Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

WASANII WAHAMASISHA VIJANA JUU YA KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI LA WAPIGAKURA.

$
0
0

 Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa Kampuni ya  Mawasiliano na Masoko,Consitantine Magavila akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO jijini Dar es Salaam.kutoka kushoto ni msanii wa Bongo Fleva George Mdemu (Gnako),Afisa mipango wa kampuni ya Open Society Intiative for Eastern Africa(OSIEA),Adam Antony,Afisa Elimu NEC,Rose Malo pamoja na Snura Mushi(Snura).
 Afisa Elimu wa NEC,Rose Malo akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na vijana walioona umhimu wa kupiga kura na kuhamasisha vijana wengine kwa njia ya nyimbo,kutokana na mwaka huu kuwa ni mwaka wa Uchaguzi mkuu hapa nchini akizungumza katika ukumbi wa Idara ya habari maelezo jijini Dar es Salaam leo. kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa Kampuni ya  Mawasiliano na Masoko,Consitantine Magavila na Afisa mipango wa kampuni ya Open Society Intiative for Eastern Africa(OSIEA),Adam Antony.

kutoka kushoto ni msanii wa Bongo Fleva George Mdemu (Gnako), Snura Mushi (Snura),Kala Masanja (Kala Jeremiah) pamoja na Boniventure Kabogo(Stamina) wakiimba kipande cha wimbo ambao utakuwa ukielimisha jamii kuhusiana na umhimu wa upigaji kura katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.


Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika Mkutano wa wanaohamasisha vijana kupiga kura katika uchaguzi mkuu mwaka huu.(Picha na Avila kakingo.)


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

VIJANA wamekuwa na changamoto ya kutoshiriki katika zoezi la kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura na kushindwa kupata haki yake msingi ya kupiga kura katika chaguzi mbalimbali zinazofanyika nchini.


Kutokana na kuwepo kwa hali hiyo Kampuni ya  Mawasiliano na Masoko kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),Shirika la Open Society International  pamoja na wasanii mbalimbali wa muziki wameanzisha kampeni maalum kwa ajili ya kuhamasisha vijana kujiandikisha katika daftari la wapiga kura katika mikoa ambayo daftari hilo halijapita.


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Idara ya habari Maelezo,Mmoja wa Wakurugenzi wa Mawasiliano na Masoko,Consitantine Magavila amesema kuwa kampeni hiyo wasanii mbalimbali wametengeneza nyimbo moja inayoenda kwa jina la Kuradili  kwa ajili ya kuhamasisha vijana kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura na hatimaye kupiga kura.


Amesema wasanii walitunga nyimbo hiyo ni Gnako,Snura,Izo Biznez,Kala Jeremiah pamoja na Stamina ambao watapita kutumbwiza katika mikoa ya Dar es Salaam,Morogoro,Mwanza, pamoja na Shinyanga na hakuna  kiingilio katika matamasha hayo yaliyolenga kufikia watu milioni nne wakiwemo vijana.


“Vijana wanaweza kuleta mabadiliko endapo watajitokeza katika kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura na hatimaye kupiga kura lakini tumeona fursa yetu ni kuwahamasisha waweze kufanya hivyo”amesema Magavila.


Nae Afisa Elimu NEC,Rose Malo,amesema kujitokeza na kampuni hiyo itasaidia vijana kuhaamasika kujiandikisha katika daftari la mpiga kura kutokana na ujumbe kutoka kwa vijana wenzao.  




MONICA MWAMNYANGE AZINDUA BARAZA LA WATUMIAJI WA USAFIRI WA ANGA HAPA NCHINI.

$
0
0
 Naibu Katibu wa wizara ya uchukuzi Monica Mwamnyange akizungumza na waandishi wa habari  kuhusiana na uzinduzi wa Baraza la watumiaji wa huduma za usarifishaji wa Anga hapa nchini mara baada ya kutoka kwenye mkutano uliofanyika katika Hotel ya New Africa jijini Dar es Salaam leo.
 Katibu mtendaji wa Baraza la watumiaji wa usafiri wa anga hapa nchini Hamza Johari akizungumza na waandishi wa habari  kuhusiana watumiaji wa usafiri wa anga kutokuweka vitu vya thamani kubwa kwenye mabegi yao wakati wa kusafiri katika mkutano uliofanyika katika Hotel ya New Africa jijini Dar es Salaam leo.
Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Baraza la watumiaji wa usafiri wa anga hapa nchini.(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA.)

WAZIRI BERNARD MEMBE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA UMOJA WA AKINAMAMA WA KIKRISTO, ZANZIBAR.

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Umoja wa Kinamama wa Kikristo (UMAKI) wa Kanisa Angikana Dayosisi ya Zanzibar mjini Unguja jana. Kulia kwake ni Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa Anglikana.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (wa pili kulia), akipata maelezo kuhusu bidhaa za ujasiriamali za kikundi cha Umoja wa Kinamama wa Kikristo (UMAKI) wa Kanisa Angikana Dayosisi ya Zanzibar, kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa Nne wa UMAKI mjini Unguja jana. Picha zote na John Badi.

OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI YAENDESHA MAFUNZO KWA TAASISI WADAU WA USIMAMIZI WA SHERIA.

$
0
0
Afisa Sheria wa NAOT, Bw. Frank Sina (kulia) akizungumza katika mafunzo hayo.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad (aliyesimama) akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria na Ofisi yake katika kuimarisha matumizi bora ya rasilimali za nchi. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo, Bibi Felista Tirutangwa na Mchambuzi wa Masuala ya Fedha kutoka Ofisi ya Rais, Bw. Stephene Likunga (Kulia).
 Washiriki wa Mafunzo ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria Juu ya Ripoti ya Ukaguzi ya CAG na Jinsi ya Kuitafsiri wakimsikiliza kwa makini Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),  Prof. Mussa Assad (aliyesimama). Mafunzo hayo yalifanyika katika Hoteli ya Den France, Dar es Salaam.
 Muwakilishi wa washiriki wa Mafunzo ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria Juu ya Ripoti ya Ukaguzi ya CAG na Jinsi ya Kuitafsiri, Bw. Stephene Likunga (aliyesimama) akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wenzake.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria Juu ya Ripoti ya Ukaguzi ya CAG na Jinsi ya Kuitafsiri.


Na Mwandishi wetu
Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi imeendesha mafunzo ya siku moja ya Taasisi Wadau wa Usimamizi wa Sheria juu ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) na jinsi ya kuitafsiri yanayofanyika katika Hoteli ya Den France jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad alisema kuwa mafunzo yanalenga kuwapa ufahamu juu ya ripoti za ukaguzi ambazo Ofisi yake inazitoa, na jinsi ya kuzitafsiri na kushughulikia masuala ya maadili yanatokana na ripoti za ukaguzi.

