Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46360 articles
Browse latest View live

UNICEF PAYS TRIBUTE TO COLLEAGUES KILLED AND INJURED IN SOMALIA ATTACK

$
0
0
 NAIROBI, 21 APRIL 2015 - With great sadness, UNICEF can now release the names of the four colleagues who were killed in a horrific attack as they travelled to work yesterday in Garowe, northern Somalia.

Those who lost their lives were:
·         Mr. Payenda Gul Abed, who had been coordinating UNICEF’s polio immunization efforts in Garowe since May 2014.
·         Ms. Brenda Kyeyune, who had managed social mobilization and communication initiatives in support of polio eradication in Somalia since 2014.
·         Ms. Woki Munyui, who had been supporting UNICEF’s education work in Somalia since 2007.
·         Mr. Stephen Oduor, who had been undertaking vital administrative work for UNICEF Somalia since 2010.
These heroes were dedicated to building a better world for children – today, all of us at UNICEF honour their sacrifice.

Five other UNICEF colleagues are being treated for injuries sustained in the attack, and we hope for their speedy recovery.


Two local security personnel, unrelated to UNICEF, were also killed as a result of the attack, and four others injured.

Our thoughts are with the families of all who died, with those who were injured, and with all our staff who continue to work tirelessly in Somalia to support women and children.

RAIS KIKWETE AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MKUU WA WILAYA YA KYERWA MAREHEMU LUTENI KANALI BENEDICT KITENGA (MSTAAFU) LEO HOSPITALI KUU YA JESHI YA LUGALO, DAR ES SALAAM

$
0
0
  Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrishi Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
  Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
 Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrishi Kikwete akifariji mjane wa marehemu baada ya kutoa heshima  zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akifariji wana familia baada ya kutoa  heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.

CBH - My Soul Official Video HD

PROF. ELISANTE OLLEGABRIEL UJUMBE WA SHIRIKISHO LA KIMATAIFA LA CHAMA CHA MICHEZO CHA MPIRA WA MAGONGO DUNIANI

$
0
0
ole1Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante OlleGabriel aliyenyoosha mkono akiongea na ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la mpira wa magongo kuhusu namna ya kuimarisha mchezo huo nchini, wa kwanza kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho hilo Bw.Seif Ahmed.(Picha na Benjamin Sawe WHVUM)
ole2Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Kimataifa la mpira wa magongo Bw.Seif Ahmed katikati akisisitiza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante OlleGabriel wa kwanza kulia wakati Shirikisho hilo lilipotembelea Ofisi za Wizara hiyo ili kujadiliana na Uongozi wa Wizara namna ya kuimarisha mchezo huo, wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Mchezo huo nchini Bw. Abraham Sykes. (Picha na Benjamin Sawe WHVUM)

