondoa utulivu na kuisambaratisha Tanzania ya sasa iliyotukuka ulimwenguni kote kama kisiwa cha amani na utulivu.

 Vyombo vya habari navyo vina wajibu mkubwa zaidi kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa usalama na amani na hata baada ya matokeo kutangazwa viendelee kudumisha amani hiyo. Hilo litawezekana tu iwapo vyombo vya habari vitaandika au kutangaza habari kwa kufuata sheria za nchi, miiko na maadili ya taaluma na fani ya uandishi wa habari ikiwa ni pamoja na kutoegemea upande wowote, kuepuka lugha za uchochezi na ushabiki wa kisiasa, kabla na wakati wa kutangaza matokeo.

 Kutokana na umuhimu huo, sisi wamiliki wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania (Bloggers) tumejadiliana na kukubaliana kwa pamoja kuhusu hatma na mustakabali wa taifa letu kuhakikisha amani na utulivu vinadumishwa wakati na baada ya uchaguzi huu wa kidemokrasia na kwa kauli moja tumetoa msimamo wetu kuhusu amani ya nchi hii. 

 Kwa ujumla, hakuna anayeweza kujisifu kuwa ana uhalali zaidi wa taifa hili kuliko mwingine, taifa hili ni letu sote, hivyo wajibu wa kulinda na kudumisha amani na usalama wa nchi ni wa kila mmoja. 

 Tunaomba Watanzania wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura kwa amani na utulivu, wasubiri matokeo kwa amani na utulivu, wapokee matokeo kwa amani na utulivu, maisha yaendelee kwa amani na utulivu, tusonge mbele kwa amani na utulivu huku tukijua kwamba kuna maisha baada ya uchaguzi, na hilo ndilo muhimu zaidi.

 MUNGU IBARIKI TANZANIA!

MAADHIMISHO YA SIKU YA TAKWIMU DUNIANI YAFANA

0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuhutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Takwimu Duniani yaliyofanyika leo katika Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni "Takwimu Bora, Maisha Bora".
 Wanafunzi wa Stashada wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika wakiwa wameshikilia bendera za nchi wanachama wanaoshikiana na nchi ya Tanzania kuendesha chuo hicho wakati wa maadhimisho ya Siku ya Takwimu Duniani yaliyofanyika leo katika Chuo hicho kilichopo jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni "Takwimu Bora, Maisha Bora".
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) wakati akihutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Takwimu Duniani yaliyofanyika leo katika Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni "Takwimu Bora, Maisha Bora". (Picha na Veronica Kazimoto)

Na: Veronica Kazimoto
WATAKWIMU vijana wameaswa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kusaidia katika ukusanyaji na upatikanaji wa takwimu bora zitakazosaidia katika kupanga mipango ya maendeleo.
Akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Takwimu Duniani yaliyofanyika leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa amesema vijana wenye taaluma ya takwimu wana nafasi kubwa katika kuhakikisha kuwa kuna upatikanaji wa takwimu bora nchini.

"Ninyi watakwimu ambao bado ni vijana mna jukumu la kuhakikisha kuwa mnatumia taaluma yenu ya takwimu katika kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi ili zitumike katika kupanga na kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo,” amesema Dkt. Chuwa.

Dkt. Chuwa amesema maadhimisho haya ya Siku ya Takwimu Duniani yana nafasi kubwa katika kutambua umuhimu wa takwimu katika kufanikisha utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii na kuboresha maisha ya wananchi.
Aidha, amesema kuwa kutokana na dunia kuzindua Mpango Mpya wa Maendeleo Endelevu (SDGs), ofisi yake imejipanga vyema katika kuhakikisha takwimu bora zinapatikana kwa wakati ili zisaidie Taifa katika kutekeleza malengo ya mpango huo.

“Kutokana na umuhimu wa takwimu katika utekelezaji wa malengo 17 na viashiria 169 vya Mpango wa Maendeleo Endelevu, Ofisi ya Taifa ya Takwimu imejipanga vyema katika kuhakikisha takwimu zote muhimu zinapatikana na kusaidia katika utekelezaji wa malengo ya mpango huu,” amesisitiza Dkt. Chuwa.

