Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

SHIGONGO AZINDUA VITABU VYAKE VITATU VIPYA KATIKA OFISI ZA GLOBAL

$
0
0
MHAMASISHAJI na mjasiriamali wa kimataifa, Eric James Shigongo, amewaasa Watanzania kutokata tamaa katika kufuatilia ndoto zao huku wakiamini kuwa wao ni watu muhimu katika maisha yao na ya jamii.

Akizungumza na vyombo vya habari mapema leo ndani ya ofisi za Global Publishers zilizoko Mwenge-Bamaga jijini Dar katika uzunduzi maalumu wa vitabu vyake vitatu, Shigongo aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kusoma vitabu ili kupata maarifa mengi ya juu ya mafanikio maishani.

 “Kila mmoja ana ndoto za kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na kuondoka mahali alipo. Wengi hushindwa kupiga hatua za mafanikio maishani kwa sababu nyingi yakiwemo mazingira waliyokulia wakiaminishwa kuwa hawawezi kufanya chochote maishani,  jambo ambalo si la kweli kwani kila mmoja anaweza kufikia ndoto zake akiamua tu kubadili fikra na namna ya kutenda mambo maishani,” alisema Shigongo.

Vitabu vilivyozinduliwa ni ‘Sheria 10 Zilizothibitishwa – Jinsi ya Kutoka Kwenye Umaskini Hadi Mafanikio’, cha pili ni ’10 Proven Secrets – How to Move From Poverty to Success’ na cha tatu ni  ’26 Secrets – How to Defeat Your Enemies and Make Millions of Dollars’.

Uzinduzi wa vitabu hivyo ni kuashiria kwake kuingia rasmi mitaani na kusambazwa kwenye kona mbalimbali ndani na nje ya nchi ambapo vinatarajiwa kubadilisha maisha ya maelfu ya wasomaji watakaofanikiwa kupata siri za mafanikio.
Mkurugenzi wa Global Publishers LTD, Shigongo Eric James (kulia), akishikilia vitabu vyake baada ya kumpatia jukumu la uzinduzi huo Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa ya Kampuni hiyo, Oscar Ndauka. Tukio hilo limefanyika mapema leo ndani ya jengo la ofisi za GlobalPublishers zilizoko Mwenge-Bamaga jijini Dar es Salaam.
Meneja Mkuu wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia), akiwa amenyanyua moja ya vitabu hivyo baada ya zoezi la kukata utepe wa uzinduzi kukamilika.  Katikati ni mtunzi wa kitabu hicho, Shigongo Eric James na Oscar Ndauka, wote wakiwa wamenyanyua vitabu hivyo. Vitabu vilivyozinduliwa ni ‘Sheria 10 Zilizothibitishwa – Jinsi ya Kutoka Kwenye Umaskini Hadi Mafanikio’, cha pili ni ’10 Proven Secrets – How to Move From Poverty to Success’ na cha tatu ni  ’26 Secrets – How to Defeat Your Enemies and Make Millions of Dollars’.
Shigongo akimkabidhi jukumu la kukata utepe Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa Oscar Ndauka (wa kwanza kushoto) huku Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Abdallah Mrisho anashuhudia zoezi hilo.

Shigongo akiwaonyesha mojawapo ya vitabu hivyo baadhi ya wanahabari waliokuwa wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo (hawapo pichani).
Shigongo akiongea machache kwenye uzinduzi huo.
Baadi ya wanahabari kutoka sehemu mbalimbali wakichukua matukio ya uzinduzi huo.
Shigongo akisisitiza jambo juu vitabu hivyo kwenye uzinduzi huo.
Meneja Mkuu wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho, akiwakaribisha wanahabari katika uzinduzi huo.
Afisa Masoko wa Global Publishers Ltd, Benjamin Mwanambuu, akiongea jambo na waandishi wa habari kabla ya zoezi la uzinduzi huo kuanza.
Wanahabari wakiwajibika.
Shigongo akisaini moja ya vitabu hivyo tayari ya kukitoa kama zawadi kwa baadhi ya wanahabari walioshuhudia uzinduzi huo.
Mmoja wa waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo akisainiwa kitabu alichopewa.
Baadhi ya waandishi na wahariri wa Global Publishers Ltd wakisainiwa vitabu hivyo.
Shigongo akisaini kitabu kimojawapo.
(PICHA: MUSA MATEJA, RICHARD BUKOS/GPL)

TUME YA TAIFA YATOA RATIBA YA MIKOA YA MBEYA,RUKWA KATAVI NA DODOMA

RATIBA YA USAJILI WA TMT SEASON 2 KWA MIKOA YA MBEYA, MTWARA NA DAR

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MAREHEMU JOHN NYERERE DAR

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa marehemu John  Nyerere, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani, jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2015. Marehemu John 
anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani kwao Butiama
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, wakati alipowasili  nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani jijini Dar es Salaam, leo kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu John Nyerere. Marehemu John 
anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani kwao Butiama
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji wanafamilia baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa  marehemu John Nyerere, wakati wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani, jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2015. 
Marehemu John anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani kwao Butiama
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, wakati  alipowasili nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani jijini Dar es Salaam, leo kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu John Nyerere.  Marehemu John anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani kwao Butiama.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini kitabu cha maombolezo cha msiba wa marehemu John Nyerere, wakati  wa shughuli za kuaga mwili huo zilizofanyika nyumbani kwa Mama Maria Nyerere Msasani, jijini Dar es Salaam leo Mei 11, 2015. Marehemu John anatarajia kuzikwa  keshokutwa nyumbani kwao Butiama.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na baadhi ya viongozi na waombolezaji nyumbani kwa Mama Maria  Nyerere Msasani jijini Dar es Salaam, leo wakati wa shughuli za kuaga mwili wa marehemu John Nyerere. Marehemu John anatarajia kuzikwa keshokutwa nyumbani 
kwao Butiama. Picha na OMR

BENKI YA NMB YATOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO WILAYANI HAI.