Prof. Assad aliongeza kuwa mafunzo hayo yanafanyika kwa kuzingatia Kifungu cha 27 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma, 2008, kama ilivyofanyiwa mabadiliko na Sheria ya Fedha Na. 10 ya mwaka 2010.

Kwa mujibu wa kifungu hiki, kinawataka wakaguzi wanaofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali mara tu wanapobaini kuwepo kwa viashiria vya ulaghai/kugushi au rushwa wanapokuwa wanafanya ukaguzi kutoa taarifa kwa CAG.

Kifungu kinaongeza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali akithibitisha kuwepo wa viashiria hivyo anapaswa mara moja kuvitaarifu vyombo vya dola vya uchunguzi na nakala ya taarifa hiyo kuiwasilisha kwa Mkurugenzi wa Mashitaka.

“Kifungu hiki kinaeleza vyombo hivyo vya dola (DCI/PCCB) kufanya uchunguzi wa kitaalamu juu ya tuhuma hizo na kukamilisha zoezi la uchunguzi ndani ya siku 60 tangu siku ya kwanza. Mara baada ya kumaliza uchunguzi huu vinapaswa kuwasilisha ripoti yao kwa Mkurugenzi wa Mashitaka kwa ajili ya maamuzi ya hatua za kisheria zinazopaswa kuchukuliwa. Mkurugenzi wa Mashitaka anapaswa kwa mujibu wa kifungu hiki kumtaarifu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu juu ya hatua alizochukua,” Prof. Assad alifafanua.

Prof. Assad alisema kuwa utekelezaji wa kifungu hiki kwa sasa unaendelea ingawa wakuu wa Taasisi wadau waliona ni vyema kuwepo na mpango maalumu wa utekelezaji wake. Kwa mujibu wa CAG, mpango huu utaongeza ufanisi zaidi katika utekelezaji wa matakwa ya sheria ya ukaguzi.

Prof. Assad aliongeza kuwa licha ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kupongezwa kutokana na utendaji kazi wake, hata hivyo, kumekuwa na malalamiko kuwa hakuna hatua za kuridhisha zinazochukuliwa. “Kwa mujibu wa maoni ya wananchi wa kawaida, hakuna hatua stahiki zinazochukuliwa dhidi ya watu wanaobainika kufuja mali za umma au kutumia mamlaka yao vibaya kama ripoti hizo zinavyokuwa zinaonesha,” alisisitiza.

Prof. Assad aliongeza kwa kuzingatia maoni hayo, mafunzo hayo yanategemea kuboresha ufanisi katika utendaji kazi kwa washiriki wa mafunzo. Aliwasihi washiriki wa mafunzo hayo wakiwa sehemu ya wadau katika maendeleo ya Tanzania hawana budi kusimamia uwajibikaji na kusimamia utawala bora ili kuongeza kasi ya maendeleo ya nchi.

Prof. Assad aliongeza kuwa mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli za mradi unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID) katika Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.

“Naishukuru sana USAID kwa kufadhili mafunzo haya kwani yanachochea uelewa wa namna bora ya kutafsiri ripoti za ukaguzi na kushughulikia masuala ya maadili yanatokana na ripoti hizo,” aliongeza Prof. Assad.

Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo, Mchambuzi wa Masuala ya Fedha kutoka Ofisi ya Rais, Bw. Stephene Likunga alimuomba CAG kuendelea kutoa mafunzo hayo kila wakati ili kuwaongezea uwezo wataalam wanaotumia Taarifa za Mkaguzi Mkuu.


“Tunaomba mafunzo haya kuwa endelevu ili kuwa tija katika kuchambua kwa kina taarifa zako kwa kina kwa faida ya umma,” alisema.

VIBALI KWA ASASI ZA KIRAIA KUSHIRIKI KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA.

150 KORTINI KWA KUJIANDIKISHA MARA MBILI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGAKURA KWA MFUMO MPYA BVR.

$
0
0
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema watu 152 watafikishwa mahakamani mkoani Njombe kutokana na kujiandikisha mara mbili katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo mpya wa ‘Biometric Voter Registration Kit’ (BVR).

Aidha, imeeleza kuwa kata 130 zimeongezeka kutokana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kufanya mabadiliko ya kiutawala katika kata, vijiji,vitongoji na Mitaa hivyo kulazimu NEC kuhairisha kwa wiki moja uandikishaji wa daftari uliokuwa ukianza jana kwa baadhi ya mikoa.

Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dk Sisti Cariah alisema hayo jana wakati akielezea kuahirishwa kwa wiki moja uandikishaji hadi Juni 16 mwaka huu kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Mara.

Akizungumzia suala la watu kujiandikisha mara mbili, alisema katika mkoa wa Njombe ambao Daftari hilo liko tayari na wiki ijayo litawekwa wazi kwa siku tano na kisha kufanyiwa marekebisho kwa siku moja na wamebaini watu 152 waliojiandikisha mara mbili.

Alisema watu hao wametenda kosa la jinai na watashtakiwa, huku akitoa onyo kwa watu kuacha kufanya hivyo kwani mashine za BVR zinagundua wanaojiandikisha zaidi ya mara moja.

Alisema wataweka wazi baadhi ya watu waliojiandikisha mara mbili kwenye mikoa yote, ambayo iko tayari.

Alisema mpaka sasa tayari wamepokea madaftari yaliyokamilika ya uandikishaji kwa mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma huku uandikishaji huo ukiwa umekamilika kwa asilimia 50 na wanatarajia kukamilisha uandikishaji mwezi Julai.

Akizungumzia suala la mipaka ya kiutawala, yaliyofanywa na Tamisemi, Cariah alisema ilifanyika wiki mbili zilizopita katika mikoa mbalimbali, jambo lililosababisha kusitisha uandikishaji katika mikoa hiyo huku mikoa ambayo tayari uandikishaji umefanyika watarekebisha wakati wa kuweka wazi daftari.

“Katika kupiga kura lazima kitambulisho kioneshe kata anayokaa mtu kwa mabadiliko haya yamefanya kata kubadilika na kuongezeka 130 hivyo kufanya madiwani watakaopigiwa kura kuongezeka hivyo kata kuendana na kitambulisho,” alisema.

Alisisitiza kuwa kutokana na changamoto hiyo mikoa hiyo mitano, itaanza uandikishaji pamoja na mikoa ya Tanga na Morogoro Juni 16 mwaka huu na baadaye Juni 25,mwaka huu wataanza uandikishaji katika mkoa wa Pwani.

