Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

WAKULIMA WA TUMBAKU WAULALALMIKIA UBADHILIFU MKUBWA WA FEDHA ULIOFANYWA NA VYAMA VYA USHIRIKA WILAYANI SIKONGE MKOANI TABORA

0
0
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia,wakazi wa Sikonge katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa CCM,wilayani Sikonge mkoani Tabora jioni ya leo,Kinana alizungumzia matatizo makubwa yanayowakumba wakulima wa zao la Tumbaku huku akionesha kabrasha la taarifa ya ukaguzi na uchunguzi wa chama cha Ushirika cha WETCO LTD,ambalo linaeleza namna wakulima wa Tumbaku walivyoibiwa mamilioni ya fedha.

Aidha,Wananchi wa Sikonge wameulalamikia ubadhilifu huo mkubwa wa fedha uliofanywa na viongozi wa vyama vya ushirika,Kufutia taarifa ya ukaguzi na uchunguzi katika vyama hivyo vya ishilika,inaelezwa kuwa kiasi cha fedha milioni 28 zimefujwa,na kwamba wamekuwa wakicheleweshewa malipo ya fedha zao na pia kutolipwa kwa wakati,jambo ambalo limekuwa likiwakera wakulima hao na kuwarudisha nyuma katika suala zima la  maendeleo.

Kinana aliongeza kusema kuwa vyama vya ushirika vimeanzishwa kwa wingi na wajanja wachache kwa ajili ya kujinufaisha wao na kuwanyona na kuwadhuruma wakulima wa Tumbaku,hivyo Kinana alisema kuwa amekisikia kilio cha wakulima hao,na ameahidi kuyafikisha malalamiko hayo kwa Rais Jakaya Kikwete na hatimaye kupatiwa ufumbuzi. 
 Wakazi wa mji wa Sikonge wakiwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika uwanja wa CCM,wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipowahutubia.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia wakazi wa Sikonge kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa CCM,mkoani Tabora.
Katibu wa NEC Itikadi,siasa na Uenezi Nape Nnauye,akiwahutubia mamia ya wakazi wa mji wa Sikonge waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa CCM,Wilayani humo mkoani Tabora jioni ya leo.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza jambo na Mbunge wa jimbo la Sikonge,Said Mkumba kuhusiana na changamoto mbalimbali zinazowakumba wakulima wa zao la Tumbaku wilayani Sikonge mkoani Tabora,ambapo inaelezwa kuwa wakulima hao wamekuwa wakilaghaiwa,kudhulumiwa na kunyonywa na vyama vya ushirika.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwasalimia wakazi wa Sikonge waliojitokeza kwa wingi kumpokea kwenye Ofisi mpya ya makao makuu ya CCM Wilayani humo.
Mbunge wa jimbo la Sikonge,Said Mkumba akiwahutubia wananchi wa sikonge jioni ya leo
Ndugu Kinana akishiriki ujenzi wa nyumba sita za kuishi vijana wa PathFinder Green City Wilayani Sikonge mkoani Tabora
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwa ameongezana na Mkuu wa Mkoa,Mh,Fatma Mwasa pamoja na Katibu wa NEC Itikadi,siasa na Uenezi Nape Nnauye wakikagua mradi wa ufugaji kuku wa asili ikiwa ni sehemu ya mradi wa Vijana wa Path Finder Green City,Wilayani Sikonge mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipeana mkono na Mmoja wa vijana waishio katika kijiji cha PathFinder Green City,mara baada ya kukabidhiwa vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwemo madawati kutoka Shirika la Viwanda vidogo vidogo (SIDO),vyenye thamani ya shilingi milioni 15
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiongozwa kwenda kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha afya kijiji cha Mazinge wilayani Sikonge,kituo hicho kitakuwa kinatoa huduma mbalimbali kama vile wagonjwa wa nje,kuhudumia Wazazi na watoto,waja wazito,sehemu ya kuhifadhia maiti,Wodi ya Wanaume na nyinginezo.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akielekezwa na vijana hao namna ya kuchambua tumbaku,na kupanga kulingana na ubora wake,katika ghala la kuhifadhia tumbaku hiyo,ambao pia ni mradi maalum wa vijana wapatao 70 katika kijiji cha PathFinder Green City,wilayani Sikonge,mkoani Tabora.
Mkufunzi wa Kilimo cha Tumbaku kutoka kampuni ya TLTC,Goodluck Mmasi akifafanua namna ya uhifadhi tumbaku kwenye maghala  na namna inavyochambuliwa,Mradi huo ni wa Vijana wa PathFinder Green City,ambao wamekuwa wakijituma kufanya shughuli mbalimbali zikiwemo na za ujenzi pia katika suala zima la kujikwamua na umasikini.
Kinana akishiriki ujenzi wa majengo sita ya mradi wa Vijana wa Pathfinder Green City kwa ajili ya kuishi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikagua mradi wa ujenzi wa jengo la utawala la Vijana wa PathFinder Green City,katika kata ya Pangale Wilayani Sikonge mkoani Tabora.
Vijana wa kijiji cha Path Finder Green City wakiimba mbele ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndgu Kinana mara baada ya kuwasili katika kijiji hicho na kukagua miradi mbalimbali,ikiwemo ya ufugaji nyuki,ulimaji wa zao la tumbaku,ufugaji wa kuku,ufundi aina mbalimbali,Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mh Fatma Mwasa.
Kinana akikagua jengo la Karakana la Mradi wa Vijana wa PathFinder Green City,katika kata ya Pangale wilayani Sikonge mkoani tabora jioni ya leo.
Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi kuhusiana na mradi wa ufugaji nyuki wa vijana wa PathFinder Green City,katika kata ya Pangale wilayani Sikonge mkoani Tabora
Sehemu ya mradi wa Vijana wa Ufugaji Nyuki katika kijiji cha Path Finder Green City kilichopo katika kata ya Pangale,wilayani Sikonge mkoani Tabora,Vijana hao wana jumla ya Mizinga ya nyuki 600 maalum kwa ufugaji nyuki.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipokelewa leo na vijana wa chipukizi katika wilaya ya Sikonge akitokea wilayani Uyui kwa ziara ya siku 10 mkoani Tabora

Kamata kamata ya bodaboda na bajaji katikati ya jiji la Dar na utaratibu kulipia kibali maalum kwa pikipiki binafsi

0
0
ZOEZI la kupiga marufuku bodaboda na bajaji zinazofanya biashara katikati ya Jiji la Dar es Salaam limegeuka biashara kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam hasa kwa watumiaji wa pikipiki hizo kwa ajili ya usafiri binafsi wa kawaida kwenda na kurudi kazini, pamoja na makampuni yanayotumia chombo hicho cha usafiri.

