Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

Faida ya kabla ya kodi ya Benki ya Exim yaongezeka kwa asilimia 42

0
0
Afisa Fedha Mkuu wa Benki ya Exim, Bw. Selemani Ponda (Katikati) akizungumza na waandishi (hawapo pichani) juu ya utendaji wa kifedha wa benki hiyo katika robo ya kwanza ya mwaka ambapo faida ya benki ya kabla ya kodi imekua kwa asilimia 42 mpaka shilingi bilioni 6.4 ikilinganishwa na kipindi hicho mwaka jana. Kushoto ni Mkuu wa Hazina wa Benki ya Exim Bw. George Shumbusho na kulia Meneja Fedha Mwandamizi Bw. Issa Hamisi. 

Afisa Fedha Mkuu wa Benki ya Exim, Bw. Selemani Ponda (wapili kulia) akizungumza na waandishi (hawapo pichani) juu ya utendaji wa kifedha wa benki hiyo katika robo ya kwanza ya mwaka ambapo faida ya benki ya kabla ya kodi imekua kwa asilimia 42 mpaka shilingi bilioni 6.4 ikilinganishwa na kipindi hicho mwaka jana. Wa kwanza kushoto ni  Meneja Msaidizi Masoko wa Benki ya Exim Bi. Anita Goshashy, Mkuu wa Hazina wa Benki hiyo Bw. George Shumbusho (wapili kushoto) na kulia ni Meneja Fedha Mwandamizi Bw. Issa Hamisi. 
========   =======  =======

BENKI ya Exim imepata faida ya shilingi bilioni 6.8 kabla ya kodi katika robo ya kwanza ya mwaka wake wa fedha, ambayo ni ongezeko la asilimia 42 ukilinganisha na mahesabu ya mapato ya mwaka jana kipidi kama hiki.

 “Tunayofuraha yakuripoti matokeo mazuri katika mwanzo huu wa mwaka,” alisema Ponda, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim. “Kukua huku kwa mapato kunaonyesha mafanikio ya hali ya juu ya benki katika vyanzo mbali mbali vya mapato. Tutaendelea kuboresha utendaji wetu ili kufikia matakwa ya wateja wetu. Benki yetu inaendelea kwenda katika mwelekeo nzuri. Tunazidi kupiga hatua katika kufikia malengo yetu. Matokeo tuliyoyapata ya kifedha katika robo hii ya kwanza ya mwaka yanatupa matumaini makubwa,” aliongeza Ponda.

Pato la jumla limeweza kukua hadi shilingi bilioni 12.5 ambayo ni ongezeko kwa asilimia 27 ukilinganisha na kipindi sawa na hichi mwaka 2013. Pato litokanalo na tozo na kamisheni limeweza kukua hadi shilingi bilioni 8, ambayo ni ukuwaji kwa asilimia 37 ukilinganisha na robo ya mwaka jana, hali iliyosababishwa na kutanuka kwa biashara ya fedha za kigeni. 

“Matumizi ya uendeshaji wa benki yalidhibitiwa na kupanda kidogo kwa asilimia 11.6 mpaka shilingi bilioni 13, yakitokana na uanzishwaji wa gharama za matawi mapya na motisha za wafanyakazi zikiwa ni jitihada za kuongeza upatikanaji wa benki kijeografia na kuimarisha shughuli zake.  Kwa hivyo, uwiano wa gharama na mapato umeshuka kwa kiasi kikubwa kutoka asilimia 75 iliyopatikana katika robo ya mwaka uliopita mpaka asilimia 64, "aliongeza.

Amana za wateja zimebaki palepale shilingi bilioni 747 ukilinganisha na robo ya mwaka uliopita. Jalada la mikopo limerekodi kupanda kwa asilimia 22 ukilinganisha na robo ya mwaka jana mpaka shilingi bilioni 538 pamoja na mizania ya benki kukua kwa asilimia 10 mpaka shilingi tilioni 1.1.

“Kipaumbele kikubwa kwetu bado kipo katika jitihada za kuimarisha nafasi yetu katika soko na kuboresha huduma ili kufikia matakwa ya wateja wetu kupitia uboreshaji wa shughuli zetu. Mwenendo mzuri wa kuwatosheleza wateja ni ishara nzuri inayoonyesha kuwa tutafikia malengo yetu kwa mwaka huu,” alisema Afisa huyo mkuu wa fedha.

Katika mchakato wa kurahisisha utoaji huduma bora kwa wateja, baadhi ya shughuli kama vile za kufungua akaunti na uanzishaji zimeweza kuboreshwa zaidi. Uanzishwaji wa “operesheni ya pamoja” umelenga katika kuongeza msukumo na motisha katika michakato yote ya kazi ili kuongeza ufanisi zaidi na kuhakikisha matakwa ya wateja yanafikiwa kikamilifu,” alisema Bw. Ponda.

Katika jitihada za kupambana na mabadiliko ya mahitaji ya wateja, Benki imeweza kuliunda tawi lake la Kariakoo kwa namna ya kuwahudumia wateja ambaowanafanya shughuli zao zaidi ya masaa ya kawaida ya benki na kuruhusiwa kupata huduma za kibenki kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa mbili usiku. Pia,"Barua pepe na SMS" zinatoa ujumbe wa papo kwa wateja kuwajulisha mihamala mbali mbali inayofanyika katika akaunti zao.

