Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

MTOTO HAPPY LIMWAMWA (9-10) AKIMBIA KIPIGO ALIPOKUWA AKIFANYA KAZI ZA NDANI NJOMBE

$
0
0
  Happy  Limwamwa (9-10) Pichani.
   Happy  Limwamwa 9-10 (kushoto) akizungumza kwa uchungu  kwa Msaidizi wa Kisheria Geophrey Kaduma, (wapili kulia) kwa manyanyaso aliyokuwa akiyapata toka kwa mama aliyekuwa amemtowa kwao Wilaya ya  Mbinga Mkoa wa Ruvuma, kwa malengo ya kufanya kazi za ndani, ndipo alipokutana na kichapo toka kwa mama huyo na mume wake na kumfanya akimbiye na kuishi mitaani.

Happy ambaye  ameokotwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bryceson Mgaya wa Mtaa wa Kambarage Kata ya Njombe Mjini  Wilaya  ya Njombe Mkoa wa Njombe, Pamoja na Mwenyekiti huyo kutowa taarifa katika kituo cha Polisi na kumtembeza katika mitaa tofauti alipokuwa akifanya kazi  zaidi ya wiki 3  bado juhudi yoyote haijazaa matunda kwa  mtoto huyo kurudishwa kwao, kwa yoyote anaye weza kumfaham mtoto huyo awasiliane na Mwenyekiti huyo wa Mtaa, 0766336403, Mwenyekiti wa Kituo cha Sheria Geophrey Kaduma, 0759601915-o655601915. wapili kushoto ni Katibu wa Kituo cha Msaidizi wa Kisheria Magy Mtalla na wakwanza kulia ni mke wa mwenyekiti wa Mtaa wa Kambarage Matha Maiseli (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
 Katibu wa Kituo cha Msaidizi wa Kisheria Magy Mtalla, akizungumza na mtoto huyo Happy  Limwamwa 9-10
Happy  Limwamwa 9-10 akiwa katika picha

AIRTEL FURSA YAENDELA KUINUA VIJANA HAPA NCHINI

$
0
0
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia),
akimkabidhi kijana Iddy Abdallah Chilumba, msaada wa mashine ya
kubangulia korosho vikiwemo meza, vifaa mbalimbali na pikipiki mpya,
kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla
iliyofanyika kwenye sehemu yake ya biashara iliyokarabatiwa na Airtel
katika Mtaa wa Relwe, Manispaa ya Mtwara jana. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Airtel Mtwara, Bartholomew Masatu (wa pili kushoto), Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Happy John (wa tatu kushoto) na Afisa
Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki.
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia),
akimkabidhi kijana Iddy Abdallah Chilumba, msaada wa vifaa mbalimbali
vya kubangulia korosho na pikipiki mpya, kupitia mpango wa Airtel
‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla iliyofanyika kwenye sehemu yake ya
biashara iliyokarabatiwa na Airtel katika Mtaa wa Relwe, Manispaa ya
Mtwara jana. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Airtel Mtwara, Bartholomew
Masatu (wa pili kushoto), Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Happy 
John (wa tatu kushoto) na Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio 
Kaniki.
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia),
akimkabidhi kijana Iddy Abdallah Chilumba, msaada wa pikipiki mpya
vikiwemo vifaa mbalimbali vya kubangulia korosho, kupitia mpango wa
Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla iliyofanyika kwenye sehemu
yake ya biashara iliyokarabatiwa na Airtel katika Mtaa wa Relwe,
Manispaa ya Mtwara jana. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Airtel Mtwara,
Bartholomew Masatu (wa pili kushoto), Meneja wa Huduma kwa Wateja wa
Airtel, Happy John (wa tatu kushoto) na Afisa Uhusiano na Matukio wa
Airtel, Dangio Kaniki.
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia),
akimkabidhi kijana Iddy Abdallah Chilumba, kadi ya pikipiki mpya
iliyotolewa msaada kwake vikiwemo vifaa mbalimbali vya kubangulia
korosho, kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla
iliyofanyika kwenye sehemu yake ya biashara iliyokarabatiwa na Airtel
katika Mtaa wa Relwe, Manispaa ya Mtwara jana. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Airtel Mtwara, Bartholomew Masatu (wa pili kushoto), Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Happy John (wa tatu kushoto) na Afisa
Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki.

Airtel Fursa Yaendela Kuinua Vijana hapa Nchini
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imemuwezesha mjasiriamali Idd
Chillumba vifaa vya kufanikisha shughuli zake za kufungasha Korosho
ikiwa ni pamoja na usafiri wa kuwezesha kusambaza bidhaa zake kwa
wateja wake kupitia mpango wake wa Airtel Fursa ambapo vitamuwezesha
kuinua maisha yake na familia yake.

Akikabidhi vifaa hivyo meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel Bi Hawa
Bayumi amesema, vifaa hivyo vitamuwezesha Bw. Chillumba kuendeleza
biashara yake ya kufungasha Korosho na kusambaza kwa uharaka zaidi kwa 
wateja wake.

Bi Bayumi amesema, mpango huo wa kuwawezesha wajasiriamali vifaa ni
sehemu ya mpango wa kampuni hiyo wa kuwawezesha vijana wenye malengo 
mazuri na maisha yao, tabia nzuri, na wenye dhamira ya kujikomboa 
kimaisha na kuwa wafanyabiashara wakubwa hapo baadae.

“Sisi kama kampuni ya mawasiliano tumeona ni vizuri kushirikiana na
vijana ili kuhakikisha tunawawezesha na kukuza mitaji yao ya biashara
na kuweza kujiinua kiuchumi, kuweza kufikia ndoto zao na vile vile
kuongeza ajira kwa vijana hapa nchini” alisema meneja huyo.

“Vifaa hivi vitamuwezesha bw. Chillumba kuongeza biashara yake na
kupanua wigo wa kutoa huduma kwa wateja wake na  usafiri huu wa
pikipiki utampa nafuu ya kusafirishia bidhaa zake kutoka sehemu moja
kwenda nyingine.” aliongeza Bi Bayumi.

Akipokea msaada huo Bw. Chillumba ameshukuru kwa vifaa na usafiri huo
na kuahidi kuendeleza zaidi biashara hiyo ili kutimiza ndoto zake za
kuwa mfanyabiashara mkubwa.

“Sikuamini kama siku moja ningeweza kufikia malengo yangu katika
biashra hii. Mimi ni mtoto wa kwanza katika familia yetu.  Nilizaliwa
miaka ishirini na nne iliyopita. Baba yangu alifariki nikiwa na umri
wa mwaka mmoja. Mama yangu hakuwa na uwezo wa kunifikisha mbali
kielimu hivyo niliishia kidato cha nne.

 Ilinilazimu kuanza maisha
mapema kwa kuanzisha biashara ya kubangua korosho,  fedha ninayopata
japokuwa ni kidogo naitumia kujikimu mimi mwenyewe, kumsaidia mama
yangu na ndugu zangu. Kutokana na msaada huu kutoka Airtel, naahidi
kuongeza juhudi na kutumia vyema msaada huu ili kuhakikisha nakuza na
kuendeleza biashara yangu na kuinua vijana wenzangu hapo baadae”
alisema Chillumba.

Kampuni ya simu ya Airtel inazunguka nchi nzima kukutana na vijana kwa
lengo la kuwapa elimu ya ujasiriamali na asha kutoa uwezeshaji kwa

vijana ili waweze kukuza mitaji yao.