MHE. SAADA SALUM MKUYA AKUTANA NA BI.SAYEH NA VILEVILE AKUTANA NA MCC/CHAMBER OF COMMERCE

$
0
0
sda1Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya wa katikati akiwa pamoja na ujumbe kutoka Tanzania walipokutana na ujumbe wa shirikala fedha la kimataifa (hawapo kwenye picha ). Kutoka kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile na kushoto ni Gavana wa Benki kuu Prof. Benno Ndulu , akifuatiwa na Gavana msaidizi wa Benki kuu ya Tanzania Bi. Natu Mwamba.
sda2Mkurugenzi wa Idara ya Afrika wa IMF kwa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara Bi. Antoinette Sayeh akiwa na ujumbe kutoka IMF wakizungumza na ujumbe kutoka Tanzania (hawapo kwenye picha).Katika kikao hicho walizungumzia zaidi suala la Tanzania kuzidisha nguvu katika kuboresha sera za kukuza uchumi.
sda3Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akifurahia jambo aliloambiwa na Bw.Herve’ Joly ambaye ni Mkurugenzi msaidizi na Mkuu wa idara ya Afrika sehemu ya Mashariki wakati wa mkutano uliofanyika kati ya ujumbe kutoka Tanzania na Shirika la fedha la Kimataifa mjini Washington DC.
sda4Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akitoa maelezo ya jinsi Tanzania inavyoboresha uchumi wake kwa Mkurugenzi wa Idara ya Afrika wa (IMF)kwa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara Bi. Antoinette Sayeh wa katikati. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile na kushoto ni Gavana wa Benki kuu Prof. Benno Ndulu , akifuatiwa na Gavana msaidizi wa Benki kuu ya Tanzania Bi. Natu Mwamba.
sda5Bw. Kamran Khan Makamu wa Rais wa shughuli za operesheni  za mfuko wa Changamoto za Milenia akizungumza katika mkutano wa (MCC/Chamber of commerce )akisikilizwa kwa makini na wa jumbe kutoka mfuko wa Changamoto za millennia na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya aliyekaa mbele.
sda6Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya, akifuatilia kwa makini mkutano huo wa mfuko wa Changamoto za millenia/Chamber of Commerce Uliokuwa ukifanyika hapa mjini Washington DC.)
sda7Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akizungumza katika mkutano huo wa Changamoto za Milenia/Chamber of Commerce uliofanyika mjini Washington DC. Aliyeko nyuma ya Mhe Waziri ni Bw. Laston Msongole ambaye ni Mtendaji Mkuu wa mfuko wa milenia wa awamu ya pili

MKUTANO WA KWANZA WA WADAU WA ZSSF WAFUNGULIWA NA RAIS DR.SHEIN

$
0
0
dk4

dk3Baadhi ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF wakiwa katika Mkutano wa siku mbili  Wadau wa ZSSF wa siku mbili ulioanza leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja sambamba na kuifungua mifuko ya kujichangia kwa Hiari ZVSSS na mfuko wa Mafao ya uzazi.
dk6Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi  Bi Fatma Ali Makame akiwa na Mtoto wake  mafao ya Uzazi  baada ya kuufungua mkutano wa kwanza wa Wadau wa ZSSF wa siku mbili ulioanza leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja (katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya ZSSF Dkt,Suleiman Rashid.dk7Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi  Ngao Bw.Omar Mwinyikondo Mkurugenzi Utumishi na Uendeshaji Wizara ya Afya  akiwakilisha Wizara yake ikiwa ni wachangiaji  Bora wa Taasisi za Serikali wakati wa utoaji wa zawadi kwa mashirika na taasisi mbali mbali zilizochangia  ZSSF wakati ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Wadau wa ZSSF wa siku mbili ulioanza leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja (katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya ZSSF Dkt,Suleiman Rashid.dk9Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi cheti cha shukrani Bi Raya Hamdani Khamis akiwa mtumishi wa muda mrefu wa ZSSF baada ya kuufungua mkutano wa kwanza wa Wadau wa ZSSF wa siku mbili ulioanza leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja (katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya ZSSF Dkt,Suleiman Rashid,[Picha na Ikulu.]
dk10Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi  Ngao Bw.Rajab Abdalla Meneja Rasilimali watu   akiwakilisha Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ wakati wa utoaji wa zawadi kwa mashirika ya Umma yaliyochangia  ZSSF baada ya kuufungua mkutano wa kwanza wa Wadau wa ZSSF wa siku mbili ulioanza leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja (katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya ZSSF Dkt,Suleiman Rashid.dk11Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi cheti cha shukrani Bi Fatma Mohamed Abass akiwa mtumishi wa Awali wa ZVSSS  baada ya kuufungua mkutano wa kwanza wa Wadau wa ZSSF wa siku mbili  ulioanza leo katika ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja (katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya ZSSF Dkt,Suleiman Rashid.

WATANZANIA WASHAURIWA KUTUMIA SUMAJKT KATIKA MIRADI

$
0
0
 Kaimu Msemaji Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Meja Josephat Musira akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam kuhusu utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Ujenzi  kupitia Kampuni ya Ujenzi ya JKT (NSCD) ikiwemo miradi ya biashara na miradi ya huduma.  Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Habari na Mahusiano wa JKT Kapteni Javan Bwai na kushoto ni  Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya. 

