Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

Rais Kikwete azindua Nyumba za gharama nafuu za NHC Mjini Songea

$
0
0
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi nyumba zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC huko Mkuzo, wilayani Songea mjini mkoani Ruvuma leo. Kutoka kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof.Anna Tibaijuka, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa Bwana David Misonge Shambwe, na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Said Mwambungu.
Ris Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua jiwe la msingi wakati wa ufunguzi wa nyumba zilizojengwa kwa gharama nafuu na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) huko Mkuzo wilayani Songea mjini Mkoani Ruvuma leo.Kushoto ni kaimu Mkurugenzi wa NHC Bwana David Misonge Shambwe na wwapili kushoto ni Waziri wa Ardhi Nyumba na makazi Prof.Anna Tibaijuka.(picha na Freddy Maro).

TONNY NGOMBALE MWIRU ASIMIKWA KUWA KAMANDA WA UVCCM

$
0
0
 Mjumbe wa kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi na Waziri  Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha akimsimika Tonny Ngombale Mwiru kuwa kama wa UVCCM kata ya Kijitonyama.
 Kamanda mpya wa Umoja wa Vijana kata ya Kijitonyama Tonny Ngombale Mwiru akiwapungia mkono wanachama wa CCM mara baada ya kusimikwa kuwa kamanda wa UVCCM kata ya Kijitonyama.
 Mjumbe wa kamati kuu ya CCM ambaye pia ni waziri kiongozi wa zamani wa SMZ Shamsi Vuai Nahodha,katibu wa UVCCM kata ya Kijitonyama Fatuma  Mgeni na kamanda mpya wa UVCCM  kata hiyo Tonny Ngombale Mwiru wakifuatilia jambo.
Kamanda mpya wa UVCCM kata  ya Kijitonyama Tonny Ngombale Mwiru akitoa nasaha mara baada ya kusimikwa kushikilia nafasi hiyo.

MKUTANO WA KUJADILI MASUALA YA KODI AFRIKA WAFANYIKA JIJINI ARUSHA

$
0
0
 Waziri wa fedha Saada mkuya akijadiliana jambo na rais wa kituo cha kimataifa cha ukusanyaji kodi na uwekezaji Daniel Witt wakati wa mkutano wa siku 3 wa majadiliano ya masuala ya kodi Afrika uliofanyika jijini Arusha jana katika hotel ya naura spring.
mkurugenzi mkuu wa TRA Rished Bade akizungumza wakati wa ufunguzi wa  mkutano wa siku 3 wa majadiliano ya masuala ya kodi Afrika uliofanyika jijini Arusha jana


 Picha ya pamoja
 vuiongozi wa kuu
 Waziri  wa Fedha Saada Mkuya akihojiwa na wanahabari.

waziri wa fedha Saada Mkuya katikati  akiwa na mkurugenzi mkuu wa TRA kulia Rished Bade na kushoto dr.Jeffrey Owens mtaalam msahuri wa kodi na mhadhiri chuo kikuu cha uchumi na biashara Viena mara baada ya waziri kufungua mkutano wa majadiliano ya masuala ya kodi unaofanyika jijini Arusha

WATUHUMIWA 17 WANAODAIWA KUJIHUSISHA NA VITENDO VYA UGAIDI WAPANDISHWA KIZIMBANI LEO

$
0
0
Baadhi ya watuhumiwa wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ugaidi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakisindikizwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), kuingia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Julai 17,2014 kusomewa mashitaka yao. Watuhumiwa 16 walisomewa mashitaka.PICHA NA PHILEMON SOLOMON  
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiimarisha ulinzi.
Watuhumiwa wakiingia ndani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Watuhumiwa wakipelekwa maabusu baada yakusomewa mashitaka yao.

AK CLASSIC COSMETICS WAMEWASHUSHIA TENA MZIGO MPYAA KABISA!

$
0
0




WALE MABINGWA WA COSMETICS ZA UKWELI KUTOKA MBELE MBELE, @AK CLASSIC COSMETICS  WAMEWASHUSHIA TENA MZIGO MPYAA KABISA!! KAMA KAWAIDA BIDHAA ZOOOTE  KUANZIA PRODUCTs ZA KUONDOA WEUSI KWAPANI, MAKE UPS,PRODUCTs ZA KUNG'ARISHA NGOZI ,MAFUTA YA KUNAKSHI NA  KUKUZA NYWELE (T444Z), BODY SHAPERs,..NA BIDHAAA ZINGINE LUKUKI MUPYAAAAAA!!EM TUONGOZANE HAPA..

 KWA MAELEZO YA KINA NA PICHA ZAIDI WATEMBELEE BLOGUNI www.akclassic.blogspot.com  KUWEKA ODA NA KUFIKISHIWA BIDHAA MPAKA ULIPO PIGA  0753-482909/0713-468393. 

WAPO KINONDONI KWA MANYANYA NA SINZA KUMEKUCHA.
PIA UNAWEZA KUWAFOLLOW INSTAGRAM @ak_classic_cosmetics

KARIBUNI SANA.