LAPF WATOA TAHADHARI KWA WASTAAFU

$
0
0
  RPC wa Mkoa wa Dodoma SACP. David A. Misime akiongea na waandishi wa Habari leo akitoa tahadhari juu ya matapeli wanaowadanganya na kuwatapeli wastaafu. LAPF kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma imefanikiwa kumkamata mtu mmoja na kumfikisha Mahakamani baada ya kujifanya ni mtumishi wa TAMISEMI, LAPF na OFISI YA KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA na kufanikiwa kuwaibiwa fedha kwa njia ya mtandao wastaafu kutoka katika mikoa mbalimbali.
   Mkurugenzi wa Huduma kwa Wanachama wa LAPF Bw. Valerian Mablangeti akitoa ufafanuzi katika mkutano huo na waandishi wa habari.
Baadhi ya washiriki.
MFUKO WA PENSHENI WA LAPF

  
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 02.09.2015
          MFUKO wa Pensheni wa LAPF unapenda kutoa kutoa tahadhari hasa kwa Wastaafu au wanaotarajia kustaafu, Idara, Wizara zote zinazoshughulika na wastaafu, Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri kujihadhari na watu wanaowapigia simu na kujitambulisha kuwa wao ni watumishi wa Mashirika ya Hifadhi za Jamii na Idara zingine za Serikali na kwamba wanashughulika na mafao ya wastaafu.


          LAPF inatoa tahadhari hiyo kwa sababu kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma tumefanikiwa kumkamata mtu mmoja kwa jina la DAVID MAGESA MAKALI @ PETER MABULA na kumfikisha Mahakamani baada ya kujifanya ni mtumishi wa TAMISEMI, LAPF na OFISI YA KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA na kufanikiwa kuwaibiwa fedha kwa njia ya mtandao wastaafu kutoka katika mikoa mbalimbali.


          Wanachofanya watu hao wanapiga simu Idara mbalimbali na kujifanya wapo TAMISEMI au Wizara nyingine na kuwataka wawatumie orodha ya wastaafu wa mwaka fulani pamoja na namba zao za simu. Inaonyeha kwa njia hiyo wameweza kupata orodha ya wastaafu takriban kutoka katika Mikoa 15 hususan kutoka Idara ya afya. 

Wakishapata orodha ya majina ya wastaafu na namba zao za simu humpigia mstaafu na kujitambulisha anatokea Wizarani na anashughulikia wastaafu ambao inaonekana walipunjwa kwenye mafao yao na inaonyesha naye amepunjwa kiasi cha milioni fulani. 

Ili aweze kumsaidia kurekebisha kumbukumbu na kumwezesha kupata fedha hizo amtumie kiasi fulani cha fedha. Mstaafu huyo akishamtumia hapatikani tena kwenye hiyo namba aliyotumia na mstaafu huyo anakuwa ameishaibiwa fedha zake.


          LAPF inatoa tahadhari kwa wastaafu wasikubaliane na watu wa aina hiyo na idara mbalimbali zichukue tahadhari kubwa na kila mara wahakikishe kinachohitajika kinatoka katika idara husika na kwa mtu sahihi.


Mfuko wa Pensheni wa LAPF unaendelea kutoa huduma bora kwa wanachama na wastaafu wake na katika kuhakikisha kuwa tunamlipa jana mstaafu wa kesho. LAPF inawakumbusha wanachama wake wanaokaribia kustaafu kuwasilisha mapema maombi ya mafao ya kusataafu (miezi sita kabla ya kustaafu) ili tuweze kuandaa mafao mapema.

         

LAPF ni Mfuko wa Pensheni ambao  pamoja na majukumu mengine, jukumu lake kuu ni kutoa mafao ya Pensheni kwa wanachama wake. Mafao yanayotolewa na LAPF ni pamoja na;

·        Pensheni ya Uzeeni.

·        Pensheni ya Ulemavu.

·        Pensheni ya Urithi.

·        Fao la Uzazi.

·        Mikopo ya kujikimu.

·        Mikopo ya elimu .

·        Mikopo ya nyumba.

·        Mikopo kwa wanachama wa kupitia Saccos.

·        Mikopo kwa Wastaafu.na

·        Msaada wa mazishi.

Kwa sasa Mfuko wa pensheni wa LAPF unaandikisha wanachama kutoka sekta zote kama vile Waalimu, Watumishi wa Afya, Wajasiliamali nk.


Imetolea na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF 

BENKI YA EXIM YASAINI MAKUBALIANO NA TAASISI YA FEDHA YA UJERUMANI ILI KUINUA BIASHARA NCHINI.

$
0
0
BENKI ya Exim Tanzania imesaini makubalino ya mkopo wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 20 (takribani 42bn/-) na kampuni binafsi ya ukopeshaji ya nchini Ujerumani, Deutsche Investitions und Entwicklungsgesellschaft  MBH (DEG), lengo likiwa ni kusaidia kuinua sekta ya biashara ndogo hapa nchini(SMEs).

Kwa mujibu wa Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya hiyo, Bw. Selemani Ponda  fedha hizo zilizo katika mfumo wa  mkopo mkubwa, zitatolewa kwa awamu mbili kwa kuzingatia maendeleo ya ukuaji katika kusaidia  sekta hiyo.

“Mkopo huu mkubwa unakuja wakati muafaka ambapo uchumi unazidi kuimarika huku tukishuhudia mapinduzi makubwa ya kibiashara. Biashara ndogo zinafanya jitihada za kila namna viingie katika kundi la kati. 

Huu ni wakati sahihi kwa benki yetu kuongeza nguvu katika sekta hii,” alisema Bw. Ponda katika taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam mwishoni mwa juma lilipita.

Alisema kuwa benki hiyo imeendelea kuwekeza katika kufanya tafiti na kuelewa mahitaji ya wafanyabiashara wadogo hapa nchini jambo lililoiwezesha benki hiyo kubuni bidhaa na huduma zinazokidhi mahitaji ya viwanda hivyo.

Kwa mujibu wa kumbukumbu za benki hiyo hadi kufikia sasa imekopesha jumla ya Tsh. 582bn/- huku 291bn/- kati ya kiasi hicho zikiwa zimetolewa kwa sekta ya biashara ndogo na zile za kati.

Bw. Ponda alisema kuwa benki hiyo inaona fursa ya kipekee kutoa mikopo katika sekta hiyo muhimu  wakati ambapo kuna maendeleo makubwa ya kiuchumi nchini.

Alibainisha kuwa benki hiyo, kwa zaidi ya muongo mmoja, imeendelea kuimarisha uhusiano mzuri na taasisi za kimataifa za kufadhili maendeleo ikiwa ni pamoja na IFC, PROPARCO, NORFUND na FMO. 

 “Kwa kusaini makubaliano haya na DEG, inadhihirisha jinsi ambavyo taasisi hizi za kimataifa za kufadhili maendeleo zina imani na benki yetu,” alisema kwa kujiamini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa taasisi za fedha barani Afrika na Amerika Kusini kutoka kampuni hiyo ya DEG Bi. Gudrun Busch alisema mkopo huo utasaidia kuongeza nguvu katika kuleta maendeleo kwenye sekta ya biashara  ndogo  na za kati kote nchini  na utasaidia kutatua changamoto mbalimbali katika ukuaji wa uchumi,



“Kwa kufanya hivi, tutakuwa tumechangia katika kuimarisha sekta ya uchumi nchini Tanzania na kutengeneza na kulinda ajira,’’ aliongeza.

KUCHAMGUA RAIS DINI NA UTAJIRI SI VIGEZO MUHIMU KWA WAPIGA KURA DAR ES SALAAM

$
0
0

ASILIMIA 46 ya wananchi wameripoti kuwa sera ndio kigezo muhimu watakachokitumia kumchagua Rais. Vigezo vingine vilivyotajwa na wananchi wengi ni uadilifu na maadili (17%). Hakuna mtu hata mmoja aliyetaja dini au utajiri kama kigezo muhimu cha kumchagua Rais na kigezo cha umri kilitajwa na asilimia moja tu ya wananchi.

Matokeo haya yametolewa na Twaweza kwenye muhtasari wa utafiti wenye jina la Je, Wanajua? Takwimu kuhusu uelewa wa wapiga kura. Muhtasari umetokana na Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaofanyika mara kwa mara kwa njia ya simu za mkononi. Matokeo yametokana na takwimu zilizokusanywa kwa wahojiwa 1,335 kutoka Tanzania Bara (Zanzibar haikuhusishwa) kati ya tarehe 12 na 26 mwezi Juni 2015.

