Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

AIRTEL YATOSHA YAENDA MIKOANI

$
0
0
Mkurugenzi wa kitengo cha Mauzo Mustapha Kapasi( kushoto) pamoja na Gaspa Mroso waakiongea na wateja wakati wafanyakazi wa Airtel walipotembea wateja wake na kutoa elimu ya huduma zao ikiwemo Airtel Yatosha.
 Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwana Sunil Colaso akiongea na meneja wa Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando  wakati wafanyakazi wa Airtel walipotembea wateja wake na kutoa elimu ya huduma zao ikiwemo Airtel Yatosha inayompa mteja,  Simkadi moja, taifa moja na bei moja.
 Meneja wa kitengo cha network, Emmanuel Luanda akisajili wateja kwenye huduma ya Airtel Yatosha wakati wafanyakazi wa Airtel walipotembea wateja wake na kutoa elimu ya huduma zao ikiwemo Airtel

Yatosha mwishoni mwa wiki hii

 Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwana Sunil Colaso Akibandika moja ya kipeperushi cha Airtel yatosha wakati wafanyakazi wa Airtel walipotembea wateja wake na kutoa elimu ya huduma zao ikiwemo Airtel Yatosha inayompa mteja,  Simkadi moja, taifa moja na bei moja.
Afisa Mauzo wa Airtel bi Theresia Kimaro Akiongea na wateja juu ya huduma ya Airtel yatosha wakati Airtel walioko Magomeni na kutoa elimu juu ya huduma mbalimbali ikiwemo ya Airtel yatosha.

==========  ============  =========
AIRTEL YATOSHA YAENDA MIKOANI


*         Uzinduzi wa huduma Yatosha wafanyika rasmi Mwanza , Kanda ya

ziwa waanza kupiga simu kwa gharama nafuu
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeendelea kusambaza huduma ya
Airtel yatosha katika mikoa mbalimbali nchini baada ya kuzindua huduma
mpya ya punguzo la upigaji simu maarufu kama Airtel YATOSHA  katika
mikoa ya kanda ya ziwa.

Airtel  sasa imeanza kuitambulisha huduma hiyo kwa wadau na wateja
wake katika mikoa mbalimbali nchini ili waweze kunufaika nayo
Huduma ya Airtel Yatosha inamuwezesha  mtumiaji wa mtandao wa Airtel
kupiga simu kwenda mitandao yote kwa gharama ya chini kabisa na hivyo
kutokuwa na haja tena ya kubadilisha kadi ya simu pindi anapohitaji
kuongea na mtu wa mtandao mwingine.

Akionge wakati wa  utambulisho wa huduma ya Airtel Yatosha kwa wadau
wa Airtel jijini Mwanza, Meneja wa kampuni hiyo kanda ya ziwa Ally
Maswanya alisema"  Tumeamua kushusha gharama hizo kutokana na maagizo ya mamlaka ya mawasiliano ambayo iliagiza gharama za simu kushushwa kutoka shilingi 112 kwa dakika hadi shilingi 34.92. 

kwa sasa huduma ya airtel yatosha ina punguzo la hadi asilimia 88 na inalenga kurahisisha mawasiliano kwa wateja wa hali zote kwa kuwawezesha kutumia kiwango kidogo cha fedha kupata muda wa maongezi wa kuanzia dakika 10 kupiga mitandao yote ,meseji bila kikomo na huduma ya internet".

Punguzo hilo la bei linatoa faraja kwa watumiaji wa mtandao huo kwa
kuwa litawawezesha kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho walikuwa
wakikitumia hapo awali. Aliongeza Maswanya.

Akiongea wakati wa halfa ya uzinduzi Mteja wa Airtel na mkazi wa
Mwanza Bi Agness Emmanuel alisema"  Aritel yatosha sasa ndio suluhisho
la mawasiliano ya simu ya bei nafuu, tunashukuru Airtel kwa kutoa
vifurushi vingi na vya bei nafuu vinavyokidhi adha ya sisi wateja.
huduma hii itatuletea urahisi wa mawasiliano bila haja ya kuwa na simu
nyingi na usumbufu wa kuwa na line nyingi. Kwakweli Airtel yatosha
itakuwa ni mkombozi katika mawasiliano.

Kwa upande wake Bwana Brighton Maisel  moja ya wateja waliohudhuria
uzinduzi huo alisema"ni kwa muda mrefu sasa mawasiliano ya simu za
mkononi kwenda mitandao mingine yamekuwa ya gharama za juu hivyo
nashukuru sana serikali kuweka sheria ya kupunguza bei kati ya
mitandaa na Airtel kwa kutii na kuja na Airtel yatosha ambayo sasa
inatuwezesha kuwasiliano kwa bei nafuu na wateja wote wa mitandao ya
simu za mkononi mingine"

Airtel wiki hii pia bado itaendelea kufanya uzinduzi wa huduma hii
katika mikoa ya Morogoro, Mbeya, Arusha, Dodoma ikiwa ni mwendelezo wa
kuwafikia watanzania na kuwaelimisha kuhusu huduma hii ya Airtel
Yatosha Kujiunga na huduma hii mteja anatakia kupiga *149*99#  na kuunganisha moja kwa moja kwenye orodha ya huduma hii na kuchagua kifurushi anachokipenda na kuweza kujipatia dakika za maongezi, ujumbe mfupi na kifurushi cha internet.

