Usikae kimya! Wafanye wabadilike
↧
↧
Umuhimu wa kudhibiti matumizi ya vyombo vya elektroniki kwa watoto na vijana
Zaidi ya asilimia 60 ya watoto wenye umri wa miaka 13 hadi 17 wanatumia zaidi ya masaa mawili kila siku kuangalia mitandao ya kijamii pamoja na vipindi mbalimbali vya Televisheni. Hii inaweza kuwa njia kubwa ya kuunganisha, lakini pia kuna hatari zinazohusiana na kutumia muda mwingi sana kwenye vyombo vya habari kijamii.
Leo hii ni nadra kukuta familia ambazo watoto na vijana wake hawajaathirika na vyombo vya habari na elektroniki kama vile televisheni, intaneti na michezo mingine tofauti ya kompyuta.
Hata hivyo utumiaji mkubwa na wa masaa mengi wa vyombo hivyo hauwahusu watoto na vijana tu, bali watu wazima pia wameathirika na jambo hilo.
Kutokana na sababu kadhaa za kimwili, kisaikolojia na kiroho, kuna udharura kwa watoto kusimamiwa vyema na wazazi, mashirika na taasisi za kielimu na kiutamaduni na kadhalika vyombo vya habari ili kupunguza madhara yanayotokana na matumizi mabaya ya vyombo hivyo vya elektroniki. Licha ya kompyuta kuwa na pande chanya tofauti za kimaendeleo, hasa katika nyanja za kielimu na huduma za mawasiliano, lakini chombo hicho pia kina nafasi hasi kwa watoto na hata kwa watu wazima.
Utumiwaji usio na udhibiti wa chombo hicho na kadhalika vyombo vingine vya elektroniki kama vile televisheni, unaweza kuyaweka hatarini maisha ya watoto kutokana na athari zake mbaya kwa ustawi wa kiroho, kisaikolojia na kijamii wa watoto hao.
Harakati zetu za kifizikia na miamala yetu tofauti ya kijamii, ni umuhimu yenye taathira kubwa kwa afya na tabia za mtoto. Kinyume chake, ikiwa mtoto atatumia muda wake mwingi katika matumizi ya michezo ya kompyuta, basi hawezi kunufaika na upande chanya wa kujenga akili yake wala harakati bora kwa ajili ya kuufikia ukamilifu wake kijamii.
Mbali na hayo, watoto pia wanaweza kukabiliwa na hatari ya kutekeleza vitendo vya ukatili na visivyo vya kikatili hata katika umri wao mdogo. Hali hiyo ambayo inaweza kufikiwa ghafla au hata kwa makusudi, huwaletea watoto na vijana madhara yasiyoweza kufidika hasa kuhusiana na masuala ya kiafya, kisaikolojia sambamba na kueneza kwa kiasi kikubwa matatizo ya kimwili na kiakili kama vile utovu wa maadili, vitendo vya ukatili, madawa ya kulevya, tabia mbaya katika jamii, kuzorota thamani za familia na kuenea jinai na uhalifu wa kila aina katika jamii.
Ukweli ni kwamba, wazazi hawajawachwa peke yao katika jukumu la kutoa malezi bora kwa watoto wao, bali wataalamu wa mambo wamefanya utafiti wa kina katika uwanja huo na kuwasaidia katika suala hilo kwa kuwasilisha njia bora za malezi ambazo zinawavutia watoto na kuwafanya waishi maisha bora katika jamii.
Watafiti hao wanasema kuwa, licha ya kwamba haiwezekani kuwatenga watoto na ulimwengu wa michezo ya kompyuta lakini tunaweza kuwaepusha na madhara ya michezo hiyo kwa kutumia njia na mbinu zinazofaa.
Udhibiti fulani wa matumizi ya kompyuta kila siku au kwa wiki, ni moja ya njia hizo. Kwa mbinu hiyo, mtoto anaweza kutumia chombo hicho kwa muda na kiwango kilichoainishwa na kila pale anapokwenda kinyume na kiwango hicho, basi anapasa kuzuiwa na kuadhibiwa.
Hata hivyo utumiaji mabavu na nguvu hauna nafasi katika hapa. Katika kesi kama hiyo njia ya mazungumzo sanjari na kumzuia kwa muda, kutumia vitu anavyovipenda mtoto huyo, inafaa kutumiwa hapa.
Wakati mwingine mtoto hutumia vyema kompyuta kwa kujinufaisha kielimu na chombo hicho muhimu cha teknolojia na kwa kweli katika hali kama hii wazazi hawapaswi kumzuia mtoto kutumia chombo hicho cha kompyuta. Lakini jambo linalopaswa kuzuiwa ni tabia ya mtoto huyo kutumia wakati wake mwingi katika kichezo isiyofaa ya kompyuta.
Moja ya nyenzo zingine za udhibiti ambazo zinaweza kutumiwa na wazazi katika kusimamia mienendo ya mtoto, ni uwezekano wa kutumia mbinu zinazodhibiti mfumo wa kompyuta. Kwa utaratibu huo watoto hawawezi kuingiza program mpya au kuweka windozi tofauti ambazo ni rahisi kuweza kuwaharibu watoto.
Njia nyingine ni pamoja na kuzuia kuondolewa program zilizopo katika kompyuta au kuzizuia zisifanye kazi, ni moja ya njia ambazo zinaweza kutumiwa katika kuwadhibiti watoto.
Miongoni mwa njia nyepesi zaidi kwa wazazi katika kumlinda mtoto wao wakati wa kutumia njia na nyenzo zinazohusiana na ulimwengu wa intaneti, ni kuweka mfumo wa kompyuta nje ya chumba chake cha kulala. Njia hiyo itawasaidia wazazi wakati wa kutumia mtoto chombo hicho nao waweze kushuhudia na kufuatilia kwa karibu michezo na shughuliza zote za mtoto huyo anapotumia kompyuta.
Kwa hakika vivutio vya kompyuta na michezo mingine ya kielektroniki kwa watoto havina kikomo, na ikiwa hakutakuwepo usimamizi madhubuti wa wazazi kwa mtoto wao, basi huenda mtoto bila kujijua, akatumia wakati mwingi zaidi kuliko inavyotakiwa na hivyo kuathiri lishe, usingizi na hata masomo yake.
Hapo ndipo wazazi wanapotakiwa kuwa macho na kuhakikisha wanasimamia vyema malezi ya mtoto wao sanjari na kumuandalia ratiba nzuri ya maisha yake na kuchunga sheria watakazomuainishia kila wiki.
Aidha wazazi wanatakiwa kumuweka mbali mtoto wao na ulimwengu wa elektroniki na michezo ya kompyuta wakati wa kipindi cha masomo.
Watafiti wanasema kuwa, kuna ulazima mkubwa wa kuzingatiwa wakati wa matumizi ya watoto kwa vyombo vya umeme kama vile kompyuta, labtop na tablet na kile ambacho kinahusiana na ulimwengu wa kielektroniki, kwani utafiti unaonyesha kwamba matumizi mengi ya vyombo hivyo kupita kiasi na kufikia kiwango cha uraibu, hupunguza uwezo wa kifikra wa mtoto.
Na kukithiri kwa maradhi hayo kwa watoto ndio mwanzo wa kufeli katika hatua zao za kielimu sanjari na kushindwa kukabiliana na mikikimikiki mingine ya kimaisha ambayo anapaswa kukabiliana nayo katika mustakbali wa maisha yake ya mbeleni.
