0 |
|
0 |
|
NAIROBI, 21 APRIL 2015 - With great sadness, UNICEF can now release the names of the four colleagues who were killed in a horrific attack as they travelled to work yesterday in Garowe, northern Somalia.
Those who lost their lives were:
· Mr. Payenda Gul Abed, who had been coordinating UNICEF’s polio immunization efforts in Garowe since May 2014.
· Ms. Brenda Kyeyune, who had managed social mobilization and communication initiatives in support of polio eradication in Somalia since 2014.
· Ms. Woki Munyui, who had been supporting UNICEF’s education work in Somalia since 2007.
· Mr. Stephen Oduor, who had been undertaking vital administrative work for UNICEF Somalia since 2010.
These heroes were dedicated to building a better world for children – today, all of us at UNICEF honour their sacrifice.
Five other UNICEF colleagues are being treated for injuries sustained in the attack, and we hope for their speedy recovery.
Two local security personnel, unrelated to UNICEF, were also killed as a result of the attack, and four others injured.
Our thoughts are with the families of all who died, with those who were injured, and with all our staff who continue to work tirelessly in Somalia to support women and children.
0 |
|
0 |
|
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrishi Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrishi Kikwete akifariji mjane wa marehemu baada ya kutoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akifariji wana familia baada ya kutoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (Mstaafu) aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ambaye alifariki jana asubuhi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho huko Morogoro.
0 |
|
0 |
|
0 |
|
0 |
|
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante OlleGabriel aliyenyoosha mkono akiongea na ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la mpira wa magongo kuhusu namna ya kuimarisha mchezo huo nchini, wa kwanza kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho hilo Bw.Seif Ahmed.(Picha na Benjamin Sawe WHVUM)
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Kimataifa la mpira wa magongo Bw.Seif Ahmed katikati akisisitiza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante OlleGabriel wa kwanza kulia wakati Shirikisho hilo lilipotembelea Ofisi za Wizara hiyo ili kujadiliana na Uongozi wa Wizara namna ya kuimarisha mchezo huo, wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Mchezo huo nchini Bw. Abraham Sykes. (Picha na Benjamin Sawe WHVUM)
0 |
|
0 |
|
0 |
|
0 |
|
0 |
|
0 |
|
Kaimu Msemaji Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Meja Josephat Musira akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam kuhusu utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Ujenzi kupitia Kampuni ya Ujenzi ya JKT (NSCD) ikiwemo miradi ya biashara na miradi ya huduma. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Habari na Mahusiano wa JKT Kapteni Javan Bwai na kushoto ni Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwasikiliza viongozi wa JKT walipotembelea jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).
Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya akitoa maelezo kwa waandishi wa habari leo walipotembelea mradi wa ujenzi wa jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT ‘’Msasani Tower’’ lenye thamani ya shilingi Bilioni 9.5 lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).
Koplo Mhandisi Lazaro Masanja kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa akitoa rai kwa wananchi na Taasisi kutumia Shirika la Uzalishaji Mali la JKT (SUMAJKT) kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa gharama nafuu. Nyuma ni jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).
Mkurugenzi Habari na Mahusiano wa JKT Kapteni Javan Bwai akitoa maelezo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio ya SUMAJKT kupitia kampuni ya ujenzi ya NSCD katika kipindi cha miaka 10 ya awamu ya nne ambapo alisema miradi 18 ya ujenzi imekamilika na miradi 9 inaendelea kujengwa . Kulia ni Kaimu Msemaji Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Meja Josephat Musira na kushoto ni Mkurugenzi wa ufundi SUMAJKT Mhandisi Fredrick Kaaya.
Waandishi wa habari wakikagua jengo la kitega uchumi cha Kanisa la KKKT ‘’Msasani Tower’’ lililopo Msasani jijini Dar es Salaam ambalo limejengwa na kampuni ya ujenzi ya JKT (NSCD).
0 |
|
0 |
|
0 |
|
0 |
|
Waziri wa Uchukuzi, Samweli Sitta (wa pili kutoka kulia) akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Awadh Massawe, wakati akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya la Mamlaka hiyo leo mchana. Wa kwanza Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka.
Mbunifu majenzi kutoka kampuni ya K &M Acrplans (T) ltd, ambao ndio washauri wa ujenzi wa Jengo hilo, Arch. Albert Mwambafu, akitoa maelezo kwa Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta ya sehemu mbalimbali za jengo hilo, leo mchana wakati Waziri huyo alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya Ujenzi wake. Jengo hilo litakuwa na ghorofa 35, lakini litakuwa na ofisi mbalimbali na Ukumbi utakaoweza kuchukua watu 1,200 kwa wakati mmoja.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Awadhi Massawe (wa tatu kutoka kushoto), akitoa maelezo ya namna ukumbi ulioko kwenye jengo utakavyokuwa kwa Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, leo mchana wakati Waziri huyo alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya ujenzi wake.
Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta akiangalia Boya ya Kupakulia mafuta la SPM, kupitia juu ya jengo jipya la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA),leo mchana wakati alipotembelea jengo hilo kuona maendeleo ya ujenzi wake.Jengo hilo linatarajiwa kukamilika mwezi Agosti mwaka huu.
Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, akitoa maelekezo kwa viongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), wakandarasi na viongozi kutoka Wizara ya Uchukuzi, baada ya kuangalia maendeleo ya jengo jipya la leo mchana. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)
0 |
|
0 |
|
Watuhumiwa wanne wamekamatwa jijini Dar es Salaam katika makutano ya barabara ya Bibi Titi na Ohio karibu na Hotel ya Serena baada ya kumpora raia wa kigeni wakiwa na gari dogo rangi ya kijivu yenye nambari za usajili T787 DBU Toyota Cienta.
Hivi karibuni kumeibuka wimbi la wahalifu kuwapora pesa na vitu vya thamani kama mikufu, bangili, hereni pia pete na vitu mbalimbali vya thamani raia wa kigeni na akina mama ambao hupenda kutembea na pochi. Wahalifu hawa hutumia gari dogo ambalo mara kwa mara hubadilishwa namba zake za usajili na wakati mwingine gari hili wanalitumia kama Tax bubu.
Leo tarehe 21/04/2015 majira ya saa 09:00 asubuhi katika eneo la Posta Mpya watuhumiwa hawa walimdangavya bwana CEES S/O JAN CONIJN, Miaka 27, raia wa Uholanzi aliyetaka kufika Klabu ya Leaders kwamba wangempeleka eneo hilo kwa kutumia gari tajwa hapo juu. Baada ya kuondoka na dereva kila baada ya mita 200 dereva huyo alikuwa anasimamisha gari na kuongeza mtu mwingine kama abiria hadi walipotimia wote wane.
Walimpeleka hadi maeneo ya Kinondoni kwa Manyanya na walipofika eneo hilo walimweleza wazi kuwa wao ni wahalifu na walimtaka awapatie pesa vinginevyo wangemuua. Aliwapatia pesa zote alizokuwa nazo Tshs 75,000/= lakini hawakuridhika ndipo walipomtaka awapatie kadi ya benki (ATM CARD) na nambari za siri (Pass Word).
Baada ya tukio hilo wakamtupa karibu na Hospitali ya Mwananyamala na wao wakageuza gari kurudi katikati ya mji. Wakati tukio hilo linatokea raia wema walishuhudia na kutoa taarifa kwa Polisi. Polisi walifuatilia haraka na kuweka mtego uliowanasa watuhumiwa wote katika eneo la makutano ya barabara ya Bibi Titi na Ohio karibu na Hotel ya Serena.
Majina ya watuhumiwa waliokamatwa ni:
1.SALUM S/O SAID MTUMWA @ MARO, Miaka 25, Mkazi wa Chang’ombe Bora.
2.ALEX S/O INNOCENT MANGUKA @ MAKA, Miaka 30, Mkazi wa Kimara Temboni.
3.MOHAMED S/O ALLY ABDALLA @ MEDY, Miaka 27, Mkazi wa Mwananyamala.
4.STEPHANO S/O ALBERT KIKINDI @ KING, Miaka 32, Mkazi wa Mwananyamala.
Walipopekuliwa watuhumiwa hawa walikutwa na simu mbalimbali za mkononi zipatazo 11 ambazo zinachunguzwa kuhusiana na mbinu ya uhalifu wanaoutumia. Pia ilikamatwa ATM CARD iliyochukuliwa kwa mlalamikaji kabla watuhumiwa hao hawajaitumia. Aidha gari namba T787 DBU Toyota Cienta linashikiliwa kwa uchunguzi zaidi.
Miongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa, wawili ambao ni MOHAMED S/O ALLY ABDALLA @ MEDY, na STEPHANO S/O ALBERT KIKINDI @ KING, tayari wanazo kesi nyingine mahakamani na wako nje kwa dhamana.
Sambamba na tukio hili oparesheni ya kuwakamata wahalifu wengine wenye mtindo huu wa kuwapora wageni au wakina mama wenye mikoba inaendelea na tunawaomba wananchi waonyeshe ushirikiano wa kutosha ili kutokomeza vitendo hivyo viovu. Aidha hakuna silaha yoyote iliyotumika au kukamatwa kama ilivyoripotiwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
S. H. KOVA,
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM,
DAR ES SALAAM.
0 |
|
0 |
|
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Mfuko wa LAPF, Yesaya Mwakifulefule (wa pili kushoto), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, Christina Mndeme, msaada wa rangi zenye thamani ya sh. milioni 3 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa maabara katika shule za Ulanga Mashariki.
