Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

VIJANA WA CCM IRINGA WAMPA NGUVU KATIBU WA MKOA HASSAN MTENGA KUKOMBOA JIMBO, LA IRINGA MJINI.

$
0
0



Mtenga katika kikao na baadhi ya vijana hao

KIU ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Iringa kukomboa jimbo la Iringa Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu inazidi kuongezeka, baada ya umoja wake wa vijana (UVCCM Manispaa ya Iringa) kuahidi kuongeza nguvu ili kuufanikisha mkakati huo.

CCM ililipoteza jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 kwa Mchungaji Msigwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayekaribia kumaliza muda wake.

Katika kikao kilichozikutanisha sekretarieti za umoja huo kutoka katika kata zote 18 za manispaa ya Iringa, Mwenyekiti wa UVCCM wa manispaa hiyo, Kaunda Mwaipyana alisema; “katika kukisaidia chama kushinda uchaguzi huo, kauli mbiu yetu ni chama kwanza mtu baadaye.”

“Tutapita katika matawi na kata zetu zote, tutafanya vikao, mikutano ya hadhara na kuwakumbusha vijana wajibu wa kukipigania chama chao ili mkakati wa kulikomboa jimbo ufanikiwe,” alisema.

Katibu wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga aliwaongezea hamasa vijana hao kwa kuwapa seti 60 za jezi na mipira watakazozitumia kuwahamasisha vijana hao kupitia mchezo wa soka.

“CCM ina vijana wengi sana katika jimbo hili, mnahitaji kukutana na kujipanga, tumieni mbinu zote za kukutana, iwe  vikao, mikutano na hata michezo na ndio maana nimewapa msaada huu,” alisema.

Aliwataka vijana wa chama hicho kujitokeza kwenye vikao visivyo rasmi vya maeneo yao wanayoishi na kuitetea CCM kwasababu majibu ya hoja nyingi za wapinzani wanayo.

Akiwakabidhi jezi hizo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM Mkoa wa Iringa, Ephraim Mhekwa alisema  CCM inayo nafasi ya kulikomboa jimbo hilo kama itajipanga vizuri.

“Pamoja na kwamba wapinzani walipata viti 65 katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka jana, wasisahau kwamba CCM ilipata viti 126; hesabu hiyo inadhihirisha chama chetu kinaungwa mkono mara mbili yao,” alisema.

Aliwataka vijana hao kuweka bendera za chama hicho kila panapostahili katika mitaa yote na akawasihi wasikubali kutumika na kukigawa chama kwa maslai ya wachache.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mahamudu Madenge alisema CCM itaendelea kuwepo hata kama watu wasiotaka kufuata utaratibu wataondoka.

“Wameondoka wengi, wengine hii leo ni viongozi wa vyama vikubwa vya siasa. Pamoja na kuondoka kwao CCM ipo pale pale na inaendelea kupata wanachama,” alisema









MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI(MUWSA) YAKAMATA WEZI WA MAJI

$
0
0
Watumishi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,wakiwa katika nyumba moja ambayo inadaiwa mmiliki wake alikuwa akiiba maji baada ya kujiunganishia kinyemera licha ya kukatiwa huduma hiyo kwa muda mrefu.
Wafanyakazi hao wakiongozwa na afisa uhusiano wa mamlaka hiyo ,Frolah Nguma na mkuu wa kanda ya Rau ,Selemani Zabron na fundi Aminiel Swai baada ya kufuatilia katika eneo hilo walibaini wapi wizi wa maji unafanyika.
Hivi ndivyo ilivyooonekana katika mauongio ya mteja wa mamlaka hiyo ambaye mtuhumiwa wa wizi wa maji alifanya usanii wa kujiungia maji bila ya kulipia huku mzigo wa kulipia ankala ya maji ikibaki kwa jirani yake aliyeunganisha bomba kwenye line yake.
Fundi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Aminiel Swai akiondoa bomba liliunganishwa kwa wizi .
Mkuu wa kanda ya Rau wa mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi Selemani Zabron akifukia eneo ambalo hujuma ya kujiunganishia maji ilikuwa imefanyika.
Mmiliki wa nyumba hii ndiye line ya kupeleka maji kwake imekutwa ikiwa imefanyiwa hujuma na kulazimika kulipa bili ya matumizi ya maji kwa nyumba mbili.
Watumishi wa MUWSA wakitazama kama maji yanatoka katika nyumba hiyo mara baada ya kuondoa bomba ambalo lilikuwa likitumika kupeleka maji katika nyumba nyingine kwa njia ya wizi.Hata hivyo katika operersheni hiyo Mtuhumiwa pamoja na mkewe walilazimika kuikimbia nyumba yao na kutelekeza watoto wao wawili wakiume wenye umri wa kati ya miaka miwili na minne.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ,LEONIDAS GAMA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA KILIMANJARO.

