Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

RAIS KIKWETE AISHUKURU NA KUIPONGEZA KAMATI YA AMANI YA VIONGOZI WA DINI MKOA WA MWANZA


UTT-PID yashiriki maonesho ya Dar Property 2015

$
0
0
Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyochini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID) ipo kwenye kushiriki maonyesho ya Nyumba na Makazi yanayofahamika kama DAR PROPERTY 2015, yaliyoanza leo Mei 2 na kutarajiwa kumalizika Mei 5, mwaka huu ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee V.I.P Hall uliopo Upanga, Jijini Dar es Salaam.

Katika maonyesho hayo, UTT-PID, inashiriki ikiwemo kutoa elimu mbalimbali na maelezo juu ya utendaji wa kazi za taasisi pamoja na huduma kwa watu mbalimbali wanaotembelea kwenye banda lao hilo ndani ya Diamond Jubilee V.I.P Hall.

Aidha, mapema leo Mei 2, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, alipata wasaha pia wa kutembelea banda hilo la UTT-PID na kupata maelekezo kadhaa ya namna ya utendaji wa kazi wa taasisi hiyo hapa nchini.

KAZI ZA UTT-PID
Kazi za UTT-PID ni pamoja na Utoaji huduma za ushahuri katika maeneo ya upembuzi yakinifu wa miradi mbalimbali, Uratibu wa fedha na huduma zinazohusiana katika maandalizi ya mapendekezo ya miradi kwa benki au taasisi za fedha, uteuzi wa watoa huduma kuhusiana na maandalizi ya zabuni na usimamizi wa majengo na mali ambao ni utoaji wa huduma fanisi za usimamizi wa majengo yaliyochini ya uangalizi thabiti wa taasisi.
Dar Property 2015.

Ni maonesho ya siku nne kuanzia Mei 2 hadi 5, ambayo wadau mbalimbali kutoka Mashirika binafsi na Taasisi za Umma zinazojihusiha na uwekezaji katika Majumba, Ardhi na Makazi wanashiriki. DAR PROPERTY, ambayo kwa mwaka huu ni ya msimu wa pili yakifanyika na kushirikisha wadau hao mbalimbali wa ndani na nje ya nchi.
IMG_6764Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick (katikati), akipata maelezo mara baada ya kutembelea banda la UTT-PID, kulia ni Uli Mtebe Afisa Mwandamizi Mahusiano na Masoko wa Taasisi ya UTT-PID.
karibu 2Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick (katikati), akipata maelezo toka kwa banda la Taasisi ya UTT-PID juu ya Miradi wanayofanya katika mikoa mbalimbali nchini, kulia ni Uli Mtebe Afisa Mwandamizi Mahusiano na Masoko wa UTT-PID. Mkuu wa Mkoa huyo alitembelea banda hilo leo Mei 2, wakati wa ufunguzi wa maonyesho hayo ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee V.I.P Hall.
karibuAfisa Masoko Bi. Kilave Atenaka wa Taasisi ya UTT-PID, akimuhudumia mmoja wa wateja waliotembelea banda la UTT-pid ndani ya maonesho ya Dar Property 2015, yanayoendelea katika ukumbi wa Diamond Jubilee VIP Hall.

MAZOEZI YANAJENGA AFYA – IGP MANGU

$
0
0
  Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP),Ernet Mangu  akimpa mkono mshindi wa  Kwanza wa Riadha  ya Half May Day Marathon katika kundi la Wanaume,Alphonce Felix wa Club ya Holili,Kilimanjaro yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam, wanaoshuhudia ni  Mkurugenzi Mkuu wa Boa  Bank Ammish Owusu, mshindi huyo amejipatia kitita cha Sh. 1100,000.
.Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP),Ernest Mangu akimpa mkono mshindi wa  Kwanza  wa  Riadha ya   Half May Day Marathon katika kundi la wanawake,Natalie Elisante Arusha) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam, wanaoshuhudia ni Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam (CP),Suleiman Kova ,mshindi huyo amejipatia kitita cha Sh. 1100,000.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP),Ernest Mangu akimpa mkono mshindi wa Pili  wa  Riadha ya Half  May Day Marathon katika kundi la wanaume ,Joseph Panga (Arusha) yaliyofanyika leo katika viwanja Polisi Ostebay jijini Dar es Salaam wanaoshuhudia ni ,Mkurugenzi wa Benki ya Boa,Ammish Owusu .

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP),Ernest Mangu  amesema michezo inajenga ukakamavu wa mwili hivyo kwa washiriki wa may day marathon wamefanyoa  afya.

Mangu ameyasema aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati  mashindano ya Half May Day Marathon yaliyofanyika katika viwanja vya Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam ,aliwapongeza washindi na kutaka waongeze juhudi ili waweze kufika mbali katika mchezo wa riadha.  Washindi wa May Marathon wamepongeza waandaji wa mashindano hayo kwani yanaongeza chachu ya kupenda mchezo huo.

Washindi hao wameyasema hayo katika mashindano  ya Half May Day Marathon yaliyofanyika katika viwanja vya Polisi Oysterba jijini Dar es Salaam ,wamesema kuwa mashindano hayo yameamsha kupenda mchezo wa riadha kuendelea kupendwa.

Akizungumza  na mshindi wa kwanza katika upande wa wanaume ,Alphonce Felix amesema ameshinda katika mashindano hayo kwani alijituma kutokana na mazoezi ya mara kwa mara na kuwataka watu wengine kushiriki mchezo huo kutokana na kujenga afya zao.

Amesema riadha ni mchezo mmoja mzuri kutokana na utaratibu kujpangia mazoezi  kwa ni riadhia ni ajira kama michezo mingine.

Mshindi wa Kwanza  kwa upande wa Wanawake ,Natalie Elisante (Arusha)amesema amewataka wasichana kushiriki katika riadha mbalimbali kwani wasichana na wanawake wanaoshiriki mchezo huo ni wachache ikilinganishwa na idadi yetu.

Tutapigania Uhuru wa Habari Siku Zote

$
0
0
UMOJA wa Nchi za Ulaya nchini Tanzania (EU) umepinga vikali vitendo vya kikatili na unyanyasaji wameokuwa wakifanyiwa na vyombo vya dola vya Serikali wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao ambapo ilitokea mwanahabari mmoja kuuwawa. Alisema hawatachoka kukemea matukio hayo ya unyanyasaji kwani yanafifisha uhuru wa habari.

 Akizungumza leo mjini Morogoro katika Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, Kiongozi Mkuu wa Mabalozi hao, Balozi Filiberto Cerianse Bregondi alisema EU itaendelea kupinga namna yoyote ya unyanyasaji kwa wanahabari makundi yote wakiwemo wa mitandao ya kijamii hadi utakapo kuwepo uhuru kamili wa vyombo vya habari. "...Tulifanya hivyo kwa mauaji yalipotokea na tutaendelea kufanya hivyo siku zote watakapo kamatwa na kupigwa wakiwa kazini...Tunajua huenda haitoshi lakini hii ni kutokana na tofauti mbalimbali za kiutendaji," alisema Balozi Cerianse .

Bregondi. Alisema kupinga unyanyasaji kwa wanahabari haina maana wanachoandika wanahabari mara zote ni cha kweli lakini ipo namna nzuri ya kushughulikia mvutano kama huo na kusaidia kupata taarifa za kina zaidi zitakazofikia muafaka. Aidha kwa upande wake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo alisema Tanzania inaongoza Afrika kwa kushindwa kuweka utaratibu mzuri wa udhibiti mawasiliano.

