Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

KATIBA ILIYOPENDEKEZWA KUKABIDHIWA OKTOBA 08, 2014 KATIKA UWANJA WA JAMHURI MKOANI DODOMA

0
0

  Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt, Rehema Nchimbi akitoa ufafanuzi kuhusu makabidhiano ya Rasimu ya katiba yatakayofanywa kati ya viongozi wa Bunge maalumu la katiba watakao kabidhi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Jakaya Kikwete na wa Zanzibar Dkt Mohamed Sheni kwa waandishi wa habari, makabidhiano hayo yatafanyika Oktoba 08, 2014 katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.(Picha na John Banda wa Pamoja Blog)
  Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt, Rehema Nchimbi kwa makini wakati alipokua akielezea kuhusu makabidhiano ya Rasimu ya katiba yatakayofanywa keshokutwa Oktoba, 08 mwaka huu katika uwanja wa jamhuri ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete na Dkt Mohamed Sheni ndiyo watakabidhiwa.

WANANCHI wa mkoa wa Dodoma na mikoa jirani wametakiwa kufika katika uwanja wa jamhuri mjini Dodoma jumatano ya oktoba 8, 2014   kwa ajili ya kushuhudia tukio la kihistoria kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dr. Ally Mohamed Shein kukabidhiwa katiba iliyopendekezwa na bunge maalumu la katiba.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Rehema Nchimbi wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo amesema Tukio hilo litafanyika hapa mjini Dodoma kwenye viwanja vya Jamhuri kuanzia saa 6:00 Mchana na Milango ya uwanja wa Jamhuri itafunguliwa kuanzia saa 12:00 asubuhi.


Mkuu huyo wa Mkoa amesema watu watakaojitokeza ili kushuhudia tukio hilo watakuwa wengi hivyo kwa kuzingatia kuwa milango ya uwanja wa Jamhuri itafunguliwa mapema, wananchi wanashauriwa kuwahi kufika viwanja vya Jamhuri na kuhakikisha kuwa kila mtu atakayehudhuria awe tayari amekaa kwenye nafasi yake ifikapo saa 5:00 asubuhi.

Dkt Nchimbi amesema tukio hilo litahudhuriwa na Marais wastaafu wa Tanzania, Marais wastaafu Zanzibar, Viongozi wa kitaifa na watendaji wakuu, Viongozi wakuu wastaafu, Maspika wastaafu, Waheshimiwa Mabalozi na wawakilishi wa Taasisi za Kimataifa, Taasisi za Kidini, Taasisi zisizo za kiserikali na wamiliki wakuu wa vyombo vya habari.


Amesema Vilevile kutakuwepo na Makundi mbalimbali kutoka mikoa ya Tanzania bara na Zanzibar. Makundi hayo ni pamoja na Wafugaji, Wakulima, Wavuvi, Wanawake, Vijana, Wazee, Wachimbaji madini wadogo, Walemavu na Wasanii.


Aidha Dkt, Nchimbi ameseama Tukio hilo la Kihistoria litatanguliwa na tukio muhimu na maalum  la kuomba Dua na Shukrani kwa kukamilika salama kwa shughuli za “Bunge Maalum la Katiba” hapa Mkoani Dodoma tofauti na nchi nyingine katika viwanja vya Nyerere Squere hapo kesho saa 10 jioni.

BENKI YA CRDB YAADHIMISHA SIKU YA WATEJA

0
0

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (kulia) akizungumza na  wateja waliofika katika tawi la Holland House jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wateja wa Benki ya CRDB. 
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB ,Esther Kitoka (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wateja waliofika katika tawi la Tabata jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wateja wa Benki ya CRDB ambapo viongozi wa benki hiyo wamekuwa wakitoa huduma za kibenki katika matawi mbalimbali ya benki hiyo. 
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (wa pili kulia) akisalimiana na wateja waliofika katika tawi la PPF Tower jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wateja wa Benki ya CRDB. Kulia ni Mkurugenzi wa tawi la PPF Tower, Can Meseyeck. 

 Meneja wa Benki ya CRDB tawi Tabata, Hawa Sasya akisalimiana na watoto wa shule ya African Nursery & Primary School ya Tabata jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Wateja wa Benki ya CRDB iliyoanza Oktoba 6.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (kushoto), Mkurugenzi wa tawi la Holland House, wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Benki ya CRDB.
Mkurugenzi wa kituo cha Radio cha Sport FM cha Dodoma, Abdallah Majura (kulia) akipongezwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay wakati maadhimisho ya Siku ya Wateja wa Benki ya CRDB wakati Mkurugenzi huyo alipotembelea tawi la Azikiwe Premier jijini Dar es Salaam.



Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (kushoto) akikata keki na Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Mussula wakati maadhimisho ya Siku ya Wateja wa Benki ya CRDB.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Mussula akimlisha keki Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyoSaugata Bandyadhiyay ikiwa ni sehemu yamaadhimisho ya Siku ya Wateja wa Benki ya CRDB.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyoSaugata Bandyadhiyay akimlisha keki  Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Mussula.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDBSaugata Bandyadhiyay (wa nne kutoka kulia), Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Azikiwe Premier, Fabiola Mussula (wa tatu kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wateja wa benki hiyo pamoja na maofisa wa CRDB.

Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa wamepozi kwa picha.
Picha ya pamoja
Wateja wa Benki ya CRDB wakipata huduma katika tawi la Holland House.

Mkurugenzi Mkuu wa Msae Investment, Wilbard Mtenga akipokea keki kutoka kwa  Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDBSaugata Bandyadhiyaywakati wa maadhimisho ya Siku ya Wateja wa benki ya CRDB.

BENKI ya CRDB inaadhimisha wiki ya huduma kwa wateja kwa kusikiliza matatizo yanayowakabili wateja wa benki hiyo.


Akizungumza alipotembelea matawi ya Holland, Premier na PPF Tower jijini Dar es Salaam, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Saugata Bandyadhiyay, alisema kuwa wanatumia wiki hiyo katika kusikiliza matatizo ya wateja ili kuboresha huduma.


Bandyadhiyay alisema pia watasikiliza kero za wateja pamoja na kupata maoni juu ya huduma inayotolewa na benki hiyo ikiwa ni pamoja na kuyatatua.


Alisema CRDB itahakikisha inatoa huduma kwa usikivu,uwajibikaji,nia, ubunifu ushirikiano na ufanisi ili kuongeza tija kwa wateja wanaowahudumia.


