Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

TTCL MKOA WA ARUSHA YAWAKUMBUKA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU SIKU KUU YA IDD EL FITR

$
0
0
b
Kaimu Meneja wa Shirika la Simu nchini(TTCL)mkoa wa Arusha na Manyara,Emmanuel Buchard(kulia) akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa makundi maalumu kwaajili ya kusherekea Siku kuu ya Idd El Fitr,kushoto ni Mratibu wa Kanda ya Kaskazini,Leonald Lemunge.
h
Kaimu Meneja wa Shirika la Simu nchini(TTCL)mkoa wa Arusha na Manyara,Emmanuel Buchard(kushoto) akitoa zawadi kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Watoto wenye ulemavu wa akili ya Kaloleni jijini Arusha,Emmy Mbilinyi  kwaajili ya kusherekea Siku kuu ya Idd El Fitr leo.
j
Kaimu Meneja wa Shirika la Simu nchini(TTCL)mkoa wa Arusha na Manyara,Emmanuel Buchard(mwenye koti) akikabidhi zawadi mbalimbali Kituo cha Watoto Yatima cha Moshono  kwaajili ya kusherekea siku kuu ya Idd el Fitr.
v
c
Watoto wenye mahitaji maalumu kutoka vituo vya St Joseph Orphanage Center(Moshono) na Shule ya Watoto wenye ulemavu wa akili ya Kaloleni wakisikiliza nasaha za Kaimu Meneja wa TTCL mkoa wa Arusha na Manyara,Emmanuel Buchard.
t
Watoto wenye mahitaji maalumu kutoka vituo vya St Joseph Orphanage Center(Moshono) na Shule ya Watoto wenye ulemavu wa akili ya Kaloleni wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la simu nchini TTCL leo.

WAKAZI WA JIJI LA MWANZA WAJITOKEZA KUMLAKI KWA SHANGWE DKT MAGUFULI JIJINI MWANZA LEO.

$
0
0
 Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia Wananchi wa jiji la Mwanza waliojitokeza kwa wingi jioni ya leo.
Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Mh.Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake,nje ya ofisi za CCM mkoa,ambao walijotokeza kumlaki kwa shange na furaha kubwa.Dkt Magufuli amewasili leo jijini Mwanza akitokea jijini Dar kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na wananchi kwa ujumla.
 Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Mh.Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi alipokuwa akiwasili jijini Mwanza jioni ya leo akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa juu wa chama cha CCM,Magufuli yuko jijini Mwanza kujitambulisha kwa Wananchi.
 Mke wa Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi Dkt.John Pombe Magufuli,Mama Janeth Magufuli akiwasalimia Wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake waliojiotokeza kwa wingi kuwapokea,Pichani kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye. 
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Mgombea Uraisi kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Mh.Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake,nje ya ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.

 Baadhi ya Wananchi wakilikimbiza gari la  Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli kwa shangwe kama waonekanavyo pichani ,wakati Magufuli lipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla jioni ya leo.
 Baadhi ya Wananchi wa jiji la Mwanza wakiwa wamefunga barabara kwa muda wakishangilia ujio wa  Mgombea Uraisi wa CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla jioni ya leo.
 kuna wengine waliacha kazi kwa muda kama hizi na kuja kwenda kushangilia ujio wa Mh.Dkt John Magufuli
  Wananchi wa Passians wakimpokea na kumshangila Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla jioni ya leo.
 Baadhi ya Wanahabari wakiwa kazini.
  Wananchi wa eneo la kona ya Bwiru wakiwa wamezuia  msafara wa Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla.
 Wananchi wa eneo la kona ya Bwiru wakiwa wamezuia  msafara wa Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili jijini Mwanza kwa ajili ya kujitambulisha kwa wanachama wa chama hicho pamoja na Wananchi kwa ujumla.
    Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh.Magesse Mulongo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa jiji hilo mapema leo mchana,kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu.
    Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera,Mh John Mongela mara baada ya katika uwanja wa ndege wa jiji la Mwanza mapema leo mchana.
   Mgombea Uraisi CCM,Mh.Dkt John Pombe Magufuli alisalimiana na wafuasi wa chama hicho wakiwemo viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mwanza,alipowasili katika uwanja wa ndege wa jiji hilo mapema leo mchana.

CATHERINE MAGIGE SASA KUWANIA UBUNGE VITI MAALUM UWT MKOA WA ARUSHA

$
0
0
SAM_3843
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) kupitia vijana Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akichukua fomu ya kuwania ubunge viti maalumu kupitia jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Arusha, anayemkabidhi ni katibu wa (UWT)mkoa wa Arusha Fatuma Hassan Tsea jana katika ofisi za umoja huo jijini Arusha.(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_3852
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) kupitia vijana Mkoa wa Arusha, Mh. Catherine Magige akimkabidhi katibu wa (UWT)mkoa wa Arusha Fatuma Hassan Tsea kiasi cha shilingi laki moja kwaajili ya fomu  ya kuwania nafasi ya ubunge viti maalumu kupitia jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Arusha,
SAM_3849
Catherine Magige akionyesha fomu ya kuwania nafasi ya ubunge viti maalumu kupitia jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Arusha,
SAM_3842
Catherine Magige akiteta jambo na akinamama waliokuja kumsindikiza kuchukua fomu,asisitiza kushirikiana na akinamama
SAM_3839
Catherine Magige akisalimiana na akinamama
SAM_3840
Catherine Magige akiingia katika jengo la CCM mkoa kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya ubunge viti maalumu kupitia jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Arusha,
SAM_3858
Hapa kampeni meneja wake Ezekiel akizungumza  na akinamama waliomsindikiza Catherine Magige kuchukua fomu ya nafasi ya ubunge viti maalumu kupitia jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Arusha,

