Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

MSAMA PROMOSHENI KUANDAA TAMASHA LA KUOMBEA AMANI HAPA NCHINI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

$
0
0
 Muandaaji wa matamasha ya injili hapa nchini, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari katika ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo. Kuhusiana na tamasha la kuombea Amani ya nchi juu ya uchaguzi utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu hapa nchiini na kushoto ni Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya tamasha la kuombea amani ya nchi yetu kuelekea uchaguzi, Hamis Pembe. Msama pia aliipongeza serikali kwa kukataza uwanja wa taifa kutumika kufanyia matukio ya kisiasa. Pia amesema kuwa katika tamasha hilo litahudhuriwa na wananchi mbalimbali pamoja na wasanii wa nyimbo za injili hapa nchini.
 
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Alex Msama jijini Dar es Salaam leo. pia amengeza kuwa kwa waimbaji waliopo tayari kwa tamasha hilo ni pamoja na Boniface Mwaitege pamoja na Christopher Mwahangira.


Picha na Avila Kakingo Globu ya Jamii.

VIJANA WAHAMASISHANA JUU YA FURSA ZILIZOPO NDANI NA NJE YA NCHI

$
0
0
Mwenyekiti na mwanzilishi wa kikundi cha vijana cha Tanzania Youth Network (TYN), Agnes Mgongo akizungumza na vijana mara baada ya kukutana  katika ukumbi wa Don Bosco  jijini Dar es Salaam leo.
Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda akizungumza na vijana mbalimbali waliounda kikundi kiitwacho Tanzania Youth Network (TYN), wakijadili changamoto mbalimbali zinazowakumba vijana pamoja na vijana kuunda vikundi mbalimbali ili kutumia fursa zilizopo hapa nchini na Nje ya nchi ameyasema hayo katika mkutano uliowakutanisha vijana hao katika ukumbi wa Don bosco jijini Dar es Salaam leo.
Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda  akipokea kitabu cha ujasiliamali  kutoka kwa Balozi wa vijana wa jumuia ya Afrika Mashariki, Eric Ngilangwa katika mkutano wa vijana uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.



 Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda, Mwenyekiti na mwanzilishi wa kikundi cha vijana cha Tanzania Youth Network (TYN), Agnes Mgongo na Katibu wa TYN, Azavery Phares wakiwa katika mkutano wa vijana uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya vijana wakiwa katika mkutano uliowakutanisha vijana mbalimbali leo jijini Dar es Salaam.
Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda akiwa katika picha ya pamoja na kikundi kilichowakusanya vijana mbalimbali kutoka Bagamoyo,Morogoro pamoja na Dar es Salaam.

Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.  

GLOBAL EDUCATION LINK (GEL) YASAFILISHA WANAFUNZI KWENDA KUSOMA NCHINI INDIA

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, Abdulmalik Mollel akiwa ameambatana na wafanyakazi wa kampuni hiyo kuwasindikiza wanafunzi 30 wanaokwenda kusoma nchini India jana Agosti 21, 2015 katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, Abdulmalik Mollel akiwaita majina wanafunzi waliokuwa wanaondoka kwenda kusoma vyuo vikuu nchini India mapema jana Agosti 21, 2015 katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, wakikagua wanafunzi vyaraka muhimu walizopaswa kusafiri nazo ikiwemo viza, vyeti, na passport.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, Abdulmalik Mollel akiwaonyesha wanafunzi sehemu ya kwenda kukaguliwa mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wanafunzi wakibadilishana mawazo mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, Abdulmalik Mollel akiwaelekeza wanafunzi jinsi ya kuingia kwenye sehemu ya ukaguzi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, Abdulmalik Mollel akiambatana na wanafunzi kuelekea sehemu ya ukaguzi.
 Wafanyakazi wa kampuni ya Global Education Link (GEL) ambao ni wakala wa vyuo vya nje ya nchi, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilisha zoezi muhimu katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam. Picha zote na Emmanuel Massaka.

MSHINDI WA SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA CAROLINA CHILELE AIBUKA NA MILIONI 20

$
0
0
Mshindi wa Shindano lala Mama Shujaa wa Chakula Msimu wa Nne mwaka 2015 Calorina Chilele Muda mchache Baada ya kutangazwa kuwa mshindi.
Afisa Kilimo Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Dkt. Kissa Kajigili , akiwapongeza Oxfam kwa kuandaa shindano la Mama Shujaa wa Chakula na washiriki wote kwa ujumla walioshiriki katika Shindano hilo, Pia alimpongeza Mshindi wa Mama Shujaa wa Chakula 2015 Carolina Chilele na kumtaka awe mfano bora pia akawe chachu ya kuinua kilimo na kuwasaidia wenye uhitaji yaani wakulima wanawake wadogo wadogo, Mwisho aliwaomba Oxfam waendelee na Shindano hili muhimu.
Jackson Yusuph Mzumba Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kibweni akitoa neno la Shukurani kwa niaba ya Serikali ya Kijiji cha Kisanga
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kisarawe Bw. Ellioth Phillemon Mwasambwite akiwashukuru Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 , na kuwaaaga rasmi, pia kumpongeza Mshindi wa Shindano hilo msimu wa Nne Bi. Carolina Chilele , Mwisho aliwapongeza Oxfam kwa kuanzisha shindano endelevu kwa Maendeleo ya wakulima hasa wanawake.
Mmoja wa akina mama ambao walikuwa wanakaa na Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula katika Kijiji cha Kisanga Bi. Sophia Shomvi akitoa neno la Shukurani kwa washiriki hao kwa  jinsi walivyo kaa vizuri pamoja na pia kuwaachia elimu kubwa wanakijiji hao. Mwisho alitoa neno la Kuwaaga Rasmi
Kiongozi wa Timu ya Urasimishaji ardhi vijijini kutoka Wizara ya Ardhi nyuma na Maendeleo ya Makazi Bw. Swagile Msananga akiwapongeza washiriki wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula 2015, pia kwa mshindi wa Shindano hilo kwa msimu wa Nne 2015 Bi. Carolina Chilele kwa ushindi wake na kumtaka kuwa mfano Bora kwa jamii kwa ujumla, Pia alisisitiza watu sio kuwa tu na ardhi lakini pia kupata umiliki wa ardhi  walizonazo.
Baadhi ya Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 wakipewa  tuzo za ushiriki wao na Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster
Mshindi wa Mama shujaa wa Chakula 2015 msimu wa Nne Carolina Chilele akipongezwa na washiriki mwenzake
Picha ya pamoja
Baadhi ya Wageni waalikwa , Wafanyakazi wa Oxfam, Ndugu jamaa na Marafiki wakiwa katika Sherehe za Fainali za Shindano la Mama shujaa wa Chakula.
Bi. Hawa Mkata aliyekuwa Mshiriki kutoka Mtwara akitoa neno la Shukurani kwa wanakijiji wote ambao waliishi nao Kijijini kwa Muda wa Siku zote 21, na zaidi zile Familia ambazo wao wamekuwa nao kwa kipindi chote cha Shindano hilo, Mwisho aliwaomba washiriki wenzake kujua kuwa wote ni washindi lakini mmoja ndio kawawakilisha kwa kuchukua zawadi ile ya Milioni Ishirini.
Eva Mgeni, Mshiriki kutoka Bagamoyo Kutoka Mkoa wa Pwani, Akitoa Shukurani zake kwanza kwa Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow ambayo kauli mbiu yake ni kuwekeza kwa wakulima wadogo wadogo wanawake inalipa kwa kuendesha shindano hili na kuwa kupitia washiriki wa shindano hilo wamejifunza mambo mengi na ya kimaendeleo, Mwisho aliwashukuru wanakijiji wote kwa ushirikiano wao na Moyo wa Ukarimu katika kipindi chote wakiwa Kijijini.
Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akitoa salam zake za Shukurani kwa wote waliofanikisha shindano la Mama shujaa wa Chakula kwenda vizuri tangu mwanzo mpaka mwisho, aliwashukuru wanakijiji cha Kisanga kwa kukubali kwao shindano lifanyike katika kijiji hicho pia aliwapongeza washiriki wote wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula na kuwasihi kuwa wote walikuwa ni washindi, Mwisho alichukua nafasi hiyo kumpongeza Mshindi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 na kumsihi aende kuwa mfano wa kuigwa kwa wakulima wenzake pia akawe Balozi mzuri na kuiwakilisha vema Oxfam
 Mshindi wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 msimu wa nne akitoa neno la Shukurani kwa ushindi alioupata , Ameshukuru shirika la Oxfam kwa kuendesha shindano hilo na kuahidi kuwa atakwenda kuwa Balozi mzuri na kusema kuwa washiriki wote ni washindi na yeye amepata zawadi hiyo kuwawakilisha wote.
Burudani ikiendelea 

Hatimaye Shindano la Mama Shujaa wa Chakula shindano linaloendeshwa na Shirika la Oxfam kupitia Programu yake ya Grow ambapo kauli mbiu ni Wekeza kwa wakulima wanawake wadogo wadogo inalipa lafika tamati ambapo kulikuwa na mchuano mkali kati ya washiriki 15 ambao walikuwa katika Kijiji cha Kisanga Wilayani Kisalawe Mkoani Pwani wakiwa na shughuli mbalimbali za Kilimo ambazo zililenga hasa katika kuwakomboa wakulima wadogo wadogo wanawake wadogo wadogo.  

