Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live

WANAHABARI WASHIRIKI MAFUNZO YA SIKU TATU YA KUANDIKA HABARI ZA UCHUNGUZI NA UKATILI WA JINSIA

0
0
 Waandishi wa habari wa mikoa ya kanda ya kaskazini ya Kilimanjaro, Arusha, Tanga na Manyara wakiwa kwenye mafunzo ya siku tatu ya kuandika habari za uchunguzi na ukatili wa kijinsia yaliyofanyika mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro na kuandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake nchini (Tamwa)
Mwandishi wa habari mwandamizi Deo Peter wa asasi ya Media Developmet Consultancy (Medoco) akizungumza mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro kwenye semina iliyoandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake nchini (Tamwa) yaliyotolewa kwa waandishi wa habari wa mikoa ya kanda ya kaskazini wakiwa kwenye mafunzo ya kuandika habari za uchunguzi na ukatili wa kijinsia yaliyofanyika mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro.Picha na Joseph Lyimo

CHUO CHA BIASHARA DAR ES SALAAM (CBE) CHATOA MSAADA WA MASHUKA KWA AJILI YA WODI YA AKINAMAMA NA WATOTO KATIKA HOSPITALI KUU YA MANZIMMOJA

0
0
Mkuu wa Chuo cha CBE  Prof. Emanuel Amani Mjema akimkabidhi Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Maalim Abdalla Mwinyi msaada wa mashuka uliotolewa na chuo hicho kwa ajili ya Hospitali Kuu ya Mnazimmoja katika hafla iliyofanyika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja mjini Zanzibar.
Mkuu wa Chuo cha Biashara cha Dar es Salaam Prof. Emanuel Amani Mjema akitoa maelezo kuhusu maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo  katika hafla ya kukabidhi mashuka katika Hospitali kuu ya Mnazimmoja Zanzibar, kulia ni  Naibu  Mkuu wa Chuo hicho anaeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri Dkt. Esther R. Mbise. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

 cb4 
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis katika picha ya pamoja na watendaji wakuu wa Chuo cha CBE  na baadhi ya maafisa wa Hospitali  ya Mnazimmoja . (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar). cb5 
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Maalim Abdalla Mwinyi Khamis akiagana na Mkuu wa Chuo cha CBE baada ya kukabidhiwa mashuka kwa ajili ya wodi ya wanawake na watoto  Hospitali Kuu ya Mnazimmoja ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 50 ya chuo hicho. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

SERIKALI YAPATA SH. BILIONI 15 ZA KULIPA MADENI YA MAHINDI

0
0
 SERIKALI Serikali imepata mkopo wa sh. bilioni 15 ambazo zitatumika kulipa kiasi cha madeni ya mazao ya nafaka ambayo wakulima wanaidai kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Iringa akiwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo katika mkoa huo.

Akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo (SACCOS) cha Mazombe kilichopo Ilula wilayani Kilolo, mwishoni mwa wiki, Waziri Mkuu alisema katika kipindi cha mwezi huu, Serikali imepata mkopo huo kutoka benki ya CRDB ambazo zimesambazwa kwenye mikoa mbalimbali ili kuwalipa wakulima hao.

Alisema hadi kufikia Machi mwaka huu, Serikali itahakikisha inamaliza kulipa madeni kwa wakulima ambao waliuza mazao yao kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA).

Akifafanua kuhusu mgao wa fedha hizo, Waziri Mkuu alisema kanda ya Arusha wamepata sh. bilioni 1.72/-; kanda ya Dodoma sh. bilioni 2.02/-; kanda ya Kipawa sh. milioni 632.3/-; kanda ya Makambako sh. bilioni 4.58/-; kanda ya Shinyanga sh. milioni 238.85/-; kanda ya Songea sh. bilioni 1.97/- na kanda ya Sumbawanga sh. bilioni 3.82/-.

Alisema fedha hizo zimegawanywa kwenye vituo, vikundi na mawakala na kuongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika itatoa sh. bilioni 15 nyingine ili zigawanywe katika kanda na kumaliza kabisa madeni ya wakulima.

Alitoa ufafanuzi huo baada kutolewa malalamiko kuwa ucheleweshwaji wa malipo hayo kwa wakulima umewafanya baadhi yao washindwe kurejesha mikopo kwenye taasisi za fedha kwa wakati.

Alisema ucheleweshwaji wa malipo hayo ulitokana na ziada ya chakula kwenye msimu wa kilimo wa mwaka 2014 kuongezeka kwa kufikia zaidi ya tani milioni 1.3, ukilinganisha na ziada ya tani 300,000 za msimu uliopita. “Serikali ililazimika kununua mazao ya wakulima zaidi ya malengo yake… matokeo hayo mazuri ya kilimo, yalitokana na msisitizo wa Serikali kuwekeza kwenye pembejeo, mbegu bora pamoja na kuingiza nchini matrekta zaidi ya 1600.

Mapema, akisoma taarifa ya chama hicho mbele ya Waziri Mkuu, Mwenyekiti wa Mazombe SACCOS, Bw. Yohanes Mwemtsi, alisema kucheleweshwa kwa marejesho ya mikopo iliyochukuliwa na wakulima kunazorotesha maendeleo ya SACCOS hiyo kwa kushindwa kujiimarisha kimtaji.

Alisema licha ya changamoto hiyo, chama hicho kimeshatoa mikopo yenye thamani ya sh. bilioni 4.3 kwa wanachama wake zaidi ya 1,300 huku kukiwa na ongezeko la wanachama wapya kwa wastani wa asilimia 10 kila mwaka.
 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, FEBRUARI 23, 2015.

TAMWA YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI WA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI JUU YA KUPAMBANA NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

0
0
WENCE AKITOA ELIMU KWA WANAHABARI WALIOKUTANA MKOANI IRINGA
WANAHABARI WAKIWA MAKINI KUMSIKILIZA MTOA ELIMU
MWANAHABARI FRANK KIBIKI AKIWA MAKINI KUFUATILIA NINI KINACHOENDELEA KWENYE MAFUNZO HAYO

 NA fredy mgunda,iringa

Waandishi wa habari wametakiwa kuandika zaidi habari zinazohusu unyanyasaji wa kijinsia hususan dhidi ya wanawake na watoto ili kuiamsha zaidi jamii inayowafanyiwa vitendo hivyo na mamlaka husika ziweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya vitendo hivyo.

Msisitizo huo ulitolewa na chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) kwa waandishi wa habari wa mikoa ya nyanda za juu kusini (IRINGA,MBEYA,SONGEA NA NJOMBE) ambapo wanahabari wameombwa kuendelea kufichua habari hizo hususan kwa wanaofanyiwa vitendo hivyo ili waweze kuelewa kwamba sheria dhidi ya ukatili huo zipo na kwamba kuna taasisi za kuwatetea.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo mwanahabari wa siku nyingi WENCE MUSHI alisema dhahiri kuwa vitendo vya unanyanyasaji vimepungua kutokana na wanaofanya ukatili huo kuelewa, na watendewa pia kuzidi kuamka, juhudi zaidi zilitakiwa kujipenyeza zaidi dhidi ya imani za kimila ambazo bado zinashikiliwa katika sehemu mbalimbali za nchi.

“Endeleeni kutumia kalamu zenu na vifaa vyenu vyote kupiga vita vitendo vyote vinavyotokana na manyanyaso ya kijinsia ambayo hasa hutokana na mfumo dume,” alisema wence akiwaomba wahabari kufanya hivyo kwa ajili ya kuendeleza juhudi za kutokomeza kabisa suala la unyanyasaji wa kijinsia.

Wence alisema jicho la waandishi wa habari linasaidia kuwaelimisha wananchi juu ya mambo mbalimbali yanafanywa kinyume cha seria,kuwaomba wanahabari kufanya habari za kichunguzi juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na unyanyasaji wake.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa TAMWA imekijita katika kufuatilia habari juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na mauwaji ya watu wenye ulemavu na kulenga hasa habari za kichunguzi ambazo zitaleta mabadiliko kwa jamii yetu.

Kwa upande wa waandishi wa habari wa nyanda za juu kusini walioshiriki warsha hiyo wamesema kuwa wanafanya kazi hiyo katika mazingira magumu,hivyo kuwaomba TAMWA kuwasaidia chombo cha usafiri kila mkoa ili waweze kuwafikia wananchi waliopo vijijini na kupata taarifa zao.

Lakini wakawataka wanahabri wengine kufanya kazi kwa kufuta weledi wao kutokana na elimu walioipata wakiwa darasa na kwenye mafunzo mbalimbali.