 Baadhi ya waandishi wa habari wakiwasikiliza viongozi wa JKT walipotembelea   jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT  ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).
 Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya akitoa maelezo  kwa waandishi wa habari leo walipotembelea  mradi wa ujenzi wa jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT  ‘’Msasani Tower’’ lenye thamani ya shilingi Bilioni 9.5 lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).

 Koplo Mhandisi Lazaro Masanja kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa akitoa rai kwa wananchi  na Taasisi kutumia Shirika la Uzalishaji Mali la JKT (SUMAJKT) kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa gharama nafuu. Nyuma ni  jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT  ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).

 Mkurugenzi Habari na Mahusiano wa JKT  Kapteni Javan Bwai  akitoa maelezo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio ya SUMAJKT kupitia kampuni ya ujenzi ya NSCD katika kipindi cha miaka 10 ya awamu ya nne ambapo alisema miradi 18 ya ujenzi imekamilika na miradi 9 inaendelea kujengwa . Kulia ni Kaimu Msemaji Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Meja Josephat Musira na kushoto ni Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya. 

Waandishi wa habari wakikagua jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT  ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).

MVUA ILIYONYESHA USIKU WA KUAMKIA LEO YASABABISHA MAFURIKO KIWANDA CHA SUKARI CHA TPC .

$
0
0
Sehemu ya maegesho ya magari katika kiwanda cha sukari cha TPC ikiwa imejaa maji yaliyotokana na mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia leo.
Eneo la kuegesha gari la zima moto katka kiwanda hicho ikiwa imejaa maji.
Hili si bwawa ni uwanja wa michezo wa Limpopo uliopo katika kiwanda cha sukari cha TPC ,kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha mafuriko katika kiwanda hicho pamojana vijiji vya jirani vinavyozunguka kiwanda hicho.
Hivi ndivyo ilivyokuwa ikionekana katika eneo la kiwanda baada ya mvua zilizonyesha usiku wa jana na kusababisha mafuriko katika kiwanda hicho.
Baadhi ya wafanyakazi katika kiwanda hicho wakitizama mafuriko yalivyo athili maeneo mbalimbali katika kiwanda hicho.
mafuriko katika eneo la kiwanda
Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wakiwa wameketi wasijue nini cha kufanya baada ya maji kuingia katika ofisi zao.
Kituo cha mafuta cha Puma kilichopo ndani ya kiwanda cha TPC kikiwa kimeenea maji.
Eneo la ofisi katika kiwanda hicho.
Hivi ndivyo ilivyoonekana wakati wa asubuhi leo .
Maji yalieneo katika maeneo mengi ya jirani na TPC.
Baadhi ya wafanyakazi katika kiwanda cha sukari cha TPC wakijaribu kuhamisha vitu mbalimbali baada ya nyumba zao kujaa maji,taarifa za awali zinadai zaidi ya watiu 100 wameathirika na mafuriko hayo huku wengine wakipoteza vyakula.hata hivyo tayari serikali mefika eneo la tukio kwa ajili ya kuangalia namna bora ya kusaidia wananchi walioathirika kutokana na mafuriko hayo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WAZIRI WA UCHUKUZI ARIDHISHWA NA MAENDLEO YA UJENZI WA JENGO JIPYA LA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA (TPA)

$
0
0
 Waziri wa Uchukuzi, Samweli Sitta (wa pili kutoka kulia) akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Awadh Massawe, wakati akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya la Mamlaka hiyo leo mchana. Wa kwanza Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka.