Betta -Hakulitambua (Official Music Video) Directed By Godfred

UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ZA UWEPO WA DAWA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI KATIKA SOKO

$
0
0

UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ZA UWEPO WA DAWA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI KATIKA SOKO
                        
Hivi karibuni kumekuwepo na taarifa zilizoripotiwa na gazeti la Tanzania Daima la kila siku kuhusu uwepo wa dawa zilizoisha muda wa matumizi kwenye duka la dawa la Core Pharmacy jijini Dar es Salaam. Taarifa hizi zimekuwa zikitolewa na mmiliki wa duka la dawa la Shine Care Pharmacy kwenye gazeti hilo. Baadhi ya dawa zilizotajwa ni Listerine antiseptic mouthwash, Pimple Gel, Misoprostol tablets 200mcg, Rabeloc IV 20mg, Mefenamic acidic tablets, Herpex – 800 DT, Inhaler 100 pg dose, Metformin Denk 850, Comprimes de carvediola 12.5mg na Cloderm cream.

Aidha, taarifa zimedai pia kuwa TFDA pamoja na kufahamishwa suala hili haikuweza kuchukua hatua zozote kwa mlalamikiwa.

TFDA inapenda kukanusha upotoshaji huo unaofanywa na chombo hicho cha habari kutokana na ukweli uliopo. TFDA ilifuatilia suala hilo na kubaini uuzwaji wa dawa moja tu ya Listerine antiseptic mouthwash (chupa 2) ambayo iliuzwa katika kipindi ambacho muda wake wa matumizi ulikuwa umebaki mwezi mmoja. Taarifa zinazoendelea kutolewa na gazeti la Tanzania Daima zinatokana na mgogoro uliopo baina ya makampuni mawili ya kuuza dawa ya Core Pharmacy na Shine Care Pharmacy.

TFDA inauhakikishia umma kwamba iko makini na ina mifumo madhubuti ya kufuatilia ubora, usalama na ufanisi wa dawa, chakula, vipodozi na vifaa tiba kwenye soko. TFDA inaviasa vyombo vya habari pia kufanya uchunguzi wa kina na kufika ofisini kwake ili kupata taarifa sahihi badala ya kutoa taarifa inazozipokea kutoka kwa wafanyabiashara.

Imetolewa na:-
MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA
EPI MABIBO EXTERNAL,
S.L.P 77150, DAR ES SALAAM
Simu: + 255 222 450512/450751/452108
Nukushi: + 255 222 450793
Barua pepe: info@tfda.or.tz

WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA WATAKIWA KUWA NA MTIZAMO MPYA UTAKAOWEZESHA UPATIKANAJI WA KATIBA MPYA

$
0
0
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Bw. Deus Kibamba akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo Julai 17, 2014 kuelezea msimamo wa JUKWAA LA KATIBA juu ya mwenendo uliopita wa bunge hilo. Picha na Cathert Kajuna wa Kajunason Blog
Kiongozi wa Shule Kuu ya Sheria nchini Kenya, Profesa Patrick Lumumba alisisitiza suala la wanasiasa kurudi bungeni na kuhakikisha katiba mpya inapatikana.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo.

 
Wajumbe wa JUKWAA LA KATIBA wakisisitiza jambo.
Na Hellen Kwavava, Dar es Salaam.
Ushauri Umetolewa kwa Wajumbe wa Bunge Maalum la katiba kuwa na Mtazamo mpya utakaoiletea nchi maslahi pindi watakaporudi bungeni katika mchakato wakutafuta katiba mpya unaotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao.
Hata hivyo kundi la Umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) limezidi kushauri wakirudi bungeni na kuendelea na majadiliano kwa msingi wa rasimu ya katiba.
Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam leo Julai 17, 2014 na mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Bw. Deus Kibamba ambapo ameeleza kwamba wabunge wanatakiwa kuachana na mtazamo wa kisiasa pamoja na lugha zisizo na staa kwenye bunge hilo kwani wanatakiwa kuzingatia uzalendo kwanza.
Aidha Bw. Kibamba amesema kwamba licha ya muda kuwa mfupi kuelekea katika uchaguzi wa mwaka 2015 wao wanapendekeza juhudi zaidi zifanyike ili kukamilisha upatikanaji wa katiba hiyo.
Naye Kiongozi wa shule kuu ya Sheria nchini Kenya Profesa Patrick Lumumba amewasihi wanasiasa wa nchini kuhakikisha katiba inapatikana kutokana na matakwa ya wananchi kwani nchini jirani zimekuwa zikiiga mambo mengi kutoka huku.
Bunge Maalum la katiba linatajiwa kuanza tena Agosti 5, 2014 mwaka huu.