 Alisema vyombo vya habari ni muhimu katika taifa na hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Taifa unaotarajia kufanyika Oktoba, alisema vyombo vya habari vinaweza kubomoa au kujenga taifa lolote. "...Waandishi ni watu muhimu katika kudumisha demokrasia nchini hivyo kuna kila sababu ya kuendelea kujifunza zaidi. 

 Maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani kitaifa yamefanyika mkoani Morogoro na kuhudhuriwa na wanahabari mbalimbali, wakongwe, wadau anuai wa vyombo vya habari huku yakiwa na kauli mbiu ya Usalama wa Vyombo vya Habari katika Dijitali: Uhandishi Mzuri unaozingatia, Usawa wa Kijinsia na faragha.Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalon Kibanda akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalon Kibanda akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Maelezo, Assah Mwambene akizungumza katika maadhimio hayo.Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Maelezo, Assah Mwambene akizungumza katika maadhimio hayo.Mwanahabari na Bloga, Majid Mjengwa akizungumza katika mkutano huo.Mwanahabari na Bloga, Majid Mjengwa akizungumza katika mkutano huo.Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Mello akizungumza.Mkurugenzi wa Jamii Media, Maxence Mello akizungumza.
Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Na Joachim Mushi.

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza katika maadhimisho ya Uhuru wa habari duniani yaliyofanyika mkoani Morogoro. Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza katika maadhimisho ya Uhuru wa habari duniani yaliyofanyika mkoani Morogoro.Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Filiberto Sebregondi akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Filiberto Sebregondi akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.
Kaimu Meneja wa Uhuru FM, Angela Akilimali (kulia) pamoja na wadau wa vyombo vya habari katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani.Kaimu Meneja wa Uhuru FM, Angela Akilimali (kulia) pamoja na wadau wa vyombo vya habari katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani.Kutoka kushoto ni Mshauri wa Masuala ya Habari Umoja wa Ulaya, Susane Mbise na Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Umoja wa Mataifa (UN), Hoyce Temu akifuatilia mijadala katika mkutano huo.Kutoka kushoto ni Mshauri wa Masuala ya Habari Umoja wa Ulaya, Susane Mbise na Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Umoja wa Mataifa (UN), Hoyce Temu akifuatilia mijadala katika mkutano huo.

WAZAZI WACHANGIA SHULE YA UFUNDI IFUNDA

$
0
0
 Mdau wa maendeleo, Jackson Kiswaga (mwenye skafu) akiwakabidhi moja ya mabati 50 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Ufundi ya Ifunda kwa ajili ya ukarabati wa jengo la taaluma na nidhamu lilounguamwaka 2013 katika shule hiyo.(picha na Denis Mlowe)

 Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini Jackson Kiswaga akikabidhi cheti kwa mhitimu wa shule ya shule ya sekondari ya Ufundi ya Ifunda kidato cha sita.(picha na Denis Mlowe). 

 Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini Jackson Kiswaga akikagua gwaride wa skauti wa shule ya shule ya sekondari ya Ufundi ya Ifunda

 Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini Jackson Kiswaga akizungumza wanafunzi na wazazi wa shule ya shule ya sekondari ya Ufundi ya Ifunda

Mkurugenzi wa Tigo Nyanda za Juu Kusini Jackson Kiswaga akivishwa skafu na moja ya skauti wa shule ya sekondari ya Ufundi ya Ifunda.



NA DENIS MLOWE, IFUNDA


WAZAZI wa wanafunzi wanaosoma shule ya sekondari ya Ufundi ya Ifunda iliyoko wilaya ya Iringa wamechangia mifuko ya saruji na misumari kwa ajili ya kuunga mkono ukarabati wa jengo la taaluma na nidhamu liloungua katika shule hiyo mchango wenye thamani ya shilingi 600,000.


Michango hiyo ambayo ilijumuisha fedha taslimu kwa lengo la kununua saruji na misumari ilitokana na juhudi za mgeni rasmi Jackson Kiswaga wa mahafari ya 14 ya shule hiyo ya kidato cha sita kuhamasisha ujenzi wa jengo hilo baada ya taarifa kutoka kwa mkuu wa shule Madi Kissuu aliyotoa kwa wazazi na kukabiliwa na changamoto ya ujenzi baada ya kuungua kwa moto.


Akizungumza katika mahafari hayo, Kiswaga ambaye alichangia mabati 50 papo hapo ili zisaidie katika ukarabati wa jengo hilo lililoungua moto mwaka 2013 alisema kuwa jukumu la uchangiaji wa sekta ya elimu sio kuachiwa serikali bali la kila mzazi anayependa maendeleo ya elimu katika nchi ya Tanzania.

  
Alisema wanafunzi ni lazima wasome kwa bidii ili watengeneze maisha yao ya baadaye kwani elimu ndio urithi pekee usiofananishwa na mali zingine za dunia kwani ni wa kudumu katika maisha yote ya binadamu hivyo juhudi ya mzazi kumuunga mkono mtoto katika kupata elimu iliyo bora na katika mazingira rafiki kwa mwanafunzi.


Kiswaga aliwataka wanafunzi hao kuacha tabia hatarishi zikiwemo utoro, uzinzi, ulevi na kila aina ya mambo yanayorudisha nyuma uelewa wao katika masomo shuleni hapo.


 “Hakuna mtu mjinga dunia kama sio kichaa au una tatizo la ubongo. Kumbukeni kuwa MUNGU aliweka masaa 24 na kila mmoja akitumia saa 24 kwa uhakika katika maisha yake lazima kuna mambo ambayo atafanya kuweza kujiletea maendeleo yake na wanafunzi pia mna masaa hayo hayo ni wakati wako sasa kuamua unataka kuwa nani kesho na njia pekee ni kushikilia masomo na hapo ndipo ukichagua yaliyo mazuri unaweza kubadilisha maisha yako na ya jamii inayomzunguka,” alisema.


Alisema Tanzania inahitaji wasomi ili ijiletee maendeleo na kushindana kiuchumi na nchi nyingine hivyo ni muhimu wanafunzi wakaendelea kuhimili vikwazo wakati wakitafuta elimu zao.


Kwa upande wake Mchungaji Kedi Patrick kutoka nchini Uganda aliyeambatana na mgeni rasmi Jackson Kiswaga, aliwataka wazazi na wanafunzi kutambua kuwa elimu ndio chanzo kikubwa cha mabadiliko katika taifa lolote hapa duniani.


Alisema kuwa urithi pekee kwa watoto ni elimu na kusisitiza kuwa unaweza kumwachia mali, lakini itakwisha, ukimwachia elimu hakika huu ndiyo urithi pekee.


Naye mkuu wa shule hiyo, Madi Kissu alisema kuwa shule hiyo inakabiliwa na changomoto nyingi zinazohitaji juhudi za pamoja kuzitatua hasa katika uchakavu wa majengo na kukosekanika kwa walimu wa masomo ya sayansi.


Katika mahafari hayo ya 14 jumla ya wanafunzi 324 wanatarajia kumaliza elimu ya kidato cha sita yaliambatana na gwaride la heshima lilotolewa na skauti wa shule hiyo sambamba na kukabidhiwa vyeti kwa wanafunzi wote na zawadi kwa walimu waliofanya vizuri katika kufaulisha masomo yao.



