Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

VIJANA WALIOFADHILIWA MASOMO YA UFUNDI VETA NA HELP FOR UNDERSERVED COMMUNITIES INC. (HUC) WAHITIMU

0
0
 NI FURAHA TELE. Mwalimu wa kozi fupi wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma (VETA) – Dar es Salaam, Bi. Bertha Ogwal, kushoto, akimkabidhi Bi. Jamila Mwenda, ripoti ya mahudhurio ya kozi ya awali ya usekretari/kompyuta, hivi karibuni. Jamila ni miongoni mwa vijana 11 toka mikoa mbalimbali nchini waliofadhiliwa masomo na shirika lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC), lenye makao yake Marekani, ambalo linayosaidia upatikanaji wa maji safi na salama ya visima, maktaba za kijamii na ufadhili wa masomo ya ufundi. (Picha zote na Nathan Mpangala wa HUC).
 Mkuu wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma (VETA) – Dar es Salaam, Bw. Samuel Ng’andu wa pili toka kushoto, akimkabidhi cheti ya mafunzo ya awali ya ufundi magari, Yasini Musa hivi karibuni. Yasin ni mmoja wa vijana waliopata ufadhili toka shirika lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC). Wengine katika picha ni Msajili wa kozi Bi. Violet Fumbo na Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji na Kozi fupi Bw. Rocky Mongi.
 Kijana Joseph Mboya (kulia) akilamba ganda lake la ufundi magari toka kwa Mkuu wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma (VETA) – Dar es Salaam, Bw. Samuel Ng’andu, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
 Mwalimu wa Umeme wa magari wa Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Huduma (VETA) – Dar es Salaam, Bw. Saidi Mbwana, akimkabidhi cheti ya mafunzo ya awali ya umeme wa magari, Bi. Neema Bungara jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Neema ni mmoja wa vijana  11 waliopata  ufadhili wa masomo ya ufundi toka shirika lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC).


HAKIKA WAKIWEZESHWA WANAWEZA. Bi. Neema Bungara akionesha ganda lake lililosheheni ‘A’ tupu. Neema ni mmoja wa vijana 11 waliopata ufadhili wa masomo ya ufundi toka shirika lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC). 

ZAIDI BOFYA  LINKS HIZI HAPA CHINI.

SHULE YA JAMII YA WAMAASAI WILAYANI HAI YAPIGA MAENDELEO YA KASI

0
0
 Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akihutubia wazazi,wanafunzi na wageni waalikwa katika siku ya shule ya The O'Brien School for the Maasai.

Siku maalumu ya shule ya msingi ya mchepuo wa kiingereza kwa watoto wa jamii ya Kimaasai iliyopo katika kijiji cha Sanya Stesheni wilayani Hai ya The O'Brien School for the Maasai
  Sehemu ya wageni kutoka nchini Marekani waliohudhuria sherehe za siku ya shule ya msingi ya mchepuo wa kiingereza ya O'Brien ya Hai
 Diwani wa kata ya Kia,Sinyoki Ole Nairuki akiwatambulisha wageni mbalimbali katika sherehe za siku ya shule ya O'Brien.
 Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga na mfadhili Bibi Kellie O.Brien wakishuhudia shughuli mbalimbali za siku ya shule ya msingi ya O'Brien.
 Wanafunzi wa shule ya O'Brien wakitoa burudani
  Sehemu ya akinamama wa Kimaasai waliohudhuria shule ya siku ya shule ya The O'Brien School for the Maasai
Buruduni mbalimbali za ngomba za asili zikiendelea.

Rais Kikwete aapisha Balozi mmojA na Wajumbe wanne wa Tume ya Operesheni Tokomeza

0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amemwapisha balozi mmoja pamoja na wajumbe wanne wa Tume ya Operesheni Tokomeza katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo mchana.Balozi aliyeapishwa ni Mhe. oseph Edward Sokoine ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.Wajumbe walioapishwa nia pamoja na Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Mstaafu Hamisi Amiri Msumi,Jaji Mstaafu Steven Ernest Ihema,Jaji Mstaafu Vincent Damian Lyimo pamoja na katibu wa tume hiyo Bwana Frederick Kapela. Pichani Balozi Joseph Edward Sokoine akila kiapo,kupokea miongozo ya kazi na kupongezwa na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
  Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete. akimkabidhi Balozi Joseph Edward Sokoine  miongozo ya kazi
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete. akimpongeza Balozi Joseph Edward Sokoine
Wajumbe wa Tume ya operesheni Tokomeza wakiwakatika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal(Wanne Kushoto) na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue(Wapili kulia) wajumbe hao kutoka kushoto ni Katibu wa Tume hiyo Bwana Frederick Kapela Manyanda, Jaji Mstaafu Vincent Damian Lyimo(wapili kushoto), Jaji mstaafu Hamisi Amiri Msumi(Watatu kushoto), na Jaji Mstaafu Steven Ernest Ihema(kulia),Wasita kushoto ni  Balozi Joseph Edward Sokoine. Picha na Freddy Maro