KAMPUNI YA TAN COMMUNICATION MEDIA YAFUTURISHA JIJINI ARUSHA

$
0
0
IMG_3297
 Mkurugenzi wa Tan Communication Media  inayo miliki kituo cha  Radio 5 chenye makao yake makuu jijini Arusha  Bw Robert Francis wakati akiwa na wageni wake waalikwa mbalimbali wakipata iftari ya pamoja kwenye hafla hiyo,hafla iliyofanyika katika studio za redio hiyo zilizopo Njiro jijiniArusha iliyohudhuriwa na Viongozi wa dini na wadau wengine.IMG_3270
Sheikh Mkuu wa Bakwata mkoa wa Arusha,Shaaban Juma aliyekuwa mgeni rasmi katika halfa hiyo iliyoandaliwa na kampuni ya Tan Communication Media.IMG_3278
Mbunge wa Arusha Godbless Lema  wa pili kutoka  kushoto naye alihudhuria halfa hiyo.IMG_3325
Mchekeshaji  kutoka nchini kenya Peter Sankale maarufu kama “Olexander Jospat”katika igizo la VIOJA MAHAKAMANI akitoa burudani baada ya Futari.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Benki ya Exim yazindua mafunzo maalum kuongeza tija kwa wafanyakazi

$
0
0
 Mkuu wa kitengo cha Oparesheni wa Benki ya Exim Tanzania, Eugen Massawe (wapili kushoto) akikata utepe kuzindua mafunzo maalum kwa wafanyakazi wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Mwandamizi wa Mafunzo na Maendeleo wa kituo cha mafunzo cha Exim Academy, Bi Priti Punatar na Kushoto ni Beatus Temba, mkufunzi katika kituo hicho.
 Meneja Mafunzo na Maendeleo wa Exim Academy, Japheth Oyugi akiwafunza baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania wanaopata mafunzo hayo mara baada ya uzinduzi wa mafunzo maalum yatakayotolewa na kituo hicho cha mafunzo jijini Dar es Salaam jana.


Benki ya Exim Tanzania imezindua mafunzo maalum, yakiwa na lengo la kuwapatia maafisa wake wapya na wa zamani wa matawi mbali mbali wa benki hiyo ujuzi katika shughuli a kibenki za kimihamala na juu ya sera za udhibiti ili kuimarisha tija kwa wafanyakazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja.

Mafunzo hayo yatakuwa yakitolewa kwa wastani wa, masaa 56 ya mafunzo kwa maafisa mpya wa matawi mbali mbali ya benki, pamoja na masaa 160 kwa mafunzo yatakayokuwa yakiendelea ya darasani kwa maafisa wote wa matawi ya benki hiyo, kila mwaka.

Akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa mafunzo hayo uliofanyika katika kituo cha mafunzo ya benki ya Exim cha 'Exim Academy' jijini Dar es Salaam jana, Meneja Mwandamizi wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya Exim, Bi Priti Punatar alisema mafunzo hayo yanalenga katika kuboresha shughuli za matawi katika mazingira yaliyo salama na kupima ujuzi wa utatuaji wa matatizo mbali mbali bila kuwepo kwa viashirio vya majanga ambayo taasisi za kifedha ukumbana nayo katika dunia halisi ya masuala ya kibenki.  

"Leo tunazindua mafunzo maalum ambayo yatawapatia maafisa wetu wa benki katika matawi mbali mbali ujuzi katika shughuli za kibenki za kimihamala na juu ya sera za udhibiti.  

"Wafanyakazi wetu watapewa mafunzo juu ya majukumu mbalimbali katika tawi ili kuwajengea uelewa zaidi juu shughuli za kibenki na kuboresha za ujuzi wao katika biashara za masuala ya kibenki. Tunatarajia kuwa njia hii mpya itasaidia kuon geza ufanisi wetu katika shughuli zetu na kutuwezesha kufikia lengo la kufikia matakwa ya mteja, "alisema.

"Mafunzo haya yataongeza ufanisi  kwa wafanyakazi wetu na tija, na hivyo kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja," alisema Bw Eugene Masawe, Mkuu wa Kitengo cha  Uendeshaji katika Benki.

Alibainisha kuwa, mafunzo hayo yatawawezesha wafanyakazi kujifunza kwa vitendo, mbinu za kuthibitika zitumikazo katika sekta kwa kutumia vifaa vya kipekee, ikiwa pia inalenga katika kuboresha na kurahisisha taratibu mbali mbali za kibenki katika benki.

"Tumeanzisha mafunzo haya tukiwa na lengo si ​​tu kuongeza jitihada za kufikia matakwa ya mteja bali pia kutoa msaada bora wa huduma kwa wateja wetu wote na kuongeza ufanisi na kupunguza makosa yanayojitokeza ya  kibenki katika shughuli zetu za kila siku.

"Kupitia mafunzo haya, wafanyakazi wetu pia watakuwa na uwezo wa kutathmini na kukabiliana na majanga yanayohusiana shughuli za kimihamala za kibenki, kukidhi mahitaji ya udhibiti, kuhakikisha wafanyakazi wanatumia fursa zote za kimauzo zinazojitokeza, hivyo kuboresha utoaji huduma kwa wateja," aliongeza Masawe.

Pia alisema kuwa mafunzo hayo yataiwezesha benki yake kufikia malengo ya kuendeleza wafanyakazi wa benki hiyo  kwa kuwa na ujuzi wa uhakika katika masuala ya kibenki na utoaji wa huduma.

