Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

RAIS KIKWETE ASAFIRI KWA TRENI YA TAZARA KATIKA ZIARA YAKE YA MKOA WA MOROGORO

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili katika kituo cha Kisaki baada ya kusafiri kwa treni katika ziara yake ya Mkoa wa Morogoro.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Joel Bendera, Mbunge wa Morogoro Kusini Mhe Innocent Kalogeris na KAtibu wa Rais Bw. Prosper Mbena wakiongea ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki mkoani Morogoro.
Mama Salma Kikwete, Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli, Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA Bw. Ronald Phiri (kulia) na viongozi wengine ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA Bw. Ronald Phiri zawadi ya picha ya jengo la makao makuu ya TAZARA akiwa ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na viongozi wengine ndani ya behewa maalum la VIP la treni la TAZARA wakati wa safari ya Rais Kikwete kuelekea Kisaki katika ziara yake ya mkoa wa Morogoro.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipanda treni ya TAZARA kuelekea Kisaki Mkoani Morogoro akiwa katika ziara yake ya mkoa huo.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakilakiwa na umati mkubwa wa watu baada ya kuwasili katika kituo cha Kisaki baada ya kusafiri kwa treni katika ziara yake ya Mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Wananchi waliojitokeza kwa wingi kumlaki baada ya kuwasili katika kituo cha Kisaki baada ya kusafiri kwa treni katika ziara yake ya Mkoa wa Morogoro.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika mkoa wa Morogoro. PICHA NA IKULU

Serikali yatoa ufafanuzi malipo ya mishahara ya watumishi ya mwezi Julai

$
0
0
Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati alipokuwa akifafanua juu ya malipo ya mishahara ya watumishi yaliyofanyika mwezi Julai mwaka huu leo jijini Dar es salaam ambapo ameonya mamlaka husika ziwe na taarifa sahihi za idadi ya watumishi ili kuondoa makosa ya kulipa mishahara hewa, endapo kutatokea makosa ya ulipaji wa mishahara hewa watachukuliwa hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani. (Picha zote na Eleuteri Mangi – MAELEZO)

TAARIFA KUTOKA TCRA: HUKUMU YA MALALAMIKO YA WASIKILIZAJI WA CLOUDS FM NA CLOUDS TV

SERIKALI YAKIPONGEZA CHUO KIKUU CHA BAGAMOYO (UB)

$
0
0
Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), Profesa Costa Mahalu akizungumza wakati wa kufunga  Mafunzo hayo ya siku 14 yaliyoshirikisha maofisa wa juu wa fani ya biashara wa Serikali za nchi nane ambayo yaliratibiwanna Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB) ambayo yalifadhiliwa na Chuo Kikuu Cha  Nordric Africa Institute.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo.

Tunajifunza..........
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Prof. Elifuraha Mtalo (wa pili kushoto) akifuatilia hotuba ya Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), Profesa Costa Mahalu
Professa Francis Matambalya akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.

Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), Profesa Costa Mahalu (katikati) akiwa na Mkuu wa Shule ya Elimu Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Prof. Elias Bayona (kushoto) na Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu ya Juu Wizara ya Elimu Dk. Jonathan Mbwambo.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Elimu ya Juu Wizara ya Elimu Dk. Jonathan Mbwambo akizungumza wakati wa kufunga Mafunzo hayo ya siku 14 yaliyoshirikisha maofisa wa juu wa fani ya biashara wa serikali za nchi nane ambayo yaliratibiwanna Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB) ambayo yalifadhiliwa na Chuo Kikuu Cha  Nordric Africa Institute.
Mkuu wa Shule ya Elimu Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Prof. Elias Bayona akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.
Mshiriki wa mafunzo hayo kutoka Malawi, Heather Kachingwe akipokea cheti chake.
Picha ya pamoja.

Na Happiness Katabazi

SERIKALI imewataka  washiriki wa mafunzo ya jinsi ya kujadili  mikataba ya Biashara na uwekezaji  kutumia taaluma hiyo waliyoipata kwaajili ya kuleta manufaa kwa mataifa Yao.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi  Msaidizi Idara ya Elimu ya Juu ya Wizara ya Elimu ya Juu,  Dk.Jonathan Mbwambo kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo, Dk.Shukuru Kawambwa  wakati akifunga  Mafunzo hayo ya siku 14 yaliyoshirikisha maofisa wa juu wa fani ya biashara wa serikali za nchi nane ambayo yaliratibiwanna Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB) ambayo yalifadhiliwa na Chuo Kikuu Cha  Nordric Africa Institute, Uppsalla cha nchini Sweeden chini ya Profesa Francis Matambalya na kuwezeshwa na Taasisi ya TANAUP/PATU  chini ya Profesa Vale Karugaba.

Dk.Mwambo Alisema kwanza serikali  inakipongeza Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), kwa kuandaa Mafunzo hayo ambayo yameshirikisha maofisa wajuu wa serikali mbalimbali Kwani kupitia Mafunzo Hao maofisa Hao wameweza kubadilishana uzoefu wa masuala ya nchi zao kuhusu Sekta ya masoko na uwekezaji.

Dk.Mwambo alisema kila kukicha baadhi ya nchi za Africa zimekiwa zikigundulika kuwa na utajiri mkubwa aridhini na mfano mzuri ni nchi ya Tanzainia ambayo imegundulika kuwa ina nishati ya gesi , madini hivyo kupitia mafunzo hayo  kwa upande wa Tanzania  Wizara ya Viwanda na Biashara iliwakirishwa na maofisa wake Wawili wameweza kupata ujuzi ambao utaki saidia serikali ya kuweza kufanya vizuri Katika uandaaji wa masoko na uwekezaji wafanyabiashara wa Kimataifa watakaokuwa wanakuja kuwekeza nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), Profesa Costa Mahalu  Alisema UB,  nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zimekuwa  zikikabiliwa na matatizo  ya jinsi ya kuandaa masoko na kuandaa mikataba yenye tija na wawekezaji hivyo kupitia Mafunzo hayo yamesaidia kuwajengea uwezo washiriki kwenda kukabiliana na Changamoto hiyo.

Profesa Mahalu  Alizitaja nchi zilizoshiriki Katika Mafunzo hayo ya Kimataifa Kuwa ni wenyeji Tanzania, Kenya,Uganda, Burundi, Rwanda, Lesoto, Kongo, Malawi ,Ethiopia , Zambia na Madagascar.

Alisema UB Katika Mwaka mpya wa masomo    inaanza kutoa Shahada ya jinsi ya kujadili mikataba ya biashara na uwekezaji  ili iweze kuwajenga wanafunzi wengi wa Watanzania waweze kuwa bora katika eneo hilo la masoko na kuandaa mikataba ya kuiingia na wawekezaji katika sekta mbalimbali.

Kwa upande wake Profesa Francis Matambalya toka  Taasisi ya Nordic Africa  ya Chuo Kikuu Cha Uppsala, cha nchini Sweden ambao ndiyo waliofadhili Mafunzo hayo Alisema Kuwa yeye ni Mtanzania na anampenda nchi yake na ataakikisha kila Mara Taasisi hiyo ya Sweden inaleta Fedha kwaajili ya kuendesha Mafunzo hayo ili nchi za Tanzania na Africa kwa ujumla ziondokane na tatizo la kutokuwa na wasomi waliobobea Katika eneo Hilo la kuandaa masoko na jinsi ya kuandika mikataba na wawekezaji wa kigeni Katika sekta mbalimbali.