CHINA NA TANZANIA ZAZINDUA UJENZI WA JENGO LA TAASISI YA MWALIMU NYERERE JIJINI DSM

0
0
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (kushoto) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (kulia) kwa pamoja wakizindua jiwe la msingi katika eneo litakapojengwa jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (katikati) na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (wa pili kulia) kwa pamoja wakimwaga mchanga kuashiria kuanza kwa ujenzi jengo la Taasisi ya  Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.Kulia ni Balozi wa China nchini Tanzania Lu Youqing.
 Viongozi mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Mama Maria Nyerere, Rais Mstaafu wa Wawamu ya tatu, Benjamini Mkapa,Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya na Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye (kulia) kuhusu picha ya mfano ya mwonekano wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere pindi litakapokamilika.
 Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu, Benjamini Mkapa (kushoto) na Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF).
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (wa pili kushoto) akisalimiana na Mama Maria Nyerere mara baada ya hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) jijini Dar es salaam wakishuhudiwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao ( kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda, Mama Maria Nyerere, Rais Mstaafu wa awamu ya Pili Ali Hassan Mwinyi na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa.
 Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao ( kushoto) akisalimiana na aliyekuwa Rais wa Bunge la Afrika, Balozi  Getrude Mongella wakati wa hafla ya uzinduzi wa jingo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa akisalimiana na Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi (Kulia) na Mama Maria Nyerere wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere.
Viongozi mbalimbali waliohudhuria uzinduzi wa jengo la Taasisi ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Mama Maria Nyerere, Rais Mstaafu wa Wawamu ya tatu, Benjamini Mkapa,Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya na Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba.Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
  Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao (wa pili kushoto) akiwa  na mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda (katikati), akiwasili eneo litakapojengwa jengo la Taasisi ya wa Mwalimu Nyerere karibu na bandari jijini Dar es salaam.

Mama Kikwete apewa Zawadi ya Kinyago

0
0
 Mkrugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi za jamii(SSRA) Bibi Irene Kisaka akimkabidhi zawadi ya kinyago cha mpingo Mke wa Rais Mama Salma Kikwete kwa kutambua mchango wake katika kumsaidia Mh.Rais katika jitihada zake za kujenga utawala bora nchini katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere(JNICC) jijini Dar es Salaam jana usiku(picha na Freddy Maro).

WADAU WAKUTANA LEO KUJADILI UTAYARI WA TANZANIA KATIKA KUPOKEA NA KUTUMIA FEDHA ZA KUPAMBANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

0
0
 Meneja Mradi wa Mazingira UNDP, Helene Gichenje akifafanua jambo kwa wadau wa mazingira wakati wa mkutano wa kujadili ripoti ya awali juu utayari wa Tanzania katika kupokea na kutumia fedha za misaada za kupambana na mabadiliko ya tabianchi
Msimamizi wa masuala ya mabadiliko ya tabinachi wa UNDP, Abbas Kitogo akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa kujadili ripoti ya awali juu utayari wa Tanzania katika kupokea na kutumia fedha za misaada za kupambana na mabadiliko ya tabianchi
Baadhi ya wadau wa mazingira waliohudhuria mkutano wa kujadili ripoti ya awali juu utayari wa Tanzania katika kupokea na kutumia fedha za misaada za kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

 Meneja Miradi wa Forum CC, Fazal Issa akifuatilia mjadala




Mtaalamu wa masuala ya mabadiliko ya tabianchi Damian Kasmiri, ambaye alikuwa mwezeshaji katika mkutano huo akifafanua baadhi ya masuala kwa wadau wa mazingira
Picha zote na tabianchi blog