0 |
|
0 |
|
0 |
|
0 |
|
.JPG)
Mhe Balozi wa Rwanda Profesa Mathilda Mukantabana akiwa katika pich ya pamoja na Balozi wa AU Mhe. Amina Salum Ali alipotembelea ofisi za Umoja wa Afrika uliopo Washington, DC nchini Marekani .Balozi Profesa Mathilda anachukua uongozi wa mikutano wa mabalozi wa Afrika katika kipindi cha mwezi April hadi July 2015 akiwakilisha kanda ya Afrika Mashariki.
0 |
|
0 |
|
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akiambata na mama Sitti Mwinyi wawasili jijini Washington DC tayari kwa tamasha maalum la Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mkuu wa utawala Lilly Munanka wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC, mara alipowasili hotelini.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wafanyakazi wa ubalozi Edward Taji.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Afisa wa Ubalozi Swahiba Mndeme.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Afisa wa Ubalozi Emmanuel Swere.
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na mmoja wa wafanyakazi wa ubalozi John Anbiah
Rais mstaafu wa awamu ya pili Mhe, Ali Hassan Mwinyi akiwa ameongozana na mama Sitti Mwinyi na baadhi ya msafara wake katika hoteli waliyofikia.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI
0 |
|
0 |
|
Mhe, balozi wa Angola Agostinho Tavares akipokelewa na afisa wa ubalozi Swahiba Mndeme alipotembelea ubalozi .
Mhe, balozi Liberata Mulamula akiwa na furaha baada ya mgeni wake kufika ofisini .
Mhe balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na mgeni wake balozi wa Angola Agostinho Tavares.
Mhe Balozi wa Angola nchini Marekani Agostinho Tavares akiweka sahihi kitabu cha wageni.
Mhe balozi wa Angola chini Marekani Agostinho Tavares akimsikiliza kwa makini mwenyeji wake balozi Liberata Mulamula alipokua akijitambulisha .
Mhe balozi Libarata Mulamula na balozi wa Angola nchini marekani Agostinho Tavares pamoja na afisa wa ubalozi Swahiba Mndeme walipokua wakibadilishana mawazo.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI
0 |
|
0 |
|
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (Katikati) akiwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa, Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka Ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, CEO wa TTCL Dr. Kamugisha Kazaura wakiweka sahihi mikataba ya mabilioni kupelekea mawasiliano vijijini.
Afisa Mtendaji Mkuu WA Mfuko WA Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na (Kutoka Kushoto) Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia John Mngodo, Mkurugenzi mkuu WA Mamlaka Ya Mawasiliano Tanzania Prof. John Nkoma,Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa, (Kutoka Kulia) CEO WA TTCL Dr. Kamugisha Kazaura, mwakilishi kutoka kampuni ya mtandao ya simu za mkononi Airtel Ronald Mitti pamoja na wawakilishi wengine wa mitandao ya simu za mkono pamoja na wafanyakazi wa Mfuko huo.
Afisa Mtendaji Mkuu WA Mfuko WA Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (Kulia) akitia sahihi mikataba ya mabilioni kupelekea mawasiliano vijijini pamoja na CEO WA TTCL Dr. Kamugisha Kazaura.
Afisa Mtendaji Mkuu WA Mfuko WA Mawasiliano kwa Wote (Universal Communications Service Access Fund – UCSAF) Eng Peter Ulanga (WA pili kulia) akibidilishana mawazo na Waziri WA Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa baada ya kutia sahihi mikataba ya mabilioni kupelekea mawasiliano vijijini.
picha ya pamoja
0 |
|
0 |
|
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum Mwalim akizindua mafunzo ya timu za kampeni, viongozi wa chama na viongozi wa serikali za mitaa wanaotokana na CHADEMA kwa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Njombe, Ruvuma, Rukwa, Mbeya na Iringa) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya chama kwenda kushinda dola na kuongoza serikali katika uchaguzi mkuu ujao.
0 |
|
0 |
|
Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) mstaafu, Jenerali George Mwita Waitara akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige kilichotokea tarehe 19 Aprili 2015, jijini Dar es salaam.
Mzee Galius Abeid akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akifunga jeneza la marehemu Magdalena Petro Magige.
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Magdalena Petro Magige likiteremshwa kutoka kwenye gari tayari kwa kutoa heshima ya mwisho kabla ya safari ya kwenda kuupumzisha kijiji cha Kamange,Tarime mkani Mara.
Ndugu na jamaa waliojitokeza kwa wingi kutoa heshima ya mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Alhaji Adam Kimbisa na Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) mstaafu, Jenerali George Mwita Waitara wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Magdalena Petro Magige.