Alisema sasa wanatumia Mashine za BVR 8,000 walizokuwa wanahitaji pamoja na vipuri vyake vyote ziliwasili yangu mwezi uliopita.

Alisema katika mkoa wa Dar es Salaam uandikishaji utaanza Julai2 mwaka huu kwa kutumia BVR zaidi ya 3,000, ambazo kila moja ina uwezo wa kuandikisha watu 120 na hiyo itatokana na kuwa mikoa nane, uandikishaji utakuwa umemalizika na zote kutumika katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

“Jijini Dar es Salaam sehemu zenye watu wengi kutakuwa na mashine hizo nyingi huku vituo vyote, vikifunguliwa kwa mara moja ikifuatiwa na Zanzibar, ambapo wataandikisha waliokosa sifa za kuandikishwa katika Daftari la ukaazi kwa ajili ya kupiga kura ya kumchagua Rais wa Muungano”alisema.

Akizungumzia changamoto ya watu kusubiri kwa muda mrefu katika vituo vya kujiandikisha, alisema hiyo inatokana na kuwa Printa za kusafisha picha zinatakiwa kubadilishwa kila baada ya wapigakura 400 kutokana na vumbi na muda huo wtau uona kama mashine zimeharibika lakini ni utaratibu wa kawaida.

Cariah alisema uandikishaji umekamilika kw amikoa mitano ya Njombe, Lindi, Mtwara, Ruvuma na Iringa na imefanikiwa kwa kiasi kikubwa na wanaendelea katika mikoa 12 sasa ambayo ni Katavi, Rukwa, Mbeya, Dodoma, Singida, Kigoma, Kagera, Simiyu, Mwanza, Geita na Shinyanga.

Akizungumzia mafanikio ya mikoa hiyo kuwa takwimu ilikuwa kuandikisha wapigakura 518,230 na waliandikisha watu 529,224, Mtwara walitakiwa 732,465 waliandikisha 727,565, Ruvuma wapigakura 783,296 waliandikishwa 826,779 na Iringa wapigakura 524,390 waliandikishwa 526,006.

LOWASSA ATIKISA SHINYANGA 7000 WAMDHAMINI URAIS.

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na motto mwenye ulemavu wa ngozi, Kabula Zacharia, anayetunzwa kwenye kituo cha kulea watu wenye ulemavu wa ngozi cha Buhangija mkoani Shinyanga, mara baada ya kupata wana CCM wa kumdhamini kufuatia kuchukua fomu za kuomba chama kimteue kuwania urais wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. . Mh. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa. (Picha na K-VIS MEDIA)
Mh. Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wana CCM waliomdhamini mkoani Shinyanga, kutoka kwa katibu wa CCM wilaya ya Shin yanga mjini Charles Sangula, Juni 11, 2015.
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, akipungia mkono wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Shinyanga, alipokuwa akiondoka ofisi za chama hicho wilaya ya Shinyanga mjini mara baada ya kupata wana CCM wa kumdhamini baada ya kuchukua fomu kuomba CCM imteue kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa.
Furaha ya kumuona Mh. Lowassa, ilitawala ukumbi mzima.
Wananchi wa mkoa wa Shinyanga, wakisukumana ili wapiti kumuona Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, alkipokuwa akiwasili kwenye ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015, ili kuomba wanachama wenzake wa chama hicho wamdhamini kufuatia kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa na chama hicho, kuwania urais wa Tanzania Oktoba 25, 2015.




Wana CCM walkiofika kumdhamini Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, wakishangilia wakati akiingia ukumbi wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa
Wana CCM walkiofika kumdhamini Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, wakishangilia wakati akiingia ukumbi wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini Juni 11, 2015. Lowassa amabaye yuko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini, alivunja rekodi ya kupatya wadhamini 7,114, idadi kubwa hadi sasa.

TIMU YA MUCOBA FC MABINGWA WA FAINALI YA KOMBE LA MUUNGANO MUFINDI 2015,MRATIBU ATANGAZA KUSTAAFU RASMI.

$
0
0

Mkuu  wa  wilaya ya Mufindi Mboni Mhita katikati  akiwa katika picha ya pamoja na   mabingwa wa mashindano ya  kombe la Muungano Mufindi timu ya Mucoba Fc ,wa kwanza kulia ni mratibu wa mashindano hayo aliyestaafu rasmi Daud Yassin na mdau mkubwa wa  soka mkoa wa Iringa Feisal Asas.

Mkuu wa wilaya ya  Mufindi Mboni Mhita  akikabidhi kombe kwa mabingwa  timu ya MUcoba FC
Mkuu wa wilaya ya  Mufindi Mboni Mhita  akikabidhi kombe kwa mabingwa  timu ya MUcoba FC
Na  MatukiodaimaBlog 
MASHINDANO  ya  kombe la  Muungano Mufindi yamefikia tamati baada ya  timu ya benki ya  wananchi wilaya ya  Mufindi  (MUCOBA FC) kuibukwa mabingwa  wa  fainali ya mashindano hayo kwa kuigagadua (kuifunga) timu ya Academ kutoka Dodoma kwa  jumla ya magoli 2-0

 Huku  mratibu  wa mashindano  hayo  Daud Yassin akitangaza  kustaafu  rasmi nafasi  yake  hiyo   baada ya  kuitumikia kwa miaka 19  hivi  sasa .


Mratibu  huyo  aliweza  kuwaaga rasmi  wapenzi wa mpira wa miguu katika wilaya ya  Mufindi mkoani Iringa baada ya  kumalizika kwa mchezo huo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa  wa  shule ya msingi wambi mjini Mafinga


. Yassin aliwashukuru  wadau  wote wa soka  waliomsaidia kwa namna moja  au nyingine kwa  miaka  19  aliyoratibu  mashindano  hayo.

 Alisema pia anawashukuru  viongozi mbalimbali, chama cha soka  wilaya ya Mufindi, chama cha soka mkoa wa lringa, shirikisho la soka nchi TFF, na ZFA kwa  kuonyesha ukaribu  wao kwa  kipindi  chote cha mashindano  hayo .

Pia  aliwaomba  radhi wadau  wote  ambao walikwazika kwa utendaji  wake endapo alikosea  katika utendaji wake na kuwa haikuwa makusudi  yake  kuwakwaza .

Amesema  kwa sasa hatajihusisha  na mambo ya soka  tena katika  wilaya  hiyo kwani kazi  aliyoifanya kwa  kipindi cha miaka  hiyo 19  ni  kubwa na wilaya ya  Mufindi na mkoa wa Iringa umetangazwa  zaidi  kupitia mashindano  hayo .