Aidha, wananchi wanaamini kuwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 utakuwa huru na wa haki - asilimia 82 wanaamini kwamba maamuzi yao yataheshimiwa. Hata hivyo, asilimia 18 wanafikiri kuwa viongozi walio madarakani watavunja sheria ili washinde. 

Asilimia 65 ya wananchi wanaamini kwamba mgombea mwenye sera nzuri atamshinda yule mwenye pesa nyingi. 

Katika suala la vyombo vya habari, asilimia 76 ya wananchi wanaamini kwamba vyombo hivyo vitaripoti kwa usahihi masuala yanayohusu uchaguzi mkuu, wakati asilimia 24 wanafikiri kuwa vyombo vya habari vitakuwa na upendeleo kwa sababu ya motisha ya fedha.

Pamoja na matumaini haya, wananchi wana wasiwasi kuhusu uwezekano wa machafuko na vurugu wakati wa uchaguzi mkuu. Hili ni jambo linalowatia shaka asilimia 54 ya wananchi (Twaweza haikukusanya takwimu kuhusu nani anaweza kuwa chanzo cha vurugu hizo). Asilimia 18 walishawahi kushuhudia vurugu kwenye vituo vya kupigia kura wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka 2014 (Sauti za Wananchi, awamu ya 30, uliofanyika mwezi Februari-Machi 2015).

Wananchi wanafahamu sheria muhimu zinazosimamia mwenendo wa vyama vya siasa wakati wa kampeni. Asilimia 75 ya wananchi wanafahamu kwamba wagombea hawaruhusiwi kugawa fedha kwa wapiga kura ili wawachague. Na asilimia 79 wanaelewa kwamba wagombea hawaruhusiwi kutoa vyakula na vinywaji katika mikutano ya kampeni. Hata hivyo, asilimia 60 ya wananchi hawajui kuwa wagombea vinatakiwa kutunza kumbukumbu za fedha na michango walizopokea na jinsi zilivyotumika.

Pia, asilimia 62 wananchi wanaijua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kupitia kazi zinazofanywa na tume hiyo. Hata hivyo, asilimia 51 wanaamini NEC ina uwezo wa kusimamia uchaguzi huru na wa haki mwaka 2015. Vile vile walipoulizwa kuhusu vipengele mahususi vya utendaji wa NEC kwenye uchaguzi wa mwaka 2010, nusu ya wananchi waliridhishwa na utoaji elimu kwa wapiga kura (49%), usahihi wa matokeo (54%) na mwenendo wa wafanyakazi wa tume (52%).

Aidan Eyakuze, Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza alisema "Kuna mengi ya kufurahia kuhusu uelewa wa wananchi juu ya wajibu wao wa kiraia kama wapiga kura. Kwanza, ni dhahiri kabisa kwamba Watanzania wanalenga sera zaidi kuliko haiba ya wagombea. Pili, wananchi wana matumaini kuwa uchaguzi utafanyika katika hali ya uhuru na haki, ingawa wana wasiwasi kwamba vurugu inaweza kutokea. Tatu, ni jambo la kufurahisha zaidi kuona wananchi  wakifahamu kuwa kupewa fedha, chakula au vinywaji ili wamchague mgombea ni kosa.


Ujumbe unaotolewa hapa kwa wagombea ni kwamba, ni lazima wajenge hoja kwa wapiga kura zinazolenga kuboresha huduma za jamii, badala ya kujikita kwenye tabia za watu binafsi. Wananchi wanataka mijadala makini kuhusu sera mbadala, ili waweze kufanya maamuzi sahihi kati ya sera hizo zinazoshindana. Hii ni changamoto mpya na inayotia hamasa kwa kila mtu –wagombea, waandishi wa habari na  wananchi wenyewe kama wapiga kura."

WATUMISHI WA UMMA WA MKOA WA MBEYA NA NYANDA ZA JUU KUSINI WATAKIWA KUJIENDELEZA KUPITIA TAWI LA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TANZANIA TAWI LA MBEYA

$
0
0

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,HAB Mkwizu, akizungumza wakati wa mahafali ya 22 ya Chuo cha Utumishi Tanzania (TPSC) na ya kwanza kwa tawi la Mbeya hivi karibuni Jijini Mbeya.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,HAB Mkwizu akimtunuku mmoja wa wahitimu wa mafahali  ya 22 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) na ya kwanza  kwa tawi la Mbeya.




Sehemu ya wahitimu wa Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Tawi la Mbeya wakiwa katika mahafali ya 22 ya Chuo hicho na ya kwanza kwa tawi la Mbeya.
Wahitimu wakiandamana chuoni hapo kuelekea kwenye mahafali
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,HAB Mkwizu akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuwasili Chuo  Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) tawi la Mbeya kwa ajili ya mahafali ya 22 ya chuo hicho na ya kwanza kwa tawi la Mbeya hivi karibuni
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,HAB Mkwizu akiwasili Chuo  Cha Utumishi wa Umma  Tanzania (TPSC) tawi la Mbeya  kwa ajili ya mahafali ya 22 ya chuo hicho na ya kwanza kwa tawi la Mbeya hivi karibuni
Chuo Cha Utumishi Tanzania (TPSC) tawi la Mbeya (Picha kwa hisani ya www.inocomm.blogspot.com)           

WAOMBAJI MIKOPO WAISHUKURU HESLB KUWAPA FURSA KUREKEBISHA TAARIFA ZAO

$
0
0
 Afisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Ezra Ndangoya akimwelekeza sehemu ya kuweka sahihi Bw. Sironga Lowassa (kulia) ambaye ni mwombaji wa mkopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 katika ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam leo (Jumatano, Septemba 2, 2015). HESLB inaendelea na kazi ya kurekebisha taarifa za wanafunzi waliokosea kujaza fomu zao za maombi.
 Afisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bi. Zahra Kitara (kushoto) akipokea viambatanisho vya maombi ya mkopo kutoka kwa Bw. Paul Yahhi (kulia) mwombaji wa mkopo ambaye fomu yake ya maombi ilikosekana baadhi ya viambatanisho jijini Dar es Salaam leo (Jumatano, Septemba 2, 2015). HESLB inaendelea na kazi ya kurekebisha taarifa za wanafunzi waliokosea kujaza fomu zao za maombi. 
 Maafisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) (kulia) wakiwahudumia waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao fomu za maombi zimegundulika kuwa na upungufu jijini Dar es Salaam leo (Jumatano, Septemba 2, 2015). HESLB inaendelea na kazi ya kurekebisha taarifa za wanafunzi waliokosea kujaza fomu zao za maombi.
 Afisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bi. Christina Chacha (kulia) akimwelekeza jambo mwombaji wa mkopo ambaye fomu yake ya maombi ilikosekana baadhi ya viambatanisho jijini Dar es Salaam leo (Jumatano, Septemba 2, 2015). HESLB inaendelea na kazi ya kurekebisha taarifa za wanafunzi waliokosea kujaza fomu zao za maombi. (Picha na Eline Maronga-HESLB)
  
Na Eline Maronga 
WAOMBAJI wa mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao fomu zao za maombi zimegundulika kuwa na upungufu wameipongeza Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kwa kuwapa fursa ya kufanya marekebisho.


Mwishoni mwa wiki iliyopita HESLB ilitangaza orodha ya waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao fomu za maombi ziligundulika kuwa na upungufu na kuwataka waombaji kufika katika ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam na kufanya marekebisho kabla au ifikapo tarehe 11 Septemba mwaka huu (2015).


Wakiongea katika ofisi za Bodi leo (Jumatano, Agosti 2, 2015), waombaji hao wamesema hatua hiyo ya Bodi imewawezesha kurekebisha fomu zao katika maeneo waliyokosea na hivyo kuweka kumbukumbu zao sawa.


“Mimi ninaishi Arusha na nilipata taarifa kupitia magazetini na nikatembelea tovuti ya Bodi na kuona jina langu kuwa sikuweka sahihi… nikaamua kuja na sasa nimeweka sahihi,” amesema Bw. Sironga Lowassa leo nje ya Ofisi za HESLB.