$
0
0
Meneja wa Benki ya NMB kanda ya kaskazini Vicky Bishubo akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni ukanda wa chini wilayani Hai.
Msaada wa magodoro uliotolewa na Benki ya NMB kwa waathirika wa mafuriko yaliyotkea hivi karibuni wilayani Hai.
Meneaja wa NMB kanda ya kasakazini Vicky Bishubo akikabidhi msaada kwa mkuu wa wilya ya Hai,Anthony Mtaka huku zoezi hilo likishuhudiwa na mbunge wa jimbo hilo Freeman Mbowe.
DC Mtaka,Mbunge Mbowe na Meneaja wa NMB ,Bishubo wakifurahia msaada huo.
Msaada mwingine uliotolewa ulikuwa ni wa Blankets.
Chakula pia kilitolewa kwa wahnga hao.
Meneaja wa NMB,Vicky Bishubo akiwa na wahanga wa mafuriko .
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Benki ya NMB imetoa msaada  wa kibinadamu wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 10 baada ya kutembelea  eneo la tukio na kujionea athari kubwa zilizosababishwa na mafuriko hayo.

Akizungumza wakati wa kutoa msaada huo Meneja wa NMB kanda ya Kaskazini, Vicky Bishubo,alitoa pole kwa familia zilizofikwa na kadhia hiyo huku akisema NMB imeguswa na tukio hilo na kwamba inatoa msaada
katika maeneo matatu.

Alisema eneo la kwanza la msaada ni chakula ambapo imetoa unga kilo 
2,000,Maharage Kilo 500,Sukari Kilo 500 na mafuta ya kula lita 1,000.

Eneo jingine ni eneo la malazi ambapo yametolewa Magondoro 70,Mablangeti 100,pamoja na marobota ya nguo huku pia Benki hiyo ikichangia mifuko 50 ya Sementi kwa ajili ya ukarabati wa shule ya msingi Elerai iliyofikwa pia na mafuriko.

“Tumesikitishwa na majanga yaliowakuta,NMB tumekuwa na desturi ya kurudisha faida yetu katika jamii kwa kusaidia majanga mbalimbali hivyo tumetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi
milioni 10”alisema Bishubo

Nao baadhi ya wahanga wa mafuriko hayo waliishukuru NMB kwa msaada huo na kutoa rai kwa watu,mashirika na taasisi mbalimbali zilizo za kiserikali na zisizo za serikali kuona umuhimu wa kuendelea kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu kutoka na adhari ziliwakumba.

Mwisho.

ZIARA YA BODI YA UTT-PID NA MENEJIMENTI YAKE ILIPOZURU CHINA YA SIKU 5 YAFANA

$
0
0
3.jpg pichaBodi ya taasisi ya UTT-PID na Menejimenti yake wakia katika picha ya pamoja na uongozi wa kampuni ya Chengdu Engineering Corporation wakati wa picha ya pamoja. Waliosimama mbele (wa pili kutoka kulia) ni mjumbe wa bodi Bi. Janeth Mmari, akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dr. Gration Kamugisha, akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs Elpina Mlaki. Wengine ni wajumbe wa bodi hiyo ya UTT-PID pamoja na wenyeji wao wa nchini humo

Bodi ya Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyo chini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID), pamoja na Menejimenti yake iliyozuru nchini China katika ziara maalum ya siku tano kwa ajili ya Mafunzo na kubadilishana uzoefu imefana na tayari bodi hiyo imerejea nchini.

Katika ziara hiyo, Bodi ya UTT-PID, ikiongozwa na mwenyekiti wake Mrs. Elipina Mlaki pamoja na Menejimenti nzima walieleza kuwa imeweza kuwa ya mafanikio makubwa huku wakiahidi kuyafanyia kazi yae yote waliojifunza nchini China.

Katika ziara hiyo, bodi na menejimenti ya UTT-PID walipata wasaha wa kutembelea maeneo mbalimbali ya miji ya nchi hiyo ikiwemo makampuni makubwa na kujifunza na kujenga na kudumisha ushirikiano wa utendaji wa kazi.
2.jpg
Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs. Elpina Mlaki (wa pili kulia) akilezea jambo katika moja ya mkutano wao waliofanya katika ziara hiyo nchini China. Anayemfuatia ni Mkurugenzi Mkuu wa UTT-PID, Dr. Gration Kamugisha pamoja na wajumbe wa bodi na Menejimenti ya UTT-PID, Wengine kushoto ni watendaji kutoka kampuni ya Chengdu Engineering Corperation ya nchini humo.

UTT-PID Mafanikio yake nchini

DAR ES SALAAM-Moja ya mafanikio ya Taasisi ya UTT-PID ni pamoja na uwekezaji na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la kisasa na ghorofa 20 mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam kwa matumizi mbali mbali ya kiofisi na biashara.

UTT-PID kwa kushirikiana na muungano wa Vyama vya Ushirika Tanzania walifanikisha ujenzi wa jengo hilo lililopewa jina la ‘’Ushirika Building’’ na kufunguliwa mwaka 2013 na Mhe Rais Jakaya M. Kikwete. Mradi huu pia unajumuisha pia ukarabati wa jengo la zamani ambao unaendela kwa kasi nzuri.

LINDI-Mafanikio mengine ya Taasisi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita ni pamoja na utekelezaji wa miradi mikubwa ya upimaji wa ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo ya viwanja 10,000 katika mkoa wa Lindi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ambapo awamu ya kwanza viwanja 2,473 vilipimwa katika Pwani za Mabano na Mmongo na hadi sasa Taasisi kwa kushirikia na Halmashauri ya Lindi wanaendeleza kazi ya uuandaji wa hati kwa ajili ya wanunuzi ikijumishwa na upanuzi wa barabara katika eneo la mradi.
IMG_6955.jpg piha
UTT-PID wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao katika baadhi ya miji ya nchini China walipotembelea kwa ziara ya mafunzo ya siku tano ya kujenga uzoefu na ufanisi wa utendaji wa kazi za Taasisi hiyo.
KAGERA-Katika mkoa wa Kagera, Taasisi kwa ushirikiano na Halmashauri ya Bukoba iliwezesha na kusimamia upimaji wa viwanja 5,000 vya matumizi mbalimbali ambapo hadi sasa viwanja 3500 vimeshagawia kwa waombaji mbalimbali.


Uwekezaji huu umeigharimu Taasisi hii zaidi ya fedha za kitanzania kiasi cha Billioni kumi ( Bilion 10) katika uendeshaji miradi mbalimbali na uwekezaji wa miundombinu kama vile maji, umeme na uchongaji wa barabara.