" Nimejifunza mengi mwaka huu mambo yalikuwa magum sana japo anawashukuru  wale waliomsaidia kufanikisha na kuwa atawaandikia rasmi kuwashukuru.....Wakiwemo  viongozi wa kisiasa mbunge  wa kaskazini  Mahamudu Mgimwa na mjumbe wa NEC na mwenyekiti  wa UWT wilaya ya Mufindi Marcelina Mkini  kwa  kumsaidia  kufanikisha mashindano hayo kwa  mwaka huu "

Mgeni  rasmi katika fainali  hiyo mkuu  wa  wilaya ya  Mufindi Mboni Mhita  mbali ya  kumshukuru mratibu  huyo wa kombe la Muungano Mufindi  ,Yassin  pia alipongeza  wadau  wote  ambao  wameyafikisha hapo mashindano  hayo na kuwa  wilaya ya Mufindi  imeweza  kutangazwa  vilivyo kupitia  soka .

Hivyo aliwataka  wadau wa soka  wilaya ya  Mufindi  kuangalia  uwezekano  wa  kuendeleza mashindano  hayo  baada ya  mratibu  wake  kustaafu  rasmi na kuwa  akiwa  mkuu wa wilaya  hiyo atahakikisha mashindano hayo yanaendelea  japo  ushauri  wa mratibu  huyo  utaendelea  kuhitajika  zaidi.


 Katika  mashindano  hayo mshindi  wa kwanza  timu ya Mucoba Fc  ilipata  zaiwa ya kombe  kubwa , pesa taslim kiasi cha Tsh  milioni 5 ,jezi  seti  nne na medali ,wakati mshindi  wa pili Dodoma Academ ikipata  kiasi cha Tsh milioni 2.5 ,seti tatu za  jezi  pamoja na medali  wakati mchezaji  bora  akipata kiasi  cha Tsh 500,000
Mratibu  wa kombe la Muungano Mufindi Daud Yassin akitangaza  kustaafu   nafasi yake hiyo
Mabingwa wa mashindano ya  kombe la Mungano Mufindi.
washindi  wa  pili wa mashindano ya  kombe la Muungano Mufindi timu ya Dodoma Academ  wakipita kuvishwa medali na Feisal Asas.

Mwalimu  wa  timu ya Mabingwa  wa fainali ya Muungano Cup akipongezwa

BAYPORT YASOGEZA MBELE OFA YA VIWANJA VYA MIKOPO VIKURUTI.

$
0
0

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

TAASISI ya Kifedha ya Bayport Financial Services inayojihusisha na mambo ya mikopo imesogeza mbele huduma yao mpya ya mikopo ya viwanja vilivyopo Vikukuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani kwa ajili ya kutoa fursa zaidi ya Watanzania kupata viwanja hivyo vilivyopimwa.

Awali ofa ya huduma hiyo ilipangwa kumalizika Juni 10 mwaka huu, lakini sasa imepelekwa mbele hadi Juni 30, ikiwa ni ongezeko la siku 20 zaidi kama njia ya kuhakikisha kwamba wale wenye nia hiyo wanafanikisha ndoto zao za kumiliki viwanja.

Akizungumza leo mchana jijini Dar es Salaam, Meneja Biashara wa Bayport Financial Services, Thabit Mndeme, alisema kwamba wamekuwa wakipokea maombi mengi kutoka kwa Watanzania wenye uhitaji wa viwanja hivyo, jambo lililowafanya wakae na kuona namna gani wataongeza siku chache kwa wananchi na wateja wao. Alisema kama ilivyokuwa mwanzo, wateja wao watalazimika kuchukua fomu za maombi ya mikopo ya viwanja hivyo katika ofisi yoyote ya Bayport, bila kusahau wakala wao ambayo ni tawi lolote la Bank of Africa (BOA), huku akitakiwa kulipa malipo ya awali kuanzia Sh 150,000.

“Kama ilivyokuwa mwanzo, mara baada ya mteja wetu kuchukua fomu na kulipa Sh 150,000 kwa kupitia benki ya BOA, ataleta nyaraka zake kwetu na atapatiwa kiwanja chake, huku gharama za kiwanja cha chini kabisa ni Sh 1,400,000, ambapo Bayport itamlipia gharama zilizosalia, huku akilazimika kulipia Sh 105,181 kwa mwezi kwa kipindi cha miezi 24,” alisema Mndeme.

Naye Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, alisema kwamba huduma yao ni muhimu kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni binafsi na wajasiriamali ambao wote kwa pamoja wanachotakiwa kufanya ni kuchukua fomu na kuchagua viwanja watakavyo, kutoka kwenye mradi huo wenye viwanja 1878, huku pia mteja akiweza kupata kiwanja kwa fedha taslimu ya kuanzia Sh 1,400,000 na kuendelea.

“Viwanja hivyo vina uwezo wa kujengwa nyumba za kupanga na kupangisha, hoteli na maduka, vituo vya elimu na ibada, hospitali na kumbi mbalimbali, huku mradi wa umeme na maji vikiwa vinapatikana ndani ya mradi huo ambao ni kilomita 50 kutoka Kisutu jijini Dar es Salaam na kilomita 6.5 kutoka barabara Kuu ya Morogoro,” alisema Cheyo.

Kwa wateja wa malipo ya fedha taslimu, mara baada ya mtu kulipa malipo ya awali katika akaunti ya Bayport iliyopo Bank of Africa (BOA) na kukabidhi nakala ya malipo na fomu za maombi kwa wakala au ofisi ya Bayport, mteja atatengewa eneo kutokana na maombi yake na kuombwa kumalizia kiasi kilichosalia, huku hati ya umiliki wa kiwanja akiipata ndani ya siku 90 baada ya kumaliza malipo yake, na wanaotaka kupata viwanja kwa njia ya mkopo kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni binafsi na wajasiriamali, wakipata hati zao baada ya kumaliza mkopo wao.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, kushoto, akizungumza jambo baada ya kutangaza kusogeza mbele huduma ya mikopo ya viwanja vya Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani, ambapo sasa huduma hiyo imepelekwa mbele hadi Juni 30, mwaka huu. Picha na Mpiga Picha wetu.

Meneja Biashara wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, Thabit Mndeme, kulia akizungumza jambo baada ya kutangaza kusogeza mbele huduma ya mikopo ya viwanja vya Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani, ambapo sasa huduma hiyo imepelekwa mbele hadi Juni 30, mwaka huu. Picha na Mpiga Picha wetu.