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama akizungumza wakati alipokutana na wafanyabiashara katika viwanja vya Kili Homes mjini Moshi kuzungumzia kero mbalimbali zinazowakabili pamoja na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazo wakabili.kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga.
Baadhi ya wafanyabiashara wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro katika mkutano huo.
Mjumbe wa kamati maalumu ya kuratibu kero za Biashara mkoa wa Kilimanjaro Patrick Boisafi akisoma kero zilizoratibiwa mbele ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama.
Baadhi ya wafanyabiashara.
Katibu wa Jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania ,tawi la Kilimanjaro,Mmasi Sambuo akisoma kero mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara Kilimanjaro mbele ya mkuu wa mkoa.
Wafanyabiashara wakifuatilia mkutano huo.
Add caption
Mfanyabiashara Ibrahim Shayo akitoa kero mbele ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakati wa mkutano wa wafanyabiashara,maofisa wa TRA,manispaa ya Moshi pamoja na mawakala wa mashine za EFD'S ulioongozwa na mkuu wa mkoa Leonidas Gama.
Baadhi ya wafanyabiashara wakitoa kero zao.
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ,TRA mkoa wa Kilimanjaro Abdul Mapembe akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali pamoja na kero zilizoibuliwa na wafanyabiashara wakati wa mkutano huo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Benki ya Exim yatangaza ongezeko la asilimia 35 la faida ya kabla ya kodi

$
0
0
 Kaimu Afisa Mkuu wa fedha wa benki ya Exim Tanzania Bw. Issa Hamisi (wa kwanza kutoka kulia) akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari  wakati akitoa  taarifa ya mapato ya mwaka 2014 ya benki ya hiyo jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Mkuu wa kitengo cha rasilimali watu wa benki hiyo , Frederick Kanga (wa pili kulia) na Mkaguzi mkuu wa ndani wa hesabu za benki hiyo, George Binde (kushoto) .
 Meneja Mwandamizi utafiti na Uchambuzi wa Biashara wa Benki ya Exim Tanzania,  Joseph Mrawa (wa pili kulia) akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari  wakati akitoa  taarifa ya mapato ya mwaka 2014 ya benki hiyo  jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Kaimu Afisa Mkuu wa fedha wa benki ya Exim Tanzania Bw. Issa Hamisi (wa kwanza kutoka kulia) Mkuu wa kitengo cha rasilimali watu wa benki hiyo , Frederick Kanga (wa pili kulia) na Mkaguzi mkuu wa ndani wa hesabu za benki hiyo, George Binde (kushoto) 
 Mkuu wa kitengo cha rasilimali watu wa benki ya Exim Tanzania, Frederick Kanga (katikati ) akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari  wakati akitoa  taarifa ya mapato ya mwaka 2014 ya benki hiyo  jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Kaimu Afisa Mkuu wa fedha wa benki ya Exim Tanzania Bw. Issa Hamisi (wa kwanza kutoka kulia) naMkaguzi mkuu wa ndani wa hesabu za benki hiyo,George Binde (kushoto) 

BENKI ya Exim Tanzania imepata ongezeko la faida (kabla ya  kodi) kwa mwaka 2014 la asilimia 35 kufikia shilingi bilioni 24.1 kutoka shilingi bilioni 17.9 kwa mwaka 2013. Benki imeendelea kuwa na mali za shilingi tilioni 1 na kuweza kukuza pato la wenyehisa kwa asilimia 23 kufikia shilingi bilioni 190 ikilinganishwa na shilingi bilioni 154 iliyorekodiwa mwaka Jana.

 "Tunafuraha kubwa kuitangaza kwenu mafanikio makubwa ya kifedha ya mwaka 2014 Desemba,” alisema Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha Bw. Issa Hamisi, akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam Jana.

Alisema kuwa benki hiyo imefanikiwa kupata faida (baada kodi) kiasi cha sh bilioni 57.3 kutoka sh billion 44.2 iliyopatikana mwaka 2013 ikiwa ni ongezeko la asilimia 30, ikilenga zaidi katika ongezeko la amana zenye gharama nafuu.

Kwa mujibu wa Bw. Hamisi, pia masuala ya ada, kamisheni na mapato ya fedha za kigeni yaliongezeka kwa asilimia 25 hadi kufikia shilingi bilioni 38 kutoka shilingi bilioni 30.4  kwa mwaka uliopita. Ukuaji huu kwa kiasi kikubwa umechangiwa na kasi ya ukuaji katika shughuli ya za biashara za fedha za kigeni, bidhaa za biashara ya fedha na ada kutoka kwenye  utoaji wa huduma  mbadala.

Mali za benki zimekuwa wakati ‘Gross NPA ratio’ ikishuka kutoka asilimia 9.60 kwa mwaka 2013 kufikia asilimia 6.83 mwishoni mwa mwaka uliyolipotiwa.

Benki hiyo pia iliweka mkakati wa miaka mitatu mwanzo kabisa wa mwaka huo 2014 ambao ulilenga kujiongezea soko lake la amana sambamba na kufikia nafasi ya uongozi katika malipo.

Bw. Hamisi aliongeza kuwa benki imeweka mkakati wa kuzidi kujiimarisha na kuimarisha watu wake, shughuli zake pamoja na teknolojia. Alisema benki imeweza kufanyakazi na makampuni bora ya kimataifa katika utoaji ushauri kwenye masuala yajulikanayo kama Enterprise-wide Risk Management, na pia kuweza kurahisisha zaidi ufanyaji wa shughuli zake kwa mwaka huo.

