President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete signs a condolence book at Zambia’s High Commissioner residence in Dar es Salaam today following the death of Zambia’s President Michael Sata early this week at a London hospital where he was receiving treatment.On the left seated is the First Lady Mama Salma Kikwete and standing second left is Zambia’s High Commissioner to Tanzania H.E. Judith Kapijimpanga(photo by Freddy Maro)
PRESIDENT KIKWETE MOURNS SATA- SIGNS A CONDOLENCE BOOK AT HIGH COMMISSIONER’S RESIDENCE.
↧
↧
SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI-DKT.BILALI
Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilali (watatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa Sekta ya afya nchini mara baada ya kufungua Kongamano la wadau hao leo jijini Dar es salaam.Wengine kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Seif Rashid.Picha zote na Frank Mvungi-MAELEZO_Dar es salaam.
Makamu wa Rais Dk. Mohemed Gharib Bilali akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Afya na ustawi wa Jamii Dk Seif Rashid leo Jijini Dar es salaam wakati wa Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya lililofanyika leo Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Wadau wa Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya wakiwa wanamsikiliza mgeni rasmi ambaye ni makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilali (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo leo jijini Dar es salaam.
…………………………………
…………………….Na Frank Mvungi-MAELEZO
Serikali imesema itaendelea kuboresha huduma za afya hapa nchini kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hosipitali za Rufaa zote nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata matatibu bora na yanayoridhisha.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali wakati akifungua Kongamano la wadau wa Afya nchini.
Serikali imesema itaendelea kuboresha huduma za afya hapa nchini kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hosipitali za Rufaa zote nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata matatibu bora na yanayoridhisha.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali wakati akifungua Kongamano la wadau wa Afya nchini.
Amesema kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata huduma bora za afya ili apate muda mzuri wa kuchangia shughuli nyingine za maendeleo akiwa mzima.
Dkt. Bilali ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutoa motisha kwa watumishi wa Sekta ya afya ili waendelee kutoa huduma bora za afya kwa wananchi.
Kwa upande wake Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid amesema Tanzania ni moja kati ya nchi nne barani Afrika zilizoweza kufikia lengo namba 4 la malengo ya millennia katika utoaji wa huduma bora za afya.
Amesema kuwa hatua imefikiwa baada ya Wizara hiyo kuamua kuanzisha idara maalum itakayohusika kuangalia ubora wa huduma zinazotolewa hapa nchini ili kuongeza tija katika Sekta ya Afya kwa kuwapa Wananchi huduma bora zinazokidhi vigezo.
Ameongeza kuwa kwa wale wanaofanya vizuri katika kutoa huduma za Afya watatambuliwa kwa mchango wao katika kutoa huduma bora.Dkt. Rashid ametaja vigezo vinavyotumika katika kuwapata watoa huduma za afya kuwa ni kutoa huduma inavyotakiwa,kutumia utaalamu sahihi katika kutoa huduma hiyo na kuzingatia viwango vilivyowekwa katika kutoa huduma za afya.
Aidha Dkt. Rashid ametoa wito kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ili waweze kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia mfuko huo kwa lengo la kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya.Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya limehusisha wadau zaidi ya 300 kutoka katika Taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Kiserikali na linafanyika kwa muda wa siku mbili ambapo baadhi ya wadau walitambuliwa kwa kutoa huduma bora za Afya ni kama vile Hosipitali ya Rufaa Mbeya,KCMC, na Bugando.
↧
NHC watathmini utekelezaji wa ujenzi wa miradi
Meneja wa NHC Mkoa wa Tabora, Erasto Chilambo akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Isikizya zilizopo wilayani Uyui mkoani Tabora kwenye semina ya mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.
Meneja wa NHC Mkoa wa Dodoma, Itandula Gambalagi akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo, Kongwa Dodoma kwenye semina ya mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.
Washiriki wa Semina hiyo Wenceslaus Tillya, Meneja wa NHC mkoa wa Temeke, Nehemia Msigwa, Meneja wa NHC Katavi na Daniel Nkya wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa likitolewa na Wataalamu Washauri wa Delloite Touche juu ya mapitio ya Mpango Mkakati wa Shirika unaomalizika mwakani, ili kuuboresha kwa kipindi kijacho. Somo hilo lilitolewa kabla ya mawasilisho ya mameneja wa mikoa.
Meneja Mshauri Taasisi inayojishughulisha na mambo ya uchumi ya Deloitte Bw.Frederick Nsemwa, Mkurugenzi wa Watushi Housing Limited, Dk Fred Nsemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu wakifuatilia somo hilo
Wataalamu washauri wa semina hiyo wakiwa pamoja na Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu, James Rhombo na Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki Benedict Kilimba wakifuatilia semina hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Susan Omari akifuatilia kwa kina soma hilo la Delloite Touche.
Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Fatuma Chillo akisisitiza jambo katika semina hiyo huku Mkurugenzi wa Fedha, Felix Maagi na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara, David Shambwe wakifuatilia.
Julius Ntoga wa Shirika la Nyumba la Taifa, William Genya, Joseph Mwanasenga, Ramadhani Macha, Elias Msese, Pauline Mrango , Hamad Abdallah na Ladislaus Bamanyisa wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa likitolewa na Wataalamu Washauri wa Delloite Touche.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akisisitiza jambo katika semina hiyo.
Humphrey Kishimbo, Meneja wa NHC, Iringa, George Magembe, Meneja Miradi wa NHC na Mektilda Mihayo, Meneja wa Mahusiano kwa Wateja wakifuatilia somo katika semina hiyo.
Washiriki wakifuatilia mada iliyotolewa na Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.
Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.wakiwa na mdau kutoka Hydraform Tanzania wakifuatilia semina hiyo
↧
SIMTANK YAMKABIDHI WAKALA GARI JIPYA DAR ES SALAAM
Afisa Masoko wa Silafrica bwana Alpesh Patel akikabidhi ufunguo wa gari aina ya Suzuki Carry jijini Dar leo kwa Mama Fatuma Wahenga kutoka kampuni ya FMJ Hardware,ambaye aliibuka mshindi wa pili kupitia promosheni iliyojulikana kwa jina la Uza na Ushinde.
Afisa Masoko wa Silafrica bwana Alpesh Patel akizungumza kwa ufupi kuhusiana na promosheni yao iliyojulikana kwa jina la Uza na Ushinde na namna washindi wanavyopatikana.
======== ======= =======
Kampuni ya Silafrica Tanzania Ltd, inayoongoza kwa kutengeneza vifaa vya plastiki leo imemkabidhi gari aina ya SUZUKI CARRY mshindi wa pili wa shindano la Uza na Ushinde ambaye ni Mama Fatuma Wahenga kutoka F M J Hardware.
Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kukabidhi zawadi hiyo Jijini Dar es Salaam Afisa Masoko wa Silafrica bwana Alpesh Patel alisema promosheni iliwahusu mawakala wote wa bidhaa za SIMTANK kwa lengo la kuhamasisha ubunifu na kujituma miongo mwa mawakala hao.