Exim Academy ni kituo cha mafunzo kilichothibitishwa kikiwa na cheti cha  ISO 9001:2008 kilichoundwa kwa ajili ya wafanyakazi wa Benki ya Exim ambacho utoa mafunzo tofauti yakiutendaji,  uongozi na utoaji wa huduma bora, na kujenga uhusiano nzuri na mteja kwa ujumla.

MBUNGE RIDHIWANI KIKWETE ATOA MSAADA WA KOMPYUTA JESHI LA POLISI JIMBONI KWAKE CHALINZE.

$
0
0
1A
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akizungumza na uongozi wa polisi Mkoa wa Pwani na Wilaya ya Kipolisi ya Chalinze pamoja na wananchi waliojitokeza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa mbalimbali kwa jeshi hilo zikiwemo kompyuta, mifuko ya Saruji pamoja na fedha vilivyotolewa na mbunge huyo, Kwa ajili ya kutatua matatizo mbalimbali yanayolikabili jeshi la polisi katika utekelezaji wa majukumu yake ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao. 

Pamoja na kukabidhi kompyuta hizo zitakazosaidia katika utunzaji wa kumbukumbu pia mbunge huyo ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi vya Mbwewe na Kiwangwa ambavyo thamani inafikia zaidi ya shilingi milioni 11, Kushoto kwake ni Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei, hafla ya makabidhiano hayo imefanyika jana kwenye kituo kikuu cha polisi Chalinze.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-CHALINZE)
1
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete kompyuta Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Kamanda ACP Ulrich Onesphory Matei zilizokabidhiwa na mbunge huyo kwa ajili ya kuboresha shughuli za jeshi hilo jimbo la Chalinze katikati ni Mkuu wa kituo cha polisi Chalinze Afande J. S. Magomi.
2
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akikata utepe kufungua ili kuonyesha kompyuta hizo huku viongozi wa jeshi hilo mkoani Pwani na jimbo la Chalinze wakishiriki shghuli hiyo.
3
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimuonyesha moja ya kompyuta Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei.
4
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei wakati alipokuwa akitoa shukurani zake kwa niaba ya jeshi la polisi mkoani Pwani mara baada ya kukabidhiwa kompyuta hizo , katikati ni mkuu wa ituo cha polisi cha Chalinze Afande J.S Magomi.
5
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Chalinze Mzee Bw. Kamis Kameza wakati alipokuwa akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa shule hiyo ambayo inajengwa na jeshi la kujenga taifa JKT kambi ya Ruvu.
6
Baadhi ya wanajeshi wa kambi ya JKT Ruvu wanaoshiriki katika ujenzi wa shule hiyo.
7
Moja ya madarasa ya shule hiyo ambayo yako katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wake.
8
Baadhi ya madarasa na maktaba ya shule hiyo yakiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi wake.
9
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na wanafunzi wa darasa la saba wa shule ya msingi ya Chalinze Mzee wakati alipokagua ujenzi wa shule hiyo.
10
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akiendelea kufanya ukaguzi wa ujenzi shuleni hapo kushoto ni Diwania wa kata ya Bwilingu Chalinze Bw. Ahmed Nasser.
11
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikweteakikagua ujenzi wa Maktaba ya shule hiyo akiwa ameongozana na Diwani wa kata ya Bwilingu Ahmed Nasser mbele na Mwalimu mkuu wa shule hiyo Khamis Kameza.
12
Baadhi ya wananchi waliohudhuria wakati wa hafla kukabidhi kompyuta kituo cha polisi Chalinze.
13
Diwani wa kata ya Bwilingu Chalinze Bw. Ahmed Nasser akizungumza wakati mbune wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete alipolokabidhi jeshi la polisi kompyuta kwa ajili ya kuboresha shughuli za jeshi hilo.

SHIRIKA LA MADINI LA TAIFA (STAMICO) LAFUNGA UPOKEAJI WA MAOMBI YA NIA (EXPRESSION OF INTEREST)

$
0
0
Ndunguru-3
SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) leo linafunga upokeaji wa maombi ya nia (expression of interest) ya makampuni yanayotaka kuingia ubia na STAMICO katika uendelezaji wa mradi uchimbaji makaa ya mawe na ufuaji umeme huko Kiwira.STAMICO ilitangaza mwezi uliopita kukaribisha maombi hayo yatakayowezesha ubia huo kupata fedha za kughramia mradi kwa asilimia 100 na kushiriki kuendesha mradi huo. 

Makampuni yenye nia ya kuwekeza kwa ubia na STAMICO yalitakiwa kuwasilisha maelezo ya kutosha kuhusu makampuni hayo pamoja na uthibitisho wa uzoefu wa kuendesha migodi ya makaa ya mawe na ufuaji umeme kwa kutumia makaa ya mawe.Makampuni hayo pia yanatakiwa kuonesha uzoefu wao katika kuendesha miradi kama hiyo sehemu nyingine Duniani ikiwemo nchi za Afrika.Aidha STAMICO inayataka makampuni yenye nia kuonesha uwezo wake wa kifedha na kiufundi. 