Naibu Waziri Fedha aifagilia UTT Microfinance

$
0
0
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba (wa pili kushoto), akikata utepe kuzindua rasmi Taasisi ya huduma za Kifedha ya UTT Microfinance, Dar es Salaam jana. Wa pili Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi Balozi Fadhili Mbaga na Mtendaji Mkuu wa UTT, Bw. James Washima (kushoto).
Naibu Waziri wa Fedha Bw. Mwigulu Nchemba (katikati), akimsikiliza kwa makini Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Kifedha ya UTT Microfinance, Bw. James Washima wakati akimuonyesha vipeperushi, Dar es Salaam jana.  Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi, Balozi Fadhil Mbaga.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kifedha ya UTT Balozi Fadhil Mbaga (kushoto) na Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo, Bw. James Washima wakimwangalia Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba.
 Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wakuu wa Taasisi ya kifedha ya UTT Microfinance, baada ya kukata utepe kuzindua taasisi hiyo, Dar es Salaam jana.



=========  ======= = =====

Naibu Waziri Fedha aifagilia UTT Microfinance

NAIBU Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali imevutiwa na utendaji kazi mzuri wa Taaisisi ya kifedha ya UTT Microfinance kuwa na matawi 10 katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa muda mfupi.

Akizungumza wakati wa kukata utepe kuzindua rasmi Taasisi hiyo Sukari House Dar es Salaam jana, Naibu Waziri amesema, Serikali imefurahishwa na dhamira ya kweli ya kufikisha huduma za kifedha karibu na wananchi kila pembe ya nchi kunakofanywa na UTT.

“Hii inaonyesha, mmeshaanza kutoa aina nane ya huduma kama mikopo, uwakala wa Bima, Uwakala wa Benki, uwakala  mkuu wa mitandao ya simu (mobile money super agent) kwa mwaka mmoja tangu kuanzishwa”.

Bw. Nchemba amesema, kazi kubwa iliyoifanya ndani ya muda mfupi na kuwa na matawi 10 katika maeneo mbalimbali ya nchi yameifurahisha na kuahidi kuwa Serikali itatoa ushirikiano wa karibu kwa taasisi hiyo ili iweze kufikia malengo iliyokusudia.

Naibu Waziri amebainisha kuwa uwa serikali iliamua kwa makusudi kuanzisha taasisi hiyo ili kuwezesha wananchi kiuchumii hususan wenye miradi, kama biashara ndogondogo na za kati ambao wamekuwa wakipata changamoto nyingi katika kupata mikopo na huduma nyingine za kifedha toka taasisi kubwa za kifedha na  mabenki ya biashara ambayo mara nyingi muundo na mfumo wa taasisi hizo huambatana na masharti magumu.

“Wengi walishindwa kupata mikopo stahiki kutokana na masharti, hususani wenye vipato vya chini, sharti la dhamana ya mali isiyo hamishika kama nyumba, kiwanja na mali, ambavyo hawana”, anasema Bw. Nchemba na kusisitiza kuwa Serikali imeanzisha UTT Microfinance kuchochea ukuaji wa uchumi na kuwainua watanzania walio wengi.

Awali kabla ya uzinduzi huo, UTT Microfinance imezindua rasmi mtandao wa matawi sehemu mbalimbali nchini kwa lengo la kufikisha huduma za kifedha karibu na wananchi hususan mikopo nafuu kwa wajasiriamaliri ambapo matawi 10 yaliyopo katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Mbeya, Mwanza na Zanzibar ulizinduliwa rasmi katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali, wakurugenzi wa mashirika, Makampuni na Taasisi mbalimbali pamoja na wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Mweneykiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya UTT MFI Balozi Fadhili Mbaga, alisema watahakikisha kuwa UTT MFI inatekeleza azma yake kwa ufanisi na pia itashirikiana kwa karibu na wadau mbalimbali.

“Tunapenda kusisitiza dhamira yetu ya kuendelea kushirikaiana na wadau mbalimbali hususan Tanzania Microfinance Association katika jitihada za jumla za kuwa na mfumo mzuri wa huduma za kifedha na mitaji midogo na kuhakikisha kuwa huduma hizi zinawafikia watanzania wengi zaidi na kuwa chachu muhimu ya maendeleo ya jamii yetu”, anasema Balozi Mbaga.

Ameishukuru serikali kwa ushirikiano inayotoa kwa taasisi hiyo na kuahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizo mbele yao kuhakikisha wanavuka malengo waliyojiwekea. ameiomba serekali isisite kuwaunganisha na wabia na washirika mbalimbali ili kuwa na mtandao mpana zaidi wenye nguvu ya kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa UTT MFI James Washima, alisema wanaamini Serikali haikufanya makosa hata kidogo katika kuanzisha UTT MFI, akiahidi kututumia uzoefu wao wa mwaka mmoja, ambao umebaini kuwa huduma za kifedha na mikopo hususan kwa wajasiriamali na watanzania wa kada za kati na chini zilisubiriwa kwa hamu kubwa sana.

Bw. Washima amesema kiu ya Watanzania kwa huduma za UTT hivyo taasisi yao imejipanga kutoa huduma nzuri. Ameahidi kuwa ndani ya miezi sita wataongeza idadi ya wafanyakazi kwani waliopo ni wachache ambapo mfanyakazi mmoja anahudumia wateja zaini ya 1,000.

 “Huu ni muitikio mzuri kutoka kwa jamii na sisi tunajitahidi kukabiliana nao kwa ufanisi” anabainisha Bw. Washima na kuongeza kuwa hivi sasa wana matawi 10,  manne yakiwa Dare s Salaam - Sukari House, Azikiwe, Kijitonyama na Chang’ombe.

Bw. Washima anayataja matawi mengine kuwa ni Arusha lililopo Ngarenaro, Meru lililopo Jengo la Posta Meru,  Dodoma lililopo Posta Dodoma, Mbeya barabara ya KKKT, Mwanza katika jengo la Posta na Zanzibar, Jengo la Posta Kijangwani.

Akizungumzia m,afanikio ndani ya mwaka mmoja wa uwepo wao, Bw. Washima anasema wameweza kukuza mtaji wa Taasisi toka  Shilingi billion 5.4 mnamo Julai mwaka 2013 na kufikia bilioni 12  Juni, 2014. Pia taasisi imefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani ya Tsh 5.316 bilioni, kwa wakopaji 6,102 – huku 84% ya wakopaji wote wakiwa ni wanawake.

Anabainisha kuwa pia wameanzisha huduma za moja kwa moja kwa muhusika (Tailor-made) kama vile mikopo kwa ajili ya Bima ya matibabu, Hati Malipo (Contract Financing loans), mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali wadogo wadogo (Group loans), Mikopo kwa ajili ya SACCOS, Mikopo maalumu kwa miradi inayolenga kuongeza thamani ya bidhaa na ajira ikiwemo viwanda vidogo vidogo, mikopo kwa wafanyakazi wa Serikali. 

Hata hivyo, pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana, Washima alieleza baadhi ya changamoto zinazowakabili ikiwa kuibuka kwa taasisi na kampuni zisizo rasmi ambazo hutoa huduma za kifedha hususan mikopo kwa watu wa kada za chini.

Mtendaji huyo amesema mengi ya makampuni haya mara huwa ya kilaghai na yenye kuchukua riba kubwa bila utaratibu maalum suala ambalo badala ya kuwasaidia watu, huwaumiza na kuwaua kabisa kiuchumi.

“Tunaiomba serikali iharakishe utungwaji wa sera ya kurasimisha huduma hizi ili zifanywe kwa utaratibu maalum na pia ziratibiwe na kudhibitiwa vizuri ili wananchi wasiendelee kutaabika na kufilisiwa na watu wasio na nia njema ambao hutumia fursa ya udhaifu wa kisera kujinufaisha” alisema Washima.