Katika matumizi ya michezo ya kompyuta au ulimwengu wa intaneti, kuna udharura wa kujitenga na mambo machafu yasiyofaa. Aidha inaelezwa kuwa, kutumia sana kompyuta na intaneti, taratibu huibua tatizo la unene, ambalo mara nyingi hupelekea watoto na hasa vijana wengi kujichukia wenyewe kutokana na tatizo hilo. Hivyo kuna haja kwa wazazi kuwaepusha watoto wao na unene na uzembe unaosababishwa na matumizi ya muda mrefu ya vyombo vya umeme hasa michezo ya kompyuta.
Wataalamu wengi wanaamini kuwa, ni muhimu kuwatenga watoto walio na umri wa chini ya miaka mitatu na aina yoyote ya matumizi ya kompyuta. Kwa maana nyingine ni kwamba, umri huo hauoani na matumizi ya kompyuta au video.
Hata hivyo ikiwa mtoto aliye na umri wa chini ya miaka mitano ataingia katika ulimwengu wa matumizi ya vyombo hivyo na kuvizoea, basi lazima awekewe sheria na vidhibiti maalumu vya kumuwezesha kukabiliana na hatari ya ulimwengu huo. Kwanza anapasa kufahamishwa ni kwa kipindi gani anatakiwa atumie vyombo hivyo na kisha baada ya hapo ajishughulishe na kazi nyingine.
Watafiti wanapendekeza kuwa, mtoto mwenye umri wa kuinukia anatakiwa atazame kwa saa moja au masaa mawili filamu na katuni, upekuzi katika intaneti na michezo mingine ya video katika kompyuta. Ikiwa mtoto kwa siku atatumia dakika 45 kucheza mchezo wa kompyuta na muda mwingine mdogo kutazama televisheni na mwingine mfupi kujishughulisha na harakati za kifizikia, basi hakutakuwepo na wasi wasi wa kuathirika afya yake. Lakini ikiwa atatumia masaa mengi kujishughulisha na michezo ya kompyuta zaidi ya kiwango kinachotakiwa, basi hatua za haraka zinapaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na hali hiyo.
Madaktari wanashauri kwamba, watoto wanatakiwa kutumia masaa mawili tu kwa siku kutazama televisheni. Televisheni ina athari nyingi muhimu kwa watoto wengi wanaosoma na hasa katika kupumzisha mwili na fikra zao.
Hivyo wazazi na walimu wanatakiwa kusimamia ni kiasi gani watoto wanapaswa kutazama televisheni. Hii ni katika hali ambayo katika miaka ya awali watoto wanaosoma shule za msingi, huwa hawana uwezo wa kupanga vyema ratiba za kutazama televisheni.
Makala haya yameandikwa kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari na Afisa Mawasiliano Serikalini Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo anapatikana kwa barua pepe; sawebenjamin@gmail.com.
↧
TAMISEMI yatoa ufafanuzi uhaba wa vyakula mashuleni
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu baadhi ya Shule za Sekondari za Bweni zilizofungwa kutokana na ukosefu wa chakula ambapo alisema shule hizo zimefungwa kimakosa kwani Serikali imeshapeleka fedha za kununulia chakula kwenye halmashauri zote nchini. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Elimu TAMISEMI Bw. Zuberi Samataba.
Naibu Katibu Mkuu Elimu TAMISEMI Bw. Zuberi Samataba akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam mpango wa Serikali kuajiri waalimu wa shule za msingi wenye elimu ngazi ya Stashahada badala ya Cheti kama ilivyo sasa. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu ajira kwa walimu wapya waliohitimu 2014/2015 na kutoa rai kwa waalimu hao kwenda kuripoti kwenye vituo vya kazi watakavyopangiwa.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini wakati wa mkutano uliofanyika leo kwenye ofisi za TAMISEMI jijini Dar es Salaam. Picha na Fatma Salum (MAELEZO)
↧
KONYAGI YAWASOMESHA WANAFUNZI WA WAKULIMA WA ZABIBU DODOMA
Mratibu wa Mpango wa Somesha mtoto wa Mkulima wa zabibu ulidhaminiwa na Tanzania Distillaries LTD (TDL) Saimon Chibehe akizungumza jambo na wakulima wa zabibu pamoja na wanafunzi wa Kata ya Handari wilayani Chamwino, Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
Mratibu wa Mpango wa Somesha Mtoto wa Mkulima wa zabibu unaodhaminiwa na Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distillaries LTD (TDL), Saimon Chibehe akizungumza jambo akizungumza na Wazazi, Walezi ambao ni wakulima wa zabibu pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mpunguzi iliyopo Manispaa ya Dodoma, mwishoni mwa wiki.
Mwanafunzi wa Kidato cha Tatu wa Shule ya Sekondari Mvumi, mkoani Dodoma, Nuru Peter akiwa katika shamba la Zabibu la Wazazi Wake wakati alipofika kumuonesha Mratibu wa Mpango wa Somesha mtoto wa Mkulima wa zabibu ulidhaminiwa na Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distillaries LTD (TDL) Saimon Chibehe (hayupo pichani) mwishoni mwa wiki.
↧
NEWZZ ALERT :BASI LA KAMPUNI YA GAMET TRANS LAPATA AJALI KIBITI-MKOA WA PWANI
Taarifa zilizoifikia Globu ya Jamii hivi punde kutoka chanzo cha kuaminika,zinaeleza kuwa Basi la kampuni ya GAMET Trans linalofanya safari zake Dar-Lindi-Masasi-Nachingwea limepata ajali maeneo ya Kibiti wilaya ya Rufiji-Utete mkoa wa Pwani baada ya kutaka kumkwepa mtu anayedaiwa kuwa na tatizo la ulemavu wa akili,lakini kwa bahati mbaya likamgonga na kufariki papo hapo,taarifa zaidi zinaeleza kuwa baada ya ajali hiyo basi hilo liliacha njia na kupinduka na kupelekea kifo cha mtu mmoja aliyegongwa na wengine waliokuwemo ndani ya basi hilo (idadi ya abiria haikujulikana mara moja) kujeruhiwa.
↧
↧
BREAKING NEWZZZZZ;RADI YAUA MWALIMU NA WANAFUNZI SITA KIGOMA
Mwalimu Merina Sekilo aliyenusurika kupigwa na radi wakati akifundisha darasa la kwanza,ambapo wanafunzi 6 walifariki
Mwalimu Veronika Mtes wa shule ya msingi Kibirizi aliyepata mshtuko baada ya tukio la radi akiwa katika hospitali ya Mawenzi mkoa wa Kigoma kwa matibabu.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya mkoa wa Kigoma,Maweni akiongeza na Waandishi wa habari juu ya tukio la radi lililotokea hivi punde na kuuwa watu 8
Na Editha Karlo Karlo wa blog ya jamii,Kigoma
WATU wanane wakiwemo wanafunzi sita na mwalimu wa shule ya msingi kibirizi mmoja pamoja na mtu wa kawaida mkazi wa eneo la Bangwe mjini hapa wamekufa baada ya kupigwa na radi huku wanafunzi wengi 15 wakijeruhiwa na radi hiyo mchana huu.
Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa kigoma(maweni)Dkt Fadhili Kabaya alisema kuwa watu hao walifikwa na mauti hayo kufiatia mvua kubwa zilizonyesha zikiambana na radi zilianza majira ya saa sita mchana.
Dkt Fadhili aliwataja waliokufa katika tukio hilo kuwa ni pamoja na mwalimu wa shule ya msingi kibiriziElinaza Mbwambo(25)mtu mwingine wa kaida ni Forcus Ntahaba(45)mkazi wa eneo la Bangwe mjini hapa.