 Mbunifu majenzi  kutoka kampuni ya K &M Acrplans (T) ltd, ambao ndio washauri wa ujenzi wa Jengo hilo, Arch. Albert Mwambafu, akitoa maelezo kwa Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta ya sehemu mbalimbali za jengo hilo, leo mchana wakati Waziri huyo alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya Ujenzi wake. Jengo hilo litakuwa na ghorofa 35, lakini litakuwa na ofisi mbalimbali na Ukumbi utakaoweza kuchukua watu 1,200 kwa wakati mmoja.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Awadhi Massawe (wa tatu kutoka kushoto), akitoa maelezo ya namna ukumbi ulioko kwenye jengo utakavyokuwa kwa Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, leo mchana wakati Waziri huyo alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya ujenzi wake.

 Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta akiangalia Boya ya Kupakulia mafuta la SPM, kupitia juu ya jengo jipya la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA),leo mchana wakati alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya ujenzi wake.Jengo hilo linatarajiwa kukamilika mwezi Agosti mwaka huu.

Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, akitoa maelekezo kwa viongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), wakandarasi na viongozi kutoka Wizara ya Uchukuzi, baada ya kuangalia maendeleo ya jengo jipya la leo mchana. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)      

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM JUU YA KUTIWA MBARONI KWA WATUHUMIWA SUGU WA KUPORA RAIA WA KIGENI NA AKINA MAMA

$
0
0
Watuhumiwa wanne wamekamatwa jijini Dar es Salaam katika makutano ya barabara ya Bibi Titi na Ohio karibu na Hotel ya Serena baada ya kumpora raia wa kigeni wakiwa na gari dogo rangi ya kijivu yenye nambari za usajili T787 DBU Toyota Cienta.

Hivi karibuni kumeibuka wimbi la wahalifu kuwapora pesa na vitu vya thamani kama mikufu, bangili, hereni pia pete na vitu mbalimbali vya thamani raia wa kigeni na akina mama ambao hupenda kutembea na pochi. Wahalifu hawa hutumia gari dogo ambalo mara kwa mara hubadilishwa namba zake za usajili na wakati mwingine gari hili wanalitumia kama Tax bubu.

Leo tarehe 21/04/2015 majira ya saa 09:00 asubuhi katika eneo la Posta Mpya watuhumiwa hawa walimdangavya bwana CEES S/O JAN CONIJN, Miaka 27, raia wa Uholanzi aliyetaka kufika Klabu ya Leaders kwamba wangempeleka eneo hilo kwa kutumia gari tajwa hapo juu. Baada ya kuondoka na dereva kila baada ya mita 200 dereva huyo alikuwa anasimamisha gari na kuongeza mtu mwingine kama abiria hadi walipotimia wote wane.

Walimpeleka hadi maeneo ya Kinondoni kwa Manyanya na walipofika eneo hilo walimweleza wazi kuwa wao ni wahalifu na walimtaka awapatie pesa vinginevyo wangemuua. Aliwapatia pesa zote alizokuwa nazo Tshs 75,000/= lakini hawakuridhika ndipo walipomtaka awapatie kadi ya benki (ATM CARD) na nambari za siri (Pass Word). 

Baada ya tukio hilo wakamtupa karibu na Hospitali ya Mwananyamala na wao wakageuza gari kurudi katikati ya  mji. Wakati tukio hilo linatokea raia wema walishuhudia na kutoa taarifa kwa Polisi. Polisi walifuatilia haraka na kuweka mtego uliowanasa watuhumiwa wote katika eneo la makutano ya barabara ya Bibi Titi na Ohio karibu na Hotel ya Serena.
Majina ya watuhumiwa waliokamatwa ni:
1.SALUM S/O SAID MTUMWA @ MARO, Miaka 25, Mkazi wa Chang’ombe Bora.
2.ALEX S/O INNOCENT MANGUKA @ MAKA, Miaka 30, Mkazi wa Kimara Temboni.
3.MOHAMED S/O ALLY ABDALLA @ MEDY, Miaka 27, Mkazi wa Mwananyamala.
4.STEPHANO S/O ALBERT KIKINDI @ KING, Miaka 32, Mkazi wa Mwananyamala.

