Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46206 articles
Browse latest View live

Article 23

0
0


Ziara ya January Makamba Kusaka Wadhamini Shinyanga.

0
0
Mh January Makamba naendelea na Ziara yake ya Kusaka Wadhamini katika mikoa mbalimbali ya Tanzania na Leo alikua katika Mkoa wa Shinyanga akiomba Uzamini.

Mh January Makamba amepokelewa kwa Bashasha Kemkem na wakazi wa Mkoa wa Shinyanga na Chama cha vijana wa Bidaboda mkoa huu walijitokeza kwa Wingi kumpokea January Makamba.
Mbunge wa Shinyanga na Naibu waziri wa Ofisi ya Makamu wa Raisi (Mazingira) Steven Masele amempokea mh January Makamba na Kuwaomba wanashinyanga kumuamini na kumpa udhani maana January ni Jembe na anaakili anauwezo wa kuongoza Nchi. January Makamba naendelea na Ziara yake ya Kusaka Wadhamini katika mikoa mbalimbali ya Tanzania na Leo alikua katika Mkoa wa Shinyanga akiomba Uzamini.

Mh January Makamba amepokelewa kwa Bashasha Kemkem na wakazi wa Mkoa wa Shinyanga na Chama cha vijana wa Bidaboda mkoa huu walijitokeza kwa Wingi kumpokea January Makamba.
Mbunge wa Shinyanga na Naibu waziri wa Ofisi ya Makamu wa Raisi (Mazingira) Steven Masele amempokea mh January Makamba na Kuwaomba wanashinyanga kumuamini na kumpa udhani maana January ni Jembe na anaakili anauwezo wa kuongoza Nchi.
Mh January Makamba akipokea Fumo ya watu waliomdhani Mkoa wa Shinyanga ambao walikua Zaidi ya 600.
Ubavu wa Mh January Makamba Akitia saini Katika kitabu cha wageni Ofisi za CCM Wilaya ya Shinyanga
Mh January Akizungumza na wakazi wa Shinyanga waliojitokeza kumsikiliza katika Viwanja vya CCM wilaya ya Shinyanga.
Mbunge wa Shinyanga Mjini Steven Masele akimzungumzia Mh January Makamba kwa Wakazi wa Shinyanga.


MWENYEKITI WA CHADEMA FREEMAN MBOWE AKISHIRIKI KAMPENI YA MAZINGIRA KATIKA SOKO LA MASAMA-MULA

0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai (Mwenye kofia katikati) akishirikiana na wananchi wa Lukeni, Kata ya Masama-Mashariki kufanya usafi katika Soko la Masama-Mula mwishoni mwa juma, katika kampeni ya kutunza mazingira kwenye jimbo hilo iliyopewa jina la 'Keep Hai Clean' ikitumia gari maalum la kukusanyia taka lenye uwezo wa kubeba tani 32 za taka ambalo Mbunge huyo alitoa msaada kwa wananchi wake hivi karibuni.

MWENGE KUZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA SH. MILIONI 1.2 MUFINDI

0
0
JUMLA ya miradi 13 yenye thamani ya Zaidi ya shilingi milioni 1.2 inatarajiwa kuzinduliwa pamoja na kuwekwa mawe ya msingi na Mwenge wa uhuru utakapokimbizwa katika Halmashauri ya wilaya ya Mufindi mapema alhamisi ya tarehe 25 mwezi huu.

Taarifa ya Ofisi ya habari na mawasiliano ya halmashauri ya Mufindi kwa vyombo vya habari imefafanua kuwa, vyanzo vya fedha zilizotumika kukamilisha miradi hiyo  vimegawanyika katika sehemu kuu nne, ambapo asilimia 10 ya fedha hizo ni kutoka serikali kuu, asilimia 12 ni Fedha za Halmashauri, wakati asilimia 13 ni  fedha za wahisani huku wananchi wakichangia  asilimia 65.

 Taarifa hiyo imeendelea kubainisha kuwa miradi hiyo 13 imegawanyika katika vijiji vya Mtili, Lugolofu, Mabaoni, Idetelo, Lugongo na kata ya Kinyanambo huku miradi mikubwa Zaidi ni pamoja na mradi wa sakosi ya Faraja wenye gharama ya Zaidi ya sh milioni 478 utakaozinduliwa katika kata ya Kinyanambo sanjari na mradi wa msitu ulioghalim Zaidi ya Sh. Milioni 180 utakao kaguliwa katika kijiji cha Lugongo.

Aidha, Mwenge wa uhuru utakabidhiwa kwa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi, katika hafla itakayo fanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari Kinyanambo majira ya saa mbili asubuhi, ukitokea Manispaa ya Iringa na badaye jioni utakesha katika kijiji cha Mabaoni Mgololo kata ya Makungu. 
Mwenge wa uhuru uliasisiwa rasmi mnamo mwaka 1960 na hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, ukiwa na shabaha ya kuleta matumaini, upendo, heshima na kuchochea maendele katika jamii za kitanzania.

VIONGOZI WA KIMASAI WARIDHIA KUACHA UKEKETAJI

0
0
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) akimpongeza Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli kwenye semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) akimpongeza Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli kwenye semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro.Susana Koillah, Mama Shughuli na mtafsiri wa lugha ya Kimasai katika semina hiyo akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) kabla ya kutafsiri mada yake kwa wanasemina. Susana Koillah, Mama Shughuli na mtafsiri wa lugha ya Kimasai katika semina hiyo akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) kabla ya kutafsiri mada yake kwa wanasemina.
Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Ofisa HIV na Elimu ya Afya Taifa wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Mathias Herman (kushoto) akitoa maelekezo kwa wana semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi shule za sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Ofisa HIV na Elimu ya Afya Taifa wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Mathias Herman (kushoto) akitoa maelekezo kwa wana semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi shule za sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.


WAKUU wa jamii ya Kimasai wa Afrika Mashariki wameridhia kuachana na mila potofu zimezopitwa na wakati ikiwemo vitendo vya ukeketaji kwa wasichana wa jamii ya kimasai ambavyo vimekuwa vikiwaathiri wasichana hao kwa kiasi kikubwa.

Kauli ya kusitisha vitendo hivyo ilitolewa juzi Wilayani Ngorongoro na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli pamoja na msaidizi wake kutoka Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni walipokuwa katika semina ya elimu ya afya ya uzazi, kupinga vitendo vya ukeketaji pamoja na mimba za utotoni.

Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Afrika Mashariki, Olaiboni Simeli alimueleza Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) na Mwakilishi wa Shirika hilo Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues kuwa jamii hiyo ya wamasai imeridhia kuacha mila zilizopitwa na wakati na itaendelea kushiriki kuelimisha jamii yao zaidi juu ya madhara ya mila hizo potofu ikiwemo ukeketaji na ndoa za utotoni.

"...Tunaishukuru UNESCO kwa kuendelea kutoa elimu hii kwetu juu ya mila potofu nasisi tunaungana nanyi kuendelea kutoa elimu kwa jamii yetu kupinga ukeketaji na ndoa za utoto tumeelezwa athari nyingi zinazowapata wasichana wanaokeketwa...kwanini tuendelee na mila zinazoleta madhara kwa watu wetu? Tushirikiane kupiga vita hivi," alisema Olaiboni Simeli akizungumza mbele ya Bi. Rodrigues.

Kwa upande wake Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Naimado Olaiboni alisema hakuna haja ya jamii ya kimasai kuendelea na mila zilizopitwa na wakati ilhali mila hizo zikiendelea kuwaathiri wamasai na kuwabakiza nyuma kimaendeleo katika nyanja mbalimbali. "...Tutaendelea kushirikiana nanyi kupinga ndoa za utotoni kwa kuwa tumeelezwa madhara yake na wataalamu leo," alisema Naimado Olaiboni.

Naye Mkuu wa Shirika la UNESCO na Ofisa Mwakilishi wa Shirika hilo Tanzania, Bi. Rodrigues alisema anapenda kuona Jamii ya Kimasai inaendeleza mila na tamaduni zao lakini zile nzuri ambazo hazina chembe ya kiunyanyasaji kwa makundi yote. Alisema ukeketaji kwa wasichanga unamadhara makubwa kwa jamii hiyo hivyo haina budi mila hizo kupuuzwa ili kumlinda mtoto wa kike na madhara yanayomkumba anapofanyiwa vitendo hivyo.

"...Napenda kuona Wamasai wanaendeleza mila na tamaduni zao lakini ziwe nzuri na zisizo na chembe ya ukatili wala unyanyasaji, tuangalie ni namna gani tunaziendeleza na kubaki katika uhalisia wetu...nawahakikishia tutashirikiana kuhakikisha hili linafanikiwa kwenu," alisema Bi. Rodrigues akizungumza katika semina hiyo.

Aidha aliwashauri jamii ya Kimasai kupunguza kuwa na idadi kubwa ya watoto na wake ilhali mume akishindwa kuihudumia familia hiyo jambo ambalo limeendelea kuchochea umaskini wa familia hizo vijijini kwani watoto wamekosa mahitaji ya msingi katika familia na kujikuta wakiishi kwa taabu.

Aliwataka Wamasai pia kupinga ndoa za utotoni kwani mabinti wadogo wanapoolewa wanakosa fursa ya elimu pamoja na kuunda familia bora kutokana na uduni wao katika masuala ya afya ya uzazi kiujumla na madhara yanayowaandama katika maisha yao. "...Ndoa za utotoni nazo ni tatizo katika jamii yetu, tuzipige vita maana mtoto mdogo anapoolewa haweza kuunda familia bora na wala uzazi wake hauwezi kuwa bora...," aliongeza Bi. Rodrigues.

Zaidi ya wanasemina 210 kutoka Kata za Ololosokwani, Arash, Soit Sambu, Oloipili, Aoliani Magaidulu wakiwemo viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari na wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii Wilayani Ngorongoro wamenufaika na semina hiyo ya jitihada za kuelimisha jamii juu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati.
Kutoka kushoto ni Mshauri na Mkufunzi wa Masuala ya Vyombo vya Habari Jamii kutoka UNESCO Tanzania, Rose Haji pamoja na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues wakifuatilia semina hiyo iliyoandaliwa na UNESCO juzi. Kutoka kushoto ni Mshauri na Mkufunzi wa Masuala ya Vyombo vya Habari Jamii kutoka UNESCO Tanzania, Rose Haji pamoja na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues wakifuatilia semina hiyo iliyoandaliwa na UNESCO juzi.Baadhi ya washiriki wa semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakifuatilia mada kwenye semina hiyo. Baadhi ya washiriki wa semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakifuatilia mada kwenye semina hiyo.Kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Emanyata Ololosokwani na Mwenyekiti warsha hiyo, Ole Daniel akitafsiri kwa lugha ya kimasai mada ya Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) alipokuwa akiwasilisha. Kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Emanyata Ololosokwani na Mwenyekiti warsha hiyo, Ole Daniel akitafsiri kwa lugha ya kimasai mada ya Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) alipokuwa akiwasilisha.Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) akimsikiliza Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli (kulia) kwenye semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) akimsikiliza Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli (kulia) kwenye semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro.Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akiwasilisha mada katika semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro. Semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akiwasilisha mada katika semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro. Semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Baadhi ya washiriki wa semina hiyo iliyoandaliwa na Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) wakichangia mada mbalimbali. Baadhi ya washiriki wa semina hiyo iliyoandaliwa na Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) wakichangia mada mbalimbali.Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akiwasilisha mada katika semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro. Semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akiwasilisha mada katika semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro. Semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Susana Koillah, Mama Shughuli na mtafsiri wa lugha ya Kimasai katika semina hiyo akisisitiza jambo. Kulia ni Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues. Susana Koillah, Mama Shughuli na mtafsiri wa lugha ya Kimasai katika semina hiyo akisisitiza jambo. Kulia ni Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues.Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akiwasilisha mada katika semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro. Semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akiwasilisha mada katika semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro. Semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Sehemu ya washiriki wa semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni (kushoto) akichangia mada katika semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro. Wengine ni wasaidizi wa Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli wakishiriki semina hiyo. Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni (kushoto) akichangia mada katika semina ya viongozi mbalimbali wa jamii ya kimasai, wazazi, viongozi wa shule za msingi na sekondari Wilayani Ngorongoro, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilaya ya Ngorongoro. Wengine ni wasaidizi wa Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli wakishiriki semina hiyo.Baadhi ya maofisa kutoka Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania wakiwapongeza viongozi wa jamii ya kimasai, Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli pamoja na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni mara baada ya semina kumalizika. Baadhi ya maofisa kutoka Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania wakiwapongeza viongozi wa jamii ya kimasai, Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli pamoja na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni mara baada ya semina kumalizika.Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli pamoja na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni wakipiga picha za kumbukumbu na baadhi ya maofisa kutoka Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania baada ya semina kumalizika. Kulia ni Ofisa Mradi Elimu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Jennifer Kotta akijiandaa kuwapongeza viongozi wakuu wa jamii ya kimasai Afrika Mashariki na Tanzania walioshiriki semina hiyo. Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Kimasai Afrika Mashariki, Mokombo Olaiboni Simeli pamoja na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni wakipiga picha za kumbukumbu na baadhi ya maofisa kutoka Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania baada ya semina kumalizika. Kulia ni Ofisa Mradi Elimu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Jennifer Kotta akijiandaa kuwapongeza viongozi wakuu wa jamii ya kimasai Afrika Mashariki na Tanzania walioshiriki semina hiyo.Ofisa HIV na Elimu ya Afya Taifa wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Mathias Herman (kulia) akisalimiana na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni (kushoto) mara baada ya semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, wakuu shule za sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi. Ofisa HIV na Elimu ya Afya Taifa wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Mathias Herman (kulia) akisalimiana na Kiongozi Mkuu wa Jamii ya Wamasai Tanzania, Sangau Naimado Olaiboni (kushoto) mara baada ya semina ya viongozi wa jamii ya kimasai, wazazi, wakuu shule za sekondari, wakuu wa idara ya afya na vitengo vya ustawi wa jamii wilayani Ngorongoro wakiwa kwenye semina hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro juzi.Imeandaliwa na www.thehabari.com, Ngorongoro .