MATUKIO BUNGENI MJINI DODOMA,JUNI 11,2015

$
0
0
1
Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anna Makinda (Mb) akiendesha kikao cha Bunge la bajeti Mjini Dodoma,juni 11,2015
2
Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda (Mb, kulia) akisalimiana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mhe. Dkt. Mary Nagu (Mb) baada ya kuwasili katika kikao cha Bunge, Dodoma.
3
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe. Celina Kombani (Mb) akijibu swali lililoulizwa leo Bungeni Dodoma na Mhe. Sylvestry Koka (Mb), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kuimarisha mfuko wa elimu ulioanzishwa katika Halimashauri na Wilaya kwa lengo la kuboresha elimu.
4
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Dkt. Festus Limbu (Mb), akiwasilisha leo Bungeni Dodoma, majumuisho ya uchambuzi wa hoja mbalimbali zilizowasilishwa kwenye kamati yake na kamati za kisekta kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2014/15 na makadirio ya mwaka 2015/16.
5
Mbunge wa Lindi Mjini, Mhe. Salum Khalfan Barwany akimuuliza swali Waziri wa Nishati na Madini, Bungeni Dodoma leo, wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

PATO LA TAIFA LAENDELEA KUKUA KWA ASILIMIA 7 NA KUFIKIA SHILINGI TRILLION 79.4 -MHE. DKT MARY NAGU

$
0
0
Na Georgina Misama -MAELEZO Dodoma
Katika mwaka wa 2014 pato la taifa limeendelea kukua kwa wastani wa asilimia7 na kufikia shilingi trillion 79.4 ikiwa ni wastani wa pato la kila mtu la shilingi 1,724,416 sawa na dola za Kimarekani 1,038 kwa mwaka.
Haya yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu Mhe. Dkt Mary Nagu (Mb) alipowasilisha taarifa ya hali ya uchumi kwa mwaka 2014 na mpango wa maendeleo ya Taifa kwa mwaka wa fedha 2015/16 leo Bungeni Dodoma.
Mhe. Nagu amesema kuwa, hili ni ongezeko la shilingi trillion 8.5 kutoka shilingi trillion 70.9 ya mwaka 2013 ambapo wastani wa pato la kila mtu lilikuwa shilingi milioni 1,582,797 sawa na dola 948.
Amesema ongezeko hilo limechangiwa na ukuaji katika sekta ya ujenzi (18.1%), usafirishaji na uhifadhi wa mizigo (12.5%), Fedha na Bima (10.8%), na Biashara na matengenezo (10%).
Mhe. Nagu amesema ukuaji wa shughuli za uchumi za kilimo ambazo zinajumuisha mazao, ufugaji, misitu na uvuvi ulichangia aslimia 3.4 ikiwa umeongezeka kidogo kutoka asilimia 3.2 mwaka 2013.
Amesema kuwa tathimini ya mchango wa shughuli mbalimbali za kiuchumi kwa mwaka 2014 unaonyesha sekta ya huduma ndio inayochangia sehemu kubwa ya pato la Taifa (41.3%), kilimo (28.9), viwanda (21.7%) na uzalishaji wa bidhaa za viwandani (5.6%).
Aidha, thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi iliongezeka kwa asilimia 2.8 toka dola 8,459.7 mwaka 2013 hadi dola milioni 8,769..3, hata hivyo, thamani ya bidhaa zilizoagizwa kutoka nje ya nchi ilifikia dola milioni 13,623.2 hivyo kusababisha urari wa biashara na huduma katika mwaka 2014 kuwa na nakisi ya dola milioni 4,853.9. Pia, akiba ya fedha za kigeni ilipungua kutoka dola milioni 4,676.2 kwa kipindi kilichoishia Desemba 2013 hadi dola 4,383.6 Desemba 2014. Akiba hiyo imeendelea kupungua hadi dola 4,064.8 mwezi Machi, 2015. Mhe. Nagu amebainisha kuwa deni la Taifa limekua na kufikia dola bilioni 19.8 Machi 2015 kutoka dola bilioni 18.67 Machi 2014. 
Amesema kwa mwaka wa fedha 2015/16 masuala muhimu yatakayo zingatiwa katika mpango wa maendeleo ni, kukamilisha miradi inayoendelea, hususani ile ya Matokea Makubwa Sasa, kuhakikisha usalama wa chakula nchini na kuboresha mazingira ya biashara na uwezeshaji. Masuala mengine yatakayozingatiwa ni kupanua fursa za ajira, kuendeleza rasilimali watu hususani katika Nyanja ya mafuta na gesi, sayansi, ubunifu, teknolojia na maabara na kukabiliana na athari za mabadoliko ya tabia nchi.
Mhe. Nagu amesema kuwa makadirio ya mahitaji ya fedha za kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa mwaka 2015/16 ni shilingi bilioni 5,979.7 ambapo shilingi bilioni 4,317.5 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 1,662.2 ni fedha za nje.

HATIMAYE WASANII WAHAMIA KIJIJINI

$
0
0
1
Katibu wa SHIWATA, Selemani Pembe (Kushoto) akisaidiana na wasanii kuingia vyombo kwenye gari la mizigo ya wasanii waliohamia kijiji cha Mwanzega, Mkuranga.2
Baadhi ya wasanii wakielekea kulima eneo la makazi waliyofikia katika kijiji cha wasanii Mwanzega, Mkuranga jana kwa ajili ya maandalizi ya kuanza maisha mapya ya kijijini.
3
Gari aina ya pick Up likiwa limesheheni magodoro, majembe, ndoo, na mabegi ya nguo za wasanii wakiondoka jijini Dar es Salaam jana kwenda kuanza maisha mapya kijiji cha wasanii Mwanzega Mkuranga.
4
Mmoja wa wasaniii Bibi Mrangi akisafisha vyombo na wenzake wakiandaa vitafunio vya chai katika kijiji cha Mwanzega Mkuranga jana.
Na Peter Mwenda
WASANIII 21 kati ya 50 walioamua kwenda kuanza maisha mapya katika kijiji cha Wasanii Mwanzega, Mkuranga wamehamia.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA), Cassim Taaalib akiongoza msafara huo jana alisema kundi la kwanza la wasanii limehamia na jingine litafuata baada ya mwezi mmoja.
Alisema wasanii hao ambao watakuwa na jukumu la kufanya mazoezi ya kuigiza filamu na tamthilia pia watakuwa wanapata mafunzo ya kilimo cha bustani na kufanya mazoezi ya michezo mbalimbali ya soka, netiboli, basketi na michezo mingine.
Mwenyekiti Taalib alisema wasanii hao watakuwa wanapata masomo ya darasani ya kilimo kwanza na tayari SHIWATA imeandaa wataalamu kwa ajili ya kutoa mafunzo hayo.
Wakiwa kambini hapo wasanii hao walisema hawaamini kama SHIWATA inaweza kutumia gharama kubwa kuwaandalia makazi mapya kwa ajili ya kutafuta maisha yao ya baadaye kupitia kilimo na kutumia vipaji vyao kukuza sanaa.
Mmoja wa wasanii hao, Yolanda Mussa alisema SHIWATA imeonesha njia ya kukomboa wasanii wake kwa njia ya kujitegemea hivyo anaiomba Serikali nayo iunge mkono na kuwapa nguvu taasisi hiyo ili kukiimarisha kijiji hicho ambacho baadaye kitakuwa chenye thamani kubwa kwa watanzania.
Kundi jingine la wasanii 30 wanatarajiwa kuandoka mwezi ujao baada ya kumaliza mafunzo yao ya sanaa na kilimo kwanza.

