Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

WIMBO MPYA: ROMA - VIVA ROMA VIVA


MIKOPO KWA WAJASIRIAMALI WA KATI NA WAFANYAKAZI‏‎

$
0
0
Je umekwama kifedha?,Hujui wapi pa kwenda? Je unahitaji kutimiza ndoto na malengo yako? usihangaike
Kampuni ya mikopo ya wezesha mzawa microfinance ltd inatoa mikopo kwa wajasiriamali wa kati na wafanyakazi wa sekta zote ikiwemo biashara,viwanda na ufugaji.

Kiwango cha mkopo kinaanzia 500,000/= hadi 50,000,000/=

Mkopo unatolewa ndani ya masaa 24
Sifa za mkopaji
.uwe ni mtanzania mwenye umri usiopungua miaka 18

.uwe n uzoefu wa biashara usiopungua

.uwe na namba ya utambulisho wa kodi (TIN)

.Uwe na mkataba wa kazi (kwa mfanyakazi)

.Uwe umeajiriwa na kampuni inayotambulika na kusajiriwa na serikali(kwa mfanyakazi)

Ofisi zetu zipo Bamaga ,jengo la Global publishers.Tupigie kwa simu namba

0715 620824

Nyote mnakaribishwa

MHE.ENG.HAMAD MASAUNI AFUNGUA MAFUNZO YA VIJANA WA TUEPO KUWAJENGEA UWEZO VIJANA KUJIAJIRI WENYEWE

$
0
0
Mmoja wa Kijana Wasio na Ajira Tanzania akisoma Quran wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Siku mbili ya kuwajengea Uwezo Vijana wa Jumuiya ya Watanzania Wasuio na Ajira Tanzania (TUEPO) yanayofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la Zamani Kikwajuni Zanzibar.
Katibu wa Jumuiya ya TUEPO Muzna Ibarahim akitowa maelezo ya mafunzo hayo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin Mhe Hamad Masauni kuyafungua mafunzo hayo ya siku mbili yanayowajumuisha Vijana wasio na Ajira kuwajengea Uwezo wa kujiajiri.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe Eng Hamad Masauni akifungua m,afunzo ya Vijana Wasio na Ajira yalioandaliwa na Jumuiya ya Watanzania Wasio na Ajira Tanzania (TUEPO) mafunzo hayo yanafanyika katika ukmbi wa zamani wa baraza la wawakilishi kikwajuni Zanzibar.

 
Mhe Eng Hamad Masauni akitowa nasaha zake kwa Vijana wanaohudhuria mafunzo ya siku mbili ya Kuwajengea Uwezo wa Kujiajiri yalioandaliwa na Jumuiya ya Watanzania Wasio na Ajira Tanzania 
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Mhe Eng, Hamad Masauni wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Vijana washiriki katika mafunzo ya Vijana Wasio na Ajira wakifuatilia ufunguzi wa mafunzo hayo uliofanywa na Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar Mhe Eng. Hamad Masauni. mafunzo hayo yameandaliwa na Jumuiya ya Watanzania Wasio na Ajira Tanzania.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Wasio na Ajira Tanzania Mwalim Ussi akitowa maelezo ya mafunzo hayo wakati wa ufunguzi na kuelezea malengo ya Jumuiya hiyo kwa Vijana kutowa mafunzo ili kuweza kujiajiri katika sekta mbalimbali Tanzania.
Mkufunzi wa Mafunzo ya Jumuiya ya Watanzania Wasio na Ajira Ndg Abel Kipapi, akitowa Mada kuhusiana na Ubunifu katika Kazi kwa Vijana Kujiajiri wakati wa mafunzo hayo ya Siku Mbili yaliowashirikisha Vijana Wasio na Ajira Tanzania kuweza kujiajiri wenyewe.  
Baadhi ya Vijana Wasio na Ajira wakifuatilia Mada iliokuwa ikiwasilishwa wakati wa mafunzo hayo

Vijana wakiwa makini wakifuatilia mafunzo hayo ili kuweza kupata ujuzi wa kujiajiri wenyewe baada ya kupata mafunzo hayo yaliotolewa na Jumuiya ya Watanzania Wasio na Ajira Tanzania.
  Mhe Eng Hamad Masauni akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Mafunzo hayo ya TUEPO
Mhe Hamad Masauni akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo baada ya ufunguzi wake. Picha na Zanzinews.com 

MGOMBEA MWENZA WA UKAWA JUMA DUNI HAJI AHUTUBIA MKUTANO WA KAMPENI IRINGA VIJIJINI

$
0
0
 Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji na akihutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Isimani Iringa vijijini.Isimani Iringa vijijini, (Picha na Francis Dande)
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji na akihutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Isimani Iringa vijijini.Isimani Iringa vijijini,
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji akiwa na mgombea ubunge jimbo la Isimani Iringa vijijini, Patrick Ole Sosopi.
Wasanii wa kikundi cha ngom za asili cha Kitimtim kutoka mkoani Iringa kikitumbuiza wakati wa mkutano wa kampeni uliohutubiwa na mgombea mwenza wa Ukawa, kupitia Chadema, Juma Duni Haji (hayupo pichani)  uliofanyika jimbo la Isimani Iringa vijijini.
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji na Makamu Mwenyekiti wa Bavicha Taifa ambaye pia ni mgombea ubunge jimbo la Isimani Iringa vijijini, Patrick Ole Sosopi wakiwasalimia wananchi waliofika katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Kimandi Iringa vijijini.
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji na akimtambulisha kwa wapiga kura mgombea ubunge jimbo la Isimani Iringa vijijini, Patrick Ole Sosopi.
 Wananchi wakifuatilia mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Isimani mkoani Iringa.
Mgombea ubunge jimbo la Isimani Iringa vijijini kupitia Ukawa, Patrick Ole Sosopi akihutubia mkutano wa kampeni.