TBL FAMILY DAY ILIVYOFANA BAHARI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
 Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wakiandika majina ya watoto waliofika pamoja na wazazi wake kwa ajili ya kuwapatia zawadi wakati ya sherehe ya siku ya familia ya TBL iliyofanyika kwenye ufukwe wa bahari beach, dar es salaam juzi.
 Ofisa Uhisano wa TBL, Dorris Malulu akiwa na mumewe wakipata mlo.
 Wakipata chakula wakati wa siku ya familia.
 Watoto wa wafanyakazi wa TBL wakiogelea wakati wa siku ya familia.

 Wafanyakazi wa TBL na familia zao wakicheza muziki
 Mabalozi wa Bia mpya ya Twist wakiwasili kwa boti katika hafla hiyo
 Mabalozi wa Bia mpya ya Twist wakiselebuka kanda ya bahari ya Hindi baada ya kushuka kwenye boti iliyowaleta kwenye ufukwe wa Bahari Beach, Dar es Salaam kushiriki siku ya familia ya Kampuni ya Bia tanzania (TBL)


 Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wakicheza muziki kando ya ufukwe wa bahari beach, dar es salaam wakati wa sherehe ya siku ya familia ya TBL.
Msaani mwenye vimbwanga katika sanaa ya maigizo na sarakasi, Emsi Amani wa kundi la Sanaa la Bantu Acrobatics akionyesha uwezo wake wa kucheza na jukwaa wakati wa siku ya familia ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

MKAGUZI NA MDHIBITI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI,PROFESA JUMA ASSAD ATEMBELEA MAONYESHO YA UTUMISHI WA UMMA YANAYOENDELEA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR

0
0
 Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali,Profesa Juma Assad akisaini katika kitabu cha wageni katika banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA) katika viwanja wa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo  anayeshuhudia ni Meneja wa Mawasiliano TFDA,Gaudensia Simwanza.
  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA).Hitt Sirro akimpa maelezo katibu Mkuu Kiongozi ,Balozi Ombeni Sefue (mwenye Kofia) katika Manonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Jijini Dar es Salaam nyuma ya Katibu Mkuu Kiongozi ni Meneja wa Mawasiliano,Gaudensia Simwaza.
 Katibu Mkuu Kiongozi ,Balozi Ombeni Sefue (Mwenyekofia) akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA).Hitt Sirro katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma  katika viwanja vya Mnazi Mmoja ,jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue( katikati )akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula la Dawa (TFDA) (Picha na Emmanuel Massaka)

JESHI LA POLISI LAKABIDHIWA MSAADA WA JEZI

0
0
Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) Mary Nzuki akipokea  Msaada wa Jezi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa African life Assurance, Bw. Julius Magabe kwa ajili ya Mashindano ya Michezo ya SADC yanayotarajiwa kufanyika Mbabane, nchini Swazland mwaka huu. picha na Tamimu  Adam- Jeshi la Polisi.

Article 15

0
0

AIRTEL FURSA YAWAWEZESHA VIJANA WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
 Meneja Huduma kwa Jamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi (wa pili kulia ), akimkabidhi zawadi ya mashine ya kushonea 'cherehani', kwa Betha Benedict (wa pili kushoto), mkazi wa Bunju Jijini Dar es Salaam baada ya kuwezeshwa na mpango wa Airtel Fursa “Tunakwezesha”. Kushoto ni mama yake Betha na kulia ni Meneja wa Airtel, Fadhili Mwasijeba.
Bertha Benedict (watatu Kulia) akionyeshwa na meneja Huduma wa jamii wa Airtel Hawa Bayumi (wapili Kulia) vifaa alivyokabidhi na Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa. Kushoto ni   Irene Paul balozi wa Airtel kupitia mpango wa Airtel Fursa,  mama yake Betha na kulia ni Meneja mauzo wa Airtel kanda ya kusini, Fadhili Mwasijeba.
 Bertha Benedict (Kulia) akisalimiana na viongozi mbalimbali wa Airtel mara baada ya kuwasili nyumbani kwake kwaajili ya kukabidhi zawadi kupitia mpango wa Airtel Fursa  (katikati), Meneja Huduma kwa jamii wa Airtel Tanzania Hawa Bayumi.
Wafanyakazi wa Airtel wakishusha zawadi  zilizokabidhiwa kwa Bertha Benedict (hayupo pichani)  mkazi wa Bunju Jijini Dar es Salaam baada ya kuwezeshwa na mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha”.
Wafanyakazi  wa Airtel wakiwa katika picha ya pamoja na Bertha Benedict (wapili Kulia) mara baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa. Kutoka kushoto ni Irene Paul balozi wa Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa, mama yake Bertha, Hawa Bayumi na Meneja mauzo wa Airtel  kanda ya kusini , Fadhili Mwasijeba


KAMPUNI  ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa Airtel Fursa ambao umelenga kuwawezesha vijana wajasiliamali wadogo wadogo nchini umetoa msaada mwingine tena jijini Dar es salaam kwa msichana mjasiriamali Bertha Benedicto.