TASAF yazindua Miradi ya kupunguza umaskini Njombe

$
0
0
Halmashauri 13 za Mikoa ya Njombe na Arusha zinaanza kunufaika na miradi ya kupunguza Umaskini ya OPEC Awamu ya tatu kwa Watu takribani Milioni 3.1 utakaotekelezwa kwa Miaka Mitatu kati ya January 2015 na Desemba 2017.

Hayo yameelezwa mapema leo hii na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, IKULU  bwana Peter Ilomo wakati akizindua kikao kazi cha kuanza kwa Viongozi na Watendaji  wa Mkoa Njombe juu ya utekelezaji wa miradi hiyo ya kupunguza umaskini kwa ufadhili wa OPEC awamu ya tatu. Bw. Ilomo amesema kuwa Lengo la utekelzaji wa miradi hiyo ni Kuboresha upatikanaji wa huduma za kiuchumi na Kijamii kwa Kaya Maskini zilizotambuliwa na kuandikishwa katika Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika Halmashauri huzo.

Aidha Bwana Ilomo amesema kuwa katika  mradi huo jamii zitatekeleza miradi ya elimu, afya na maji pale patakapoonekana pana upungufu wa huduma hizo . Nae Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF amezitaja Halmashauri zitakazohusika kwa katika Mikoa hiyo kuwa ni Ludewa, Makete, Njombe, Wanging'ombe na Halmahshauri za Mji Makambako na Njombe ambazo zote ni za Mkoa wa Njombe na akazitaja za Mkoa wa Arusha  kuwa ni Longido, Monduli, Ngorongoro, Arusha, Meru, Karatu na Halmashauri ya Jiji la Arusha.

Pamoja na miradi ya kupunguza umaskini ya OPEC, TASAF pia inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika halmashauri zote nchini ikiwa ni pamoja na Unguja na Pemba na tayari. Zifuatazo ni picha za matukio mbalimbali katika kukao hicho.
Mkurugenzi mtendaji wa TASAF akitoa maelezo ya utangulizi juu ya miradi ya kupunguza umasikini ya OPEC awamu ya tatu.
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo akizindua mkutano wa kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya kupunguza umasikini ya OPEC awamu ya tatu Mjini Njombe leo.
Kaimu mkuu wa Mkoa wa Njombe ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba akielezea hali halisi ya utekelezaji wa  shughuli za TASAF katika mkoa wa Njombe.
Meneja wa miundombinu mhandisi Elisifa kinasha akielezea madhumuni ya mkutano wa TASAF awamu ya tatu.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kazi wakisikiliza na kunukuu hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo toka kwa katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu bw.Peter Ilomo (Hayupo pichani).

Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kazi wakisikiliza na kunukuu hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo toka kwa katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu bw. Peter  Ilomo (Hayupo pichani).
Meneja wa fedha Bw.Godwinne Mkisi akitoa mada juu ya uratibu wa kutuma fedha.
Afisa wa uratibu toka TASAF bw.Quintus Kassese  akiwasilsha mada juu ya mpango wa kunusuru kaya masikini.
Mtendaji Toka TASAF Beatrice Mbyallu akiwa na Baadhi ya Watendaji wa TASAF  wakifuatilia kwa makini michango ya washiriki
Katibu mkuu ofisi ya Rais Ikulu Peter Ilomo (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa kazi kutoka Halmashauri za mkoa wa Njombe

MWAMNYANGE AZINDUA BARAZA LA USHAURI TCAA

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Monica Mwamyange akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Ushauri wa Watumiaji wa Huduma ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA-CCC) na semina ya wadau wa usafiri wa anga Dar es Salaam leo.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Monica Mwamyange akimkabidhi zawadi Mwenyekiti wa Baraza  la Ushauri wa Watumiaji wa Huduma ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA-CCC, Shaban Mtambalike wakati wa uzinduzi wa baraza hilo la nne tangu kuanzishwa kwake. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri wa Watumiaji wa Huduma ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA-CCC), Hamza Johari akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi huo. 


 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu-Wizara ya Uchukuzi, Monica Mwamnyange (walioketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza hilo na wadau wa Sekta ya usafiri wa Anga.
****************
Na Father Kidevu Blog
USHINDANI mdogo katika utoaji wa huduma za usafiri wa anga kutokana na kuwepo kwa mashirika machache ya ndege yanayotoa huduma nchini.

Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na  Katibu Mtendaji wa baraza la Ushauri wa Watumiaji wa Huduma ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA-CCC), Hamza Johari wakati wa uzinduzi wa baraza hilo na semina kwa wadau wa usafiri wa anga nchini.

Johari alisema endapo kama nchini kungekuwa na watoa huduma wengi wa usafiri wa anga basi kungepelekea kushuka kwa gharama za usafiri na kuwepo kwa huduma bora miongoni mwao.

“Siku zote tunaamiani kama ushindani wa kutosha gharama zinakwenda chini, huduma zinakuwa bora, na ni mdogo kwasababu soko na miundominu haijaweza kutandaa nchi nzima, ”alisema Johari.

Aidha Johari alisema pindi nchi itakapokuwa na miundombinu bora ya viwanja vya ndege, na utaratibu mzuri wa huduma za anga nchini anaamini huduma zitaboreka zaidi.

Mapema akifungua baraza hilo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Monica Mwamunyange amewataka kuwa karibu na wadau wa sekta ya usafiri wa anga nchini ili kuweza kutoa huduma bora na zenye ufanisi nchini.

Mwamunyange alisemwa ipo haja ya baraza kulifanyia kazi dhana ya ushirikishwaji na utoaji wa elimu kwa walaji kuwa ya vitendo zaidi.