Ipo haja ya kurudisha vituo vya kijamii (Community Centres)

$
0
0

Baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii wakiwa katika picha ya pamoja.
Baadhi ya Maafisa Habari kutoka sekta mbalimbali wakiwa kwenye warsha,wakijadiliana na kutafuta  njia   mbadala itakayosababisha wananchi kujua mambo mbalimbali ya kimaendeleo  ya nchi ili kujua hali halisi ya uchumi wa nchi inavyoendelea na mengineyo.

Pichani ni baadhi ya wamiliki wa mitandao ya kijamii wakijadiliana moja ya mada iliyohusu haia ya kurudisha vituo vya kijamii (Community Centres),katika masuala mazima ya kuilemisha na kuifahamisha jamii mambo mbali yakiwemo ya kimaendeleo,Warsha hiyo ilifanyika kwa  kwa hisani kubwa ya kitengo cha mawasiliano cha wizara ya fedha na wanahabri wengine wakiwemo wa mitandao ya kijamii,ambapo mijadala mbali mbali ya jinsi ya kuwasiliana na wananchi wa kawaida   ilikuwa ikijadiliwa.


===========  =========  ========

Ipo haja ya kurudisha vituo vya kijamii ( Community Centres).

Ipo haja ya kurudisha vituo vya kupashana habari vya kijamii(Community

Centres) ili kuboresha utaratibu wa wananchi wa kawaida kupata taarifa
za kimaendeleo kwa wakati muafaka.


Tangu kuondoka kwa utaratibu wa vituo hivi ambavyo vilikuwa vikisaidia
kuwapasha wananchi walio mbali na miji, taarifa mbali mbali kuhusiana na
maendeleo ya nchi, kumekuwa na hali ya sintofahamu zinazopelekea
wananchi hawa kupotoshwa na wanasiasa na kusababisha wananchi hawa
kutokuwa na imani na serikali.

Zamani, wananchi walikuwa wakivitumia vituo hivi ambavyo vilikuwepo
katika kila kata, hata kwa kuangalia tu taarifa za habari na vipindi
mbali mbali vya kimaendeleo, jambo ambalo siku hizi halipo kabisa.

Hii ni moja ya hoja iliyojadiliwa na wamiliki wa mitandao ya kijamii kwa
kushirikiana na kitengo cha mawasiliano cha wizara ya fedha ambapo,
mijadala mbali mbali ya jinsi ya kuwasiliana na wananchi wa kawaida
ilikuwa ikijadiliwa.


Katika Warsha hiyo ya siku ambayo pia ilihudhuriwa na maafisa habari
kutoka sekta mbali mbali za kimaendeleo, wadau walikuwa wakitafuta njia
mbadala itakayosababisha wananchi kujua mambo mbalimbali ya kimaendeleo  
ya nchi ili kujua hali halisi ya uchumi wa nchi inavyoendelea.


Akifungua mjadala, Ingiahedi Mduma, Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano cha  Wizara ya fedha, amesema taarifa za kimaendeleo za nchi ni haki ya kila

mwananchi kujua na ndio maana sasa wameamua kukaa chini na kuumiza
kichwa katika kutaka kujua jinsi ya kuwafikia asilimia kubwa ya
wananchi, mijini na vijijini.

Warsha hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Kilimanjaro Parh Hotel, maeneo
ya Misugusugu, wilayani Kibaha, mkoa wa Pwani ambapo pia mikakati mbali  mbali ya kimaendeleo ilijadiliwa.

KAGASHEKI: TEKELEZENI WAJIBU KWA KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU

$
0
0

                                                  

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Khamis Kagasheki amewataka wafanyakazi wa wizara hiyo kutekeleza wajibu wa kutekeleza kazi kwa ubunifu na uadilifu huku wakizingatia Sheria, Kanuni na taratibu zinazosimamia utendaji kazi. Balozi Kagasheki alitoa rai hiyo wakati akifungua rasmi mkutano wa 20 wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika jijini Dar es Salam.


Mhe. Waziri aliwataka wajumbe wa wajumbe wa baraza hilo kutambua kuwa Baraza ni chombo muhimu kwa ajili ya kuongeza ufanisi na tija katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara.


“Tumieni vema nafasi mlizonazo kuhakikisha kuwa haki na wajibu wa Mwajiri na Mtumishi vinapewa kipaumbele katika utekelezaji wa majukumu yenu kwa kulinga maslahi ya pande zote mbili kwa manufaa ya Taifa zima.


“Moja ya changamoto mliyonayo kama Baraza hili ni kuhakikisha watumishi wanazingatia nidhamu na maadili katika utumishi wa umma.  Ninafahamu mazingira ya kazi na hasa katika vituo vyetu si ya kuridhisha, lakini ni vyema tukahimiza watumishi kufuata kikamilifu Sheria, Kanuni na taratibu za utendaji wa kazi”, anasema Kagasheki.


Anasema wajumbe wakitekeleza wajibu wao  kama Wajumbe wa Baraza, watarahisisha kazi ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara. Aidha, aliwataka katika utekelezaji wa majukumu yeao kuhakikisha wanaimarisha ushirikiano, utendaji kazi kama timu moja kwa uwazi na kuaminiana hususan katika maamuzi yanayohusu wengi.

camera ya jiachie ndani ya heka heka za jiji la Dar live live

makumbusho culture center patakuwa hapatoshi

sheria mkononi:ABOMOLEWA NYUMBA NA KUCHOMEWA VYOMBO VYA NDANI AKIDHANIWA MSHIRIKINA ILEMI MBEYA.