RAIS SHEIN ASHIRIKI KWENYE BARAZA LA IDD EL FITRI BWAWANI

$
0
0
id1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein akitoa Mkono wa Iddi kwa wananchi mbali mbali waliofika  viwanja vya Ikulu mjini Unguja leo katika kusherehekea Sikukuu ya Idd el Fitri,[Picha na Ikulu.]
id2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Viongozi na Mashekhe waliofika Ikulu Mjini Unguja leo kwa madhumuni ya kupokea mkono wa Idd na kusoma Dua katika Sikukuu ya Idd el Fitri inayoadhimishwa Duniani kote,[Picha na Ikulu.]
id3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein akipokea salamu ya heshma ya gwaride maalum la kikosi cha Polisi FFU leo wakati wa Baraza la Idd katika Kusherehekea Sikukuu ya Idd el Fitri, Sherehe za Baraza Idd lilifanyika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]
id5
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za Baraza la Iddi el Fitri zilizofanyika leo katika ukumbi wa Salama bwawani Hotel Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]
id6
Baadhi ya Wake wa Viongozi na wananchi mbali mbali wakisikiliza hutuba ya Rais waZanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein aliyoitoa leo katika kusherehekea Sikukuu ya Idd elFitri katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]
id9
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein(wa pili kulia) akijumuika na Viongozi na waislamu mbali mbali katika swala ya Suna ya Idd el Fitri iliyoswaliwa kitaifa leo katika viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]

…………………………………………………….
Na RAMADHANI ALI/MAELEZO ZANZIBAR 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Muhamed Shein amewataka wananchi wa Zanzibar kuyatumia mafunzo  waliyopata katika mwezi mtukufu wa Ramadhani  kuendelea  kupendana,  kusaidiana na kuhurumiana.
Alisema katika kipindi chote cha mwezi wa Ramadhani wananchi waliongeza juhudi katika uchamungu na kutafuta radhi zake hivyo ametaka  kuendeleza ut
amaduni wa kufanya mambo  mema katika maisha ya kila siku.
Rais Ali Muhamed Shein alieleza hayo leo alipokuwa akizungumza na wananchi katika Baraza la Idd  El Fitri lililofanyika Ukumbi wa Salama Hoteli ya Bwawani mjini Zanzibar
Aliwashukuru masheikh, walimu na wanazuoni waliojitolea katika maeneo mbali mbali  ya Zanzibar kuendesha darsa na kutoa mawaidha juu ya njia  bora ya kuitekeleza ibada ya saumu na kuhimiza mshikamano
Alisema tafauti za  dini na itikadi za kisiasa visiwe chanzo cha kuleta mfarakano  katika jamii na kila mtu anapaswa kuiunga mkono   Serikali  na kutoa mchango katika kuleta maendeleo.
 Aliwataka viongozi wa siasa kwa upande wao kufanya siasa kwa kuzingatia misingi ya katiba na maadili ya vyama vyao na kwa mujibu wa sheria zilizowekwa za utawala bora.
Aliwakumbusha wanasiasa kwamba ni jukumu lao kushindana bila ya kulaumiana, bila ya kukejeliana na pia wanaweza kushinadana bila ya kudharauliana na kuhasimiana.
Dkt. Shein alisema vyama vya siasa vimeanzishwa na vitaendelea kuwepo kwa lengo la kushindana kwa sera na kuchochea maendeleo ya wananchi hivyo amewataka wanasiasa kuhubiri Umoja na amani katika vikao vyao.
“Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa ni ushahidi unaotosha wa kuleta amani na maendeleo yanayokusudiwa, ”alisisitiza Rais wa Zanzibar.
Aliwataka viongozi wa kisiasa, dini, viongozi wa kijamii  na wananchi wote kuona  kuwa jukumu la kuhimiza utiifu wa sheria, kusimamia amani, utulivu na usalama wa nchi ni la watu wote.
“Zanzibar ni nchi yetu sote na Tanzania ni nchi yetu sote, hivyo sote ni wamoja na sote tunajukumu la kuishi kwa amani umoja na mshikamano”alieleza Dkt. Shein.
Aliwanasihi wananchi,  hasa vijana kuendeleza amani na utulivu na kujiepusha na vitendo vitakavyopelekea kuvunja amani na umoja uliopo kwani hakuna mbadala wa amani inapotoweka.