Naye Bi. Enid Mneney, ambaye ni mhitimu wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari St. Mary Goreth iliyopo Moshi, anasema baada ya kuona jina lake katika tovuti ya Bodi, aliamua kwenda katika ofisi za Bodi ambako alifanikiwa kuweka sahihi.


“Mimi niliona jina langu kwenye tovuti kuwa sikuweka sahihi yangu, nimekuja na tayari nimeweka sahihi …ninashukuru kwa kupata fursa hii,” amesema Bi. Mneney mara baada ya kurekebisha taarifa zake katika ofisi za Bodi, eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bodi mwishoni mwa wiki iliyopita, jumla ya fomu za waombaji wa mikopo 7,788 kati ya 68,445 zilizopokelewa na kuhakikiwa zimegundulika kuwa na upungufu na kuwataka waombaji kusoma majina yao katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz).


Kwa mujibu wa taarifa hiyo, taarifa muhimu zinazokosekana ni pamoja na sahihi za waombaji, nakala za vyeti vya kuzaliwa vya waombaji, sahihi na picha za wadhamini na baadhi ya fomu za maombi kutosainiwa na wanasheria na maafisa wa serikali za mitaa kama maelekezo yanavyotaka.

KITENGE ATEULIWA KUWA BALOZI WA STARTIMES

$
0
0
Mtangazaji wa michezo wa Kituo cha Radio cha E-FM 93.7 , Maulid Kitenge ameteuliwa na kampuni ya StarTimes kuwa balozi wa kampuni hiyo katika hafla fupi ya kumtambulisha Kitenge kuwa Balozi mpya wa StarTimes iliyofanyika makao makuu ya Kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam.

WANAMUZIKI WAANZA KUPATA BIMA YA AFYA

$
0
0
Mwaka 2004, John Kitime ambaye kwa sasa ndie Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (Tanzania Musicians Network-TAMUNET) alihudhuria Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Muziki Duniani –International Federation of Musician (FIM). Katika mkutano huo moja ya maazimio ya mkutano ule ilikuwa kila nchi ihakikishe inaanzisha utaratibu wa Bima ya Afya kwa wanamuziki wake. 

Mara baada ya kurudi Tanzania, kwa kushirikiana na viongozi wengine wa TAMUNET, Kitime alianza kufuatilia uwezekano wa kupata huduma ya Bima hiyo kwa wanamuziki.

 Kwa bahati mbaya hakukuwa na njia yenye gharama nafuu ya malipo ya Bima hiyo ambayo mwanamuziki wa kawaida angeweza kuyamudu. 

Kulikuwepo na kampuni ambayo iliweza kutoa huduma hiyo kwa gharama ya dola 300 kwa mwaka kwa mwanamuziki mmoja,kampuni nyingine za bima zilizotembelewa hazikuonyesha ushirikiano katika jambo hilo. 

TAMUNET iliwasiliana pia na mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa katika kipindi hicho mfuko ulikuwa hauna mamlaka ya kuhudumia watu waliokuwa nje ya ajira ya serikali na mashirika ya umma. 

TAMUNET iliwasiliana na Mganga Mkuu wa Serikali, ambaye alishauri TAMUNET kuwasiliana na NGO moja ambayo ilikuwa na makao yake makuu Sinza, na kweli NGO hiyo ilikubali kuwa ingeweza kutoa huduma ya Bima ya Afya kwa wanamuziki kwa gharama ya shilingi 3000/- tu.

kwa mwezi, lakini huduma hii ilikuwa ni kwa hospitali kadhaa tu jijini Dar es Salaam, lakini lilionekana ni bora kuliko kukosa kabisa, lakini muda mfupi baadae NGO hiyo ilisema haishughuliki tena na huduma hiyo bali imeelekeza nguvu zake kwa watoto wa mtaani. 

Hapo ilifuatia miaka kadhaa ambayo hakukuweko na njia yoyote iliyowezekana ya kupata huduma hiyo, TAMUNET ilijaribu pia kuwasiliana na mifuko mingine, lakini kila mara iligonga ukuta aidha kwa ahadi ambazo zilikuwa zikipigwa kalenda bila kutekelezwa.


Mwaka 2015 hatimae ndipo mlango umefunguka, Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa NHIF, uliitarifu TAMUNET kuwa umeanzishwa mpango wa Bima kwa Kikoa ambao ungewawezesha wanamuziki nao kupata Bima ya Afya kwa gharama nafuu.

 TAMUNET iliuchangamkia mpango huo kwa kuwa imekuwa na ajenda ya chama hiki kwa miaka zaidi ya kumi.



Wanamuziki wanachama wa TAMUNET tayari wameanza kufaidi huduma ya bima ya Afya kwa mwaka mzima, hii ni baada ya kulipia shilingi 76,800/-Mpango huu utaondoa aibu ya wanamuziki kuchangiwa fedha za matibabu kila wanapougua, kwani itakuwa busara kwa wapenzi na washabiki wa muziki kuchangia mwanamuziki wanaempenda apatiwe Bima ya Afya kuliko kumchangia fedha za matibabu ya muda mfupi. 

Baadhi ya wanamuziki ambao tayari wana bima za afya chini ya mpango huu ni Louiza Nyoni, Abdul Salvador, Rashid pembe, na wengine wengi wamekwisha anza taratibu za kupata huduma hii.
Wasanii katika semina kuhusu BIma Ya Afya iliyofanyika BASATA karibuni
Mwezeshaji Catherine kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya akitoa maada katika semina ya wasanii kuhusu Bima ya Afya.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makond aliyekuwa mgeni rasmi katika semina ya Bima ya Afya kwa wasanii

Mwenyekiti wa TAMUNET akipokea kadi za kwanza za Bima ya Afya za wanamuziki, katika ofisi za Mfuko wa BIma ya Afya wa Taifa.
John Kitime akiwa na kadi yake ya Bima ya Afya aliyoipata hivi karibuni

Kadi za Bima ya Afya za wanamuziki mbalimbali.


Louiza Nyoni akionyesha kadi yake mpya ya Bima ya Afya
Ushirikiano wa Mfuko wa Bima ya Afya na TAMUNET unaweka uwezekano wa mwanamuziki kuanza kuchanga hata fedha kidogokidogo ili kuweza kufikisha kiasi kinachotakiwa.

 Wanamuziki wanaweza kupiga simu au kutuma ujumbe kwenye simu namba 0763722557 ili kupata maelezo ya namna ya kujiunga na huduma hii.

 Ukiwa mwanamuziki wa Hiphop, taarab, muziki asili, dansi bongofleva, huduma hii ni kwa ajili yako kumbuka WAJANJA HUJIWEKEA BIMA YA AFYA- NA WEWE NI MMOJA WA WAJANJA

RAIS JAKAYA KIKWETE ATUNUKU NISHANI MAOFISA 30 WA MAJESHI

$
0
0
 Baadhi ya Maafisa Waandamizi, Wakaguzi, Wakaguzi Wasaidizi, Stesheni Sajini, Sajini na Koplo wa Vikosi vya Majeshi ya Ulinzi na Usalama wakifuatilia masuala mbalimbali wakati hafla ya utoaji wa nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania, nishati ya utumishi wa muda mrefu na nishani ya utumishi wa muda mrefu na tabia iliyofanyika jana (Jumanne Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam.
  Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Asha-Rose Migiro (kulia) akifuatilia masuala mbalimbali wakati hafla ya utoaji wa nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania, nishati ya utumishi wa muda mrefu na nishani ya utumishi wa muda mrefu na tabia iliyofanyika jana (Jumanne Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi.
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akifuatilia masuala mbalimbali wakati hafla ya utoaji wa nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania, nishati ya utumishi wa muda mrefu na nishani ya utumishi wa muda mrefu na tabia iliyofanyika jana (Jumanne Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam.
  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania, Jenerali Adolf Mwamunyange (kushoto), Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Ernest Mangu na Kamishna Jerenali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Minja wakisoma ratiba ya hafla ya utoaji wa nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania, nishati ya utumishi wa muda mrefu na nishani ya utumishi wa muda mrefu na tabia iliyofanyika jana (Jumanne Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu msaafu Joseph Warioba wakisoma ratiba ya hafla ya utoaji wa nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania, nishati ya utumishi wa muda mrefu na nishani ya utumishi wa muda mrefu na tabia iliyofanyika jana (Jumanne Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama  Rais Dkt. Jakaya Kikwete akimtunuku ACP Vincent Mosses Karata nishani ya utumishi wa muda mrefu Tanzania katika hafla iliyofanyika ikulu Jijini Dar Es Salaam jana( Jumanne Septemba 1, 2015).


   Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Dkt. Jakaya Kikwete akimtunuku Brigedia Jenerali Jacob Gideon Kingu nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania katika hafla iliyofanyika ikulu Jijini Dar Es Salaam jana( Jumanne Septemba 1, 2015).
 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa majeshi ya vikosi vya Ulinzi na Usalama mara baada ya hafla ya utoaji wa nishani kwa Maafisa Waandamizi, Wakaguzi, Wakaguzi Wasaidizi, Stesheni Sajini, Sajini na Koplo wa Vikosi vya Majeshi ya Ulinzi na Usalama wakati wa hafla ya utoaji wa nishani ya utumishi uliotukuka Tanzania, nishati ya utumishi wa muda mrefu na nishani ya utumishi wa muda mrefu na tabia iliyofanyika jana (Jumanne Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam.
1   Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Dkt. Jakaya Kikwete akimtunuku ACP Bakari Namkaa Ndembo nishani ya utumishi mrefu Tanzania katika hafla iliyofanyika jana jumanne (Septemba 1, 2015) Ikulu Jijini Dar es Salaam.


(PICHA NA ISMAIL NGAYONGA- MAELEZO)

VODACOM YAMWAGA VIFAA VYENYE THAMANI YA MILION 4.9 KWA TIMU ZA LIGI KUU(VPL)2015/2016

$
0
0
 Baadhi ya waandishi wa vyombo vya habari mbalimbali nchini wakiwa kwenye hafla fupi ya kukabidhiwa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 4.9 kwa timu zote zinazoshiriki ligi kuu ya mpira wa miguu ya Vodacom Tanzania bara(VPL)leo vilivyokabidhiwa na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.
 Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa akiongea na waandishi wa habari na wawakilishi wa vilabu mbalimbali wa timu zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara,wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 4.9 kwa timu zote zinazoshiriki ligi hiyo leo vilivyokabidhiwa na mdhamini mkuu wa ligi kampuni ya Vodacom Tanzania,kushoto ni Meneja Masoko wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania,(TFF)Peter Simon.
 Vijana wakitambulisha jezi mpya za nyumbani na ugenini za timu ya African Sport ya Tanga na vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa msimu wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara 2015/2016 zilizokabidhiwa rasmi leo na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.
 Wanamitindo  wakipita kuitambulisha jezi mpya za nyumbani na ugenini za timu ya Majimaji na vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa msimu wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara 2015/2016 zilizokabidhiwa rasmi leo na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, Boniface Wambura(kushoto) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(watano toka kushoto)akiwa kwenye picha na mwakilishi wa timu ya Azam FC pamoja na wanamitindo  waliokuwa wakiitambulisha jezi mpya  za nyumbani na ugenini na vifaa mbalimbali vya timu ya Azam FC  vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara  2015/2016.Vifaa hivyo  vilikabidhiwa leo jijini Dar es Salaam na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, Boniface Wambura(kushoto) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(watano toka kushoto)akiwa kwenye picha na mwakilishi wa timu ya Coastal Union pamoja na wanamitindo  waliokuwa wakiitambulisha jezi mpya  za nyumbani na ugenini na vifaa mbalimbali vya timu hiyo vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara  2015/2016.Vifaa hivyo  vilikabidhiwa leo jijini Dar es Salaam na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.


 Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania,Boniface Wambura(kushoto) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(watano toka kushoto)akiwa kwenye picha na mwakilishi wa timu ya Mbeya FC pamoja na wanamitindo  waliokuwa wakiitambulisha jezi mpya  za nyumbani na ugenini na vifaa mbalimbali vya timu hiyo vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara  2015/2016.Vifaa hivyo  vilikabidhiwa leo jijini Dar es Salaam na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania,Boniface Wambura(kushoto) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(watano toka kushoto)akiwa kwenye picha na mwakilishi wa timu ya Yanga sports club ya jangwani jijini Dar es salaam pamoja na wanamitindo  waliokuwa wakiitambulisha jezi mpya  za nyumbani na ugenini na vifaa mbalimbali vya timu hiyo vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara  2015/2016.Vifaa hivyo  vilikabidhiwa leo jijini Dar es Salaam na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania,Boniface Wambura na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanamitindo waliokuwa wakizitangaza jezi mpya za timu 16 zitakazoshiriki katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara 2015/2016 wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa jezi hizo na vifaa mbalimbali vyenye thamni ya zaidi ya shilingi milioni 4.9  na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania kwa timu zote zitakazoshiriki katika ligi hiyo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania,Boniface Wambura(kushoto) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(watano toka kushoto)akiwa kwenye picha na mwakilishi wa timu ya Simba Sports Club ya Msimbazi jijini Dar es Salaam pamoja na wanamitindo  waliokuwa wakiitambulisha jezi mpya  za nyumbani na ugenini na vifaa mbalimbali vya timu hiyo vyenye thamani ya shilingi Milioni 4.9 kwa ajili ya msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara  2015/2016.Vifaa hivyo  vilikabidhiwa leo jijini Dar es Salaam na mdhamini mkuu wa ligi hiyo kampuni ya Vodacom Tanzania.

KAMPUNI ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania, ambayo ni mdhamini mkuu wa Ligi kuu ya mpira wa miguu Tanzania bara leo imekabidhi vifaa kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo vyenye thamani ya shilingi milioni 490,000,000/=
Akikabidhi vifaa hivyo leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha  Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twissa,alisema kuwa  kwa mara nyingine tena katika kuhakikisha ligi ya soka nchini inaenda vizuri Vodacom inakabidhi  vifaa mbalimbali vya ligi ambavyo ni jezi mbalimbali, viatu vya mazoezi na mechi, soksi, vilinda ugoko, nguo za mazoezi, nguo za kawaida, gloves na vifaa vingine vingi vinavyohitajika.

“Tunajisikia furaha  kukabidhi vifaa hivi siku ya leo tukiwa tunatekeleza  matakwa ya mkataba wa udhamini, ni imani yetu kwamba timu zitakazoshiriki ligi zimejiandaa vya kutosha kwa msimu mpya wa ligi  wa 2015/2016”Alisema Twissa.


Twissa alisema Vodacom inaendelea kudhamini ligi kuu kwa sababu soka ni mchezo unaopendwa sana hapa nyumbani ukiwa na washabiki wengi hivyo inapenda kuona wananchi ambao baadhi yao ni wateja wake  wanapata burudani ya mchezo waupendao pia siku zote inaamini kuwa michezo ni ajira kubwa duniani kote,ikiendelezwa inaweza kubadilisha maisha ya watu wengi na taifa kunufaika kwa mapato makubwa ya kodi kutoka katika sekta hii.
Aliwataka wadhamini wengine kujitokeza ili kuboresha  zaidi ligi ya Tanzania na kuongeza  maslahi kwa wachezaji wanaoshiriki katika ligi “Tukiunganisha nguvu timu zetu zinaweza kuwa na wachezaji wa kimataifa pia ni muhimu  kwa wadau mbalimbali kuanza kuwekeza katika timu za vijana chipukizi kwa kuwa vipaji vinaanzia ngazi ya chini ambako vinapaswa kuibuliwa na kuendelezwa ”Alisema Twissa.
Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi,Boniface Wambura aliishukuru Kampuni ya Vodacom,  na kuvitaka vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Vodacom kuheshimu chapa ya mdhamini wakati wote wa mechi za ligi.
“Ninatoa mwito kwa vilabu  vyote kutumia jezi zenye nembo ya mdhamini katika kuhakikisha ligi inafanikiwa kama inavyotakiwa,”alisema.
Aliongeza kuwa  TFF isingependa kutumia kanuni na sheria kuadhibu klabu inayokwenda kinyume, bali kila klabu izingatie masharti ya mdhamini  kama ambavyo anavyotimiza haki yake ya kuwapatia vifaa.


