Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

MAADILI YA UCHAGUZI KWA AJILI YA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI YA MWAKA 2015

$
0
0
 (Chini ya Kifungu cha 124 A cha Sheria ya Uchaguzi Na. 1 ya mwaka 1985 (sura ya 343)
Sisi Vyama vya Siasa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa pamoja tumekubaliana kuwa na uchaguzi huru, wa haki, uwazi, na wa kuaminika. 

Na kwamba Amani, Ustawi wa Nchi, Usalama wa Raia, Uhuru wa Vyama vya Siasa na Utii wa Sheria, Kanuni na taratibu za uchaguzi ndio msingi wa uchaguzi ulio huru, haki na wenye kuzingatia ushiriki wa makundi yote ya jamii katika uchaguzi. Tunajipa, na tunakubaliana kuwajibika kuyatekeleza maadili haya yanayotokana na kifungu cha 124A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi ya mwaka 1985, (sura 343). 

Tutafanya jitihada za wazi kuhakikisha maadili haya yanajulikana na kuheshimiwa na wagombea na wanachama wote wa Vyama vya Siasa.
2.0 Maadili kwa Vyama vya Siasa na Wagombea katika kuendesha shughuli za Siasa wakati wa Kampeni.
2.1 Wajibu wa Vyama vya Siasa na Wagombea.
  1. (c)  Vyama vya Siasa vifanye mikutano ya Kampeni kwa kuzingatia ratiba rasmi iliyoratibiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi au Wasimamizi wa Uchaguzi katika kutangaza sera zao. Aidha, mikutano yote itafanyika kati ya saa 2:00 asubuhi na saa 12:00 jioni. Bila kuathiri muda ulioelezwa hapo juu, Vyama vya Siasa vinaweza kutumia vipaza sauti kuanzia saa1:00 asubuhi hadi saa 2:00 usiku kutoa matangazo ya mikutano itakayofuata. 
  1. (k)  Viongozi wa Vyama vya Siasa, Wagombea au Wafuasi wao wahakikishe kuwa majengo wanayotumia kufanya kampeni sio ya ibada au sehemu zinazotumiwa kwa ajili ya ibada. Vile vile, Vyama vya Siasa vihakikishe kuwa havitumii Viongozi wa dini kupiga kampeni kwa ajili ya Vyama vya Siasa au Wagombea wao. 


    1. (f)  Viongozi wa Vyama vya Siasa na Wagombea wao hawaruhusiwi kuchafua, kubandua au kuharibu matangazo ya kampeni ya Vyama vingine vya Siasa na matangazo ya Uchaguzi yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

NUH MZIWANDA: SIONI TATIZO KWA MSANII KUONESHA MAHABA KWA CHAMA ANACHOKIPENDA

$
0
0
Nuh Mziwanda amewataka wasanii kuwa wazalendo kwa kuonyesha hisia zao za vyama vya siasa na kuonyesha ushirikiano katika kuhamasisha.

Akizungumza na Planet Bongo ya East Africa Radio leo, Nuh alisema maendeleo yatakayopatikana ni manufaa kwa watanzania wote kwa ujumla.

“Wewe ukiwa msanii sio kwamba sio mwananchi wa kawaida,” alisema.

“Wewe pia unahitaji kutawaliwa vizuri. Unahitaji utawala mzuri ambao utaongoza hata kazi zako ziende vizuri.
 Kwahiyo ni vyema mtu ukajua upo upande gani, huo ni upendo wa nchi yako na ni mzalendo. Kila binadamu anapenda uongozi mzuri ndio maana kila mtu akiwa na akili timamu ana haki ya kuchagua chama anachokitaka,” aliongeza.

“Lakini sisi wasanii tusijisahau tukawa tunashindwa kuweka hisia zetu kwaajili ya maslaHi ya nchi yetu. Unaogopa kuweka wazi wewe ni chama gani, unampenda mwanasiasa gani! Sisi ni vioo vya jamii tunaangaliwa pia na watu na kuna watu wahitaji ushauri au ufafanuzi juu ya viongozi waliotangaza nia. Kwa sisi inatubidi tuwe mfano kwanza kabla ya wananchi.”

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA WANGANGA WAKUU LEO JIJINI DAR

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal,akizungumza na wananchi kwenye ufunguzi wa  mkutano wa Mwaka wa waganga wakuu wa Mikoa,halmashauri na wakurugenzi wa Hospitali za Rufaa hapa nchini  katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ubungo Plaza jijini Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal akimkabidhi tunzo kwa wataalamu waoshiriki jitihada za kudhibiti Ugonjwa wa Ebola Afrika Mashariki, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt Dnan Mmbando jijini Dar es Salaam leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed  Gharib Bilal akimkabidhi tuzo wataalam walioshiriki jitihada za kudhibiti ugonjwa wa Ebola Afrika Mashariki Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt.Stephen Kebwe jijin Dar es Salaam leo.
 Sehem ya wananchi waliohudhulia katika mkutano huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib  Bilal akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mabalimbali leo jijini Dar es Salaam .
(Picha na Emmanuel Massaka)

WAGOMBEA WAACHE KUTUMIA UDINI NA UKANDA–NAPE

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye (Pichani) amewataka wagombea wa vyama mbalimbali vya siasa kuacha kutumia Udini au Ukanda kutokana na kufanya hivyo ni kuigawa nchi.
  
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mnauye amesema kuwa kuna watu katika kampeni wamejitokeza kutumia udini na ukanda vitu ambayo ni kinyume na maadili ya uchaguzi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
 
Amesema kuwa baadhi ya wagombea wameonekana katika ibada wakitaka wachaguliwe katika nafasi walizogombea hali ambaya italeta mpasuko wa  udini dhidi ya watu wengine. 
 
AIDHA Nape amesema kuwa kutokana maadili yaliyotolewa na NEC wagombea wafuate katika kuendesha kampeni ambazo haziwagawi watu.
 
