Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

Wafanyakazi wa African Barrick Gold watoa msaada kwa wagonjwa wa saratani

$
0
0
Wafanyakazi wa kampuni ya uchimbaji madini ya African Barrick Gold (ABG) wakiongozwa na afisa wa kampuni hiyo, Blandina Munghezi (wa pili kushoto), wakikabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali yakiwemo maboksi ya sabuni za kufulia na kuogea, mafuta ya kula, jozi za khanga na vitenge kwa Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI), Sophia Kissuda Lesso, kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa wanawake waliolazwa katika taasisi hiyo, jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni shemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.
Wafanyakazi wa kampuni ya uchimbaji madini ya African Barrick Gold (ABG) wakikabidhi msaada wa vitu mbalimbali yakiwemo maboksi ya sabuni za kufulia na kuogea, mafuta ya kula, jozi za khanga na vitenge kwa wagonjwa waliolazwa kwenye Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) iliyopo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni shemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. 
Wafanyakazi wa kampuni ya uchimbaji madini ya African Barrick Gold (ABG) wakikabidhi msaada wa vitu mbalimbali yakiwemo maboksi ya sabuni za kufulia na kuogea, mafuta ya kula, jozi za khanga na vitenge kwa wagonjwa waliolazwa kwenye Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) iliyopo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni shemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. 
Wafanyakazi wa kampuni ya uchimbaji madini ya African Barrick Gold (ABG) wakikabidhi msaada wa vitu mbalimbali yakiwemo maboksi ya sabuni za kufulia na kuogea, mafuta ya kula, jozi za khanga na vitenge kwa wagonjwa waliolazwa kwenye Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) iliyopo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni shemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani. 

RAIS KIKWETE AMTEMBELEA MZEE YUSUF MZIMBA ALIYELAZWA MUHIMBILI KWA KUGONGWA NA BODABODA

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali na kumpa pole Mzee Yusuf Mzimba, mmoja wa wazee marufu wa Klabu ya Dar es salaam Young Africans (YANGA) ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akiuguza majeraha kufuatia kugongwa na BodaBoda wiki iliyopita Barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam. Mzee Mzimba amevunjika mguu wa kushoto na kupata majeraha ya usoni na mikononi. Hadi jana hali yake ilikuwa inaendelea vyema na Rais Kikwete amempa pole nyingi kwa maumivu aliyoyapata na kumtakia apate nafuu ya haraka. PICHA NA IKULU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, leo Jumapili Machi 10, 2013 amemtembelea Mzee Yusuf Mzimba, mmoja wa wazee wa Klabu ya Dar es salaam Young Africans (YANGA), ambaye amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam, akiuguza majeraha kadhaa kufuatia kugongwa na pikipiki maarufu kama 'Bodaboda' wiki iliyopita katika barabara ya Nyerere.

========  =======  ==========

Rais Kikwete, ambaye amewasili leo kutokea Afrika Kusini katika ziara ya kikazi ya siku tatu, amempa Mzee Mzimba pole na kumuombea apate nafuu ya haraka.

Katika ajali hiyo Mzee Mzimba amevunjika mguu wa kushoto na kupata majeraha madogo usoni na mikononi.

Kwa mujibu wa madaktari na wauguzi hali yake inaendelea vyema baada ya kutibiwa, ikiwa ni pamoja na kuvishwa Plaster of Paris (Piopio).

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
10 Machi, 2013

Wanyarwanda waja kutumbuiza Pasaka Dar

$
0
0
 IDADI ya wasanii wa nje watakaokuja kutumbuiza kwneye Tamasha la Pasaka mwaka huu imezidi kuongezeka na sasa Wanyarwanda nao wamethibitisha kushiriki.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema jana kuwa kwaya ya Ambassadors of Christ ya Kigali Rwanda inayotamba na albamu ya Mtegemee Yesu imethibitisha kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Machi 31 mwaka huu jijini Dar es Salaam. “Watakuja kung’arisha tamasha la mwaka huu na wamejipanga vya kutosha kuhakikisha mashabiki wanapata burudani ya nguvu, nia yetu ni kuwa na wasanii wakubwa Afrika na hilo ndilo tutakalolifanya mwaka huu.

“Kabla ya Jumatano tutatangaza msanii mkubwa mwingine ambaye bado tunaendelea na mazungumzo naye kuhakikisha mambo yanakuwa safi, ili aje kutumbuiza kwenye tamasha letu,” alisema Msama. Alieleza kuwa katika albamu yao hiyo ina nyimbo nane ambazo ni JY’ Ushima Uwite, Mtegee Yesu, Ndifuza Kugerayo, Iyana Iby’ Isi, Yesu Niwe Mungeri, Parapanda, Abasaruzi na Nenda.

Wasanii wengine wa nje ya Tanzania ambao tayari wamethibitisha kushiriki tamasha hili ni , Ephraim Sekeleti wa Zambia na Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya. Wasanii wa Tanzania ni Rose Muhando, Upendo Nkone na John Lissu.

Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31 na  litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.


hatimaye mshindi wa droo ya kwanza ya Ascend Y200 aenda china

$
0
0

 .Mshindi wa droo ya Ascend Y200 ya mwaka jana bw. Christian Evarist Mkama akiongea na waandishi wa habari uwanja wa ndege wa kimataifa JK Nyerere kabla ya safari kuelekea nchini China. 
.Mshindi wa droo ya Ascend Y200 ya mwaka jana bw. Christian Evarist Mkama akiwa na mama mzazi bi. Eva Christian Amuko na mjomba wake bw. Fortunatus Christian Amuko uwanja wa ndege JK Nyerere kabla ya safari kuelekea nchini China

Tigo Tanzania imempeleka bw. Christian Evarist Mkama nchini China ambaye ni mmoja kati ya washindi wawili wa droo ya kwanza ya Ascend Y200 ambayo ilifanyika mwaka jana tarehe 19 Desemba.
 
