Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

RFB yafanikiwa kufanya maboresha ya barabara kwa kiwango cha lami nchini

$
0
0
unnamed (100)
Meneja Mfuko wa Barabara Bw.Joseph Haule akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam hivi karibuni alipokuwa akiwasilisha ripoti ya mafanikio ya utekelezaji wa Mfuko wa Barabara kwa  Serikali ya awamu ya nne.
unnamed101
Naibu Meneja Masuala ya Kiufundi Bw. Ronald Lwakatare kutoka Taasisi ya Mfuko wa Barabara akizungumza na waandishi  wa habari hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
……………………………
Na Lorietha Laurence-Maelezo
Bodi ya Mfuko wa Barabara nchini(RFB) imefanikiwa kufanya maboresha ya barabara kwa kiwango cha lami katika kipindi cha miaka kumi ya uongozi wa Serikali ya awamu ya nne wa Mhe. Jakaya Kikwete.

Akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam Jana Bw.  Joseph Haule amesema kuwa matengenezo hayo yamefanikisha ujenzi wa  barabara kuu  zinazounganisha mikoa mbalimbali nchini kukamilika kwa asilimia 89 huku zile za Wilaya na Miji kwa asilimia 57.  

“ kazi kubwa ya Mfuko huu ni kukusanya mapato kupitia vyanzo mbalimbali   ikiwemo tozo za barabarani na  ushuru wa mafuta na baadaye  kuzigawa kupitia taasisi zinazohusika na ujenzi wa barabara ikiwemo TANROADS, Wizara ya Ujenzi na Ofisi ya Waziri Mkuu “ alisema  Bw. Haule

Aidha aliongeza kuwa  Mfuko huo umefanikisha ujenzi wa daraja  la Mabatini jijini Mwanza ,daraja la Mwanhunzi  na daraja la Mbutu  linalounganisha Igunga na Shinyanga   pamoja na ununuzi wa vivuko  kikiwemo kile cha Mv Malagarasi.Mbali na hayo Bw.Haule aliongeza kuwa Bodi hiyo inaendelea kuhakikisha barabara  zinatunzwa  kwa  kudhibiti magari ya mizigo yanayozidisha uzito unaochangia uharibifu wa barabara  kwa kuanzisha mfumo wa kisasa wa kamera  utakaokuwa unaratibiwa na mfuko huo.

Mfuko huo  umefanikiwa  kuanzisha ujenzi wa barabara kwa kutumia mawe ambao ni wa gharama nafuu na wa kudumu kwa muda mrefu,hata hivyo miradi hiyo imeanza kutekeleza katika mikoa ya Kigoma na Mwanza.

Kutokana na mtandao wa barabara  kufanyiwa matengenezo ya mara kwa mara imesaidia kuongeza ubora wa barabara na kupanua wigo wa biashara kati ya Tanzania na nchi za jirani ikiwemo Zambia,Malawi,Burundi,Rwanda na Uganda.

Mbali na mafanikio hayo Mfuko huounakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa bajeti kutokana na fedha zinazopatikana kutokukidhi  mahitaji.

MKUU WA MKOA WA DODOMA MHE. CHIKU GALLAWA AMEFANYA ZIARA YA UKAGUZI KWENYE SOKO LA WAMACHINGA LA REHEMA NCHIMBI COMPLEX MJINI DODOMA AGOSTI 12, 2015

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa (wa pili kushoto) akitembelea soko la wamachinga la Rehema Nchimbi Complex Mjini Dodoma wakati wa ziara yake ya ukaguzi sokoni hapo mapema leo, Wengine ni viongozi wa soko hilo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa akikagua eneo la vyoo vya soko la wamachinga la Rehema Nchimbi Complex Mjini Dodoma wakati alipotembelea soko hilo mapema leo.

 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa (katikati) akibadilishana mawazo juu ya changamoto za biashara na wamachinga wa soko la Rehema           Nchimbi Complex wakati wa ziara yake ya ukaguzi sokoni hapo mapema leo, wengine ni viongozi wa Wilaya ya Dodoma na viongozi wa soko hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Gallawa akiwa kwenye Picha ya pamoja na wafanyabiashara wa soko la machinga la Rehema  Nchimbi Complex baada ya kumalizika kwa ziara yake ya ukaguzi sokoni hapo mapema leo, wengine ni viongozi wa Wilaya ya Dodoma.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MGONJWA ANAYEHISIWA KUWA NA UGONJWA WA KUTOKWA DAMU MKOANI KIGOMA

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII



TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MGONJWA ANAYEHISIWA KUWA NA UGONJWA WA KUTOKWA DAMU MKOANI KIGOMA


 Utangulizi


Ugonjwa wa Ebola umeendelea kuenea katika nchi za Afrika ya Magharibi ambapo hadi sasa nchi tatu ambazo ni Guinea, Liberia na Siera Leone, zimeendelea kutoa taarifa za wagonjwa wapya. Aidha, mpaka tarehe 19 Julai 2015, idadi ya wagonjwa waliothibitishwa kuwa na ugonjwa huu ni 27,705 na vifo 11,269. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imejiandaa vyema kudhibiti ugonjwa huu iwapo utaingia nchini ikiwa ni pamoja na kutengeneza mpango kazi wa udhibiti wa ugonjwa huu wa miaka mitatu kuanzia 2015 hadi 2017.



Historia ya Mgonjwa

Mnamo tarehe 9 Agosti 2015, mgonjwa mwenye umri wa miaka 39 kutoka katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu alipokelewa katika hospitali ya Mkoa wa Kigoma Maweni akiwa na dalili za kutokwa na damu sehemu mbalimbali za mwili hasusan kwenye fizi, macho na masikio. Vile vile alikuwa na dalili za kuchoka na mwili kuwasha. 

Mgonjwa huyu hakuwa na homa. Alipata matibabu katika hospital hiyo na kwa bahati mbaya mnamo tarehe 10 Agosti, 2015 mgonjwa huyu alifariki dunia. Mgonjwa huyu alikuwa hana historia ya kusafiri kutoka nje ya mkoa wa Kigoma wala kutembelewa na mtu aliyesafiri kutoka nchi za Afrika Magharibi zenye ugonjwa wa Ebola.



Mgonjwa huyu alikuwa ni mkimbizi wa kutoka nchi ya Burundi ambaye ameishi katika kambi ya Nyarugusu kwa miaka mitatu. Mgonjwa huyu alikuwa mmojawapo wa wakimbizi waliokuwa wasafirishwe katika mpango wa kawaida chini ya Shirika la Kimataifa linalohudumia wakimbizi kwenda Marekani. Safari hiyo ilikuwa ianze tarehe 9 Agosti 2015.