Washiriki hao walikaa kijijini kwa muda wa siku 21  hatimaye kufikia kumpata mshiriki mmoja ambaye amejishindia kiasi cha Tsh 20,000,000 fedha ambazo zitanunua pembejeo za Kilimo. Fainali hizo zilifanyika katika Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es salaam


MISS TANZANIA USA: MAJAJI WAMPOKONYA USHINDI DOREEN PANGA NA KUMVIKA TAJI AEESHA KAMARA NJE YA UKUMBI

$
0
0
Aeesha Kamara sasa ndiye mshindi wa Miss Tanzania USA pageant
  Miss Africa 2014-15 akipata picha ya pamoja na Doreen Panga baada ya kuvikwa taji la Miss Tanzania USA 
Miss Africa 2014-15 akipata picha ya pamoja na Aeesha Kamara baada kuvikwa taji na maamuzi ya majaji ambao hawakukubaliana na mshindi aliyetangazwa kwanza.

Doreen Panga kutoka New York usiku wa Aug 22, 2015, alivuliwa taji la Miss Tanzania USA na majaji wa shindano hilo nje ya ukumbi taji alilolivaa kwa dakika 45 na kumvika Aeesha Kamara wa Maryland kwa madai kwamba Doreen Panga hakua chaguo lao. 

Majaji hao Peter Walden, Elaine Roecklein, Tee Thompson, Bertini Huemegni, Tina Semiti Magembe, Mayor Mlima, Uche Ibezzue wakiongozwa na Michael Lewis McBride kwa pamoja walikataa kukubaliana na mshindi aliyetangazwa na kufanya kikao nje ya ukumbi wakati watu wakiondoka ondoka nao wakisikitishwa na maamuzi ya kutangazwa mshindi huku na kama majaji wangekaa kimya basi masahabiki wa shindano hilo wangepelekea lawama kwa majaji.Jaji Dr. Secelela Malecela japo kwamba alipingana na Doreen Panga kutangazwa mshindi lakini hakukubaliana na majaji wenzake Doreen avuliwe taji na apewe Aeesha Kamara aliyekua chagua la majaji wengine, yeye alipendekeza kwa kua kosa lishafanyika waachane nalo wahakikishe mwakani halitokei tena. Wazo lake lilipingwa na majaji wenzake pale pale.

Shindano hilo lilianza vizuri kwa nyimbo za Taifa za Marekani na Tanzania zilizoongozwa na watoto Brian akiwa kwenye kinanda na dada yake Briana akiwa kwenye kipza sauti,

Baadae walitambulishwa ma miss wa kesho watoto wa DMV wenye umri wa miaka 9 na 12 na baada ya hapo waliingia malikia wenyewe huku wakisindikizwa na wimbo wa Diamond wa mdogo mdogo na baadae kujitambulisha kwa majaji.

Washiriki wa miss Tanzania USA walikua Rechel Mujaya kutoka Atlanta, Joyce Mkapa toka New York, Doreen Panga toka New York, Aeesha Kamara toka Maryland, Aziza Gama toka Maryland na Brenda Panga toka New York. Washiriki walianza shindano kwa kujielezea wakifuatia na shindano la vipaji na baadae kujibu maswali ya majaji.

Pia katika shindano hilo kulikua na burudani mbalimbali akiwemo Mr Tz ambaye aliitambulisha singo ya wimbo wake mpya uliotoka mwei uliopita, Wasanii wengine walikua kutoka Ivory Coast na Jamaica.

Baada ya hapo ndipo kulitangazwa mshindi kuwa ni Doreen Panga ushindi ambao waliowengi hawakukubaliana nao wakiwemo majaji na mkurugenzi na mwanzilishi wa Miss Africa USA ambao walisikika wakinong'ona huku wakiulizana imekuaje bila kupata majibu.

Wakati majaji wakiwa nje ya ukumbi wakitafakali imekuaje tumeacha shughuli zetu tumekuja hapa tunatoa maamuzi sasahihi halafu mtu anatuzarau maamuzi yetu. Mashabiki walianza kuondoka baada ya shindano hilo kufikia ukingoni na wengine wakimtupia lawama wandaaji kwa kuvurunda shindano.

Majaji walipokua wakijadiliana wafanye nini walikuja na kuazimia kwa kauli moja  lazima wampe ukweli mwandaaji kwamba hawakufurahika na kilichotokea ndani ya ukumbi. Mwandaaji wa Miss Tanzania USA aliitwa ndipo majaji wakatoa dukuduku lao na mwandaaji akajitetea kwamba mshindi amesema hataweza kushiriki mashindano hayo na ameamua kumpa taji mshindi wa pili ambaye alikua Aziza Gama, baada ya kusikia hayo majaji walimwita Doreen Panga na kumuuliza sababu yake ya kutaka kumvisha taji mshindi wa pili ni nini yeye akawajibu ni kutokana na kazi zangu ninazofanya hospitali sitaweza kupata muda wa ushiriki kwa hiyo badala yake nitampa taji mshindi wa pili.

Majaji walishindwa kuafikiana na Doreen na kuamua kupiga kura upya ndipo wote kwa pamoja kasolo Dr Secelea Malexela walimchagua Aeesha Kamara kwamba ndiye aliyestahiki kuvigwa taji na ndio aliyekua chaguo lao.

Doreen Panga akavuliwa taji na kuvikwa Aeesha Kamara huku Doreen akionesha kutokubaliana na majaji lakini wao ndio waamuzi wa mwisho na kitendo walichokifanya ni kulinda heshima yao.

Sasa Miss Tanzania USA ni Aeesha Kamara.

KILOMETA 6,276 ZA BARABARA ZAJENGWA NCHINI KWA MIAKA 10

$
0
0
Wakati wakandarasi walipokuwa wanajenga daraja hili katika eneo la Miangalua kwenye barabara ya Tunduma-Sumbawanga mwaka 2011. Barabara hiyo sasa imekamilika.
Barabara ya Mwanza-Musoma iko katika hali nzuri. 
Ujenzi wa barabara ukiendelea katika baadhi ya miradi nchini.
Ujenzi wa barabara ya Iringa-Dodoma umekamilika kwa asilimia 95, bado maeneo machache tu likiwemo hili la Mlima Nyang'oro ambapo Wachina wameuchonga ili kupunguza kona katika umbali wa kilometa 15. (Picha zote na Daniel Mbega wa www.brotherdanny.com).

 Na Daniel Mbega, brotherdannyblog
Sumbawanga: NAJIWEKA vyema kwenye kiti na kutazama nje kupitia dirishani. Japokuwa giza limetanda majira haya ya saa 4:30 usiku, lakini ninaweza kuhisi jinsi basi hili nililopanda la kampuni ya Majinjah linavyotafuna lami.

Abiria mwenzangu wa jirani ananiambai tutaingia saa sita kasoro usiku mjini Sumbawanga mjini. Nafarijika japo uchovu ni mwingi, maana kuketi kwenye basi kwa saa takriban 15 siyo mchezo ingawa tulipata nafasi mara kadhaa za kupumzika 'kuchimba dawa' na kupata mlo.

“Barabara yote ni lami tupu ndugu yangu, kasoro tu ni haya matuta kutoka Tunduma hadi Sumbawanga, lakini yamesaidia kupunguza mwendokasi,” ananieleza.
Tunduma tumeondoka kama saa tatu hivi kuzikabili kilometa 222 hadi Sumbawanga, lakini safari hii ya kutoka Dar es Salaam inayokadiriwa kuwa na umbali wa kilometa 1,000 imekuwa siyo ndefu licha ya uchovu wa kiuno na mgongo kutokana na kuketi tangu saa 12 alfajiri. Faraja pekee ni kwamba ninatumia siku moja tu kufika Sumbawanga, tofauti na miaka mitano iliyopita ambapo nililazimika kutumia siku mbili huku nikiingia gharama za ziada za kulala Lodge pale Mbeya kutokana na kutokuwepo na usafiri wa uhakika kutokana na ubovu wa barabara.