Kwa kuwa mshindi wa droo hii amejishindia tiketi ya bure ya kwenda na kurudi nchini China pamoja na kulipiwa gharama zote za safari,chakula na dola 200 kwa siku za matumizi.
 
Akiwa nchini china mshindi huyu atakaa siku nne na atatembezwa na kuonyeshwa sehemu mbalimbali za mji wa Guangzhou, na kupelekwa kwenye sehemu za utalii ya mlima Lotus.
 
Promosheni ya AscendY200 ilizinduliwa mwaka jana 2012 mwezi wa kumi(oktoba) kwa jumla kutakuwa na droo tano za Ascend Y200 na kila droo itakuwa na washindi wawili kwa jumla ya washindi kumi watapatikana kwenye droo hizi.
 
Kushiriki kwenye shindano hili mteja wa Tigo inambidi awe amenunua simu ya Ascend Y200 kwenye maduka ya Tigo yaliyosajiliwa na kujisajili kwenye kifurushi cha A-Smart package

Mh. Lowassa aongoza harambee ya kuchangia miradi ya maendeleo Wilayani Butiama

$
0
0

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza machache kabla ya kuanza harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara chini ya usimamizi wa Padri Wojciech Adam (hayupo pichani) wa kanisa Katoliki la Kiabakari lililopo wilayani humo,Hafla hii ilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere akizungumza machache wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara chini ya Padri Wojciech Adam wa kanisa Katoliki la Kiabakari,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.ambapo Mgeni Rasmi katika harambee hiyo,alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Padri Wojciech Adam wa kanisa Katoliki la Kiabakari akitoa historia fupi ya mradi huo toka kuanza kwake mpaka walipofikia wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.ambapo Mgeni Rasmi katika harambee hiyo,alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini,Mh. Nimrod Mkono akizungumza machache wakati wa kukabidhi mchango wake na kuahidi kuendelea kuchangia ili kuhakikisha ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara inafanikiwa huku akisikilizwa kwa makini na Mgeni Rasmi wa Harambee hiyo,Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa pamoja na Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini,Mh. Nimrod Mkono akikabidhi mchango wake kwa Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere huku akisaidiwa na Mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo,Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
 Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara,iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media,Ansbert Ngurumo ampa mkono Mama Maria Nyerere mara baada ya kutoa ahadi yake ya kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo katika wilaya ya Butiama mkoa wa Mara.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimkabidhi picha Boss Mkuu wa Mgahawa wa BreakPoint mara baada ya kununua kwenye mnada aliouendesha yeye mwenyewe.Katikati ni Mke wa Baba wa Taifa,Mama Maria Nyerere.

" Only if Ezinma was a boy! ( Chinua Achebe, Things Fall Apart) .

$
0
0



Ndugu zangu,



Leo ni siku yangu ya kuzaliwa. Nawashukuru wote mlionitumia salamu za kunitakia heri, pia nyote mnaoendelea kunitakia heri. Ahsanteni sana.

Wahenga walisema; Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Nitasimulia kidogo ya utoto wangu; Wazazi wangu wamechangia sana kunifanya niwe hivi nilivyo sasa. Kwa baba yangu, watoto wote tulikuwa sawa, hata dada zangu walikuwa muhimu kwake.

Tofauti na Okwonkwo kwenye Things Fall Apart ambaye hakuridhika kwa kumpata mwana aitwaye Nwoye ambaye alifanana kitabia na baba yake Okonkwo. Huyu Okonkwo hakumpenda baba yake, Unoka. Na binti yake Ezinma alikuwa na sifa ya uhodari , mweye akili sana pia. Hata hivyo, Okwonkwo hakufurahia, maana alikuwa msichana!

Ndio, nimekuwa hivi nilivyo kutokana na malezi niliyoyapata pia. Mathalan, mama yangu alifanya kazi Idara ya Kupiga Chapa ya Serikali- Government Press. Alifahamu haraka yale niliyoyapenda tangu utotoni. 

Ni picha na machapisho. Hivyo, kila aliporudi kutoka kazini aliniletea picha na baadae hata vitabu vya machapisho. Si ajabu kuwa nimekuwa mwandishi na mpiga picha pia.

Nilijua kusoma na kuandika hata kabla sijaanza darasa la kwanza.
Na ilifika mahali mama aliniletea hata vitabu vya bajeti za Wizara kabla ya hata kusomwa Bungeni. Lakini alinisisitiza, kuwa nisiwaambie watu wengine nilichosoma mpaka kiwasilishwe Bungeni kwanza!

Niwachekeshe, sikulijua jina langu ' Maggid' mpaka nilikaribia kuanza darasa la kwanza. Maana, nilipozaliwa, Machi 11, 1966 ndugu walikuja kumwona mtoto ( Mimi). Na dada wa mama ( Mama mkubwa) aliniangalia na kutamka; " Huyu ni Mjengwa". Kwamba nilifanana sana na baba yangu.

Tangu hapo nikaitwa ' Mjengwa'. Lakini jina rasmi kwenye cheti changu cha kuzaliwa ni ' Maggid'. Maana, baba yangu, pamoja na kuwa alikuwa ni Mkristo kwa jina la ' John Mjengwa) alikuwa na mfanyakazi mwenzake, rafiki yake wa karibu sana raia wa Misri. 

Nilipozaliwa mimi alimjulisha rafiki yake; " I have got a baby boy!"
Naye akamwambia; " Call him Maggid!" Basi, ikawa hivyo.