“Uchaguzi huu watu wasitumie udini au ukanda kwani unagwa watanzania hivyo kila mtu afanye kampeni za kiistarabu na NEC ichukue hatua kwa watu wanaotumia udini”amesema Nape.

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YATOA TAARIFA KUHUSU MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WA MWEZI AGOSTI, 2015

$
0
0
 Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Iphrahim Kwesigabo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana kuhusu mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Agosti, 2015. Kulia ni Kaimu Meneja wa Idara ya Takwimu za Ajira na Bei, Ruth Minja.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale
UWEZO wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 62 na senti 97 mwezi Agosti, 2015 kutoka mwezi Septemba, 2010 ikilinganishwa na shilingi 62 na senti 98 iliyokuwa mwezi Julai, 2015.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Iphrahim Kwesigabo wakati akitoa taarifa kuhusu mfumuko wa bei wa taifa wa mwezi Agosti, 2015 kwa waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo.

Kwesigabo alisema mfumuko wa bei wa mwezi Agosti 2015 unaopimwa kwa kipimo cha mwezi umeongezeka kwa asilimia 0.02 ikilinganishwa na asilimia 0.41 iliyokuwa mwezi Julai, 2015.

"Fahirisi za bei zimeongezeka hadi 158.81 mwezi Agosti, 2015 kutoka 158.78 mwezi Julai, 2015.

Alisema kuongezeka kwa fahirisi za bei kumechangiwa hasa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula, baadhi ya bei za bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa fahirisi ni pamoja na gesi kwa asilimia 2.0, mafuta ya taa kwa asilimia 2.3, mazulia kwa asilimia 1.4, dizeli kwa asilimia 3.8 na petroli kwa asilimia 8.3.

Gwesigabo alisema kuwa mfumuko wa bei wa Taifa kwa kipimo cha mwaka unapima kiwango cha badiliko la kasi ya bei za bidhaa na huduma zote zinatumiwa na kaya binafsi.

Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwezi Agosti, 2015 umebaki kuwa asilimia 6.4 kama ilivyokuwa mwezi Julai 2015.

Aliongeza kuwa hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2015.

Alisema Fahirisi za bei zimeongezeka hadi 158.81 kwa mwezi Agosti, 2015 kutoka 149.31 mwezi Agosti, 2014.

Alisema Mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Agosti 2015 umepungua hadi asilimia 10.2 kutoka asilimia 10.6 ilivyokuwa mwezi Julai 2015.

Alisema mfumuko wa bei kwa baadhi ya nchi za Afrika Mashariki mfumuko wa bei nchini una mwelekeo unaokaribiana na baadhi ya nchi nyingine za Afrioka Mashariki ambapo mfumuko wa bei kwa mwezi Agosti 2015 nchini Kenya umefikia asilimia 5.84 kutoka asilimia 6.62 mwezi Julai, 2015 na Uganda umefikia asilimia 4.80 kutoka asilimia 5.4 mwezi Julai, 2015.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com

RAIS KIKWETE APOKEA TUZO YA KIONGOZI BORA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amepokea Tuzo ya Kiongozi Bora Afrika Mashariki kutoka katika taasisi ya East Africa Book of Records yenye makao yake makuu jijini Kampala Uganda.Pichani kiongozi wa Taasisi hiyo Dkt.Paul Bamutize akimkabidhi Rais Kikwete tuzo hiyo wakati wa hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaanm leo asubuhi.Sambamba na Tuzo hiyo Rais kikwete amepokea tuzo ya kuitambua Tanzania kama taifa bora Afrika Mashariki kwa kudumisha Amani na Utulivu,Huduma bora za jamii,na maendeleo makubwa ya kiuchumi katika kipindi cha miaka kumi
(picha na Freddy Maro)

ZAIDI YA WANAFUNZI LAKI SABA 7.7 WANATARAJIWA KUFANYA MTIHANI WA KUMALIZA DARASA LA SABA SEPTEMBA 9 HADI 10 MWAKA HUU

$
0
0

Zaidi ya wanafunzi laki saba 7.7 wanatarajiwa kufanya mtihani wa kumaliza darasa la saba katika vituo zaidi ya elfu 16 nchni nzima kuanzia Septemba 9 hadi 10 mwaka huu. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Daktari Charless Msonde amesema kati ya wanafunzi hao wavulana laki tatu na  sitini na moja elfu sawa na asilimia 45.6, wasichana ni laki nne na kumi na nne elfu sawa na asilimia 53.4, ambapo masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na maarifa ya jamii. 
 
Amezitaka kamati za mitihani za mikoa na wilaya kuhakikisha taratibu za mitihani zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vituo vya mitihani vinakuwa salama, hususani katika kipindi hiki ambacho baadhi ya viwanja vya shule za msingi vinatumiwa na vyama vya siasa kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu.

JKT KUBORESHA MAZINGIRA YA MAFUNZO ILI YAWE NA TIJA ZAIDI KWA WAHITIMU NA TAIFA

$
0
0

Jeshi la kujenga taifa JKT limesema linaendelea na harakati za kuboresha mazingira ya mafunzo kwa vijana wa mujibu wa sheria na wale wa kujitolea ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu na upatikanaji wa vifaa vya mafunzo vinavyojumuisha sare pamoja na viatu ili kuyafanya mafunzo hayo kuwa bora na yenye kuwajenga vijana katika moyo wa uzalendo kwa nchi yao.

Mkuu wa jeshi la kujenga taifa JKT.Meja Jenerali Raphael Muhunga amesema hayo wakati akifunga mafunzo ya JKT kwa vijana wa mujibu wa sheria yaliyopewa jina la oparesheni Kikwete mwaka 2015 katika kambi ya mafunzo ya kikosi cha jeshi cha 841 Mafinga mkoani Iringa na kueleza kuwa lengo la kushughulikia changamoto hizo za vifaa vya mafunzo ni kuboresha mafunzo hayo ili yalete tija zaidi kwa taifa na wahitimu wenyewe.
 