MAKAMU MWENYEKITI WA CCM (BARA) PHILIP MANGULA AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA CHINA LI YUANCHAO

0
0
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Ndugu Philip Mangula akimkabidhi zawadi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa  China Li Yuanchao mara baada ya kumaliza mkutano .
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa  China Li Yuanchao akionyesha zawadi aliyopewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula mara baada ya kumaliza mkutano baina ya viongozi wawili.
 Viongozi wa CCM wakiwa kwenye mkutano wa Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa  China Li Yuanchao(hayupo pichani) kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa China Nchini Tanzania Lu Youqing akifafanua jambo wakati wa Semina ya Ujamaa iliyohusisha CCM na CPC kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula akizungumza wakati wa Semina inayohusu Umuhimu wa Ujamaa na Kukua kwa Uchumi,wengine pichani(kushoto) ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Abdala Bulembo ,Mwakamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM Mboni Mhita ,Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM Ndugu Sixtus Mapunda ,Profesa Max Muya ,na Makwaia wa Kuhenga.
 Mr Ma Zhongji kutoka Ubalozi wa China akisaidia kutafsiri wakati wa Semina ya Ujamaa iliyohusisha CCM na CPC iliyofanyika kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maafisa kutoka CCM Makao Makuu wakifuatilia kwa makini Semina inayohusu Umuhimu wa Ujamaa katika Kukua kwa Uchumi iliyofanyika katika ukumbi wa Kivukoni,Serena Hotel Dar es Salam.
 Mheshimiwa Kingunge Ngombale Mwiru akizungumza na Waandishi wa Habari nje ya Hotel ya Serena jijini Dar Es Salaam  na kuwaeleza kuwa Watu wanajenga Ujamaa wenyewe haujengwi na Viongozi peke yao.

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kukamilika kwa Semina inayohusu Ujamaa iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ambapo Mangula liwaeleza waandishi hao kuwa Ujamaa unatakiwa Ueleweke,Utekelezwe na Uendelezwe,Semina hiyo iliwahusisha vyama vya CCM na CPC kutoka China.

Waziri mkuu Pinda ahudhuria mkutano wa benki ya dunia,awataka wajasiriamali walioko katika sekta isiyo rasmi kurasimisha biashara zao.

0
0
 Waziri Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Pinda akizungumza na waandishi wa habari  nje ya Hotel ya Serena ambapo alihudhuria Mkutano wa Tano unaohusu masuala ya Uchumi,kulia kwake ni mkurugenzi wa benki ya Dunia nchini Ndugu Philippe Dongier
 Mkurugenzi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Philippe Dongier akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa kivukoni Serena Hotel jijini Dar es Salaam, akiwa pamoja na Mwandishi wa Mada Ndugu Jacques Morisset ambapo aliwaeleza waandishi hao Tanzania ina nafasi kubwa ya kupanua wigo wa ajira kwa kutengeneza mazingira ya kufanyia kazi yenye ubora hasa kwenye  miji inayokuwa kwa kasi hii itasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa Vijana na Wanawake.
 Mkurugenzi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Philippe Dongier akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa kivukoni Serena Hotel jijini Dar es Salaam, akiwa pamoja na Mwandishi wa Mada Ndugu Jacques Morisset ambapo alikiri pamoja na kukua kwa uchumi lakini bado uchumi haujafungua au kutengeneza ajira kwa wananchi .
 
Na Benedict Liwenga-MAELEZO. 
WAZIRI Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Pinda amesema kuwa wakati umefika wajasiriamali nchini wanaoendesha shughuli zao katika sekta isiyo rasmi kuboresha shughuli zao ili waweze kuzirasimisha kwa ajili kuboresha maisha yao na Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Pinda amesema hayo jana (leo) jijini Dar es salaam wakati wa Uzinduzi wa taarifa ya Hali ya Uchumi wa Tanzania-Toleo la Tano iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Dunia.

Taarifa hiyo inalenga kutoa Sera na hatua za kuchukua kuwezesha kupanuka kwa biashara katika miji na majiji nchini kwa ajili ya kuongeza ajira zaidi kwa wananchi na hasa vijana. 

Aidha, Mheshimiwa Pinda alitoa wito kwa vijana nchini kujiajiri katika sekta mbalimbali kama vile kilimo na kukiendesha katika mfumo ulio rasmi ili kiweze kuwakomboa katika maisha yao na kuwasaidia kupata ajira.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Burundi na Uganda Bwana Philip Dongier ametoa wito kwa watunga Sera nchini kuweka msisitizo katika kuendeleza ukuaji wa viwanda ili kutengeneza idadi kubwa ya ajira mpya na zenye tija kwa wananchi.

Bwana Dongier aliongeongeza kuwa changamoto nyingi zinazowakabili wajasiriamali wadogo katika kusaka ajira ni fursa zinazotokana na mchakato wa kupanuka kwa haraka kwa miji huku makisio ya hivi karibuni yakionesha kwamba ifikapo mwaka 2030 watanzania wengi watakuwa wakiishi mijini kuliko vijijini.

