Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AENDELEA NA ZIARA YAKE JIMBO LA ARUMERU MAGHARIBI MKOANI ARUSHA

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi kwa kupeleka zege kwenye eneo husika wakati wa ujenzi wa daraja la Kisongo,ambalo lilikuwa kero kubwa kwa wananchi kutokana na barabara ya eneo hilo kulika na mmomonyoko wa udongo.

Ujenzi wa daraja la Kisongo ukiendelea kwa kasi,ambapo pia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana alikagua na kushiriki ujenzi wake.
Baadhi ya wananchi wa Kisongo wakipita juu ya barabara ambayo imeanza kuathirika na mmomonyoko wa udongo.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuweka zege wakati wa ujenzi wa kituo cha afya cha Manyire,ujenzi wa kituo hicho unatarajia kuisha mwaka huu ambapo kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni 500 zitakuwa zimetumika kukamilisha ujenzi huo.

  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa kutoka wilaya ya Arumeru Magharibi Ndugu Mathias Manga wakati wakiwasili kata ya Mlangarini tayari kushiriki ujenzi wa Kituo cha Afya cha kijiji cha Manyire.
  Shule ya Sekondari Sokoni II kama ionekanavyo pichani,ikiendelea kujengwa vyumba 12 vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo ambayo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alishiriki ujenzi wake na kuzungumza na baadhi ya wazazu (hawapo pichani).Ujenzi wa vyumba hivyo mpaka vitakapokamilika vinatarajia kugharimu kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni mia tisa
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ngaramtoni ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa CCM ya sasa haitofanya makosa, na kuwahakikishia kila atakayefanya makosa itabidi aubebe msalaba wake.
Moja ya shina la wakereketwa la Mateves lililofunguliwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana 
 Mbunge wa jimbo la Arumeru Magharibi Ndugu Goodluck Ole Medeyeakizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nduruma ambao walikuwa na malalamiko juu ya mradi wa maji wa Nduruma kuonekana kupelekwa mashambani badala ya maeneo wanayoishi wananchi.Ndugu Kinana wa pili kushoto alikuwepo kusikiliza malalamiko hayo na kuwapatia majibu.
Mmoja wa Wananchi akitoa malalamiko kuhusiana na mradi wa maji wa kijiji cha Nduruma mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana (hayupo pichani).
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ngaramtoni ambapo alitoa sababu mbali mbali za dalili za kufa kwa upinzani nchini.
Mbunge wa jimbo la Arumeru Magharibi Ndugu Goodluck Ole Medeye akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya shule ya msingi Ngaramtoni,Arusha.

Usalama wa kutosha Tamasha la Pasaka

$
0
0
Mjumbe wa Kamati ya maandalizi ya tamasha la Pasaka, Khamis Pembe, akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu tamasha hilo litakalofanyika Aprili 5.  Kushoto ni Mwenyekiti wa tamasha hilo, Alex Msama. (Picha na Francis Dande).
 Mwenyekiti wa Tamasha la Pasaka, Alex Msama akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu tamasha hilo litakalofanyika Aprili 5. Kushoto ni Mwenyekiti wa tamasha hilo, Alex Msama.

NA LOVENESS BERNARD

KAMATI ya Tamasha la Pasaka, imewahakikishia usalama wapenzi wa muziki wa Injili na Watanzania kwa jumla katika tamasha hilo litakalokata utepe Aprili 5 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mjumbe wa Kamati hiyo, Khamis Pembe, alisema tayari wamewasiliana na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna (CP), Suleiman Kova.

Alisema maandalizi ya Tamasha la Pasaka yamekamilika asilimia 90 na mwaka huu litakuwa la aina yake.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Alex Msama, alisema mwaka huu tamasha linaadhimisha miaka 15 tangu lianzishwe na wanatarajia kumwalika Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi kujumuika nao, kwani ndiye alikuwa mgeni rasmi wakati linaanzishwa.

Msama aliwataja waimbaji wengine watakaokuwepo katika tamasha hilo kuwa ni pamoja na John Lisu na Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama huku wakiwa katika mazungumzo na mwimbaji nguli wa nyimbo za Injili, Rose Muhando, kutokana na maombi ya wapenzi wengi wa tamasha hilo.

Airtel yakabadhi wakaazi wawili wa Mkoa wa Manyara magari aina ya Toyota IST

$
0
0
 Staff Sergeant wa wilaya ya Hanang Janet Mungolya akimkabithi funguo mshindi wa gari aina ya Toyota IST Bwn Mohamed Ahmed Khamisi mara baada  kuibuka mshindi wa droo ya wiki ya nne ya promosheni ya Airtel yatosha Zaidi.  Bi Emiliana ni mfanya biashara ndogo ndogo  na mkazi wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara akishuhudia ni meneja mauzo wa Airtel kanda ya kaskazini bwana Brighton Majwala
 Staff Sergeant wa wilaya ya Hanang Janet Mungolya akimkabithi funguo mshindi wa gari aina ya Toyota IST Bi Emiliana Tarmo HHaway mara baada  kuibuka mshindi wa droo ya wiki ya tano ya promosheni ya Airtel yatosha Zaidi.  Bi Emiliana ni mkulima na mkazi wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara akishuhudia ni meneja mauzo kanda ya kaskazini bwana Brighton Majwala
 Mshindi wa gari aina ya Toyota IST kupitia promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi bwana Mohamed Ahmed Khamisi akiwasha gari lake mara baada ya kukabithiwa gari yake katika halfa iliyofanyika katika uwanja wa mnada wa edasak wilaya ya Hanang mkoani Manyara

 Mshindi wa gari aina ya Toyota IST kupitia promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi Bi Emiliana Tarmo HHaway akifungua gari yake mara baada ya kukabidhiwa katika hafla iliyofanyika katika uwanja wa mnada wa edasak wilaya ya Hanang mkoani Manyara
Burudani katika hafla hiyo iliyofanyika katika uwanja wa mnada wa edasak wilaya ya Hanang mkoani Manyara.