Hatua zilizochukuliwa

  1. Mgonjwa huyu alipatiwa matibabu katika hospitali ya Maweni Kigoma mpaka mauti ulipomkuta.
  2. Uongozi wa Afya Kigoma unafuatilia ndugu wa karibu wa mgonjwa huyu, pamoja na wahudumu wa Afya waliomuhudumia mgonjwa huyu kuona kama wataonyesha dalili zinazofanana na ugonjwa aliokuwa nao mgonjwa huyu. Ufuatiliaji huo umeanza tarehe 9 Agosti 2015. Mpaka leo hakuna mtu mwingine, aliyeonyesha dalili za ugonjwa huu.
  3. Sampuli ya mgonjwa huyu imechukuliwa na kupelekwa kwenye maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii, ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii iliyopo Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi ili kujua chanzo cha ugonjwa huu.
  4. Mazishi ya marehemu huyo yamefanyika chini ya uangalizi wa Afya mkoa, kwa kuzingatia Utaratibu wa Kanuni za Kimataifa za kuzuia maambukizi.





Hitimisho

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kuwahakikishia wananchi kuwa mpaka sasa, hakuna uthibitisho wowote kuwa mgonjwa huyu amekufa na ugonjwa wa Ebola. Aidha kwa kuwa ugonjwa bado unaendelea nchi za Afrika Magharibi, Wizara inazidi kusisitiza wananchi kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa wa Ebola na magonjwa mengine ya kuambukiza. Ikiwa ni pamoja na

  • Kuepuka kugusa au kuingiwa na mate, damu, mkojo, jasho, kinyesi, machozi  na majimaji mengine yanayotoka  mwilini mwa mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa  wa Ebola kupitia sehemu zenye michubuko au vidonda.
  • Kuepuka kushughulikia maiti ya mtu aliyekufa akiwa na dalili za ugonjwa wa Ebola; badala yake watoe taarifa kwa uongozi wa kituo cha kutoa huduma za Afya kwa ushauri. Wataalam watasimamia maziko ikiwa kifo kitatokea.
  • Wananchi waepuke mila na desturi zinazoweza kuchelewesha kupata huduma muhimu na kuzidi kueneza ugonjwa wa Ebola.
  • Kutoa taarifa mapema kwa viongozi wa  Serikali na watoa huduma za Afya katika ngazi zote pale anapotokea mtu mwenye  dalili za ugonjwa wa Ebola.
  • Kuwahi katika vituo vya kutolea huduma za  Afya pale mtu anapohisiwa kuwa na dalili za  ugonjwa huu.
  • Kunawa mikono mara kwa mara ili kuepuka kusambaza ugonjwa ikiwa mtu atakuwa ameshika mgonjwa au mazingira yenye maambukizi.
  • Kutumia kemikali za kuua vijidudu kutakasa mikono.





Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii itatoa taarifa pindi majibu ya maabara yatakapopatikana.







Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali – Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii



12 Agosti, 2015

PRESS CLUB ZNZ YAFANYA UCHAGUZI NA KUSISITIZWA MAADILI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

$
0
0
 Katibu Mkuu msaafu wa Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Suzan Peter Kundambi katikati akitoa taarifa ya mwaka kwa Wanachama wa Jumuiya hiyo katika mkutano wa Mwaka wa ZPC ulioambatana na uchaguzi. Mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
 Wajumbe walioshiriki uchaguzi wa Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) wakipiga kura kuchagua uongozi mpya katika mkutano wa Mwaka wa Jumuiya hiyo ambao uliambatana na uchaguzi huo ambao uliofanyika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
 Wajumbe walioshiriki uchaguzi wa Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) wakipiga kura kuchagua uongozi mpya katika mkutano wa Mwaka wa Jumuiya hiyo ambao uliambatana na uchaguzi huo ambao uliofanyika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
Mweyekiti mpya wa Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) kulia akipongezana na aliyekuwa mpinzani wake katika nafasi ya Uenyekiti Suleiman Abdallah mara baada ya kutangazwa rasmi kuwa Mwenyekiti mpya katika uchaguzi uliofanyika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
Katibu Mpya wa Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Faki Mjaka akiomba kura kwa Wanachama (hawapo pichani)kabla ya kufanyika Uchaguzi huo. Katibu huyo anashika nafasi ya Suzan Peter mara baada ya kushika nafasi hiyo katika mkutano wa Mwaka wa Jumuiya hiyo uliambatana na uchaguzi huko ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.



Na Mwashungi Tahir-Maelezo Zanzibar
WAANDISHI wa habari nchini wamesisitizwa kulinda maadili ya kazi zao ikiwemo kutumia kalamu zao vizuri hasa kipindi hiki wanapoelekea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Imeelezwa kuwa ikiwa waandishi watatumia vibaya kalamu zao basi wanaweza kuvuruga hali ya amani na utulivu na kuweka nchi katika hali ya machafuko.

Hayo yalielezwa na Meneja Bima ya Maisha Tawi la Zanzibar Aisha Rubenic Makorogo, wakati akifungua mkutano mkuu wa Jumuiya ya Waandishi wa Habari uliombatana na Uchaguzi wa kuwachagua viongozi wapya uliofanyika katika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.

Alisema, kazi muhimu ya wanahabari ni kuona wanaendelea kutoa elimu kwa jamii na kutokubali kutumiwa vibaya na watu wenye maslahi binafsina badala yake wafanye majukumu yao kwa kutenda haki kwa pande zote ili nchi iweze kuvuka salama.

Aidha alisema, tasnia ya habari ni tasnia muhimu katika jamii ambayo inategemewa na kila mtu kwani inaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa wanachi wanaoishi mijini na vijijini kupata habari zinazotokea nchini kupitia vyombo wanavyofanyia kazi.

Meneja huyo, aliwaomba waandishi kufanya kazi kwa ueledi wa juu ili kuona nchi yao inaendelea kuwa na hali ya utulivu na usalama.Hata hivyo, aliwaomba wanachama wa ZPC kuchagua viongozi ambao wataweza kuiimarisha na kufanya Jumuiya yao iondokane na utegegemezi wa misaada huku wakiwa wabunifu ambao watachagua njia mbadala itakayowaletea kipato katika jumuiya yao.

“Ili kuweza kufanikiwa na jumuiya yenu kuimarika zaidi basi ni vyema kujenga mshikamano na wanachama wenu na kuwa wabunifu wa kutegemea vyanzo vingi vya kujiingizia mapato ili kuikuza jumuiya yenu,” Aliwaasa Meneja Aisha.Sambamba na hayo aliwaomba wanajumuiya hao kujiunga na Bima ya maisha ambayo inatoa fursa nyingi kwa malengo ya maisha ya baadae kwa mwanachama.

Nae Mjumbe mstaafu wa Kamati Tendaji wa Jumuiya hiyo Suleiman Seif Omar, akitoa shukrani kwa niaba ya wanajumuiya wenzake waliahidi kuendelea kudumisha maadili ya kazi zao na wajibu wao katika kuitumikia jamii.

Akizungumza kwa niaba ya Viongozi wapya Mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo Abdalla Abdul-rahman Mfaume aliwaomba wajumbe kuzidisha mashirikiano na kuwaahidi kufanya kazi kwa moyo mmoja ili kuiletea ZPC maendeleo na Taifa kwa ujumla.