SERIKALI YAZINDUA UJENZI WA KITUO KIKUBWA CHA TIBA YA MOYO NCHINI

$
0
0
 Mkurugenzi wa Elimu ya juu kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi Stadi, Prof. Sylivia Temu akizungumza wakati wa uzinduzi mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa chini ya usimamizi wa  Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS).
 Mkurugenzi wa Elimu ya juu kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi Stadi, Prof. Sylivia Temu (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa chuoChuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS), wawakilishi kutokakutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya afya baada yauzinduzi mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa chini ya usimamizi wa  (MUHAS).
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS), Prof Ephata Kaaya akizungumza wakati wa uzinduzi mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa chini ya usimamizi wa  (MUHAS).
Muwakilishi kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika Bw. Demissie Dejene akizungumza wakati wa uzinduzi mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa chini ya usimamizi wa  Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS)
Na Mwandishi wetu,
SERIKALI imezindua mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana kwa niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi Bw. Shukuru Kawambwa, Mkurugenzi wa Elimu ya juu nchini, Prof. Sylivia Temu alisema mradi huo unaotekelezwa na serikali kwa ushirikiano na benki ya maendeleo ya Afrika  ni mojawapo ya miradi minne ya afya inayotekelezwa kwenye ukanda wa afrika mashariki ikilenga kutatua changamoto mbalimbali za kiafya.
 
“Kila nchi ya Afrika Mashariki ina mradi wa aina yake kwenye sekta hii muhimu na kwa upande wetu sisi umejikita katika kukabiliana na magonjwa ya moyo na utakuwa chini ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) na utakwenda sambamba na ujenzi wa kampasi mpya ya chuo hicho unaondelea huko eneo la Mloganzila hapa jijini Dar es Salaam,’’ alibainisha.
Akizungumzia faida za mradi huo Prof Temu alisema utasaidia kupunguza vifo vitokanavyo na magonjwa ya moyo hapa nchini sambamba na kupunguza gharama zinazolikabili taifa kwa sasa kutokana na kusafirisha idadi kubwa ya wagonjwa wa moyo kwa ajili ya kutafutaa matibabu nje ya nchi.
“Lakini pia kupitia kituo hiki kitakacho kuwa kikubwa kabisa hapa Afrika Mashariki tunarajia kwamba tafiti nyingi za masuala ya kiafya hasa kwenye eneo hili la magonjwa ya moyo zitakuwa zikifanyika hapa nchini na pia kupitia MUHAS tuzalisha wataalamu wengi wa magonjwa hayo kwa manufaa ya vyuo vingine ndani na nje ya nchi,’’ aliongeza.
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha MUHAS, Prof Ephata Kaaya alisema chuo chake kimejipanga kutekeleza mradi huo mkubwa utakaotekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza utahusisha mafunzo pamoja na maandalizi ya vifaa huku awamu ya pili ikuhusisha ujenzi kamili wa kituo hicho.
“Tafsiri ya uzinduzi huu ni kwamba MUHAS tunapewa heshima ya kusimamia kituo hiki muhimu na kikubwa kabisa kwa Afrika masshariki na hakitahudumia watanzania pekee bali nchi zote wanachama kutokana na ukweli kwamba na nchi nyingine pia nazo zinaendesha miradi yenye hadhi kama hii ila katika Nyanja tofauti za kiafya,’’ aliongeza
Akizungumza kwenye uzinduzi huo pia  Meneja Miradi ya Jamii kutoka benki ya Maendeleo ya Afrika Bw. Hamis Simba alizitaja baadhi ya sababu zilisababisha benki hiyo kufadhiri mradi kuwa ni pamoja na wao kuvutiwa na mikakati ya Tanzania na nchi za Afrika Mashariki kwa ujumla katika kukabiliana na magonjwa ya moyo.

JUKWAA LA SANAA LAFANA, MSANII MKONGWE AISHIYE MAREKANI SALMA MOSHI AWALIPIA WASANII BIMA YA AFYA

$
0
0

Jukwaa La Sanaa la BASATA wiki hii lilipata wazungumzaji wa aina yake na kulifanya kuwa jukwaa lililochangamka na kuwa na mazungumzo ya zaidi ya masaa matano. Wasanii takriban 70 walikaa wakichambua maada mbalimbali kuhusu mustakhabari wa sanaa katika nchi yetu. Jambo ambalo liliingiza changamoto katika jukwaa hili, ni kuweko katika meza kuu wasanii wawili ambao walianza sanaa nchini na hatimae kuhamia ughaibuni ambako ndiko wanaishi kwa sasa.