Mama Salma Kikwete ajiunga na waombolezaji kwenye msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja Banza Stone aliyezikwa leo jijini Dar es salaam

$
0
0

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akilakiwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrer Mngereza alipowasili kujiunga na familia na waombolezaji katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015. Marehemu Banza Stone, aliyefariki jana mchana baada ya kuugua kwa muda mrefu,  amezikwa jioni hii katika makaburi ya Sinza. Marehemu Banza Stone atakumbukwa kwa umahiri wake wa utunzi na uimbaji alipokuwa na bendi mbalimbali zikiwemo Twanga Pepeta, Tot na Extra Bongo.
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Ubungo Mhe. John Mnyika  alipowasili kujiunga na familia na waombolezaji katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitambulishwa kwa Katibu wa bendi ya TOT, Gasper Tumaini, ambako marehemu Banza Stone aliwahi kufanya kazi enzi za uhai wake
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpa pole kaka wa marehemu alipowasili kujiunga na familia na waombolezaji katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa pole kwa wana familia na waombolezaji katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
   Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimfariji mama mzazi wa marehemu  katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
   Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na kiongozi wa bendi ya African Stars Twanga Pepeta Asha Baraka  katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.

   Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimfariji Haji Ramadhani Masanja, mtoto wa marehemu   katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na  Haji Ramadhani Masanja, mtoto wa marehemu   katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu  Ramadhani Masanja “Banza Stone” likitolewa nyumbani tayari kwa mazishi Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015.
 Waombolezaji wakilia kwa uchungu wakati mwili wa Banza Stone ukipelekwa mazikoni
 Mama Salma Kikwete, Asha Barka na mama wa marehemu wakiwa na nyuso za huzuni wakati  mwili wa merehemu Banza Stone ukipelekwa mazikoni
 Mama Salma Kikwete akiagana na kiongozi na mwimbaji wa African Stars wana Twanga Pepeta ambaye alifanya kazi kwa karibu na Banza Stone tokea kuanza kwa bendi hiyo
Mama Salma Kikwete akiaga waombolezaji katika msiba wa mwanamuziki Ramadhani Masanja “Banza Stone” Sinza Lion jijini Dar es salaam leo Jumamosi Julai 18, 2015. 
PICHA NA IKULU

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AJUMUIKA NA WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU KATIKA SWALA YA EID EL FITRI KITAIFA MKOANI GEITA.

$
0
0
ED1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na Baadhi ya Viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, (BAKWATA) na wananchi katika swala ya Sikukuu ya Eid El-Fitri iliyofanyika Kitaifa kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi  Kalangalala, katika Halmashauri ya Mji wa Geita, leo Julai 18, 2015. 
ED2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Kaimu Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir Ally, baada ya kumalizika kwa swala ya Sikukuu ya Eid El-Fitri kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi, Kalangalala, mkoani Geita, leo Julai 18, 2015. 
ED3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwahutubia waumini wa dini ya Kisslamu wakati wa swala ya Sikukuu ya Eid El-Fitri iliyofanyika Kitaifa kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kalangalala, katika Halmashauri ya Mji wa Geita, leo Julai 18, 2015. 
ED5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Kaimu Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir Ally, baada ya kumalizika kwa swala ya Sikukuu ya Eid El-Fitri kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi, Kalangalala, mkoani Geita, leo Julai 18, 2015. 
ED7
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki swala ya Sikukuu ya Eid El-Fitri na waumini wa Dini ya Kiislamu iliyofanyika Kitaifa wa Mkoani  Geita  leo Julai 18, 2015. Picha na OMR

EDMUND RUTARAKA AELEZEA MATARAJIO YAKE YA UBUNGE MOSHI MJINI NI BAADA YA KUCHUKUA FOMU.

$
0
0
Katibu Msaidizi wa CCM ,manispaa ya Moshi,Donatha Mushi akimkabidhi Edmund Emanuel Rutaraka fomu ya kugombea nafasi ya kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi kuwa mgombea wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi mjini .Zoezi hili lilifanyika katika ofisi za CCM wilaya ya Moshi mjini.

Picha ya Video imepigwa na Dixon Busagaga wa Globu ya jamii Kanda ya Kaskazini.

MKURUGENZI MKUU WA CERT YA UINGEREZA AUNGA MKONO KAULI YA WANAUSALAMA MITANDAO

$
0
0
Bwana Chris Gibson, Mkurugenzi mkuu wa CERT (Computer Emergence Response Team) ya Nchini Uingereza yenye dhamana ya kubaini na kudhibiti uhalifu mtandao nchini humo ametangaza rasmi kuunga mkono kauli  ya mwaka huu ya wanausalama mitandao ambayo Niliizungumzia rasmi na kuitolea ufafanuzi katika mkutano wa wanausalama mitandao tulipo kutana jijini Johannesburg mwaka huu mwezi wa Tano mwishoni.