“tunawashukuru mawakala wetu kwa juhudi zao na kujitoa katika kuuza bidhaa zetu, hivyo promosheni hii ililenga kuheshimu mchango wao, natumia fursa hii kuwashukuru mawakala wetu wote walioshiriki katika promosheni hii kwa kujitoa kwao na kufanya kazi kwa juhudi” Alisema Patel.
Bwana Alpesh pia alimshukuru Mama Wahenga kwa juhudi zake katika mauzo na kuwaomba mawakala wengine kuongeza bidii ili kujiweka katika nafsi ya zawadi kutoka SIMTANK siku zijazo.
Akipokea zawadi hiyo Mama Wahenga alishukuru SIMTANK kwa zawadi na juhudi zao katika kuboresha maisha ya mamilioni ya watanzania wanotumia huduma za maji safi na salama yaliyohifadhiwa katika tanki imara na salama SIMTANK kutoka Silafrica.
“Kwanza nawashukuru, nitatumia gari hili kupandisha mauzo yangu kwa kuwafikia wateja wengi kwa wakati hivyo nitatimiza ndoto zangu za kuwa wakala kiongozi katika biashara ya kuuza SIMTANK.” Alisema, Mama Wahenga.
SIMTANK walianza biashara yao miaka 20 iliyopita kwa lengo la kutoa huduma za kuhifadhi maji safi na salama katika vyombo imara salama na vyenye ubora katika nchi za Tanzania na Kenya, Kwa sasa SIMTANK ndiyo bidhaa inayoongoza na kuaminiwa katika soko kwa matumizi ya tekinolojia ya hali ya juu na matumizi ya malighafi imara.
↧
MWEZI WA USALAMA MITANDAO UMEFIKIA TAMATI - YALIYOJIRI NA MAZINGATIO YAKE.
Mwezi huu wa Oktoba mataifa mbali mbali yamekua yakiadhimisha kwa kukuza ufuhahamu kwa watu wake juu yamatumizi salama ya mitandao. Ni wazi ya kuwa mitandao inapotumika vibaya inaweza kuleta athari kubwa sana kwa jamii, na tayari matukio mengi kutoka maeneo mbali mbali tayari tumeendelea kuya shududia.
KATIKA MWEZI HUU: kwa uchache kabisa nitaangazia matukio baadhi nikianzia na kutokea nchini "MAREKANI" Raisi wa Marekani Alipitisha agizo muhimu kwa taifa hilo kuhusiana na matumizi ya kadi ili kufanyia miamala ya kibiashara ikiwa ni katika kukabiliana na matukio ya hivi karibuni nchini mwake.tukio ambalo limeibua mijadala mbali mbali huku mataifa mengine yakiaswa kulifanyia kazi na kuboresha baada ya uchambuzi wa tukio hilo kufanywa na wataalam mbali mbali wa maswala ya usalama mitandao.
"KENYA" kupitia mkutano wake mkuu wa mwaka unao wakutanisha wataalam na wafanya maamuzi katika maswala ya TEHAMA walipata kuangalia kwa karibu maswala mbali mbali ya kiusalama mitandao kwa kina na kuyatafutia ufumbuzi.
"TANZANIA" pia kupitia Warsha iliyofanyika na kushirikisha mataifa mbali mbali iliyofanyikia Tume ya Taifa Sayansi COSTECH mjadala wa kina ulio jikita kwenye maswala ya usalama mitandao ulioibua mazuri mengi ikiwa ni pamoja na kuendeleza ushirikiano baina ya washiriki pamoja na kubadilishana ujuzi na taarifa za msingi katika maswala ya usalama mitandao.
"CERT - EU" inayosimamia mwaswala ya usalama mitandao katika nchi wanachama za bara ulaya walianza rasmi kujumuisha taarifa zinazopatikana hapa kwenye tovuti yao huku mijadala mbali mbali ya kiusalama mitandao kupitia foramu mbali mbali yakijadili taarifa zinazopatikana hapa.
"BBC - SWAHILI" na Vyombo vingine vya Habari Nchini vilionekana kuhamasisha matumizi salama ya mitandao, hatua ambayo naipongeza sana – Hii ni kwa sababu , vyombo vya habari vimekua na nafasi kubwa sana katika kuhakikisha wananchi wanapata ufahamu mzuri wa matumizi salama ya mitandao ili kuweza kujiweka salama wao na taifa lao kwa ujumla.
Kwa wale ambao kwa namna moja au nyingine hawakubahatika kufatilia kampeni hii ya mwaka huu ya mwezi wa kukuza ufahamu juu ya matumizi salama ya mitandao wanaweza kupitia taarifa nilizo ziandika nikiambatanisha na viambatanishi muhim kufafanua umuhimu wa kuadhimisha mwezi huu kama inavyoweza kusomeka katika link zifuatazo.
WITO: Kusha kwa mwezi huu maalum wa kukuza uelewa wa matumizi salama mitandao haumaanishi juhudi za kukuza uelewa kwa taifa juu ya matumizi salama mitandao ziishie hapa bali iwe ni fursa tosha kabisa kwa kila mmoja wetu kuchukua yale yaliyopatikana kwenye kampeni za mwezi huu kuyafanyia kazi.
Tujenge tabia ya kujifunza zaidi na kuhakiki tunautambuzi yakinifu yakua kila mmoja anajukum la dhati la kuhakikisha anajiweka salama awapo mtandaoni na anakua na matumizi salama ya mtandao ili kuwa na mafanikio chanya yatokanayo na ukuwaji wa matumizi ya teknolojia nchini.
↧
↧
DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA WAWEKEZAJI LA UKANDA WA ZIWA TANGANYIKA LEO SUMBAWANGA MKOANI RUKWA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma. kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014 katika Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga, Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni kumi na tano kwa wajasiriamali wadogo wadogo wa Sumbawanga kwenye Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma. kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014 katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni kumi kwa wajasiriamali wa Halmashauri ya Mpanda mjini kwenye Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma. kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014 katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia mashati ya vitenge alipotembelea banda la Mkoa wa Katavi kwenye maonesho wakati wa Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma. kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014 katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia ndizi za aina mbalimbali alipotembelea banda la Mkoa wa Kigoma kwenye maonesho wakati wa Kongamano la Uwekezaji la Ukanda wa ziwa Tanganyika linalojumuisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma. kongamano hilo linafanyika leo 01 Nov 2014 katika Uwanja wa Nelson Mandela Sumbawanga Mkoani Rukwa. Picha na OMR
↧
TANZANIA NA BURUNDI ZA SAINI MKATABA WA MIAKA 50 KUSAFIRISHA UMEME KUTOKA MRADI WA RUSUMO
Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania , Profesa, Sospeter Muhongo (kushoto) na Waziri wa Nishati na Madini wa nchi ya Burundi, Mhe. Come Manirakiza wakitia saini mkataba wa miaka 50 wa usafirishaji wa umeme kutoka Mradi wa Rusumo kwenda nchini humo katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam jana. Mradi huo unazihusisha nchi tatu za Tanzania, Rwanda na Burundi.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa, Sospeter Muhongo (kushoto), akibadilishana hati na Waziri wa Nishati na Madini wa nchi ya Burundi, Mhe Come Manirakiza, baada ya kutiliana saini mkataba wa miaka 50 wa usafirishaji wa umeme kutoka Mradi wa Rusumo kwenda nchini humo katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam jana. Mradi huo unazihusisha nchi tatu za Tanzania, Rwanda na Burundi.
Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe Issa Mtambuka (wa pili kushoto mbele) akiwa na maofisa wengine kwenye sherehe hiyo.
↧
SUNDERLAND AFC NA SYMBION POWER WASHEREHEKEA UIDHINISHAJI WA UJENZI WA UWANJA MPYA WA MICHEZO YA UMMA JIJINI DAR-ES-SALAAM.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wageni waalikwa, wafanyakazi mbalimbali wa Kampuni ya Symbion pamoja na wananchi wakati wa hafla ya kutoa Kibali chake kwa Chuo cha Michezo cha Sunderland kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Raymond Mushi akitoa maelezo machache kabla ya kumkaribisha rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete kwa ajili ya kutoa hotuba pamoja na kutoa Kibali chake kwa Chuo cha Michezo cha Sunderland kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Symbion Bwana Paul Hinks akitoa maelezo yake juu ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Biashara wa Chama cha Michezo cha Sunderland, Bi. Gary Hutchinson akitoa maelezo machache kabla ya kumkaribisha rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete kwa ajili ya kutoa hotuba pamoja na kutoa Kibali chake kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Biashara wa Chama cha Michezo cha Sunderland, Bi. Gary Hutchinson akimkabidhi zawadi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kutoa Kibali chake kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwaonyesha jezi yenye jina la Tanzania kwa wageni waalikwa pamoja na wananchi waliohudhuria hafla ya kutoa Kibali kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Mtoto akimkabidhi chepe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete kwa ajili ya kuchotoea udongo kuweka katika mche wa mnazi wakati wa hafla ya kutoa Kibali kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya Symbion wakati wa hafla ya kutoa Kibali kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA, MAELEZO-DSM)
↧
RAIS KIKWETE AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MAREHEMU MEJA JENERALI AIDAN ISIDORE MFUSE LEO
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha Maombolezo wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda
Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho na kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifariji familia ya marehemu wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda
Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akifariji familia ya marehemu wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda
Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Rais Mstaafu Mhe Benjamin William Mkapa akitoa heshima za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Mwinyi na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli wakitoa heshima zao za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2, 2014
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu Mhe Benjamin William Mkapa, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi, Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Samuel Ndombe wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar
es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2,
2014. PICHA NA IKULU
es slaam leo Novemba 1, 2014 kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Jumapili Novemba 2,
2014. PICHA NA IKULU
↧
↧
WAZIRI WA AFYA MH. SEIF RASHIDI AZINDUA RASMI GHETTO RADIO KATIKA HOSIPITALI YA TEMEKE JIJINI DAR.
Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid akikabidhiwa Rasmi msaada wa Vifaa na Vitu mbalimbali vitakavyo tumika katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke kutoka kwa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Baadhi ya Wadau mbalimbali walioshiriki katika Sherehe hiyo ya Uzinduzi Rasmi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Baadhi ya Wauguzi wakiwa katika uzinduzi huo Rasmi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali wakijiandaa kuelekea kutoa Msaada wa vitu mbalimbali katika vyumba vya wagonjwa
Wakiwa wanaelekea Wodini
Kulia ni Mkurugenzi wa Sibuka George Ndagali akiwa katika Wodi ya watoto kukabidhi zawadi za watoto na mama zao, katikati ni Mwanamuziki Mkongwe wa Bongo Flava Juma Nature ambaye ni Balozi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Balozi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Juma Nature akiwa anatandika Shuka moja wapo katika Wodi ya watoto kuashiria kukabidhi mashuka hayo.
Baadhi ya Timu ya wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid akiongea na Wauguzi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke, Wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi Rasmi wa Radio hiyo, ambayo lengo lake ni kuwakomboa vijana wa Mtaani pamoja na vipindi vingine vya kuelimisha Jamii na Burudani, Pia amewashukuru kwa kutoa msaada wa vifaa mbalimbali ambavyo vitasaidia katika Hospitali hiyo leo Tarehe 1.11.2014
Mkurugenzi wa Sibuka George Ndagali akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm iliyo fanyika katika katika Hosipitali Teule ya Mkoa wa Temeke Ambapo Ghetto Radio Imeweza kufunguliwa Rasmi Katika Mkoa huo nakuweza kutoa Msaada Vifaa Mbalimbali pamoja na Madawa Ambavyo Vyote kwa ujumla vimegharimu kiasi Cha Shilingi Milioni sita na Laki sita.
Mkurugenzi wa Ghetto Radio Matt Brouwer akizungumza neno wakati wa uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Ambapo Bw.Brouwer Alisema kuwa Ghetto Radio ilianzishwa nchini Kenya Miaka Sita iliyopita nakuweza kuwasaidia vijana mbalimbali Hivyo wameweza kuingia Nchini Tanzania Ilikuendeleza kuwapa vijana Fursa Na elimu INayo Tolewa na Kituo Hicho Kwa Hapa Nchini
Mganga Mkuu wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke Amaani K. Malima akitoa neno la Shukurani kwa Timu nzima ya Ghetto Radio ya Sibuka Fm kwa kufanya uzinduzi wa Radio yao katika Hospitali hiyo pia kutoa Msaada wa vitu mbalimbali vitakavyo saidia katika eneo hilo.
Meneja wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Edward Lukaka akitoa maelezo machache ya malengo ya Radio hiyo pia kueleza mikakati ya kuendelea kutoa msaada wa vifaa mbalimbali vya tiba katika Vituo zaidi vya Afya.
Mkurugenzi wa kituo cha afya cha Iran Nchini Tanzania Dkt. Farhad Arjomandi akiwashukuru Ghetto Radio ya Sibuka FM kwa kuanzisha Kituo hicho pia na wao wametoa vifaa vya matibabu kwa ajili ya kushiriki uzinduzi huo wa Radio
Mwenyekiti wa Red Cross Mkoa wa Dar es salaam Leonard Masonu akitoa neno la Shukurani
Hivi ni Baadhi ya vitu ambavyo vimetolewa na Ghetto Radio ya Sibuka Fm katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke wakati wa uzinduzi Rasmi wa Radio hiyo
↧
RC NJOMBE AKABIDHI CHETI CHA WILAYA WANGINGOMBE.
Na James Festo, Wangin'gombe.
MKUU wa mkoa wa Njombe hapo juzi amekadhidhi cheti kwa Halmashauri ya Wilaya Wanging'ombe kinachoonyesha makao makuu ya Wilaya hiyo ikiwa ni mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa wilaya hiyo cheti ambacho kimetoa kauli ya serikali itakayoondoa utata wa makao makuu.