Aidha Bw Hamisi aliongeza kuwa benki imendelea jitihada za kupanua wigo wa huduma zake kwa kuongeza idadi ya matawi mawili kwenye nchi tatu ambazo inatoa huduma zake vikiwemo visiwa vya Comoro na nchini Djibouti.

“Mafanikio haya ni mwangaza tosha katika utendaji wetu wa sasa na siku zijazo….kwa sasa Exim imejenga msingi imara kitu ambacho kinatuhakikishia mafanikio zaidi kwa mwaka huu 2015,’’ aliongeza Bw Hamisi.

Benki imeendelea kujidhatiti katika urejeshaji wa kile ikipatacho toka kwa jamii. Katika mwaka huo benki ilijikita zaidi katika kusaidia taasisi za elimu, hospitali na taasisi nyinginezo.

WATU 24 WANAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA KUFUATIA AJALI MBAYA YA GARI LA ABIRIA ( HIACE ) ILIYOTOKEA LEO ASUBUHI KIWIRA MKOAINI MBEYA.

$
0
0
"Ajali ya Hiace imeua watu 24 eneo la Uwanja wa ndege Kiwila Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya. Wadau Niko eneo la tukio, mpaka sasa miili 22 imefanikiwa kutolewa. Kwani Hiace hii ilitumbukia mtoni na bado miili miwili imenasa, ndiyo inatolewa muda huu,

Watu wawili tu ndio wamepona akiwemo kondakta. Ajali hii imetokea wakati Coaster zinazofanya safari zake kati ya Mbeya na Kyela kugoma hivyo baadhi ya hiace za mjini kuamua kubeba abiria. Inaonekana ni ugeni Wa barabara, speed na gari kukosa break za kuaminika.",

Hiyo ni taarifa tuliotumiwa sambamba na picha ndani ya chumba chetu cha habari mapema leo asubuhi kuhusiana na tukio hilo la kusikitisha.

MUNGU AZILAZE ROHO ZA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN.

BASATA YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA MSANII CHIJWELE CHE MUNDUGWAO

$
0
0
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa kifo cha Msanii wa muziki wa asili Chijwele Chemundugwao kilichotokea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam leo mapema Asubuhi ya Alhamisi ya tarehe 16/04/2015 baada ya kuugua kwa muda mrefu. 

Che mundugwao ni msanii wa muziki wa asili na mdau wa muda mrefu wa sekta ya Sanaa nchini. Amekuwa na mchango mkubwa katika kukuza muziki wa asili nchini na baadaye kupitia Chama cha Muziki wa asili (TAFOMA) nchini alishiriki kikamilifu kwenye mchakato wa uanzishwaji wa Shirikisho la Muziki ambalo linaviunganisha vyama vya wasanii wanamuziki nchini.

Mchango wake katika muziki wa asili na katika kujenga mfumo wa utawala wa wasanii nchini hautasahaulika kamwe. 

Ni mdau aliyeacha misingi katika sekta ya muziki na amejitolea kwa kiasi kikubwa katika kuufikisha muziki huu mahali ulipo leo.

Baraza, wasanii na wadau wote wa Sanaa hatuna budi kuendelea kuenzi mema yote aliyotuachia marehemu Che mundugwao hasa katika kupenda kujitolea muda mwingi kufanikisha ufanisi kwenye sekta ya Sanaa.

Baraza linatoa pole kwa ndugu wa marehemu, shirikisho la muziki, wasanii na wadau wote wa Sanaa kwa msiba huu. 

Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Amen

Godfrey Mngereza
KATIBU MTENDAJI

Benki ya CBA kuuza nyumba za kampuni Avic kwa mikopo ya masharti nafuu.

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CBA Tanzania  Bw.Julius Mcharo (kulia) akibadilishana mkataba na Naibu Meneja wa kampuni ya Avic International Real Estate Bw.Liu De Xzang (kushoto) muda mfupi baada ya kusaini mkataba ambapo CBA itawakopesha wateja wanaotaka kununua nyumba zilizojengwa na kampuni hiyo katika eneo la kigamboni jijini Dar es Salaam.Anayeshuhudia nyuma kulia ni Mwanasheria wa CBA ,Bi.Lilian Musingi.Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CBA Tanzania  Bw.Julius Mcharo (katikati) akiwa pamoja na maofisa wa CBA na  Avic International Real Estate wakiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani)  muda mfupi kabla ya kusaini mkataba ambapo CBA itawakopesha wateja wanaotaka kununua nyumba zilizojengwa na kampuni hiyo katika eneo la kigamboni jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CBA Tanzania  Bw.Julius Mcharo (kulia) akibadilishana mkataba na Naibu Meneja wa kampuni ya Avic International Real Estate Bw.Liu De Xzang (kushoto) muda mfupi baada ya kusaini mkataba ambapo CBA itawakopesha wateja wanaotaka kununua nyumba zilizojengwa na kampuni hiyo katika eneo la kigamboni jijini Dar es Salaam.Anayeshuhudia nyuma kulia ni Mwanasheria wa CBA ,Bi.Lilian Musingi.Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki ya CBA,Bi.Hyasintha Mwimanzi akiwaleza waandishi wa habari  utaratibu wa mkopo wa nyumba utakavyokuwa muda mfupi baada ya muda mfupi baada ya kusaini mkataba ambapo CBA itawakopesha wateja wanaotaka kununua nyumba zilizojengwa na kampuni  ya Avic International Real Estate   katika eneo la kigamboni jijini Dar es Salaam.Wengine pichani ni wakuu wa taasisi hizo na maofisa waandamizi waliokuwepo kushuhudia utiaji saini makubaliano hayo.