$
0
0

Wananchi wenye hasira kali wakibomoa nyumba ya mama Atupele Kalile akidhaniwa kuwa mchawi maeneo ya ilemi Mbeya.
Wengine wameshaingia ndani na kuanza kutoa vyombo nje tayari kwa kuvichoma
Mtoto wa mama Atupele akijaribu kuokoa vitu vya mama yake visichomwe moto na wanakijiji.
Vyombo vinazidi kutolewa ndani ilivichomwe moto
Tayari wameshaanza kuchoma moto vyombo vya mama Atupele
Mwingine anaendelea kubomoa nyumba ya mama Atupele
KWA PICHA ZAIDI BOFYA MBEYA YETU BLOG. Jiachie Blog inalaani  kwa udi na uvumba tukio hili na mengineyo ya namna hii ya kujichukulia sheria mkononi .

Exim Bank launches mobile banking service

$
0
0

Exim Bank Tanzania Managing Director Anthony Grant
======  =============  =======
Exim Bank launches mobile banking service.

EXIM Bank, Tanzania’s sixth largest bank in terms of total deposits and assets has launched its mobile banking service that will enable the bank’s customers access their accounts via mobile phones.

A statement issued by the Exim Bank Tanzania Managing Director Anthony Grant in Dar es Salaam yesterday said the launch of the bank’s mobile banking service marks the bank’s ongoing commitment to meet the customer’s needs for instant and straightforward access to their finances.

Grant said the mobile banking service will allow customers to access their bank accounts details, make instant transfer of funds between own accounts or to any registered third party beneficiaries and pay registered utility bills and credit card bills.    

“Internet and mobile banking services are the primary gateways for information and support for our customers. This new service reaffirms Exim Bank’s commitment to offer stress-free banking and convenience banking services to our customers.

“Technology is quickly changing the way people do business and manage their needs for financial information and control. With this launch, we are thrilled to enable the benefits of anytime, anywhere banking to our clients,” he said. He added that the entry into the mobile market marks another milestone in the bank’s integrated e-commerce platform strategy which raises the bar for an enhanced customer experience.

“This is just start of our journey to deliver an e-mobile solution that will really make a difference to our customers,” he added. He however cautioned the bank’s customers to be cautious with their passwords urging that revelation of their password may lead to theft of their money. Exim Bank earlier this year announced to open two more branches across the country as part of the bank’s aggressive expansion plan aimed at extending services closer to people and to date, the bank boosts the existing branch network of 25 branches across the country

Over 60 delegates from across Tanzania mainland and Zanzibar took part in a Copa Coca-Cola seminar held in Dar today

$
0
0
 Coca-Cola Brand Manager Tanzania Maurice Njowoka delivers his speech at the opening ceremony of the Copa Coca-Cola Directive Seminar held at the National Stadium in Dar es Salaam Tuesday, March 26, 2013.


Tanzania Football Federation (TFF) President Leodegar Tenga emphases a point as he addresses over 60 delegates from across Tanzania at the opening ceremony of the Copa Coca-Cola Directive Seminar held at the National Stadium in Dar es Salaam Tuesday, March 26, 2013.


A section of over 60 delegates from across Tanzania mainland and Zanzibar follow a speech by TFF President Leodegar Tenga at the opening ceremony of the Copa Coca-Cola Directive Seminar held at the National Stadium in Dar es Salaam Tuesday, March 26, 2013.

 Participants to a one-day Copa Coca-Cola directive seminar, including TFF President Leodegar Tenga, take a souvenir picture at the National Stadium in Dar es Salaam Tuesday, March 26, 2013.

==========  ============  ===============

COCA-COLA BRAND MANAGER MAURICE NJOWOKA POINTS AT COPA COCA-COLA DIRECTIVE SEMINAR HELD AT THE NATIONAL STADIUM DAR ES SALAAM, MARCH 26, 2013



I am glad to be here today representing Coca-Cola, the company that sponsors the national youth football championships - Copa Coca-Cola.

§  Ladies and gentlemen, we at Coca-Cola feel proud and satisfied by the achievement that Copa Coca-Cola has brought to the face of the Tanzanian football throughout the period of six years of our partnership with the Tanzania Football Federation.

§  You will all agree with me that Copa Coca-Cola has now become a cradle of football players in Tanzania in such a way that its products are evident at every stage of football competition ranging from the First Division League, the Premier League to the youth and senior national soccer teams.

§  I wish to sincerely thank you regional administrators for your time and dedication to ensure that Copa Coca-Cola runs smoothly every year in your respective. Your commitment is indeed what has helped to position this tournament as a distinguished pillar of soccer development in Tanzania today.

§  As you take part in this seminar, I would like to reemphasise Coca-Cola’s commitment to supporting the youth football tournament which is played not only in Tanzania but in other parts of the continent. Our aim to use this as a platform to facilitate easy identification of football talents and encourage active and healthy lifestyles among the youth. We also understand that football today is one of the means by which young people can be gainfully employed and Coca-Cola is proud to make this contribution.

§  Ladies and gentlemen, beginning this year 2013, Copa Coca-Cola changes the target age group from Under-17 to Under-15 football tournament. The reasons why we have decided to migrate down to the younger age bracket is because we want to reach out to more youthful players as recommended by the World Football Organization (FIFA). Also this event now starts in April and climaxes in September.

§  All other setup and the format of the tournament remains normal; that it is an annual grassroots football competition which starts from district to the national level, involving teams from across Tanzania mainland and Zanzibar.