Wakaazi wa wawili wa wilaya ya Hanang Mkoani Manyara kwa pamoja wamezawadiwa magari yao aina ya Toyota IST mara baada ya kuibuka washindi katika droo za promosheni ya Airtel yatosha Zaidi inayoendeshwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel .

 Mpaka sasa jumla ya washindi 37 wameshapatikana kutoka katika mikoa mbalimbali ikiwa bado promosheni inaendelea na magari mengi bado yanasubiri washindi ili wakabithiwe akiongea wakati wa halfa ya kukabidhi magari kwa wateja wa Airtel Mkoani Manyara.

Meneja wa Airtel Kanda ya Kaskazini Bwana Brighton Majwala alisema: "Tunajisikia furaha kuendelea kupata washindi wa rika tofauti kutoka katika maeneo mbalimbali nchini, nasikia furaha kupata washindi kutoka katika kanda yangu.

"Hivyo naendelea kuwaasa watumiaji wa mtandao wa Airtel na wale ambao hawajajiunga kufanya hivyo na kupata nafasi ya kujishindia. promosheni bado inaendelea na magari bado yapo kinachotakiwa kufanya ni kununua na kujiunga na kifurushi chako cha Airtel yatosha zaidi na kupata nafasi ya kujishindia. nawapongeza sana washindi wetu wa leo na washindi wote ambao wameshapatikana mpaka sasa.

"Na nachoweza kusema ni kwamba Airtel tunajivunia kuwa sehemu ya kubadili maisha ya watanzania wengi hasa walio na kipato cha chini na kuwawezesha kufikia ndoto zao huku tukiendelea kurahisisha shughuli zao za kiuchumi na kijamii kupita huduma zetu na promosheni kama hizi. ni matumaini yetu kwa kupitia promosheni hii ya Airtel yatosha zaidi watanzania wengi wataguswa na kuboreshewa maisha yao". 

 Kwa upande wake Bwana Mohamed Ahmad Khamis ambaye ni mshindi wa gari aina ya Toyota IST alisema "Nimesikia furaha kubwa sana leo kupata ushindi huu mkubwa, kwangu hii imekuwa kama ndoto, mimi ni mtumiaji mzuri sana wa huduma za Airtel na ninazo line tatu za Airtel na hii moja leo imenipa ushindi. kwakweli nimeamini kabisa Airtel yatosha zaidi na inabadilisha maisha ya watanzania.

"Nimekuwa na ndoto za kumiliki gari lakini leo Airtel imeniwezesha kufikia malengo yangu na kunipa ushindi huu mkubwa na kuniwezesha kumiliki gari langu, nawashauri watanzania hasa wale wasioamini kuhusu promosheni hizi sasa waamini na kujua kwamba ni kweli promosheni hii na ni ya uhakika kwani mimi nimeshinda bila kuwa na taarifa yeyote. nawashukuru sana Airtel yatosha zaidi".

Naye mama Emiliana Tarmo Hhaway ambaye alizidiwa na furaha hadi kushindwa kuongea kwa lugha ya kiswahili alisema: "Nnamshukuru Mungu sana kwa kuniwezesha kushinda gari hili lakini pia nawashukuru sana Airtel kwa kuniwezesah kushinda. mimi nimenunua kifurushi cha Airtel yatosha cha shilingi mia tano na leo namiliki gari la mamilioni ya pesa ni jambo la kustaajabu sana. gari hili sasa litaniwezesha katika shughuli zangu za kilimo, kutoa mazao shambani kwenda sokoni, litanisaidia katika shughuli zangu za kijamii, kusaidia majirani hasa tukiwa na wagonjwa na nyingine nyingi. nasema asante sana kwa Airtel na kwa ushindi huu 
 Droo ya wiki ya 7 ya promosheni ya Airtel Yatosha inategemea kufanyika siku ya Alhamisi jioni ambapo washindi wengine 7 wa wiki hii watapatikana na kutangazwa

Rais Kikwete awasili Burundi kulihutubia Bunge la EAC

$
0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Maua kutoka kwa watoto waliokuja kumlaki katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Bujumbura ambapo alianza ziara ya kikazi ya siku mbili.
 Rais wa Burundi Pierre Nkurunzinza akimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bujumbura leo jioni.Rais Kikwete yupo nchini Burundi kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo anatarajiwa kulihutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 Rais Kikwete na mwenyeji wake Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipokea heshima wakati nyimbo za Taifa za nchi zao zikipigwa
 Rais Kikwete na mwenyeji wake Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakikagua gwaride liloandaliwa na jeshi la Burundi.
Rais Kikwete akiwa na Mwenyeji wake Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi jijini Bujumbura jana  jioni. Picha na Freddy Maro.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya  Jumatano, Machi 18, 2015 amewasili nchini Burundi kwa ziara ya kikazi ya siku mbili nchini humo. 

Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa mji mkuu wa Burundi wa Bujumbura, Rais Kikwete amepokelewa na Rais wa Burundi Mheshimiwa Pierre Nkurunzinza na pamoja na mamia kwa mamia ya wananchi wa Burundi. 

Rais Kikwete ambaye amewasili Burundi akitokea Dodoma ambako alikuwa katika ziara ya kikazi pia leo Machi 19, 2015, atahutubia Bunge la Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki (EALA) katika nafasi yake ya Uenyekiti wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) katika hotuba ya The State of the East African Community Address.
 Saa chache baada ya kuwasili Bujumbura, Rais Kikwete amehudhuria chakula cha jioni ambacho ameandaliwa na Rais Nkurunzinza kwenye Hoteli ya Panoramique. 