Katika risala yao wahitimu hao wapatao zaidi ya elfu wamesema moja ya changamoto zilizowakabili katika muda wote wa mafunzo ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya kujifunzia ikiwemo buti na kombati pamoja na muda wa mafunzo kuwa mfupi hali iliyowalazimu kufanya mafunzo yao katika mazingira magumu huku wakikabiliwa na mambo mengi ya kujifunza katika muda huo mfupi ambapo mkuu wa kambi ya jeshi hilo kikosi cha 841 Mafinga luteni kanali Martin Mkisi amewapongeza wakufunzi wa mafunzo hayo kwa uvumilivu na ubunifu.
 
Ufungaji wa mafunzo hayo umeambatana na maonesho mbalimbali ya vijana hao wahitimu walioonesha ukakamavu na ustadi walioupata mafunzoni ikiwemo kucheza kwata, kuchoma singe kucheza karate na kuruka vikwazo maonesho yaliyodhihirisha jinsi vijana hao walivyoiva kimafunzo.

TASWIRA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KWA WANAWAKE KUPITIA VIPODOZI VYA LUV TOUCH MANJANO

$
0
0
  Mkurugenzi Mtendaji   8020 Fashion na  Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation Shamim Mwasha Akitoa Mada kwenye Semina ya Kuwawezesha  Wanawake Kuwa Wajasiriamali kupitia Vipodoz Vya Luv Touch Manjano Iliyoandaliwa na Manjano Foundation Kwa Lengo la Kuwajengea Udhubutu Wanawake  Kufanya biashara pia namna ya Kujiwekea Akiba na Kutumiza Malengo yao.
Washiriki wa Mafunzo hayo  wakisikiliza kwa Makini Mada Mbalimbali zilizokuwa Zikijadiliwa.
 Mafunzo ya Ujasiriamali kwa Mwanamke wa Kitanzania kwa Kutumia Vipodozi vya LuvTouch Manjano yanaendelea.Mradi huo ulianzishwa kuwejengea Uwezo wanawake Kwenye Ujasiriamali yakisimamiwa na Taasisi ya Manjano Foundation.
 Lengo la Mradi huo ni kuona kwamba wanwake hawa wanajisimamia na kujikita vizuri kwenye Biashara ya Vipodozi na kujua Mbinu Mbalimbali za Biashara zao kwa lengo la kumuongezea ajira mwanamama na kuondoa dhana za ukosefu wa ajira kuwa chungu ya yeye kujiwezesha katika kujikimu mahitaji yake ya msingi, yaani aweze kujipatia Chakula, Malazi na Mavazi kwa kupitia ujasiriamali.
 Pamoja na mafunzo ya biashara, washiriki hawa watanufaika na utaalamu (Proffessional Makeup Artist).Taasisi ya Manjano Foundation, ambayo imeanzisha jukwaa kwa ajili ya kuandaa miradi na programu ambazo zitamuinua mwanamke wa Kitanzania kwa kumwondolea ugumu wa kipato na ambayo itakuwa ni chachu ya kubadili yale yote yaliyoyazunguka maisha yake. Taasisi hii limekwishazindua mradi wenye kubeba bendera yake, Manjano Dream-Makers, mradi unaokusudia kuzaa kizazi kipya cha wajasiriamali wanawake kwa kutumia kipodozi cha LuvTouch Manjano tu
 Mradi huu Uzinduliwa mwezi Mei mwaka huu na Mama Tunu Pinda. 
Mafunzo haya yametolewa kwa zaidi ya Wanawake 30 ambapo wengi wao tayari wameshaanza kunuafaika na kipodozi pendwa cha LuvTouch Manjano ambapo wamewezeshwa
 
Washiriki hao wakiwa kwenye Picha ya Pamoja

ZAIDI YA WANAFUNZI LAKI 7 WA DARASA LA 7 WANATARAJIWA KUANZA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI KWA MUDA WA SIKU MBILI KUANZIA KESHO.

$
0
0


Zaidi ya wanafunzi laki saba 7.7 wanatarajiwa kufanya mtihani wa kumaliza darasa la saba katika vituo zaidi ya elfu 16 nchni nzima kuanzia Septemba 9 hadi 10 mwaka huu. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Daktari Charless Msonde amesema kati ya wanafunzi hao wavulana laki tatu na  sitini na moja elfu sawa na asilimia 45.6, wasichana ni laki nne na kumi na nne elfu sawa na asilimia 53.4, ambapo masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na maarifa ya jamii. 
 
Amezitaka kamati za mitihani za mikoa na wilaya kuhakikisha taratibu za mitihani zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vituo vya mitihani vinakuwa salama, hususani katika kipindi hiki ambacho baadhi ya viwanja vya shule za msingi vinatumiwa na vyama vya siasa kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu.


MAGUFULI AHIDI KUFUFUA VIWANDA MKOANI TANGA KUPUNGUZA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA

$
0
0
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akifafanua jambo mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Tanga waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni,uliofanyika katika viwanja vya Tangamano jioni ya leo mjini Tanga. 
  Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa mji wa Tanga kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya angamano,jioni ya leo ambapo aliahidi kuboresha Bandari ya Tanga, kujenga Viwanda vya matunda na samaki ili kuweza kupunguza tatizo kubwa la ajira kwa vijana.
 Naibu Waziri wa Sheria na Katiba,ambaye pia ni mgombea Ubunge viti maalum upande wa akina Mama mkoa wa Tanga (UWT),Mh Ummy Mwalimu akimuombea Kura za kutosha mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli ili aweze kuibuka mshindi na kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano.
 Wakazi wa mji wa Tanga waliofika kwenye mkutano huo wakishangilia jambo. 
 Nyomi la watu . 
 Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli akisalimiana na  Naibu Waziri wa Fedha na mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba  Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba
  Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli Mhe. January Makamba akihutubia wakazi wa mji wa Tanga kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Tanga na vitongoji vyake wakiwa wamefurika kwenye viwanja vya Tangamano kwenye mkutano wa kampeni za CCM,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.