Wakuu wa taasisi za CBA na Avic International Real Estate wakifanya majadiliano na maofisa wao muda mfupi baada ya kusaini mkataba ambapo CBA itawakopesha wateja wanaotaka kununua nyumba zilizojengwa na Avic International Real Estate   katika eneo la kigamboni jijini Dar es Salaam


Benki ya CBA Tanzania imeingia mkataba na kampuni ya uwekezaji katika ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ya Avic International Real Estate(T) yenye makao makuu yake nchini China ambapo itatoa mikopo wenye riba nafuu kwa watanzania wanaotaka kununua nyumba.
Mkataba wa makubaliano umefikiwa leo katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo na kuhudhuriwa na maofisa waandamizi kutoka taasisi hizi mbili.

Akiongea  baada ya kusaini makubaliano Mtendaji Mkuu wa CBA,Bw.Julius Mcharo,alisema kuwa ni wakati mwingine imetokea fursa kwa watanzania ambayo itawawezesha kumiliki nyumba zao nzuri zilizojengwa  na kampuni ya Avic kwa ubora wa hali ya juu katika eneo la Kigamboni jjijini Dar es salaam.

Bw.Mcharo alisema CBA imejipanga kubadilisha maisha ya watanzania na kuhakikisha wanapata makazi bora kwa kushirikiana na wawekezaji katika sekta ya ujenzi wa nyumba. “Benki yetu imejipanga kuhakikisha inatoa mikopo ya riba nafuu kwa wananchi wanaotaka kununua nyumba za makazi na tumepanga muda mrefu wa malipo ambao hauwaumizi wanunuaji wa nyumba ambapo makato ya mkopo yanafanywa hadi kufikia miaka 20”.Alisema.

Naye Meneja wa kitengo cha wateja binafsi wa benki hiyo Bi.Hyasinta Mwimunzi,alisema nyumba za mradi zinazouzwa ni za makazi zenye ukubwa wa vyumba vya kulala 2 na sebule bei yake inafikia dola 150,000 ambazo zinalipwa kwa kipindi cha miaka mpaka 20 na riba yake ni nafuu ambayo sio zaidi ya asilimia 16 kwa fedha za kitanzania na dola 8 wa watakaokopa kwa fedha za kigeni.

  Meneja Msaidizi wa kampuni ya Avic International Real Estate,Bw.Liu De Xiang,alisema wanafurahi kufanya kazi na benki kubwa na yenye uzoefu wa kutoa mikopo ya nyumba ya CBA Tanzania.

Alisema kampuni  itaendelea kuwekeza katika sekta ya ujenzi wa nyumba za makazi za gharama nafuu hapa nchini na amewataka watanzania wachangamkie fursa ya mikopo ya kununua nyumba na alizipongeza taasisi za fedha ambazo zimeanza kutoa mikopo ya ununuzi wa nyumba kwa wananchi.

Kigamboni ni moja ya eneo ambalo serikali inafanya jitihada za kuliboresha kuwa mji wa kisasa na hivi sasa taasisi na makampuni mbalimbali yanaendelea kuwekeza kwenye eneo hilo lililopo katika manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.

KIWANDA CHA TUMBAKU MOROGORO CHAFANYA SHERERE KUFUNGA MSIMU NA KUFUNGUA MSIMU MPYA

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akitoa hotuba yake wakati wa sherehe za kumaliza msimu uliopita na kukaribisha msimu mwingine pamoja na kutoa zawadi kwa wafanyakazi waliotumikia kampuni hizo kwa muda mrefu pamoja na wafanyakazi bora zilizofanyika Kiwandani hapo.

Katika Hotuba yake Mkurugenzi Huyo alisema Makampuni hayoyamesaidia Mkoa wa Morogoro kuanza kuinuka kiuchumi kutokana na kutoa ajira za msimu takribani 3000 kila mwaka na kusaidia kupunguza matatizo ya uhalifu yaliyokuwa yakifanywa na vijana wasio kuwa na shughuli  za kujiingizia kipato. 
Mkurugenzi mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akikabidhi zawadi kwa wafanyakazi waliofanya kazi kwa muda mrefu Ambao wamefanya kazi kwa zaidi ya Miaka 15 Mfululizo.
Mkurugenzi mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akiwapakulia Chakula waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa tafrija hiyo
Mkurugenzi wa Ufundi wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) Henry Lembert Akiwahudumia wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa Sherehe ya Kufunga Msimu.

Mkurugenzi mkuu w David Crowhorst akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda hicho
 Picha ya Pamoja ya waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda cha Tumbaku  cha Mkoani Morogoro

MSD YABORESHA HUDUMA ZA UTOAJI TAARIFA KWA WATEJA WAKE.