Maombi ya makampuni hayo pia yanatakiwa kuonesha namna gani yatakavyotumia utaalamu na huduma za ndani kama ilivyoainishwa kwenye Sheria ya Madini ya mwaka 2010.Makampuni ambayo maombi yake yatakubaliwa na STAMICO yatakaribishwa kuchukua nyaraka za zabuni na kuwasilisha michanganuo yao ya kiufundi na kifedha.Uendelezaji wa mradi Kiwira umegawanyika katika sehemu nne ambazo ni upanuzi wa mgodi uliopo wa chini ya ardhi, ujenzi wa mgodi wa wazi, ununuzi na ufungaji wa mitambo ya kufua umeme na ujenzi wa njia za kusafirisha umeme. 

Upanuzi wa mgodi wa chini utakaoongeza uzalishaji wa makaa ya mawe kutoka tani 150,000 kwa mwaka hadi tani 300,000 kwa mwaka wakati mgodi mpya wa wazi unategemea kuzalisha tani milioni 1.2 za makaa ya mawe kwa mwaka.Uendelezaji wa mradi huu pia utahusisha ujenzi wa mtambo wa kufua umeme wa Megawati 200 na ujenzi wa njia ya kusafirisha yenye urefu wa km 100 toka eneo la Kiwira Wilayani Ileje hadi Mbeya mjini.Ujenzi wa mgodi wa Kiwira ulianza mwaka 1983 na kukamilika 1988 kwa gharama za Sh.4.29 bilioni, ukiwa ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. 

 Mwezi Juni, 2005 mgodi wa Kiwira ulibinafsishwa kwa kampuni ya Tan Power Resources (TPR) kwa asilimia 70 na Serikali ilibaki na asilimia 30.Ubia huu ulilenga zaidi katika kuzalisha umeme wa MW 200 kwa kutumia makaa ya mawe ifikapo 2009.Katika kipindi cha kuanzia Juni, 2005 hadi Julai,2009 zilifanyika kazi mbalimbali za kuendeleza mgodi huu. 

Miongoni mwa kazi hizo ni upembuzi yakinifu na usanifu wa mgodi, upembuzi yakinifu kwa ajili ya kufua umeme wa MW 200 na kusainiwa kwa mkataba wa mauzo ya umeme wa MW 200 na TANESCO mnamo mwezi Agosti 2006.Kazi nyingine ni kusainiwa kwa mikataba ya ujenzi na utengenezaji wa mitambo, kukamilika kwa tathmini nne za mazingira na kukamilika kwa upimaji wa njia ya umeme ya kV 220 kutoka eneo la mgodi kwenda Mbeya. 

Mwezi Julai,2009 Serikali iliamua kuurudisha mgodi wa Kiwira Serikalini kwa asilimia 100 kutokana na kukwama kwa uendelezaji wa Mgodi chini ya TPR na kushindwa kuwalipa wafanyakazi mishahara yao kwa muda mrefu tangu mwezi Agosti,2008.Baada ya majadiliano ya muda mrefu, tarehe 28, Novemba 2011 Serikali na TPR zilifikia muafaka wa Serikali kuuchukua mgodi kwa asilimia 100. 

Mtaji unaohitajika kuendeleza mgodi huu ni takriban Dola za Marekani Milioni 400 ambazo zinaweza kupatikana kwa njia mbili;kwa kumtafuta mbia mwenye uwezo wa fedha au kwa kukopa katika taasisi mbalimbali za fedha.Aidha STAMICO inaangalia uwezekano wa kufanyia ukarabati mashine ya kufua umeme ya MW 6 iliyopo katika mgodi huu ili umeme utakaozalishwa uuzwe TANESCO.Katika mwaka wa fedha 2014/15, Serikali imeitengea STAMICO Shs. bilioni 5 kwa ajili ya usimamizi na uangalizi wa mgodi katika kipindi hiki cha mpito.

Airtel yaja na 'Tourist pack' yashusha gharama za simu na Intaneti kwa Watalii

$
0
0
 Wakwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Bw, Sunil Colaso akifuatiwa na  Meneja Masoko wa Airtel bi, Prisca Tembo ,na Mwenyekiti wa shirikisho la  wadau wa Utalii Tanzania Bwana Gaudence Temu , wakionyesha vifurushi vya bidhaa mpya ya Airtel Tourist Pack , wakati wa uzinduzi wa kifurushi hicho kitakacho wawezesha watalii kuwasiliana na familia zao mara wawapo nchi katika utalii, uzinduzi hu umefanyika leo katika makao makuu ya Airtel Daressalaam
 Mkurgenzi mtendaji wa Airtel Tanzania bw, Sunil Colaso akionyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) kifurishi chenye vocha maalum na laini ya Airtel kwaajili ya watalii wanaoingia nchini kitakachojulikana kama Airtel Tourist pack, uzinduzi huo umefanyika leo  ambapo Watalii watakaofaidika ni wale wanaotoka Amerika, India, Italia na Uingereza kufaidika na 'Airtel Tourist pack'


*        Watalii toka Amerika, India, Italia na Uingereeza kufaidika na 'Airtel Tourist pack'
*        Airtel yapunguza gharama za kupiga simu na intaneti kwa watalii  toka Amerika, India, Italia na Uingereeza

Dar es Saalam, Juni 17, 2014, Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imekuja na ubunifu mpya wa bidhaa itakayojulikana kama AIRTEL TOURIST PACK maalum kwa wageni/watalii wanaotembelea nchini toka mataifa mbalimbali ikiwa ni muendelezo wa Airtel kuendelea kutoa huduma bora ya mawasiliano nafuu kwa kuwaweza kuwasiliana na ndugu na familia zao wawapo kwenye utalii wao.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Bw, Sunil Colaso alisema" Huduma hii mpya ya "Vifurushi vya watalii" itapunguza usumbufu kwa mtalii/mgeni kukosa mawaliano bora ya simu au Intaneti awapo katika sehemu mbalimbali ya vivutio vya utalii nchini.