Taarifa ya Hali ya Uchumi ambayo huchapishwa mara mbili kwa mwaka na Benki ya Dunia inaeleza kwamba kuna uwezekano wa uchumi wa Tanzania kuendelea kukua asilimia 7 kwa mwaka. 
 
 

RAIS KIKWETE ATAJA MISINGI MIKUU MITANO YA UTHIBITISHO WA KUSHAMIRI KWA UTAWALA BORA NCHINI

0
0


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone:255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametaja misingi mikuu mitano ambayo utekelekezaji wake unathibitisha kushamiri kwa utawala bora nchini.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa pamoja na kwamba utawala bora unaendelea kushamiri nchini, bado taasisi za usimamizi wa masuala ya utawala bora zina nafasi ya kuboresha kazi yao na kupanua kwa kiasi kikubwa zaidi utawala bora.

Rais Kikwete aliyasema hayo usiku wa jana, Jumatatu, Juni 23, 2014, wakati alipozungumza baada ya kuwa ametunukiwa Tuzo ya Kutambua Mchango Wake wa Kuimarisha Utawala Bora nchini ambayo imetolewa na taasisi nane za usimamizi nchini.

Taasisi hizo ni Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCB), Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Jamii (SSRA), Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACCGen-D), Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (IAG-D) na Sekretarieti ya Tume ya Maadili.

Hiyo ni mara ya kwanza kwa Tuzo hiyo kutolewa nchini na ilikabidhiwa kwa Rais Kikwete wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa kwa ajili ya wajumbe wa Mkutano wa Mwaka wa Wakaguzi wa Hesabu za Serikali kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) mjini Dar Es salaam.

Mkutano huo wa mwaka pia unahudhuriwa na wajumbe waalikwa kutoka nchi za Ujerumani, Afrika Kusini, Uganda, Sweden, Sierra Leone, Nigeria, Niger, Ghana, Kenya, Zambia, Rwanda, Burundi na Ethiopia. Akizungumza baada ya kukabidhiwa Tuzo hiyo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Bwana Ludovick Utoh, Rais Kikwete alisema kuwa Tanzania ina utawala bora kwa sababu inadumisha misingi yote mikuu ya utawala bora.

Aliitaja misingi hiyo kuwa ni kushamiri wa demokrasia, uhuru wa kutoa maoni na wa vyombo vya habari, haki ya kila Mtanzania kuishi, utawala wa sheria, kutoingiliana kwa mihimili mitatu ya Serikali.

Rais Kikwete ambaye amesema kuwa amepokea Tuzo hiyo kwa niaba ya viongozi wenzake katika Serikali – Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Katibu Mkuu Kiongozi, Makatibu Wakuu na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama – amesema kuwa utawala bora ni jambo muhimu na halina mbadala wake.

“Tanzania tumeruhusu uhuru mkubwa kwa wananchi wetu kushiriki katika shughuli zao. Serikali yetu haitishi watu wake. Hatufanyi hivyo. Ziko nchi zinaishi kwa kutisha raia wake na nyie mnazijua, “alisema Rais Kikwete.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM



24 Juni, 2014

RAIS KIKWETE ATUA MALABO, EQUTORIAL GUINEA, KUHUDHURIA MKUTANO WA 23 WA UMOJA WA AFRIKA

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili mji mkuu wa Equatorial Guinea wa Malabo leo Juni 24, 2014 kuhudhuria Mkutano wa Umoja wa Africa –African Union (AU).

Akiwa Malabo, Mheshimiwa Rais Kikwete pia atakuwa Mwenyekiti wa kikao cha wakuu wa nchi wanachama wa AU kitakachojadili mazingira. Rais Kikwete na ujumbe wake anatarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa wiki.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Waziri Mkuu wa Equatorial Guinea Mhe Vicente Ehate Tomi alipowasili  katika katika uwanja wa ndege wa Malabo, Equatorial Guinea, leo Juni 24, 2014
PICHA NA IKULU
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa katika uwanja wa ndege wa Malabo, Equatorial Guinea, leo Juni 24, 2014

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM.