PSPTB YAFANYA SEMINA YA UTAFITI KWA WANAFUNZI WA BODI YA WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI

0
0
Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi PSPTB imeendesha mafunzo kwa wanafunzi wa fani ya ununuzi na ugavi wanaofanya tafiti kama sehemu ya mafunzo yao ya shahada ya
Ununuzi na ugavi.

Mafunzo hayo yalifunguliwa tarehe 16 Februari 2015 na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi Dr. Clemence Tesha, ambaye aliwaasa wanafunzi hao wazingatie mafunzo hayo ili kuongeza ubora wa kazi za utafiti watakazofanya kwa ajili ya kupata shahada ya juu ya ununuzi na ugavi. Aidha, alisisitiza kuwa wanapaswa kuzingatia maadili katika kufanya utafiti, jambo ambalo ndio msingi na matakwa ya Bodi. wanafunzi wanatakiwa kufanya utafiti wao wenyewe na sio kuchukua kazi zilizofanywa na wanafunzi/watafiti wengine au kufanyiwa na watu wengine maana kufanya hivyo ni kuvunja sheria. 

Pamoja na kuwajengea uwezo wa kufanya utafiti, pia wanafunzi wanajengewa uwezo wa kujiamini, kuandika ripoti na kujieleza na hata kuwasilisha ripoti katika sehemu zao za kazi. Hivyo lengo kuu la semina hii ni kuwajengea uwezo wa kuandika, kujieleza na kutoa huduma bora kwa taifa, kwani ufaulu wa mwanafunzi, unategemea sana uwezo wake wa kuitetea kazi yake, ambapo katika mtihani huo mwanafunzi atawasilisha kazi yake mbele ya wataalam, ili kupima uwezo wake.
New Picture (88) 
Mr. Godfred Mbanyi, Mkurugenzi wa Mafunzo PSPTB akitoa neno katika ufunguzi wa semina ya utafiti iliyofanyika kwenye ukumbi wa TEC Kurasini Dar es Salaam tarehe 16/2/2015
New Picture (89)
Mkurugenzi wa mafunzo Mr. Godfred Mbanyi akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa PSPTB Dr. Clemence TEsha kufungua semina ya utafiti katika ukumbi wa TEC Kurasini Dar es Salaam. Tarehe 16/02/2015
New Picture (90) 
Picha ya pamoja ya Mkurugenzi mtendaji wa PSPTB na washiriki wa semina ya Utafiti iliyofanyika Katika ukumbi wa TEC Kurasini Dar es Salaam tarehe. 16/2/2015.
New Picture (91)Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB Dr. Clemence Tesha(aliyeketi katikati), mwezeshaji wa semina Dr. Eli Tumsifu (aliyeketi kushoto) na Mr. Godfred Mbanyi Mkurugenzi wa mafunzo (aliyeketi kulia) katika picha ya pamoja na washiriki wa semina
New Picture (92) 
Washiriki wa Semina ya utafiti wakimsikiliza mwezeshaji Dr. Eli Tumsifu toka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwenye semina ya utafiti iliyofanyika katika ukumbi waTEC Kurasini Dar es Salaam tarehe. 16-20 Februari 2015
New Picture (93) 
Dr. Eli Tumsifu akiwa na washiriki wa semina ya utafiti ya PSPTB ndani ya ukumbi wa TEC Kurasini Dar es Salaam tarehe 16-20 Februari 2015
New Picture (94) 
Washiriki wa semina ya utafiti ya PSPTB wakiwa na Mkurugenzi mtendaji wa PSPTB Dr. C. Tesha (aliyeketi katikati), Dr. Eli Tumsifu Mkufunzi wa semina (aliyeketi kushoto) na Mkurugenzi wa mafunzo wa PSPTB Mr. Godfred Mbanyi (aliyeketi kulia) wakati wa semina yautafiti iliyofnyika 16-20 Februari 2015 katika Ukumbi wa TEC Dar es Salaam.

MAKALA;NAOMBA MAJIBU YA MASWALI HAYA KUFUNGIWA KWA MISS TANZANIA

0
0
NA MICHAEL MAURUS.
 
KARIBUNI wasomaji wangu katika safu hii ambayo huwa inawajia kila Jumatatu, ikilenga kupashana hili au lile kuhusiana na masuala ya michezo na burudani.
 
Japo katika mada hii nimejitambulisha kama Kocha Mchezaji, lakini ni vema ikafahamika hilo halinizuii kujadili masuala mengine kama burudani kwani wapo ‘makocha’ wenzangu ambao huwa wanajihusisha na burudani, mfano mzuri akiwa ni kocha wa makipa wa Yanga, Juma Pondamali ambaye ni mkali wa muziki wa kizazi kipya.
 
Baada ya muda mrefu kujadili mambo ya soka, leo ninageukia tasnia ya urembo. Kwa wale wasiofahamu, mambo ya urembo nipo nayo karibu kwani nilishawahi kuibuka mwandishi bora wa Vodacom Miss Tanzania 2007 nikapata fursa ya kwenda Miss World nchini China kuripoti shindano la mwaka huo, nikiongozana na mrembo Richa Adhia.
 
Pia, nimekuwa jaji wa mashindano hayo kwa ngazi za vitongoji kwa takribani miaka minne, lakini pia kwa miaka mitano nimekuwa Jaji Mkuu wa kipengele cha michezo katika fainali za Miss Tanzania.
 
Kwa hayo, inatosha kunifanya kuwa miongoni wanafamilia wa mashindano hayo hivyo kuwa na haki ya kutosita kujadili suala lolote linalohusiana na tasnia hiyo.
 
Desemba 14, mwaka jana, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), lilitangaza kuyafungia mashindano ya Miss Tanzania kwa muda wa miaka miwili kutokana na kile kilichodaiwa ukiukwaji mkubwa wa taratibu na sheria za uendeshaji wa mashindano hayo.Hatua hiyo ilionekana kuwashutua wengi kutokana na umaarufu wa mashindano hayo.
 
Binafsi sikutaka kukurupuka kuandika lolote badala yake niliamua ‘kuingia msituni kusaka ndondo’ za kutosha kuniwezesha kuwatendea haki BASATA, Lino International Agency ambao ndio waandaaji wa mashindano hayo pamoja na wadau wa urembo kwa ujumla.
 
Hatimaye nimefanikiwa katika hilo na leo nimeona ni vema nikatoa dukuduku langu ambalo naamini mwisho wa siku, wadau halisi wa urembo watapata majibu iwapo hatua hiyo ya kufungiwa kwa mashindano hayo ni sahihi au la.
 
Kutokana na ‘document’ nilizofanikiwa kuzipata baada ya kuhaha kwa muda mrefu, kuna mambo ambayo wadau wa urembo ningependa tuyatafakari kwa kina bila kujali itikadi zetu juu ya mashindano ya Miss Tanzania au uhusiano wetu na Mkurungezi wa Lino, Hashim Lundenga.
 
Kwa mujibu wa barua kutoka Basata kwenda Lino International Agency yenye kumbukumbu BST/PR/LIAL/VIII/14 ya Desemba 12, 2014 juu ya kufungiwa kwa mashindano ya Miss Tanzania, sababu iliyotolewa juu ya uamuzi huo ni kutokana na ‘ukiukwaji mkubwa wa taratibu na sheria za uendeshaji wa mashindano hayo.
 
Barua hiyo ilisomeka kuwa uamuzi huo umelenga kurejesha heshima katika tasnia ya mashindano ya urembo nchini na kwamba Baraza linaamini kuwa muda huu uliotolewa kwa Lino utatosha kujirekebisha na kujipanga upya.
 
Baraza hilo lilionya kuwa endapo kasoro zilizojitokeza hazitarekebishwa ndani ya kipindi hicho, halitasita kuendelea kuifungia Lino hadi hapo kasoro zote zilizobainishwa zitakaporekebishwa.
 
Barua hiyo iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mtendaji wa Basata, nakala yake ilitumwa kwa Katibu Mkuu WHVUM, Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Sanaa la Taifa, Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Utamaduni, Wakurugenzi wa Maendeleo wa mikoa, ikiagizwa aione Afisa Utamaduni wa Mkoa na Wakurugenzi wa Maendeleo wa Wilaya, ikiagizwa aione Afisa Utamaduni wa Wilaya.
 
Lakini kabla ya kufungiwa kwa shindano hilo, kuna barua ambayo Basata waliwaandikia Lino iliyotolewa Oktoba 7, mwaka jana yenye kumbukumbu no. BST/PR/LIALl/VOL. 7/159 ambayo iliwataka Lino kuwaondoa kambini warembo katika orodha ya ushiriki wa mashindano hayo ya taifa wale waliopatikana kutokana na mawakala ambao hawajasajiliwa na Basata, mpaka hapo watakaposajiliwa.
 