Ni imani yangu kuwa wageni watafurahia huduma hii kutokana na ubora wa mawasilano ya Airtel hasa katika maeneo ya pembezoni mwa miji ambako ndiko vivutio vingi vya utalii vinakopatika.

"Kifurushi hiki cha watalii kitakuwa na muda wa maongezi  wa dakika 30 za kupiga simu za nje, dakika 10 za kupiga simu za ndani ya nchi, SMS 10 kwenda mtandao wowote ndani na nje ya nchi pamoja na kifurushi cha intaneti cha 1GB vitakavyodumu kwa muda wa siku 30" alieleza Bw, Colaso

Kifurushi cha watalii Airtel Tourist Pack pia kinakuja na Laini ya simu na vocha ambapo, hii ni kwa yule mteja ambae hana laini ya Airtel au anataka kujiunga na kufaindika na huduma

Mtumiaji wa "Kifurushi cha watalii" Airtel Tourist pack atatakiwa kusajili namba yake pale tu anapofanya manunuzi kwa kutoa kitambulisho au pasi ya kusafiria.  Usaliji huo utakuwa wa muda kwa siku 30 na baada ya hapo mtalii atatakiwa kutoa kopi ya kitambulisho au pasi ya kusafiria kwaajili ya usajili wa kudumu.

Huduma hii ya vifurushi kwa wageni wakutoka nje ya nchi kwa simu ni ya kwanza kutoka Airtel na inampatia mteja uhuru wa kuwasilina  na ndugu jamaa na marafiki nyumbani kwa gharama nafuu zaidi kuliko ilivyokuwa awali, wateja watafurahia huduma za internet kwa kujiunga na mitandao ya kijamii, kutuma picha na video kwa gharama nafuu wakati wote . Aliongeza Colaso

Kwa upande wake mgeni rasmi, Mwenyekiti wa wadau wa Utalii nchini Bw, Gaudence Temu alisema "kwa niaba ya wadau wote wa utalii, ninaipongeza sana Airtel kwa kuanzisha huduma hii ya vifurushi vya mawasiliano kwa watalii wanaoingi nchini. Huduma hii inaendana na mahitaji ya wageni wetu na inakwenda sambamba na dhamira yetu sisi wadau ya kuendelea kutoa huduma bora katika soko.

"kwa kupitia mtandao wa Airtel ulioenea zaidi maeneo ya vijijini wageni wetu sasa watakuwa na uhakika wa mawasiliano bora na kwa gharama nafuu wakati wote" alieleza Bw, Temu

Mwenyekiti huyo pia alitoa ushauri kwa wadau wote wa biashara ya utalii kuchangamkia fulsa hiyo kwa kuwajulisha wageni wanaoingia nchini ili waweze kufaidika na punguzo hilo ambalo kwa msimu huu wa utalii hutumia gharama kubwa katika mawasiliano.

"Migahawa na Hoteli, wadau wa usafirishaji, watembezaji watalii na wadau wote hii ni fulsa kwetu kuwapa habari njema wateja wetu wanapoingia nchini kwamba kuna Tourist pak yenye faida zote hizi" alimaliza kwa kusema Bw, Temu

Vifurushi vya watalii zitapatikana katika maeneo yote ya biashara katika maeneo ya kuingia nchini kama zile viwanja vya ndege vya Dar es saalam(JKIA), Zanzibar, Arusha na KIA. Pia zinapatikana katika hoteli na migahawa ya kitalii.

Nchi zitakazofaidika na huduma hii kwa sasa ni pamoja na Amerika, India, Italia na Uingereeza

MANGULA AKUTANA NA KATIBU MKUU WA CAPP JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip Mangula akimkaribisha Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan kwenye ofisi Ndogo za CCM Lumumba.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip akiwa kwenye mazungumzo na Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan kwenye ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam,Julai 18,2014.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip Mangula akiagana na Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan
Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip Mangula akiagana na Balozi wa Sudani nchini Tanzania Dk.Yassir Mohamed Ali nje ya Ofisi Ndogo za CCM Lumumba ambapo Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) alikuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan.(Picha na Adam Mzee wa CCM Blog)

KIKUNDI KAZI CHA SERIKALI ZA MITAA CHA POLICY FORUM CHATOA TAMKO LAKE JUU UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

$
0
0

 Mwenyekiti wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa kilicho chini ya Taasisi ya Policy Forum,Bw. Hebron Mwakageda (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutoa tamkoa lao la Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotaraji kufanyika mwaka huu.
Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Policy Forum,Bw. Israel Ilunde akifafanua jambo wakati mkutano huo na Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutoa tamkoa lao la Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotaraji kufanyika mwaka huu.Kulia ni Mwenyekiti Mwenza wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa kilicho chini ya Taasisi ya Policy Forum,Bi. Regina Katabi.