Benki pia imeendelea na jitihada zake za kutanua huduma zake. Benki hivi karibuni imefungua tawi jipya katika kisiwa cha Anjouni mjini Domoni. Kituo cha biashara cha kipekee mkoani Arusha, cha tatu katika jiji na cha 26 nchini kilizinduliwa rasmi katika robo hii. Benki pia inampango wa kufungua tawi jipya mkoani Tabora ambalo litafanya jumla ya matawi kuwa 32 nchi nzima.  Kulingana na utendaji mzuri katika robo hii ya kwanza na fursa zilizopo katika uchumi, Benki ya inalenga kuboresha zaidi utendaji katika robo ikijikita zaidi katikakampeni za kimauzo na kuongeza ufanisi zaidi.

People with albinism: Pillay urges more protection after barbaric killing in Tanzania

0
0
South African Navanethem Pillay, U.N. High Commissioner for Human Rights, speaks during a press conference at the European headquarters of the United Nations in Geneva, Switzerland, Thursday, June 30, 2011. Pillay told reporters she was "disappointed" that China welcomed Sudan's President Omar al-Bashir during a visit this week, rather than arrest him to ensure he stands trial. She said that "the whole world favors trial" for al-Bashir for his role in the civil war in Sudan that killed more than 2 million people. (AP Photo/Keystone, Martial Trezzini) GERMANY OUT - AUSTRIA OUT
UN High Commissioner for Human Rights Navi Pillay.
UN High Commissioner for Human Rights Navi Pillay called Thursday for increased protection for people with albinism, after the barbaric murder of a 40-year-old woman with albinism in north-western Tanzania on 12 May.

“This killing and the terrible circumstances surrounding it sadly demonstrate that the human rights situation of people with albinism in Tanzania and other countries, remains dire,” Pillay said.

According to police reports, Munghu Lugata was brutally murdered Monday night at her home in Mwachalala, a village in Simiyu region, north-western Tanzania. Her attackers chopped off her left leg above the knee, two of her fingers and the upper part of her left thumb, apparently while she was still alive.

These attacks, which are often motivated by the use of body parts for ritual purposes, have claimed the lives of at least 73 people with albinism in Tanzania since 2000. Ms Lugata’s murder is the first reported killing of someone with albinism in Tanzania in 2014.

Pillay welcomed the rapid response of the police, who arrested two local witchdoctors on 13 May.

“The fight against impunity is a key component for prevention and deterrence of the crimes targeting this exceptionally vulnerable community,” Pillay said, while noting that victims often face significant difficulties in bringing their cases to justice, fearing retaliatory attacks or further stigmatization. Without effective and affordable access to justice, many cannot claim their rights.

The High Commissioner stressed that States’ obligation to investigate and prosecute perpetrators of such crimes is particularly critical due to the vulnerability of people with albinism. States must also ensure access to effective remedies, redress and rehabilitation, including medical and psychological care for survivors and victims’ families.

“All over the world, people with albinism continue to face attacks or suffer terrible discrimination, stigma and social exclusion,” said the High Commissioner. The UN Human Rights Office has received reports of more than 200 cases of attacks against people with albinism in 15 countries between 2000 and 2013, but it is believed the actual number could be much higher.

The High Commissioner also expressed concern about the appalling living conditions in at least of Tanzania’s 13 centres for displaced children and adults with special needs. These centres host hundreds of children with albinism who have been abandoned by their families or have fled their homes out of fear of being attacked or killed. Some are administrated by the Government while others are run by faith-based organizations.

The 13 shelters are overcrowded, with very poor health and hygiene conditions. Many of the children with albinism living there reportedly suffer from skin cancer, partly due to the lack of awareness of the staff about a number of simple steps that can be taken to prevent this disease. Cases of sexual abuse have also been reported in some of these centres. Due to the very limited human and financial resources, teaching and learning materials are reported to be almost non-existent in most of them.

“I urge the Tanzanian authorities to take urgent measures to assess and address the situation in these centres, including allegations of sexual harassment and abuse, and the poor living conditions. The staff working with people with albinism should be trained on their special needs, in particular with regard to basic preventive measures to avoid skin cancer,” Pillay said.

The High Commissioner also called upon the Tanzanian authorities to take urgent concrete measures to protect people with albinism, and to actively engage in the fight against stigma attached to albinism through education and awareness-raising campaigns.

TAARIFA YA MSIBA

0
0
 Bwana Salvatory Rweyemamu wa Kinondoni Dar es Salaam, anasikitika kutangaza kifo cha mtoto wake mpendwa Private Brian Salvarory Rweyemamu aliyefariki alfajiri ya kuamkia leo tarehe 15 Mei,2014 katika hospitali ya Jeshi Lugalo alipokuwa akitibiwa.

Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa Bwana Salvatory Rweyemamu Kinondoni jirani na Vijana (Mango Garden).


Habari ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki walioko Dar es Salaam, Kagera, Malawi, Afrika Kusini, Uingereza na Canada.



RAIS KIKWETE AFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA ANGA (ICAO) IKULU JIJINI DAR

0
0
Rais Jakaya Kikwete akimkaribisha Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la  Anga (ICAO) Raymond Benjamin Ikulu jijini Dar es Salaam, Katibu huyo yupo nchini kwa ziara ya Kikazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK. Jakaya Kikwete akiongea na Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la  Anga (ICAO) Raymond Benjamin, wakati alipofika Ikulu jijini Dar es Salaam, Katibu huyo yupo nchini kwa ziara ya Kikazi kuanzia Mei 14 hadi 18 Mei 2014.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya Pamoja na Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Anga (ICAO) Raymond Benjamin, wakati alipofika Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ziara ya Kikazi kuanzia Mei 14 hadi 18 Mei 2014.Kushoto ni Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe, pamoja na viongozi wakuu wa TCAA.
Rais Jakaya Kikwete akiagana na mgeni wake Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la  Anga (ICAO) Raymond Benjamin, baada ya kumalizika kwa maongezi yao ya kikazi yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na baaddhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania TCAA wakati walipokuwa katika ziara ya kikazi na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) Raymond Benjamin ambaye yupo nchini kuanzia Mei 14 hadi Mei 18 2014.Tanzania ni miongoni mwa nchi 24 za ESAF zilizoko Kusini Mashariki mwa Afrika na Majukumu yake ni Pamoja na Kuendeleza sere,Maamuzi , Kanuni na Mapendekezo,Mipango ya uendeshaji wa sekta Usafiri wa anga inayoratibiwa na ICAO, Pamoja na kutoa misaada ya Kiufundi. 