 Dkt Magufuli akisisitiza jambo mbele ya maelfu ya wananchi (hawapo pichani) jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika uwanja wa Tangamano.
Wananchi wakifuatilia mkutano wa kampeni wa Dkt John Pombe Magufuli mjini Tanga .
  Naibu Waziri wa Fedha na mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba  Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akihutubia wakazi wa Tanga mjini kwenye mkutano uliofanyika kwenye uwanja wa Tangamano. 
  Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Bumbuli Mhe. January Makamba na Naibu Waziri wa Fedha na mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba  Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa kampeni jioni ya leo katika uwanja wa Tangamano,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli alihutubia na Kumwaga sera zake kwa wananchi,ikiweno na kuomba ridhaa ya kuwaongoza katika miaka mitano ijayo.
 Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Mzee Yusuph Makamba akihutubia wakazi wa Tanga mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika ndani ya viwanja vya Tangamano.
 Maelfu ya Wananchi wakimsikiliza Dkt Magufuli alipokuwa akimwaga sera zake na kuwaomba wananchi hao wajitokeze kwa wingi Oktoba 25 na kumpigia kura ya ndio ili aibuke mshindi na kupewa ridhaa ya kuiongoza Tanzania katika awamu ya tano.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga wananchi wa mji wa Tanga waliofika kwenye mkutano hadhara wa kampeni,uliofanyika jioni ya leo katika viwanja vya Tangamano mjini humo na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu.

RAIS KIKWETE APOKEA UJUMBE KUTOKA KWA WAZIRI MKUU WA INDIA NARENDRA MODI

$
0
0
 unnamedx
Mjumbe maalum wa Waziri Mkuu wa India Narendra Modi ambaye pia ni Waziri wa nchi anayeshughulikia Maendeleo ya Ujasiriamali Mhe.Shri Rajiv Pratap Rudy akiwasilisha kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete barua yenye ujumbe kutoka kwa kiongozi huyo wa India ikulu jijini Dar es Salaam Septemba 8, 2015 .
c
Rais Dkt.Jakaya Mrisjo Kikwete akisoma barua yenye ujumbe kutoka kwa waziri Mkuu wa India mara baada ya kukabidhiwa ikulu jijini dar es Salaam Septemba 8, 2015
(Picha na Freddy Maro)

SHEREHE ZA TUZO YA KIONGOZI BORA AFRIKA MASHARIKI KWA RAIS KIKWETE IKULU

$
0
0

unnamed
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amepokea Tuzo ya Kiongozi Bora Afrika Mashariki kutoka katika taasisi ya East Africa Book of Records yenye makao yake makuu jijini Kampala Uganda.
Pichani kiongozi wa Taasisi hiyo Dkt.Paul Bamutize akimkabidhi Rais Kikwete tuzo hiyo wakati wa hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam Septemba 8, 2015 . asubuhi.Sambamba na Tuzo hiyo Rais kikwete amepokea tuzo ya kuitambua Tanzania kama taifa bora Afrika Mashariki kwa kudumisha Amani na Utulivu,Huduma bora za jamii,na maendeleo makubwa ya kiuchumi katika kipindi cha miaka kumi.
1
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kumbukumbu maalum ya taasisi ya East Africa Books of Records mara baada ya kupokea tuzo maalum ya kiongozi bora Afrika mashariki kwa kudumisha amani nchini na katika jumuiya ya 
Afrika Mashariki kwa ujumla hususani Kenya baada ya uchaguzu mkuu na Burundi hivi karibuni.Kushoto akishuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Africa Book of Records Dkt.Paul Bamutize na kulia ni Mkuu wa kitengo cha utafiti katika taasisi hiyo Bwana Luzindana Adam Buyinza.
4
Rais Dkt.Jakaya Mrisho akitoa hotuba yake baada ya kupokea Tuzo ya Kingozi bora Afrika Mashariki.
3
Mwakiulkishi kutoka ubalozi wa Uganda nchini Tanzania Bwana Stephen Kiyingi akitoa hotuba yake na ushuhuda jinsi Tanzania ilivyopiga hatua kubwa ya maendeleo katika miaka kumi iliyopita.
2
Baadhi ya Wageni walihudhuria hafla hiyo ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
7
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza mabalozi kutoka nchi za Afrika ya Mashariki muda mfupi baada ya kupokea Tuzo.
6
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, mabalozi kutoka nchi za Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Tassisi ya East Africa Book of Records ikulu jijini Dar es Salaam leo.
  5
Wataalamu wa Utafiti kutoka Taasisi ya East Africa Book Of Records wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada kutunikiwa Tuzo hiyo.Kutoka kjushoto ni Kiongozi wa Taasisi hiyo Dkt.Paul Bamutize,Watatu kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Utafili cha taasisi hiyo Bwana Luzindana Adam Buyinza na kulia ni Afisa mwandamizi wa Taasisi hiyo Bwana Kato Issa.
(Picha zote na Freddy Maro)

MAGUFULI ALIVYOITEKA TANGA

Bayport yazindua huduma mpya ya Jibayportphonishe

$
0
0
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, kushoto, akizungumza jambo katika uzinduzi wa huduma mpya ya mikopo ya simu za mikononi aina ya Huawei ijulikanayo kama 'Jibayportphonishe', uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Micka Mavoa, Mkurugenzi wa Cape View, Kampuni inayoshirikiana na Bayport katika huduma hiyo ambayo mteja akikopa simu atapelekewa hadi mahala anapohitaji ifike. Picha na Mpiga Picha Wetu.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, Taasisi ya kifedha ya Bayport Financial Services, imezindua huduma yake mpya ya kukopesha (Smartphone) simu za mikononi aina ya Huawei zenye thamani ya Sh 140,000, ikiwa na lengo la kuwawezesha Watanzania ambao ni watumishi wa umma na wafanyakazi wa kampuni binafsi zilizoidhinishwa kumiliki simu wakati wowote ili ziwakwamuwe katika suala zima la mawasiliano ya simu za mikononi, huduma inayotambulika kama 'Jibayportphonishe'.