Wakati huo, ukilala Mbeya unalazimika tena kuamka mapema kuwahi basi ambalo licha ya kuondoka saa 12 alfajiri, bado litafika Sumbawanga saa 8 mchana.Jirani yangu ananiambia kwamba sasa unaweza kwenda na kurudi Sumbawanga mara mbili ukitokea Mbeya kwani mabasi ni mengi na njia ‘inateleza’.

“Wametukomboa sana, magari hayajazi kama zamani, unasafiri kwa raha na kwa wakati – muda wowote unaotaka,” ananieleza.Ndiyo. Nakumbuka safari moja wakati nikitokea Sumbawanga jinsi basi lilivyokuwa limejaza abiria mpaka sehemu ya kupita ikakosekana. Walioketi walikuwa wachache kuliko waliosimama, sasa piga hesabu lilikuwa na abiria wangapi! Hata kondatka mwenyewe alilazimika kupita kwa kuinama juu ya siti ili kwenda nyuma kuwapanga abiria waliosimama na kuchukua nauli. Ilikuwa ni hatari.

 

Lakini leo barabara hii imetandikwa lami na imekuwa sehemu ya barabara zenye urefu wa jumla ya kilometa 6,276 ambazo zimetengenezwa na utawala huu wa Awamu ya Nne, huku sehemu kubwa yabarabara hizo ikiwa imesimamiwa na Dk. John Pombe Joseph Magufuli kama Waziri wa Miundombinu.

Nimezunguka karibu nchi nzima nikifanya habari za uchunguzi kwa miaka kumi iliyopita. Mazingira ya wakati ule na ya sasa ni tofauti kabisa, maeneo ambayo yalikuwa hayafikiki, hivi sasa hali ni nzuri. 
Tangu Januari hadi Juni 2015 pekee nimezunguka karibu kilometa 20,000 hapa nchini. Nimezunguka nikitokea Iringa kwenda Arusha kupitia Dodoma-Singida hadi Manyara; nimezunguka kutoka Dar es Salaam-Kiteto-Kondoa hadi Babati; nimepita Babati-Kondoa-Mayamaya hadi Dodoma; nimepita Mwanza-Shinyanga-Tabora-Mpanda hadi Sumbawanga mpaka Mbeya; nimetoka Dar es Salaam-Njombe-Songea hadi Mbambabay; nimetoka Mwanza-Musoma hadi Sirari; nimezunguka Mwanza-Sengerema-Geita hadi Bukoba; nimetoka Bukoba kupita Kahama hadi Dar es Salaam; nimetoka Shinyanga-Maswa-Bariadi hadi Lamadi; na maeneo mengine mengi kwa miezi sita.
Hakika nilichokiona kinastahili kupongezwa kwamba kimefanyika. Ingawa barabara kadhaa zimesimama kutokana na kukosekana kwa fedha kufuatia msukosuko wa wafadhili kushindwa kutoa fungu, lakini nyingi kati ya hizo zimekamilika na kuiunganisha vyema Tanzania.
Nilipita wakati fulani ilipoanza kutengenezwa barabara hii, nadhani ilikuwa mwaka 2011 nikiwa katika harakati zangu za kuandika habari za maendeleo vijijini. Barabara hii ilimegwa katika vipande vitatu ili kuharakisha ujenzi wake na kuzingatia ubora.

Kipande cha kwanza kilikuwa kutoka Tunduma hadi Ikana chenye urefu wa kilometa 63.2 ambacho kilijengwa na kampuni ya Consolidated Contractors Group kwa gharama ya Dola 82.521 milioni; Kipande cha pili chenye urefu wa kilometa 64.2 kilikuwa kutoka Ikana hadi Laela na kilijengwa na kampuni ya China Newera (64.2km Ikana-Laela) kwa Dola 46.812 milioni; na kipande cha mwisho kilikuwa kutoka Laela hadi Sumbawanga chenye urefu wa kilometa 95.31 ambacho kilijengwa na kampuni ya Aarsleff-Interbeton J.V kwa gharama ya Dola 130.038 milioni. Kwa hiyo kilometa zote 222.71 ziligharimu jumla ya Dola 259.371 milioni ambazo ni fedha za wahisani na fedha za ndani.

Ni fedha nyingi sana lakini haziwezikuzidi thamani halisiya barabara hii ambayo licha ya kuwakomboa wananchi wa pembezoni hasa katika mikoa ya Mbeya, Rukwa na Katavi, lakini pia itasaidia kuiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa sababu ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 112 kutoka Sumbawanga-Matai hadi bandari ya Kasanga katika Ziwa Tanganyika unaendelea chini ya kampuni ya China Railway 15th Bureau Group Corporation - CR15G kwa gharama ya Dola 80.912 milioni.

Dk. Magufuli, ambaye sasa ni mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), anazifahamu karibu barabara zote nchini na hatua zilikofikia. Alipoingia kwa mara ya kwanza bungeni mwaka 1995 baada ya kushinda katika jimbo la Chato akiwa na miaka 36 tu,  Rais Benjamin Mkapa akamteua kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Miundombinu. Kazi ya Ubunge na unaibu waziri ilimpeleka salama hadi mwaka 2000.

Uchaguzi wa mwaka 2000 ulipoitishwa, Dk. Magufuli aligombea na kushinda kwa mara ya pili. Rais Mkapa akamteua kuwa Waziri wa Wizara ya Miundombinu, wadhifa aliodumua nao hadi kipindi cha uongozi wa Mkapa kilipomalizika.

Mwaka 2005 alishinda ubunge kwa mara ya tatu, lakini safari hii aliingia katika orodha ya wabunge waliopita bila kupingwa. Rais Jakaya Kikwete akamteua kuongoza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi hadi mwaka 2008 alipohamishiwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambayo aliiongoza hadi mwaka 2010.

Mwaka 2010 akagombea tena ubunge, lakini safarihii akapambana na mgombea wa Chadema, Rukumbuza Vedastus Albogast ambaye alitoa upinzani mkubwa ingawa hatimaye Magufuli alishinda kwa asilimia 66.39 dhidi ya asilimia 26.55 za mpinzani wake. Rais Kikwete akamrudisha katika Wizara ya Ujenzi ambako yuko hadi hivi sasa.

Tangu kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, wengi walikuwa wakimtaja Magufuli kwamba anafaa kuwania urais, lakini yeye alikaririwa akisema wakati huo kwamba hana mpango huo.

Hata makada wenzake walipoanza kuonyesha nia kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka huu, yeye hakuwa na papara na iliwashangaza wengi Mei 29 alipoamua kujitosa kimya kimya, akachukua fomu na kuondoka, bila mbwembwe wala madoido kama walivyofanya wengine.

Wanaomfahamu wanasema nguvu yake kubwa iko kwenye elimu yake, lakini kukaa muda mrefu kwenye wizara zake na mambo makubwa aliyoyafanya katika wizara alizopata kuziongoza, pamoja na uwezo wake wa kutoa maamuzi magumu kila mara vinampa sifa ya kuwa rais anayefaa katika kipindi hiki ambacho rushwa, ufisadi na ukosefu wa maadili vimetamalaki.

Udhaifu wake pekee unaotajwa na walio karibu yake ni kufanya maamuzi ya haraka, jambo ambalo linaweza kurekebishwa kwa kuwa ndani ya Taasisi ya Urais kuna washauri makini.


UJENZI WA BARABARA

Katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya awamu ya nne, barabara zenye urefu wa jumla ya 6,276.82km zimejengwa kwa gharama ya Dola 102,654.98 milioni, nyingi kati ya hizo zikiwa za lami na hivyo kuutengeneza mtandao imara wa miundombinu ya barabara.

Kujengwa kwa barabara hizo kumerahisisha hata usafiri ambapo leo hii magari ya abiria na mizigo kutoka Dar es Salaam kwenda Musoma, Mwanza, Kagera na Kigoma hayahitaji kuzunguka Nairobi bali yanakwenda moja kwa moja.

Hivi sasa usafiri wa kutoka Dar es Salaam kwenda Sumbawanga ni wa siku moja badala ya siku mbili, kama ilivyo kwa usafiri wa Dar es Salaam kwenda Mbinga, jambo ambalo miaka 10 iliyopita lilikuwa ndoto.