Kwa mujibu wa barua hiyo, kushindwa kufanya hivyo, hatua zifuatazo zitachukuliwa dhidi ya Lino ambazo ni kusimamisha shindano, kufungiwa shughuli za uendeshaji wa shughuli za sanaa kwa muda usiojulikana na kufutiwa usajili.
 
Baada ya barua hiyo, ilifuata nyingine ya Novemba 21 mwaka jana ambayo ilikuwa ikitoa onyo kali kwa Lino ikirejea maazimio ya kikao kati ya Lino na Basata cha Oktoba 3, 2014 katika ukumbi wa baraza hilo.
 
Barua iliyo ilisema kuwa Lino walikiuka kwa makusudi taratibu za baraza hilo kwa kuwatumia mawakala wasiosajiliwa, kuanza mchakato wa mashindano bila kuwa na kibali cha uendeshaji wa matukio, kutokuwasilisha mikataba ya washiriki wa mashindano kwa wakati na kutowasilisha taarifa za mashindano kwa wakati.
Mambo ya kujiuliza juu ya kufungiwa kwa mashindano hayo.
 
Barua ya kwanza ya Basata kwenda Lino Oktoba 7 takribani siku sita kama si tano kabla ya kufanyika kwa shindano, baraza hilo liliagiza warembo ambao mawakaal wao hawajasajiliwa waenguliwe. Je, ilikuwa ni halali kufanya hivyo kwa warembo ambao walishafanya maandalizi yaliyoambatana na kutumia fedha zao kujiandaa kwa shindano hilo?
 
Je, ingekuwa ni kuwatendea haki wadhamini ambao walitumia mamilioni yao kwa maandalizi ya shindano hilo kuwaengua warembo waliotajwa zaidi ya 10 kutokana na makosa ya mawakala wao ambao kimsingi wanawajibika moja kwa moja kwa Basata ambao ndio wanaotoa vibali?
 
Basata kwa kushirikiana na Lino walishindwa vipi kuwabana mawakala hao tangu ngazi za vitongoji? Kama walishindwa wote, kwanini lihukumiwe shindano pekee ikizingatiwa mara nyingi Basata huwa wanatuma wawakilishi wao katika mashindano ya vitongoji, ikiwa ni pamoja na kualikwa wakati wa semina za mawakala kuelekea mashindano hayo ya urembo?
 
Lakini baada ya shindano kufanyika, Basata waliitisha kikao cha tasmini ya mashindano hayo ambapo wajumbe kadhaa, akiwamo Kocha Mchezaji, walitoa mapendekezo yao juu ya kuboresha kasoro zilizojitokeza, ikiwamo suala la uwazi wa mikataba, uboreshaji wa zawadi na mashindano kwa ujumla. Kinachoshangaza, kwanini badala ya Basata kutoa nafasi kwa mapendekezo ya wajumbe kufanyiwa kazi na Lino, waliamua kulifungia shindano?
 
Lakini inakuwaje baraza hilo litoe onyo kwa Lino na siku chache baadaye wanalifungia shindano, nini maana ya onyo lao? Lakini hatua ya kufungia shindano kwa miaka mwili, limelenga katika kulijenga au kumkomoa mtu? Je uamuzi huo umewafikiria vipi mabinti ambao wamekuwa wakihaha huku na kule kusaka ajira bila mafanikio, wengine wakidiriki hata kujidhalilisha ili kupata ajira?
 
Leo hii tunawaona watu maarufu kama Wema Sepetu, Jokate Mwegelo, Faraja Kota, Nancy Sumari, Richa Adhia na wengineo ambao maisha yao yameboreka kwa kiasi kikubwa baada ya kutengeneza majina yao kupitia mashindano ya Miss Tanzania, Basata wanapolifunmgia shindano hilo, wamewafikiriaje mabinti wa kitanzia wenye ndoto za kufuata nyayo za akina Jokate au Nancy?
 
Naomba kwa leo niishie hapa nikitarajia kupata maoni ya wasomaji wa safu hii na wa urembo kwa ujumla ili wiki ijayo tuweze kuhitimisha mada hii.
Nawatakia wiki njema.

MAKALA YA SHERIA: NAMNA YA KUMDAI FIDIA ALIYEVUNJA MKATABA AU KUKIUKA MAKUBALIANO YENU

0
0

Kawaida unapokuwa umeingia katika mkataba au makubaliano katika jambo lolote lile kunakuwa na masharti ambayo unapaswa kuyatimiza au kutimiziwa. Na hapa nazungumzia mikataba yote uwe wa kuuza mbuzi au ule wa kujenga ghorofa mia, yote ni mikataba. Masharti hayo huwa ndio makubaliano yenyewe au twaweza kusema kuwa ndio mkataba wenyewe. Kila upande unawajibika  juu ya utekelezaji wa masharti hayo. Yeyote anayefikia hatua ya kukiuka masharti hayo au hata kukiuka sharti moja tu, hana namna ila kukubaliana na  hatua na utaratibu wa kisheria kuhusu  uvunjwaji au ukiukwaji wa mikataba.

1.KUKIUKA MKATABA AU MAKUBALIANO.

Uvunjaji wa mkataba unaweza kutokea katika njia nyingi. Moja ni ile ya kawaida ambapo mtu huamua kujitoa kwa kusema,kutamka au kuandika kuwa sasa sitafanya hili na lile hata kama lipo katika makubaliano yetu.  Pili njia nyingine  ya kuvunja mkataba ni pale ambapo mtu hasemi kwa kutamka kwamba sasa sitafanya hili wala lile isipokuwa hatimiza wala hatekelezi kile mlichokubaliana. Ifahamike kuwa mtu anapoingia mkataba na mtu mwingine  au kampuni na kampuni  au kampuni na mtu sheria inalazimisha kutekeleza kwa usahihi yale yote yaliyokubaliwa  katika mkataba huo. Utekelezaji wa baadhi ya masharti na kuacha mengine au kutotekeleza yote kabisa ni uvunjaji au ni kujitoa katilka mkataba kwa mujibu wa sheria. Aidha nasisitiza kuwa ili mtu ajitoe katika mkataba sio lazima aseme kuwa nimejitoa katika mkataba. Kitendo cha kutofuata makubaliano  kama yalivyokubaliwa  ni kujitoa katika mkataba moja kwa moja.

2.KUMDAI FIDIA ALIYEKIUKA MKATABA AU MAKUBALIANO.

Si vyema mtu akafanya makubaliano na mtu mwingine halafu akapotea bila kutekeleza kile kilichokubaliwa. Ni sababu hii inayonifanya kuwaambia watu kuwadai fidia wale wanaokiuka masharti. Kudai kulipwa fidia baada ya kuvunjwa mkataba ni takwa la kisheria na hivyo si ukorofi kama ambavyo mtu anaweza kufikiri.

Kusoma zaidi BOFYA HAPA

MWILI WA MAREHEMU MEZ B WAPUMZISHWA KATIKA MAKABURI YA WAHANGA, DODOMA

0
0

IMG-20150223-WA0036
Pichani ni Mama mzazi wa Mez B akiwa ameshikiliwa na ndugu baada ya kuingia viwanja vya Mashujaa ili kutoa heshima za mwisho. Marehemu Mez B baada ya kuagwa na mashabiki wa mziki pamoja na ndugu jamaa na marafiki mwili wake ulielekea kupumzishwa katika makaburi ya Wahanga Maili mbili. PICHA ZOTE KWA HISANI YA DJ CHOKA

Mungu ailaze roho ya marehemu Mez B mahali pema peponi
Amin
IMG-20150223-WA0037IMG-20150223-WA0038
Baadhi ya wasanii waliohudhuria msiba huu wa Mez B wakiwa kwenye majonzi mazito
IMG-20150223-WA0039IMG-20150223-WA0040IMG-20150223-WA0041IMG-20150223-WA0042IMG-20150223-WA0044
Mtangazi wa Citizen TV anayejulikana kwa jina la Mzazi Willy Tuva akifanya mahojiano na msanii wa Bongo Fleva Janjaro.

CHF a stepping stone to a better life to every Tanzanian

0
0
unnamed
The Director of Community Health Fund (CHF), Mr Rehan M(centre standing ) opening three days on January 21, 2015 in Dar es Salaam, to the leaders of the SACCOs of entrepreneurs when they organize a seminar aiming to give them educational on community health fund other are leaders of the SACCOS.
4
....................................................................

By Damas Makangale, Dar es Salaam, Tanzania.