MICHEPUKO NI HASARA,BAKI NJIA KUU UPATE FAIDA

0
0

ONESHO LA KITALII LA S!TE LATAMBULISHWA RASMI INDABA

0
0
 Baadhi ya washiriki wa taasisi za Serikali katika Banda la Tanzania wakati wa maonesho ya INDABA Afrka Kusini.

Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji na Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Bibi Devota Mdachi akitoa maelezo kuhusu vivutio vya utalii vya Tanzania kwa mmoja wa watu waliotembelea banda la Tanzania katika maonesho ya INDABA huko Durban Afrika Kusini.



Na Geofrey Tengeneza Onesho la Kimataifa la Utalii la Tanzania lijulikanalo kama Swahili International Tourism Expo (S!TE) linaroratibiwa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB na litakalokuwa likifanyika kila mwaka mwezi Oktoba katika eneo la Mlimani City jijini Dar es salaam limetambulishwa rasmi kwa wadau mbalimbali waliohudhuria maonesho ya Kimatatifa ya Utalii ya INDABA huko Durban Afrika Kusini. 

Akizungumza wakati wa kutambulisha onesho hilo, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Mh. Radhia Msuya amewaambia washiriki wa INDABA kuwa onesho hilo litakuwa likifanyika kila mwaka na kwa kuanzia mwaka huu litafanyika tarehe 1 -4 Oktoba. 

Amesema kuwa S!TE linatarajiwa kuwa onesho la pilii kwa ukubwa barani Afrika baada ya lile la INDABA na amewakaribisha wadau na makampuni yote yaliyoshiriki maonesho ya INDABA kushiriki pia onesho hilo la S!TE. 

 Maonesho ya INDABA hufanyika Durban Afrika Kusini kila mwaka mwezi Mei ambapo mwaka huu yalifanyika kuanzia tarehe 10-12 Mei na waoneshaji kutoka Tanzania  uliongozwa na mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB Profesa Isaya Jairo. Jumla ya makampuni 41 kutoka Tanzania yalishiriki katika maonesho hayo.

Video mpya ya wimbo wa Mb Doogy 'Baby Mbona Umenuna' ni balaa

0
0
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam.
MWIMBAJI wa muziki wa kizazi kipya, Mbwana Mohamed Mb Doggy, pichani chini, amekamilisha video ya wimbo wake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Baby Mbona Umenuna’.
Video ya wimbo huo imetengenezwa chini ya Abby Kazi, ambaye ameikamilisha mapema wiki hii, huku akijiandaa kuisambaza katika vituo vya televisheni sanjari na kuingizwa kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Qs Mhonda J Entertainment, Joseph Mhonda, alisema kwamba video ya wimbo huo imeandaliwa kwa kiwango cha juu ili kuwapatia burudani kamili wadau na mashabiki wa Bongo Fleva.

Alisema mashabiki watakaobahatika kuitazama video hiyo watapata burudani kamili kutoka kwa msanii huyo mwenye uwezo wa juu katika kona ya muziki wa kizazi kipya.

“Hii ni moja ya video nzuri za msanii Mb Doggy ambaye kwa sasa anajiandaa kuteka tena soko la muziki wa Bongo Fleva, akikumbukia nyimbo zake za zamani zilizomuweka juu, ikiwamo Latifa, Si Uliniambia na nyinginezo.

“Naamini kwa pamoja mashabiki wa msanii huyu watashuhudia uwezo wa Mb Doggy ambaye kwa kiasi fulani ni mmoja ya watu wenye ubora wa sauti na ujuzi wa kuandika nyimbo nzurim,” alisema.

Mb Doggy aliachia wimbo wa Baby Mbona umenuna mapema mwezi uliopita, ambapo sasa amefanikiwa kutengeneza video yake iliyoandaliwa kwa kiwango cha juu kwa ajili ya kumuweka katika mazingira mazuri.

Airtel yadhamini Mafunzo ya waandishi

0
0

Mwenzeshaji wa Mafunzo ya waandishi wa habari bwana Ndimata Tegambwage akiongea wakati wa uzinduzi wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania imedhamini mafunzo ya wapigapicha yatakayofanyika kuanzia kesho katika kituo cha Msimbazi  jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na MP5 2011 Entertainment.  Pichani katikati ni  Afisa mawasiliano na Matukio bi Dangio Kaniki akifatiwa na mratibu wa semina Mpochi Selemani.


KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imesema itaendelea kuwajengea
uwezo wapiga picha za habari kwa kuendela kuwapatia mafunzo ili wapate
ujuzi zaidi kwa kuwa wao ni balozi katika kuipasha jamii habari.

Hayo yalisemwa Jijini Dar es Salaam jana na Afisa Uhusiano na Matukio
wa Kampuni ya Airtel  Dangio Kaniki alipokuwa akizungumza katika
ufunguzi wa mafunzo ya siku nne kwa wapiga picha wa habari kuwajengea
uwezo kufanya kazi katika mazingira hatarishi.