UTT MFI ni Taasisi ya huduma za fedha na mikopo iliyoanzishwa mnamo Juni 2013 kwa lengo la kutekeleza sera za serikali katika uwezeshaji kiuchumi hususan kwa wajarisiamali, watumishi wa umma, wakulima, wenye viwanda vidogo, watu wasio na ajira rasmi na wananchi wote kwa ujumla.

UTT MFI pia inalenga kuwapa fursa wamiliki wa Vipande vya UTT AMIS kutumia vipande vyao kama dhamana wakati wa kuchukua mikopo, kupanua wigo na kurahisisha uwekezaji wa vipande vya UTT na hivyo kukuza utamaduni wa kuwekeza kwa wananchi.

VIFAA VYA KUBAINI DALILI ZA AWALI ZA UGONJWA WA EBOLA KUPITIA JOTO LA MWILI VYAWASILI NCHINI, KUANZA KUTUMIKA VIWANJA VYA NDEGE.

$
0
0
 Picha inayoonyesha moja ya kifaa (kamera) nne zilizoagizwa na Serikali kupimia dalili za ugonjwa wa Ebola maeneo ya viwanja vya ndege. Kifaa  hicho kina uwezo wa kutunza picha na kumbukumbu za msafiri, muda , joto la msafiri, tarehe aliyoingia nchini pia uwezo wa kupata takwimu kutoka kwenye hali ya majimaji au jasho la Binadamu pindi kinapoelekezwa kwake.
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Kebwe Steven Kebwe akiongea na waandishi wa habari eneo la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati wa kupokea na kukabidhi vifaa vya kupima dalili za ugonjwa wa Ebola. Wengine ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Dharula na Maafa (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Cosmas Mwaifani. 
 Naibu Waziri wa Afya Dkt. Kebwe Steven Kebwe akiangalia kwa karibu taarifa zilizorekodiwa na moja ya kifaa (kamera) nne zilizoagizwa na Serikali kupimia dalili za ugonjwa wa Ebola maeneo ya viwanja vya ndege.Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.


=========  =======  ========


 Sehemu ya vifaa vya kubaini hatua za awali za ugonjwa wa Ebola kwa kupima hali ya joto la mwili kwa wasafiri kutoka nje nchi wanaotumia viwanja vya ndege  vilivyokuwa vimeagizwa na Serikali vimewasili jijini Dar es salaam.


Vifaa hivyo vinavyohusisha kamera 4 zenye uwezo wa kubaini joto la mwili wa msafiri kwa umbali wa mita 100 bila  kumgusa muhusika vimewasili leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam kutoka nchini Afrika ya Kusini vilikonunuliwa.


Akikabidhi vifaa hivyo kwa wataalam wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Kebwe Steven Kebwe amesema kuwa kuwasili kwa vifaa hivyo ni moja ya juhudi za Serikali za kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa salama kwa kuuzuia ugonjwa huo kuingia nchini.


Amesema vifaa hivyo vitapelekwa katika maeneo ya viwanja vya ndege na maeneo yanayotumiwa na raia wa kigeni kuingia nchini vikiwemo vya Dar es salaam, Zanzibar, Kilimanjaro,Mbeya na Mwanza.


Ameongeza kuwa Serikali inaendelea na mpango wa kuagiza vifaa zaidi vya kuwezesha shughuli ya upimaji wa afya kwa wasafiri wanaotembea (scanners) zitakazowezesha kubaini afya za wasafiri wengi zaidi kwa wakati mmoja bila kulazimu kuwasimamisha.


Aidha, amewataka wataalam hao wa afya kufanya kazi zao kwa weledi mkubwa kwa kuhakikisha wanawapima abiria wote wanaotoka nje ya nchi bila kujali hadhi walizonazo ili kuweza kubaini kama wana maabukizi au dalili za ugonjwa wa Ebola.


“Nataka mfanye kazi yenu kwa kuzingatia weledi wa taaluma yenu na kwa kuzingatia yale mliyojifunza,mvitumie vifaa hivyo kupima kila abiria ili kubaini joto lake bila kujali cheo wala hadhi yake maana janga hili ni kubwa” Amesema Dkt. Kebwe.


Kuhusu utunzaji wa vifaa hivyo amewataka wataalam hao kuhakikisha wanavitunza vifaa hivyo ili viweze kudumu na kutimiza malengo yaliyokusudiwa ya kuwasaidia wananchi kutokana na vifaa hivyo kugharimu fedha nyingi kila kimoja.


Katika hatua nyingine Mh. Kebwe amefafanua kuwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inaendelea na shughuli ya utoaji wa Elimu ya Afya kuhusu ugonjwa wa Ebaola ili kuwawezesha wananchi kuchukua tahadhari na kuzielewa dalili za ugonjwa huo na namna ya kujingika endapo utagundulika nchini.


Amesema tayari  kamati mbalimbali za wataalam zimeshaundwa ili kuwezesha zoezi la utoaji wa elimu na mafunzo kwa wataalam wa ndani ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na janga hilo.


Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa nchini (MSD), Cosmas Mwaifwani ambaye ofisi yake imehusika katika uagizaji wa vifaa hivyo nchini Afrika ya Kusini  amesema kuwa mahitaji ya vifaa hivyo kwa sasa yameongezeka kutokana na umuhimu wake na jinsi vinavyofanya kazi kwa ufanisi mkubwa.


Amesema upimaji kwa kutumia vifaa hivyo unatumia teknolojia ya kubaini mionzi ya joto kutoka katika mwili wa binadamu pindi vinapoelekezwa katika maeneo ya macho na masikio ya mwili wa binadamu.


Amefafanua kuwa vifaa hivyo vinauwezo wa kutunza picha na kumbukumbu za msafiri, muda , joto la msafiri na tarehe aliyoingia nchini na kuongeza kuwa vifaa hivyo vina uwezo wa kupata takwimu kutoka kwenye hali ya majimaji au jasho la Binadamu pindi kinapoelekezwa kwake.


Mwaifwani ameeleza kuwa MSD inaendelea kuimarisha uwezo wake kwa kuongeza vifaa zaidi kutoka Ubelgiji na China na kufafanua kuwa Bohari hiyo imejiandaa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola kwa kujenga uwezo wa kuwa na dawa za kutibu hali ya magonjwa yanayoambatana na homa hiyo.


Naye Mkurugenzi wa Viwanja vya ndege nchini, Moses Malaki akizungumza kwa niaba ya Viwanja vya ndege nchini ameielezea hali hiyo ya upatikanaji wa vifaa  katika maeneo hayo kuwa itaongeza ufanisi wa uchunguzi wa afya kwa wasafiri na kuondoa usumbufu kutokana na uwezo wa vifaa hivyo kumpima msafiri akiwa mbali.

WASANII WATAKAOTUMBUIZA TAMASHA LA FIESTA 2014 JIONI YA LEO JIJINI TANGA WAMJULIA HALI MZEE NJENJE NYUMBANI KWAKE SAHARE.

$
0
0
 Mwanamuziki Mkongwe hapa nchini,almaarufu kama Mzee Njenje akizungumza machache mbele ya wasanii mbalimbali wa bongofleva waliofika nyumbani kwake Sahare,nje kidogo ya jiji la Tanga,kumjulia hali kutokana na maradhi yake yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda sasa.