Aliwataja wanafunzi waliofariki ambao wote ni wa darasa la kwanza kuwa ni Yusuph Ntahoma(8)Hassan Ally(9)Fatuma Sley(7)Zamda Seif(8)Shukranmi Yohana(7) na Warupe Kapupa(10).
Alisema walipokea majeruhi kumi na tano lakini kati yao kumi wametibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumba baada ya hali zao kuwa nzuri na watano wamelazwa wanaendelea na matibabu katika hospital ya Mkoa wa Kigoma.
Akisimulia tukio hilo mwalimu aliyekuwa anafundisha darasani Mwalimu Merina Sililo alisema kuwa akiwa darasani akiendelea kufundisha ghafla aliona wingu zito jeusi limetanda hadi akashindwa kuendelea kuandika ubaoni.
''Manyunyu yalianza kidogo kidogo ikaja mvua kubwa na radi pamoja na miungurumo mikali sana iliyopelekea wanafunzi kuanguka ovyo darasa na kuzima na mara niliona moto umetanda katika chumba kuzima cha darasa na mimi nilianguka chini na kupoteza fahamu''alisema mwalimu huyo
Alisema apozinduka alijikuta katika hospital ya Mkoa wa maweni akipatiwa matibabu baada ya kuletwa kwa msaada wa waalimu wenzie.
''Kwakweli ni mungu tu mwenyewe ndo ameninusuru kwani nilirushwa mmara tatu na radi na watoto wote wote darasani walikuwa wananiangukia mimi wengine walikuwa wanakimbia ovyo nje''alisema Mwalimu huyo
↧
MAKONDA AKUTANA NA WANANCHI WA KAWE MZIMUNI KUTATUA MGOGORO WA ARDHI
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akizungumza na wananchi wa Kawe Mzimuni alipofika kutatua mgogoro wa ardhi kati yao na taasisi moja ya kiislamu inayomiliki Shule ya Sekondari ya Seminari ya Qiblatain D $B iliyopo eneo hilo Dar es Salaam leo asubuhi.
Katibu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa eneo hilo Mgili Wambura alimwambia DC Makonda kuwa eneo hilo tangu zamani ilikuwa ni barabara hivyo wanashangaa kuvamiwa hivyo alimuomba Makonda kusaidia kuondoa mvutano huo.
Mmoja wa wakilishi wa shule hiyo ya Sekondari ya Seminari ya Qiblatain D $B, Hamad Iddi Almas alimwambia DC Makonda (hayupo pichani), kuwa eneo hilo linamilikiwa na taasisi yao tangu siku nyingi.
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,
Paul Makonda.
Wananchi wa Kawe Mzimuni wakiwa kwenye ukuta walioubomoa kutokana na kujengwa eneo la barabara.
Na Dotto Mwaibale
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda amezitaka pande mbili zinazogombania ardhi maeneo ya Kawe Mzimuni kufika na vielelezo vya umiliki wa eneo hilo ili kumaliza mgogoro huo.
Mwito huo ameutoa wakati akizingumza na wananchi wa eneo hilo Dar es Salaam leo asubuhi ambao walijichukulia sheria ya kubomoa ukuta uliojengwa na mwananchi mmoja wa eneo hilo kuwa ulijengwa kwenye barabara.
Mbali na kubomoa ukuta huo wananchi hao wanavutana la taasisi moja ya dini ya kiislamu inayomiliki Shule ya Sekondari ya Seminari ya Qiblatain D $B iliyopo eneo hilo kuwa imemega eneo la Shule ya Msingi ya Ukwamani.
"Nimekuja hapa baada ya kusikia mgogoro uliopo wa kugombea ardhi nafikiri ofisa mipango mji wa Manispaa alifika hapa kuzungumza nanyi naomba baada ya siku saba pande zote zinazovutana zije na vielelezo ofidsini kwangu hapo tutajua nani mmiliki wa eneo hilo" alisema Makonda.
Katibu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa eneo hilo Mgili Wambura alimwambia Makonda kuwa eneo hilo tangu zamani ilikuwa ni barabara hivyo wanashangaa kuvamiwa hivyo alimuomba Makonda kusaidia kuondoa mvutano huo.
Mmoja wa wakilishi wa shule hiyo ya Sekondari ya Seminari ya Qiblatain D $B Hamad Iddi Almas alimwambia Makonda kuwa eneo hilo linamilikiwa na taasisi yao tangu siku nyingi jambo lililosababisha wananchi kuanza kuzomea wakipinga umiliki huo.
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda amezitaka pande mbili zinazogombania ardhi maeneo ya Kawe Mzimuni kufika na vielelezo vya umiliki wa eneo hilo ili kumaliza mgogoro huo.
Mwito huo ameutoa wakati akizingumza na wananchi wa eneo hilo Dar es Salaam leo asubuhi ambao walijichukulia sheria ya kubomoa ukuta uliojengwa na mwananchi mmoja wa eneo hilo kuwa ulijengwa kwenye barabara.
Mbali na kubomoa ukuta huo wananchi hao wanavutana la taasisi moja ya dini ya kiislamu inayomiliki Shule ya Sekondari ya Seminari ya Qiblatain D $B iliyopo eneo hilo kuwa imemega eneo la Shule ya Msingi ya Ukwamani.
"Nimekuja hapa baada ya kusikia mgogoro uliopo wa kugombea ardhi nafikiri ofisa mipango mji wa Manispaa alifika hapa kuzungumza nanyi naomba baada ya siku saba pande zote zinazovutana zije na vielelezo ofidsini kwangu hapo tutajua nani mmiliki wa eneo hilo" alisema Makonda.
Katibu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa eneo hilo Mgili Wambura alimwambia Makonda kuwa eneo hilo tangu zamani ilikuwa ni barabara hivyo wanashangaa kuvamiwa hivyo alimuomba Makonda kusaidia kuondoa mvutano huo.
Mmoja wa wakilishi wa shule hiyo ya Sekondari ya Seminari ya Qiblatain D $B Hamad Iddi Almas alimwambia Makonda kuwa eneo hilo linamilikiwa na taasisi yao tangu siku nyingi jambo lililosababisha wananchi kuanza kuzomea wakipinga umiliki huo.
↧
MASHINE ZA BVR AWAMU YA PILI KUPELEKWA MIKOA SABA
Tume ya Taifa ya Uchaguzi Nchini Tanzania itaanza kusambaza mashine za BVR 248 katika mikoa saba nchni Tanzania Kuanzia katikati mwa wiki ijayo.
Mikoa iliyopangwa kuanza kupokea mashine hizi ni mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa, Wakati zozi likianza mikoa hiyo nyingine zitakuwa zinapelekwa katika mikoa ya Katavi, Mbeya na Dodoma. Mikoa mimgine ni Singida Tabora Geita na Kigoma.
Mkuu wa kitengo cha Ufundi wa idara ya Daftrari/ICT wa NEC Dr Sisit Cariah, Akizungumza na mwandishi wetu amesema kwamba mpaka sasa wanachi wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvumna na Iringa wakae tayari kwani muda wowote watatangaziwa vituo vya kujiandikisha.
Mkuu wa kitengo cha Ufundi wa idara ya Daftrari/ICT wa NEC Dr Sisit Cariah, Akizungumza na mwandishi wetu amesema kwamba mpaka sasa wanachi wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvumna na Iringa wakae tayari kwani muda wowote watatangaziwa vituo vya kujiandikisha.
Pamoja na mshine hizo 248 Tume ya taifa ya uchaguzi imewaandaa wataalamu 248 ambao watakuwa na jukumu la kutoa elimu kwa wataalamu wengine 50 kwa kila mmoja nchi nzima kwa ajili ya kuharakisha uandikishaji kwa mfumo wa BVR.