Walipopekuliwa watuhumiwa hawa walikutwa na simu  mbalimbali za mkononi zipatazo 11 ambazo zinachunguzwa kuhusiana na mbinu ya uhalifu wanaoutumia. Pia ilikamatwa ATM CARD iliyochukuliwa kwa mlalamikaji kabla watuhumiwa hao hawajaitumia. Aidha gari namba T787 DBU Toyota Cienta linashikiliwa kwa uchunguzi zaidi.

Miongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa, wawili ambao ni MOHAMED S/O ALLY ABDALLA @ MEDY, na STEPHANO S/O ALBERT KIKINDI @ KING, tayari wanazo kesi nyingine mahakamani na wako nje kwa dhamana.

Sambamba na tukio hili oparesheni ya kuwakamata wahalifu wengine wenye mtindo huu wa kuwapora wageni au wakina mama wenye mikoba inaendelea na tunawaomba wananchi waonyeshe ushirikiano wa kutosha ili kutokomeza vitendo hivyo viovu. Aidha hakuna silaha yoyote iliyotumika au kukamatwa kama ilivyoripotiwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

S. H. KOVA,
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM,
DAR ES SALAAM.

MFUKO WA LAPF WATOA MSAADA WA RANGI ZENYE THAMANI YA SH.MILIONI 3 KUMALIZIA UJENZI WA MAABARA YA SHULE WILAYANI ULANGA

$
0
0
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Mfuko wa LAPF, Yesaya Mwakifulefule (wa pili kushoto),  akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro,  Christina Mndeme, msaada wa rangi zenye thamani ya sh. milioni 3 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa maabara katika shule za Ulanga Mashariki.

INTRODUCING BRANDY NEW VIDEO TOKA KWA''AMOUR GENIUS''

BALOZI WA RWANDA NCHINI MAREKANI MHE. MATHILDA MUKANTABANA ATEMBELEA AFISI ZA UMOJA WA AFRIKA WASHINGTON, DC.

$
0
0

Mhe Balozi wa Rwanda Profesa Mathilda Mukantabana akiwa katika pich ya pamoja na Balozi wa AU Mhe. Amina Salum Ali alipotembelea ofisi za Umoja wa Afrika uliopo Washington, DC nchini Marekani .Balozi Profesa Mathilda anachukua uongozi wa mikutano wa mabalozi wa Afrika katika kipindi cha mwezi April hadi July 2015 akiwakilisha kanda ya Afrika Mashariki.

RAIS MSTAAFU MHESHIMIWA ALI HASSAN MWINYI AWASILI JIJINI WASHINGTON DC.

$
0
0
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akiambata na mama Sitti Mwinyi wawasili jijini Washington DC tayari kwa tamasha maalum la Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mkuu wa utawala Lilly Munanka wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC, mara alipowasili hotelini.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wafanyakazi wa ubalozi Edward Taji.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Afisa wa Ubalozi Swahiba Mndeme.
  Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Afisa wa Ubalozi Emmanuel Swere.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wafanyakazi wa ubalozi John Anbiah
     Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akiwa ameongozana na mama Sitti   Mwinyi na baadhi ya msafara wake katika hoteli waliyofikia.
                                  PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI

BALOZI MPYA WA ANGOLA ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON DC.

$
0
0

 Mhe, balozi wa Angola Agostinho Tavares akipokelewa na afisa wa ubalozi  Swahiba Mndeme alipotembelea ubalozi .
 Mhe, balozi Liberata Mulamula akiwa na furaha baada ya mgeni wake kufika ofisini .
 Mhe balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na mgeni wake balozi wa Angola Agostinho Tavares.
 Mhe Balozi wa Angola nchini Marekani Agostinho Tavares akiweka sahihi  kitabu cha wageni.
 Mhe balozi wa Angola chini Marekani Agostinho Tavares akimsikiliza kwa makini mwenyeji wake balozi Liberata Mulamula alipokua akijitambulisha .
Mhe balozi Libarata Mulamula na balozi wa Angola nchini marekani Agostinho Tavares pamoja na afisa wa ubalozi Swahiba Mndeme walipokua wakibadilishana mawazo.
               PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA) YASAINI MIKATABA KUPELEKA MAWASILIANO VIJIJINI.