  • It is our belief that COPA Coca-Cola, and the various sports that we support, such as Sprite Slam Basketball, will continue to draw out the best among the Tanzanian youth, providing them with opportunities to shine at international level. In the past six years, we have witnessed outstanding performance at international level of Copa Coca-Cola Dreams which played alongside other national youth Copa Coca-Cola teams in Brazil (2007/2008) and South Africa (2009/2010/2011/2012).

  • In addition to world-class football exposure, Copa Coca-Cola has a lot more to offer to individual players and teams. Top three teams receive medals, certificates and cash prizes in recognition of their outstanding performances as well as Best Player, Top Scorer, Best Goalkeeper, Best referee and the Most Disciplined Team.

  • Copa Coca-Cola was launched in Tanzania in 2007. However, Coca-Cola’s involvement in football, and sports in general, dates back to 1928 with the sponsorship of the Olympic Games and football since 1930. The Coca-Cola Company has had a formal association with FIFA since 1974 and has been official sponsor of FIFA World Cup since 1978.

  • In closing, I once again take this opportunity to thank each one of you for making time to be here and urge you to continue with the same spirit of excellence.

Ø  The Directive Seminar involving more than 60 delegates from across Tanzania mainland and Zanzibar was officially opened by TFF President Leodegar Tenga and this is what he had to say:


§  Re-emphasized on strict observation of age limit by Regional Football officials.

§  Underlined the importance of Copa Coca-Cola to the development of football in Tanzania such that all youth national teams are now composed of players from Copa Coca-Cola.


§  He said that beginning this year Copa Coca-Cola will also involve girls football teams

§  Urged Coca-Cola to continue supporting this important football property.

§  Upheld the successful partnership between Coca-Cola, TFF and the government for the past six years of Copa Coca-Cola existence in Tanzania. 

waziri Terezya Huvisa awataka wananchi wa jiji la dar kuzingatia usafi wa mazingira

$
0
0

Waziri nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Bibi Terezya Huvisa amewataka wananchi wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake kuzingatia usafi wa mazingira katika maeneo yao. Aliyasema hayo wakati wa ziara ya ukaguzi wa usafi wa mazingira aliyoifanya katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam.

Bibi Huvisa alitembelea barabara ya Morogoro eneo la Magomeni mtaa wa Dosi na Suni ambapo alikagua usafi katika maeneo hayo na kuongea na wananchi swala lazima la kutunza mazingira. Mitaa hiyo imejaa mirundikano ya uchafu hivyo Waziri aliwapa muda wa wiki moja kuhakikisha wamezoa na kutokomeza uchafu wote ambao uanzunguka maeneo yao. Wenyeviti wa mitaa hiyo Ally Bacho na Ally Kondo walimuahidi Waziri kuwa watatekeleza agizo hilo kwa haraka sana kwa kushirikiana na wananchi
wa mitaa yao.

Pia alitembelea eneo la Kimara Baruti sokoni na kuwasisitiza wauzaji wa mahali hapo kuzoa takataka ziliozunguka eneo hilo la soko na kuziondoa mahali hapo. Aliendelea na ziara eneo Kiluvia madukani na Bibi Huvisa alishirikiana na wananchi wa eneo hilo kukusanya, kuzoa taka na kuzichoma taka zote zilizokuwa zimetupwa pemebezoni ya barabara.

Eneo la Kiluvia B kitongoji cha Tanesco Waziri aliongea na wananchi na pia alishirikiana nao kusafisha takataka walizokuwa wametupa katika eneo lao na karibia na barabara. Ziara ya Bibi Huvisa iliishia Ubungo mataa amabapo alizungumza na wafanyabiashara ndogondogo kuhusu usafi na akawaagiza kuanza mara moja usafi wa eneo hili wanalofanyia biashara na yeye atapita kukagua. Katika mtaa wa Mlimani City wafanyabiashara wanaouza viatau pembezoni mwa barabara waliamuriwa kuondoka na Waziri Huvisa kwa sababu eneo hilo wanachafua mazingira.

Katika ziara hiyo Waziri aliongozan ana wataalamu kutoka Baraza la Mazingira Nchini (NEMC), Kamanda wa Polisi wa kikosi cha mazingira nchini Kamishina wa Polisi Mayunga na wataalamu wa mazingira toka ofisi ya Makamu wa Rais.