"Tutaendela kuwapatia mafunzo wapiga picha ili wapate ujuzi zaidi
katika utendaji wao wa kazi kwa kuwa mabalozi wetu,na tutawatafutia
vifaa vya kisasa kwa ajili ya kufanyia kazi katika mazingira
hatarishi"alisema Dangio

Mafunzo hayo yanaendeshwa na Baraza la Habari (MCT),na kudhaminiwa na
kampuni ya Airtel kwa kushirikiana na kampuni ya MP5 2011
yanashirikisha wapiga picha kutoka magazeti na TV.

Akizungumza katika mafunzo hayo mshiriki Suleiman Mpochi ambae pia ni
mratibu wa mafunzo hayo alisema watanufaika nayo kwa kuwa watajifunza
mbinu mpya za kufanya kazi katika mazingira hatarishi pamoja na
kufuata maadili ya taaluma ya waandishi wa habari.

Kampuni hiyo ni mara ya tatu inadhamini mafunzo hayo kwa wapiga picha
za habari ambamo Mwezeshaji katika mafunzo hayo Mkongwe wa Habari
katika fani ya habari Ndimara Tegambwage aliiomba kampuni kuendela
kudhamini mafunzo hayo na kuwapatia zana za kisasa za kazi wapiga

FILAMU YA JOTI SANDUKU LA BABU KUINGIA SOKONI HIVI KARIBUNI

0
0
Msanii  Lucas Mhavile ‘Joti’baada ya kukaa kimya kwa mda sasa ameibuka na filamu yake ya Joti Sanduku la Babu ambayo amecheza katika husika tofauti tofauti filamu hiyo itakuwa ikisambazwa na   Kampuni ya proin promotions ya jinini Dar es salaam

akizungumzia filamu hiyo Joti alisema kuwa amekuja kivingini kwani kitu alichofanya katika filamu hiyo aijawai kutokea wala kufanywa na mtu yoyote yule katika tasinia hii ya filamu nchini

 hivyo wapenzi wangu wakae mkao wa kula tu kwani wakati wowote kuanzia sasa itakuwa inaingia sokoni kwani filamu hii si yakukosa mana unambiwa uzee mwisho chalinze mjini kila mtu honey

hivyo wapenzi wa filamu nawaomba wanunue nakala alisi ya filamu hiyo pindi itakapotoka ambapo nimelezea mambo mbalimbali ya ujana usichana pamoja na uzee

 mbali na hivyo filamu hiyo imebeba mambo matatu muhimu kwanza ina burudisha pia ina elimisha na kupata ujumbe muhimu kabisa katika jamii inayotuzunguka'

filamu hiyo ya kwanza tangu joti aweke kando mambo ya filamu na kujingiza katika mambo ya uchekeshaji kupitia luninga sasa ameludi tena katika filamu yake mwenyewe inayokwenda kwa jina la  joti sanduku la babu

TUTAINISHA FURSA ZA KUIVUSHA TANZANIA KIMATAIFA

0
0
Naibu Katibu Mtendaji (Biashara za Kimataifa na Mahusianao ya Kiuchumi) mpya wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bw. Paul Sangawe (Kulia) akila kiapo cha utii na utumishi mbele ya Rais Dkt. Jakaya Kikwete (Kushoto).
=====  ====== =====
Na Saidi Mkabakuli.
Serikali imeweka wazi mkakati wa kuainisha fursa za kipaumbele zitakazoiwezesha kuivusha nchi kikanda na kimataifa kwa kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama inavyobainishwa na Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Miaka Mitano (FYDP I) unaosimamiwa na  Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.

Mkakati huo umewekwa wazi na Naibu Katibu Mtendaji mpya wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, anayeshughulikia Biashara za Kimataifa na Mahusianao ya Kiuchumi Bw. Paul Sangawe mara baada ya kula kiapo cha kuitumika nafasi hiyo. Bw. Sangawe amesema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuongeza mauzo ya bidhaa na huduma pamoja na kufaidika na misaada kutoka nchi marafiki na mashirika ya kimataifa.

Kwa mujibu wa Mpango Wa Maendeleo Wa Taifa  Mwaka 2012/13 thamani ya mauzo ya bidhaa na huduma nje ilikuwa dola za Kimarekani 6,796.3 milioni mwaka 2011, ikilinganishwa na dola 5,805.0 milioni mwaka 2010 sawa na ongezeko la asilimia 17.1. hivyo mkakati wetu ni kuongeza hali hii,” alisema Bw. Sangawe.

Kwa mujibu wa Mpango huo thamani ya bidhaa za kukuza mitaji zilizoagizwa toka nje iliongezeka hadi dola za Kimarekani 3,560.5 milioni kutoka dola 2,715.2 milioni mwaka 2010, sawa na ongezeko la asilimia 31.1. Ongezeko hili lilichangiwa zaidi na kuongezeka kwa uagizaji wa mitambo hasa ile ya viwandani.

Aidha, thamani ya uagizaji wa bidhaa za kati iliongezeka hadi dola za Kimarekani 4,139.0 milioni mwaka 2011, kutoka dola 2,741.2 milioni mwaka 2010, sawa na ongezeko la asilimia 51.0. Uagizaji wa mafuta kwa wingi ulitokana na matatizo yaliyojitokeza ya kutozalishwa kwa kiasi kinachohitajika cha umeme unaotokana na maji, hivyo kupelekea mitambo mingi ya mashine kuendeshwa kwa kutumia umeme unaozalishwa na mafuta.