Ikafika wakati nikamwuliza baba yangu; " Nakaribia kuanza shule, sasa shuleni nitaitwa 'Mjengwa Mjengwa'. Baba akaniangalia na kunijibu akitabasamu; " Wewe jina lako ni Maggid!".

Hakika, hata nilipoanza darasa la kwanza, wenzangu darasani walinishangaa sana, maana, kila mwalimu alipoita jina langu, ilinichukua sekunde kadhaa kabla ya kujibu ' Nipo!'. Sikulizoea jina hilo. Leo napenda zaidi kuitwa ' Maggid' kuliko ' Mjengwa'! Na shuleni kila siku ya ukaguzi sikupona. Nilichapwa bakora kwa vile nilikuwa na nywele za kipilipili!

Kubwa kabisa ni kuwa, nimelelewa katika mazingira ya kuheshimu wanadamu wenzangu bila kujali tofauti zetu; iwe za kidini au kikabila. Hata wazazi wangu walikuwa wa imani tofauti; Uislamu na Ukristo. Na pale Ilala nilikokulia watoto wote tulicheza pamoja bila kuziangalia tofauti zetu za kikabila na kidini. Tulichanganyika. 

Hata hii leo, huwa nasikitishwa sana na tabia za baadhi yetu kuendekeza tofauti zetu za kidini, kikabila na hata kirangi, badala ya kuangalia mambo ambayo wanadamu tunafanana nayo. Na ni mengi sana kuliko tofauti zetu.

Ahsanteni Sana.
Maggid,
Iringa

mashindano ya nyama choma ndani ya viwanja vya lidaz club jijini dar jana.

$
0
0
 Mdau akikata kiu na kitu bariiidi.








Mambo yazidi kunoga Tamasha la Pasaka

$
0
0

KWAYA ya Kinondoni Revival  (pichani juu) na kundi la Glorious Celebration ni miongoni mwa burudani zitakazokuwepo kwenye Tamasha la Pasaka Machi 31 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama jana ilieleza kuwa makundi hayo ya jijini Dar es Salaam tayari yamethibitisha ushiriki wao pamoja na mwimbaji mahiri Upendo Kilahiro ambaye pia atashiriki.

Niseme mambo yanaenda vizuri na leo (jana) kuna msanii tunamalizana naye kutoka Afrika Kusini, nina imani wakati wowote kuanzia Jumanne (leo) tutamtangaza kwa mashabiki wetu, nia ni kulifanya tamasha liwe zuri zaidi," ilisema taarifa hiyo.

Wasanii wengine wa Tanzania ambao watashiriki tamasha hilo mwaka huu ni Rose Muhando, John Lissu na Upendo Nkone, wakati wa nje ya Tanzania ni Ephraim Sekeleti wa Zambia anayetamba na albamu zake za Acha Kulia na Mungu Mwenyewe. 

Wasani wengine wa nje watakaokuja ni Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya, ambapo pia mwaka huu kuna ingizo jipya ambalo ni kwaya ya Ambassadors of Christ ya Kigali Rwanda inayotamba na albamu ya Mtegemee Yesu.
Kundi la Glorious Celebration likiwa kwenye moja ya kazi zake jukwaani.


Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31 na  litaendelea Aprili mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora Iringa na Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Tamasha la mwaka jana baadhi ya waimbaji mahiri waliokuwepo ni Rose Muhando, Rebecca Malope, Christina Shusho, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Solomon Mukubwa, Atosha Kissava, Ephraim Sekeleti, kundi la Glorious Celebration, kwaya ya Kinondoni Revival na Mwinjilisti Faraja Ntaboba kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Airtel yadhamini tuzo za Mwanamakuka 2013

$
0
0
 
Mshindi wa pili wa tuzo za Mwanamakuka bi  Leila Mwambungu  (katikati) akifurahi kwa pamoja  na Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde (kulia)  wakati wa kukabidhiwa   mfano wa hundi ya shillingi million tatu mara baada ya kuibuka mshindi wa pili wa  tuzo za mwanamakuka . Akishuhudia kushoto ni  Mke wa makamu wa raisi Asha Bilali na wa pili kushoto ni mwenyekiti  wa Unit of women Friends Esther Wakati.i
 Mwenyekiti wa Unit of women Friends Esther (kushoto)  akikabidhi Afisa uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde cheti cha shukrani kwa Airtel kushiriki na kudhamini tuzo za mwanamakuka kwa mwaka 2013. Akishuhudia ni mtunza fedha Mwate Madinda.
Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde(kulia) akikimkabithi mshindi wa pili wa mwanamakuka bi  Leila Mwambungu  mfano wa hundi ya shillingi million tatu mara baada ya kuibuka mshindi wa pili wa  tuzo za mwanamakuka . wakishuhudia  kulia katikati ni mwenyekiti  wa Unit of women Friends Esther Wakati, kushoto ni  msimamizi wa mwanamakuka award Maryam Shamo akifatiwa na Mke wa makamu wa raisi Asha Bilali.

 Balozi mstaafu bi Mwanaidi Maajar (katikati) akitoa mkono wa shukrani kwa  Afisa Uhusiano wa Airtel  bi Jane Matinde kuishukuru Airtel Tanzania kwa kudhamini tuzo za Mwanamakuka 2013. Wakishuhudia ni  Mke wa makamu wa raisi Asha Bilali na wa pili kushoto ni mwenyekiti  wa Unit of women Friends Esther Wakat

Waandaaji na wadhamini wa tuzo za mwanamakuka 2013 wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Mke wa makamu wa raisi Asha Bilali wakati wa sherehe za tuzo hizo

TIGO YAPELEKA CHINA WASHINDI wengine wawili WA DROO YA ‘ASCEND Y200’.