Mkutano huo mkuu ulimchagua Abdalla Abdul-rahman Mfaume kuwa Mwenyekiti wa jumuiya hiyo baada ya kupata kura 40 na kumshinda mpinzani mwenzake Suleiman Abdalla ambae amepata kura tisa,Katibu Mtendaji wa ZPC Faki Mjaka ambaye hakuwa na Mpinzani alipata kura 46 na Naibu Katibu Mwinyimvua Nzukwi alipata kura 37 baada ya kumshinda Takdir Ali aliyeata kura 13.

Makamo Mwenyekiti wa Jumiya hiyo ni Abdalla Pandu aliyepata kura 28 na kumshinda Rahma Suleiman aliyepata kura 23. Mshika fedha Halima Tamim Thuwein aliyekuwa Mgombea pekee alipata kura 49 .Wajumbe sita wa kamati tendaji ni Aziza Hassan, Ghania Mohammed, Mwashamba Haji Juma,  Ishaka Omar, Maulid Hassan Kipevu na Saleh Hassan.

UNITED BANK FOR AFRICA TANZANIA RECOGNIZES BEST EMPLOYEE OF THE SECOND QUARTER

$
0
0
EMPLOYEE OF THE QUARTER-3
Relationship Manager Nicholaus Shimba (right) receiving his certificate from the COO Mr. Chris Byaruhanga (left) in recognition of his significant performance in the second quarter.
EMPLOYEE OF THE QUARTER-2
Relationship Manager Nicholaus Shimba giving a word of thanks after receiving his certificate in recognition of his significant performance in the second quarter.
Pic 3
Fellow staffs look on in joy for the overwhelmed Relationship Manager Nicholaus Shimba (right) receiving his certificate from the COO Mr. Chris Byaruhanga (left).
Pic 2
One of the staff taking an autograph enjoying the moment with the winner of the employee of the quarter Nicholaus Shimba (right).
Pic 1
A cross section of employees enthusiastically listening to the speech of the MC of the day M/S Queen Odunga the Customer Service Quality Officer not in pictures as she announces the employee of the second quarter.

Recognizing staff performance is very important, United Bank for Africa Tanzania is making sure that employees have a very conducive and motivated working environment.

Following the employee’s recognition scheme that aims at recognizing and rewarding examples of high achievement and desirable behavior, encourage excellence and commitment from employees and raises the high morale of employees by showing appreciation of their efforts, Mr. Nicholaus Shimba was announced on Friday as the employee of the second quarter for April to June 2015.

“We take great pleasure in recognizing Nicholaus Shimba as the United Bank for Africa Tanzania employee of the quarter for the period of April through June 2015.” The Chief Operating Officer Mr. Chris Byaruhanga said when handing over the award to the winner. He continued to say “the selection was based on Nicholaus’s demonstrated, sustained, superior performance in the execution of his duties.”

“I am so overwhelmed; I thank you my fellow staff for this achievement, if it were not for the dedicated Wholesale Banking team that I work with, this wouldn’t have happened. He continued to commend the bank for recognizing his efforts “United Bank for Africa is a very good employer they motivate us to do better thus performing with great zeal. Let’s continue to support each other so that the time comes when we are all up to our game.” Advised the employee of the second quarter winner, Nicholaus Shimba, Relationship Manager Wholesale Banking.

This scheme is intended to create a positive working environment, show employees how much they are valued and appreciated, aid in retention and recruitment, and foster a spirit of healthy competition.

“Please join me in congratulating Mr. Nicholaus Shimba and be encouraged to be one of the employees of the next quarter, to get the sport award and be the team of the month in the coming awards. Let’s be recharged, work hard and deliver results. Together we can make things happen!” Urged Mr. Mathias Ninga the Head of Human Capital Management and Resources.

The rest of the staff were happy with the selection conveying that Nicholaus is a very hardworking and dedicated chap with a systematic way of handling his responsibilities, “you see him struggle with his team to retain our customers and making things happen in a timely manner. He really deserves the recognitions” they acknowledged.

The occasion ended with the motivated employees asking the winner to sign autographs in their notebooks as way of appreciating this achievement. Working hard comes with a reward and with United Bank for Africa it is an affirmative recognition.

MODEWJI BLOG YARUDI HEWANI BAADA YA KWIKWI YA MASAA 45

$
0
0
modewjiblog logo
Baada ya kwikwi ya saa takribani 48 wataalamu wa Modewji blog wanakurejeshea hewani Blog yako pendwa.

Watundu wanaovuruga mambo mtandaoni (hackers) walijaribu kuimiliki blog hii kwa kufanya majaribio zaidi ya mara 300 yaliyosababisha mifumo ya kiusalama, kufanyakazi ya ziada kuihami Modewjiblog.
Hata hivyo wataalamu wetu wameziba mianya iliyokuwa imesababisha hali hiyo na sasa tupo pamoja nanyi.

Tunashukuru kwa uvumilivu wenu, tuko pamoja na endelea kuperuzi nasi.
Kwa mawasiliano zaidi tutumie email: info@modewjiblog.com
Imetolewa na Operation Manager, Zainul Mzige.

Rais Kikwete aongoza Kikao Cha Halmashauri Kuu mjini Dodoma leo

$
0
0
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu Mwenyekiti Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,Makamu Mwenyekiti Bara Ndugu Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakipiga makofi pamoja na wajumbe wengine muda mfupi baada ya kuingia katika ukumbi wa White House Makao Makuu ya CCM Mjini Dodoma tayari kuendesha kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM leo jioni.
 Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Waziri Kiongozi Mstaafu Shamsi Vuai Nahodha wakijadiliana jambo muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Halmashauri kuu ya CCM mjini Dodoma leo.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dkt.John Pombe Magufuli wakiteta muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Halmashauri kuu ya CCM mjini Dodoma leo. 
Picha na Freddy Maro.

MAKALA YA SHERIA: JE TRAFIKI ANARUHUSIWA KUKUNYANG”ANYA LESENI?

$
0
0
Na  Bashir  Yakub.
Kumekuwepo  na  sintofahamu   nyingi  kwa  madereva  na  watumiaji  wengine  wa  vyombo  vya  usafiri. Sintofahamu  hii  imekuwa  ikiletwa  na   baadhi  ya  mambo  ambayo  hayaeleweki  sawasawa  katika  suala  zima  la  usalama  barabarani   na  sheria  zake. Wadau   wa  barabarani wamekuwa  wakilaumiana,  madereva  wakiwalaumu  askari  wa  barabarani  kwa  uonevu  huku  askari  wa  barabarani  wakiwalaumu  madereva  kwa  ukorofi   na  ukosefu  wa  utii  wa sheria  bila  shuruti. Lakini  swali  hapa  ni  kwanini  iwepo  mivutano  na  hali  kuna  sheria. Sheria  inasemaje  kwa  kila  jambo  ambalo  wadau  hawa  wanatofautiana?. 

1.UBABE  WA  ASKARI  WA  BARABARANI.