Bertha ambaye amelelewa katika Kituo cha Kulea watoto cha Dogodogo Center Kilichopo Bunju Jijini Dar es Salaam na kuhitimu mafunzo ya mwaka mmoja ya ufundi wa kushona nguo kituoni hapo amepatiwa vifaa mbalimbali pamoja na cherehani ya kisasa ili kuendeleza ujuzi wake.

Akiongea wakati wa makabithiano Meneja wa mahusiano ya jamii wa Airtel Bi Hawa Bayumi alisema  “ Airtel tumeona ni vyema kupitia mpango wetu wa Airtel Fursa kumpatia vifaa na mashine hii ya kisasa ya kushonea Bi Bertha Benedecto  kwa lengo la kumwezesha kuendesha shughuli zake za kiuchumi kwa ufanisi zaidi.  Sambamba na hilo  tumeweza kumpeleka kwenye mafunzo ya kumsaidia  kujijenga, kuweka mahesabu yake na kuendesha biashara yake ili aweze kukuza biashara na kuisaidia familia yake”.

Tunaamini hii ni nafasi ya pekee kwa vijana wadogo kati ya umri wa miaka 17 mpaka 24 walioko katika maeneo mbalimbali ya nchi kuweza kufaidika na mpango huu wa Airtel Fursa wenye lengo la kuwawezesha vijana wajasiriamali wadogo wadogo kukuza mitaji na biashara zao kwa ujumla. Aliongeza Bayumi”

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Bertha amesema vifaa hivyo vitamwezesha kuendesha maisha yake na familia kwa ujumla huku Mama yake Immaculate Makinda akiishukuru Airtel kwa kuwa mkombozi kwao.

Bertha alisema, “nawashukuru sana Airtel kwa kuweza kufanikisha ndoto zangu. Kwa kuweza kunipatia vifaa hivi vya kisasa. Nimekuwa nikipata ugumu wa kupata wateja kwani sikuwa na vitendea kazi vya kutosha vitakavyoweza kukidhi mahitaji ya wateja wangu lakini sasa naamini nitapata wateja wengi sana na kuinua biashara yangu”

Kwa upande wake Mratibu wa Dogodogo Centre, bw.Issa Buzohela alisema, anaiomba kampuni ya Simu ya Airtel  kuendelea kukisaidia kituo hicho na kuinua vipaji vya vijana kwani nchi yetu imezungukwa na vijana wenye vipaji mbalimbali lakini hawana uwezo wa kuendeleza vipaji vyao.

Mpaka sasa Airtel Fursa  imeshawawezesha vijana mbalimbali na kuboresha shughuli zao za kiuchumi kwa kuwapatia vitendea kazi  na kuwaingiza katika warsha za mfunzo ya Airtel Fursa ili waweze kutimiza ndoto zao.
 Meneja Huduma kwa Jamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi (wa pili kulia ), akimkabidhi zawadi ya mashine ya kushonea 'cherehani', kwa Betha Benedict (wa pili kushoto), mkazi wa Bunju Jijini Dar es Salaam baada ya kuwezeshwa na mpango wa Airtel Fursa “Tunakwezesha”. Kushoto ni mama yake Betha na kulia ni Meneja wa Airtel, Fadhili Mwasijeba.
Bertha Benedict (watatu Kulia) akionyeshwa na meneja Huduma wa jamii wa Airtel Hawa Bayumi (wapili Kulia) vifaa alivyokabidhi na Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa. Kushoto ni   Irene Paul balozi wa Airtel kupitia mpango wa Airtel Fursa,  mama yake Betha na kulia ni Meneja mauzo wa Airtel kanda ya kusini, Fadhili Mwasijeba.
 Bertha Benedict (Kulia) akisalimiana na viongozi mbalimbali wa Airtel mara baada ya kuwasili nyumbani kwake kwaajili ya kukabidhi zawadi kupitia mpango wa Airtel Fursa  (katikati), Meneja Huduma kwa jamii wa Airtel Tanzania Hawa Bayumi.
Wafanyakazi wa Airtel wakishusha zawadi  zilizokabidhiwa kwa Bertha Benedict (hayupo pichani)  mkazi wa Bunju Jijini Dar es Salaam baada ya kuwezeshwa na mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha”.
Wafanyakazi  wa Airtel wakiwa katika picha ya pamoja na Bertha Benedict (wapili Kulia) mara baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa. Kutoka kushoto ni Irene Paul balozi wa Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa, mama yake Bertha, Hawa Bayumi na Meneja mauzo wa Airtel  kanda ya kusini , Fadhili Mwasijeba


KAMPUNI  ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa Airtel Fursa ambao umelenga kuwawezesha vijana wajasiliamali wadogo wadogo nchini umetoa msaada mwingine tena jijini Dar es salaam kwa msichana mjasiriamali Bertha Benedicto.

Bertha ambaye amelelewa katika Kituo cha Kulea watoto cha Dogodogo Center Kilichopo Bunju Jijini Dar es Salaam na kuhitimu mafunzo ya mwaka mmoja ya ufundi wa kushona nguo kituoni hapo amepatiwa vifaa mbalimbali pamoja na cherehani ya kisasa ili kuendeleza ujuzi wake.

Akiongea wakati wa makabithiano Meneja wa mahusiano ya jamii wa Airtel Bi Hawa Bayumi alisema  “ Airtel tumeona ni vyema kupitia mpango wetu wa Airtel Fursa kumpatia vifaa na mashine hii ya kisasa ya kushonea Bi Bertha Benedecto  kwa lengo la kumwezesha kuendesha shughuli zake za kiuchumi kwa ufanisi zaidi.  Sambamba na hilo  tumeweza kumpeleka kwenye mafunzo ya kumsaidia  kujijenga, kuweka mahesabu yake na kuendesha biashara yake ili aweze kukuza biashara na kuisaidia familia yake”.