Siku ya Takwimu Duniani huadhimishwa kila baada ya miaka mitano tarehe 20 Oktoba ambapo kwa mwaka huu maadhimisho haya yameongozwa na Kauli mbiu isemayo “Takwimu Bora, Maisha Bora”.

ASKARI MOSHI,WANAVYOJIWEKA TAYARI KWA UCHAGUZI WA KESHO

0
0
Baadhi ya viongozi wa ngazi ya Juu Katika jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika maandalizi ya mazoezi.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro.Fulgence Ngonyani akipokea taarifa fupi toka kwa kiongozi wa kikosi cha kutuliza ghasia.

Askari Polisi wa vikosi mbalimbali vya jeshi hilo mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika zoezi maalum.
RPC Ngonyani akiongoza matembezi ya askari Polisi ikiwa ni sehemu ya mazoezi.
Kikosi cha kutuliza Ghasia ,FFU.
Matembezi yakiendelea kupita maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi.
Asakari Polis wakiimba nyimbo katika zoezi hilo.
Wakati mwingine mchakamchaka ulichukua nafasi.
Hatimaye mazoezi hayo yakafikia tamati katika viwanja vya Polisi vilivyoko katika ofisi za FFU.
Baadhi ya viongozi wa jeshi hilo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

DKT JAKAYA KIKWETE NA DKT JOHN POMBE MAGUFULI WAWASILI JIJINI MWANZA MCHANA HUU KUHITIMISHA SHUGHULI ZA KAMPENI

0
0
 Mwenyekiti wa CCM,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na Mgombea Urais wa chama hicho Dkt John Pombe Magufuli,mara baada ya kuwasili katika uwanja wa CCM Kirumba kuhitimisha shughuli za kampeni nchini kote,ambapo hapo kesho wananchi wanatarajia kupiga kura ya kuwachagua viongozi wawatakao.
 Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Kikwete na Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli wakielekea jukwaani kwa pamoja mara baada ya kupokelewa katika uwanja wa CCM Kirumba ambapo umati mkubwa watu umejitokeza kushuhudia tukio hilo adhimu.
 Mara baada ya kuwasalimia Wananchi kwa pamoja wakirejea meza kuu.

 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kupitoa chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwasili ndani ya uwanja wa CCM Kirumba huku akilakiwa na melfu ya wakazi wa jiji la Mwanza waliofurika hivi sasa kwenye hitimisho la mikutano ya kampeni.
 Wakazi wa jiji la Mwanza wakishangilia wakati Mgombea Urais wa CCM alipokuwa akiwasili ndani ya uwanja wa CCM Kirumba hivi punde kuhitimisha mikutano ya kampeni,ambapo kesho Wananchi nchini watapiga kura kuwachagua viongozi wawatako kuwatumikia katika awamu ya tano.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwasili ndani ya uwanja wa CCM Kirumba huku akilakiwa na melfu ya wakazi wa jiji la Mwanza waliofurika hivi sasa kwenye hitimisho la mikutano ya kampeni.
PICHA NA MICHUZI JR-MWANZA

AMSHA AMSHA YA MWANZA, KUELEKEA MKUTANO WA KUFUNGA KAMPENI ZA CCM

0
0
 Leo ni Leo Mwanza... maana wakazi wa jiji La Mwanza na vitongoji vyake wamejitokeza kwa wingi kumpokea mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli. Huku Maelfu ya watu wamejitokeza kwenda CCM Kirumba jijini Mwanza kuhudhuria mkutano wa kufunga kampeni leo Oktoba 24, 2015.
 Kila mmoja akijikaza kujongea CCM Kirumba, Mwanza.

 Akina mama nao wamo.....
 Vijana wamehamasika kweli kweli....
 Leo hapakaliki...

MKURUGENZI WA SHIRIKA LA MISAADA LA UINGEREZA AKUTANA NA RAIS.

0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana  na Mkurugenzi wa Shirika la misaada la Uingereza DFID Vel Gnanendran alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kuzungumza na Rais leo (katikati) Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bibi. Dianna Melrose.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na mgeni wake Mkurugenzi wa Shirika la misaada la Uingereza DFID Vel Gnanendran alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
 [Picha na Ikulu.]