Kauli hii ya ushirikiano nilipo izungumzia, wataalam wote katika mkutano huo waliiunga mkono na sasa kupitia mkutano wa wanausalama mitandao wanchi ya uingereza uliokamilika Jijini London Mkuurugenzi mkuu wa CERT ya nchini Uingereza amesisitizia  hili kwa kusema vita dhidi ya uhalifu mtandao itakua ngumu kama ushirikiano utakua hafifu.

Itakumbukwa mwaka 2013 CERT ya uingereza ilizindua CISP – Cybersecurity Information Sharing Partnership, iliyodhamiria kutoa fursa ya kukuza ushirikiano wa kubadilishana taarifa za uhalifu mtandao nchini humo huku mashirika binafsi na serikali zikitegemewa kupiga hatua dhidi ya uhalifu mtandao.

Hili la kushirikiana kwa taarifa za uhalifu mitandao baina ya makampuni pamoja na serikali nililitolea ufafanuzi katika mkutano wa wanausalama mitandao 2014 Nchini Cyprus na kusema imefika wakati makampuni yakawa na tabia ya kutoa twakwimu stahiki za uhalifu mtandao sanjari na inteligensia ya uhalifu huu ili kuhakiki namna ya uhalifu huu unavyo fanyika unabainishwa na kutoa fursa ya udhibiti kupatikana mapema.

Maelezo hayo ambayo baadae yaliweza kuingizwa katika moja ya jarida la usalama mitandao, Nilielezea kwa kina namna hatua ya ushirikiano wa kupeana taarifa za uhalifu mtandao baina ya Makampuni inavyoweza kusababisha uhalifu ulioathiri kampuni moja au nchi moja kutojirudia kwa nyingine kwani tayari kutakua na ufahamu wa uhalifu usika kutokana na kushirikiana katika kubadilishana taarifa za uhalifu mtandao baina ya makampuni au Nchi.

Aidha, katika kuongezea juu ya hili bado naona changamoto kubwa  kwa mataifa mengi ikiwemo Tanzania ni kutokuwepo na mikakati madhubuti ya kutambua na kubaini uhalifu mtandao sanjari na kuchukua hatua za haraka kudhibiti mara unapokua umetokea kituambacho kimeendelea kusababisha uhalifu huu kuendelea kushika kasi zaidi hivi sasa.
Takwimu zinaonyesha Asilimia zaidi ya 71 ya uhalifu mtandao umeendelea kutikisa anga ya usalama mitandao na kubainika kwake kumechukua  zaidi ya miezi mitatu kitu ambacho ni hatari na kinarudisha nyuma ushindi dhidi ya uhalifu mitandao.

Nchini Marekani Udukuzi uliogundulika wiki mbili zilizo pita uliosababisha taarifa za watu zaidi ya Milioni Arubaini na moja kuibiwa na wahalifu mtandao ambapo kwa sasa taarifa hizo zimeendelea kuzua  mijadala mirefu baina ya wanausalama mitandao baada ya kubainika uhalifu huo umechelewa kugundulika na tayari athari kubwa imeonekana kutokana na tukio hilo, jambo ambalo limepelekea  mkuu wa FBI wa Nchi ya Marekani kuthibitisha mategemeo yake ya matukio kadhaa mfano wa hilo kutokana na udhaifu wa ugunduzi wa mapema wa matukio ya uhalifu mtandao.

Hili bado libaki kua funzo kwetu kwani yote hayo yanayo jiri katika mataifa mengine yanaweza kujirudia barani Afrika na hasa Nchini Tanzania. Udhaifu wa kuto shirikiana katika kupeana taarifa za uhalifu mtandao bado ni changamoto kwetu nabado tumekua tukitegemea mabadiliko katika udhibiti wa uhalifu huu.
 
Mfano, uhalifu Mtandao Aina Ya “Spearfishing” bado umeendelea kutoa athari kubwa  nchini Tanzania na kumekua na jitihada ndogo za kukuza uelewa dhidi ya uhalifu huu huku kuubaini na kudhibiti kua bado kuko chini. CERT ya nchini Tanzania yenye dhamana ya kubaini na kuzuia uhalifu mtandao kabla ya kuleta athari Nchini inakila sababu ya kujifunza zaidi kutoka kwa wengine na kuhakiki inaingiza katika vitendo yale ya msingi yanayopatikana ili kuhakiki Taifa linaendelea kubaki salama.

Aida, Nitoe wito kua kama ilivyo udhibiti wa uhalifu wa kawaida ambapo unapelekea mtu momoja kuweka milango, Madirisha na mengineo na baadae kuunda vikundi binafsi vya sungu sungu kuweza kuimarisha ulinzi na baadae kutegemewa Polisi wenye dhamana ya ulinzi wa raia na mali zao kuuendeleleza ulinzi – Dhana hii lazima ielekezwe katika mitandao ambapo kila mmoja anapaswa kujua anadhamana ya kujiweka salama binafsi na kuunganisha nguvu baina ya vikundi vidogo huku vitengo venye dhamana ya kulida mitandao katika ngazi ya taifa kuendelea kutoa msaada stahiki.