Dr Sisit Ameeleza kwamba wamefanikiwa kufanya maboresho makubwa katika mashine hizi ikiwa ni pamoja na kubadilisha upangaji wa vifaa (settings), mfumo endeshi (Software) na upande wa Vichapishio (printer) ambazo sasa zimetengenezewa Nchini Ufaransa umeboreshwa na nirahisi kusafishwa.
Mafunzo yaliyoendeshwa hapa Jijini Dar es Salaam yamechukua siku moja na yamezingatia sana upande wa Vichapishio (printer), Visoma alama za vidole (Finger Print Scaner) na Kamera kutambua macho mekundu. Ameongoza kwamba printer za sasa ni rahisi kusafishwa na hata kuweka kifaa kipya baada ya cha zamamni kuharibika vimerahisishwa.
Kuhusu uchukuaji wa alama za vidole, amesema kwamba kwa sasa tatitzo la mashine ya kuchukua alama za vidole wamelifanikisha kwa asilimia mia. Kwani kwa wale ambao hawana alama za vidole mashine zimewekewa mfumo wa alogarithim mpya ambao uatatambua kila aina ya kidole.
Hata hivyo Kamera zimewekewa mfumo mpya wa kutambua macho mekundu na kurekebisha rangi ya macho mekundu (Red eyes) Bila kukwamisha zoezi la uandikishaji.
Mtarajio ni kwamba zoezi lauandikishaji liwe limekamilika ndani ya kila siku 28 tokea kila mkoa unapopokea mashine hizi. Vilevile Dr Sisit ameishukuru serekali kwa kufanikisha upatikanaji wa Vifaa “serekali imejitahidi kuandaa upatikanaji wa mashine hizo, na usafirishaji kwa njia ya ndege kwenda nchi nzima.
Kila halmashauri na mkoa utachukua angalau siku 28 kukamilisha mkoa utakapo pokea Vifaa” Dr Sisit amesema.Mwisho amesema kwamba mashine nyingine 1,600 zitawasili wakati wowote na kwamba serikali imetoa Dola za Marekani milioni 72 (Sh. bilioni 133).
Kila halmashauri na mkoa utachukua angalau siku 28 kukamilisha mkoa utakapo pokea Vifaa” Dr Sisit amesema.Mwisho amesema kwamba mashine nyingine 1,600 zitawasili wakati wowote na kwamba serikali imetoa Dola za Marekani milioni 72 (Sh. bilioni 133).
Kuwasili kwa mashine hizo, kunaifanya Nec kupokea mashine 2,098, huku ikisubiri mashine 5,902, ili kukamilisha 8,000 zinazotakiwa. Alisema vifaa hivyo vinanunuliwa na serikali kupitia kampuni ya Lithotech Export ya Afrika Kusini, ambayo imeingia mkataba na Nec na inaviagiza China.
↧
BALOZI SEIF ALI IDDI AWAKUMBUSHA WANANCHI KUWAUNGA MKONO VIONGOZI WANAOWASIMAMIA HARAKATI ZA MAENDELEO YAO.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi msaada wa Vipaza sauti Amiri wa Jumuiya ya Sherehe za Siku Kuu ya Iddi Matemwe Ustaadhi Kundi Choum Haji kutekeleza ahadi aliyoip[a Jumuiya hiyo wakati wa sherehe za siku kuu ya Iddi el Hajj iliyopita.
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akimkabidhi mchango wa Shilingi 400,000/- kwa kila kikundi miongoni mwa vikundi 14 vya Ushirika wa Akina Mama vilivyomo ndani ya Wilaya ya Kaskazini “ A “.
Balozi Seif akikabidhi Seti moja ya Jezi na Mipira kwa kila Timu ya Soka miongoni mwa timu nne zilizomo ndani ya Jimbo la Matemwe.
Balozi Seif akiangalia hodhi linalojengwa kwa ajili ya kuhifadhia maji kwenye Msikiti Mkuu wa Kijiji cha Mvuleni Kidoti Jimbo la Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Balozi Seif akiuagiza Uongozi wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa wa Kijiji cha Mvuleni kufanya Tathmini ya uenzi wa Vyoo ili uwahi kufunguliwa katika muda muwafaka uliopangwa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewakumbusha Wananchi hasa akina Mama Nchini kuwaunga mkono Viongozi wenye muelekeo wa kuwasimamia vyema katika harakati zao za Maendeleo, kiuchumi na ustawi wa Jamii.
Alisema takwimu ya idadi ya watu Nchini inaoonyesha wazi kwamba Wanawake ndio wenye uwezo wa kutumia kura zao katika kuchaguwa Viongozi watakaowafaa kwenye maeneo yao kutokana na wingi wao.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa kumbusho hilo wakati akikabidhi Vipaza Sauti kwa ajili ya Jumuiya ya Kuhifadhi Quran pamoja na Sherehe za Siku Kuu ya Kiislamu ya Kijiji cha Matemwe Wilaya ya Kaskazini “A” Mkoa wa Kaskazini Unguja akitekeleza ahadi aliyoitowa wakati wa Siku Kuu ya Mfunguo Tatu uliopita akiwa mgeni rasmi.
Balozi Seif alisema huu ni mwaka muhimu kwa Taifa la Tanzania ambapo Wananchi wanapaswa kuwa makini katika kufanya uamuzi muafaka wa kura ya maoni pamoja na uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba.
Alisema uwamuzi wa Wananchi hao endapo hautazingatia hatma yao ijayo ya miaka mitano kwa kuchaguwa viongozi makini na imara wasijetafuta visingizio vya lawama kwa viongozi watakaowaweka madarakani.
Mapema Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akitekeleza ahadi yake ya kuviwezesha Baadhi ya Vikundi vya Ushirika vya akina Mama wa Wilaya ya Kaskazini “A “ alisisitiza umoja na mshikamano miongoni mwa Wananchi wa Wilaya hiyo.
Mama Asha alisema mshikamano huo ndio njia pekee itakayowawezesha wananchi hao kuendelea na shughuli zao za kujitafutia riziki katika hali ya amani na utulivu.
Alitanabahisha kwamba yapo Mataifa kadhaa duniani yakiwemo yale ya Bara la Afrika ambayo baadhi ya wananchi wake walijaribu kuichezea amani na hivi sasa tayari wameshatumbukia katika dimbwi la vurugu zilizozaa maafa yaliyoacha makovu yatayoendelea kukumbukwa milele na Mataifa hayo.
↧
↧
MGODI UNAOTEMBEA WA KAMBI MBWANA
Chadema na ngoma ya kitoto haikeshi
NI dhahiri Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamejitoa katika mbio za kuitwaa nchi hii kwa amani inayojengwa na demokrasia makini iliyojengwa kwenye nchi yetu.
Hii ni kwa sababu wenyewe wameshindwa kusimamia hoja makini, badala yake wameingia kwenye vioja na vituko visivyokuwa na kichwa wala mguu. Zaidi, tunashuhudia mtafuruku, kushindwa kuelewana na kuonyeshana tamaa kwa viongozi au wanachama wenye mvuto na majina kadhaa.
Wakati Chadema wakisisitiza amani na shauku ya kutaka kuichukua nchi hii, wao wenyewe wamekosa umoja na dhamira ya dhati ya kuwashawishi Watanzania wenye mlengo wa demokrasia isiyokuwa na ghasia kwa ajili ya kulinda mustakabali wa Taifa letu.