$
0
0
Pichani kulia ni Meneja Ubunifu wa Ofa za Kampuni ya Tigo,Bwa.David Sekwao akizungumza na mmoja wa washindi wa promosheni ya Ascend Y200 kwa njia ya simu iliyozinduliwa rasmi mnamo Oktoba 2012,inayomuwezesha mteja kununua samrtphone yenye kiwango na hadhi ya aina ya Ascend Y200 kwa punguzo la hali ya juu,Pichani kati ni Meneja wa Tigo,Bwa.William Mpinga na Muwakilishi kutoka michezo ya Bahati Nasibu nchini,Bwa.Bakari Maggid wakishuhudia tukio hilo lililofanyika leo kwenye hotel ya Holiday Inn,jijini Dar

Pichani kati ni Meneja wa kampuni ya Tigo,Bwa.William Mpinga  akifafanua kuwa kwa "Mara nyingine tena Tigo inaendelea kuweeka tabasamu katika nyuso za thamani za wateja wetu kwa kuwapa fursa ya kujifunza na kuonja tamaduni mpya.Tunayo furaha kwa mara ya pili kuwa na shindano letu la Promosheni yetu bomba ya ‘Ascend Y200’ na kutangaza washindi mbalimbali ambao wataondoka hivi karibuni Dar-es-salaam kwenda China. 

 Siyo kwamba tunabadilisha tu namna wateja wetu wanavyowasiliana kupitia aina hii mpya ya smartphone zenye ubora wa hali ya juu katika nyanja mbalimbali za mawasiliano,  bali pia tunabadilisha maisha ya Watanzania kwa kubadilisha uzoefu na kumbukumbu za maisha yao kwa kuwapatia bidhaa bora zenye thamani katika maisha yao yote.alisema Bw William Mpinga, Meneja wa Kampuni ya Tigo.






TIGO YAMPELEKA CHINA MSHINDI MWINGINE WA DROO YA ‘ASCEND Y200’..
Dar es Salaam Tanzania Machi 11, 2013:  Tigo Tanzania leo hii imetangaza Washindi wa awamu ya pili ya droo ya  ‘Ascend Y200’;

Simon Richard Simon (36) mkazi wa Ubungo, Dar-es-salaam na Frederick Wilfred Mgaya (24) mwanafunzi chuo Kikuu Kishiriki cha Tiba cha KCMU-Moshi na mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro; wamejishindia zawadi ya kugharamiwa na Tigo gharama zote za kutembela miji mikubwa nchini China.

Meneja Usanifu na Ofa wa kampuni ya Tigo Bw. David Sekwao alisema “Promosheni ya ‘Ascend Y200’ ilizinduliwa rasmi mnamo mwezi Oktoba mwaka 2012 kwa 2012 inayomuwezesha mteja kununua smartphone yenye kiwango na hadhi ya juu aina ya ‘Ascend Y200’ kwa punguzo la hali ya juu. Droo ya kwanza ya Promosheni ya ‘Ascend Y200’ ilifanyika mnamo Disemba 19, mwaka 2012, ambapo washindi wawili wenye bahati safari ya kutembelea miji mbalimbali mashuhuri nchini China zilizogharamiwa na Tigo. Kutakuwa na droo nyingine tano ambapo jumla ya washindi wawili watachaguliwa katika kila droo, na kufanya idadi yao kuwa jumla ya washindi kumi.”

Aliongeza kuwa, zawadi hiyo ya safari ya China kwa washindi hao itajumuisha, Malazi, posho ya chakula kwa siku 3 katika hoteli ya  Dragon Hotel iliyopo katika jiji la Guangzhou China, kutembelea vivutio mbalimbali kwa nusu siku jijini Guangzhou, mapumziko ya siku nzima katika milima ya Lotus nchini humo, pesa za matumizi binafsi kiasi cha Dola 200 za Kimarekani kwa kila mshindi pamoja na gharama zote za usafiri wa ndege.

Kigezo cha  kushiriki shindano la Promosheni ya ‘Ascend Y200’,  wateja wa Tigo wanatakiwa kununua smartphone yenye kiwango na hadhi ya juu aina ya ‘Ascend Y200’ kwa punguzo la hali ya juu katika duka lolote laTigo lililosajiliwa na kujiunga na pakeji ya A-Smart.

"Mara nyingine tena Tigo inaendelea kuweeka tabasamu katika nyuso za thamani za wateja wetu kwa kuwapa fursa ya kujifunza na kuonja tamaduni mpya.Tunayo furaha kwa mara ya pili kuwa na shindano letu la Promosheni yetu bomba ya ‘Ascend Y200’ na kutangaza washindi mbalimbali ambao wataondoka hivi karibuni Dar-es-salaam kwenda China. 

 Siyo kwamba tunabadilisha tu namna wateja wetu wanavyowasiliana kupitia aina hii mpya ya smartphone zenye ubora wa hali ya juu katika nyanja mbalimbali za mawasiliano,  bali pia tunabadilisha maisha ya Watanzania kwa kubadilisha uzoefu na kumbukumbu za maisha yao kwa kuwapatia bidhaa bora zenye thamani katika maisha yao yote.alisema Bw William Mpinga, Meneja wa Kampuni ya Tigo.


Mpinga aliendelea kufafanua kuwa, "Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wateja wetu wote wa Tigo kwa mchango  wao katika kukuza na kuendeleza promosheni hii na pia kuwaomba wale wote ambao bado hawajanunua smartphone yenye kiwango na hadhi ya juu aina ya ‘Ascend Y200’ kwa punguzo la hali ya juu kupata yao sasa, ili na wao waweze kupata nafasi ya kushinda safari ya kwenda China na kukamilisha furaha ya maisha yao.”