Naye Meneja wa akaunti tawi la Premier, Nellie Mwambapa, aliwataka wateja kuhakikisha wanafika na kuandika maoni yao ikiwa ni pamoja na kuleza mapungufu ili CRDB iendelee kutoa huduma bora.

Lisu ashambulia jukwaa kwa saa mbili Diamond

0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira akikata utepe wakati wa uzinduzi wa album ya nyimbo za injili ya ‘Uko Hapa’ yenye nyimbo 18 ya mwimbaji,  John Lisu wakati wa uzinduzi wa album hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, mwishoni wiki. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama ambaye ni mdhamini wa uzinduzi huo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Mahusiano na Uratibu),Stephen Wasira akionyesha album ya  ‘Uko Hapa’ yenye nyimbo 18 ya mwimbaji,  John Lisu wakati wa uzinduzi wa album hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, mwishoni wiki. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama ambaye ni mdhamini wa uzinduzi huo.
 John Lisu akiimba kwa hisia kali wakati wa uzinduzi wa Album yake ya 'Uko Hapa'
Mary Lisu (kushoto), akiimba sambamba na John Lisu wimbo mpya ujulikanao kwa jina la Mfalme ambao Albam yake iko jikoni wakati wa uzinduzi wa Album ya John Lisu ya 'Uko Hapa' uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
 Waimbaji wa John Lisu wakiwajibika jukwaani wakati wa uzinduzi wa Album ya 'Uko Hapa'.
Mary Lisu akiimba wimbo wa mpya ujulikanao kwa jina la Mfalme ambao Albam yake iko jikoni wakati wa uzinduzi wa Album ya John Lisu ya 'Uko Hapa' uliofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee.


Na Mwandishi Wetu

MWIMBAJI  nguli wa muziki wa Injili Tanzania, John Lisu juzi alikonga nyoyo za mamia ya wadau waliojitokeza katika uzinduzi wa albamu yake ya Uko Hapa yenye nyimbo 18, uliofanyika katika Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.


Uzinduzi huo uliofanyika mbele ya mgeni rasmi, Waziri wa Waziri Nchi Ofisi ya Rais-Mahusiano na Uratibu, Stephn Wassira, ulikuwa na mvuto mkubwa sio tu kutokana na umahiri wa mwimbaji huyo, pia maandalizi yaliyofanywa na wadhamini.


Lisu alipopanda jukwaani, alifanya kweli kwa kuimba nyimbo zaidi ya tano zilizopo katika albamu hiyo iliyozinduliwa.


Lisu aliyepanda jukwaani saa 12 jioni, alidhihirisha uwezo wake wa kushambulia jukwaa kwa kuimba hadi saa mbili bila kuonesha kuchoka.


Uzinduzi wa albamu hiyo uliofanywa na  Waziri Wasira, iliwekwa baraka baada ya kuzinduliwa na maaskofu watano  wa Makanisa tofauti.


Hao ni Askofu Lawrance Kametta (TAG-Jimbo la Mashariki), Askofu Deo Rubala (Word Alive Centre), Askofu Bruno Mwakibolwa, Mtume Peter Nyaga (RGC-Miracle Centre) na Machungaji Paul Safari (DPC).


Lisu alilitumia jukwaa hilo lililolipuka kwa shangwe za mashabiki alipoimba na mkewe, Nelly wimbo wake mpya wa Mfalme ambao unatarajia kuwemo katika albamu yake mpya ambayo ipo katika maandalizi.


Aidha, Lisu kabla ya kuimba na mke wake (Nelly), alitumia jukwaa hilo kuwatambulisha watoto wake mapacha na kuwabariki ambako pia alitoa ushuhuda baadaye watakuwa wachungaji.


Pia, jukwaani aliimba mojawapo ya nyimbo zake na muimbaji kutoka Kenya, Timoth Kaberia.Aidha, Lisu alitumia fursa hito kutoa shukrani kwa waliofanikisha safari yake ya muziki huo. 


DVD hizo zilizozinduliwa ambazo idadi yake ni 18 zimegawanyika sehemu mbili ni pamoja na Wakusifiwa, Wastahili sifa, uko juu, Inuka, Uko Hapa, Nijaze, Nitaongozwa, Wastahili Bwana, Roho Mtakatifu na Mtakatifu.


Nyingine ni Yu Hai Jehovah, Atikisa, Upendo Upendo, Mataifa Yakujue, Umejawa na Ukuu, Fungua Macho, Haleluya na Mungu Ibariki.


 Naye Mkurugenzi wa Msama Promotions ambao ni wadhamini wa uzinduzi huo, Alex Msama, alishukuru mapendekezo ya mabadiliko yaliyopendekezwa katika Katiba mpya ambayo yanawatambua wasanii.



Alisema kutambulika huko kumetokana na mshikamano uliopo katika ya wasanii na serikali hivyo alitoa wito kwa wasanii kuongeza jitihada za ufanikishaji wa kazi zao.

UNESCO YAAHIDI KUVIENDELEZA VYOMBO VYA HABARI JAMII KUKUZA DEMOKRASIA

0
0
DSC_0120
Mwalikishi wa Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa redio jamii, Bi. Rose Haji Mwalimu akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues kwenye sherehe za uzinduzi wa kituo hicho cha redio jamii Uvinza FM uliofanyika wilayani Uvinza mkoani Kigoma.

Kutoka kushoto ni Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Mkurugenzi Mtendaji wa Uvinza FM Radio Bi. Nuru Kalufya, Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya na Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mwalimu Hadijah Nyembo.

Na Mwandishi wetu, Uvinza.

Shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeahidi kuendelea kuzisaidia redio jamii kwa lengo la kuhakikisha sauti za wanyonge zinapazwa na kusikika ili kukuza demokrasia nchini.

Mwalikishi wa shirika hilo ambaye pia ni mshauri na mkufunzi wa redio jamii Bi Rose Haji Mwalimu aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Redio Jamii cha Uvinza FM kilichozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya.

Bi Haji alisema kwamba jitihada hizo ni kutokana na ukweli kwamba watu wengi wanaishi vijijini ambako hawapati fursa ya kupata habari kwa wepesi kwa ajili ya maendeleo yao kwa sababu wanaishi katika sehemu ambazo hazifikiki kwa urahisi kutokana ya miundombinu duni ya mawasiliano.

“Takwimu zinaonyesha kwamba nchini Tanzania watu wenye uwezo wa kuangalia telelvisheni ni asilimia 7 tu, kwa hiyo redio bado inachukua nafasi kubwa zaidi ya upatikanaji wa taarifa kwa haraka, wepesi, urahisi na kwa mapana zaidi,” alisema Bi. Rose Haji.