The promise by the goverment to increase more people in the Community Health Fund (CHF) to help reduce the number of people having to draw money from their pockets to access health services in the country is somehow sucessful and in the right track thanks the giant scheme National Health Insurance Fund (NHIF). The then Tanzania Minister for Health and Social Welfare, Dr Hussein Mwinyi pledged on 5th January 2013 during the discussion with a team of visiting Parliamentarians from the United Kingdom (UK) House of Commons who also took time to inspect UK Department For International Development (DFID) projects in the country.

 However, the minister said much as the fund had been introduced in the recent past, it had yet to pick up as intended. “In Tanzania there is growing commitment to the expansion of health insurance to achieve a ‘universal health system,’ whereby all those in need of medical care can access affordable services,” he said.Speaking to this reporter in an exclusive interview last week in Dar es Salaam, the Director of CHF, Mr Rehani Athumani said that the scheme is a voluntary body established by the Parliament act No.1 of 2001 and the scheme was first introduced as a pilot project in 1996 in Igunga district and was later rolled over to all other Councils. 


CHF is a pre-payment, council based, scheme aimed at facilitating the community to access health care at an affordable premium that is determined by the community itself.He said that the membership size of the fund has increased from 468,611 by the end of June, 2011 to 474,760 by the end of June, 2012, which is equivalent to 1.3% annual growth and likewise the number of beneficiaries has increased from 2,498,920 to 2,502,794, equivalent to 0.2% annual growth rate.“We are now seeking to increase more people across the country as we have 5,602,374 people countrywide depending on the scheme for their health facilities,” he saidMr Athumani explained further that the scheme always worked shoulder to shoulder with municipalities and local goverment leaders as they have invited 139 municipalities in the collaboration across the country. 

The contribution that members of the scheme require to inject starts from Tsh.5,000 to Tsh.20,000 and allows them together with their beneficiaries to have acces of health facilities to Dispensaries, Local hospitals and Religious health centres.The NHIF benefits package consists of eleven services which include; Registration and Consultation Fees, Outpatient services, medicines, diagnostic, tests, inpatient services, surgical services, physiotherapy and rehabilitative services, optical services, dental services, retirees health services and medical and orthopedic appliances.The Director of CHF, Mr Athumani a soft - spoken person said initially the fund encountered various challenges mainly lack of awareness on the priniciples that underlie the concept of social health insurance. 

He said that in order to tackle that challenge, the fund embarked on intensive and extensive awareness creation to key stakeholders.Stakeholders have gained a better understanding of the concept of social health insurance as evidenced by the increase of the base.To be recognised, the massive contribution of the NHIF in the health sector in Tanzania for the last fifteen years since its establishment it won the International Social Security Association (ISSA) Good Practice Award for Africa 2011 for improvements in its health insurance scheme. 

The ISSA Good Practice Award, which was presented at a ceremony in Arusha on 5th December, was presented to the NHIF for its strategic approach in improving its medical benefits’ package and health-care facilities, which has resulted into greater availability of medical services and an increase in number of the population which has access to health insurance in the country.An international jury which selected the winning entries also awarded three Certificates of Merit with special mention for good practices in social security to several other entries, including the National Social Insurance Fund of Cameroon. It was awarded for a project for processing and verifying the authenticity of civil status documents and certificates of school attendance. 

The National Social Insurance Institute of Cape Verde was awarded for its modernization project titled "new attitudes for new challenges," while the Rwanda Social Security Board received accolades for its strategy for extension of social security coverage to the informal sector.The International Social Security Association (ISSA) is the world's leading international organization bringing together national social security administrations and agencies.

 Commenting on the Rwanda Health Insurance and the contribution to the improvements of health facilities, Mr Athumani said that the Rwanda based scheme is one of the successful health service in the East African region.Rwanda is one of the most extensive community based health insurance schemes operated in Sub-Saharan Africa covering over 90 per cent of the population. 

Several studies, so far, have documented the success of the Mutuelle de Santé in addressing the two prime objectives of health insurance in a low- income setting, namely to increase access to health care and to reduce the burden of catastrophic health spending particularly for the poorer groups of society. It is a fact that the efforts that have been undertaken by the goverment of Tanzania through the Ministry of Health and Social Welfare and the National Health Insurance Fund (NHIF) will in the long run see a tremendous improvement of health services to majority of Tanzanians living rural and urban areas.

WATUMISHI WALIOKAA ZAIDI YA MIAKA 10 WAHAMISHWE - PINDA

0
0
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bibi Amina Masenza aandae orodha ya watumishi wa mkoa huo ambao wamekaa kwenye nafasi za ajira kwa zaidi ya miaka 10 na kumpelekea ili wafanyiwe utaraibu wa kuhamishiwa vituo vingine.

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatatu, Februari 23, 2015) wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Iringa waliofika kusikiliza majumuisho ya ziara ya siku sita ya Waziri Mkuu kwenye mkoa huo. Mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ulioko Mafinga, wilayani Mufindi.

“Tafuta wote waliokaa zaidi ya miaka 10. Ni lazima tuwabadilishe... niletee orodha mapema iwezekanavyo,” alisema Waziri Mkuu. Alisema nia ya zoezi hilo ni kuongeza ufanisi kwani watumishi wakikaa sehemu moja kwa muda mrefu wanakuwa butu kwa kukosa ubunifu kwenye kazi zao, wanaota mizizi na kugeuka kuwa chanzo cha matatizo katika baadhi ya sehemu.

Alimtaka pia Mkuu huyo wa mkoa pamoja na timu yake wasimamie vizuri ukusanyaji wa mapato ili kuongeza kiwango cha mapato cha mkoa huo. “Na siyo hilo tu, simamieni vizuri matumizi ya fedha zilizopangwa kwenye miradi mbalimbali ili kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi mnaowaongoza,” alisisitiza.

Alisema mkoa wa Iringa ni wa pili kwa kuwa na kiwango cha juu cha pato la mwanachi wa kawaida baada ya Dar es Salaam ambao ndiyo unaongoza nchini. “Katika taarifa ya Mkuu wa Mkoa, tulielezwa kwamba pato la mwananchi wa Iringa katika mwaka 2013 lilikuwa ni wastani wa shilingi 1,660,532/- ambazo ni sawa na shilingi 138,377/- kwa mwezi au shilingi 4,612/- kwa siku”. 

Alisema pato la mwananchi wa Iringa linakua vizuri ikilinganishwa na mwaka 2006 ambapo pato hilo lilikuwa shilingi 589,607/- na limeongezeka hadi kufikia shilingi 1,660,532/- mwaka 2013. 

Alivitaja viashiria vya kukua kwa uchumi kuwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za kisasa zenye umeme, elimu bora, afya bora na upatikanaji wa vifaa vya mawasiliano kwenye ngazi ya kaya. 

Alisema kulingana na taarifa ya Shirika la Fedha Duniani (IMF), Tanzania imeondolewa kutoka miongoni mwa nchi 10 barani Afrika zenye umaskini mkubwa na kwamba sasa Tanzania ni miongoni mwa nchi 20 duniani ambazo uchumi wake unakua kwa kasi kubwa.

“Kukua kwa pato la mkoa kumechangiwa hasa na kuwepo kwa mashamba makubwa ya tumbaku, chai, viwanda vya chai, misitu na viwanda vya mbao. Tukitumia vizuri fursa hizi, na tukijipanga vizuri tutaweza kuongeza pato la mkoa kuzidi hapa tulipo,” alisema.

Aliwataka watendaji wote katika ngazi zote, wawe na dhamira ya kuwaletea wananchi maendeleo na hivyo kuwaondolea umaskini na kuongeza pato lao kwa kila mmoja. “Ninawasihi sana viongozi wa mkoa tutangulize maslahi ya wananchi na siyo maslahi yetu binafsi. Tukifanya hivyo, wananchi wataona kweli tunawasaidia na tunastahili kuwaongoza,” aliongeza.

Waziri Mkuu amemaliza ziara ya siku sita katika mkoa wa Iringa na leo anakwenda Makambako, Njombe kuzindua uandikishaji wa Daftari la Mpiga Kura. Baadaye mchana, ataelekea Mbeya kuanza ziara ya kikazi ya siku sita kukagua shughuli za maendeleo katika mkoa huo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 24, 2015.

Wananchi wanaiona rushwa kama upotevu wa fedha zao na wangependa Rais achukue hatua

0
0
 Wananchi wanaiona rushwa kama upotevu wa fedha zao na wangependa Rais achukue hatua,Lakini ni wachache tu wanaounga mkono adhabu kali kwa viongozi wala rushwa

24 Februari 2015, Dar es Salaam: Wananchi saba kati ya kumi (69%) wanasema rushwa zilizoripotiwa kwenye ripoti ya mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ni upotevu wa fedha zao (za umma). Zaidi ya nusu ya wananchi (55%) wanaamini kuwa aina hii ya rushwa inagusa sana maisha ya yao ya kila siku, na watatu kati ya kumi (31%) wangependa kutaarifiwa kuhusu matokeo ya ukaguzi kupitia vipindi vya redio vinavyorushwa kila wiki kwa muda wa nusu saa.