MIKOA MINGINE- Miradi mengine mikubwa iliyofanywa na Taasisi inajumuisha pamoja na wa Mapinga Bagamoyo ambapo uwekezaji wa miundombinu husika kama maji, umeme na barabara umekwisha fanyika, sehemu nyingine ni pamoja na Kingolowira na Kiegea Morogoro, Soga Kibaha na Sengerema Mwanza.
IMG_6985.jpgyyy
Mwenyekiti wa Bodi ya UTT-PID, Mrs. Elpina Mlaki (mwenye skafu nyekundu) wakisikiliza maelezo kwa umakini kutoka kwa wataalamu wa kampuni ya Chengdu Engineering Corporation walipotembelea katika nchi ya China kwa ziara ya mafunzo ya siku tano. (kulia kwake) ni mjumbe wa bodi hiyo, Mrs. Janeth Mmari.
IMG_6971.jpg uuuMwanasheria wa UTT-PID, Bi Tuzo Mpiluka (kushoto) akiwa pamoja na Afisa Majengo mwandamizi wa UTT-PID, Ndugu Sebastiaan Ivambi (katikati) wakiwa pamoja na mwenyeji wao Mr. Donny Yang wa Power China, katika ziara hiyo ya siku tano, nchini China ya jujenga uzoefu.
IMG-20141003-WA0000.jpgww
Moja ya miradi ya UTT-PID uliopo Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani, Tanzania, ambapo uwekezaji wa miundombinu husika kama maji, umeme na barabara umekwisha fanyika, kama unavyoonekana pichani katika sehemu ya mradi huo.

​​ KESI YA MAUAJI YA ALBINO YA AARON NONGO YAANZA KUSIKILIZWA TENA

$
0
0
 
Na Daniel Mbega, Mwanza

KESI ya mauaji ya Aaron Nongo mwenye ulemavu wa ngozi (albino) imeanza kusikilizwa tena leo hii kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza baada ya kusimama kwa miezi takriban mitano.

Shauri hilo namba 213 la mwaka 2014 liko mbele ya Jaji Robert Makaramba, ambaye ndiyo kwanza ameanza kulisikiliza baada ya jaji wa awali, Ashery Sumari, kupewa uhamisho.

Washtakiwa katika kesi hiyo walikuwa watano, lakini leo hii mahakama imearifiwa kwamba mmoja – Paulo Budeba Genji maarufu kama Lumalija – alifariki dunia Novemba 22, 2014 katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure, wakati akiwa mahabusu.

Taarifa hiyo ilitolewa na kiongozi wa mawakili wa upande wa mashtaka, Emil Kiria, ambaye aliiomba mahakama, akirejea Kifungu cha 284 (a) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, kwamba inapotokea hali kama hiyo mashtaka dhidi ya mtu huyo yanafikia kikomo, ombi ambalo lilikubaliwa na mahakama.

Washtakiwa waliobakia kwenye kesi hiyo ni Chacha Jeremia, Mathew Jeremia Mlimi, Paschal Lugoye Mashiku na Alex Joseph maarufu kama Bugwema Silola Jangalu. Kesi hiyo ambayo inaendelea tena kesho katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, iko katika hatua ya ushahidi ambapo shahidi wa sita wa upande wa mashtaka atatoa ushahidi wake.

Leo hii mashahidi wawili wametoa ushahidi wao na kufanya idadi ya mashahidi waliokwishatoa ushahidi wao kufikia watano mpaka sasa. Marehemu Nongo aliuawa Juni 26, 2009 majira ya saa tatu usiku akiwa nyumbani kwake Ibanda Relini, jijini Mwanza ambapo wauaji hao walimkata usoni na kisha kumkata miguu yake yote miwili na kutoweka nayo pamoja na meno mawili ya mbele. 

RED CROSS YAKABIDHI MSAADA KWA WAHANGA WA MAFURIKO ZANZIBAR

$
0
0

 Mwakilishi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania { RED CROSS } Bwana Shaaban Ali Iddi akikabidhi msaada wa Viatu Pair 90 kwa Katibu wa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d kwa ajili ya watoto wa familia zilizopata maafa ambao wapo Kambini  Skuli ya mwanakwerekwe “C”.
 Katibu wa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d akiushukuru Uongozi wa Red Cross kwa misaada yao ya Kibinaadamu waliyotoa kwa ajili ya familia zilizopatwa na maafa wiki iliyopita. 
Uongozi wa Chama cha Msalaba mwekundu Tanzania ukimsikiliza Katibu wa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d hayupo pichani akitoa nasaha zake baada ya kupokea msaada uliotolewa na Uongozi huo.


Chama cha Msalaba mwekundu Tanzania { red Cross } kimekabidhi msaada wa viatu Pair 90 kwa ajili  ya watoto wa familia zilizowekwa Kambini  katika Skuli ya Sekondari ya Mwanakwerekwe “C” baada ya Nyumba zao kujaa maji ya mvua.

Msaada huo umefuatia Mvua za Masika zilizotokea usiku wa kuamkia Tarehe 3 Mei mwaka huu na kuleta maafa makubwa yaliyosababisha zaidi ya  Nyumba 700 kuathirika  ndani ya Mkoa wa Mjini Magharibi na kuzikosesha makaazi Familia zilizokuwa zikiishi katika nyumba hizo.

Ujumbe  wa Red Cross Mkoa wa Mjini Magharibi ukiongozwa na Mwakilishi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho Bwana Shaaban Ali Iddi umekabidhiwa msaada huo kwa Katibu wa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar  ambae pia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Dr. Khalid Salim Moh’d hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi Bwana Shaaban Ali Iddi alisema Uongozi wa Red Cross ulifikia hatua ya kutoa msaada huo baada ya kugundua kwamba  idadi kubwa ya watu waliohifadhiwa kwenye kambi ya dharura ya Mwanakwerekwe “C” ni Watoto wadogo. 

Alisema Red Cross imeguswa na tukio hilo la mafuriko hivyo licha ya juhudi wanazochukuwa za kutoa misaada mbali mbali ya huduma lakini pia ikawajibika kuongeza msaada huo wa Viatu ambao kwa kiasi kikubwa utawasaidia watoto hao.