Tunaamini hii ni nafasi ya pekee kwa vijana wadogo kati ya umri wa miaka 17 mpaka 24 walioko katika maeneo mbalimbali ya nchi kuweza kufaidika na mpango huu wa Airtel Fursa wenye lengo la kuwawezesha vijana wajasiriamali wadogo wadogo kukuza mitaji na biashara zao kwa ujumla. Aliongeza Bayumi”

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Bertha amesema vifaa hivyo vitamwezesha kuendesha maisha yake na familia kwa ujumla huku Mama yake Immaculate Makinda akiishukuru Airtel kwa kuwa mkombozi kwao.

Bertha alisema, “nawashukuru sana Airtel kwa kuweza kufanikisha ndoto zangu. Kwa kuweza kunipatia vifaa hivi vya kisasa. Nimekuwa nikipata ugumu wa kupata wateja kwani sikuwa na vitendea kazi vya kutosha vitakavyoweza kukidhi mahitaji ya wateja wangu lakini sasa naamini nitapata wateja wengi sana na kuinua biashara yangu”

Kwa upande wake Mratibu wa Dogodogo Centre, bw.Issa Buzohela alisema, anaiomba kampuni ya Simu ya Airtel  kuendelea kukisaidia kituo hicho na kuinua vipaji vya vijana kwani nchi yetu imezungukwa na vijana wenye vipaji mbalimbali lakini hawana uwezo wa kuendeleza vipaji vyao.

Mpaka sasa Airtel Fursa  imeshawawezesha vijana mbalimbali na kuboresha shughuli zao za kiuchumi kwa kuwapatia vitendea kazi  na kuwaingiza katika warsha za mfunzo ya Airtel Fursa ili waweze kutimiza ndoto zao.

KATIBU MKUU KIONGOZI ATEMBELEA BANDA LA MAMBO YA NJE KWENYE WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue kwenye Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Habu Mkwizu.
Balozi Sefue akisaini Kitabu cha Wageni katika Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Balozi Sefue akisoma Kitabu cha Sera ya Mambo ya Nje huku akisikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Yahya.
Katibu Mkuu Kiongozi,  Balozi Sefue (katikati), Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya (kushoto) wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Manejimenti ya Utumishi wa Umma,  Bw. Habu Mkwizu alipokuwa akiwaelezea jambo.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Taasisi zake wakifurahia jambo na Naibu Katibu Mkuu mara baada ya Katibu Mkuu Kiongozi  kutembelea Banda la Mambo ya Nje.
Juu na Chini ni Balozi Yahya akihojiwa na Mwandishi wa Habari kutoka TBC kuhusu mafanikio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mkufunzi kutoka Chuo cha Diplomasia Bw. Ally Masabo naye akihojiwa na Mwandishi wa TBC
Afisa Mambo ya Nje, Bw. Batholomeo Jungu akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi waliojitokeza kutembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje wakati wa Maonesho ya Utumishi wa Umma.  
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Glory Mboya akisaini Kitabu katika Banda la Maonyesho la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililopo katika maonyesho Utumishi wa Umma Jijini Dar es Salaam
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya akitizama mfano wa Majengo yanayojengwa katika Banda la Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolijia.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa tatu kulia), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Balozi Simba Yahya (wa nne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka Wizarani na Taasisi zake. 
Naibu Katibu Mkuu Balozi Simba Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Wizara na Taasisi zake.
Picha na Reginald Philip

IGP MANGU AFUNGA RASMI MAFUNZO YA UONGOZI WA MAGEREZA DARAJA LA PILI DAR ES SALAAM

0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufunga Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili kwa Maafisa wa Jeshi la Magereza. (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
4
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu akipokea Salaam ya heshima kutoka kwa Gwaride lililoandaliwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili(kushoto katika Jukwaa) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
1
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi wa Magereza Daraja la Pili ambayo yamefungwa rasmi leo Juni 22, 2015 katika Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
6
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja (kulia) akifurahia onesho Maalum la Maafisa wa Jeshi la Magereza kutoka Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani (katikati) ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu (kushoto) ni Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylivester Ambokile wakifurahia onesho hilo kama wanavyoonekana katika picha.

9
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa umakini matukio mbalimbali katika sherehe hizo za kufunga Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili(wa kwanza kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(katikati) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Erasmus Kundy.
2
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu akimvisha cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza Mhitimu wa Mafunzo ya Uongozi wa Magereza Daraja la Pili ambaye amefanya vizuri kwa upande wa Gwaride, Stafu Sajini Boniphace Felix. Mhitimu huyo amevishwa cheo hicho kwa niaba ya Wahitimu 216 wa Mafunzo hayo.
3
Wahitimu wa Mafunzo ya Uongozi wa Magereza Daraja la Pili wakipita mbele ya Mgeni rasmi IGP Ernest Mangu (hayupo pichani), katika mwendo wa haraka wakitoa heshima leo Juni 22, 2015 katika Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga. Jumla ya Wahitimu 216 wamehitimu Mafunzo Uongozi Daraja la Pili na kupandishwa cheo cha Mkaguzi Msaidizi wa Magereza.
  5
Maafisa wa Jeshi la Magereza wakionyesha umahiri mkubwa wa mbinu mbalimbali za kujihami  na adui kama wanavyoonekana kikakamavu katika picha wakati wa hafla fupi ya kufunga Mafunzo ya Uongozi Daraja la Pili.
   8
Kikundi cha kwaya kinachoundwa na Maafisa wa Jeshi la Magereza wa Chuo cha Maafisa Magereza, Ukonga kikitumbuza mbele ya Mgeni rasmi, IGP Ernest Mangu(hayupo pichani)katika sherehe za kufunga Mafunzo hayo ya Uongozi Daraja la Pili, Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga.