WANANCHI WA MOROGORO MJINI WAMNUNULIA FOMU ABOOD ILI AENDELEE KUWA MBUNGE WAO JIMBO MOROGORO MJINI

$
0
0
 
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Akipokea Michango ya wanafunzi waliojitokeza Kumchangia Mbunge huyu ili achukue Fomu ya Kugombea tena Ubunge wa Jimbo hilo Kupitia Chama cha Mapinduzi Mara Baada ya Kuridhishwa na Utendaji Kazi wa Mbunge huyo ambaye amefanya Mammbo mengi ya Maendeleo Ikiwemo Kuwalipia Ada zaidi ya wanafunzi 500 Wasiokuwa na uwezo wa Kujilipia ada na wanaoishi Katika Mazingira Magumu
 Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Akipokea Kiasi cha Shilingi 50000/= kutoka Kikundi cha Tushikamane Kata ya Kilakala kwa lengo la kumtaka mbunge huyo achukue fomu ya Kugombea Tena Ubunge wa Jimbo Morogoro Mjini .
 
Wanachama wa Kikundi hicho wamesema  wamesukumwa kufanya hivyo Mara baada ya kurishishwa namna Mbunge huyo anavyovisaidia vikundi nvya wajasiriamali wa Jimbo hilo.Hadi sasa Makundi Mbalimbali na wananchi Binafsi wamejitokeza   Kumchangia na Kumshawishi Mbunge huyo kuchukua fomu na kugombea tena awamu nyingine ya ubunge wa jimbo holo..
 

MWENYEKITI WA ALBINO TANZANIA AJITOSA UBUNGE KOROGWE VIJIJINI, AAHIDI KULETA MAENDELEO

$
0
0
Mwenyekiti wa Chamacha Albino Tanzania (TAS), Bw. Ernest Kimaya (kushoto) akiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda wakati wa maadhimisho ya Siku ya Walemavu wa Ngozi Tanzania kwenye viwanja vya Garden Mjini Iringa Mei 4, 2010. 
Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) ndugu Ernest Kimaya akimfariji Mama Maria Chambanenge wakati akipatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mkoa Rukwa kufuatia kukatwa mkono wake wa kushoto na watu walioshirikiana na mume wake na ambao walitiwa mbaroni na polisi mwaka 2013.
 Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) Ernest Kimaya akisisitiza jambo kwa wanahabari kufuatia kuvamiwa na kukatwa mkono kwa Mama Maria Chambanenge wa mkoani Rukwa Februari 19, 2013.
 Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania, Ernest Kimaya, akitoa nasaha zake wakati wa maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Albinism Duniani katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Juni 13, 2015. 
Rais Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma, wakiwa na Bw. Kimaya wakiwasikiliza watoto wenye albinism wakiimba wakati wa maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Albinism Dunia kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Juni 13, 2015.
Mwenyekiti wa TAS, Ernest Kimaya, akimpokea Rais Kikwete katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro Juni 12, 2015. Rais Kikwete ndiye aliyekuwa mgeni rasmi wa maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Albinism Duniani jijini Arusha 2015.
Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania Bw. Ernest Kimaya akisoma nakala za Katiba Inayopendekezwa yenye maandishi yaliyokuzwa mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro Machi 15, 2015.

Mwakalebela ajitosa tena Iringa mjini

$
0
0
ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Fredrick Mwakalebela mwishoni mwa wiki iliyopita alichukua fomu ya kuwania ridhaa ya ubunge wa Jimbo la Iringa mjini na kuwatahadharisha wenzake kuacha siasa za majitaka zinazofanywa na baadhi ya watangaza nia.

Mwakalebela ambaye mwaka 2010 alijitosa kuwania ubunge  katika jimbo hilo ambapo alikusanya idadi kubwa ya waliomshabikia na kumhitaji  lakini kutokana na baadhi ya changamoto zilizojitokeza alishindwa kuwatumikia alisema bado ana dhamira ya kuwatumikia Iringa mjini kwa sababu bado ana dhamira ya kweli kuwaletea maendeleo wakazi wa jimbo hilo.Alisema siasa za majitaka zitasababisha kuligawa jimbo hilo kwa Wapinzani ambao macho na masikio yao wameyatega katika chama hicho kinachoshikilia dola.

Mwakalebela alisema Iringa mjini kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kutekelezwa kupitia ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hivyo wao kama wagombea wazingatie ilani hiyo ili kutolipoteza kwa mara nyingine jimbo hilo.

Aidha Mwakalebela alisema  iwapo atashindwa kupata ridhaa ya wakazi wa Iringa Mjini yuko tayari kutoa ushirikiano kwa atakayefanikiwa kupata ridhaa kwa sababu wana CCM wanatakiwa kuwa na nguvu moja ambayo inatakiwa kupata ushirikiano.