Vilevile, thamani ya mafuta yaliyoagizwa katika mwaka 2011 ilikuwa dola milioni 3,228.7 ikilinganishwa na dola milioni 2,024.2 mwaka 2010. Uagizaji wa bidhaa za matumizi ya kawaida uliongezeka hadi dola 2,128.0 milioni kutoka dola 1,709.2 milioni mwaka 2010, sawa na ongezeko la asilimia 24.5.

Bw. Sangawe ameongeza kuwa Serikali inajikita katika kutambua masoko kwa bidhaa za Tanzania na vyanzo vipya vya uwekezaji katika uchumi wa Dunia na Kikanda ili kuwezesha sekta binafsi kuchangia kufanikisha utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo ili kuwezesha nchi kuchanmkia fursa za masoko ya kimataifa ikiwemo AGOA na nchi za jumuiya za Ulaya.

“Kipaumbele itakuwa ni kutumia rasilimali chache kuchochea uwekezaji wa sekta binafsi pamoja na kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuvutia uwekezaji katika maeneo ya kipaumbele na ya matokeo makubwa,” aliongeza Bw. Sangawe.

Serikali imeaandaa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano ukiwa na lengo la kuwa na mfumo madhubuti wa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025. Lengo la Dira ni  kuibadili Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025.

MWIMBAJI WA MUZIKI WA DANSI HAPA NCHINI AMINA NGALUMA AFARIKA DUNIA.

0
0
Mmoja wa Waimbaji nyota wa muziki wa dansi waliowahi kuwika haka nchini,amefariki dunia muda mfupi uliopita.

Mwimbaji huyo aliyetamba sana na band ya Tam Tam na Double M iliyokuwa ikiongozwa na Mwanamuziki nyota pia wa muziki wa dansi hapa nchini Muumin Mwinjuma,amefia nchini Thailand alikokuwa akifanya kazi kwa muda mrefu.

Mtu mmoja wa Karibu na Amina Ngaluma,Mwanahamis Omary wa jiji Dar ameiambia Saluti5 kuwa mwimbaji huyo amefariki baada ya kuugua kwa siku kadhaa

Moja ya nyimbo zilizompatia sifa nyingi mwimbaji huyo ni Mgumba No 1 aliouimba akiwa bendi ya African Revolution a.k.a Tam Tam chini ya Muumin Mwinyjuma a.k.a Kocha wa Dunia.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAHALI PEMA PEPONI -AMEN
Chanzo hapa

MADIWANI WA CUF WILAYANI URAMBO WASHIRIKI MAPOKEZI YA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA NA UJUMBE WAKE

0
0
 Madiwani wa Chama cha CUF,wilayani Urambo wakimpokea kwa bashasha kubwa katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akiwasili katika wilaya ya Urambo,mapema leo akitokea wilayani Sikonge.Shoto ni Diwani wa CUF,Mh.Kandola Nyanda wa kata ya Nsenda na kati ni Diwani wa CUF,Kata ya Usoke,Mh.Kadada Mohamed,ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya elimu,afya na maji katika halmashauri ya Urambo mkoani Tabora.Pichani nyuma ya Kinana ni Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Ndugu Nape Nnauye akifurahia jambo.
Diwani wa CUF,Mh.Kandola Nyanda wa kata ya Nsenda akimpokea kwa bashasha kubwa katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akiwasili katika wilaya ya Urambo,mapema leo akitokea wilayani Sikonge.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mh Fatma Mwasa akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Urambo,Mh.Samwel Sitta mara baada ya kuwasili kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana Wilayani Urambo mapema leo.
 Mbunge wa Urambo Mashariki Mh.Samwel Sitta akimkaribisha katika jimbo lake Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na ujumbe wake mapema leo.
 Katibu Mkuu wa CCM ,Ndugu Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa Urambo Mashariki Mh.Samwel Sitta,Pichani kati ni Mkuu wa Mkoa,Mh.Fatma Mwasa pamoja na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Ndugu Nape Nnauye.
  Katibu Mkuu wa CCM ,Ndugu Kinana pamoja na Mbunge wa Urambo Mashariki Mh.Samwel Sitta wakishiriki ujenzi wa jengo la maabara katika shule ya sekondari Uyumbu,katika kata ya Uyumbu wilayani Urambo mkoani Tabora-
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe wake wakielekea kwenye ukaguzi wa mradi wa jengo la Zahanati ya Izengatogilwe,Wilayani Urambo.Zahanati hiyo itakuwa ina uwezo wa kuhudumia watu wapatao zaidi ya Elfu  mbili,kutoka kijiji cha Izenga,Tebela,Msumbiji na Isongwa. 
 Ndugu Kinana akitoka kukagua moja ya chumba cha zahanati hiyo ya  Izengatogilwe,Wilayani Urambo,yenye uwezo wa kuhudumia watu wapatao zaidi ya Elfu  mbili,kutoka kijiji cha Izenga,Tebela,Msumbiji na Isongwa. 
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana pichani kati,shoto ni Mbunge wa Urambo Mashariki Mh.Samwel Sitta pamoja na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Ndugu Nape Nnauye wakipata picha ya pamoja na kikundi cha Sungu Sungu
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiweka jiwe la msingi kwenye mradi wa akina mama,mashine kati  ya nne za kukamulia mafuta ya Alizeti,Wilayni Urambo mkoani Tabora
 Ndugu Kinana akipata maaelezo mafupi ya mradi huo wa mashine ya kukamulia Alizeti
 Ndugu Kinana akikagua shamba la mahindi linalomwagiliwa kwa njia ya Matone,linalomilikiwa na kikundi cha Hiyari ya Moyo kilichopo katika kijiji cha Ndolobo,Wilayani Urambo. 
 Ndugu Kinana akikagua mradi wa ujenzi wa jengo la wodi ya akina Mama Wanaosubiri kujifungua,liitwalo Mayulindila.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na vijana wa chipukizi wa CCM,katika mpaka wa Sikonge na Urambo,katika kijiji cha Izimbili,tarafa ya  Usoke Wilayani Urambo kwa ziara ya siku mbili,ambayo itaambatana na wilaya ya Kaliua mkoani Tabora,ambapo Kinana atakuwa na ziara ya siku 11 mkoni humo,ambapo kilele chake itakuwa siku ya jumapili,ambapo mkutano wa hadhara utafanyika.