“ Baraza linatakiwa kuwashirikisha wadau wake katika mambo mbalimbali yanayoendelea katika seklta nzima ya usafiri wa anga lakini pia wanapaswa kutoa elimu ya mara kwa mara ya haki na wajibu wa mlaji,”alisema Mwamunyange.

Baraza lina takiwa kuangalia maslahi ya mtumiaji wa huduma za usafiri wa anga na kutoa elimu ambayo itamfanya mlaji awe na uwelewa wa kutosha wa huduma za anga.

Aidha Mwamunyange amesema kwa sasa huduma za usafiri wa anga nchini zinakabiliwa na changamoto kutoka kwa walaji ambapo wanashindwa kutofautisha huduma zitolewazo na mashirika yatuayo huduma za gharama nafuu nay ale yaliyozoeleka.

Wadau wa usafiri wa anga pia walipata fursa ya kushiriki semina baada ya uzinduzi huo na mada mbalimbali zilijadiliwa ikiwa ni pamoja na huduma kwa wateja, uwajibikaji wa mtoa huduma anaposababisha madhara, ndege za bei nafuu na masuala ya usalama.

Uzinduzi wa baraza hilo la nne la Ushauri wa Watumiaji wa Huduma ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA-CCC), baada ya kuteuliwa na Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta ambapo pia wajumbe wa Baraza lililopita waliagwa.

Makamba Avunja rekodi ya mapokezi na wadhamini mkoani Iringa

$
0
0

Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM,Mh. January Makamba akiagana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Bi Jesca Mambatavangu mara baada ya January kusaini kitabu cha wageni katika ofisi za Chama.
Mh. January Makamba akikabidhiwa fomu yenye majina ya wanachama waliomdamini na Mwenyekiti wa CCM wilya, Abeid Kiponza. Fomu hiyo in idadi ywa wanachama 630 waliojitokeza kumdhamini ikiwa ni kutoka wilaya ya Iringa Mjini na Kilolo.
Mh. January Makamba akihutubia wananchi na wanachama wa CCM wilaya ya Iringa Mjini walijitokeza kumsapoti na kumdhamini. January amepata sahihi 630 za wanachama wa CCM kumdhamini, idadi hiyo ni ya wilaya ya Iringa Mjini na wilaya ya Kilolo. 

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

JARIDA LA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TOLEO LA 71

Dkt Shein KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO W AFRIKA

$
0
0
Na Miza Kona na Rahma Khamis Maelezo Zanzibar              

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yatakazofanyika Jumamosi ijayo katika Uwanja wa Amani Zanzibar.

Maadhimisho hayo yataambatana mashindano ya mbio za  Marathon ambazo zitawashirikisha bega kwa bega na familia ambapo ni watoto wa kike na kiume, baba na mama ili kuonesha malezi bora katika familia.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi na Utumishi Mhe. Haroun Ali Suleiman kwa niaba ya Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii Vijana. Wawake na Watoto Mhe. Zainab Omar Moh’d wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko katika Ofisi hiyo Mwanakwerekwe.

Amesema mbio hizo zimeandaliwa kusheherekea mafanikio yaliyopatikana katika kupunguza vifo vya watoto nchini pamoja na mashirikiano ya  wazee na jamiii katika kumlinda na kumlea mtoto katika mazingira bora.

Amefahamisha kuwa madhumuni ya sherehe hizo ni kuunga mkono juhudi za kimataifa za kuhakikisha kwamba watoto wanapata nafasi ya kuwa hai na kuishi na afya bora.

Aidha ameeleza kuwa takwimu zinaonesha kuwa idadi ya watoto wanaokufa ulimwenguni chini ya miaka mitano imepungua karibu nusu kutoka mwaka 1990  watoto  milioni 12 hadi kufikia 2012 ni watoto milioni 6.6

Nae Balozi wa Save the Children Suleiman Nyambui amesema mbio zitawashirikisha zaidi ya watoto na wazee zaidi 70 ambapo watakimbia mita 400 kwa kupokezana kila baada ya mita mia moja 100.

Mbio hizo zimeandaliwa na Save the Children International pamoja na Wizara ya Uwezeshaji Ustawi wa Jamii Vijana, Wanawake na Watoto ambapo kilele cha sherehe hizo zitakuwa tarehe 16 Juni huko katika viwanja vya Maisara Unguja.

CHUMBA CHA HABARI CHA GAZETI LA JAMBO LEO NA STAA SPOTI CHAZIZIMA KWA HUZUNI BAADA YA KUFIWA NA MENEJA WAO MZEE RAMADHANI KIBANIKE

$
0
0

 Marehemu  Ramadhani Kibanike enzi za uhai wake.
Mwanahabari Grace Gurisha akisaidiwa na wenzake baada ya kuishiwa nguvu muda mfupi baada ya kupata taarifa hizo za kifo cha Meneja  Ramadhani Kibanike.

Na Dotto Mwaibale


KAMPUNI ya JL Comunications inayochapisha magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti, imepata pigo baada ya aliyekuwa Meneja wake Mkuu Ramadhani Kibanike kufariki.


Kibanike amefariki dunia leo mchana nyumbani kwake Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mrefu.


Akitoa taarifa ya kifo hicho kwa wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Theophil Makunga alisema Kibanike alikumbwa na mauti leo mchana.


Taarifa hiyo ambayo iliwashtua wafanyakazi wa Kampuni hiyo na hata kupelekea baadhi yao kupoteza fahamu, ilisababisha pia kusimama kwa muda kwa shughuli za Kampuni hiyo.



Mipango ya mazishi bado inapangwa, na msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata Jijini Dar es Salaam. 

 Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Julian Msacky na Mwandishi wa Habari, Stela Kessy (kulia), wakiendelea na kazi huku wakiwa na hudhuni baada ya kupokea taarifa ya kifo cha Kibanike leo jioni.
 Mwanahabari Celina Mathew akilia kwa uchungu baada ya kupokea taarifa hiyo.
 Ofisa Matangazo, Kinai akiwa amepigwa butwaa kutokana na  kifo hicho.
 Wanahabari Nyendo Mohamed (katikati), Edith Msuya (kulia) na  Magendela Hamisi wakiwa katika hali ya huzuni kufuatia kifo hicho.
 Mwanahabari Magendela Hamisi akitafakari juu ya kifo hicho.
 Msanifu kurasa wa gazeti la Jambo Leo, Elizabeth Mkeleja alishindwa kujizuia kulia.
 Dereva wa Ramadhani Kibanike akiwa katika huzuni baada ya kupokea taarifa ya kifo hicho.
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com- simu namba 0712-727062)

BALOZI DKT. DIODORUS BUBERWA MGENI RASMI KATIKA UTOWAJI WA ZAWADI KWA WASHINDI WA ‘NA MIMI NIPO- ONLINE ARTS & SCIENCE COMPETITION LILILO ANDALIWA NA FASDO.