Wabunge wa Bunge la EALA pia wamehudhuria chakula hicho cha jioni. Rais Kikwete ataondoka Burundi mara baada ya kuhutubia EALA kurejea mjini Dodoma kuendelea na ziara yake.

TBL YATOA MSAADA WA SH. MIL. 56 ZA KISIMA CHA MAJI MKURANGA

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, Luteni Mstaafu Abdallah Kihato (wa pili kulia), akipokea Hundi ya Sh. Milioni 56 kutoka kwa Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya Kusini, Bw. Victor Kavishe (wa pili kushoto) kwa ajili ya kusaidia mradi wa maji katika Kijiji cha Magoza, kilichoko Kata ya Kiparang'anda. Kushoto ni Meneja Mahusiano wa TBL, Bi. Emma Urio na Diwani wa Kata hiyo, Bi. KAru Karapina.
  Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kanda ya Kusini, Bw. Victor Kavishe (wa pili kushoto, akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, Luteni Mstaafu Abdallah Kihato, Hundi ya Sh. Milioni 56 zilizotolewa na Kampuni hiyo kwa ajili ya kusaidia mradi wa Maji katika Kijiji cha Magoza, kilichoko Kata ya Kiparang'anda. Kushoto ni Mkuu wa Mahusiano TBL,Bi. Emma Urio na Diwani wa Kata hiyo, Bi. Karu Karavina.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya GCL, Bw. Gerald Mosha (kushoto) akiomba dua pamoja na wananchi wa Kijiji cha Magoza kwa ajili ya kufanikisha mradi wa maji.

Diwani wa Kata ya Kiparang'anda Bi. Karu Karapina akikabidhi zawadi mbalimbali zilizotolewa na wananchi wa Magoza kwa ajili ya TBL.

 Akionesha Hundi aliyopewa na TBL

 Diwani wa Kata ya Kiparang'anda, iliyoko Mkuranga, mkoani Pwani, Bi. Karu Karavina akiishuikuru Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), baada kampuni hiyo kutoa Hundi ya Sh. Milioni 56 za mradi wa maji katika kijiji cha Magoza.. Walioketi kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Luteni Mstaafu Abdallah Kihato na Meneja Uhusiano TBL, Emma Urio.
 Afisa Uhusiano wa TBL. Bi. Doris Malulu akiungana na kinamama wa Kijiji cha Magoza kuomba dua ili maji yapatikane katika kijiji hicho.
 Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bi. Emma Urio akizungumza na wananchi wa Magoza, kabla ya kampuni hiyo kukabidhi sh. milioni 56 za mradi wa maji.

EU WAMPA TUZO MAMA HELEN- KIJO BISIMBA

$
0
0
MAMA
Umoja wa Ulaya umemtunuku Mama Helen Kijo- Bisimba (pichani) kutokana na mchango wake kwa ajili ya kutetea na kulinda haki za binadamu nchiini.

Tuzo hiyo, ilitolewa juzi na EU siku ya Jumanne wiki hii jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Mwaka wa Maendeleo Ulaya 2015.

Balozi wa Umoja wa Ulaya bwana Filberto Sebregondi alitoa tuzo hizo na kusema kuwa lengo lake ni kusimamia haki kwenye masuala ya kiulimwengu ikiwemo kupambana na umasikini na kuhamasisha raia kujihusisha na maendeleo. Wengine waliotunukiwa tuzo katika hafla hiyo pamoja na Mama Bisimba ni wanamziki Keisha Saban, Fareed Kubanda (FID Q), na Balozi Mpungwe, pamoja na Paul Ndunguru ambae ni msanii na mchoraji.

EU imekuwa mstari wa mbele kupambana na vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu hususani ukatili dhidi ya Wanawake na watoto ikiwemo vitendo vya ukeketaji, ndoa za utotoni, na mauaji ya vikongwe. Vilevile, EU imekuwa mstari wa mbele kupinga mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na kupinga adhabu ya kifo.

WATU WENYE UHITAJI MBALIMBALI WAPATIWA MISAADA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya ilala bwana  JEREMIAH MAKORERE wa tatu kushoto akiwakabidhi watu wenye ulemavu wa ngozi maarufu kama ALIBINO baadhi ya misaada ambayo imetolewa na taasisi hiyo kama njia moja wapo ya kusaidiana,hafla hiyo imefanyika jijini dar es salaam.

STORY NA EXAUD MTEI
 Viongozi wa dini nchini Tanzania wameaswa kutumia muda mwingi katika kutoa elimu kwa waumini wao waachene na matendo mbalimbali yasiyo mpendeza mungu.