MAHAFALI YA NANE YA CHUO CHA WAALIMU WA SHULE ZA AWALI CHA NEW MONTESSORI TEACHERS COLLEGE YALIVYOFANA

$
0
0
 Muhitimu Crasiana Laurence akikata keki maalumu ya 
mahafali hayo.
 Mgeni rasmi, Haris Kapiga akimkabidhi cheti mmhitimu, 
Violet William.
  Mgeni rasmi, Haris Kapiga akimkabidhi cheti muhitimu, 
Edina Adamu.
Wahitimu wa Chuo cha Ualimu wa Shule za Awali katika chuo cha New Montesorri wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo hicho pamoja na wageni waalikwa huku wakiwa na vyeti vyao kwenye mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika Dar es Salaam jana.  
Mkurugenzi Mtendaji na Mkuu wa Chuo hicho, Denis Msangi akizungumza na wahitimu katika mahafali hayo yaliyofanyika Shule ya Msingi ya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.
 Mgeni rasmi katika mahafali hayo, Haris Kapiga akisisitiza jambo wakati akizungumza na wahitimu hao wapatao 45.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Hildelly Solution (T) Ltd, Hilda Ngaga, akizungumza katika mahafali hayo.
 Wahitimu wakiwa katika mahafali hayo.

 Wageni waalikwa na ndugu na jamaa wa wahitimu hao wakifuatilia kwa karibu matukio yote katika mahafali hayo.
 Wahitimu.

 Katibu Muhtasi wa Chuo hicho, Shakila Ramadhan akizungumza na wahitimu hao.(Imeandaliwa na mtandao wa http://www.habarizajamii.com/)

Umoja wa Ulaya, UN; Tutapigania Uhuru wa Habari Siku Zote

$
0
0
Na Joachim Mushi, Morogoro 

UMOJA wa Nchi za Ulaya nchini Tanzania (EU) umepinga vikali vitendo vya kikatili na unyanyasaji wameokuwa wakifanyiwa na vyombo vya dola vya Serikali wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao ambapo ilitokea mwanahabari mmoja kuuwawa. Alisema hawatachoka kukemea matukio hayo ya unyanyasaji kwani yanafifisha uhuru wa habari.

Akizungumza leo mjini Morogoro katika Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, Kiongozi Mkuu wa Mabalozi hao, Balozi Filiberto Cerianse Bregondi alisema EU itaendelea kupinga namna yoyote ya unyanyasaji kwa wanahabari makundi yote wakiwemo wa mitandao ya kijamii hadi utakapo kuwepo uhuru kamili wa vyombo vya habari. "...Tulifanya hivyo kwa mauaji yalipotokea na tutaendelea kufanya hivyo siku zote watakapo kamatwa na kupigwa wakiwa kazini...Tunajua huenda haitoshi lakini hii ni kutokana na tofauti mbalimbali za kiutendaji," alisema Balozi Cerianse Bregondi. 

Alisema kupinga unyanyasaji kwa wanahabari haina maana wanachoandika wanahabari mara zote ni cha kweli lakini ipo namna nzuri ya kushughulikia mvutano kama huo na kusaidia kupata taarifa za kina zaidi zitakazofikia muafaka. Aidha kwa upande wake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo alisema Tanzania inaongoza Afrika kwa kushindwa kuweka utaratibu mzuri wa udhibiti mawasiliano. 

Alisema vyombo vya habari ni muhimu katika taifa na hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Taifa unaotarajia kufanyika Oktoba, alisema vyombo vya habari vinaweza kubomoa au kujenga taifa lolote. "...Waandishi ni watu muhimu katika kudumisha demokrasia nchini hivyo kuna kila sababu ya kuendelea kujifunza zaidi. 

Maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari duniani kitaifa yamefanyika mkoani Morogoro na kuhudhuriwa na wanahabari mbalimbali, wakongwe, wadau anuai wa vyombo vya habari huku yakiwa na kauli mbiu ya Usalama wa Vyombo vya Habari katika Dijitali: Uhandishi Mzuri unaozingatia, Usawa wa Kijinsia na faragha.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza katika maadhimisho ya Uhuru wa habari duniani yaliyofanyika mkoani Morogoro. Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza katika maadhimisho ya Uhuru wa habari duniani yaliyofanyika mkoani Morogoro.Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Filiberto Sebregondi akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani. Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Filiberto Sebregondi akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani..Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani. Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani.

TAARIFA KWA UMMA :UFAFANUZI JUU YA KANUNI YA UWIANISHAJI WA MAFAO YA PENSHENI 2014


ZARI ALL-WHITE PARTY ILIVYOFANA MWISHONI MWA WIKI.

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platinumz ambaye ni balozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzania akiimba jukwaani Zari White Party iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. App hiyo inawaletea wateja burudani ya muziki kiganjani. Picha zote na Cathbert Angelo Kajuna wa Kajunason Blog.
Mchumba wa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platinum... Bibie Zari the bossylady akiwashukuru Watanzania waliofika katika Zari White Party lililofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.

Umati wa Watanzania waliohudhuria katika Zari White Party lililofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mmoja ya vingozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzania akitoa maelezo machache kwa wateja waliofika katika Zari White Party iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. App hiyo inawaletea wateja burudani ya muziki kiganjani.
Msanii wa Kizazi Kipya, Nikki wa Pili kutoka kundi la Weusi akipozi katika zuria jekundu.
Msanii Shetta nae hakuwa nyuma kushow love mbele ya zuria jekundu.

Wafanyakazi wa Vodacom wakiwa amepozi katika zuria jekundu.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platinumz ambaye ni balozi wa Mziiki ambayo ni program ya simu za mkononi (mobile app) ya Vodacom Tanzania akiwa amepozi na mkewe mtarajiwa Zari katika Zari White Party iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Waliopo pembeni ni Madame Ritha, Msanii Ney Wa Mitego. Wengine ni Msanii A.K.A (kushoto) toka nchini Afrika Kusini.
---
Mziiki ni huduma ya muziki ya Afrika ambayo inatoa huduma hiyo kwa muziki wa kitaifa na kimataifa, inajivunia kwa kiasi kikubwa kuwa sehemu ya wadhamini wa pati ya Zari All-White party iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mziiki ni sehemu ya kuendeleza wasanii wa ndani na nje ya Afrika ambapo watumiaji wa simu za smartphones za Android, iOS na BlackBerry wanapata nafasi ya kusikiliza nyimbo mbalimbali kwa kupitia simu zao za mkononi.Wateja wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom kwa kutumia intaneti ya wi-fi wanaweza kuperuzi na kupata nyimbo ambazo wanaweza pia kuziweka katika miito yao ya simu pia kuzisambaza kwa rafiki zao bure kwa kipindi cha mwezi mzima ambao ni ofa.

Huduma hii inapatikana katika vifurushi vyote vya Lite na Premium, na huduma ya Lite inapatikana pia kwa watumiaji wote wa mtandao wa wi-fi ambao wanaweza pia kuperuzi moja kwa moja bila malipo yoyote kila mahali mtandao wa Vodacom unapopatikana. Tangu Mziiki izinduliwe mwezi Mei mwaka jana, imefanikiwa kuingiza zaidi ya wasanii 1000 wa Afrika ambao wanafanya vizuri mpaka sasa.