Wasanii Salma Moshi aliyekuwa akijulikana kama Salma Nyoka, msanii wa kwanza wa kike kuchezea nyoka katika jukwaa, na ambaye alikuwa kiongozi wa vikundi vilivyotamba kama DDC Kibisa Cultural Troupe Super Mama Cultural Troupe na Ujamaa Cultural Troupe, na Abbu Omar, mwanamuziki aliyewahi kupigia bendi kama Urafiki na UDA Jazz ambae kwanza alihamia Kenya na kupiga na kurekodi na makundi kama Simba wa Nyika na Les Wanyika na pia kurekodi album kadhaa akiwa na kundi lake ambaye hatimae alihamia Japan ambako amekuwa akiishi kwa kupiga muziki na akiwa na waTanzania wengine kama Lista na Fresh Jumbe.

Mazungumzo yaligusia nyanja mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kuwa na mikataba kabla ya kazi, kuboresha kazi ili kuweza kuuza nje, namna ya kujitambulisha  duniani kwa kuwa na websites na blogs, na pia serikali kubadilika na kuweko mfumo wa uongozi wa sanaa kuanzia ngazi ya wilaya hadi Taifa. Katika mkutano huo, John Kitime Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki aliongelea fursa ya Bima ya Afya kwa wasanii, ambapo Salma Moshi alijitolea kuwalipia nusu ya ada wasanii wanne, na kumlipia bima kamili Mzee Kassim Mapili ambaye kwa sasa anasumbuliwa na moyo na figo. Abbu Omar pia aliamua kulipia Bima yake na kueleza kuwa katika nchi ya Japan ni lazima kila mwananchi kuwa na Bima ya Afya, kwani ugonjwa hauji kwa taarifa na matibabu ni gharama kubwa.

Mkutano huo ulianza saa tano na kulazimishwa kusimamishwa saa kumi, kwani wasanii bado walikuwa na mengi ya kuwauliza wasanii hawa nguli walioweza kuendeleza maisha ughaibuni kupitia sanaa

Salma Moshi na Mzee Kassim Mapili
Abbu Omari mwanamuziki aishiye Japan akitoa mada. Kulia ni msanii mkongwe aishiye Marekani Salma Moshi aliyepata kujizolea umaarufu kwa kucheza na nyoka miaka ya nyuma

Picha ya pamoja

Salma Moshi akiwa na baadhi ya wasanii aliowalipia sehemu ya Bima ya Afya IMETAYARISHWA NA www.johnkitime.co.tz
Kwa kusoma zaidi BOFYA HAPA

DAWASCO SACCOS YAZINDULIWA RASMI

$
0
0
 SHIRIKA la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO), imezindua rasmi mfuko wa akiba na mikopo (Saccos) kwaajili ya wafanyakazi wa shirika hilo katika harakati za kujikomboa kiuchumi na kuimarisha umoja miongoni mwao.

Akiongea na wafanyakazi katika uzinduzi huo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Mhandisi Cyprian Luhemeja amewahimiza wafanyakazi kuitumia Saccos hiyo kujikomboa kiuchumi na kuondokana na utozwaji mkubwa wa riba kutoka kwa baadhi ya taasisi za fedha, hali inayowaumiza watumishi wengi nchini.

Uanzishwaji wa mfuko huo umelenga kuwasaidia wafanyakazi kutatua matatizo ya haraka yanayojitokeza ndani na nje ya maisha ya kazi na kuiweka Saccos hiyo kama sehemu ya Dawasco kujipanua zaidi katika kujali maslai ya wafanyakazi wake.

Saccos ya Dawasco imezinduliwa ikiwa na mtaji wa kuanzia wa Tsh Milioni 95 na jumla ya wanachama736 huku Ndugu Ramadhani Mtindasi akichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Saccos hiyo na nafasi ya Makamu Mwenyekiti ikienda kwa Erasto Emmanuel.

Mara baada ya uchaguzi huo, viongozi hao wamehaidi kuleta mapinduzi na mabadiliko ya uendeshaji wa mfuko huo kwa kuhakikisha unatoa unafuu kwa kila mwanachama na kuweka masharti rafiki ili kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.

MEMORIAL OF LATE PETER INNOCENT MWOMBELA


NGUMI KUPIGWA CHANIKA SEPTEMBA 26

$
0
0
Na Mwandishi Wetu

BONDIA Said Mbelwa anatarajia kupanda uringoni kwa mara nyingine tena kugombania mkanda wa taifa wa chama cha ngumi za kulipwa PST dhidi ya bondia George Dimoso mpambano .
Mpambano utakaofanyika Septemba 26 katika ukumbi wa Butihama Villa Club uliopo chanika mpambano huo wa raundi kumi ulioratibiwa na 
Kocha wa kimataifa nchini Rajabu Mhamila 'Super D' utakuwa ni wa kumaliza ubishi baada ya mpambano wa kwanza Dimoso kudundwa kwa point

Super D aliongeza kuwa siku iyo pia kutakuwa na mipambano mingine mikali itakayowakutanisha mabondia mbalimbali nchini ambapo 

bondia Seleman Zugo atapambana na Abdallah Ruwanje na Adam Ngange atakabiliana na Shabani Mtengela na Said Uwezo atapambana na Hassan Mgosi uku Hamza Mchanjo ataoneshana kazi na Ally Maiyo mipambano yote ya utangulizi ni ya raindi sita

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi
pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha

KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI ATEMBELEA KAMBI YA WAKIMBIZI NYARUGUSU.