Asilimia 90 ya miradi hiyo imesimamiwa na Dk. Magufuli akiwa Waziri wa Miundombinu katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015na bado miradi mingine inaendelea kujengwa japo imesimama kidogo kutokana na ufinyu wa bajeti.

Kampuni za Kichina zimepata mikataba mingi ya ujenzi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, kampuni 14 kutoka China zimeingia jumla ya mikataba 58 ya ujenzi wa kilometa 3,140.85 yenye thamani ya Dola 1.75 bilioni.

Kampuni ya China Henan International Cooperation Group Co., Ltd. (CHICO) ambayo ilipata mkataba wenye thamani ya Dola 206 milioni kutoka Wakala wa Barabara Zambia kujenga barabara ya Mansa-Luwingu yenye urefu wa kilometa 175, peke yake imeingia mikataba 13 nchini Tanzania ya barabara zenye urefu wa kilometa 705.2 zikiwa na thamani ya Dola 490.26 milioni.

Hizi ni pamoja na barabara za Singida-Iguguno (76km) yenye thamani ya Dola 20.55 milioni; Sekenke-Shelui (33km) yenye thamani ya Dola 12.51 milioni; Mwandiga-Manyovu (60km) wenye thamani ya Dola 32.54 milioni; Kigoma-Kidahwe (35.7km) kwa Dola 19.56 milioni; Bonga-Babati (19.20km) kwa Dola 11.95 milioni; Tabora-Urambo (42km) kwa Dola 31.17 milioni; Kyaka-Bugene (59.1km) kwa Dola 51.6 milioni; Dareda-Minjingu (84.6km) kwa Dola 51.6 milioni); Kidahwe-Uvinza-Ilunde (76.6km) kwa Dola 47.5 milioni; Isaka-Ushirombo (132km) kwa Dola 88.223 milioni; Kilwa Road Phase III (1.5km) kwa Dola 3.4 milioni; Nyanguse-Musoma (85.5km) kwa Dola 3.3 milioni; na Kagoma-Lusahunga (154km ) kwa ubia na kampuni ya CRSG kwa gharama ya Dola 116.2 milioni.

China Sichuan International Cooperation Co., Ltd (SIETCO) inajenga barabara zenye urefu wa 283.9km zenye thamani ya Dola 123.03 milioni ambazo ni Isuna-Singida (63km) kwa Dola 18.5 milioni; Tarakea-Rongai-Kamwanga (32km) kwa Dola 8.8 milioni; Iringa-Migori (95.1km) kwa Dola 51.123 milioni; na Migori-Fufu Escarpment (93.8km) kwa Dola 44.7 milioni, wakati kampuni ya CICO inajenga barabara ya Nangurukuru-Mbwemkuru yenye 95km kwa thamani ya Dola 23.82 milioni.

Kampuni ya China Geo-Engineering Corporation International Ltd (CGC INT'L) inajenga barabara zenye urefu wa 525.9km zikiwa na thamani ya Dola 151.2 milioni. Barabara hizo ni Shelui-Nzega (112km) kwa Dola 12.6 milioni; Kyamorwa-Buzirayombo (120km) kwa Dola 29.822 milioni; Manyoni-Isuna (54km) kwa Dola 18.4 milioni; Arusha-Namanga (104.2km) kwa Dola 49.64 milioni; Chalinze-Tanga Phase I (125km ) kwa Dola 25.9 milioni na ndiyo kampuni iliyojenga Daraja la Mkapa (Daraja la Umoja 10.7km) linalounganisha Tanzania na Msumbiji kwa gharama ya Dola 14.9 milioni.

Katika orodha hiyo, ipo kampuni inayomilikiwa na serikali ya China, Hydropower Engineering and Construction Company (SINOHYDRO) ambayo ilipata mikataba 12 nchini Tanzania ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa jumla ya 779.95km zenye thamani ya Dola 434.36 milioni. Barabara hizo ni Sengerema-Usagara (40km) kwa gharama ya Dola 21.724 milioni; Buzirayombo-Geita (100km) kwa Dola 25 milioni; Geita-Sengerema (50km) kwa Dola 24.034 milioni; Dodoma-Mayamaya (43.65km) kwa Dola 25 milioni; Manyoni-Itigi-Chaya (89.3km) kwa Dola 66.56 milioni; Puge-Tabora (56.1km) kwa Dola 35.085 milioni; Handeni-Mkata (54km) kwa Dola 34.81 milioni; Korogwe-Handeni (65km) kwa Dola 38.4 milioni; Katesh-Dareda (73.8km) kwa Dola 38.94 milioni; Singida-Katesh (65.1km) kwa Dola 31.34 milioni; Tanga-Horohoro (65km) kwa Dola 42.43 milioni; na Peramiho Junction-Mbinga (78km) kwa Dola 48.444 milioni.

CHIKO ilijenga barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es Salaam yenye urefu wa 4km kwa thamani ya Dola 7.9 milioni, China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) ilipata mikataba minne ya kujenga barabara zenye urefu wa 145.6km kwa thamani ya Dola 95 milioni. Barabara hizo ni Magole-Turiani (48.6km) kwa Dola 25.43 milioni; Tabora-Urambo (52km) kwa Dola 36.3 milioni; Dumila-Rudewa (45km) kwa Dola 25.5 milioni na Jangwani Depot kwa ajili ya mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar es Salaam (BRT) kwa Dola 7.81 milioni.

(Imeandaliwa na www.brotherdanny.com. Simu: 0656-331974)

JEMBE FM MWANZA YAFUNGUA MILANGO KWA VYAMA VYA SIASA KUTANGAZA MIKUTANO LIVE.

$
0
0
 Mbio za kampeni ya uchaguzi mkuu 2015 tayari zimeanza. Ni wasaa sasa kwa wagombea wa vyama mbalimbali kupishana huku na kule vijiji kwa vijiji, kata kwa kata, wilaya kwa wilaya, mkoa kwa mkoa wakifanya mkutano ya kampeni za siasa kutambulisha wagombea wao na kuzinadi sera zao al-muradi wapate ridhaa ya wananchi. 

Zoezi hilo ni gumu ila sisi kama jEMBe fM tunalirahisisha!! Sasa ili upate kuwafikia wananchi wengi ndani ya muda mfupi jEMBe fM imefungua milango kwa kutoa huduma ya matangazo ya moja kwa moja yaani LIVE toka viwanja vya mikutano tena full kiwango (HATUBAHATISHI) kwa maelezo zaidi piga simu kitengo cha masoko katika namba ±255282506068 au fika katika ofisi zetu zilizopo jengo la PPF ghorofa ya 6.
@jembenijembe

HARAMBEE YA KUCHANGIA MKOA WA KUSINI PEMBA

$
0
0
1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba jana wakati alipohudhuria katika Harambee ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam,Picha zote na Ikulu.
2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba jana wakati alipohudhuria katika Harambee ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam.
7
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi Bi.Naila Jidawi Mwakilishi wa Kampuni ya Pennyroyal inayojenga Mradi Mkubwa wa Kitalii wa aina yake katika Kijiji cha Matemwe Mbuyutende Kaskazini Unguja, kasha lililouzwa kwa shilingi za Kitanzania Million saba   katika   Harambee ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam jana,
6
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akipokea fedha kutoka kwa Bi.Naila Jidawi Mwakilishi wa Kampuni ya Pennyroyal inayojenga Mradi Mkubwa wa Kitalii wa aina yake katika Kijiji cha Matemwe Mbuyutende Kaskazini Unguja, Dola za Kimarekani Elfu kumi  katika   Harambee ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam jana.
5
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Bw.Said Salim Bakhresa(katikati) na Bw.Azizi salim wakiwa ni miongoni mwa wachangiaji    katika   Harambee ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam.
4
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein (katikati) pamoja na viongozi wengine wakiwa katika chakula wakati wa uchangiaji wa  Harambee ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam jana.
3
Baadhi ya Viongozi mbali mbali na wananchi na wapenzi wa CCM waliohudhuria katika hafla ya kuchangia mfuko wa maendeleo wa CCM Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Serena Hotel Jijini Dar es Salaam jana,chini ya mgeni rasmi   Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.