Huduma hii imechaguliwa sana kwa ajili ya kuhakikisha Waafrika wanafurahia muziki wao ambapo inaendelezwa na Spice Africa, na ilianzia Tanzania lakini kwa sasa inazidi kukua katika nchi mbalimbali.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Spice Africa, Arun Nagar, alisema ‘Huduma ya hii ya kidijitali inalenga zaidi kuibua vipaji katika nchi za ukanda wa Jangwa la Sahara Afrika ambapo pia ni nafasi nzuri kwa wasanii mbalimbali kutangaza kazi zao’.

‘Tunajivunia kuwa sehemu ya wadhamini wa sherehe za Zari-White Party ambapo pia tuna imani kuwa Watanzania wengi watazidi kufurahia huduma zetu’ Nagar aliongeza kuwa Mziiki ni huduma ambayo inapatikana kirahisi mno kwa kutumia simu za mkononi kwa kupata huduma ya muziki wa wasanii wa ndani na nje ya Afrika.

Diamond Platnumz, ambaye ni balozi wa Mziiki Tanzania, alisema ‘Mziiki imekuwa katika nafasi ya kutoa kipaumbele kwa wasanii mbalimbali kwa ajili ya kupata changamoto kwa wasanii wakubwa kitaifa na kimataifa’ “Muziki wetu umezidi kufanya vizuri katika nchi mbalimbali, na Mziiki inatoa ofa kwa wadau mbalimbali wa muziki kusikiliza nyimbo wanazozipenda kwa kupitia katika viganja vyao,” alisema Diamond Platnumz.

Burudani mbalimbali zilizotolewa katika sherehe hizo za Zari White Party ikiwa ni pamoja na muziki kutoka kwa DJ, muziki wa live kutoka kwa wasanii kama vile Diamond Platnumz na Shetta wakati msanii mwalikwa atakua AKA, kutoka Afrika Kusini.

Zari All-White Party 2015 imedhaminiwa na Vodacom na Mziiki kwa kushirikiana na SK Entertainment, Clouds Entertainment, Prime Time Promotions, Johnny Walker Gold label ( Serengeti Breweries) ambapo ilianza The All-White Parties mwaka 2009 nchini Uganda na Tanzania inafanyika mwaka huu kwa mara ya kwanza.

Kasi ya Utekelezaji miradi ya NHC Mtwara yafurahisha bodi ya shirika hilo

$
0
0
Mkurugenzi wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa, Subira Mchumo akielekeza jambo wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye mradi wa nyumba za gharama nafuu Masasi, mkoani Mtwara ambapo pamoja na mambo mengine amesifu kasi ya ujezi wa nyumba hizo unaozingatia viwango na muda na akawataka wafanyakazi wa NHC kuchapa kazi ili kufikia malengo yao waliyojiwekea. Kulia ni Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maagi, wa pili ni Eliaisa Keenja wa NHC, Meneja wa NHC mkoa wa Mtwara, Joseph John na Injinia wa mradi huo Leonard Kazoba.
Mkurugenzi wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa, Subira Mchumo akimsikiliza Mhandisi wa mradi huo Leonard Kazoba wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye mradi wa nyumba za gharama nafuu Masasi, mkoani Mtwara.
Mkurugenzi wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa, Subira Mchumo akimsikiliza Mhandisi wa mradi huo Leonard Kazoba wakati wa ziara yake aliyoifanya kwenye mradi wa nyumba za gharama nafuu Masasi, mkoani Mtwara.
Baadhi ya Nyumba za gharama nafuu  zilizoko mkoani Mtwara.

MDAU ADAM MZEE ALIVYOUKACHA UKAPERA MWISHONI MWA WIKI JIJINI DAR.

$
0
0
Mr &Mrs.Adam Mzee.
 Mrs.Adam Mzee  mara baada kufunga pingu za maisha.
 Marafiki wakiwa katika picha ya pamoja na maharusi,waliosimama kutoka kushoto ni,Merry Geofrey,Sheila Simba,Hafidh Kido ,John Bukuku,Suleiman Mwenda,Micky, Said Mwishehe,Sharifa,Neema Mwangomo,Abdala Kiluke,Mringi Petro ,katika Harusi ya Adam Mzee iliyofanyika katika Ukumbi wa Kivukoni,Serena Hotel.

Adam Mzee ni mtumishi wa Chama Cha Mapinduzi Makao Makuu ,Idara ya Itikadi na Uenezi,na ni mmiliki wa  blog maarufu ya Kamerayangu na Lilian ni mtumishi wa NMB Makao Makuu.
 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi,Ndugu Abdurahman Kinana wa pili kulia,na Katibu wa Nec,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wa tatu kutoka kushoto,wakiwa na Mr & Mrs Mzee.
 Maharusi wakituzwa na Ndugu na marafiki wakati wakutoa zawadi.
 Maharusi wakiwa na wapambe wao,katika picha ya pamoja na wanakamati walipoenda kutoa zawadi na kuwapogeza maharusi.

NHIF YASHAURIWA KUTOA HUDUMA NJE YA NCHI

$
0
0

anayetoa maelezo  ni afisa matekelezo wa NHIF mkoa Arusha, Desderius Buhiye  
muongoza watalii Julius Mwenda akiuliza swali juu ya mfuko huo, utakavyowasaidia wakiwa nje ya mkoa.

  Mfuko wa Taifa wa bima ya Afya(NHIF), umeshauriwa kuanzisha utaratibu wa kuingia ubia na hospitali za nchi jirani, ili kuwawezesha wanachama wake, kupata huduma bora za matibabu wakiwa nje ya nchi.

Wito huo, ulitolewa  na wanachama wa chama cha waongoza watalii Tanzania(TTGA),katika semina ya kupatiwa elimu juu  huduma za mfuko huo, kuhusiana na fao jipya la wanavikundi.

Raphael Njavu alisema, wao kama waongoza watalii wamekuwa wakifanyakazi hadi nje ya nchi, hasa nchi jirani hivyo mfuko huo, utazame uwezeno wa kuingia ubia na hospitali za nje.

"kama sio ubia basi NHIF ijitahidi kuboresha hospitali za wilaya za mipakani ni   ili wanachama waweze kupata huduma bora badala ya kulazimika kurudi mijini"alisema.

Hata hivyo, Afisa matekelezo mfuko wa NHIF mkoa wa Arusha, Desderius Bushiye akijibu hoja hiyo, alisema mfuko huo unaendelea kuboresha huduma za afya  na sasa hospitali nyingi hata za mipakani zimekuwa zikitoa huduma za bima.

"kwa wale ambao wanasafiri wilaya zote mfuko unatoa huduma na   hata Zanzibar kuna hospitali kubwa ambazo zinatoa huduma kwa wanachama wa mfuko wa taifa wa bima ya afya"alisema.

Alisema mfuko wa Taifa ya bima ya afya, umeanzisha utaratibu wa kuwapa  uanachama wanachama wa vikundi, kwa kulipia Tsh 76,800 kwa mwaka ili kuhakikisha watanzania wengi wanakuwa na uhakika wa kupata huduma bora za afya popote walipo nchini.