Baadhi  ya  askari  wa  barabarani  wamekuwa  ni  wababe  sana. Wanahoji  mambo  ambayo   si  wajibu  wao  kuyahoji  na  hawataki  dereva  aulize  lolote  kuhusu  kuhoji  kwao  mambo  hayo. Wanataka  kila  wanachosema  dereva atii  hata  kama anaona  hakipo  kwa  mujibu  wa  sheria. Matokeo  yake  mtu  anaandikiwa  faini  za  makosa  mengi  ilimradi  tu  kumkomoa. Askari wengine  wamefikia  hatua  ya  kuwapiga madereva  vibao.  Binafsi  nimewahi  kushuhudia  askari  wa  usalama  barabarani  akimnasa  kibao  dereva wa  daladala. Ni  ubabe  uliovuka  mipaka  na  hakika  ni  uvunjaji  wa  sheria  uliopitiliza .

2.  JE  TRAFIKI  ANARUHUSIWA  KUMNYANGANYA  DEREVA  LESENI.

Masuala ya usalama  barabarani   yanaainishwa  ndani  ya  Sheria  ya  Usalama barabarani ( The  Road  Traffic Act) ambayo  ndio  hueleza  wajibu   na  haki  za  kila  mdau  na  mtumiaji  wa  barabara. Katika  sheria  hii  hakuna  pahala pameandikwa  kuwa  trafiki  achukue  leseni  ya  dereva  kwa  kuwa  dereva  ametenda  kosa   fulani. Maana  fupi  ya hili  ni  kuwa  trafiki  haruhusiwi  kuchukua  leseni  ya  dereva.  Anachoweza kufanya  trafiki  ni  kile  kilichoainishwa  na  kifungu  cha  17  cha  sheria hiyo  ya  usalama  barabarani. Kifungu  hicho  kinampa  trafiki  mamlaka  ya  kukagua  na kujiridhisha   na  uhalali  wa  leseni  ya  dereva. Hakisemi  aichukue. Kinasema  aikague  basi.  Kukagua  na  kuchukua  ni  mambo  mawili  tofauti.  

Kama  hivyo  ndivyo  basi  yafaa  kueleweka  kuwa   kitendo  cha  askari  kumsimamisha  dereva  na  kisha  kumpokonya  leseni  yake  ni  kinyume  cha  sheria.  Dereva  anao  wajibu  wa  kulinda   haki  hii  kwa  kulikataa  hili na kuhakikisha trafiki  hamfanyii  kitendo  hiki.  Kumbuka  kuwa  wakati  askari  wa barabarani  akitekeleza  wajibu  wake  wa kisheria  na  wewe  dereva  unayo  haki  ya  kutetea  haki  zako  za  kisheria. Hakuna  aliye  juu  ya  mwingine kwani  anatekeleza  wajibu  nawe  unalinda  haki.


VIJANA WALIOTIMIZA MIAKA 18 WAASWA KUPIGA KURA ILI KUCHAGUA VIONGOZI WANAO WATAKA.

$
0
0
Na Avila Kakingo,Globu ya jamii.
VIJANA waliotimiza miaka 18 kwa mwaka huu waaswa kupiga kura ili kumchagua kiongozi wanaemtaka na watambue mchango wao katika jamii kwa kupiga kura  kwaajili ya maendeleo ya taifa letu.

Nae Mwenyekiti wa  asasi isiyo ya kiserikaliTanzania People  with Disabilities Organization (TAPWAO), Michael  Mwanzalima ameomba tume ya uchaguzi  kutoa vipaumbele kwa  walemavu wa viungo mbalimbali siku ya kupiga kura ili isiwe kikwazo kwao katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu ili waweze kuwachagua viongozi wanao wafaa.

 Hayo yamesemwa na  vijana mbalimbali waliohudhuria katika mdahalo wa “ELEKEA UCHAGUZI 2015 NA VIJANA ”ulioandaliwa na  kampuni ya Tanzania Bora Initiative (TBI) ikiwa na nia ya kuadhimisha siku ya vijana dunia katika mdahalo uliofanyika katika hoteli ya New Afrika Dar es Salaam leo.

Pia katika mdahalo uliohusisha vijana mbalimbali hapa nchini ikiwa na wacheza muvi,waimba mziki wa kizazi kipya (Bongo freva) na vijana kutoka makampuni mbalimbali wakijadiliana kuhusiana na UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA 25 MWAKA HUU, vijana watashiriki vipi ili kuchagua kiongozi wanae mtaka.

Pia katika mdahalo huo uliambatana na  uzinduzi rasmi wa kampeni ya njia ya mtandao ya habari ujulikanao kama  UCHAGUZI 2015# KURA YETU.

 Mbunge wa viti maalumu (CCM) Maria Salungi akichangia maada kuhusiana na kijana anajitambuaje katika kuhamasika kupiga kura Oktoba 25 mwaka huu ili waweze kumchagua kiongozi wanae mtaka, kwa kuwa baadhi ya vijana ni mara yao ya kwanza upiga kura.
Le Mutus akizungumza katika mdahalo ulioandaliwa na Tanzania Bora Initiative uliofanyika katika hoteli ya New Afrika jijini Darr es salaam jana.
 Mwigizaji wa Bongo Muvi Rose Ndauka akichangia maada kuhusiana na waandishi wa habari vijana wanaweza kusaidia zaidi katika kufikisha ujumbe kwa vijana wengine ili waweze kwenda kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu utakao fanyika Oktoba 25 aliyazungumza hayo katika mdahalo uliofanyika katika hoteli ya New Afrika jijini Darr es salaam jana.
Mwenyekiti wa  asasi isiyo ya kiserikali hapa nchini ya Tanzania People  with Disabilities Organization (TAPWAO), Michael  Mwanzalima akizungumza katika mdahalo uliofanyika katika hoteli ya New Afrika jijini Darr es salaam jana, yeye akiwakilisha walemavu akiomba rai kwa  Tume ya uchaguzi kuwawekea mazingira rafiki katikauchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25 waweze kupiga kura bila  kikwazo chochote.
 Baadhi ya vijana waliohudhulia katika mdaholo uliofanyika katika hoteli ya New Afika jijini Dar es Salaam.
 wageni waalikwa wakiwa katika mdahalouliofanyika katika hoteli ya New Afika jijini Dar es Salaam.
Manzilishi wa kampuni ya Ekihya na mwenyekiti wa mdaholo uliofanyika katika hoteli ya New Afika jijini Dar es Salaam.akizungumza na vijana waliohudhulia mdahalo huo.


 Hamfrey Pole pole akizungumza katika mdahalo uliofanyika katika hoteli ya New Afika jijini Dar es Salaam. akiwaasa vijana wajitokeze katika upigaji kura wa mwaka huu utakaofanyika Oktoba 25 ili kuwachagua viongozi bora na sio bora viongozi.
Bandi ya muziki ambayo jina lake halikuweza kupatikana ikitumuiza katika  mdaholo uliofanyika katika hoteli ya New Afika jijini Dar es Salaam.
  Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

SHIWATA yakabidhi nyumba 16 Mkuranga

$
0
0
 Wasanii wakipata maelekezo kutoka kwa Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib (hayupo pichani) utaratibu wa kutunza nyumba walizogaiwa kwenye kijiji cha Wasanii Mwanzega, Mkuranga juzi .
 Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib akitoa ufafanuzi wa makazi mapya ya kijiji cha M\Wasanii Mwanzega, Mkuranga baada ya kugawa nyumba 16 kwa wasanii hao.
Picha ya pamoja.
 