RAIS KIKWETE ATEUA MAKATIBU WAKUU WANNE WAPYA

0
0
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete usiku wa Ijumaa, Oktoba 23, 2015, amewateua Makatibu Wakuu wanne wapya wa wizara mbalimbali.
Aidha, Rais Kikwete amewateua Naibu Makatibu Wakuu wapya watano, amewateua Makatibu Tawala wa Mikoa wawili na pia amewahamisha Naibu Makatibu Wakuu wawili.
Kwa mujibu wa uteuzi huo, Rais Kikwete amemteua Ndugu Hab Mkwizu kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma; Profesa Elisante Ole Gabriel kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo; Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na Mhandisi Omari Chambo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini.
Aidha, kwa mujibu uteuzi huo, Rais Kikwete amemteua Mhandisi  Paul M. Masanja kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini; Dkt. Maria Mashingo kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Ndugu Zidikheri  Mgaya Mundeme kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.
Wengine walioteuliwa kuwa Naibu Makatibu Wakuu ni Ndugu Tixon T. Nzunda ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Ndugu Emmanuel Kalobelo ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.
Walioteuliwa kuwa Makatibu Tawala wa Mikoani Ndugu Eliakim Maswi ambaye anakuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara na Mhandisi Madeni Kipande ambaye anakuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi.
Katibu Mkuu ambaye anahamishwa ni Bibi Sihaba Nkinga ambaye anakwenda kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Naibu Makatibu Wakuu wanaohamishwa ni Ndugu John T. Mngodo ambaye anahamishiwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kutoka Wizara ya Uchukuzi na Ndugu Mwamini Juma Malemi ambaye anakwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Wateuliwa hao wote wataapishwa asubuhi ya Jumamosi, Oktoba 24, 2015, Ikulu mjini Dar es Salaam.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
24 Oktoba, 2015



VIJANA WA NCHI MWANACHAMA WA MAZIWA MAKUU KUSHUHUDIA MAMBO YA UCHAGUZI MKUU HAPA NCHINI

0
0
Balozi wa maziwa makuu nchini Kenya, katika wizara ya mambo ya nje, Muburi Muita,MBS  akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya ushiriki wa vijana katika uchaguzi mkuu utakaofanyika kesho Oktoba 25 mwaka huu pamoja na ushiriki wa vijana katika uchaguzi huo. 
Mwenyekiti wa wa kamati ya uchaguzi wa  vijana wa nchi za maziwa makuu ,Adv.Kabyemela Lushagara akitoa maada katika mkutano wa vijana wa nchi mwanachama wa maziwa makuu pamoja na kuzungumza na baadhi ya vijana wa nchi za maziwa makuu leo katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam kuhusiana jinsi democrsia jinsi ilivyokua hapa nchini na ushiriki wa wapiga kura kesho Oktoba 25 mwaka huu.


Baadhi ya vijana walioshiriki mkutano wa vijana wa nchi za maziwa mkuuu wakimsikiliza mtoa mada leo katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam.  
Baadhi ya wadau na vijana wa nchi za mwanachama wa maziwa makuu wakimsikiliza Balozi wa maziwa makuu nchini Kenya, katika wizara ya mambo ya nje, Muburi Muita,MBS  leo wakati akiipongeza Tanzania kuendeleza uchumi pamoja na kushirikiana na nchi mwananchama kuunda uchumi wa nchi Balozi pia alipongeza nchi kwa kukua wa demokrasia 

Balozi wa maziwa makuu nchini Kenya, katika wizara ya mambo ya nje, Muburi Muita,MBS  akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa nchi mwananchama wa maziwa makuu  leo jijini Dar es Salam.

TAMKO LA BARAZA LA WAISLAMU WA TANZANIA(BAKWATA)

0
0

UCHAGUZI UNAOTARAJIWA KUFANYIKA KESHO UTAKUWA HURU, HAKI NA WENYE UTULIVU: DK.SHEIN

0
0


STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

Zanzibar                                                              24.10.2015
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesisitiza kuwa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika kesho utakuwa huru, haki na wenye utulivu na kuwahakikishia washirika wa maendeleo likiwemo Shirika la Misaada la Uingereza (DFID) kuwa Zanzibar itaendea kuwa na amani kwani ndio msingi wa maendeleo.