DKT BILAL AZINDUA SHEREHE ZA KIJADI ZA WASUKUMA WILAWANI MAGU MKOA WA MWANZA

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhiwa Usinga na wazee wa kijiji cha kisesa wilayani Magu baada ya kusimikwa kuwa kiongozi wa kabila la wasukuma na, wakati wa Sherehe za kijadi na maadhimisho ya siku ya ngoma na nyimbo za kabila la kisukuma zilizofanyika Wilayani magu mkoani Mwanza jana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipiga  Ngoma  kuashiria uzinduzi wa Mashindano ya Ngoma na Nyimbo katika Maadhimisho ya Tamasha la Jadi la Wasukuma  kwenye Uwanja wa Kisesa Wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza jana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsalimia Mtoto  fredrik  Emmanuel  Mara Baada ya Kumalizika kwa Sherehe za Uzinduzi wa tamasha la Ngoma na Nyimbo za Kabila la wasukuma zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kisesa Wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza jana
 Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha kisesa mkoani mwanza, Wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.  Mohammed Gharib Bilal,  alipokua akiwahutubia  kwenye Uzinduzi wa Mashindano ya Ngoma na Nyimbo za kabila la kisukuma zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kisesa Wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza jana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia Ngoma ya Kabila la Wasukuma wakati wa Tamasha la siku ya Bulabo  zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kisesa Wilayani Magu Mkoa wa Mwanza jana. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.  Mohammed Gharib Bilal, akiagana na wananchi  wa kijiji cha kisesa baada ya kuzindua  Mashindano ya Ngoma na Nyimbo za kabila la Wasukuma zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kisesa Wilayani  Magu Mkoni Mwanza jana .

FILAMU MPYA YA KISWAHILI ILIYOCHEZWA NCHINI UHOLANZI KUINGIA MTAANI HIVI KARIBUNI

0
0
Filamu mpya ya kiswahili iliyochezwa nchini Uholanzi chini ya Director mpya Hija Salehe.Filamu yenye mafunzo,ucheshi na vingi vihoja ndani ya wasanii wapya wenye mvuto na ujuzi mwingi ndani yake.tazama kibwagizo tu kidogo uhondo unakuja hivi karibu.Jina la filamu ni NIMPENDE NANI Kutana na wasanii wenye makeke kama Omary Abbas,Khatib Mustapha,Nicolas Gabino,Mrembo anayekubalika Sonia Kasuka,Shamim Sudi,na wengine kibao ambao ni gumzo katika filamu hii mpya ya kiswahili.

TANZIA: KIPA WA KIVULE VETERAN AFARIKI DUNIA

0
0

 Marehemu Kipa Fundi Kipande (wa pili kutoka kushoto waliosimama akiwa na kikosi cha Kivule Veteran kabla ya kupambana na timu ya Pugu Kajiungeni hivi karibuni
=========  ==========  ============
TIMU ya Kivule Veteran ya Kitunda, Dar es Salaam inasikitika kutanga kifo cha kipa wake namba moja Fundi Kipande (44) aliyefariki jana nyunmbani kwake Kivule baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kivule Veteran, Peter Mwenda alisema marehemu Kipande atakumbumbukwa mengi aliyofanya na kujitolea kwa hali na mali kuiimarisha timu hiyo.

Mwenyekiti Mwenda alisema marehemu nKipande alitumia muda wake kuwahamasisha wachezaji wenzake kucheza kwa ari na kulinda goli lake anapokuwa uwanjani kila timu yake ilipocheza katika michezo ya kirafiki na mashindano.

Marehemu Kipande aliyesaidiana na Jesse John (mtangazaji wa TBC Taifa)kulinda lango la Kivule Veteran alikuwa kivutio kikubwa manjonjo aliyekuwa anayaonesha alipokuwa golini.

Kutokana na msiba huo shughuli zote za michezo ya kirafiki na mashindano yamesimamishwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Kila mchezaji na washabiki wa timu hiyo wametakiwa kufika klabu iliyopo karibu na ofisi za mchezaji wa zamani wa Simba, Qureshy Ufunguo kusaini kitabu cha maombolezo.

Marehemu Kipande alisafirishwa jana hiyo hiyo kwenda kuzikwa nyumbani kwao Kidodi, Kilombero mkoani Morogoro.

Ameacha mke na watoto wawili wa kike, Mungu ilaze roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amen.

Katika "HUYU NA YULE" ya NJE-NDANI wiki hii......

0
0
Photo Credits: Bongo Celebrity 
Katika NJE NDANI wiki hii, mbali na habari kutoka Afrika, utasikia mahojiano yangu na NURU THE LIGHT.

Msanii, Mjasiriamali, Mtangazaji, Blogger na Mwanaharakati ambaye amekuwa mkarimu sana kujiunga nami kutoka Stockholm Sweden
Kazungumza mengi mema.