Mwakilishi huyo wa Mkutano Mkuu wa Red Cross Taifa aliyaomba Mashirika na Taasisi nyengine za Kitaifa na Kimataifa kuendelea kuguswa na Tukio hilo na kutoa misaada kwa jukumu hilo si vyema ikaachiwa pekee Serikali Kuu.

Akipokea Msaada huo  Katibu wa Kamatio ya Taifa ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar ambae pia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rsis wa Zanzibar Dr. Khalid Salum Moh’d aliipongeza Red Cross kwa jitihada zake inazoendelea kuchukuwa katika kusaidia huduma za Kijamii. 

Dr. Khalid alisema Viongozi na Wanachama wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania muda wote wamekuwa karibu na Serikali hasa wakati yanapotokea matukio ya majanga na maafa.

Katibu huyo wa Kamati ya Taifa ya kukabiliana na Maafa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa Red Cross kwa hatua yake hiyo ambayo itasaidia kupunguza machungu ya Watoto hao, wengi kati yao wamepoteza vitu vyao vyote zikiwemo nguo na hata madaftari ya Skuli.

Alisema Kambi ya dharura ya Mwanakwerekwe “ C “ hivi sasa ina zaidi ya watoto 74 walio chini ya umri wa miaka 14  wanaoendelea kuhifadhiwa ambao watafaidika na msaada huo wa viatu.

“ Asilimia kubwa ya Watoto hao waliopo Kambini wamepoteza Vitu vingi ikiwemo Madaftari ya Skuli, Nguo, Viatu na vitu vyengine muhimu wanavyotumia ambavyo vingi kati yao tayari Idara ya Maafa kupitia Taasisi na Mshirika hisani wameshapatiwa “. Alifafanua Da. Khalid Salum Moh’d.

Pia  aliyashukuru na kuyapongeza Mashirika na Taasisi za Umma na hata zile Binafsi zilizojitolea kutoa misaada mbali mbali ya Kibinaadamu na kuziomba zisichoke kwa vile bado mahitaji zaidi kwa waathirika hao yanahitajika.

Katibu huyo wa Kamati ya Taifa ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar alieleza kwamba Serikali imeandaa mpango maalum wa  usafiri kwa watoto wote waliopo Kwenye Kambi ya dharura Mwanakwerekwe “C” kuendelea na masomo yao kwenye skuli mbali mbali wanazotoka.

Dr. Khalid aliwatoa hofu Wazazi wa Watoto hao kwamba Gari zilizoandaliwa zimepangwa kuwachukuwa  watoto hao na kuwapeleka kwenye Skuli zao waanze masomo kama kawaida na kuwarejesha Kambini  baada ya kumaliza masomo yao kwa kila kipindi watachokuwapo kambini hapo.

KUELEKEA JEMBEKA FESTIVAL JJ BAND WAACHIA NGOMA MPYA 'NISHIKE'

$
0
0
Hayawi hayawi hatimaye yamekuwa, ile band ambayo kwa walio mbali basi walikuwa wakisikia simulizi zake toka kwa wenyeji kwamba inafumua burudani ya kijanja ile kisawasawa toka kiota chenye hadhi ya kitalii Jembe Beach Resort Mwanza, JJ Band ndiyo ninao wazungumzia, basi wamekuja na single yao ya kwanza mpya inayoitwa 'NISHIKE'

Kazi imefanyika ndani ya studio za One Love FX zilizoko Ilemela jijini Mwanza, chini ya mkono wa mtayarishaji mkali Tiddy Hotter, yule aliye tengeneza ngoma kama Changamka ya Director Shahib, Tumewaka - G Nako ft Godzillah, Mimi na wewe - Dynna Nyange, Listen - Belle Nine, Itika - Josline na nyingine kali kibao.

Kazi tamu kwa sikio, yenye hisia na inayochezeka bado mbichi kabisa isikilize kwa nafasi ikiwa ni amsha amsha ya kuelekea tarehe 23 May 2015 ambapo barabara zote za jiji la Mwanza zitaelekea CCM Kirumba katika tamasha kubwa la burudani 'JEMBEKA FESTIVAL 2015' OYOMBA YES - PAMOJA SANA 

LOOKING FOR AN AMAZING CAREER OPPORTUNITY?

$
0
0


Position Title: Sales And Marketing Executives

R&N Solutions LTD is looking for Three (3) enthusiastic, passionate, and dynamic Sales And Marketing Executives to become part of our team. These positions offer growth potential, and the ability to be creative within a positive, growing environment with unlimited earning potential.  Successful candidates will also have an opportunity to build expertise through continuous training and development to ensure their success.

Responsibilities Include But Are Not Limited To:

  • Utilize elevated levels of marketing and sales to maximize sales performance; meet sales goals.

  • Develop new business opportunities through cold calls and leads generation

  • Develop and execute monthly sales and marketing plans that targets expansion to our existing customers as well as new ones.

  • Comply with all sales related policies and procedures

  • Provide the highest level of customer service and support to customers.

  • As a member of our team, you will help customers with their purchases and answer any questions they may have, as well as provide support and assistance to your colleagues.

Qualifications/ What We Are Looking For?

  • 1-3 years of relevant sales and marketing experience

  • University degree or College Diploma preferably in Sales/Marketing or Business Management.

  • Excellent communication & interpersonal skills. Must be fluent in English and Swahili.

·         Abililty to qualify leads and opportunities whether presented to you or if you have to source your own leads.

·         Candidate with openness, approachability and sincerity

·         Candidate wit enthusiasm and passion for assisting customers and helping to understand their unique needs

·         With integrity and drive to succeed with passion for continuous learning and self development.

·         With ability to get past the gate-keepers and in front of the decision-makers.

  • Initiate all aspects of the sales process including scheduling appointments; making initial presentation; understanding customers needs and requirements; researching industries; building rapport with potential customers; explaining the details of our products and services capabilities;

To Apply: Send In Your CV and Cover Letter To careers@rnsolutionsltd.com before 25th May 2015


Thanks in advance to all candidates for applying. However,only short-listed candidates will be contacted for interview. 

THE GOVERNMENT OF TANZANIA EXPANDS ITS NEW BIRTH REGISTRATION SYSTEM TO MWANZA

$
0
0
Baby Veronica being registered
Baby Veronica being registered.
The new system is set to drastically increase the number of children under 5 with birth certificates.