$
0
0
Shirika la FASDO (Faru Arts and Sports Develepment Organization) leo hii limetoa zawadi kwa washindi wa shindano la Na Mimi Nipo- Online Arts and Science Competition katika ukumbi wa  kituo cha utamaduni cha Urusi nchini (Russian Tanzania Cultural Center).

Shindano hilo linalohusisha vipaji vya uchoraji, sanaa za mikono na ubunifu wa kisayansi lililozinduliwa mwezi Februari mwaka huu kwa lengo la kutambua vipaji vya vijana wenye umri kati ya miaka 12 hadi 24 limefikia kilele chake leo hii kwa kuwapata washindi sita, wawiliwawili kutoka katika fani za Uchoraji, Sanaa za Mikono na Ubunifu wa Kisayansi. 

Zoezi la kutoa zawadi kwa washindi hao lilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa, Mkurugenzi wa Kituo cha utamaduni cha Urusi nchini hapa, Alexander Tsykunov na wageni waalikwa.

Akizungumza na washiriki pamoja na wageni waalikwa katika Sherehe hizo Balozi wa Tanzania Nchini Ubelgiji aliwapongeza sana vijana kwa kuwa na vipaji vya hali ya juu na kusisitiza kuwa eneo hili la sanaa ya Uchoraji linatakiwa kupewa kipaumbele, aliongeza kuwa Tanzania sasa inatakiwa kuwa na maeneo zaidi kwa ajili ya kukuza sanaa hizi, na katika kuendeleza na kusapoti sanaa , Mh.Balozi Buberwa amechangia Tsh 1,000,000.

Washiriki walikuwa 27 lakini waliopata zawadi walikuwa ni washiriki 6 ambao walizingatia umri kati ya miaka 12 hadi 24 na washindi hao ni pamoja na Thomas Mwakilima, Anhony Tendwa, Primus Mapunda, Philipo Frolian, Cornelio Malya na Anderson Msangi washindi wote wamepata zawadi Dola 300.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa akizungumza wakati wa sherehe hiyo.
Meza Kuu, kuanzia kushoto ni Mratibu Mkuu wa FASDO nchini, Joyce Msigwa,  Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa, Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Urusi nchini, Alexander Tsykunov na mwisho ni Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Tedvan Chande. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Tedvan Chande akizungumza jambo wakati wa sherehe hizo.
Mratibu wa shindano hilo, Joyce Msigwa akizungumza jambo.
Mshereheshaji wa sherehe hizo ambaye pia ni Mratibu Msaidizi, Tunukiwa Daudi akifafanua jambo.
Mzee Nabora Akizungumza Jambo wakati wa Sherehe hizo
Baadhi ya  washindi wakiwa wanakabidhiwa zawadi zao
 Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa akitazama baadhi ya kazi ambazo wamefanya vijana hao.
Burudani ya sanaa ikiendelea.
 Baadhi ya washiriki wachoraji wakiendelea na Mafunzo
 Kushoto ni mwanafunzi kutoka Chuokikuu cha Mzumbe ambaye pia ni mbunifu mavazi akitoa somo kwa baadhi ya washiriki
 Mmoja ya washiriki akiwa anaendelea kuchora wakati wa Sherehe hizo
 Picha ya Pamoja

WASIRA AWAHIMIZA WAKAZI WA MTWARA KUWEKEZA KATIKA UZALISHAJI WA MAZAO YA KILIMO NA UVUVI

$
0
0
 Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira akiongea na baadhi ya wanachama wa CCM mkoani Mtwara alipofika kuomba kudhaminiwa
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira akipokewa na baadhi ya wanachama wa CCM mkoani Mtwara alipofika kuomba kudhaminiwa

Na Woinde Shizza.
WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira,amewahimiza wakazi wa Mtwara kuwekeza katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na uvuvi ikiwa ni sehemu ya shughuli za kiuchumi zitakazowanufaisha kutokana na kugundulika kwa gesi asilia katika ukanda wa kusini mwa nchi.


Wasira ambaye pia ni Mbunge wa Bunda alikuwa akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliomdhamini ili apitishwe na chama hicho kuwania Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.


Alisema ingawa zipo fursa nyingi zitakazowanufaika Watanzania  kutokana na sekta hiyo mpya (gesi), lakini mazao ya kilimo na uvuvi yanaweza kuwa miongoni mwa shughuli zitakazowanufaisha wananchi wengi hasa wa hali ya chini.



Mtwara ni eneo lililowahi kukumbwa na machafuko kutokana na hisia tofauti zilizokuwapo kuhusu manufaa yanayopaswa kuwafikia wakazi wa mkoani Mtwara, hasa kuhusu ujenzi wa viwanda na kuibadili gesi ili itakaposafirishwa isiwe katika mali ghafi.


Hata hivyo, Wasira alisema anatarajia kufungua fursa nyingi zaidi za kiuchumi kwa ajili ya wananchi kama atateuliwa na CCM na hatimaye kushinda katika Uchaguzi huo.


Hakuelezea kwa undani kutokana na kuwa wakati wa kampeni bado haujafika, bali sasa hivi anatafuta udhamini ndani ya CCM.


Wakati huo, Wasira na mtia mwingine, Makongoro Nyerere, wameelezea kuridhika na namna wanavyoshiriki mchakato wa kusaka Urais kwa kutumia magari, tofauti na watia nia waliowekeza fedha nyingi kiasi cha kutumia usafiri wa angani katika maeneo mengi.


Waliyasema hayo walipokutana kwenye ofisi za CCM mkoa wa Mtwara, ambapo Makongoro, alirukaruka na kumkumbatia Wasira. Tukio hilo lilitafsiriwa kuwa ni ishara za umuhimu wa kufanya ushawishi kwa amani pasipo kuiathiri CCM, wanachama ama Watanzania kwa ujuma.


“Hizi ndizo siasa tunazozitaka ndani ya CCM na Tanzania yetyu, sio wagombea wengine wanaotumia utajiri na fedha zao kuwakandamiza wadogo na kuibua mafarakano kwenye jamii,” akasikika kiongozi mmoja wa CCM (jina tunalo) akisema.


Wasira, alikwenda pia katika mkoa wa Lindi ambapo alifadhiliwa. Leo (alhamis) ataelekea mkoani Mwanza kuendelea na ziara ya kuomba udhamini kwa wana-CCM wa mikoa ya kanda ya Ziwa Victoria.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images