Jiunge nami, MUBELWA BANDIO Jumamosi (June 28) katika NJE NDANI ya Kwanza Production na Border Radio kuanzia saa sita mpaka saa nane mchana kwa saa za Marekani ya mashariki kupitia www.kwanzaproduction.com ama www.bordermediagroup.com

SUMATRA YAPATA MKURUGENZI MKUU MPYA

0
0


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA UCHUKUZI




 

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Kwa mujibu wa Sheria ya Wakala wa Serikali No. 30 ya mwaka 1997, Kifungu Na. 9 ikisomwa pamoja na Marekebisho yake ya Mwaka 2009, Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Dkt. Harrison G. Mwakyembe(MB) amemteua Bw. Gilliad Wilson  Ngewe  kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kuanzia tarehe1/6/2014.

Kabla ya Uteuzi huo Bw. G. W. Ngewe , alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA kuanzia tarehe 12/3/2014 ambapo awali alikuwa ni Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti wa Usafiri wa barabara, SUMATRA.
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge namba 9 ya mwaka 2009 ili kusimamia usafiri wa Nchi kavu na Majini Tanzania.
Imetolewa na:
Katibu Mkuu



Wizara ya Uchukuzi.

Makamu wa Rais wa China atembelea Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA).

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (kulia) akiangalia jengo la Makao Makuu ya Ofisi ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) mara baada ya kuwasili Makao Makuu ya shirika hilo leo jijini Dar es Salaam kwenda kuangalia miundo mbinu ikiwemo mabehewa na injini za treni za shirika hilo.  
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (kushoto) akiangalia ramani ambayo reli ya TAZARA inapita kuanzia kituo cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Makao Makuu ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuangalia miundo mbinu ikiwemo mabehewa na injini za treni za shirika hilo. Kulia ni Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (katikati) akielekea katika moja ya treni ya Shirika la Reli la TAZARA kwa ajili ya kuelekea katika moja ya kituo cha Mizigo cha treni ya TAZARA kilichopo Yombo jiji Dar es Salaaam.

 Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa amekaa ndani ya moja ya treni ya abiria tayari kuelekea katika kituo cha Mizigo cha treni ya TAZARA kilichopo Yombo jiji Dar es Salaaam. Kulia ni mgeni wake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao.

 Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe akishuka toka ndani ya treni ya abiria ya TAZARA kuelekea katika kituo cha mizigo cha TAZARA kilichopo mtaa wa Yombo jijini Dar es Salaam.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao akishuka toka ndani ya treni ya abiria ya TAZARA kuelekea katika kituo cha mizigo cha TAZARA kilichopo mtaa wa Yombo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupatiwa maelezo ya kina kuhusiana na reli hiyo
 Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimpa maelezo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (kulia) kuhusiana na shughuli zifanywazo na kituo cha kuhifadhia mizigo inayobebwa na treni ya Shirika la TAZARA wakati alipotembelea katika kituo hicho leo jijini Dar es Salaam.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (kushoto) akimshukuru Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe (kulia) mara baada ya kupata maelezo mazuri kuhusu kazi zifanywazo na Makao Makuu ya Shirika la TAZARA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na mwenyeji wake Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe (kulia) mara baada ya kukamiliha ziara ya kutemebelea Makao Makuu ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) leo jijini Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.

NATIONAL CONSULTATION FOR LOCALIZATION OF THE POST 2015 DEVELOPMENT AGENDA IN TANZANIA

0
0
DSC_0137
The guest of honour, Deputy Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Regional Administration and Local Governments, Mr. Jumanne Sagini delivers his key note address to the invited guests.

The findings from these consultations formed a major input towards building the Post-2015 Development Agenda: the ‘Future we want’. This consultation process was led by ESRF and it targeted the Government (both the Central and Local Government Authority (LGAs)); Civil Service Organizations (CSOs); youth, women, children, the elderly, private sector, research and academic institutions.

Based on the 2012 Post MDGs Development Agenda consultations, a total of 11 priority areas and the respective strategic actions were proposed by Tanzania to the United Nations. These priority areas are meant to define the future Tanzanians want.
DSC_0092
The Executive Director of Ecomomic and Social Research Foundation (ESRF), Dr.Hoseana Lunogelo gives his welcoming remarks at the the workshop. Others are the guest of honour Deputy Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Regional Administration and Local Governments, Mr. Jumanne Sagini (centre) and Acting UN Resident Coordinator and UNICEF Representative, Dr. Jama Gulaid.
DSC_0068
The Guest of honour Deputy Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Regional Administration and Local Governments, Mr. Jumanne Sagini (left) Acting UN Resident Coordinator and UNICEF Representative, Dr. Jama Gulaid (centre) and UNDP Economist, Rogers listens attentively the speech of ESRF, Executive Director.
DSC_0111
Acting UN Resident Coordinator and UNICEF Representative, Dr. Jama Gulaid gives his opening speech at the opening workshop on Localization of Post-2015 Development Agenda to invited dignitaries.
DSC_0118
Above and Below: Some section of invited dignitaries from the government, NGOs, Private Institutions and UN officials.