UJUMBE WA VIJANA KULAANI VITENDO VIOVU VYA KUMVUNJIA HESHIMA BABA WA TAIFA.

0
0
  Vijana wazalendo na wapenda Amani ambao wamemtembea Mama Maria wakiongozwa na Kiongozi wao anayejulikana kwa Jina la Mohamed Nyundo, wamesema wako pamoja na familia hiyo na kwamba wamesikitishwa na kampeni inayoendelea ya kumchafua Baba wa Taifa, kumkebehi na kumtuhumu kwa Uzushi na uzandiki.

Mama Maria Nyerere amezungumza na vyombo vya habari nyumbani kwake Msasani, na kuwataka vijana waliokwenda kumtembelea kuzunguka nchi mzima kuwaambia ukweli watanzania juu ya Maisha halisi ya mwalimu na mchango wake katika ujenzi wa Taifa huru la Tanzania.


Kumekuwepo na kampeni yenye nia ovu iliyoasisiwa hivi karibuni ya kuharibu taswira na heshima ya Baba wa Taifa Mwalimu Kambarage Nyerere katika jamii ya kitanzania na kimataifa. Kampeni hiyo inayoendeshwa na vibaraka wa nchi za magharibi na Ulaya, wazandiki na maadui wa Amani ya Tanzania imeendelea kusambazwa kwa kasi na kwa gharama kubwa.

Kutokana na kuwepo kwa Kampeni hiyo, jumuiko la Vijana Wazalendo na wapenda Amani  tumeamua kutoa tamko hili la kulaani na kupinga vitendo viovu vya baadhi ya watu kumtuhumu, kumkebehi na kumtukana Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwa kutambua Mchango wa Baba wa Taifa kama muasisi wa Taifa hili, mpigania Uhuru shupavu, Shujaa aliyekuwa na mapenzi ya dhati kwa watu wake na kwa kutambua umahiri na jitihada za kujenga Taifa lenye Muungano, Umoja, Amani na Utulivu, jumuiko la Vijana wazalendo limeamua kuukumbusha Umma wa watanzania juu ya mchango wa utumishi uliotukuka wa Mwalimu Nyerere katika ustawi wa Taifa letu, lakini pia kuhamasisha watanzania hasa Vijana kuenzi kwa Vitendo moyo wa kujituma,weledi na busara za kiuongozi, pamoja na ushujaa na ushupavu wa Mwalimu Nyerere.

Sisi Jumuiko la Vijana wazalendo, tumeona ni vyema kuja kumfariji Mama yetu, Mama Maria Nyerere pamoja na familia nzima ya Mwalimu Nyerere na Kwamba sisi kama wananchi na Vijana makini tutaendelea kuwa pamoja na familia katika kupinga na kulaani vitendo hivyo viovu vya kejeli, matusi, tuhuma na kebehi zinazoelekezwa kwa Baba wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwa masikitiko makubwa, tumeshitushwa na kufadhaika kuona chombo kikubwa na taasisi muhimu ambayo ni muhimili mkubwa wa Serikali kama Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania linakuwa ndio uwanja wa matusi ya kumtukana muasisi wa Taifa hili, imetusikitisha na kutufedhehesha. Imefika wakati sasa, kwa Bunge Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kudhibiti na kuondoa kinga yake kwa wale wote ambao kwa ujinga na kutumika wameamua kuanzisha na kuendesha kampeni kabambe ya kutia doa taswira na heshima ya Baba wa Taifa.

Imetolewa na:
                                                       
Mohamedi Nyundo.
Kiongozi wa Jumuiko la Vijana Wazalendo na Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Pwani.

RAIS KIKWETE AENDA KUMFARIJI SALVA NYUMBANI KWAKE KINONDONI

0
0

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ofisi ya Rais Ikulu Bwana Salva Rweyemamu Kinondoni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mwanaye Private Brian Salva Rweyemamu kilichotokea jana katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini baada ya kuugua kwa muda mfupi. Marehemu Private Brian anatarajiwa kuzikwa kesho mchana(Jumamosi) katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipa pole Bibi Isabela Salva Rweyemamu ambaye ni mama wa Marehemu Private Brian Salva Rweyemamu wakati alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa marehemu Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiwafariji Mkurugenzi wa Mawasiliano Ofisi ya Rais Ikulu Bwana Salva Rweyemamu na Mkewe Isabela Salva Rweyemamu ambao ni wazazi wa Marehemu Private Brian Salva Rweyemamu nyumbani kwao Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuifariji familia ya Marehemu Private Brian Salva Rweyemamu nyumbani kwao Kinondoni jijini Dar es Salaam leo(picha na Freddy Maro)

WANANCHI WA IRINGA WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA VIRUSI VYA UKIMWI

0
0
Mratibu wa kuthibiti ukimwi halmashauri ya manispaa ya iringa sekta ya  afya BONAVENTURA  KALUMBETE amewataka wananchi wa  manispaa ya iringa kuendelea kujitokeza kwa wingi katika upimaji wa virusi vya ukimwi , magojwa ya zinaa, na katika huduma ya tohara.