Na Monica Sapanjo – Afisa habari, Ofisi ya Makamu wa Rais

JK AFUNGA MAFUNZO YA JKT KWA VIONGOZI LEO

$
0
0
Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi mbunge wa viti maalum Ester Bulaya leo katika kambi ya RUVU JKT.Rais Kikwete amefunga rasmi mafunzi hayo leo yaliyofanyika kwa wiki tatu.
Wabunge Halima Mdee na Ester Bulaya pamoja na wenzao wakila kiapo wakati wa kuhitimu mafunzo ya muda mfupi yaliyofanyika katika kambi ya jeshi la Kujenga Taifa Ruvu JKT huko kibaha Mkoani Pwani leo.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe, akipokea cheti cha kuhitimu mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi kutoka kwa kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Muhingo Rweyemamu wakati wakimaliza mafunzo ya JKT, katika Kambi ya Mgambo kikosi cha 835 wilayani Handeni Mkoa wa Tanga. 
Zote za Tanga na Hussein Semdoe.
wakwanza katika mstari wa kushoto ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe anayefuata ni Mbunge wa Kinondoni Iddi Azani, wakiwa kwenye Paredi ya kumaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT Kikosi cha 835 Mgambo JKT kambi iliyopo katika Kata ya Mgambo ilayani Handeni Mkoa wa Tanga.
wakwanza kushoto ni Mbunge wa Kinondoni Iddi Azani pamoja na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ZItto Kabwe, wakihitimu mafunzo ya JKT katika kambi ya 835 Mgambo JKT iliyopo Tarafa ya Mzundu wilayani Handeni Mkoa wa Tanga.
Mbunge wa Kinondoni Iddi Azani, akiapa wakati wa kumaliza mafunzo ya JKT katika Kambi ya 835 ya Mgambo JKT, iliyopo katika Tarafa ya Mzundu wilayani Handeni Mkoa wa Tanga.
Mbunge wa Biharamulo, Dk Athanas Mbassa, akiapa wakati wa kumaliza mafunzo ya JKT katika Kambi ya 835 ya Mgambo JKT, iliyopo katika Tarafa ya Mzundu wilayani Handeni Mkoa wa Tanga. 
Mbunge wa Kiwani Pemba, Abdallah Haji Ali, , akiapa wakati wa kumaliza mafunzo ya JKT katika Kambi ya 835 ya Mgambo JKT, iliyopo katika Tarafa ya Mzundu wilayani Handeni Mkoa wa Tanga.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe, akiapa mbele ya kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Muhingo Rweyemamu, hayupo pichani, wakati wakimaliza mafunzo ya JKT, katika Kambi ya Mgambo kikosi cha 835 wilayani Handeni Mkoa wa Tanga.
Mbunge Viti maalum Raya Khamis , akiapa wakati wa kumaliza mafunzo ya JKT katika Kambi ya 835 ya Mgambo JKT, iliyopo katika Tarafa ya Mzundu wilayani Handeni.
Baadhi ya Wabunge walikuwa wakichukua mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi katika Kambi ya Mgambo kikosi cha 835 wilayani Handeni Mkoa wa Tanga.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na waheshimiwa wabunge waliohitimu mafunzo maalumu ya JKT leo

Mbunge wa Mtera Mh. Livingstone Lusinde 
"Kibajaji"  (wa tatu toka kulia) akipiga kwata leo huko  Ruvu

kumekucha tamasha la pasaka;WAIMBAJI KUTOKA KENYA, DRC WATUA DAR

$
0
0
 Mwimbaji wa nyimbo za injili, Solomon Mukubwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu maandalizi yake katika tamasha la Pasaka 2013.
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Faraja Ntaboba akiimba kwa hisia moja ya nyimbo zake mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati Maalumu inayoratibu tamasha hilo la kimataifa, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu maandalizi ya tamasha hilo.

DAR ES SALAAM, Tanzania

WAKATI muimbaji Sipho Makhabane wa Afrika Kusini akitarajiwa kutua Ijumaa, waimbaji wa nyimbo za injili kutoka Kenya na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wamewasili jana jijini Dar es Salaa, tayari kwa ajili ya kutumbuiza katika Tamasha la Pasaka, litakaloanza Machi 31 kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa Kamati Maalumu inayoratibu tamasha hilo la kimataifa, Alex Msama aliwataja waimbaji waliowasili jana kuwa ni Solomoni Mukubwa (Kenya) na Faraja Ntaboba (DRC).

Msama aliwataka wapenzi, mashabiki na wadau wa muziki wa injili kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo, ambalo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ili kuunga mkono juhudi za kampuni yake kuandaa tamasha hilo kwa malengo mbalimbali ikiwemo kueneza injili ya Mungu na kusaidia makundi maalumu.

Kuhusu waimbaji, Msama alisema kuwa hadi kufikia Ijumaa, wakali wote wa nyimbo za injili kutoka nje watakuwa wamewasili jijini tayari kwa tukio hilo linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa Dar es Salaam na mikoa yote ambayo tamasha huilo litarindima.

Aidha, mkali wa aina hiyo ya muziki kutoka Kenya, Mukubwa, alisema kuwa amejiandaa vya kutosha katika tamasha la mwaka huu ambalo limebeba ujumbe wa Upendo na Amani.

“Wakati wa Uchaguzi wa Nchini Kenya tuliimba na kuhamasisha Amani na Upendo na kwa kupitia tamasha hili tutaimba nyimbo za kuhamasisha Amani na Upendo hapa Tanzania,” alisema Mukubwa. 

Naye mwimbaji kutoka DRC, Ntaboba alisema kuwa, watu wajitokeze kwa wingi katika tamasha hilo na kupata burudani itakayokwenda sambamba na mafundisho ya dini.

Msama aliongeza kuwa idadi ya waimbaji imeongezeka baada ya kujitokeza kwa nyota mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Ntutuma kutoka Kenya, ambapo baada ya tamasha hilo kutikisa kwenye jijini Dar es Salaam, itakuwa zamu ya Dodoma, Iringa, Mbeya, Mwanza kabla ya mashambulizi kuhimishwa mkoani Mara.

Zantel yafungua duka jipya la kuhudumia wateja Muzamil,Zanzibar

$
0
0
 Minister of Tourism, Culture and Sports Hon. Said Ali Mbarouk.  cutting a ribbon to officiate the launch of the dealer shop at Muzamil centre, Zanzibar. Looking is the Director of Next Telecom, Zanzibar Mr. Mohamed Chanja
Zantel’s Zanzibar Commercial Director, Mohamed Mussa (middle)briefs the Minister of Tourism, Culture and Sports Hon. Said Ali Mbarouk (right) on the services offered at the just launched dealer shop. Looking is the Director of Next Telecom, Zanzibar Mr. Mohamed Chanja


Zantel’s Zanzibar Commercial Director, Mohamed Mussa and  Director of Next Telecom, Zanzibar Mr. Mohamed Chanja posing in front of the newly opened shop.