Na Peter Mwenda

MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) imegawa nyumba nyingine 16 kwa wanachama wake waliokamilisha ujenzi ambako mpaka sasa wanachama 120 wamekabidhiwa nyumba zao katika kijiji cha Wasanii cha Mwanzega, Mkuranga.

Katika hafla ya kukabidhi nyumba hizo jana, Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema mpango wa ujenzi wa nyumba hizo ni endelevu mpaka hapo ekari 300 zilizotengwa kwa ujenzi zitajengwa nyumba kwa mpango wa kuchangiana.

Taalib alisema aina za nyumba zinazojengwa kwa sasa ni za matofali ya saruji ya chuma kimoja kwa sh. 750,000, nyumba za vyumba viwili na sebule kwa sh. 3.8 na nyumba kubwa ya sh. mil. 6.4.

Alisema kipa wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa, Hamisi Kinye anatarajia kukabidhiwa nyumba yake Desemba mwaka huu sambamba na wasanii wengine Lilian Ndelwa, Edson Mwela, Happyness Magere, Asheri Kazeba, Jaqueline Joseph na Suzan Moshi ambao wamebadilisha nyumba walizokuwa wakabidhiwe za udongo na sasa watachukua nyumba zilizojengwa kwa saruji.

Mwenyekiti Taalib alisema SHIWATA imeandaa mpango mkakati wa kuingiza umeme na maji katika kijiji hicho kabla ya Desemba na tayari kikundi cha wasanii kimepiga kambi ya kujiandaa kurekodi tamthilia ya maisha ya Bongo katika kijiji hicho.

Mmoja wa wasanii aliyekabidhiwa nyumba ya sh. mil. 6.4, Mwajuma Kisengo alisema ametimiza ndoto yake ya kushirikiana na wasanii wenzake kuishi katika kijiji cha Mwanzega, Mkuranga.

WATHAMINI MADINI VITO WAASWA KUWA WABUNIFU

$
0
0
 Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo (Kulia), akimwongoza Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Mhandisi Ngosi Mwihava kuingia Ukumbi wa Semina ya Wathamini Madini ya Vito na Almasi nchini, iliyofanyika Agosti 12 na 13 katika Hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza.
 Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT) Archard Kalugendo, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Mhandisi Ngosi Mwihava, Kaimu Kamishna wa Madini nchini Mhandisi Ally Samaje na Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Mrimia Mchomvu, wakijadili jambo muda mfupi kabla ya kuanza kwa Semina ya Wathamini Madini ya Vito na Almasi nchini, iliyofanyika Agosti 12 na 13, 2015 katika Hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza.
Meza Kuu – wakiwa katika Semina ya Wathamini Madini ya Vito na Almasi nchini. Semina ilifanyika Agosti 12 na 13, 2015 katika Hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza. Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Mhandisi Ngosi Mwihava, Kaimu Kamishna wa Madini Ally Samaje na Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Mrimia Mchomvu.

WATHAMINI MADINI VITO WAASWA KUWA WABUNIFU
Na Veronica Simba - Mwanza

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava amewataka Wathamini Madini ya Vito na Almasi nchini kuendelea kuwa wabunifu ili kutafuta majibu na suluhisho kwa changamoto zinazoikabili tasnia ya vito nchini.

Aliyasema hayo alipokuwa akifungua Semina ya Nne ya Wathamini Madini ya Vito na Almasi nchini iliyofanyika Agosti 12 na 13, mwaka huu katika Ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest, jijini Mwanza.

Mwihava alisema kuwa changamoto mbalimbali zinazoikabili tasnia hiyo zitaweza kuondolewa endapo watumishi katika kada hiyo watajituma kufanya kazi kwa uaminifu, weledi na ubunifu wa hali juu. “Napenda kuwakumbusha kwamba Watanzania wanataka kuona faida stahiki kutoka katika sekta ya madini hasa itokanayo na almasi na vito vingine; kadhalika hata mimi nataka kuona matokeo yanayopimika na malengo hayo kutimia na hata kuzidi viwango wanavyotarajia,” alisema Kaimu Katibu Mkuu.

Akifafanua zaidi, Mwihava aliongeza kuwa angependa kuona Soko la uhakika kwa Madini yanayopatikana nchini hususan Almasi na Vito ili Watanzania wanaojishughulisha na biashara hiyo wajue utaratibu wote.

Alisema kuwa angependa kuona wataalam hao wakitumia ipasavyo mitandao iliyopo katika kuwavutia wafanyabiashara na wakataji wa vito kuja nchini kununua na kuwekeza katika tasnia husika.

Aidha, Mwihava aliongeza kuwa angependa kuona wataalamu hao wa Madini ya vito na almasi wakitumia ujuzi wao katika kuwasaidia wadau wa tasnia husika kupata tafsiri sahihi na kuzingatia Sheria ya Madini ya mwaka 2010 pamoja na Kanuni zake.

“Nawaagiza mzingatie maadili na miongozo ya kazi katika utekelezaji wa majukumu yenu; msome na kuzingatia Sera ya Madini ya mwaka 2009, Sheria ya Madini ya mwaka 2010 pamoja na kanuni zake na Mkataba wa Huduma kwa Mteja,” alisisitiza Mwihava.

Vilevile, Kaimu Katibu Mkuu alitahadharisha kuwa yeyote atakayefanya kazi kinyume na matarajio, kwa kupokea rushwa, wizi au kufanya jambo jingine lolote kinyume na maadili ya utumishi wa Umma na kusababisha kuathiri juhudi zinazofanywa na Wizara, hatavumiliwa.

Akizungumzia mchango wa Serikali katika kuinua tasnia ya Madini ya vito na almasi, Mwihava alisema Wizara imeahidi kuongeza mapato yatokanayo na sekta ya madini ili kuongeza uwezo kwa Serikali kujitegemea katika bajeti yake.

“Endapo azma hii itafanikiwa, uchumi wetu kama Taifa utakua, fursa za ajira zitaongezeka na kipato cha Watumishi kitaboreshwa. Aidha, wananchi watapata huduma stahiki, muingiliano wa biashara utakua na hivyo kuchochea ufikiaji wa malengo ya Dira ya Taifa, yaani kuwa nchi yenye kipato cha kati ifikapo 2025.”

Alisisitiza kuwa suala muhimu zaidi ni kuhakikisha Watanzania wanaridhishwa na utendaji kazi wa watumishi wa Serikali hususan walioko katika kada husika na kuwaonyesha Watanzania kwamba wana uwezo wa kusimamia sekta husika kwa niaba yao na pia wananchi waone kwa maneno na vitendo kwamba kazi hiyo inafanyika vizuri.