Dk. Shein aliyasema hayo katika mazungumzo kati yake na Kiongozi wa Shirika la Misaada la Uingereza anayefanya kazi zake nchini Tanzania Mhe. Vel Gnanendran, huko Ikulu mjini Zanzibar.


Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alimueleza kiongozi huyo wa Shirika la DFID ambaye alifuatana na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Mhe. Dianna Melrose kuwa Zanzibar itaendelea kuwa visiwa vya amani na utulivu katika kipindi chote cha uchaguzi mkuu na hata baada ya uchaguzi.


Dk.Shein alisema kuwa hatua za maendeleo zilizofikiwa na Zanzibar sambamba na amani na  utulivu uliopo ndivyo viliyoyapelekea mashirika mbali mbali ya Kimataifa ulimwenguni kuendelea kuiunga mkono Zanzibar likiwemo Shirika la DFID kwa kuthamini na kutambua juhudi zake hizo.


Dk. Shein alimuhakikishia kiongozi huyo wa Shirika hilo kuwa Zanzibar itaendelea kushirikiana na Shirika hilo kwa lengo la kuleta maendeleo endelevu nchini.


Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alisema kuwa juhudi kubwa zimechukuliwa na vyombo vya ulinzi kwa kuendelea kusimamia amani na utulivu pamoja na vyama vya siasa wakati wote wa kampeni hivyo ni matarajio yake kuwa hatua hiyo itaendelezwa hata kwa siku za usoni ikiwemo siku ya kupiga kura hapo kesho.


Aidha, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuwahimiza wawekezaji kutoka nchini Uingereza kuja kuekeza Zanzibar katika sekta mbali mbali za maendeleo ikiwemo sekta ya kilimo pamoja na  utafiti wake.


Sambamba na hayo, Dk. Shein alisisitiza haja ya kuweko mpango maalum wa nafasi za masomo nchini Uingereza kwa vijana wa Zanzibar ikiwa ni pamoja na kupitia Shirika hilo la DFID.


Dk. Shein aliwaeleza viongozi hao kuwa Zanzibar itaendeleza uhusiano na ushirikiano kati yake na Shirika hilo la DFID.


Nae  Kiongozi huyo wa Shirika la DFID Mhe.  Vel Gnanendran alimueleza Dk. Shein kuwa Shirika hilo limeazimia kuiunga mkono Zanzibar kwa kutambua juhudi zake katika sekta za maendeleo.


Alisema kuwa juhudi zilizochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha sekta zake za maendeleo zinahitaji kupongezwa na kuungwa mkono ili zizidi kuimarika.


Aidha, kiongozi huyo alimpongeza Dk. Shein kwa kuendelea kusimamia amani, utulivu na mshikamano hapa Zanzibar na kueleza kuwa hiyo ndio nguzo pekee itakayoendelea kuikuza Zanzibar kiuchumi na kimaendeleo.


Balozi wa Uingereza Mhe. Dianna Melrose kwa upande wake alimuhakikishia Dk. Shein kuwa nchi yake inatambua na inathamini uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu kati ya Zanzibar na Tanzania nzima pamoja na Uingereza uliopo ambao aliahidi kuuendeleza.


Balozi Melrose alimueleza Dk. Shein kuwa wawekezaji wengi wa nchi hiyo wanavutiwa kuja kuekeza Zanzibar kutokana na kuwepo kwa amani na utulivu sambamba na vivutio kadhaa vya utalii.


Kwa upande wa mashirikiano katika sekta ya elimu alisema kuwa juhudi za makusudi zinaendelea kuchukuliwa na zitachukuliwa katika kuhakikisha nafasi za masomo kwa Zanzibar  nchini humo zinaongezeka.

Sambamba na hayo, Balozi huyo alimpongeza Dk. Shein kwa kuisimamia vyema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye mfumo wa Umoja wa Kitaifa ambayo imepata mafanikio makubwa na kuwa kigezo ndani na nje ya bara la Afrika.


Pia, Balozi huyo aliisifu na kuipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Shein kwa kutoa fursa sawa ya kufanya Kampeni zilizokuwa huru na amani kwa vyama vyote hapa nchini.


Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar


Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822

E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

YALIYOJIRI KWENYE MSAFARA WA WAENDESHA BAISKELI KUTOKA MBEYA KWENDA JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Rais wa Chama cha Waendesha Baiskeli Tanzania, Godfrey Jacks Muhagama, ambaye pia ni miongoni mwa waendesha baiskeli kwenye msafara huo ulioanzia Mbeya akitoa maelezo ya namna shughuli hiyo ilivyofanikiwa.
 Mwakilishi wa Norwegian Church Aid nchini Tanzania, Tale Hungnes akiwapongeza waendesha baiskeli mara baada ya kufika Dar es Salaam wakitokea kwenye mpaka wa Malawi na Tanzania, Kasumulo Mbeya.
 
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr. Rashid Rutengwe akisaini madai ya haki ili kuweka imani yake kwa viongozi wa kiserikali ambao watakwenda kwenye mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP21 utakaofanyika desemba mwaka huu huko Paris, Ufaransa.
Wanafunzi wa shule za msingi Wambi na Nyamalala, James Lyimo (kulia) na Vannesa Mgata wakionyesha mti waliokabidhiwa kwaajili ya kupanda katika shule zao
Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Tanzania, Gilbert Mworia akikabidhi mti kwa viongozi wa dini Mufindi, Mkoani Iringa, kutoka kulia ni Imamu wa Msikiti Mkuu wa Mafinga na Mch. Annuai Mwinuka wa KKKT, Jimbo la Mufindi Usharika wa Mafinga, zoezi hilo lililofanyika kwenye shule za Msingi Wambi na Nyamalala zote za Mafinga.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr. Rashid Rutengwe akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waendesha baiskeli na viongozi wa msafara huo
Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Nizar Suleiman akitoa maelezo juu ya msafara wa kampeni ya uhamasishaji juu ya mabadiliko ya tabianchi, baada ya kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwenye shule ya Sekondari Kola Hill.
Waendesha baiskeli wakiwa katika eneo la Ruaha Mbuyuni
Mwakilishi wa Norwegian Church Aid nchini Tanzania, Tale Hungnes akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waendesha baiskeli, walipofika kwenye mji wa Ilula, Mkoani Iringa.
Baadhi ya akina mama wa mji wa Makambako wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa vijana wahamasishaji wa elimu ya mabadiliko ya tabianchi wa YouthCAN Tanzania
Msafara wa waendesha baiskeli ukiingia kwenye mji wa Ilula Mkoani Iringa
Esther Joshua ambaye ni mwanamke pekee kwenye msafara wa kuendesha baiskeli kutoka Mbeya mpaka Arusha, hapa akiwa nje kidogo ya mji wa Mafinga kuelekea Iringa Mjini.
Waendesha baiskeli wakielekea jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Muhongo Rweyemamu akipanda mti kwenye shule ya Sekondari Kola Hill, Mkoani Morogoro ambayo ni sehemu ya kampeni hiyo

Na Dotto Kahindi

Msafara wa Kampeni ya uhamasishaji juu ya mabadiliko ya tabianchi kupitia uendeshaji wa baiskeli ambao ulianza Octoba 17 mwaka huu kwenye mpaka wa Tanzani na Malawi umefika jinini Dar es Salaam ambako utasimama kupisha zoezi zima la uchaguzi mkuu kabla ya kuelekea Namanga Arusha.

Msafara huo ambao umekuwa ukipata mapokezi makubwa kutoka kwa viongozi mbalimbali wa serikali, dini na wananchi kwa ujumla, ukiwa Mkoani Morogoro ulipata mapokezi makubwa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa huo Dr. Rajab Rutengwe.

Mkuu huyo wa mkoa amewapongeza waendesha baiskeli na kuwaita ni mashujaa na mabalozi wazuri wa kuhamasisha jamii kutunza  mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Msafara huo ambao umeanzia Msumbiji kupitia Afrika Kusini Botswana, Zimbabwe, Zambia, Malawi na sasa Tanzania, utafikia kilele chake mjini Nairobi Kenya mwezi novemba mwaka huu.

Dr. Rutengwe amesema kuwa jambo la kutunza mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi ni muhimu na ni jambo la kila mmoja wetu.
Amewakemea viongozi wa serikali wanaoshirikiana na wananchi kuharibu mazingira kwa kukata miti na kuuza mikaa na kuahidi kuwashughulikia baada ya uchaguzi mkuu kumalizika.