The Deputy Minister of the Ministry of Constitutional and Legal Affairs of the United Republic of Tanzania, Honorable Ummy Ali Mwalimu, launched today in Mwanza the new simplified birth registration initiative for children under-five in Tanzania. The event took place in Mwanza, the second largest city in mainland Tanzania. Mwanza will be the second region, after Mbeya, to benefit from the new, easily accessible and free birth registration system which is set to register over 400,000 children under-five by December 2015.

This new birth registration system, which is being supported by a generous contribution from the Government of Canada through the Department of Foreign Affairs, Trade, and Development, was first field tested in 2012 in Temeke, the largest district of the city of Dar es salaam and in 2014 was officially launched in Mbeya. According to the Acting Chief Executive Officer of RITA, Ms. Emmy Hudson, this simplified system marks a significant shift in accelerating birth registration in Tanzania after years of stagnation.

“RITA has embarked on several initiatives to improve birth registration in Mainland Tanzania, especially to newborn babies to ensure that each baby is captured and registered shortly after birth and closest to home. Through this initiative we see this dream realized and thank our development partners for unwavering support. Temeke and Mbeya have set good examples and we hope to register even better results in Mwanza.”


The 2010 Tanzania Demographic and Health Survey showed that only 16 per cent of children in Tanzania under the age of five were registered with civil authorities, and only about 8 per cent have a birth certificate.[1] Registration in Zanzibar is much more widespread than on the mainland with 78.7 per cent of under-fives registered (63 per cent with a certificate) versus 14.6 per cent registered (6.2 per cent with a certificate) on the mainland.
Prior to the roll-out of the Birth Registration Initiative in Mbeya it was estimated that only 8.7 per cent of the under-five population had a birth certificate. In less than two years after the roll-out, Mbeya saw approximately a 48 per cent increase and now it is estimated that nearly 56 per cent of under-fives in Mbeya have a certificate.

[1] See Tanzania Demographic and Health Survey (2010), pg. 27.
[2] Ibid. and See p.28, Table 2.11 Birth Registration for Children Under Five
Baby Veronica and her Birth Certificate
Baby Veronica and her Birth Certificate.
The new decentralized birth registration and certification system capitalizes on the existing health infrastructure and personnel to register newborn babies soon after birth or within 12 months when visiting health facilities for vaccinations. Registration information is uploaded using mobile phone technology to a centralized data-base resulting in real-time data availability, and a certificate is issued the same day.
This new birth registration and certification system will be operational in Mwanza soon after today’s launch. With financial support from the Canadian Government, this new system will also be rolled out over the next five years to ten additional regions, namely, Mara, Shinyanga, Simiyu, Geita, Iringa, Njombe, Tabora, Kagera, Kigoma and Dodoma.
Paul Speech
UNICEF Tanzania Deputy Representative, Paul Edwards.
UNICEF Tanzania Deputy Representative, Paul Edwards, commended the Government of Tanzania for its commitment to prioritizing child rights and reaffirmed UNICEF’s commitment and support towards making birth registration and certification a reality for all children.
“With this initiative RITA has taken an important step towards facilitating birth registration. Registration Assistants are now able to upload information instantly over mobile phones, making data available in ‘real time.’ This type of information is crucial in planning for Tanzania’s future. And it goes without saying that the certificate itself provides protection for children - proof of age informs the State as to who is a child, and provides protection against the exploitation of children and child marriage.”
Tigo Lake Zone Director, Ally Maswanya said: “The support provided by Tigo towards this initiative is in line with the company’s corporate social responsibility strategy which aims at empowering community with information and communication technology tools such as mobile phones. The under-five birth registration initiative demonstrates our commitment as telecommunication experts and attests the potential of mobile technology in development programs.”
The VSO Country Director Jean Van Wetter praised the strong partnership between Government, UN, private sector and civil society: “Birth registration is fundamental to guarantee child rights and further improve the social services delivery system in the country.”

Benki ya Exim yazindua kampeni maalumu kuhamasisha matumizi ya kadi zake mpya za ‘Faida’.

$
0
0
 Meneja Bidhaa wa Benki Ya Exim Tanzania, Aloyse Maro (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa waandishi wa habari kutangaza uzinduzi wa kampeni mpya ya benki hiyo inayolenga kuhamasisha wateja juu ya matumizi ya kadi mpya ya Faida Debit Card, ambayo imeimarishwa zaidi kiusalama, jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni Meneja Masoko Msaidizi wa benki hiyo, Anita Goshashy (kushoto) na Zawadi Kanyawana kutoka kitengo cha Huduma za Rejareja za Kibenki (katikati)


Meneja Bidhaa wa Benki Ya Exim Tanzania, Aloyse Maro (katikati)akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano wa waandishi wa habari kutangaza uzinduzi wa kampeni mpya ya benki hiyo inayolenga kuhamasisha wateja juu ya matumizi ya kadi mpya ya Faida Debit Card, ambayo imeimarishwa zaidi kiusalama, jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni Meneja Masoko Msaidizi wa benki hiyo, Anita Goshashy (kushoto) na Zawadi Kanyawana kutoka kitengo cha Huduma za Rejareja za Kibenki (kulia).

BENKI ya EximTanzania imezindua kampeni inayolenga kuwahamasisha wateja wake juu ya matumizi ya kadi zake mpya za  ‘Faida Chip and PIN Debit card’ ambazo zimeundwa  kwa kuzingatia vigezo vya kiusalama zaidi.
Kwa mujibu wa Meneja Bidhaa wa benki hiyo Bw. Aloyce Maro hatua hiyo ni sehemu ya jitiahada za benki hiyo kuhakikisha kwamba huduma zake zinatolewa kwa uhakika na usalama zaidi kwa faida ya wateja wake.
“Lengo kubwa la kampeni hii ni kuwahamasisha wateja wetu juu ya matumizi ya kadi zetu mpya za  ‘Faida Chip and PIN Debit card’ ambazo zinatumia ‘chip’ badala ya ‘magnetic strip’ lengo likiwa kuongeza usalama wa akaunti za wateja wetu’’ alisema Bw. Maro wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jana jijini Dar es Salaam.
Matumizi ya kadi hizo yanaelezwa kuongeza usalama na amani miongoni mwa watuamiaji wake kwa kuwa zina uwezo wakipekee katika kuhifadhi na kutambua  taarifa za mtumiaji na hivyo kuondoa hofu ya wizi wa namna yoyote ile, kwa mujibu wa Bw. Maro.
“Kadi hii inauwezo mkubwa wa kuhifadhi taarifa pamoja kumtambua mmiliki wake.Uwezo huu ndio siri ya mafanikio yake kwa kuwa inauwezo wa kuwazuia kabisa watu wenye nia ovu na akaunti ya mteja hususani kwa kufanya jaribio la namna yoyote la wizi,’’ alisema Bw. Maro.
Akiizungumzia zaidi kadi hiyo Bw. Maro alisema inauwezo wa kumuwezesha mtumiaji wake kuweza  kuifikia akaunti yake na kufanya miamala  kutoka kwenye  mashine za kutolea fedha zenye uthibitisho wa ‘MasterCard’ pamoja na zile za POS ulimwenguni kote bila usumbufu wowote.
Aidha Bw. Maro aliwahamasisha wateja wa benki hiyo ambao bado hawajachukua kadi zao wajitokeze kuzichukua kwenye matawi ya benki hiyo ili waanze kufaidi matumizi yake. 