Halmashauri ya jiji sasa imeanza kuwatoza watu binafsi na makampuni yanayotumia chombo hicho shilingi 500 kwa siku kila bodaboda inapoingia mjini wakidai ni tozo ya chombo hicho kupata idhini ya kuingia mjini kwa kila siku.

Wakizungumza na mtandao huu jana baadhi ya wananchi wamelalamikia kitendo cha Halmashauri ya Jiji kugeuza zuio la kufanya biashara ya bodaboda katikati ya jiji aina ya biashara ya kujipatia fedha kwa kutoza shilingi mia tano kwa siku kwa kila pikipiki za watu binafsi na makampuni zinapoingia mjini.

Mkazi wa Jiji, Jackson Chalamila alisema tayari amelipia kibali cha miezi sita yaani shilingi 90,000 kama tozo ya kuingia mjini kila siku na ameruhusiwa kuingia mjini na pikipiki yake anayodai huitumia kama chombo cha usafiri kwenda na kurudi kazini kila siku za kazi.
Baadhi ya madereva wa pikipiki wanaozitumia kama vyombo vya usafiri binafsi kwenda na kurudi kazini wakihoji juu ya mkanganyiko huo katika ofisi za Jiji la Dar es Salaam, juzi. Hata hivyo hawakupata majibu zaidi ya kukuta tangazo lililositisha upokeaji wa toza za kuingia mjini na vibali.

"...Binafsi nimelipia kutokana na usumbufu ambao ninaupata toka kwa mgambo wa jiji kila siku wanatukamata ukiwaonesha kitambulisho cha kazi kinachokuonesha kuwa wewe hufanyi biashara ya bodaboda hawakitambui na wanasema unatakiwa kuwa na kibali, hivyo nikalazimika kukata baada ya kulipia shilingi 90,000," alisema Chalamila.

Aliongeza kuwa hata hivyo utaratibu huo si wa haki bali ni namna ya kuwanyonya wananchi kwani mtu hawezi kulipishwa tozo za kuingia mjini kwa chombo anachokitumia kama usafiri wake wa kwenda na kurudi kazini, ilhali magari hayalipi tozo yoyote ya kuingia mjini.
Tangazo lililobandikwa na Jiji kusitisha zoezi la ukusanyaji wa tozo/vibali vya kuingia mjini na pikipiki.

"Huu ni utapeli mtupu, sisi tunalipa kodi kama ilivyo kwa magari binafsi na ni chombo cha moto mtu unakitumia kama usafiri wako iweje ulipishwe kila siku unapoingia mjini? Mbona watu wanaotumia magari kama usafiri binafsi hawalipi wanapoingia mjini? Huu ni wizi...," alisema.

Mwandishi wa habari hizi alifika hadi ofisi ya Jiji kutaka kupata ufafanuzi juu ya malalamiko hayo ya baadhi ya wafanyakazi wanaotumia pikipiki kwa ajili ya shughuli zao binafsi na kutozwa ushuru wa kuingia mjini, lakini haikufanikiwa kumpata msemaji wa jiji ambapo walizi walidai ametoka nje ya ofisi kikazi.

Mwandishi wa habari hii alishuhudia tangazo lililowekwa na Jiji la kuwarifu wananchi kuwa limesitisha malipo ya tozo za pikipiki kuingia mjini hadi hapo itakapotangazwa tena, ili kutoa nafasi kwa jiji kukagua vibali vilivyotolewa na kuvihakiki kabla ya kuendelea. Hata hivyo baada ya mkanganyiko huo baadhi ya watu waliolipia walianza kufika katika ofisi hizo wakitaka kurejeshewa fedha zao na wengine kuhoji kadhia hiyo.

tamasha la mtu kwao laanza leo.

0
0
 mmoja wa wawadau wa utamaduni akiwa anawaonyesha malagwanani jinsi ya kutumia mishale
 wanafunzi wakiwa wanapewa mafunzo ya kutengeneza magari ya mabati
 machifu wakibadilishana uzoefu na ukabila wao
 malagwanani wa kimasai wakiwa katika picha ya pamoja






 chifu wa  kinadi  ambayo ipo katika wilaya ya Itilima  mkoani Simuyu  Wenceslaus Clement  akiwa anabadilishana mawazo na malagwanani wa kimasai
 mkutunzi wa kabila la wabarabaigi akiwa anawaonyesha malegwanani wa kimasai mishale ya sumu ambapo alisema kuwa mishale hiyo ina sumu kali ambayo imetengenezwa na miti aina saba ambayo ikikupiga tu auwezi kukimbia ata hatua ishirini kabla ujaanguka na dawa yake aipatikani hospitalini zaidi ya wao wenyewe wanaotengeneza mishale hiyo kukupa dawa




 maandalizi ya machalari yakiendelea
 chifu   Gilbert Rugal Isambe akiwa anapokea maelezo ya jinsi ya kutengeneza nguo za kabila ya kibarabaigi  kutoka kwa mkufunzi wa kabila hilo ambalo jina atukuweza kulipata
 mnyama aina ya ngamia nae pia aliletwa kwa ajili ya kuwa kivutio katika tamasha hili na hapa wananchi na wanafunzi wakiwa wanawaaangalia wanyama hao
 mwanadada wa libeneke la kaskazini akiwa amejumuika na waimbaji wa ngoma ya kichaga wakiwa wanacheza pamoja hii yote ni kuuenzi utamaduni wetu
 wanafunzi wa shule za msingi nao walikuwepo wanaendelea kuburudika na ngoma
 vyakula vya jadi vikiwa vinaendelea kupikwa live


 picha ya juu na chini ni maandamano ya machifu kutoka mikoa mbalimbali yakiwa yanaingia katika uwanja wa sheikh Amri Abeid kwa ajili ya sherehe za tamasha la  MTU KWAO lililoanza kufanyika jijini hapa
waandishi wa habari akiwemo mdada wa woindeshizza blog wakiwa wanaburudika na chakula cha jadi ya kimasai kiitwacho loshoro