Akizungumzia umuhimu wa milima ya Uluguru, Nguu na Ukaguru anasema ni muhimu kwa kuwa ni moja ya vyanzo vya maji ambayo huwanufaisha watu wa mikoa ya Morogoro, Dodoma, Pwani na Dar es Salaam. 

“Sisi watu wa Morogoro tukiwa wabinafsi kwa kuharibu vyanzo vya maji kwa kufanya uharibifu kwenye milima ya Uluguru, Nguu na Ukaguru tutakuwa tunawaua wenzetu wanaotegemea milima hiyo” anasema Dr. Rutengwe

Akitoa taarifa ya msafara huo, Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Nizar Suleiman anasema kuwa lengo la msafara huo ni kujenga uelewa kwa jamii juu ya mabadiliko ya tabianchi kwa kupitia uendeshaji wa baiskeli na kutumia vijana kutoka kwenye taasisi za kidini nchini kufikisha elimu hiyo.

Anasema msafara huo utahusisha pia uchukuaji wa saini za wananchi ili kuweka imani zao kwa viongozi wa kiserikali ambao watakwenda kwenye mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP21 utakaofanyika desemba mwaka huu huko Paris, Ufaransa.

Msafara huo unatarajiwa kuendelea tena novemba 3 mwaka huu, ukitokea jijini Dar es Salaam kuelekea Namanga Mkoani Arusha ambapo utakabidhiwa kwa waendesha baiskeli wa Kenya.

MWANZA YAFUNIKA KATIKA HITIMISHA YA KAMPENI ZA CCM

0
0
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza walifika kuhudhuria uwanja wa CCM kirumba katika hitimisho la Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli akiingia uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati ufungaji wa kampeni.
Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli akisindikizwa kuingia uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati ufungaji wa kampeni.
Mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Mama Samia Suluhu Hassan akisalimia wananchi wakati akiingia ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati ufungaji wa kampeni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati ufungaji wa kampeni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Mgombea Mwenza Mama Samia Suhulu, akipokelewa ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Wanakibajaji nao hawakuwa nyuma.
Chege na Temba wakitoa burudani.
Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimia na Kada wa CCM, Wema Sepetu ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Makada wa CCM, Steve Nyerere na Wema wepetu wakiongea ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Kazi ni Kazi.... Asha bokooooo akionyesha umahili wa kupiga PUSH UPS....
Asha boko katika ubora wake....
Wema Sepetu katika ubora wake.
Rais ni Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea machache mtambulisha ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Ujumbe!
Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli akitoa sera zake kwa wananchi waliofika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati ufungaji wa kampeni.
Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli akiwa na mgombea wa Ubunge wa jimbo la Nyamagana L. Mabula.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwanadi wagombea ubunge wa Mwanza....  Kulia ni mgombea wa Ubunge wa jimbo la Nyamagana L. Mabula na mgombea wa Ubunge wa jimbo la Ilemela Anjelina Mabula.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiburudika na Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli pamoja na wanakibajaji ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.

JAJI MTAAFU LUBUVA AZUNGUMZA KUHUSU UCHAGUZI MKUU 25/10/2015

0
0
Baadhi ya waandishi wa habari  wakimsikiliza   Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) Jaji Mstaafu Damian  Lubuva kuhusu  alipokuwa akizungumzia masuala mbalimbali ya Uchaguzi Mkuu, ikiwemo kusisitiza mwisho wa kampeni za uchaguzi huo kuwa ni leo saa 12: 00 jioni. 
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) Jaji Mstaafu Damian  Lubuva  akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dares Salaam kuhusu masuala mbalimbali  ya Uchaguzi Mkuu, ikiwemo kusisitiza mwisho wa kampeni  za uchaguzi huo kuwa ni leo saa 12: 00 jioni.  
Kulia  ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Emmanuel   Kavishe.