DSC_0131
DSC_0226
Commissioner Ahmed Makame Haji from Zanzibar Planning Commission (right) with others invited dignitaries.
DSC_0211
Senior Research Associate of ESRF, Dr. Oswald Mashindano gives his presentation on the background to post 2015 Development Agenda consultations and noted that Tanzania has not done enough to reduce poverty and stimulate economic growth.
DSC_0235
DSC_0263
Director of Programmes from Econoomic and Social Research Foundation (ESRF), Dr. Tausi Kida elaborates on snapshot of key Findings: LGA's, CSO's & Zanzibar Consultations.
DSC_0079
A cross section of journalists who attended the workshop.
DSC_0002
UNIDO Representative: Mr. Emmanuel KALENZI (left) exchanges views with the Director of Programmes, Economic and the Social Research Foundation (ESRF), Dr. Tausi Kida.
DSC_0159
The guest of honour, Deputy Permanent Secretary – Prime Mister's Office, Regional Administration and Local Governments, Mr. Jumanne Sagini in a jovial mood with one of the participants while heading to have a group photo.
DSC_0170
The guest of honour, Deputy Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Regional Administration and Local Governments, Mr. Jumanne Sagini in a group photo with invited dignitaries.
DSC_0044
The guest of honour, Deputy Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Regional Administration and Local Governments, Mr. Jumanne Sagini arrives at the ESRF conference hall accompanied by the UN Acting Resident Coordinator and UNICEF Representative, Dr. Jama Gulaid in front of them is the Director of Programmes of Economic and Social Research Foundation (ESRF), Dr. Tausi Kida.

By Damas Makangale, MOblog Tanzania
TANZANIA has recorded an impressive improvement in performance of primary school enrolment. They have achieved remarkable enrolment of 93% after abolishing school fees in public schools with the aim of meeting the Millennium Development Goals (MDGs).

Speaking at the National Consultations Workshop on Localization of the Post-2015 Development Agenda in Dar es Salaam recently, Permanent Secretary in the Prime Minister’s Office, Regional Administration and Local Government, Jumanne Sagini said that the country has also managed to reduce the number of deaths of children under five years old, improve gender equality and access to quality services such as safe water and health facilities.

“Tanzania has made good progress in implementing the agreement of the strategic growth and reducing poverty… Implementation of the MDG agenda was through National Strategy for Economic Growth and Reduction of Poverty commonly known as Mkukuta and Zanzibar strategy for Economic Growth and Reduction Poverty (Mkuza),”
DSC_0014
Ambassador Celestine Mushy, Director of the Department for Multilateral Cooperation in the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation greets one of the invited guests and stakeholders before the official opening ceremony at the workshop on Localization of Post 2015 Development Agenda.
“The vision for these agendas was to move Tanzania from being underdeveloped by alleviating poverty and stimulating economic growth,” he said.
He emphasized that the initiatives have led Tanzania to reduce HIV prevalence from 9.4 % (2000) to approximately 5% in 2014.
Sagini added that despite those successes there still remain challenges to eradicate poverty, improving maternal health, safe water services and provision of quality education in the country.
Acting UN Resident Coordinator, Dr Jama Gulaid said that since 2000, Tanzania has made substantial progress in promoting the MDG however the country’s has had slow progress on other areas such as poverty and maternal mortality.
“It is likely that the clock will run out before important goals have been achieved, as the deadline gets closer, various countries have taken additional measures to accelerate the achievement of MDG.”
He said that the framework for the next set of goals is evolving but there is a strong focus on sustainable development and on specific goals concerning climate change, food and hunger.
Dr Gulaid explained that the workshop, organized by Economic and Social Research Foundation (ESRF), presents opportunities for all of them to examine key aspects of the post 2015 agenda. Furthermore, Tanzania was one of the selected countries which participated in the Post MDG consultation process in December 2012.