WAZIRI NYALANDU AKAGUA MENO YA TEMBO YALIYOKAMATWA NA ASKARI WANYAMAPORI WILAYANI NAMTUMBO

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Lazaro Nyalandu na Ofisa Wanyamapori akikagua meno ya tembo yaliyokamtwa na askari wa wanyamapori toka kwa majangili Likuyu Sekamaganga Namtumbo mkoani Ruvuma mwishoni mwa wiki iliyopita.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Lazaro Nyalandu na Ofisa Wanyamapori akikagua ngozi za wanyamapori zilizokamatwa na askari wa wanyamapori toka kwa majangili Likuyu Sekamaganga Namtumbo mkoani Ruvuma mwishoni mwa wiki iliyopita.

INTERNATIONAL CONVENTION OF LIONS IN DAR ES SALAAM

$
0
0


International Director Raju Manwani decorates the International President's lapel pin on Chairman of the Convention Lion Dr. T.M. Jafferji. Standing in the centre is Past International Director Lion Dr. Manoj Shah.

District Governor of Uganda, Tanzania and South Sudan Lion Night Ndyarugahi addresses convention delegates at the last Cabinet Meeting.
The latest additional country, South Sudan joined Sub District 411B . The other two countries areTanzania and Uganda. The Sub District 411A comprises Kenya, Ethiopia and Seychelles.

Immediate Past District Governor Lion Wilson Ndesanjo (4th right) being awarded Appreciation Certificate of International President jointly by Chief Guest International Director Raju Manwani and PID Dr. Manoj Shah. Third from right is Governor Night Ndyarugahi, the first lady to become a Governor in Sub District 411B.

MORE NEWS CLICK HERE


MHE.FREEMAN MBOWE AMSHUKURU MAGUFULI NA SERIKALI YA CCM KWA KAZI NZURI


RAIS KIKWETE AHITIMISHA ZIARA RASMI YA ALGERIA, AREJEA NYUMBANI

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi mbalimbali katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Raymond Mushi alipowasili kutoka Algeria katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es salam Suleiman Kova, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Raymond Mushi, Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sophia Mjema na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda alipowasili kutoka Algeria katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipanda ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Houari Boumediene jijini Algiers Jumatatu May 11, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini humo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiaga wenyeji wake katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Houari Boumediene jijini Algiers Jumatatu May 11, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini humo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya kumbukumbu na Marubani na Wafanyakazi wa Shirika la ndege la Tassili la Algeria baada ya kuwsili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria.
 PICHA NA IKULU 

BANDA LA TANZANIA LATIKISA MAONESHO YA INDABA

$
0
0
 Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Mh. Radhia Msuya (katikati)  katika picha ya pamoja na waoneshaji kutoka taasisi za serikali katika maonesho ya INDABA AFrika Kusini. Wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania bii Devota Mdachi.

Waoneshaji kutoka tasisi za Serikali katika maonesho ya INDABA Durban Afrika Kusini wakiwa kazini kuitangaza Tanzania.


Na: Geofrey Tengeneza.
Banda la Tanzania katika maonesho ya Kimataifa ya INDABA yaliofanyika katika jiji la Durban nchini Afrika Kusini lilikuwa miomgoni mwa mabnda yaliyon’gara zaidi kwa kuvutia watu waliotembelea maonesho hayo ambayo kwa mwaka huu yalifanyika kwa siku tatu kuanzia 9 hadi tarehe 11/5/2015.


Katika maonesho hayo ambayo ni makubwa zaidi barani Afrika na ya tatu kwa ukubwa duniani baada ya ya yale ya ITB Ujerumani na WTM Uingereza Tanzania iliwakilishwa na makampuni 30 zikiwemo pia taasisi za Serikali kama vile TTB, Tanapa na Ngorongoro.



Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Bibi Radhia Msuya alipata fursa ya kutembelea maonesho hayo na kuzungumza na waoneshaji kutoka Tanzania na kuwapongeza kwa namna walivyojipanga kushirki katika maonesho hayo chini ya uratibu wa Bodi ya Utalii Tanzania –TTB.

KUNDI LA VIJANA MARAFIKI WA LOWASA WAFIKA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO.

$
0
0

Safari ya siku tatno kwa ijana hao ikahitimishwa katika kilele cha Uhuru Peak ,kama wanayoonekana ijana hao wakiongozwa na mratibu wa marafiki wa Lowasa Kanda ya Kaskazini ,Noel Nnko(mwenye koti la rangi nyekundu kulia).
Safari ya kurudi kiasi ilikuwa tatizo wakati mwingine baadhi yao walilazimika kupewa msaada kwenye kifaa maalumu cha kushushia wageni waliopata maatizo .
Baadhi ya vijana ambao ni marafiki wa Lowasa wakiwa katika safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro.
Kundi la marafiki wa Lowasa kutoka kana ya Kaskazini wakiwa katika kituo cha Kibo ,wakiwa katika maandalizi ya kuanza kwenda kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Sehemu ya juu ya mlima Kilimanjaro ikiwa imefunikwa kwa theruji.
Kundi la Marafiki wa Lowasa wakiwa katika kituo cha Stella,kikiwa ni kituo cha mwisho kuelkea kilele cha Uhuru .
Mandhari mbalimbali zinayoonekana wakati wa kuupanda Mlima Kilimanjaro.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

TANZANIA MEDIA IN THE FRONTLINE: JOURNALISTS TARGET POLITICAL HATE IN UPCOMING ELECTION

$
0
0
hate specch banner
Journalists and African media leaders from the region are meeting this week to highlight the role of media and journalism in combating hate-speech and intolerance in the upcoming election campaign.