Kuanzishwa kwa huduma hiyo ya mikopo ya simu za mikononi kumekuja siku chache baada ya taasisi hiyo pia kuzindua huduma ya bima ya magari, pikipiki na bajaj, ambapo zote kwa pamoja ni mkombozi kwa Watanzania, wakiwamo wale wenye kipato cha chini na cha kati.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo asubuhi, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, alisema kwamba kuanzishwa kwa huduma hiyo kutaifanya jamii iwe katika kiwango kizuri cha mawasiliano, hivyo kukuza pia uchumi wao.
Mkurugenzi wa Cape View, Micka Mavoa, kulia akizungumza jambo.

Alisema kwamba badala ya mtumishi wa umma na wale wa kampuni binafsi zilizoidhinishwa kuwekeza kidogo kidogo ili wanunuwe simu watakazo, sasa wanaweza kukopeshwa simu hizo na kupelekewa hadi katika maeneo yao wanayopatikana. Alisema simu hizo zitaambatana na ofa ya intaneti MB 500 bure kila mwezi kwa miezi sita kutoka katika Kampuni ya Simu za Mikononi ya Vodacom Tanzania, huku mteja akilazimika kulipa Sh 9000 kila mwezi, katika kipindi cha miezi 24.


BI. SAMIA SULUHU AHAIDI UMEME KILA KIJIJI RUVUMA, VIWANDA VYA MAHINDI NA KAHAWA

$
0
0
Mgombea mwenza wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu (katikati) akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, Martin Mtonda (kushoto) na mgombea udiwani wa CCM.
MGOMBEA mwenza wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu ameanza ziara yake mkoani Ruvuma akiinadi ilani ya chama hicho huku akiahidi neema kwa wakulima wa kahawa na mahindi wa mkoa huo.

Bi. Samia Suluhu ambaye amehutubia mikutano mitatu katika majimbo mawili ya mkoa wa Ruvuma yaani Jimbo la Nyasa na Mbiga Vijijini, akizungumza katika mikutano yake amesema serikali itakayoundwa na CCM endapo itashinda itahakikisha inashusha umeme katika vijiji vyote vya mkoa huo kwa awamu ili kuchochea maendeleo ya wananchi.

Alisema kwa kuwa mkoa huo unazalisha mazao ya mahindi na kahawa serikali itahakikisha inaanzisha viwanda eneo hilo vya kusaga na kuandaa unga wa mahindi kwa wakulima na kuwawezesha ili wauze unga na kunufaika zaidi tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo wamekuwa wakilanguliwa.

Alisema viwanda vingine ambavyo Serikali ya CCM itavianzisha ni pamoja na viwanda vya kubangua kahawa na kuiandaa kikamilifu tayari kwa kutumika, jambo ambalo alisema licha ya kuongeza thamani ya zao hilo itaongeza ajira kwa vijana na kuchochea uchumi wa wakulima eneo hilo.
Akizungumzia miundombinu ya barabara ambayo bado ni changamoto kwa mkoa huo hasa vijijini alisema serikali itakayoundwa na CCM chini ya uongozi wa Dk. John Pombe Magufuli pamoja na yeye watahakikisha wanajenga na kuboresha barabara za maeneo hayo ili ziweze kupitika kwa uhakika.

Hata hivyo kiongozi huyo amesema Serikali itakayoundwa na CCM endapo itashinda Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015 imejipanga kuboresha vizuri huduma za afya kuondoa ukiritimba na rushwa, elimu kwa kutoa elimu bure toka darasa la kwanza hadi kidato cha nne pamoja na ujenzi wa mabweni na uwezeshaji vijana na akinamama kiuchumi popote walipo mjini na vijijini.

Ziara ya mikutano ya kampeni ya mgombea mwenza huyo wa urais tiketi ya CCM, inaendelea leo katika Mkoa wa Ruvuma na ataingia Jimbo la Tunduru kuendelea kuinadi ilaya ya chama hicho kuomba ridhaa kwa wananchi ili waweze kurejeshwa madarakani na kuunda dola.
Pichani juu ni baadhi ya wananchi na wanaCCM wakiwa wamefurika katika kiwanja cha Kijiji cha Maguu Wilaya ya Mbinga kumsikiliza mgombea mwenza wa urais kupitia tiketi ya CCM alipokuwa akiinadi ilani ya chama hicho.


Pichani juu ni baadhi ya wananchi na wanaCCM wakiwa wamefurika katika kiwanja cha Kijiji cha Maguu Wilaya ya Mbinga kumsikiliza mgombea mwenza wa urais kupitia tiketi ya CCM alipokuwa akiinadi ilani ya chama hicho.

 
Baadhi ya wananchi na wanaCCM wa Kijiji cha Maguu wilayani Mbinga wakimsubiri mgombea mwenza wa urais, CCM, Bi. Samia Suluhu. 


Pichani juu ni baadhi ya pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda zilizompokea mgombea mwenza wa CCM urais, Bi. Samia Suluhu mara baada ya kuingia Wilaya ya Mbinga zikiwa zimeegeshwa pembeni huku mkutano wa hadhara ukiendelea. 

Mmoja wa wajumbe wa kamati ya kampeni ya mgombea mwenza, Bi. Asumpta Mshama akizungumza na wanaCCM na wananchi (hawapo pichani) katika Kijiji cha Maguu, Wilaya ya Mbinga. 
Mgombea mwenza wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu (kulia) akizungumza na Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu, kabla ya kuanza kuhutubia katika mikutano wake wa kampeni.  
Mgombea mwenza wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu (katikati) akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM ambao ni wenyeji wake mkoa wa Ruvuma.
Mgombea mwenza wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu (katikati) akizungumza na mmoja wa vijana walemavu waliohudhuria mkutano wake wa hadhara Kijiji cha Maguu. Bi. Suluhu alimsaidia fedha kijana huyo. 