=========   ========  ========


Zantel yafungua duka jipya la kuhudumia wateja Muzamil,Zanzibar


Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel, imefungua duka jipya eneo la Muzamil, mtaa wa Mlandege hapa Zanzibar ikiwa na lengo la kuwarahishia wateja wake huduma pamoja na kuongeza wigo wa huduma kwa wateja.


Ufunguzi wa duka hilo unaenda sambamba na uboreshaji huduma wa kampuni ya Zantel pamoja na kuwezesha wateja wake kupata huduma kama simu, muda wa maongezi, modem pamoja na kadi za simu.

Duka hilo, lililo chini ya Next Telecom, pia litawawezesha wateja wa Zantel kutoa na kuweka pesa zao kupitia huduma ya EzyPesa.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo, ambao pia ulihudhuriwa na meneja wa Mauzo wa Emirates na Precision Air, Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel hapa Zanzibar, Mohamed Mussa, alitoa shukrani za pekee kwa wateja wa mtandao huo kwa kuendelea kutumia huduma zao.


“Kampuni yetu imejikita katika kuhakikisha huduma zetu zinamfikia kila mtu hapa Zanzibar. Hivyo tuna uhakika duka hili litarahisisha sana huduma kwa wakazi wa Mlandege’ alisema Mussa.

Ufunguzi wa duka hilo pia ulihudhuriwa na Waziri wa Utalii, Utamaduni na Michezo hapa Zanzibar, Mheshimiwa Said Ali Mbarouk ambaye aliipongeza Zantel kwa kuwa kampuni kubwa hapa Zanzibar lakini pia kwa kushinda tuzo ya mlipa kodi bora.


 “Duka hili linaashiria namna kampuni ya Zantel ilivyo makini katika kuwapa wateja wake huduma bora na kwa urahisi. Huduma bora kwa wateja ndio msingi mkubwa wa ukuaji wa biashara’ alisema Mheshimiwa Mbarouk.

Mheshimiwa Mbarouk pia aliwaasa Zantel waendelee kutoa huduma bora kwa Wazanzibari huku pia akisisitiza ufunguzi wa maduka mengine ya aina hiyo ili kuwarahishia watuamiaji wengi wa simu.


Duka hilo jipya litakalokuwa likifanya kazi Jumatatu hadi Jumamosi, kuanzia saa tatu hadi saa kumi na moja jioni, linatarajiwa kupunguza msongamano kwenye maduka mengine ya Zantel yaliyopo Darajani, Mfereji wa Wima, Mchangani and Kokoni. 

Rais Kikwete akagua mradi wa ufugaji kuku kambi ya ruvu jk

MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA ILALA MH.JERRY SILAA AZINDUA RASMI ZIARA YA KUTEMBELEA MAKUMBUSHO YA KIHISTORIA KATIKA MANISPAA YA ILALA.

$
0
0

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Muheshimiwa Jerry Silaa akiwakaribisha washiriki wa Miss Utalii Tanzania 2012/13 katika Manispaa ya Ilala.

Washiriki wa Miss Utalii Tanzania 2012/13  Taifa  wakiwa katika Moja ya Kumbukumbu hizo.

kutoka kwa Mdau;Sitapanda tena Precision Air!

$
0
0

Mdau Michuzi, tafadhali naomba uniwekee hii post, usinibanie.  Siku ya Jumamosi (23 Machi 2013) nilikuwa na safari ya kutoka Arusha kurudi Dar es Salaam kwa kutumia usafiri wa ndege wenye ‘jina kubwa’ hapa Tanzania, Precision Air! Kama unavyofahamu, siku hizi wana-flight za moja kwa moja kutokea Arusha Airport kwahiyo nilikuwa sina wasi wa kupanda shuttle mpaka KIA ili kuweza kurudi kwa familia yangu Dar es Salaam.

Mimi na abiria wenzangu tulitakiwa kuondoka Arusha saa 7 na dakika 20, kumbuka tangia saa 4:45 tulikuwa airport kwa kukamilisha utaratibu wa check-in time.  Kwenye saa 6 mchana tuliambiwa tukafanyiwe ukaguzi wa mwisho wa usalama kabla ya kuondoka lakini cha kushangaza baada ya nusu saa kuna mfanyakazi mmoja wa shirika hilo aliyejitokeza  na kwa bila kutumia lugha ya staha alituamrisha kuwa sasa tumebakia na option mbili; kupitia Zanzibar au kusafirishwa hadi KIA nakuwahi ndege inayofuata kuelekea  majumbani kwetu Dar es Salaam. BILA HATA KUTOA SABABU AMA KUTUOMBA RADHI! Abiria tuliwaka kweli kweli! Hapo tumeshachoka, tunanjaa, na hako kajamaa hata hakataki kutusikiliza!

Anyways, Precision Air waliweza kuruhusu abiria kama 10 kupitia Zanzibar – Nairobi – Dar es Salaam (ambayo hata hivyo sijui kama walifika saa ngapi), huku sisi masalia wengine kama 25 hivi tukapandishwa kwenye mkweche wa basi kuelekea KIA (picha nimeambatanisha hapo kwenye email). Hapo hapo sisi tuliopandishwa kwenye hiyo basi iliyochoka na kutoa harufu kweli kweli hatukuambiwa hata hiyo ndege tutakayoenda kuipanda KIA inafika na kuondoka saa ngapi. Ni cha kushangaza sana kwamba mfanyakazi wa Precision Air aliyetuamrisha kwenda KIA alikuwa hana majibu haya!