KALUMBETE amesema kuwa ameridhishwa na mwitikio  wanao uonyesha kwa kujitokeza kwa wingi katika upimaji wa magonjwa hayo.

Mratibu huyo ameongeza kuwa waliojitokeza kupima virusi vya ukimwi mwezi uliopita jana ni  2,541,na waliojitokeza kupima magonjwa ya zinaa ni 306 wakati waliojitokeza kupata huduma ya tohara ni 356 hali inayoonesha kuwa elimu juu ya uthibiti wa magojwa ambukizi imeenea mkoani hapa.


KALUMBETE amesema mkoa wa iringa umefanikiwa kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka nafasi ya kwanza kitaifa kwa  asilimia 15.7 mwaka 2007/2008 hadi kufikia nafasi ya pili kwa sasa ikiwa na asilimia 9.1 wakati nafasi ya kwanza ikishikiliwa na mkoa wa njombe kwa asilimia 14.8.


Aidha amewataka vijana kuwa na tabia ya  kupima afya  kabla ya kuanza mahusiano .

CHINA NA TANZANIA ZATILIANA SAINI MKATABA WENYE THAMANI YA DOLA LAKI MIA MOJA

0
0
 Baadhi ya viongozi toka pande zote mbili wakiwa katika sherehe ya utiaji saini mkataba wa thamani ya dola laki moja za kimarekani kwaajili ya ununuzi wa vifaa vya ofisi za Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania uliofanyika leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.

 Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah akitoa maelezo juu ya kazi mbalimbali zifanywazo na Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania leo wakati wa sherehe fupi ya utiaji saini mkataba wathamani ya dola laki moja za kimarekani kati ya Chama cha Kupunguza matumizi ya silaha na Maridhiano cha China na Ofisi za Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania.

 Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) akiwakabidhi zawadi baadhi ya wajumbe alokuja nao mgeni wake.

 Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) akimkabidhi zawadi mgeni wake Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan (kushoto) mara baada ya kutia saini mkataba wa makubaliano wenye thamani za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam. 
 Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan wakitia saini mkataba huo wa thamnai za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam. 
 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan (kushoto) akimkabidhi zawadi Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) mara baada ya utiaji saini mkataba wa makubaliano wenye thamani za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.

Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (aliyekaa kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan (aliyekaa mstari wa mbele kushoto) mara baada ya utiaji saini mkataba wa makubaliano wenye thamani za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.

PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.

MWAKILISHI WA JIMBO LA KIEMBESAMAKI ATEMBELEA KITUO CHA AFYA CHA KIEMBESAMAKI ZANZIBAR

0
0
 Wauguzi wa kituo cha Afya cha Kiembesamaki wakimskiliza mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (hajupo pichani)alipoende kutembelea kituoni hapo.
 Muuguzi dhamana wa kituo cha Afya cha Kiembe Samaki Bi. Azida Othman akielezea changamoto wanazokabiliana nazo kituoni hapo ikiwa pamoja na kukosa Daktari dhamana wa kituo hicho kwa mda sasa, wa mwanzo kulia Diwani wa Jimbo la Kiembesamaki Bwa. Kharib Mohammed na wakatikati ni Mhe. Mahmoud Thabit Kombo.
 Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Mahmoud Thabit Kombo kushoto akiteta na Diwani wake Bwa. Kharib Mohammed.

Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na Kamati ya Afya yakituo hicho na Wauguzi alipoenda kutembelea kituo hicho ili kujua changamoto wanazokabiliana nazo ili kuzipatia ufumbuzi.(Picha na Makame Mshenga- Maelezo Zanzibar).

KINANA AWAHUTUBIA WANANCHI WA URAMBO,ASIMIKWA UCHIFU WA KABILA LA WANYAMWEZI.

0
0
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu  Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa jimbo la Urambo,katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Mwananchi Skwea mjini Urambo,mkoani Tabora.

Ndugu Kinana akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnaye yuko katika ziara ya mikoa mitatu ya Tabora,Singida na Manyara,ya kuimarisha uhai wa chama,kukagua miradi mbalimbali ya maenedeleo inayotekelezwa na kusimamiwa na Serikali ya CCM,na pia kusikiliza matatizo ya wananchi na kuyapatia ufumbuzi.


Katika mkutano huo wa hadhara uliowakutanisha Wana Urambo kwa wingi,Kinana pia alisimikwa Uchifu wa kabila la Wanyamwezi.Kubwa zaidi Kinana pia alikabidhi piki piki 16 na baiskeli 95 kwa ajili ya watendaji wa chama cha CCM katika kata na matawi,zilizotolewa na Wabunge Mh,Samwel Sitta wa jimbo la Urambo Mashariki na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora,Mh.Magreth Sitta.
 Baadhi ya Wananchi wa Mji wa Urambo wakiwa wamefurika kwenye uwanja wa Mwananchi Skwea,wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kwenye mkutano wa hadhara,uliofanyika Wilayani Urambo,Kinana akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnaye yuko mkoani Tabora kwa ziara ya siku 11,za kuimarisha uhai wa chama,kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya CCM,na kusikiliza matatizo mbalimbali ya wananchi.
Wabunge Mh,Samwel Sitta wa jimbo la Urambo Mashariki akiwahutubia wakazi wa Mji wa Urambo, na kulia ni Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora,Mh.Magreth Sitta.

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikabidhi moja ya piki piki 16 kwa mmoja wa makatibu wa Kata,Bwa.Baraka ambazo zilizotolewa na Wabunge Mh,Samwel Sitta wa jimbo la Urambo Mashariki na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tabora,Mh.Magreth Sitta.

  Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikabidhi baiskeli kwa mmoja wa viongozi wa chama hicho,Bi Fatma Ulaya mjini Urambo katika mkutano wa hadhara

 Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnaye akiwahutubia Wananchi wa Mji wa Urambo kwenye uwanja wa Mwananchi Skwea 

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwa ameketishwa kwenye Kigoda akifanyiwa tambiko mara baada ya kusimikwa Uchifu wa kabila la Wanyamwezi.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu  Abdulrahman akikabidhiwa silaha ya jadi Mkuki,na mmoja wa wazee wa Kinyamwezi mara baada ya kusimikwa Uchifu wa kabila hilo mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Urambo.

Rais Kikwete aongoza Harambee ujenzi wa Kanisa la KKKT Bumbuli

0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia wimbo wa wanabumbuli mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip kwa ajili ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Kilutheri la Bumbuli, Kushoto ni askofu mkuu wa KKKT DKt.Gerhas  Malasusa, Watatu Kulia ni Dkt.Steven Munga wa Lushoto na kulia ni mbunge wa Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na teknolojia Mh.January Makamba Katika harambee hiyo jZaidi ya Shilingi milioni mia tatu zilipatikana
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na watu walioshiriki katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la KKKT Bumbuli jana iliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam jana jioni.Walioketi mbele Wapili kushoto ni Mkuu wa Kanisa la KKKT Tanzania Askofu Dkt. Gerhaz Malasusa,Askofu wa Lushoto Steven Munga(Wanne kushoto) na Watano kushoto ni Mbunge wa Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh.January Makamba.Zaidi ya Shilingi milioni mia tatu zilikusanywa katika harambee hiyo ikiwa ni ahadi,vifaa vya ujenzi na fedha taslimu .
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Naibu waziri Mawasiliano  Sayansi na Technolojia na mbunge wa Bumbuli January Makamba wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Bumbuli Shughuli hiyo imefanyika katika Hotel ya Golden Tulip
.Picha na Freddy Maro

RATIBA YA MAZISHI YA PRIVATE BRIAN SALVA RWEYEMAMU, NA WASIFU WAKE

0
0
MAZISHI LEO JUMAMOSI TAREHE 17.05.2014 

SHUGHULI ZOTE ZITAFANYIKA NYUMBANI KWA BW. SALVA RWEYEMAMU KINONDONI, MKABALA NA VIJANA HOSTEL NA MANGO GARDEN, JIJINI DAR ES SALAAM

SAA      1.00:  ASUBUHI KIFUNGUA KINYWA - NYUMBANI


SAA 4.00-5.00:  CHAKULA CHA MCHANA - NYUMBANI


SAA 5.00-6.00: KUAGA MWILI - NYUMBANI


SAA 6.00-7.00: MISA KATIKA KANISA KATOLIKI MWANANYAMALA


SAA  8.00 Mchana: SHUGHULI ZA MAZISHI MAKABURI YA KINONDONI
---------------------------------------------------------------
WASIFU WA PRIVATE  BRIAN SALVA RWEYEMAMU


Rwechungura Brian Salvatory Rweyemamu, aliyefariki dunia alfajiri ya juzi, Alhamisi, Mei 15, 2014 ni mtoto wa kwanza wa Salva Rweyemamu na Isabella Kafumba Rweyemamu. Alizaliwa Desemba 27, mwaka 1987, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar Es Salaam.
Alipata elimu ya awali katika Shule ya Awali ya Mama wa Kiganda, Kinondoni na Kwa Mama Kate eneo la Chang’ombe, Dar es Salaam kabla ya kuhamia Kenya ambako alianza darasa la kwanza katika Shule ya Msingi ya Top Hill na Lukenya. Hatimaye alihamia kwenye mji Mkuu wa Ubelgiji wa Brussels ambako aliendelea na elimu ya msingi mwaka 1996.


Brian alijiunga na shule ya Bweni ya Trinity Exeter nchini Uingereza ambako aliendelea na kumalizia elimu ya msingi. Ili kumrudisha katika mazingira ya Kitanzania, Bwana Brian alirudia tena darasa la saba katika Shule ya Msingi ya Julius Nyerere iliyoko Mbezi Beach, Kinondoni, Dar Es Salaam, mwaka 1998.


Alijiunga na Shule ya Sekondari ya St. Albans ya mjini Pretoria, Afrika Kusini, mwaka 1999, ambako alikaa miaka minne kabla ya kujiunga na Shule ya Sekondari ya Kaboja nje kidogo ya mji mkuu wa Uganda wa Kampala ambako alimaliza kidato cha sita mwaka 2005.


Alijiunga na Chuo Kikuu nchini Malaysia ambako alichukua masomo ya International Trade, masomo ambayo yalikuwa bado yanamdai credits za semester ya mwisho kabla ya kuaga dunia.


Alijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kambi ya Mlale, Songea, 2010 na kumaliza kumaliza mafunzo yake mwaka 2011 na hatimaye alijiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF) ambako alifanya na kumaliza mafunzo katika Kambi ya Mafinga mjini Iringa mwaka 06/12/2013 kabla ya kuajiriwa na JWTZ mwishoni mwa mwaka jana.


Aliomba na kupewa likizo yake ya kwanza ndani ya JWTZ wiki mbili zilizopita ambako alikaa nyumbani kwa siku chache kabla ya kushambuliwa na malaria kali wiki iliyopita. Alilazwa Jumamosi iliyopita tarehe 10/05/14 katika Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugalo akiwa na malaria na kupoteza fahamu.

Alianza kupata fahamu kwa mbali siku ya Jumanne usiku na kujaribu kuongea siku ya Jumatano. 

Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images