Kwa kuimba wimbo wa demokrasia, Chadema hao hao waliikosa katika chama chao, ndio maana wakaamua kuingia kwenye mgogoro mzito na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wao, Zitto Kabwe, waliyeamua kumtimua kama mbwa koko baada ya kuonyesha nia ya kugombea nafasi ya juu ya uongozi katika chama hicho Kikuu cha Upinzani kwa sasa.
Kwa kupitia Mwenyekiti wao Taifa, Freeman Mbowe kwa kushirikiana na ofisi nyingine za Chadema, waliamua kumuwekea zengwe Kabwe. Alinyukwa kiasi cha kumkatisha tamaa kwenye chama hicho alichoshiriki kukijenga kwa nguvu zake zote. Inashangaza leo hathaminiki.
Leo hii Zitto amekuwa kiongozi mkuu wa Chama Cha Alliance For Change and Transparency (ACT), ikiwa ni siku chache baada ya kuvuliwa ubunge wake kwa madai kuwa alikwenda Mahakamani kukishtaki chama chake cha Chadema, kama Katiba yao inavyosema.
Hata hivyo, huo ni mchezo uliwekwa kwa ajili ya kumuondoa kundini. Kwenye siasa suala la kuhujumiana ni jambo la kawaida. Wenyewe wanasema hakuna adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu.
Hayo na mengine mengi, utagundua ni mwendelezo wa ishara ya kuwa ngoma ya kitoto haikeshi. Ilikuwa lazima Chadema ianguke. Hakukuwa na njia ya kuwanusuru hususan kwa mwaka huu wa Uchaguzi. Ukiacha suala la Zitto ambaye mwelekeo wake unaonekana kuwa ni mwiba mkali kwao. Amekuwa akiungwa mkono na Watanzania wengi.
Aidha, Chadema wenyewe na Chama Cha Wananchi (CUF) wanaonekana kunyukana chini kwa chini kufuatia majina na majimbo waliyopanga kuachiana katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Majimbo kadhaa yamekuwa machungu nay a moto. Wanachama hao na vyama vyao vilivyojiunga kwenye Muungano wa UKAWA havielewani. Majimbo kama vile Morogoro Mjini, Mikumi, Segerea, Ukonga, Kigamboni yameonekana dhahiri kutaka kuvunja muungano huo.
Kule wilayani Handeni duru zinaonyesha kuwa msuguano upo kati ya CUF na Chadema. CUF wanasema wao wanapaswa kusimamisha mgombea maana ndio chama chenye nguvu ukitoa CCM.
Lakini Chadema nao wanaona wao ndio wenye uwezo wa kuisumbua CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Huu ni mtihani mkubwa kwa wapinzani, hususan hawa waliojiunga kwenye kivuli cha UKAWA.
Vyama kama vile Chadema, CUF, NCCR Mageuzi na NLD kamwe hawawezi kuisumbua tena CCM kwa mwaka huu. Vyama hivi vitasumbuana vyenyewe ndani ya muungano wao wa UKAWA. Baada ya hapo, watasumbuana tena na wapinzani wenzao kama vile ACT ya Zitto, ADC ya Hamad Rashid Mohammed ambaye naye anaonyesha kugombea urais Visiwani Zanzibar.
Huu ni zaidi ya moto. Ni zaidi ya ngoma ya kitoto kwa Chadema. Chama hiki kilichokuwa na nguvu kutoka kwa makundi ya vijana, kimeyumba baada ya kukubali kuyumbishwa na viongozi wao.
Hili lazima lisemwe. Na kuna kila sababu Watanzania, hususan wale wanaopenda vyama vilivyokuwa kwenye mgongo wa UKAWA wakajiandaa kisaikolojia. Kamwe CCM haitatumia nguvu kubwa kushinda kwenye uchaguzi huu. CCM itashinda kiulaini kabisa.
Hakuna kiongozi wa juu wa Chadema, CUF atakayekubali mgombea wa ACT ashinde katika uchaguzi huu. Ikitokea hilo, watakuwa tayari kumsaidia mtu wa CCM kushinda. Hii inaitwa ‘bora tukose wote tuheshimiane’.
Na wataheshimiana kweli. Zitto huyu wanayemsema na kumdhalilisha mchana na usiku, kamwe hayupo tayari kuona Chadema na wenzao wa UKAWA wanamshinda, hivyo atafanya kila awezalo kuona nao wanaanguka katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Wafurukutwa wa vyama hivyo wajiandaye. Na wajiandaye pia kupokea matokeo ya kushindwa kwa minajiri ya kulinda usalama wa nchi yetu. Hakuna kinachoweza kuwafanya washinde na kushika dola.
Mpaka sasa hawajui nani atasimama kwenye kiti cha urais kati ya Dkt Willbroad Slaa na Profesa Ibrahim Haruna Lipumba. Hawa wote wana nguvu kwenye vyama vyao. Na wote wanaheshimika katika nchi hii.
Pamoja na heshima hiyo,ili kofia ya UKAWA ikae sawa kichwani, lazima asimamishwe mmoja kwa ajili ya kugombea urais na kuchuana na wagombea wengine kutoka CCM nk.
Huo ni mwiba mwingine wa UKAWA. Kelele zinazopigwa kwa sasa ni Slaa anafaa zaidi ya Lipumba au Lipumba anafaa zaidi ya Slaa. Ukiangalia vigezo wanavyotoa vinaelemea kwenye udini, ukabila au uvyama vyao. Watu hao hawatumii vigezo husika kwa maslahi ya Tanzania, bali vyama.
Hii haiwezekani. Ni katika hilo, bado nabaini kuwa vyama hivi ni kama vile ngoma ya kitoto kamwe haiwezi kukesha. Watapambana sana, watachuana mno, ila mwisho wa siku, hawana madhara.
Bado wana safari ndefu ya kuweza kuifanya CCM kiwe chama cha upinzani katika nchi hii yenye kila zuri la kujivunia. Huo ndio ukweli wa mambo. Kama wapinzani hao, hususan Chadema wangekuwa na nia njema ya kuwa wapinzani wa kweli, kamwe wasingeleta chuki na ubinafsi wao kwa wao.
Leo hii wametunga wimbo wao wa msaliti. Wanamtukana sana Zitto. Wanamdhalilisha mno Zitto. Wanamdhalilisha mtu ambaye Watanzania wengi walionza kufuatilia siasa mwaka 1995 hadi leo wanamuona wao ndio kiongozi wao mwenye uzalendo kwa Taifa lake.
Jambo hili linazidi kuwa chungu kwa Chadema, maana wengi wao wanajua alionewa aidha kwa kabila lake au udini wake. Ikumbukwe kuwa, wapo watu waliomtetea Zitto wakisema alizuiwa kugombea uenyekiti kwa sababu yeye si Mchaga wala Mkristo.
Jambo hili linaweza kuwa si kweli, ila kwa sababu linatolewa dhidi ya mtu aliyefukwa kwenye chama hicho, basi aghalabu baadhi yao wanahisi kuna ukweli ndani yake.
Sidhani kama huu ni mwendo mzuri kwa siasa za Tanzania. Ni dhahiri vyama visivyokuwa na dira vinaendelea kupiga jaramba hali ya kuwa hawana uwezo wa kuwa na madhara dhidi ya CCM. CCM inayoheshimika kwa wakubwa na wadogo.
Inayopendwa na wake kwa waume. Lolote wanalotaka kulisema leo, litawekwa katika kundi la ngoma ya kitoto isiyokesha. Je, Chadema wanafahamu makosa yao? Wanaojiita wana UKAWA wanajua mapungufu yao? Kwamba bado wanajiamini kuwa wataiondoa madarakani CCM kwa mwaka huu 2015? Kwa lipi?