BARAZA LA USHAURI LA WATUMIAJI USAFIRI WA ANGA TCAA-CCC WASHIRIKI KIKAMILIFU WIKI YA UTUMISHI WA UMMA MNAZI MMOJA DAR ES SALAAM

0
0
Kikosi kazi cha Watumishi wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafiri wa Anga (TCAA-CCC) wakiwa tayari kutoa huduma kwa wageni mbalimbali watakaotembelea banda hilo katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Athuman Bakari, Aziza Tamim na Debora Mligo.
Watumishi wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafiri wa Anga (TCAA-CCC)wakitoa huduma kwa wageni mbalimbali waliotembelea banda hilo leo.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga (TCAA-CCC), Hamza Johari akizungumza jambo wakati wa mahojiano na waandishi wa habari waliotembelea banda hilo.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga (TCAA-CCC), Hamza Johari akiwa katika mahojiano na waandishi wa habari wa Magazeti ya serikali(Daily News na Habarileo) waliotembelea banda hilo Dar es Salaam jana.
 Debora Mligo na Aziza Tamim wa TCAA-CCC wakiwasikiliza wageni waliotembelea banda hilo.
Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Charles Chacha  akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga (TCAA-CCC) liliopo kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto   ni  Katibu Mtendaji wa Baraza Hamza Johari ,waelimishaji na wahamasishaji  wa baraza hilo Debora Mligo na Athuman Bakari.
Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) Charles Chacha  (mwenye suti)  katikati akiwa katika picha na  ya Pamoja na wafanyakazi wa Baraza la Ushauri la watumiaji Huduma za Usafiri wa anga (TCAA-CCC)wakati alipotembelea kwenye banda lhilo  kwenye maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

SERIKALI YA AWAMU YA NNE YAFANIKIWA KUIMARISHA UMOJA,AMANI NA UTULIVU MIONGONI MWA WANANCHI

0
0
Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Angelina Madete akiwaeleza waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mafanikio ya serikali ya nne ikiwamo kujenga umoja, amani na utulivu miongoni mwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi. Picha na Hassan Silayo-MAELEZO.02
Mkurugenzi wa Muungano, Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Baraka Rajab Baraka akitoa wito kwa wananchi kulinda, kuudumisha na kuendeleza muungano ili kuwa na nchi yenye umoja, amani na usalama, wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Angelina Madete.03
Kaimu Mkurugenzi Uzingatiaji na Ufuatiliaji wa Sheria kutoka Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC) Ruth Lugwisha akiwaasa wananchi kubadili tabia na kuacha kutumia mifuko ya plastiki isiyoruhusiwa ili kuepuka uchafuzi wa Mazingira na Athari zake, wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi.

…………………………………………….

Na Frank Mvungi-MAELEZO
Serikali imeendelea kuimarisha umoja,amani na utulivu miongoni mwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kipindi cha miaka kumi.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Angelina Madete wakati wa mkutano na vyombo vya habari leo jijini Dar es salaam.
Mhandishi Madete alisema kuwa suala la muungano ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya awamu ya nne kwa dhumuni la kuimarisha umoja na utulivu nchini.
“Serikali ya awamu ya nne inajivunia uimarikaji wa Umoja, amani na utulivu miongoni mwa wananchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani ilikuwa ni moja ya kipaumbele kilichowekwa na serikali hii katika kipindi cha miaka Kumi ya Uongozi wa Rais Dkt. Jakaya Kikwete.” Alisema Mhandisi Madete.
Mhandishi Madete aliongeza kuwa Taasisi za Muungano kama Ulinzi na Usalama,Uhamiaji na Uraia,Fedha , Sarafu na Mawasiliano zimeendelea kuimarika kwa kutoa huduma bora kwa wananchi katika kipindi cha Serikali ya awamu ya nne.
Akifafanua Madete amesema katika kipindi cha awamu ya nne wananchi wa pande zote mbili za muungano wameendelea kunufaika na shughuli za kiuchumi na kuongeza ajira kupitia utekelezaji wa program za maendeleo ikiwemo mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF),Progamu ya usimamizi wa Bahari na Pwani (MACEMP) na mradi wa kutoa mikopo kwa ajili ya miradi midogomidogo (SELF).
Miradi mingine ni program ya maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) , mradi shirikishi wa program za maendeleo ya kilimo( PADEP) na program yamaendeleo ya Mileninia ambayo kwa pamoja imewanufaisha wananchi kwa kuwaletea maendeleo endelevu.
Mafanikio mengine ni ujenzi wa majengo ya Taasisi za Muungano ikiwemo kukamilika kwa ujenzi wa Ofisi ya Makamu wa Rais,Mtaa wa Lithuli,Dar es salaam,awamu ya pili ya ujenzi wa ofisi ya Makamu wa Rais Tunguu-Zanzibar umekamilika kwa kiwango kikubwa.
Pia ujenzi wa Tawi la Benki Kuu lililopo Gulioni Zanzaibar umekamilika ambapo majengo mengine yaliyojengwa ni pamoja na uhamiaji,Makao makuu na Ofisi za BungeTunguu na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).
Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kuratibu shughuli za Muungano na kudumisha ushirikiano kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Pia itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa Muungano kwa wananchi wote.

SHIRIKA LA BIASHARA LA TAIFA ZANZIBAR (ZSTC) LAFANYA MKUTANO NA WAKULIMA WA KARAFUU MKOA WA KUSINI UNGUJA.

0
0
Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Dkt. Idrissa Muslih Hijja akifungua Mkutano wa Wakulima wa zao la Karafuu wa Mkoa Huo uliofanyika Skuli ya Dunga.5
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Mwanahija Almas Ali akizungumza na wakulima wa zao la Karafuu katika mkutano uliofanyika Skuli ya Dunga.4
Afisa kutoka Wizara ya Kilimo na Maliasili Badru Mwemvura akitoa tathmini ya ugawaji wa miche ya mikarafuu inayotolewa na Wizara ya Kilimo na Maliasili katika mkutano wa wazalishaji wa zao la karafu wa Mkoa Kusini Unguja.1