UNESCO ni shirika la Umoja wa Mataifa ambalo kwa muda mrefu limekuwa likitoa msaada kwa redio jamii Tanzania katika kuzianzisha, kuzipatia vifaa na kuzijengea uwezo kiufundi na mafunzo ili zijiendeshe zenyewe.
Redio zilizoanzishwa na UNESCO ziko chini ya mtandao maalum ujulikanao kama Mtandao wa Vyombo vya Habari Jamii Tanzania (COMNETA).
DSC_0285
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya akifanyiwa mahojiano mafupi ndani ya studio za redio jamii Uvinza FM na Mtangazaji wa kituo hicho, Kadisilaus Simon mara baada ya kuzindua rasmi redio hiyo.

Mtandao huo, hutekeleza miradi mbalimbali inayolenga kuharakisha maendeleo ya wananchi na ushirikishwaji wa wananchi kupitia redio jamii hususan matumizi ya Tehama, mchakato wa Rasimu ya Katiba, uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2015.
 
Takribani Redio za Jamii zipatazo 30, ikiwemo ya Uvinza zinatekeleza mradi maalum wa Uchaguzi unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la (UNDP) kwa kushirikiana na UNESCO, Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bara na Unguja (NEC na ZEC) na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini (RPP).
“Redio zipatazo 30 zimeshapatiwa mafunzo yanayohusu maadili ya vyombo vya habari, jinsia, na masuala ya jinsi ya kuandika habari za migogoro kwa mtazamo chanya.

Viongozi wa serikali za mitaa pia watashiriki katika mradi huu kuhakikisha uhalali wa mradi huo, wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na makundi maalum pia katika kuhakikisha mwendelezo wa utamaduni wa kuvumiliana, kujadiliana bila kugombana ili kuwezesha uchaguzi mkuu ujao ufanyike kwa amani na utulivu.

“Nina uhakika kuwa ushirikiano huu utaendelea baada ya mafunzo haya na kwamba redio jamii zitaleta mabadiliko makubwa kuhakikisha kuwa migogoro haina nafasi katika jamii zetu. Vyombo vya habari vina wajibu wa kuhakikisha kuwa vinaelimisha jamii juu ya athari za migogoro na kuhamasisha utulivu, amani na uvumilivu katika jamii, ” alisema Bi. Rose Haji Mwalimu.

Wakati huo huo mwakilishi huyo wa UNESCO Bi Mwalimu ameuomba uongozi wa halmashauri na wanajamii wa Uvinza kushirikiana na Redio Jamii Uvinza FM katika mradi huu ambao utawanufaisha sana wanajamii wa Uvinza na Kigoma kwa ujumla katika kuharakisha maendeleo.
DSC_0308
Mtangazaji wa kituo cha redio jamii Uvinza FM, Kadisilaus Simon akitekeleza majukumu yake kwa furaha kabisa mara baada ya kupewa baraka na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya.

“Redio hii ni yenu sio ya Kalufya, yeye ameianzisha kwa ajili ya maendeleo ya Uvinza, kitumieni, kitunzeni na mshiriki kikamilifu ili mpaze sauti zenu kwa maendeleo yenu na kudumisha Amani, upendo na utulivu kuelekea uchaguzi Mkuu mwaka 2015,” alisema Bi Mwalimu.

Nae Meneja wa huduma za kijamii wa Airtel Tanzania, Hawa Bayumi, Bi. Hawa Bayumi alisema kwamba Kampuni hiyo kwa kushirikiana na UNESCO bila kujali biashara, imejikuta inalazimika kujihusisha na masuala ya kijamii katika maendeleo kama shukrani za pekee kwa jamii kuruhusu minara ya kampuni kujengwa sehemu zao.

“Ikiwa ni njia ya kuishukuru jamii kwa kuiruhusu kampuni kujenga minara yake sehemu zao za kuishi, njia pekee ni kutoa msaada kwa wanajamii hao kuleta mabadiliko katika changamoto zilizopo ambazo ni umaskini, unyanyasaji wa kijinsia, na imani potofu za kishirikina kwa kuboresha miundombinu na mawasiliano”, alisema Bi. Bayumi.

Kwa kupitia redio jamii Bi. Bayumi amesema changamoto hizo zitaisha kwa kuhakikisha vipindi bora vinatayarishwa na kuhamasisha elimu kwa watoto, afya masuala ambayo yanaipa kampuni ya Airtel alama kuwa ilichangia maendeleo katika halmashauri ya Uvinza.

Kampuni ya simu ya Airtel imeahidi kuendelea kushirikiana na asasi husika hususan redio za kijamii kwa lengo la kukuza majadiliano ya kidemodrasia nchini.

ROSE MUHANDO AFYATUA "JIWE"

0
0
 Msanii maarufu namba moja wa Africa Mashariki wa nyimbo za injili amefyatua  kibao cha pili kingine kilichotengenezwa katika studio za Sony Music Africa, ambapo kibao cha kwanza kiliitwa Wololo kilichobeba albam ya Yesu Kung’uta chini ya usimamizi wa Rock star 4000.
Wimbo wa jiwe umetengenezwa na kuchezwa na Rose Muhando ambapo kupangiliwa na kuzalishwa na Yusuph Mayige katika Studio ya Sony Music Afrika na kuendelezwa na  kuongezewa vionjo na  Rockstar 4000.

" Rose Muhando asema wimbo huu unatambulisha kuwa naniataendelea kuitawala hii dunia na kila kilichomo ndaniyake, katika dunia hii ya sasa , tunapoteza uaminifu nakumsahau Mungu katika kutawala kila kitu. 

Ni miminatakiwa kuweka muda wa kumkumbuka na kumsifuyeye kwa njia ileile tunayotumia katika kusifu nyota zetukwa majina tunayoyajua wenyewe ila mungu wetu nimkuu kuliko majina yote makuu, Mungu Mwamba, “Jiwe”.

 Rose Muhando amejulikana kuwa msanii mahiri na wa kwanza Afrika Mashariki na pia amefanikiwa kukutana na viongozi wakubwa wa serikali akiwemo Mheshimiwa Rais wa muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete, Rais mstafu wa Kenya mheshimiwa Daniel Arap Moi na viongozi wengi wa siasa.
Kwa takwimu ya usambazaji wa muziki Rose Mhando amekuwa msanii wa kwanza  kuongoza mauzo ya muziki wa injili Afrika mashariki.
DVD ya albamu yake inatarajiwa kufyatulia msimu wa  krismasi.