Serikali yamiliki kiwanda cha general tyre kwa asilimia 100

$
0
0

indexxNa Lorietha Laurence-Maelezo
………………………………………….Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kumiliki kiwanda cha kutengeneze magurudumu ya magari cha General Tyre kwa asilimia 100 baada ya kununua hisa 26zenye thamani ya Dola Moja milioni kutoka kwa kampuni ya Continental AG.
 Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ya Msajili wa Hazina wakati wa makabidhiano ya nyaraka za ununuzi wa hisa hizo Katibu Mkuu Kiongozi ,Balozi.Ombeni Semfue anasema jitihada za kuhakikisha kuwa serikali inamiliki hisa hizo zilianza tangu mwaka 2012 kwa kufanya mazungumzo ya awali na mwekezaji.
 “Kufuatia hatua hii ya kuweza kumiliki hisa kwa asilimia 100 sasa tutakuwa na fursa ya kuzalisha magurudumu yetu wenyewe na hivyo kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kilichokuwa kikitumia kununua magurudumu kutoka nje” alisema Balozi.Semfue.
 Aidha anaendelea kufafanua kuwa hatua itakayofuata ni kutamfuata mwekezaji atakayeshirikiana na Shirika la Maendelao la Taifa (NDC) katika kuzalisha magurudumu kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
 Balozi.Semfue anampongeza Rais Mhe. Jakaya Kikwete kwa kufanikisha zoezi zima la kuhakikisha serikali inamiliki hisa za kiwanda cha General Tyre kwa asilimia 100 na hivyo kufufua uchumi wa jiji la Arusha na Taifa kwa ujumla. 
 Naye Msajili wa Hazina Lawrence Mafuru anasema mpaka serikali kuweza kumiliki hisa hizo ni hatua kubwa sana kutokana na vikwazo mbalimbali vilivyokuwa vikiwekwa na mwekezaji wa kiwanda hicho kilichoanzishwa mwaka 1969.
 “Haikuwa kazi rahisi kumiliki hisa hizi bila ya jitihada kubwa iliyofanywa na serikali katika kumshawishi mwekezaji baada ya kuona hana kuwa hakuwa tayari kuwekeza na hivyo kurejesha umiliki kwetu” alisema Mafuru.
 Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Mhe. Uledi Musa, anaeleza kuwa kiwanda hicho kitatoa fursa za ajira zaidi kitakapoanza kuzalisha tofauti na awali ambapo kiliweza kuajiri wafanyakazi 360.

TMT 2015 #mpakakieleweke kimeeleweka kwa Denis Laswai

$
0
0
Mshindi wa TMT 2015 #mpakakieleweke, Denis Laswai akiwa ameinua mikono juu kuashiria ishara ya kumshukuru Mungu Mara baada ya Kutangazwa Mshindi wa TMT 2015 #mpakakieleweke msimu wa pili katika fainali iliyofanyika usiku wa kumkia leo katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar Es Salaam.
Mshindi wa shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2015 #mpakakieleweke Denis Laswai kutoka Kanda ya Kaskazini Arusha akiruka juu kwa furaha mara baada ya kutangazwa Mshindi wa Kitita cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania mara baada ya kuibuka kinara kwenye fainali hiyo ya TMT iliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar Es Salaam.
Majaji wa Shindano la TMT wakifuatilia matukio yanayoendelea katika fainali ya shindano la TMT 2015 linaloendelea kufanyika katika ukumbi wa Makumbusho huku ikirushwa live kupitia Live na Kituo cha ITV
 Baadhi ya wahudhuriaji wakifuatilia matukio live
 Mshindi wa TMT #reachforthestars msimu wa Kwanza Mwanaafa Mwinzago akifurahia jambo mara baada ya Mshindi wa TMT msimu wa pili kutangazwa katika fainali ya TMT iliyofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa
 Walimu wa washiriki wa TMT 2015 #mpakakieleweke Mwl Issa (Kushoto) akiwa na Mwalimu wenzake Dkt Mona Mwakalinga wakifuatilia shindano la TMT
 Mtangazaji wa Radio One/ITV Rehema Nyamaka (kulia) akiwa na shostito wake wakifuatilia shindano hilo lililokuwa likirushwa live na kituo cha Runinga cha ITV usiku wa Kumakia leo
 Meneja Mradi wa TMT Saul Mpock (Kushoto) akimpongeza Mshindi wa TMT 2015 #mpakakieleweke Denis Laswai (Katikati) huku akipongezwa pia na Bi Jennifer Kway, Mhasibu wa Kampuni ya Proin Promotions Ltd ambao ndio waandaaji wa shindano la TMT kwa Msimu wa Pili Sasa.
Baadhi ya wasanii mbalimbali wa tasnia ya filamu, wadau kutoka Basata na washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya ishirini bora wakifuatilia fainali hiyo.
 Mwenyekiti wa Makampuni ya Proin, Mh Johnson Lukaza (Kulia) akimpongeza mshindi wa TMT 2015, Denis Laswai mara baada ya kutangazwa kuwa kinara wa TMT 2015 #mpakakieleweke
 Wadau wakiwa kwenye dhuria jekundu
Haji Mboto kazini
 Ruby akitoa burudani wakati wa fainali hiyo iliyofanyika usiku wa kuamkia leo na kupelekea Denis Laswai kutoka Mkoani Arusha Kuibuka Mshindi wa TMT 2015 #mapakkieleweke
 Watu mbalimbali wakifuatilia fainali ya TMT katika ukumbi wa makumbusho ya taifa usiku wa kumakia leo
Washiriki wa TMT 2015 #mpakakieleweke waliofanikiwa kuingia hatua ya kumi bora wakiwa mbele ya majaji na watazamaji wa fainali hiyo iliyokuwa ikirushwa live kupitia ITV.Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog
Shindano la TMT hatimaye limefikia mwisho usiku wa kumkia leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa mara baada ya Kijana Denis Laswai kutoka Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha Kuibuka kidedea kwa kuwagaragaza Washiriki wenzie tisa waliofanikiwa kuingia hatua ya fainali na kuondoka na Kitita cha Shilingi Milioni Hamsini za Kitanzania huku washiriki tisa kuondoka na kifuta jasho mara baada ya shindano hilo kumalizika.
Shindano la TMT limechukua takribani miezi minne tangua kuanza kwa Mwaka 2015 huku likiwa limetembelea kanda sita za Tanzania na ha hatimaye kupata washindi wapatao 20 kutoka katika kanda hizo ambao waliingia katika mjengo wa TMT na kuanza kupatiwa mafunzo ya sanaa na walimu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam
Mara baada ya washindi hao kupatikana na kuingia ndani ya mjengo wa tmt washiriki kumi waliweza kuaga mashindano hayo katika hatua ya mchujo na kubakiwa na washiriki wengine kumi ambao ndio waliofanikiwa kuingia hatua ya fainali.
Mara baada ya mshindi wa TMT 2015 #mpakakieleweke kupatika hapo usiku wa kumkia leo washiriki hao kumi watatengeneza filamu ya pamoja huku wakinufaika na filamu hiyo kuanzia utengenezaji wake hadi kuuzwa .
Mshindi wa TMT 2015 #mpakakielewe ni mshindi wa msimu wa pili wa shindano hili lililofanyika takribani kwa mwaka wa pili sasa huku Mshiriki wa kwanza kabisa akiwa ni Binti mdogo kutoka Kanda ya Kusini Mkoani Mtwara Mwanaafa Mwinzago ambae mara baada ya kushinda alipata nafasi ya kusomeshwa na kampuni ya Proin Promotions Ltd bila zawadi yake kuguswa. Washiriki kumi bora watakuwa chini ya mkataba wa kampuni ya Proin Promotions Ltd ambao ndio waratibu na waendeshaji wa shindano hili kubwa Afrika Mashariki na Kati huku shindano hili likiwa limepigwa tafu na Paisha, Pepsi, Camgas, Precision Air, Global Publishers, Data Vision International, I-View Studio, Van Maria Boutique, Hartman Barber Shop, na Hussein Pamba Kali

WANACHAMA WA CHADEMA ZAIDI YA 500 LUDEWA WAHAMIA ACT WAZALENDO WACHUKIZWA KUKATWA KWA MSHINDI WA KURA ZA MAONI

$
0
0
New Picture
Wanachama wa Chadema wilaya ya Ludewa mkoa wa Njombe wakiandamana kupinga maamuzi ya chama hicho kukata jina la mshindi wa kura za maoni na kumteua aliyeshindwa ,mbali ya kuandamana pia wanachama hao zaidi ya 500 walikihama chama hicho na kujiunga na ACT Wazalendo.
New Picture (9)
Wanachadema wakiwa nje ya ofisi ya chama wilaya walikokwenda kurudisha kadi kabla ya kuhamia ACT wazalendo.
New Picture (3)
Wanachadema wakiwa nje ya ofisi ya ACT Wazalendo ambako walifika kuomba kujiunga huko.
New Picture (10)
Wanachadema wakirudisha kadi za chamna hicho na kujiunga na ACT wazalendo.
New Picture (11)
Kadi zikiwa zimekusanywa kwa kuchomwa moto.
New Picture (12)
Hivi ndivyo kadi zinavyoteketezwa kwa moto baada ya wana Chadema kujiengua na chama hicho na kujiunga na ACT wazalendo
.
New Picture (2)  New Picture (4)New Picture (5)
Hasira za kukatwa kwa mshindi wa kura za maoni Ludewa.
New Picture (1)
Wanachama wa Chadema waliohamia ACT wazalendo wakiwa na mabango ya kukituhumu chama hicho kwa kukiuka Demokrasia.
New Picture (6)New Picture (7)New Picture (8)     New Picture (13)

BALOZI MPYA WA TANZANIA NCHINI MAREKANI MHE, WILSON MASILINGI AWASILI WASHINGTON DC.