Alisema ligi ya mwaka huu itakuwa bora kutokana na maandalizi yote  kukamilika mapema pia timu zitazoshiriki zimeziandaa vya kutosha kuhakikisha ligi inakuwa na msisimko na ushindani mkubwa.

MAMA SALMA KIKWETE ASHIRIKI KWENYE MAZISHI YA MDHAMINI WA TAASISI YA WAMA MAREHEMU HULDA KIBACHA

$
0
0
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete akipokewa na Mama Zakhia Meghji, Makamu Mwenyekiti wa WAMA wakati alipowasili nyumbani kwa Marehemu Mama Hulda Kibacha, Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA aliyefariki dunia tarehe 28.8.2015.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akishiriki kwenye ibada ya kumwombea Marehemu Hulda Kibacha, Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA iliyofanyika nyumbani kwa marehemu eneo la Ada Estate tarehe 2.9.2015. Aliyekaa kushoto kwa Mama Salma ni Mheshimiwa Zakhia Meghji na kulia ni binti wa marehemu Nampombe Kibacha.
 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mdhamini wa Taasisi ya WAMA Mama Hulda Kibacha aliyefariki dunia tarehe 28.8.2015 hapa Dar Es Salaam. Marehemu Kibacha aliwahi kufanya kazi Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).  
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka udongo kaburini ulimolazwa mwili wa Mama Hulda Kibacha aliyekuwa Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA. Marehemu Hulda Kikbacha alizikwa kwenye makaburi ya Kinondoni tarehe 2.9.2015.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (katikati) kwa kushirikiana na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro (kushoto) na Mama Zakhia Meghji (kulia) wakiweka shada la maua kwenye kaburi LA Marehemu Hulda Kibacha aliyezikwa katika makaburi ya Kinondoni tarehe 2.9.2015.


 Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Hulda Kibacha.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya WAMA, Ndugu Zakhia Meghji akitoa salamu maalum za Taasisi hiyo wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mdhamini na Mjumbe wa Bodi hiyo Marehemu Hulda Kibacha.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiaagana na Binti wa Marehemu Nampombe Kibacha mara baada ya Mazishi ya Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA, Mama Hulda Kibacha.
PICHA NA JOHN LUKUWI. 

MAGUFULI AFUNGA KAZI MJINI MTWARA

$
0
0
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli,akiwahutubia wananchi wa mji wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye mkutano wa kampeni unaoendelea jioni hii katika uwanja wa Mashujaa.
Wakazi wa mji wa Mtwara wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM,unaofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa CCM,wakimsikiliza mgombea Urais wa chama hicho Dkt John Pombe Magufuli.
 Mgombea Ubunge wa jimbo la Mtwara mjini,Murji Asnein Mohamed akiwasalimia maelfu ya wananchi wa mji wa Mtwara waliofurika kwenye uwanja wa Mashujaa kwenye mkutano wa kampeni za CCM,jioni ya leo ambapo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli anatarajia kuwahutubia wananchi hao 
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akijiachia jukwaani pamoja na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara,ambapo Dkt Magufuli anatarajia wakuwahutubia wananchi hao waliofurika kwa wingi.
  Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akijiachia jukwaani pamoja na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara,ambapo Dkt Magufuli anatarajia wakuwahutubia wananchi hao waliofurika kwa wingi.
 Wakazi wa mji wa Mtwara ambao wamejitokeza kwa wingi hivi sasa ndani ya uwanja wa Mashujaa, mjini Mtwara kumsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha CCM,Dkt John Magufuli
 Wananchi wakiwa wamekusanyika ndani ya uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara hivi sasa,kumsikiliza Dkt John Pombe Magufuli
  Wananchi wakiwa wamekusanyika ndani ya uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara hivi sasa,kumsikiliza Dkt John Pombe Magufuli.
Msanii wa Muziki wa Kizazi kimya,Ali Kiba akiimba mbele ya maelfu ya wananchi wa Mtwara jioni ya leo kwenye mkutano wa Kampeni wa CCM,ambapo Dkt John Pombe Magufuli anatarajia kuwahutubia.

RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA BIASHARA TANZANIA (TNBC) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi muda mfupi kabla ya kufungua na kuendesha mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi muda mfupi kabla ya kufungua na kuendesha mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
Katibu Mtendaji wa Baraaa la Biashara la Tanzania (TNBC) Bw. Raymond Mbilinyi akiongelea juu ya  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
 Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015.

 
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Washiriki wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015
  Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisoma muhtasari wa  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka akisoma hotuba kabla ya kumkaribisha Rais Kikwete Kufungua  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015.
  Rais Kikwete akifungua rasmi  mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015.
  Rais Kikwete akifungua rasmi mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015.

 Rais Kikwete akiongoza mkutano wa nane wa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka, Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi 

  Rais Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na secretariate ya TNBC  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka,
   Rais Kikwete katika picha ya pamoja na watumishi wa  TNBC  katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 2, 2015. Wengine toka kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi wa Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahaya Mzee, Mwenyekiti wa Tanzania Private Sector Foundation Dkt. Reginald Mengi Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue  na Karibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Florens Turuka, 
PICHA ZOTE NA IKULU

MMLIKI WA ST. MATHEW ACHOMOLEWA KESI YA TALAKA NA MGAWANYO WA MALI

$
0
0
court_gavel
Na Mwandishi wetu
MAHAKAMA ya Mwanzo Mbagala, Dar es Salaam imesema haiwezi kumuamuru Mmiliki wa nne za Shule za Sekondari, St Mathew na St Marks ,Thadei Mtembei kutoa talaka kwa Magreth Mwangu kutokana na ndoa yao kuwa batili.

Akisoma hukumu hiyo leo, Hakimu Rajab Tamambele alisema ndoa aliyofunga Mwangu pamoja na Mtembei ambayo ni ya kimila ni batili kwa kuwa mdai hakutoa cheti cha ndoa hiyo ilipofungwa.
Alisema kwa misingi hiyo, mahakama haiwezi kumuamuru Mtembei kutoa talaka kwani aliwasilisha cheti cha ndoa ya mke mmoja aliyoifunga mwaka 1985.
pia alisema mahakama hiyo haiwezi kugawa mali kama ambavyo mdai ameiomba mahakama, ambapo amesisitiza kuwa mgawanyo wa mali unatokana na ndoa halali ambayo baba na mama wanaishi pamoja.

‘’Mashahidi wote wameeleza kuwa Mtembei na Mwangu walikuwa wanakutana hoteli ya Sleep Inn. Kwa hivyo mahakama inaona kuwa uhusiano kati ya mdai na mdaiwa ulikuwa wa kimapenzi pekee au hawara na kwa lugha ya kistaarabu tunaita mzazi mwenzie,’’ aliongeza Tamambele.
Alifafanua kuwa kulipa mahari ambapo mdai aliieleza mahakama kuwa alitolewa ng’ombe watano, sio njia ya kufunga ndoa bali ni kuelekea kufunga ndoa.

Aliendelea kusema kuwa kitendo cha baba kupewa mahari akiwa peke yake bila ya kuwa na mzee wa kabila hilo kuthibitisha, sio sahihi katika sheria za ndoa.

Akisoma hukumu hiyo kwa saa moja, Hakimu Tamambele alisema kuwa watoto watatu kati ya Mtembei na Mwangu ni batili kwani wamezaliwa nje ya ndoa, hivyo mahakama haiwezi kuamuru watoto hao kupatiwa matunzo.