ZIARA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA WILAYANI NKASI PAMOJA NA SHEREHE ZA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

$
0
0
Godfrey Mwanansao Afisa Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi akitoa maelezo ya ubunifu wa kinyago kinachoonyesha baadhi ya michezo kwa kinamama kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa akikagua mabanda ya wadau wa siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa Wilayani Nkasi tarehe 08.03.2013. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo Iddi Kimanta.
Meneja wa PSI Mkoani Rukwa Issa Ismail akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya juu kazi za shirika hilo Mkoani Rukwa na katika maonyesho hayo. Kulia kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ni Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Kimanta, Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ramadhan Juma, Mbunge wa Nkasi Kaskazini CCM Ali Kesi na Kamanda wa Polisi Mkoani Rukwa Jakob Mwaruanda.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Samson Mashalla akijionea baadhi ya bidhaa zilizokuwa zikionyeshwa na kuuzwa katika mabanda hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akizungumza na wananchi katika viwanja vya sabasaba Mjini Namanyere katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani mwishoni mwa juma.

 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na wananchi Wilayani Nkasi katika maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani yaliyofanyika Wilayani humo kimkoa tarehe 08.03.2013. Aliwataka wanawake kuwa mstari wa mbele katika kujikwamua kiuchumi kwa kujishughulisha na shughuli za ujasiriamali na kujiunga kwenye vikundi vitakavyowawezesha kupata mikopo, aliwataka pia kuzingatia uzazi wa mpango katika kujiletea maendeleo yao wenyewe. 
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Kimanta akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nkasi katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa katika Wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akizungumza na wananchi wa Kata ya Wampembe kujibu kero zao alipotembelea kata hiyo tarehe 09.03.2013. Moja ya kero kubwa za wananchi wa kata hiyo wapatao alfu kumi na tisa (19,000) ni ukosefu wa huduma muhimu ya mawasiliano ya simu za aina zote, umeme, barabara, na Zahanati katika vijiji viwili vya kata hiyo. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiangalia daraja la muda lililoharibika katika kijiji cha Ng'unde Kata ya Wampembe Wilayani Nkasi tarehe 10.03.2013 alipotembelea Kata hiyo kuzungumza na wananchi kujua kero zao. Alimuagiza Mkurugenzi wa Wilaya ya Nkasi kwa kushirikiana na wananchi kujenga daraja hilo katika kiwango kinachostahiki.   (Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS CHARLES KITWANGA ATEMBELEA VIWANDA MKOANI MWANZA

$
0
0
 Naibu  Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga akipata Maelezo ya Utengenezaji wa Samaki na   Meneja udhibiti ubora wa kiwanda cha samaki cha Vicfish Bw Jacob Maiseli wakati wa Ziara ya kulembeleana kukagua Uchafuzi wa Mazingira JIjini Mwanza. 
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga akitoa Maelekezo kwa  Meneja Udhibiti Ubora Bw Jacob Maiseli kuhusu   Mfumo wa Maji taka wa Kiwanda cha Samaki cha Vicfish cha Jijini Mwanza aliofanya Ziara ya kutembelea na KujioneaUchafuzi wa Mazingira.{Picha na Ali Meja] 
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga akionyeshwa vifaa vya kufungia samaki kabla ya kusafirishwa nje ya nchi na meneja udhibiti ubora wa kiwanda cha samaki cha Vicfish mjini Mwanza Bw Jacob Maiseli. 

Naibu Wazir Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Mbao za Plastiki Bw G Vedagiri wakiketi katika Meza iliyotengenezwa kwa Maplastiki kwenye Kiwanda cha Plastiki Jijini Mwanza Wakati wa Ziiara ya Kukadua Shughuli za Uchafuzi wa Mazingira.
===== =========  =======

Uelelwa mdogo kwa wananchi juu ya suala zima la uhifadhi na usimamazi wa mazingira, imeelezwa kuwa ni moja ya changamoto ya usimamiz wa mazingira katika jiji la mwanza. Hayo yameelezwa leo na Afisa Mazingira wa mkoa mwa Bw. Charles Amani wakati akiota taarifa kwa naibu wazir Ofisi ya Makamu wa Rais katika Ziara ya kutembelea viwanda mjini Mwanza. Pamoja na changamoto hiyo mkoa pia unakabilina na upungufu wa vifaa vya udhibiti wa taka ngumu na kutokuwepo kwa teknolojia ya ufuatiliaji wa uchafuzi wa mazingira kwa hewa kutoka viwandani na kwenye magari pamoja na kutokuwa na dampo la kisasa.

Bw. Amani maeeleza kuwa pamoja na changamoto hizo, jiji la mwanza limekuwa likiongoza kwa usafi wa mazingira kwa kipindi cha miaka saba mfululizo, kutekelezaji wa kampeni ya upandaji miti pamoja na miradi mbali mbali ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kushirikiana na sekta binafsi. Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Charles Kitwanga ameeleza kuwa lengo la ziara  yake mkoani Mwanza si kufungia viwanda bali ni kutaka kuwa na msimamo wa pamoja na kuzingatia  na kutekeleza sheria ya usimamizi wa mazingira, ili iwe yenye manufaa kwa watanzania, “lengo la kuja ni kuhakikisha sheria inafuatwa” alisisitiza.

Mh. Waziri aliongeza kwa kusema kusema kuwa ni vyema Halmashauri na wizara husika zikajipanga ili kuona namna ya kuwapatia sehemu mbadala wananchi wanaoishi milimani bila kuwabugudhi, ili kule nako kupangwe ili kuwe na mazingira endelevu.