$
0
0
 Mkurugenzi  wa  Idara  ya Wakimbizi  kutoka  Wizara    ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke (kushoto) akizungumza  na watumishi wa mashirika  mbalimbali yaliyoko katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kulia) aliyetembelea kambi hiyo jana.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kulia), akizungumza na watumishi mbalimbali (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kutembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Kambi hiyo inahifadhi wakimbizi  kutoka nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.
 
 Daktari wa Hospitali ya Kambi ya Wakimbizi ya  Nyarugusu, Florence Mshana(aliyeshika karatasi), akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(kushoto),  alipotembelea hospitali hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Kambi hiyo inahifadhi wakimbizi kutoka nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.
 Mkuu wa Ofisi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) Kasulu, Amah Assiama-Hillgartner( kushoto),  akitoa maelezo kwa Katibu  Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani,  Mbarak Abdulwakil(katikati),  aliyetembelea hospitali  hospitali hiyo wakati wa ziara yake katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (katikati), akiongozana na Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu (B), Fredrick Nisajile (kulia) na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR) Ofisi ya Kasulu, Amah Assiama –Hillgartner (kushoto) wakati wa ziara ya Katibu Mkuu kambini hapo jana. Kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma inahifadhi wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Burundi.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwaki l(katikati), akiongozana na Mkuu wa Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu (B), Fredrick Nisajile (kulia) na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR) ofisi ya Kasulu, Amah Assiama –Hillgartner (kushoto) wakati wa ziara ya Katibu Mkuu katika  makazi ya wakimbizi  yaliyopo Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil, akimsikiliza mmoja wa maofisa wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) alipotembelea ndani ya mahema wanakoishi wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI, WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

BEI YA MADAFU HII LEO

TASWA KUTOA TUZO KWA RAIS KIKWETE PAMOJA NA WANAMICHEZO WANAOFANYA VIZURI

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kitatoa tuzo kwa Rais Jakaya Kikwete pamoja na wanamichezo 10 waliofanya vizuri zaidi katika miaka 10 akiwa Rais wa Tanzania.
 
Tukio hilo ambalo pia litahudhuriwa na Rais Kikwete, litafanyika Oktoba 8, mwaka huu ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam likiwa na lengo la wanamichezo kumuaga Rais Jakaya Kikwete.
 
TASWA itakabidhi tuzo maalum kwa Rais ikiwa ni kuthamini mchango wake kwa maendeleo ya michezo wakati wa miaka 10 ya uongozi wake na imebariki tukio hilo kama  ‘JK na Wanamichezo’.
 
Licha ya kutoa tuzo kwa Rais na wanamichezo 10 waliofanya vizuri zaidi, pia TASWA itatoa vyeti maalum kwa kampuni mbalimbali zilizosaidia kwa kiasi kikubwa kudhamini michezo katika miaka 10 ya Rais Kikwete.
 
Maandalizi muhimu yamekamilika kuhusiana na tukio hilo, ambapo wawakilishi kutoka vyama vyote vya michezo hapa nchini pamoja na wanamichezo wataalikwa kuhudhuria tukio hilo la kihistoria.
 
TASWA inamshukuru Rais Kikwete kwa kukubali kujumuika nasi siku hiyo ili kuagana na wanamichezo, ambao wameshuhudia mambo mazuri akiwafanyia katika uongozi wake, ambao utafikia tamati baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
Pia TASWA inaishukuru Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa ushirikiano mkubwa iliotoa kuhakikisha tukio hilo linafanikiwa.
 
 
Tayari wadhamini mbalimbali wamejitokeza kusaidia na tunaomba wengine watuunge mkono, ambapo Jumanne Oktoba 15, TASWA itafanya mkutano na waandishi wa habari kutangaza mdhamini mshiriki mmoja, mkutano utakaofanyika ukumbi wa City Sports Lounge, Dar es Salaam.
 
TASWA imeona kuna haja ya wanamichezo kuagana na Rais Kikwete na kumpa tuzo kutokana na masuala mbalimbali aliyofanya kwa miaka yake 10 katika kusaidia kukuza michezo na sanaa hapa nchini.
 
Baadhi ya mambo hayo ni serikali yake ilivyolipia  makocha wa michezo ya soka, netiboli na ngumi na pia serikali ilipeleka wanariadha wetu China, Ethiopia na New Zealand kwa maandalizi ya mashindano ya kimataifa.
Pia tutamkumbuka Rais Kikwete kwa uamuzi wa kurejesha michezo shuleni pamoja na mashindano ya michezo kwa shule za msingi na sekondari (UMISHUMTA na UMISETA). 
 