The meeting, organised by the International Association of Women in Radio and Television (IAWRT) and the Ethical Journalism Network (EJN), opens in Dar Es Salaam today (Tuesday) and comes after fresh regional conflict with recent terrorist attacks in Kenya and fears of genocidal violence in Burundi.

The meeting will involve a workshop at the Peacock Hotel on how journalists and media can help stop the spread of hateful political propaganda and will reinforce the Africa-wide campaign,Turning the Page of Hate, which was launched last year in Kigali to mark the 20th anniversary of the Rwandan genocide.

Among the speakers will be Mohammed Garba, President of the Federation of African Journalists and Imelda Lulu Urio, from the Tanzanian Legal and Human Rights Centre.

“This conference could not come at a more important time for Tanzanian journalists,” said Rose Haji Mwalimu, head of IAWRT for Tanzania. “Media here are in the frontline of a struggle for democracy and pluralism. We have to ensure that we keep a lid on the voices of hate and, at the same time, give people the right to free speech.”


This challenging task will involve helping journalists to identify hate-speech and to lower the temperature of confrontation that often comes at election time, she said. The journalists and media will be encouraged to use a special 5-point test for hate-speech that has been developed in co-operation between media and the United Nations human rights commission.

“The violence in recent months inspired by terrorists in Kenya and the continuing shadows over Burundi suggest that it’s a matter of urgency for journalists to eliminate the voices of intense hatred and incitement,” said Aidan White, Director of the EJN. “This meeting comes only a few months before the hotly-contest general election in Tanzania when the political temperature will rise and media have to guard against being used by hate-mongers.”

In recent years, Tanzania has seen much foul play by candidates from all parties with hate speech and threats on all sides. There have been reports of acid attacks, kidnappings and killings. This meeting will focus on practical actions for journalists to help reduce the level of confrontation.

The meeting will:
1. Call upon government and all political leaders to respect the freedom of the press and ensure that journalists operate in a safe environment;
2. Call on media and journalists to boycott hate speech or any language that can stir violence;
3. Promote ethical standards at all levels of the press, broadcasting and online communications;
4. Call on politicians to ban hate speech in their own ranks;
5. Call upon citizens to boycott meetings or activities where candidates or political activists use hateful, violent and discriminatory language to promote their brand of politics.
6. Reiterate the need for all media to be aware of legal restrictions, including the Newspaper Act of 1976 that could see media banned for hate speech;
7. Call upon the Tanzanian Parliament to review provisions in the Statistics Act as well as the Cyber Crime Act which may violate the freedom of the press as well as the right to information.
“None of this will be easy,” said Rose Haji Mwalimu, “But this is an important opportunity for journalists and media to strengthen their role in ensuring the coming elections are a beacon for democracy and not an excuse for settling political score by acts of hatred and violence.”
More information:
Rose Haji Mwalimu:rohamu2004@yahoo.co.uk or 0754270856/0655434444
Aidan White: aidanpatrickwhite@gmail.com or 00447946291511

TEITI yawanoa waandishi wa habari za biashara juu ya uwazi katika sekta ya madini nchini

$
0
0
41Mwenyekiti wa Mpango wa Uhamasishaji wa Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi asilia na Mafuta (Tanzania Extractive Industries Transparency Initiative (TEITI), Jaji Mstaafu, Mark Bomani akifungua warsha ya siku moja kwa wadau na wandishi wa habari za biashara, mkutano uliofanyika Ledger Plaza Bahari Beach Hotel jijini Dar es Salaam, Mei 7, mwaka huu.
1Afisa mahusiano Mkuu wa TEITI, Catherine Mbatia akimkaribisha rasmi Mwenyekit wa TEITI, Jaji Mark Boman kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Warsha hiyo iliyowakutanisha wandishi wa habari za biashara na wadau mbalimbali ikiwemo wadau wa madini.
6
Meneja Mahusiano, Alex Modest, (kulia)akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika semina hiyo watatu kulia ni Meneja mikakati kutoka (TBDC) George Kibakaya (kushoto) Mwenyekiti TEITI,Jaji Bomani,wa pili kushoto mwandishi mchambuzi, John Bwire,(katikati) ni Halfani Halfani kutoka (Oil Gas Association Tanzania-OGAT).
2
Afisa mahusiano Mkuu wa TEITI, Catherine Mbatia akielezea juu ya TEITI, wakati wa Warsha hiyo iliyowakutanisha wandishi wa habari za biashara na wadau mbalimbali ikiwemo wadau wa madini.
13
Mwenyekiti TEITI, Jaji Bomani (kushoto ) akichangia mada katika warsha hiyo, wengine ni Mwanahabari na mchambuzi John Bwire, akifuatiwa na Halfani Halfani wa OGAT, Meneja mikakati kutoka (TBDC) George Kibakaya pamoja na Godvictor kutoka kampuni ya madini ya Geita.
14
Wadau wa sekta ya madini na wanahabari wakifuatilia mada katika warsha hiyo.