Ndugu zangu, tumefika KIA bado tukakuta bonge la foleeeeni linatusubiria mpaka kufika ticketing counter! Huku tukiambulia machungu ya safari maana mpaka sasa hakuna mtu aliyetuomba radhi (kumbe makubwa zaidi yalikuwa mbioni kujitokeza)! Tumefika counter kwa nguvu zote ndo tunapewa taarifa kwamba ndege inayofuata inaondoka saa 2 na dakika 20 USIKU! Ambayo nayo ilipata delay mpaka saa 4 zaa USIKU! YAANI NIKAJIKUTA NIMEFIKA NYUMBANI SAA 6 ZA USIKU! UCHOVU, NJAA NA BADO SIJAOMBWA RADHI!!!

Maskini pia kuna wazungu wa watu ambao walikuwa wana International flight hiyo saa 4 usiku nao wakaponzwa na huu uzembe wa Precision Air!!! Embu angalia jinsi ilivyoweza kutzalilisha kitaifa pia!

Jamani wadau, Precision Air sio ndege yakupanda!!! Kama mnasafari zenu ni bora mkachungulie ndege zingine..bahati mbaya ushindani kwetu si sana ndo maana hata hii shirika la ndege inajitia kiburi kiasi hiki!!!

Kwangu mi binafsi sitapanda tena ndege ya Precision Air!! Nikikosa ndege ingine ni bora nikapande basi..ntajipangilia mi muda wangu binafsi wa kufika.

Kama Precision Air hawataweza kujirekebisha ni bora wakaifunga hiyo biashara, maana ni dhahiri kwamba hawaiwezi!

Napenda kuwasilisha.

Mdau.

Askofu Kulola ampa tuzo ya heshima Msama

$
0
0

KANISA la EAGT hivi karibuni lilimtunuku tuzo Mkurugenzi wa makampuni ya Msama Promotions kwa kutambua mchango wake katika uchangiaji wa maendeleo ya jamii.

Akizungumza  baada ya kukabidhi  tuzo hiyo, juzi Askofu Philemon Phiri  wa jimbo la Mikocheni akimwakilisha Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Moses Kulola alisema tuzo hiyo kwa Msama ni utambuzi wa anayoyafanya katika kusaidia jamii.


Askofu Phiri alitumia fursa hiyo kumpongeza Msama kwa  uandaaji wake bora wa matamasha ya Pasaka na kueleza kuwa mungu amempa ufunuo ambao ni endelevu. Naye Msama alishukuru tuzo hiyo na kueleza kwamba tamasha la Pasaka litaendelea kila leo tena kimataifa zaidi hadi duniani.

Katika hatua nyingine mwimbaji nguli wa muziki wa Injili wa Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi nchini Kenya, amesema atatumia tamasha la pasaka kutambulisha wimbo wake  wa Kiti Chako uliopo kwenye albamu yake mpya ya Sifa za Mungu.


Akizungumza na Pata Habari, baada ya kuwasili kutoka nchini Kenya kwa ajili ya kuhudhuria tamasha la pasaka linalotarajiwa kufanyika Jumapili hii katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam alisema, atautambulisha wimbo huo ambao una ujumbe mzito wa neno la mungu.


Kwa mujibu wa Mukubwa albamu yake hiyo ni zaidi ya nyingine alizowahi kurekodi hii kwa sababu ameimba ushuhuda wa maisha yake  baada ya kupata matatizo ya kukatwa  mkono  wake.


“Nashukuru  kupata  tena  nafasi  ya kuwa mmoja wa waimbaji kwenye tamasha la mwaka huu, nimejiandaa vya kutosha mashabiki wafike kwa wingi kupata ujumbe mzito wa neno la mungu pia nitatambulisha wimbo wangu mpya siku hiyo” alisema Mkukubwa.



Alisema albamu yake hiyo inanyimbo saba, ambazo ni Kiti chako, Shukrani ya punda, Nitaishi wakitazama, Habari njema, raha yangu, sijafika, Sifa za mungu, Nimewasamehe wote.


Kwa upande wa Faraja Ntaboba, alisema kauli mbiu ya tamasha la pasaka la mwaka huu inayosema kuwa ‘Amani na Upendo’ imempa moyo sana,  inagusa Afrika nzima kwa kuwa  kuna watu wanalia  kwa kupoteza  amani.


Aidha  mwimbaji  huyo  alitoa  wito  kwa  mashabiki  wa tamasha hilo linalotarajia kufanyika mikoa mitano, kuwa wasisherehekea tu bali waje wakijua amani inatafutwa,  aliahidi kufanya mambo makubwa siku ya Jumapili.


Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31 na litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 Uwanja wa Samora mkoani Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

KING CLASS MAWE ATAMBA KUMGALAGAZA MWAMAKULA MEI MOSI

$
0
0
SUPER D KUSHOTO AKITOA MAELEKEZO KWA KING CLASS

BONDIA 
Ibrahimu  Class 'King Class Mawe' anaendelea kujiandaa  kumkabili Amosi Mwamakula katika pambano la utangulizi wakati wa mchezo wa kati ya Francis Cheka na Thomas Mashali.

Pambono la raundi nane linatarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa PTA Sabasaba, Dar es Salaam Mei Mosi mwaka huu, linatarajiwa kuwa la vuta nikuvute kutokana na kila mmoja kujigamba kujiandaa vema.