Mzee Njenje amewaasa wasanii hao ambao amekiri wazi kuwa wanafanya vizuri katika anga ya muziki wao,kupata muda mwingi wa kupumzika ikiwemo na suala la kutoendekeza masualaua ya anasa kama vile ulevi,ngono na mengineyo ambayo huchangia kuporomoka kwa wasanii wengi,amesema kuwa Muziki wa sasa una ushindani mkubwa hivyo kila msanii anapaswa kujituma kwa namna anayoona inafaa ili kutimiza malengo yake sambamba na kuitangaza nchi kwa ujumla.
 Wasanii wa Muziki wa Kizazi kipya,Rachael na Linah wakiwa wamepozi katika picha ya ukumbusho na Mzee Njenje.
 Msanii wa muziki wa Kizazi Kipya,Alli Kiba akizungumza jambo na Mzee Njenje. 
Mzee Njenje akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya watakaotumbuiza jioni ya leo kwenye tamasha la Fiesta 2014 linalofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga,Wasanii hao walikwenda kumsabahi mkongwe huyo wa Muziki hapa nchini,Nyumbani kwake Sahare,nje kidogo ya jiji la Tanga ambako ndiko anaendelea kupata matibabu yake ya maradhi yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda sasa,Mzee Njenje amesema kuwa kwa sasa anamshukuru Mungu anaendelea vizuri na afya yake inazidi kuimarika kadiri ya siku zinavyozidi kwenda.  
 Baadhi ya Wasanii mbalimbali ambao Watatumbuiza kwenye tamasha la Fiesta jioni ya leo ndani ya uwanja wa Mkwakwani ,wakiwasili nyumbani kwa Mzee Njenje,Sahare,nje kidogo ya jiji la Tanga kumjulia hali.

Rais Kikwete atawazwa kuwa chifu msaidizi wa waluguru na chifu kingalu huko kinole, morogoro, apewa jina la Chidukila

$
0
0
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14, akijiandaa kumtawaza Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Chifu Msaidizi wa kabila hilo katika sherehe za aina yake zilizofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi ya Kinole, kata ya Makuyuni, Morogoro vijijini Agosti 22, 2014.  Rais Kikwete pia alipewa jina la CHIDUKILA, lenye kumaanisha "muibukaji", kwa maana ya kwamba Rais Kikwete ana uhuru wa kuibuka kijijini Kinole bila taarifa wala kusubiri kualikwa.
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14, akijiandaa kumvika mgolole Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kumtawaza kuwa Chifu Msaidizi wa kabila hilo katika sherehe za aina yake zilizofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi ya Kinole, kata ya Makuyuni, Morogoro vijijini Agosti 22, 2014
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14, akimvika  mgolole Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kumtawaza kuwa Chifu Msaidizi wa kabila hilo
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14, akimvipa pama lililosukwa kwa ukindu  Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kumtawaza kuwa Chifu Msaidizi wa kabila hilo
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14, akimkabidhi kifimbo maalumu Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kumtawaza kuwa Chifu Msaidizi wa kabila hilo
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14, akimuonesha  Rais Jakaya Mrisho Kikwete namna ya kuweka kifimbo maalumu begani wakati wa kumtawaza kuwa Chifu Msaidizi wa kabila hilo
 Mke wa Chifu Kingalu akimkabidhi Mama Salma Kikwete shuka katika sherehe hizo
 Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila akifurahia wakati wa sherehe hizo
 Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila akifurahia kifimbo maalumu alichokabidhiwa wakati wa sherehe hizo
 Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila akiongea na wananchi wakati wa sherehe hizo
 Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila akihutubia  wakati wa sherehe hizo
 Umati wa wananchi ukimsikiliza Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila wakati wa sherehe hizo
 Hotuba ikiendelea 
 Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila akisikiliza maelezo Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Morogoro Injinia Juliana J. Msaghaa akieleza juhudi za upatikanaji wa maji safi na salama wilayani humo wakati wa sherehe hizo
 Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila  wakati wa sherehe hizo
  Chifu Msaidizi wa Waluguru Chidukila akifurahia pama lake wakati wa sherehe hizo
 CHIFU wa Waluguru Kingalu Mwanabanzi wa 14 akibadilishana mawazo na Rais Kikwete wakiwa na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli (kulia), Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe Joel Bendera na kushoto ni msaidizi wa Chifu Kingalu
 Mama Salma Kikwete akihutubia wananchi wakati wa sherehe hizo, akisisitiza umuhimu wa kinamama kujiunga na SACCOS pamoja na kupambana na ugonjwa wa Fistula kwa wakati muafaka
Rais Kikwete akiwaaga wananchi wa Kinole baada ya sherehe hizo.
PICHA NA IKULU

RAIS JAKAYA KIKWETE UZINDUA JENGO JIPYA LA SACCOS

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua pazia kuzindua jengo jipya la Chama cha Kuweka na Kukopa (SACCOS) cha kijiji cha Kinole, Morogoro vijijini Agosti 22, 2014
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akikata  utepe  kuzindua jengo jipya la Chama cha Kuweka na Kukopa (SACCOS) cha kijiji cha Kinole, Morogoro vijijini Agosti 22, 2014. Wengine ni Mama Salma Kikwete (kulia),  Mbunge wa Viti Maalum Dkt Lucy Nkya (wa [ili kulia) na Mwenyekiti wa SACCOS ya Kinole Mzee Issa Ramadhani Kambi
 Rais Kikwete akikagua jengo jipya la SACCOS ya Kinole baada ya kulizindua
 Rais Kikwete akiwa ameongozana na Chifu Kingalu na Mwenyekiti wa SACCOS ya Kinole Mzee Issa Ramadhani Kambi baada ya kuzindua jengo la chama hicho kijijini Kinole
 Rais Kikwete na Chifu Kingalu wakiwatuza wacheza ngoma vijana wa kijiji cha Kinole waliokuwa wakitoa burudani kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Rais Kikwete akimtambulisha Chifu Kingalu kwa Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014.
 Mama Salma Kikwete akiongea na baadhi ya kinamama kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Mbunge wa viti maalumu Dkt Lucy Nkya akiongea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Umati wa wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Joel Bendera akitoa muhtasari na kukaribisha wasemaji kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe Stephen Masele akielezea mikakati ya serikali ya kusambaza umeme vijijini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wananchi na kueleza mikakati ya serikali katika kuendeleza na kuboresha miundombinu nchini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Mbunge Mhe Innocent Kalogeris akiongea kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Rais Kikwete akiongea na mtoto Rebecca Mbena ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Kinole wakati wa  mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
  Mama Salma Kikwete  akiongea na mtoto Rebecca Mbena ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Kinole wakati wa  mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
  Mama Salma Kikwete  akiongea na mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Kinole wakati wa  mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014
 Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Chifu Kingalu  Mama Salma Kikwete  akiongea na mtoto Rebecca Mbena ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Kinole wakati wa  mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Kinole Agosti 22, 2014. PICHA NA IKULU

Real Madrid Legends yainyuka Tanzania 3-1

$
0
0
 Rais Jakaya kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Tanzania 11
 Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Real Madrid Legends.
 Luis Figo (kushoto), akiruka juu kupiga mpira wa kichwa.
 Hekaheka langoni mwa Tanzania.
 Mohamed Mwameja akiwa ameshika kiuno baada ya kufungwa goli la kwanza.

 Rais Jakaya Kikwete akifurahia jambo na kocha Msaidizi wa Tanzania 11, Jamhuri Kiwhelo 'Julio' mara baada ya mchezo.
 Kiungo wa timu ya Real Madrid Legends, Christian Karembeu akichukua picha ya kumbukumbu na Rais Jakaya Kikwete.