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Huduma kwa Wateja na Shughuli za Kanda Bohari ya dawa (MSD), Edward Terry,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika ukumbi wa habari MAELEZO jijjini Dar es Salaam leo kuhusu utendaji na mipango ya Bohari ya Dawa (MSD) na Ofisa Uhusiano Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD),Etty Kusiluka.

Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

 BOHARI ya dawa (MSD) imeboresha huduma  kwa wateja wake kwa kutoa taarifa zinazomhusu mteja kwa kuziweka wazi katika tovuti yao.
 Akizungumza na wandishi wa habari  katika ukumbi wa  Idara ya Habari MAELEZO jijini Dar es Salaam leo.Kaimu Mkurugenzi Huduma kwa Wateja na Shughuli za Bohari ya Dawa (MSD), Edward Terry,  amesema kuwa taarifa hizo ni za mali inayopatikana gharani, taarifa za kiasi cha fedha za wateja kilichopo katika kila akaunti,fomu za marejesho pamoja na bei za bidhaa na bei zake.


Pia Terry amesema kuwa wateja wenye mahitaji ya dawa au vifaa wanatakiwa kuandika barua kuelezea mahitaji yao pamoja na maelekezo mhimu ya kifaa husika na kutatuliwa na kitengo cha manunuzi ya bohari hiyo.

MAZISHI YA DKT OMAR MAKAME SHAURI ZANZIBAR

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu kulia akijumuika na Viongozi na Waislamu mbali mbali katika kumswalia aliyekuwa katibu Mkuu Wizara ya Afya na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Marehemu Dkt.Omar Makame Shauri katika Msikiti wa Kidombo Wilaya ya Kaskazini A Unguja kabla ya mazishi yake leo,[Picha na Ikulu.]
2
aadhi ya wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislamu wakilibeba jeneza la aliyekuwa katibu Mkuu Wizara ya Afya na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Marehemu Dkt.Omar Makame Shauri aliyezikwa leo kijijini kwao Kidombo Wilaya ya Kaskazini A Unguja,
3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,Makamo wa kwanza wa Rais Maalim Seif Sherif na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi (katikati) wakiwa na Viongozi wengine na Wananchi katika mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Marehemu Dkt.Omar Makame Shauri aliyezikwa leo  kijijini kwao Kidombo Wilaya ya Kaskazini A Unguja,
4
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein(katikati)akitia udongo kufukia kaburi laaliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Marehemu Dkt.Omar Makame Shauri aliyezikwa leo  kijijini kwao Kidombo Wilaya ya Kaskazini A Unguja,

APPLICATION FOR TRAINING AND EMPLOYMENT OPPORTUNITIES

$
0
0
The Director General of the Tanzania Meteorological Agency wishes to re-announce availability of training opportunities for Meteorological Technicians within the Agency. This announcement was earlier made on 12 December 2014. For those who have already applied are not supposed to re-apply.

Qualifications:

  1.  Form six leavers with two principal passes in mathematics and physics. Passes in chemistry and geography will be an added advantage.

  2.  Should be not more than 22 years of age by 12 December 2014.

  3.  Women are highly encouraged to apply.


Mode of application:

Applicants are required to pay a non-refundable processing fee of TShs. 10,000 through NMB Bank, A/C Name-Tanzania Meteorological Agency, A/C No. 20101000013.


Duly filled application forms with detailed curriculum vitae, copies of certified academic certificates, three referees, a recent photograph, daytime telephone numbers and bank pay in slip should be mailed to:


Director General,

Tanzania Meteorological Agency,

P.O. Box 3056,

Fax: + 255-22-2460735

Dar es Salaam.

Email:met@meteo.go.tz


Deadline : 22/April/2015


Please note that application forms may be downloaded from the TMA website wwww.meteo.go.tzor obtained from Tanzania Meteorological Agency Headquarters, 3rd  floor,  Ubungo Plaza, Morogoro Road, Dar es Salaam


It should be noted that applications sent without application forms will not be considered and only short listed candidated will be contacted.



Successfully candidates will be required to undergo one year training course at the Agency’s National Meteorological Training Centre, Kigoma. Employment will only be granted after successful completion of the Course.

MABARAZA YA WAFANYAKAZI TAASISI ZA ELIMU YA JUU YATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

$
0
0
Naibu Waziri wa Fedha (Sera) Mhe. Mwigulu Nchemba (katikati) akiwa ameambatana na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania Dkt. Joseph Kihanda (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara Prof. Isaya Jairo kabla ya kuzindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) lililojumuisha wawakilishi kutoka matawi 6 ya taasisi hiyo katika mikoa ya Kigoma, Singida, Mwanza , Mtwara, Dar es salaam na Mbeya.
Naibu Waziri wa Fedha (Sera) Mhe. Mwigulu Nchemba wakati akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) leo mjini Bagamoyo.
Wajumbe wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiimba wimbo wa mshikamano daima kabla ya kuanza kwa mkutano wao leo mjini Bagamoyo.