“Nachukizwa na siasa za majitaka kwa sababu hazitusaidii hasa kwa changamoto tulizonazo ambazo zinatakiwa kutatuliwa na watia nia kama Mwakalebela na wengine ambao wana dhamira ya kufikia ujumbe wa jamii bungeni,” alisema Mwakalebela.  Mwakalebela mwenye marafiki Uswisi, Australia, America, Denmark, Qatar,  Hispania na Scandinavia anajitakasa kupitia mafanikio aliyoyatekeleza alipokuwa  TFF ametoa wito kwa wakazi wa Iringa  kutofanya makosa kama yaliyotokea mwaka 2010.

Mwakalebela aliyasema hayo muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kuwania ridhaa hiyo aliyoichukua CCM Mkoani Iringa ambako alilakiwa na mashabiki lukuki waliojitokeza kumsindikiza.

DKT JOHN POMBE MAGUFULI ALIVYOPOKELEWA JIJINI MWANZA KWA KISHINDO

RAIS KIKWETE AREJEA NYUMBANI USIKU HUU BAADA YA KUKAMILISHA ZIARA YA KIKAZI YA USWISI

$
0
0
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mfanyakazi wa Shirika la Ndege la Uswisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam mara baada ya kurejea nyumbani baada ya ziara ya kikazi mjini Geneva
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam mara baada ya kurejea nyumbani baada ya ziara ya kikazi mjini Geneva. PICHA NA IKULU

Akiwa mjini Geneva, Rais Kikwete ameongoza vikao vya  Jopo la Kimataifa Linalopendekeza Jinsi Dunia inavyoweza kukabiliana na majanga yajayo ya magonjwa ya milipuko ambalo kazi yake imeungwa mkono na nchi 21 ambazo zilichangia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola.

Miongoni mwa mikutano ambayo Rais Kikwete ameiongoza katika Makao ya Umoja wa Mataifa (UN) mjini Geneva ni pamoja na yeye na wanajopo wenzake kutoa maelezo kuhusu maendeleo ya kazi yao kwa nchi ambazo zilichangia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone.

Nchi hizo ambazo zimeunga mkono kazi ya Jopo hili katika mkutano huo ni Venezuela, Umoja wa Ulaya (EU), Uholanzi, Finland, Shirikisho la Russia (Russian Federation), Norway, China, Ubelgiji, India, Ujerumani, Marekani, Uswisi, Canada, Brazil, Denmark, Uingereza, Israel, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Dunia (WB), Jamhuri ya Korea na Japan.

Pamoja na kwamba wajibu mkuu wa Jopo hili siyo kuchunguza ugonjwa wa Ebola na madhara yake, bado ugonjwa huo ni msingi mkuu wa kazi ya Jopo hilo ambalo wajibu wake ni kutumia uzoefu wa Ebola kutoa mapendekezo ya jinsi dunia inavyoweza kukabiliana na majanga ya magonjwa ya milipuko katika siku zijazo.

Ugonjwa wa Ebola ambao ulilipuka katika nchi hizo tatu za Afrika Magharibi mwishoni mwa mwaka 2013 mpaka sasa umeua watu 11,000 katika nchi hizo na kusababisha mshtuko mkubwa duniani.
Hiyo ilikuwa mara ya 24 kwa ugonjwa huo kulipuka katika Afrika tokea ulipolipuka kwa mara ya kwanza mwaka 1976, miaka karibu 40 iliyopita, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wakati huo ikiitwa Zaire.

Hata hivyo, katika milipuko ya kwanza 23, ugonjwa huo uliua watu wachache zaidi kuliko mlipuko wa 24.Jopo hilo limeambiwa kuwa tofauti na matarajio ya dunia kuwa ugonjwa huo ulikuwa unamalizika katika nchi hizo hasa katika Liberia, umeanza kupata kasi tena na nchi hizo tatu zinakisiwa kuwa na wagonjwa karibu 70.

Jopo hilo lenye Wajumbe sita liliteuliwa Aprili, mwaka huu, na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mheshimiwa Ban Ki Moon na kufanya vikao vyake vya mwanzo Mei, mwaka huu, katika makao makuu ya UN, mjini New York, Marekani.

Mbali na kukutana na nchi zilizochangia mapambano dhidi ya Ebola, Rais Kikwete na Jopo lake limepata nafasi ya kumsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, wakati ugonjwa huo unalipuka Dkt. Luis Gomes Sambo wa Angola ambaye aliwaeleza wajumbe historia ya ofisi ya kanda hiyo iliyoko mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo, katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Aidha, Wajumbe wa Jopo wamemsikiliza Mkurugenzi mpya wa Kanda, Dkt. Matshidizo Rebecca Moeti ambaye amezungumza kwa njia ya mkutanomtandao (teleconference) kutoka mjini Brazzaville. Dkt. Moeti alianza kazi yake Januari Mosi, mwaka huu, 2015.

Vile vile, Wajumbe wa Jopo wamesikiliza jitihada za Jamhuri ya Rwanda kukabiliana na magonjwa ya mlipuko kupitia kwa Waziri wa Afya wa nchi hiyo, Agnes Binagwaho ambaye naye alizungumza kwa mkutanomtandao kutoka Kigali, Rwanda.