$
0
0
    Balozi mpya atakayeiwakilisha Tanzania nchini Marekani Mhe Wilson Masilingi akiwa amefuatana  na Mkewe  Marystella Masilingi pamoja na mwanae Nelson Masilingi wawasili kituoni kwake Washington DC, awali ya hapo Mhe Wilson Masilingi alikua Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi.
Mhe Wilson Masilingi mara baada ya kutua Washington DC akisalimiana na atakayekua dereva wake Virgilio Paz maarufu kama Bong.
Safari ya Mheshimiwa Balozi pamoja na mama ikianza kuelekea Hotelini kwake ambapo atapumzika kwa muda kabla ya kuingia nyumbani kwake Bethesda ,Maryland.
Mhe Wilson Masilingi mara baada ya kufika Hotelini kwake akisaidiwa mlango na Afisa wa Ubalozi Swahiba Habib Mndeme.
Mhe Balozi Wilson Masilingi akisalimiana na baadhi ya Maafisa na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani waliofika kumlaki pichani ni mmoja wa Maafisa Andrew Mugendi Zoka.
Mama Marystella Masilingi naye hakua nyuma kusalimiana na baadhi ya Wafanyakazi na Maafisa wa Ubalozi wa Tanzania.
Mhe Wilson Masilingi akiwa na bashasha tele kuona kwa jinsi gani Tanzania House walivyo na upendo na kuonyesha ushirikiano wao wa dhati kwenye tukio hilo muhimu.
Mhe Wilson Masilingi alifuatana na Mtoto wake Nelson Masilingi.
Maafisa wa Ubalozi Swahiba Mndeme pamoja na Alfred Swere wakiteta jambo kidogo.
Mhe Balozi Wilson Masilingi pamoja na Familia yake kwenye picha  ya pamoja na Mwambata wa Jeshi Col. Adolph Mutta.
Mhe Wilson Masilingi alipata fursa kidogo kutembelea mitaa ya jijini akiwa ameongozana na Mwambata wa Jeshi Col. Adolph Mutta

Baadhi ya Wafanyakazi na Maafisa wa Tanzania House wakiwa Hotelini alipofikia Mhe Wilson Masilingi.
   PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI KWA PICHA ZAIDI UNGANA NASI PUNDE.

CCM YAZINDUA KAMPENI ZAKE KWA KISHINDO JIJINI DAR LEO,MAELFU WAFURIKA KUSHUHUDIA TUKIO HILO

$
0
0
 Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli pamoja na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan wakionyesha Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015-2020  katikati ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye aliwakabidhi ilani hiyo kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM Jangwani.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi wa kampeni kwenye viwanja vya Jangwani.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 -2020
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan ilani ya uchaguzi ya CCM kwenye uzinduzi wa kampeni uliofanyika viwanja vya Jangwani.
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikweteakizungumza baada ya kukabidhi ilani kwa mgombea wa CCM
 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha.



 Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia) akiwa pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM jijini Dar es Salaam.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar es salaam waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam.


 Umati wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwa wamefurika kwa wingi kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM Jangwani.





 Hii ndio CCM
 TOT wakitoa burudani kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM jijini Dar es Salaam.
 Wasanii wa bongo wakiwa jukwaani.











WAZIRI MKUU AKABIDHI MSAADA WA MAGARI YA WAGONJWA KWA HOSPITALI ZA WASSO NA ENDULENI

$
0
0
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Florens Turuku (mwenye tai) akieleza umuhimu wa magari ya wagonjwa kwa Hospitali za Wasso na Enduleni za Wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati wa kukabidhi msaada wa magari hayo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye ameyapta kutoka kwa wafadhili wa nchini Japan, leo Jijini Dar es Salaam, Tarehe 24 Agosti, 2015.
 Wakuu wa Idara na Vitengo Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Florens Turuku (mwenye tai) akieleza umuhimu wa magari ya wagonjwa kwa Hospitali za Wasso na Enduleni za Wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati wa kukabidhi msaada wa magari hayo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye ameyapta kutoka kwa wafadhili wa nchini Japan, leo Jijini Dar es Salaam, Tarehe 24 Agosti, 2015.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Florens Turuku (mwenye miwani) kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi Katibu Tawala Msaidizi (Utawala) mkoani Arusha Richard Kwitega, funguo za magari ya wagonjwa kwa Hospitali za Wasso na Enduleni za Wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, gari hizo Waziri Mkuu amezipata kutoka kwa wafadhili wa nchini Japan, leo Jijini Dar es Salaam, Tarehe 24 Agosti, 2015.
Katibu Tawala Msaidizi (Utawala) mkoani Arusha Richard Kwitega akijaribu kuwasha moja ya gari la wagonjwa  ambalo limetolewa msaada kwa Hospitali za Wasso na Enduleni za Wilayani Ngorongoro mkoani Arusha kutoka kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amepata gari hizo kutoka kwa wafadhili wa nchini Japan, leo Jijini Dar es Salaam, Tarehe 24 Agosti, 2015.

MAWAKALA WA AIRTEL MONEY MKOA WA DAR ES SALAAM WAPATA MAFUNZO

$
0
0
 Meneja Mafunzo ya Biashara wa Airtel Tanzania, Ayubu Kalufya akitoa

elimu kuhusu huduma mpya ya ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, wakati wa mafunzo kwa mawakala wa Airtel Money wa mkoa wa Dar es Salaam jana.


 Meneja Mauzo wa Airtel Tanzania Kanda ya Ilala, James Moilo akitoa
elimu kuhusu huduma mpya ya ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, wakati wa mafunzo 
kwa mawakala wa Airtel Money wa mkoa wa Dar es Salaam jana.
 Wakala wa Airtel Money Tabata, Sabas Ngwira akiuliza swali kuhusu huduma mpya ya ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, wakati wa mafunzo kwa mawakala wa  Airtel Money wa mkoa wa Dar es Salaam jana.
  Wakala wa Airtel Money Ukonga, Grace Kimaro  akiuliza swali kuhusu
huduma mpya ya ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, wakati wa mafunzo kwa mawakala 
wa Airtel Money wa mkoa wa Dar es Salaam jana.
 Sehemu ya Mawakala wa Airtel Money mkoa wa Dar es Salaam wakifuatilia

mafunzo kuhusu huduma mpya ya ‘Timiza Mikopo kwa Wakala’, iliyofanyika
jijini jana.

KAMPUNI ya Simu za Mkoni ya Airtel imetoa semina kwa Mawakala wa Airtel Money zaidi ya 400 kwa lengo la kuwaongezea mbinu mbalimbali za


 ujasiriamali huku wakinufaika kupitia huduma ya mikopo kwa wateja maarufu kama Timiza Mkopo kwa Wakala.




Kupitia semina hiyo mawakala wa Kampuni hiyo wataweza kuona fursa
mbalimbali za kibiashara na kutumia mikopo hiyo isiyo na dhamana
watakayopata kutoka Airtel kukuza biashara zao na kuongeza mitaji.


Akizungumza wakati wa Semina hiyo Meneja Mauzo wa Airtel Money Moses
Alphonce alisema kupitia mafunzo hayo mawakala wataweza kuongezea
faida zaidi na hatimaye kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha nchini.




“Wajasiriamali wengi wamekuwa wakitumia mikopo wanayopata kwa ajili ya matumizi ya kawaida, kupitia semina hii, mbali ya kuwaunganisha mawakala wetu wa Jijini pia watafahamu mbinu bora za kutenganisha fedha za mtaji na binafsi,” alisema Alphonce



Kuhusiana na namna mawakala hao wanavyoweza kuchangia kukuza uchumiAlphonce alisema, fedha watakazokopa zinaweza kuanzisha biashara nyingine  itakayoingiza kipato na kutoa ajira kwa ndugu na jamaa wanaowazunguka.