WAFANYABIASHARA WAFANYA MKUTANO KUJADILI MASWALA YA KIBIASHARA YA AFRIKA MASHARIKI

0
0
Ofisa mikopo kwa wateja wadogowadogo wa Benki ya KCB Tanzania,Teresia Soko akitoa mada kuhusiana na baadhi ya huduma za benki hiyo kwa Wafanyabiashara mbalimbali wa mipaka ya Tanzania,Ambao walikutana jijini Arusha kujadili mikakati ya kibiashara katika soko la jumuiya ya afrika mashariki.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika mashariki Richard Sesibera(kushoto)akiteta jambo na Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara wa Jumuiya ya Afrika mashariki,Felix Mosha,wakati wa mkutano wa wafanyabiashara mbalimbali kutoka mikoa ya pembezoni mwa Tanzania.Mkutano huo uliandaliwa na Benki ya KCB Tanzania na kufanyika jijini Arusha.
Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,Felix Mosha akitoa mada wakati wa mkutano ulioandaliwa na Benki ya KCB Tanzania kwa wafanyabiashara wa mikoa iliyopo mipakani mwa Tanzania.Waliokutana jijini Arusha,kujadili mashwala mbalimbali ya kibiashara katika soko la jumuiya ya afrika mashariki. 

PROIN PROMOTIONS YATANGAZA RASMI KUDHAMINI LIGI YA MPIRA WA MIGUU KWA WANAWAKE LEO JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Katibu wa Michezo kutoka Kampuni ya Proin, Godlisten Anderson akitambulisha viongozi wa kampuni ya Proin Promotions kwa waandishi wa habari wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari uliofanyika leo katika Hoteli ya Southern Sun. Kampuni ya Proin imetangaza kudhamini ligi ya mpira wa miguu kwa Wanawake inayotarajiwa kuanza Mwezi wa Nane.
Rais TFF, Mh Jamal Malinzi na Mwenyekiti wa makampuni ya Proin, Mh Johnson Lukaza wakitia saini katika mkataba wa makubaliano ya udhamini wa ligi ya mpira wa miguu kwa wanawake itakayoanza mwezi wa Nane.
Raisi wa TFF, Mh Jamal Malinzi (kushoto) akibadilishana mkataba wa udhamini na Mwenyekiti wa Makampuni ya Proin, Mh Johnson Lukaza (katikati) mara baada ya kumaliza kutiliana saini katika mikataba hiyo mbele ya waandishi wa habari leo katika mkutano uliofanyika katika Hoteli ya Southern Sun.
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira Cha Wanawake, Bi Lina Muhando akiongea na Waandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Sourthen Sun wakati Kampuni ya Proin ilitangaza kudhamini ligi ya wanawake inayotarajiwa kuanza Mwezi wa Nane.
Rais Wa TFF, Mh Jamal Malinzi akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kuweka saini katika Mkataba wa Udhamini kati ya Proin Promotions na TFF

MKUU WA MKOA WA RUKWA AONANA NA WATAFITI KUTOKA TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO UYOLE MBEYA KUJADILI KUINUA KILIMO CHA NGANO MKOANI RUKWA

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na watafiti kutoka taasisi ya Utafiti wa Kilimo Uyole iliyopo Mkoani Mbeya walipomtembelea ofisini kwake leo kutambulisha mpango wa SARD (Strategic Agriculture Reseach Development) unaodhaminiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika ADB (Africa Development Bank). Mpango huo una lengo la kupunguza utegemezi wa chakula nchini kwa kuongeza uzalishaji wa vyakula mbalimbali ikiwemo zao la ngano ambalo ni sehemu ya mradi huo Mkoani Rukwa.
Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alisisitiza juu upatikanaji wa masoko ya kudumu kwa mazao yatakayozalishwa katika mpango huo badala ya kuwekeza nguvu katika uzalishaji pekee.
Ndugu Anthony Elanga mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Uyole Jijini Mbeya ambae pia ni Mratibu wa Utafiti wa Zao la Ngano Tanzania akizungumza katika kikao hicho. Amesema mpango huo utahusisha wakulima na vikundi vya wakulima ambao watapatiwa elimu na kuwezeshwa mikopo mbalimbali ya kuendeleza kilimo cha ngano Mkoani Rukwa.
Mkutano ukiwa unaendelea.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)

WATATU WAKAMATWA NA MENO 25 YA KIBOKO NA VIPANDE 8 VYA MENO YA TEMBO

0
0
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova akionesha sehemu ya  vipande 8 vya meno ya tembo vilivyodakwa huko Tabata Kisiwani jijini Dar es salaam
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova akikagua gari linalotuhumiwa kutumika
Sehemu ya mali zilizokamatwa


Jeshi la Polisi Kanda Maalum limefanikiwa kukamata vipande zaidi ya ishirini (20) vinavyodhaniwa kuwa ni meno ya Tembo vilivyokuwa vimehifadhiwa nadni ya mfuko maarufu kwa jina la kiroba.