Yapo mambo mengi ambayo tukiyataja yote aliyofanya kuhusu michezo yatachukua nafasi kubwa, hivyo tuna kila sababu wanamichezo kujitokeza na kuagana na Rais wetu.
Ahsanteni,
Juma Pinto
Mwenyekitii TASWA
11/09/2015.

TANZANITE YAING’ARISHA TANZANIA KATIKA MAONESHO YA VITO BANKOK

$
0
0
 Wanunuzi wa madini wakikagua madini ya vito kutoka kwa mfanyabiashara wa madini wa Tanzania katika banda la Tanzania kwenye maonesho kimataifa ya 56 ya Madini ya vito na usonara yanayofanyika mjini Bankok, Thailand.
 
 Ofisa kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA), Bi. Stella akimpatia maelezo mmoja kati ya wanunuzi wa madini ya vito waliofika katika banda la Tanzania kutaka maelezo ya jinsi ya kuweza kununua madini hayo ya vito yanayopatikana Tanzania.
 Picha ya pamoja kati ya ujumbe kutoka Wizara ya Nishati na Madini ya Tanzania na maofisa waandamizi wanaosimamia maonesho ya kimataifa ya Madini ya vito mara baada ya ufunguzi rasmi kufanyika jijini Bangkok, Thailand.
 Wanunuzi wa Madini ya vito waliofika katika banda la Tanzania wakipata maelezo kutoka kwa maofisa wa Wizara ya Nishati na Madini waliopo kwenye banda la Tanzania.
Wanunuzi mbalimbali wa madini ya vito waliofika katika banda la Tanzania wakijadiliana namna ya kununua madini ya vito kutoka kwa Wafanyabiashara wa Tanzania.

TRENI YA ABIRIA YA LEO YAAHIRISHWA HADI KESHO SEPTEMBA 12, 2015 SAA 11 JIONI!

$
0
0
KAMPUNI YA RELI TANZANIA
TAARIFA  KWA VYOMBO VYA HABARI YA  KUAHIRISHA SAFARI YA TRENI KWENDA  BARA  LEO IJUMAA SEPTEMBA 11, 2015, HADI KESHO JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2015  SAA  11 JIONI!
  
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unasikitika kuwataarifu  abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa kutokana na ajali ya treni ya mizigo iliyotokea kati ya Ngerengere na Kinonko jana mkoa wa  Morogoro , safari ya  treni ya abiria kwenda Bara  iliopangwa kuondoka  leo saa 11 jioni imeahirishwa hadi kesho Jumamosi Septemba 12, 2015  saa 11 jioni.
Mafundi wa TRL wako katika eneo  la ajali tokea jana wakifanya kazi kwa lengo la  kuhakikisha njia inafunguliwa kwa wakati ili huduma ya  treni za kampuni zirejeea kama kawaida mapema hapo kesho.
Uongozi wa TRL unawaomba radhi wale wote watakaopatwa na usumbufu wowote utakaojitokeza.
Atakaye soma taarifa  hii amwarifu na mwenziwe!

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Elias Mshana
TRL Makao Makuu,
Dar es Salaam.
Septemba 11, 2015

RUKSA WACHIMBAJI WADOGO KUMILIKI LESENI KADRI WAWEZAVYO

$
0
0
 Ofisa Madini Mkazi wa Kahama, Bibi Sophia Omar, akifungua mafunzo kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini kuhusu matumizi ya huduma mpya ya utoaji wa leseni za madini kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yamefanyika leo Septemba 11, 2015 mjini Kahama ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo nchi nzima.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Wadogo wa Madini Mkoani Shinyanga (SHIREMA), Bibi Bahati Kalekwa akitoa neno la shukrani kwa Wizara ya Nishati na Madini kuandaa na kuendesha mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini kote kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao. Wilayani Kahama, mafunzo hayo yamefanyika leo, Septemba 11, 2015.
 Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni, Wizara ya Nishati na Madini, Juma Masoud akiwasilisha mada kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni wilayani Kahama, kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao. Semina hiyo imefanyika Septemba 11, 2015 mjini Kahama ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara husika kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini kote.

 
Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni cha Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Nuru Shabani, akiwasilisha mada kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni wilayani Kahama, kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao. Semina hiyo imefanyika Septemba 11, 2015 mjini Kahama ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara husika kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini kote.

Na Veronica Simba - Kahama
Serikali imesema wachimbaji wadogo wa madini wanaruhusiwa kumiliki idadi yoyote ya leseni za madini ilimradi waweze kuzifanyia kazi.

Hayo yamesemwa leo Septemba 11, 2015 mjini Kahama na Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni, Mhandisi Nuru Shabani wakati akiwasilisha mada kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao, wakati wa semina iliyofanyika mjini humo.

“Mchimbaji mdogo anaruhusiwa kumiliki idadi yoyote ya leseni anazoweza kumudu kuzifanyia kazi. Kwa upande wa wachimbaji wakubwa, wao wanaruhusiwa kumiliki leseni zisizozidi 20 lakini pia sheria inawataka wawe na uwezo wa kuzifanyia kazi,” amesema Mhandisi Shabani.