Si kweli, hivyo Watanzania wote wajipange kulinda amani ya nchi yetu kwa kujiandaa kisaikolojia, hususan wale waliokuwa na mtazamo kuwa huenda kuna chama cha upinzani kinaweza kushinda katika uchaguzi wa mwaka huu, ambao tayari unaonekana CCM itashinda.
↧
WAZIRI NYALANDU AANZA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI
Waziri wa Maiasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dk Adrehem Meru, wakipata maelekezo kuhusiana na mipaka ya hifadhi ya Taifa ya Saadan kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Saadan, Alhaj Hassan Nguruma (katikati) walipotembelea kutatua mgogoro uliohusu wananchi na hifadhi hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Katibu mkuu wake Adrehem Meru wakiwa katika boti katika mto wami juzi walipotembelea hifadhi hiyo kwa ajili ya kutatua mgogoro wa mpaka katika ya hifadhi hiyo na wananchi.
Mhifadhi Mkuu wa Saadan, Alhaj Hassan Nguruma(katikati) akitoa maelezo kwa Waziri wa Maiasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dk Aderehem Meru kuhusiana na mogoro wa mipaka baina ya hifadhi hiyo na wawekezaji wa shamba linalopakana na hifadhi hiyo. Waziri Nyalandu aliamuru mipaka ya zamani izingatiwe ili kumaliza mgogoro huo.
Waziri wa Maliasili na utalii Lazaro Nyallandu na Katibu mkuu wake Adrehem Meru wakikagua mto Wami ambao awali ulikuwa mpaka wa Hiadhi ya Saadana na kupanuliwa kitu kilichosababisha kuwapo kwa mgogoro wa muda mrefu wa mipaka. Wazir Nyalandu aliamuru mgogoro huo kumalizwa mara moja kwa kuzingatia mipaka ya zamani.
↧
NAMNA YA KUMSHITAKI DAKTARI ALIYESABABISHA MADHARA AU KIFO KWA MGONJWA.
Wako watu wengi wameathirika kutokana na matendo yanayotokana na uzembe,kutojali au makusudi ya madaktari. Wapo waliopata vilema vya muda kutokana na uzembe huo, wapo waliopata vilema vya maisha na wapo waliouliwa na madaktari hawa hawa.
Ajabu ni kuwa ukifanya tathmini ya haraka utaona kuwa watu wote waliopata madhila kutoka kwa madaktari huhusisha madaktari wa serikali na katika hospitali za serikali. Si rahisi kukuta jambo la ajabu la kitabibu limehusisha hospitali binafsi. Swali langu ni kuwa, ewe Mtanzania daktari amekusababishia tatizo iwe ugonjwa wa kudumu, ulemavu wa muda au wa kudumu, au hata kifo cha ndugu au jamaa, umechukua hatua gani baada ya tukio hilo ?. Umekaa kimya ukiwa umeridhika au umekaa kimya kwakuwa hujui la kufanya ?.
1.INARUHUSIWA KUMSHITAKI DAKTARI KWA KUSABABISHA
MADHARA KWA MGONJWA WAKATI WA TIBA.
Wapo wanaodhani kuwa madaktari hawashitakiwi kwa kutomhudumia vyema mgonjwa. Hili si kweli daktari ni mtumishi sawa na watumishi wengine na kosa lolote la uzembe, kutojali au makusudi analofanya na kusababisha madhara kwa mgonjwa sheria inaruhusu kumchukulia hatua daktari huyo. Sawa na mtumishi mwingine akitenda kosa kazini anaadhibiwa ndivyo ilivyo kwa madaktari pia. Kwa mujibu wa sheria daktari amepewa wajibu wa hali ya juu kuhakikisha anatumia taaluma yake, weledi na uadilifu katika kutoa huduma ya tiba na kuepuka kabisa hatua au namna yoyote inayoweza kuleta madhara kwa mgonjwa.
Takwa hili kwa daktari ni takwa la kisheria na wala si hiyari. Kwa hiyo watu waelewe kuwa suala la daktari kutoa matibabu kwa umakini ni lazima. Kitu kikiwa lazima (mandatory) katika sheria maana yake ni kuwa kutofanyika kwake hutoa haki ya mtendewa kushitaki. Hivyo ndivyo ilivyo kwa madaktari. Kwa namna yoyote anapokosa umakini katika kutoa tiba basi ni ruhusa kwa mtendewa kushitaki.
↧
TANZANIA YASHIRIKI MIKUTANO YA MAJIRA YA KIPUPWE ULIOANZA RASMI MJINI WASHINGTON DC
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier, akipata maelezo kutoka kwa Bw. Said Ngosha Magonya, ambaye ni Kamishina wa Fedha za Nje kuhusu utaratibu uliopangwa na Tanzania katika Mikutano hii ya majira ya kipupwe.
Mikutano ya Majira Kipupwe imeanza rasmi Mjini Washington DC.
Mikutano ya majira ya Kipupwe imeanza rasmi tarehe 14/4/2015 na kuhudhuriwa na nchi mbalimbali wanachama zaidi ya 188.
Mikutano hii huudhuriwa na maelfu ya wafanyakazi kutoka serikalini, waandishi wa habari, Mashirika na Taasisi zisizo za kiserikali, Sekta binafsi pamoja na kamati za kifedha.Taasisi hizo kwa pamoja zitajadili maendeleo ya kazi za Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa.
Tanzania ni nchi wanachama katika Mikutano hiyo.Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum Mkuya ndiye kiongozi wa ujumbe kutoka Tanzania na ni Gavana katika mikutano hii, akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile ambaye ni Gavana msaidizi kwa upande wa Benki ya Dunia (WB), aidha Gavana wa Benki kuu Prof. Benno Ndulu ni Gavana msaidizi kwa upande wa Shirika la Fedha la Kimataifa(IMF).
Imetolewa na:
Msemaji wa Wizata ya Fedha
Ingiahedi C. Mduma
14/4/2015
Washington DC.
↧
↧
Airtel yakabidhi magari kwa washindi 8 wa Mkoa wa Dar es saalam
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Lilian Festo Mjimba katika hafla iliyofanyika Makao
Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni washindi wengine wa droo hiyo.
Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni washindi wengine wa droo hiyo.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Lilian Festo Mjimba katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Mama lishe Efgenia Mathew Mushi katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni washindi wengine wa droo hiyo.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Kinyozi Juma Ally Songoro katika hafla iliyofanyika
Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.
Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za gari jipya aina ya Toyota IST, kwa mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Kinyozi Juma Ally Songoro katika hafla iliyofanyika
Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.
Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania, Frank Filman (kulia), akikabidhi mfano wa funguo za magari mapya aina ya Toyota IST, kwa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, (kutoka kushoto), Subeti Salim Subeti, Kuruthumu Seleman Forogo, Juma Ally Songoro, Liliani Festo Mjimba, Christone Edick Mbalamula, Efgenia Mathew Mushi na Obel Samwel Mwamugiga katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana.
Mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Subeti Salim Subeti akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), funguo ya gari jipya aina ya Toyota IST, baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel Tanzania,
Frank Filman (kushoto), katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni watoto wa mshindi huyo.
Frank Filman (kushoto), katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia ni watoto wa mshindi huyo.
Mmoja wa washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Airtel Yatosha Zaidi’, Kuruthumu Seleman Forogo akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), funguo ya gari jipya aina ya Toyota IST, baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari wa Airtel
Tanzania, Frank Filman (kushoto), katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Anayeshuhudia ni kaka wa mshindi huyo, Yasin Juma.