Kwa habari zaidi kuhusu Rose Muhando tembelea:
Facebook: http://www.facebook.com/officialRoseMuhando

Twitter: http://www.twitter.com/Rose_Muhando


BINTOU SCHMILL The African-German Female Boxer became the new junior welterweight European Champion!!!

0
0
BINTOU  SCHMILL ALSO KNOWN AS THE VOICE

The African-German Female Boxer became the new junior welterweight European Champion!!!

Frankfurt, Germany,

The popular African-German base female boxer Bintou  Schmill (30) also known as the Voice beat a serbean female boxer Champion Mirjana Vujic on K.O on the third round.

Bintou Schmill is undefeated. She already ringed as professional Boxer 9 times, with an incredible record of 9 Wins and 8 K.O.s .The recent fight on 26th of september 2014 was in the city hall in Saalbau Frankfurt-Nied, where she won the title by knockout in the third round. These put her at the center of media’s attention worldwide. It was her highly publicized fight the world watched .On this very day she became the new European junior welterweight champion to own the belt awarded by IBF.

Bintou Schmill is common know as „The Voice“ or the lioness that breaks here and there, you better stay away from her during the ring. “ I determine to set a record on every corner“ she insists! All these comes from her hardworking and rigorous training. The strength, quick fist and her notable defensive abilities, always intimidate her opponents!.

Any brave hearted out there to sponsor and make a name with Bintou? Bintou needs you to make it happen… a man is a man because of another man –UBUNTU

For more information write to
 Africans support your children and make them proud NOW! http://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=iEmjbWJr"



The Link is: 

TMF yalipongeza Bunge Maalum la Katiba kwa kuingiza katika Katiba vipengele vitatu vinavyolinda maslahi ya wanamuziki

0
0
Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania (TMF), Addo Novembar (katikati) akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) wakati akilipongeza Bunge Maalum la Katiba kwa kuingiza katika Katiba vipengele vitatu vinavyolinda maslahi ya wanamuziki. 
Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Kasimu Mapili (kulia), akiimba na kupiga gitaa lake wakati Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania (TMF), Addo Novembar (katikati), alipozungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu kulipongeza Bunge la Katiba kwa kuingiza katika Katiba vipengele vitatu vinavyolinda maslahi ya wanamuziki. Afya ya Mapili imeimarika baada ya kuugua ugonjwa wa moyo.

Shirikisho la Muziki Tanzania (TMF), limeunga mkono rasimu ya mabadiliko ya katiba kwa kile walichodai kuwa kimegusa maslahi yao hivyo wataipigania kwa nguvu zote kuhakikisha inapita.

Akizungumza kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, Mwenyekiti wa TMF Addo November alisema kuwa kwa miaka mingi wasanii walikuwa wakililia sheria ambayo italinda maslahi yao ambayo kwa mara ya kwanza tangu uhuru upatikane wataanza kula matunda ya kazi zao baada ya katiba mpya kupita.

"Wasanii wamekuwa wakifanya kazi kubwa lakini hawanufaiki na kazi zao, wasanii wa zamani ukiangalia walifanya makubwa kwenye tasnia hii ya sanaa lakini baadhi yao wamekufa ni maskini wa kutupwa, na wengine mpaka sasa wanaishi maisha ya dhiki hayalingani na thamani ya kazi waliyokuwa wanafanya.

"Nchi za wenzetu wasanii wamekuwa wakiishi maisha ya mazuri na kuendesha magari ya kifahari, lakini kwa Tanzania ni tofauti magari ya kifahari yanaendeshwa na wanasiasa, wasanii wananyonywa, tunashukuru katiba hii imetambua haki za wasanii kwa kuingiza vipengele vitatu ambavyo vitalinda maslahi ya wasanii na kuwainua kiuchumi.

Novemba alivitaja vipengele hivyo ni ibara ya 15 (1.e) ambayo inasema kuweka mazingira kwa wasanii kunufaika na kazi zao, ibara ya 38 (iii) inayosema kufanya ugunduzi, ubunifu na utafiti wa sanaa, sayansi na mapokeo ya asili.

"Ibara ya 56 (1) inasema kila mtu atakuwa na uhuru wa kushiriki kwenye mambo yanayoendeleza na kukuza sanaa, taaluma, ubunifu na ugunduzi. "Kipengele cha (iii) Serikali itakuza na kuendelza utafiti, ubunifu na ugunduzi katika sanaa, sayansi na teknolojia kwa kutunga sheria ambazo zitalinda hakimiliki na haki za wabunifu, watafiti na wasanii.

Novemba alisema Wasanii kutambuliwa kama kundi maalum, sababu zikiwa ukubwa wa kundi hili, ambalo liko katika kila kijiji nchini, na machango wa pato la Taifa la kundi hili ambao kwa mujibu wa ripoti ya WIPO ya 2010, wasanii walichangia asilimia nne ya GDP, na walichangia asilimia tano ya ajira nchini.

"Kitendo cha rasimu hii kuweka wazi katika Katiba umuhimu wa ulinzi wa mali itokanayo na ubunifu 'Intellectual property' sheria ambayo italinda maslahi ya wasanii, tutaipigania kwa nguvu zote tupo tayari kufanya kampeni nchini nzima kuipigania ili ipite, tunaiunga mkono kwa asilimia 100 na kesho (leo) viongozi wenzetu watamsindikiza Rais kuipokea rasimu hiyo.


Aliwataja viongozi wa Shirikisho ambao watamsindikiza Rais Jakaya Kikwete kupokea rasimu hiyo kuwa ni katibu Abdul Salvador, Makamu Mwenyekiti Samweli Mbwana na Mweka Azina Mwinyi Ally.

TUWAPELEKE WATOTO WETU KATIKA CHANJO YA SURUA NA RUBELLA OKTOBA 18-24

0
0
SURUA na rubella ni magonjwa hatari yanayoenezwa haraka kwa njia ya hewa, kutoka kwa mtu mwenye vimelea vya ugonjwa huo kwenda kwa mwingine.

Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa dalili za magonjwa haya mawili zinafanana, hivyo ni vigumu kutofautisha. Wataalamu hao wanasema dalili kuu ni homa na vipele vidogovidogo.

Chanjo ya surua-rubella hutoa kinga kamili dhidi ya magonjwa haya. Dozi ya kwanza hutolewa kwa mtoto anapofikia umri wa miezi 9 na dozi ya pili akiwa na mwaka mmoja na nusu (miezi 18).

Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imekutana na wadau wake wa masuala ya chanjo jijini Dar es Salaam jana, kuzungumzia mkakati wa kampeni za chanjo ulio na lengo la kuwafikia walengwa wengi zaidi ili kuongeza idadi ya watu wenye kinga dhidi ya magonjwa ya surua na rubella. 
Endelea kusoma zaidi hapa : FATHER KIDEVU BLOG

TAMASHA KUBWA LA KARIBU MUSIC FESTIVAL KUFANYIKA BAGAMOYO

0
0
 Meneja wa tamasha la Karibu Music Festival, Richard Lupia akizungumza katika mkutano na waandishi wa Habari Dar es Salaam hii leo juu ya maandalizi ya tamasha hilo.
 Meneja wa tamasha la Karibu Music Festival, Richard Lupia akizungumza katika mkutano na waandishi wa Habari Dar es Salaam hii leo juu ya maandalizi ya tamasha hilo. Kushoto ni Mratibu wa Tamsha, Issam Ramadhan na Kulia ni Afisa Habari wa Karibu Music Festival, Said Hashim.
Meneja wa tamasha la Karibu Music Festival, Richard Lupia akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa Habari Dar es Salaam hii leo juu ya maandalizi ya tamasha hilo. Kushoto ni Mratibu wa Tamsha, Issam Ramadhan
 ********
Na Father Kidevu Blog
Tamasha kubwa la Karibu International Music Festival, linataraji kufanyika nchini kwa mara ya kwanza katika Pwani ya viwanja vya Taasisi ya Sanaa Bagamoyo (TASUBA).

Waratibu wa Tamasha hilo Karibu Cultural Promotions kupitia kwa Meneja wa Onesho hilo, Richard Lupia, amesema litafanyika kwa siku tatu kuanzia Novemba 7-9 Mwaka huu wa 2014.

Lupia amesema vikundi zaidi ya 30 na wasanii zaidi ya 500 kutoka kila kona ya dunia wanaopiga muziki wa dansi,Reggae, Hip Hop, Taarab, Ngoma za Asili, Bongofleva na Ghani wanataraji kushiriki.

“Lengo kuu la Tamasha, pamoja kukazia katika kurasimisha tasnia ya muziki kuwa na umakini zaidi, lakini kingine ni kukuza uchumi wa eneo husika la Bagamoyo ambalo ni la kihistoria, pamoja na kuhakikisha sanaa ya asili ya mtanzania inapata kuonekana katika jukwaa la kimataifa,”alisema Lupia.

Tofauti na matamasha mengine yaliyowahi kufanyika Tanzania Bara, hili
litakuwa likitumia ala kwa asilimia mia moja, wasanii wote watakaoshiriki,
watalazimika kutumia muziki wa ala kuimba na sio Playback.

Ukiachana na burudani, wasanii pia watapata nafasi ya kujifunza jinsi ya
kuunadi muziki wao duniani kwa njia mbali mbali ambako kutakuwa na warsha kutoka kwa wataalamu mbali mbali toka pembe zote za dunia.

Tamasha litakuwa likiendeshwa mchana na usiku ambapo mchana sanaa za michoro, mavazi na kuchonga zitakuwa zikioneshwa eneo la tamasha huku semina na mijadala ya jinsi ya kuupeleka muziki wa tanzania katika hatua nyingine za kimaendeleo zikiwa zinaendelea.

Mpaka sasa zaidi ya vikundi 100 vimeomba kushiriki tamasha kutoka pembe mbali mbali za dunia, tuko katika kuvichuja na kuangalia ubora wao, na Mungu akipenda, wiki ijayo tutakuja tena kuwaambia majina ya wasanii watakaoshiriki tamasha hili linalotarajiwa kuwa kubwa kuliko yote Afrika ya Mashariki.

Lengo la kuja hapa mbele yenu kwa leo lilikuwa ni kuwajulisha kuhusiana na
hili na kutoa rasmi ombi letu kwenu la kusambaza ujumbe kuhusiana na fursa hii kwa wasanii wetu kujifunza kutoka kwa wenzetu, jinsi wenzetu kutoka nchi zinazoendelea, wanavyofaidika na sanaa yao ili na sisi tuweze kujikomboa.

Tunatanguliza shukrani zetu kwa kuhudhuria kwanza, lakini kingine tunaomba ushirikiano, bado sisi ni wachanga, tujitahidi kuhakikisha kwamba muziki wa Tanzania unafika katika kilele cha mafanikio.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO MSIBA WA PROFESSA KIVASI

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Rogath Kivasi, wakati alipofika kutoa pole nyumbani kwa marehemu Goigi jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mke wa ,marehemu Prof. Amelia Kivasi, wakati alipofika nyumbani kwa marehemu Goigi jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2014 kwa ajili ya kutoa pole msiba wa Prof. Rogath KIvasi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waombolezaji wakati akiondoka baada ya kutoa pole na kusaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa Professa Rogath Kivasi, Goigi jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2014. Picha na OMR.

Msiingize dini katika siasa, Rais awaambia mabalozi

0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi wa dini alipowasili katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam kufungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi wa dini alipowasili katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam kufungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi wa dini alipowasili katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam kufungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea machapisho toka kwa mwandaaji wa Mkutano wa viongozi wa dini chini ya taasisi ya Programme for Christian-Muslim Relations in Africa (PROCMURA) yenye makao yake makuu mjini Nairobi, Kenya, 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na washiriki wa Mkutano wa  viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika pich ya pamoja na wafanyakazi wa hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam wanaowahudumia washiriki wa Mkutano  wa viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini katika hoteli ya White Sands jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa  siku nne ulioanza jana  unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence. PICHA NA IKULU

Msiingize dini katika siasa, Rais awaambia mabalozi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa kuna ushahidi sasa unaothibitisha kuwa baadhi ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wamekuwa wanachaganya dini na siasa wakitumia dini kuunga mkono baadhi ya vyama vya siasa na shughuli za kisiasa nchini.

Aidha, Rais Kikwete amewaomba mabalozi hao “kuiokoa” Tanzania katika majanga makubwa yanayoweza kuipata kwa kutumia dini kuendeleza siasa, hatua ambayo ameielezea kama “njia ya hatari kweli kweli.”

Rais Kikwete alikuwa anazungumza usiku wa jana, Jumatatu, Oktoba 6, 2014, wakati wa chakula cha usiku ambacho alikula na viongozi wa dini nchini ambao wanaendelea na mkutano wao wa mwaka kwenye Hoteli ya White Sands ya Dar Es Salaam.