Awali cheti hicho kilikosewa katika uchapaji wa eneo maalumu la kujengwa kwa makao makuu, ambapo kilionyesha makao makuu yalitakiwa kuwepo Wanging'ombe badala ya Igwachanya yaliposasa na kusababisha kuibuka tena kwa mvutano juu ya sehemu sahihi ya makao makuu ya wilaya hiyo licha ya kutangazwa na serikali.
Akizungumza katika Makabidhiano ya Cheti hicho yaliyofanyika katika baraza la madiwani wa halmashauri hiyo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi aliwataka watendaji wa halmashauri hiyo kupanga mipango yake vema kwani cheti wameshakipata ambacho kinaonyesha uhalali wa wilaya hiyo na kuacha malumbano ya kisiasa.
" kuna waliotaka iwe wangin'gombe wengine iwe igwachanya na wengine walitaka iwe Mdandu, lakini mwenye uamuzi wa mwisho ni Rasi kwa mujibu wa sheria kwenye gazeti la serikali la mwezi april mwaka jana ilitangaza kuanzishwa kwa halmashauri 19 ikiwemo hii ya kwenu" alisema Msangi
"Kwa bahati mbaya spika wa bunge alikosea kuandika jina la makao makuu itakuwa wangin'gommbe imetuchukua mda mrefu kufuatilia lakini hatimaye tumefanikiwa na leo nimekuja rasmi kuwakabidhi cheti chenu" aliongeza Mkuu wa Mkoa.
Aidha Msangi aliwataka viongozi hao kuitumia fursa hiyo kama chachu ya kufanya maendeleo ikiwemo kuweka mji huo katika mpango mzuri wa majengo kwani endapo wakifanya kosa katika hilo itasababisha kutokuwepo kwa muonekano mzuri wa mji.
"kazi ni kwako mtu wa mipango miji tusifanye kosa kama walivyofanya wenzetu kwenye miji mingine hapa nchini, tufanye kitu ambacho kitakuwa tunu kwa wananchi ambao watakuja kuishi miaka mingi ijayo" alisema Msangi.
Kwa Upande wake Kamanda wa Tume ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoani Njombe Bw. Charles Nakembetwa aliwataka watumishi wa halmashauri hiyo kuongeza bidii katika shughuli za maendeleo bila ya kuhusiha masuala ya rushwa.
"nyinyi ni wapya mkifanya kosa leo kitakuwa ni kilio cha halmashauri milele na milele..wewe kama mtumishi unaweza kusema unapita tu sawa lakini hata wewe unandugu zako watanzania ambao watakuja kutumia majengo, barabara hizo hizo ulizoamua kujenga chini ya kiwango
kwa sababu ya tamaa yako" alisema Nakembetwa.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe Bw. Antony Mahwata alimuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa wataendelea kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na kuishukuru ofisi ya mkuu wa mkoa kwa juhudi walizozifanya hadi kupatikana kwa cheti hicho.
"kwa niaba ya wenzangu tunashukuru serikali ikishasema hilo ni agizo tunatakiwa kulitekeleza tutahakikisha kila kitu kinajengwa kwa kiwango kinachotakiwa na tunashukuru pia kupata cheti ambacho kinaonyesha uhalali wa Halmashauri yetu"alisema Mahwata.
Aidha katika bejeti ya mwaka 2014/2015 jumla ya shilingi milioni 14 zilitegwa kwa ajili ya upimaji wa viwanja katika eneo la Mjini Igwachanya wilaya ambayo inatoka katika wilaya mama ya Njombe na ina jumla ya Kata 17.
MKUU wa mkoa wa Njombe hapo juzi amekadhidhi cheti kwa Halmashauri ya Wilaya Wanging'ombe kinachoonyesha makao makuu ya Wilaya hiyo ikiwa ni mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa wilaya hiyo cheti ambacho kimetoa kauli ya serikali itakayoondoa utata wa makao makuu.
Awali cheti hicho kilikosewa katika uchapaji wa eneo maalumu la kujengwa kwa makao makuu, ambapo kilionyesha makao makuu yalitakiwa kuwepo Wanging'ombe badala ya Igwachanya yaliposasa na kusababisha kuibuka tena kwa mvutano juu ya sehemu sahihi ya makao makuu ya wilaya hiyo licha ya kutangazwa na serikali.
Akizungumza katika Makabidhiano ya Cheti hicho yaliyofanyika katika baraza la madiwani wa halmashauri hiyo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Captain Mstaafu Asseri Msangi aliwataka watendaji wa halmashauri hiyo kupanga mipango yake vema kwani cheti wameshakipata ambacho kinaonyesha uhalali wa wilaya hiyo na kuacha malumbano ya kisiasa.
" kuna waliotaka iwe wangin'gombe wengine iwe igwachanya na wengine walitaka iwe Mdandu, lakini mwenye uamuzi wa mwisho ni Rasi kwa mujibu wa sheria kwenye gazeti la serikali la mwezi april mwaka jana ilitangaza kuanzishwa kwa halmashauri 19 ikiwemo hii ya kwenu" alisema Msangi
"Kwa bahati mbaya spika wa bunge alikosea kuandika jina la makao makuu itakuwa wangin'gommbe imetuchukua mda mrefu kufuatilia lakini hatimaye tumefanikiwa na leo nimekuja rasmi kuwakabidhi cheti chenu" aliongeza Mkuu wa Mkoa.
Aidha Msangi aliwataka viongozi hao kuitumia fursa hiyo kama chachu ya kufanya maendeleo ikiwemo kuweka mji huo katika mpango mzuri wa majengo kwani endapo wakifanya kosa katika hilo itasababisha kutokuwepo kwa muonekano mzuri wa mji.
"kazi ni kwako mtu wa mipango miji tusifanye kosa kama walivyofanya wenzetu kwenye miji mingine hapa nchini, tufanye kitu ambacho kitakuwa tunu kwa wananchi ambao watakuja kuishi miaka mingi ijayo" alisema Msangi.
Kwa Upande wake Kamanda wa Tume ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoani Njombe Bw. Charles Nakembetwa aliwataka watumishi wa halmashauri hiyo kuongeza bidii katika shughuli za maendeleo bila ya kuhusiha masuala ya rushwa.
"nyinyi ni wapya mkifanya kosa leo kitakuwa ni kilio cha halmashauri milele na milele..wewe kama mtumishi unaweza kusema unapita tu sawa lakini hata wewe unandugu zako watanzania ambao watakuja kutumia majengo, barabara hizo hizo ulizoamua kujenga chini ya kiwango
kwa sababu ya tamaa yako" alisema Nakembetwa.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe Bw. Antony Mahwata alimuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa wataendelea kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na kuishukuru ofisi ya mkuu wa mkoa kwa juhudi walizozifanya hadi kupatikana kwa cheti hicho.
"kwa niaba ya wenzangu tunashukuru serikali ikishasema hilo ni agizo tunatakiwa kulitekeleza tutahakikisha kila kitu kinajengwa kwa kiwango kinachotakiwa na tunashukuru pia kupata cheti ambacho kinaonyesha uhalali wa Halmashauri yetu"alisema Mahwata.