Awali Katibu Mkuu wa TTGA  Emmanuel Mollel alisema wanachama wake, wamekubali kujiunga na mfuko huo, ili kuwa na uhakika wa kupata huduma za afya popote walipo nchini.
"sisi kama chama tumekubali kujiunga na NHIF na tunauhakika sasa wanachama wetu watatoa huduma bora kwa watalii wakiwa na afya njema"alisema.


habari kwa hisani ya libeneke la kaskazini blog

KATIBU MKUU WA UVCCM SIXTUS MAPUNDA AHARIBU MIPANGO YA WAPINZANI MKOANI IRINGA

$
0
0


 katibu mkuu wa uvccm taifa sixtus mapunda akiwapa maneno ya kishujaa wakazi wa mkoa wa iringa
 juliana shonza akiwahutubia wananchi wa mkoa wa iringa
 viongozi chama cha mapinduzi wakiwa katika meza wakifuatia mkutano unavyoendele

na fredy mgunda,iringa.

katibu mkuu wa uvccm taifa afanya ziara ya jimbo la kilolo kwa lengo la kukijenga chama  na kuangalia maendeleoya chama hicho  hasa ngazi vijana lakini akiwa katika ziara hiyo aliongozana na mwenyeji wake   katibu wa uvccm mkoa wa iringa.

akihutubia wakati wa mkutano uliofanyika katika kijiji cha kitumbuka kata ya ilole katibu wa uvccm mkoa wa iringa elisha mwampashi aliwataka wanachama wa chama hicho kuondoa unyonge dhidi ya wapinzani wake kwa kuwaambia ukweli wananchi juu ya maendeleo yanayofanywa na chama hicho.

aidha mwampashe amesema kuwa ifike wakati viongizi wa chama hicho kuacha kujidanganya kwa kuwapa taarifa viongozi  za matumaini juu ya maendeleo ya chama hicho. “tunatakiwa tubadilika sasa kwa kuwapa taarifa za ukweli viongozi wetu ili wanapoondoka wajue  nini cha kufanya ili kuondoa dosari ambazo zinzkuwa zikijitokeza,tuenaelekea kwenye uchaguzi mkuu ambao utafanyika hapo “alisema mwampashe

kwa upande wake katibu wa uvccm taifa  sixtus mapunda amewapongeza wananchi na wanachama wa tarafa ya ilole kwa ujumla  kwa ushindi walioupata wakati wa serikali za mitaa ambao unaashilia chama hicho kuendelea kupendwa kata tarafa hiyo.

lakini mapunda aliwatoa hofu wananchi wa kijiji cha kitumbuka kwa kusema amesikia na kujionea baadhi ya matatizo yanayoikabili kata ya ilole na kuwaahidi kuyafikisha kwa mbunge wao na kutafuta njia ya kuyatatua kwa kuwa profesa petter msola ni msikivu.

“tatizo la kufikisha nguzo za umeme katika eneo hili ni tatizo dogo ambalo linatatulika kwa haraka na kuwaahidi wananchi kulifanyia kazi mapema ,suala la barabara alisema kuwa amejionea yeye mwenyewe kuwa  si nzuri na inahatarisha maisha kwa kuwa pindi mvua itakaponyesha barabara hiyo itakuwa kama mto”.alisema mapunda.



ALIYEKUWA  kada maarufu  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema ) Taifa Juliana Shonza ambae alijiuzulu na chama hicho na kijiunga na CCM amewataka wakazi wa jimbo la Iringa mjini kuungana kulipokea jimbo kutoka kwa mbunge Mch Peter Msigwa.

Shonza ametoa kauli hiyo leo wakati akiwahutubia wakazi wa jimbo la Iringa mjini wakati wa mkutano wa uzinduzi wa matawi unaofanywa na katibu mkuu wa Uvccm Taifa sixtus Mapunda.

Alisema jimbo la Iringa mjini ni jimbo ambalo wananchi walichagua mbunge kwa hasira na kuwa badala ya kutegemea maendeleo wamejikuta wakifanya maandamano yasiyo na kikomo kila uchwao.

Shonza alisema kuwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini amekuwa ni mtu wa kujipigania mwenyewe kimaisha badala ya kujishughulisha kuwaletea wananchi maendeleo.

Hivyo alisema ni vema wananchi wa Iringa mjini kujipanga kwa hafla ya kulipokea jimbo hilo kutoka kwa mpangaji mbunge Msigwa aliyepanga bila kujua kama kapangishwa hivyo kushindwa kulipa kodi.

Akielezea juu ya hofu ya muungano wa vyama vinavyounda katiba ya wananchi (ukawa) alisema kuwa Chadema ni chama ambachokinataka kupanda kupitia ukawa.

Kwani alisema Chadema ndio chama kilichokituhumu CUF kuwa ni CCM  B na kuwa ni chama cha kishoga imekuwa leo kuungana 

Hivyo kuwataka watanzania kupima na kutoa maamuzi magumu pindi uchaguzi utakapo fika.

Nae mjumbe wa kamati ya utekelezaji Uvccm Taifa Secky Kasuga alisema wananchi wa jimbo la Iringa walianzimisha jimbo hilo na sasa mwenye Nyumba anahitaji Nyumba Yake hivyo lazima mpangaji kuondoka.

"Tunalazimika kuchukua Nyumba yetu baada ya mpangaji kushindwa kufagia nyumba"

Katibu mkuu wa UVccm Taifa Sixtus Mapunda alisema kilio cha maendeleo kwa jimbo la Iringa kimetokana na mchanganyo uliofanywa na wananchi kwa kumchagua mbunge mrudisha nyuma maendeleo.

Alisema mbunge amekuwa kikwazo kikubwa kwani bungeni wakati wa vikao vya bajeti yeye anatoka nje ya bunge na wakati wa vikao vya kupanga shughuli za maendeleo halmashauri yeye anashiriki kuita maandamano.

" Tunawaombeni wana Iringa mtusaidie kurejesha jimbo kwa kumtoa mbunge mpinga maendeleo katika jimbo la Iringa mjini ambalo maendeleo yanaletwa kwa nguvu na ccm"

Bw Mapunda asema anawashangaa wapinzani kwa kuikataa katibu inayopendekezwa ambayo unazungumzia pia Haki ya kuishi hivyo  kupinga Kwao wanapinga hadi haki ya wao kuishi.

Alisema kuwa hoja Yao ni kutaka serikali tatu na si vinginevyo na kuwa wananchi lazima wapigie kura ya ndio katiba hiyo na pindi muda wa serikali tatu utakapofika basi itafanyika hivyo na si sasa.

Kuwa kuutaka utanganyika ni kuutaka ukoloni hivyo lazima kujitambua kuwa wakati wa kuongozwa na wakaloni umepita.





MAALIM SEIF SHARIFF AKABIDHIWA PESA ZA KUGOMBEA URAIS-ZANZIBAR

$
0
0
 
  Mwenyekiti wa CUF zoni ya Mjini Unguja Massoud Khamis, akimkabidhi fedha taslim Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, ili aweze kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar wakati utakapofika.
  Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akionyesha fedha alizokabidhiwa kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea urais.
 Mwenyekiti wa CUF zoni ya Mjini Unguja Massoud Khamis, akimkabidhi Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, cheti cha heshima kutokana na uongozi wake.

Baadhi ya viongozi na wanachama wa CUF waliojitokeza katika hafla ya kumkabidhi fedha Maalim Seif iliyofanyika nyumbani kwake Mbweni. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar)
====================
Uongozi wa Zoni ya Mjini wa Chama cha Wananchi CUF umemkabidhi Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Shariff Hamad Shl.Million mbili na Laki tano kwa ajili ya kuchukua Fomu ya kugombea Nafasi ya Urais Zanzibar wakati utakapofika.

Hafla ya kukabudhi Fedha hizo ilifanyia Jioni ya Jana Nyumbani kwa Maalim Seif Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar na kuhudhuriwa na Viongozi mbali mbali wa Chama hicho.