3 
Baadhi ya wakulima wa zao la karafuu wakifuatilia mkutano huo uliofanyika Skuli ya Dunga.
………………………………………………………………….
Habari Picha- na Makame Mshenga- Maelezo Zanzibar. 
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Mwanahija Almas Ali amewataka wakulima wa zao la Karafuu kuunga mkono  juhudi zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha ubora wa zao la Karafuu za Zanzibar  unabakia ili kukidhi vigezo vya sifa vya Kimataifa.
Akizungumza  katika mkukutano wa Wakulima wa Karafuu wa Mkoa Kusini Unguja uliofanyika Skuli ya Dunga amesema lengo la Serikali katika kilimo cha zao la Karafuu ni kuona linaendelea kuwa tegemeo katika kuingiza fedha za kigeni na kusaidia kukuza Uchumi hivyo linahitaji kulindwa na kila Mwananchi kwa kuongeza uzalishaji na kulinda ubora.
Mwanahija ameeleza kuwa Karafuu ni zao la Kilimo lenye faida kubwa katika kuimarisha uchumi na ametaka kila mmoja ashiriki katika kulikuza na kuliendeleza ili kuhuisha ustawi wa wakulima na wananchi kwa jumla.
“Kukuza Kilimo cha Karafuu ni sawa na kukuza maendeleo ya Zanzibar, jitihada za makusudi zinahitajika ili lengo la Serikali liweze kufikiwa,” alisisitiza Mkurugenzi Mwendeshaji ZSTC.
Amewataka wakulima wa zao hilo kuchukua jitihada za makusudi kuhakikisha usafi wa Karafuu  unaimarika kwa vile  hadaa na uchafuzi wa zao hilo ni hasara kwa wakulima, wananchi na Taifa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZSTC Kassim Maalim Suleiman amewataka  Wakulima wa zao la Karafuu kutumia utaalamu wa kisasa na kuachana kuendeleza Kilimo hicho kwa mazoea.
Aidha amewashauri Wakulima hao kufungua akaunti benki ili waweze kuingiziwa fedha  moja kwa moja baada ya kuuza Karafuu zao na kuachana na tabia iliyozoeleka ya kutembea na fedha nyingi mifukoni.
Akifungua mkutano huo Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Dkt. Idrissa Muslih Hijja amelipongeza Shirika  la Biashara la Taifa Zanzibar  kwa kuwa karibu na Wakulima wa zao hilo.
Amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuendeleza juhudi za kupambana na baadhi ya watu wanaoendelea kusafirisha zao hilo kwa njia ya magendo licha ya kuwa vitendo hivyo vimepungua kwa sasa.  
Afisa kutoka Wizara ya Kilimo na Maliasili Badru Mwemvura amesema Wizara inaendelea kuchukua jitihada za kuimarisha zao la Karafuu kwa kuatika miche na kutoa bure kwa Wakulima.
Alisema lengo lilikuwa ni kuotesha miche 500, 000 kwa mwaka Unguja na Pemba ili kufufua  zao la Karafuu kuanzia  mwanzoni mwa miaka ya 2000 kutokana na kushuka uzalishaji wa zao hilo.
Hata  hivyo amesema kuanzia mwaka 2012 hadi mwaka uliopita lengo hilo liliongezeka na kufikia  1,000,000 baada ya Wizara kushajiisha jamii kuotesha miche ya mikarafuu kupitia skuli za wakulima.
Ameongeza kuwa miche ya mikarafuu inagawiwa bure kwa Wakulima kupitia kwa masheha, maafisa Kilimo na misitu wa Wilaya na kila mkulima hupatiwa miche 35 hadi 40 na Wizara  imekuwa ikifuatilia kwa karibu maendeleo ya uotaji wake.
Mwemvura  amesema pamoja na juhudi hizo bado zipo changamoto nyingi ikiwemo mahitaji ya miche kuwa kubwa kuliko uwezo wa kuotesha, huduma dhaifu kwa mikarafuu michanga na baadhi ya wakulima kutaka miche mingi kuliko uwezo wa kuipanda na kuihudumia                                          
Wakitoa michango yao baadhi ya Wakulima wamelalamikia ugawaji mbaya wa miche ya mikarafuu unaofanywa na Maafisa wa Kilimo kwa kutoa miche yenye ubora kwa wakubwa na wengine kupewa miche dhaifu ambayo mingi ya miche hiyo inakufa.
Aidha Wakulima hao wamesisiza juu ya usimamizi wa Sheria ili ziweze kusaidi kulinda ubora wa zao hilo la Karafuu na kutomuonea muhali mtu yoyote.

SIMBA SPORT CLUB WAZINDUA TOVUTI YAKE

0
0
AfisaMtendajiMkuuwa EAG Group Imani Kajula Akimwelezea Jambo Rais wa Simba Sport Club Evans Aveva (Aliyekaa) Wakati wa Uzinduzi wa Tovuti ya Club Hiyo ,Anayeshuhudia ni Makamu wa Rais wa Club ya Simba Geofrey Nyange ‘Kaburu

Simba Sports Club leo hiiimezindua tovuti yake Ili kukuza  mawasiliano  na  wadau wake mbalimbali  hususani; wanachama, wapenzi, vyombo  vya  habari na wadau wengine muhimu. 

Akizungumza  wakati  wauzinduzi  huo  Rais  wa  Simba Evans Aveva  alisema ‘’Katika dunia na zama  za  utandawazi  tovuti  ndio  na  mitandao   ya   jamii   ndio  njia  kuu ya mawasiliano. Sisi  tuliliona  hili  na  leo  hii  nafurahi  kuwa  Simba Sports Club itazindua  rasmi  tovuti  yake  ambayo  itakuwa  jukwaa  kuu la mawasiliano  na utoaji wa taarifa zake za  club ya   Simba. Natarajia wengi wenu mtaitumia kikamilifu na muhimu zaidi mtatupa mrejesho chanya kuhusu  tovuti yetu’’. 

AfisaMtendajiMkuuwa EAG Group Imani Kajula ambao ni washauri watekeleza ji wa Masokona Biashara wa Simba alisema ‘’Tovuti hii sio tuitaiwezesha Simba kuwapa wadau wake taarifa mbalimbalibali pia  itatumika  kwa  ajili  ya uuzaji  wa  vifaa  vya  Simba, Bidhaa  mbalimbali  mpya  na  muhimu  zaidi  kuwaunganisha   wanachama, mashabiki  na wapenzi wa  Simba  kutumia   mitandao  ya  jamii  iliyo   rasmi  ya  Simba Sports Club’’. 

Mkutano   huo  wa  wandishi  wa  habari   ulitumika  kutaarifu   Wanachama, Wapenzina  Vyombo   vya   habari   juu   ya  kocha   mpya   wa   Simba. Alizungumza  wakati  wakumtambulisha   kocha   mpya   wa   Simba, Rais   Aveva   alisema ‘’Baada ya kupitia  vyeti  na  maombi   ya  makocha   mbalimbali, Napenda  kuwa taarifu kuwa Klabu ya Simba imeingia  kwenye  mkataba  wa   kuifundisha   na   kocha Dylan Kerr raia   wa   Uingereza. Ni kocha   mwenye    uzoefu   wa   zaidi   ya   miaka 30, akiwa  amefanya  kazi  Nchi  mbalimbali  zikiwemo    Uingereza, Scotland, Vietnam   na    AfrikayaKusini’’. 