Wakati huohuo, kamanda wa police wa kikosi maalum cha mazingira Nchini Bw. George Mayunga ameeleza kuwa jeshi la police lipo tayari kupambana na wahalifu wa mazingira,ili kujenga mazingira endelevu.


Na Evelyn Mkokoi           

 Mwanza..

RAIS KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA KOCHA ATHUMANI KILAMBO LEO

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako katika mazishi ya  mchezaji mkongwe wa Yanga na baadaye Kocha wa Pan Africa Marehemu Athumani Kilambo leo Machi 11, 2013 katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam. wengine toka kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika. Ndugu Adam Malima Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es salaam Mhe Ranmadhani Madabida na kulia ni Mwenyekiti wa Yanga Bw. Yusuf Manji.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo kwenye kaburi la mchezaji mkongwe wa Yanga na baadaye Kocha wa Pan Africa Marehemu Athumani Kilambo leo Machi 11, 2013 katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam. Marehemu Kilambo, ambaye alifariki jana usiku baada ya kuugua saratani ya koo kwa takriban miaka miwili, atakumbukwa kama beki imara wa Yanga na Kocha stadi wa Pan Africa ambaye aliiwezesha Klabu hiyo kutwaa ubingwa wa taifa mwaka 1982. Pia amefundisha nyota wengi wa  kandanda nchini wakiwemo kina Kassim Manara, Adolf Richard, Mohamed Mkweche, Juma Pondamali na wengineo wengi ambao walichezea Taifa Stars kutokea Yanga na Pan.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiondoka baada ya kuongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya  mchezaji mkongwe wa Yanga na baadaye Kocha wa Pan Africa Marehemu Athumani Kilambo leo Machi 11, 2013 katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.PICHA NA IKULU.

UK PREMIER: IN THE SHADOW OF THE SUN/Q&A.

$
0
0

Ndugu zangu wapendwa nawasalimu katika jina la alie juu yeye atupae uzima. Naomba niwajulishe watz wote waishio UK kuwa ndugu yetu Josephat Torner  alieshiriki katika BBC Documentary ya albino killings in Tanzania iliyoonyeshwa mwaka jana ameshawasili tokea jana tayari kushiriki katika film nyingine itakayoonyeshwa siku ya Ijumaa tarehe 15 Mach 2013.

Josephat Torner angependa sana kukutana na Watanzania waishio huku nje ili atueleze uzito wa hili swala Na jinsi tutakavyoweza kisaidiana. Tunawaomba watanzania tujitokeze kwa wingi tumuunge mkono huyu ndugu yetu kwa jitihada zake na ujasiri wake kwani ni kazi inauohitaji moyo sana na inaumiza roho sana kusikia mateso wanayoyapata hawa wenzetu wenye ulemavu wa ngozi.
Filmed over six years, In the Shadow of the Sun tells the story of two men with albinism in Tanzania, Josephat Torner and 15-year-old Vedastus, who are pursuing their dreams in the face of virulent prejudice. Through his intimate portrait, filmmaker Harry Freeland reveals a story of deep-rooted superstition, heartfelt suffering, and incredible strength.

Please note: All Human Rights Watch Film Festival screenings will start promptly at the advertised time.

SHOWING AT:
SOHO CURZON
FRIDAY 15 MARCH 2013
TIME: 18:30
ADVISED 16

Msama awataja Wasanii watakaoshiriki Tamasha la Pasaka 2013


MKURUGENZI MKUU WA WIPO FRANCIS GURRY AWASILI NCHINI TANZANIA KUHUDHURIA MKUTANO WA SIKU MBILI UNAONZA KESHO

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry (wa pili kulia) akipokelewa na mwenyeji wake Mkurugenzi wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara Odilo Majengo (kulia) kwa niaba ya Waziri Dkt. Abdallah Kigoda mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndeege wa Kimataifa wa Mwl. JK Nyerere jijini Dar. Wa Pili kushoto ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou. (Picha na Zainul Mzige wa Mo Blog)
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou wakielekea katika chumba maalum cha wageni maalum kwenye Uwanja huo.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akibadilishana mawazo baadhi ya maafisa mbambali wa Wizara.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akizungumza na mwenyeji wake Mkurugenzi wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara Odilo Majengo.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry katika tete a tete na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dkt. Alberic Kacou.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akipitia moja ya magazeti maarufu nchini Tanzania la The Citizen ambalo limeandika habari kuhusiana na mkutano aliokuja kuhudhuria. Kushoto ni Dkt. Alberic Kacou.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akisaini daftari la wageni katika chumba maalum cha wageni maalum mara baada ya kuwasili nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akiteta jambo na Mkurugeni Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dkt. Alberic Kacou wakati akijiandaa kuondoka katika Uwanja wa ndege. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara Odilo Majengo.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akiingia kwenye gari maalum kuelekea hotelini.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akiwasili hotelini na kulakiwa na baadhi ya maofisa wa WIPO.
Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry akipewa maelekezo machache kuhusiana na taratibu za mkutano wa kujadili Changamoto za Maendeleo katika Bara la Afrika katika mkutano nchini Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa World Interllectual Property Organization (WIPO) Francis Gurry awasili nchini Tanzania leo kuhudhuria mkutano utakao zungumzia pamoja na mambo mengine Changamoto za Maendeleo katika Bara la Afrika. Katika Mkutano huo wa siku mbili unaotarajiwa kuanza kesho pia wadau watazungumzia nafasi ya WIPO katika Kuchochea Maendeleo barani Afrika. Mkutano huo utakaohitimishwa kesho kutwa utamalizika kwa kwa kuwa na kipindi cha majadiliano na kutoa maoni, ambapo wadau watatoa mitazamo yao kuhusiana na ajenda zilizowasilishwa na kutafuta mwelekeo wa pamoja.