Tukio hili lilitokea tarehe 30/04/2014 katika kiwanda cha Nondo Steel Master kilichopo eneo la Mbozi Road (W) kipolisi Chang’ombe (M) kipolisi Temeke baada ya Polisi kupokea taarifa kuwa katika kiwanda hicho kuna mfuko wa kiroba wenye bidhaa hiyo umefichwa. Baada ya taarifa hizo askari kikosi cha Upelelezi walifika kiwandani hapo na kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Kiwanda hicho aitwaye HITESH S/O PATEL walifanya upekuzi. 

Katika upekuzi huo polisi walifanikiwa kukamata vipande 25 vya meno yadhaniwayo kuwa ni ya KIBOKO vikiwa vimehifadhiwa ndani ya mfuko wa kiroba ukiwa umefichwa kwenye Roll ambayo ni Malighafi maalum ya kutengenezea nondo. 

Kwa mujibu wa taarifa ya maafisa wa wanyamapori ni kwamba kwa idadi ya vipande hivyo 25 ni sawa na VIBOKO 6 waliouawa ambapo meno ya Kiboko mmoja yana thamani ya Dolla za Kimarekani 1500 sawa na Shilingi za Kitanzania zaidi ya (Millioni Mbili Laki Nne na Sabini na Tano) Tshs.2,475,000.

 Hivyo kwa idadi ya VIBOKO sita thamani yake ni sawa na shilingi za kitanzania THS; 14,850,000/= (million kumi na nne, mia nane na hamsini elfu tu). 

Katika tukio hilo, polisi inawashikilia watu wawili ambao ni RASHID S/O ABDALLAH, Miaka 19, mwingine ni HEMED S/O JUMA @ KASIMU, Miaka 25. Washitakiwa hao watafikishwa mahakamani kujibu shitaka linalowakabili pindi upelelezi utakapokamilika.

 Aidha katika tukio lingine mnamo tarehe 5/5/2014 huko maeneo ya Tabata Kisiwani karibu na uwanja wa Twiga Mkoa wa Kipolisi Ilala, Polisi wamefanikiwa kumkamata MUSA S/O LUCAS KIFARU akiwa naa vipande 8 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilogram 13.5 ambavyo thamani yake T.Shs.49,500,000/= vikiwa vimehifadhiwa kwenye begi lenye rangi ya blue na nyeusi. Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa .

ACCESS BANK WATOA MSAADA WA KOMPYUTA KWA SHULE YA SEKONDARI AZANIA

0
0
 Ofisa Masoko Mwandamizi Access Bank, Muganyizi Bisheko (kulia) akimkabidhi moja ya kompyuta Mkuu wa Shule ya Sekondari Azania, Mwl. Benald Ngonzie (kushoto), wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni wanafunzi wa shule hiyo. Benki hiyo jana ilitoa msaada wa kompyuta 10 kwa shule hiyo zenye thamani ya zaidi ya Sh2 milioni.
 Ofisa Masoko Mwandamizi Access Bank, Muganyizi Bisheko (kulia) akimkabidhi moja ya kompyuta kwa wanafunzi waliowawakilisha wenzao, anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Benald Ngonzie. Benki hiyo jana ilitoa msaada wa kompyuta 10 kwa shule hiyo zenye thamani ya zaidi ya Sh2 milioni.
  Ofisa Masoko Mwandamizi Access Bank, Muganyizi Bisheko (kulia) akimkabidhi moja ya kompyuta makamu wa rais wa shule ya sekondari ya Azania, Johnson Kaaya, wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni Mkuu wa shule hiyo, Mwl. Benald Ngonzie. Benki hiyo jana ilitoa msaada wa kompyuta 10 kwa shule hiyo zenye thamani ya zaidi ya Sh2 milioni.
  Mkuu wa shule ya Sekondari ya Azania, Mwl. Benald Ngonzie akiongea na wanafunzi mara baada ya makabidhiano ya kompyuta kwa shule hiyo iliyotolewa na  Access Bank. Benki hiyo jana ilitoa msaada wa kompyuta 10 kwa shule hiyo zenye thamani ya zaidi ya Sh2 milioni.
Ofisa Masoko Mwandamizi Access Bank, Muganyizi Bisheko akiongea na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhi kompyuta kwa shule hiyo. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
---
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam. 
Shule ya sekondari ya Azania inakabiliwa na uchakavu wa miundombinu ikiwamo majengo na ubovu wa vyoo, hali inayohatarisha afya za wanafunzi hao kutokana na kuwapo kwa majimaji anayoweza kuzalisha mbu waenezao ugonjwa wa Malaria na Dengue.

Akizungumza jana baada ya kupokea msaada wa kompyuta 10 kutoka katika benki ya Access, Makamu Mkuu wa shule hiyo Elizabeth Ngoda alisema shule hiyo ni kongwe kwa sasa kutokana na kujengwa muda mrefu hivyo inahitajika ukarabati wa kina.

"Shule ni kongwe na imezalisha viongozi mbalimbali na sasa imechakaa, majengo yanahitajikukarabatiwa na vyoo havitoshi, lakini tunawashukuru Access Bank kwa kutuletea kompyuta hizi, kwani tulikuwa na kompyuta 25 awali ambazo hazikukidhi mahitaji kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi," alisema Ngoda na kubainisha kwamba shule ina wanafunzi 2000 na wafanyakazi 115.

Ngoda alitoa wito kwa wadau wengine pamoja na wanafunzi waliowahi kusoma katika shule hiyo,kujitolea kwa hali na mali ili kuirudisha Azania katika hali nzuri ya kimazingira. Makamu wa rais wa shule hiyo Johnson Kaaya aliwashukuru wadau hao huku akitoa wito kwa makampuni mengine kuchangia katika kurekebisha kasoro kadhaa zilizopo shuleni hapo hasa miundombinu.

"Tunaahidi kuzitumia kompyuta hizi katika kuleta ufanisi na si vinginevyo, tunaomba hii iwe chachu kwa makampuni mengine kusaidia zaidi kwani changamoto kubwa hapa shuleni kwetu ni uchakavu wa majengo, hatuna viti, vyoo vibovu na pia tunapata taabu kipindi cha joto kwani hakuna feni," alisema Kaaya.