Wananchi pia wanaamini kuwa Rais anapaswa kuchukua hatua juu ya matokeo ya ripoti ya CAG: Takriban wananchi sita kati ya kumi (57%) wanaamini kuwa Rais anawajibu wa kufuatilia masuala ya ukaguzi wa hesabu za serikali. Taasisi nyingine zinazotajwa kuwa na wajibu wa kufanya hivyo ni pamoja na Baraza la Mawaziri (16%) na mahakama (11%). Mbali na Rais, hakuna taasisi au mtu binafsi aliyetajwa na wananchi kwa zaidi ya 20% kuwa anawajibu wa kushughulikia masuala ya ukaguzi wa hesabu za serikali.

Matokeo haya yametolewa na Twaweza kwenye muhtasari mfupi wenye jina la Walezi wa Uwajibikaji: Ufahamu na maoni ya wananchi kuhusu taasisi za usimamizi. Muhtasari huu umetokana na takwimu kutoka utafiti wa Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaofanyika mara kwa mara kwa njia ya simu za mkononi. Matokeo yametokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,474 katika maeneo mbalimbali Tanzania Bara (Zanzibar haimo kwenye matokeo haya) kati ya miezi ya Septemba na Oktoba 2014.

Licha ya kuwepo kwa taarifa za wazi juu ya makosa ya rushwa na haja ya Rais kuchukua hatua, wananchi wana hisia kinzani linapokuja suala la adhabu kwa viongozi wenye matumizi mabaya ya fedha za umma. Mwananchi mmoja tu kati ya ishirini (6%) anafikiri kuwa wale wanaopatikana na hatia ya rushwa wanapaswa kuondolewa katika ofisi za umma, na ni mmoja tu kati ya wananchi sita (15%) anayefikiri kuwa wala rushwa wanapaswa kufungwa. Adhabu sahihi kwa wala rushwa iliyotajwa na wananchi wengi (32%) ni kufukuzwa kazi, kunyang’anywa pensheni, kunyang’anywa mafao na kulipa pesa walizofuja (30%).

Wananchi waliulizwa pia kuhusu ufahamu wao kuhusu taasisi kuu tatu za usimamizi wa fedha. Hizi hushiriki katika mchakato wa kuandaa na baadaye kufuatilia ripoti ya mwaka ya ukaguzi wa fedha nchini Tanzania; Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu (NAOT), Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu ilionekana kujulikana zaidi kuliko taasisi nyingine kati ya hizi tatu. Mwananchi mmoja kati ya watatu (34%) ameshawahi kumsikia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na mmoja kati ya sita (16%) anaweza kuelezea kwa usahihi kazi zake. Kwa kamati za bunge zenye wajibu wa usimamizi wa hesabu za serikali kuu na hesabu za serikali za mitaa, takwimu ziko chini zaidi. Wananchi watatu kati ya kumi (29%) wamewahi kusikia kuhusu PAC na zaidi ya mmoja kati ya kumi (13%) anaweza kueleza kazi zake kwa usahihi, wakati mwananchi mmoja tu kati ya wanne (26%) ameshawahi kuisikia kuhusu LAAC na mmoja kati ya kumi (11%) anaweza kueleza kazi za kamati hii.

Kwa taasisi zote tatu, wananchi wana wasiwasi juu ya uwezo wa taasisi hizi kufanya kazi bila kuingiliwa, na pia hawana uhakika na mafanikio ya taasisi hizi. Chini ya mwananchi mmoja kati ya wanne anaamini taasisi hizi za usimamizi zina uhuru wa kufanya kazi zao: kuhusu CAG (25% wanaamini ana uhuru kamili), LAAC (21%) na PAC (23%) wanaamini hivyo. Hakuna mwananchi aliyeweza kutaja mafanikio yoyote halisi ya taasisi hizi tatu. Kwa mfano, chini ya 5% ya wananchi walidhani kuwa moja ya taasisi hizi imewahi kugundua kashfa za rushwa au kuwaweka hadharani viongozi wa umma wala rushwa ndani ya kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Wananchi wengi pia wana uhakika kuwa kuna aina nyingi za rushwa ndani ya serikali, lakini wana wasiwasi kama rushwa hizi zitatajwa kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Wananchi tisa kati ya kumi (88%) wanafikiri kuwa rushwa hutolewa ili kupata cheo serikalini au kushinda zabuni, wakati zaidi ya wananchi watatu kati ya kumi (34%) wanafikiri kuwa kesi hizi za rushwa zitaandikwa kwenye ripoti ya CAG.

Elvis Mushi, Mtafiti Mkuu wa Sauti za Wananchi alitoa maoni juu ya matokeo haya na kusema "Ni dhahri wananchi wanaathirika na rushwa na wana imani ndogo na taasisi muhimu za usimamizi wa fedha kuweza kushughulikia madai yao. Hili linaeleweka ukizingatia kuwa rushwa kubwa serikalini imeibuliwa mara kwa mara lakini inaonekana haishughulikiwi ipasavyo kuzuia vitendo hivi visitokee tena. Sehemu ya tatizo ni kwamba taasisi zetu za uwajibikaji hazina meno halisi ambayo yangeweza kutumika kutoa adhabu kali kwa wanaopatikana kujihusisha na vitendo vya rushwa."

"Wakati huo huo," aliendelea kusema "wananchi hawatetei kuwepo kwa adhabu kali dhidi ya wale wanaotumia vibaya fedha za umma. Tunakosa muunganiko kati ya matamanio yetu ya kupunguza rushwa na kuongeza uwajibikaji, na kutokuwa tayari kutumia adhabu kali kufikia malengo hayo. Kinachotakiwa ni uongozi imara katika ngazi zote kuhakikisha kuwa mifumo ya uwajibikaji inafanya kazi kwa ufanisi, na kuelimisha umma kwa ujumla na wale walio madarakani juu ya taratibu na njia za kushinikiza uwajibikaji.”

IAA launches new campus in Mwanza City

0
0
 Mwanza acting regional commissioner Baraka Konisaga (C) cuts a ribbon to launch the new campus for Institute of Accountancy Arusha (IAA) in Buzuruga area, Nyamagana District, Mwanza Region over the weekend. Looking from Right is IAA rector Prof Johannes Monyo and from Left is IAA Governing Board Rukia Adamu.
 Institute of Accountancy Arusha (IAA) rector, Prof Johannes Monyo speaks with reporters shortly after the institute launches their new campus in Mwanza.
 A traditional dancer intertaining guests when the Institute of Accountancy Arusha (IAA) launches new campus in Buzuruga area, Nyamagana District, Mwanza Region over the weekend.
Mwanza acting regional commissioner Baraka Konisaga (C) shake hands with IAA governing board members after arriving at IAA new campus in Buzuruga area, Nyamagana District, Mwanza Region over the weekend. First from Left is IAA's Deputy Rector, Academics, Research and Consultacy, Dr Faraji Kasidi.

========  =======  =========

The Institute of Accountancy Arusha (IAA) has opened a new campus at Buzuruga area, Nyamagana District in Mwanza Region with the aim of reaching a one third of Tanzania’s population living in the Lake Zone.

Already the IAA has established a campus building at Quality Plaza along Nyerere Road in Dar-es-Salaam City and Babati in Manyara.
The Institute has grown from offering full time certificates to undergraduates, postgraduate and Masters programmes.

Speaking at the launch of the campus over the weekend, Mwanza acting Regional Commissioner Baraka Konisaga said the government will continue to invest in the construction of schools and higher learning institutions that’s why the region has provided a plot for the IAA to establish a campus.

Konisaga also called on the accountancy institute to speed up the establishment of more branches countrywide in a move to produce more accountants who will help in developing the economy. 

He also said that the government will continue to cooperate with various universities and higher learning institutions in improving Tanzanian education, a move that will see more graduates compete in local and international markets.

He said the establishment of IAA Mwanza campus will help many people from Lake Zone and neighbouring countries to use the college to train in various fields provided by the institution.

“Mwanza community commends IAA for establishing their campus in the region. We urge them to provide all courses that are offered by the institution because Mwanza is largest region after Dar es Salaam, therefore, many youths need educational services,” he said.

Chairperson of the IAA Governing Board Rukia Adamu said that their goal of opening a branch in Mwanza is due to the high number of students enrolling into IAA main campus, and is part of their 2012-2017 strategic plans, which is to establish two campuses.