PPF YAONESHA NJIA YA KUSAIDIA KIKUNDI CHA Habari Group

$
0
0


WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki (pichani akibonyeza  kitufe) amewataka waandishi wa Habari wa Kike kutumia kalamu zao katika kuandika mambo yanayohamasisha amani na utulivu nchini.

Pia aliwataka kutumia kalamu zao katika kuandika na kuibua vitendo vya unyanyasaji na vya kikatili wanavyofanyiwa wanawake nchini. 
Hayo aliyasema hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Lamada , wakati wa uzinduzi wa kikundi cha Habari Group kinachojumuisha waandishi mbalimbali wa habari hapa nchini.

Alisema ni vyema wakatumia fursa zao katika kufichua viashiria mbalimbali vya fujo kwa kuwa endapo itatokea uvunjifu wa amani wanaoathirika zaidi ni wanawake na watoto. 
Kikundi cha habari kinajihusisha na ununuaji wa hisa, kukopeshana na kufanya miradi mbalimbali ya kikundi na mmoja mmoja hivyo aliwataka wanakikundi kujibidiisha zaidi na kuongeza wanachama wake.

“Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ni moja ya maadhimio 12 ya ulingo wa Belgin hivyo mnachofanya hapa ni katika kujikwamua wenyewe kiuchumi na kama mnavyofahamu wanawake wanamajukumu mengi katika familia na pia kutingwa na mambo mengi katika tasnia yenu lakini mmethubutu kufanya hivyo hivyo endeleeni,”alisema Kagasheki

Pia alitoa wito kwa wanawake kuhakikisha kuwa majukumu waliyonayo yasiwe kikwazo kwao kushiriki katika kukuza uchumi. 
Alisema kinachotakiwa ni kuondoa fikra kuwa haiwezekani na kuhakikisha wanapiga vita mambo yanayomgandamiza mwanamke kwa kuondoa fikra kwamba haiwezekani kujikwamua kiuchumi.

Naye mlezi wa kikundi hiko ambaye pia ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angella Kairuki alisema atakuwa bega kwa bega na wanakikundi hiko katika kuhakikisha kuwa kinasonga mbele.

“Nimefurahishwa sana na wazo la wanahabari hawa na nina ahidi nitakuwa nao bega kwa bega katika kuhakikisha kuwa kikundi kinakua zaidi na kuwatafutia fursa mbalimbali za kukiendeleza pia,”alisema Kairuki.

Naye Meneja Uhusiano wa PPF Lulu Mengele alisema wamekuwa katika mstari wa mbele katika kutoa mikopo kwenye  saccos nchini kwa wanachama wao sehemu za kazi.

Alisema tayari wametoa mikopo kwa wanachama wake kwenye maeneo ya kazi  41 yenye thamani sh bil 48.7 lengo likiwa ni kumsaidia mwanachama akiwa kwenye ajira.

Aliendelea kueleza  kuwa PPF inachukua jukumu la kusomesha watoto wa wanachama ambao wazazi wao wamefariki kuanzia chekechea hadi kidato cha nne ambapo kwa sasa tayari wanasomesha 1333 katika shule mbalimbali.

Alisema PPF inatoa mafao saba ambapo aliyataja kuwa ni pamoja na uzee,ugonjwa,kiinua mgongo,kifo ,elimu,kujitoa, sambamba na kuandikisha wanachama kutoka kwenye sekta mbalimbali na kupata taarifa zaidi kupitia simu ya mkononi.


Naye mratibu wa kikundi cha habari group Rabia Bakari akisoma risala mbele ya mgeni rasmi alisema kikundi kinahitaji zaidi ya milioni 10 ili kila mmoja
aweze kupata mkopo kwa wakati bila kupeana kwa zamu ili kuharakisha shughuli za maendeleo.

”Kwa sasa katika akaunti yetu tumefanikiwa kuwa na milioni mbili na nusu tu, hivyo tunahitaji zaidi ya milioni 23 ili kufanikisha malengo tuliyojiwekea,”alisema Rabia. 

Mara baada ya mgeni rasmi kuzindua kikundi kulifanyika harambee ambapo zilichangwa zaidi ya sh mil 6 ambapo mgeni rasmi alitoa mil 2 na mama mlezi wa kikundi alitoa 1.5 mbunge wa Busega Dk.Titus Kamani alitoa laki 2, Jumuia ya kukuza uchumi Ilala laki sita ,TAMADA laki 2 pamoja na wadau wengine

KUNDUCHI KWANZA YAFANIKISHA MAZOEZI PAMOJA NA HARAMBEE

$
0
0

Jana tarehe 10 Machi, 2013 wanamichezo kutoka Kawe Beach, Kawe Social & Sports Club, Msasani Jogging & Sports Club, Naamanga Sports Club, Biafra Sports Club pamoja na wenyeji Kunduchi Kwanza walikusanyika pamoja na kufanya mazoezi ya mbio za pole pole (jogging) ambazo ziliwakutanisha zaidi ya wanamichezo 100 pamoja na wadau wengine. Mbio hizo zilianzia Makao Makuu ya klabu ya Kunduchi Kwanza Malanja kupitia mbuyuni, Afrikana, kipita shoto (round about) cha Kawe na kisha kurudia njia hiyo hiyo hadi Malanja. 
Kundi la Msasani  

Kundi la mwisho



Michael Juma aka Mopao (mwenye bukta nyeusi mbele) akiongoza Earobics 


Mara baada ya mazoezi ya mbio pamoja na aerobics, wanamichezo waliendelea kupata mapumziko mafupi na burudani mbalimbali zilizoandaliwa.
Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel (mwenye bukta ya bluu) akijadiliana jambo na wadau