Nje ya vikao hivyo, Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu Mstaafu wa UN, Mheshimiwa Kofi Annan. Katika mkutano huo kwenye Hoteli ya Intercontinental, viongozi hao wawili wamezungumzia masuala mbali mbali ya kimataifa, ikiwamo hali ya Burundi.

Rais pia amekutana kwa mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kituo cha South Centre ambacho kina makao yake mjini Geneva, Dkt. Martin Kohr. Kituo hicho kilianzishwa chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kwa nia ya utekelezaji wa Ripoti ya Kamisheni ya Nchi Zinazoendelea (South-South Commission), ambayo iliongozwa na Mwalimu.

MAPOKEZI YA MAGUFULI MKOANI GEITA LEO

$
0
0
Mgombea Urais alieteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Wanaccm na Wananchi wa Mkoa wa Geita, Wakati aliposimama kuwasalimia akitokea jijini Mwanza kuelekea Kijijini kwake Chato. Hapa ni Kivukoni Busisi Mkoani hapo, mapema asubuhi ya leo.
Mgombea Urais alieteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia maelfu ya Wanaccm na Wananchi wa Mkoa wa Geita, mara baada ya kuwasili mapema leo asubuhi.
Msafara wa Mgombea Urais alieteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli ukiwasili kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Geita. PICHA ZOTE NA MICHUZIJR

HAPPY BIRTHDAY MWANALIBENEKE KRANTZ MWANTEPELE

$
0
0
 
Leo tarehe 19 July ni siku ya kuzaliwa Mwanalibeneke la blogu  Krantz Mwantepele ambaye ni Mkurungezi Mtendaji wa MWANAHARAKATI MZALENDO MEDIA pia Mkurungezi Mtendaji wa KAJO ITECH kwa  niaba ya wasomaji  wetu tunapenda kukutakutakia maisha marefu na yenye baraka na fanaka tele.
 
 Mungu akupe maisha marefu na kukupa mwongozo sahihi kwa ndoto zako za kuweza kutengeneza ajira kwa vijana wenye nia na ari ya kujiajiri .
Mnaweza kutembelea blog zinazomilikiwa na Mwanaharakati Mzalendo Media .
 
Mwanaharakati Mzalendo Blog link www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com
Harakati360 link www.harakati360.blogspot.com
Mzalendo Times link www.mzalendotimes.blogspot.com
Na hivi karibuni kutazinduliwa MZALENDO ONLINE TV
Pia unaweza kumfuata Krantz katika mitandao ya kijamii kama
 Facebook kwa jina la Mwanaharakati mzalendo  https://www.facebook.com/MWANTEPELE
Instagram/ twitter  @ mzalendo89
 ” HAPPY BIRTHDAY KRANTZ “

WAZIRI MKUU AKATAA KUGOMBEA TENA UBUNGE

$
0
0
IMG_0007
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amekataa ombi la wananchi wa  jimbo lake la uchaguzi la Katavi la kumtaka agombee tena ubunge katika jimbo hilo ili kuendeleza mipango mbalimbali ya maendeleo aliyoianzish.

Akizungumza baada ya Ibada ya Jumapili katika kigango cha Kanisa Katoliki cha Kibaoni wilayani Mlele (Jumapili, Julai 19, 2015), Waziri Mkuu Pinda amesema anamshukuru Mungu kwa nafasi aliyopewa ya kulitumikia Taifa akiwa Waziri Mkuu kwa miaka minane na anaamini wakati umefika wa yeye kuwaachia wengine nafasi ya ubunge wa jimbo la Katavi.

Amesema yeye ataendelea kuwa karibu na wananchi wa Katavi wakati wote  na kwa vile atakuwa na muda wa kutosha atashiriki kikamilifu katika mikakati mbalimbali ya kuwaletea maendeleo wananchi ili waweze kujikwamua kutoka kwenye umaskini.

Mheshimiwa Pinda aliwaasa wananchi wa jimbo la Katavi wawe makini katika kuchagua mbunge na madiwani na kamwe watoa rushwa na wabadhirifu wasipewe nafasi katika uchaguzi ujao.

Akimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu, Paroko wa Parokia ya Usevya wilayani Mlele, Padri Aloyce Nchimbi aliwaasa wananchi wa Wilaya ya Mlele kumuenzi Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda hata atakapokuwa amestaafu kwani bado watahitaji busara na uzoefu wake katika kujiletea maendeleo.