Mkutano huo wa siku nne ulioanza jana unajulikana kama Tanzania Christian & Muslim Religious Leaders’ Initiative for Peace and Co-existence ni mwendelezo wa mikutano ya viongozi wa dini kubwa za Kikiristo na Kiislam nchini kwa lengo la kujenga na kuleta amani na maelewano nchini. Mkutano wa mwisho ulifanyika mwaka juzi, 2012 kwenye Hoteli hiyo hiyo.


Aidha, Mkutano huo ambao moja ya wadhamini wake ni taasisi ya Programme for Christian-Muslim Relations in Africa (PROCMURA) yenye makao yake makuu mjini Nairobi, Kenya, unahudhuriwa na mabalozi 15 wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na mashirika kadhaa ya kimataifa likiwemo lile la Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP).

Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika Mkutano huo ni wa Ujerumani, Iran, Marekani,

TRAFIKI WATEMBELEA KIWANDA CHA TBL ARUSHA

0
0
 Mratibu wa Usalama afya na mazingira mahali pa kazi wa Kiwanda cha Bia nchini TBL Arusha Heavy Kassena akiwaonyesha baadhi ya maeneo na shughuli zinazofanywa kiwandani hapo askari wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Arusha, pembeni yake ni Ofisa Uhusiano wa TBL Makao Makuu Dorris Malulu, wakati wa ziara iliyofanyika kiwandani hapo juzi.
 Mratibu wa Usalama afya na mazingira mahali pa kazi wa Kiwanda cha Bia nchini TBL Arusha Heavy Kassena akiwaonyesha shughuli zinazofanywa kiwandani hapo baadhi ya askari wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Arusha waliotembelea kiwandani hapo juzi.
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Arusha Marrison Mwakyoma akitembelea kiwanda cha Bia TBL Arusha wakati wa ziara ya askari wa usalama barabarani waliotembelea kiwandani hapo hivi karibuni kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kikazi.
 Mtaalamu wa upishi wa Bia katika Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) kilichopo mkoani Arusha Jacob Mgome akiwapa maelezo askari wa kikosi cha usalama barabarani waliotembelea kiwandani hapo juzi.

 Mtaalamu wa upishi wa Bia katika Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) kilichopo mkoani Arusha Jacob Mgome akiwapa maelezo askari wa kikosi cha usalama barabarani namna Shayiri inavyopokelewa kiwandani hapo wakati wa ziara ya askari hao
 Mtaalamu wa kitengo cha kutibu maji yanayotumika kiwandani hapo akiwapa maelezo askari wa usalama barabarani namna maji hayo yanavyosafishwa na kisha kurejea tena kiwandani hapo kwa ajili ya kumwagilia bustani wakati wa ziara ya maofisa hao juzi.
 Askari wa usalama barabarani mkoa wa Arusha wakiwa ndani ya kiwanda cha Bia kilichopo Arusha wakati wa ziara yao ya kikazi ya kutembelea kiwanda hicho juzi.


 Mtaalamu wa upishi wa Bia katika Kiwanda cha Bia (TBL), Arusha Jacob Mgome akiwaonyesha askari wa usalama barabarani waliotembelea kiwandani hapo namna maji yanaytotumika kupikia Bia yanavyopitishwa.
Askari wa Ulinzi katika kIWANDA cha TBL Arusha akiwaonyesha namna kifaa maalumu cha kupimia kilevi kwa askari wa usalama barabarani walipofanya ziara yao ya kikazi kiwandani hapo juzi.

NEW VIDEO_G FRANK_FT_ABDU KIBA-AYAYA

0
0

KINANA ATINGA ISIMANI IRINGA AWATAKA VIONGOZI WASIKWEPE MAJUKUMU YAO YA KUWATUMIKIA WANANCHI

0
0
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsifia Mbunge wa Jimbo la Isimani,  William Lukuvi kwa uchapakazi wake mzuri wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Magozi, Kata ya Ilolo Mpya, Iringa Vijini leo. Kinana alimjia juu Waziri wa Maliasili na Utalii, Nyalandu kwa kushindwa kutafutia ufumbuzi migogoro ya wananchi.Pia aliwataka wananchi kuacha kukwepa majukumu yao ya kuwatumikia Wananchi. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa  CCM, Nape Nauye akihutubia katika mkutano huo
 Kinana akisalimiana na wananchi alipowasili kushiriki ujenzi wa jengo la CCM tawi la Luganga Kata ya Ilolo Mpya.

 Kinana na Lukuvi wakitoka kukagua ujenzi wa Zahanati ya Magozi Kata ya Ilolo Mpya, Isimani
 Kinana na Lukuvi wakijadiliana jambo baada ya kukagua ujenzi huo.
 Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana na Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Lukuvi wakishiriki kufyatua tofali za ujenzi wa jengo la Ofisi ya CCM

 Kinana na Lukuvi wakisaidia kufyatua tofali za kujengea jengo hilo la CCM
 Wanachama wa CCM Shina namba 6 katika Kijiji cha Magozi, Kata ya Ilolo Mpya wakicheza kwa furaha wakati Kinna alipofika kuzungumza nao
 Kinana akizungumza na wananchama wa shina hilo. Kulia kwake ni Balozi wa shina hilo Chengula Mlula

 Wamasai wakiingia kwenye mkutano kutumbiza kwa ngoma ya asili

 Wasanii wakicheza ngoma ya asili ya kabila la wasukuma


 Lukuvi akimkabidhi kompyuta na mashine ya kudurufia Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Pawaga Charles Mgimwa kwa ajili ya matumizi ya shule
 Mgimwa akifurahia msaada huo
 Katibu wa CCM Wilaya ya Iringa Vijijini, Amina Imbo (kushoto) akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa UWT wa wilaya hiyo, Shakila Kiwanga wakati wa mkutano huo
 Mbunge wa Jimbo la Isimani, ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi akielezea miradi inayyotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM jimboni humo.
 Mmoja wa wananchi akiuliza swali kwa Katibu Mkuu Kinana kuhusu mgogoro wa ardhi  wa wanakijiji na Jeshi la Magereza.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ishengoma akijibu swali hilo ambapo alisema kuwa kwa asilimia kubwa wamelitafutia ufumbuzi na kwamba kilichobaki ni wizara husika kwenda kupima na kuweka alama za mipaka.

RAIS dk. SHEIN AMFUTA KAZI MWANASHERIA MKUU SMZ NA KUMTEUA MWANASHERIA MPYA

0
0


RAIS wa Zanzibar na Mweneykiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein amemteua Mh. Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa leo na Katibu wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abdulhamid Yahya Mzee, Dkt Shein amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 55(1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Mheshimiwa Said Hassan anachukua nafasi ya aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mh. Othman Masoud Othman ambaye Uteuzi wake umefutwa kwa mujibu wa Vifungu vya 53, 54 (1) na 55 (3) vya Katiba ya Zanzibar ya 1984 na Kifungu 12(3) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Namba 2 ya 2011.