Wadau wakipata supu

Wenyeji Kunduchi Kwanza wakifuatilia matukio
Mwenyekiti wa Kawe Social and Sports Club almaarufu Mzee Risasi (menye fulana nyeupe akiwa na wadau
Baada ya mapumziko na burudani mbalimbali, wanamichezo walijumuika tena pamoja kwa ajili ya tukio mahususi kwa ajili ya siku hiyo ambapo wana Kunduchi Kwanza pamoja na wanamichezo na wadau wengine wote waliohudhuria walipata fursa ya kumpa pole Mmiliki wa Malanja Executive Inn ambaye pia ni mlezi na mdhamini wa klabu ya Kunduchi Kwanza baada ya kuunguliwa na ukumbi wa Malanja sehemu ambayo pamoja na kutumika kwa ajili ya matukio mbalimbali ya kijamii wana Kunduchi kwanza walikuwa wakiutumia kwa ajili ya mikutano yao. 
Wana Kunduchi Kwanza wakiwa kwenye mkutano ndani ya Malanja Hall kabla ya kuungua
Zoezi la kutoa pole lilifanyika pamoja na harambee ya kuchangia ujenzi wa ukumbi huo ambapo wanamichezo wote waliokuwepo walichangia kwa kadri ya uwezo na vilabu vyote vilivyoshiriki navyo vilichangia.  
MC akiwakaribisha Kunduchi Kwanza (pichani) kusalimiana na wadau

Wana Kunduchi Kwanza

Wana Kawe Social & Sports Club wakisalimia wadau 

wana Msasani Jogging wakiongozwa na Katibu Mkuu wao ndugu Mangula

Wana Namanga Sports Club 

Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel akitoa pole za klabu yake

Sehemu ya pesa taslimu zilizochangwa mara tu baada ya kuanza harambee

Mweka Hazina wa Kunduchi Kwanza (kulia) akiwa na Malanja 

Kamati ya kusimamia zoezi la harambee wakijiandaa kumkabidhi rambi rambi mhanga bwana Massawe almaarufu Malanja
Katika harambee hiyo wanamichezo pamoja na wadau wote walionyesha kuguswa sana ajali hiyo ambapo kwa muda mfupi tu zilipatikana pesa taslimu zaidi ya shilingi laki nne na ahadi zaidi ya shilingi pia toka katika vilabu vilivyoshiriki harambee hiyo.

Pia wadau walichangia vifaa ambapo klabu ya Kawe wao waliahidi kuchangia zaidi ya viunga mia moja vya makuti mara tu ujenzi utakapoanza pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu.  Mwakilishi wa Kunduchi Veterani pamoja na wanachama wao wote waliahidi kuchangia viti 10 katika harambee hiyo pia. 


Kunduchi Veterani
Jumla ya michango yote ilikuwa takriban shilingi milioni moja na laki mbili na nusu. Akizungumza baada ya kukabidhiwa mchango huo, bwana Malanja alitoa shukrani kwa wanamichezo wote walioshiriki katika harambee hiyo na pia alieleza namna alivyoguswa na upendo walioonyesha wana Kunduchi Kwanza tangu ilipotokea ajali hiyo ya moto mpaka sasa ambapo wamekuwa wakimpa moyo na kuahidi kutoa ushirikiano wao pindi ujenzi utakapoanza. 
Mzee risasi akiwa na Malanja

Mopao na mzee Ole
Akipokea shukrani hizo kwa niaba ya wanamichezo na wadau mweka hazina wa Namanga bwana Michael J Juma almaarufu Mopao alimhakikishia bwa Malanja kuwa kwa mchango huo wanamichezo wameonyesha ni jinsi gani wana upendo kwakwe na kumuomba aupokee kwa moyo mmoja kwa hicho ndicho wadau walichojaaliwa kukipata kwa wakati ule. 

Mdau akichagiza kwa dansi kuashiria kukamilika kwa harambee

Wadau wakiserebuka

Baada ya kumalizika kwa harambee, wanamichezo na wadau wengine waliendelea kupata burudani mbalimbali zilizokuwa zikitolewa. 
Baadhi ya wana Kunduchi Kwanza wakiongozwa na Katibu Msaidizi Bi Sizya Risasi (wa kwanza kulia)

KITUO CHA MITINDO HOUSE CHAPOKEA MSAADA WA VYAKULA TOKA VODACOM TANZANIA

$
0
0

Afisa ustawi wa jamii wa Vodacom Tanzania,Bw.Ndehagati Biduga,akimkabidhi mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Mitindo House kilichopo jijini Dar es Salaam,msaada wa mchele,msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni mbili ulitolewa na Vodacom Tanzania kupitia kampeni yake ya pamoja na Vodacom inayoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo, hivi karibuni.
Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha Mitindo House,Bi.Khadija Mwanamboka wakwanza kutoka kushoto waliosimama,akiwapa muuongozo baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha rasiliamali watu cha Vodacom waliotembelea kituo hicho kutoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali vywenye thamani ya shilingi milioni mbili,katika mwendelezo wa kampeni ya pamoja na Vodacom inayoendeshwa na wafanyakazi wa kampuni  hiyo,Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MKURUGENZI WA 'CITIBANK'S'

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi wa Citibank's, Patrick Dewide, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Machi 12, 2013 kwa mazungumzo. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi wa Citibank's, Patrick Dewide na Mkurugenzi Mtendaji wa Citibank Tanzania, Joseph Carasso (kushoto) wakati walipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Machi 12, 2013 kwa mazungumzo. Picha na OMR
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images