Mradi wa bomba la gesi asilia kukamilika kama ilivyopagwa - Profesa Muhongo

$
0
0
 Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe Joseph Simbakalia akimkaribisha Waziri wa Nishati na Madini pamoja na ujumbe alioambatana nao akiwemo balozi wa China nchini Bw…. Mara baada ya kufika ofisini kwake kuelezea uwepo wapo katika mkoa huo
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe John Simbakalia  akimweleza Waziri wa Nishati na Madini jambo linalohusu sekta ya umeme ambapo Prof. Muhongo anaisimamia ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
 Mkandarasi anayehusika na usambazaji wa umeme vijijini Bwana  Luta (mwenye shati nyeupe), mara baada ya kusimamishwa na Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo ili kuelezea maendeleo aliyoyafikia katika kukamilisha mradi huo kulia kwake ni Mkurugenziwa Huduma za Ufundi (REA) Injinia Bengiel H. Msofe.
 Prof Muhongo na balozi wa China wakikgua mtambo wa kuchujia maji uliopo katika maeneo ya makazi ya watumishi ambao utawasaidia wananchi wanaozunguka eneo hilo kupata huduma ya maji safi na salama. 
 Waziri wa Nishati na Madini na ujumbe wake wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba za kuishi watumishi wa mtambo wa kufua gesi lililopo katika eneo la Madimba Mkoani Mtwara
Baadhi ya nyumba zitakazotumika kwa kuishi watumishi wa eneo la kuchakata gesi Madimba ni nyumba za kisasa zilizojegwa kwa ubora mkubwa sana kama zinavyoonekana.
--------------------------
Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo akiambatana na Balozi wa China nchini Dk. Lu Youging wamefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bomba la gesi linalotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa watanzania na hivyo kuchangia kuiingiza nchi kati ya nchi zenye uchumi wa kati ifikapo 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari balozi alisema ziara za kukagua bomba la gesi zinalenga katika kuhakikisha kazi inayofanyika ni bora na ipo katika viwango vinavyotakiwa na kuifanya nchi yake kuwa sehemu ya mradi na maendeleo ya nchi.
Kwa upande wake Prof. Muhongo amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo na kukiri kuwa kila mara afanyapo ziara kwenye miradi hiyo anakuta mabadiliko makubwa yanayomfanya kufurahia juhudi ya wakandarasi itakayopelekea mradi kukamilika kwa wakati uliopagwa mezi desemba 2014.
“Jamani ni nani walikuwepo tulipokuwa tukikabidhiwa eneo hili kwa ajili ya kuanza mradi? Eneo hili lilijaa mikorosho tu, lakini sasa tunaona kazi kubwa ya ujenzi iliyofanywa na wakandarasi hawa.
Aidha Muhongo alipotakiwa kueleza manufaa watakayoyapata wananchi wa Lindi na Mtwara alishangaa kuona kuwa bado watu hawaoni manufaa hayo na kuwaeleza waandishi wa habari kutosubiri yeye ndio aseme wakati wao wenyewe wanashuhudia wananchi wakipata ajira, huduma za jamii zikiboreka, wakipewa kipaumbele katika masuala ya elimu.
Hata hivyo Muhongo amewaeleza wanamtwara kuwa wasitegemee manufaa ya kuwepo kwa rasilimali ya gesi ni kuwagawia pesa aidha wanatakiwa kujiendeleza kielimu na kutumia fursa zinazojitokeza ikiwa ni pamoja na ufadhili wa masomo vilivyo ili waweze kujikwamua kimaisha na kushiriki katika kunufaika na gesi iliyogunduliwa katika eneo lao.
Akizungumzia suala la kukamilika kwa mradi huo msimamizi wa ujenzi wa bomba hilo Injinia Balthazar Mrosso alisema limekamilika kwa asilimia 70 na maeneo yaliyosalia ni yale yanayohitaji umakini mkubwa ikiwa ni pamoja na maeneo yanayoathiriwa na mafuriko pembezoni mwa mto wa Ruvu ambako kazi ya kuchimba mashimo ili kufukia mabomba hayo inaendelea, maeneo yenye miinuko na madaraja.
Akielezea suala la kukamilika kwa miradi ya kusambaza umeme vijijini Prof. Muhongo amesema miradi yote nchini inatakiwa kukamilika ifikapo juni 2015 na kuagiza mkandarasi asiye na uwezo wa kufanya hivyo kurudisha mradi huo apewe mtu mwenye uwezo.