Kabla ya Uteuzi huo Mheshimiwa Said Hassan Said alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Uteuzi huo umeanza tarehe 07, October, 2014

 IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 07, October, 20114

TASAF YAPIGA HODI KANDA YA ZIWA VICTORIA.

0
0
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF umeanza  hatua ya kutambua kaya maskini katika mikoa ya Mwanza,Shinyanga,Tanga, Morogoro,Pwani na Simiyu ikiwa ni utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya maskini PSSN unaoratibiwa na mfuko huo nchini kote kwa awamu. Akifungua warsha ya kuwajengea uelewa viongozi wa wilaya ya Maswa ,Mkuu wa wilaya hiyo Luteni Mstaafu Abdallah Kihato ametoa wito kwa wananchi kuzingatia miongozo ya TASAF ili waweze kunufaika na mpango huo. 

Amesema serikali wilayani humo itatoa ushirikiano kwa wataalamu wa TASAF na watendaji wengine ili zoezi la kuzibaini kaya maskini liweze kufanikiwa. Kwa upande wake meneja fedha wa TASAF Bw. Njego Nyamukowa kwa niaba ya mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga amesema utekelezaji wa mpango huo unafanyika kwa mafanikio makubwa .
 Mtaalam kutoka TASAF Bw. Hamis Kikweppe akitoa maelezo juu ya Mpango wa kunusuru kaya maskini wakati wa warsha ya kujenga uelewa kwa timu ya wawezeshajio wa wilaya ya Maswa mkoani Simiyu. (2)
 Meneja wa Fedha wa TASAF Bw.Njego Nyamuko aliyeshika kipaza sauti mbele akitoa maelezo juu ya Mpango wa kunusuru kaya maskini unaoendeshwa na TASAF katika warsha ya kuwajengea uelewa viongozi wa wilaya ya Maswa.
 Mkuu  wa wilaya ya Maswa Luteni Mstaafu Abdallah Kihato akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya kujengewa uwezo juu ya mpango wa kunusuru kaya maskini katika wilaya ya Maswa.

KATIBA INAYOPENDEKEZWA YAOMBEWA DUWA NJEMA

0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi akihutubia wakati wa dua ya kuiombea Katiba mpya Inayopendekezwa.

KATIBA INAYOPENDEKEZWA YAOMBEWA DUWA NJEMA
 
Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma.
 
08/10/2014
 
DUA ya shukurani ya kuiombea Katiba mpya Inayopendekezwa imefanyika jana mjini Dodoma na viongozi mbalimbali wa dini toka madhehebu mbalimbai yakiwemo ya Kiislamu, Kikristo, Wasabato, Wahamadiya, Jamaat Khan, Singh Temple na CCT-Dodoma.
 
Akiongea wakati wa dua hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, Mhe. Dkt. Rehema Nchimbi alisema kuwa katika mchakato mzima wa kusaka katiba mpya, shughuli mbaoimbali za maendeleo zikiwemo shughuli za kibiashara, shughuli za kibenki, wanafunzi na shughuli nyingine za kiofisi ziliweza kuendelea kama kawaida pasipo shari yoyote hadimchakato wa kuipata Katiba ulipofikia.
 
Dkt. Nchimbi alieleza kuwa, kuna watu waliotumia muda wao mwingi katika kuhakikisha kuwa mchakato unafikia lengo kwa kukesha usiku na kufanya dua maalum ya kuiombea katiba hiyo ili iweze kupatikana na aliongeza kuwa wapo waliofanya kazi kubwa kwa kukesha huku wakifanya kazi ndani ya Bunge Maalum kwa ajili ya kufanikisha  mchakato huo.
 
“Kipindi hiki cha mchakato wa Katiba, Watanzania na marafiki zetu tumeongea na Mungu kwa namna isiyo ya kawaida, tumekutana hapa kukiri kwa maana tulimuita Mungu naye ametuitikia, hakika  yeye ndiye aliyetufanya kuipata Katiba hii”, alisema Mhe. Nchimbi.
 
Nao Viongozi wa dini mbalimbali walipata wasaa wa kutoa dua zao kwa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kuiombea nchi amani pamoja na Katiba yenyewe kwani itakuwa mkombozi kwa Watanzania.
 
Akiongea kwa niaba ya Baraza la Wazee wa Dodoma, Mhe. Balozi Job Lusinde alisema kuwa ni jambo la busara kuomba dua kwa Mungu kuhusu mchakato wa kupata Katiba na pia ni wasaa wa kumshukuru Mungu kwa kuwawezesha wale wote waliojitolea kufanikisha kuipata Katiba hiyo.
 
Aidha, alisema kuwa tangu Dkt. Nchimbi awe Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, watu wameshuhudia msimamo wake kuhusu umuhimu wa umoja, upendo, mshikamano kwa wananchi wote wa Dodoma kwani ameweza kuzishirikisha dini zote, na kuwaunganisha, pia amekuwa wa kwanza katika kuutukuza mji wa huo wa Dodoma.
 
“Ndugu zangu wananchi wa Dodoma, tumshukuru RC wetu wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi pamoja na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama kwa kutupa muda wa dua kama hii ya leo”, alisema Balozi Lusinde.
 
Mchakato wa Katiba mpya unatarajiwa kufikia hatua nyingine hapo kesho ambapo Marais toka Tanzania Bara na Zanzibar, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein watakabidhiwa Katiba Inayopendekezwa siku ya tarehe 8 Oktoba mwaka huu.

Hotuba ya Dkt. Hamisi Kigwangalla, Mbunge wa Jimbo la Nzega na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya TAMISEMI Alipopokelewa Jimboni Nzega Baada ya Kutangaza Nia Kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

0
0
Awali ya yote nianze kwa kumshukuru mwenyezi mungu, mwingi wa rehema na mwenye kurehemu, kwa kutujalia afya njema na kutukutanisha hapa siku hii adhimu ya leo, maana ni kwa utashi wake tu tunaweza kuyafanya haya yote.

Nitumie fursa hii kwa namna ya kipekee kuwashukuru nyote kwa kuacha shughuli zenu kuja kunipokea na kushiriki mkutano huu. Mmenipa heshima kubwa sana na mimi nawajibika tu kusema ‘ahsanteni sana’.