 
Nzuri sana........
Mfunga wa mabao ya timu ya Real Madrid, Reuben akipokea mpira baada ya kupiga 'hat trick' katika mchezo huo.
Beki wa timu ya Tanzania 11, Shadrack Nsajigwa akichuana na mshambuliaji wa Real Madriad Legends, Luis Figo wakati wa mchezo wa Kimatifa wa Kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Mshambuliaji wa timu ya Real Madriad Legends, Luis Figo akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa Tanzania 11 wakati wa mchezo wa Kimatifa wa Kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Mshambuliaji wa timu ya Real Madriad Legends, Luis Figo akimiliki mpira mbele ya beki wa Tanzania 11, Shadrack Nsajigwa wakati wa mchezo wa Kimatifa wa Kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
Rais Jakaya Kikwete akikabidhi kombe kwa mchezaji wa Real Madriad Legends baada ya kuibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Tanzania 11 katika mchezo maalum wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)


 Benchi la ufundi la Tanzania 11
 Luis Figo akisalimiana na wachezaji wa Tanzania 11.

 Peter Manyika akisalimiana na Luis Figo.

10 BORA YA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) WAVAMIA STUDIO ZA TIMES FM 100.5 FM JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Waendeshaji wa Kipindi cha Filamu Monata kinachorushwa na Kituo cha Redio cha TIMES FM 100.5 wakiendelea na majukumu katika studio za kituo hiko cha Redio Kilichopo Kawe Jijini Dar Es Salaam wakati wa Kipindi cha Filamu Monata leo wakati washiriki 10 Bora wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) walipotembelea Studio hizo 
Jaji wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) na Presenta wa Kipindi cha Filamu Monata cha TIMES FM, 100.5 Dar Es Salaam akiendelea na kipindi wakati washiriki 10 bora walipotembelea Kituo hiko leo kwaajili ya Mahojiano na waendeshaji wa Kipindi hiko.
 Mmoja wa Washiriki 10 Bora wa Tanzania Movie Talents (TMT) akijibu maswali kutoka kwa Waendeshaji wa Kipindi cha Filamu Monata kinachorushwa na Kituo cha Redio cha TIMES FM, 100.5 Dar Es Salaam.
Mshiriki Wa Tanzania Movie Talents (TMT) akijibu maswali.
 Washiriki 10 Bora wa Tanzania Movie Talents (TMT) wakiwa ndani ya Studio za TIMES FM, 100.5 Dar es Salaam.Picha Zote na Josephat Lukaza
Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) kufanyika tarehe 30 August 2014 katika Ukumbi wa Mlimani City kuanzia Saa 7.30 Usiku huku viingilio vikiwa Shilingi elfu 50 kwa VIP na Elfu 30 kwa kawaida
Burudani Kali kutolewa siku hiyo ya Fainali Huku Mc Pilipili akitoa burudani na Christian Bella

Rais Kikwete atunuku Kamisheni Kwa maofisa wapya wa Jeshi

$
0
0
Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa zawadi na kumpongeza luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe baada ya kuibuka mwanafunzi bora wakati wa hafla ya kuwatunuku kamisheni maafisa wapya 179 wa jeshi la Wananchi waliohitimu vyema mafunzo yao katika chuo cha Jeshi Monduli Mkoani Arusha jana.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitunuku kamisheni kwa maafisa wapya 179 wa jeshi waliohitimu vyema mafunzo yao ya muda mrefu katika chuo cha jeshi Monduli Mkoani Arusha jana.
Maofisa wapya wa Jeshi wakila kiapo mbele ya Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kuwatunuku kamisheni iliyofanyika katika chuo cha jeshi kilichopo Monduli Mkoani Arusha jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wapya wa jeshi baada ya kuwatunuku kamisheni katika sherehe zilizofanyika katika chuo cha jeshi Monduli mkoani Arusha jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe aliyeibuka mwanafunzi bora(Best Oficer Cadet Traineer Overall) wakati wa mafunzo ya muda mrefu ambapo maafisa 179 wa jeshi walihitimu vyema na kutunukiwa kamisheni katika chuocha jeshi Monduli jana.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mwanafunzi Bora katika kozi ya muda mrefu ya jeshi Luteni Usu Mohamed Ramadhani Mgalawe(watatu kushoto) pamoja na wazazi wake muda mfupi baada ya Rais Kuwatunuku kamisheni maofisa 179 wa jeshi katika chuo cha Monduli Mkoani Arusha jana.
Mtoto mdogo akimsalimia Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kumalizika kwa sherehe za kuwatunuku kamisheni Maofisa 179 wa jeshi katika chuo cha jeshi Monduli Mkoani Arusha jana. (picha na Freddy Maro)

Nakumatt wafungua Supermarket nyingine Arusha

$
0
0
Mwonekano wa Supermaket mpya ya mtandao wa maduka ya Nakumatt Holdings Ltd jijini Arusha baada ya kuzinduliwa jana kwenye eneo la TFA Arusha.
Mwonekano wa Supermaket mpya ya mtandao wa maduka ya Nakumatt Holdings Ltd jijini Arusha baada ya kuzinduliwa jana kwenye eneo la TFA Arusha.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC)Dk Richard Sezibera(kushoto) akiwa Mkurugenzi Mtendaji wa Nakumatt Holdings Ltd,Atul Shah akiangalia bidhaa mbalimbali kwenye Supermarket mpya ilifunguliwa eneo la TFA jijini Arusha.
Wafanyakazi wa duka jipya la Nakumatt jijini Arusha waki 'pose' kwa picha ndani Supermarket hiyo ambayo ni inaungezea hadhi mji wa Arusha ambao ni kitalii na taasisi za kimataifa.

‘MADINI HOUSE’ KUJENGWA ARUSHA, Kuwa na huduma za kibenki, Helkopita kutua moja kwa moja kituoni

$
0
0
Afisa Madini Mkaazi Tunduru Fredrick Mwanjisi (kushoto) akifurahia jambo wakati akimwongoza Katibu Mkuu Nishati na Madini Eliakim Maswi (wa pili kushoto) kutembelea eneo itakapojengwa ofisi ya Madini Tunduru. Wengine katika picha ni ujumbe wa Maafisa walioongozana na Katibu Mkuu na watumishi wa ofisi ya Madini Tunduru.
Jengo ambalo litatumika kama  Makao Makuu ya Ofisi ya Madini Kanda ya Ziwa Nyasa mjini Songea. Jengo hilo limenunuliwa na Wizara na litaanza kutumika mara baada ya ukarabati. Wengine katikati ni Kaimu MKurugenzi Idara ya Utawala Wizara ya Nishati na Madini, Caroline Msika na wengine ni maafisa wWizara ya Nishati na Madini na Maafisa wa Madini Kanda waliofuatana na Katibu Mkuu.
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Paul Masanja, (wa kwanza kushoto) akitafakari jambo mara baada ya kukagua kiwanja kitakapojengwa ofisi ya Madini ya Kamishna Mkaazi wa Madini, Nachingwea. Wa pili kushoto ni  Katibu Mkuu  Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, wa kwanza, wengine ni  Afisa Madini Mkaazi Nachingwea, Mhandisi Mayigi Makolobela (wa pili kulia) na wa kwanza kulia ni Mjiolojia kutoka ofisi ya Madini Mtwara.
=======   ========   =======

Na Asteria Muhozya, Songea
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Paul Masanja ameeleza kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini itajenga kituo maalum cha kuuza na kununua madini ya vito kutokana na nchi kuwa na hazina kubwa ya madini jambo ambalo pia litachangia katika kuyaongezea thamani madini hayo. 