Akikabidhi Fedha hizo Mwenyekiti wa Zoni ya Majini Masoud Khamis alisema wameamua kumlipia Kiongozi huyo baada ya kutangaza nia yake ya kugombea katika nafasi hiyo.

Aidha alisema kuwa wapo baadhi ya Watu wanadai Maalim Seif hatakiwi kugombea Nafasi hiyo kutokana na kujilipia Fomu kwa Pesa zake hivyo wameona ipo haja ya kumlipia ili kuonesha Mapenzi ya dhati kwake.

"Wanasema wewe Maalim hutakiwi unajitakisha ndio maana kila ufikapo muda wa uchaguzi Unajilipia Fomu mwenyewe kwa hiyo tunawajibu kuwa wewe ni chaguo letu na ni Mtu wa Watu" Alisema Mwenyekiti huyo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad, amesisiza nia yake ya kugombea tena nafasi ya Urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu ujao.

Maalim Seif ameishukuru kamati hiyo kwa uamuzi wa busara waliochukua, hali inayoonyesha kuwa wananchi wa Zanzibar wanaendelea kuwa na imani naye kutokana na mwelekeo wake wa kutaka kuleta mabadiliko ya kweli kwa Zanzibar.

Amesema iwapo wananchi watakipa ridhaa Chama hicho kuongoza Serikali ya Umoja wa Kitaifa baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu,  kitatandika misingi imara ya utawala bora, uchumi na kuendeleza umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.

Ameyataja mambo mengine ya msingi kuwa ni pamoja na kurejesha heshima ya Zanzibar katika jamii ya Kimataifa, kuimarisha huduma za kijamii ziliwemo afya na elimu, pamoja kuandaa mazingira ya kuongeza ajira kwa vijana.

Amesema tofauti na chaguzi zilizopita, Chama hicho kimejiandaa vizuri kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao, na kuwaomba wananchi waendelee kukiunga mkono ili kiweze kupata ushindi mkubwa na kuweza kuongoza serikali.

Mapema akisoma risala ya kamati maalum ya (CUF) zoni ya mjini, mjumbe wa kamati hiyo Bw. Salim Abdallah Salim amesema wameamua kumdhamini Maalim Seif kutokana na utendaji wake ndani ya chama hicho pamoja na matumaini aliyonayo kwa Wanzibari.

Aidha kamati hiyo imetoa tamko rasmi la kumuunga mkono Maalim Seif kugombea nafasi ya Urais wa Zanzibar wakati utakapofika, na kutoa wito kwa vijana kutafuta vitambulisho vya Mzanzibar Mkaazi (ZAN ID) na kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao.

NEWS ALERT: BALOZI MULAMULA ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, BALOZI SIMBA NAIBU WAKE

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Balozi Liberata Rutageruka Mulamula (kulia) kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 

Kwa sasa Balozi Mulamula ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico.


Rais Kikwete pia amemteua Balozi Hassan Simba Yahya (chini) kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara hiyo  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.  



Kwa sasa Balozi Yahya ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Wizarani hapo.


Uteuzi huu umeanza tarehe 2 Mei, 2015


Imetolewa na;
Premi Kibanga,

Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,

Ikulu - Dar es Salaam.


4 Mei, 2015

MAMA SALMA KIKWETE AHUDHURIA TAMASHA LA ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIJANA KATIKA SHULE YA SEKONDARI WAMA NAKAYAMA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akimpokea Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete wakati alipowasili kwenye uwanja wa mpira wa Shule ya Sekondari Nyamisati iliyoko wilayani Rufiji kwa helicopter tarehe 2.5.2015. Mama Salma alikwenda Rufiji kwenye tamasha la Elimu ya Afya ya Uzazi kwa vijana katika Shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama ambayo inamilikiwa na Taasisi ya WAMA ambapo Mkuu wa Mkoa wa Pwani alikuwa Mgeni Rasmi.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa WAMA Mheshimiwa Zakhia Meghji (kushoto) wakiingia kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari Nwama-Nakayama kuhudhuria Tamasha la Elimu ya Afya ya Uzazi kwa Vijana wa Shule hiyo tarehe 2.5.2015.

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM SAID MECK SADIKI MGENI RASMI MAADHIMISHO YA WIKI YA CHANJO TANZANIA

$
0
0
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki akiongea na wananchi mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Chanjo Tanzania Mkoa wa Dar es Salaam ambapo aliwataka wananchi kujitokeza kwawingi kupata chanjo hiyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said  Meck Sadiki akiongea na wananchi mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Chanjo Tanzania Mkoa wa Dar es Salaam ambapo aliwataka wananchi kujitokeza kwawingi kupata chanjo hiyo, kushoto ni  Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema.
 Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema akiongea na wananchi mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Chanjo Tanzania Mkoa wa Dar es Salaam
 Wasanii wa kikundi cha  Hamasa wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa  alipokuwa akiongea na mananchi walio jitokeza katika Maadhimisho ya Wiki ya Chanjo Tanzania Mkoa wa Dar es Salaam  katika viwanja vya Zakhiem.

Mtoto Mbahi Simon (Miezi 2), aliyepagatwa na mama yake Joyce Joseph(30), mkazi wa Charambe akipatiwa chanjo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Sadick katika maadhimisho ya wiki ya chanjo Tanzania, yaliyofanyika viwanja vya Mbagala   Zakhiem Jijini Dar es Salaam.
 Mtoto Najath Husein akishikwa kwa uangalifu na mama yake Asia Omary wakati alopokuwa akipatia Chanjo ya Pepopunda na Muuguzi.
Baadhi ya Wananchi waliojitokeza
 Mganga Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, mama Mugisha kulia.akiwaongoza Viongozi malimbali kwenda katika Banda maalumu lililo andaliwa kwa Mkuu wa Mkoa kuwapatia chanjo watoto waliofika katika maadhimisho hayo kupatiwa chanjo.
Mjomba Band ikitoa burudadani wakati Maadhimisho hayo (PICHA ZOTE  NA KHAMISI MUSSA).

……………………………………………………………..
SALHA MOHAMED
 
“KINGA ni bora kuliko tiba,”. Hii ni moja ya misemo ambayo watanzania wengi hupenda kuitumia pale ambapo kuna tahadhari au uhitaji wa jambo fulani kufanyika ili kuepusha janga fulani.
Hali hiyo inakuja pale tu mtu huyo kushindwa kupata huduma za afya hadi anapozidiwa kwa ugonjwa fulani ndipo apate tiba kwa daktari.Chanjo ni silaha kali katika kinga na udhibiti wa magonjwa ya maambukizi,