“By opening Mwanza campus, we have achieved our five year-goal which is to establish two campuses that we have introduced before the target year,” she said.

She pointed that post graduate courses in Mwanza campus will begin in March. She named some courses that will be offered at the campus as Postgraduate Diploma in Accountancy, Postgraduate Diploma in Banking and Finance, Postgraduate Diploma in Banking and Finance, Postgraduate Diploma in Procurement and Supplies Management, Postgraduate Diploma in Financial Management.

Others are Master’s in Information Security, Master’s in Information Security, Masters in Software Engineering, MBA in Logistics Management, Information Technology Management, MSc- Finance and Investment, and MBA in Procurement and Supplies Management.

For his part, IAA rector Prof Johannes Monyo said that after successful launching of Mwanza campus, the institute plans to fulfill other goals that are within their five year strategic plan that started in 2012 and ends in 2017.

“We thank Mwanza regional authorities for providing us with land for setting up this institute. We promise to provide all required courses as agreed by our governing board of directors,” he said.

Prof Monyo also said that with good collaboration with Galgotius University in India, people in Mwanza and Lake Zone will get an opportunity to learn Masters of Science in Software Engineering, Computer Application and Masters of Science in Information Security. 

“We are also teaming up with Coventry University to ensure our students access different courses offered outside the country, at affordable fees. Therefore, some courses offered by Coventry University will also be included in our curriculum,” he said. 

He added: “Some officials from Coventry University will be here any time from now to give us a go ahead on providing their courses. This follows an inspection of our campus which they carried out a few months ago to see whether our environment is conducive for providing some courses and they were satisfied,” he said.

Prof Monyo went on to say that teaming up with Coventry University would add quality to their education since the latter is recognised as a ‘modern university in UK’, an award it received two years ago. 

He further noted that moving closer to the community would help many parents to afford paying for their students because they would study near their homes.

“Our mission is to provide high quality education in all fields of management, science and social sciences, with significant focus on accountancy. We will use technology to ensure that the Institute’s graduates are competitive in the global job market,” he said.

The Institute of Accountancy Arusha (IAA) is a parastatal educational institution established by the Institute of Accountancy Arusha Act of 1990. The overall control and supervision of the Institute is vested in its Governing Council.
 

Mhadhiri wa chuo kikuu Mzumbe awataka maafisa ugavi na manunuzi nchini kuzingatia ubora na viwango

0
0
TA1
TA2
Mkuu wa Idara ya Cartels (Makubaliano yanayodhirisha ushindani) kutoka Tume ya Ushindani Dar es Salaam,Shedrack Nkelebe akisisitiza jambo kwenye semina hiyo iliyohusisha wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa.
TA3
wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali nchini wakifuatilia semina ya juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA4
Wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali nchini wakifuatilia semina ya juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA5
Washiriki wa semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja leo iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA6
Washiriki wa semina hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja leo iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa
TA7
Bi Martha Mapalala kutoka mmoja wa waratibu wa semina hiyo inayofanyika mkoani Tanga.
...................................................................................
NA MWANDISHI WETU,TANGA MAAFISA Ugavi nchini wametakiwa kuzingatia ubora wa vitu vinavyonunuliwa kwenye maeneo yao jambo ambalo litapelekea kuondoka bidhaa feki kwenye soko.

Wito huo ulitolewa leo na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Noel Mrope wakati wa semina ya wataalamu wa manunuzi na ugavi kutoka taasisi mbalimbali juu ya manunuzi yanayozingatia thamani (Value for Money) iliyofanyika kwenye hotel ya Tanga Beach Resort mjini hapa.

Semina hiyo ilikuwa na lengo la kuwajengea uwezo maafisa hao juu yaumuhimu wa kufanya manunuzi yanayozingatia thamani halisi ya fedhailiyoendeshwa na bodi ya taaluma ya manunuzi na ugavi nchini (PSPTB).

“Pamoja na kuzingatia sheria za Manunuzi lakini kwa kinachonunuliwakuanzia fedha zilizotumika kwenye manunuzi kwa sababu hali hii itawezesha kuondoa uwepo wa bidhaa feki zinazosambazwa kwenye masoko “Alisema Mdhahiri huyo.

Aidha alisema kuwa mambo ya muhimu yaliyotiliwa mkazo kwenye seminahiyo ni namna ya wataalamu hao kuangalia thamani ya kitu na jinsi ganikinaweza kutumika katika kupandisha thamani yake na ubora ili mwisho wa siku watu wengi waweze kukitumia kitu hicho. “Katika jambo hili lazima wataalamu wa manunuzi kuhakikisha kwa pamoja wanafuata taratibu za manunuzi kwa kuzingatia sheria lengo likiwa kuona uthamani na ubora wa kitu ikiwemo thamani ya fedha halisi iliyotumika “Alisema.

Alisema kuwa kuwa kimsingi maafisa hayo wanatakiwa wanapokwendakununua vitu wasikimbilie bei ya chini bali waangalie ubora na thamani ya kitu halisia ili kuweza kuzipa changamoto bidhaa zisizokuwa na kiwango kukosa soka na hatimaye kuondoka kwenye soko la ushindani.

Hata hiyo alisema kuwa wananchi wanapobaini kuna vitu vimefanyikakwenye Halmashauri yao chini ya kiwango wanapaswa kulalamika kupitiamaeneo husika ili kuweza kukabiliana na hali hiyo.

WAZIRI MKUU AZINDUA UANDIKISHAJI WAPIGA KURA KITAIFA

0
0

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezindua zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia mfumo wa Biometric Voter Registration (BVR) na kuwataka viongozi wa siasa wawahimize wanachama wao wajitokeze kwa wingi bila kujali tofauti za kiitikadi.

Ametoa wito huo leo mchana (Jumanne, Februari 24, 2015) wakati akizungumza na viongozi mbalimbali na wananchi waliofika kushuhudia uzinduzi huo uliofanyika kwenye kata ya Lumumba, Halmashauri ya Mji wa Makambako, mkoani Njombe.

“Ninawasihi viongozi wa siasa tuwahimize wanachama wetu waende kujiandikisha kwa wingi. Tuache kauli za kukatisha tamaa, tuache kauli za kejeli sababu zoezi hili ni jema na lina nia ya kuwawezesha Watanzania wote kutumia haki yao ya kupiga kura,” alisema.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwaomba Watanzania wenye vitambulisho vya uchaguzi vya zamani na wale wasio na vitambulisho wajitokeze kwa wingi kushiriki zoezi hilo.

“Wale waliokwishafikisha miaka 18, na wale ambao watatimiza miaka 18 ifikapo Oktoba, mwaka huu wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwa sababu wasipofanya hivyo hawataweza kupiga kura kama hawatajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,” aliongeza.

Akiwa uwanjani hapo, Waziri Mkuu alishuhudia uandikishaji wa wakazi watatu wa kata hiyo ambapo zoezi zima lilidumu kati ya dakika tatu na dakika tano. Kisha alikabidhi kadi kwa mpigakura wa kwanza kuandikishwa ambaye alitumia dakika tatu kamili.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema amefurahishwa na taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva kwamba zoezi la uandikishaji lililoanza jana katika mji wa Makambako lilizidi matarajio ya Tume ya kuandikisha wapigakura 1,850.


“Nimefarijika sana na taarifa ya Mwenyekiti... Mlianza na kata tisa zenye vituo 54 na mlitarajia kuandikisha watu 1,850 lakini badala yake mmepata watu 3,014. Hili limenipa faraja sana. Ninawapongeza sana kwa hatua hiyo,” alisema.

Mapema, akitoa taarifa kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu kufanya uzinduzi huo, Jaji Lubuva alisema ana imani wadau mbalimbali wataendelea kuhamasisha wananchi washiriki zoezi la uboreshaji daftari la wapiga kura. Alisema uboreshaji wa daftari hilo utafanyika kikanda na kwamba wamepanga kutumia siku saba kwa kila kituo huku akisisitiza kwamba hakuna mtu atakayebakizwa bila kuandikishwa wakati ameshafika kituoni.

Aliwataka watu wanaokwenda kujiandikisha wawe na vitambulisho vyao vya zamani vilivyotolewa na Tume ya taifa ya Uchaguzi kwani tayari vina taarifa zao kwa hiyo vitapunguza muda wa mtu kuandikishwa. “Kadi za Tume (NEC) au za NIDA kwa wale wachache ambao wanazo, wakija nazo zitapunguza muda wa uandikishai sababu zina taarifa kwenye kanzidata,” alisema.