 Masanja ameyasema hayo  mjini Songea wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Nishati na Madini Eliakim Maswi kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na wizara ikiwemo kuonana na Makamishna Wasaidizi wa Kanda, Maafisa Madini Wakaazi, Watumishi wa Shirika la Umeme Tanzania, kuangalia shughuli za wachimbaji wadogo wakiwemo wafanyabiashara wa madini na wawekezaji katika sekta ya madini. 

 Kamishna aliongeza kuwa, kituo hicho kitakuwa na huduma zote muhimu zikiwemo za kibenki ambazo zitawawezesha wachimbaji na wafanyabiashara kutokutafuta huduma muhimu zinazoendana na shughuli hizo nje ya kituo hicho. “Shughuli zote za uuuzaji na ununuzi madini ya vito na usonara zitafanywa katika kituo hicho. 

Kutakuwa pia na helkopita itakayotua moja kwa moja katika jengo hilo jambo ambalo litawezesha uwepo wa usalama katika biashara nzima ya kuuza na kununua madini,” alisisitiza Masanja. 

 Aidha, aliongeza kuwa, ili kuiwezesha sekta hiyo kupaa kwa kasi na kuchangia katika ukuaji wa uchumi, wizara imeamua kuanza kwa kuboresha ofisi za kanda za madini ikiwa ni pamoja na kununua maeneo maalum kwa ajili ya kujenga ofisi hizo ili kuboresha utendaji wa sekta ya madini nchini na kuwa na ofisi za uhakika. 

 “Tunataka kupitia sekta ya madini kuiwezesha serikali kuongeza mapato yake na kutoka hapa tulipo kiuchumi. Jambo hilo linawezekana ndio sababu tunaanza na kuboresha sehemu za kazi ili kuwawezesha watumishi kufanya kazi katika mazingira mazuri zaidi na kuongeza uwajibikaji,”aliongeza Masanja. 

Katika hatua nyingine, Kamishna Masanja amewataka Makamishna Wasaidizi wa Kanda na Makamishna Wakaazi walioteuliwa hivi karibuni kutimiza wajibu wao vizuri na kufikia lengo la makusanyo ambayo wizara imewapangia na kwa wale wasiotekeleza agizo hilo la makusanyo ndani ya kipindi cha miezi mitatu wataondolewa katika nafasi zao. 
“Tumeamua kupaa kupitia sekta hii, asiyeweza kutekeleza jambo hili kama tulivyokubaliana, tutamwondoa na kuwapa wengine wenye uwezo wa kufanya hivyo. Tunataka kufanya kazi kwa kasi na kisasa zaidi,” alisisitiza Masanja. 

Wakati huo huo, aliwata watumishi wote walioko katika ofisi za Kanda kuwa waadilifu, wawajibikaji, wawazi na wabunifu ili kuweza kutekeleza majukumu yao kikamilifu ikiwemo kufuata sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma. 

Vilevile, aliongeza kuwa, wizara imejipanga kuanza kutumia mfumo wa kieletroniki kuanzia mwezi Septemba kwa ajili ya waombaji wa leseni jambo ambalo litasaidia kurahisisha zoezi la uombaji wa leseni na kuondoa manungu’niko miongoni mwa waombaji.

WABUNGE WA CCM WAUNGURUMA HUKO MTERA MKOANI DODOMA

$
0
0
IMG-20140824-WA0005
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wananchi katika kijiji Iringa Mvumi Jimbo la Mtera mkoani Dodoma ambapo Chama cha mapinduzi kimeendelea kuuelimisha umma juu ya masuala ya Maendeleo, utekelezaji wa ilani, maandalizi ya uchaguzi wa serikali za vijiji na mitaa, bunge la katiba na mambo yanayohusu maendeleo ya katika vijiji na wilaya zetu. Pia kuwakumbusha juu ya thamani ya muungano wetu na vipengele muhimu vinavyojadiliwa ndani ya katiba.IMG-20140824-WA0006
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akiendelea kutema cheche katika mkutano huo.
IMG-20140824-WA0007
Umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo ukiwasikiliza wabunge mbalimbali wa Bunge la Jamhuri ya muungano ya Tanzania waliokuwa wanahutubia katika mkutano huo.
IMG-20140824-WA0008
Mbumge wa ji,bo la Sikonge Mh. Said Mkumba akiwahutubia wananchi katika mkutano huo.
IMG-20140824-WA0010
Wananchi wakisikiliza kwa makini Mbunge wa Chalnze Ridhiwani Kikwete alipokuwa akiwahutubia
IMG-20140824-WA0011
Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akiwahutubia wananchi wa jimbo lake katika kijiji cha Iringa Mvumi mkoani Dodoma.
IMG-20140824-WA0012
Mbunge wa Jimbo la Nkenge mkoani Kagera , Asumpta Mshana akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Iringa jimbo la Mtera jana nyuma ni mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde
IMG-20140824-WA0013
Baadhi ya wananchi wakiwa wamekaa kwenye mapaa y nyumba huku wakifuatilia kutano huo.
IMG-20140824-WA0014
Umati wa wananchi aliohudhuria katika mkutano huo.
IMG-20140824-WA0015
Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akiwahutubia wananchi wa jimbo lake katika kijiji cha Iringa Mvumi mkoani Dodoma.
IMG-20140824-WA0017
Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akipanda jukwaani kuwahutubia wananchi wa jimbo lake katika kijiji cha Iringa Mvumi mkoani Dodoma baada ya mbunge wa jimbo la Chalinze Mh Ridhiwani Kikwete kuwahutubia.
IMG-20140824-WA0019IMG-20140824-WA0020
Mbunge wa jimbo la Mtera Mh. Livingstone Lusinde akiendelea kutema cheche mbele ya wananchi wa jimbo lake katika kijiji cha Iringa Mvumi mkoani Dodoma.

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI AFANYA UTEUZI WA BARAZA LA MAWAZIRI, MANAIBU WAZIRI, WAKUU WA MIKOA NA WAKUU WA WILAYA .

$
0
0
Mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri na Uteuzi wa Naibu Waziri.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri na pia kumteuwa Naibu Waziri kama ifuatavyo-

(a) Mhe. Dkt. Sira Ubwa Mamboya ameteuliwa kuwa Waziri wa Kilimo na Maliasili akijaza nafasi ilioachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Suleiman Othman Nyanga.

(b) Mhe. Juma Duni Haji ameteuliwa kuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano akichukuwa nafasi ilioachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Rashid Seif Suleiman ambaye sasa anakuwa Waziri wa Afya.

 (c) Mhe. Rashid Seif Suleiman ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya akijaza nafasi ya Mhe. Juma Duni Haji ambaye sasa anakuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano.

(d) Mhe. Mahamoud Thabit Kombo ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Afya akijaza nafasi ilioachwa wazi na Mhe. Dkt. Sira Ubwa Mamboya ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Kilimo na Maliasili.

Na pia amefanya mabadiliko ya baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya.
Aidha, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amefanya mabadiliko ya baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya kama ifuatavyo:-

(1). Major Mstaafu Juma Kassim Tindwa ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Kaskazini Unguja akijaza nafasi ilioachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Bwana Pembe Juma Khamis.

(2). Bibi Mwajuma Majid Abdulla ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Kusini, Pemba akijaza nafasi ilioachwa wazi na Major Mstaafu Juma Kassim Tindwa ambaye amehamishiwa Mkoa Kaskazini, Unguja.

(3). Bwana Omar Khamis Othman ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, Pemba akijaza nafasi ilioachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Bwa. Dadi Faki Dadi.

(4). Bwana Ayoub Mohamed Mahmoud ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Magharibi akijaza nafasi ilioachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Bwa. Hassan Mussa Takrima.