SOMA ZAIDI HAPA


Marufuku Kupiga Kelele Tanzania

$
0
0
 Na victor Mariki – Ofisi ya Makamu wa Rais.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Maku wa Rais - Mazingira, Mh. Binilith Mahenge, amezindua Kanuni mpya ya Mazingira itakayodhibiti uchafuzi wa mazingira unaotokana na makelele yanayosabishwa na shughuli mbalimbali katika jamii .

Akizungumza katika uzinduzi wa Kanuni hizo  jijini Dar es Salaam, Mh. Mahenge alisema kuwa Ofisi yake ilishazitangaza Kanuni hizo katika Gazeti la Serikali tangu tarehe 30/01/2015 kulingana na Sheria ya Usimazi wa Mazingira ya mwaka 20104.

Aidha Mh. Mahenge aliongeza  kuwa Sheria hiyo ya Mazingira ya mwaka 2004 iliyoanza kutumika rasmi  tarehe 1 Julai, 2015 inaiwezesha  Ofisi yake kuandaa na kuunda kanuni mbalimbali za mazingira ili kudhibiti uchafuzi wa mazingira nchini.

Hata hivyo alifafanua kuwa kanuni mpya za kudhibiti kelele, hazitadhibiti kelele zitokanazo na ving`ora vya magari ya Polisi, magari ya zimamoto, magari ya kubebea wagonjwa pamoja na  mizinga wakati wa magwaride katika sherehe za kitaifa.

Kanuni hizi zimeundwa kuitikia wito wa malalako kuotoka kwa wadau mbalimbali waliokuwa wakiilalamikia serikali kuhusu uchafuzi mkubwa wa mazingira unaotokana na kelele katika kumbi za starehe, uchmbaji wa madini pamoja namitetemo inayosabishwa na minara ya simu

HALI YA UCHUMI TANZANIA SASA NI SHWARI

$
0
0
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya akimsikiliza kwa makini Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier walipokutana katika mikutano hii ya kipupwe inayoendelea hapa Mjini Washington DC.Wengine ni ujumbe kutoka Tanzania pamoja na timu ya wataalam kutoka Benki ya Dunia.
2
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum akifuatilia kwa makini maswalialiyokuwa akiulizwa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier hayupo kwenye picha. Kulia ni katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar Bw.
3
Ujumbe wa Mkutano huo kutoka pande zote mbili yaani Tanzania na Benki ya Dunia, wakimsikiliza kwa makini Mchumi mwandamizi kutoka Benki ya Dunia.
4
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akijadiliana jambo na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier kabla ya kikao kuanza rasmi.
5
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akiandika kwa makini hoja na mapendekezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier.
6
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akijibu na kueleza kwa umakini hoja na mapendekezo yaliyokuwa yametolewa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier.

…………………………………………………
Wakati Tanzania ikiendelea kupambana na umaskini , Benki ya Dunia imesema kuwa,” tumefurahishwa sana na mwenendo mzuri wa usimamizi wa fedha na bajeti”. Hayo yalisemwa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier katika mkutano ambao waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya Salum alikuwepo.
Mambo mbalimbali yalizungumziwa katika mkutano huo ambapo suala la upatikanaji wa fedha kusaidia bajeti ya serikali lilipewakipaumbele.Maboresho katika Sekta ya umeme nalo jambo mojawapo liliopewa uzito kwani Nchi wahisani wamepata moyo wakuachia misaada baada ya kuona Serikali imeweza kulishughulikia suala zima la IPTL.
“ Nchi wahisani wamekubali kuendelea kutoa misaada kwa asilimia mia, hii ni kwa sababu tu! serikali yenu imekubali kuchukua hatua dhidi ya tatizo la IPTL”, alisema Philippe.
Akizungumza na waandishi wa habari Mhe. Mkuya alisema kuwa, suala la kuboresha Pension nalo lilizungumziwa na chombo hiki kitasaidia serikali katika kuboresha malipo ya uzeeni (pension) na kuwezesha mashirika ya “pension” ili yaweze kuwa na uwezo wa kusaidia wastaafu. Aidha tumekubaliana kuwa watatusaidia katika suala zima la kuboresha uwazi serikalini na mazingira ya biasha Tanzania.Aliongeza Mkuya.
Jambo lingine lililochukua uzito katika majadiliano hayo ni suala la kufanya ukaguzi Bandarini. Hili limejitokeza baada ya kubainika kuwa kuna baadhi ya wafanya biashara sio waaminifu hivyo benki ya Dunia imeitaka Serikali kuangalia upya maamuzi ya mwanzo ya serikali yakuto kagua mizigo, na kusema kuwa wanasubiri majibu juu ya kubadilisha utaratibu wa mwanzo. Tanzania imekubali kukaa kwa pamoja Wizara na Fedha na TRA ili kurudisha majibu na mkakati ambao kama serikali watakuwa wamekubaliana.
“Kumekuwa na madai mengi ambayo yanadaiwa na makandarasi na wafanyabiashara wadogo, tutajitahidi kuyalipa iliyaishe lakini kwa wale wenye nyaraka halali, tunaenda kupiga marufuku kwa Afisa masuuli wote kuwa kuanzia sasa hakuna kufanya malipo yoyote kama hakuna fedha kwa ajili ya shughuli hiyo”.Alisema Mkuya.
“ Hii itasaidia kupunguza madeni. Ninasema haya kwani ndicho kitu tulichokubaliana kwenye mkutano huu”. Alisistiza Mkuya.
Mikutano hiyo bado inaendelea hapa mjini Washington DC. Hali ya hewa ni baridi kiasi.
Imetolewa na Msemaji :Wizara ya fedha
Ingiahedi C.Mduma
Washington DC
16/04/2015