$
0
0
1
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (Katikati) akiwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa, Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka Ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  Prof. John Nkoma, CEO wa TTCL Dr. Kamugisha Kazaura wakiweka sahihi mikataba ya mabilioni kupelekea mawasiliano vijijini.
2
Afisa Mtendaji Mkuu WA Mfuko WA Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na  (Kutoka Kushoto) Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia John Mngodo, Mkurugenzi mkuu WA Mamlaka Ya Mawasiliano Tanzania Prof. John Nkoma,Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa, (Kutoka Kulia) CEO WA TTCL Dr. Kamugisha Kazaura, mwakilishi kutoka kampuni ya mtandao ya simu za mkononi Airtel Ronald Mitti pamoja na wawakilishi wengine wa mitandao ya simu za mkono pamoja na wafanyakazi wa Mfuko huo.
3
Afisa Mtendaji Mkuu WA Mfuko WA Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (Kulia) akitia sahihi mikataba ya mabilioni kupelekea mawasiliano vijijini pamoja na CEO WA TTCL Dr. Kamugisha Kazaura.
4
Afisa Mtendaji Mkuu WA Mfuko WA Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga  (WA pili kulia) akibidilishana mawazo na Waziri WA Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa baada ya kutia sahihi mikataba ya mabilioni kupelekea mawasiliano vijijini.5
picha ya pamoja

CHADEMA YAZINDUA MAFUNZO YA TIMU ZA KAMPENI KWA VIONGOZI WA CHAMA NA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum Mwalim akizindua mafunzo ya timu za kampeni, viongozi wa chama na viongozi wa serikali za mitaa wanaotokana na CHADEMA kwa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Njombe, Ruvuma, Rukwa, Mbeya na Iringa) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya chama kwenda kushinda dola na kuongoza serikali katika uchaguzi mkuu ujao.

majonzi yatawala wakati wa kumuaga BIBI MAGDALENA PETRO MAGIGE

$
0
0
  Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) mstaafu, Jenerali George Mwita Waitara akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige kilichotokea tarehe 19 Aprili 2015, jijini Dar es salaam.
 Mzee Galius Abeid akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akifunga jeneza la marehemu Magdalena Petro Magige.
 Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Magdalena Petro Magige likiteremshwa kutoka kwenye gari tayari kwa kutoa heshima ya mwisho kabla ya safari ya kwenda kuupumzisha kijiji cha Kamange,Tarime mkani Mara.
 Ndugu na jamaa waliojitokeza kwa wingi  kutoa heshima ya mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Alhaji Adam Kimbisa na Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) mstaafu, Jenerali George Mwita Waitara wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.

 Ndugu na Jamaawakitoa heshima za mwisho
 Ilikuwa ni majonzi kwa kila mtu wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa Bibi Magdalena Petro Magige.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa heshima ya mwisho kwa Bibi Magdalena Petro sanjali na Mama Norah P. Mukami.
 Watoto wa marehemu Magdalena Petro Magige wakitoa heshima za mwisho kwa mama yao mpendwa aliyefariki tarehe 19 Aprili 2015.

 Ndugu , Jamaa na marafiki waliojitokeza kuja kutoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao Bibi Magdalena Petro Magige aliyefariki  tarehe 19 Aprili jijini Dar es Salaam.
 Padri Valence Matungwa akitoa somo wakati wa misa maalum ya kumuaga marehemu Magdalena Petro Magige,Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 Padri Ladislaus Kapinga akiongiza ibada wakati wa kumuaga marehemu Magdalena Petro Magige
 Mtoto wa Marehemu Norah P. Mukami akipokea ekaristi takatifu wakati wa misa maalumu ya kumuaga Magdalena Petro Mukami.