Aidha katika bejeti ya mwaka 2014/2015 jumla ya shilingi milioni 14 zilitegwa kwa ajili ya upimaji wa viwanja katika eneo la Mjini Igwachanya wilaya ambayo inatoka katika wilaya mama ya Njombe na ina jumla ya Kata 17.
↧
MSONDO YAADHIMISHA MIAKA YAKE 50 KWA MAFANIKIO MAKUBWA JIJINI DAR
Bendi Kongwe ya Muziki wa Dansi hapa nchini iliyodumu kwa miaka 50 toka kuanzishwa kwake mwaka 1964,Msondo Ngoma Music Band imesherehekea jubilei yake hiyo iliyofanyika Novemba 1,2014 katika viwanja vya TCC Club,Chang'ombe jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha mashabiki wake lukuki kutoka sehemu mbali mbali.
Mgeni Rasmi katika Sherehe hizo ya kusherehekea Jubilei ya miaka 50 ya Bendi ya Msondo Ngoma,alikuwa ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Prof. Elisante Ole Gabriel ambaye pia aliwatunuku vyeti vya heshima wanamuziki mbali mbali walioitumia Bendi hiyo toka ilipoanzishwa mpaka sasa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Prof. Elisante Ole Gabriel akipokea Cheti cha heshima kutoka kwa Muwakilishi wa Mfuko wa PSPF,Abdul Njaidi ambao ni sehemu ya Wadhamini wa Bendi hiyo ikiwa ni sehemu ya heshima kwa Mh. Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchango wake mkubwa kwa wasanii mbali mbali hapa nchini.Cheti hicho kimetolewa na Bendi ya Msondo Ngoma.Picha Zote na Othman Michuzi.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akimkabidhi Cheti cha heshima Kiongozi wa Bendi ya Msondo Ngoma,Mzee Said Mabela.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akimkabidhi Cheti cha heshima mpiga solo hodari wa Bendi ya Msondo Ngoma,Abdul Ridhwan "Panga mawe"
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Prof. Elisante Ole Gabriel akimkabidhi Cheti pamoja na fedha taslim sh. Laki 5,Mke wa Marehemu Mzee Muhidin Maalim Gurumo katika hafla hiyo ya kutimiza miaka 50 ya kuanziswa kwa Bendi hiyo.
Mmoja wa Waanzilishi wa Bendi hiyo,John Simon (Kapten Mstaafu) akizungumza machache pamoja na kutoa historia fupi ya kuanza kwa bendi hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akimkabidhi Cheti pamoja fedha taslim sh. Mil. 5,Hassan Moshi William (mtoto wa Marehemu TX Moshi Willian) kwa niaba ya baba yake.
Mtangazaji Mkongwe hapa nchini na mwenye historia na Muziki wa Tanzania,Masoud Masoud (kulia) akionyesha moja ya CD za bendi ya Msondo Ngoma zilizokuwa zikinadiwa kwenye sherehe hizo mbele ya Wadhamini.
Safu ya waimbaji wa Bendi ya Msondo Ngoma ikiongozwa na Nguli Shaaban Dede (katikati) wakifanya vitu vya mbele ya mashabiki wao lukuki waliofika kwenye Viwanja vya TCC Club,Chang'ombe jijini Dar.
Mpiga Tumba wa Msondo Ngoma akifanya yake.
Hassan Moshi William (mtoto wa Marehemu TX Moshi Willian) akionyesha uhodari wake kiasi kwamba hata pengo la mzee wake kuhisi limezibwa.
Rapa wa Bendi ya Msondo Ngoma,Roman Mng'ande akifanya mambo.
Baba la Mababa,Mzee Said Mabela akiendeendelea kuzikonga nyoyo za Mashabiki wa Msondo.
Abdul Ridhwan "Panga mawe"
Shaaban Dede akiimba kwa hisia.
Juma Katundu.
Mkaanga chipsi wa Msondo akizicharaza kweli kweli.
Wakongwe wengine hawa wakiimba wimbo wao wa Tanzania.
Ilifika zamu ya Twanga Pepeta na huyu si mwingine bali ni Saleh Kupaza.
Kalala Junior.
Kalala na Msafiri Diof wakienda sawa na Mashabiki wao.
Msafiri Diof.........
Taswira juu ya Taswira katika Sherehe za Miaka 50 ya Msondo Ngoma.
Kalala Junior na Saleh Kupaza wakifanya yao ikiwa ni sehemu ya Usindikizaji wa Sherehe za Miaka 50 ya Msondo Ngoma.
Madansa wa Twanga Pepeta Juu kwa Juu
Mandela wa Twanga Pepeta
Wacheza Shoo wa Twanga Pepeta ni Hatariiiiiiiii...
Wadau wakijipatia taswira muhimu.
Msondo Umekolea kwa Mdau huyu.
Wadau.
Romariiiiiiiiiii Romariooooooo na Trampet yake.
Mdau akichukua taswira muhimu.
Dar Modern Taarab "watoto wa mjini" wakisindikiza sherehe hizo.
Msondo Ngoma iliyozikonga nyoyo za Mashabiki wao hakuna mtu kukaa chini.
Msongo Ngoma staili.
Bendi ya Vijana Jazz ilikuwepo kuwasindikiza kwakongwe wenzao.
Bint wa Kiongozi wa Bendi ya Vijana Jazz Marehemu Hemed Maneti akitoa burudani safii.
Hakuna kazi ngumu kama ya kupuliza hii kitu,inahitaji pumzi kubwa sana kama wanavyoonekana wanamuziki hawa wa Vijana Jazz.
Nyomiiii.
MC Zomboko.
↧
WAZAZI wameaswa kuwaruhusu watoto wa kike kujiunga katika sekta ya bahari
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Kairuki, akiongea na wajumbe wa Umoja Wanawake walio katika Sekta ya masuala ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) wakati wa kufunga mkutano wa sita wa mwaka wa umoja huo uliomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Kairuki (kushoto), akimkabidhi cheti Mwenekiti Msaidizi WOMESA tawi la Tanzania Dkt. Tumain Gurumo ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo cha Ubaharia cha Dar es salaam (DMI) (kulia) wakati wa hafla ya kufunga mkutano wa sita wa mwaka wa Umoja Wanawake walio katika Sekta ya masuala ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) uliomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wajumbe mkutano wa sita wa mwaka wa Umoja Wanawake walio katika Sekta ya masuala ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) wakiwa katika mkutano huo uliomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Wajumbe wa mkutano wa mwaka wa WOMESA wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Ramsmi Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Kairuki (wa tano kutoka kulia waliokaa) ya mara baada ya kufunga wa mkutano huo. (Picha na Eleuteri Mangi –MAELEZO)
.
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
WANAWAKE walio katika Sekta ya masuala ya Bahari wameaswa kupanua wigo wa wanachama walio katika sekta hiyo ili kuongeza ufanisi na tija katika kutekeleza majukumu yao.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Kairuki, alipokuwa akifunga mkutano wa sita wa mwaka wa wa Umoja wanawake walio katika Sekta ya masuala ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) unaomalizika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Bi. Kairuki alisema kuwa sekta hiyo katika nchi wanachama ni muhimu kulingana na unyeti wake licha ya kukumbwa na changamoto ya kuwa na wataalamu wa kike wachache jambo ambalo WOMESA imelitambua na wanalifanyia kazi kupitia mikutano na semina mbalimbali.