(5). Bibi Hanuna Masoud Ibrahim ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake akijaza nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Bibi Mwanajuma Majid Abdulla ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Kusini, Pemba. Utezi huo umeanza leo tarehe 24 Agosti 2014.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI ZANZIBAR.

MAKANISA SINGIDA YAONYA MATUSI NA UBAGUZI BUNGENI

$
0
0
DSC00479
Askofu wa kanisa la Evanglist Assembels of God Tanzania (E.A.G.T) Singida mjini, John Mafwimbo akizungumza kwenye mkutano wa Injili uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi mjini Singida.Pamoja na mambo mengi, askofu Mafwimbo amewasihi wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, kufanya mambo waliyotumwa na Watanzania na si vinginevyo.

Na Nathaniel Limu, Singida
Makanisa ya Kipentekoste mkoani Singida, yameungana na Watanzania wengine kuwaomba wajumbe wa Bunge Maalum la kuandaa Katiba mpya,kujiepusha na mambo/vitendo ambavyo hawakutumwa na wananchi na badala yake washikamane na wavumiliane ili waweze kufanikisha kupatikana kwa katiba itakayoendeleza amani na utulivu uliopo nchini.

Makanisa hayo ambayo ni pamoja na Free Pentekoste Tanzania na Evangelist Assembles of God Tanzania (E.A.G.T.),yamedai kwamba matusi, dharau, ugomvi na kejeli za aina mbalimbali hazitachangia kupatikana kwa Katiba inayotarajiwa na Watanzania.
Wamedai vitendo hivyo, vitachangia pamoja na mambo mengine kubomoa umoja na undugu uliojengeka kwa miongo mingi na vitakaribisha vitendo viouvu kama vinavyofanywa na vikundi vya Boko haramu na Alshabab.

Akizungumza kwenye mkutano mkubwa wa injili uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi mjini Singida, Askofu wa E.A.G.T, John Mafwimbo alisema ni wakati sasa kwa waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini kufunga kwa ajili ya kufanya maombi kuliombea Bunge Maalum la Katiba,liweze kutekeleza yale yote waliyotumwa na Watanzania.
DSC00490
Mchungaji wa kanisa la Free Pentekoste Tanzania Singida mjini, Boniface Ntandu, akiwahubiria waumini wa madhehebu ya dini mbalimbali waliohudhuria mkutano wa injili uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi.

"Tuwaombee bila kuchoka wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,waweze kututengenezea/kutuboreshea vizuri Katiba na wala wasituchanganye,ili sisi huku waumini wa madhehebu ya dini na Watanzania wengine wasiokuwa na dini tuje tufanye uamuzi sahihi wakati wa kuipigia kura Katiba hiyo",alifafanua.

Akifafanua zaidi, Mafwimbo, alisema kazi ya wajumbe nikuwajengea Watanzania mazingira mazuri ili waje kupigia kura Katiba itakayokidhi mahitaji yao ya zaidi ya miaka 50 ijayo.
Kwa hali hiyo, Askofu Mafwimbo amewashawishi wajumbe hao kuimarisha utamaduni wa kuvumiliana, kupendana na kumaliza tofauti zao wao kwa wao.

"Niwakumbushe tu wajumbe wetu, kwamba Watanzania ni waumini wazuri wa amani na utulivu. Kitendo hicho kimeendelea kuchangia nchi yetu kupaa kimaendeleo na wakati huo huo, sisi waumini tunaendelea kuabudu kwa uhuru mpana bila usumbufu wa aina yo yote",alisema na kuongeza kwa kusema; "Endapo hatutapata katiba stahiki,tutakuwa tunakaribisha vurugu kama zile zinazofanywa na makundi ya boko haramu".
DSC00471
Moja ya kwaya zilizokuwa zikihubiri kwa njia ya nyimbo kwenye mkutano wa injili ulioandaliwa na mwimbaji wa nyimbi za injili mkoa wa Singida, Elineema Babu.
DSC00478
Baadhi ya waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini,waliohudhuria mkutano wa injili unaoendelea kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi mjini Singida.(Picha zote na Nathaniel Limu).

KAMPUNI YA MSAMA PROMOTION NA JESHI LA POLISI WAKAMATA KAZI FEKI ZA WASANII

$
0
0
1
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari kwenye kituo cha polisi cha Urafiki wakati akitangaza kukatatwa kwa watuhumiwa 17 wanaorudufu kazi za wasanii kinyume na utaratibu yaani kazi feki katika jiji la Dar es salaam na baadhi ya mikoa ambapo kazi feki za wasanii zilizokamatwa thamani yake ni shilingi milioni 12, Kulia ni ASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho ambaye amesema amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa 17 ambao wanasubiri kupelekwa mahakamani.
2
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na KAMASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho wakionyesha CD feki zilizokamatwa jijini Dar es salaam
4
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama na ASP Denis Moyo mkuu wa upelelezi wa kituo hicho wakionyesha CD feki zilizokamatwa jijini Dar es salaam
5Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua zaidi kuhusu wizi huo wa kazi a wasanii unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara na kuwanyonya wasanii.
6
Kituo cha polisi cha Urafiki

Madini Migodini yapo Salama- Maswi

$
0
0
1.  Meneja wa Kampuni ya TANCOAL  (wanne kulia) Tan Brereton  na  Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo Emmanuel Constantinides (wa tatu kulia) wakimwonesha Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi  na ujumbe wake namna shughuli za himbaji Makaa ya Mawe zinavyofanyika.

 Gari la kubeba kupakia Makaa ya Mawe likiendelea na kazi hiyo katika Mgodi wa Ngaka unaomilikiwa na kampuni TANCOAL.
 Mashine ya kusaga makaa yam awe katika viwango mbalimbali kulingana na mahitaji ya wateja ikiendelea na kazi ya kusaga mawe katika Mgodi wa Mkaa ya Mawe wa Ngaka unaomilikiwa kwa ubia na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na kampuni ya Australia.
 Gari la kubeba makaa ya Mawe katika mgodi wa Ngaka likimwaga makaa sehemu maalum kutoka mgodini kabla ya kusagwa katika viwango mbalimbali kulingana na mahitaji y wateja.
 
=======  ========  ======
Madini Migodini yapo Salama- Maswi
ØAeleza TMAA wapo kuhakiki   mwenendo wa uzalishaji,uuzaji
ØMwekezaji  asisitiza Makaa ya Ngaka yana ubora wa juu
Na Asteria Muhozya, Mbinga
Katibu Mkuu  wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi amewataka watanzania kuondoa dhana kuwa madini  yanayochimbwa katika migodi mbalimbali nchini yanaibwa  na wawekezaji wakubwa na kusisitiza kuwa, Wizara  kupitia Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), wapo katika migodi yote nchini kuhakikisha kwamba madini hayo hayatoroshwi .

Maswi  ameyasema hayo alipotembelea Mgodi wa kuchimba Makaa ya Mawe  wa kampuni ya  Tancoal eneo la Ngaka wilayani Mbinga inayomilikiwa kwa ubia kati ya Kampuni ya Australia na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) na kuongeza kuwa, TMAA wapo katika kila mgodi  kujua kiasi cha madini kinachochimbwa, kinachouzwa na kwa  ajili ya kuhakiki vyeti vya mauzo ya madini hayo kuhakikisha kuwa vinakwenda sambamba na kiasi cha mrahaba kinachotolewa na wawekezaji.

Kwa upande wake Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Paul Masanja alisisitiza hoja ya Katibu Mkuu Maswi na kuongeza kuwa, Wizara kupitia maafisa wa TMAA wamekuwa wakifanya ukaguzi kuhakikisha kwamba serikali inapata mrahaba stahili kupitia madini yanayouzwa na kutoa mfano kwa madini ya Makaa ya Mawe ya Ngaka kwamba serikali inapata asilimia 100 ya mrahaba.