*Imeandaliwa na www.thehabari.com

TANZANIA YAHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUWASAIDIA WAKIMBIZI

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,  akizungumza wakati wa  Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu dhana ya wajibu wa kuwalinda raia, ambapo alisema licha ya kuasisiwa kwa dhana hiyo dunia bado imeendelea kushuhudia  maisha ya watu wasiokuwa na hatia yakiendelea kupotea  kwa sababu tu Jumuiya ya Kimataifa inashindwa kutumiza wajibu wake kwa wakati.
 Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa Majadiliano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu  dhana ya kuwalinda raia (R2P) majadiliano yaliyojielekeza katika kutathimini mafanikio na changamoto za utekelezi wa dhana hiyo ikiwa ni miaka kumi tangu kuasisiwa  kwake.
 Picha hii  ya maktaba ni ya  wakimbizi  katika kambi moja nchini Tanzania,  ambao jana  jumanne akizungumza katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UN Balozi Tuvako Manongi amesema kutoka na wimbi kubwa linaloendelea la wakimbizi  kukimbilia mataifa mengine kutafuta usalama wao. Jumuiya ya kimataifa haina budi kushirikiana na bila  kubagua katika  kuwalinda na  utoaji wa huduma na misaada ya kibinadamu kwa wakimbizi.

Na Mwandishi Maalum,  New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  imetoa wito kwa   Jumuiya ya Kimataifa wa kushirikiana katika  wajibu wa kuwalinda na kuwapatia misaada ya kibinadamu,  wakimbizi wanaokimbia machafuko, vita na  migogoro katika nchi zao.
Wito huo  umetolewa   siku  ya jumanne na Balozi Tuvako Manongi,Mwakilishi wa  Kudumu  wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,   wakati  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  lilipokutana  kwa majadiliano  ya  siku moja kuhusu utekelezaji wa dhana juu ya wajibu wa kulinda raia (R2P) mafanikio na changamoto zake.

Dhana  ya wajibu wa kuwalinda raia  dhidi ya  mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita,  mauaji ya kikabila na uhalifu dhidi ya  binadamu   ilianzishwa mwaka 2005 wakati  wa mkutano wa Kimataifa  uliofanyika mwaka huu, ambapo viongozi wakuu  wa  nchi na serikali walikubaliana kwamba wajibu wa kwanza wa kuwalinda raia  dhidi ya udhalimu wa aina yoyote ile ni wa serikali yenyewe husika.

Kupitia dhana hiyo ya R2P  viongozi hao walikubaliana pia kwamba ikiwa itadhihirika kuwa serikali ya nchi husika inashindwa kuwalinda raia wake kwa sababu zozote zile basi  jumuiya ya kimataifa inapashwa  kuchukua maamuzi ya kuwalinda raia hao.

Akichangia majadiliano hayo  ambayo yaliyofunguliwa na Katibu Mkuu   Ban Ki moon, Katika   Balozi Manongi, ameeleza kwamba,  dhana ya  kuwalinda raia inapashwa pia kuhusisha tatizo la wakimbizi wanaokimbia nchi zao kwa sababu mbalimbali na kwenda kutafuta usalama katika mataifa mengine.

Akasema ,  Tanzania ambayo kwa miaka mingi imekuwa  ikiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi  kutoka mataifa mbalimbali,  kwa uzoefu wake  inatambua dhahiri kuwa ushirikiano wa kimataifa ni muhimu  sana na kwamba Jumuiya ya kimataifa inatakiwa kuuboresha na kuimarisha ushirikiano huo.

 “Tatizo  linaloendelea hivi sasa la  wimbi kubwa la wakimbizi wanaokimbilia  Ulaya wakitokea Syria, Libya na  kwingineko,  ni changamoto yetu sote,  ni changamotoya kimataifa, wakimbizi hawa  na wengineo wanapashwa kulindwa na kusaidiwa kwa mujibu  wa sheria za kimataifa zikiwamo sheria za haki za binadamu  ”.

 Akasema  Balozi Manongi.
“ Tanzania   kama nchi ambayo kwa miaka mingi imekuwa  ikiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi,  inatambua kwamba  ushirikiano wa kimataifa ni muhimu katika kuwasaidia wakimbizi.  Ni   Muhimu basi  tuimarisha na kuboresha misingi ya  kusaidiana  katika kulibeba jukumu hili” akasema Balozi Manongi
Akizungumzia  Zaidi kuhusu dhana ya  wajibu wa kuwalinda raia,  dhana ambayo  tafsiri yake bado  haijapokelewa vema  miongoni mwa nchi wanachama   Balozi amesema. Tanzania inaamini kwamba kanuni za sheria za kimataifa zikiwamo zile za  uhusiano na ushirikiano baina ya  nchi marafiki ni muhimu  katika  kuielewa,  kutafsiri  na utekelezaji wa dhana ya wajibu wa kuwalinda raia kutoka na ukweli kwamba  ni dhana ambayo  haijjitegemei.

Aidha   Mwakilishi huyo wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  amebainisha kuwa,  ingawa wajibu wa kwanza wa utekelezaji wa wajibu wa kuwalinda raia  ni wa Nchi au Serikali husika,  lakini  nchi  hiyo inaposhindwa kutimiza wajibu wake huo,  basi Jumuiya ya Kimataifa inapashwa kusaidia kwa kuiwezesha nchi hiyo kutekeleza wajibu huo.

Awali Akifungua majadiliano hayo Katibu Mkuu, Ban Ki Moon,  asema,   ni jambo la kusitikisha sana kwamba  miaka kumi tangu kuasisiwa   kwa dhana hiyo ya R2P   bado watu wengi wakiwamo watoto  wameendelea kupoteza maisha  kutokana  na sababu mbalimbali zikiwamo za vita na migogoro.