4
Mwandishi Mwandamizi wa Mtandao wa Modewji blog, Andrew Chale (kushoto) akifuatiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la Business Times, Damas Makangale, pamoja na wandishi wengine waki 'note' vitu muhimu kwenye warsha hiyo.
9
Mwandishi wa habari na mchambuzi, John Bwire akitoa mada katika warsha hiyo juu ya umuhimu wa kuwajengea uwezo wajasiliamari wa ndani ili kunufaika na sekta ya madini tuliyonayo
12
Godvictor kutoka kampuni ya Madini Geita, akitoa mada juu ya uwazi wa makampuni hapa nchini hasa katika sualala ulipaji wa kodi na mifumo ya kisheria ya biashara hiyo ya sekta ya madini ambapo alibainisha kuwa baadhi ya makampuni yamekua yakitumia sheria ya Kimataifa hivyo uwepo wa baadhi ya makapuni hayo kutoweka wazi mikataba yao ni kuogopa ushindani katika soko la Kimataifa.
17
Mwanahabari mwandamizi Joseph Mwamunyange (kushoto) akiwa na wadau wa sekta ya madin, Kulia ni mtaalam wa uchambuzi wa data katika sekta ya madini kutoka taasisi ya Global Witness Rachel Owens wakati wa warsha hiyo
19 
Picha juu na chini Wanahabari wakiendelea na majukumu yao .. kwenye warsha hiyo
2023
Mwanahabari Joseph Mwamunyange akiendesha mjadaraa juu ya uwazi katika masuala ya upatikanaji wa habari kwa uwazi hasa za sekta nyeti za madini na fedha.
24
Prof. Handley Mwafenga (TMAA) akitoa mada juu ya uwajibikaji na uwazi katika sekta ya madini katika warsha hiyo..
2529
Mjumbe wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) George Kibakaya ali
30
Wadau wa sekta ya madini wakichangia mada katika warsha hiyo..
31
Dr. Camillius Kasalla kutoka (CSO) akitoa mada namna ya vyama vya kijamii NGOs juu ya umuhimu wake katika ufuatiliaji wa mambi ya uwazi katika sekta ya madini..
37
33
Samuel Osei Bekoe kutoka taasisi ya NRGI ya nchini Ghana akitoa mafunzo kwa wandishi wa habari (Hawapo pichani) ya namna ya kupata habari kupitia mitandao ya intaneti hasa ya takwimu na mahesabu ya masuala ya fedha na madini.
38
..mafunzo hayo
36
Samuel Osei Bekoe kutoka taasisi ya NRGI ya nchini Ghana akitoa mafunzo kwa wandishi wa habari (Hawapo pichani) ya namna ya kupata habari kupitia mitandao ya intaneti hasa ya takwimu na mahesabu ya masuala ya fedha na madini.
 
40
Mwenyekiti wa Mpango wa Uhamasishaji wa Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi asilia na Mafuta (Tanzania Extractive Industries Transparency Initiative (TEITI), Jaji Mstaafu, Mark Bomani akiwa na vitabu vya ripoti ya nne, vikiwa katika lugha mbili ya kiswahili na kiingereza akivionesha kwa wadau na wandishi wa habari za biashara, mkutano uliofanyika Ledger Plaza Bahari Beach Hotel jijini Dar es Salaam, Mei 7, mwaka huu.



Na Andrew Chale, Modewji blog.
Mwenyekiti wa Mpango wa Uhamasishaji Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi Asilia na Mafuta (TEITI) Jaji Mark Boman amewataka waandishi wa habari kutoa taarifa sahihi zenye lengo la kuielimisha jamii hasa pindi wanaporipoti habari za sekta ya madini hapa nchini.

Akizungumza wakati wa semina ya waandishi wa habari za biashara na uchumi ya siku moja iliyofanyika hivi karibuni Ledger Plaza Bahari Beach Hotel, jijini Dar es Salaam, Jaji Bomani alisema taarifa sahihi hasa za masuala ya uchumi zinahitajika kwani zikitolewa tofauti zinaweza kusababisha mkanganyiko kwa wananchi.

Alisema taasisi hiyo ilianzishwa kuwa lengo la kufuatilia sekta ya madini kwani hapo awali ilionekana kutowanufaisha wananchi. “Awali kuliwa na mkanganyiko wa kwamba sekta ya madini haiwanufaishi wazawa hivyo Serikali ilichukua hatua na kuunda kamati ya kushughulikia tatizo hilo kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta hiyo ya madini,”alisema.

Alisema chombo hicho kilianza kutoa ripoti za ufuatiliaji wa sekta za Serikali kwa makini na fedha zinazolipwa. Alisema Ripoti ya nne ambayo ni ya mwaka 2014 inaonyesha kwamba mapato ya Serikali yamekuwa yakiongezeka kila mwaka tofauti na ripoti ya kwanza iliyokuwa na hitilafu ya Dola milioni 30.

Alisema mafanikio ya utaratibu huo umesaidia taasisi za Serikali kuhakikisha kwamba kila fedha inayotoka au kulipwa inakuwa ya maandishi ili kuwa na taarifa sahihi.

Naye Mjumbe wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) George Kibakaya alieleza kuwa, kiasi cha gesi asilia kilichogunduliwa ni futi za ujazo tirioni 55 hivyo ni vyema kujipanga vizuri ili kuhakikisha kinakuza uchumi wa nchi.

Aidha, katika semina hiyo wandishi wa habari walipata pia fursa ya kujifunza namna ya upatikanaji wa data kwa njia ya mtandao huku wakishahuriwa kuwa pindi wanahabari watafutapo data, kuweza kuwasiliana na wataalam husika iliondoa mkanganyiko ikiwemo idara za kifedha, wataalamu wa hesabu pamoja na mifumo sahihi ya data hasa kupitia mifumo ya inteneti.

Mafunzo hayo ya kuripoti habari kwa kutumia uchambuzi wa data, yalitolewa na Samuel Osei Bekoe kutoka taasisi ya NRGI ya nchini Ghana ambaye alitoa wito kwa wandishi wa habari wa Tanzania hasa wanaotaka kuandika habari za kiuchunguzi katika uripoti wa mahesabu na data kuzingatia vyanzo vya taarifa vya kina na vyenye uhakika.

Ambapo alishahuri kuwa licha ya upatikanaji wa data hizo kuwa mgumu na wa sili kwa baadhi ya sekta, aliwataka wandishi kutumia vipengele muhimu na kwa ufupi bila kuweka mambo mengi ambayo yataweza kumchanganya msomaji.

Akitolea mfano wa taarifa za kiuchumi kwa Tanzania ama nchi zingine, ambapo endapo wataingia kwenye mitandao ya taasisi ya kifedha, Ikiwemo IMF, Benki kuu na zingine zimekuwa na uwazi hivyo wanaweza kupata huko taarifa ambazo zinaweza kuwasaidia kuripoti na kuleta changamoto katika nchi huku akisisitiza kutaja chanzo cha taarifa ama ripoti hiyo.

Pia wadau mbalimbali wakiwemo wataalamu wa madini na wandishi wa habari walitoa mada mbalimbali zilizojadiliwa kwa kina katika semina hiyo kwa mfumo wa mdaharo.
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images