Ndugu na Jamaawakitoa heshima za mwisho
Ilikuwa ni majonzi kwa kila mtu wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa Bibi Magdalena Petro Magige.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa heshima ya mwisho kwa Bibi Magdalena Petro sanjali na Mama Norah P. Mukami.
Watoto wa marehemu Magdalena Petro Magige wakitoa heshima za mwisho kwa mama yao mpendwa aliyefariki tarehe 19 Aprili 2015.
Ndugu , Jamaa na marafiki waliojitokeza kuja kutoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao Bibi Magdalena Petro Magige aliyefariki tarehe 19 Aprili jijini Dar es Salaam.
Padri Valence Matungwa akitoa somo wakati wa misa maalum ya kumuaga marehemu Magdalena Petro Magige,Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Padri Ladislaus Kapinga akiongiza ibada wakati wa kumuaga marehemu Magdalena Petro Magige
Mtoto wa Marehemu Norah P. Mukami akipokea ekaristi takatifu wakati wa misa maalumu ya kumuaga Magdalena Petro Mukami.
0 |
|
0 |
|
Wakili Sambwee Shitambala akizungumza jambo na baadhi ya wadau na wasanii wa muziki wa Kizazi kipya mkoa wa Mbeya katika tafrija iliyo fanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Gorden City hotel, uliopo eneo la Sae na hii ni baada ya kuzindua albamu ya msanii berdon mnyama iendayo kwa jina la "Jionee",iliyo sapotiwa na media mbali mbali ikiwemo vituo vya radio zote za jiji la mbeya sambamba na Michuzi Media Group.picha na Fadhiri Atick (Mr.Pengo) globu ya jamii Mbeya.
Msanii anae fanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya Jijini Mbeya, Berdon Mnyama ambae ndie alie zindua albamu yake hivi karibuni iendayo kwa jina la Jionee akizungumza na baadhi ya wadau na wasanii wa muziki wa kizazi kipya katika hafra hiyo iliyofanyika hivi karibuni jijini mbeya.
Wakili Sambwe Shitambala (shoto) akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa wasanii Berdon Mnyama na Petronia kwa lengo la kumpongeza kwa kazi kubwa anayo ifanya juu ya kudhamini na kuwajali vijana hususani wasanii katika tasnia mbalimbali mkoani mbeya.
baadhi ya wasanii na wadau wa sanaa walio hudhuria katika hafra hiyo iliyo fanyika hivi karibun jijini mbeya.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
0 |
|
0 |
|
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Vyuo Vikuu vya Afrika ya Kati na Kusini (ESAURP),Profesa Teddy Maliyamkono akifanya mahojiano mafupi na Waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mkutano wa kuwajengea uwezo sekta biashara zisizo rasmi iliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wadau na Wanahabari wakifuatilia mkutano wa uzinduzi wa mradi wa kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo na wakati kuhuisha biashara zao ili kupata huduma za kibenki iliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ufundi wa FSDT, Sosthenes Kewe alizungumza mbele ya wadau na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa mradi wa kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo na wakati kuhuisha biashara zao ili kupata huduma za kibenki,Bwa.Kewe amesema kuwa taasisi yake imesaidia mradi huu kwa kuwa unaendana na kazi yao ya kuwezesha wajasiriamali wadogo na wakati na hivyo kuchangia katika kukuza uchumi, kutengeneza ajira na kupanua vyanzo vya kodi.
Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi (PDB),Omary Issa akifanya mahojiano mafupi na Waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mkutano wa kuwajengea uwezo sekta biashara zisizo rasimi iliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
ZAIDI ya biashara milioni tatu hazijasajiliwa na mamlaka za utambuzi wa biashara hizo kutokana na kuwa mazingira magumu ya kusajili biashara hizo ikichangiwa na rushwa.
Hayo ameyasema Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya Rais-Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi (PDB),Omary Issa wakati mkutano wa kuwajengea uwezo sekta ya biashara isiyo rasmi, uliofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Issa amesema wajasirimali wamekuwa wakilipa kodi lakini zinaishia katika mifuko ya watu na kuisababishia serikali kukosa mapato. Amesema wajasiriamali wakirasimishwa katika mpango huu wataongeza mapato kuliko ilivyo sasa kwa kulipa watu wanaoingiza mifukoni mwao na kuacha serikali kukosa kodi hizo.
Aidha amesema asilimia 40 ya biashara ndogo hazijasajiliwa na mamlaka zinahusika na kufanya wajasiriamali hao kushindwa kupata mikopo katika taasisi za kifedha.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Vyuo Vikuu vya Afrika ya Kati na Kusini (ESAURP),Profesa Teddy Maliyamkono amesema mradi huu wa kurasimimisha biashara utasaidia kukua biashara zao.
Amesema watu wamekuwa wakifanya biashara hazikui kutokana na mitaji yao kuwa midogo na kukosa fursa kukopa katika taasisi za fedha.