Mwihava alihitimisha kwa kuwataka washiriki wa semina hiyo kuitumia kama fursa muhimu ya kujitathmini, kubadilishana uzoefu, kupeana mbinu za utendaji bora, kutafuta majibu ya changamoto mbalimbali zinazowakabili na kukumbushana maadili mema ya kazi na utumishi wa umma.

Alitoa changamoto kuwa anatarajia baada ya semina husika, wataalam hao wa sekta ya Madini vito na almasi watakuja na mkakati wa kuboresha ukusanyaji mapato ya Serikali kutoka katika tasnia ya almasi na vito, ili kuisadia Wizara kufikia malengo ya makusanyo na kuboresha utendaji wao. 

NHIF YATOA “DARASA” KWA BLOGGERS WA TANZANIA KUHUSU UCHAGIAJI WA BIMA YA AFYA CHINI YA MPANGO WA “KIKOA”

$
0
0
 MKURUGENZI wa Huduma na Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ya Jamii Tanzania, NHIF, Eugine Mikongoti
 MKURUGENZI wa Huduma na Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ya Jamii Tanzania, NHIF, Eugine Mikongoti, akifafanua jambo wakati alipokuwa akiwasilisha mada juu ya mpango wa uchangiaji binafsi, KIKOA, wakati wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa kwa pamoja kati ya NHIF, na Mtandao wa Bloggers Tanzania (TBN).Warsha hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Kurasini jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Bloggers wakimsikiliza  Mkurugenzi wa huduma na Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ya Jamii Tanzania, NHIF, Eugine Mikongoti, alipokuwa akiwasisilisha mada iliyohusu mpango wa uchangiaji binafsi, KIKOA kwenye warsha ya siku moja iliyoandaliwa kwa pamoja kati ya NHIF na Mtandao wa Bloggers Tanzania (TBN).Warsha hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Kurasini jijini Dar es Salaam.
  MKURUGENZI wa Huduma na Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ya Jamii Tanzania, NHIF, Eugine Mikongoti,akiwasilisha mada juu ya mpango wa uchangiaji binafsi, KIKOA, wakati wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa kwa pamoja kati ya NHIF, na Mtandao wa Bloggers Tanzania (TBN).Warsha hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Kurasini jijini Dar es Salaam.
 
 Baadhi ya Bloggers wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye Warsha hiyo
 Wadau wakifuatilia jambo
 Bloggers wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye warsha hiyo 
  Baadhi ya Bloggers wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye Warsha hiyo
Blogger Mzee Kitime akichangia jambo katika semina hiyo ya iliyoandaliwa kwa pamoja kati ya NHIF na Mtandao wa Bloggers Tanzania (TBN).Warsha hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Kurasini jijini Dar es Salaam.

MGEJA,GUNINITA WANGATUKA CCM ,WAJIUNGA CHADEMA

$
0
0
  Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja akizungumza na waandishi wa (habari  hawapo pichani )juu ya kungatuka katika chama hicho na kujiunga na Chadema leo katika ukumbi wa Idara ya habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Kulia ni John Gudinita.
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, John Gudinita akitangaza kujiuzuru katika chama hicho na Kujiunga na Chadema leo majira ya saa tano katika ukumbi wa Idara ya habari Maelezo jijini Dar es Salaam. kushoto Sheik Rajab Katimba na kulia ni Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja.
Aliyekuwa.Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga,Hamis Mgeja akionesha kuwa yeye ni chandema kwa sasa.
Wandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa CCM,Mkoa wa Shinyanga,Hamis Mgeja wakati akitangaza kujiuzuru katika chama hicho na Kujiunga na Chadema leo majira ya saa tano katika ukumbi wa Idara ya habari Maelezo jijini Dar es Salaam.

(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja amengatuka uanachama wa CCM pamoja kujiuzuru nafasi  ya Uenyekiti wa chama hicho.


Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam,Mgeja amesema kuwa ametafakari sana na kuona aungane na chama hicho.


Mgeja amesema kuwa anaondoka kwenda kutafuta mabadiliko katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kuongeza kuwa wametumikia chama hicho kwa muda mrefu lakini sasa imefika wakati wa kuondoka.


Aidha amesema kuwa CCM ya sasa imekuwa na vitu ambavyo vinafanywa na watu baadaye kuikigharimu chama kutokana na kuacha msingi wa kukubali maoni ya wanachama.


Wakati huo huo katika mkutano huo aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam,John Guninita naye amengatuka katika chama hicho na  kujiunga ba Chadema kuongeza nguvu Ukawa.


Guniinita amesema kuwa sasa umefika wakati wa kuondoka kutokana na Chama kuacha kusikiliza wanachama wake na badala yake kuendeleza chuki ndani ya Chama.

KONGAMANO LA VIJANA MKOANI MBEYA WAKATI WA KUAZIMISHA SIKU YA VIJANA DUNIANI.

$
0
0
 Mgeni Rasmi ambaye ni Afisa Vijana Halmashauri jiji la Mbeya  Onah Temu akitoa hotuba katika siku ya Vijana Duniani ambayo kwa Mkoa wa Mbeya ilifanyikia Ukumbi wa Chuo kikuu Cha Mzumbe Kampasi ya Mbeya.
 Maandamano kuelekea katika Ukumbi ambapo vijana wanakutana kwa ajili ya Sherehe yao
 Mratibu wa Mradi wa Restless Fadhiri Mtanga akitoa mada kuhusu Maendeleo ya Vijana 
 Wakili Stephen John akiwashauri vijana kuto tumika na wanasiasa
 Muwezeshaji wa Sherehe hiyo ya Vijana  Mwadawa Mbando akiendelea kutoa utaratibu
 Vijana wakisikiliza kwa makini watoa mada kaika sherehe hiyo iliyofanyika ukumbi wa Mzumbe Mbeya
 Mmoja wa vijana kulia akipokea zawadi baada ya kupokea zawadi
 William Otuku akitoa Maada kuhusu afya ya Uzazi kwa vijana

 Picha ya pamoja 

KATIKA maadhimisho ya siku ya Vijana duniani yaliyofanyika Kimkoa katika ukumbi wa Chuo kikuu cha Mzumbe Kampasi ya Mbeya, Vijana wamekumbushwa kuhusiana na afya ya uzazi kwa vijana pamoja na maendeleo yao.

Aidha katika kongamano hilo ambalo liliandaliwa na mashirika binafsi ya Restless Developmentna Young & alive initiative ambalo lilihudhuriwa na Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu na shule za Sekondari za Jiji la Mbeya.
Akizungumza katika kongamano hilo mwakilishi wa Shirika la Young & Alive Initiative, William Otuku, alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuwakumbusha vijana kuhusiana na maswala yanayohusu afya ya uzazi kwa vijana ili waweze kuwa na uwezo wa kushiriki shughuli za maendeleo wakiwa salama.

Aliongeza kuwa kauli mbiu ya siku hiyo ni kuhakikisha vijana wanashirikishwa na kuhusishwa  katika kupanga maamuzi mbali mbali hivyo hayo yote yanaweza kutimia endapo wataelimishwa kuhusiana na afya ya Uzazi ili waliomashuleni waendelee kufanya vizuri na kusaidia kutoa elimu kwa ambao hawako mashuleni.