Kutumia chanjo kwa kinga na udhibiti wa magonjwa ya maambukizi kwa kutumia chanjo ni mafanikio makubwa waliyoyapata binadamu katika mapambano dhidi ya magonjwa ya maambukizi.Naweza kusema kuwa chanjo ni dawa inayotengenezwa kwa kutumia vijidudu au virusi vinavyosababisha magonjwa ya maambukizi, na virusi hivyo vikiingia kwenye mwili wa binadamu, mwili huo utatoa kitu fulani ambacho kinaweza kuzuia virusi hivyo visiingie tena mwilini.
Watu wengi wamekuwa wakisema chanjo husababisha magonjwa mbalimbali, hiyo siyo kweli, chanjo haisababishi magonjwa katika mwili wa binadamu bali inaweza kulinda afya ya binadamu kutokana na maradhi mbalimbali kutokana na maradhi.
Kutokana na umuhimu wa chanjo katika kinga ya mwili na udhibiti wa magonjwa ya maambukizi, nchi mbalimbali duniani zinatilia maanani sana kazi ya kutoa chanjo.
Tanzania ni mojawapo ya nchi hizo ambapo hivi karibuni Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Said Sadick, ameadhimisha kilele cha wiki ya chanjo Tanzania ambayo huadhimisha Afrika nzima na lengo ni kuhamiasha jamii kutumia huduma za chanjo.
Hakika ni jambo la kujivunia kwani mikakati na juhudi zinazofanywa na Wizara kupitia mpango wa Taifa wa chanjo katika kupunguza magonjwa na vifo vya watoto vinavyozuilika kwa chanjo.
Sadick anasema Kiwango cha matumizi ya chanjo kwa watoto ni zaidi ya asilimia 100 kwa sababu watumishi wamekuwa wakichanja watoto hata nje ya mkoa wa Dar es Salaam.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo inasema chanjo ni zawadi ya maisha, pia imethibitika kuwa chanjo ni mkakati muafaka katika kutokomeza magonjwa na kupunguza vifo vya watoto na kupunguza gharama za matibabu.
“Takwimu za kitaalamu zimethibitisha kuwa chanjo huzuia takribani vifo milioni 2 hadi 3 kila mwaka vinavyotokana na maradhi yanayozuilika kwa chanjo duniani,
“Mtakumbuka 1990, tulishuhudia wodi za surua zikifungwa na vifo kupungua na pia kupooza kutokana na polio kutoweka, hivi leo, kuna watu hawajawahi kuona mgonjwa wa polio alivyo,” alisema
Anasema mafanikio hayo ni matokeo ya kuwekeza katika chanjo ambapo jumla ya watoto 1,682,015 kati ya 1,733,967 ambayo ni sawa na asilimia 97 ya watoto walio na umri wa chini ya mwaka mmoja kwa 2014 walipata chanjo.
Anafafanua kuwa mafanikio hayo yametokana na serikali kufanikiwa kutoa chanjo kwa watoto walengwa kiasi cha kufikia asilimia 90 ya kiwango cha chanjo kinachokubalika kitaifa na kimataifa kwa watoto walio chini ya mwaka mmoja.
Anaongeza kuwa bado kuna changamoto ya watoto ambao hawajapata au hawajakamilisha ratiba ya chanjo kulingana na umri wao, ambapo watoto hawa wapo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa na kuhatarisha afya ya jamii nzima.
“Magonjwa yanayolengwa na mpango wa Taifa wa chanjo kwa sasa ni Kifua kikuu, Dondakoo, Kifaduro, Polio, Surua, Rubella, Pepopunda, Homa ya ini, Homa ya uti wa mgongo, Kichomi, Kuhara na Saratani ya mlango wa kizazi,” alisema Sadick
Ili kulinda vizuri afya ya binadamu, hivi sasa, wanasayansi na wataalam wa tiba zimepatikana chanjo mpya za kuzuia magonjwa ya shingo ya mlango wa kizazi na kuzuia ugonjwa wa polio ambapo zingine bado zipo katika hatua ya mbalimbali za majaribio zikiwemo za Ukimwi na Malaria.
Hatua hiyo ya serikali kwakushirikiana na wizara ya afya imejitahidi katika kuhakikisha chanjo za magonjwa hayo zinapatikana na kutolewa bila malipo kwa watoto wanaostahili chini ya miaka mitano.
Amezitaka halmashauri kuhakikisha kuwa wanapoandaa mipango, huduma za chanjo zipewe kipaumbele zikiwemo huduma za mkoba ili kumfikia kila mtoto, upatikanaji wa mitungi ya gesi kwenye vituo.
Uhamasishaji jamii kuhusu umuhimu wa huduma za chanjo, mafuta kwa ajili ya usambazaji wa chanjo, Usimamizi elekezi na mafunzo ya chanjo kwa watumishi wapya yanatolewa kwa wakati muafaka.
Pia, anaongeza kuwa wazazi walezi na familia kupeleka watoto wanaostahili kupata chanjo vituoni ili wakapate chanjo hizo stahiki kwa ratiba ili kujikinga na maradhi kama polio ambao ni hatari kwa watoto.
“Kila mmoja anawajibu anawajibu kuhakikisha mtoto wake, mtoto wa jirani au mototo yoyote yule anapewa haki ya kupata chanjo na asiwe hatari kwa wengine dhidi ya magonjwa ya mlipuko, ambapo walengwa ni watoto wote walio chini ya umri wa miaka mitano ambao hawajapata au hawajakamilisha ratiba ya chanjo kulingana na umri,”anasema.
“Napenda kuihakikishia jamii kuwa chanjo zote zinatolewa nchini ni salama na zimedhibitishwa na Shirika la Afya Duniani na nchi zote za dunia ikiwemo Tanzania,” anasema
Aidha mamlaka ya chakula na dawa imekuwa ikikagua chanjo zote zinazoingia nchini ili kuhakikisha kuwa chanjo zote zinazoingia ni zile tu zenye ubora na zimepitiwa na Shirika la Afya Duniani.
Kwahali  hiyo jamii inapaswa kujua umuhimu wa kupeleka watoto wao kupata chanjo kwani tayari serikali imetuhakikishia usalama wa chanjo hizo kwa watoto.

SEMINA YA USAMBAZAJI WA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2012 YAFANYIKA MKOANI MOROGORO

$
0
0
 Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii Ephraim Kwesigabo kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu akitoa maelezo mafupi wakati wa Semina ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyofanyika leo mjini Morogoro. 
  Kamishna wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 Hajjat Amina Mrisho Said akitoa maelezo mafupi ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wakati wa Semina ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyofanyika leo mjini Morogoro.
 Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Dkt. Rajab Rutengwe akiwahutubia washiriki wa Semina ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyofanyika leo mjini Morogoro.
 Baadhi ya washiriki wa Semina ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyofanyika leo mjini Morogoro wakifuatilia kwa makini Semina hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Dkt. Rajab Rutengwe (katikati) akiwa na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu, Zanzibar na baadhi ya washiriki wa Semina ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyofanyika leo mjini Morogoro.( PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).
==========  ========  =========  =========
SEMINA YA USAMBAZAJI WA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2012 YAFANYIKA MKOANI MOROGORO
  
Na Veronica Kazimoto
Morogoro
4 Mei, 2015.
 
Usambazaji wa matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni muhimu ili kila ngazi ya utawala iweze kuzipata, kuzielewa na kuzitumia takwimu zitokanazo na Sensa hiyo kwa ajili ya kutunga sera, kuandaa na kutathimini utekelezaji wa mipango ya maendeleo pamoja na kufanya maamuzi sahihi.
 
Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Dkt. Rajab Rutengwe wakati akifungua Semina ya siku moja ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyofanyika mjini Morogoro.
 
"Ni matumaini yangu kwamba, ninyi nyote mliokusanyika hapa  mtazitumia vizuri takwimu hizi ili ziwasaidie katika kuweka vipaumbele vya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wa mkoa wa Morogoro", amesema Dkt. Rutengwe.
 
Mkuu huyo wa Mkoa amesisistiza kuwa ni wajibu wa kila Ofisa wa Serikali mkoani Morogoro kuhakikisha takwimu zinazotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 zinakuwa msingi wa mipango  ya maendeleo na kuwa kigezo cha kufanya maamuzi katika kuweka mstakabali wa mkoa wa Morogoro.