“ Ninasikitiza kueleza  kwamba miaka  kumi  tangu kuanzishwa kwa dhana  hii, dunia imeendelea kushuhudia  matukio ya watu  kupotezesha maisha yao kwasababu tumeshindwa kuwalinda. Tunaendelea kushuhudia watu wakipoteza maisha huko Sudan ya Kusini, Sudan katika jimbo la Darfur, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Libya, Syria, Yemen, Mali,  Jamhuri ya Afrika ya Kati  na kwiengineko”.akaeleza Ban Ki Moon. 

Na kwa sababu hiyo Katibu  Mkuu amependekeza  mambo  kadhaa ambayo  anaamini yatasaidia  kuongeza kasi ya utekelezaji wa dhana hii.
Baadhi ya Mambo  hayo ni,    nchi wanachama na hasa Baraza Kuu la Usalama, kuwa tayari  kwa kuweka mazingira ya kisiasa  ya  kuzuia na  kuitikia pale  inapojidhirisha  kuwapo kwa dalili za kutokea kwa uhalifu, utoaji wa tahadhari na kuchukua hatua. 

Wazungumzaji wengine katika   mkutano huo  wamelinyoshea  kidole   Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa na hasa katika matumizi ya kura ya Veto  yanayofanywa na wajumbe wa kudumu wa baraza hilo.

Baadhi ya wachangiaji wameeleza kwamba ili kanuni ya wajibu wa kuwalinda raia  iweze kutekelezwa kwa haraka na kwa wakati, wajumbe wa  watano wa kudumu wa  Baraza Kuu la Usalama, wanapashwa  kuonyesha utashi wa kisiasa na kuacha kutumia kura hiyo  kwa maslahi binafsi.

Wajumbe wengine , licha ya kuelezea  nchi zao kutoridhishwa  kwa  tafsiri  ya dhana  ya wajibu wa  kuwallinda raia lakini pia wamesema  hawakubaliani na matumzi ya nguvu kuingilia nchi nyingine kwa  na hata kuwaondoa   madarakani viongozi kwa  kisingizio    utekelezaji wa dhana ya wajibu wa kuwalinda raia. 

 Wajumbe wengine wameeleza  wazi wazi kupinga  kwao  hoja ya  kutaka  kuingizwa kwa  dhana hiyo ya R2P  katika ajenda  za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.  Sababu  zikiwa ni pamoja na kuwa  dhana hiyo bado inautata  na inahitaji kuendelea  kujadiliwa  miongoni mwa nchi wanachama.

UMEME WA PUMBA ZA MCHELE, MASHUDU YA PAMBA WATUMIKA KUENDESHEA MITAMBO YA TBL MWANZA

$
0
0
 Meneja wa kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Mwanza, Raymond Richmond,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampuni hiyo  kutumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba,kama chanzo cha nishati ya umeme kinachotumika kuendeshea mitambo.Kushoto ni Meneja wa Maji na Nishati wa kampuni hiyo, Sunday Kidolezi.
Meneja wa kiwanda cha Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza, Raymond Richmond, akizungumzia mradi wa matumizi ya mapumba ya mchele na mashudu ya pamba,ambacho ni chanzo cha nishati ya kuendesha mitambo kiwandani hapo.Nishati ni rafiki wa mazingira  kwa sababu haina hewa ukaa.Wanaokoa Dola za Kimarekani (USD) 400,000 hadi 500,000 kwa mwaka ambazo zingetumika kununua mafuta mazito na dizeli ya kuendeshea mitambo .
Waandishi wa habari wakiongozwa na  Meneja wa Kiwanda cha kampuni ya Bia (TBL) Mwanza, Raymond Richmond(wa kwanza kushoto), kwenda kutembelea mtambo unaotumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba kuzalisha nishati ya umeme inyotumika kuendesha mitambo ya kiwanda hicho.Kulia ni Meneja wa Maji na Nishati wa TBL, Sunday Kidolezi.

 
Meneja wa Nishati na Maji wa Kampuni ya Bia (TBL)Mwanza, Sunday Kidolezi (wa kwanza kulia),wakiwa na waandishi wa habari wakati wakitembelea mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba.wa Kwanza kutoka kushoto (mwenye shati jeupe), Ni Meneja wa Kiwanda hicho, Raymond Richmond.
Meneja wa Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza,Raymond Richmond (mwenye shati jeupe) akiwaonesha waandishi wa habari mtambo unaozalisha nishati ya umeme kwa kutumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba kwa ajili ya kuendesha mitambo ya kiwanda hicho.anaoshuhudia ni Meneja wa Maji na Nishati wa kampuni hiyo,Sunday Kidolezi (mwenye fulana ya mistari).Mwingine ni mwandishi wa habari wa kampuni ya The Guardian, Daniel Mkate,ambaye ni miongoni mwa  waandishi wa habari waliotembelea kiwanda hicho.
Raymond Richmond, Meneja wa kampuni ya Bia (TBL) Mwanza,akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani), mapumba ya mchele,yanayotumika kuzalisha nishati ya umeme wa kuendesha mitambo ya kiwanda hicho.Kulia ni Meneja wa Maji na Nishati wa kampuni hiyo.
Mwandishi wa habari, Daniel Mkate (kushoto) akiwauliza maswali, Meneja wa  Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza, Raymond Richmond na Meneja wa Maji na Nishati wa kampuni hiyo, Sunday Kidolezi, kuhusu  changamoto ya upatikanaji wa mali ghafi hiyo na madhara yake katika kuzalisha nishati na athari za mazingira.
Wafanyakazi wa kiwanda cha Kampuni ya Bi (TBL) Mwanza,wakijaza mapumba kwenye magunia, kabla ya kuingizwa kwenye mtambo wa kuzalisha umeme kiwandani hapo.Hapo ni katika eneo  linalotumika kupakulia shehena ya mapumba hayo ya mchele, kutoka kwa msambazaji.
Meneja wa kiwanda cha Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza,Raymond Richmod, akiwaonyesha waandishi wa habari, Daniel Mkate wa TRhe Guardian (nyuma) na Henry Kavirondo wa Chanel Ten,mashine inayosukuma mapumba ya mchele na mashudu ya pamba, kwenda kwenye mtambo wa kufua umeme unaotumika kuendesha mitambo ya kiwanda hicho.Kulia ni Meneja wa Maji na Nishati wa kampuni hiyo, Sunday Kidolezi.
Wafanyakazi wa kiwanda cha Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza,wakijaza mapumba ya mchele kwenye mashine kwa ajili ya kuyasukuma kadi kwenye mtambo wa kuzalisha nishati ya umeme, unaotumiwa kuendesha mitambo ya uzalishaji ya kiwanda hicho.
Meneja wa Maji na Nishati wa kiwanda cha Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza, Sunday Kidolezi, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhudu mradi huo wa uzalishaji wa nishati ya umeme,unaotumika kuendesha mitambo ya kiwanda cha kampuni hiyo kwa kutumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba.Wa kwanza kushoto ni Meneja wa kiwanda cha kampuni hiyo,Raymond Richmond.