Mhandisi Shabani ametoa ufafanuzi huo kufuatia swali lililoulizwa na mmoja wa washiriki wa semina hiyo, ambaye alitaka kufahamu idadi ya leseni anazopaswa kumiliki mchimbaji mdogo wa madini.

Akifafanua zaidi kuhusu umuhimu wa wamiliki wa leseni kuzifanyia kazi, Mhandisi Shabani amesema, kwa yeyote anayemiliki leseni na kuliacha eneo husika pasipo kulifanyia kazi, sheria inaelekeza kuwa mtu huyo anyang’anywe leseni yake.

Amesema, mfumo mpya wa utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao umeweka mazingira wezeshi kwa mmiliki wa leseni ambaye hafanyii kazi eneo lake, kutambulika kwa urahisi na hivyo hakuna namna ambayo mhusika anaweza kufanya udanganyifu kwa Serikali kwa kuhodhi eneo pasipo kulifanyia kazi.

Wizara ya Nishati na Madini ilizindua mfumo wa kutoa huduma za leseni kwa njia ya mtandao mapema mwezi Juni mwaka huu mjini Dodoma ili kutoa huduma za haraka, kuongeza uwazi na kumuwezesha mteja kusimamia leseni zake mwenyewe.

Ni kwa kuzingatia umuhimu wa matumizi ya mfumo huo mpya kwa wadau wa sekta ya madini nchini, Wizara kupitia Kitengo cha Usimamizi wa Leseni inaendesha zoezi nchi nzima kuwaelimisha wadau hao namna mfumo huo unavyofanya kazi.

PPF YATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI, SHULE YA MSINGI YA JESHI LA WOKOVU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, (kushoto), na Afisa wa Fedha Mwandamizi wa Mfuko huo, Angel Mukasa, (kulia), na Mfanyakazi mwingine wa Mfuko huo, Omari Bundile, (wapili kushoto), wakigawa mafuta maalum yanayotumiwa na watu wenye ulemavu wa ngozi, pamoja na sare za shule na viatu kwa wanafunzi hawa wenye ulemavu wa ngozi wa shule ya msingi ya Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam leo Septemba 11, 2015. Katika kutekeleza sera ya mfuko ya kusaidia jamii, PPF, imetoa vifaa mbalimbali ikiwemo, sare za snhule, viatu na mafuta hayo maalum, Meneja Uhusiano wa Mfuko huo Lulu Mengele aliwaambia waandishi wa habari. (Picha na K-VIS MEDIA/Khalfan Said)

 Latifa Musa,(kulia), akitoa shukrani kjwa niaba ya wenzake baada ya watoto wenye ulemavu wa ngozi wa shule ya msingi ya Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam, kupatiwa msaada na Mfuko wa Pensheni wa PPF

 Watoto wenye ulemavu wa ngozi kwenye shule ya msingi ya Jeshi la Wokovu, Kurasini jijini Dar es Salaam, wakiwa kwenye hafla fupi ya kukabidhiwa msaada kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF, shuleni hap oleo Ijumaa Septemba 11, 2015

Watoto wenye ulemavu wa ngozi, wakiteta jambo, baada ya kupatiwa msaada wa vifaa yakiwemo mafuta maalum yanayotumiwa na watu wenye ulemavu wa ngozi
 Picha ya pamoja ya maafisa wa PPF, Walimu na wanafunzi wa shule ya msingi ya Jeshi la Wokovu
 Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi ya Jeshi la Wokovu, Flora Millinga, akizungumza kwenye hafla hiyo
 Lulu akiwa na baadhi ya watoto
 Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, akizungumza na watoto hao wakati wa kutoa msaada wa vitu mbalimbali Septemba 11, 2015

 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Janet Ezekiel, (kulia), akizungumza jambo na baadhi ya watoto hao
 Kikundi cha Kwaya kikitoa burudani
Angel Mukasa, akizungumza na baadhi ya watoto

UZINDUZI WA MFULULIZO WA VIPINDI VYA MAMA MISITU KUHUSU UZALISHAJI WA MKAA ENDELEVU WAFANYIKA NEW AFRIKA HOTELI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Natural Resource Forum (TNRF), Joseph Olila, akizungumza na wanahabari wakati akitoa taarifa chokozi katika uzinduzi wa mfululizo wa vipindi vipya vya runinga kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini uliofanyika Hoteli ya New Africa Dar es Salaam leo asubuhi.
 Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu. Kutoka kushoto ni  Mkurugenzi wa Taasisi ya Natural Resource Forum (TNRF), Joseph Olila, Mkurugenzi, Idara ya Misitu na Nyuki wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Gladness Makamba, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa uzinduzi huo, Msaidizi wa Balozi, Ubalozi wa UFINI ambao ni wafadhili wa mama misitu, Simo-Pekka Parviainen na Ofisa Mradi Ubalozi wa Finland, William Nambiza.
Mshauri wa Ufundi Weizara ya Maliasili na Utalii, Thomas Sellaine (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mkurugenzi Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA), Rahima Njaidi (kushoto), akielezea shughuli zinazofanywa na mtandao huo.
Mkuu wa Mradi ya Kilimo, Kipato na Ajira wa Shirika la Maendeleo la Uswisi, Ueli Mauderli (kulia), akizungumza katika uzinduzi huo.
 Wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Wanahabari wakichukua taarifa za uzinduzi huo.
 Mkutano wa uzinduzi huo ukiendelea.
 Mwezeshaji, Faustine Ninga kutoka Taasisi ya Natural Resource Forum (TNRF), akitoa maelekezo mbalimbali.
 Meneja Kampeni Mama Misitu, Gwamaka Mwakyanjala (kushoto), akizungumza katika uzinduzi huo.
 Balozi wa Mama Misitu, Asha Salimu (kushoto), akizungumza katika uzinduzi huo.
 Wasainii walioigiza namna ya utunzaji wa miti. Kulia ni Philemon Robari na Mohammed Titima.
Maofisa mbalimbali waliopo kwenye mradi huo wa Mama Misitu wakiwa katika uzinduzi huo.