Naye Ofisa Masoko Mwandamizi wa Access Bank, Muganyizi Bisheko alisema msaada huo ni katika mwendelezo wa mchakato wa kusaidia sekta ya elimu nchini hasa katika upane wa teknolojia ya abari na mawasiliano ambayo imeonekana kuwa kikwazo kikubwa katika utafutaji wa ajira kwa vijana ambao humaliza shule bila kuwa na utaalamu wa kompyuta.
"Tunaamini kupitia kompyuta hizi wanafunzi wataweza kujifunza programu mbalimbali ambazo zitawasaidia katika kukuza elimu yao hapa shuleni na katika maisha yao," alisema Bisheko.

Wanaharakati Waandamana jijini Dar es salaam Kupinga Utekaji wa Wasichana Nigeria

0
0
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi. Lilian Liundi (aliyeshika kipaza sauti) akisoma barua maalumu iliyotumwa kwa ubalozi wa Nigeria nchini Tanzania kuonesha wanaharakati hao kupinga utekaji wa wasichana uliofanyika Nigeria. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi. Lilian Liundi (aliyeshika kipaza sauti) akisoma barua maalumu iliyotumwa kwa ubalozi wa Nigeria nchini Tanzania kuonesha wanaharakati hao kupinga utekaji wa wasichana uliofanyika Nigeria.Mkurugenzi wa WiLDAF, Dk. Judith Odunga, akizungumza kupinga ukatili uliofanywa kwa wanafunzi wa kike kutekwa na kitendo cha Jeshi la Polisi nchini Tanzania kuzuia maandamano hayo ya wanaharakati.  
Mkurugenzi wa WiLDAF, Dk. Judith Odunga, akizungumza kupinga ukatili uliofanywa kwa wanafunzi wa kike kutekwa na kitendo cha Jeshi la Polisi nchini Tanzania kuzuia maandamano hayo ya wanaharakati.Viongozi wakuu wa Mtandao wa Mashirika Huru ya Kijamii (CSOs) wakipokea mabango yenye jumbe anuai za kupinga vitendo vya kikatili vilivyofanywa  na wanamgambo wa Boko Haram. Viongozi wakuu wa Mtandao wa Mashirika Huru ya Kijamii (CSOs) wakipokea mabango yenye jumbe anuai za kupinga vitendo vya kikatili vilivyofanywa na wanamgambo wa Boko Haram.Baadhi ya wanafunzi wa kike na wanaharakati wakiandamana kupinga vitendo vya kikatili vinavyofanywa na kundi la wanamgambo wa Boko Haram. Baadhi ya wanafunzi wa kike na wanaharakati wakiandamana kupinga vitendo vya kikatili vinavyofanywa na kundi la wanamgambo wa Boko Haram. Kwa habari kamili na picha zaidi BOFYA HAPA

ASKOFU SIXBERT PAUL WA KANISA LA VICTORIOUS KUTUNUKIA SHAHADA LA UDAKTARI YA HUDUMA JUMAPILI HII; ROSE MUHANDO NAYE KUPATA CHETI CHA HESHIMA CHA UIMBAJI

0
0

Askofu Sixbert Paul wa kanisa la Victorious la mjini Moshi akizungumza na wandishi wa habari kuhusiana na hafla ya kutunukiwa shahada la udaktari ya huduma



Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini, Askofu Sixbert Paul wa kanisa la Victorious la mjini Moshi akizungumza na wandishi wa habari kuhusiana na hafla ya kutunukiwa shahada la udaktari ya huduma
litakalofanyika jumapili hii. 


Askofu Sixbert Paul wa kanisa la Victorious la mjini Moshi akizungumza na wandishi wa habari kuhusiana na hafla ya kutunukiwa shahada la udaktari ya huduma




Na Mwandishi wetu, Moshi
CHUO kikuu cha Africa, African Graduate University, Chenye makao yake nchini, Sierra Leone kinatarajia kumtunuku shahada ya udaktari ya huduma, Askofu Mkuu Sixbert Paul, wa kanisa la Victorious, lenye makao yake makuu mjini Moshi, mkoani Kilimajaro, katika hafla itakayofanyika Jumapili hii.


Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Askofu Sixbert alisema atakabidhiwa shahada hiyo jumapili ya May 18 mwaka huu katika kanisa la Victorious lililopo Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Askofu Sixbert alisema pamoja na yeye kutunukiwa shahada hiyo, pia mwimbaji wa nyimbo za injili Rose Mhando,atatunukiwa cheti maalumu cha kutambua mchango wake wa kueneza injili kupitia uimbaji.


Alisema katika hafla hiyo mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Meya wa Mji wa Mshi Bw. Jafary Michael, na kwamba viongozi mbalimbali kutoka nchi za Afrika Kusini, Zambia,Uganda , Kenya  na Kongo watahudhuria, akiwemo mpatanishi wa masuala ya kijeshi  anayefanya kazi na umoja wa mataifa Brigedia Timoth Kazembe ambaye anatoka nchini Zambia.

MISS DAR CITY CENTRE 2014 TALENT SHOW KUTIKISA MAISHA CLUB

0
0
 Warembo wanaowania taji la Miss Dar City Center 2014 wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mkutano na waandishi wa Habari hii leo.
Mratibu wa shindano hilo, Judith Michael akizungumza na wanahabari, pamoja nae ni Mkufunzi wa warembo hao. 
 *********
Na Father Kidevu Blog 
WANYANGE 20 wanao wania taji la Miss Dar City Center kesho Mei 16 mwaka huu watawasha moto vikali katika ukumbi wa Maisha Clab wakati wa shindano lao la Vipaji.

Shindano hilo litaongozwa na wasanii, Rich Mavoko, Bonge la Nyau na TID ‘Mnyama’ wanataraji kuwaongoza warembo hao kuwania taji la Vipaji 'Miss Talent Dar City Center 2014."