Akitoa ufafanuzi kuhusu mfumo wa uandikishaji wa BVR, Jaji Lubuva alisema mfumo huo siyo sawa na mfumo wa upigaji kura wa kielektroniki (e-voting) kama ambavyo wengi wanadai bali mfumo huo unafanya kazi kwa kutumia alama muhimu za mpigakura.

“Mfumo huu unatumia alama zaidi kwanza ikiwa ni picha na zaidi ni macho ya mhusika, pili ni alama za vidole na tatu ni saini ya mhusika. Mfumo huu unaweza pia kuchukua alama za mtu mwenye ulemavu wa kuona ama ulemavu wa mikono,” alisema.

Alisema uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura ni hatua ya kisheria na kwamba Tume itajitahidi kuhakikisha inafuata hatua zote wakati wa zoezi hilo.

Waziri Mkuu ameondoka Makambako na anaelekea Mbeya kuanza ziara ya kikazi ya siku sita kukagua shughuli za maendeleo katika mkoa huo.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, FEBRUARI 24, 2015.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA CCM

0
0


Wizara yatangaza utoaji ruzuku awamu ya pili

0
0


 Katika picha ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava.

Wizara yatangaza utoaji ruzuku awamu ya pili

ØNi ya wachimbaji wadogo madini

ØBRN kupima utekelezaji, tathmini



Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam

Matokeo ya utekelezaji wa utoaji wa ruzuku kwa wachimbaji Madini wadogo nchini Awamu ya Pili yanatarajiwa kufanyiwa tathmini na ufuatiliaji kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).


Hayo yamebainishwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava wakati akiongea katika Kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa kupitia Televisheni ya Taifa TBC1 mapema leo, ambapo amefafanua kuhusu taratibu za maombi ya namna ya kupata ruzuku kwa wachimbaji wadogo wa madini Awamu ya Pili.


Mhandisi Mwihava ameeleza kuwa, ili kupata matokeo bora ya namna ruzuku hiyo itakavyotumiwa na wachimbaji wadogo watakaokidhi vigezo vya maombi na kunufaika na ruzuku hiyo, mpango wa BRN utatumika ipasavyo kuhakikisha kwamba fedha hizo zinatumika kama ilivyopangwa.

“BRN itatumika kufuatilia utekelezaji wa ruzuku. Wizarani tuna Sehemu ya Ukaguzi wa Migodi, lakini pia tuna Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), hawa wote watashirikiana kufanya tathmini yenye matokeo tunayotarajia,” amesisitiza Mhandisi Mwihava.



Ameongeza kuwa, kiwango cha ruzuku kwa wachimbaji wadogo Awamu ya Pili kimeongezwa kufikia Dola za Marekani 100,000/-, ruzuku ambayo inalenga katika kuendeleza uchimbaji mdogo ili uwe na tija; kuwakwamua wachimbaji wadogo kiuchumi na kuongeza pato la taifa.


Aidha, ameeleza kuwa malengo mengine ya ruzuku hiyo kwa wachimbaji wadogo wa Madini kuwa ni kuendeleza mkakati wa kurasimisha shughuli za uchimbaji mdogo wa madini na kutoa mitaji ili kusaidia ukuaji wa tasnia ya uchimbaji mdogo wa madini.Malengo mengine ni pamoja na uongezaji thamani ya madini wenye Matokeo Makubwa Sasa.


Ameongeza kuwa, Serikali imedhamiria kuwasaidia wachimbaji wadogo nchini kuwawezesha kuwa wachimbaji wa kati, jambo ambalo limefanya Serikali kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika utoaji ruzuku na mikopo awamu ya kwanza.


“Tunataka kuwasaidia mitaji, kuwapatia vifaa na kuhakikisha wanapata uelewa wa namna ya kufanikisha shughuli zao kupitia wataalamu wetu. Tunalenga kuwafanya wakue hadi kuwa wachimbaji wakubwa”, ameongeza Mwihava.


Aidha, Mhandisi Mwihava ametumia fursa hiyo kuwataka wachimbaji wadogo kuzitumia ofisi za madini zilizoko mikoani kwa ajili ya kuchukua fomu za maombi kuanzia tarehe 2 Machi na kuwataka kuzirejesha fomu hizo katika ofisi hizo ifikapo tarehe 27 Machi, 2015, zikiwa na viambatanisho vyake.


Katika hatua nyingine, Mhandisi Mwihava amesema kuwa, migodi inayoshirikisha watoto wadogo katika shughuli za uchimbaji madini watanyanga’nywa leseni zao endapo itabainika kuwa, migodi hiyo inawashirikisha watoto, na hivyo kuwataka wachimbaji kufuata sheria na taratibu.


“Watoto kushiriki katika shughuli za uchimbaji ni makosa. Watakaobainika watanyang’anywa leseni zao. Wizara inapinga si haki kwa watoto kufanya shughuli za uchimbaji madini”, alisisitiza Mwihava.


Awamu ya pili ya utoaji ruzuku kwa wachimbaji wadogo nchini, inatekelezwa kupitia Wizara ya Nishati na Madini, chini ya Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP), unaopata fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia.

SHIRIKA LA SPECSAVER LA NORWAY LITATOA HUDUMA YA UPIMAJI WA MACHO NA KUTOA DAWA KWA WANANCHI WA ZANZIBAR BILA MALIPO KATIKA SKULI YA KIEMBESAMAKI

0
0
 Naibu Waziri wa Afya  Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na wandishi wa habari kuhusu  ujio wa madaktari wa Shirika la Specsaver la Norway ambao watatoa huduma ya macho bila malipo kwa kushirikiana na wataalamu wazalendo wa Zanzibar katika skuli ya Kiembesamaki.
  Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo (hayupo pichani)  katika mkutano huo uliofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja Zanzibar. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).
Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akijibu masuala ya waandishi wa habari kuhusiana na kuwasili madaktari wa Shirika la Specsaver ambao watafanya uchunguzi wa macho kwa muda wa siku tano katika Skuli ya  sekondari ya Kiembesamaki, (kulia) Mkuu wa kitengo cha macho Zanzibar Dkt. Slim Mohammed Mgeni.

ZIARA YA WAZIRI WA HABARI BUNGI ZANZIBAR

0
0
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar Mhe. Said Ali Mbarouk akikagua Jenereta linalotarajiwa kutumika pindi umeme utakapokosekana kituoni hapo.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar Mhe. Said Ali Mbarouk akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali mara baada ya kumaliza ziara yake kituoni hapo.
Aliyenyoosha mkono ni Mkurenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) Nd. Hassan Abdalla Mitawi akitoa maelezo kwa Waziri wa Habari Zanzibar. 
 Ni Mnara wa kurushia matangazo wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) ulioko Bungi Wilaya ya Kati Unguja. (Picha na Miza Othman Maelezo-Zanzibar).
 Ni chumba chenye mitambo ya kurushia matangazo (Transmitter) kilichopo katika Kituo cha Bungi Unguja.
 Wa kwanza kulia ni fundi mkuu wa kituo hicho Nd. Ali Aboud Talib akitoa maelezo ya kiufundi kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar Mhe. Said Ali Mbarouk wa kushoto. (Picha na Miza Othman Maelezo-Zanzibar).

Na Abdulla Ali Maelezo-Zanzibar                                  


Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar Mhe. Said Ali Mbarouk amesema zaidi ya shilingi milioni 100 za Kitanzania  zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa kituo kipya cha kurushia matangazo cha Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC). 

Hayo ameyasema wakati wa ziara yake ya kutembelea kituo hicho kilichopo Bungi Wilaya ya Kati Unguja.

Amesema lengo la ziara hiyo ni kuangalia ufanisi wa kazi kwa watendaji wa kituo hicho na kusisitiza kuwa ni jukumu la Wizara kufanya hivyo ili kuimarisha dhana ya uwajibikaji kwa watendaji wake.

Amesema kwa sasa Serikali inaweza kuendesha mitambo ya kurushia matangazo iliyopo kituoni hapo bila ya kutegemea mafundi kutoka nje ya Nchi kama vile China kwani ina mafundi wa kutosha wenye uweledi katika fani ya uhandisi wa mitambo ya Redio na Televisheni.

Aidha ametanabahisha kuwa Serikali ina jukumu la kuwaongezea ujuzi baadhi ya mafundi hao kwa kuwapeleka kusoma nje ya Nchi ili waende sambamba  na mabadiliko ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya Umma.

Waziri huyo amewataka mafundi wa kituo hicho kurekebisha matatizo madogo madogo yaliyopo kituoni hapo ikiwemo kufunga mafeni pamoja na viyoyozi (Air Condition) ili kuzifanya mashine hizo zidumu kwa muda mrefu na kupunguza hasara ya kuungua mara kwa mara kutokana na joto kali linakuwemo katika vyumba hivyo vya kurushia matangazo.