Waziri Mkuu yuko kijijini kwake Kibaoni, wilayani Mlele kwa ajili ya mapumziko mafupi.Leo saa 10 jioni ndiyo mwisho wa kurejesha fomu za ubunge ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA TEMEKE ABBAS MTEMVU ARUDISHA FOMU WENGI WAMPONGEZA

$
0
0
 Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Temeke kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Abbas Mtemvu (wapili kulia), akirudisha  Fomu katika Ofisi za Chama hicho kwa Katibu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Temeke Yona Sengerema (kulia) Dar es Salaam jana,hivyo mtemvu akiwa anatetea Jimbo lake tena . walio kushoto ni baadhi ya viongozi mbalimbali wa Jimbo la temeke wa chama hicho waliomsindikiza mbunge huyo (PICHA ZOTE  NA KHAMISI MUSSA)
 Katibu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Temeke Yona Sengerema (kulia) akihakiki Fomu za Mbunge huyo mara alipokuwa akirudisha Ofisini hapo
 
  Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Temeke kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Abbas Mtemvu (wapili kulia aliye kaa) akiwa ofisini hapo 
 
  Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Temeke kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Abbas Mtemvu (wa katikati) akiongea na waandishi wa habari mara alipo kuwa amewasilisha fomu.
 Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania, Mariam Kisangi, akiongea jambo  na waadishi wa habari mara baada ya Mbunge huyo kurudisha fomu 
 
Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Temeke kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Abbas Mtemvu  akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa chama hicho.wakiwemo madiwani na wenyeviti walio msindikiza mbunge huyo.
 
  Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Temeke kupitia Chama cha Mapinduzi
(CCM) Abbas Mtemvu  akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama
wa chama hicho.wakiwemo madiwani na wenyeviti walio msindikiza mbunge
huyo

MTEMVU APOKEA MSAADA WA VYAKULA,NGUO ULIOTOLEWA NA KAMPUNI YA GOODONE KWA AJILI YA KITUO CHA YATIMA CHA ALQAM,TANDIKA DAR

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Good One, Wu Ya Hui (kushoto), akimkabidhi msaada wa vyakula na nguo, sabuni na vyombo Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu vilivyotolewa kwa Kituo cha Kulelea Yatima cha Darul Arqam cha Tandika, Dar es Salaam jana. Msaada huo uliombwa na mbunge huyo kwa kushirikiana na aliyewahi kuwa Makamu wa Rfais wa TFF, Athuman Nyamlani. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mtemvu akipokea sabuni kwa ajili ya kituo hicho
 Mtemvu akipoea  balo la nguo za mitumba

 Mtemvu akizungumza mkatika  hafla hiyo ambapo aliipongeza kampuni hiyo ya Goodone kwa kuwa na moyo wa kutoa msaada huo
 Mtemvu akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Goodone watoto wanaolelewa kituoni hapo pamoja na uongozi wa kituo hicho
 Wakiomba dua
 Baadhi ya watoto yatima wanaolelewa kituoni hapo
Msaada uliotolewa kituoni hapo

VIJANA CCM WAJITOKEZA KWA WINGI KUCHUKUA FOMU ZA UBUNGE JIMBO LA MOSHI MJINI.

$
0
0
Mtia nia wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi mjini,Priscus Tarimo,akikabidhiwa fomu ya nafasi hiyo na katibu wa CCM manispaa ya Moshi,Loth Ole Nesele katika ofis za chama hicho za Wilaya ya Moshi mjini.
Mtia nia ya kugombea Ubunge jimbo la Moshi mjini,Priscus Tarimo,akitoa maelezo yake kwa Katibu Msaidizi wa CCM wilaya ya Moshi mjini Donatha Mushi alipofika kwa ajili ya zoezi la uchukuaji wa fomu.
Priscus Tarimo akizungumza na na wanahabari( hawako pichani) muda mfupi baada ya kumaliza zoezi la uchukuaji wa fomu za kuwania kuteuliwa katika nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM jimbo la Moshi mjini.
Naibu kamanda wa Vijana wa CCM,manispaa ya Moshi ,Edmund Rutaraka akipokea fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho kutoka kwa katibu msaidizi wa CCM wilaya ya Moshi mjini,Donatha Mushi.
Kada wa Chama cha Mapinduzi manispaa ya Moshi ,Daudi Mrindoko akiwa ameambatana na mkewemalipofika kucukua fomu katika ofisi za CCM wilaya ya Moshi mjin,Fomu hizo zilikabidhiwa kwake na katibu msaidizi wa chama hicho Donatha Mushi.
Mwakilishi wa jamii ya Bantu Union ,Omary Mwaliko akirejesha fomu za kuwania kuteuliwa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi mjini mara baada ya kuzijaza

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MHARIRI WA GAZETI LA MTANZANIA,KHAMIS MKOTYA ACHUKUA FOMU ZA UBUNGE KUPAMBANA NA NKAMIA JIMBO LA CHEMBA,DODOMA

$
0
0
 Mhariri Msanifu wa Gazeti la Mtanzania,Khamis Mkotya akipokea fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya Ubunge katika wilaya ya Chemba kutoka kwa Katibu wa Wilaya hiyo CCM,Asia Mohammed jana katika ofisi za chama hicho wilayani Kondoa.(Picha na Ramadhan Hassan)
Mhariri Msanifu wa gazeti la mtanzania Khamis Mkotya akionesha fomu alizokadhiwa jana katika ofisi za chama hicho Wilayani Kondoa za kuomba ridhaa ya kuchaguliwa na Chama cha Mapinduzi kugombea Ubunge katika Jimbo la Chemba. (Picha na John Banda)
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images