Akizunguumza na waandishi wa Habari Dar es Salaam leo mratibu wa Shindano hilo, Judith Michael Amesema warembo wote 20 wapo katika hali nzuri na wamejifua vya kutosha kwaajili ya shindano hilo la vipaji.

“Tunaamini shindano la mwaka huu litakuwa zuri sana warembo wamejiandaa vya kutosha, tunapenda kwaalika wadau mbalimbali wa masuala ya urembo waje kwa wingi Club Maisha siku hiyo ya Ijumaa ili waweze kushuhudia wenyewe jinsi warembo wa jiji letu walivyojaliwa vijapaji hakika miss Tanzania yupo Dar City Centre,” alisema Judith.

Aidha Judith amesema shindano la Miss Dar City Centre litafanyika Mei 24 mwaka huu katika ukumbi wa Escape One Mikocheni ambapo pia ameahidi shindano hilo kuwa la aina yake.

Judith amewataja warembo wanao wania taji hilo kuwa ni pamoja na Naomy Kisaka,  Nasreen Abdul, Gladys Matson, Habiba Israel, Jenny Zahn,
Doreen Elias, Winniefrida   Msusa, Grace Mella na Rehema Athumani.

Wanyange wengine ni Francisca Simon, Salha Suleiman, Dorica Daud, Agriphina Yelezwa, Sabina Thomas, Jihan Dimachk, Aziza Thabiti, Hatma Rshidi Nyembo na Neema Sisamo.

Huku wadhamini wa Shindano hilo la Miss Dar City Centre ni Prima Total Hair Collection,Gumbo Investment Diamond Bureau Dechange, Father Kidevu Blog, Maisha Club,Q Plus, Zanzi Cream, Clouds Fm, Machapta, Flamour Cosmetics, Valley Spring, Best Point Hotel, Atik Aluminium, Jambo Leo, Blog Ya Wananchi na Skylight Band.

Miss Uni College Temeke Jumamosi Dar Live, Snura kuliteka jukwaa

0
0
Mratibu wa mashindano ya Miss Uni-College Temeke, Silas Michael (katikati) akiwatambulisha baadhi ya warembo ambao Jumamosi watapanda jukwaani kwenye ukumbi wa Dar Live kuwania nafasi ya mshindi wa kwanza. Mashindano hayo yatapambwa na burudani kutoka kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Snura Mushi “Mamaa Majanga” .

Msanii wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Snura Mushi “Mamaa Majanga” atapamba mashindano ya Miss Uni-College Temeke 2014 yaliyopangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Dar Live Mbagala Jumamosi.

Mbali ya Snura ambaye atafanya shoo kwa kutumbuiza nyimbo zake zote kwa mara ya kwanza, pia bingwa wa masindano ya Tikisa dance 2012 Hassan Jigoro naye atapamba mashindano hayo yatakayoshirikisha juma ya warembo 12 kutoka vyuo mbali mbali vya elimu ya juu vilivyomo manispaa ya Temeke.

Warembo hao ni Martha Mashaka, Sarah Joseph, Diana Joachim Kato, Theola Benedict, Eliana Lucumay, Nyangeta Kuboja, Naila Haroun Yusuph, Martha Manzawa, Susan Joseph, Karen Swai, Sarah Jacob na Flora Kimaro.

Warembo hao wanatoka vyuo vya Kumbukumbu ya ya Mwalimu Mwalimu Nyerere, Chuo Cha Utalii, TIA na Magogoni. Mshindi wa kwanza atazawadiwa Sh 300,000 na vocha ya manunuzi yenye thamani ya Sh250,000 kwenye dula la Robby One fashion,wakati mshindi wa pili atapata Sh250,000 na vocha ya manunuzi ya Sh250,000 na wa tatu Sh 200,000 na wanne na wa tano watapata sh100,000 kila mmoja.

Pia kutakuwa na zwadi ya kifuta jasho ya Sh50,000 kwa warembo waliobaki na zawadi ya simu tatu za Huwawei kwa warembo watakaoonyesha nidhamu ya hali ya juu, kujiamini na mrembo bora katika muonekano pichani.

Mashindano hayo yamedhaminiwa na Continental outdoor, Global Publishers, Robby One fashion, Clouds Media group, Leluu Saloon, New Habari Corporation,Mesho decoration, Millard Ayo, salut5, Huwawei , Lamada Hotel, Shamoo Hotel.

Tanzania Yapokea Msaada wa sh .Bilion 151 kutoka Sweden

0
0
Waziri wa Fedha Saada Mkuya (kulia) na Balozi wa Sweden nchini Lennarth Hjermaker (kushoto) wakiweka saini katika mkataba wa programu ya kukuza stadi za kusoma,kuandika na kuhesabu wenye thamani ya shilingi Bilioni 151 ,leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha Saada Mkuya (kulia) akibadirishana mkataba na Balozi wa Sweden nchini Lennarth Hjermaker (kushoto) baada ya kutiliana saini mkataba wa programu ya kukuza stadi za kusoma,kuandika na kuhesabu wenye thamani ya shilingi Bilioni 151 ,leo jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Sweden nchini Lennarth Hjermaker (kushoto) akajadiliana jambo na Waziri wa Fedha Saada Mkuya (katika) na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Shukuru Kawambwa, baada ya kutiliana saini mkataba wa programu ya kukuza stadi za kusoma,kuandika na kuhesabu wenye thamani ya shilingi Bilioni 151 ,leo jijini Dar es Salaam.( Picha Zote na Lorietha Laurence-Maelezo)

THE GOVERNMENT PLANS TO IMPROVE EMPLOYMENT POLICY

0
0
IMG-20140514-WA0059
Dr. Coffi Agossou, ILO Senior Labour Statistics Specialist facilitating the session during the Intergrated Labour Force Survey (ILFS) Data Production and Management training organised by the ILO for senior officials in labour Market Information System from 12 to 16 May 2014 in Morogoro.
IMG-20140514-WA0055
Participants on Intergrated Labour Force Survey training organised by the ILO from 12 to 16 May in Morogoro. Sitting from left is Dr. Coffi Agossou (ILO), Dr. Albina chuwa(DG-NBS) Flora Minja(ILO) and Sparreboom Theodoor (ILO).
IMG-20140514-WA0062
ILO Officials who participated the training.
IMG-20140514-WA0061
By Staff Writer, MOblog Tanzania.