Nae  Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii Ephraim Kwesigabo kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu akitoa maelezo mafupi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, amesema lengo la Semina hiyo ni kuwaelimisha wadau katika ngazi ya Mkoa, Wilaya na Halmashauri juu ya matumizi ya takwimu za Sensa ya Watu ili waweze kuzitumia katika kupanga na kutathmini program mbalimbali za maendeleo katika ngazi husika.
 
"Dumuni lingine la Semina hii ni kuhamasisha matumizi ya takwimu rasmi katika shughuli zetu za kikazi, ili lengo la kutumia takwimu za Sensa kuboresha maisha ya Mtanzania liweze kutimia", amesema Kwesigabo.
 
Kwesigabo amefafanua kua Semina hiyo ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi itasaidia kujua ni maeneo yapi mkoa wa Morogoro umepiga hatua na maeneo ambayo yanapaswa kutiliwa mkazo ili kuweza kufikia malengo ya kitaifa na kimataifa.
 
Jumla ya washiriki mia moja na kumi (110) kutoka ngazi ya Mkoa, Wilaya na Halmashauri zote mkoani Morogoro wameshiriki katika Semina ya Usambazaji wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 kwa lengo la kupata elimu juu ya matumizi ya takwimu zinazotokana na Sensa hiyo.

MVUA ZA MASIKA ZASABABISHA ATHARI KUBWA VISIWANI ZANZIBAR

$
0
0
                                   
Mvua za masika zinazoendelea kunyesha Visiwani Zanzibar zimesababisha hasara kubwa ikiwemo upotevu mali na mifugo, uharibifu wa miundombinu pamoja na kusababisha vifo vya watu.

Hayo yamweelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe. Mohamed Aboud Mohamed wakati akitoa taarifa kwa wananchi kuhusiana na athari za mvua hizo katika ukumbi wa  Karume House, Mjini Zanzibar.

Amesema mvua hizo zimesababisha mafuriko katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi na kupelekea athari kubwa katika maeneo hayo ikiwemo vifo vya watu, uharibifu wa nyumba za makaazi na upotevu wa mali na mifugo, ambapo hadi sasa watu wawili (2) ambao ni Nd. Juma Hamad (25) mkaazi wa Mwanakwerekwe na mtoto mmoja (1) mkaazi wa Kinuni anaekisiwa kuwa na miaka 8 wamepoteza maisha wakiwa wote wawili ni kutoka Wilaya ya Magharibi Unguja. 

Aidha Waziri Aboud amesema kuwa maiti ya mtoto imeshapatikana na kuzikwa jana Tarehe 3/5/2015 na maiti ya Nd. Juma Hamad bado haijapatikana na juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Amefahamisha kuwa maeneo yaliyoathirika zaidi na mvua hizo ni pamoja na Magomeni, Jang’ombe, Nyerere, Sebleni, Sogea, Mwanakwerekwe, Welezo, Kisauni, Tomondo, Mombasa, Kinuni, Mtopepo, Chumbuni, Kwahani, Mpendae, Bububu na Kwaalinato, ambapo maeneo yote hayo yanapatikana ndani ya Mkoa wa Mijini Magharibi.

Ametanabahisha kuwa, kwa vile mvua bado zinaendelea kunyesha ni vyema wananchi wakachukua tahadhari ili kujiepusha na athari zaidi zinazoweza kujitokeza, ikiwemo wazazi kuangalia watoto wao na kuhakikisha hawachezi karibu na maeneo yanayotuama maji, kwa wale wanaoishi mabondeni ni vyema wakahama sehemu hizo.

Waziri Aboud pia amewataka wananchi waliochimba mashimo katika maeneo ya makaazi wawe waangalifu kwa kuyafunika haraka iwezekanavyo , kuchemsha maji wanayoyatumia, kuhifadhi chakula ili kuepukana na maradhi ya miripuko pamoja na kufuata kanuni za afya ikiwemo usafi binafsi na maeneo yanayowazunguka.

Vilevile amewataka wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu kwani Serikali itaendelea kushirikiana nao ili kuhakikisha kuwa hali ya maisha kwa wananchi hao inarudi kama kawaida pamoja na kuwapa pole wale wote waliopoteza jamaa na mali zao.

Na Abdulla Ali-Maelezo Zanzibar    .

IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, asikitishwa na mtindo wa “Tegesha” unaofanywa na wananchi eneo la kuzunguka mgodi wa North Mara

$
0
0
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, akizungumza na mama huyu mkazi wa kijiji cha Nyakunguru, kilicho jirani na eeno la mgodi wa North Mara, huko Nyamongo wilayani Tarime mkoa wa Mara, wakati alipofanya ziara ya kutembelea maeneo yanayozunguka mgodi huo Jumatatu Mei 5, 2015 ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (Wapili kushoto), akizungumza jambo wakati alipotembelea eneo la ujenzi wa nyumba moja kwa mtindo unaoitwa na wakazi wa Nyamongo “Tegesha”, mita chache kutoka uzio wa mgodi wa North Mara, ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji. Naibu waziri amesikitishwa na mtindo huo ambapo wananchi hususan wanotoka nje ya eneo la Nyamongo, hujenga majengo haraka haraka eneo la kuzunguka mgodi huo kwa matarajio ya kujipatia malipo makubwa ya fidia kinyume na tathmini iliyofanywa awali.
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (kushoto), akisalimiana na Meneja Uendelezaji wa kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo, wakati alipofika kwenye kijiji cha Nyakunguru, kilicho jirani na mgodi wa North Mara, Mara ulioko Nyamongo, wilayani Tarime mkoa wa Mara Jumatatu Mei 4, 2015, ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji  Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga,(Watatu kulia), Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Jimmy Ijumba, (Wapili kulia) na Mkuu wa Mahusiano ya Serikali wa kampuni ya Acacia, Alex Lugendo.
 Meneja Uendelezaji wa Mgodi wa dhahabu wa North Mara, Abel Yiga, (kushoto), akimpatia maelezo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga wakati waziri huyo alipotembelea maeneo yanayozunguka mgodi huo ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga, (Watatu kulia), na kaimu kiongozi wa kitengo cha mahusiano ya kijamii ya mgodi wa North Mara, Zakayo Kalebo. (kushoto)
 Meneja Unedelezaji wa Kampuni ya Acacia, inayomiliki migodi ya Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara, Asa Mwaipopo, (katikati), akimpatia maelezo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (kushoto), wakati wa ziara yake ya kutembelea mgodi wa North Mara ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji. Kulia ni Mkuu wa Mahusiano ya Serikali wa kampuni ya Acacia, Alex Lugendo
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Kitwanga, (kushoto), akisalimiana na Meneja Uendelezaji wa kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo, wakati alipofika kwenye kijiji cha Nyakunguru, kilicho jirani na mgodi wa North Mara, Mara ulioko Nyamongo, wilayani Tarime mkoa wa Mara Jumatatu Mei 4, 2015, ili kufahamu jitihada za mgodi kuendeleza miradi ya kijamii na changamoto ambazo Jamii na Mgodi zinapata kutokana na shughuli za uchimbaji  Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga,(Watatu kulia), Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Jimmy Ijumba, (Wapili kulia) na Mkuu wa Mahusiano ya Serikali wa kampuni ya Acacia, Alex Lugendo.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images