“Vijana tunawapa elimuya afya  ya uzazi ili waweze kuwa imara katika kushiriki shughuli za maendeleo za kijamii pamoja na kuwaepusha na vitendo ambavyo vitaweza kuwaondolea katika hatari ya kupata magonjwa yanayoweza kuepukika” alisema Otuku.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa  Shirika la Restless Development,Fadhili Mtanga, alisema lengo la kongamano hilo ni kujadiliana kwa pamoja kuhusiana na changamoto ambazo zinawakabili vijana pamoja na kubadilishana mawazo juu ya kuweza kutatua na kukabiliana na vikwazo vya maendeleo kwa vijana.

Alisema lengo la kuwahusisha wanafunzi ni kutokana na kuwa na kundi kubwa la vijana wanaoanzia umri kati ya miaka 15 hadi 35 ambao ni kundi kubwa katika jamii hivyo ni rahisi kwao kupeleka mabadiliko kwa wananchi wengine ambao hawakubahatika kuhudhuria kongamano hilo.

“Sisi tumewalenga zaidi vijana ambao ni wanafunzi kwa sababu tunaamini wanakubalika kaika jamii na nirahisi kwao kutoa elimu ambayo iaweza kuwafikia wahusika kwa haraka zaidi” alisema Mtanga.

Naye Mgeni rasmi katika Kongamano hilo, Afisa Vijana wa Jiji la Mbeya, Ona Temu kutoka Ofisi ya Maendeleo ya Jamii Jiji la Mbeya, alipongeza kwa wadau kujitokeza na kuandaa kongamano hilo kwa kutambua mchango wa vijana katika jamii.

Alisema vijana wanapaswa kuutumia vizuri umri kati ya miaka 18 hadi 40 kwa kujenga na kutafuta uchumi ili kipindi cha miaka 40 hadi 60 anabaki kuwa msimamizi wa shughuli ambazo alizifanyia kazi kipindi cha ujana wake.

Aliongeza kuwa kipindi cha umri wa zaidi ya miaka 60 ni muda wa kufaidi matunda na kupumzika kwani utakuwa tayari umeshafanya kazi ya kutafuta na kuzisimamia vizuri kwa malengo makubwa.


PATO LA TAIFA ROBO YA KWANZA YA MWAKA 2015 LAFIKIA SHILINGI TRILIONI 21.9

$
0
0
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Morrice Oyuke (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu pato la taifa robo ya kwanza ya mwaka kuanzia Januari hadi machi 2015. Kushoto ni Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa, Daniel Masolwa.
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Morrice Oyuke (kulia), akisisitiza jambo katika mkutano huo.
Wapiga picha za habari na wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.


Na Dotto Mwaibale

MATOKEA ya Takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka bei za miaka inayohusika yameonyesha kuwa thamni ya pato la taifa katika kipindi cha robo ya kwanza ya 2015 ilikuwa ni sh. 21.9 trilioni ikilinganishwa na sh. 18.6 trilioni ya robo mwaka ya kwanza mwaka 2014.

Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Morrice Oyuke, wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu pato la taifa robo ya kwanza ya mwaka kuanzia Januari hadi machi 2015.


Oyuke alisema pato la Taifa kwa bei za mwaka 2007 katika kipindi cha robo mwaka ya kwanza linaonyesha kuwa jumla ya thamani ya shilingi 10.6 trilioni kwa mwaka 2015 ikilinganishwa na sh.trilioni 9.9 trilioni katika kipindi kama hicho kwa mwaka 2014.

"Hii inamanisha kuwa pato la taifa liliongezeka kwa kasi ya asilimia 6.5 katika kipindi cha robo ya kwanza mwaka 202015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 8.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2014" alisema Oyuke

Oyuke alisema kuwa shughuli za kiuchumi za kilimo na mifugo zilikuwa kwa kasi ya asilimia 2.6 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 3.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com



Airtel Fursa yaandaa semina ya Daraja la mafanikio kwa Vijana Mjini Mtwara.

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Fatma Salum Ally akifungua mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, yaliyofanyika kwenye Ukumbi VETA mjini Mtwara jana.
 Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi akizungumza wakati wa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, yaliyofanyika kwenye Ukumbi VETA mjini Mtwara jana.
 Meneja wa Airtel Mtwara, Bartholomew Masatu akitoa mada kuhusu fursa mbalimbali zinazoweza kuwakwamua vijana kiuchumi, wakati wa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, yaliyofanyika kwenye Ukumbi VETA mjini Mtwara jana.
 Mkufunzi kutoka Mpango wa Anzisha na Boresha Biashara yako (SIYB) ulio chini Shirika la Kazi Duniani (ILO), Fidelis Madaha akitoa mada wakati wa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, yaliyofanyika kwenye Ukumbi VETA mjini Mtwara jana.

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Fatma Salum Ally (kulia), akijadiliana jambo na vijana walionufaika na fursa za Airtel (kutoka kushoto), Iddy Salum Chilumba, Godfrey Frank Manjavila na Prisca George Chilumba baada ya kufungua mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, yaliyofanyika kwenye Ukumbi VETA mjini Mtwara jana. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (wa pili kulia) na Meneja wa Airtel Mtwara, Bartholomew Masatu.



Vijana mkoani Mtwara wametakiwa kutumia fursa za uwepo wa nishati ya mafuta na gesi katika kukuza biashara zao na uchumi wa mkoa huo.
Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa mafunzo ya ujasiriamali mkoani humo, baadhi ya vijana hao wamesema kuwa fursa zilzizopo mkoani humo ni lazima ziwanufaishe vijana ili waendane na ukuaji wa uchumi wa mkoa huo.

Kampuni ya Airtel Tanzania, kupitia mradi wake wa “Airtel Fursa Tunakuwezesha” imewapatia mafunzo na kuwawezesha mitaji baadhi ya vijana wa manispaa ya mtwara kwa lengo la kuwawezesha kumudu uendeshaji  biashara zao na kukuza mitaji yao.

Idd Abdallah ni mjasiriamali aliyenufaika na mafunzo hayo ambaye anasema kuwa kwa sasa amepata muongozo mzuri utakaokuza biashara zake na kuzifanya kwa weledi mkubwa zaidi.“Hii ni fursa ya kipekee kwangu kama kijana na ninaishukuru sana Airtel kwa mafunzo yenye manufaa kwangu na vijana wenzangu wa hapa mtwara” Alisema Abdallah.

Nae mkuu wa wilaya ya Mtwara bi.Fatuma Ally, alisema “mafunzo haya yatapanua wigo wa ufahamu kwa vijana hawa ambapo aliwataka kujituma kwani fursa zipo nyingi mkoani humo.
“Mtwara kuna maeneo mengi sana yenye fursa kwa vijana kujiendeleza hivyo nawataka vijana kutumia fursa na mafunzo haya kuhakikisha wanajiendeleza kiuchumi” alisema mkuu huyo wa wilaya.