“Ni jukumu lenu WOMESA kushirikiana kwa pamoja ili kuongeza idadi ya wataalamu katika sekta hii mkianzia na wasichana waliopo shuleni na vyuo mbalimbali vya elimu” alisema Bi. Kairuki.
Pamoja na mkutano huo, Bi. Kairuki amewaambia wajumbe hao wa mkutano kuwa anaamini wamepta na kuboresha ujuzi walionao kwa kuwa wameshirikishana na kubadilishana uzoefu kutoka nchi wanachama wa WOMESA ambapo maarifa hayo yataendelea kuwaongezea tija na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao kama akina mama na watalaam katika masuala ya bahari.
Akimkaribisha Mgeni Rasmi, Mwenyekiti wa WOMESA kanda ya Afrika kutoka Mauritius Bi. Meenaksi Bhirugnath-Bhookun amesema kuwa WOMESA inakabiliwa na changamoto ya kuwa na wanawake wachache katika sekta ya bahari.
Aidha Bi. Meenaksi amesema kuwa katika mkutano wao wa mwaka wamefikia makubaliano ya kuongeza wanachama kupitia mamlaka za masuala ya bahari, Idara mbalimbali zinazohusu masuala ya bandari, shule za sekondari na vyuo mbalimbali katika nchi wanachama.
Naye Mwenekiti Msaidizi WOMESA tawi la Tanzania Dkt. Tumain Gurumo ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo cha Ubaharia cha Dar es salaam (DMI) amesema kuwa sekta ya bahari inafursa nyingi amewaasa wazazi wawaruhusu watoto wa kike kujiunga kwenye elimu ya bahari ambapo bado kuna fursa nyingi ili waweze kuboresha maisha yao na taifa kwa ujumla.
Dkt. Tumain amewato wasiwasi wazazi na watoto wa kike ambapo amesema kuwa teknolojia imekuwa na imepanua wigo wa wanawake kwenye masuala ya bahari, hivyo wanawake wanaweza kama walivyo wanaume katika sekta hiyo.
katika mkutano huo, WOMESA wamezindua mpango makakati wa miaka mitano unaoanza mwaka 2014 hadi 2019 ikiwa ni mpango wa kuuimarisha umoja huo katika ngazi ya kitaifa na kanda.
Mkutano wa sita wa WOMESA, mwaka huu umeongozwa na kauli mbiu inayosema “Wanawake katika sekta ya bahari baada ya 2014: Wakijenga jukwaa endelevu”.
Nchi zilizoshiriki mkutano huo wa mwaka ni Tanzania, Kenya, Komoro, Mauritius, Namibia na Visiwa vya Shelisheli.
Nchi nyingine ni wanachama ambazo hazikushiriki mkutano wa mwaka huu kutokana na sababu mbalimbali ni Angola, Sudani, Lesotho, Uganda, Somalia, Eritrea, Botswana, Rwanda, Madagaska, Afrika Kusini, Msumbiji, Burundi, Malawi, Djibout, Zimbabwe, Ethiopia na Zambia.
MWISHO.
↧
↧
DkT. Kigwangala ahimiza amani nchini
Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala akizungumza na vikundi mbalimbali mbalimbali vya Joging vilivyoshiriki katika tamasha la Mbio za Amani lililoshirikisha wawakilishi kutoka pande mbalimbali za nchi na kupokelewa na mbunge huyo ambye alikuwa mgeni rasmi, Dr. Khamis Kigwangala amewaasa wanasiasa kutoleta siasa za uchochezi hasa katika mchakato mzima wa Katiba mpya ambapo amesema waachwe wananchi wenyewe waisome waielewe na wao wataamua kama wataipigia kura ya Ndiyo au Hapana, mapokezi hayo yamefanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam leo.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala akijitolea damu kwa kitengo cha Damu salama ambacho kikilishiriki sambamba na tamasha hilo kuhamasisha wanamichezo hao ili wajitolee damu katika kuokoa maisha ya wahitaji wa damu.
Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala akishiriki katika zoezi la viungo mara baada ya kupokea vikundi hivyo vya Jogging kutoka maeneo mbalimbali nchini.
Kutoka kushoto ni Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo BMT Bw. Dioniz Malinzi na Bw. Jimmy mmoja wa viongozi wa shirikisho la vyama vya Jogging wakishiriki kuimba wimbo wa taifa katika tamasha hilo.
Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala akipokea vikundi vya Jogging katika viwanja vya Mnazi Mmoja mara baada ya kumaliza mbio za Amani.
Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala akipokea vikundi vya Jogging katika viwanja vya Mnazi Mmoja mara baada ya kumaliza mbio za Amani.Bw.Abdulla Mohamed Mwenyekiti wa Mipango ya Maandalizi ya tamasha hilo akimkabidhi jenzi Mwenyekiti wa Barza la Michezo BMT Bwa Dioniz Malinzi.
Mdau wa michezo na aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Kanali Mstaafu Iddi Kipingu akizungumza na vikundi hivyo.
Mbunge wa jimbo la Nzega Dr. Khamis Kigwangala akishiriki kuchezo kigoma cha Amani mara baada ya kupokea vikundi vya Jogging katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Bw. Dioniz Malinzi Mwenyekiti wa Baraza la Michezo BMT akizungumza jambo na vikundi hivyo kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja wakati wa Tamasha la Mbio za Amani.
Vikundi hivyo vikiimba wimbo wa Taifa.
.......................................................................
Wanasiasa wameaswa kudumisha amani, upendo na mshikamano wa Tanzania, ili kuepuka vurugu zinazoweza kujitokeza ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikisababishwa na makundi ya wanasiasa, kwa kutoa ujumbe kwa wananchi unao chochea kuvurugukika kwa amani ya Tanzania.
Akizungumza na wanamichezo wa vilabu mbalimbali vya kukimbia (Jogging) kutoka Tanzania bara na Zanzibar, katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, mbunge wa jimbo la Nzega, ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya Tawala za mikoa na seikali za mitaa, Dk. Hamis Kigwangala, amesema wakati bunge maalum la Katiba lilipokuwa likitunga katiba inayopendekezwa, kuliibuka baadhi ya wanasiasa, waliokana kushiriki katika bunge hilo na kutofautiana katika baadhi ya mambo kuingizwa katika katiba hiyo, huku wale waliobaki ndani ya bunge maalumu la katiba kwa asilimia takriban 85 wakiheshimu maamuzi ya watanzania na kuhakikisha katiba mpya inapatikana.
Hivyo amewataka wanasiasa pamoja na kuwa mapendekezo yao hayakuingia ndani ya katiba wasiwe chanzo cha kutokuridhika kwao kulazimisha na watanzania wengine wasiridhike na kwamba watanzania waachwe siku ya kuipigia kura katiba inayopendezwa itakapo tangazwa, watanzania waipigie kura ya ndio au hapana na kwamba waamue kwa utashi wao bila uchochezi wa wanasiasa.