Mimi hapa ni aidha mtoto wenu, mjukuu wenu ama mdogo wenu, mnapoacha shughuli zenu kuja kunisikiliza mimi, mnakuwa mmenitwisha mzigo mzito sana. Ninajiona nawajibika kwenu kutoa utumishi uliotukuka. Ninajipa deni la kuongeza bidii kubuni miradi itakayotatua shida zetu hapa Nzega, kupigana kuondoa umaskini, ujinga na maradhi.
Sote tuliopo hapa ni mashahidi, kuwa tumefanya mengi katika miaka hii minne ya uwakilishi wangu, maana kati ya hayo, mengi tumefanya pamoja nanyi. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

Raisi Kikwete asifu juhudi za NSSF kuwezesha mradi wa daraja la kigamboni na ujenzi wa nyumza za gharama nafuu

0
0
Waziri wa ujenzi, Dk. John Magufuli akielezea jinsi wizara yake ilivyojipanga kuhakikisha kuwa malengo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni unaofadhiliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), inafikiwa na kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam. Rais Kikwete alitembelea mradi huo pamoja na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za garama nafuu zilizopo Kijichi Dar es Salaam.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dk. Ramadhan Dau (wa pili kulia) akimweleza jambo Rais Jakaya Kikwete wakati wa ziara ya rais kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni ambayo inafadhiliwa na NSSF, pamoja na kuweka jiwe la msingi katika  mradi wa nyumba za garama nafuu zilizopo Kijichi Dar es Salaam.
 Rais Jakaya Kikwete akiongea na wahusika wa ujenzi wa daraja la Kigamboni inayofadhiliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).
  Waziri wa ujenzi, Dk. John Magufuli akielezea jinsi wizara yake ilivyojipanga kuhakikisha kuwa malengo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni unaofadhiliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), inafikiwa na kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam. Rais Kikwete alitembelea mradi huo pamoja na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za gharama nafuu zilizopo Kijichi Dar es Salaam.

Rais Jakaya Kikwete ametembelea daraja la Kigamboni, Dar es Salaam, jana, ambapo ameagiza changamoto zilizoanishwa zitatuliwe haraka kabla mradi haujamalizika. Akizungumza wakati wa kupokea taarifa ya ujenzi huo, Rais Kikwete alisema utekelezaji wa mradi unapaswa kwenda sambamba na utatuzi wa changamoto hizo.

Mapema wakati akiwasilisha taarifa ya mradi huo, Makamu Mwenyekiti wa Mradi huo, John Msemo, alisema zipo changamoto chache ambazo zinapaswa kutatuliwa kwa ushirikiano na serikali.
Alizitaja changamoto hizo kuwa pamoja na zile za wembamba wa baadhi ya barabara pamoja na msongamano wa magari. Alitoa mfano wa barabara za Vijibweni-Mjimwema, Bendera Tatu-Kamata na Gerezani- Ohio kuwa ni nyembamba.

Pia aliutaja msongamano wa magari katika makutano ya barabara ya Kilwa- Mandela, Chang'ombe-Mandela na Nyerere (Tazara) kuwa unapaswa kushughulikiwa. Akizungumzia suala hilo, Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, alisema tayari serikali imeanza kushughulikia changamoto hizo, ambapo imeongea na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) pamoja na kutenga fedha katika bajeti kwa ajili ya upanuzi wa barabara hizo.

Dk. Magufuli alisema katika bajeti ya mwaka huu, fedha zimetengwa kulipa fidia kwa ajili ya barabara ya Vijibweni-Mjimwema ili iongezwe upana na kwamba, ile ya Ohio-Gerezani mazungumzo yanaendelea na ADB.

Daraja la Kigamboni linalojengwa kwa ushirikiano wa serikali na wadau na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ambapo linatarajiwa kukamilika Juni, mwakani na kuzinduliwa na Rais Kikwete. Baada ya kutembelea mradi huo, Rais alikagua ujenzi wa nyumba 1,120 zilizojengwa na NSSF katika eneo la Mtoni Kijichi, Kigamboni, ambapo aliupongeza uongozi wa shirika hilo kwa kukamilisha mradi huo wa nyumba za watu wa kipato cha kati na chini.

Rais alizindua mradi huo na kuiagiza Manispaa ya Temeke kuangalia uwezekano wa kuijenga vizuri barabara inayokwenda mahali nyumba hizo zilipo pamoja na kutengeneza miundombinu nyingine muhimu ikiwemo maji. Mapema wakati wa ziara hiyo, Rais ambaye alisherehekea siku yake ya kualiwa jana, alikabidhiwa kadi maalumu ya kumtakia maisha marefu na Mkurugenzi Mkuu wa Nssf, Dk. Ramadhan Dau.

FINCA WAZINDUA HUDUMA YAO MPYA YA FIKA NA FINCA

0
0
 Mkuu wa Huduma za Kibenki wa FINCA,Bwa.Gershom Mpangala akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani),kuhusiana na taasisi hiyo ya Kifedha kuzindua kampeni yake mpya  iliyojulikana kwa jina la Fika na Finca,kampeni inayolenga kuwafikia Watanzania wote kupitia huduma za kibenki na kuwasaidia kutimiza malengo ya kimaendeleo waliyojiwekea,Mkutano huo umefanyika kwenye moja ya Ofisi zao zilizopo Mwembechai Jijini Dar.Pichani kati Kaimu Afisa Mwendeshaji Mkuu wa FINCA Tanzania ,Bwan.Daniel Mhin pamoja na Meneja tawi la Magomeni Bwa.Cassian Clovis
Pichani kati ni Kaimu Afisa Mwendeshaji Mkuu wa FINCA Tanzania ,Bwan.Daniel Mhina akifafanua zaidi kuhusiana na Faida za akaunti za akiba za Finca kuwa ni nyingi,ikiwa ni pamoja na urahisi wa kufungua na kuendesha akaunti,taratibu za kufungua akaunti zina mahitaji madogo,kutoa na kuweka pesa bure kwenye matawi yote nchini na usalama wa fedha za mteja kupitia mfumo wa bayometriki unaotumiwa na benki hiyo.Bwan Daniel alisema kuwa kupitia matawi ya FINCA inahudumia wateja zaidi ya 120000 ambao wanahudumiwa na zaidi ya wafanyakazi 700 nchini. pichani shoto ni Mkuu wa Huduma za Kibenki wa FINCA,Bwa.Gershom Mpangala pamoja na Meneja tawi la Magomeni Bwa.Cassian Clovis.
 Baadhi ya Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo wa FINCA uliofanyika jijini Dar leo.
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images