Kauli hiyo leo imetolewa na mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya ilala bwana JEREMIAH MAKORERE aliyemwakilisha mkuu wa wilaya ya ilala katika hafla fupi iliyoandaliwa na taasisi ya kiislam ya AL-MARID kwa ajili ya utoaji wa misaada mbalimbali kwa watu wenye uhitaji maalumu wakiwemo walemavu ambapo amesema kuwa kama maeneo ya ibada yatatumika ipasavyo yanaweza kuwabadilisha wananchi wakawa na roho ya kumuogopa mungu.
Baadhi ya waliopata misaada hiyo wakichambua kuona bidhaa walizopatiwa
Bwana MAKORERE amesema kuwa kumekuwa na matendo mengi ya ukiukwaji wa haki za binadamu ambayo yanafanywa na watanzania wachache kutokana na kuwa mbali na mungu ambapo amezitaka taasisi mbalimbali za kidini kuwa katika mstari wa mbele katika kukemea hali hiyo.
Akitolea mfano wa mauaji yanayoendelea kushika kasi nchini tanzania ya watu wenye ulemavu wa ngozi amesema kuwa  pamoja na jitihadi kubwa zinazoonyeshwa na serikali ya tanzania katika kutoa elimu pamoja na kudhibiti bado  matendo hayo yanazidi kuongezeka kutokana na watu kutokuwa na hofu ya mungu hivyo akazitaka taasisi za kidini zote kwa umoja wao kuungana kuhakikisha kuwa hofu ya mungu inarejea mioyoni mwa watanzania ili kukemea matendo ambayo yanaonyesha kuvuruga amani ya Tanzania.
Mwakilishi wa mgeni rasmi bwana JEREMIAH MAKORERE akimkabidhi msaada kiongozi mmoja wapo wa kidini kutoka dhehebu la Budha, ambaye naye alifika katika hafla hiyo,hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi kutoka kila aina ya dhehebu nchini tanzania bila ubaguzi wa hali yoyote
Katika hafla hiyo fupi iliyofanyika jijini Dar es salaam taasisi ya kiislam ya AL-MARID imetoa msaada wenye thamani ya shilingi million 42 kwa makundi ya watu mbalimbali nchini yenye uhitaji maalumu wakiwemo walemavu wa ngozi,watoto yatima,wanafunzi na makundi mengine ambapo zaidi ya wahitaji 270 walikuwepo katika hafla hiyo kupokea zawadi hizo.
Baadhi ya misaada ikiwa tayari kutolewa kwa walengwa
Akizungumza na mtandao huu msemaji na muweka  hazina wa taasisi hiyo SHEKH RAJAB KATIMBA amesema kuwa  tasasisi yao imekuwa na utamaduni wa kutoa misaaada mara kwa mara katika makundi mbalimbali nchini ambapo kwa safari hii wamefanyia jijini dare s salaam na baadhi ya vitu waliivyotoa kama msaada ni pamoja na nguo,vyakula,vifaa vya wanafunzi vya shule,pamoja na misaada mingine ya kibinadamu.









ONESMO OLE NANGOLE AKIMPONGEZA KINANA NA NAPE


Have your cars inspected before importation: EAA urged

$
0
0
 The East Africa Auto-Mobile Service Company Operations Manager, Mr. Dean Stout speaks to the journalists in Dar es Salaam recently, on the importance of vehicles inspection especially for the cars imported from Japan.
Tanzania Bureau of Standards (TBS), Engineer Tumaini Mtitu speaks to the attendees of the Car Inspection Seminar prepared by the East Africa Auto-Mobile Service Company in Dar es Salaam recently, on the importance of vehicles inspection especially for the cars imported from Japan

Representatives from a Japanese automobiles firm have called upon Tanzanians to import vehicles that have been inspected, illustrating that by doing so they will be avoiding unnecessary additional costs.

Mr Stout Dean Lawrence, The International Operations Manager for the Japan-based East Africa Automobile Service Company Limited said in Dar es Salaam on Tuesday that importing uninspected vehicles pose as a risky doing as it may lead to further inconveniences to the buyer.

“Buyers should have a clear understanding that not all vehicles from Japan come in commendable quality, buyers should have the tendency to buy vehicles that has passed through inspection so as to maintain the quality and avoid incurring inconveniences,” he clarified.

Recently the company signed a three-year agreement with Tanzania Bureau of Standards (TBS) that enables it to have the mandate to conduct pre-shipment inspection of motor vehicles being exported from Japan to Tanzania.

According to the firm’s Tanzania country manager, Mr. Josia Nguku, East Africa Automobile Company Limited will inspect all the vehicles and make sure that there is value for money in what Tanzanians import.

JENNIFER MGENDI AACHIA ALBAMU YA WEMA NI AKIBA

$
0
0
 Mwimbaji wa siku nyingi wa nyimbo za injili nchini, Jennifer Mgendi, ameachia albamu yake mpya mapema wiki hii.

Akizungumza na blogu hii  Mgendi amesema albamu hiyo ina jumla ya nyimbo saba ambazo ni Wema ni Akiba, Nani kama Mungu?, Nakungoja aliomshirikisha Mchungaji Abiudi Misholi, Kimbilia Msalabani, Nakuhitaji Roho, Tenda nishangae na Wastahili.

Akizungumzia video ya albamu hiyo, Mgendi amesema maandalizi ya video yameanza na video itazinduliwa Juni 28 katika kanisa la DCT Tabata Shule katika tamasha litakaloambatana na shukurani ya kutimiza miaka 20 tangu aanze uimbaji. 

Mbali na uimbaji Jennifer pia ni muandaaji wa filamu mbalimbali za kidini hadi sasa akiwa na filamu tano Joto la roho, Pigo la faraja, Teke la Mama, Chaimoto na Mama Mkwe.


ZIARA YA MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI LONGIDO ARUSHA

$
0
0
20
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akipewa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC maelezo ya uendelezaji wa eneo la Usa-river lililonunuliwa na NHC kwa ajili ya kujenga Jiji la kisasa hapo jana.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Williama Vangimembe Lukuvi jana alifungua nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido na kuwataka wananchi kununua nyumba hizoili NHC iweze kujenga zingine kusaidia Wilaya hiyo kupata makazi bora. Picha zote na Muungano Saguya- Longido, Arusha
19
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akiondoka eneo la Meru Residential arpatments alipomaliza kukagua nyumba za makazi zilizojengwa na NHC na kuuzia wananchi hapo jana.
18
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akimweleza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi juu ya mpango wa NHC wa kujenga maduka makubwa ya kibiashara ili kuhudumia wananchi na wakazi walionunua nyumba za makazi za Meru alipomtembeza Waziri huyo hapo jana
9
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa nyumba na kuingia ndani kukagua nyumba hizo.