Katika Tamasha hilo lililopewa jina la Mbio za amani 2014, Dk, Kigwangala pia amehimiza umuhimu wa kufanya michezo kila wakati, kwani michezo ni Afya, Furaha, Amani, Upendo na Ajira, huku akivitunuku vyeti baadhi ya vilabu vya Jogging kwa kushiriki katika tamasha hilo.
Tamasha hilo limeshirikisha wanamichezo wa vilabu vya Jogging kutoka Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam, ambapo limeandaliwa na Faita Jogging & Sports Club ya jijini Dar es Salaam, huu ukiwa ni mwaka wa tatu kuandaliwa.
↧
IGP MSTAAFU PHILEMONI MGAYA ASHEREHEKEA MIAKA 85 YA KUZALIWA,WAZIRI MKUU MSTAAFU MSUYA AWAASA WATANZANIA.
WAZIRI Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya amewaomba watanzania kuwa na tabia ya utii wa sheria, uaminifu na uadilifu katika nafasi zao wanazozitumukia katika Taifa la Tanzania.
Msuya aliyasema hayo katika sherehe ye kuadhimisha miaka 85 ya kuzaliwa ya aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Philemoni Mgaya iliyofanyika katika Hotel ya Protea , Court Yard jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu alieleza kuwa tabia aliyoionyesha Mgaya wakati wa utumishi wake serikalini inapaswa kuigwa na watanzania wote.
“Huyu ndiye Mtanzania halisi aliyelelewa vizuri kuitumikia nchi yake. Hana makuu, ni mkweli na mwadilifu. Akiahidi kufanya jambo fulani analitekeleza bila kuchelewa. Tunahitaji uwajibikaji wa namna hii,” Msuya alisisitiza.
Alisema kuwa Mgaya alikuwa kiongozi hodari ambaye alisimamia vyema kiapo na kazi zake na kipindi chake cha uongozi alikuwa akitoa amri zinatekelezwa mara moja.
Naye Mshauri wa kimataifa wa Kujitegemea wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Limited James Rugemalira alitoa wito kwa watanzania kuendele kuunga mkono jitihada za kuendeleza maeneo mbalimbali ya kiuchumi ikiwemo viwanda.
Aliwasihi wadau kutoa ushirikiano kwa kampuni yake inayosambaza bia aina ya Windhoek Larger na Windhoek Draught ambayo inadhamira ya kujenga kiwanda cha kuzalisha bia hizo hapa nchini.
“Tunatafuta maeneo Kilimanjaro, Tanga na Bukoba ili tuweze kujenga kiwanda hapa nchini. Tumedhamilia kufanya hivyo na tutafanya,” Rugemalira alisisitiza.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Benedicta Rugemalira aliwashukuru wananchi kwa kukubali kujumuika pamoja katika hafla hiyo na kumwomba Mzee Mgaya aendelee kuwapa mwongozo wa namna ya kuenenda katika maisha.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT) Alex Malasusa aliwaomba watanzania kuwa na moyo wa unyenyekevu na kujitolea kulitumikia taifa katika utumishi wao kama ilivyokuwa kwa IGP mstaaafu Mzee Mgaya.
Wageni wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Waziri wa Habari na Utangazaji Fenera Mukangara, Katibu Mkuu Msaaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Bakari Mwapachu, Balozi Antoni Nyaki na wazee wengine maarufu kama Timothy Msangi.
Mara Baada ya Ibada katika Kanisa la Azania Front wakati wa kuadhimisha miaka 85 ya kuzaliwa ya aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Philemoni Mgaya
Baadhi ya waumini mbalimbali wakiwa nje baada ya Ibada
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Mstaafu Philemoni Mgaya akiwa katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake
Keki
Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya akimpongeza aliyekuwa IGP Philemoni Mgaya
Mzee Timothy Msangi akieleza Historia fupi ya IGP Mstaafu Philemoni Msangi
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT) Alex Malasusa akitoa salam za Pongezi kwa IGP mstaafu.
Mshauri wa kimataifa wa Kujitegemea wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Limited James Rugemalira akitoa pongezi zake kwa IGP Mstaafu na kuelezea Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Limited
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Benedicta Rugemalira akitoa salam za Pongezi kwa IGP mstaafu
Waziri wa Habari na Utangazaji Fenera Mukangara akimpa mkono wa Pongezi IGP mstaafu
Wakiwa katika Furaha
Watu mbalimbali wakiwa katika Sherehe hiyo
Burudani ya nguvu
↧
SURPRISE BIRTHDAY PARTY YA PETER WALDEN YAFANA HUKO BOWIE MD.
Designer wa nguo (PSW) Peter Walden na mkewe Frida Walden wakiwa wenye nyuso za furaha wakati kusheherekea Birthday yake nyumbani kwake huko Bowie Md Jumamosi Novemba mosi,2014. Birthday boy akiwa na mama yake. Cake ya Birthday iliyowekwa nembo ya nguo za Peter (Perfect Gentleman by PSW).
Justus na mkewe. Bw,Adoko, Sharon na mkewe Jackie Adoko. Na Dj Mwajuma kushoto na Mariam wakifanya vitu. Stanley na Irene na mtoto wao. Bw.Alex na Kwiz a.k.a Lady Gaga. Kutoka kushoto Frida Walden,Captain Steve Mhina,Peter Walden,Mama yake Peter. Bw.Amani Moshi na mkewe Amina.Kwa picha zaidi ungana na http://sundayshomari.com/
Justus na mkewe. Bw,Adoko, Sharon na mkewe Jackie Adoko. Na Dj Mwajuma kushoto na Mariam wakifanya vitu. Stanley na Irene na mtoto wao. Bw.Alex na Kwiz a.k.a Lady Gaga. Kutoka kushoto Frida Walden,Captain Steve Mhina,Peter Walden,Mama yake Peter. Bw.Amani Moshi na mkewe Amina.Kwa picha zaidi ungana na http://sundayshomari.com/
↧
MDAHALO WA KUJADILI KATIBA WAVUNJIKA,VURUGU KUBWA ZAIBUKA UKUMBINI,JAJI WARIOBA ATOLEWA MKUKU UKUMBINI
Jaji Joseph Warioba akitoa mada.
Mabango yakiwa juu.
Vujo zinaanza.
Mmoja wa vijana waliokuwa wakitoa maneno ya kashfa kwa Jaji Warioba akiwanyooshea vidole viongozi wa meza Kuu.
Baadhi ya viti vilivyovujwa.
Jaji Warioba akitoka katika ukumbi huku akisindikizwa na askari kanzu.
Jaji Warioba akisindikizwa na makachero wa Polisi.
Jaji Warioba akiwapungia mkono wananchi waliokuwa wamefurika nje ya jengo la Ubungo Plaza ambako mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika.Wananchi walikuwa nje ya jengo la Ubungo Plaza wakimshangilia Jaji Warioba wakati akitoka katika ukumbi wa mdahalo huku wakimuita 'Rais Rais'.(Picha zote na Francis Dande).