Aliendelea  kusema ‘’Tunaamini   ujuzi   na   uzoefu wake wa  ukocha na pia kama mchezaji wa kiwango cha juu  utakuwa   chachu   ya   kuifanya   Simba    ifanye    vizuri’’

Ansaf, RCT waishauri Serikali ushuru wa mchele

0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge akizungumza na waandishi wa habairi jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele,
Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania, Julius wambura akifungua semina  hiyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge akizungumza na waandishi wa habairi jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele,
Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania, Julius wambura akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
 Mkulima wa Mpunga kutoka Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita akizungumza na waandishi wa habri kuhusu soko la mchele linavyoathirika na mchele wa kutoka nje.
 Washiriki wa mkutano huo. 
Slyvatus Kashanga akitoa mada kuhusu jitihada za kuboresha sekta ya Mpunga ili kulinda matarajio ya wazalishaji wa mchele wa Tanzania.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX



BARAZA la Mchele nchini (RCT) kwa kushirikiana na taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na masuala ya kilimo (ANSAF), wameishauri serikali kutekeleza na kuendeleza sheria ya tozo ya ushuru wa forodha ya asilimia 75 kwa mchele unaotoka nje ya Shirikisho la Afrika Mashariki ili kuwaboreshea bei wakulima wa hapa nchini.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima wa mchele, Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge, alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia mkulima wa hapa nchini aweze kupata bei inayoendana na uhalisia wa zao hilo.


Rukonge alisema mchele mwingi unaoingizwa hapa nchini umekuwa haulipiwi kodi, jambo linalosababisha madhara makubwa kwa mkulima, ikiwemo kushindwa kujiendeleza katika kilimo hicho na kuongeza kwamba kwa sasa mawaziri wa shirikisho hilo wapo mbioni kutaka kubadilisha ushuru huo uwe chini ya asilmia 75, jambo ambalo halikubaliki.


Naye Mwenyekiti wa Baraza la Mchele Tanzania (RCT), Julius Wambura, alisema serikali inatakiwa kupanua wigo wa ukusanyaji wa takwimu za bei ya mchele ili kila mwananchi aweze kupata taarifa sahihi na kwa wakati.



Kama vile haitoshi, Wambura aliomba serikali kuwezesha bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko ianze kazi ili iweze kutekeleza majukumu yake pamoja na kuweka madaraja na viwango vya ubora vinavyotakiwa kwa walaji wa mchele wa ndani na masoko ya nje.

BALOZI SEFUE ATEMBELEA BANDA LA PPF, NA KUSIFU HUDUMA ZAKE.

0
0
 KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, (aliyekaa), akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, (kushoto), alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye wa Maonyesho ya Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam Juni 22, 2015
 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG), Profesa Mussa J. Assad, (kushoto), akipatiwa maelezo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, (kulia), wakati alipotembelea banda la PPF kwenye Maonyesho yanayoendelea ya Wiki ya Utumishi wa Umma, kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Juni 22, 2015



Balozi Sefue, akisaini kitabu cha wageni baada ya kutembelea banda hilo

MATUKIO KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA-JUNI 21,2015

0
0
1
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Peramiho na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge,Jenista Mhagama bungeni mjini Dodoma Juni 22, 2015. (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)
2
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama akiteta na Mbunge wa Kibakwe na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene bungeni mjini Dodoma Juni 22, 2015.
3
Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda akteta na Mbunge wa Nkenge, Asumta Mshama kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.4
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mwanasheria  Mkuu wa Serikali, George masaju kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma juni 22, 2015.

5
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Sanya (kushoto ) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.
6
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu la Parokia ya Karatu kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma juni 22, 2015. Kushoto kwake ni Mbunge wa Viti Maalum, Cecilia Paresso.
7
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na watoto wa Shirika la Moyo Mtaktifu wa Yesu wa Parokia ya Karatu, kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.
8
9
Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai akiteta na Mbunge wa Viti Maalum Maria Hewa kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 22, 2015.
10
Waziri  Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Mafia , Abdulkarim Shahah  (kulia) na Mbunge wa Moshi Mjini Philemon Ndesamburo (katikati) kwenye jengo la Utawala la  Bunge mjini Dodoma juni 22, 2015.

BERNARD MEMBE APATA WADHAMINI WILAYANI CHAMWINO -DODOMA, ATEMBELEA MNARA WA KUMBUKUMBU YA MW. NYERERE KATIKA KIJIJI CHA CHAMWINO IKULU

0
0
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akilakiwa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliofika kwenye viwanja vya Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Chamwino Ikulu, wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kumdhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho. 
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akiangalia kikundi cha ngoma za asili wakati alipowasili kwenye viwanja vya Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Chamwino Ikulu, wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho.
 Mzee Aidan Mazego (kushoto), akitoa salamu za baraka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (katikati) alipofika kwenye Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Chamwino Ikulu, wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kulia ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Dodoma, Mzee William Kusila.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Chamwino Ikulu, Joseph Seganje kuhusu Mnara wa kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyeishi katika kijiji hicho, kuanzia Julai 10.1971 hadi Oktoba 30.1971 akihimiza siasa ya ujamaa na kujitegemea nchi nzima, wakati Waziri Membe alipofika wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wa pili (kushoto) ni Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Janeth Mashele.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akisoma falsafa za Mwl. Nyerere alipotembelea Mnara wa kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyeishi katika Kijiji cha Chamwino Ikulu, kuanzia Julai 10.1971 hadi Oktoba 30.1971 akihimiza siasa ya ujamaa na kujitegemea nchi nzima, wakati Waziri Membe alipofika wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wa tatu (kushoto) ni Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Janeth Mashele.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akitazama picha za matukio mbalimbali ya Mwl. Nyerere alipotembelea Mnara wa kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyeishi katika Kijiji cha Chamwino Ikulu, kuanzia Julai 10.1971 hadi Oktoba 30.1971 akihimiza siasa ya ujamaa na kujitegemea nchi nzima, wakati Waziri Membe alipofika wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma Juni 22.2015, kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kushoto ni Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Dodoma, Mzee William Kusila na (wa tatu kushoto) ni Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Janeth Mashele.

Viewing all 46206 articles
Browse latest View live




Latest Images