3
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akisalimiana na wafanyakazi wa NHC waliokuwa wamejipanga kumpokea Waziri Lukuvi kufungua nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido.
2
Hizi ni nyumba za gharama nafuu zilizokamilika kujengwa na NHC Wilayani Longido na ambazo ziko tayari kuuzwa kwa wananchi. Ufunguzi wa nyumba hizi ulifanywa jana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi
1
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akikagua maandalizi ya ufunguzi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido, Arusha kabla ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi kufanya ufunguzi huo jana.
New Picture (127)New Picture (126)
Mbunge wa Longido Mhe. Lekule Laizer akilishukuru Shirika la Nyumba kwa kuiweka Wilaya ya Longido katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC katika Halmashauri mbalimbali za Wilaya hapa nchini.
New Picture (125)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akihutubia halaiki ya wananchi wa Longido (hawapo pichani)waliohudhuria ufunguzi alioufanya wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani humo.
New Picture (124)
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Daudi Ntibenda akilishukuru Shirika la Nyumba kwa kujengwa nyumba Wilayani Longido eneo ambalo ni kame na lenye changamoto kubwa ya kutekeleza ujenzi wa nyumba bora
New Picture (123)
Watendaji wa Wizara ya Ardhi Mkoani Arusha na wananchi wakifuatilia matukio ya ufunguzi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido jana.
New Picture (122)
Mkuu wa Wilaya ya Longido Bw. Ernest Kahindi alitoa nasaha zake wakati wa ufunguzi rasmi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido jana.
New Picture (121)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akitoa maelezo kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi ya mradi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa Wilayani Longido.
New Picture (120)
Wananchi wa Wilaya ya Longido wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali zilizotolewa wakati wa ufunguzi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido
New Picture (119)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akikagua vyumba mbalimbali vya nyumba bora zilizojengwa na NHC Wilayani Longido.
New Picture (117)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akifungua rasmi nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Daudi Ntibenda, Mbunge wa Longido Mhe. Lekule Laizer na Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu.
New Picture (116)
Wafanyakazi wa NHC nao hawakuwa nyuma kumpokea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi alipowasili mradi wa NHC Longido kufanya ufunguzi rasmi.
New Picture (115)
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mikoa na Utawala wa NHC Bw. Raymond Mndolwa akisalimiana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi alipowasili Longido kufungua rasmi nyumba za ghrama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Longido.
New Picture (114)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akimpokea kwa furaha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi alipowasili katika mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC ili kufanya ufunguzi rasmi.
New Picture (113)
Msafara wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi ukiingia eneo la mradi wa nyumba za gharama nafuu zilijengwa na NHC Wilayani Longido ili kufungua rasmi nyumba hizo baada ya kukamilika ujenzi wake.
New Picture (111)
Hizi ni nyumba za gharama nafuu zilizokamilika kujengwa na NHC Wilayani Longido na ambazo ziko tayari kuuzwa kwa wananchi. Ufunguzi wa nyumba hizi ulifanywa jana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi
New Picture (127)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi akikagua nyumba za makazi zilizojengwa na NHC eneo la Levolosi Jijini Arusha.Nyumba hizi zinauzwa kwa wananchi.

MADIWANI WA MANISPAA YA LINDI WATEMBELEA MRADI MAPINGA SATELLITE WA UTT-PID ULIOPO BAGAMOYO

$
0
0
Diwani wa Kata ya Nachingwe, Lindi Mjini, Omary Chitanda (katikati) akiuliza swali kwa mtaalamu wa mradi huo
Diwani wa Kata ya Nachingwe, Lindi Mjini, Omary Chitanda (katikati) akiuliza swali kwa mtaalamu wa mradi huo.

*Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID) ilianza kazi zake Julai 1, 2013. Taasisi hii ilirithi kazi za miradi zilizokuwa zinafanywa na Taasisi mama yaani UTT.

Andrew Chale wa Mo dewji blog aliyekuwa Bagamoyo.

Baadhi ya Madiwani wa Manispaa ya Lindi Machi 17, wametembelea miradi mbali mbali ya UTT-PID iliyopo Dar es Salaam ikiwemo ule wa Bagamoyo wa New Mapinga Satellite. Madiwani hao waliweza kujifunza mambo mbalimbali dhidi ya mradi huo ulivyoandaliwa na kufanya kazi na namna ulivyopangiliwa kwa ustadi mkubwa.

Katika ziara hiyo inayotarajia kumalizika Machi 19, mwaka huu. Madiwani hao wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaaa ya Lindi, Frank Magali alipongea juhudi za UTT-PID kwa kufanikisha ziara hiyo kwani wamejifunza mengi na pindi watakaporejea Lindi, watakuwa mfano wa kuigwa.

“Kule kwetu Lindi pia tuna mradi uliopo katika hatua mbaali mbali na UTT-PID tayari wamesha pima baadhi ya viwanja katika mfumo kama huu wa kisasa tunaojifunza hapa hivyo itatusaidia sana kwa sasa” alisema Meya Magali.