Kwa upande wake Mtaalamu wa Biashara wa Financial sector Deepening
Trust(FSDT)   Innocent Ephram ambaye alikuwa Mwezeshaji wa semina hiyo
amesema wajasiriamali wengi wameshindwa kukuza biashara zao baada ya
kuchanganya matumizi ya biashara na ya kwao binafsi.

 “Kupitia warsha hii wajasiriamali watapata fursa ya kufahamu athari za
kuchanganya matumizi ya biashara na maisha ya kila siku, jambo ambalo
linachangia hasara na kufa kwa mtaji,” alisema Mtaalam huyo kutoka FSDT.

Baadhi ya mawakala hao kutoka Manispaa zote tatu za Mkoa wa Dar es Salaam akiwemo Salama Sinani,Gorich Mlaki na Sabas Ngwillah walisema mafunzo hayo  sasa yamewapa mwanga wa kuifanya kazi hiyo kama ajira na tofauti na awali  ambapo waliiona kazi ya uwakala kama jambo la ziada tu.

“Nilikuwa naona kazi ya uwakala kama kazi ya ziada, sasa nitaweza kuchukua mkopo kupitia Timiza Mkopo kwa Wakala nitaanzisha biashara nyingine   itakayonikomboa kuondokana na umaskini,” alisema Gorich Mlaki anayefanyia  kazi zake Hospitali ya taifa Muhimbili jijini.



Agosti 18 mwaka huu Airtel ilizindua mkopo huo utakaoanzia Shilingi 50,000
hadi 500,000 utakawanufaisha zaidi ya mawaka 20,000 wa Airtel Money



utaendeshwa na Airtel kwa kushirikiana na Afb Tanzania.

MAKAMU WA RAIS MHE. DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL AKUTANA NA MABALOZI WATEULE LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi mteule wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt. Gen. Charles Lawrence Makakala na Balozi Mteule wa Tanzania Nchini Uholanzi Mhe. Irene Florence Mkwawa Kasyanju wakati Mabalozi hao kwa pamoja walipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake Ikulu Dar es salaam leo. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal katikati akiwa katika picha ya pamoja naBalozi mteule wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt. Gen. Charles Lawrence Makakala na Balozi Mteule wa Tanzania Nchini Uholanzi Mhe. Irene Florence Mkwawa Kasyanju wakati Mabalozi hao kwa pamoja walipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake Ikulu Dar es salaam leo (Picha na OMR) 

MWAKILISHI WA MAREKANI AMTEMBELEA WAZIRI CHIKAWE OFISINI KWAKE JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Mwakilishi Maalumu wa Marekani katika Eneo la Maziwa Makuu, Thomas Perriello (katikati) akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) wakati wa mazungumzo yao kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Marekani na Tanzania. Hata hivyo, Mwakilishi huyo aliipongeza Tanzania kwa kupokea na kuhifadhi Wakimbizi nchini. Kushoto ni Naibu Balozi wa Marekani nchini, Bibi Virginia Blaser. Mwakilishi huyo akiambatana na Naibu Balozi, walimtembelea Waziri Chikawe ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akimfafanulia jambo Mwakilishi Maalumu wa Marekani katika Eneo la Maziwa Makuu, Thomas Perriello (katikati) wakati wa mazungumzo yao kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Marekani na Tanzania. Hata hivyo, Mwakilishi huyo aliipongeza Tanzania kwa kupokea na kuhifadhi Wakimbizi nchini. Kushoto ni Naibu Balozi wa Marekani nchini, Bibi Virginia Blaser. Mwakilishi huyo akiambatana na Naibu Balozi, walimtembelea Waziri Chikawe ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (katikati) akimkaribisha Mwakilishi Maalumu wa Marekani katika Eneo la Maziwa Makuu, Thomas Perriello (wapili kushoto), Naibu Balozi wa Marekani nchini, Bibi Virginia Blaser (kushoto), pamoja na wasaidizi wa viongozi hao wanaoiwakilisha Marekani (kulia), kabla ya kuanza mazungumzo yao kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Marekani na Tanzania. Hata hivyo, Mwakilishi huyo aliipongeza Tanzania kwa kupokea na kuhifadhi Wakimbizi nchini. Mwakilishi huyo akiambatana na Naibu Balozi, walimtembelea Waziri Chikawe ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo. 
Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

PRESIDENT MUSEVENI ADDRESSES EALA IN KAMPALA

$
0
0
 President Yoweri Museveni shakes hands with the Deputy Clerk of EALA, Alex Obatre as Executives of the EAC and Parliament of Uganda look on
 H.E. Yoweri Kaguta Museveni signs the visitors book at the Parliament of Uganda as the EALA Speaker, Rt. Hon Daniel F. Kidega looks on  
 H.E. President Museveni stresses a point at the Special Sitting.  On right is the EALA Speaker, Rt Hon Daniel F. Kidega.

EAST African Legislative Assembly, Arusha, August 24, 2015:  President Yoweri Kaguta Museveni Friday addressed the 1st of the 4th Session of 3rd Assembly at the Parliament of Uganda in Kampala.

In his address, the President termed prosperity and security of the region as two key ingredients necessary to keep integration process on track.  He urged the EAC to support prosperity of the producers in the agricultural sector to support integration.  

“Prosperity is about services, markets and it is important to leverage and take advantage of the market”, H.E. Museveni said. The President maintained that it was time for the region to consolidate on the gains realised in the region

The President said that Uganda was key to export its agricultural products in the EAC region including sugar products.  “Uganda is today producing more sugar than it needs.  Following the discussions with H.E. President Uhuru Kenyatta recently, we have agreed to open the market for this products further”, he said.  

The President maintained that Uganda was similarly open to receiving goods from Kenya under the integration arrangement. President Museveni said Kenyan exports to Uganda are estimated at $700 million up from $200 million in 1986 compared to imports worth $150 million up from $12 million in the same period.


He thanked President Kenyatta for agreeing to remove non-tariff barriers, deepen commercial ties and widen the regional market. President Museveni remarked that Uganda produces about 465,000 tonnes of sugar annually against a consumption of 320,000 tonnes, leaving it with a 145,000-tonne surplus.

He called on the EAC bloc to negotiate together with other blocs in the globe. “We have a reasonable market now and we can effectively compete. Let us negotiate with China and other big players”, he said.

The President called on Partner States to add value to production in order to enjoy competitiveness. “The Federal Republic of Ethiopia which has a population of 90 Million people, today assembles its automobile industries and this has led to creation of employment of over 160,000 jobs for the locals.   Automobile assemblage can reduce costs by 57%,” he said.

President Museveni said he submitted proposals to the Summit of EAC Heads of State to explore the possibility of local assemblage of vehicles.    “We need to create jobs, transfer technology for the region to be prosperous”, President Museveni told the attentive audience.

The President maintained that the EAC was on course and its progress irreversible. The President noted that the Community was on the verge of prosperous economic development and better quality of life for its citizens following the significant progress in a number of socio-economic and political spheres.

The Head of State hailed the forefathers of EAC for their visionary leadership. “I hail President Moi and Mwinyi who together with myself resurrected integration after seeing the benefits. I am grateful to them and we have since moved together, making tremendous progress” he added.

He lauded EALA for initiating the EAC Creative and Cultural Industries Bill saying it gave citizens such as performing artists to advantage of integration and to widen their markets.

On Security, the Head of State said that strategic security was key.  “We must put our interests fast and secure ourselves from those who want to dominate us, he said, adding that it was time for challenges such as NTBs to be weeded out once and for all.

He said Uganda was mapping strategies to be a first world country in the next 20 years and thus deemed it necessary to fight for its competitive space.  ‘Even if these were to happen, the question is how secure would Uganda be by itself?The President paused.

The Head of State said the region was opening up and clearing up strategic bottlenecks to be more prosperous.  He said the market fragmentation was now been consolidated. 
He however cited the challenges of insecurity faced in Burundi, South Sudan and Congo and said solutions were necessary.

H.E. Museveni said a better infrastructure was now been realized and said the region was on the way to deepening economic integration. The President gave a nod to EALA Speaker’s request on modalities to streamline assent of Bills during the meeting of the EAC Heads of State. 

“The principle of jointly signing (assent) of Bills when we sit as Summit is a good idea if we can finalise on the modalities”, H.E. Museveni said. The Head of State remarked that what the region now needed was to strengthen competitiveness, address costs doing business and reduce risks.