YALIYOJIRI KWENYE MSAFARA WA WAENDESHA BAISKELI KUTOKA MBEYA KWENDA JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Rais wa Chama cha Waendesha Baiskeli Tanzania, Godfrey Jacks Muhagama, ambaye pia ni miongoni mwa waendesha baiskeli kwenye msafara huo ulioanzia Mbeya akitoa maelezo ya namna shughuli hiyo ilivyofanikiwa.
 Mwakilishi wa Norwegian Church Aid nchini Tanzania, Tale Hungnes akiwapongeza waendesha baiskeli mara baada ya kufika Dar es Salaam wakitokea kwenye mpaka wa Malawi na Tanzania, Kasumulo Mbeya.
 
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr. Rashid Rutengwe akisaini madai ya haki ili kuweka imani yake kwa viongozi wa kiserikali ambao watakwenda kwenye mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP21 utakaofanyika desemba mwaka huu huko Paris, Ufaransa.
Wanafunzi wa shule za msingi Wambi na Nyamalala, James Lyimo (kulia) na Vannesa Mgata wakionyesha mti waliokabidhiwa kwaajili ya kupanda katika shule zao
Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Tanzania, Gilbert Mworia akikabidhi mti kwa viongozi wa dini Mufindi, Mkoani Iringa, kutoka kulia ni Imamu wa Msikiti Mkuu wa Mafinga na Mch. Annuai Mwinuka wa KKKT, Jimbo la Mufindi Usharika wa Mafinga, zoezi hilo lililofanyika kwenye shule za Msingi Wambi na Nyamalala zote za Mafinga.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr. Rashid Rutengwe akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waendesha baiskeli na viongozi wa msafara huo
Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Nizar Suleiman akitoa maelezo juu ya msafara wa kampeni ya uhamasishaji juu ya mabadiliko ya tabianchi, baada ya kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwenye shule ya Sekondari Kola Hill.
Waendesha baiskeli wakiwa katika eneo la Ruaha Mbuyuni
Mwakilishi wa Norwegian Church Aid nchini Tanzania, Tale Hungnes akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waendesha baiskeli, walipofika kwenye mji wa Ilula, Mkoani Iringa.
Baadhi ya akina mama wa mji wa Makambako wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa vijana wahamasishaji wa elimu ya mabadiliko ya tabianchi wa YouthCAN Tanzania
Msafara wa waendesha baiskeli ukiingia kwenye mji wa Ilula Mkoani Iringa
Esther Joshua ambaye ni mwanamke pekee kwenye msafara wa kuendesha baiskeli kutoka Mbeya mpaka Arusha, hapa akiwa nje kidogo ya mji wa Mafinga kuelekea Iringa Mjini.
Waendesha baiskeli wakielekea jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Muhongo Rweyemamu akipanda mti kwenye shule ya Sekondari Kola Hill, Mkoani Morogoro ambayo ni sehemu ya kampeni hiyo

Na Dotto Kahindi
Msafara wa Kampeni ya uhamasishaji juu ya mabadiliko ya tabianchi kupitia uendeshaji wa baiskeli ambao ulianza Octoba 17 mwaka huu kwenye mpaka wa Tanzani na Malawi umefika jinini Dar es Salaam ambako utasimama kupisha zoezi zima la uchaguzi mkuu kabla ya kuelekea Namanga Arusha.

Msafara huo ambao umekuwa ukipata mapokezi makubwa kutoka kwa viongozi mbalimbali wa serikali, dini na wananchi kwa ujumla, ukiwa Mkoani Morogoro ulipata mapokezi makubwa kutoka kwa Mkuu wa Mkoa huo Dr. Rajab Rutengwe.

Mkuu huyo wa mkoa amewapongeza waendesha baiskeli na kuwaita ni mashujaa na mabalozi wazuri wa kuhamasisha jamii kutunza  mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Msafara huo ambao umeanzia Msumbiji kupitia Afrika Kusini Botswana, Zimbabwe, Zambia, Malawi na sasa Tanzania, utafikia kilele chake mjini Nairobi Kenya mwezi novemba mwaka huu.

Dr. Rutengwe amesema kuwa jambo la kutunza mazingira ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi ni muhimu na ni jambo la kila mmoja wetu.
Amewakemea viongozi wa serikali wanaoshirikiana na wananchi kuharibu mazingira kwa kukata miti na kuuza mikaa na kuahidi kuwashughulikia baada ya uchaguzi mkuu kumalizika.