Hawa Bayumi ni Meneja Maendeleo ya Jamii wa Airtel, alisema hiyo ni fursa inatolewa na Airtel kwa lengo la kusaidia vijana kupata fursa ya kujiajiri na kupata mitaji kupitia mpango huo.
“Kwetu sisi Airtel tunaona ni fahari kuwawezesha wajasiriamali kwa mafunzo na mitaji ili waweze kuendeleza biashara zao na kukuza mitaji pia. Alisema Bayumi.

Ugunduzi wa gesi na mafuta mkoani hapa, vijana wanapaswa kujituma kwa kuongeza elimu na mitaji ili waweze kuwa sehemu ya wanufaika na kuondoka na hali ya kuwa watazamani wa tunu hiyo.

BENKI YA EXIM TANZANIA YAFUNGUA TAWI JIPYA ZANZIBAR

$
0
0
Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim Tanzania Bw Selemani Ponda (wa pili kulia) akizundua tawi jipya la benki hiyo lililopo eneo la Mwanakwerekwe, Zanzibar wakati wa hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika Zanzibar hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni baadhi ya maofisa wa benki hiyo pamoja na wageni waalikwa.

TAMASHA LA KIMATAIFA LA SANAA NA UTAMADUNI KUFANYIKA SEPTEMBA 21-27, 2015 WILAYANI BAGAMOYO

$
0
0
 Mwenyekiti wa Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, John Mponda (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu tamasha hilo litakalofanyika kwa mara ya 34 kuanzia tarehe 21-27 Septemba katika ukumbi na viunga vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo ambao ndio wenyeji na waandaaji wa tamasha hilo kongwe Tanzania. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maonyesho ya tamasha hilo, Christa Komba na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi na Majukwaa, Frank Sika.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Maonyesho ya tamasha hilo, Christa Komba (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi na Majukwaa, Frank Sika (kushoto), akizungumzia maonyesho yanavyofanyika katika majukwaa.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Taarifa hiyo ikichukuliwa na wanahabari.


TAMASHA la kimataifa la sanaa na utamaduni Bagamoyo liliasisiwa mwaka 1981 na Chuo cha Sanaa Bagamoyo ambacho kwa sasa ni Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo. Lengo kuu la Tamasha kwa wakati huo ilikuwa ni kuwapa nafasi wanafunzi wa chuo cha sanaa kuonyesha kwa vitendo yale waliojifunza kwa mwaka mzima kwa kuwashirikisha wakazi wa Bagamoyo, baada ya Tamasha hilo kufanikiwa uongozi wa chuo uliamua tamasha hilo lifanyike kila mwaka kwa kushirikisha Vikundi mbalimbali vya ndani na nje ya nchi ili kubadilishana Uzoefu  na hivyo kujizolea umaarufu ndani na nje ya Tanzania.

Tamasha la kimataifa la sanaa na utamaduni Bagamoyo mwaka huu litafanyika kwa mara ya 34 kuanzia tarehe 21-27 Septemba katika kumbi na viunga vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo ambao ndio wenyeji na waandaaji wa tamasha hilo kongwe Tanzania.

Tamasha la mwaka huu linabeba Kauli mbiu isemayo ‘SANAA NA UTAMADUNI KATIKA UCHAGUZI HURU NA WA AMANI’  Aidha kutakuwa na mada ndogondogo zitakazotolewa kupitia kongamano na warsha zitakazohusu  Haki za binadamu, Rushwa na kupinga Mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino)

Tamasha la mwaka huu litahusisha Ngoma za Asili, Maigizo, Sarakasi, Mazingaombwe, Muziki wa kisasa na asili, Sanaa za Ufundi  na bidhaa mbalimbali.

Hadi sasa jumla ya vikundi 48 kutoka ndani na nje ya Tanzania vimethibitisha kushiriki,ambapo vikundi 43 ni kutoka ndani ya Tanzania na vikundi 5 kutoka nchi za Kenya, Namibia, Afrika Kusini, Korea na Congo.
Hadi kufikia sasa hakuna mdhamini yoyote aliyejitokeza kudhamini Tamasha hili na hii imepelekea vikundi kujigharamia na TaSUBa kugharamia Uendeshaji,hivyo Taasisi inatoa wito kwa wadau mbalimbali wa sanaa,Makampuni,Taasisi za serikali na zisizo za serikali kujitokeza kudhamini tamasha hili muhimu kwa mustakabali wa sanaa na utamaduni wa Mtanzania.

Kwa yeyote anayehitaji kuchangia tamasha hili anaombwa awasiliane na Kamati ya maandalizi kwa mawasiliano hapo chini. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com

Mkutano wa Masuala ya Serikali Mtandao kufanyika jijini Arusha Agosti 17

$
0
0

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. HAB Mkwizu (katikati) akizungumza na vyombo vya habari leo katika ukumbi wa Habari (MAELEZO) kuhusu mkutano wa Serikali Mtandao utakaowakutanisha Watendaji Wakuu na Maofisa wa Ngazi na Fani Mbalimbali kutoka Serikalini utakaofanyika jijini Arusha Agosti 17-20,2015.

JWTZ YAKANUSHA KUWANYANG'ANYA KADI ZA KUPIGIA KURA MAOFISA NA ASKARI WAKE

$
0
0

Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wakati akikanusha jeshi hilo kuwanyang'anya kadi za kupigia kura maofisa na askari wake kama ilivyodaiwa na kiongozi mmoja wa chama cha siasa. Kulia ni Msaidizi wa Kanali Lubinga, Meja Joseph Masanja na kushoto ni Kapteni Swaleh Omari.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale

JESHI la Wananchi Tanzania (JWTZ), limekanusha kuwanyang'anya kadi za kupigia kura maofisa na askari wake kama ilivyodaiwa na mmoja wa viongozi wa chama kimoja cha siasa na kutolewa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.


Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kanali Ngemela Lubinga alisema madai hayo siyo ya kweli na  kuwa jeshi hilo halijafanya hivyo na wala haliwezi kufanya hivyo.

"Wanajeshi hawaruhusiwi kuwa wanachama wa chama chochote cha kisiasa na kuwa mwanajeshi haruhusiwi kuwa shabiki wa chama chochote cha kisiasa.
Lubinga alisema Jeshi la Wananchi Tanzania linafanya kazi zake kama 'professional state organ duniani na kuwa mwanajeshi anayekiuka huchukuliwa hatua za kinidhamu za kijeshi wala si za kiraia. Alisema Jeshi la Wananchi Tanzania limesikitishwa na kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi huyo.

"Wananchi na viongozi wa kisiasa mnaombwa mfanye kazi zenu za kisiasa na zisianzishwe hoja nje ya maeneo hayo ya kisiasa kwani lugha hizo za upotoshaji zinaweza kuleta hofu, ukakasi na wasiwasi kwa wananchi" alisema Kanali Lubinga.

Kanali Lubinga alisema jeshi hilo linaendelea na shughuli zake kama kawaida halipendi litolewe kauli za upotoshaji, kusikoeleweka ufuatwe utaratibu wa kuuliza kupata majibu ya uhakika kwani wananchi wanaimani na jeshi lao.

Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com
 

Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images