Mkutano wa Injili Washington DC...WAZO LA JIONI (April 17, 2015)

$
0
0
Mch Wilbert Nfubhusa
Katika WAZO LA JIONI hii ya leo (Aprili 17, 2015), Mch Wilbert Nfubhusa ameendelea kuzungumzia kuhusu WAZO KUU la Mkutano huu ambalo ni KUFANANA NA YESU
Pia, alielezea ushuhuda aliosimuliwa na wakimbizi toka Burundi
Japo unafurahisha, lakini unafunza sana
KARIBU

Zaidi ya 74% ya wanandoa wamepata elimu ya afya ya uzazi na jinsia

$
0
0
 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Digital Opportunity Trust Bw. Eliguard Dawson akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Mbagala Zakheem uliopo wilayani Temeke leo wakati wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke.

 Afisa Vijana wa Kituo cha Vijana UMATI –Temeke jijini Dar es Salaam akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati  wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo hicho na kufanyika katika Mtaa wa Mbagala Zakheem uliopo wilayani Temeke leo

 Baadhi ya Vijana wakifuatilia maigizo kutoka kwa makundi mbalimbali ya vijana yaliyokuwa yakutoa elimu ya kuhusu afya ya uzazi na jinsia kwa nija ya sanaa ya maigizo wakati wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke leo

 Kikundi cha sanaa kutoka kundi la Mkubwa na Wanawe wakiigiza kuhusu matumizi ya njia za uzazi wa mpango wakati wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke na kufanyika katika mtaa wa Mbagala Zakheem leo

 Kikundi cha sanaa kutoka kundi la Mkubwa na Wanawe wakiigiza kuhusu matumizi ya njia za uzazi wa mpango wakati wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke na kufanyika katika mtaa wa Mbagala Zakheem leo.

 Kikundi cha sanaa cha Ndio Sisi Group wakiigiza kuhusu matumizi ya njia za uzazi wa mpango wakati wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke na kufanyika katika mtaa wa Mbagala Zakheem leo

 Kikundi cha sanaa cha Ndio Sisi Group wakiigiza kuhusu matumizi ya njia za uzazi wa mpango wakati wa tamasha la Jamvi la Vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke na kufanyika katika mtaa wa Mbagala Zakheem leo. 
Mmoja wa vijana waliohudhuria Jamvi la vijana lililoandaliwa na  Kituo cha Vijana cha UMATI –Temeke na kufanyika katika mtaa wa Mbagala Zakheem akipata huduma ya ushauri nasaha ambayo ilikuwa ikitolewa bure wakati wa tamasha hilo leo.Picha na Frank Shija, WHVUM


TIMU YA HARAKATI YA IMETOSHA YATEMBELEA KITUO CHA BUHANGIJA, MKOANI SHINYANGA

$
0
0
Ilikua mishale ya saa kumi kamili jioni ujumbe wa harakati za Imetosha ulipowasili katika kituo cha Buhangija cha kulea watoto wenye mahitaji maalumu mjini Shinyanga. Sauti za furaha za watoto zilisikika zikiimba nyimbo za kukaribisha ujumbe wa wana harakati hao ambao wako Mwanza kutambulisha harakati za Imetosha ambazo ni kupambana na kupinga unyanyapaa, ukatili na mauaji kwa watu wenye Ulemavu wa ngozi.
 Akiongea na watoto kituoni hapo Mwenyekiti wa harakati za Imetosha Masoud Ali (Kipanya) alisema Imetosha inatambua umuhimu wa haki ya kuishi kwa kila binadamu ndio maana Imetosha imeanzisha harakati za kutokomeza mauaji na unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.  “Tunatambua hapa kati yenu kuna vipaji vya aina mbalimbali hivyo pamoja na kupambana na harakati za kupinga na kutokomeza mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi tupo hapa kuwatia moyo kuwa mna uwezo mkubwa ndani yenu hivyo msijidharau” alisema Masoud.
Wajumbe wa Imetosha

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI

Mtanange wa Yanga na Etoile Du Sahel ya Tunisia uwanja wa Taifa

$
0
0
Mchezaji wa Timu ya Etoile Du Sahel ya Tunisia, Bounedjah Baghdad akiangalia namna ya kuwatoka wachezaji wa Yanga, Mbuyu Twite na Amissi Tambwe wakati wa mchezo wa Kimataifa wa Kombe la Shirikisho unaoendelea kupigwa hivi sasa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam. Kipindi cha pili kimeanza hivi punde na matokeo ni 1-1.Picha zote na Othman Michuzi.
 Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa akiruka daluga la Beki wa Timu ya Etoile Du Sahel ya Tunisia wakati wa mchezo wa Kimataifa wa Kombe la Shirikisho unaoendelea kupigwa hivi sasa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam. Kipindi cha pili kimeanza hivi punde na matokeo ni 1-1.
 Wachezajiwa Timu ya Yanga, wakishangilia ushindi sambamba na mashabiki wao.
Kiungo wa Timu ya Etoile Du Sahel ya Tunisia, Franck Kom aruka juu kuwania mpira wa kichwa wakati wa mchezo wa Kimataifa wa Kombe la Shirikisho unaoendelea kupigwa hivi sasa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam. Kipindi cha pili kimeanza hivi punde na matokeo ni 1-1.