“Nawapongeza sana TanCoal ni wasikivu, maafisa wa TMAA huwa wanafanya ukaguzi kila baada ya miezi mitatu kujua kiasi kinachozalishwa na kinachouzwa hivyo, tunakwenda nao vizuri,” alisisitiza Masanja.

Naye  Mkurugenzi wa Tancoal  Tan Brereton ameeleza kuwa,  mgodi wa wa Ngaka ni mradi mkubwa kwa Tanzania na kuongeza kuwa, uwepo wa mgodi wa makaa ya mawe wa Tancoal ni mafanikio na maendeleo makubwa kwa Tanzania kutokana na  kuwezesha ajira kwa wataalamu mbalimbali nchini ikiwemo serikali kupata kodi na mirahaba kupitia mgodi huo jambo ambalo litawezesha kuboresha huduma za kijamii.

Aidha, amezitaja faida  za nyingine za mgodi huo kuwa, uwepo wa Mgodi huo utawezesha Tanzania kuzalisha kiasi kikubwa cha nishati ya umeme kutokana na uwepo wa kiasi kikubwa cha makaa hayo katika mgodi wa Ngaka  na kueleza kuwa, makaa ya mawe kutoka katika mgodi huo yana ubora wa kiwango cha juu tofauti na madini yanayochimbwa nchini Afrika Kusini.

“Makaa ya Ngaka yana ubora wa hali ya juu sana tofauti na makaa ya nayochimbwa Afrika Kusini kwasasabu madini haya hayahitaji kusafishwa kabla ya matumizi tofauti na mengine ambayo husafishwa kabla ya kutumiwa ,alisisitiza Tan.

Aidha ameongeza kuwa,  kampuni hiyo ina uwezo wa kuzalisha kiasi cha tani  480,000  za makaa ya mawe kwa mwaka na kuongeza kuwa, tayari kampuni hiyo imesaidia huduma mbalimbali za kijamii katika maeneo ya afya,shule ,maji na kuwaendeleza vijana na kutumia zaidi ya shilingi milioni mia sita na kuongeza kuwa, kampuni hiyo imekwisha toa kiasi za bilioni 2 kama kodi na mrahaba  kwa serikali.

Kwa mujibu wa Tan, ameeleza kuwa, makaa yanayozalishwa na kampuni hiyo yanatumika katika viwanda vya  saruji vya Mbeya Tanga Lake,  kampuni ya METL na viwanda vya karatasi viwanda vya nguo.
 


Benki ya Exim yaijengea maliwato Shule ya Msingi Kilakala

$
0
0
 Mkuu wa matawi (Cluster Head) wa Benki ya Exim Tanzania, Bi Agnes Kaganda (wapili kushoto) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kilakala, Bw. Abdul Kuratasa kwapamoja wakifungua jiwe la msingi kuonyesha makabidhiano rasmi ya maliwato iliyojengwa na benki hiyo. Hafla hiyo ilifanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Wakishuhudia ni Kaka Mkuu wa Shule Seif Ahmed (wa kwanza kushoto), Dada Mkuu wa shule Naomi Shakila (wa kwanza kulia) na mlezi wa shule hiyo Dkt. Ellen Otaru (wa pili kulia). Na mpiga piga wetu.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kilakala, Bw. Abdul Kuratasa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa maliwato iliyokabidhiwa na Benki ya Exim Tanzania katika hafla iliyofanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. 
========  =======  ======

 
BENKI ya Exim Tanzania imekabidhi vyoo vya kisasa kwa Shule ya Msingi Kilakala iliyopo katika wilaya Temeke jijini Dar es Salaam ikiwa ni jitihada za benki hiyo kuboresha hali ya usafi na mazingira ya kujifunzia shuleni hapo. 

Ujenzi huo wa matundu kumi ya vyoo na mfumo safi wa maji ni moja kati ya miradi ya kimaendeleo iliyotekelezwa na kugharamiwa na Benki ya Exim Tanzania katika shule hiyo ya Kilakala iliyo chini ya benki tangu mwaka 2012 ikiwa kama benki mlezi.       

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano shuleni hapo jana Mkuu wa Matawi/Cluster Head wa Benki ya Exim, Agnes Kaganda, alisema benki yake imeamua kupiga jeki mradi huo ikitambua umuhimu wa usafi kwa afya ya wanafunzi na walimu na mchango wake katika maendeleo kitaaluma kwa shule hiyo.  
                 
“Shule ilikuwa na maliwato yenye matundu nane tu ikiwa na wanafunzi 2739. Kutokana na Benki ya Exim kuongeza matundu mengine kumi, tunaamini kuwa hali hii sasa italeta ahueni kwa wote, walimu na wanafunzi hapa shuleni,” alisema.

Alisema kuwa mbali na matundu hayo kumi, wavulana nao wana sehemu maalum ya maliwato ikiwa na maji yanayotembea ili kuiweka maliwato katika hali ya usafi muda wote.

“Tunaamini kuwa, kwa kuboresha hali ya usafi ya shule kutasaidia kuzuia wanafunzi haswa wasichana kutoruka vipindi vya masomo ili kutafuta vyoo visafi au wanafunzi kutoambukizwa magonjwa ya kuambukizwa. Hii itawasaidia wao kuelekeza zaidi jitihada zao katika masomo, na hivyo kuweza kufanya vizuri zaidi darasani,” alisema Kaganda.

Alibainisha kuwa sasa ni juu ya uongozi wa shule na jamii inayoizunguka shule kuhakikisha kuwa maliwato hiyo inatumika vizuri ili iweze kutumika na wanafunzi wengine wanaoweza jiunga na shule hiyo siku za usoni.

 “Ningependa kuuasa uongozi wa shule na wanafunzi kuhakikisha kuwa maliwato hii inatunzwa na inabaki kuwa safi. Lengo hili litatimia tu endapo tutaweza kuiweka maliwato yetu katika hali ya usafi,” aliongeza. 

Alibainisha kuwa Benki ya Exim imekuwa ikiibadilisha shule taratibu tangu ilipokuwa benki mlezi, ambapo sasa shule hiyo inajivunia kuwa na maktaba ya kipekee, wanafunzi wakisoma wamekaa kwenye madawati yaliyotolewa na benki, na sasa shule ina mfumo nzuri wa maji safi, vikitajwa kwa uchache. Miradi yote ikifadhiliwa na benki kama sehemu yashughuli mbali mbali za kijamii.

Naye, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Bw. Abdul Kuratasa alipongeza jitihada za benki katika kufuatilia maendeleo ya shule tangu ilipoichukua kama benki mlezi na kusema kuwa sasa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kilakala wanafurahia matumizi ya vifaa vya kisasa kama shule nyingine za binafsi. 

Alisema kuwa mchango huo wa maliwato ni moja kati ya hatua ambazo zinapaswa kuigwa na makampuni mengine ili kuboresha sekta ya elimu nchini.

“Naipongeza benki kwa jitihada zake kuhakikisha kuwa tunaboresha mazingira ya kujisomea ya shuleni hapa. Dhamira ya benki katika kusimamia maendeleo ya shule imekuwa thabiti tangu ilipoichukua shule yetu kuwa benki mlezi mnamo Agosti mwaka 2012.

“Tungependa kuishukuru Benki kwa kutujengea maliwato na tunahaidi kuwa tutaitunza vyema kwa ajili ya wanafunzi wengine katika siku za usoni,” alisema Bw. Kuratasa.

 
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images