Mtoa mada katika mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa, Jaji Joseph Warioba akitoa mada kabla ya mkutano huo kuvunjika katika ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Saam leo.
Baadhi ya vijana walioingia na mabango ndani ya ukumbi wa mkutano wakiwa na mabango yaliyokuwa yakisomeka ‘Katiba inayopendekezwa tumeipokea tunaiunga mkono’.
Mlinzi wa Jaji Joseph Warioba (kushoto) akimkinga kwa mikono ili asipate madhara baada ya mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa kuvamiwa na kundi la vijana na kusababisha uvunjifu wa amani.
Jaji Joseph Warioba akiangalia usalama wake kabla ya kuondolewa mlinzi wake katika ukumbi wa Ubungo Plaza ambapo mdahalo wa kuijadili Katiba inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika kabla ya kuvunjika.
Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akimzuia mmoja wa vijana aliyekuwa na jazba mara baada ya kutokea kwa vurugu katika mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekeza.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku (katikati) akisindikizwa kuingia katika chumba cha VIP mara baada ya kuvunjika kwa mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa. Mdahalo huo uliandalia na taasisi hiyo.
Vijana wakiwa na mabango.Mabango yakiwa juu.
Vujo zinaanza.
Mmoja wa vijana waliokuwa wakitoa maneno ya kashfa kwa Jaji Warioba akiwanyooshea vidole viongozi wa meza Kuu.
Baadhi ya viti vilivyovujwa.
Jaji Warioba akitoka katika ukumbi huku akisindikizwa na askari kanzu.
Jaji Warioba akisindikizwa na makachero wa Polisi.
Jaji Warioba akiwapungia mkono wananchi waliokuwa wamefurika nje ya jengo la Ubungo Plaza ambako mdahalo wa kujadili Katiba inayopendekezwa ulikuwa ukifanyika.Wananchi walikuwa nje ya jengo la Ubungo Plaza wakimshangilia Jaji Warioba wakati akitoka katika ukumbi wa mdahalo huku wakimuita 'Rais Rais'.(Picha zote na Francis Dande).
↧
↧
BENKI YA MKOMBOZI YATANGAZA MAUZO YA AWALI YA HISA ZAKE,YAWAOMBA WATANZANIA WAJITOKEZE KUZINUNUA
Pichani kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Mkombozi,Bwa Masha J. Mshomba akizungumza mbele ya Wanahabari (hawapo pichani),mwishoni mwa wiki jijini Dar kuhusiana na kuwafahamisha Watanzania kuhusu mauzo ya awali ya hisa za benki yao ya Mkombozi,ikiwemo pia na kuwaomba Watanzania washiriki katika ununuzi wa hisa za Benki hiyo ya Mkombozi,shoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Mkombozi Bwan. Edwina Lupembe.
↧
MBUNIFU SHERIA NGOWI AFUNIKA KATIKA MAONYESHO YA MAVAZI YA 'MERCEDES BENZ FASHION WEEK AFRICA 2014' NCHINI AFRIKA KUSINI
Mbunifu wa kimataifa wa mavazi kutoka Tanzania, Sheria Ngowi amedhihirisha kuwa yeye ni nguli katika ubunifu baada ya kufinika katika onyesho la mavazi la kimataifa lijulikanalo kama Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 lililofanyika juzi Ijumaa mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Ngowi alionyesha mkusanyiko wa mavazi aliyoyaita 'PRIDE' yaani kujivunia, kama moja ya njia za kumuenzi Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere pamoja na viongozi mashuhuri waliopigania uhuru Afrika. Afrika Kusini ilizizima na kuduwaa kwa muda usiopungua dakika 15 pale ambapo mavazi mbali mbali yaliyobuniwa na Ngowi yalipokuwa yakioneshwa katika ukumbi wa Melrose Arch.
Sheria Ngowi alionyesha mkusanyiko wa mavazi aina ya suti yenye ubunifu na ueledi wa hali ya juu kwa kutumia vitambaa vya kisasa na kale vilivyonakshiwa kwa maua na rangi za kuvutia kama nyekundu, zambarau, machungwa, nyeupe na nyeusi huku mengine yakiwa bila maua lakini yaliyong'aa kwa kutumia rangi imara kama blu, kahawia na kijivu.
Onyesho hilo la Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 lilihudhuriwa na watu mbali mbali wakiwemo viongozi wa umma kutoka Afrika kusini, Balozi wa Tanzania Afrika Kusini, Radhia Msuya, wabunifu wa mavazi kutoka nchi za Afrika kama Taibo Bacar kutoka Mozambique, David Tlale kutoka Afrika Kusini, waandishi wa habari kutoka sehemu mbali mbali za dunia na wadau wa mitindo.
Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 ni onyesho la kimataifa linalofanyika nchini Afrika Kusini mara moja kwa mwaka likikusanya zaidi ya wabunifu wa mavazi 35 kutoka Afrika kwa ajili ya kuonesha ubunifu wa mavazi yao ambapo kwa mwaka huu Sheria Ngowi ni mbunifu pekee aliyechaguliwa katika onyesho hilo kutoka Tanzania.
Sheria Ngowi anasifika kwa ubunifu wa mavazi aina ya suti, kanzu,sare za makampuni, mashirika, shule na hafla mbalimbali kama harusi.Mbunifu huyu alifungua rasmi ofisi zake zilizopo Masaki, mtaa wa Buzwagi mkabala na Ubalozi wa Angola mwaka mmoja na nusu uliopita ambapo alianza kazi kwa kuwatengenezea mavazi watu kutoka nchi mbalimbali duniani.
Pongezi nyingi kwa Sheria Ngowi, unaipeperusha vyema bendera ya Tanzania kwa kipaji chako na kazi zako nzuri.
↧
MBUNGE MBATIA ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI YA BISHOP MOSHI JIMBONI VUNJO.
Mbunge wa Kuteuliwa James Mbatia akiongozana na mkuu wa Shule ya sekondari ya Bishop Moshi, Sophia Mushi na viongozi wengine wa shule hiyo pindi alipotembelea mazingira ya shule. |
Mbunge wa Kuteuliwa James Mbatia akiongozana na mkuu wa Shule ya sekondari ya Bishop Moshi, Sophia Mushi akitembelea bweni la wasichana katika shule hiyo. |
Mh Mbatia akizungumza jambo mara baada ya kuingia katika chumba maalumu cha kujifunzia Komputa na kukuta bado shule hiyo wanatumia komputa zilizopitwa wakati. |
Mh Mbatia akitizama baadhi ya vitabu katika maktaba ya shule hiyo,kulia ni mkuu wa shule hiyo Sophia Mushi. |
Darasala la Komputa. |
Mh Mbatia akitizama moja ya kifaa kilichopo katika maabara ya shule hiyo kijulikanacho kama Fume Chamber ambacho maabara nyingi za shule ni nadra kupatikana. |
Mh Mbatia akitizama Bweni la Wavulana baada ya kutembelea shuleni hapo. |
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya kaskazini,
↧
More Pages to Explore .....