Diwani wa Kata ya Nachingwea, Manispaa ya Lindi, Omari Chitanda akielezea namna alivyojifunza kwenye mradi huo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani)
Diwani wa Kata ya Nachingwea, Manispaa ya Lindi, Omari Chitanda akielezea namna alivyojifunza kwenye mradi huo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani).
Kwa upande wake, Diwani wa Nachingwea, Omari Chitanda alieleza kuwa, wamepata kuielewa vyema UTT-PID na naamna ya ufanyaji wake wa kazi.
“tunaipongeza UTT-PID kwani imetufungulia mwangaza wa kimaendeleo. Tutakapo rejea Lindi tutaenda kufanya mambo ya kimaendeleo katika kuubadilisha mji wetu” alisema Diwani Chitanda.
Aidha kwa upande wake msimamizi wa mradi huo wa Mapinga kutoka UTT-PID, Godfrey Charles alisema kuwa hdi sasa mradi huo umefanikiwa kwa kiwango ambapo tayari vimebaki viwanja vichache kati ya zaidi ya 500 vilivyochukuliwa.
Madiwani na maofisa kutoka UTT-PID wakifuatilia kwa makini maelezo ya msimamiz wa mradi huo wa Mapinga uliochini ya UTT-PID (Hayupo pichani
Madiwani na maofisa kutoka UTT-PID wakifuatilia kwa makini maelezo ya msimamizi wa mradi huo wa Mapinga uliochini ya UTT-PID (Hayupo pichani).
Pia madiwani hao, walipata elimu pamoja na ufanyaji wa kazi wa UTT-PID na wadau wanaoshirikiana nao huku hadi sasa ikiwa inasimamia miradi mbalimbali ikiwemo mikoa ya Pwani, Morogoro, Kagera, Dar es Salaam, Lindi na mikoa mingine hapa Nchini.
Aidha, kwa upande wa Madiwani hao walipongeza UTT-PID kwa hatua hiyo ya kuwapa elimu sambamba na kutembelea baadhi ya miradi inayoendeeshwa na taaisis hiyo.
..
New Mapinga Satellite town located 30km from Mwenge along new Bagamoyo road with hundreds of serviced plots for residential, commercial and trade purpose ready for sale. The town is fully installed with electrical, water and roads facilities.
DSCN9635
DSCN9651
DSCN9663
madiwani wa Lindi wakijadili jambo
Madiwani wa Lindi wakijadili jambo.

Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Umiliki Silaha wasomwa kwa mara ya Pili Bungeni .

$
0
0
Na Anitha Jonas – MAELEZO,Dodoma.
Naibu Waziri  wa Mambo ya Ndani Mhe.Pereira Silima amesoma Muswada wa Sheria ya Kupendekeza kutungwa kwa  Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Silaha ya mwaka 2014 Bungeni Dodoma kwa mara ya pili tarehe 19 Machi 2015.
Mhe.Silima alisema Serikali imeona umuhimu wa kutunga Sheria hii ya Udhibiti wa  Umiliki wa silaha kutokana na kukabiliana na tatizo la kuwepo na watu wengi wanao kumiliki silaha kinyume na sheria pamoja na kufanya matumizi mabaya ya silaha.
“Serikali imekubaliana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa na mfumo wa kisheria baada ya kusaini na kuridhia maazimio ya kudhibiti uzagaaji wa  silaha haramu na sheria hii inaelekeza wazi kuwa mtu anaweza kumiliki silaha akiwa na umri wa kuanzia miaka 25,”alisema Mhe.Silima.
 Mhe.Silima aliendelea kusema kuanzia mwaka 2000 mpaka 2013 serikali ilikamata zaidi ya silaha 34,156 zilizokamatwa katika operesheni mbalimbali na silaha hizo ziliteketezwa.
Kwa upande wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Mhe.John Chiligati aliipongeza serikali kupitia kifungu chake cha 19 kinachoeleza kuwa sihala zote zitawekwa alama ya utambuzi wa kitaifa,Pia baada ya sheria hii kupitishwa suala hilo lizingatiwe.  
“Kamati inapenda kuishauri Serikali katika kifungu cha 20(2) kuondoa adhabu ya kulipa faini kwa mtu anayemiliki silaha kinyume na sheria na badala yake ni kutumikia kifungu kisichozidi miaka mitano”,alisema Mhe.Chiligati.
Mhe.Chiligati aliendelea kusema kamati imeridhia marekebisho ya Serikali ya kuongeza idadi ya wajumbe wa kamati ili iwe na uwakilishi mpana  kutoka sekta binafsi,Pia Kamati imeshauri kifungu cha 5(3) kisomeke  kuwa mtu yeyote atakuwa na sifa za kuteuliwa kuwa mjumbe wa kamati endapo ni raia wa Jamhuri ya Muungano.
Naye Mbunge wa Nkasi Kusini Mhe.Desderius Mipata ameipongeza Serikali kwa kuunda Sheria itakayo dhibiti umiliki wa silaha  nchini, pia ameishauri serikali kuangalia ni namna gani itadhibiti maduka yanayouza silaha nchini.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA WA WASHIRIKA MAJENZI YA KIJANI WA AFRIKA MASHARIKI, JIJINI ARUSHA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Mkutano mkuu wa kwanza wa Washirika Majenzi ya Kijani wa Afrika Mashariki, uliofanyika leo Machi 19, 2015 kwenye Hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, PSPF, Adam Mayingu, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa kwanza wa Washirika Majenzi ya Kijani wa Afrika Mashariki, uliofanyika leo Machi 19, 2015 kwenye Hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemiah Mchechu, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa kwanza wa Washirika Majenzi ya Kijani wa Afrika Mashariki, uliofanyika leo Machi 19, 2015 kwenye Hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha.