Kocha wa King Class Mawe, Rajabu Mhamila 'Super D' alisema kuwa bondia wake anajianaa vema kwa ajili ya  kumchakaza Mwamakula bila ya huruma ili
kuendelea kujiwekea rekodi nzuri.

"Bondia wangu yuko katika maandalizi ya kutosha kuhakikisha anafanya vizuri katika pambano hilo la utangulizi kati ya Cheka na  Mashali" alisema Super D.Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD  za mafunzo ya mchezo  huo zenye mapambano makubwa ya mabondia wa ndani na nje ya nchi.

Aliongeza kuwa baadhi ya mapambano yaliyomo ni katika CD na DVD hizo ni ya Kalama Nyilawila dhidi ya Francis Cheka, Mbwana Matumla na Fransic Miyeyusho, Said Mundi na King Class Mawe. nyingine zitakuwa.



Sipho Makhabane kutua nchini kesho tayari kutumbuiza tamasha la pasaka

$
0
0

MWANAMUZIKI nguli wa muziki wa Injili nchini Afrika Kusini, Sipho Makhabane anatarajia kutua nchini kesho majira ya saa moja usiku akiwa na msafara wa watu 14.

Akizungumza na Pata habari jana, Mkurugenzi wa Msama Promotions ambao ndio waandaaji wa Tamasha la Pasaka, Alex Msama alisema kuwa matayarisho ya kumpokea Sipho yamekamilika na kesho atatua nchini tayari kwa ajili ya kushiriki kwenye tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.


Mbali ya Sipho, Msama alibainisha kuwa mwanamuziki Ephraim Sekeleti kutoka nchini Zambia nae anatarajia kutua nchini kesho.

Mwisho




TIGO BEI MOJA KUPIGA SIMU KWENDA MITANDAO YOTE

$
0
0

Meneja wa Chapa ya Tigo bw. William Mpinga akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya kupiga simu kwenda mitandao yote ndani ya nchi kwa bei moja na punguzo la 20% kupiga nje ya nchi, kushoto kwake Mtaalam wa ofa za bidhaa za Tigo Bi.Jacqueline Nnunduma.

========  ======= =======

ar-es-salaam Tanzania, 27th March 2013: Tigo Tanzania leo imezindua ofa ambayo inatoa nafasi ya kipekee na thamani kubwa sana kwa wateja wake kuweza kupiga simu kwa gharama nafuu zaidi za kiwango kimoja kwenda mitandao mingine ndani ya nchi kufurahia dakika nyingi zaidi za mawasiliano kuliko ilivyokuwa awali.

Pia, ofa hiyo inatoa fursa kwa wateja wa Tigo kupiga simu kwa mitandao mingine nje ya Tanzania kwa punguzo la 20%. Kiwango hicho kimoja cha kupiga simu, baada ya kuwezeshwa, kitamwezesha mteja kupiga simu kwenda mitandao mingine kwa masaa 24 kwa siku saba.

“Tigo inawajali sana wateja wake na inatambua umuhimu wa kuwapatia huduma bora tena kwa gharama nafuu ambayo wataweza kuimudu, na huduma bora ambayo inaendana kabisa na thamani ya fedha zao.

Kwa huduma hii ya upigaji simu kwenda mitandao mingine kwa viwango sawa, wateja wetu wa Tigo wataweza kufurahia kupiga simu kwenda mitandao mingine waipendayo kwa gharama nafuu kabisa; sanjari na kupiga simu nje ya nchi kwa punguzo la 20%..” alifafanua Wiliam Mpinga, Meneja Chapa wa Tigo.

Aliendelea kufafanua kuwa, huduma hiyo pia itakuwa mkombozi mkubwa kwa wateja wote wa Tigo ambao wanafanya biashara mbalimbali ama kufanya kazi na makampuni mbalimbali ambapo itakuwa ni fursa nzuri kwao kuwasiliana na wateja wao ndani na nje ya nchi.

Vile vile huduma hii itawawezesha wateja wetu kuwa na mazungumzo marefu kwa njia ya simu pasipo bughudha ya aina yeyote. Bw. Mpinga aliendelea kufafanua kuwa, “Kwa mara nyingine tena tumetoa nafasi nzuri kwa wateja wetu wa Tigo ambao tunawathamini sana kufurahia uhuru wa kuongea kwa muda mrefu na kwa ghrama nafuu, na tunatoa wito kwa wananchi wengine kujiunga na Tigo ili waweze kunufaika na huduma hii.

Kwa huduma hii ya viwango sawa vya kupiga simu kwenda mitandao mingine, tunaoa fursa kwa wateja wetu kumpigia mtu yeyote anayependa, kwa kumpa uhuru wa kuwasiliana na yeyote anapenda..” Kutumia huduma hii, metja wa Tigo anapaswa kujisajili na huduma ya Time, kisha apige namba *149*90# ambapo atwezeshwa moja kwa moja kujiunga na huduma hiyo kwa wiki nzima.

Breaking News AIRTEL YATOSHAAAAAAAAA Inaendeleaaaaaaa

$
0
0


Another Great Weekend offer from Airtel

To prove that Airtel Yatosha!!!?  Airtel brings India closer to you.
Airtel customers can now make weekend calls to India for ONLY 2/= Tsh per second. Use Tsh 3,000/= to get 25 minutes bundle every Saturday and Sunday and get talking!

Simply SMS the word INDIA to 15022
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images