Picha zaid zitawajia baadae kidogo.

UMOJA WA TAASISI ZA HIJJA ZANZIBAR ZAANDAA KONGAMANO KWA MAHUJAJI WATARAJIWA

$
0
0
………………………………………………………………………………….
Na Ramadhani Ali –Maelezo Zanzibar
Waislamu wa Zanzibar wanaotegemea kutekeleza Ibada ya Hijja mwaka huu wameshaurfiwa kukamilisha mipango ya safari hiyo mapema ili kuziwezesha Taasisi zinazosafirisha mahujaji kuweza kukamilisha taratibu mpya zilizowekwa na Serikali ya Saudi Arabia.
Akizungumza katika Kongamano la mahujaji watarajiwa lililofanyika  ukumbi wa Beit al Yamin Malindi, Afisa kutoaka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Ustaadh Khalid Mohammed Mrisho amesema Serikali ya Saudi Arabia imefanya mabadiliko makubwa ya taratibu za maandalizi ya Hijjah kuanzia mwaka huu.
Amesema wamefanya maamuzi hayo baada ya malalamiko yaliyokuwa yakitolewa na  mahujaji kutokana na vitendo vya udanganyifu  vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya Taasisi zinazosafirisha mahujaji kutoka mataifa mbali mbali duniani.
“Baadhi ya viongozi wa Taasisi zinazosafirisha mahujaji walikuwa wakiwatoza fedha mahujaji wao kwa ajili ya kulipia Viwanja vya ndege vya Makka na Madina lakini walikuwa hawalipi na mahujaji kuzuiliwa kwa saa kadhaa,”alisema Ustaadh Khalid.
Taasisi nyengine alisema zilikuwa zinawaahidi mahujaji kuwakodia nyumba nzuri za karibu  katika miji mitakatifu ya Makka na Madina lakini wanapofika huko huwekwa kwenye nyumba mbovu  na wengine hukosa huduma ya chakula.
Amesema katika kukabiliana na matatizo hayo Serikali ya Saudia Arabia kuanzia sasa imeziagiza Taasisi  zinazosafirisha mahujaji kufanya taratibu zote za maandalizi ya safari, makaazi na matembezi kwa njia ya mtandao na kulipa gharama zote wakiwa nchini mwao.
Amesema iwapo taratibu hizo hazikukamilika hujaji atakosa visa ya kuingia Saudi Arabia na atakuwa amekosa kutekeleza ibada ya Hijjah kwa mwaka huo.
Ameongeza kuwa  mwaka huu nchi hiyo imeweka hadi tarehe 27 Juni kuwa ni siku ya mwisho  kukamilisha taratibu za mahujaji na baada ya tarehe hiyo mtandao huo utakuwa umefungwa na itakuwa hakuna njia nyengine.
“Lengo la uwamuzi huo wa  Saudi Arabia  ni kuwaondoshea mahujaji usumbufu usiowalazima  wakati wa kutekeleza  ibada hiyo,”alisisitiza Ustaadh Khalid.
Amewakumbusha mahujaji watarajiwa kuwa waangalifu na mizigo yao  wakati wa safari na wanapokuwa  nchini humo  na watakaporejea kuchukua kiwango cha mizigo kinachokubalika kwenye ndege.
Akifungua Kongamano hilo lililoandaliwa na Umoja wa Taasisi za Hijja Zanzibar (UTAHIZA) Mwenyekiti wa Bodi Sheikh Khamis Abdulhamid amewasisitiza waislamu wenye uweze kutekeleza ibada ya hijja ili kukamilisha uislamua wao.
Mwaka huu Tanzania imepewa nafasi 3,000  kupeleka mahujaji nchini Saudi Arabia ambapo ibada hiyo hutekelezwa kila mwaka mwezi wa mfunguo tatu

ZITTO ATEMBELEA KITUO CHA ALBINO BUHANGINJA MKOANI SHINYANGA

$
0
0
 
1
Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, akizungumza na watoto walemavu wenye albinism,walemavu wa macho na viziwi waliopo kwenye kituo cha kuwahifadhi cha Buhanginja Mkoani Shinyanga jana.
345
Mwalimu wa kituo cha Shule maalum kwa watoto walemavu wenye albinism, walemavu wa macho na viziwi waliopo kwenye kituo cha kuwahifadhi cha Buhanginja Mkoani Shinyanga, Peter Francis, akiwapa maelezo ya kituo hicho viongozi wa ACT-Wazalendo walipofanya ziara kwenye kituo hicho sehemu wanazo lala watoto.Picha na Said Powa.6
Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, akizungumza na mmoja wa watoto hao.
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images