NAIBU INSPEKTA JENERALI WA POLISI AFUNGA MAFUNZO YA WAKAGUZIWASAIDIZI WA JESHI LA POLISI CCP-MOSHI

$
0
0
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi,DIGP, Abdulrahmani Kaniki akikagua gwaride la wakaguzi wasaidizi wa polisi wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo ya maofisa hao katika chuo cha polisi Moshi.
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi,DIGP, Abdulrahmani Kaniki akimvisha cheo wp 2704 ssgt Batuli kuwa mkaguzi msaidizi wa jeshila polisi wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo ya maofisa hao katika chuo cha polisi Moshi.
Wahitimu wa kozi ya mkwaguzi msaidizi wa jeshi la polisi wakipita kutoa heshima kwa mgeni rasmi wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo ya maofisa hao katika chuo cha polisi Moshi.
Wahitimu wa kozi ya mkwaguzi msaidizi wa jeshi la polisi wakiimba kumkaribisha mgeni rasmi wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo ya maofisa hao katika chuo cha polisi Moshi. Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.

Nyalandu atakiwa kushughulika na matatizo ya wananchi

MAMA WA MITINDO ASIA IDAROUS KUPAMBA SIKU YA MWANAMKE DUNIANI ZANZIBAR MACHI 22

$
0
0
11072283_933753296658934_392071823375109477_n
..burudani kutolewa na Baby J, Coconut na Zanzibar One Modern taarab
Na Andrew Chale wa Modewji blog

Machi 22 mwaka huu Kisiwa cha Unguja, Zanzibar kinatarajiwa kuwa na tukio moja kubwa litakalowakutanisha Wanawake mbalimbali na kusheherekea siku ya Mwanamke Dunia, ndani ya ukumbi wa Bwawani Hoteli.

Katika tukio hilo, linatarajiwa kuwa pia na shamra shamra ikiwemo za mitindo ya mavazi kutoka kwa gwiji wa mitindo Nchini, Mama Asia Idarous Khamsin atakaye onesha mavazi mbalimbali siku hiyo akiwa sambamba na Mbunifu wa mavazi wa Zanzibar, Matilda Revelian wa Matty Designs.

Sherehe hizo zimeandaliwa na kikundi cha akina mama cha Zanzibalicious Women Group, chenye maendeleo makubwa kwa sasa hapa nchini.
IMG_9704
Usiku huo utapambwa na burudani mbalimbali akiwemo mwanamuziki Baby J. Wengine ni bendi ya Coconut na Zanzibar One Modern taarab.

Aidha, Asia Idarous Khamisin amekisifia kikundi kilichoandaa halfa hiyo ya siku ya Mwanamke Duniani kwa Zanzibar, kwani ndio kwa mara ya kwanza Zanzibar wanawake na kusheherekea siku hiyo ya mwanamke duniani.
Usiku huo kiingilio kinatarajia kuwa sh. 35,000 kwa viti vya kawaida na sh 50,000 kwa upande wa V.I.P.

Aidha, kwa wadau wanaotaka tiketi wanaweza kutembelea katika maduka yaliyopo Mlandege Al Bashaer Tour, Magereza Ms Saloon, Michenzani Sas Saloon au kupitia mawasiliano ya simu ya namba: 0777418324, au 0777868766, 0715080399

TANZANIA, JAPAN WATILIANA SAINI UJENZI WA KITUO CHA UFUNDI STADI ILEJE

$
0
0
1
Signing the grant contract, witnessed by Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, and Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner. Front line from the left: Mr. Mussa Otieno, District Executive Director, Mr. Simon Mwango'nda, Executire Director of the recipient organisation, Integrated Rural Development Organisation, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan.


MKATABA wa Ujenzi wa kituo cha mafunzo ya ufundi stadi katika Wilayani Ileje, Mkoani Mbeya umetiwa saini. Mradi huo uliobuniwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene na Simon Kamiyoge umelenga kuwawezesha wakazi wa Ileje kuwa na taaluma ya ufundi na baadae kutumika kuendelea wilaya hiyo.

Mkataba huo ulitiwa saini kati ya Kazuyoshi Matsunaga wa ubalozi wa Japan nchini na na Mwakilishi wa Integrated Rural Development Organisation (IRDO) Simon Kamiyoge wakishuhudiwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Janet Mbene , Mbunge wa Ileje Rosemary Staki na Mkuu wa wilaya ya hiyo Mohamed Maliyao Mwala, na Mwenyekiti wa halmashauri ya Ileje Musa J. Otieno na maofisa wengine wa wilaya hiyo.

Kaimu Balozi wa Japan Kaziyoshi alisema amefurahishwa sana kutiwa saini kwa mkataba huo kwa kuwa unamkumbusha miaka 70 iliyopita katikati ya vita kuu ya pili ya dunia ambapo Japan ilijikuta katika uharibifu mkubwa pamoja na kubomolewa kwa majengo ya shule.
Alisema katika vita hiyo Japan ilijikuta si tu hawana shule bali hakukuwa na nyumba, maji, umeme hamna chochote kile lakini sasa hivi Japan ni ya tatu kiuchumi.
2
Discussion between Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan, and Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade. From left: Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner, Hon. Mohamed Maliyao Mwala, Chairperson of Ileje District Council, Mr. Mussa Otieno, District Executive Director, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan.


Amesema pamoja na kuwa na uchumi mkubwa Japan haina gesi, haina dhahabu wala almasi kama ilivyo Tanzania.Alisema siri ya maendeleo makubwa ya Japan ni elimu na wafanyakazi wenye ujuzi unaotakiwa.

Alisema kuonesha ukuaji wa ujuzi alisema kwamba kampuyni maarufu ya magari ya Toyota, kabla ya vita ilikuwa ni kampuni ya nguo . Lakini baada ya vita ilijibadilisha kuwa kampuni ya magari, na sasa ni namba moja duniani.