‘’Mdaiwa anatakiwa kushukuru kitendo cha mdai kujenga nyumba tatu kwa ajili ya watoto kwani wengine hawawezi kufanya kitu kama hicho. Kila mzazi anatakiwa kuwatunza watoto hao, ’’ alisema.

Akizungumzia kuwakilishwa kwa mdaiwa, alisema kwa mujibu wa sheria ya kama mdaiwa ni mgonjwa anaweza akawakilishwa ambapo mtoto wake, Peter ndiye alichukua nafasi ya kumuwakilisha baba yake.

Aidha, alisema haki ya kukata rufaa kwa mdai iko wazi na kwamba inatakiwa kukatwa kwa siku 45.

Katika kesi hiyo ambayo ilifunguliwa Juni 5, mwaka huu, Mwangu aliiomba mahakama kumuamuru mdaiwa kutoa talaka, matunzo ya watoto na ya machumo ya pamoja yenye thamani ya Sh milioni 800.

Alisema kesi hiyo ilikuwa na jumla ya mashahidi nane ambapo watano kutoka upande wa mdai na watatu upande wa mdaiwa.

Alisema mdai alifungua kesi kupitia ofisi ya Ustawi wa jamii na ilipoanza kusikilizwa mdai alisema walianza mahusiano mwaka 1995 ambapo walizaa watoto watatu na walijenga shule nne, nyumba pamoja na hoteli tatu za Dar es Salaam na Bukoba.

SUCCOS KUANZISHA MIRADI YENYE LENGO LA KULETA AMANI NCHINI

$
0
0
TAASISI ya Succos Dar es salaam Foundation imeanzisha miradi iliobeba ujumbe wa kudumisha amani, upendo na umoja nchini yenye lengo la kuwasaidia wahitaji mbalimbali ili kuondokana na umasikini nchini.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Meneja Mradi Deogratius Paso amesema kuwa kupitia miradi hiyo itaendesha semina mbalimbali ambazo zitasaidia kudumisha amani na kupunguza umasikini nchini hasa kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

 “Tumelenga mambo mbalimbali ambayo yatakua chachu ya kuendeleza amani nchini na kujikwamua na umasikini nchini ambapo taasisi yetu inatambua kuwa mdau wetu mkubwa ni Serikari ya Jamuhuli ya Muungano wa Tanzania na kupitia serikari za mitaa itatusaidia kuwatambua wahitaji” alisema Deogratius.

Deogratius alisema kuwa taasisi yake imelenga kuandaa tamasha la michezo lenye lengo la kujumuika na kushirikiana kwa umoja, kujenga uwezo wa kuwapa elimu waitaji mbalimbali na kupunguza umasikini kupitia ujasiliamali.

Kupitia ujasiliamali huo, kutakuwa na miradi mbalimbali ambayo itakuwa endelevu kwa kuwahamasisha vijana kushiriki katika Mkuu wa mwaka huu wa kuwachagua Rais, Wabunge na Madiwani na hatimaye kupata viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano itakayopewa ridhaa na wananchi wenyewe.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA MANUNUZI YA UMMA KWA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI JIJINI ARUSHA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua Kongamano la Manunuzi ya Umma kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, lililofunguliwa leo Sept 2, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC Jijini Arusha.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kuhusu kadi mpya ya Selcom ya kufanyia huduma ya manunuzi na malipo mbalimbali kutoka kwa Meneja wa Mradi wa Kampuni ya Selcom Tanzania, Gallus Runyeta, wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya maonesho baada ya kufungua Kongamano la Manunuzi ya Umma kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, lililofunguliwa leo Sept 2, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC Jijini Arusha. Kadi hiyo inatarajia kuzinduliwa rasmi mwezi Oktoba mwaka huu. Katikati ni Meneja Mawasiliano wa Selcom, Sabrina Munir. 


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kuhusu hudua za SSRA kutoka Afisa Mawasiliano wa SSRA, Sarah Kibonde,  wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya maonesho baada ya kufungua Kongamano la Manunuzi ya Umma kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, lililofunguliwa leo Sept 2, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC Jijini Arusha.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kuhusu hudua za Max Malipo kutoka kwa Samwel Nzunda, wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya maonesho baada ya kufungua Kongamano la Manunuzi ya Umma kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, lililofunguliwa leo Sept 2, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC Jijini Arusha.
 Picha za pamoja baada ya ufunguzi wa kongamano hilo.
 Picha za pamoja baada ya ufunguzi wa kongamano hilo.
 Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo, wakimsikiliza Makamu wa Rais, Dkt. Bilal.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya viongozi, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Philemon Luhanjo, baada ya uzinduzi wa Kongamano hilo. 
Picha na OMR

UKAWA KUWANUFAISHA WAKULIMA WA KOROSHO NA UFUTA MIKOA YA KUSINI

$
0
0
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji akiwasili katika jimbo la Mtama katika mkutano wa kampeni uliofanyika mkoani Lindi ambapo katika hoyuba yake aliwaambia wananchi wa mkoa wa Lindi kuwa endapo serikali ya Ukawa itaingia madarakani itaboresha bei ya ufuta na korosho ili kuwanufaisha wakulima wa zao hilo. (Picha na Francis Dande)
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji akihutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Mbunge wa jimbo la Mkanyageni, Habib Mnyaa akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Mbunge wa Lindi mjini akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Tunausapoti Ukawa.....
Mwenyekiti mstaafu wa CCM, John Guninita akizungumza wakati wa kampeni katika jimbo la Mtama mkoani Lindi. 
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji akisalimiana na mfuasi wa Ukawa wakati alipowasili katika mkutano wa kampeni katika jimbo la Mtama mkoani Lindi. 
Wafuasi wa Ukawa wakishangilia.
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema,Juma Duni Haji akiteta jambo na mbunge wa Mkanyageni, Zanzibar, Habib Mnyaa wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Mtama mkoni Lindi 
Mgombea Mwenza wa Ukawa kupitia Chadema,Juma Duni Haji akiteta jambo na mbunge wa Lindi mjini, Salum Barwani wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Mtama mkoni Lindi

Wafuasi wa Ukawa wakiwa na mabango yao.
Wafuasi wa Ukawa wakishangilia.
Wafuasi wa Ukawa wakishangilia.
Wafuasi wa mgombea wa Ukawa jimbo la Mtama kupitia Chadema, Seleman Mathew wakimsindikiza mgombea huyo huku wakiwa juu ya gari yake wakati akiwasili kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoni mkoani Lindi, uliohutubiwa na mgombea mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji. 
Wafuasi wa mgombea wa Ukawa jimbo la Mtama kupitia Chadema, Seleman Mathew wakimsindikiza mgombea huyo.
Wafuasi wa mgombea wa Ukawa jimbo la Mtama kupitia Chadema, Seleman Mathew wakimsindikiza mgombea huyo huku wakiwa juu ya gari yake wakati akiwasili kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoni mkoani Lindi, uliohutubiwa na mgombea mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji. 
Mgombea ubunge wa Ukawa jimbo la Mtama, Suleiman Mathew kupitia Chadema akiwa amebebwa juu na wafuasi wake wakati akiingia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Sokoni mkoani Lindi, uliohutubiwa na mgombea mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji. 
Mgombea ubunge wa Ukawa jimbo la Mtama, Suleiman Mathew kupitia Chadema akiwa amebebwa juu na wafuasi wake wakati akiingia katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Sokoni mkoani Lindi, uliohutubiwa na mgombea mwenza wa Ukawa kupitia Chadema, Juma Duni Haji. 
Mfuasi wa Ukawa akishangilia wakati wa mkutano wa kampeni katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Mgombea wa Ukawa kupitia Chadema katika jimbo la Mtawa, Suleiman Mathew.