MFULULIZO wa vipindi vipya vya runinga kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini. Kampeni ya Mama Misitu (MMC), inazindua mfululizo wa vipindi vya kuelimisha jamii kuhusu uzalishaji na faida za mkaa endelevu kijamii, kimazingira na kiuchumi.


Vipindi hivyo mfululizo vimetengenezwa katika wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro ikiwa ni sehemu ya jitihada za pamoja kati ya Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA), Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), Shirika la Kuendeleza Teknolojia  za Asili (TATEDO) na Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ili kuleta mabadiliko na kurasimisha sekta ya mkaa iweze kutoa ajira endelevu na kipato kwa jamii za vijijini na mijini.


Inakadiriwa kuwa mkaa na biashara za kuni huzalisha takriban (dola bilioni 1) za mapato kwa zaidi ya wazalishaji, wasafirishaji na wafanyabiashara laki tatu (300,000) katika mwaka 2012. Mahitaji ya mkaa nchini Tanzania yameongezeka kwa kasi na kwa kiasi kikubwa.


Mkaa endelevu ni mkaa unaozalishwa kwa njia endelevu kutoka katika Misitu ya Hifadhi ya Jamii bila kuchangia ukataji miti na uharibifu wa mazingira. Hata hivyo, uzalishaji wa aina hii ya mkaa bado haujajulikana. Kampeni hii mpya ina lengo la kuleta mabadiliko kupitia ubunifu wa vipindi mfululizo vya runinga ambavyo vinazinduliwa leo.


Nishati zitokanazo na tongamotaka (biomas)  ni nishati muhimu sana nchini Tanzania itakayoendelea kutumika angalau zaidi ya miaka 20 ijayo. Kwa sasa, mkaa mwingi huzalishwa kinyume na utaratibu kutoka katika misitu ya hifadhi na misitu ya vijiji isiyo na mipango ya matumizi endelevu. Kutokana na usimamizi hafifu wa uzalishaji wa mkaa, imesababisha ukataji miti na uharibifu wa misitu kuongezeka nchini Tanzania.


Kampeni ya Mama Misitu na washirika wake (TFCG na MJUMITA) inalenga kuleta mabadiliko katika sekta ya mkaa kutoka tatizo kuwa fursa kubwa muhimu. Hivyo, vipindi vya runinga vya Mama Misitu pamoja na jumbe muhimu za mawasiliano zitasambazwa nchini Tanzania ili kuibua mjadala wa pamoja juu ya kuboresha utawala bora wa rasilimali misitu na kuleta faida kwa watanzania.



Mama Misitu ni kampeni ya mawasiliano yenye lengo la kuboresha utawala bora wa misitu ya Tanzania na kupunguza uvunaji haramu wa mazao ya misitu ili watu wa Tanzania wanufaike zaidi na rasilimali misitu zao.


Kwaya tatu kuombea amani uchaguzi Mkuu

$
0
0
KWAYA tatu za muziki wa Injili Tanzania zinatarajia kuwa mojawapo ya wadau watakaoiombea amani Tanzania kuelekea uchaguzi Mkuu kupitia Tamasha la Amani linalotarajia kufanyika Oktoba 4.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama pamoja na kwaya hizo maombi hayo ya amani yatashirikisha waimbaji wengine wa Tanzania na nje.

Msama alizitaja kwaya hizo ni pamoja na Kwaya ya Uinjilisti ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Kwaya ya Mtakatifu Andrew Anglican ya Dodoma sambamba na kwaya ya Wakorintho wa pili ya Mafinga mkoani Njombe.

Msama alisema Watanzania wajiandae kupata neno la Mungu lenye lengo la kuombea amani nchi yao kupitia viongozi wa dini na wadau wengine.
"Suala la amani linatakiwa kuzungumzwa na kila mmoja, hivyo ni wakati wa kuunganisha nguvu pamoja kwa lengo hilo," alisema Msama.

Msama alisema kamati yake inaendelea na mchakato wa kufanikisha tamasha hilo ambalo litaunganisha nguvu kumfikia Mungu kwa maombi.

