Radio 5 FM 105.7 imeandaa "kampeni ya RADIO 5 viwanjani" katika mkoa wa Arusha ambapo itawakutanisha watangazaji na madjs na wasikilizaji wao katika kumbi za starehe kwa takribani wiki tano ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki wa Redio hiyo kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima huku mashabiki wakijipatia zawadi mbalimbali katika kampeni hiyo(katika picha ni Mtangazaji wa kituo cha Redio 5 Julius Kamafa aliyejizolea umaarufu mkubwa jijini Arusha kupitia kipindi chake cha funiko base kinachosikilizwa zaidi na vijana akishow love na msikilizaji wake katika kampeni ya "Redio 5 viwanjani"ndani ya ACTIVE CLUB - Mbauda jijini Arusha
Timu kazi ya Redio 5 wakifatilia show
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akiwa anauliza maswali kwa vijana wa Arusha waliofika katika kampeni ya Redio 5 viwanjani ndani ya ACTIVE CLUB - Mbauda jijini Arusha.
Meneja ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo akifurahia jambo katika kampeni ya Redio 5 viwanjani iliyofanyika jijini Arusha
Mtangazaji maarufu aliyejizolea umaarufu mkubwa kupitia kipindi chake cha love cuts Semio Sonyo akimuuliza maswali shabiki wa redio 5 katika kampeni ya Redio 5 viwanjani yenye nia ya kuwashukuru wasikilizaji wa kituo hicho kwa kuwa pamoja kwa mwaka mzima. Meneja ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo kushoto akieleza nia ya kampeni hiyo itakayofanyika katika bar mbalimbali jijini hapa ambapo pia wasikilizaji wa kituo hicho watajizolea zawadi mbalimbali zikiwemo T-shart,vikombe,vinywaji kutoka TBL
Shabiki wa Redio 5 aka chali ya Arachuga akionyesha kiduku cha Arushaaaa
Mtangazaji wa kituo hicho Julius Kamafa aliyeshikilia T-Shart akionyesha manjonjo yake
Mtangazaji wa kituo cha Redio 5 Julius Kamafa aliyejizolea umaarufu mkubwa jijini Arusha kupitia kipindi chake cha funiko base kinachosikilizwa zaidi na vijana akishow love na msikilizaji wake katika kampeni ya "Redio 5 viwanjani"
Mtangazaji wa Redio 5 Mwangaza Jumanne wa kipindi cha kurekebisha tabia"mishemishe"akifanya yake katika kampeni ya Redio 5 ndani ya ACTIVE CLUB - Mbauda,
Mtangazaji wa Redio 5 Mwangaza Jumanne akimkabidhi msanii Reggaa kikombe mara baada ya kushinda kwa kujibu maswali vizuri...msanii huyu anatamba na kibao chake kipya kiitwacho MCHUMBA akishirikiana na msanii mwenzake G BLESS wote wanatoka U.S.O(united streets olmatejoo)
Mwanaisha Suleiman mtangazaji wa kituo hicho anayewika katika kipindi cha "mishemishe pamoja na rusha roho"akiwa anamkabidhi msikilizaji wa redio 5 kikombe cha chai chenye nembo ya kituo hicho Hapa Mwanaisha Suleiman akiwa anakabidhi zawadi ya t-shart kwa shabiki wa Redio 5
Shabiki wa Redio 5 akiwa anafurahia t-shart yake
Wafanyakazi wa Redio 5 wakiwa katika pozi wakati kampeni ya Redio 5 viwanjani ikiwa inaendelea
Mdau wa redio 5 Ray kulia,Pamela Mollel mmiliki wa mtandao wa kijamii http://jamiiblog.co.tz/ na Tonnie Kaisoi mtangazaji wa Redio5 wakishow love Burudani ilichukua nafasi yake ,hapa machali ya Archuga wakifanya yao ndani ya ACTIVE CLUB - Mbauda
Mtangazaji wa Redio 5 Wilfred Mdingi ambaye alikuwa MC katika shughuli hiyo akifanya yake jukwaani
Msanii kutoka Arusha Juma Ujanja akimiliki jukwaa vilivyo kwa kutoa burudani kwa mashabiki wake
Msanii SS boys kutoka Arusha akitoa burudani kwa mashabiki wake
Umati wa mashabiki wa Redio 5 waliojitokeza katika "kampeni ya Redio 5 viwanjani"
(Habari picha na Pamela Mollel wa Jamiiblog)