MAZISHI YA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA MICHEWENI PEMBA ND.JABU KHAMIS MTWANA YALIYOFANYIKA JANA KIJINI KWAO WILAYA YA MICHEWENI

$
0
0
 Jeneza lililobeba mwili wa marehemu.
 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akishiriki katika mazishi ya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Micheweni Pemba.

AIRTEL YANG’ARA KATIKA MAONYESHO YA BIASHARA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya viwanda na Biashara Uledi Abbas Musa (
Kushoto) akimkabithi kikombe Afisa masoko na biashara wa Airtel ,
Emmanuel Raphael mara baada ya kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel
kuibuka mshindi wa pili  katika maonyesho ya Biashara ya Afrika
Mashariki ya mwaka huu.  Katika maonyesho hayo Airtel ilipata makombe
manne katika vipengele mbalimbali ikiwemo, Mtoa huduma bora , Mtoa
huduma bora katika sekta ya mawasiliano,  ubora katika mawasiliano ya
habari na tecknologia  pamoja na mshindi wa pili wa maonyesho kwa
mwaka huu. Akishuhudia (katikati) ni mwenyekiti wa Tanzania Chamber of
Commerce , Industrial and Agriculture Elibariki Mmari

Afisa masoko na biashara wa Airtel, Emmanuel Raphael katika picha na
makombe mara baada ya kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kuibuka
washindi katika vipengele mbalimbali katika maonyesho Biashara ya
Afrika Mashariki ya mwaka huu

Wafanyakazi wa Airtel kwa pamoja wakiwa na makombe yao mara baada ya
kukabithiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya viwanda na Biashara Uledi
Abbas Musa mara baada ya kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kuibuka
washindi katika vipengele mbalimbali katika maonyesho Biashara ya
Afrika Mashariki ya mwaka huu


·         Yazawadiwa vikombe vinne vya ubora wa huduma na bidhaa.
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imepokea
vikombe vinne katika maonyesho ya Biashara ya Afrika Mashariki kufatia
ubora wake katika kutoa huduma na bidhaa za kibunifu kwa wateja wake.

Maonyesho haya ya Biashara ya Afrika Mashariki ni maarufu kwa
kuonyesha aina mbalimbali za bidhaa ikiwemo bidhaa za matumizi ya
kawaida na ya viwanda, huduma, mashine na teknologia.  Na maonyesho
haya yametoa fulsa ya kukutanisha wadau pamoja na kubadilishana uzoefu
wa kibiashara na kuwawezesha ushirikiano wa biashara  katika nchini za
ukanda wa mashariki.

Akiongea wakati wa halfa hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na
Biashara, Uledi Abbas Musa alisema” Maonyesho haya yana lengo la
kuwapatia makampuni yaliyoko katika ukanda wa Afrika ya Mashariki
fulsa ya kujitangaza na kukuza biashara zao lakini pia kuwapatia
nafasi ya kuboresha mahusiano ya kudumu na wateja wao. Leo najisikia
furaha kuwazawadia kampuni ya simu za mkononi ya Airtel  kwa kuonyesha
ubora wake katika huduma, bidhaa, tecknologia za kibunifu na kwa kuwa
washindi wapili katika maonyesho  ya mwaka huu”
Aliongeza kwa kusema” Airtel imedhihirisha dhamira yake ya kutoa
huduma za kibunifu na za uhakika za mawasiliano ya simu za mkononi na
kutokana na hilo tumeona ni muhimu kuwapongeza na kuwazawadia kwa
jitihada zao”

Kwa upande wake Afisa Masoko na bidhaa wa Airtel , Bwana Emmanuel
Raphael alisema” huu ni mwaka watano mfululizo sasa kwa Airtel
kushiriki katika maonyesho haya tukuwa na lengo la kufikia wateja wetu
, kutoa elimu ya huduma na bidhaa tunazotoa pamoja na kuboresha
mahusiano nao. Maonyesho haya pia yamekuwa ni fulsa muhimu kwetu
kuonyesha bidhaa na huduma zetu za kibunifu na za kisasa na pia ni
nafasi pekee ya kushikiana na makampuni mengine yanayoshiriki kila
mwaka”.

“Napenda kuwashukuru waandaaji wa maonyesho haya kwa kutambua na kuona mchango wetu na tunahaidi kuendelea na dhamira yetu ya kutoa hudumabora na za kibunifu zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu.” 

AliongezaRaphael Katika halfa hiyo, Airtel ilipokea makombe manne ya ubora katikavipengele vya  namba moja kwenye kutoa huduma, namba moja katika sektaya mawasiliano, namba moja katika teknologia ya mawasiliano ya habarina namba mbili katika maonyesho ya mwaka huu. 

Nchi zilizo shirikikatika maonyesho ya mwaka huu ni pamoja na Tanzania, Kenya, Uganda,Rwanda and Burundi
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images