The government through National Bureau of Statistics (NBS) is conducting its fifth Labour Force Survey this year which would foster the development of quality employment policies across the country.

Speaking to invited dignitaries during the workshop on Labour Force Data Production and Management organized by the International Labour Organization (ILO) and the World Bank in Dar es Salaam today, NBS, Director General, Dr Albina Chuwa said that the survey would provide labour market information.

“ Labour Market Information which will be used in a variety of ways including macroeconomic monitoring and human resources development planning, formulating and monitoring employment policies and programs, measurement of the relationship between employment, income and other social and economic characteristics,” she said.

She said that the NBS statistics guides the government in formulating policies and programs that would respond to the national needs and mostly labour market demands. “In this respect, NBS in collaboration with other stakeholders within and outside the country strives to provide quality data that meets the user needs at National and International levels,” she added.
Dr Chuwa noted that Labour Force Survey (ILFS) provide key labour market indicators which are used by the government to monitor and evaluate the performance of the country’s economy.

“However, due to the changes in population structure and the labour market dynamics, labour statistics from 2006 do not reflect the real status of labour market in the country; compelling the government to conduct the 2014 labour Force Survey that would provide realistic and updated labour statistics,” she said.

She further said that Tanzania like other countries is in need to explore the performance of the labour market in the economy and would help determining the weaknesses emerging in the country’s economy.
Dr Chuwa pointed out that Tanzania has made a great effort in developing the Labour Market Information System which has two modules for employers and job seekers.

RAIS KIKWETE AZINDUA MPANGO MKAKATI WA KUONGEZA KASI YA KUPUNGUZA VIFO VYA UZAZI NA VYA WATOTO LEO

0
0
  Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akionesha jedwali la  alama za ufuatiliaji wa utendaji wa huduma za afya ya mzazi na mtoto wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Kuongeza kasi ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto katika ukumbi wa mikutani wa kimataifa wa Mwalimu Julis Nyerere jijini Dar es salaam leo. Pamoja naye ni naibu Waziri wa Afya Dkt Kebwe Sthephen Kebwe. 
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi kitabu Bibi Halima Shariff, mmoja wa wadau wa afya kutoka katika kundi la marafiki wa maendeleo. pamoja na kitabu hicho pia kuna  jedwali (score-card) la  alama za ufuatiliaji wa utendaji wa huduma za afya ya mzazi na mtoto wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Kuongeza kasi ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto katika ukumbi wa mikutani wa kimataifa wa Mwalimu Julis Nyerere jijini Dar es salaam leo. Pamoja naye ni naibu Waziri wa Afya Dkt Kebwe Sthephen Kebwe.

  Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete na wagemi wengine wakifuatilia maelezo wakati wa  uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Kuongeza kasi ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto katika ukumbi wa mikutani wa kimataifa wa Mwalimu Julis Nyerere jijini Dar es salaam leo. Pamoja naye ni naibu Waziri wa Afya Dkt Kebwe Sthephen Kebwe.
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Kuongeza kasi ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto katika ukumbi wa mikutani wa kimataifa wa Mwalimu Julis Nyerere jijini Dar es salaam leo.  PICHA NA IKULU.

NEW AUDIO: Witnesz Feat. Ochu Sheggy – Think about it

0
0
10376459_10203551940270317_716031196_o
Kuwa wa kwanza kusikiliza Single mpya ya Msanii Witnesz aliyemshirikisha Ochu Sheggy "THINK ABOUT IT" hapa chini.

Ako Labamba yajitosa Miss Ubungo

0
0
CLABU ya Ako Labamba ya jijini Dar es Salaam imejitosa kudhamini shindano la Miss Ubungo litakalofanyika mwezi ujao.
Baadhi ya washiriki wa Miss Ubungo 2014 wakiwa katika pozi. 
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja Miradi wa Kampuni ya AKO Group Ltd, Honesty Minde, alisema wameamua kudhami ni shindano hilo ili kusaidia kulifanikisha.

Alisema wameamua kuwasaidia waandaaji wa shindano hilo ili kukuza sanaa ya urembo, wakiamini kuwa ndio dira ya maendeleo kwa Watanzania wote.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika pozi kwenye clabu ya Ako Labamba.
“Tuliamua kuwapa maeneo ya kufanya mazoezi pamoja na huduma nyingine muhimu kwa waandaaji na warembo wao. “Naamini kwa pamoja tutafanikisha kwa vitendo mafanikio makubwa ya Miss Ubungo mwaka huu, ukizingatia kuwa ndio lengo letu,” alisema.

Wadhamini wengine katika shindano hilo ni Sigmark Tanzania, Prima Hair, Smart Bol, Handeni Kwetu Blog, MG Hostel, City Park Hotel, Milladayo.com, Dartalk na Nelson Fashion.