Alisema siri ya Toyota ni kuwa na wataalamu wenye ujuzi na kuwa na malengo ya wazi yanayoambatana na tamaa ya kufanikiwa katika malengo hayo.
Lengo la Toyota lilikuwa kushindana na viwanda vya Marekani na hivyo walinunua gari kutoka Marekani na kulivunja katika vipande 4000 na baadae mafundi wa Toyota wakaigiza vipande hivyo na kuunga gari kwa mikono yao wenyewe.
3
Speech by Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires. From left: Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires, Mr. Joseph Safe Mchome, District Land, Natural Resources and Environmental Officer, Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade.
Katika hatua za mwanzo magari yaliyotengenezwa yalikuwa mabaya sana lakini siku zilivyokwenda walitoa gari nzuri zaidi na sasa ni namba moja duniani.
Kwa sasa Toyota si tu kampuni yenye wataalamu tu lakini pia wataalamu hao hupewa motisha ya kuweza kutekeleza malengo yote.
Kaimu alisema kwamba kwa kuangalia uzoefu wa zamani wa kiutendaji , Japan inaamini ili kuendeleza ni lazima kutengeneza namna ya mradi unaohamasisha vijana na pia kuwapa utaalamu wa kuutumia na katika dhana hiyo wanatoa msaada kuijenga Ileje ijayo.
4
Shaking hands after the speech. From left: From left: Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires, Mr. Joseph Safe Mchome, District Land, Natural Resources and Environmental Officer, Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade.

Kituo hicho kinatarajiwa kuwanoa vijana kitaalamu katika masuala ya ufundi stadi ili vijana hao waweze kutekeleza ndoto zao na za eneo lao wanalotoka na taifa.

Mradi huo uliotiwa saini ni wa shilingi milioni 160.
Balozi huyo alitoa shukurani kwa timu ya watu waliofanikisha kupatikana kwa mradi huo na kusema wanaandaa vyema wakazi wa Ileje kwa maendeleo yao wenyewe.Alisema serikali ya Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha kwamba Tanzania inasonga mbele katika kufunzi za wataalamu.
5
Discussion between Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan, and Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, at the planned construction site of vocational training centre. From left: Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires.
6
Gift from Ileje District. From left: Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires, Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner.

Benki ya Posta yawapa msaada waathirika mvua ya mawe Kahama

$
0
0
Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Shinyanga Lawrence Munisi (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kahama na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Benson Mpesya (kushoto) msaada wa tani saba na nusu za saruji kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokana na mvua yam awe yaliyotokea kijiji cha Mwakata Wilaya ya Kahama. 
 Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Shinyanga Lawrence Munisi (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kahama na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Benson Mpesya (kushoto) msaada wa tani saba na nusu za saruji kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokana na mvua yam awe yaliyotokea kijiji cha Mwakata Wilaya ya Kahama.Mkuu wa Wilaya ya Kahama na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Benson Mpesya (kulia) akitoa shukrani kwa Benki ya Posta mara baada ya kupokea msaada wa tani saba na nusu za mifuko ya saruji zilizotolewa na benki hiyo. 
Mkuu wa Wilaya ya Kahama na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Benson Mpesya (kulia) akitoa shukrani kwa Benki ya Posta mara baada ya kupokea msaada wa tani saba na nusu za mifuko ya saruji zilizotolewa na benki hiyo.Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Shinyanga Lawrence Munisi akizungumza na wajumbe wa kamati ya maafa kabla ya kukabidhi msaada uliotolewa na benki hiyo. 
Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Shinyanga Lawrence Munisi akizungumza na wajumbe wa kamati ya maafa kabla ya kukabidhi msaada uliotolewa na benki hiyo.


 BENKI ya Posta tawi la Shinyanga imetoa msaada wa mifuko ya saruji tani saba na nusu yenye thamani ya sh. milioni 3 kwa ajili ya waathirika wa mvua ya mawe katika Kijiji cha Mwakata wilaya ya Kahama. Msaada huo umekabidhiwa jana na Meneja wa Tawi la Benki ya Posta, Shinyanga Lawrence Munisi kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya. 

Akikabidhi msaada huo Meneja wa Tawi la Benki ya Posta Shinyanga, Lawrence Munisi alisema Benki ya Posta imeguswa na tukio zima la maafa ya mafuriko na mvua ya mawe iliyoleta madhara kwa wananchi hivyo imeamua kuchangia msaada wa mifuko ya saruji isaidie kwa wananchi walioathirika na janga hilo.

 “Kwa niaba ya Benki ya Posta, tunatoa pole kwa wale wote waliokumbwa na maafa haya ya mafuriko, na kwa msaada huu wa mifuko ya saruji tunaamini inaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa sana waathirika wote,” alisema Munisi akikabidhi msaada huo. Aidha kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa, Mpesya alitoa shukrani za dhati kwa niaba ya waathirika wote na kuziomba taasisi nyingine na hata watu wenye uwezo kuiga mfano wa Benki ya Posta.

 “Kwa kweli tunashukuru sana kwa msaada huu mliotoa Benki ya Posta, na tunaamini msaada huu utasaidia sana katika kurudisha mazingira mazuri kwa wale wote waliopatwa na maafa haya...Tunaomba pia taasisi nyingine ziunge mkono, maana hili janga ni la Taifa na takribani watu wengi sana wamepoteza malazi na mahitaji yao mengine muhimu," alisema Mpesya. 

Mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na upepo mkali iliyonyesha hivi karibuni katika Kijiji cha Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga ilisababisha maafa ambako watu kadhaa walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa. Nyumba kadhaa zilianguka na nyingine kuezuliwa paa kutokana na upepo mkali ambapo baadhi ya familia zimekosa makazi.

MWENYEKITI WA CHADEMA WILAYA YA MONDULI AJIUNGA NA CCM

Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images