Tanzania, Frank Filman (kushoto), katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam jana. Anayeshuhudia ni kaka wa mshindi huyo, Yasin Juma.
Airtel yakabithi magari kwa washindi 8 wa Mkoa wa Dar es saalam
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imekabithi magari kwa
washindi wake waliokuwa wamesalima kwa mkoa wa Dar es saalamu
walioibuka washindi katika droo za mwisho za promosheni ya Airtel
yatosha zaidi.
Washindi waliokabithiwa magari yao ni pamoja na kuruthumu Seleman
(42) mfanyabishara ndogondogo, Lilian Mgimba (24) mfanyabishara
ndogondogo, Christ Mbalamula (27) mjasiliamali , Juma Songoro(24)
Mwanafunzi wa chuo cha IFM , Subeti Salum Subeti (43) kondactor wa
daladala, Isgnenia Mushi(35) mfanyabishara ndogondogo,Charles Msakwa
(45) Mwalimu, na Obed Muamugija (24) Mwanafunzi wa chuo cha IFM.
Akiongea wakati wa kukabithi magari hayo Mkurugenzi wa kitengo cha
teknolojia habari wa Airtel Bw, Frank Filman alisema “ nawashukuru
sana wateja wetu kwa kutumia huduma zetu hususani huduma ya Airtel
yatosha zaidi ambayo mbali na kuwazawadia wateja wanaotumia vifurushi
kupitia promosheni ya Airtle Yatosha zaidi tumewawezesha wateja wetu
kupata huduma bora, za nafuu zinazokithi mahitaji yao ya kupiga simu,
kutuma ujumbe mfupi pamoja na huduma ya internet.
Leo tunajifuraha kukabithi magari kwa washindi 8 waliosalia katika
mkoa wa Dar es saalam, tunawaahidi washindi wengi waliosalia kutoka
kanda ya kaskazini na kanda ya ziwa kuwa watakabithiwa magari yao
ndani ya wiki moja kuanzi sasa.
Tunawapongeza wateja Wetu wote waliobahatika kujishindia magari
kupitia promosheni hii tangu ianze na tunaamini tumeweza kuwawezesha
kufanya shughuli zao za kijamii na za kiuchumi kwa urahisi zaidi na
kuboreesha maisha yao na jamii ya Tanzania kwa ujumla
Tunawaahidi kuendelea kutoa huduma za mawasiliano bora, zenye ubunifu
huku tukiendelea kuwafikia watanzania wengi zaidi na kuwazawadia
kupitia promosheni kama hii ya Airtel Yatosha Zaidi.
Promosheni ya Airtel yatosha imeshafikia mwisho wake lakini huduma
yetu ya Airtel yatosha bado inaendelea hivyo natoa wito kwa watanzania
kuendelea kujiunga na vifurushi hivi na kufurahia huduma bora zenye
gharama nafuu kwa wakati wote. aliongeza Filman.
Kwa upande wake moja ya washindi wa promosheni hii bi, Kuruthumu
Seleman alisema” mpaka sasa sijaamini kwamba nimeshinda gari, kwakweli
nawashukuru sana Airtel kwa kuanzisha promosheni hii. Kwakweli sikuwa
na wazo kama naweza kushinda, haya ni maajabu kwakeli kumbe kila
mtanzania anaweza kupata nafasi ya kushinda kupitia promosheni hizi za
Airtel.
Nafurahia ushindi huu kwa sasa kwani nilikuwa natamani kuwa na usafiri
na kupunguza adha nayoipata katika shughuli zangu za mama lishe, sasa
nauhakika wa kusafirisha chakula changu kwa usalama zaidi na kuwafikia
wateja wangu kwa wakati, naamini biashara yangu itaboreshwa na kukua
na kuwa ya ufanisi zaidi sasa kulinganisha na ilivyokuwa awali”
Promosheni ya Airtel yatosha ilizindualiwa mwanzoni mwa mwezi wa
februari mwaka huu na kufika mwisho wake mwanzoni mwa mwezi Aprili
ambapo jumla ya wateja 60 wamejishindia na kukabithiwa magari yao
aina ya Toyota IST. Airtel iliwazawadia wateja wake gari aina ya
Toyota IST kila siku kwa muda wa siku 60
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imekabithi magari kwa
washindi wake waliokuwa wamesalima kwa mkoa wa Dar es saalamu
walioibuka washindi katika droo za mwisho za promosheni ya Airtel
yatosha zaidi.
Washindi waliokabithiwa magari yao ni pamoja na kuruthumu Seleman
(42) mfanyabishara ndogondogo, Lilian Mgimba (24) mfanyabishara
ndogondogo, Christ Mbalamula (27) mjasiliamali , Juma Songoro(24)
Mwanafunzi wa chuo cha IFM , Subeti Salum Subeti (43) kondactor wa
daladala, Isgnenia Mushi(35) mfanyabishara ndogondogo,Charles Msakwa
(45) Mwalimu, na Obed Muamugija (24) Mwanafunzi wa chuo cha IFM.
Akiongea wakati wa kukabithi magari hayo Mkurugenzi wa kitengo cha
teknolojia habari wa Airtel Bw, Frank Filman alisema “ nawashukuru
sana wateja wetu kwa kutumia huduma zetu hususani huduma ya Airtel
yatosha zaidi ambayo mbali na kuwazawadia wateja wanaotumia vifurushi
kupitia promosheni ya Airtle Yatosha zaidi tumewawezesha wateja wetu
kupata huduma bora, za nafuu zinazokithi mahitaji yao ya kupiga simu,
kutuma ujumbe mfupi pamoja na huduma ya internet.
Leo tunajifuraha kukabithi magari kwa washindi 8 waliosalia katika
mkoa wa Dar es saalam, tunawaahidi washindi wengi waliosalia kutoka
kanda ya kaskazini na kanda ya ziwa kuwa watakabithiwa magari yao
ndani ya wiki moja kuanzi sasa.
Tunawapongeza wateja Wetu wote waliobahatika kujishindia magari
kupitia promosheni hii tangu ianze na tunaamini tumeweza kuwawezesha
kufanya shughuli zao za kijamii na za kiuchumi kwa urahisi zaidi na
kuboreesha maisha yao na jamii ya Tanzania kwa ujumla
Tunawaahidi kuendelea kutoa huduma za mawasiliano bora, zenye ubunifu
huku tukiendelea kuwafikia watanzania wengi zaidi na kuwazawadia
kupitia promosheni kama hii ya Airtel Yatosha Zaidi.
Promosheni ya Airtel yatosha imeshafikia mwisho wake lakini huduma
yetu ya Airtel yatosha bado inaendelea hivyo natoa wito kwa watanzania
kuendelea kujiunga na vifurushi hivi na kufurahia huduma bora zenye
gharama nafuu kwa wakati wote. aliongeza Filman.
Kwa upande wake moja ya washindi wa promosheni hii bi, Kuruthumu
Seleman alisema” mpaka sasa sijaamini kwamba nimeshinda gari, kwakweli
nawashukuru sana Airtel kwa kuanzisha promosheni hii. Kwakweli sikuwa
na wazo kama naweza kushinda, haya ni maajabu kwakeli kumbe kila
mtanzania anaweza kupata nafasi ya kushinda kupitia promosheni hizi za
Airtel.