MSHINDI WA ‘CHEMSHA BONGO YA BRAZIL’ AKABIDHIWA CHAKE

0
0
Afisa Masoko wa Azam TV, Shah Mrisho (kulia) akimkabidhi zawadi zake Afande Jamila.
Afande Jamila baada ya kukabidhiwa zawadi zake.
Akiwa na tabasamu wakati akihojiwa na wanahabari.
Afisa Masoko wa Global Publishers, wachezashaji wa Bahati Nasibu hiyo, Innocent Mafuru, akiongea na wanahabari baada ya mshindi kukabidhiwa chake.
Afisa Masoko wa Azam TV, Shah Mrisho, akiwaeleza jambo wanahabari (hawapo pichani).

MSHINDI wa Chemsha Bongo ya Brazil inayoendeshwa na gazeti la Championi, Afande Jamila Omari Mkele, leo amekabidhiwa king'amuzi na dishi kutoka Azam TV pamoja na televisheni ya kisasa (flat screen) kutoka kampuni ya Sony baada ya kushinda shindano hilo.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika ofisi za Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Amani, Risasi,  Ijumaa,  Championi na Ijumaa Wikienda.
PICHA : RICHARD BUKOS / GPL     

FFU wa Ngoma Africa band wapanda tena jukwaani baada ya maombolezo ya msiba wa Iraki Hudu (RIP)

0
0


BAADA YA MAOMBELEZO YA KIFO CHA SWAHIBA WAO IRAKI HUDU(RIP)

FFU wa NGOMA AFRICA BAND  WAPANDA TENA JUKWAANI UGHAIBUNI !

Frankfurt,Ujerumani.

Bendi ya Muziki wa dansi Ngoma Africa band alimaarufu  " FFU-Ughaibuni"  walipanda tena jukwaani jumamosi ya 21 Juni 2014 katika Ditzenbach Festival,nje kidogo ya mji wa Frankfurt,kule Ujerumani.
Bendi hiyo maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya yenye makao yake nchini Ujerumani ilikuwa katika maombolezo ya siku saba kutokana na kifo cha layekuwa Swahiba wao wa karibu bondia mkongwe hayati IRAKI HUDU aka Kimbunga(RIP) ambaye alifariki 13.juni 2014 mjini Dar-es-salaam. Baada ya maombolezo hayo bendi hiyo sasa inaendelea na taratibu zake za maonyesho huko ughaibuni.
wasikilize ffu-ughaibuni at www.ngoma-africa.com  au http://www.ngoma-africa.com   

MARCIO MAXIMO ASAINI MKATABA NA YANGA.

0
0


Kocha mkuu wa zamani wa timu ya Taifa, taifa Stars Marcio Maximo 
amesaini mkataba  wa kuwa kocha mkuu na timu ya Yanga kwa muda wa 
miaka miwili. makubaliano hayo yamefikiwa jana, wakala  anaye 
mwakilisha Ally Mleh wa kampuni ya Manyara Sports Management 
amethibitisha hilo.

"Ni kweli kocha Marcio Maximo amekubali kuingia mkataba na timu ya  Yanga ambapo anatarajiwa kuanza kazi rasmi tarehe 27/06/2014 ambapo  atafuatana na msaidizi wake Leonardo Neiva. Mazungumzo ya makubaliano   hayo yalichukua muda mrefu kidogo hatimaye tumefikia
makubaliano.Tunashukuru mungu kila kitu kimekamilika.

Kwa niaba ya Marcio Maximo napenda kuushukuru uongozi wa klabu yaYanga, shukrani za pekee kwa mwenyekiti wa Yanga ndg Yusuf Manji namakamu wake Clement Sanga,  kwa kweli wameonyesha  umakini naprofessional kwa muda wote wa  majadiliano. Nawaombawachezaji,wanachama na wapenzi wote wa yanga tumpe ushirikiano.

Baada ya kumaliza mkataba wake wa kuifundisha Taifa Stars nchini
aliingia mkataba na timu kubwa nchini brazil  mpaka mkataba wake
ulipoisha.Kwa wakati huu kulikuwa na mazungumzo na timu mbalimbali
Zilizotoa  ofa nchini China, Ethiopia na Afrika kusini lakini Yanga
wamefanikiwa kumnasa kocha huyo.

Maximo anatarajia kuwasili kesho siku ya Alhamis saa saba mchana

 
Maximo ilikuwa awasili nchini baada ya fainali za kombe la dunia lakini kutokana na mkataba alioingia na Yanga imebidi afupishe mkataba wa kazi ya 'commentator' aliyokuwa akiifanya nchini Brazil ili awahi kuandaa program zake Yanga.

Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images