Taarifa Kwa Umma Kuhusiana Na Tuhuma Za Tanzania Daima

0
0

KINGUNGE AWATAKA WATANZANIA KUONDOKANA NA IMANI POTOFU JUU YA TIBA ASILIA

0
0
2 (14)Mlezi wa Chama Cha Utabibu wa Dawa Asilia Tanzania (ATME), Kingunge Ngombale (kushoto), akifungua mafunzo kwa wahariri na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu tiba asilia  katika ukumbi wa mikutano NIMR jijini Dar es Salaam. (kulia), Mwenyekiti wa Chama cha Utabibu wa Dawa Asili Tanzania (ATME), Bw.Simba Abdulrahmani.
Kingunge amewataka Watanzania kuondokana na imani potofu dhidi ya tiba asili na badala yake watumie ili kupona maradhi mbalimbali yanayowakabili 3 (9)Lucey Samwel, kutoka kitengo cha Tiba asilia Wizara ya Afya akiwakilisha mada ya sera ya Afya, Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala, pamoja na taarifa mbalimbali zinazohusu Tiba Asilia na udhaifu katika usimamizi wa sheria ya TATM ya mwaka 2002.4 (6)Mkurugenzi wa Paseko T.H.P, Othman Shem akielezea kuhusiana na Tiba Asili Tanzania na changamoto zake.5 (4)Mwanasheria kutoka AUDA, Onesimo Munuo (kushoto), akielezea mapungufu ya utekelezaji ya Tiba asili na mbadala.6 (3)9 Wahariri na waandishi wa vyombo vya habari mbalimbali walihudhuria katika mafunzo hayo.
10 (1)Mlezi wa Chama Cha Utabibu wa Dawa Asilia Tanzania (ATME), Kingunge Ngombale. Akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo

madaktari walalamikia kutokamilika kwa miradi ya ujenzi vituo vya afya kwa wakati,wakulima wa tumbaku waangusha kilio chao cha kutolipwa fedha zao mbele ya Kinana wilayani sikonge

0
0
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya ujenzi wa jengo la upasuaji na Dk.Sylvanus Kabutura Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya cha Kata ya Kitunda wilayani Sikonge,Daktari Kabutura  alimueleza Katibu Mkuu wa CCM changamoto kubwa uhaba wa maji katika kituo hicho,na pia kutokamilika kwa jengo kubwa la huduma za upasuaji na huduma nyingine zaidi ya mwaka,jambo ambalo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana hakufurahishwa nalo,kwani kumekuwepo na malalamiko makubwa kutoka kwa wananchi wilayani humo kwa ukosefu wa huduma mbalimbali za afya kwa Wananchi kufuatia kutokamilika kwa jengo hilo na miradi mingine mbalimbali ya zahanati iliyosababishwa na Mkandarasi aliyepewa tenda ya ujenzi wa miradi hiyo,kwa wakati.
  Mbunge wa Jimbo la Sikonge Said Mkumba akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (shoto),kati Dk.Sylvanus Kabutura Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya cha Kata ya Kitunda wilayani Sikonge,pamoja na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnaye wakimsikiliza.

Akitolea Ufafanuzi zaidi kuhusua suala hilo,Mbunge wa Jimbo la Sikonge,Mh Said Mkumba ameeleza kuwa,Mkandarasi wa ujenzi wa vituo hivyo vya Afya,ameshindwa kumaliza kazi kwa wakati,wakati mkataba ulianza mnamo 28/10/2009 na ulipaswa kumalizika 2/5/2011,lakini mpaka sasa vituo hivyo na zahanati havijakamilika,jambo ambalo limekuwa likikwamisha maendeleo katika suala zima la Afya wilayani humo.

Mh.Mkumba alizidi kubainisha kuwa kupitia Mradi wa Kupunguza vifo kwa akina mama Support to Martenal Mortality Project Reduction (SMMRP).Jumla ya vituo saba vya kutolea huduma za Afya Wilayani Sikonge vilitakiwa kujengwa,vikiwa ni Kipili,Kitumbi,Tumbili,Pangale,Kitunda,Mazinge na Kisanga,ambapo jumla ya shilingi bilioni 2,051,723,850 zimelipwa kwa mkadarasi huyo,lakin hata hivyo kazi hiyo haijakamilika mpaka sasa. 
Wananchi wa  kijiji cha Lukula,katata ya Kitunda wakimsikiliza  Mbunge wa Jimbo la Sikonge Said Mkumba,wakati akielezea mambo mbalimbali waliyoyatekeleza kupitia chama chake cha CCM,na pia akionesha ni namna gani amekuwa akikerwa na kunyonywa kwa Wakulima wa zao la Tumbaku,wilayani humo kupitia Vyama vya Ushirika,ambavyo vimefuja kiasi kikubwa cha fedha na kuwaacha wakulima hao katika sintofahamu huku maisha yao yakiendelea kuwa duni siku hadi siku.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Mgambo kitongoji cha Lukula  kata ya Kitunda wilayani Sikonge mkani Tabora ambapo aliwaomba radhi wakulima wa Tumbaku kwa kadhia waliyo nayo kutokana na kunyonywa na kutopata haki zao za malipo kwa miaka 3.Kinana aliongeza kuwa pamoja na kuwaomba radhi wakulima hao wa Tumbaku,amesema waruhusiwa kuuza tumbaku yao wanapotaka,kwa sababu vyama vya ushirika vya msingi vimekuwa vikiwadhulumu kwa kiasi kikubwa wakulima hao.Aidha Kinana ameahidi suala hilo la dhuluma kwa Wakulima wa tumbaku na sualal la Zahanati kuyafikisha kwa Dkt.Rais Jakaya Kikwete.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Mbunge wa Jimbo la Sikonge Said Mkumba wakiwasomea wananchi wa kijiji cha Lukula maeneo yatakayopata umeme mwaka huu katika wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.
 Mkulima wa zao la Tumbaku Lameck Mnyama akitoa ushuhuda na malalamiko ya wakulima wa zao hilo,kwa namna ambavyo vyama vya ushiriki  vimekuwa vikiwaibia na kushindwa kuwalipa fedha zao kwa wakati
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikazia jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mh.Fatma Mwasa na  Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnaye wakimsikiliza mara baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara katika kijiji  cha Lukula katika kata ya Kitunda,wilayani Sikonge.
 Mmoja wa Wasanii wa ngoma ya asili ya Kisukuma ZEZE akitumbuiza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Lukula,kata ya Kitunda,wilayani Sikonge mkoani Tabora,ambapo katibu Mkuu wa CCM,aliwahutubia wananchi hao.
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images