Aidha Msama alisema baada ya kumalizika kwa tamasha hilo jijini Dar es Salaam, Oktoba 6 tamasha hilo litafanyika Morogoro, Oktoba 8 (Iringa), Oktoba 10 (Makambako), Oktoba 11 (Mbeya), Oktoba 13 (Dodoma), Oktoba 14 (Singida), Oktoba 15 (Tabora), Oktoba 16 (Shinyanga) na Oktoba 18 (Mwanza).

JIMBO LA IRINGA MJINI LILIKOSA MBUNGE MAKINI SASA NI ZAMU YANGU UBUNGE -MWAKALEBELA

$
0
0
Mgombea   ubunge  jimbo la  Iringa mjini Frederick Mwakalebela  akiomba kura kwa  wananchi wa kata ya Mshindo  leo  wakati wa mkutano wake wa kampeni
Wananchi   wakiwa katika  mkutano  huo wa kampeni leo
Aliyekuwa  mgombea  ubunge  katika mchakato wa ndani ya  chama Michael Mlowe  akimnadi Mwakalebela
Katibu  wa CCM Iringa mjini Bw Elisha Mwampashi  akimnadi  Mwakalebela
Wana CCm na  wananchi wa kata ya  Mshindo   wakisukuma  gari alipopanga mgombea  ubunge wa CCM Bw  Mwakalebela na mgombea  udiwani wa kata  hiyo Bw Ibrahim Ngwada leo
Wanananchi  na  wana CCm wakisukuma gari la Mwakalebela
Na matukiodaima Blog
MGOMBEA Ubunge wa jimbo la Iringa kupitia chama cha mapinduzi ( CCM) Frederick Mwakalebela amesema jimbo la Iringa Mjini limekosa kunufaika na fursa za maendeleo kwa kuwa halikuwa na mbunge makini wa kuleta maendeleo .


Hivyo amewataka wananchi wa jimbo la Iringa Mjini kuecha kujutia kukosa maendeleo na badala yake kumchagua kuwa mbunge wao ifikapo Octoba 25 mwaka huu.

Mwakalebela ametoa kauli hiyo leo wakati wa mkutano wake wa kampeni za Ubunge kwenye kata ya Mshindo  alisema iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo atahakikisha anasogeza maendeleo ya haraka kwa wananchi wa Jimbo la Iringa ambao kwa miaka mitano wamekosa kupata maendeleo hayo .

Kwani alisema hakuna sababu ya kujutia na badala yake kutumia nafasi hiyo kujutia miaka mitano ambayo wamepumzika pasipo kushuhudia maendeleo yoyote katika jimbo hilo la Iringa mjini.

Kuhusu nini atafanya baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge alisema ni pamoja na kuboresha miundo mbinu ,kuanzisha saccos ya vijana ,kuanzisha mfuko wa elimu wa jimbo kwa kutumia sehemu ya mshahara wake ,kuwawezesha wazee kupata matibabu ya bure na kuboresha sekta ya michezo.


Wakati aliyekuwa Mgombea Ubunge katika mchakato wa kura za maoni Balozi Augustino Mahiga alisema matumaini mapya ya jimbo la Iringa yatapatikana kwa kuchagua diwani ,mbunge na Rais toka CCM .

Kwani alisema kuwa majuto ya wanajimbo la Iringa ambayo wanayo kwa sasa ni kutokana na kukosa mbunge Makini wa kuwatumikia wananchi na badala yake kuwa na mbunge wa maandamano na fujo bungeni.

TIMU YA KAMATI YA AMANI YA VIONGOZI WA DINI YAJIFUA NA MABALOZI, YAKABIDHIWA MIPIRA

$
0
0


 Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum (wa tatu kushoto) na wenzake wakichezea mpira kujaribu viwango vya mipira hiyo baada ya kukabidhiwa na Kamanda wa kanda maalumu ya Dar es Salaam, suleiman Kova (wa pili kulia), wakati wa mazoezi ya timu ya Kamati ya Amani inayoundwa na Viongozi wa Dini. Mazoezi hayo yalifanyika leo asubuhi kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam, sambamba na timu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zaoTanzania,kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wakirafiki kati yao unaotarajia kuchezwa hivi karibuni. Picha na www.sufianimafoto.com
 Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova (kulia) akimkabidhi mpira Nahodha wa timu ya Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini, Skei Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Sheikh Alhad Mussa Salum, baada ya mazoezi ya timu hiyo na timu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Nchini, yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini leo asubuhi kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kirafiki unaotarajia kuchezwa hivi karibuni.

Mazoezi ya pamoja...
 Suleiman Kova, akisalimiana na Mabalozi baada ya kuwakabidhi mipira leo asubuhi.
 Picha ya pamoja ya Timu ya Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini na Mabalozi baada ya mazoezi yao ya pamoja yaliyopigwa kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar leo asubuhi.
  Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum, akijaribu kumpiga chenga Balozi wa Denimark, wakati wa mazoezi yao ya pamoja kwenye Uwanja wa Karume Dar es Salaam leo asubuhi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kirafiki. 
 Mazoezi ya Viungo.....
 Nahodha akizungumza na wachezaji wake baada ya mazoezi 
Majadiliano baada ya mazoezi...

Picha na www.sufianimafoto.com
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images