Akizungumzia umuhimu wa milima ya Uluguru, Nguu na Ukaguru anasema ni muhimu kwa kuwa ni moja ya vyanzo vya maji ambayo huwanufaisha watu wa mikoa ya Morogoro, Dodoma, Pwani na Dar es Salaam. 

“Sisi watu wa Morogoro tukiwa wabinafsi kwa kuharibu vyanzo vya maji kwa kufanya uharibifu kwenye milima ya Uluguru, Nguu na Ukaguru tutakuwa tunawaua wenzetu wanaotegemea milima hiyo” anasema Dr. Rutengwe

Akitoa taarifa ya msafara huo, Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Nizar Suleiman anasema kuwa lengo la msafara huo ni kujenga uelewa kwa jamii juu ya mabadiliko ya tabianchi kwa kupitia uendeshaji wa baiskeli na kutumia vijana kutoka kwenye taasisi za kidini nchini kufikisha elimu hiyo.

Anasema msafara huo utahusisha pia uchukuaji wa saini za wananchi ili kuweka imani zao kwa viongozi wa kiserikali ambao watakwenda kwenye mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP21 utakaofanyika desemba mwaka huu huko Paris, Ufaransa.

Msafara huo unatarajiwa kuendelea tena novemba 3 mwaka huu, ukitokea jijini Dar es Salaam kuelekea Namanga Mkoani Arusha ambapo utakabidhiwa kwa waendesha baiskeli wa Kenya.

CCM YATIKISA JIJI LA MWANZA,YAFUNGA KAMPENI ZAKE KWA KISHINDO

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni. 
 Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza waliojitokeza kushudua kilelel cha hitimisho la kampeni za chama cha Mapinduzi CCM katika uwanja wa CCM kirumba.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea machache mtambulisha ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akimnadi Mgombea Urais kupitia CCM Dk.  John Pombe Magufuli wa pili kutoka kulia, Mgombea Mwenza Mama Samia Hassan Suluhu na wagombea ubunge wa majimbo ya Ilemela Anjela Mabula wa kwanza kushoto  na Stanslaus Mabula Nyamagana wa tatu kutoka kushoto
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akimnadi Mgombea Urais kupitia CCM Dk.  John Pombe Magufuli wa pili kutoka kulia,na wagombea ubunge wa majimbo ya Ilemela Anjela Mabula wa kwanza kushoto  na Stanslaus Mabula Nyamagana wa tatu kutoka kushoto.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwanadi wagombea ubunge wa Mwanza.Kulia ni mgombea wa Ubunge wa jimbo la Nyamagana Stanslaus Mabula na mgombea wa Ubunge wa jimbo la Ilemela Anjela Mabula.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiburudika na Mgombea wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Dk. Magufuli pamoja na wanakibajaji ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati wa hitimisho la kampeni.

Umati wa maelfu ya wananchi wa jiji la Mwanza wakifuatilia kufungwa kampeni za chama cha Mapinduzi CCM katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

KUDUMISHA AMANI WAKATI WA UCHAGUZI

0
0
WATANZANIA wametakiwa  kuendelea kudumisha amani hasa kipindi  cha uchaguzi kwani bado nchi yetu inasifika kwa amani dunia kote
kauli hiyo imetolewa na  mwanaharakati wa amani Mhonda Joseph wakati akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es Salaam.


Mhonda amesema wananchi wahakikishe  amani inakuwepo  na hata  wageni wanaoishi hapa  kutokana na historia ya miaka ya nyuma  ya hapa nchini kuwa ya amani.

Aidha  amewataka watanzania wasikubali  baadhi ya watu  wachache kuja kuchochea utovu wa amani na wakumbuke amani ikipotea ni vigumu kuirudisha pindi itakapotoweka.


lakini pia Mhonda ameeleza kuwa  hatua tuliyofikia ya kuwa na vyama vingi  ni moja ya maendeleo  ni mhimu kuhakikisha  tunachagua kiongozi bora  atakao watumikia watanzania wote kutokana na hali ya ugumu wa maisha kwa  sasa.




hata hivyo amewataka mawakala kuhakikisha wanafanya kazi zao bila kukubali kufanya vurugu pindi wanaposimamia wakati wa kuhesabu
Viewing all 46193 articles
Browse latest View live




Latest Images