Muhongo alimtaka mkandarasi Luta kuelezea hatua aliyofikia katika kusambaza umeme huo katika mkoa wa Mtwara ambapo alieleza kuwa suala la kusafisha mkuza limekamilika pamoja na kusambazwa na kusimikwa kwa nguzo kwa eneo Fulani. Aidha Mkandarasi Luta alimhakikishia Profesa Muhongo kuwa mradi huo utakamilika kwa wakati.
Akitanabaisha nia ya dhati ya kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati Muhongo alisema kuanzia mwezi huu hadi mwezi Oktoba atakagua miradi yote ya REA II na kwa wakandarasi watakaoonesha kutoridhisha kupokonywa miradi. “Hatutasubiri kufika mwezi juni ndipo tuanze kufukuzana na kukamilika kwa miradi mpaka desemba wakandarasi watakaoonesha kuzubaa watapokonywa na kupewa mtu mwingine awe mzawa au mgeni” alisisitiza Muhongo.
Tangia kuanza kutekelezwa kwa mradi huo mkubwa wa Bomba la gesi hii ni mara ya tatu kwa profesa Muhongo kuzungukia maeneo hayo kujionea jinsi kazi inavyofanyika na kukiri kufurahishwa na kasi ya wakandarasi hao.

WAZIRI LAZARO NYALANDU AKUTANA NA BALOZI WA HESHIMA WA UTALII BEVERLEY, LOS ANGELES MAREKANI

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Heshima wa Utalii wa Tanzania nchini Marekani Bw. Ahmed Issa (kushoto) na Bw. Abdul Majid baada ya kupokea taarifa ya mikakati wanayoitumia kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania kwa wamarekani jana Beverly, Los Angeles.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kulia) akiagana na Balozi wa Tanzania wa Heshima wa Utalii nchini Marekani Bw. Ahmed Issa mara baada ya kumaliza mazungumzo juu ya masuala kadhaa ya kuvutia Watalii wa Marekani nchini Tanzania jana Beverly, Los Angeles.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kulia) akizungumza na  Balozi wa Heshima wa Utalii wa Tanzania nchini Marekani Bw. Ahmed Issa juu ya mikakati mbalimbali ya kuvutia watalii wa kimarekani kutembelea Tanzania jana Beverly, Los Angeles.

Mikakati inayotumiwa na Balozi wa Heshima wa Utalii wa Tanzania Bw. Ahmed Issa kutangaza utalii ni pamoja na matumizi ya magari yenye picha za vivutio vya utalii wa Tanzania katika majiji mbalimbali katika California - Marekani kama inavyoonekana katika picha.

MFALME WA REGGAE JHIKOMAN ADATISHA KATIKA INTERNATIONAL AFRICAN FESTIVAL TUBINGEN,UJERUMANI

$
0
0
Tubingen,Ujerumani, Mwanamuziki maarufu wa reggae barani Afrika Jhiko Manyika aka Jhikoma kutoka Bagamoyo,Tanzania,alifanikiwa kuwadatisha akili washabiki wa muziki nchini ujerumani siku ya alhamisi 17 julai 2014 katika maonyesho makubwa ya kimataifa 5th International African festival Tubingen 2014,yanayofanyika katika viwanja vya Festplatz,mjini Tubingen,Ujerumani. 

Mwanamuziki huyo nguli wa reggae amepewa heshima zote za kimataifa kwa uwakilishaji wake kama balozi wa reggae wa Afrika.ratiba ya maonyesho hayo inaonyesha kuwa Jhikoman atapanda tena jukwaani siku ya jumapili 20.Julai 2014 jioni kwa ajili ya maombi maarumu ya washabiki waliotaka kumuona tena mflame huyo wa reggae.

 Pia taarifa zimetosha kuwa jumamosi 19 julai 2014 saa 2.00 usiku FFU-Ughaibuni aka Ngoma Africa band watatumbuiza katika maonyesho hayo. www.jhikoman.com

Waziri wa Mazingira atoa onyo kali kwa kiwanda cha NIDA Textile Mills Ltd kwa kukiuka taratibu za usafi

$
0
0
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk. Binilith Mahenge (mwenye shati la drafti) akipiga picha maji yanayopita kwenye mto Kibandu kutoka kiwanda cha NIDA Textile Mills Ltd.Kulia ni Diwani wa Kata ya Kigogo Richard Chengula.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk.  Binilith Mahenge (kulia) akipiga picha bomba linalotiririsha maji machafu kutoka kiwanda cha NIDA kilichopo Kigogo Mkuyuni jijini Dar es Salaam, 
 Bomba linalotiririsha maji machafu kutoka kiwanda cha NIDA kilichopo Kigogo Mkuyuni jijini Dar es Salaam, 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk. Binilith Mahenge (katikati) akiongozwa na Meneja Mkuu wa NIDA Textile Mills Ltd Imran Lohya kupanda kwenye tenki la maji yanayutumika na kiwanda hicho.

Kairuki: Wananchi tumieni wasaidizi wa kisheria kutatua migogoro

$
0
0
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Jasmine Kairuki akiongea na waandishi wa habari katika mkutano wa majumuisho ya ziara yake ya siku tano katika taasisi zinazotoa msaada wa kisheria jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo imemalizika leo (Ijumaa, Julai 18, 2014). Wengine ni Wajumbe wa Bodi ya Sekretarieti ya Msaada wa Kisheria (LAS) Dkt. Hellen Kijo-Bisimba (kulia) na Bi. Theodosia Muhulo.
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images