Nafurahia ushindi huu kwa sasa kwani nilikuwa natamani kuwa na usafiri
na kupunguza adha nayoipata katika shughuli zangu za mama lishe, sasa
nauhakika wa kusafirisha chakula changu kwa usalama zaidi na kuwafikia
wateja wangu kwa wakati, naamini biashara yangu itaboreshwa na kukua
na kuwa ya ufanisi zaidi sasa kulinganisha na ilivyokuwa awali”
Promosheni ya Airtel yatosha ilizindualiwa mwanzoni mwa mwezi wa
februari mwaka huu na kufika mwisho wake mwanzoni mwa mwezi Aprili
ambapo jumla ya wateja 60 wamejishindia na kukabithiwa magari yao
aina ya Toyota IST. Airtel iliwazawadia wateja wake gari aina ya
Toyota IST kila siku kwa muda wa siku 60
↧
UFUNGUZI WA KIKAO KATI YA UONGOZI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA KAMATI YA KUDUMU YA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia Ofisi za Viongozi wa Kitaifa wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Gamaha (hayupo pichani). |
Kikao kikiendelea.Picha na Reginald Philip |
↧
AJALI NYINGINE TENA;BASI LA JORDAN LAPINDUKA NZEGA,LIKITOKEA JIJINI MWANZA KWENDA ARUSHA.
Pichani juu ni mmoja wa majeruhi akisaidiwa na msamaria mwema mara baada ya kupata ajali.
Mtu mmoja amefariki dunia huku wengine 25 wakijeruhiwa katika ajali ya basi la abiria la Jordan lenye usajili wa namba T 650 AQZ lililokuwa likitoka jijini Mwanza kwenda mkoani Arusha na kupinduka leo wilayani Nzega,Tabora.Mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.
Baadhi ya Majeruhi mara baada ya ajali hiyo kutokea.
Baadhi ya Abiria wakiwa nje ya basi la Jordan mara baada ya kupinduka wilayani Nzega mkoani Tabora na kupelekea kifo cha mtu mmoja.
Mmoja wa abiria akifanya mawasiliano baada ya kunusurika kifo basi la Jordan mara baada ya kupinduka wilayani Nzega mkoani Tabora na kupelekea kifo cha mtu mmoja.
↧
Tanzania kufungua Ubalozi nchini Kuwait
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Mhe. Skeikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah, Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait. Waziri Membe alifanya ziara ya siku moja nchini humo tarehe 14 Aprili, 2015 kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Waziri Membe akimtambulisha kwa Mhe. Skeikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah, Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya.
Mazungumzo ya ushirikiano yakiendelea.
↧
↧
MADEREVA CHUKUENI TAHADHARI KUBWA KONA ZA IYOVI,ENDESHA KWA UMAKINI KUEPUSHA AJALI
wewe ni dereva wa basi la abiria ama gari binafsi ?hebu chukua hatua ya kupunguza ajali leo kwa kujihadhari na kona hizi na Iyovi na Kitonga na kona nyingine kali kama hizi nchini kwani maisha yako ni dhamani kubwa na uhai wake bado tunautamani
Vema kuheshimu alama za barabarani na kuacha mbwembwe uwapo barabarani katika kona kali kama hizi
Katika kona kama hizi zingatia alama za usalama barabarani usiwe na haraka ya kulipita gari la mbele
Hapa ni eneo ambalo watu 19 walipoteza maisha kwa fuso kugongana na basi na Nganga na kisha kuwaka moto uzembe ukiwa ni wa dereva wa basi aliyetaka kulipita gari la mbele katika kona kali
Usilipite gari katika kona
Alama zote za barabarani ni msaada kwa maisha yako lazima uziheshimu
Kona zote ni hatari kwa usalama wako hivyo usihame saiti yako ili kukimbia ajali
Lazima unapotaka kulipita gari la mbele uwe una uwezo wa kuona mbali zaidi ya mita 100 ama zaidi
Dereva makini halipiti gari la mbele katika kona
↧
TAASISI YA IMETOSHA FOUNDATIONS KUTUMA UJUMBE MZITO JIJINI MWANZA
Balozi Henry Mdimu akiongea na vyombo vya habari |
Taasisi isiyo ya ki serikali ya Imetosha Foundation inayopinga unyanyapaa, ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino kwa njia ya elimu, inatarajia kutuma ujumbe mzito kanda ya ziwa hapo kesho kwa maandalizi ya ujio wa timu nzima ya taasisi hiyo iliyojikita kwenye kubadilisha mtazamo (mind set) wa watu juu ya janga hili. Ujumbe huo utaongozwa na mwenyekiti wa taasisi hiyo Bw Masoud Kipanya, Balozi Henry Mdimu Mgaya na katibu Salome Gregory,wajumbe watakaongozana na viongozi hao ni pamoja na Mkala Fundikira, Isaya Mwakilasa (wakuvwanga aka Baba Andunje) Zaytun Biboze, Kelvina John na msanii wa muziki wa reggae Jhikoman Manyika.
Mwenyekiti Masoud Kipanya akiongea katika kilele cha matembezi ya hamasa yaliyofanyika jijini Dar |
Dhumuni la safari hiyo itakayoupeleka ujumbe huo mpaka mkoani Shinyanga ni kwenda kujitambulisha kwa viongozi wa serikali na usalama wa mikoa na za kanda hiyo iliyoathiriwa sana na janga la ukatili na mauaji ya watu wenye ualbino. Taasisi ya Imetosha imepanga kwenda kanda ya ziwa baadaye mwezi ujao ambapo timu itaenda maeneo yaliyoathiriwa na kutoa elimu kwa wakazi wa maeneo hayo kuwa si kweli kwamba ukiwa na kiungo cha mtu mwenye ualbino utapata mafanikio, elimu hizo zitatolewa kwa njia ya filamu mbali mbali, michezo ya kuigiza na matamasha ya muziki.
Hoteli ya Green Palm utakapofikia ujumbe wa Imetosha Foundation jijini Mwanza aka the Rock City. |
Ujumbe huu ukiwa mjini Mwanza utakuwa chini ya udhamini wa hoteli ya Green Palm iliypo maeneo ya Bwiru, vile vile kampuni ya Mwananchi communication ltd (MCL) inayozalisha gazeti bora la Mwananchi na mengineyo itachapisha habari zote kuhusiana na msafara huo wa Imetosha kanda ya ziwa. Meneja wa hotel .
Isaya Mwakilasa wa (Orijino komedi) Henry Mdimu na familia ya Isaya aka Wakuvwanga |
ya Green Palm Bw Juma Herman ameuambia mtandao huu kuwa "imekuwa rahisi kwetu (Green Palm Hotel) kudhamini makazi na usafiri kwa taasisi hiyo kwa kuwa inachofanya ni kitu chema basi nasi tumeona ni vema tuwatie nguvu kwa kuwapatia malazi na usafiri wa ndani kwa kipindi chote watakachokuwa jijini Mwanza, kwa kweli sasa imetosha ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye ualbino" aliongeza.
Wakiongea na mtandao huu kwa nyakati tofauti Mwenyekiti Masoud Kipanya na Balozi Henry Mdimu walisema wanashukuru sana kwa kitendo cha Green Palm na Mwananchi communictaion na kuwa ni vya kuigwa na makampuni mengine ili kuiwezesha taasisi hiyo kufikia malengo yake. Taasisi ya Imetosha haina vyanzo vya fedha hivyo kutegemea wahisani kama Green Palm Hotel na Mwananchi communication.
Maktaba Baadhi ya wajumbe wa Imetosha wakijiandaa kwenda katika mchezo wa Simba na Yanga |
↧
Bayport Financial Services yazidi kuchanja mbuga, yazindua tawi la 80 wilayani Ileje, mkoani Mbeya
↧
More Pages to Explore .....