In attendance were key government officials led by the Prime Minister of the Republic of Uganda, Rt Hon Dr Ruhakana Rugunda, EALA and Parliament of Uganda Members and representatives of the diplomatic corp among others.

In his welcome remarks, the Speaker of the EALA, Rt. Hon Daniel F. Kidega noted that the Sitting was taking place at an irreversible time in the regional integration process. He called on the Summit of EAC Heads of State to hasten the process of the Monetary Union and inevitably the Political Federation.  He told President Museveni and the Summit of the EAC Heads of State to revisit the issue of the fast-tracking the Political Federation

“This will enable us to be stronger and more united for without the Political Union, we shall remain vulnerable to world forces,” Rt. Hon Kidega noted.The EALA Speaker noted that the Assembly had made progress since December 2014 and cited some of the milestones realized.

“Since I took over the Speakership of the Assembly in December 2014, the Assembly has passed a total of 6 Bills, 5 Resolutions, adopted 12 Reports and asked the Council of Ministers to respond to sets of questions deemed vital to strengthening the EAC. 

We have also received 2 petitions from the youth and the regional Workers’ Union and the employer association. Both petitions are currently under review by the relevant Committees of EALA.  Our representative function has continued to be felt through engagements with different stakeholders even though this is an area we need to further strengthen”, he said.

The Assembly which commenced business on August 16th, 2015 has debated and adopted two key Committee Reports; one on investment Strategies in the region and another on the Legal Framework and implementation policies on the rights of Children.  It has also commenced on debate on the EAC Cultural and Creative Industries Bill, 2015.

The Speaker cited challenges facing the Assembly as that concerning the Assent of Bills stating that it was necessary to speed up the processes.“Whilst it is purely in order for Heads of State to receive briefs, before assenting to Bills, the logistical mode of having to move from one Partner State to another in itself present challenges.

We are of the view that the region takes advantage of the Summit sittings which can create opportune moment for the Summit Members to exercise their mandate as stipulated under Article 63.  Your Excellency, we shall seek your further advice on this matter” Speaker Kidega said. 

The Speaker also called on the stakeholders to ensure electioneering in the region does not disrupt nation building.“Unpatriotic politicians and citizens the Speaker noted, can stir emotions leading to disruption in society, erosion of investor confidence and lull in economic programmes, Speaker Kidega said. He urged stakeholders in the Partner States to reverse the trend.

There are undeniably some positive democratic milestones that we can be proud of as a region. There are also grave mistakes that we have made and that we must steer clear of in future.  We appeal to all actors concerned with elections as a matter of necessity to ensure citizens’ enjoy their fundamental political and civil liberties, promote a culture of peace and tolerance and insulate electoral management bodies from undue pressures. 

In this way, we stand to secure the future of our region for posterity, the regional Assembly Speaker stated.   Moving the vote of thanks, Hon Saoli Ole Nkanae noted that Uganda had progressed following the leadership of President Museveni.

“I have followed your history closely. Came from humble beginnings.  In the short span, he has transformed country from sectarian dictatorship that was non-performing to an economic country with opportunities for all”, Hon Nkanae said.

“Your role in resurrecting the EAC Community is laudable and we note that you have continued to fast-track integration and offer good leadership”, the legislator said.

 Hon Nkanae said that EALA was committed to actively playing its mandate to strengthen integration.

TATIZO LA MAJI KILOLO NA ISMANI LAISUMBUA SERIKALI WADAI KUTOKUTHAMINIWA NA VIONGOZI

$
0
0
WANANCHI wa vijiji vya Ilole, kitumbuka, Ilambilole, Ikengeza, Chamdindi  na vingine vilivyopo Katika wilaya ya Kilolo na Ismani mkoani Iringa wailalamikia serikali kwa kushindwa kutatua kero ya maji iliyodumu kwa muda mrefu Katika maeneo hayo.

Wakizungumza kwa huzuni mbele ya mkuu wa mkoa wa Iringa aliyefanya ziara ya kugagua miradi ya maji Katika wilaya hizo Mh Amina Masenza wananchi hao walisema kumekuwa na ubabaishaji wa kisiasa juu ya namna ya kupelekewa maji jambo ambalo linawafanya waweze kutumia maji yasiyo salama kwa afya zao.

Wananchi hao walisema kumekuwa na miradi ya maji mingi ambayo ilitajiwa kuwanzishwa Katika wilaya zao lakini mpaka sasa hakuna utekerezaji wowote juu ya kutatua kero hizo pamoja na kuwa na vyanzo vizuri vya maji.
 “mh mkuu wa mkoa tumeahidiwa sana juu ya kuletewa maji safi huku vijijini matokeo yake hakuna lililofanyika tumekuwa watu wa kudanganywa kabisa hata tukiangalia umbali wakilipo chanzo cha maji hata wangesema tuchimbe mitalo wenyewe tungechimba ila wanatudanganya na siasa zao hatuyajui maji ya baridi toka tunazaliwa tunatumia maji ya chumvi tuoneeni huruma jamani” walisema wananchi

Akijibu kero za wananchi hao mkuu wa mkoa Amina Masenza alisema kumekuwa na watumishi wa serikali ambao wamepelekwa kusomea utalamu huo lakini bado hawafanyi kazi sawasawa na elimu zao ambapo ameahidi kulishughulikia jimbo hilo pamoja na kusimamia miradi mipya iliyopo ili iweze kuwanufaisha wananchi kwa kupata huduma hiyo kwa urahisi.

“nimesikia kilio cha wananchi sitakubali haya yaenelee kutokea wakati kuwa watu wanapelekwa kusoma na serikali halafu hafanyi inavyotakiwa tafadhari nataka kuona kazi mnayo ifanya ili wananchi hawa waweze kupata maji kwa wakati kulinga na elimu zenu haiwezekani wananchi wangu wakawa wanaumia na nyie mpo hapa haitawezekana”alisema Masenza

Aidha aliwaagiza watendaji wa halmashauri na wataalamu wa sekta ya maji kufanya uchunguzi Katika maeneo ambayo yanalalamikiwa na wananchi ili kubaini chanzo cha tatizo na kukiondoa ili kuruhusu upatikanaji wa huduma hiyo ikiwa n sambamba na wafugaji wanaotumia maji ya mto kunywesha mifungo yao swan a watumiaji wengine wa kawaida ili kulinda usawa Katika matumizi ya maji.

“ninawaagiza kuanzia leo nendeni kuchunguza nini tatizo nataka majibu kuanzia sasa na mniambie tatizo ninini linalofanya wananchi hawa wasipate maji mradi umefika na pia wanaelimishwa juu ya matumizi ya mita na wale wanaonywesha mifugo kwa mito wanatakiwa kulipiwa maji kwa kadiri na idadi ya mifugo aliyonayo”alisema masenza

Kwa upande wake Injinia wa Maji na meneja mradi wa Maji vijijini Bw Endru Kisaru alisema kwasasa wanaongeza nguvu ya udhibiti wa matumizi ya maji kwa kufunga mita kwani kwa sasa Katika jimbo la ismani idadi ya watumiaji inakaribia 15000 ambapo kila kaya inaweza kulipa kiasi cha sh 5000 kwa mwaka ambapo tayari Unit 267 zimefungwa Katika maeneo hayo hivyo amewahakikishia wananchi kwa tatizo na kero hiyo ya maji itamalizika kwa wakati muafaka


“tutajitahidi kutengeneza miundombinu ya maji itakayo hakikisha tunawafikishia huduma ya maji wananchi wengi zaidi nawaomba wananchi wawe na uvumilivu wakati tunaendelea kutatua baadhi ya changamoto zilizopo”alisema kisaru.

MUZIKI MNENE BANGO KIMARA

$
0
0
 Mr Jimmy Jiam akiwa na mshindi kwa  kuweka  stika za kutosha kwenye sehemu yake ya biashara na kupata t-shirt yake mpya ya EFM aliyozawadia na bwana E kufuatia.
 Mamalishe akikabidhiwa zawadi na bwana E Mr Jimmy Jiam baada ya kuweka stika kwenye sehemu yake ya kazi eneo la Kimara, jijini Dar Es Salaam.
Bwana E Mr jimmy Jiam akimpa zawadi na kumshurukuru mfanyabiashara kwa kusikiliza 93.7 EFM na ku weka bango la EFM kwenye eneo lake la biashara. 

Bwana E anapokutana na shabiki wa 97.3 EFM dereva wa bodaboda akiwa amevaa T-shirt ya EFM Muziki Mnene na akiwa ameweka stika ya EFM kwenye helmet yake. 
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images