USIKU WA JIONEE ULIVYOFANA JIJINI MBEYA

$
0
0
Wakili Sambwee Shitambala akizungumza jambo na baadhi ya wadau na wasanii wa muziki wa Kizazi kipya mkoa wa Mbeya katika tafrija iliyo fanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Gorden City hotel, uliopo eneo la Sae  na hii ni baada ya kuzindua albamu ya msanii berdon mnyama iendayo kwa jina la "Jionee",iliyo sapotiwa na media mbali mbali ikiwemo vituo vya radio zote za jiji la mbeya sambamba na Michuzi Media Group.picha na Fadhiri Atick (Mr.Pengo) globu ya jamii Mbeya.
 Msanii anae fanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya Jijini Mbeya, Berdon Mnyama ambae ndie alie zindua albamu yake hivi karibuni iendayo kwa jina la Jionee akizungumza na baadhi ya wadau na wasanii wa muziki wa kizazi kipya katika hafra hiyo iliyofanyika hivi karibuni jijini mbeya.
 Wakili Sambwe Shitambala (shoto) akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa wasanii Berdon Mnyama na Petronia kwa lengo la kumpongeza kwa kazi kubwa anayo ifanya juu ya kudhamini na kuwajali vijana hususani wasanii katika tasnia mbalimbali mkoani mbeya.
 baadhi ya wasanii na wadau wa sanaa walio hudhuria katika hafra hiyo iliyo fanyika hivi karibun jijini mbeya.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

PDB YAKIRI KODI ZA BIASHARA SIZIZO RASMI HUISHIA KATIKA MIFUKO YA WATU NA SIO SERIKALI.

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Vyuo Vikuu vya Afrika ya Kati na Kusini (ESAURP),Profesa Teddy Maliyamkono akifanya mahojiano mafupi na Waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mkutano wa kuwajengea uwezo sekta biashara zisizo rasmi  iliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wadau na Wanahabari  wakifuatilia mkutano wa uzinduzi wa mradi wa kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo na wakati kuhuisha biashara zao ili kupata huduma za kibenki iliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Ufundi wa FSDT, Sosthenes Kewe alizungumza mbele ya wadau na waandishi wa habari  kuhusiana na uzinduzi wa mradi wa kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo na wakati kuhuisha biashara zao ili kupata huduma za kibenki,Bwa.Kewe amesema kuwa taasisi yake imesaidia mradi huu kwa kuwa unaendana na kazi yao ya kuwezesha wajasiriamali wadogo na wakati na hivyo kuchangia katika kukuza uchumi, kutengeneza ajira na kupanua vyanzo vya kodi.
Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi (PDB),Omary Issa akifanya mahojiano mafupi na Waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mkutano wa kuwajengea uwezo sekta biashara zisizo rasimi  iliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

ZAIDI ya biashara milioni tatu hazijasajiliwa na mamlaka za utambuzi wa biashara hizo kutokana na kuwa mazingira magumu ya kusajili biashara hizo ikichangiwa na rushwa.

Hayo ameyasema Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi (PDB),Omary Issa wakati mkutano wa kuwajengea uwezo sekta ya biashara isiyo rasmi,  uliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Issa amesema wajasirimali wamekuwa wakilipa kodi lakini zinaishia katika mifuko ya watu na kuisababishia serikali kukosa mapato. Amesema wajasiriamali wakirasimishwa katika mpango huu wataongeza mapato kuliko ilivyo sasa kwa kulipa watu wanaoingiza mifukoni mwao na kuacha serikali kukosa kodi hizo.

Aidha amesema asilimia 40 ya biashara ndogo hazijasajiliwa na mamlaka zinahusika na kufanya wajasiriamali hao kushindwa kupata mikopo katika taasisi za kifedha.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Vyuo Vikuu vya Afrika ya Kati na Kusini (ESAURP),Profesa Teddy Maliyamkono amesema mradi huu wa kurasimimisha biashara utasaidia kukua biashara zao.

Amesema watu wamekuwa wakifanya biashara hazikui kutokana na mitaji yao kuwa midogo na kukosa fursa kukopa katika taasisi za fedha.
Viewing all 46360 articles
Browse latest View live




Latest Images