Waziri Mbarouk amewataka wafanyakazi kuwa wabunifu katika utendaji wao wa kazi na kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa lengo la kuliimarisha shirika hilo kwani matangazo yake ni muhimu ndani na nje ya Nchi ikiwemo mwambao wa Kenya ambao wanategemea kwa kiasi kikubwa matangazo ya ZBC.

Nae fundi mkuu wa kituo hicho Nd. Ali Aboud Talib amesema wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uchakavu wa  nyaya za kurushia matangazo (Cable) kutokana na kutumika kwa muda mrefu, kuwepo kwa msitu mkubwa kutokana na kukosekana kwa wafanyakazi wa kusafisha eneo hilo.

Vilevile amesema tatizo la usafiri ni usumbufu mkubwa kwao kwani hadi sasa kituo hicho kina gari moja ambayo haitoshelezi kwa kazi za kila siku pamoja na Taa za Mnara wa kurushia matangazo kuwa haziwaki.

Aidha amesema mashine za kurushia matangazo (Transmitter) hazina uwezo mkubwa ukilinganisha na vyomo vyengine vya habari vilivyopo Nchini kwani hadi sasa ZBC inatumia mashine yenye uwezo wa masafa ya 1 kilowatts ambapo vyombo vyengine vinatumia mashine zenye uwezo wa masafa hadi 4 kilowatts.

Fundi huyo amewataka wananchi kuwa wazalendo kwa kuangalia Televisheni yao ya nyumbani (ZBC) ili kuipa thamani ndani na nje ya Nchi jirani kwa kuwa na watazamaji wengi.
 

      IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.
 


WARSHA KUHUSU NAFASI YA VYOMBO VYA HABARI KATIKA KUZUIA UKATILI DHIDI YA WATOTO NCHINI TANZANIA YAFUNGULIWA LEO KILIMANJARO

0
0
 
 Julieth Swai Mwakilishi kutoka UNICEF akizungumza jambo
 Baadhi ya washiriki wa Warsha wakifuatilia kwa makini
 Mmoja wa  washiriki wakiuliza maswali katika warsha hiyo.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa ushirikiano na UNICEF wameandaa warsha ya siku tatu inayohusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuzuia ukatili dhidi ya watoto nchini Tanzania.

Warsha hiyo inayofanyika mjini Moshi inashirikisha wawakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Wawakilishi kutoka Mkoa wa Kilimanjaro, Wawakilishi kutoka wilaya za Hai na Moshi Manispaa, wawakilishi kutoka UNICEF pamoja na wawakilishi wa redio 14 zinazorusha kipindi cha Walinde Watoto.

Wengine ni wawakilishi kutoka Baraza la Habari Tanzania, mwakilishi kutoka Csema pamoja na waandaaji wa kipindi cha Walinde Watoto kampuni ya True Vision Production.

Akifungua warsha hiyo, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Kilimanjaro, Paul Shayo alilishukuru shirika la Watoto Duniani (UNICEF) kwa kazi nzuri ambazo wamekuwa wakizifanya kwa kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha kuwa Haki za Watoto zinatekelezwa hapa nchini. 


Paul alitaja aina za ukiukwaji wa haki za mtoto hapa nchini kuwa ni pamoja na kuolewa katika umri mdogo, kutumikishwa katika mashamba na ukatili dhidi ya watoto. Hata hivyo aliendelea kuzitaja athari mbalimbali zinazotokana na ukiukwaji wa haki hizo kuwa ni pamoja na watoto kukatishwa masomo na kukosa haki ya kuendelezwa na kwamba ndoa za utotoni zina madhara kiafya hasa wanapopata ujauzito na kujifungua katika umri mdogo. 

Paul alimalizia kwa kutoa rai kwa washiriki wa warsha hiyo na kuwataka wakawe chachu ya kuzuia ukatili dhidi ya watoto katika maeneo waliyotoka na kushirikiana na wadau waliopo katika ngazi za vijijini, mikoani na mijini kadri inavyowezekana ili kuwalinda watoto na kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.

Vipindi vya Walinde Watoto vinarushwa na redio 14 ambazo ni Radio Jamii Kilosa, Country FM, Boma Hai FM, Radio Quran, ZBC pamoja na Redio Kitulo.

Nyingine ni TBC Taifa, Bomba FM, Faraja FM, Uplands FM, Ice Fm, Radio Maria, Radio Kwizera na Zenj FM. Vipindi hivi vinapatikana pia katika tovuti ya www.walindewatoto.org na kupitia www.facebook.com/WalindeWatoto




 Kimela Bila Mwandaaji wa Kipindi cha Walinde Watoto akizungumza katika Warsha hiyo
 Mathias Haule, Afisa Maendeleo ya Jamii maswala ya Ukatili dhidi ya Watoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto akielezea Sheria ya Mtoto
 Neema Kimaro, Mratibu wa kipindi cha Walinde Watoto kutoka True Vision Production akiendelea na maandalizi ya warsha
Rose Minja, Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya familia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,
akijibu maswali ya washiriki wa Warsha inayohusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuzuia ukatili
dhidi ya Watoto nchini Tanzania
 Wawakilishi kutoka redio 14 zinazorusha kipindi cha Walinde watoto

 Washiriki wa Warsha inayohusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuzuia ukatili dhidi ya watoto nchini Tanzania
***

RAIS KIKWETE AKAGUA UJENZI WA MAABARA,APOKEA NA KUGAWA VITABU VYA SAYANSI SHULE YA SEKONDARI MTAKUJA VILIVYOCHAPISHWA NA WATU WA MAREKANI

0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua maabara katika Shule ya  Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani. Wa kwanza kulia ni Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi, akifuatiwa na mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akipokea baadhi ya vitbu vya sayansi toka kwa  Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Vitabu hivyo ambavyo vimesambazwa katika shule zote za serikali nchi nzima vimechapishwa kwa msaada wa Watu wa Marekani.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma kikwete, Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,na viongozi wengine wakiangalia jinsi somo la sayansi likifundishwa katika darasa la Kidatu cha pili Shule ya
Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma kikwete, Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,na viongozi wengine wakisalimia wanafunzi katika   darasa la Kidatu cha pili Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko
Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa na Watu wa Marekani
 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, wakiongea na mkandarasi wa maabara ya  Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako  pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyotolewa na Watu wa Marekani
  Rais  Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete  na Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress wakiwa na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam wakiwa na vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani

  Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam wakiimba kwa furaha katika sherehe ya kukabidhiwa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani
  Kikundi cha utamaduni cha jeshi la polisi kikitumbuiza katika sherehe ya kukabidhiwa vitabu vya sayansi vilivyotolewa na Watu wa Marekani
 Baadhi ya maafisa wa ubalozi wa Marekani wakiwa katika katika sherehe ya kukabidhiwa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani
 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akipokea baadhi ya vitbu vya sayansi toka kwa  Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Vitabu hivyo ambavyo vimesambazwa katika shule zote za serikali nchi nzima vimechapishwa kwa msaada wa Watu wa Marekani.
 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na  Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress akigawa vitabu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja ya Kunduchi jijini Dar es salaam. Vitabu hivyo, ambavyo pia vimesambazwa katika shule zote za serikali nchi nzima vimechapishwa
kwa msaada wa Watu wa Marekani.
  Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na  Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress katika picha na baadhi ya  wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja ya Kunduchi jijini Dar es salaam baada ya kuwagawia vitbu vya sayansi. Vitabu hivyo, ambavyo pia vimesambazwa katika shule zote za serikali nchi nzima vimechapishwa kwa msaada wa Watu wa Marekani.
 Mwanafunzi wa Kidatu cha pili D, Khairat Nassor, akitoa ushuhuda wa jinsi wanafunzi walivyokuwa na nafuu baada ya kupatikana vitabu vya sayansi katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja ya Kunduchi jijini Dar es salaam. Vitabu hivyo, ambavyo pia vimesambazwa katika shule zote za
serikali nchi nzima vimechapishwa kwa msaada wa Watu wa Marekani.
Mama Salma Kikwete akiagana na walimu wenzake baada ya sherehe za kukabidhi vitabu vya sayansi. katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja ya Kunduchi jijini Dar es salaam. Vitabu hivyo, ambavyo pia vimesambazwa katika shule zote za serikali nchi nzima vimechapishwa
kwa msaada wa Watu wa Marekani. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Paul Makonda baada ya kuwasili katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam leo tayari kwa kukagua ujenzi wa maabara na pia kupokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa  na Watu wa Marekani.
. PICHA NA IKULU
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live




Latest Images