MULTICHOICE AFRICA KICKS OFF THE BIGGEST CONTENT SHOWCASE IN AFRICA

$
0
0
D3A_2835
MC's during the official opening of MultiChoice Africa Content Showcase Extravaganza, IK (right) and Eku at the Outrigger Beach Resort in Mauritius.(Photos by MultiChoice and Zainul Mzige of Modewjiblog).

It was a magical night filled with #OnlyTheBest of African entertainment when MultiChoice Africa kicked off its second #OnlyTheBest Content Showcase Extravaganza in spectacular style at the Outrigger Resort.
The star-studded guestlist read like the who's who of Africa's entertainment and media.

The guests walked down the African media Walk of Fame onto a red-carpet that opened up to a sensational night of dazzling entertainment. The event, dubbed 'Night of a Thousand Stars' saw all the glitz and glamour of Hollywood, Bollywood and Nollywood come to life on the island paradise, as guests that include Genevieve Nnaji, Rita Dominic, Desmond Elliot and Ramsey Nuoah were given the full movie-star treatment.

 Flavour, Stonebwoy and The Mavins kept the guests on their feet with their popular hits while the night's MCs IK and Eku kept the glamorous proceedings running smoothly.Guest also experienced host IK who also brought his popular show, 'High Lites with IK', to the stage in Mauritius with a delightful interview with Nigerian crooner Banky W alongside music by DJ Sousa.
D3B_6272
Red carpet treatment for the guest #OnlyTheBest.
MultiChoice Africa's CEO Tim Jacobs also took to the stage to welcome guests with a promise that the video entertainment service provider will do all it can to make only the best content available to its subscribers on any platform, on any device and at any time.

“We believe television is an extremely powerful tool that can educate, entertain and inform. The evolution of this medium has become fast and furious and as a business we are constantly evolving to stay ahead,” said Jacobs at a glittering ‘Night of a Thousand Stars’ event. “MultiChoice’s business is built around three key pillars: people; content - in the form of great entertainment, news and sport - and the latest cutting-edge technology. Our mission is to ensure that our subscribers do not miss out on any of the stories, events or moments that are shaping our future.”
Jacobs lauded the success of MultiChoice’s GOtv DTT (Digital Terrestrial Television) offering, which currently operates in 8 countries, bringing low-cost digital television to homes and supporting governments in freeing up vital broadcast spectrum by switching from analogue to digital signal.
He also acknowledged the challenges which the business faces. “Our growth over the last 20 years has been a result of massive investments we have made in people, content and technology – but as with any business, not all of these investments or changes have hit the spot…. so we have from time to time re-evaluated our position and made changes to our strategies. At the end of the day however it is really our subscribers we have to thank for staying with us, trusting us to deliver the best television experience and customer service to make their experience world class,” said Jacobs.
D3B_6293
M-Net Regional Director West Africa, Wangi Mba-Uzoukwu (right) and Eku the MC flanked by another guest.
M-Net Regional Director West Africa, Wangi Mba-Uzoukwu, reminded guests that M-Net has a near 30-year history on the continent, where it started with a daily 12-hour broadcast on a single channel. Now, having changed the way television is viewed across the continent, the broadcaster leads the way in producing, acquiring and showcasing the best entertainment content in Africa. “Our first broadcast in 1986 led to other firsts like the launch of SuperSport and the Mzansi Magic, Zambezi Magic, Jango Magic and Africa Magic channels; and with the creation of exciting, genre-defining and iconic content like Carte Blanche and Tinsel, M-Net continues to shape cultures, build bridges and empower talent across Africa even as we remain synonymous with all things entertainment on the continent,” said Mba-Uzoukwu.
She echoed Jacobs’ sentiments about the need for constant evolution, to stay ahead of the video entertainment service provision field. “We are launching and redefining channels and we continue to expand our content offerings to viewers across the continent. Our ongoing and significant investments in local productions have positioned Africa on the entertainment global arena and with new technology we continue to reach even more people, ensuring that no one ever misses the M-Net Magic. Our investment drive remains geared not only towards the industries in which we play, but also in the people who power them,” said Mba-Uzoukwu.
The MultiChoice Africa Content Showcase is a dynamic 5-day content extravaganza, which sees a host of DStv’s biggest channels, including Sony, SuperSport, Zee TV, A+E, Disney, MTV Base, BET, Comedy Central, BBC and M-Net previewing their latest and greatest content, soon to be seen across the video entertainment services provider’s platforms. To keep track of happenings at the MultiChoice Africa Content Showcase, follow @multichoice_africa on Instagram, @mcashowcase on Twitter, or via #OnlyTheBest.
D3B_6334
Celebrities upon the arrival at Marquee where the event took place.
D8A_0828
The guests walked down the African media Walk of Fame.
IMG_6403
Flags from different countries include Tanzania which participate at the MultiChoice Content Showcase Extravaganza in Mauritius.
D3A_1719
MultiChoice Africa's CEO, Tim Jacobs giving a welcoming note.
IMG_6500
M-Net Regional Director West Africa, Wangi Mba-Uzoukwu speaking to the guests.
D3A_2492
IK welcoming Banky W on the stage.
IMG_6470
Entertainment to the guests.
IMG_6524D3B_7252IMG_6579IMG_6621IMG_6503
Nights of thousand stars #OnlyTheBest.
D3B_7081
Nigerian Artist, Mr. Flavour rocking the stage.
IMG_6780
Good times #OnlyTheBest: Nigerian actress and singer who won the Africa Movie Academy Award for Best Actress in a Leading Role in 2005, Genevieve Nnaji feeling Mr' Flavours tune along side Nigerian actor Ramsey Nouah who also won the Africa Movie Academy Award for Best Actor in a Leading Role in 2010.
IMG_6783
Nigerian Celebrities having good times at the MultiChoice Showcase Content Extravaganza in Mauritius.
IMG_6785
Sing along with Mr. Flavour (not in picture) during his performance.
IMG_6738
Banky W, Rita Dominic, Desmond Elliot, Ramsey Nouah, and Genevieve Nnaji.
IMG_6739
Feeling the music....!
IMG_6786
It's unforgettable night. #OnlyTheBest
IMG_6875
Donjazzy, Prince Mavin, Tiwa Savage Korede Bello, Aphro DIJA, Reekado Banks and Dr. SID performing DOR rmx.
D3B_7367
IMG_6933
Genevieve Nnaji in a jovial mood.
IMG_6934
Ramsey Nouah and Genevieve Nnaji chatting.
IMG_6891
MC's IK and Eku introduce the dancers.
IMG_6953
M-Net Regional Director West Africa, Wangi Mba-Uzoukwu (third right) poses for a photo with Nigerian Celebrities.
IMG_6972
Terry Mapurisana from ZBC News (left) with Nigerian Artist, Banky W.
IMG_6334
Paul Owere from The Citizen News Paper and IK taking a selfie.
IMG_6364
Lorraine Lusinje from Times Group in Malawi taking a selfie with IK.
IMG_6966
Public Relations Officer, MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi poses for a photo with Nigerian Actress, Genevieve Nnaji.
IMG_6343
Catching up on a few issues; Public Relations Officer, MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (left), General Manager Corporate Affairs, MultiChoice Africa, Caroline Creasy (right) and centre is Masembe Tambwe from Daily News Paper from Tanzania.
IMG_6340
From left: Public Relations Officer, MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi, General Manager Corporate Affairs, MultiChoice Africa, Caroline Creasy and Paul Owere from The Citizen News Paper poses for a photo during the official opening of MultiChoice Africa Content Showcase Extravaganza in Mauritius.
IMG_6971
Public Relations Officer-MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi chatting with the Nigerian Artist, Banky W after the official opening of MCA Content Showcase in Mauritius.

Serikali yasaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa daraja la Salenda

$
0
0
Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali na wajumbe kutoka Benki ya Exim ya Korea baada ya kusaini hati ya mkataba wa makubaliano ya mkopo wa Dola za Kimarekani milioni 91.032 ambazo ni sawa na Sh. Bilioni 154.39 za Kitanzania zilizotolewa na Benki ya Exim ya Korea kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Salenda leo jijini Dar es salaam.


(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)

Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images